16 Jul 2010


Urban Pulse Production inawaletea burudani na matukio yaliojiri ndani ya Michuano ya kumtafuta Miss & MR East Africa UK 2010 yaliyofanyika  3rd July 2010 Mjini London.

Katika kinyang'anyiro hicho binti Randa Shelbly kutoka Eritrea alinyakua kombe la miss east Africa UK wakati mchizani Degnite Abdeta Dauggie ndio alichukua Mr East Africa UK.

Wadau karibuni kushuhudia tukio hili la kipekee kwa kubofya hapo chini.

Libeneke Oye

asanteni na Wote Mbarikiwe

Frank Eyembe
Urban Pulse Creative



14 Jul 2010

Nimekumbana na swali hili tangu udogoni:Alianza kuku,au lilianza yai?Kama alianza kuku,alitoka wapi ilhali sote twajua kuku anatoka kwenye yai?Na kama lilianza yai,lilitoka wapi wakati tunafahamu kuwa yai hutagwa na kuku?Baada ya kukosa jibu lenye mantiki niliamua kuachana na swali hali maana kujihangaisha kutafuta jibu ilikuwa kazi bure.Nahisi hata nawe msomaji umeshakumbana na swali hilo mara kadha wa kadha.

Lakini hatimaye kitendawili hicho kimepata ufumbuzi.Kwa mujibu wa gazeti la bure la Metro,watafiti wa Kiingereza wanasema kuwa kuku ndiye aliyeanza kabla ya yai kwa vile yai linaweza kupatikana tu kwa chembechembe za protini zinazopatikana katika mifuko ya uzazi ya kuku.

"Imekuwa ikidhaniwa kwa muda mrefu kuwa yai ndilo lililoanza kabla ya kuku lakini sasa tuna ushahidi wa kisayansi kuwa kwa hakika alianza kuku kabla ya yai",alisema Dakta Colin Freeman kutoka Chuo Kikuu cha Sheffield,aliyeshirikiana na watafiti kutoka Chuo Kikuu cha Warwick.

"Protini hiyo ilitambuliwa kabla na ilihusishwa na uzalishaji wa yai lakini kwa kuchunguza kwa undani tumegundua namna gani protini hiyo inavyowezesha hatua hiyo (ya kutengeneza yai).

Protini hiyo-inayofahamika kitaalam kama ovocledidin-17 (OC-17) inafanya kazi kama kichocheo (catalyst) kuharakisha maendeleo ya yai.

Wanasayansi hao walitumia kompyuta yenye uwezo wa hali ya juu (supercomputer) ifahamikayo kama HECToR,ambayo ipo jijini Edinburgh,Scotland, kukuza (zoom) hatua zinazoonyesha jinsi yai linavyozalioshwa.

Ilibainika kuwa OC-17 ni muhimu katika kuanzisha kukomaa (crystallization)-hatua ya awali katika uundwaji wa gamba la yai.Protini hiyo hugeuza calcium carbonate kuwa chembechembe za calcium (calcite crystals) ambazo ndizo zinazounda gamba la yai,huku zikitengeneza gramu 6 za gamba katika kila masaa 24.

Profesa John Harding,pia kutoka Chuo Kikuu cha Sheffield,alisema kuwa ugunduzi huo unaweza kuwa na matumizi mengine pia."Kufahamu namna gani kuku wanatengeneza mayai ni jambo la kupendeza lakini pia linaweza pia kutupatia vidokezo katika namna ya kutengeneza vitu vipya".

Imetafsiriwa kutoka gazeti la Metro toleo la leo.

13 Jul 2010


A politician had an accident and dies.

His soul reaches the Paradise and found St. Peter at the entrance.

-- "Welcome to Paradise! Before you could get in, there is a little problem... We rarely seen politicians here, you know… So we do not know what to do with you..."

-- "I see, no problem just let me enter." says the politician.

-- "I though I would like to let you in but I have higher orders as it´s known… We will do the following: You pass one day in Hell and one day in Heaven. You can then choose where to spend eternity."

-- "It is not necessary, I have already decided. I want to stay in Heaven." says the politician.

-- "Sorry, but we have our rules."

So, St. Peter takes him to the elevator and he comes down, down to Hell. The door opens up and he sees himself in the middle of a beautiful golf course.

In essence, the club where were all his friends and other politicians with whom he had worked. All very happy.

He was greeted, embraced and then they started to talk about the good times when they got rich at the expense of the people.

They played golf, relaxed and then ate lobster and caviar.

Who was also present was the devil, a very friendly guy who spent all the time dancing and telling jokes. They enjoyed themselves so much that before they realize it was time to go.

After a lot of redundant hugs and words of farewell he enter into the elevator.

He rises, rises and the door opens up again. St. Peter was expecting him.

-- Now it´s the time to visit the Paradise.

He spends 24 hours in paradise among a group of happy souls who go from cloud to cloud playing harps and singing. All went very well and before he noticed the day comes to an end and St. Peter returns.

-- "Now what? You spent one day in Hell and one day in Heaven. Now choose your eternal home."

He thought for a minute and answered:

-- "Look, I never thought to make this decision… The Paradise is very good but I think I'll be much better in Hell."

Then St. Peter takes him back to the elevator and he comes down, down to hell.

The door opens up and he saw himself in the midst of a massive ground full of garbage and a horrible smell. He saw all his friends with the clothes torn and very dirty searching the rubble and putting it in black bags. He also saw some of his friends in dispute to take pieces of rotten food.

The devil put the arm by the politician´s shoulder.

-- "I do not understand?" Mumble the politician. -- "Yesterday I was here and it even had a beautiful golf course, a club, lobster, caviar and we danced and had fun all the time. Now I see that it´s only full of very smelly garbage and my friends are totally tear down!"

The devil looks at him… Ironically smiles and says:

-- "Yesterday we were in campaign season before election. Now we have your vote... I´m sorry, this is the reality!"

SOURCE Hubpages

Kuna tofauti moja ya msingi katika Twitter na Facebook (social media nazizipendelea zaidi),nayo ni namna watu wawili wanavyounganishwa na huduma hizo.Wakati nikiomba kuunganishwa na mtumiaji wa Facebook,na kukubaliwa inamaanisha nitaweza kuona profile yake na updates mbalimbali,kwenye Twitter habari ni tofauti.Nikiamua "kumfuata" (following) mtu,haimaanishi kuwa mtu huyo automatically naye "atanifuata".

Lakini katika mazingira ya kawaida,na pengine kistaarabu,kama mtu ameamua "kukufuata" huko Twitter,unapungukiwa nini ukirejesha "fadhila" kwa kumfuata mtu huyo?Au ndio usupastaa kwamba wanaokufuata ni wengi kuliko unaowafuata?Ofkoz,inaweza kuwa vigumu "kumfuata" kila "anayekufuata" ukiwa na "wafuasi" maelfu kadhaa lakini si vigumu kama wafuasi wako ni mia na kitu tu.

Naandika haya nikitambua kuwa uamuzi wa mtu kukufuata ni suala la mtu binafsi.Na kwa vile mtu ahajalazimishwa kumfuata mtu mwingine inaweza kupelekea hoja yangu kuonekana haina umuhimu.Nachojaribu kupigia mstari hapa ni ustaarab wetu wa Kiafrika.Katika mazingira ya kawaida,kama jana nilikutana nawe nikakusalimu,leo pia tumekutana nikakusalimu na kesho inakuwa hivyohivyo,basi kistaarabu inatarajiwa kuwa kesho kutwa nawe utaanzisha salamu.Kinyume cha hivyo,tafsiri itakuwa aidha unaringa au huhitaji salamu yangu.Ni katika mantiki hiyohiyo,kama mtu ameamua kukufuata (hata kama wewe ni maarufu mara elfu kuliko huyo mfuasi) basi ni tarajio la mfuasi huyo kuwa nawe utamfuata.Si lazima lakini ni katika masuala ya ustaarab tu.

Kama unaafikiana nami,basi pengine fanya jambo la kupendezesha roho za wale wanaokufuata lakini wewe hujaamua kuwafuata:WAFUATE PIA.Haigharimu chochote,haikupunguzii umaarufu ulionao,na zaidi,itakufanya uonekane huna dharau.

Ni ushauri wa bure tu.

10 Jul 2010

Kwa mara ya tatu ndani ya wiki moja askari wa jeshi la polisi amejiua kwa kujipiga risasi.Haya si matukio ya kuyachukulia kimzaha kwani licha ya ukweli kuwa vifo vya askari hao ni pigo na doa kwa jeshi hilo lakini pia inawezekana kesho na keshokutwa,Mungu aepushie mbali,tunaweza kusikia askari amemwagia risasi raia kadhaa wasio na hatia kabla ya kutoa uhai wake mwenyewe.Kuna tatizo ndani ya jeshi hilo lakini kama ilivyo ada kwenye maeneo mengine wahusika wanaendelea kujifanya mbuni kwa kuficha vichwa kwenye shimo huku mwili ukibaki nje.

Nilibahatika kufanya kazi na polisi kwa muda mrefu tu na kwa hakika utawahurumia ukisikia na kuona matatizo wanayokabiliana nayo kimaisha na kiutendaji kazi.Kubwa zaidi ni hali ya maisha yao hususan kwenye suala la makazi.Nenda Kilwa Road,Oysterbay au Temeke na shuhudia mazingira wanayoishi wanadola hao,na utakubaliana nami kuwa si vigumu kwao kukumbwa na shinikizo la kisaikolojia.Hebu tafakari kuhusu askari anayekesha lindoni Masaki,Mikocheni,Upanga,Oysterbay,nk kwa vigogo na kushuhudia watu wanavyokula keki ya taifa wakati mwanadola huyo anaishi maisha ya chini kabisa licha ya mchango wake mkubwa katika usalama wa nchi.Ni dhahiri anaweza kupatwa na mawazo kuwa maisha na kazi aliyonayo havina thamani.

Lakini pia kuna unyanyasaji unaotawala kwenye vyombo vyetu vya dola ambapo viongozi ni miungu watu huku wakipata maslahi manono kupindukia ukilinganisha na wale wanaowaongoza.Na hiyo sio huko polisi tu bali hata katika ofisi nyinginezo-za dola na zisizo za dola-ambapo viongozi hujijengea ukuta mrefu wa kuwatenganisha na wanaowaongoza.Vikao kati ya viongozi na watumishi wa ngazi za chini hutawaliwa na vitisho vinavyokwaza kero na malalamiko ya askari wa ngazi za chini kusikika.

Pasipo kutafuta ufumbuzi wa haraka katika wimbi hili la polisi kujiua kwa risasi basi tuwe tayari kushuhudia balaa.Silaha haziui watu,bali watu hutumia silaha kujiua au kuua wengine.Sasa kama askari wetu tunaowakabidhi silaha wanaweza kujiua kama njia ya ufumbuzi wa matatizo yao binafsi,yayumkinika kubashiri kuwa siku moja wanaweza kabisa kuua watu wengine kabla ya kujiua wao wenyewe.

Tusipoziba ufa tutajenga ukuta.Hebu soma habari kamili katika kiungo kifuatacho

Hebu soma habari kamili kwa kubonyeza KIUNGO HIKI.

9 Jul 2010

UJUMBE KUTOKA URBAN PULSE: Karibuni tena wadau wote wa kuangalia sehemu ya pili ya mada ya Uraia Pacha kutoka kwa Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa Bernard Membe wakati akitoa hotuba kwenye Diaspora hapa Mjini Ukerewe tarehe 26.3.2010

Pia Mh Membe alisoma ujumbe kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Jakaya Kikwete akiwasifu na Kuwapongeza Watanzania katika Diaspora. Tafadhali Bonyeza chini kuangalia Video

8 Jul 2010


Imetumwa na mdau FRANK EYEMBE wa Urban Pulse

7 Jul 2010


Demokrasia katika jamii isiyojali utawala bora ni sawa na kufukia makaratasi ardhini kwa matarajio ya kuota mmea wenye matunda ya noti.Ni mithili ya kualika timu ya Taifa ya Brazil kwa mabilioni ya shilingi kisha mechi husika ituache na bili kubwa pasipo manufaa yoyote.Hebu tafakari.Mwezi Oktoba Watanzania kwa mamilioni yao watapiga kura kumchagua Rais na Wabunge.Japo shughuli hiyo ni ya siku moja tu,maandalizi yake yanagharimu mabilioni ya shilingi.Wenyewe wanasema ndio gharama ya demokrasia.Lakini baada ya uchaguzi,wengi-kama sio wote-wa tutakaowachagua watasahau kabisa kwanini tumewachagua,huku wakiwa bize kutafuta namna ya kufidia gharama walizotumia kuingia madarakani.

Zamani hizo tuliambiwa kuwa demokrasia ni pamoja na uwepo wa vyama vingi vya siasa.Takriban miongo miwili baadaye Watanzania wameshuhudia namna uwepo wa vyamahivyo vingi vya siasa ulivyoshindwa kulikwamua taifa letu kutoka kwenye lindi la umasikini.Sanasana umasikini umekuwa ukizidi kuongezeka huku wanasiasa wetu wakibadili kauli mbiu kila baada ya muhula (kwa mfano kutoka Ari Mpya,Kasi Mpya na Nguvu Mpya kuwa Ari Zaidi,Kasi Zaidi na Nguvu Zaidi).Tumeshuhudia pia mlolongo wa sera,mikakati,mpingo na vitu kama hivyo,from MKUKUTA to MKURABITA to KILIMO KWANZA.Na kwa mawazo mapya hatujambo,shughuli ipo kwenye utekelezaji.

Siku chache zilizopita nilitundika makala kuhusu utata wa kauli za Waziri wa Sheria na Katiba Mathias Chikawe na zile za Makamu Mwenyekiti wa CCM Pius Msekwa kuhusu suala la uanzishwaji Mahakama ya Kadhi.Wakati Waziri Chikawe aliahidi kuwa mahakama hizo zingeanza kazi mwakani,Msekwa alitamka bayana kuwa suala hilo haliwezekani.Hadi leo hakuna ufafanuzi uliotolewa kuhusu suala hilo ila kilicho bayana ni kuwa CCM imeamua kuachana nalo baada ya kuliingiza kwenye manifesto yake ya Uchaguzi mwaka 2005.Kwa vile sie ni mahiri zaidi wa kuhangaika na mambo kwa mtindo wa zimamoto tunasubiri liwake la kuwaka ndipo tuanze kuhangaika namna ya kudhibiti.Taasisi zenye majukumu ya kuwa proactive (yaani kuazuia majanga kabla hayajatokea) ziko busy zaidi na kuhakikisha CCM inarejea madarakani kwa ushindi wa kishindo badala ya kujishughulisha na jukumu lao la msingi la kulinda na kutetea ustawi wa taifa letu.Kwao,siasa (yaani CCM) ndio nchi na ndio kila kitu.

Majuzi umejitokeza utata mwingine wa kauli kati ya mawaziri wawili waandamizi kuhusu suala la uraia wa nchi mbili (dual citizenship).Na kichekesho ni kwamba tofauti na ule mgongano wa kauli kati ya Chikawe na Msekwa,safari hii mgongano wa kauli za mawaziri hao umejiri ndani ya jengo la Bunge katika kikao kinachoendela cha bajeti ya mwaka 2010/11.Awali,Waziri wa Mambo ya Ndani Lawrence Masha alilieleza Bunge Tukufu kuwa serikali imeamua kuwa huu sio wakati mwafaka kwa suala la uraia wa nchi mbili,na kwamba serikali anaangalia uwezekano wa kuanzisha ukaazi wa kudumu (permanent residency).Waziri Masha alieleza kuwa serikali inaandaa hoja kuhusu suala hilo la permanent recidency kwa minajili ya kuileta bungeni ijadiliwe. "Huu sio wakati mwafaka kuruhusu uraia wa nchi mbili,serikali inaangalia uwezekano wa kuanzisha ukaazi wa kudumu badala ya uraia wa nchi mbili", alisema Masha.

Wakati Masha akisema hivyo,Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bernard Membe alilieleza Bunge hilohilo kuwa serikali imeridhia suala la uraia wa nchi mbili na kwamba Wizara yake iko kwenye mchakato wa kuwasilisha suala hilo kwenye kikao cha Barza la Mawaziri.Pia Membe alieleza kuwa anafanya mawasiliano na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) ili kupata baraka zao kutokana na suala hilo kuwa la Muungano.Akihitimisha hoja ya bajeti ya wizara hiyo, kwa mwaka wa fedha 2010/2011, Waziri Membe alisema siyo dhambi, Watanzania kutafuta riziki nje ya nchi na ni haki yao kubaki na uraia wa Tanzania.Alisema wakati umefika kwa Watanzania, kupatiwa haki yao ya msingi kwani licha ya kuwa ni manufaa kwao pia ni manufaa kwa nchi kutokana na fursa ya kuongeza pato la taifa.

Kadhalika,inadaiwa kuwa Waziri Membe aliwaeleza Watanzania waliohudhuria mkutano wa Diaspora jijini London hivi karibuni kwamba suala hilo limeshajadiliwa na baraza la mawaziri na linasubiri kuwasilishwa bungeni ili upitishwe au kupingwa na wabunge.Mimi sikuhudhuria Mkutano huo wa Diaspora kwa vile niliamini ungenipotezea muda wangu tu kwa sababu viongozi wetu ni mahiri sana katika kuahidi mambo mazuri kwenye hadhara,na hujifanya wasikivu sana lakini utekelezaji ni zero,sifuri,zilch!

Ni dhahiri kwamba mmoja kati ya mawaziri hawa anadanganya.Wakati sina la kusema kuhusu kauli ya Waziri Masha,kauli za Waziri Membe huko Bungeni na London zinaleta utata unaoweza kuyumkinisha kuwa kuna urongo wa namna flani.Je kauli ipi ni sahihi kati ya hiyo alotoa London kuwa suala hilo limeshajadiliwa na Baraza la Mawaziri na hiyo ya bungeni kuwa suala hilo bado liko wizarani huku likifanyiwa mchakato wa kulipeleka kwenye Baraza la Mawaziri?

Unajua kwanini mmoja wao anadanganya?Sababu ni kadhaa,lakini kwa ufupi,moja,ni kwa vile mdanganyifu huyo anafahamu bayana kuwa wabunge wanaoelezwa suala hilo wapo bize zaidi kufikiri namna watakavyorudi bungeni baada ya uchaguzi (sambamba na kuwazia posho zao nono za vikao vya bunge) kuliko kumkalia kooni waziri aeleze kinagaubaga.Ndio maana mwanzoni mwa makala hii nilibainisha uselessness ya demokrasia yetu.Tunapoteza mabilioni ya shilingi (sambamba na muda wetu kusikiliza porojo za "mkituchagua tufafanya hiki na kile") kuwachagua watu wa kutuwakilisha bungeni lakini wakishafika huko wanakuwa bize zaidi na maslahi yao binafsi.

Pili,anayedanganya kati ya mawaziri hao anafahamu kuwa aliyemteua hatamwajibisha.Kama kuna mtu alimudu kumzuga Rais kwa kuchomekea ishu kadhaa kwenye muswada wa sheria za gharama za uchaguzi na kisha akasalimika,kwanini basi mdanganyifu huyo katika suala hili la uraia mbili awe na hofu?

Tatu,waziri anayedanganya kati ya hao wawili anafahamu udhaifu wa Watanzania katika kudai haki zao za msingi.Kiongozi anaweza kudanganya waziwazi kwenye umati wa watu lakini bado akaishia kupigiwa makofi na vigeregere.Ule wimbo wa "Ndio Mzee" wa Profesa Jay unawakilisha hali halisi ya namna Watanzania wengi wanavyoridhia kuzugwa na wanasiasa wababaishaji.Hebu angalia namna harakati za kuirejesha tena madarakani CCM zinavyopamba moto huko nyumbani.Kwa mgeni,anaweza kudhani labda chama hicho ni kipya na hakihusiki kabisa na kashfa za ufisadi,kubebana,kubomoa uchumi wetu na madudu mengine chungu mbovu yanayoifanya Tanzania kuwa miongoni mwa nchi masikini kabisa duniani licha ya raslimali lukuki iliyojaaliwa kuwa nazo.Binafsi naamini kuwa unyonge huo wa Watanzania umechangiwa sana na siasa za chama kimoja ambapo kiongozi alikuwa mithili ya Mungu-mtu,hakosei,lazima ashangiliwe hata akiongea utumbo,sambamba na suala la kujikomba kwa viongozi kwa matarajio ya kujikwamua kwa namna moja au nyingine.

Na kwa vile vyama vya upinzani vimetuthibitishia kuwa uwezo wao katika kuing'oa CCM madrakani ni kama haupo,basi mazingaombwe kama hayo ya Chikawe na Msekwa,na haya ya sasa kati ya Masha na Membe yataendelea kuwepo kwa muda mrefu sana.Unaweza kuhisi kama nimekata tamaa vile kwa namna ninavyoandika.Hapana,ila safari yetu ni ndefu sana,na tatizo sio urefu tu bali ni kiza kilichotanda kwenye njia yetu ambayo imejaa mashimo kadhaa.Ni sawa na kipofu kumsaka paka mweusi kwenye chumba chenye giza ilhali paka huyo hayumo chumbani humo.

6 Jul 2010

Kushoto ni Urban Pulse Director Baraka Baraka,TV Personality Sporah Njau,Landlady Lucy na Young Moogs
Urban Pulse CEO Frank Eyembe na Jackson Mugisha,Mtanzania Pekee Aliyeshiriki Kwenye Mr & Miss East Africa
Wageni na Washindani
Producer wa Muziki Josh Mbajo na Producer wa Filamu Frank Eyembe
Mc Moseh na Urban Pulse
Fyah Sister First Lady wa Urban Pulse
Kundi la Utamaduni Kutoka Zimbabwe
Washindani Wakiwa Katika Mavazi ya Kitamaduni
Urban Pulse Princes Ordain na Young Jos Wakifunika
Baadhi ya Warembo
Mshindi Randa Shelby Kutoka Eritrea
Mshindi Dawggie kutoka Ethiopia
Washindi
Warembo

4 Jul 2010

Kwanza naomba samahani kwa kupotea kwa zaidi ya wiki sasa.Afya iliyumba kidogo.Napenda kutumia fursa hii kuwashukuru wote walionitumia meseji za kunitakia afya njema.Bwana Amesikiliza sala na dua zenu.

Jana,katika pitapita zangu mtandaoni nilikutana na habari kwamba Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki,Juma Mwapachu,amewashukia wasomi wa vyuo vikuu kwa kuwapotosha wananchi kuhusiana na serikali kujiunga na soko la pamoja la Jumuiya ya Afrika Mashariki lililofunguliwa majuzi.

Kwa mujibu wa habari hiyo,Balozi Mwapachu alitoa kauli hiyo kufuatia ya baadhi ya wasomi kudai kuwa soko hilo linaweza kuwaathiri watanzania katika ushindani wa ajira.Akizungumza jana kwenye ufunguzi wa maonyesho ya 34 ya biashara ya kimataifa yanayoendelea jijini Dar es Salaam, Balozi Mwapachu alisema wasomi hao ambao wamesomea uchumi, wameshindwa kusema ukweli kuhusiana na kujiunga na soko hilo, na kusababisha wananchi kuingia uoga.

Alisema wasomi walipaswa kuwa mstari wa mbele kuwaelimisha wananchi kuhusu jumuiya hiyo na faida zake badala ya kuwapotosha wananchi kuhusu suala hilo na kusababisha baadhi ya nchi wanachama wa jumuiya hiyo kuhofia.

Alisema kabla ya kufungua milango hiyo aliweza kuzunguka katika kila nchi kwa ajili ya kuzungumza na wadau mbalimbali kuhusu suala hilo, lakini wananchi wamekuwa waoga na kusababisha kutoa maoni mbalimbali ya kupotosha.

"Niwashaangaa sana wasomi tena wamesomea uchumi, lakini wamekuwa wa mbele kuwapotosha wananchi kuhusu soko la pamoja la jumuiya ya Afrika Mashariki, hii imesababisha wanachi washindwe kujiamini na kufikiri kuwa wanaweza kukosa ajira,"alisema Mwapachu.

Alisema watanzania wengi wanawaogopa wakenya kwa madai kuwa wanaweza kushindwa kuingia kwenye ushindani wa soko la ajira.

Nadhani kwa mtu mwenye uelewa mkubwa kama Balozi Mwapachu kutoa kauli hizo ni jambo la kusikitisha sana na ni uthibitisho mwingine wa namna maslahi binafsi na ya kisiasa yanavyowekwa mbele ya maslahi ya taifa,sambamba na kupuuza ushauri wa kitaalam.

Yayumkinika kuamini kuwa kwa wadhifa wake kama Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo,ni lazima Mwapachu aipigie debe ili iendelee kuwepo kwani kinyume chake ni kuwa hatakuwa na ajira.Hata hivyo,laiti Mwapachu angeangalia mantiki ya hoja za wasomi (ambazo kwa hakika ziko shared na hata "wasio wasomi") badala ya kuwashambulia kama kundi la kijamii (yaani kujadili hoja badala ya kumjadili mtoa hoja)angeweza kabisa kufahamu kwanini wanaonyesha wasiwasi wao.

Hivi kama kabla ya ujio wa soko la pamoja la Jumuiya hiyo tayari wageni (licha ya hao wanaotoka Kenya na nchi nyingine za Jumuiya) tayari soko la ajira na bidhaa limetawaliwa kwa kiasi kikubwa na wageni,kwanini basi tusihofu kuwa "kuhalalisha" huko kutapelekea hali kuwa mbaya zaidi kwa Watanzania?

Na wakati Mwapachu anatoa porojo zake kuhusu mafanikio ya soko la pamoja,mbona hatuambii yeye na viongozi wenzie wa Kitanzania wameshafanya jitihada zipi kuhamasisha Watanzania kumudu ushindani uliopo na ujao?Siafikiani na mawazo potofu ya Mwapachu kuwa tatizo la Watanzania ni uoga.Na hata kama tatizo lingekuwa ni uoga basi bado hoja ingekuwa iwapo uoga huo ni halali au potofu kwani uoga kama uoga sio dhambi au kosa kama unajengwa kutokana na mantiki.Tatizo la msingi linalowakabili Watanzania kukabiliana na changamoto za mfumuko wa nguvu za nje katika soko la ndani la ajira na bidhaa ni complex sana,na makala hii fupi haiwezi kujadili yote bali itaangalia kwa ufupi.

Kwa upande wa biashara,kuna tatizo sugu la urasimu ambalo kwa kiasi kikubwa linachangiwa na ufisadi.Urasimu kuanzia kwenye utaratibu wa kuandikisha biashara hadi kwenye masuala ya kodi.Sijawahi kufanya biashara lakini nina marafiki kadhaa wanaojaribu kumudu maisha yao kwa kujihusisha na biashara.Kwa kifupi,ajira ya Mtanzania kwa kutegemea biashara ni suala gumu sana.Katika mazingira ya kawaida sio rahisi kwa biashara kudumu kwa angalau miezi kadhaa kama mhusika hatokuwa tayari kutoa chochote kitu kwa wahusika.Yayumkinika kusema kuwa ili biashara halali ishamiri vema ni lazima ikaribishe illegality ya namna flani,yaani uharamu wa biashara ili kuwa halali.

Na wakati Watanzania wengi tu wangependa kujishughulisha na biashara zao kihalali ili wamudu maisha yao,wanakumbana na ushindani kutoka kwa wenzao "wanaobebwa" na vigogo.Hivi mfanyabiashara anayelipa mlolongo wa kodi huku anauza bidhaa za ndani atamudu vipi kupambana na mfanyabiashara anayeagiza vitu kutoka nje (huku vingine vikiwa feki) lakini anavilipia kodi pungufu au halipi kodi kabisa?Ni dhahiri biashara ya huyo "anayebebwa" itashamiri zaidi kuliko ya huyo mnyonge anayejikongoja peke yake.

Lakini pia kuna suala la utamaduni wa kuthamini baidhaa za nje kuliko za ndani.Baadhi ya wachambuzi wanaeleza kuwa miongoni mwa madhara ya utandawazi ni kuibuka kwa mapambano kati ya vitu vya nje dhidi ya vya ndani au vya asili.Hapa simaanishi kuwa kila element ya utandawazi ni mbaya.Sasa kama serikali yetu inaagiza kila kitu kutoka nje kwa ajili ya matumizi yake huku ikiwaacha mafundi seremala wetu "wakidodewa" na samani zao,na hiyo ni kabla ya ufunguzi wa soko hilo,sasa kwanini wasomi wasihofu kuwa soko hilo linaweza kuwa habari mbaya zaidi kwa Watanzania wengi?

Tukija kwenye ajira,hali ndio mbaya zaidi.Wakati Watanzania wamekuwa mahiri zaidi kupeleka watoto wao Kenya na Uganda,wenzetu hao wamekuwa wakileta nguvu kazi yao ya ziada kuchukua nafasi mbalimbali za kazi.Na kama ilivyo kwenye suala la bidhaa,waajiri wetu nao wanaelekea kuwa na ugonjwa uleule wa kuthamini zaidi wageni kuliko wazawa.Mwapachu alipaswa kutueleza ni Watanzania wangapi wana ajira nchini Kenya,Uganda au Rwanda kulinganisha na raia wa nchi hizo waliokamata ajira hapo nyumbani kabla ya ujio wa soko la pamoja.Najua hawezi kusema hilo sio kwa vile hana takwimu (na inawezekana kabisa akawa hana) bali anafahamu kuwa kwa kweka hilo bayana atalazimika kuungana na hofu walionayo wasomi na Watanzania wengine.

Kilichoua Jumuiya ya awali ya Afrika Mashariki ni kuweka siasa mbele ya maslahi ya nchi.sambamba na kupuuza ushauri wa wataalamu.Na akina Mwapachu ambao walikuwa watu wazima muda huo wanataka kurejea makosa hayohayo.Wanajifanya vipofu wa ukweli kwamba ni vigumu kuwa na ushirikiano wa maana palipo na viwango tofauti vya maendeleo kati ya nchi husika.Tunafahamu vema uchumi wa Kenya,Uganda na Rwanda unavyofanya vema zaidi ya uchumi wetu.Sasa kama tunafahamu hilo kwanini basi tusihofu kuwa soko hili jipya linaweza kufanya hali kuwa mbaya zaidi?Au Mwapachu na wenzake wanadhani kuwa ukigusana na tajiri nawe unapata utajiri?They are completely wrong.Mahusiano ya mwenye uwezo wa kiuchumi na mwenye uwezo duni mara nyingi huishia kumnufaisha zaidi mwenye uwezo kwani nguvu ya uchumi inapelekea kuwa na nguvu kwenye maeneo mengine pia.

Akina Mwapachu wanapaswa kufuatilia kwa karibu mambo yanayoyumbisha jumuiya ya Ulaya ambapo nchi kama Uingereza zimeendelea kuwa na msimamo wa kujihusisha kwa kiasi flani tu na sio kwa asilimia 100 kwa vile wanatambua kuwa kuna nchi zenye uchumi duni zinazotarajia ushirikiano huo uwanufaishe wao zaidi at the expense of wale wanaojimudu.

Mwisho,ili Tanzania ijikomboe kutoka uchumi unaomilikiwa kwa zaidi ya asilimia 90 na wageni ni lazima siasa iwekwe kando,ushauri wa kitaalamu uzingatiwe,na kubwa zaidi,maslahi ya taifa yawekwe mbele ya maslahi binafsi.Vinginevyo,soko la pamoja la Afrika Mashariki litaishia kuwa soko la bidhaa na ajira kwa Wakenya,Waganda,Wanyarwanda na Warundi na sie "tukiishia kunufaika" kwa uwepo wa akina Mwapachu kama viongozi wa jumuiya ilhali uchumi wetu ukizidi kuelekea shimoni.

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.