Picha zote hapo juu ni za mtu mmoja.Alipanda ndege huko Hong Kong akiwa "kibabu" na kuteremka Kanada akiwa kijana.Actually,huyu ni kijana halisi lakini alijivika kinyago na kuonekana kikongwe,lengo lake likiwa kuingia nchini Kanada kuomba ukimbizi.
6 Nov 2010
4 Nov 2010
4.11.10
Evarist Chahali
APPLE, iPHONE4
No comments
Scores of iPhone users were late to work on Monday, after a bug in the software meant the device's alarm clock feature failed to adjust to Daylight Saving Time. Skip related content
Hundreds of angry comments were posted on the social networking website Twitter about the glitch on the Apple device, which occured even though the rest of the phone's features updated the time automatically.
"Well done Apple - you've made me decide I need to use a proper alarm clock rather than relying on my iPhone," one user tweeted.
"Stupid iPhone alarm clock went off an hour late. What a great start to the week," said another.
Australian iPhone users experienced similar problems three weeks ago, although alarms went off an hour early there rather than an hour late.
Apple said at the time that a software patch was being developed to resolve the issue. The technology giant has not yet issued an official response to the British version of the glitch.
The popular gadget has suffered a turbulent year. The latest iPhone 4 model has been blighted by problems with its antennae, proximity sensor and security system.
The latest fault can apparently be avoided by using one-off alarms instead of pre-set daily wake-up calls.
4.11.10
Evarist Chahali
DIAMOND, URBAN PULSE
No comments
Baada ya kutua na kutulia ndani ya UK Diamond alifanikiwa kufanya promo pamoja na kuongea na fans wake
asante
Urban Pulse creative
asante
Urban Pulse creative
3 Nov 2010
MGOMBEA urais kupitia tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo, (Chadema), Dk Willibrod Slaa amesema, atayakataa matokeo ya urais yatakayotangazwa na Tume ya Uchaguzi (NEC) kwa kuwa kumefanyika wizi mkubwa wa kura.Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Dk Slaa alisema, kama NEC inaitakia mema nchi hii, ifute matokeo yote ya urais na uchaguzi urudiwe upya.
Dk Slaa ambaye pia ni Katibu Mkuu wa chama hicho, alisema wamekuwa wakifuatilia matokeo ya nchi nzima kwa umakini mkubwa na wamegundua kuna wizi mkubwa wa kura kwenye nafasi za urais na ubunge.
"Kuna uchakachuaji mkubwa wa kura na kazi hiyo inafanywa na usalama wa taifa,"alisema Dk Slaa
Chanzo: Mwananchi
ENDELEA KUFUAtILIA BLOGUNI HAPA
3.11.10
Evarist Chahali
DIAMOND, URBAN PULSE
No comments
Habari za kuthibitisha kutoka Urban Pulse zinathibitisha kuwa Msanii Diamond tayari katua Ndani ya UK tayari kwa ajili ya kukamua show ya Urban Tour kwa ajili ya kuchangia kupigana vita dhidi ya Malaria. Show yake ya kwanza itafanyika katika Mji wa Milton keynes Jumamosi hii tarehe 6.11.10 ndani Ya Club OPUSPRICE
Price £10.00 BEFORE MIDNIGHT MORE AFTER
VIP £20.00
WOTE MWAKARIBISHWA,
URBAN PULSE CREATIVE MEDIA
30 Oct 2010
30.10.10
Evarist Chahali
DOKTA WILBROAD SLAA
3 comments
Ndugu Watanzania wenzangu wote kwa ujumla mtakaosoma ujumbe huu, Salaam toka Mbeya Vijijini, ndio tumeanza mikutano midogo ya kufunga kazi asubuhi hii na tutahitimisha baadaye.
Ninashukuru sana kwa maneno ya heri kwa siku yangu ya kuzaliwa hapo jana na ningekuwa sina shukrani kama ningeacha ipite bila kusema asante kwa maneno mema mliyonipatia humu na kwenye facebook na hata waliopata nafasi kwa njia ya simu. Ninawashukuru vile vile kwa mashauri mbalimbali, na pia kwa sala na dua zenu.
Ninashukuru sana na ninaona fahari kuwa ni mwanachama mwenzenu.
Kampeni zote zinaisha leo na kesho ni siku ya Uchaguzi Mkuu kama mnavyofahamu. Kwa upande wangu nimetembelea karibu maeneo yote ya nchi yetu kubwa, nimekutana na watu mbalimbali na nimeona mengi. Nimeona mengi yenye kutia matumaini na faraja na nimena mengine ya kuhuzunisha na kukatisha tamaa. Yote kwa ujumla yake yamenipa picha ya kuelewa zaidi Taifa letu hasa kuhusu mafanikio tuliyoyapata mpaka hivi sasa na changamoto tulizonazo.
Ninaelewa vizuri zaidi sasa kupitia mang’amuzi binafsi hali ya Taifa letu ilivyo na ya kwamba ni lazima tubadili mwendo na huko tunakokwenda maana tutafika mahali ambapo tutashindwa hata kujiuliza tulifikaje. Watu makini hawawezi kuendelea na njia ambayo wanajua wamepotea. Kuendelea kung’ang’ania kwenda wakati mnajua mmeshapotea ni kutukuza kiburi cha kujiona. Taifa letu limepotea njia na hata kama tukijitahidi kwa nyimbo na masimulizi mbalimbali kuhalalisha huko tunakokwenda bado tutakuwa tumepotea.
Ni kwa sababu hiyo nilipoombwa kugombea Urais nilitambua uzito wa mzigo huu mkubwa kwani utahusiana moja kwa moja na kubadilisha mwelekeo wa taifa letu na kuanza kutengeneza pale palihorabiwa, kuinua kilichoanguka na kumwagilia kilichoanza kunyauka. Hili linahitaji mawazo mapya, uthubutu wa kiuongozi na mtazamo mpya wa nini Taifa letu linahitaji. Ndugu zangu, Taifa letu linahitaji mabadiliko makubwa ili tuweze kujipa sisi wenyewe na watoto wetu nafasi ya kuweza kufanikiwa huko mbeleni.
Mabadiliko haya siyo mabadiliko ya mapambo yaani kuhamimisha maua na vitambaa sebuleni wakati nyumba inanuka na nichafu. Wote mliosikiliza au kumwangalia mgombea mwenzangu jana ni wazi hana ahadi ya mabadiliko yoyote makubwa isipokuwa mwendelezo wa yale yale yaliyotufikisha hapa. Ni kutokana na hilo natambua kuwa kura ya kesho siyo kura ya kawaida; siyo kura kama ya 2005 au ya miaka kabla yake.
Kura ya kesho ni kura ya kuchagua kuendelea na vile tulivyo kwa miaka mitano ijayo au kubadilika ili tuanze upya kwa njia sahihi na kwenda ambako sote tunakujua tunataka kwenda. Ninaamini tunachohitaji ni mabadiliko yatakayoanzisha mwamko wa kuanza kulijenga upya taifa letu. Hili ndilo lililonifanya nikubali pale Chama changu kiliponiomba ninyanyue bendera ya Chadema kwenye uchaguzi huu katika nafasi ya Urais.
Naweza kuwaahidi mengi na kwa maneno matamu ya kila aina. Hata hivyo ninawaahidi kitu kimoja kwa uhakika wa asilimia 100. Mkinichagua kuwa Rais wenu na mkiwashawishi ndugu, jamaa na marafiki zenu kufanya hivyo nami nikachaguliwa, nitawapatia uongozi ambao utaifanya miaka 49 iliyopita kuwa ni ya masimulizi ya njozi za jinamizi kwani nitaongoza timu ya watu ambao watakuwa wamejitokea muda, elimu, ujuzi na vipya vyao katika kujenga taifa letu upya. Katika miaka mitano ijayo tutafanya mambo ambayo CCM na utawala wake imeshindwa kufanya kwa karibu miaka hamsini.
Tutawapa nafasi Watanzania hatimaye nao wafurahia matunda ya uhuru wao na vile vile kuweza kuanza kujenga Taifa la kisasa ambalo litakuwa ni tamanio nakinara cha mabadiliko ya kiutawala, kiuchumi na kiutendaji katika Bara letu. Tuna uwezo, tuna sababu na tuko tayari kuwatumikia.
Naomba sana kura zenu hapo kesho ili niwe Rais wenu katika awamu ya tano. Kura yako ina nguvu ya kubadilisha mwelekeo wa taifa letu. Usiuze, usiache kuitumia na pale utakapoitumia itumie kwangu, kwa wagombea Ubunge Chadema na wagombea wetu wa Udiwani ili tuweze kuhakikisha yote tuliyowaahidi tutayatimiza na zaidi.
Msiwe na shaka, hata toka Ikulu nitaendelea kuwa mwanachama mwaminifu wa mitandao hii na kuwapa taarifa mbalimbali moja kwa moja na kujibu maswali mtakayokuwa nayo kuhusu serikali yenu pale inaponipasa mimi kutolea kauli. Asanteni!!
Mungu Ibariki Tanzania Mungu Ibariki Afrika.
DR W P SLAA - MGOMBEA WA URAISI CHADEMA
26 Oct 2010
26.10.10
Evarist Chahali
UCHAKACHUAJI
4 comments
Nimetumiwa barua pepe yenye habari ifuatayo nami naiwasilisha kama ilivyo
Taarifa kutoka Tunduma, mpakani mwa Tanzania na Zambia mkoani Mbeya zinasema kuwa lori la kampuni ya Azam linalomilikiwa na mfanyabiasha maarufu Bakhresa leo hii tarehe 18 Oktoba, 2010, limekamatwa likiwa na shehena kubwa la karatasi za kupigia kura zitakazotumika uchaguzi mkuu Oktoba 31.
Maafisa wa TRA tunduma walishtuka baada ya kukuta karatasi hizo za kupigia kura zimefichwa kwenye shehena ya vipodozi. Inasemekana kuwa mzigo huo wa karatasi za kupiga kura ulitokea Afrika Kusini na ulipakiwa kwenye gari la Azam kutoka kwenye gari lililotoka na mzigo kutoka Afrika Kusini.
Taarifa zinasema kuwa lori hilo linashikiliwa na TRA na mzigo huo umekuwa sealed. Kuna hofu kuwa vigogo wenye njama za kuiba kura wanaweza kujaribu kufuta ushahidi kuhusu kukamatwa kwa karatasi hizi za kupiga kura.
Kwa mujibu wa taarifa hizo, karatasi hizo za kupiga kura tayari zimewekewa tiki kumchagua Jakaya Kikwete wa CCM na lengo ni kuwa zisambazwe kwenye vituo mbalimbali vya kupigia kura nchini na zihesabiwe kama kura halali.
Tafadhali mwenye taarifa zaidi kutoka mpakani Tunduma atupatie ukweli wa jambo hili
" ........ Wadau huu ni ukweli mtupu magari mawili ya A.A.Bahresa (named Azam on board)T 501AEM na T 263 AJN yako hapa kituo kikuu cha polisi mkoa Mbeya,binafsi nimeona hizo karatasi za kura ambazo JK kapigiwa kura ya ndio na ziko kama karatasi milioni tano kwa haraka haraka hope police watatoa taarifa kamili,wametutoa nje sijui wanazichakachua "
![]() |
| Add caption |
![]() |
25 Oct 2010
Siku moja nilikuwa na mazungumzo na babu mmoja wa Kiskotish.Kwa vile ilikuwa ni safari ya masaa kadhaa kwenye treni kutoka mji mkuu wa Uingereza,London kuelekea mji wa kaskazini mashariki mwa Scotland,Aberdeen,tulipata wasaa wa kuongea mengi.Babu huyo ameshawahi kukaa Tanzania,na anajua maneno mawili matatu ya Kiswahili.Swali moja aliloniuliza,na ambalo limeendelea kuumiza kichwa changu hadi leo ni kwanini Tanzania ni masikini licha ya utajiri mwingi ilionao na watu wakarimu,wapenda amani na wenye kiu ya maendeleo.Sio siri,nilijiumauma kutoa jibu la kueleweka.
Uzuri kuhusu hawa wenzetu ni kwamba hawajui kumwonea mtu aibu.Babu huyo alinieleza waziwazi kuwa nimeshindwa kumpa jibu la kuridhisha sio kwa vile sifahamu kwanini Tanzania ni masikini bali nimeona aibu tu ya kutoa jibu sahihi.Na huo ni ukweli.Nilijua nikimwambia kwamba tatizo kubwa kwa maendeleo ya Tanzania ni uongozi,angeweza kuniuliza "kwani viongozi hao ni wakoloni au Watanzania wenzenu?"
Katika maongezi yetu babu huyo alinipa fundisho moja muhimu ambalo nadhani sote tunapaswa kulitilia maanani.Alinieleza kuwa zamani hizo wakati Uingereza inajengwa,Waingereza hawakuwa wanafikiria kuhusu mahitaji yao tu bali pia mahitaji ya vizazi vijavyo.Alifafanua kuwa kadri anavyoelewa,Waingereza wengi wanajibidiisha sio tu kwa ajili ya leo bali hata miaka 200 ijayo.Akanipa mfano wa namna walivyojenga treni za chini ya ardhi,hospitali zao kuubwa kama kijiji kizima,vyuo vilivyotapakaa sehemu kubwa za miji na maendeleo mengineyo.
Akatanabaisha kuwa wengi wa walioshiriki katika ujenzi huo wa Uingereza ya leo kwa sasa ni marehemu.Na akanikumbusha kuwa japo wakati wanajituma kujenga nchi yao walikuwa wanafahamun kuwa watafaidi matunda ya jitihada zao kwa muda mfupi tu kabla Mungu hajawachukua lakini hiyo haikuwakatisha tamaa kwa vile walifahamu kuwa vizazi vijavyo vingetaraji waliowatangulia wangetumia nafasi zilizokuwepo muda huo kuwaandalia mazingira mazuri ya kuishi.
Nifupishe stori.Jumapili ijayo tuna Uchaguzi Mkuu ambao binafsi nauona kama tukio muhimu kabisa kwa historia ya nchi yetu.Takriban miaka 50 baada ya uhuru kuna wenzetu wengi tu ambao wanaishi katika mazingira mabovu kuliko kabla ya ujio wa mkoloni.Lakini pia,kuna wachache ambao angalau wanamudu mahitaji ya msingi ya kila siku.Ni kundi hili ambalo ningependa kuelekeza rai yangu kwao.
Hebu tutafakari stori za huyo babu niliyekutana nae kwenye treni.Laiti kizazi chao kingeridhika na hali waliyokuwa nayo wakati huo basi huenda Uingereza ya leo isingekuwa imepiga hatua kama ilivyo sasa.Laiti wangekuwa wabinafsi wa kufikiria maslahi yao tu wasingejihangaisha na mipango ya maendeleo ambayo matunda yake yangeonekana baada ya vifo vyao.Lakini kwa vile waliweka mbele maslahi ya jamii badala ya maslahi binafsi,hawakusita kujenga msingi wa jamii ya Uingereza kwa wakati huo na karne kadhaa baadaye.
Tunaweza kuendelea kuwalaumu wakoloni kwa kukwaza maendeleo yetu.Lakini wakoloni walishaondoka takriban miaka 50 iliyopita.Sasa badala ya kupiga hatua,kuna nyakati tunajikuta tunarudi nyuma zaidi ya wakati wakoloni wanaondoka.
Na japo siwatetei wakoloni,lakini angalau wao walikuwa na excuse.Hawakuwa Watanzania wenzetu.Hawakuwa na uchungu na nchi yetu wala vizazi vijavyo.Vipi kuhusu viongozi wetu wa sasa?Hivi sio hawa waliosomeshwa bure buleshi lakini leo wanakataa katakata kuwa elimu ya bure haiwezekani?Kama iliwezekana wakati huo ambapo hatukuwa na maendeleo ya kutosha,kwanini ishindikane wakati huu ambapo tumeweza kugundua vyanzo mbalimbali vya mapato?
Tukiridhika na mishahara inayotuwezesha kwenda Twanga Pepeta kial wikiendi,au vikao vya bia kila jioni kisha tukasahau kuwa kuna wenzetu (na wengi wao ni ndugu zetu kabisa) huko vijijini hawana uhakika wa kifungua kinywa,wamesahau ladha ya chumvi kwenye mlo kwa vile chumvi imegeuka anasa japo iko kibwena huko Uvinza,sukari imegeuka muujiza hata huko Kilombero ambako wana kiwanda cha sukari na miwa inayozalisha sukari inaozeana mashambani.Kuna wenzetu ambao wali nyama au ugali nyama ni milo inayowezekana kwenye sherehe,misiba au wanapobahatika mara moja kwa mwaka kupelekwa hotelini licha ya maelfu kwa maelfu ya ng'ombe,mbuzi,kondoo na wanyama pori lukuki,sambamba na mchele,mahindi,mihogo,mtama,nk.
Sasa hali hii itaendelea hadi lini?Tunaweza kupuuza shida za wenzetu hawa ambao ni wengi kuliko sie lakini ni dhahiri kuwa ndani kabisa ya nafsi zetu tunateseka tunapokumbuka kuwa punje za wali tunazosafisha kwa minajili ya kuzitupa zinahitajika kwa udi na uvumba katika nyumba moja au nyingine.Hivi kama hawa "wazungu" na ubinafsi wao (hawa familia ni baba,mama na watoto.Habari za shangazi,binamu,mjomba,babu,bibi ni kama kachumbari kwenye mlo: inapendeza lakini sio muhimu). waliweza kuvikumbuka vizazi vijavyo na hivyo kujenga nchi zao hadi kufikia zilipo leo,wakni sie ambao familia ni zaidi ya mume,mke na watoto?
Kuna wenzetu wanaokumbatia mafisadi kwa vile tu wanahofia kuwa mafisadi hao wakiondoka basi nao hawatakuwa na namna ya kumudu maisha yao.Hiyo si kweli kwani hata nyakati za mkoloni kuna waliokuwa wanatumikia wakoloni na kuwakandamiza waafrika wenzao,lakini watu hao waliendelea kuwa hai,huru na kumudu maisha yao...tena kwa njia halali pasipo hofu ya kuonekana wasaliti.
Kura utakayopiga Jumapili ijayo ni zaidi ya kura yako binafsi.Ni kura kwa ajili ya memba wote wa ukoo wako (ambao katika mazingira ya kawaida kuna wengi tu wenye kuhangaika na maisha ya kila siku),rafiki zako wa zamani ambao baada ya kukosa nafasi ya kuendelea na masomo wakajaribu bahati zao kwenye kilimo lakini jitihada zao zinakwazwa na vyama vya ushirika vinavyojua kukopa zaidi kuliko kuuza mazao.Ni pamoja na wale ambao waliamua kufany kazi za wito kama ualimu au uuguzi lakini sasa wanajiuliza kama "wanafanya kazi ya Kanisa" kwani licha ya mshahara kuwa kijungujiko lakini pia hauna uhakika wa kufika katika muda stahili.Kuna wale jamaa zako walioamua kujiari lakini wanaandamwa na polisi na kubambikiwa kesi za bangi,uzururaji,nk kila wanaposhindwa kutoa rushwa kwa askari au mgambo.
Wafikirie hawa wakati unapiga kura.Weka kando mafanikio yako binafsi.
Na kwa wale wanaoteseka kwa vile watawala wamekuwa bize zaidi na kuongeza idadi ya magari yao ya kifahari,kuongeza idadi ya mahekalu yao,kuongeza idadi ya nyumba ndogo zao,na matumizi mengine ya anasa kama hayo,huu ndio wakati wenu wa kulipa kisasi.Kama mlibebwa kwa malori kwenda kwenye mkutano wa Kikwete au mgombea mwingine wa CCM,well,hakuwaomba bali walijipendekeza wenyewe.Hivi hamsangai ukarimu huu wa ghafla umetoka wapi?Hamjiulizi kuwa wakati mnahangaika kupeleka wagonjwa na akina mama wajawazito hospitalini kwa vile hakuna magari ya vimulimuli wao walikuwa wantembelea magari ya thamani huku wakiwatimulia vumbi,lakini ghafla leo wanawabeba kwenye malori mkawasikilize.MSIDANGANYIKE.Mkishawapa kura,hamtawaona tena mpaka mwaka 2015.
Japo nimesema kuwa uchaguzi huu una umuhimu wa kipekee,lakini ni muhimu kukumbuka kuwa tulikuwa na chaguzi kama hizi huko nyuma,na wa karibu zaidi ni wa mwaka 2005.Hivi hamkupata matumaini Kikwete alipoahidi maisha bora kwa kila mmoja wenu.Je mmeshayaona maisha hayo bora?Kama bado,kwanini mnataka kumwamwini tena safari hii japo amekaa madarakani miaka mitano na ameshindwa kutimiza ahadi aliyoweka mwenyewe bila kushikiwa mtutu wa bunduki (hakulazimishwa)?
Na yule mbunge aliyeahidi miujiza lakini akaishia kuongeza kitambi chake na idadi ya watoto kupitia hawara zake,kwanini umpe tena kura?Unataka aendelee kukusanifu?Maana ulifanya makosa mwaka 2005 ukiamini kuwa ahadi zake zilionyesha anakujali.Lakini miaka hii mitano iliyopita inatosha kukuthibitishia kuwa huyo ni tapeli wa kisiasa,na hakuna tapeli anayeaminika.Lakini sio yeye tu bali hata chama chake.
Hesabu umri wako.Halafu jiulize lini ulianza kuisikia CCM.Kumbuka magapi wameahidi katika miaka yote hiyo uliyokuwa unawafahamu.Linganisha maendeleo yako na hao wenye CCM halisi.Kwanini bado unaendelea kukiamini chama hiki?Kama waliahidi 1995 hawakufanya,lakini wakarejea tena kuahidi mwaka 2000,na hawakufanya.Na bila aibu wakarejea tena mwaka 2005,na safari hii wakiahidi kuwa wanajua matatizo yako na ya familia yako.Wakaahidi pia kuwa maisha yako yatakuwa bora kwa vile hilo linawezekana.Na wakaonyesha namna watakavyowezesha maisha bora kwa kila Mtanzania.Je wametimiza?
Lakini pengine wameshindwa kutimiza kwa sababu za kibinadamu.Sasa kwanini badala ya kukuomba msamaha na kueleza kwanini wameshindwa kukuletea maisha bora,wanakufanya mjinga kwa kukuahidi yaleyale waliyoahidi mwaka 2005 na kutoyatekeleza?Kumbuka: ukiwachagua tena hutokuwa na sababu ya kuwalaumu kwani wameshakuthibitishia kwa miaka kadhaa kuwa hawawezi kukusaidia lakini ukaendelea kuwaamini.Sasa,japo inakera kuona unaendela kuwaamini matapeli hawa,ni muhimu kukumbushana pale tunapokosea.Kufanya kosa si kosa bali kurejea kosa.Na umesharejea makosa hayo mara kadhaa.Sasa umefika wakati wa kusema IMETOSHA.
Nimalizie kwa kukumbusha kuwa katika uchaguzi huu tumebahatika kumpata Nyerere wa pili.Huyu ni Dokta Wilbroad Slaa.Kama ambavyo Nyerere alijitoa mhanga kuhakikisha mkoloni anaondoka,Dokta Slaa amethibitisha kuwa ni mzalendo mwadilifu ambaye ameamua kupambana na mafisadi hadi watokomee.Kama aliweza kuwakalia kooni mafisadi alipokuwa mbunge tu,jiulize atakayofanya atapokabidhiwa urais.Wakati akiwa mbunge silaha yake pekee ilikuwa ni maneno,lakini tukimkabidhi dola atakuwa na nyenzo mbalimbali za kuipeleka nchi yetu inapostahili kwenda.
Usihadaishwe na wasiwasi kuhusu wizi wa kura.Kuiba wataiba lakini ili waweze kuiba za kutosha kuwabakiza mafisadi madarakani itategemea zaidi idadi ya kura tutakazompa Dokta Slaa.Ni rahisi kuiba kura chache lakini ni vigumu kuiba maelfu au mamilioni ya kura.Wingi wa kura kwa Dokta Slaa utakuwa silaha muhimu ya kuwatia aibu mafisadi katika kujaribu kuchakachua kura au matokeo ya uchaguzi huo.
INAWEZEKANA.TIMIZA WAJIBU WAKO
23 Oct 2010
23.10.10
Evarist Chahali
USALAMA WA TAIFA
5 comments
Makala yangu katika jarida la Raia Mwema toleo la wiki iliyopita ililenga kuchokoza mjadala kuhusu "mashushushu".Nilijaribu kutengeneza mazingira ya kumwezesha msomaji kuhitimisha iwapo madai ya mgombea urais kwa tiketi ya Chadema,Dokta Wilbroad Slaa,kuwa Serikali ya Rais Jakaya Kikwete imesambaza Maafisa Usalam wa Taifa nchi nzima ili wamsaidie Kikwete kurejea Ikulu (wachakachue kura).Katika toleo la wiki hii la jarida hilo,jamaa mmoja anayejiita Almas Kajia ametoa majibu kwa niaba ya Idara yab Usalama wa Taifa.Nasema "anayejiita" kwa vile ameshindwa japo kuweka barua pepe yake au namba ya simu just in case ningehitaji kumjibu one to one.
Kazi ya mashushushu ni usalama si kuhujumu uchaguzi
Almasi Kajia
Oktoba 20, 2010
RAIA Mwema namba 155 la Oktoba 13-19, 2010 liliandika makala iliyokuwa ikiuliza kama mashushu hutumiwa kuhujumu uchaguzi.
Makala hiyo iliyochapishwa katika safu hii ya Raia Mwema Ughaibuni ya Evarist Chahali anayeishi Uskochi, ilikuwa na kichwa kidogo cha habari “Dk. Slaa aibua madai fikirishi”.
Mashushu ambao mwandishi anaulizia kama wanaweza kutumiwa kuhujumu uchaguzi ni maafisa Usalama wa Taifa wa Tanzania na uchaguzi anaozungumzia ni Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 31, 2010.
Katika makala yake, mwandishi ameanza kwa kujisifu kwamba ana ufahamu wa kutosha juu ya Usalama wa Taifa au intelijensia, ameisomea fani ya Usalama wa Kimataifa na kwamba anaijua vizuri Idara ya Usalama wa Taifa ya Tanzania.
Pamoja na sifa, tambo na majigambo yote haya, mwandishi anasema anachojaribu kuandika hakisemeki au hakizungumziki na anasema kwa kutekeleza kile anachotaka kukifanya lazima tujiulize maswali magumu na pengine ya kuogofya.
Napenda niseme kwamba kuanzia mwanzo kabisa katika kupitia makala yote ya mwandishi huyu hakuna chochote alichoandika ambacho hakizungumziki na hakuna swali lolote gumu wala la kuogofya ambalo amelidhihirisha katika makala yake.
Nilichogundua katika makala yake ni kuwa kama huo si mtindo wake wa kuwavutia wasomaji napenda kuamini kwamba yeye ni mshika bango wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na ameendeleza tu yale yanayofanywa na chama hicho yasiyofurahisha kila mtu, ni mambo yanayorandana na afanyayo Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na mgombea urais kupitia chama hicho, Dk. Willibrod Slaa.
Hata hivyo, ameeleza mambo ya msingi sana katika kuthibitisha kwamba amejifunza fani ya usalama wa kimataifa kwa kusema kwamba uimara wa taifa lolote duniani unategemea uimara wa idara yake ya usalama wa taifa na kulegalega kwa mambo katika nchi yoyote duniani kunaashiria upungufu wa idara hiyo.
Lakini katika hali ambayo sikutarajia, mwandishi anakiri kwamba kwa miaka mingi sasa, Idara ya Usalama wa Taifa ya Tanzania ni miongoni mwa idara bora duniani. Hilo pengine lilitokana na maelezo yake kwamba anaifahamu vya kutosha Idara hiyo.
Wapo waandishi wengine ambao wamekuwa wakiandika habari kama hizo, lakini wakiwa na mitazamo inayotofautiana. Jambo ambalo linanishangaza au pengine linanitia shaka katika makala yake ni kama Idara anayoisifu hivyo imekwishakupoteza sifa hizo na kama ni hivyo je, hiyo ndiyo sababu ya yeye kuanza kuwa na shaka kama Idara hiyo sasa inaweza kutumika kuhujumu matokeo ya uchaguzi?
Amesema idara ya usalama wa taifa duniani kote hufanya kazi kwa siri kubwa kabisa na usiri huo ni sehemu ya utekelezaji wa kazi zake. Anasema usiri ni muhimu kabisa na wa lazima katika ukusanyaji wa taarifa nyeti.
Jambo ambalo wasomaji walitakiwa walijue kutoka kwa mwandishi ni ikiwa usiri wa Idara ya Usalama wa Taifa ndio utakaotumika kuhujumu matokeo ya uchaguzi na kama hilo ndio lengo ni kwa nini Idara hiyo ifanye hivyo, kwa kutumiwa na CCM au kwa utashi wake yenyewe?
Mwandishi amezitaja nchi za Uingereza na Marekani kama mifano kwamba mara chache wakuu wa vyombo vya intelijensia huitwa kutoa ufafanuzi kwa mambo yanayohusu usalama wa Taifa wa nchi hizo.
Kwamba aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Central Intelligence Agency (CIA) ya Marekani, George Tennet aliitwa kueleza juu ya ushahidi kwamba Iraki ilikuwa na mipango ya kutengeneza silaha za maangamizi.
Anasema katika nchi hizo mbali na kuondoa katika orodha baadhi ya mambo ambayo ni siri, mabunge yao yana kamati zinazoshughulikia masuala ya usalama na zinawaita viongozi wa idara hizo kutoa ufafanuzi katika masuala yanayohusu intelijensia pale inapokuwa lazima kufanya hivyo.
Suala hili halifanyiki kwa siri anayoizungumzia mwandishi na kama nia yake ingekuwa ni kulifahamu hilo angemuuliza Dk. Slaa ambaye amekuwa mbunge kwa miaka 15 na anafahamu kwamba ipo Kamati ya Bunge ambayo inafanya kazi kama zile zinazofanywa na mabunge ya Uingereza na Marekani.
Amerejea swali lake kama Idara ya Usalama wa Taifa inaweza kutumiwa na CCM kuhujumu uchaguzi na akaunganisha masuala mengine mawili kwamba; hakuna ofisa usalama atakayefurahi na tuhuma za Slaa zikibainika kama ni uongo na Watanzania watakuwa na hofu kama itabainika kwamba tuhuma hizo ni za kweli.
Swali kwamba Idara ya Usalama wa Taifa ilikuwa wapi wakati ukitokea ujambazi wa EPA na je, Idara hiyo ilikuwa ikifanya nini wakati mikataba ya kifisadi ikitokea. Mwandishi anajihami mapema kwa kusema kwamba maswali haya yatazua uhasama kati yake na idara hiyo.
Labda niseme tu kwamba si maofisa wa Idara ya Usalama tu watakaochukia bali Watanzania hawatafurahi kuona tuhuma hizi za Dk. Slaa ambazo ni za uongo zinazidi kuendelezwa na watu wenye hadhi za kisomi kama mwandishi mwenyewe kwa ahadi ambazo nina hakika hazitatimia.
Wananchi wa kawaida ambao wamekwishakuelewa kwamba Chadema ina tabia ya kuzua mambo na ambao wanaamini kwamba nchi hii ina ulinzi wa kutosha, hawawezi kuingiwa na hofu kwa kutegemea tu propaganda za askari wetu kutoka Uskochi.
Ninachotarajia mimi ni kwamba Idara ya Usalama wa Taifa haitamjibu mwandishi. Nililo na uhakika nalo ni kwamba itanyamaza bila kusema chochote kwa kuwa mwandishi mwenyewe amesema kuwa Idara hiyo inafanya kazi zake kwa siri kubwa kabisa.
Ninahisi kwamba mara zote Idara hii inaacha wajinga wajielimishe wenyewe. Swali kwamba Idara ya Usalama wa Taifa ilikuwa wapi wakati ufisadi wa EPA ukitokea sio la msingi bali jambo la muhimu ambalo Mtanzania wa kawaida anaweza kusema ni kwamba suala la EPA limeshughulikiwa sana na Serikali na baadhi ya wahusika wamefikishwa mahakamani.
Naamini kwamba ufisadi si sera ya Serikali wala ya Chama tawala-CCM- na ni vyema ikubalike kwamba, kwa sasa pengine tofauti na ilivyokuwa huko nyuma, ufisadi ni suala la mtizamo na hulka ya mtu kuliko kuonekana kama mtindo wa maisha wa baadhi ya Watanzania.
Serikali ya Tanzania inazingatia utawala wa sheria na tungejali sana suala la mtu kumiliki vitu kama gari, nyumba nzuri, vitu ambavyo wengine hawana, mtu huyu akaonekana kuwa fisadi, Watanzania wengi wangeishia jela.
Amezungumza mengi ikiwa ni pamoja na ikiwa Msajili wa Vyama vya Siasa ambaye shughuli zake si za siri anaonyesha wazi kuipendelea CCM kwa kuingilia majukumu ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi, hali ikoje katika Idara ya Usalama wa Taifa.
Nilijaribu kuhoji pale mwanzo kama mwandishi alikuwa anahisi nini juu ya usiri aliousifia sana, usiri wa Idara ya Usalama wa Taifa, kama usiri huo ndio utatumika kuhujumu matokeo ya uchaguzi.
Kinachojidhihirisha hapa ni kwamba mwandishi anataka Watanzania waamini kwamba Idara ya Usalama wa Taifa kwa kutumia kigezo cha usiri, inaingilia Tume ya Taifa ya Uchaguzi kama alivyofanya Msajili wa Vyama vya siasa kwa nia ya kuhujumu matokeo ya uchaguzi (kama kweli alifanya hivyo).
Inaonekana anaamini kwamba usiri huu ndiyo utakaotumika kukipatia ushindi CCM kwa kuihujumu Chadema.
Lakini kila mtu anajua kwamba kazi ya Idara hiyo kama chombo cha usalama ni kuhakikisha Usalama wa Taifa ambao ni pamoja na uchaguzi kuendeshwa kwa amani, si kuuhujumu.
Inavyoonekana, mwandishi mara zote anaiangalia Idara ya Usalama wa Taifa kama chombo chenye uamuzi wa mwisho kwa kila kitu na anasema kwamba Idara hiyo inamfahamu mmiliki wa Kagoda, ama kwa njia zisizo rasmi au njia rasmi.
Hivi kama kweli kazi za Idara hiyo ni za siri ni vipi itathubutu kutekeleza au hata kama imetekeleza, ieleze wazi kwamba imefanya hivi na hivi kwa watuhumiwa wa aina yoyote, achilia mbali wa Kagoda.
Binafsi nina shaka juu ya uelewa wake wa usalama wa kimataifa na ufahamu wake juu ya Idara hii ambayo anadai ni moja ya idara bora duniani na inayotenda kazi zake kwa usiri.
Ni utaalamu gani anaozungumzia mwandishi unaoweza kutumika kushinikiza Serikali kwa njia zilizo rasmi na zisizo rasmi. Nimejaribu kudadisi kwa wajuzi wa masuala ya Usalama wa Taifa, nikaambiwa kwamba kazi ya idara hiyo duniani kote ni kutoa ushauri na si kushinikiza kama mwandishi anavyotaka tuamini.
Nilitaka kujua kama ameifahamu Idara hiyo vipi kwa kuhadithiwa au pengine alishawahi kuwa mtumishi kwenye chombo hicho nyeti? Kwa yote mawili nilipata jibu moja kwamba hata kama alihadithiwa au alifanya kwenye Idara hiyo, kulingana na kanuni za usiri ambao ameukiri yeye mwenyewe, hawezi kusimama hadharani na kusema kwamba amekuwa mtumishi wa chombo hicho.
Anasema pia kwamba idara ya usalama wa taifa kote duniani ni kama nusu jeshi (paramilitary) na viongozi wake wanaogopwa kupindukia na uamuzi wao hauhojiwi.
Katika udadisi wangu, niliambiwa mambo mawili kwamba kuogopwa kupindukia kunatokana na usiri wa idara zenyewe na nikaamini kwamba usichokijua ni sawa na usiku wa giza.
Kwamba wanaoiogopa idara ni wasioifahamu na anachotaka kusema mwandishi ni kwamba wasomaji waendelee kuiogopa Idara yao ya Usalama wa Taifa.
Nafikiri hilo si la lazima kwa sababu wananchi wana haki ya kukifahamu chombo ambacho kwanza kinahakikisha kuwa Taifa ni salama na kinatumia kodi za wananchi katika utendaji wake wa kazi wa kila siku. Hakuna sababu ya kukiogopa, ni chombo chao na ambacho kimewekwa kisheria.
Mwandishi ametaka pia wasomaji wake wapime madai fikirishi ya Dk. Slaa ambayo yametolewa kama tuhuma ikiwa hadithi au ni kitu kinachowezekana. Ukiyavulia nguo maji sharti uyakoge na kwa hilo mwandishi haamini kwamba anachosema Dk. Slaa ni hadithi tu, anaamini kwamba ni ukweli ingawa hoja yake imejengwa katika nadharia tu.
Ukisoma kwa makini utagundua kuwa Bwana Almasi Kajia (tukiamini kuwa hilo ndilo jina lake halisi) ameelemea zaidi kwenye kujadili wasifu wangu kama mwandishi badala ya kujibu maswali muhimu niliyotoa katika makala ya mwanzo.Lakini kwa vile sipendi malumbano,naweza kufupisha kwa kuhitimisha kuwa makala yake imeshindwa kuthibitisha kuwa HAIWEZEKANI IDARA YA USALAMA WA TAIFA KUTUMIWA NA SERIKALI YA KIKWETE KUCHAKACHUA KURA.Yah,anaweza kusema madai ya Dokta Slaa ni nadharia kwa vile hata fedha za EPA zilipoibiwa tuliambiwa kuwa huo ni uzushi tu (na wahusika wakatishia kumfikisha Dokta Slaa mahakamani).
Haihitaji taaluma ya usalama japo wa mgambo kutambua kuwa fedha za EPA ziliibiwa wakati taasisi zenye jukumu la kuzuwia zikiwa kazini.Mkataba wa kitapeli wa Richmond ulisainiwa wakati wenye jukumu la kuuzuwia wanakenua meno tu.Same story kuhusu Kiwira,IPTL,Buzwagi,Meremeta,Tangold na skandali nyingine za ufisadi.
Wakati naandaa makala hiyo sikutegemea pongezi kutoka kwa wahusika.Nafahamu kuwa hawapendi kukosolewa sio kwa vile wako sahihi bali wanatambua kuwa aina yoyote ile ya ukosoaji inawafumbua macho kuonyesha udhaifu na mapungufu yao.Na hawataki hilo lijulikane kwa vile linaweza kupelekea Nguvu ya Umma kudai majibu kwa nguvu.
Mafisadi wangependa sana kuona kila Mtanzania akiwa mbumbumbu.Wanasali kwa bidii kusijitokeza wahaini wa kuhoji maswali magumu.Si mmesikia tishio kwa gazeti la Mwananchi kwa vile tu haliandiki kile watawala wamezowea kusikia?Wameleweshwa na sifa kiasi kwamba ukiwakosoa ni sawa na kuwatukana.
Finally,naomba kuthibitisha kuwa nilipoandika kuwa naifahamu taasisi hiyo vizuri nilikuwa na sababu zangu za msingi.Sihitaji kufafanua kwa vile hayo ni mambo binafsi.Lakini they and I know very well kuwa hilo la kuifahamu vyema halina ubishi.Mambo mengine hayawezi kuzungumzwa hadharani.
Nilichofarijika ni kile alichowahi kutamka Rais wa zamani wa Marekani,George W.Bush kwamba "ukisema au kufanya jambo flani,kisha watu waka-react basi ujue ulichoongea kimewagusa" maana laiti ingekuwa upumbavu au uzushi tu,Bwana Almasi asingepoteza muda wake kunijibu.
AJIKUNAYE UJUE KAWASHWA
Subscribe to:
Comments (Atom)













