5 Aug 2010

SHIRIKA la Mpango wa Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), limesema rushwa iliyojitokeza katika mchakato wa kura za maoni za CCM, ni hatari kwa mustakabali wa taifa.

Kufuatia hali hiyo shirika hilo limewataka Watanzania hasa vijana, kutokubali kununuliwa katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba mwaka huu.
“Katika vitu vya kushangaza ni jinsi wagombea ubunge na udiwani wa CCM walivyokuwa wakishindana kutoa rushwa ili wachaguliwe na wananchi,” alisema Meneja Mradi wa Kusaidia Uchaguzi wa UNDP, Oskar Lehner.

Lehner alisema hayo jana jijini Dar es Salaam katika kongamano la siku mbili lililowakutanisha zaidi ya vijana 140 kutoka mashirika mbalimbali yasiyokuwa ya kiserikali na wale wa vyuo vikuu.

Kwa mujibu wa Lehner, uuzaji wa shahada za kupigia kura katika uchaguzi, ni sawa na kuuza malengo ya baadaye katika maisha ya watu hivyo ni vyema Watanzania wakafahamu kwamba mustakabali wa maendeleo ya nchi upo katika kipindi hiki cha Uchaguzi Mkuu.

UNDP inatoa kauli hiyo baada ya vyombo mbalimbali vya habari kuripoti rushwa katika mchakato mzima wa kura za maoni za CCM kuwapata wabunge na madiwani watakaogombea katika uchaguzi ujao.

“Angalieni jinsi matendo ya rushwa yalivyoripotiwa katika mchakato wa kampeni na upigaji kura za maoni ya kuchagua mgombea ubunge na udiwani wa CCM," alisema na kuongeza.

“Wananachi na hasa vijana mjihadhari na kujiepusha na rushwa katika uchaguzi, eleweni kuwa, kuuza shahada yako ya kupigia kura, ni sawa na kuuza malengo ya baadaye katika maisha yako,"

“Mafanikio na maendeleo ya baadaye ya nchi, yapo katika mikono yenu hasa katika kipindi hiki cha Uchaguzi Mkuu.”

CHANZO: Mwananchi

RAIS Jakaya Kikwete amewekewa pingamizi kortini kugombea urais mwaka huu kwa madai ya matumizi mabaya ya madaraka na ufujaji wa fedha za umma katika safari zake za nje.

Hayo yameelezwa na Mwalimu Mstaafu na Mkazi wa Dar es Salaam, Bw. Paul Mhozya ambaye amefungua kesi katika Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam kupinga mgombea huyo katika uchaguzi wa Oktoba 31, mwaka huu.

Akizungumza na Majira jana, Bw. Mhozya alisema amefungua pingamizi hilo chini ya hati ya dharura akiitaka mahakama kulisikiliza mapema kabla kampeni kuanza, hivyo akaishauri CCM kuteua mgombea mbadala mapema, badala ya kusubiri uamuzi wa mahakama.

Katika hati ya mashtaka yenye sababu kumi za kuiomba mahakama imuengue Rais Kikwete kwenye kinyang'anyiro cha urais Bw. Mhozya anasema, rais ametumia nafasi aliyopewa kwa mambo binafsi, amekiuka katiba na kuvunja haki za binaadamu pamoja na matumizi holele ya fedha za watanzania kwa mambo yake mwenyewe.

Gazeti la The Citizen toleo la jana lilimkariri Bw. Mhozya kuwa aliwahi kufungua kesi ya kikatiba kama hiyo mwaka 1993 dhidi ya Rais Mstaafu, Ali Hassan Mwinyi kuwa alivunja katiba kwa kuruhusu Zanzibar kujiunga na Jumuiya ya Kiislamu (OIC), lakini ikatupwa na Jaji Barnabas Samatta kuwa mamlaka ya kumwondoa rais madarakani yalikuwa mikononi mwa bunge peke yake, chini ya kifungu cha 46A cha katiba.

Bw. Mhozya alisema amefikia uamuzi wa kufungua kesi hiyo kutokana na ujeuri uliooneshwa na Rais Kikwete katika miaka mitano ya uongozi wake, hivyo ni vema akazuiwa kuurudia kwa kumzuia asirudi madarakani.

Alisema anayo orodha ndefu ya mambo mabaya aliyofanya Rais Kikwete wakati wa uongozi wake, ambayo anatarajia kuyatumia kama ushahidi na uthibitisho wa malalamiko aliyopeleka mahakamani, ambayo anaamini yatakubaliwa na kumwondoa kwenye kinyang'anyiro.

"Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi (NEC), Jaji Lewis Makame alikwishasema kuwa tume iko tayari kupokea pingamizi dhidi ya mgombea yoyote kwa maslahi ya umma na kuwa itachukua hatua stahili, ninasubiri kauli ya mahakama na ninaamini itasikiliza hoja zangu na kuzifanyia kazi," alisema.

Alisema kuwa yeye kama Mtanzania anayo mamlaka chini ya ibara ya 30 (3) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kufungua kesi dhidi ya uvunjaji wa ibara yoyote ndani ya katiba hasa zinazohusu haki za binaadamu.

Ibara ya 30 (3) inasema "Mtu yeyote anayedai kuwa sharti lolote katika Sehemu hii ya Sura hii au katika sheria yoyote inayohusu haki yake au wajibu kwake limevunjwa, linavunjwa au inaelekea litavunjwa na mtu yeyote popote katika Jamhuri ya Muungano, anaweza kufungua shauri katika Mahakama Kuu"

Bw. Mhozya anasema pamoja na kuwa Rais ana kinga kisheria lakini Kikwete hana kinga ya kuwekewa pingamizi kama mgombea kwa sasa, ndio maana akaamua kufungua kesi hii wakati huu badala ya kusubiri atakaposhinda na kuwa rais, kwani atakuwa na uwezo wa kutumia kinga yake.

Alisema katika kipindi cha uongozi wake rais amefanya safari za ughaibuni zisizo za lazima nyingi kwa fedha za umma, jambo ambalo limesababisha wananch wengi kuishi maisha ya taabu na umaskini mkubwa, huku akidai kuwa urais ni suala binafsi, akisema kuwa ndio maana alimteua mwanawe kumtafutia wadhamini.

Alisema sheria inaitaka NEC kutoa muda wa ziada kwa chama ambacho mgombea wake amekufa au ameshindwa kuendelea kukiwakilisha, ili chama hicho kiweze kuteua mgombea mwingine, hivyo anaamini kuwa baada ya pingamizi hilo kukubaliwa mahakamani, NEC itawaamuru CCM kufanya hivyo kwa kuwaongezea muda.

"Sasa kwa vile sheria inasema NEC itawaongezea muda wa kuteua mgombea mwingine, mimi nashauri wakateua kabisa mgombea mwingine na kumshauri niliyemwekea pingamizi kujitoa, hii itaepusha kupoteza muda pindi pingamizi likikubaliwa, hakuna jinsi," alisema Bw. Mhozya.



Alisema yeye anahofia zaidi mustakabali wa nchi na vizazi vijavyo kuliko anavyohofia maisha yake, hivyo pamoja na vitisho anavyopata bado hataogopa kusimamia ukweli na kuwafichua waovu kama anavyofanya.

"Nimetoka mahakamani leo (jana), nilikwenda kuwaona makarani wa wanipatie 'samansi'(hati ya kuhudhuria mahakamani iliyo na tarehe ya kusikilizwa kesi) lakini walisema bado haijatoka naamini itatoka hivi karibuni ili tukasikilizwe. Matatizo yapo na nilikwisha yazoea," alisema Bw. Mhozya.

CHANZO: Majira

Wakati hayo yakimkumba JK,aliyekuwa Mbunge wa CCM (Bariadi) Andrew Chenge a.k.a Mzee wa Vijisenti nae anakabiliwa na tishio la pingamizi kutoka kwa mmoja ya wana-CCM waliokuwa wakiwania nafasi ya kupitishwa kugombea ubunge kwa tiketi ya chama hicho
. Bonyeza HAPA Kusoma Zaidi Kuhusu Chenge.

Natoa wito kwa wanachama walioomba nafasi lakini wakakosa, jamani msiwe chanzo cha mifarakano ndani ya chama, KAZI ZIPO NYINGI,TUNAWEZA KUTEUANA, fanyeni kazi ya ushindi kwa chama chetu,” .Hayo si maneno yangu bali ya Rais Jakaya Kikwete aliyoyatoa siku alipochukua fomu za kuogombea tena urais kwa tiketi ya CCM.Ni kweli kazi zipo nyingi ikiwa ni pamoja na kilimo au biashara lakini haiingii akilini kwa watu waliokataliwa na wananchi kupewa nafasi kwa mlango wa "kuteuana".

Hili ni tatizo sugu katika siasa za Tanzania.Utakuta mtu ameboronga sehemu moja kisha anahamishiwa sehemu nyingine.Yayumkinika kusema kuwa kuteua "rejects" hao sio tu matumizi mabaya ya ruhusu inayotolewa na katika kufanya teuzi mbalimbali bali pia ni dharau ya moja kwa moja kwa wananchi.

Haiwezekani kwamba nchi yenye watu zaidi ya milioni 40 iwe na kikundi kidogo tu cha watu wenye uwezo wa kuwa viongozi.Na kibaya zaidi kikundi hicho kikijumuisha watu waliokataliwa na wananchi katika chaguzi au maombi yao ya kutaka wachaguliwe kuongoza.

Na ukiingia kiundani zaidi kuangalia tabia hii isiyopendeza,unaweza kuyumkinisha kuwa hata uteuzi wa Dkt Gharib Bilal unaangukia kwenye eneo hilohilo.Bilal alitaka ridhaa ya vikao vya CCM kuwa mgombea wa Zanzibar lakini "kura hazikutosha".Hata hivyo,katika kile kinachoelezwa kama kujenga mshikamano miongoni mwa wana-CCM,Bilal aliteuliwa na JK kuwa mgombea mwenza wake.Kwa maana nyingine,mtu aliyekataliwa na kikundi kidogo (kikao cha CCM kilichpiga kura kumpata mgombea urais wa Zanzibar) anaweza kuwa Makamu wa Rais wa Watanzania milioni 40 na ushee pindi JK akishinda katika uchaguzi ujao.

Tumekuwa tukishuhudia teuzi za mabalozi wetu nje ya nchi,wenyeviti wa bodi za wakurugenzi wa taasisi mbalimbali,wakuu wa mikoa na wilaya na nafasi mbalimbali zinazojazwa kwa teuzi zinazofanywa na rais zikijazwa na "rejects"-watu walionyimwa ridhaa ya kuongoza na wananchi lakini wanaishia kuwa viongozi kwa mlango wa nyuma.Yaleyale ya aliyekuwa Katibu Mkuu wa UWT,Hasna Mwilima.Kikundi kidogo katika jumuiya hiyo ya akinamama wa CCM kilimkataa,huku sababu kuu ikitajwa kuwa ni uongozi mbovu.Lakini siku chache baadaye,Rais akamteua mwanamama huyo kuwa Mkuu wa Wilaya.Busara kidogo tu zinaweza kubainisha kuwa kuwa mtu alokataliwa kuongoza UWT hawezi kuwa "rais wa wilaya" (DC) lakini kwa vile Katiba inamruhusu Rais kuteua yeyote amtakaye,analotaka liwe litakuwa.

Ni katika mazingira haya ndio maana tetesi kuwa Lowassa,Waziri Mkuu aliyelazimishwa kujiuzulu kutokana na ufisadi wa Richmond,atarejea madarakani pindi JK akishinda hapo Oktoba zinazidi kupata nguvu kwa vile Rais akiamua iwe na itakuwa.Na kwa vile Watanzania wanasifika kwa upole wao,hakutokuwa na "kelele" za kupinga uteuzi huo.

Nguvu anazopewa Rais kwenye Katiba hazimaanishi ajifanyie mambo anavyotaka bali ni kwa minajili ya kuwatumikia Watanzania kwa ufanisi.Lakini kwa upande mwingine,lawama zinaweza kuelekezwa kwa taasisi zinazomshauri Rais kuhusu teuzi mbalimbali (ikiwa ni pamoja na kuchunguza 'usafi' na uwezo wa wateuliwa watarajiwa) kwa sababu inaelekea kwa wao,kila jina linaloletwa na Rais ni 'safi'.Professionalism na ethics zinawekwa kando kwa minajili ya kumfurahisha mkuu wa nchi.

1 Aug 2010

Taarifa zinaeleza kuwa msanii mkongwe wa muziki wa Bongoflava,Joseph Mbilinyi a.k.a Sugu,ameshinda kura za maoni za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)kuwania nafasi ya kuogmbea ubunge wa jimbo la Mbeya Mjini.

Kila la heri Mr Sugu.Jitihada zako zinapaswa kuwa fundisho kubwa kwa idadi kubwa ya wasanii (hususan wa Bongoflava) ambao kwa wao photo-ops (kuuza sura) na watawala wetu is everything despite having been USED AND ABUSED by same watawala kila unapojiri uchaguzi.

That's wassup,Sugu!

Baada ya kusubiriwa kwa muda mrefu,hatimaye kampuni ya HTC imetangaza rasmi kwamba watumiaji wa simu aina ya HTC DESIRE watapatiwa toleo jipya (version 2.2) la mfumo wa kuendesha simu (operating system -OS- ya Android linalofahamika kama Frozen Yorghut (Mtindi wa Mgando) kwa kifupi Froyo.Kwa mujibu wa taarifa mbalimbali,Froyo itaanza kusambazwa hewani (OTA-over the air) wiki hii kwa wenye HTC Desire ambazo "hazijafungwa" (unlocked) na baadaye kwa "zilizofungwa" (locked) kabla ya kusambazwa kwa simu nyingine zinazotumia OS hiyo ya Android.

Inatarajiwa kuwa Froyo itaziboresha zaidi simu za Android,kwa mfano HTC Desire,ambayo inalinganishwa kwa karibu na "mama wa simu zote",Apple iPhone.Binafsi,nimekuwa nikitumia HTC Desire kwa takriban miezi mitano hivi na kwa hakika ni simu iliyojitosheleza kwa takriban kila kitu.Tatizo pekee hadi sasa,na ambalo limepatiwa ufumbuzi kwenye toleo la Froyo,ni kutoweza kuhifadhi Apps (applications) kwenye memory card hivyo kupelekea simu kuwa na Apps za muhimu tu ilhali kuna maelfu kwa maelfu ya Apps kwenye "soko" la vidude hivyo (Market).

29 Jul 2010

TANZANIA imetajwa katika ripoti ya Kipimo cha Hali ya Rushwa Afrika Mashariki (EABI), kuwa na taasisi zinazoongoza kwa rushwa kwa nchi za Afrika Mashariki.

Akizungumza na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Mratibu wa sekretarieti ya Jukwaa la Wazi (TRAFO), Kaiza Buberwa, alisema kuwa utafiti huo ulifanywa kwa kushirikisha sampuli 10,469 na watu 3,231 walihojiwa kwa Tanzania.

Alisema kuwa katika utafiti huo uliofanyika chini ya wataalamu wa nchi husika, ulifanyika Febrauari na Machi ambapo nchi za Kenya, Burundi, Tanzania, Rwanda na Uganda zilihusishwa.


. Buberwa alisema taasisi zinazoongoza kwa rushwa katika Afrika Mashariki ni Jeshi la Polisi, Mahakama, Jeshi la Ulinzi na Kujenga Taifa, Wakala ya Usajili wa Vifo na Vizazi (RITA), Magereza, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi katika kutoa huduma kwa wananchi, sambamba na ajira.


Alisema kuongoza kwa taasisi hizo ni kutokana na sampuli hiyo ya watu hao, ambao walizitaja taasisi zilizokithiri kwa rushwa wakati wa kupata huduma za kijamii.

Buberwa alisema kwa kuongoza kwa rushwa katika idara nyeti za serikali kwa Afrika Mashariki, Jeshi la Polisi limechukua nafasi ya tano kwa asilimia 65.1 na Mahakama kuwa nafasi ya 10 kwa asilimia 56.4 katika utoaji wa huduma katika misingi ya rushwa.

Aidha, alisema kuwa katika ripoti hiyo haisemi Tanzania hakuna rushwa wala rushwa kidogo, ripoti inasema kwamba ni kwa kuzingatia idadi ya matukio ya vitendo vya rushwa katika idara kadhaa za umma wakati wa kutoa huduma kwa wananchi ikilinganishwa na nchi za Burundi, Kenya, Uganda na Rwanda.

Buberwa alisema kuwa baadhi ya Watanzania asilimia 85.8 wanaamini kuwa hali ya rushwa Tanzania ni mbaya, wakati asilimia 40.6 wanaamini serikali hatimizi wajibu wake katika kuondoa rushwa na kuimarisha utawala bora.

Alisema taasisi nyingine zinazofuata katika rushwa kwa utoaji wa huduma kwa jamii ni Jeshi la Ulinzi na Kujenga Taifa (JKT) asilimia 74.2, Wakala ya Usajili wa Vifo na Vizazi (RITA), asilimia 66.2, Magereza asilimia 61.9, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) asilimia 46.8, Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi asilimia 47.9.

CHANZO: Tanzania Daima

.

Ni dhahiri kwamba kila Mtanzania mzalendo na mwenye uchungu na nchi yetu anatamani kuona mambo yakibadilika huko nyumbani.Nchi yetu ina takriban miaka 50 tangu ipate uhuru mwaka 1961.Ukiondoa uvamizi wa nduli Idi Amin mwaka 1978-79,nchi yetu imeendelea kuwa na sifa ya kipekee ya amani na utulivu huku tukishuhudia "nyumba za majirani zetu zikiteketea".Chama tawala CCM kimekuwa kikijigamba kuwa amani na utulivu huo ni matokeo ya sera zake nzuri na uongozi uliotukuka.Haihitaji kuwa mwanafunzi wa siasa kama mie kufahamu kuwa amani na utulivu tulionao unasababishwa na uvumilivu wa Watanzania.Na ni uvumilivu huo huo unaowafanya CCM watuone wajinga,watupelekeshe watakavyo na waifilisi nchi yetu huku tukifahamu fika namna ya kuwadhibiti.Imetosha.Uvumilivu una mwisho,na mwisho huo ni sasa.

Na hata hilo suala la amani na utulivu lina utata kinamna flani.Wachambuzi wa siasa wanabainisha kuwa kutokuwa na machafuko au vita si viashiria kamili vya amani na utulivu.Hebu jiulize msomaji mpendwa,wazee wetu wastaafu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wana amani gani wakati fedha zao ziliibiwa na wajanja (mafisadi)  katika serikali ya CCM?Je wakulima wanaokopwa na vyama vya ushirika kila unapojiri msimu wa mavuno wana amani gani wakati wanashuhudia namna mavuno yao yanavyorutubisha vitambi vya mafisadi wa vyama vya ushirika?Mabaamedi wana amani gani katika mishahara ya kijungujiko wanayopewa (na inayokatwa kila siku kila glasi au chupa inapovunjika)?Watoto zetu au wadogo zetu wana amani gani wanaposoma kwenye shule zisizo na madawati huku walimu wao wakinyong'onyea kutokana na mazingira duni ya kazi?Na je watumishi wa umma wana amani gani ilhali wanapodai haki zao wanaishia kudharauliwa kuwa kura zao hazihitajiki (as if mishahara yao ni fadhila kwa kumchagua kiongozi)?

Na madereva wa daladala na mabasi ya mikoani wana amani gani ilhali askari wa usalama barabarani wanawakamua kila siku kana kwamba rushwa ni sehemu ya sheria za usalama barabarani?Na huko magerezani kuna Watanzania wangapi wasio na amani kwa vifungo vya kubambikizwa kesi,kushindwa kutoa rushwa kwa polisi au hakimu au uonevu pasipo sababu?Na dada na mabinti zetu wenye sifa stahili za kupata ajira wana amani gani ilhali kila wanapofanya maombi ya kazi wanakumbana na masharti ya "ngono kwanza,kisha ajira"?Na wagonjwa wetu wana amani gani wanapolazwa sakafuni katika wodi za hospitali mbalimbali (na hii ilimtoa machozi Supamodo Naomi Campbell)?

Mtanzania ana amani gani wakati kila siku anashuhudia namna nchi yake inavyozidi kuhujumiwa na mafisadi?Wanaoamini katika utawala wa sheria wana amani gani wanaposhuhudia mtu kama Lowassa anapewa air time kwenye televisheni ya taifa inayoendeshwa kwa fedha za walipa kodi (na mahijiano hayo hayafanyikii gerezani)?Yani fedha za walipa kodi zinatumika kusafisha watuhumiwa wa ufisadi!

Na walalahoi wana amani gani wanaposhuhudia serikali waliyoiweka madarakani,na iliyoahidi maisha bora kwa kila Mtanzania,ikielekeza nguvu kubwa katika kukumbatia mafisadi huku viongozi wa serikali hiyo wakiishi maisha ya kifahari kana kwamba Tanzania ni nchi ya "dunia ya kwanza"?Na wasafiri wanaotegemea huduma za Reli ya Kati au Tazara wana amani gani wakati usafiri wao unategemea kudra za Mwenyezi Mungu ?

Yapo mengi ya kueleza kuhusu namna CCM inavyofanya kila jitihada ya kubomoa hata kile kidogo kilichobaki kwenye "amani na utulivu".Ni dhahiri kuwa chama hiki kimevimbiwa madarakana na hakijali kuona Tanzania ikielekea kwenye korongo lenye kina kirefu.CCM inaweza kufanya kila hila ili ibaki madarakani kama ilivyowazuga Waislamu mwaka 2005 kuwa ingewapatia Mahakama ya Kadhi,lakini baada ya ushindi wa "kishindo" kwenye uchaguzi mkuu uliopita suala hilo limeendelea kuwa ngonjera tu huku akina Msekwa wakisema hili,Pinda akisema lile na Chikawe akiongea vile.Huku ni kuchochea vurugu.

Tanzania haiwezi kupiga hatua katika mfumo wa sasa wa kifisadi ambapo madaraka yanatolewa kwa minajili ya ushkaji huku watawala wakijiona miungu watu wenye uwezo wa kufanya watakayo hata kama yanapelekea kuhatarisha "amani na utulivu" wetu.

It's high time to say enough is enough.Na namna pekee ya kuwaadhibu CCM ni kuwanyima kura katika uchaguzi mkuu ujao.Binafsi,nina imani kubwa na Dokta Wilbroad Slaa,mgombea urais kwa tiketi ya Chadema.Ameonyesha ukomavu wa hali ya juu katika kutetea hali zetu na kupambana kwa dhati dhidi ya ufisadi.Nafasi adimu kama hizi huwa hazijirudii.Tukifanya kosa la kuiacha CCM madarakani hapo Oktoba tutaishia kujilaumu.Nia tunayo,sababu tunazo (tena elfu kidogo) na uwezo tunao (siku ya kupiga kura).Mnaopewa rushwa ili muichague CCM pokeeni kwa vile rushwa hiyo ni fedha mlizoibiwa.Wato rushwa hao hawana uwezo wa kushinikiza muwapigie kura hasa ikizingatiwa kuwa hamkuwaomba wawahonge na wanachowanhonga is in fact fedha zenu wanazowaibia kwa ufisadi.

Inawezekana ukitimiza wajibu wako

27 Jul 2010


Mtunzi wa kitabu hiki maridhawa si mwingine bali ni mchambuzi na mwandishi mahiri wa makala,Mwalimu Nkwazi Nkuzi Mhango,Mtanzania mwenye makazi yake nchini Kanada.Licha ya ualimu na uandishi wa habari,Mhango pia ni mwanaharakati wa haki za binadamu.Miongoni mwa safu maarufu za Mwalimu Nkwazi (pichani chini) ni zile zinazopatikana katika gazeti la Tanzania Daima,ambapo hutumia jina la MPAYUKAJI MSEMAOVYO.Kadhalika,mwandishi huyu ni hodari katika fani ya kublogu,na "uwanja wake" unafahamika kama Free Thinking Unabii .Vilevile,unaweza kusoma makala za Mwalimu Nkwazi katika jarida la The African Executive
Usikose nakala ya kitabu hiki ambacho kinakuja wakati mwafaka kabisa kwa Watanzania waliochoshwa kuona nchi yao ikigeuzwa "shamba la bibi" na mafisadi wanaopita huku na huko "kuomba ridhaa yetu" warejee madarakani kutufisadi zaidi.

26 Jul 2010

Pichani juu  kitabu cha cha sanaa cha comic kinachoitwa TOM & JENNY IN TANZANIA  ambacho kilikuwa kinasubiriwa kwa muda mrefu, na sasa kitabu kimetoka.Unaweza kukipata jijini Dar es salaam na vilevile wachapishaji wanaweza kuwatumia wasomaji walio nje ya Dar es salaam na Tanzania kwa ujumla.
----------------------------------------------------------------------
Joe
Baseline Africa

Alma
Alma akiwa na playwriter Greg Freeman
Alma na cast nzima ya BEAK STREET
Alma Eno, Natasha Whites na Alice Transfield
Msanii wa maigizo na filamu mwenye asili ya kitanzania Alma Eno, ameng'ara na kutikisa ulimwengu wa Theatre mjini London kwenye onyesho la mchezo uitwao BEAK STREET ulioandikwa na mwandishi maarufu Greg Freeman, na kuongozwa na Ken McClymont.

BEAK STREET ni mchezo wa kijangili ulio kwenye ulimwengu wa Mapaka. Mchezo huo umekuwa ukionyeshwa kwenye kitongoji cha West End mjini London, ambacho ni maarufu kwa majumba ya maigizo,sinema na starehe. Beak Street imeonyeshwa kwa wiki 24 sasa katika majumba ya Tabard Theatre na Theatre Delicatessen (Sekunde 30 kutoka Selfridges)

Alma Eno anacheza silka mbili kwenye igizo hili; kwanza anacheza paka teja ambaye anaweza kuuza mtu yeyote kwa maziwa ya unga.

Vilevile anacheza silka ya Chorus ambayo anakuwa nafsi ya jangili Beak. Onyesho lake limesifiwa sana na wahakiki na sasa amefanikiwa

kuingia mkataba wa kuigiza kwenye mchezo mpya wa Zip Postcode Wars ambao unaendeshwa na gwiji Ray Shell.

Alma ambaye ni mwigizaji wa kulipwa, alipata shahada yake ya sanaa na maigizo kutoka chuo maarufu cha Mountview Academy of Theatre and Art. Chuo hiki kina sifkia kwa kutoa waigizaji maarufu wa kimataifa kama Amanda Holden,Nick Moran, Ayub Khan Din mwandishi wa mchezo na sinema ya East is East and director Edward Hall. Da Eno pia ameshawahi kucheza kwenye kipindi cha televisheni ITV hapa Uingereza kiitwacho Collision. Vilevile yuko kwenye filamu ya British Art iitwayo Boggie Woogie.

Maneno ya Critics chini

Freeman and Ken have once again dipped into the absurd with their new production Beak Street - a dark comedy of noir shadows, mean streets and gangster cats, where only one thing is really certain:cats , they aint known for their loyalty

"A testament to freeman's faith in his imagination and ours"-Time Out Critics' Choice ****

"This is a fine and powerful play that pulls no punches"-Chiswick Times

"Iron-rod narrative and polished script.. imaginative staging.. all makes Beak Street excellent value for money"-Extraextra.com
------------------------------------------------------------------------
Baraka

URBAN PULSE

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.