7 Nov 2011


CHANZO GLOBAL




So homosexuality is unAfrican? What about living on handouts?

For a country that once had ambitions of becoming a self-reliant nation, Tanzania is a surprisingly donor-dependent place.

The Arusha Declaration, Julius Nyerere’s blueprint for socialism and self-reliance, argued that dependency on external economic assistance would be detrimental to the country’s independence.

In a brief but closely argued document, a strong case was made for reliance on our own resources and treating foreign aid with care, especially shunning financial grants, for whereas loans and credit lines impose the responsibility of repayment, free money makes the recipient a virtual beggar and keeps him beholden to the donor.

And yet Tanzania, even under the old man himself, went ahead and accepted foreign money, loans and grants, in huge sums, especially in sectors such as education, health and water and sanitation.

The dependency grew so great that when Olof Palme, the Swedish social democrat who had underwritten Nyerere’s education programme, lost power, Tanzanians felt the impact probably more acutely than the Swedes.

The rightwing government that came in scrapped the whole aid package to Tanzania, declaring, rather cruelly, that we had become a bottomless pit.

Since then our education programmes have struggled, our schools have staggered along, and our rulers have remained largely clueless as to what we need to do to liberate ourselves from the mire of growing dependency.

Indeed, a few years ago we reached some benchmark that convinced our donor countries that we had become a highly indebted poor country (HIPC). And we celebrated with a beggar’s dance, bowl in hand.

Our government has continued to borrow and to receive cash handouts in what has come to be known as general budget support (GBS) that gives it unfettered licence to place those monies wherever it pleases.

At some stage in the past, our beggar practices were streamlined in such a way that we could only borrow or beg to meet capital, or development programmes.

Now we can borrow to pay government employees and other charges (OT), which gives dependency a new and menacing dynamic.

This has meant that when a donor government decides to withdraw its GBS grant, the beggar government finds itself in an awkward situation, for whereas a road construction programme can easily be put off or postponed, civil service pay and running the government cannot.

So, when the Brits announced, a couple of weeks ago, that they intend to cut their GBS handouts, the Tanzanian government put on a brave face, making it appear like it was a small matter. But it’s likely to hurt.

All this was, of course, before David Cameron made his remarks about his intention to cut aid to governments that suppress homosexual rights, so we don’t know what the real motive for the aid cut was.

African men are a macho lot, and for many the very idea of a man-on-man sexual partnership is anathema.

Woman-on-woman also. A man was created specifically to have liaison with a woman, and a woman was created as a tool, exclusively to serve the man, in both productive and reproductive pursuits.

It is inconceivable that two such tools would dream of having a liaison other than with the man.

Rather like the tractor dating the combine harvester on the farm.

Apart from the viewpoint of a woman being a centre for economic and biological production, I do not have much against those who claim that homosexuality is un-African.

But let us push this macho thing to its logical conclusion.

No self-respecting African man would let another man pay for his and his wife’s and his children’s upkeep.

Indeed, a man who allows that to happen would be considered as having been married by the provider man, call them economic homos. Rejecting the one, reject the other too.

SOURCE: The East African

6 Nov 2011

CCM dhaifu mtaji imara wa urais CHADEMA, CUF

Uskochi
NIANZE makala hii kwa kutoa salamu za pongezi kwa jarida hili la Raia Mwemaambalo limetimiza miaka minne tangu kuanzishwa Oktoba 30, 2007. Binafsi, jarida hili limekuwa sehemu muhimu ya maisha yangu tangu nilipopewa fursa ya kuandika safu hii.
Lakini kubwa zaidi ni jinsi jarida hili lilivyosimama imara na kuwa sauti ya wasio na sauti (wanyonge), likifukua ufisadi na kuhabarisha umma pasipo upendeleo.
Pasi na shaka yoyote, Raia Mwema linastahili kuitwa gazeti la rekodi, yaani unaloweza kulitumia kunukuu chochote kile bila hofu kuwa huenda kimekosewa au kimeandikwa kwa unazi. Sitoi sifa hizi kwa vile ni mwandishi wa makala gazetini humu lakini ninaamini kila anayependa kuhabarishwa kwa ufasaha na umakini ataafikiana nami kuwa Raia Mwema limeonyesha njia sahihi ya uandishi wa habari na makala.
Baada ya pongezi hizo za dhati nielekee kwenye mada ya wiki hii. Mada hii ni mwendelezo wa ile ya wiki iliyopita ambayo iliangalia mazingira yanayotarajiwa ya chama tawala katika kuelekea Uchaguzi Mkuu ujao hapo mwaka 2015.
Wiki hii ninajaribu kuangalia hali ilivyo katika vyama viwili, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na Chama cha Wananchi (CUF), ambavyo kwa sasa vinastahili kuitwa vyama vikuu vya upinzani.
Urais ndani ya CUF
Kuna msemo mmoja wa Kiingereza ambao katika tafsiri yake ya Kiswahili ni kama hivi: “Jambo zuri si lazima liwe jambo sahihi.” Kwa mfano, kumpatia chakula kingi mtu mwenye njaa kali kunaweza kusababisha kumuua mtu huyo bila kukusudia.
Mantiki ya usemi huo ni kwamba kuna nyakati tunafanya mambo kwa kuamini ni vizuri kufanya hivyo, lakini matokeo yake yanaweza kuwa mabaya kuliko matarajio. Kwa kurejea msemo huo wa Kiingereza, sote tunafahamu kuwa mtu mwenye njaa kali anahitaji chakula.
Lakini kabla ya kumpatia chakula ni vema kumpatia kinywaji cha moto kama vile chai au uji (kama wanavyofanya watu waliofunga). Kumpatia mtu huyo ugali mwingi kunaweza kusababisha akavimbiwa na pengine kuishiwa pumzi au hata kumpotezea uhai.
Chama cha CUF kililazimika kukaa meza moja na wapinzani wao wa CCM huko Zanzibar na hatimaye kufikia mwafaka na kuunda Serikali ya Umoja wa Kitaifa. Hilo lilikuwa jambo zuri (kama kumpatia chakula mtu mwenye njaa kali).
Lakini matokeo ya uamuzi huo wa busara yameiacha CUF huku Bara (na pengine hata huko Zanzibar) ikiwa haina mwelekeo. Kimsingi, chama hicho ni nusu ya serikali inayotawala kwa vile kimetoa Makamu wa Kwanza wa Rais kuongoza Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
Na katika kutekeleza kanuni ya uwajibikaji wa pamoja, CUF hawawezi kuinyooshea kidole CCM huko Zanzibar pindi mambo yakienda kombo.
Naomba ieleweke kuwa si kama ninailaumu CUF kwa kukubali mwafaka na CCM bali ninachoonyesha hapa ni madhara yasiyokusudiwa ya uamuzi huo. Ni vigumu kubashiri chama hicho kitaendeshaje kampeni “za maana” mwaka 2015.
Katika mazingira ya siasa za Zanzibar ni dhahiri kuwa kutakuwa na umuhimu wa kuendelea na serikali ya umoja wa kitaifa baada ya Uchaguzi Mkuu ujao.
Lakini ili hilo liwezekane itabidi kampeni katika uchaguzi huo ziwe za “kistaarabu” (ambalo ni jambo zuri isipokuwa tu linaweza kupunguza hamasa ya kisiasa kwa baadhi ya wapigakura).
Hoja hapa ni kwamba kama CCM itashinda na kisha kuunda serikali ya pamoja na CUF kuna haja gani basi ya kufanya kampeni za nguvu ambazo hazitabadili picha ya matokeo ya uchaguzi huo?
Na hata kama CUF wataamua waendeshe kampeni za nguvu ili kupata ushindi mkubwa, watawezaje kuonyesha kuwa CCM haistahili ushindi ilhali vyama vyote viwili vilikuwa madarakani (na hivyo kustahili sifa kwa mema au lawama kwa mabaya waliyofanya katika muhula wa 2010-2015)?
Kwa nini mazingira ya Zanzibar ni muhimu kwa hatima ya CUF kwa nchi nzima? Kwa sababu kila anayefahamu siasa za nchi yetu anatambua kuwa nguvu kubwa ya chama hicho ipo huko Visiwani. Lolote linalotokea huko linakigusa chama hicho kwa upande wa Bara na Muungano kwa ujumla.
Urais ndani ya CHADEMA
Sote tunakumbuka yaliyoikumba NCCR-Mageuzi baada ya mgombea wake Augustine Mrema kubwagwa na mgombea wa CCM, Rais Mstaafu Benjamin Mkapa, katika uchaguzi wa mwaka 1995.
Licha ya kushindwa katika chaguzi mbili mfululizo (mwaka 2005 na mwaka jana), CHADEMA imeendelea kuwa imara huku mgombea wake katika uchaguzi uliopita Dk. Willibrod Slaa akiendelea kuwa na hadhi ileile aliyokuwa nayo kama mgombea urais.
Kulikuwa na hofu kuwa laiti Dk. Slaa angeshindwa kwenye uchaguzi uliopita basi angepotea kabisa kwenye ulingo wa siasa za nchi yetu lakini hali imekuwa tofauti kabisa. Licha ya kubaki Katibu Mkuu tu wa CHADEMA (wadhifa aliokuwa nao kabla ya kugombea urais na kushindwa), mwanasiasa huyo ameendelea kuwa na mvuto mkubwa huku mikutano anayohutubia ikiendelea kupata wasilikizaji.
Lakini si Dk. Slaa pekee ambaye ameendelea kuwa na umaarufu na mvuto bali hata chama chake kimemudu kubaki tishio kwa chama tawala CCM.
Ukifuatilia kwa karibu malumbano ya kisiasa yanayoendelea nchini, unaweza kudhani kuwa bado tupo kwenye kampeni za Uchaguzi Mkuu uliopita au uchaguzi mwingine utafanyika hivi karibuni tu.
Moja ya mitaji mikubwa ya CHADEMA ni msimamo wake kuhusu mustakabali wa taifa. Chama hicho kimefanikiwa kwa kiasi kikubwa kujitambulisha na kukubalika kama kitovu cha harakati za mapambano dhidi ya ufisadi.
Bahati nzuri kwa CHADEMA ni namna CCM inavyoshindwa kujiondoa kwenye utando wa ufisadi, ambapo pamoja na mambo mengine suala la kujivua magamba ni kama kuafikiana na CHADEMA kuwa CCM ni kichaka cha mafisadi na hivyo chama hicho kikongwe hakina budi kujisafisha.
Mtaji mwingine wa CHADEMA ni mshikamano miongoni mwa viongozi wake wakuu na wa kada ya kati. Sina hakika sana hali ipo vipi katika ngazi za chini lakini kwa kiasi kikubwa CHADEMA inainyima usingizi CCM.
Kama mazingira yatabaki jinsi yalivyo sasa, kuna uwezekano wa CHADEMA kumteua tena Dk. Slaa kuwa mgombea wake hapo 2015. Mwanasiasa pekee anayeweza kubadili hali hiyo ni Naibu Katibu mkuu wa chama hicho, Kabwe Zitto, ambaye aliwahi kunukuliwa akisema kuwa angegombea urais kwenye uchaguzi mkuu ujao.
Mtaji mwingine mkubwa kwa CHADEMA ni hali ya mambo ndani ya CCM na mazingira yanavyotarajiwa kuwa katika mchakato wa chama hicho tawala kupata mgombea wake katika Uchaguzi Mkuu ujao (ambayo niliyaelezea kwa kirefu katika makala iliyopita).
Kama kuna nafasi yoyote kwa CHADEMA au chama kingine cha upinzani kuindoa CCM madarakani ni mwaka 2015 kwani kuna kila dalili kuwa sokomoko linaloendelea ndani ya chama hicho tawala litadumu hadi kitakapofanikiwa kupata mgombea wake. Laiti CHADEMA wakiafikiana mapema kuhusu mgombea wao katika uchaguzi huo basi watakuwa na muda wa kutosha kuandaa mazingira ya ushindi huku CCM wakiendelea kupigana vikumbo.
Lakini kuna busara moja ya kuzingatia katika msemo ufuatao: “Siasa si kama fumbo la hesabu ambapo siku zote 2 kujumlisha 2 jibu ni 4. Katika siasa jibu linaweza kuwa 100 au kwa kukatisha tamaa zaidi jibu likawa 0.” Licha ya kuwa siasa ni mchezo mchafu, kipindi cha miaka minne kabla ya Uchaguzi Mkuu ujao ni kirefu sana katika siasa na lolote linaweza kutokea kinyume kabisa cha uchambuzi huu.
Katika moja ya makala zijazo nitaingia kwa undani kujadili mambo yanayoweza kuikwamisha CHADEMA (au chama kingine cha upinzani) kuing’oa CCM kwenye Uchaguzi Mkuu ujao. Lakini kwa leo tuishie hapa

5 Nov 2011

Mustakabali Wa Chadema Mwanza


4 Nov 2011




Waziri Membe asema kama ni misaada yao basi
Raymond Kaminyoge 
TANZANIA imesema ipo tayari kukosa  misaada yote kutoka Serikali ya Uingereza  na kamwe haiwezi kuruhusu sheria inayotambua mashoga na kuhalalisha ndoa za jinsia moja.Msimamo huo mzito wa serikali umekuja siku chache baada ya Waziri Mkuu wa Uingereza, David Cameron, kutamka kwamba nchi yake ina mpango wa kusitisha misaada yake kwa nchi ambazo sheria na katiba zao, hazitambui mashoga na ndoa za jinsia moja.

Cameron alikaririwa akithibitisha kuwa tayari amewajulisha juu ya suala hilo Wakuu  wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Madola waliokuwa wakihudhuria mkutano wa Jumuiya hiyo uliomalizika siku nne zilizopita,  mjini Perth , Austaralia ambao pia ulihudhuriwa na Rais Jakaya Kikwete.

Waziri Mkuu huyo kutoka chama cha Conservative ambacho kilishinda uchaguzi Mei mwaka jana, alisema  suala hilo la mashoga na ndoa za jinsi moja ni moja ya mambo yanayoongoza sera ya serikali yake kuhusu misaada kwa mataifa mbalimbali na kwamba tayari imeanza kutekelezwa katika maeneo kadhaa duniani.

Kauli ya Cameron imechukuliwa kama kielelezo cha ukoloni mamboleo ambao Uingereza inajaribu kuupandisha daraja  kwa mataifa yanayoendelea kwa kigezo cha misaada  

Akizungumza na waandishi wa habari  jijini Dar es Salaam, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard Membe,  alisema pamoja na umasikini wake, Tanzania kamwe haitaruhusu upuuzi huo kwa kigezo cha misaada.

“ Tanzania ni nchi maskini lakini hatutakubali kuruhusu upuuzi huo eti kwa sababu ya misaada yake na fedha zao, lakini ushoga si utamaduni wetu, hata sheria zetu zinakataa,” alisema Membe.

Alifafanua kuwa katika kuonesha msimamo wa kutokukubaliana na masharti hayo, Tanzania imeshikilia msimamo thabiti kupinga  upuuzi huo ambapo  Januari mwaka huu,  ilimkataa balozi shoga ambaye aliteuliwa na nchi yake kuja kuiwakilisha hapa  nchini. Hata hivyo Waziri Membe hakutaja jina la balozi huyo wala nchi  anayotoka.
“Niwape siri moja ambayo tuliificha lakini leo ngoja niwaambie, mwanzoni mwa mwaka jana nililetewa barua  kunijulisha ujio wa balozi mmoja anayekuja kuiwakilisha nchi yake, mwanamume mwenye ndoa ya jinsia moja. Nilikwenda kumweleza Rais Jakaya Kikwete kuhusu wasifu wa balozi huyo mtarajiwa naye akajibu kwa maneno matatu, yarabi toba! Mkatae!” 
Waziri Membe alifafanua kuwa serikali ilimkataa balozi huyo kwa kuwa ni kinyume cha utamaduni wetu na sheria za nchi kuwa na watu wenye tabia hizo.

Alisema alimjulisha waziri wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo kwamba balozi huyo haruhusiwi kuja kufanya kazi nchini kwa kuwa ni kinyume na utamaduni wetu.  “ Waliendelea kuniomba kwamba balozi huyo akija hatatoka kwenye makazi yake akiwa na mwenza wake hivyo watu hawatamuona lakini tulimkataa kabisa, wakatuelewa,” alisema Membe.

 Alieleza kuwa  tamko hilo la Waziri Mkuu Cameron linaweza kusababisha hatari ya kuvunjika kwa uhusiano miongoni mwa nchi wanachama wa Jumuiya ya Madola na koloni mama  Uingereza na waziri huyo atabeba lawama hizo

 Akisisitiza msimamo huo wa serikali, Membe,  alisema  Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971 kifungu cha tisa, kinatambua ndoa ya jinsia mbili tofauti,  yaani mume na mke.  “ Sheria hizi tunazozitumia hivi sasa tumezirithi kutoka Uingereza ambako leo wanatukuza ndoa za jinsia moja na ushoga,” alisema Membe.
Suala la kile kinachoitwa haki za binadamu kuhusu ushoga ilikuwa moja ya ajenda ambazo viongozi kadhaa walishindwa kuafikiana katika mkutano  Perth .
Hoja ya  kukomesha vizuizi dhidi ya ushoga na ndoa za jinsi moja lilikuwa moja ya mapendekezo yaliyokuwamo katika ripoti ya ndani kuhusu matarajio ya baadaye ya Jumuiya hiyo ya Madola.
  
Itakumbukwa kwamba, Malawi tayari imeathirika na mpango huo wa Uingereza kwa sehemu ya misaada yake kusitishwa kutokana na msimamo wa nchi hiyo kuhusu kile Uingereza na nchi za Magharibi zinazokiita haki za mashoga. Ikumbukwe pia kuwa, mjadala mzito ulioibuka katika Bunge la Uganda mwaka 2009 kuhusu ndoa za jinsi moja ilikuwa sehemu ya utekelezaji wa sera hiyo ya Uingereza na washirika wake.
CHANZO: Mwananchi






Vigogo watafuna marejesho ya EPA
Thursday, 03 November 2011 21:27
Leon Bahati na Furaha Maugo
KAMATI ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC), imebaini ufisadi mwingine wa mabilioni ya fedha kwenye marejesho ya zile zilizochotwa awali kifisadi katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA).Fedha hizo zaidi ya Sh50 bilioni zilizorejeshwa na Rais Jakaya Kikwete kutangaza kuwa zitatumika kwa ajili ya kuendeleza shughuli za kilimo nchini, zinadaiwa kuchotwa kwenye Benki ya Rasilimali Tanzania (TIB) kwa amri iliyotoka kwa vigogo serikalini.

Mkurugenzi wa TIB, Peter Noni alikiri jana mbele ya POAC kuwa sehemu ya Sh20 bilioni zilizotolewa na Hazina kwenda kwenye benki hiyo kwa ajili ya dirisha la kilimo, Serikali iliamuru zitolewe kama mkopo kwa wafanyabiashara ambao iliwataja kwa majina.

"Mbaya zaidi, baadhi ya wafanyabiashara waliopewa mikopo hiyo wanaonekana kukwama kurejesha, huku wakitoa ahadi ambazo hawazitekelezi," Noni alisema.

Wabunge wengi wa POAC walionyesha kushangazwa na jinsi serikali ilivyoingilia kati TIB na kuchagua watu ambao wanapaswa kupatiwa mikopo.Huku miongoni mwa wabunge hao wakisema wana taarifa za vigogo walioingia mlango wa nyuma na kuchukua tena fedha hizo katika mazingira ya kifisadi, waliendelea kumbana Noni kwa maswali.

Ingawa baadhi ya wabunge walimtaka mkurugenzi huyo wa TIB awataje kwa majini vigogo hao, Makamu Mwenyekiti wa POAC, Deo Filikunjombe, alisita na kumtaka Noni asitaje majina hayo.

Miongoni mwa wabunge waliotaka majina ya vigogo hao yawekwe hadharani ni Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Ester Bulaya aliyesema, “Nina habari kuwa baadhi ya vigogo walihusika katika kupata mikopo hiyo… Naomba uyataje majina yao.”

Filikunjombe, alisema hakuna haja ya kutaja majina ya vigogo hao ambao alisema miongoni yamo kwenye taarifa waliyopatiwa kuhusu utendaji mzima wa TIB.

Lakini Noni ambaye alikuwa anasaidiwa pia na wasaidizi wake kujibu baadhi ya maswali mazito yaliyoulizwa na wabunge, alisema hakuna tatizo kutaja baadhi ya kampuni zilizohusika kwenye mikopo hiyo ambayo sasa inawatoa jasho TIB.

Noni alitaja mbele ya kamati hiyo kuwa moja ya kampuni zilizochukua fedha hizo na sasa zinaonyesha wasiwasi katika kuzirejesha ni Simon Group Ltd.Nyingine ni kampuni tano za kuuza maua nje ya nchi zenye makao yake makuu mjini Arusha, zikiwepo Tengeru Flowers na Mount Meru Flowers.

Kuhusu Kampuni ya Simon Group, ambayo ilielezwa kuwa ilikopeshwa Sh5 bilioni Noni alisema; “Tumekutana nao mara kadhaa na kutoa ahadi lakini hawakuzitekeleza.”

Aliongoza kuwa kampuni za kuuza maua nje ya nchi zilieleza tatizo lililowafanya kushindwa kurejesha mikopo hiyo kulingana na makubaliano kwamba, ni hasara waliyoipata kutokana na mdororo wa kiuchumi duniani.

Alifahamisha kuwa kutokana na hali hiyo, Serikali iliwaonea huruma na kuwaongezea kipindi cha miaka miwili kulipa deni hilo, muda ambao pia umeonekana kutotosha.

Ila akaahidi kwamba TIB itaanza mchakato wa kuwabana wadeni hao kwa kunadi mali ambazo ziliwekwa rehani wakati wa kuchukua mikopo hiyo.

“Uandaaji na usafirishaji wa maua walisema unahitaji gharama kubwa… Walilazimika kupitia Nairobi (Kenya)… Serikali iliona huruma ikawaongezea kipindi cha kulipa deni hilo,” alisema Noni huku wabunge wengi wakionyesha shauku ya kuendelea kumbana kwa maswali.

Miongoni mwa maswali yaliyoulizwa ni kwa nini TIB ilikubali kutoa mkopo kwa biashara ambazo hazitabiriki? Noni aliweka wazi kwamba, benki hiyo haikuhusika katika mchakato wa kuchambua na kuridhia mikopo kutolewa kwa kampuni hizo.

Filikunjombe ambaye ni Mbunge wa Ludewa, alishangazwa na jinsi Serikali ilivyoingilia uhuru wa TIB na kuweka wazi kwamba si mara ya kwanza Serikali kuingilia mashirika ya umma kiutendaji na kwamba, historia inaonyesha kila ilipofanya hivyo iliziingiza taasisi hizo kwenye mzozo.

“Serikali iliwahi kuingilia kati na kushawishi Tanesco (Shirika la Umeme Tanzania) kuingia mikataba (ya kuzalisha umeme wa dharura) na Richmond na Dowans na kusababisha mzozo,” alitoa mfano Filikonjombe.

Hivyo, akaonya TIB kuhusu kupokea maagizo holela Serikalini kwa sababu mzigo wa matatizo yatakayotokea, itajiweka kando na kuiachia taasisi hiyo ya umma lawama na vibano kutoka kwa wananchi.

Mapendekezo ya Kamati
Ili kuikoa benki hiyo, Filikunjombe alitoa mapendekezo sita ambayo miongoni mwake ni kuitaka TIB ijitegemee na kufanya kazi zake kama shirika la umme lenye uwezo wa kufanya maamuzi yake ya kiutendaji bila kuingiliwa na wanasiasa serikalini.

“Mhakikishe hamuingiliwi na Wizara ya Fedha au Serikali katika suala la utoaji wa mikopo,” alishauri Filikonjombe.
Mapendekezo mengine ni muundo wa manunuzi katika taasisi yao uendane na sheria ya manunuzi, kuwa ni mikakati ya kushindana kibiashara na benki nyingine na kuhakikisha kuwa mtaji unakua.

Katika hatua nyingine, POAC ilishangazwa kuona kuwa kati ya zaidi ya Sh50 bilioni zilizokusanywa kwenye marejesho ya fedha zilizochotwa EPA, ni Sh20 bilioni pekee zilizoifikia TIB.
Wabunge hao walielezea kushangazwa na kitendo cha Menejimenti ya TIB kupokea fedha hizo tu na kushindwa kuishinikiza Serikali itoe fedha zaidi.

Noni alisema kuwa TIB haikuwa na mamlaka ya kuishinikiza Serikali ili iipatie fedha zote za marejesho ya EPA.
“Sisi tulichopewa ndiyo hicho. Hatukuwa na sababu ya kudai fedha zaidi,” alisema huku akizidi kuzua mtafaruku wa maswali kwa wabunge hao.

Wabunge wengi walionyesha kuamini kuwa fedha zote zilipelekwa TIB baada ya Serikali kuahidi kuwa fedha za marejesho hayo zitapelekwa kwenye shughuli za kilimo.

TIB ndiyo benki iliyoanzishwa na Serikali kwa malengo ya kuinua kilimo nchini ambacho kinategemewa na asilimia 80 ya Watanzania.Wananchi wengi wanaojishughulisha na kilimo nchini ndio wanaogubikwa na wimbi la umasikini kuliko sekta nyingine.

Hata hivyo, Serikali imeamua kuanzisha kampeni ya Kilimo Kwanza, yenye lengo la kufanya sekta hiyo kuwa yenye manufaa na inayoweza kuleta utajiri tofauti na mwonekano wa sasa wa kuwa ni ya kundi la wasio na taaluma.
Taarifa nyingine zilizopatikana jana baada ya kamati hiyo kumaliza kikao chake ni kwamba sehemu ya marejesho ya fedha za EPA, mbali na zile Sh20 bilioni zilizopelekwa TIB, zilitolewa kwa moja kwa moja kwa kampuni za pembejeo za kilimo.

Hata hivyo, baadhi ya wabunge walielezea kutokuwa na imani kama fedha hizo zilitumika kikamilifu kwa ajili ya pembejeo hizo za kilimo.

Mmoja wa wabunge kutoka CCM ambaye hakutaka jina lake kutajwa gazetini alisema kuna uwezekano fedha hizo zimeliwa na wajanja.

“Hata ukiangalia suala la marejesho halikuwekwa wazi, maana Rais (Kikwete) mwenyewe alisema zimekusanywa Sh53 bilioni, mara wengine wakasema 60 bilioni na wengine 70 bilioni.Alisema kama ufisadi uliweza kupenya hadi fedha zilizotolewa kwenye taasisi makini ya benki (TIB) basi hakuna shaka hata zilizotolewa kimyakimya ziliingia kwenye mikono hiyo ya mafisadi.

Hata hivyo, gazeti la serikali liliwahi kumnukuu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Mohamed Muya, akisema katika mgawanyo wa fedha za EPA, wizara hiyo ilipewa Sh40 bilioni ambapo Sh30 bilioni zilitumika kwa ruzuku ya pembejeo ya mbolea hali ambayo imesaidia katika uzalishaji. 



“Kutokana na ruzuku hizi, hata idadi ya wakulima wanaopata vocha za ruzuku hiyo imeongezeka kutoka wakulima 500,000 hadi wakulima milioni 1.5 mwaka huu na kupitia Kamati ya Maafa na ya Usalama wa Chakula, hali ya chakula mwaka huu ni nzuri kuliko mwaka jana,” alisema Muya. 



Alisema katika fedha hizo za EPA, Sh10 bilioni zilizobaki zilitumika katika maeneo matatu ya kilimo ambayo ni Mfuko wa Pembejeo ambao ulipewa Sh3 bilioni, Wakala wa Mbegu wa Taifa Sh1 bilioni na kutatua matatizo ya visumbufu kama vile nzige, kweleakwelea na viwavijeshi Sh6 bilioni.

CHANZO: Mwananchi


Body Dear Friend,

Let this message not surprise you, I am contacting you due to the problem in my family since the problem of my country and the death of my beloved father and my half brother Saif al-Arab who died by NATO air strike.

I am Aisha Gaddafi daughters of Muammar Gaddafi, the embattled president of Libya; I am currently residing in West Africa, unfortunately as a refugee. Our investments and bank accounts in several countries have been freeze by the London.

Insha Allahu, I will make you a part of my family heritage, if you can help me out at this difficult time of my life. All I need from you is for you to open an online account in at least 2 banks, one in Indonesia and the other in Benin Republic. I have accounts with big sums of money in these banks. All you do is to open an online account with these banks and I will transfer all my money to your accounts. I don't want anybody to know about this or my accounts will be freeze. There is an international conspiracy to seize our family accounts/investments around the world.

If you are interested to assist me in this regards kindly get back to me as soon as possible for more details on how to proceed. Needless to say that I will compensate you handsomely once the transfer is effected into your nominated bank account.

Please get back to me for more detail and make sure you keep this issue strictly confidential for my own safety.

Your urgent reply means a lot to me.

Yours sincerely

Aisha Gaddafi

2 Nov 2011


KWA NIABA YANGU BINAFSI NA  WASOMAJI WA BLOGU NINATOA SALAMA NYINGI ZA POLE KWA PRODUCER WA SPORAH SHOWSOPHIA MWANAUTA, KWA MSIBA MKUBWA WA KUONDOKEWA NA MDOGO WAKE MPENDWA.

HAKUNA MANENO MWAFAKA TUNAYOWEZA KUKUPA KATIKA KIPINDI HIKI KIGUMU LAKINI MAANDIKO YANATUFUNDISHA KUWA SOTE NI WAJA WA MUUMBA NA HUTUCHUKUA KATIKA MUDA NA WAKATI ATAKAO YEYE.LAKINI KWA VILE MWENYEZI MUGNU NI MWINGI WA HURUMA NA UPENDO BASI SIO TU ATAWALIWAZA WAFIWA KATIKA KIPINDI HIKI KIGUMU LAKINI PIA ATAMJAALIA MAREHEMU PUMZIKO LA AMANI

YEYE NDIYE MUUMBA,ANAPOMCHUKUA MMOJA WETU NI KWA VILE LICHA YA KUWA TULIMPENDA MAREHEMU LAKINI MOLA ALIMPENDA ZAIDI NA KUAMUA KUMCHUKUA.

POLE SANA SANA SOPHIA.MOLA AKUJAALIE WEWE BINAFSI NA FAMILIA,NDUGU NA JAMAA NGUVU NA MOYO WA KUSTAHILIMILI MAJONZI MLIYONAYO

INNA LILLAHI WA INNA ILAYHI RAJI'UN

من المؤكد أننا ننتمي إلى الله وإنا إليه راجعون يجب

SURELY WE BELONG TO ALLAH AND TO HIM SHALL WE RETURN



Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.