25 Jun 2011

Kabla ya kuwaletea habari na picha kuhusu ziara ya wabunge kadhaa waliokuja hapa Uingereza kufuatilia malipo ya fedha za rada,ninaomba kuweka bayana mtizamo wangu katika suala hili.Kwanza,naona kilichofanywa na wabunge hao ni mithili ya kuuza ng'ombe kwa ajili ya kesi ya kuku.Nilitamani walioongea na wabunge hao kuwauliza umuhimu wa wao kuwepo Uingereza muda huu ambapo kikao cha Bunge la Bajeti kinaendelea huko Dodoma.Kuna dharura gani kwa wao kuja hapa muda huu badala ya kusubiri kikao hicho cha Bunge kimalizike?Je wanawatendea haki wapiga kura wao?Na nani anawawakilisha wapiga kura wao wakati huu?

Nimesema hii ni sawa na kuuza ng'ombe kwa ajili ya kumudu kesi ya kuku kwa vile kila mbunge aliyekuja analipwa mamilioni ya fedha kama posho za kujikimu.Waheshimiwa hawa wanadai fedha za rada zitatumika kuendeleza elimu ya watoto huko nyumbani.Swali la kwanza,kwanini wasingeokoa fedha zinazotumika kama posho zao kwa muda wote watakapokuwa hapa Uingereza,kisha fedha hizo zikaelekezwa kwenye elimu ya watoto wetu huko nyumbani?Binafsi,nadhani suala hilo lingeweza kabisa kushughulikiwa na ubalozi wetu hapa Uingereza unless watuambie kuwa hawana imani na utendaji kazi na Balozi wetu Peter Kallaghe (ambaye ninamfahamu vizuri kuwa ni mchapa kazi mahiri tangu alipokuwa huko Foreign Affairs na Ikulu--nimefanya nae kazi pasipo kufahamiana,just in case you doubt my assessment of him).

Lakini la muhimu zaidi ni ukweli kwamba historia inatufundisha kwamba fedha za aina hii husihia mifukoni mwa wajanja wachache.Sana sana zitawezesha kumalizika kwa ujenzi wa mahekalu ya vigogo,kama sio kuongeza idadi ya nyumba ndogo zao na misururu ya magari yao ya kifahari.Hivi waheshimiwa hawa wanaweza kutuambia kwanini wanatolea macho hayo mamilioni ya rada ilhali wameshindwa kuhoji kuhusu marejesho ya fedha za EPA?Vipi kuhusu zile fedha za mfuko wa pembejeo?Vipi kuhusu "stimulus package" yetu ya kizushi?

Let's be honest,na nilitegemea sana wanahabari waliotuwakilisha kwenye press conference ya wabunge hao wangeibua hoja hizi,waheshimiwa hawa wamekuja Uingereza kutalii tu.Period!So far,katika habari husika hawatuelezi namna gani ujio wao utawezesha fedha hizo kupatikana,na kutuhakikishia kuwa kweli zitaelekezwa kwenye elimu ya watoto wetu.Remember,kamwe tatizo la viongozi wetu halijawahi kuwa kwenye upungufu wa maneno matamu bali utekelezaji wa ahaid wanazojiwekea wao wenyewe.

Anyway,naomba kuwasilisha habari husika kama nilivyotumiwa na Miss Jestina

Wabunge wanne waliokuja Uingereza kuzungumzia mgogoro wa pesa za kampuni inayouza vifaa vya ulinzi –BAE Systems wamefafanua namna zitakavyotumiwa. Wakiongea katika Ubalozi wetu Uingereza mjini London, Ijumaa mchana, viongozi hao walihimiza wanachofanya ni kufuatilia matokeo ya mahakama ya sheria inayochunguza rushwa (Serious Fraud Office-SFO) maana kadri muda unavyokwenda ndivyo riba inaongezeka.
Wabunge walikutana na House of Lords ambao ni maofisa na viongozi wa ngazi za juu sana wenye usemi mzito katika masuala ya kisisiasa Uingereza.

Mwezi Desemba mwaka jana SFO iliiamuru kampuni ya BAE kulipa faini paundi laki tano na kuipa serikali ya Tanzania paundi 29.5 milioni sawa na shilingi 75.3 bilioni za kitanzania kama pesa za kujisafisha uso. Toka tamko hilo litokee miezi sita iliyopita imezuka migogoro kadhaa.
Upande mmoja BAE system wanataka fedha zisipewe serikali ya Tanzania bali kwa mashirika ya fadhila toka nchi za nje upande mwingine uongozi wa Tanzania unasisitiza serikali inao mfumo imara utakaohakikisha fedha zitawafikia wahusika.

Mgogoro ulianza mwaka 1999 wakati Tanzania ilipotaka kununua vifaa vya kusaidia ulinzi wa viwanja vya ndege toka kampuni ya BAE. Ilidaiwa kuwa mfanya biashara Shailesh Vithlani wa kampuni ya Merlin aliyefanya dili kati ya BAE na Tanzania alipewa asilimia 30 ya pesa ya mauzo kama hongo. Pesa hizo ziliwekwa katika akaunti yake ya benki Uswisi. Wahusika wengine ni aliyekuwa Wakili wa Serikali, Andrew Chenge na Gavana wa benki kuu, Idriss Rashid. Wote hawajashtakiwa na Vithlani anadaiwa kujificha Uswisi, ilhali SFO imetoa tamko afikishwe mahakamani.

Akijibu swali kuhusu kutokuelewana huku, mwenyekiti wa msafara Mbunge Job Ndugai ambaye ni Naibu Spika wa Bunge la Taifa, alisema si vizuri BAE kutuingilia au kutueleza nini cha kufanya na pesa hizo ambazo ni maslahi yetu .
“Sisi tunafahamu mfumo gani utakaohakikisha pesa hizo zinatumika sawasawa, zikienda kwa mashirika ya ufadhili ni kama zimetolewa kwa watu wa nje.”

Mbunge mwingine, John Momose Cheyo ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya Bunge inayohusika na Hesabu za Umma, aliwahakikishia wanahabari kwamba katika miaka kumi toka tukio hilo la 1999 vyombo vya serikali dhidi ya rushwa vimebadilika na kuimarika. “Matumizi halali ya fedha yatakahakikisha pesa zitatumika kujenga elimu,” alisema Mbuge huyo wa Bariadi Mashariki.

Toka SFO ilipoamuru BAE Systems ilipe faini kwa mahakama na fidia kwa Tanzania yametokea pia madai kwamba wapo walioandikia BAE barua pepe kuwa wasiilipe serikali ya Tanzania pesa hizo.
Wabunge wanasisitiza pesa zitaendeleza elimu.

Mbunge Maalum, Angellah Kairuki ambaye ni pia Naibu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Haki na Utawala, alielezea kwamba ingawa pesa hizo zinaonekana nyingi lakini hazitasuluhisha matatizo yote ya elimu nchini, mathalan, kuongeza mishahara ya waalimu.
Alitoa mifano ya ukosefu wa madaftari, vyoo na vitabu vya kusaidia waalimu kufundisha. Mifano hiyo inayolenga shule za msingi na sekondari inatokana na matizo makubwa ya wanafunzi kujisaidia porini na kukosa vifaa muhimu vya elimu.

Mbunge Mussa Zungu wa Ilala, na vile vile Naibu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge inayohusika na Ulinzi, Usalama na Mambo ya Nje, alikumbusha kwamba tatizo halikuanzwa na Watanzania. “Ni suala lililoamuliwa na mahakama ya Uingereza; sisi tuchohitaji ni kuendeleza elimu.”

Habari imeandikiwa na Freddy Macha akishirikiana Jestina George pamoja na
URBAN PULSE CREATIVE

MUNGU IBARIKI AFRIKA, MUNGU IBARIKI TANZANIA

Na kwa kumalizia,tuache kumchosha Mungu kwa kutaka aibariki nchi yetu ilhali sie wenyewe hatujibidiishi kuifanya Tanzania kuwa lulu ya Afrika na pengine dunia kwa ujumla.Au tunamtaka Mungu aibariki nchi yetu ili mambo yakizidi kwenda mrama tumlaumu yeye badala ya kujilaumu kwa uzembe wetu?

Pia naomba kutoa wito kwa wanahabari wenzangu (hoping hamto-mind kukosolewa),let's go beyond the "photo-op" cancer inayowasumbua wengi wa wanahabari wenzetu huko nyumbani.Picha ni muhimu lakini la muhimu zaidi ni kuwabana viongozi wababaishaji kila wanapojipendekeza kuleta porojo zao.Mtakumbukwa kwa kuuwakilisha umma vyema na sio picha.Sorry guys,I think you could have done better than just reporting what they said.You just gave them a free pass na pengine bado hawaamini kama wamesalimika kuulizwa maswali magumu na Watanzania waliopo "dunia ya kwanza".


Mshairi Muyaka Al Ghassany (1776-1840 ) toka Mombasa aliwahi kusema hivi:

Vita vyako Fahamu
Havimdhuru Karimu
Ila wewe Bahaimu
Jujue Utaumia

Katika hali isiyo ya kawaida Jumuiya ya wa Swahili Tanzania imemjia juu Spika Anne Makinda juu ya kauli yake ya kuwakebehi watu wa Kariakoo ambako wengi wao wana asili ya Kiswahili.

Tamko rasmi la Jumuiya ya waswahili limekuja baada ya kauli ya makinda iliyojaa dharau na kebehi kwa wabunge kuwa wasiwe kama watu wa Kariakoo. Klabu ya Saigon nayo imesema itatoa tamko lao rasmi kesho juu ya haya matamshi machafu na ya dharau ya spika Anna Makinda.

Anne Makinda labda alitakiwa kurudi darasani na akapigwe brash kuhusu umuhimu wa Kariakoo na watu waliowahi kuishi kariakoo na Makinda should know better than most kuwa hicho chama kilichomweka kwenye hicho kiti alichokalia kilizaliwa Kariakoo na na kusema ukweli ni kuwa dharau aliyoitoa Anna Makinda kwa kariakoo itakuwa si kwa wafanya bishara ndogo ndogo walipo pale bali ni pamoja na waswahili wengine kama akina Mwinjuma Mwinyikambi, Kiyate Mshume, Jumbe Tambaza, Sheikh Hassan bin Amir and Sheikh Suleiman Takadir ambao walikuwa ni wakaazi wa Kariakoo.

Labda Makinda angeongea na wenzie wakampeleka maeneo ya makuu 4 yaliyoifanya kariakoo :

1.Kariakoo

2.Gerezani

3.Kisutu

4.Mission Quarter.

Spika Anna angejua watu wa Katiakoo wameshiri vipi kwenye kwenye uhuru wa nchi hii asingeweza kuwatukana wabunge kwa dharau kama alivyofanya leo.

Najua Makinda hawezi kumwomba ZUNGU au wabunge wengine wa Dar lakini sitoshangaa kuwa huyu mama akawa hajui hata hiyo TAA ilikuwa na makao makuu wapi na sacrifice zipi mzee Bin Sudi aliziingia kutoa lile jengo mwaka 1930!

Anna kama ulijuwa hujui basi ujue kuwa jengo hili ndio TANU ilizaliwa na mpaka leo lipo pale mtaa wa kariakoo na Mtaa Mpya ulipoungana

Kama ulikuwa hujui basi upande wa Magharibi wa Kariakoondiko ilikokuwa Mission Quarter (NYUMA YA TBL) na eneo hili lilitengwa maalim kwa ajili ya kuwalinda wahamiaji na waswahili waliokuwa wengi kariakoo na ambao waliishhi kwa amani na utulivu kwa miaka zaidi ya 70 mpaka leo hii ambako Pspika wa Bunge unatoa kauli zenye nia ya kuvunja amani na utulivu baina ya watu wa kariakoo

Kwa kuonyesha kuwa Waswahili wa Kariakoo walikuwa hawana kinyongo ndio maana majina ya mitaa imebaki vile vile kama vile mtaa wa Masasi, Likoma, Ndanda, Muhonda, Muheza , Magila na sasa hivi mmetuletea jina la mpuuzi wenu yule (MAKAMBA) na mkampa mtaa jina ili hali hana lolote la maana linalomsabahisha na Kariakoo (when time will come TUTALIONDOA)

Lakini wana JAMII FORUM msimlaumu sana huyu Anna Makinda kwani naye anafuata nyayo za baba yake Mwalimu Nyerere ambaye alianza kupandikiza mbegu mbaya za kudharau not only waswahili lakini wana kariakoo kwa ujumla.

Watu wengine maarudu ambao walikuwa ni wana Kariakoo walikuwa wakazi wa MISSION QUATER ni babu yangu bwana THOMAS PLANTAN ambaye alikuwa ni rais wa African Association na al Marhum mzee JOHN RUPIA ambaye alikuwa ni tajiri mkubwa sana enzi zile.

Anna Makinda kama hujui basi kwa taarifa yako tuu ni kuwa nyumba ya Al Marhum John Rupia ilikuwa mtaa wa Likoma na Magila, nyumba hii mpaka leo ipo na ndiko African Association ilianzishwa mwaka 1929. Nyumba hii mpaka leo ipo japi si katika hali yake ya zamani.

Lakini pia nataka nikujulishe kuwa Mission Quarter ndiko kulikokuwepo kiwanda cha kuchapisha cha mwafrica wa kwanza ambacho kilikuwa cha mzee wangu MASHADO PLANTAN ambaye alikuwa ni mtu wa kusini na alikuwa anachapisha JAMII FORUM ya enzi hizo ilikuwa ikiitwa ZUHURA ambayo Nyerere alikuwa analitumia sana kupiga debe dhidi ya wakoloni!

Lakini yote hayo Makinda kwako unaona ni upuuzi tuu kwani kariakoo pia ina eneo linaitwa GEREZANI ambako ilikuwa ni nyumbani kwa Omari Londo, Ally Sykes, Zuberi Mtemvu, Mashado Plantan, Muhsin Mende and Dossa Aziz. Hawa walikuwa ni majabali na wazalendo waliokutana na Nyerere baadae. Kwa kuonyesha tuu kuwa sisi si wafuata bendera, ZUBERI MTEMVU, MUHSIN MENDE na MASHADO PLANTAN waliamua kujiondoa TANU na kuanzisha chama kingine cha upinzani kwa jina la TANGNYIKA AFRICAN CONGRESS na hapo ndiko zilianza tofauti kubwa na baba yako Nyerere.

Anna makinda unaposema waBunge wasiwe kama watu wa kariakoo unamaana hutaki wawe INDEPENDENT THINKERS kama akina Mzee Mshume Kiyate, Sheikh Hassan bin Ameir, Sheikh Suleiman Takadir, Idd Faizi, Idd Tosiri, Bantu Kasella Bantu, Abdulwahid Sykes and Dossa Aziz?

Kwa kuendelea kukuambia tuu umuhimu wa kariakoo ni kuwa ile open space inayotazamana na viwanja vya Mnazi Mmoja ilikuwa ni plot ya JOHN RUPIA ambayo aliitoa kama zawadi kwa TANU ili wajenge ile centre. Of course kwa sababu ya serikali yako ilivyokuwa haithamini historia na heritage ili nyumba ilivynjwa wamejenga gorofa pale bila kuzingatia au kuweka kumbukumbu yoyote ile, na huyo baba yenu Nyeree mnaye sema kuwa mnahifadhi ujumbe wake historia kaye nyingi iliyokuwa mle ndani iliishia kutupwa bila mazingatio yoyote yale ya kuhifadhi yaliyokuwa mle.

Sehemu nyingine ambayo leo hii umeitukana ni Soko la kariakoo ambalo Nyerere alikuwa haishi kwenda pale....bila kusahau kuwa hata shirika la masoko kariakoo lilikuwa linatoa SCHOLARSHIP kuwasomesha watu mpaka University of Dar.

Leo Hii spika wa Bunge umeamua kuwatukana :

WASHOMVI ambao walikuwa wanafanya baishara ya samaki

WAZARAMO ambao walikuwa wanafanya baishara ya nazi

WANYAMWEZI (wanawake) ambao walikuwa wanafanya baishara ya tumbaku kavu huku wanaume wakifanya biashara ya viazi ziliskukuwa zinalimwa Kigamboni

WALUGURU walikuwa wanafanya biashara za machungwa na mboga za majani

WAARABU walikukuwa wanafanya biashara ya ngano, mabucha ya nyama, na viungo mbali mbali

WAHINDI walikuwa wanashindana sana na WAARABU kwenye biashara mbali mbali

Je Anna Makinda unajua kama Nyerere aliwahi kufanya kazi soko la kariakoo kama Market Master? Je unajua kama ofisi yake ilikuwa kwenye junction ya mtaa wa Tandamti ( siku hizi mnauita mtaa wa Mshume Kiyate) na mtaa wa Swahili?

Matusi uliyowatukana wana Kariakoo leo ni matusi ambayo umewatukana wa Swahili wa Mwembe Togwa (siku hizi mnapaita Fire), Umewatukana wakari wa Ronald Cameroon Road ( sikuhizi United Nations Road) na wengineo wengi...lakini wansiasa wenye calibre za wewe Anna Makinda ndio hao hao mlioamua kuquestion maamuzi ya mzee Kitwana Kondo alipokuwa meya mwaka 1995 alipoa mua kubadili jina la mtaa wa Tandamti na kuita mtaa wa Mshume Kiyate ...tena mlipiga makelele mkisaidiwa na waandishi wa habari ambao hawaijui historia ya kariakoo kwa kuuliza huyu Mshume Kiyate ni nani? Nyie nyie ndio mlilalamika mitaa mingine ya kariakoo ilipobadilishwa na kupewa majina ya Tatu Binti Mzee, Max Mbwana, Omari Londo halafu leo hii unathubutu kututukana sisi wana Kariakoo!

Onyo kwa Anna Makinda na wanasiasa wenye tabia za kudharau watu wa kariakoo kama Cyrill Chami na wengineo, Wana Kariakoo na Waswahili wa zama hizi hatutonyamaza kwani vyombo vya kulalama tunavyo na haki zetu tunazijua na mkiendelea na dharau zenu basi mjue kuwa pamoja kuwa waswahili hatutonyamaza na kama ikiwezekana tujibu mapigo basi tutaangalia namna bora zaidi za kuwajibu lakini hatutokaa kimya...maana leo mmeanza na waswahili na watu wa kariakoo kesho tunajua mtahamia kwa wa chagga na watu wa Moshi kesho kutwa mtahamia kwa nyakyusa na watu wa Mbeya na Iringa

Tofauti ni kuwa sasa tumelimika na tunaouwezo wa kuona mnapoanza kutuletea dharau bila kujali wakazi na watu wa kariakoo nao ni wapiga kura kama watu wa kwenu

Muyaka al Ghassany pia alisema hivi:
Yu wapi Firauni
Yuwapi wapi Karuni
Na Shadadi Maluuni
Wote wameangamia

Anna Makinda leo umeamua kuwatukana wana Kariakoo, historia ya Kariakoo na wanaotafuta rizki zao Kariakoo na Waswahili wanaoishi pale lakini ukae ukijua kuwa kuna leo na kesho na sisi hili hatutosahau. Mshazowea kututukana lakini at some point someone has to stand up and say no hatukubali. Labda umesahau kuwa kwa waswahili wa Kariakoo kuna 2 extremes ambazo naona ushazowea ile moja tuu

CHANZO: Jamii Forums

24 Jun 2011

Kijana,heri kwa siku yako ya kuzaliwa.Nakutakia kila la heri katika maisha yako na usisahau kumtanguliza Mungu katika kila ufanyalo.Salamu kwa Mzee Kispuni (kushoto pichani chini) na dadangu Mama K.

Waziri Mkuu Pinda akimwaga machozi Bungeni mwaka 2009
Kwa kifupi tu,Jaji mtajwa katika habari ifuatayo hastahili kuendelea na wadhifa wake.Hili ndio tatizo la kuteua majaji weeeengi mpaka wababaishaji kama hawa wanapata fursa.Pia habari hii imenikumbusha lile tukio la Waziri Mkuu Mizengo Pinda kulia Bungeni alipobanwa kuhusu kauli yake kuhusu wauaji wa maalbino (aliropoka kuwa wauaji hao nawe wauawe)

Jaji aangua kilio akijitetea
Thursday, 23 June 2011 21:49

Hadija Jumanne
JAJI Atuganile Flora Ngwale wa Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam kitengo cha Ardhi, jana alishindwa kujitetea kuhusu kushindwa kwake kujaza fomu zinazohusu mali na madeni yake, kwa mujibu wa sheria ya maadili ya viongozi wa umma.

Jaji huyo alishindwa kufanya hivyo mbele ya Baraza la Maadili ambako aliangua kilio na hivyo kusababisha wanasheria kushindwa kumhoji.

Hali hiyo ililazimisha baraza kusitisha usikilizaji wa shauri hilo.Wakati akiangua kilio, jaji huyo alilieleza baraza kwamba alishindwa kujaza fomu hizo na kuomba msamaha.Wakati akiangua kilio, jaji huo alisema "sina mali yoyote, kazi ndio maisha yangu, watoto wangu wanategemea kazi hii siwezi kudharau mtu, naomba mnisamehe, nimejifunza Mungu wangu,"alisema jaji huyo.

Jaji Ngwale alisimama katika baraza hilo ili kuanza kujitetea, lakini ghafla aliangua kilio kwa sauti ya juu huku akiomba baraza hilo limuonee huruma kwa kutojaza fomu."Ni kweli sijajaza fomu na kama kuna mtu aliniona nimejaza fomu hizi ajitokeze ndani ya baraza hili la maadili," alisema.

"Kazi hii ndio maisha yangu, kazi hii ndio faraja ya watoto wangu hivyo naitegemea sana sina mali zozote za kunitesa na kuniita katika Baraza la Maadili,"alisema Ngwale huku akimwaga machozi.

Baada ya Barazakuona Jaji Ngwale ameshindwa kujitetea kwa njia ya mdomo, lilimtaka atoe utetezi wake kwa njia ya maandishi na kulazimika kusitisha kuendelea na shauri hilo.Mbali na baraza hilo kusitisha kuendelea kusikiliza shauri hilo, pia wanasheria wa sekretarieti ya maadili na hawakupata nafasi ya kumhoji Jaji Ngwale kutoka na hali hiyo.

Baada ya baraza hilo kusitisha kuendelea kusikiliza shauri hilo walimuomba jaji huyo aondoke mbele ya baraza hilo, lakini jaji huyo alikaidi agizo la wanasheria hao na badala yake aliendelea kulia mpaka baraza hilo lilipomuomba mmoja wa wanasheria ambembeleze na baada ya kubembelezwa alikubali kwenda kutoa maelezo yake kwa njia ya maandishi na baadaye aliruhusiwa kuondoka.

Baraza hilo litaendelea leo kwa ajili ya kuhoji watu wanne ambao hawakujaza fomu hizo za maadili ya umma mwaka jana, miongoni mwa watu hao watakaohojiwa ni pamoja na Diwani wa Kata ya Kanazi Mathias Bisoma Mgatta, Mkurugenzi wa Shirika la Hifadhi ya Jamii la Taifa (NSSF), Crecencius Magori.

Wengine ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Tafiki Mwanza, Francis Bayona Katunzi na Diwani wa Mpanda mjini Ally Juma Nsokolo.

CHANZO: Mwananchi

23 Jun 2011


 
Ndugu, Jamaa, na Marafiki, Watanzania wote;
Kwa masikitiko makubwa tunawataarifu ya kwamba, tumepokea habari za msiba wa mwenzetu EDGAR KILEKE (KAKA DICK). Msiba umetokea leo huko Leicester Uingereza. Marehemu Edgar amefariki baada ya kuugua cancer ya Ini. 

Mipango ya kusafirisha mwili wa marehemu kueleke anyumbani kwa mazishi inafanyika. Tunawaomba wote, kwa moyo wa upendo na utoaji, tusaidiane ili tukamilishe maandalizi haya na mwenzetu ili aweze kwenda kupumzishwa kwenye makao yake ya milele huko nyumbani Tanzania. Tunatanguliza shukurani za dhati kwa michango yenu. Wanaoweza kuwatembelea wafiwa na kutoa pole mnakaribishwa na msiba upo kwenye address hapo chini:

89 Stevenson Drive
LE3 9AD
Leicester

Kwa maelezo ya ziada wasiliana na;
Asaa Ali  07951644936
au

Fauzia Musa 07943962628

Kama hutaweza kufika Leicester, unaweza kutuma mchango wako kwa:
A A KAKOZI
Account Number 85065992
Sort Code: 09-01-27
Bank: Santander


Bwana ametoa na Bwana ametwaa jina lake libarikiwe.


Asanteni.


R.I.P EDGAR!!


Imetumwa na Miss Jestina


Mgao wa Tanesco ukiwa kazini
Sio siri kwamba kinachowapa jeuri mafisadi kuwapalekesha Watanzania ni upole kupita kiasi walionao wanachi.Watu wanalipa kodi-kwenye mishahara kwa walioajiriwa,katika VAT kwenye manunuzi ya bidhaa mbalimbali,na utitiri mwingine wa kodi-lakini faida ya kodi hiyo inaonekana zaidi kwenye ukubwa wa vitambi vya viongozi wetu,thamani ya magari na mahekalu yao,na kuongezeka kwa idadi ya vimada na nyumba ndogo zao.

Sasa Tanesco wamekuja na kali kubwa kwa kutangaza mgao wa umeme usio na kikomo,masaa kumi kwa kila siku ya wiki.Ukienda huko Twitter utasikia "aah Tanesco wamechukua umeme wao".Wengine wanaishia kuitukana Tanesco kwa matusi ya "sehemu za siri za mama yake Tanesco".Hizi zote ni dalili za watu walioishiwa na mbinu zakudai haki zao.Hivi "kumtukana mama yake Tanesco" kutafupisha mgao wa umeme?

Imefika wakati Watanzania watambue kuwa mara nyingi HAKI HAITOLEWI KAMA ZAWADI BALI HUDAIWA...KWA NGUVU IKIBIDI.Hakuna uwezekano wa tatizo la mgao wa umeme kuisha kwa njia za kistaarabu.Utatuzi hauwezi kupatikana kwa vile sekta ya nishati,kama ilivyo ya madini ni kitega uchumi kikubwa kwa mafisadi wetu.Kukatika umeme kunawaingizia baadhi ya majambazi hao mamilioni ya shilingi kila siku.

Nina tatizo kubwa zaidi na Wtanzania wa tabaka la kati.Hawa ndio tunaokutana nao huko Twitter na Facebook...Kiingereza kiiingi huku nchi inateketea.Hawa ndio tunaowaona wakijirusha kwenye kumbi mbalimbali za "starehe".Kuna starehe gani kuwepo kwenye ukumbi unaobadilisha taa kutoka rangi moja kwenda nyingine (kwa kutumia jenereta) kisha kurudi nyumbani na kukumbana na kiza na joto kwa vile "Tanesco wamechukua umeme wao" na feni haiendeshwi kwa mafuta ya taa!

Kwanini nailamu middle class yetu?Ni kwa vile hiki ni kiungo muhimu kati ya tabaka tawala na tabaka la walalahoi.Hawa ndio wenzetu wenye shahada au stashahada katika fani moja au nyingine.Hawa ni watu wenye upeo na wanaweza kuihamasisha jamii kutambua na kudai haki zao.Wengi katika tabaka hili ni walalahoi wanaojaribu kuiga maisha ya wale wa tabaka la juu.

Uchaguzi ni wenu.Kujifanya mmezowea maumivu na mafisadi waendelee "kupeta" au kuweka kando "ubishoo na usistaduu" na kuungana na tabaka la walalahoi kuhamasisha mabadiliko katika nchi yetu.Akina sie tunatekeleza wajibu kwa namna kama inavyofanya makala hii.Sasa ni wajibu wa kila mmoja wetu kutimiza wajibu wake ili kuinusu nchi yetu.

Enewei,hebu soma stori husika hapa chini
Tanesco yatangaza mgawo wa saa 10 kwa siku nchi nzima
Wednesday, 22 June 2011 21:06

Waandishi Wetu
SHIRIKA la Umeme (Tanesco), limetangaza mgawo mkubwa wa umeme usio na kikomo, utakaokuwa kwa saa 10, siku saba kwa wiki nchi nzima.

Maafisa wa shirika hilo na Wizara ya Nishati na Madini wamesema mgawo huo umetokana na upungufu wa maji katika bwawa la Mtera na transfoma zake kuzalisha umeme mdogo kuliko mahitaji.Kwa mujibu wa tangazo la ratiba ya mgao huo lililotolewa na Tanesco jana, mgao huo utakuwa wa kati ya saa sita hadi 10 kwa siku ambapo maeneo yatabadilishana muda wa mgawo.

Hata hivyo, tangazo hilo la Tanesco limekuja wakati maeneo mengi nchini yakiwa na mgawo wa muda mrefu na ambao unachukua muda wa saa zaidi ya zilizotangazwa jana na shirika hilo hali iliyosababisha malalamiko kwa wananchi.

Kwa mujibu wa ratiba hiyo mgawo huo utakuwa wa kila siku kuanzia Jumatatu hadi Jumapili ambapo baadhi ya maeneo yatakosa umeme mchana na mengine yatakosa usiku.Tanesco ilisema katika baadhi ya maeneo umeme utakatika kuanzia saa 2.00 asubuhi hadi saa 12.00 jioni, wakati maeneo mengine yatakosa umeme kuanzia saa 12.00 jioni hadi saa 5.00 usiku.

Akizungumza katika maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma jana, Mhandisi Mkuu wa Tanesco, Juliana Pallangyo alisema mgawo huo unatokana na kupungua kwa kina cha maji katika bwawa la Mtera.

Alisema mahitaji ya umeme ni megawati 850 wakati uzalishaji ni megawati 600 hali inayochangia upungufu wa umeme.

“Mahitaji yaliyopo ni makubwa wakati umeme unaozalishwa ni mdogo, tunashindwa kumudu mahitaji ya watu wote kwa wakati mmoja na ndiyo maana tunakuwa na mgawo,” alisema Pallangyo.Aliongeza kuwa licha ya matatizo hayo shirika hilo lina malengo ya kusambaza umeme vijijini ambako bado hakujafikiwa na umeme.

Katibu adai mgawo utakuwa historia

Akizungumzia kuhusu mgawo huo, Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini, David Jairo alisema mgawo huo unaweza kuwa historia katika miaka miwili ijayo na kwamba hali ya sasa inatokana na upungufu wa maji katika bwawa la Mtera ambalo linaweza kufungwa kwa sababu hiyo.

Katika hatua nyingine, Jairo alisema Serikali ya China itatoa mkopo wa dola za Marekani 778 milioni sawa na Sh1,167,000 bilioni, kwa Serikali ya Tanzania kwa ajili ya kufunga bomba kubwa la kusafirisha gesi kutoka mkoani Mtwara hadi Dar es Salaam, itakayosaidia kuongeza uzalishaji wa umeme nchini.

Alisema hatua hiyo itafanyika endapo Serikali ya Tanzania itafikia makubaliano na Serikali ya China katika mazungumzo baina yao yanayotarajia kuyafanya wiki ijayo.Iwapo mpango huo utafanikiwa kampuni ya China Petrolium Company ndiyo itakayozalisha umeme.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Jairo alisema, kiasi hicho cha fedha ni kulingana na upembuzi yakinifu uliofanywa na kwamba gesi itakayozalishwa itasaidia kupunguza tatizo la umeme na uharibifu wa mazingira nchini.

Alisema bomba linalozalisha gesi kwa sasa kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam ni dogo likiwa na ukubwa inchi 30 hivyo uzalishaji wake pia ni mdogo.“Sisi kama wizara tunajitahidi kuweka mipango ya muda mfupi ya kukabiliana na tatizo la umeme lililopo nchini kwa hiyo Serikali ya China itatupa fedha hizo kama mkopo kwa ajili ya kuzalisha gesi hiyo,”alisema Jairo

CHANZO: Mwananchi

22 Jun 2011


TUNAFURAHI KUWATANGAZIA KUANZISHWA KWA HUDUMA YA BURE YA KUWATAFUTA NDUGU,JAMAA,MARAFIKI NA WATU WOWOTE WALE TULIOPOTEANA NAO KITAMBO.HUDUMA HII INAPATIKANA KATIKA BLOGU YA "TAFUTA PATA" AMBAYO ANUANI YAKE NI

UNACHOTAKIWA KUFANYA NI KUTUPATIA JINA LAKO KAMILI,JINA LA UNAYEMTAFUTA,NA NAMNA ANAVYOWEZA KUWASILANA NAWE (KWA MFANO KWA BARUA-PEPE,SIMU,NK).UNAWEZA KUTUFAHAMISHA KUHUSU TAARIFA ZAKO AMBAZO USINGEPENDA ZICHAPISHWE BLOGUNI (KWA MFANO NAMBA YAKO YA SIMU AU BARUA PEPE).KAMA UTAKUWA NA PICHA YA UNAYEMTAFUTA ITAKUWA VIZURI LAKINI SI LAZIMA.

KARIBUNI SANA TUWEZE KUTAFUTA NA KUWAPATA NDUGU,JAMAA NA MARAFIKI TULIOPOTEZANA NAO.

Tafuta-Pata,Inc


Police in Essex arrest teenage 'mastermind' behind worldwide hacking gang after attacks on CIA
19-year-old man is suspected of leading the notorious Lulz Security hacking group

LulzSec tweeted it did NOT hack into Britain's census information as one website claimed

By Rebecca Camber, Colin Fernandez and Lucy Collins

Last updated at 12:30 AM on 22nd June 2011

A British teenager is suspected of masterminding computer hacking attacks on the CIA, the U.S. Senate and Sony from his bedroom.

Ryan Cleary, 19, was arrested at his family's home in Essex in a dramatic swoop following a joint inquiry by Scotland Yard and the FBI.

He was held hours after the UK's serious crime unit came under online siege from the hacking group known as LulzSec.

Latest victim: Hacker group Lulz Security has brought down the website of the Serious Organised Crime Agency. The FBI and Scotland Yard yesterday arrested a 19-year-old man in Wickford, Essex, on suspicion of being the group's ringleader

Ryan Cleary, 19, who lives in this house in Wickford, Essex, is accused of being a 'major player' within LulzSec

LulzSec wasted no time in claiming responsibility for Monday's Soca attack on its Twitter page

The self-styled 'pirate ninjas' recently declared on Twitter their intention to break into government websites and banks and leak confidential documents.
On Monday the Serious and Organised Crime Agency - dubbed 'Britain's FBI' - was forced to temporarily take its website off-line after hackers bombarded it.

Ryan, a loner whose family says 'lives his life online', faces the prospect of extradition to the U.S where he could face 60 years' behind bars for allegedly hacking into the CIA and Senate websites.
Detectives believe he is a 'major player' with LulzSec, which has been linked to recent attacks on games firm Sony in which details and passwords of millions of users were accessed.

LulzSec has claimed its other victims include the NHS and Nintendo.

Ryan's mother Rita, 44, said her son suffers from agoraphobia and attention deficit disorder and had not left his bedroom for four years.
Earlier this year, the mother of two was fined £100 for allowing her older son to grow cannabis at their home after plants worth £4,300 were seized.

Mrs Cleary, who is on incapacity benefit, claimed her son needed the drugs to ease his epilepsy symptoms.
Speaking at the family's home in Wickford, she said Ryan was an introverted boy who 'lives his life online'.

She added: 'He has a history of mental problems. 'He left school at 15.

'He has stayed in his room for the last four years in front of his computer.

'He is bright, but does not have any social skills.'

The teenager attended Heath School, in Stanway, Colchester, a school for children with special needs, and is said to have constantly spoken in 'computer jargon'.

Police arrived at the house on Monday night and are said to have spent five hours talking to Ryan.

In his bedroom they found two computers with huge screens and an air conditioning unit to regulate the heat they generated.
Apart from a mass of computer data, his bedroom was like that of many teenage boys with photographs of scantily-clad women on the walls.

Ryan's brother Mitchell, 22, said: 'He is not the sort of person to do anything mad.

'He stays in his room - you will be lucky if he opens the blinds. I barely see him. I am more of a football person - he is more of an inside person.’

Another family member, who did not want to be identified, said: ‘He is a recluse and he never leaves the house.’

Neighbours said his father Neil is a musician who had played the tuba at the Royal Albert Hall, worked with names such as Andrew Lloyd Webber and played at a private function for Princess Diana.

Ryan was first 'outed' online as a member of LulzSec in May by members of the rival hacker group Anonymous.

Yesterday neighbours told of their shock at his arrest. One, James Rounce, said he presumed Ryan had been at university as he had not seen him for so long.

He said: ‘You could tell he was very bright just from the way he spoke and presented himself.

‘I knew he was into computers because we would often take in parcels for him and when I asked about them his mother said he was working from home and it was something to do with IT.’

Last night Ryan, who uses the online name ViraL, was being questioned in a police station in central London under the Computer Misuse Act and Fraud Act.

A Scotland Yard spokesman said it was liaising closely with the FBI, adding: 'The arrest follows an investigation into network intrusions against international business and intelligence agencies by what is believed to be the same hacking group.

'Searches at an address in Wickford, Essex, following the arrest last night have led to the examination of a significant amount of material.'

The arrest of a Briton in relation to hacking attempts in the U.S. will prompt comparisons with Gary McKinnon.

McKinnon, 45, who is battling extradition to the U.S., faces 60 years behind bars for hacking into Pentagon and Nasa computers between February 2001 and March 2002 while searching for evidence of ‘little green men’.

Last night the LulzSec group sought to distance itself from Ryan.

On Twitter, the group said: 'Ryan Cleary is not part of LulzSec. We house one of our many legitimate chatrooms on his server, but that’s it.'
On the offensive: Lulz Security announced its operation to bring down high-profile websites on Twitter

WHO ARE LULZ SECURITY?

Lulz Security's rise to prominence has been extraordinarily fast.

The hacking group first emerged in May and in the past few weeks has attacked the websites of some of the world's leading corporations and governments.

It is regularly abbreviated to LulzSec, which breaks down into two parts - Lulz refers to 'LOL' (laugh out loud), while Sec is short for security.

The group specialises in locating websites with poor security and then stealing information from them and posting it online.

The attacks do not appear to be financially motivated - instead, LulzSec seems content to receive international recognition for embarrassing some of the world's largest companies.

Not all the attention has been negative, either, as some cyber experts have praised LulzSec for exposing the inadequacy of online defences without maliciously exploiting these weaknesses.

The first LulzSec attack on record took place against the Fox.com website in late April - the hackers gained access to emails and passwords of hundreds of employees.

In a matter of weeks, the group has claimed responsibility for breaching the security of conglomerates including Nintendo, Sony, the NHS, the CIA and Soca.

SOURCE: Daily Mail

20 Jun 2011


Tunisia's Ben Ali sentenced in absentia to 35 years

TUNIS (Reuters) - A Tunisian court sentenced former president Zine al-Abidine Ben Ali in absentia on Monday to 35 years in jail, six months after his ouster in a revolution helped inspire the "Arab Spring."

Ben Ali, who has been in Saudi Arabia since he was forced from office, was found guilty after just one day of deliberation of theft, illegally possessing jewellery and large sums of cash.

The same sentence was handed down to his wife Leila Trabelsi, a former hairdresser whose lavish lifestyle and clique of wealthy relatives was for many Tunisians a symbol of the corruption of Ben Ali's time in office.

Ben Ali flew to Saudi Arabia on January 14 after mass protests against his 23-year rule. While he was in office, members of his extended family built stakes in the country's biggest businesses and accumulated vast fortunes.

Tunisia's revolt electrified millions across the Arab world who suffer similarly from high unemployment, rising prices and repressive governments. Ben Ali's has been watched closely in Egypt, where former president Hosni Mubarak is due to stand trial over the killing of protesters.

In a statement issued by his lawyers earlier on Monday, Ben Ali denied all the charges against him, saying that he was the victim of a political plot. He said he had been tricked into leaving the country.

During the hearing, a prosecutor had asked the judge to hand down "the most severe punishments for those who betrayed the trust and stole the money of the people for their personal gain .... They did not stop stealing for 23 years."

The judge, who read out the verdict and sentence in the Palace of Justice in the Tunisian capital, also ruled Ben Ali and his wife would have to pay fines totalling 91 million Tunisian dinars (40.6 million pounds).

The judge said the verdict on other charges, relating to illegal possession of drugs and weapons, would be pronounced on June 30, according to a Reuters reporter who was in the courtroom.

FLIGHT FROM TUNISIA

Earlier, Ben Ali's lawyers had given the first detailed account of the events that led to his departure from Tunisia.

At the time, thousands of protesters had gathered in the centre of the capital Tunis to demand that he step down, the culmination of three weeks of demonstrations which police tried to disperse by firing on the crowds.

The statement issued by his lawyers said that the head of presidential security had come to Ben Ali in his office and told him "friendly" foreign intelligence services had passed on information about a plot to assassinate the president.

He was persuaded to get on a plane that was taking his wife and children to safety in Jeddah, Saudi Arabia, but with the intention of returning immediately, the statement said.

"He boarded the plane with his family after ordering the crew to wait for him in Jeddah. But after his arrival in Jeddah, the plane returned to Tunisia without waiting for him, contrary to his orders.

"He did not leave his post as president of the republic and hasn't fled Tunisia as he was falsely accused of doing," the statement said.

Ben Ali's version of events is unlikely to elicit sympathy from the majority of Tunisians. They are now enjoying relative freedom after decades when most people would not speak openly for fear of arrest by the secret police.

In his statement released on Monday, Ben Ali said the weapons he was accused of possessing illegally were gifts from other heads of state and the jewellery had been given as gifts to his wife by foreign dignitaries.

The money and drugs had been planted in his home and the presidential palace after his departure as part of the plot against him, he said in the statement.

SOURCE: Reuters


Sio siri kwamba Rais Jakaya Kikwete anapenda sana kusafiri.Kuna vijimikutano vya kimataifa mbavyo kwa hakika visihitaji Tanzania iwakilishwe na Rais na badala yake akaenda Waziri Mkuu au kwa stahili kabisa Waziri wa wizara husika.Lakini asipokwenda yeye,watajuaje kama Kikwete ndiye Rais wa Tanzania?

Tuweke hilo kando.Tatizo jingine la Kikwete ni kutoa kauli ambazo yayumkinika kuamini kuwa hazijafanyiwa tafakuri ya kutosha.Huku nyuma,alishawahi kusema haelewi kwanini Tanzania ni masikini,na Waziri Mkuu wake,Mizengo Pinda, akaakisi kauli hiyohiyo.Sasa kama Rais hajui chanzo cha umasikini wa nchi anayoongoza,anafanya nini hapo Ikulu?

Safari hii kaibuka na madai kwamba kinachokwaza maendeleo yetu ni ukosefu wa fedha.Fedha zipi hizo?Mbona yeye kiguu na njia huku safari zake zikilibebesha taifa mzigo mkubwa wa gharama?Na fedha zipi anazozungumzia ilhali wabunge wetu wanalipwa mamilioni ya posho kwa "ku-rubber stamp" kila kinachowasilishwa kwao na serikali huku jitihada kubwa zaidi wanayofanya ni kubamiza meza (pongezi) kama sio kuwazomea wabunge wa upinzani?

Hebu soma porojo zake hapa chini

JK: Ukosefu wa fedha unakwamisha maendeleo
Sunday, 19 June 2011 20:57
Mwandishi Wetu
RAIS Jakaya Kikwete amesema ukuaji wa kasi wa uchumi na maendeleo katika Bara la Afrika unakwamishwa na ukosefu wa fedha za kutosha za kugharimia miradi ya maendeleo. 
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu jana, Rais Kikwete alikuwa akizungumza kwenye siku ya kwanza ya mkutano wa Kimataifa wa mwaka huu wa Taasisi ya Smart Partnership Dialogue ambao pia unajulikana Langkawi International Dialogue 2011, ulioanzishwa rasmi mwaka 1995. 
Rais Kikwete alisema kwamba njia za jadi za kupata fedha za kutosha ili kuharakisha ukuaji kasi wa uchumi, hazina uwezo wa kutoa fedha za kutosha kwa ajili ya maendeleo. 
Rais Kikwete alisema kutokana hali hiyo ni lazima nchi za Afrika zitafute namna nyingine mpya ya kugharimia maendeleo ya bara hilo na watu wake. 
“Tatizo ni ukosefu wa fedha za kutosha kugharimia miradi inaweza kuzitoa nchi za Afrika na watu wake katika umasikini kwa haraka zaidi,” Rais Kikwete, mjini Kuala Lumpur, Malaysia. 
Shabaha kuu ya Smart Partnership ama Langkawi International Dialogue ni kufanya majadiliano ya kimataifa ya jinsi ya kuharakisha maendeleo ya kiuchumi duniani. Mada kuu katika mkutano wa mwaka huu ni ‘Enhancing Smart Partnership for Socio-Economic Transformation’. 
Akishiriki katika mjadala huo, Rais Kikwete aliwaambia mamia ya washiriki tatizo kubwa linalokwamisha ukuaji kasi wa uchumi na maendeleo katika Afrika ni ukosefu wa fedha za maendeleo kwenye sekta binafsi, sekta ya umma na kwa Serikali. 
Rais alisema chanzo kikuu cha fedha za maendeleo kwa nchi masikini za Afrika ni misaada ya maendeleo (ODA), lakini sasa fedha za ODA zimekuwa zikipungua na wakati mwingine hazipatikani.
“Hata ukitofautiana na kampuni yenye asili ya nchi inayotoa misaada, basi utanyimwa misaada hata kama kampuni yenyewe ndiyo yenye makosa,” alisema Rais Kikwete. 
Rais alisema wakati mwingine inakuwa vigumu kuvutia fedha za maendeleo kutoka nje. 
“Hakuna fedha za kutosha kwenye masoko ya fedha ya ndani na msingi mzima wa kifedha ni dhaifu sana. Msingi wa fedha wa ndani ni dhaifu na hata msingi wa fedha za kigeni wa nchi zetu ni masikini,”alisema Rais Kikwete. 
Rais alisema hali hiyo imezifanya nchi za Afrika kujikuta katika wakati mgumu wa kutimiza wajibu na majukumu yake katika kuwaletea wananchi maendeleo. 
“Hivyo, sisi katika Afrika tunahitaji kutafuta na kuangalia njia nyingine za ubunifu zaidi za jinsi ya kupata fedha za maendeleo,” alisema Rais Kikwete. 
Mapema mkutano huo ulifunguliwa na Waziri Mkuu wa Malaysia, Dato’ Sri Mohammed Najib Tun Abdul Razak ambaye hotuba yake ilizungumza masuala mengi na matatizo mengi yanayoikabili dunia kwa sasa pamoja na umuhimu wa ushirikiano baina ya nchi zinazoendelea.

CHANZO: Mwananchi

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.