25 Jan 2012


Rais Kikwete amefungua milango

Rais Kikwete msibani kwa Marehemu Mbunge Regia
Rais Kikwete msibani kwa Marehemu Mbunge Regia
KWA mara ya pili ndani ya takriban kipindi cha wiki moja, Tanzania imepoteza wabunge wawili. Kabla majonzi hayajatuisha kutokana na kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalumu kupitia CHADEMA, Regia Mtema, taifa likapatwa na msiba mwingine wa Mbunge wa Arumeru Mashariki kwa tiketi ya CCM, Jeremiah Sumari.
Kila kifo kinaacha pengo lakini kifo cha kiongozi (awe wa familia kama mzazi au wa jamii) kinaacha pengo linalowagusa na kuwaathiri wengi. Japokuwa yayumkinika kuhisi kuwa katika zama hizi za siasa za kuendekeza maslahi kuna wanaofurahi vifo vya viongozi kwa vile vitatoa nafasi ya wao kugombea, ukweli unabaki kuwa ni vigumu kupata mrithi atakayelingana kwa kila kitu na marehemu (hasa katika utekelezaji wa majukumu).
Kama nilivyoandika katika makala ya wiki iliyopita kuhusu kifo cha Regia, njia bora ya kumuenzi marehemu Sumari ni kudumisha mema yote aliyofanya wakati wa uhai wake. Kwa wanaofikiria kumrithi nafasi yake (na kwa atakayeteuliwa kumrithi nafasi ya Marehemu Regia) changamoto kubwa itakuwa kwenye kuwaenzi viongozi hao kwa kuwajibika ipasavyo. Japo utendaji kazi bora wa kiongozi anayerithi madaraka kutoka kwa kiongozi marehemu hauwezi kurejesha uhai, kwa kiasi fulani unasaidia kupunguza machungu ya wananchi walioathiriwa na pengo lililotokana na kifo husika.
Katika mila na desturi za kiafrika, shughuli ya msiba inatawaliwa na majonzi na kwa kiasi kikubwa ni kumbukumbu kwa kila aliyehai kuwa sote “tulitoka kwenye udongo na tutarejea kwenye udongo.” Misiba inapaswa kutukumbusha kuwa sote ni wasafiri na kila nafsi ya mmoja wetu itaonja mauti.
Moja ya matukio yaliyotawala msiba wa Regia ni habari kwamba Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willbroad Slaa, alikwepa kusalimiana na Rais Jakaya Kikwete. Habari hiyo ilichukua uzito mkubwa kiasi cha kukaribia kufunika tukio la huzuni lililowakutanisha viongozi hao huko Ifakara.
Kwa sababu anazozijua mwenyewe, jamaa mmoja aliamua kusambaza waraka katika blogu kadhaa ndani na nje ya nchi kukemea kitendo hicho cha Dk.  Slaa. Mtu huyo ambaye hakufanya jitihada za kuficha itikadi yake ya siasa, akaenda mbali zaidi na kudai kuwa kilichosababisha Katibu Mkuu huyo wa CHADEMA kutosalimiana na Rais ni amri iliyotolewa na mwenza wa Dk. Slaa (Josephine).
Pengine kwa kuelewa kuwa kukalia kimya jambo hilo kungeibua maneno zaidi, hatimaye Dk. Slaa alieleza kilichomfanya ashindwe kusalimiana na Rais Kikwete. Kwa wanaojua protokali, mtu hakurupuki tu na kwenda kusalimiana na kiongozi mkuu wa nchi hasa ikizingatiwa kuwa kumkaribia kiongozi huyo (hata kama ni kwa nia nzuri) kunawafanya walinzi wake watafsiri kama tishio la usalama kwake.
Kadhalika, Dk. Slaa alieleza bayana kuwa kilichompeleka Ifakara ni kumzika Regia na si vinginevyo. Kwa lugha nyingine, alimaanisha kuwa isingehitaji kutokea kifo cha mbunge au kiongozi wa chama ndipo “mahasimu wawili” (kama ‘wazushi’ wa habari hiyo walivyojaribu kutuaminisha) wakutane na kupeana mikono.
Lakini kama kuwasuta wanaokuza matukio madogo, siku chache baadaye vyombo vya habari vilitawaliwa na picha inayomwonyesha Rais Kikwete na Dk. Slaa wakipeana mikono baada ya mazungumzo kati ya Rais na viongozi wa CHADEMA yaliyofanyika Ikulu ya Magogoni, Dar es Salaam.
Sijui waliozusha kuwa Josephine alimkataza Dk. Slaa wanasemaje kuhusu hilo. Labda watazusha kuwa alimtoroka mwenza wake kama sio kuzusha kuwa kiongozi huyo wa CHADEMA aliamua kuambatana na viongozi wenzie Ikulu ili kujisafisha kutokana na tukio la Ifakara.
Inasikitisha kuona mambo ya msingi yakigubikwa na porojo zisizo na mashiko. Binafsi, moja ya mambo ya msingi yaliyonigusa na kunipa matumaini mapya ni jinsi Rais Kikwete na takriban uongozi wake mzima (serikalini na huko CCM) walivyoweza kuweka kando tofauti za kiitikadi na kumzika Regia kama kiongozi wa Watanzania na si mbunge wa CHADEMA pekee.
Mara kadhaa nimekuwa nikishutumiwa kwa kumkosoa au kumlaumu Rais Kikwete. Lakini siku zote nimejitahidi kusisitiza kuwa lawama hizo na kukosoa hakumaanishi chuki au husuda bali ni kwa minajili ya ustawi wa taifa letu.
Natambua kuna uwezekano wa baadhi ya wasomaji kuhisi nimefikia hatua ya kumpongeza Rais Kikwete kwa vile tukio husika linaihusu CHADEMA (ambayo nimekuwa nikituhumiwa kuipendelea na baadhi ya watu, huku wengine wakidai mimi ni mwanachama wa chama hicho.)
Yeyote aliyesoma salamu za rambirambi zilizotolewa na Rais Kikwete kwenda kwa familia ya marehemu Regia na CHADEMA hatoshindwa kubaini kuwa zilikuwa zimetoka moyoni kwa dhati. Hakukuwa na hata chembe ya tofauti za kiitikadi bali hisia za kibinadamu pindi zinapopatikana habari za kifo.
Naomba nisisitize kuwa tukio hilo sio pekee au la kwanza kwa Rais Kikwete kuonyesha kile wanachokiita Waingereza ‘human side’ (ubinadamu wake, kwa tafsiri isiyo rasmi). Mara nyingi mkuu huyo wa nchi ameonyesha kuguswa kwa dhati kila anapokuwa kwenye matukio ya huzuni.
Japo wakati mwingine huishia kulaumiwa kuwa ‘haisaidii kuonyesha uchungu ilhali janga husika lingeweza kuzuilika’ (kwa mfano kwenye matukio ya milipuko ya mabomu huko Mbagala na Gongo la Mboto), hiyo haindoi ukweli kuwa ameguswa na matukio hayo.
Lakini pamoja na pongezi hizi kwa Kikwete na CCM kwa ujumla pengine ni muhimu kukumbushana kuwa kama tunaweza kushikamana wakati wa misiba kwa nini basi iwe vigumu kufanya hivyo nyakati nyingine?
Kwa lugha nyingine, kwa nini tusubiri hadi kiongozi wa chama cha upinzani afariki ndipo tuonyeshe kuwa tofauti za kiitikadi haziondoi ukweli kuwa sote ni Watanzania tunaoweza kutofautiana kimtizamo au kiitikadi pasipo umuhimu wa ‘kuong’oana’ macho.
Japo Kikwete si mahiri katika kuendekeza siasa za uhasama (aidha kwa vile si muumini wa dhana hiyo au anatumia wasaidizi wake kukwepa lawama zinazoweza kuelekezwa kwake), kiujumla chama anachoongoza, yaani CCM, kimekuwa kikifanya jitihada kubwa kuuaminisha umma kuwa vyama vya upinzani ni mithili ya mikusanyiko ya maharamia wasioitakia mema nchi yetu.
Ukisikiliza hotuba za baadhi ya viongozi wa CCM wanapovizungumzia vyama vya upinzani unaweza kabisa kutamani kwenda Idara ya Uhamiaji kuhoji iwapo viongozi hao wa upinzani ni raia halisi wa nchi hii. Hivi haiwezekani kukosoana pasipo kupandikiza chuki ya uadui miongoni mwetu?
Katika tafiti za kitaaluma, kuna hatua ambapo mtafiti huwezi kubashiri matokeo ya utafiti husika kwa kuzingatia dhana alizotengeneza (hypothesis). Japo makala hii si sehemu ya utafiti lakini ningependa kutengeneza dhana kuu mbili zinazoweza kubashiri matokeo fulani.
Ya kwanza, kwa vile Rais Kikwete na CCM wameweza kututhibitishia kuwa tofauti zao za kiitikadi na CHADEMA si za kiadui, na ndio maana wameshiriki kikamilifu katika msiba wa marehemu Regia, Tanzania inaingia kwenye zama mpya za siasa za upendo na kukosoana kistaarabu.
Ya pili, kwa vile siku chache baada ya msiba wa mbunge wa CHADEMA, Rais Kikwete aliwaalika viongozi wa CHADEMA kufanya majadiliano nao, tunaanza kushuhudia ukurasa mpya wa ushirikiano kati ya Rais (na pengine CCM kwa ujumla) katika uongozi wa nchi.
Matokeo yanayotarajiwa ni kwamba badala ya muda mwingi wa ujenzi wa taifa letu kutumika kunyoosheana vidole, kuitana majina ya ajabu ajabu na upuuzi mwingine, sasa tunaweza kuona uongozi wa nchi ukifanya kazi bega kwa bega kwa lengo la kuikomboa Tanzania yetu kutoka katika lindi la umasikini (licha ya rasilimali lukuki tulizojaliwa) na kuunganisha nguvu kukabiliana na kundi la maharamia walioigeuza nchi yetu kuwa ‘shamba la bibi’ kwa ufisadi.
Unaweza kudhani labda aya tatu za hapo juu nimeziandika nikiwa ndotoni. La hasha. Kila nililoandika linawezekana kwani sababu (ya kushirikiana) ipo, na uwezo wa kufanya hivyo upo (kama ilivyothibitika katika tukio hilo la msiba wa marehemu Regia), ila kinachokosekana ni nia tu.
Ni matarajio ya safu hii kuwa Rais Kikwete (ambaye naamini anasoma makala hizi au anasimuliwa na wasaidizi wake) hatorudi nyuma katika kufungua sura mpya ya siasa za maelewano na ushirikiano kwa manufaa na ustawi wa Tanzania yetu. Penye nia pana njia.




Tim Gunn reveals he hasn't had sex in 29 years, but doesn't feel like 'less of a person' for it 

The 'Revolution' host says he's been celibate since the end of a 'very intense relationship'

Wednesday, January 25 2012, 12:10 PM

 Fashion consulant Tim Gunn arrives for the finale of the Bravo TV reality show "Project Runway" at the Tribeca Grand Hotel.

JAMES KEIVOM/NEW YORK DAILY NEWS

Tim Gunn revealed his celibacy Tuesday, but added, 'I don't know what's around the corner.'

Tim Gunn made it very clear Tuesday that nothing will be off limits on his new daytime talk show, "The Revolution" — including himself.
The "Project Runway" mentor opened up about his nearly 30-year sexual dry spell on the show, but said he had nothing to be ashamed of.
"I haven't had sex in 29 years," he revealed. "Do I feel like less of a person for it? No. Not even remotely."
Gunn, 58, explained that a former lover had so scarred him in all matters intimate that he just hasn't had a sexual relationship since.
"I was in a very intense relationship for a long time and my partner ended it, saying quite frankly that he was impatient with my sexual performance," he said. "It was at the cusp of AIDS, and I think a lot of people simply retreated because they were concerned about their health.
"I'm a perfectly fulfilled person ... but it's very psychological," he said.
Gunn, who is openly gay, added that just because he has gone nearly three decades without sex doesn't mean he isn't open to possibilities down the line, however.
"I have feelings. It's not as though I am some barren forest," he said. "I don't want to imply to anyone that I have a mandate that says no sex. I don't know what's around the corner.
"I'm happy to be healthy and alive, quite frankly."
SOURCE: NYDaily News


This summary is not available. Please click here to view the post.

24 Jan 2012


23 Jan 2012



ABOUT THIS PROJECT

"Haba na haba, hujaza kibaba." (Little and little fills the measure) -Tanzanian Proverb
Thank you for visiting our Kickstarter page! The music you heard in the video above is called 'muziki wa dansi', a unique style of music indigenous to Tanzania.
More than 100,000 hours of music like this is sitting idle and all but forgotten on deteriorating reel-to-reel tapes at the headquarters for the Tanzanian Broadcasting Corporation in Dar es Salaam. The Radio Tanzania archives are running out of time and it's our goal to digitize and preserve them before it's too late. Remarkably, our project coincides with the 50th anniversary of Tanzania's independence from colonial rule. It's the perfect time to celebrate Tanzanian culture by preserving and reviving  this treasure of national heritage.
In fact, the music we are determined to protect is the product of Tanzania's struggle for self-determination, cultural identification, and political and economic development after over a hundred years of colonialism and oppression. Tanzania's first president, Julius K. Nyerere, created Radio Tanzania and a Ministry of Culture specifically to encourage musical expression and to promote national unity. There is more than just "musiki wa dansi," too. The archives contain radio dramas, educational programming, field recordings of indigenous tribal music, Congolese-inspired rhumba, and more. You can here additional tracks and read about them here.
I plan to use my own savings (approx. $5,000) to make a preliminary trip to Tanzania to film the 50th anniversary musical celebrations and to begin the digitization. The Kickstarter funds will be used to purchase equipment for the digitization, to pay royalty fees to musicians and the Tanzanian government, and to produce a "Best of Radio Tanzania" compilation CD with extensive liner notes, photographs, and lyric translations. In order to make the digitization sustainable and directly beneficial to the local community, we are going to establish a Radio Tanzania Digitization workshop that will train Tanzanians in the digitization process and will employ locals to run the workshop in our absence.
We also hope to film several short pieces about the archives and the digitization process. Many of the musicians whose work is contained on the reel-to-reels are still alive and making great music. Several of them have expressed interested in being interviewed and filmed performing. Ultimately, we hope to make a film about this music and the story of the archives. Our first priority, however, is to get these reel-to-reels converted so the music is not lost. But we won't be able to do it without you. Thank you for your time and support!
Please visit our website, TanzaniaHeritageProject.org for more information aboutthe archivesour team, and our plan.
Also please check out a sample of some of the music on our Soundcloud account: http://soundcloud.com/user1962241
    ASK A QUESTION
    Have a question? If the info above doesn't help, you can ask the project creator directly.


    22 Jan 2012


    20 Jan 2012



    Unaweza kusema "aah,"kwani wasomaji laki tano ni wengi?Mbona kuna blogu kadhaa zimeshafikisha wasomaji milioni na ushee?" You could say that again,lakini kwangu haya ni mafanikio makubwa.Ni kweli kwamba blogu hii imekuwa hewani kwa takriban miaka 6 sasa,na pengine ingetarajiwa kuwa ingeshakuwa imetembelewa na idadi kubwa zaidi ya wasomaji kuliko hao laki 5 waliokwishatembelea hadi sasa.Ukweli mchungu ni kwamba Watanzania wengi si wapenzi wa habari zisizo za watu binafsi,au zile zisizoambatana na picha za "flani kafanya hiki,kavaa kile,kafumaniwa,kampora flani,nk."

    Kuendesha blogu ya habari,uchambuzi na maoni kunataka moyo hususan iwapo bloga husika anatamani kuona wasomaji wengi wanatembelea blogu yake.Moja ya mambo ninayojivunia ni ukweli kwamba tangu ianzishwe,blogu hii ime-focus kwenye malengo yaleyale ya awali pasipo kushawishika kuingia kwenye nyanja nyingine kwa minajili tu ya kupata wasomaji wengi.Kinachonifariji zaidi ni uwepo la wasomaji waaminifu,yaani watu ambao angalau mara kadhaa kwa wiki ni lazima waipitie blogu hii hata kama haina post mpya.Ninafahamu kuhusu hilo kupitia michanganuo mbalimbali ya takwimu za wasomaji wa blogu inayoonyesha mahali walipo wasomaji  (kwa mfano Google Analytics,Stat Counter,nk).

    Na kwa vile tangu mapema leo asubuhi "kaunta" ilikuwa inaonyesha kila dalili ya kutimia idadi hiyo ya wasomaji,niliamua kuongeza "feature" mpya ambapo sasa msomaji anaweza kuisoma blogu hii katika mionekano (sura) mbalimbali kama zinavyoonyesha picha zifuatazo.

    Mwonekano wa CLASSIC

    Mwonekano wa FLIPCARD

    Mwonekano wa MAGAZINE

    Mwonekano wa MOSAIC

    Mwonekano wa SNAPSHOT

    Mwonekano wa TIMELINE

    Mwonekano wa SIDEBAR
    Ili kwenda kwenye minekano hiyo,cha kufanya ni kubonyeza maandishi  mekundu "yanayotembea" kama inavyoonyesha picha ifuatayo


    Utahamishiwa kwenye ukurasa utakaokupa uchaguzi wa kuamua unataka kuisoma blogu hii kwa mwonekano upi kati ya mionekano iliyotajwa hapo juu.Ukitaka kurejea kwenye mwonekano wa asili wa blogu hii (kama unavyoonekana katika picha ifuatayo),cha kufanya ni kurejesha nyuma ukurasa kwa ku-click kimshale ←
     ambapo utarejeshwa ukurasa wa awali hadi hatimaye kurejea kwenye ukurasa wenye mwonekano wa asili/kawaida wa blogu hii


    NAOMBA KUTOA SHUKRANI NYINGI KWA KILA MMOJA WENU ANAYEKUMBUKA KUTEMBELEA BLOGU HII.NAWASHUKURU PIA WALE WOTE WANAONITUMIA MICHANGO KWA NJIA YA MAONI NA NINAWAKARIBISHA WASOMAJI WOTE KUTUMA MAONI.

    WAKATI TUNAINGIA AWAMU YA PILI KUELEKEA WASOMAJI MILIONI MOJA,NINAPENDA KUWAHAKIKISHIA UBORA WA HALI YA JUU WA CONTENTS NA MWONEKANO WA BLOGU HII,SAMBAMBA NA MAREKEBISHO MBALIMBALI YENYE LENGO LA KUBORESHA BLOGU YENU HII.

    ASANTENI SANA NA MUNGU AWABARIKI


    Dk Slaa: Kwa nini sikumsalimia JK 


    Thursday, 19 January 2012 20:42
    Fredy Azzah 
    KATIBU Mkuu wa Chadema Dk Willibrod Slaa  amesema kuwa, hakuweza kusalimiana na Rais Jakaya Kikwete kutokana na Jiografia ya eneo la makaburini lilivyopangwa na watu wa usalama wa taifa pamoja na kamati ya mazishi kutomruhusu kufanya hivyo.

     
    Hata hivyo Dk Slaa alisisitiza kuwa, kwa upande wake, kwenye msiba siyo sehemu ya kwenda kwa ajili ya kusalimiana na watu ama kurekebisha mambo yaliyoharibika bali ni sehemu ya kumwombea marehemu.

     “Siyo hulka ya Dk Slaa kutumia misiba kama sehemu ya kusalimiana, wala kutengeza mambo yaliyoharibika, mimi huwa naenda kwenye msiba kwa lengo moja tu la kumwombea marehemu, huwa simtazami hata mtu aliyekaa pembeni yangu,” alisema Dk Slaa alipozungumza kwa njia ya simu  jana.  

    Alifafanua kuwa, katika eneo la makaburi kulikuwa na mabanda matano ambayo yalipangwa kwa ajili ya Askofu, Rais, Viongozi wa vyama vya siasa, mwili wa marehemu  na familia na banda jingine lilikuwa la watu wengine waliohudhuria mazishi hayo. 

    “Sasa kutoka alipokuwa amekaa Rais mpaka kwenye banda nilipokuwa mimi, kulikuwa na umbali wa karibu  mita 20, sasa mlitaka nikimbie kumsalimia Rais nivunje protokali kisha nikamatwe na usalama wa taifa,” alisema Dk Slaa. Alisema alikuwa mtu wa kwanza kufika makaburini kwa lengo la kuangalia jinsi kaburi la mbunge wa chama chake lilivyochimbwa kisha akaonyeshwa sehemu ya kukaa na watu wa usalama wa taifa.

     Alisema kuwa, hata katika wakati wa kuaga mwili wa Marehemu Regia Mtema, katika ukumbi wa Karejee, kulikuwa na utaratibu kama huo ambapo ilitengwa sehemu ya kukaa Makamu wa Rais, Spika wa Bunge, Kiongozi wa Kambi ya Upinzani na Makamu wake na yeye Dk Slaa akawekewa sehemu yake kama Katibu wa Chama alichokuwa akikitumika marehemu.

     “Mimi sipendi kuweka siasa kwenye mambo kama ya msiba, Dk Slaa siyo kichaa siyo kichaa aanze kukimbia kumsalimia Rais. Katika sehemu kama ile Rais huwa anakuja baada ya watu wote wakiwa wameshakaa, yeye ndiye hupita na kuanza kusalimia watu na hamjaona hata sehemu moja aliponyoosha mkono kunisalimia nikamkwepa,” alisema Dk Slaa:

     “Msiba siyo mahali pa kutengeza urafiki, au kutengeza mambo yaliyo haribika, pale ni ibada tu na kumuombea marehemu siyo sehemu ya kufanya siasa” alisisitiza Dk Slaa. Jana baadhi ya vyombo vya habari viliripoti kuwa, Dk Slaa alishindwa kusalimiana na Rais Jakaya Kikwete katika mazishi ya Regia Mtema yaliyofanyika kijijini kwao Ipangalala Morogoro juzi.Regia alifariki dunia Januari 14 kwa ajali ya gari iliyotokea katika eneo la Ruvu mkoani Pwani.  


    CHANZO: Mwananchi

    Jasusi ChatBot

    Categories

    Blog Archive

    © Evarist Chahali 2006-2022

    Search Engine Optimization SEO

    Powered by Blogger.