22 Jul 2011


Usanii wa Wachina katika kufoji umekwenda hatua ya juu zaidi baada ya bloga mmoja kugundua maduka makubwa (malls) matatu ya bidhaa za kampuni ya Apple (inayotengeneza iPhone,iPads,nk).Kichekesho ni kwamba maduka hayo ni feki kwa vile hayana kibali cha kampuni ya Apple.Lakini to make matter even worse,biahdaa zote za Apple zinazouzwa kwenye maduka hayo nazo ni feki pia.Kama hiyo haitoshi,hata wafanyakazi wa maduka hayo nao "waliingizwa mjini" kwani siku zote walikuwa wanaamini kuwa wao ni waajiriwa wa Apple ya Marekani.

Halafu hawa ndio watu tunaowaamini kama mapatna wetu wa maendeleo katika jitihada zetu za kujiweka mbali na "Wazungu"!! Angalia picha hizi na video








Mwanamama mmoja na mumewe huko Aberdeen,Scotland walikumbwa na kiwewe baada ya kukumbana na bonge la dude kwenye ufukwe wa Bahari ya Kaskazini.Well,dude hilo halikuwa hai bali kiufasaha ni masalia ya "sea monster" (sijaui tafsiri yake kwa Kiswahili ni ipi)?Pata picha ndio ungekuwa wewe peke yako...Hadi sasa haijafahamiaka masalia hayo ni ya kiumbe gani wa baharini lakini wataalam wanabashiri kuwa inawezekana ni ya papa muuaji (killer whale) au papa rubani (pilot whale)

Papa muuaji  

Papa rubani

20 Jul 2011



Majaribio yameanza ya kinga inayotokana na mimea kutumika kama kinga dhidi ya virusi vinavyosababisha upungufu wa kinga ya mwili (UKIMWI).Kinga hiyo inatengenezwa kwa kutumia majani ya tumbaku iliyozalishwa maabara,ikitarajiwa kuwa ufanisi wake utapunguza gharama ya dawa za kurefusha maisha ya waathirika wa ugonjwa huo,na kwa muda mrefu kupata tiba ya kudumu ya ugonjwa huo.

Vidonge vilivyotengenzwa kutokana na mimea vinafanyiwa majaribio kwa kundi la wanawake hapa Uingereza,hasa kuangalia ufanisi wake.Watengenezaji wa vidonge hivyo wanategemea vitasaidia kupatikana kwa kinga dhidi ya maambukizo ya virusi vinavyosababisha ukimwi lakini mafanikio makubwa yanatarajiwa kwenye ukweli kwamba molekyuli zinazotarajiwa kuwa na ufanisi ni nafuu zaidi kwa minajili ya gharama.

Majaribio hayo katika miili ya binadamu yameidhinishwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Madawa na Huduma za Afya ya hapa Uingereza,na inafanyika huko Guildford katika taasisi ya utafiti wa afya ya Chuo Kikuu cha Surrey.

"Pharma-Plant" ni mradi ulioanzishwa miaka saba iliyopita ukiwa na lengo la kutumia mimea iliyozalishwa maabara kupunguza gharama ya uzalishaji wa vidonge kwa ajili ya tiba mbalimbali.Wanasayansi wanadhamiria kutengenza madawa yenye ufanisi lakini kwa gharama nafuu,na kuzisaidia nchi masikini duniani.

Habari hii imetafsiriwa kutoka katika gazeti la Guardian.Kwa habari kamili soma HAPA

19 Jul 2011


Rais Kikwete kutembelea Afrika Kusini 
Monday, 18 July 2011 21:28

Mwandishi Wetu
RAIS Jakaya Kikwete, jana alianza ziara ya kihistoria ya kidola nchini Afrika Kusini, ikiwa ni ziara ya kwanza ya aina yake, kufanywa na Rais wa Tanzania katika nchi hiyo.

Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu, Rais Kikwete anafanya ziara hiyo kwa mwaliko wa Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma, ambaye utawala wake umekuwa uhusiano wa karibu na Tanzania, tangu aliposhika madaraka ya kuongoza taifa hilo kubwa kiuchumi kuliko mengine, katika Afrika.

Rais Kikwete na ujumbe wake unaojumshia pia mkewe, Mama Salma Kikwete, uliondoka nchini jana mchana kwenda Pretoria, kwa ziara hiyo ya siku nne.Pamoja na kwamba marais wa Tanzania waliomtangulia Rais Kikwete wametembelea Afrika Kusini mara nyingi kwa shughuli mbalimbali, lakini hakuna kiongozi aliyepata kualikwa kufanya ziara rasmi, ya kiserikali ama ya Kidola, tangu nchi hiyo ilipoingia katika mfumo wa demokrasia mwaka 1994.

Kwa mujibu wa ratiba ya ziara hiyo, Rais Kikwete na ujumbe wake, watapokelewa rasmi leo asubuhi katika Jumba la Serikali, mjini Pretoria.Tayari Rais Zuma na mkewe walikwishajipanga kwa sherehe za makaribisho zitakazofuatiwa na mazungumzo rasmi ya Kiserikali kati ya Tanzania na Afrika Kusini.

Mazungumzo hayo, yatafuatiwa na utiaji saini wa mikataba na makubaliano katika nyanja mbalimbali kati ya nchi hizo mbili.Baadaye, viongozi hao wawili watahutubia mkutano wa waandishi wa habari na baada ya hapo, Rais Kikwete atatembelea Uwanja wa Uhuru akiandamana na Rais Zuma.

Mchana viongozi hao watahudhuria chakula cha mchana kikiwashirikisha pia wafanyabiashara wa Tanzania na Afrika Kusini ambao watazungumza na kuelezea umuhimu wa kuimarisha uhusiano wa kibiashara na kiuchumi kati ya nchi hizo mbili.Jioni, Rais Zuma ataandaa dhifa ya kitaifa kwa ajili ya Rais Kikwete na ujumbe wake .

Keshokutwa, Rais Kikwete na ujumbe wake watakwenda Cape Town, ambako miongoni mwa mambo mengine ujumbe huo utatembelea Kisiwa cha Robben ambako wapigania uhuru maarufu wa Afrika Kusini, akiwamo Rais Mstaafu Nelson Mandela, walifungwa kwa miaka mingi na makaburu. Rais Kikwete atarejea nyumbani keshokutwa asubuhi.

CHANZO: Mwananchi 

LABDA AKIREJEA KUZURURA TATIZO LA UMEME LITAKUWA LIMEPATA UFUMBUZI. 




Kama kuna kosa ambalo Watanzania watalijutia kwa muda mrefu sana ni lile walilofanya mwaka 2005 na kisha kulirudia mwaka jana kumchagua Jakaya Kikwete kuwa Rais wa nne wa Tanzania.Tusiume maneno,mengi ya matatizo yanayoikabili nchi yetu kwa sasa ymesababisha,yanasababishwa au yamechangiwa au yanachangiwa na ubabaishaji wa Kikwete.

Ni nani mwenye akili timamu asiyefahamu kuwa wakati kelele dhidi ya ufisadi zinaelekezwa kwa "mapacha watatu" waliobaki wawili (ie Lowassa na Chenge,na Ristam aliyejiuzulu),Kikwete ni sehemu muhimu kabisa ya tuhuma zinazoelekezwa kwa wanasiasa hao.Hapa simaanishi kuwatetea mafisadi hao bali ninachojaribu kupigia mstari ni ukweli kwamba Kikwete hana tofauti na Lowassa,Chenge au Rostam.Na hilo halihitaji ufafanuzi.Yeye anajua,mapacha watuatu waliobaki wawili wanajua,na kila Mtanzania mwenye akili tiammu anajua.Kwanini hadi leo Kikwete bado ni Rais wetu ni swali gumu kulijibu just like lile la kwanini alichaguliwa mara ya kwanza mwaka 2005 na baadaye 2010 ilhali wanamjua walikuwa wanatambua bayana kuwa hana sifa za kushika wadhifa huo mkubwa kabisa katika nchi yetu.

Anyway,lengo la makala hii sio kujadili ubabaishaji wa Kikwete katika utendaji kazi wake bali lengo ni kukemea kwa nguvu kubwa uhuni uliofanywa na Kikwete wa kufanya harusi ya mdogo wake kwenye Ikulu ndogo ya Bagamoyo.Hivi kwa kuwa Rais,Kikwete anadhani kuwa Watanzania wametoa urais kwa ukoo wake mzima?Kwanini asikodi ukumbi kwa fedha zake kisha akamfanyia sherehe mdogo wake?

Kama huelewi kwanini ninalamika,Ikulu iwe ile ya Magogoni au hizo ndogo za wilayani na mikoani ni mahala patakatifu-kama alivyowahi kusema Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere.Si mahala ambapo kila Tom,Harry and Dick anaweza kufanya atakalo.Lakini licha ya utakatifu huo wa Ikulu,ifahamike kuwa mahala hapo panaendeshwa kwa fedha za walipakodi.Kwa mantiki hiyo,kufanyia sherehe mahala hapo ni sawa na kuwabebesha gharama Watanzania kwa ajili ya harusi ya ndugu wa Kikwete.Sidhani hata waliompigia kura mwaka jana au 2005 walitamani kuona kura waliyompigia Jakaya inageuzwa kuwa mithili ya kuupigia kura ukoo wake mzima.

Huu ni uhuni unaopaswa kukemewa vikali.Rais anaweza kuzurura nje ya nchi atakavyo (inaelekea kama hakuna namna ya kumwelewesha kuwa safari zake za mara kwa mara nje ya nchi ni mzigo mkubwa kwa Watanzania) lakini kamwe tusiruhusu nafasi ya Urais ikageuzwa kuwa kama cheo cha kifamilia.

Madhara ya kumwacha Kikwete aendelee na madudu yake ni kwamba anaweza kumaliza muda wake hapo 2015 na kuiacha Tanzania ikiwa jina tu-haina maadili,haina raslimali,na kibaya zaidi,nafasi ya urais ikaishia kuwa na heshima ndogo kuliko ya mwenyekiti wa serikali ya mtaa.

PICHA: Kwa hisani ya Global Publishers

18 Jul 2011


BRILLIANT BUDGET SPEECH, HONGERA SANA! 
Nd. Mnyika,
Nimesoma hotuba yako bungeni hapa chini kwa makini sana na kupata faraja kubwa – hongera nyingi, na kama wasemavyo wataliano – BRAVISSIMO!  Pia nimefurahi zaidi baada ya kuona baadhi ya yale ninayoandika na kushauri, hususan maswala ya urani (uranium), kupewa hisa watanzania, STAMICO na TPDC, maswala ya kulinda na kuhufadhi vizuri mazingira ya nchi wakati wa uchumbaji wa madini, haja ya kuchunguza na kubadilisha mikataba mibovu ya madini ikiwa ni pamoja na ulaghai wa kampuni kama Williamson Diamonds, TanzaniteOne, uzembe uliofanyika kuingia mikataba mibovu ya gesi asilia n.k., haya mambo yote umeyachambua ipasavyo na hata kwenda mbele zaidi kwa kuweka bayana baadhi ya mambo mengine ambayo mimi kama mtaaalamu sikuwa nayafahamu kuwa yanatendeka Tanzania hivyo kuweza kunipa habari ambazo zitanisaidia kuyachambua kitaalamu, tena kwa kina. Nimepaka rangi baadhi ya sehemu kwenye hotuba yako kuonyesha yale ambayo yamenigusa zaidi na mambo ambayo niliwahi kuyakemea na kusisitiza yachunguzwe na kubadilishwa kwa muda mrefu.
Nadhani utakuwa umesoma barua zangu za hivi karibuni zinazohusu maswala ya madini nchini Mongolia na Sudani Kusini – ziko hapa. Ni matumaini yangu mtazichambua barua hizi pamoja na wenzako wa kambi ya upinzani Bungeni na muangalie namna gani mnaweza kuhakikisha yale muhimu kwa taifa letu yanaweza yakatekelezwa Tanzania. Ndani ya barua hizo utaona pia maoni yangu kuhusu mauaji ya Tarime uliyoniuliza hapo awali ingawa msimamo wangu kuhusu hili jambo niliwahi kuzungumzia vikali kwenye baadhi ya barua zangu zikiwezo hizi hapa: 1 (soma kuhusu mamillionea wa kimya kimya - Silent Millionaires – walivyowadanganya watu wetu Bulyanhulu. Baadhi ya hawa mamillionea ni/au walikuwa wafanyakazi wa serikali). Soma pia hapa 2, pamoja na hapa 3.
Pia hapa chini nakutumia tovuti za makala kadhaa ambazo nadhani ni muhimu kuzisoma hasa baada ya kuona kuwa ni mambo ambayo uliyazungumzia kwenye hotuba yako na mimi pia nimekuwa nikisisitiza kwa muda mrefu yafanyiwe kazi na serikali. Ni matumaini yangu utaendela na msimamo wako imara wa kuibana serikali ifanye marekebisho pale ambapo inaonekana kuwa rasilimali za taifa haziwanufaishi watanzania, na wale waliongia nchini kama wawekezaji wa kigeni, na hata raia na makampuni yetu ya Tanzania, wanakiuka na kuvunja sheria za sekta ya madini. Ni muhimu makosa makubwa tunayoyafanya kwenye sekata ya madini, gesi asilia na petroli yarekebishwe, tena haraka sana. Kama ulivyoeleza kwenye hotuba yako, hakuna sababu yeyote ya msingi watanzania waishi kwenye umaskini wa kutupwa huku wakiwa na utajiri mkubwa wa madini kama tulionao, utajiri ambao serikali yetu inautoa, hata niseme, kuutupa kwa wageni – hii si sahihi hata kidogo. Nitashukuru kama utakuwa unaniarifu mara kwa mara maendeleo ya jitihada zenu kufanikisha azma hii.
Ahsante, na pongezi nyingi kwa ujasiri na uimara wako Bungeni.
Shaaban
Moscow, Urusi.     


MNAKARIBISHWA NYOTE KWENYE SABATO YA WAGENI TAREHE 23/07/2011

Kanisa la wasabato ( Angaza Swahil UK)  linapenda kuwakaribisha  watu wote    kutoka sehemu mbali mbali za Uingereza katika sabato ya wageni itakayofanyika tarehe 23/07/2011 kuanzia saa 3.00 asb hadi saa 11.00 jioni.
Siku hiyo itakuwa ya pekee kweli kwani vikundi mbali mbali vya nyimbo vitakaribishwa kuimba kutoka kwenye kila dhehebu  .Pia watoto wataonyesha programme mbali mbali.

 THEME: NJOO UJUE UNA NINI MKONONI MWAKO

Baada ya ibada ya mchana tutakusanyika pamoja kwa ajili ya chakula na vinywaji.Usipange kukosa lete rafiki yako .Kama hauna usafiri i wasiliana nasi.KARIBU NYOTE

ANUANI
St Barnabas C Of E Church
Elm Road, Reading, RG6 5TS


 


16 Jul 2011


School of Public Policy Building Bridges
Tanzanian Student Wins Research Award
Most young people in Tanzania have never heard of the Maryland School of Public Policy. But through the generosity of those who saw the promise in Emmanuel Sulle, he has completed his first year of studies at the School and has also won the Conservation Research in Eastern Africa’s Threatened Ecosystems (CREATE) Research Award from the Frankfurt Zoological Society. Sulle will study the impact of microcredit institutions (in this case Community Conservation Banks) which are in place within the Serengeti ecosystem in Tanzania. Sulle will conduct the field research in Tanzania during the winter break of 2011-2012.
"Emmanuel is a wonderful example of the School's bridge across the oceans--of using the tools of public policy to improve the quality of life and to make a big impact on the world," says MSPP Dean Don Kettl.
Sulle was working as a Research Associate at the Tanzania Natural Resource Forum when he was encouraged by Professor Robert Nelson to apply to the MSPP program. Nelson’s son Fred, who worked 12 years in Tanzania on wildlife conservation, had worked with Sulle on two research studies – most recently the published report on “Biofuels, land access and rural livelihoods in Tanzania”.
“We need more people like Emmanuel,” said Bob Nelson, who also serves as Sulle’s informal mentor.
  “Unfortunately, they are hard to identify.”
Sulle is currently in Tanzania collaborating with the Maliasili Initiatives to undertake two research projects on “Wildlife Management Areas and Pastoralist Livelihoods: An Assessment,” and “Analysis from Northern Tanzania and Community-based Conservation in the Tarangire-Manyara Corridor: An Assessment of Existing Models and Experiences.”
“Emmanuel is in a position to take his MSPP education and make a serious policy impact in Tanzania,” says MSPP Student Affairs Assistant Director, Taryn Faulkner.
Sulle earned his BA in Economics from St. Augustine University of Tanzania (SAUT) in 2008. He has carried out a variety of research projects commissioned by, or in collaboration with MISERIOR-Germany, Fulbright, Tanzania Natural Resource Forum, Sand County Foundation, and Health and Development International Consultants. He has authored and co-authored a number of research reports on tourism revenue transparency, wildlife management areas, as well as biofuels, land access, and rural livelihoods in Tanzania.
“I am interested to see rational use of natural resources as a tool for poverty reduction in developing countries,” Sulle said.

HONGERA SANA,NDUGU EMMANUEL.KILA LA HERI.

12 Jul 2011


Ndugu zangu wapendwa,kwa niaba ya familia ya Chahali naomba kuwasilisha shukrani za dhati kwa wote ambao kwa namna moja au nyingine mmeungana nasi kwa maombi kwa baba Mzee Philemon Chahali ambaye hali yake bado ni mahututi kufuatia ajali ya kugongwa na pikipiki huko Ifakara,Alhamisi iliyopita.

Ningetamani sana kutoa shukrani kwa kutaja jina la kila mmoja wenu lakini naomba nitoe shukrani za jumla.Nawashukuru sana bloggers wenzangu ambao licha ya kunisaidia kuweka tangazo la maombi ya sala kwa baba mmekuwa mkinitumia meseji na barua pepe za kunipa moyo pamoja na sala/dua zenu.Katika kuonyesha upendo wa hali ya juu,dada yangu blogger wa hapa UK Rachel Siwa aliweka maombi kwenye misa ya Jumapili iliyopita huko Coventry.Tunakushukuru sana dada Rachel na Mungu akubariki.Bloga mwenzangu Miss Jestina naye amekuwa akitujulia hali ya Mzee mara kadhaa kwa siku,bila kuwasahau wadogo zangu Jackie Lawrence (La Princessa) na Faith Charles Hillary (Candy1World) ,na Mtakatifu Simon Kitururu,bloga Malkiory  Matiya na Nova Kambota

Huko Twitter nimekuwa nikipata sapoti ya kutosha tangu zilipojiri habari za ajali.Dada zangu Maria Sarungi na Lilly  Melody,pamoja na wasanii wetu mahiri kabisa Hamisi Mwinjuma (Mwana FA) na Joseph Haule (Profesa Jay) ni miongoni mwa wana-Twitter wenzangu ambao wamekuwa mstari wa mbele kunifariji.

Kwa bahati mbaya,ukweli mchungu kuhusu maisha ni kwamba mpaka upate tatizo ndio unaweza kufahamu upendo wa watu wanaokuzunguka.Kuna watu nilikuwa sifahamiani nao kabisa lakini baada ya kusikia habari za ajali iliyomkumba baba wamekuwa ni nguzo muhimu kutusapoti.Kwa kweli ninawashukuru sana na Mungu awabariki sana kwa upendo wenu.Ni imani ya familia yetu kuwa sala zenu na zetu zitamsaidia Mzee Chahali sio tu kupata nafuu bali kupona kabisa.

Kwa vile inaniwia vigumu kublog kutokana na tatizo linalonikabili,naomba pia kutumia fursa hii kuwashukuru wasomaji wote wa blogu hii na watu wengineo walionipigia kura katika Tuzo la Blogu za Kitanzania (Tanzanian Blog Awards) ambapo japo sikuibuka mshindi lakini nimepata matokeo ya kupigiwa mstari.Kwa kifupi,blogu hii imeshika nafasi ya pili katika categories za Best Inspiration Blog na Best News Blogs na imeshika nafasi ya tatu katika category ya Best Political Blog.Ukiangalia kwenye hizo categories mbili za mwanzo utagundua kuwa aliyeshika nafasi ya kwanza ni bloga ambaye blogu yake imeshatembelewa na wasomaji zaidi ya milioni 12 wakati blogu hii "inasuasua" na wasomaji 424538 hadi dakika hii.Kwangu hayo ni mafanikio makubwa sana lakini si mafanikio yangu pekee bali ya wadau wote wa blogu hii.Namshukuru kila aliyenipigia kura,na japo hatukuibuka washindi wa jumla,kushiriki kwenye tuzo hizo na kukamata nafasi za juu ni tuzo kubwa sana.

Naomba nimalizie kwa kurejea tena shukrani zangu na za familia yangu kwenue nyote mnaoshirikiana nasi kwenye maombi kwa ajili ya Mzee Philemon Chahali.Ni matumaini yetu kuwa Bwana anasikiliza sala/dua zetu na atamjalia baba uponyaji kwa vile Mungu ni mwema na mwenye upendo.

ASANTENI SANA

7 Jul 2011


Nasikitika kuwafahamisha kuwa baba mzazi Mzee Philemon Chahali amepata ajali mbaya asubuhi hii huko Ifakara.Amegongwa na pikipiki ambazo ndio usafiri mkuu wa huko.Kwa mujibu wa habari nilizonazo hadi muda huu,hali yake ni mbaya,ambapo licha ya kuvnjika mguu pia ameumia kichwani.Kibaya zaidi ni kwamba umri wake ni kwenye miaka ya 80 kwa hiyo mshtuko tu wa ajli unaweza kumwathiri sana.

Basi naomba kutumia fursa hii kuomba sala zenu.Sie Wakristo tunaamini kuwa wanapojumuka wengi kufanya sala basi Mungu naye anakuwepo.Natumaini kwa sala zenu na za familia yetu Mungu atamjalia baba apone na kurejea katika hali yake ya kawaida.

Natanguliza shukrani zangu za dhati.Asanteni 

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.