25 Jan 2012

This summary is not available. Please click here to view the post.

24 Jan 2012


23 Jan 2012



ABOUT THIS PROJECT

"Haba na haba, hujaza kibaba." (Little and little fills the measure) -Tanzanian Proverb
Thank you for visiting our Kickstarter page! The music you heard in the video above is called 'muziki wa dansi', a unique style of music indigenous to Tanzania.
More than 100,000 hours of music like this is sitting idle and all but forgotten on deteriorating reel-to-reel tapes at the headquarters for the Tanzanian Broadcasting Corporation in Dar es Salaam. The Radio Tanzania archives are running out of time and it's our goal to digitize and preserve them before it's too late. Remarkably, our project coincides with the 50th anniversary of Tanzania's independence from colonial rule. It's the perfect time to celebrate Tanzanian culture by preserving and reviving  this treasure of national heritage.
In fact, the music we are determined to protect is the product of Tanzania's struggle for self-determination, cultural identification, and political and economic development after over a hundred years of colonialism and oppression. Tanzania's first president, Julius K. Nyerere, created Radio Tanzania and a Ministry of Culture specifically to encourage musical expression and to promote national unity. There is more than just "musiki wa dansi," too. The archives contain radio dramas, educational programming, field recordings of indigenous tribal music, Congolese-inspired rhumba, and more. You can here additional tracks and read about them here.
I plan to use my own savings (approx. $5,000) to make a preliminary trip to Tanzania to film the 50th anniversary musical celebrations and to begin the digitization. The Kickstarter funds will be used to purchase equipment for the digitization, to pay royalty fees to musicians and the Tanzanian government, and to produce a "Best of Radio Tanzania" compilation CD with extensive liner notes, photographs, and lyric translations. In order to make the digitization sustainable and directly beneficial to the local community, we are going to establish a Radio Tanzania Digitization workshop that will train Tanzanians in the digitization process and will employ locals to run the workshop in our absence.
We also hope to film several short pieces about the archives and the digitization process. Many of the musicians whose work is contained on the reel-to-reels are still alive and making great music. Several of them have expressed interested in being interviewed and filmed performing. Ultimately, we hope to make a film about this music and the story of the archives. Our first priority, however, is to get these reel-to-reels converted so the music is not lost. But we won't be able to do it without you. Thank you for your time and support!
Please visit our website, TanzaniaHeritageProject.org for more information aboutthe archivesour team, and our plan.
Also please check out a sample of some of the music on our Soundcloud account: http://soundcloud.com/user1962241
    ASK A QUESTION
    Have a question? If the info above doesn't help, you can ask the project creator directly.


    22 Jan 2012


    20 Jan 2012



    Unaweza kusema "aah,"kwani wasomaji laki tano ni wengi?Mbona kuna blogu kadhaa zimeshafikisha wasomaji milioni na ushee?" You could say that again,lakini kwangu haya ni mafanikio makubwa.Ni kweli kwamba blogu hii imekuwa hewani kwa takriban miaka 6 sasa,na pengine ingetarajiwa kuwa ingeshakuwa imetembelewa na idadi kubwa zaidi ya wasomaji kuliko hao laki 5 waliokwishatembelea hadi sasa.Ukweli mchungu ni kwamba Watanzania wengi si wapenzi wa habari zisizo za watu binafsi,au zile zisizoambatana na picha za "flani kafanya hiki,kavaa kile,kafumaniwa,kampora flani,nk."

    Kuendesha blogu ya habari,uchambuzi na maoni kunataka moyo hususan iwapo bloga husika anatamani kuona wasomaji wengi wanatembelea blogu yake.Moja ya mambo ninayojivunia ni ukweli kwamba tangu ianzishwe,blogu hii ime-focus kwenye malengo yaleyale ya awali pasipo kushawishika kuingia kwenye nyanja nyingine kwa minajili tu ya kupata wasomaji wengi.Kinachonifariji zaidi ni uwepo la wasomaji waaminifu,yaani watu ambao angalau mara kadhaa kwa wiki ni lazima waipitie blogu hii hata kama haina post mpya.Ninafahamu kuhusu hilo kupitia michanganuo mbalimbali ya takwimu za wasomaji wa blogu inayoonyesha mahali walipo wasomaji  (kwa mfano Google Analytics,Stat Counter,nk).

    Na kwa vile tangu mapema leo asubuhi "kaunta" ilikuwa inaonyesha kila dalili ya kutimia idadi hiyo ya wasomaji,niliamua kuongeza "feature" mpya ambapo sasa msomaji anaweza kuisoma blogu hii katika mionekano (sura) mbalimbali kama zinavyoonyesha picha zifuatazo.

    Mwonekano wa CLASSIC

    Mwonekano wa FLIPCARD

    Mwonekano wa MAGAZINE

    Mwonekano wa MOSAIC

    Mwonekano wa SNAPSHOT

    Mwonekano wa TIMELINE

    Mwonekano wa SIDEBAR
    Ili kwenda kwenye minekano hiyo,cha kufanya ni kubonyeza maandishi  mekundu "yanayotembea" kama inavyoonyesha picha ifuatayo


    Utahamishiwa kwenye ukurasa utakaokupa uchaguzi wa kuamua unataka kuisoma blogu hii kwa mwonekano upi kati ya mionekano iliyotajwa hapo juu.Ukitaka kurejea kwenye mwonekano wa asili wa blogu hii (kama unavyoonekana katika picha ifuatayo),cha kufanya ni kurejesha nyuma ukurasa kwa ku-click kimshale ←
     ambapo utarejeshwa ukurasa wa awali hadi hatimaye kurejea kwenye ukurasa wenye mwonekano wa asili/kawaida wa blogu hii


    NAOMBA KUTOA SHUKRANI NYINGI KWA KILA MMOJA WENU ANAYEKUMBUKA KUTEMBELEA BLOGU HII.NAWASHUKURU PIA WALE WOTE WANAONITUMIA MICHANGO KWA NJIA YA MAONI NA NINAWAKARIBISHA WASOMAJI WOTE KUTUMA MAONI.

    WAKATI TUNAINGIA AWAMU YA PILI KUELEKEA WASOMAJI MILIONI MOJA,NINAPENDA KUWAHAKIKISHIA UBORA WA HALI YA JUU WA CONTENTS NA MWONEKANO WA BLOGU HII,SAMBAMBA NA MAREKEBISHO MBALIMBALI YENYE LENGO LA KUBORESHA BLOGU YENU HII.

    ASANTENI SANA NA MUNGU AWABARIKI


    Dk Slaa: Kwa nini sikumsalimia JK 


    Thursday, 19 January 2012 20:42
    Fredy Azzah 
    KATIBU Mkuu wa Chadema Dk Willibrod Slaa  amesema kuwa, hakuweza kusalimiana na Rais Jakaya Kikwete kutokana na Jiografia ya eneo la makaburini lilivyopangwa na watu wa usalama wa taifa pamoja na kamati ya mazishi kutomruhusu kufanya hivyo.

     
    Hata hivyo Dk Slaa alisisitiza kuwa, kwa upande wake, kwenye msiba siyo sehemu ya kwenda kwa ajili ya kusalimiana na watu ama kurekebisha mambo yaliyoharibika bali ni sehemu ya kumwombea marehemu.

     “Siyo hulka ya Dk Slaa kutumia misiba kama sehemu ya kusalimiana, wala kutengeza mambo yaliyoharibika, mimi huwa naenda kwenye msiba kwa lengo moja tu la kumwombea marehemu, huwa simtazami hata mtu aliyekaa pembeni yangu,” alisema Dk Slaa alipozungumza kwa njia ya simu  jana.  

    Alifafanua kuwa, katika eneo la makaburi kulikuwa na mabanda matano ambayo yalipangwa kwa ajili ya Askofu, Rais, Viongozi wa vyama vya siasa, mwili wa marehemu  na familia na banda jingine lilikuwa la watu wengine waliohudhuria mazishi hayo. 

    “Sasa kutoka alipokuwa amekaa Rais mpaka kwenye banda nilipokuwa mimi, kulikuwa na umbali wa karibu  mita 20, sasa mlitaka nikimbie kumsalimia Rais nivunje protokali kisha nikamatwe na usalama wa taifa,” alisema Dk Slaa. Alisema alikuwa mtu wa kwanza kufika makaburini kwa lengo la kuangalia jinsi kaburi la mbunge wa chama chake lilivyochimbwa kisha akaonyeshwa sehemu ya kukaa na watu wa usalama wa taifa.

     Alisema kuwa, hata katika wakati wa kuaga mwili wa Marehemu Regia Mtema, katika ukumbi wa Karejee, kulikuwa na utaratibu kama huo ambapo ilitengwa sehemu ya kukaa Makamu wa Rais, Spika wa Bunge, Kiongozi wa Kambi ya Upinzani na Makamu wake na yeye Dk Slaa akawekewa sehemu yake kama Katibu wa Chama alichokuwa akikitumika marehemu.

     “Mimi sipendi kuweka siasa kwenye mambo kama ya msiba, Dk Slaa siyo kichaa siyo kichaa aanze kukimbia kumsalimia Rais. Katika sehemu kama ile Rais huwa anakuja baada ya watu wote wakiwa wameshakaa, yeye ndiye hupita na kuanza kusalimia watu na hamjaona hata sehemu moja aliponyoosha mkono kunisalimia nikamkwepa,” alisema Dk Slaa:

     “Msiba siyo mahali pa kutengeza urafiki, au kutengeza mambo yaliyo haribika, pale ni ibada tu na kumuombea marehemu siyo sehemu ya kufanya siasa” alisisitiza Dk Slaa. Jana baadhi ya vyombo vya habari viliripoti kuwa, Dk Slaa alishindwa kusalimiana na Rais Jakaya Kikwete katika mazishi ya Regia Mtema yaliyofanyika kijijini kwao Ipangalala Morogoro juzi.Regia alifariki dunia Januari 14 kwa ajali ya gari iliyotokea katika eneo la Ruvu mkoani Pwani.  


    CHANZO: Mwananchi

    19 Jan 2012







    Kwa nini Lowassa na mabilioni yake makanisani ahofie nguvu ya umma?

    NIANZE makala hii kwa kuwasilisha salamu za rambirambi kufuatia kifo cha Mbunge wa Viti Maalumu (CHADEMA), Regia Mtema. Nilishitushwa sana nilipopata taarifa za kifo chake kupitia mtandao wa Twitter hasa kwa vile siku chache tu zilizopita nilisoma bandiko lake moja katika ukumbi wa majadiliano wa mtandao wa Jamii Forums.
    Japo nilikuwa sifahamiani naye lakini nilijisikia faraja sana kuona “mwana wa pakaya” (mtoto wa nyumbani) mwenzangu anavyofanya sie wazaliwa wa Wilaya ya Kilombero tujisikie ufahari.
    Moja ya mambo magumu kabisa maishani ni kusema maneno yanayojitosheleza kwa wafiwa. Lakini hiyo si sababu ya kutosema japo machache yanayoweza kuifariji familia ya marehemu Regia, wana Kilombero, viongozi na wanachama wa CHADEMA na Watanzania kwa ujumla.
    Tulimpenda Regia lakini Mwenyezi Mungu alimpenda zaidi na kwa vile ndiye aliyemuumba basi ameamua kumchukua. Kwa waumini, tunachoweza kufanya ni kuiombea roho ya marehemu, na sote kwa ujumla tunaweza kumuenzi vizuri zaidi mbunge huyo shupavu kwa kutekeleza yale yote aliyosimamia na kupigania.
    Pengine mwenye changamoto zaidi kutokana na kifo hiki cha ghafla ni Mbunge wa Jimbo la Kilombero kupitia CCM, Abdul Mteketa. Kuna mengi ambayo dada yetu Regia alikuwa akipigania kwa ajili ya ustawi wa Jimbo la Kilombero (sambamba na maeneo mengine nchini kutokana na ubunge wa viti maalumu kumfanya kuwa mithili ya ‘mbunge wa kila jimbo’).
    Kama Rais Jakaya Kikwete alivyoonyesha mfano kwa kuweka pembeni itikadi za kisiasa wakati anatoa salamu za rambirambi za kifo cha mbunge huyo, Mteketa naye anaweza kuweka kando tofauti kati ya chama chake CCM na CHADEMA na kuendeleza yale yote yaliyoanzishwa na mbunge mwenzie (ambaye walipambana kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010).
    Hiyo si tu itakuwa namna bora zaidi ya kuomboleza kifo hicho bali pia kuwasaidia wana-Kilombero ambao kwa hakika wamepoteza tunu na lulu muhimu kwa jimbo hilo.
    Baada ya salamu hizo naomba kugeukia kauli ya hivi karibuni ya aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, ambaye alizungumzia kuhusu matumizi ya nguvu za umma kuishinikiza mambo mbalimbali.
    Kasoro ya kwanza katika kauli hiyo ya Lowassa aliyoitoa katika harambee ya kuchangia ujenzi wa shule ya sekondari ya kanisa la FCTP huko Bigabiro, mkoani Kigoma, ni kuyaeleza matumizi hayo ya nguvu za umma kuwa yanaendeshwa na baadhi ya vyama fulani. Japo hakutaja jina la chama lakini ni wazi alikuwa anailenga CHADEMA.
    Kwa nini Lowassa hayuko sahihi katika hili? Hivi chama kisicho na dola kama CHADEMA kinawezaje kulazimisha utashi wa wananchi kushiriki kwenye harakati hizo? Kumshawishi mlalahoi akatishe siku yake shambani akahudhurie maandamano yanayokihusisha chama cha siasa ni suala gumu mara kadhaa ya urahisi alionao Lowassa kuwakusanya marafiki zake matajiri kumwaga fedha kwenye harambee zao.
    Binafsi, ninaitafsiri kauli hiyo ya Lowassa kama dharau kubwa kwa wanyonge wanaolazimika kutumia nguvu ya sauti yao kudai stahili zao.
    Hivi Lowassa anadhani wananchi wanaojitokeza kwenye maandamano au harakati nyingine kushinikiza masuala mbalimbali wanafanya hivyo kama anasa, hasa ikizingatiwa kuwa wanafahamu fika uwezekano wa kulala rumande kama si kufunguliwa mashtaka pindi Jeshi la Polisi likijisikia kuwanyanyasa?
    Tunaweza kumhurumia Lowassa katika hili kwa vile sidhani kama ameshawahi kulazimika kutumia nguvu kudai haki yake. Yeye ni miongoni mwa kikundi kidogo cha wateule wachache ambao miaka nenda miaka rudi wapo madarakani, huku mahitaji yake yakishughulikiwa na wasaidizi wake.
    Raha ya kuwa na wasaidizi, wapambe na watoa huduma ni kwamba kwa kiasi kikubwa jukumu la kuhakikisha kila jambo lipo sawa kwa ‘bosi’ linakuwa mikononi mwa watu hao.
    Katika hotuba yake kwenye harambee hiyo Lowassa alikaririwa akidai (namnukuu) “Nguvu ya umma tunayoshuhudia kwenye maandamano ya baadhi ya vyama vyetu, ingekuwa inatumika kwa kiwango kile kile kufanya kazi za kujitolea kwenye miradi ya maendeleo kama ujenzi wa sekondari zetu, hakika taifa lingepiga hatua kubwa ya maendeleo, lakini linapokuja suala la kufanya kazi nguvu ya umma hutoweka.”
    Kwa lugha nyingine Lowassa anahitimisha kuwa mahala pekee ambapo nguvu ya umma inatumika ni kwenye maandamano ya baadhi ya vyama vyetu. Huyu ndiye ambaye licha ya kuwa Waziri Mkuu huko nyuma ameshika nafasi kadhaa za uongozi serikalini na ndani ya CCM kwa miaka kadhaa.
    Je, ni kweli hajawahi kuona nguvu inayotumika na Watanzania kujiletea maendeleo yao licha ya kukwazwa na majambazi wanaotumia fursa zao kuwafisadi?
    Moja ya mambo yanayotufanya Watanzania tuendelee kumlilia Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere ni jinsi alivyotuunganisha bila kutumia dini au urafiki na matajiri kuhamasisha maendeleo ya jamii na nchi yetu kwa ujumla.
    Nyerere alitambua umuhimu wa nguvu ya umma katika kuleta mabadiliko yanayokusudiwa hususan kukiwa na usimamizi mzuri usioambatana na maslahi binafsi.
    Uhuru wetu kutoka kwa mkoloni ulipatikana kutokana na wanyonge wa Tanganyika kuchoshwa kunyanyaswa na kukandamizwa na wakoloni na kuunganisha nguvu zao wakihamasishwa na Nyerere na wapigania uhuru wenzie na hatimaye tukapata uhuru wetu. Leo hii Lowassa anabeza harakati zenye mwelekeo kama huo.
    Historia imetuonyesha jinsi nguvu ya umma ilivyoweza kuangusha tawala mbalimbali za kidhalimu, mifano mizuri ikiwa ni huko Afrika Kusini walivyopambana na utawala wa makaburu na Ulaya ya Mashariki walivyokabiliana na udikteta wa kikomunisti.
    Na hivi karibuni tumeshuhudia nguvu ya umma ikiwang’oa madikteta Hosni Mubarak wa Misri, Ben Ali wa Tunisia na Muammar Gaddafi wa Libya.
    Lakini kwa kile kinachoweza kutafsiriwa kama unafiki wa Lowassa ni ukweli kwamba yeye alikuwa miongoni mwa waliopongeza nguvu za umma nchini Misri huku akishauri watawala wetu kujifunza katika kilichojiri nchini humo. Ikumbukwe kuwa harakati za Misri zililenga zaidi kuutokomeza utawala wa kidikteta wa Mubarak ilhali nguvu ya umma huko nyumbani imeelemea zaidi kwenye kudai haki za msingi sambamba na kukemea maovu, hususan ufisadi. Sijawahi kusikia kuwepo kwa maandamano yenye wito wa kumng’oa Rais Kikwete madarakani kwani kwa mujibu wa sheria zetu kufanya hivyo ni uhaini pasipo mjadala.
    Lakini licha ya kupongeza nguvu za umma huko Misri, ingekuwa miujiza kwa Lowassa kuunga mkono harakati kama hizo huko nyumbani kwani yeye ni miongoni mwa waathirika wake. Nguvu ya umma ikihamasishwa na CHADEMA ilimtaja mwanasiasa huyo kwenye orodha ya mafisadi (list of shame) na hadi leo hajachukua hatua za kisheria kudai amekashifiwa.
    Tukiweka kando kauli hiyo ya Lowassa, labda tujiulize kidogo kuhusu hayo mamilioni yanayochangwa na marafiki zake kwenye hafla mbalimbali makanisani. Hivi Watanzania wenzetu hao wenye uwezo wa kutoa sadaka za mamilioni wanatoa wapi fedha hizo?
    Na katika hili ninayalaumu sana makanisa yanayoweka mbele fedha pasipo kujiuliza fedha hizo zinazomwagwa kwao zinatoka wapi.
    Wakati wa uhai wake, Baba wa Taifa alionyesha upinzani mkubwa kwa wanasiasa wenye utajiri wa kupindukia lakini usio na maelezo ya kutosheleza. Ifahamike kuwa utajiri si dhambi iwapo umepatikana kihalali.
    Lakini kila mwenye uelewa anaweza kupatwa na wasiwasi kuona mwanasiasa mmoja akizunguka huku na kule kumwaga mamilioni ya shilingi makanisani. Huyu mtu ana fedha kiasi gani? Amepata wapi?
    Jingine ambalo pengine ni muhimu zaidi kwa Watanzania hasa wakati tunaelekea kwenye mchakato wa Uchaguzi ujao mwaka 2015 ni hadhari iliyotolewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa, Bernard Membe kuhusu wanasiasa wanaotumia nyumba za ibada kujisafisha.
    Waziri Membe alisema amani ya taifa imo shakani kama viongozi wa kidini wataruhusu nyumba za ibada kuwa kimbilio la wanasiasa na wao kutumika katika kuwasafisha, hali hiyo inaweza kusababisha mgawanyiko katika jamii.
    Lowassa kama muumini yeyote yule ana uhuru wa kutoa michango ya fedha nyingi na marafiki zake matajiri. Kadhalika, ni haki yake ya kikatiba kuongea lolote lile alimradi havunji sheria za nchi. Sasa kama yeye ana uhuru wa kumwaga mamilioni makanisani na kukemea walalahoi wanaotumia nguvu ya umma kushinikiza mambo mbalimbali, kwa nini basi asitambue kuwa walalahoi hao wanaotumia haki hiyo hiyo anayotumia yeye?
    Wanasema uhuru bila nidhamu ni uhuni, na kwa msingi huo japo ninatambua uhuru alionao Lowassa kuzungumzia masuala ya kisiasa kwenye nyumba za ibada, uhuru huo unaweza kuwa na madhara makubwa katika taifa letu. Kama walalahoi anaowakemea Lowassa ni werevu na wanafanya harakati zao nje ya nyumba za ibada basi ni vema wanasiasa wetu nao wakaepuka kugeuza sehemu hizo takatifu kuwa majukwaa ya kisiasa.
    Nimalizie kwa nukuu hii kutoka kwa Waziri Membe; “Kuweni macho na wanasiasa wanaokimbilia kwenu (viongozi wa dini), msikubali kutumiwa kwa kulinda maslahi ya wanasiasa, fanyeni kazi zenu za kuwajenga waumini wenu kwa mujibu wa mafundisho ya imani zenu, mkiruhusu kutumiwa na wanasiasa amani ya nchi mtaivuruga.”




    Kwanza Tunapenda wasalimu wakubwa wetu Shikamoo na vijana wenzetu Mambo vipi..  Tunatambua kuwa Wanavyuo wenzetu walimu walikuwa hawana kazi kwa muda mrefu Jambo ambalo liliwafanya wengi kuwa na wasi wasi na mwajiri wao. Tunapenda kuwapa tarifa kupitia mtandao wenu wa Matukio na wanavyuo (www.tzwanavyuo.blogspot.com)  kuwa, Walimu wahitimu wote  Jana usiku majira ya sa saba Nafasi hizo zilitangazwa Rasmi, Pia sisi Tunapenda kuwasilisha majina ya wanafunzi ambao wamechaguliwa Tunaomba mchukue Muda wenu kutazama kwa umakini majina yenu yote yapo hapa. Hongereni sana.


    Imeandaliwa na,
    Matukio na Wanavyuo Crew 

    18 Jan 2012













    Picha zote kwa hisani ya Jamii Forums

    Jasusi ChatBot

    Categories

    Blog Archive

    © Evarist Chahali 2006-2022

    Search Engine Optimization SEO

    Powered by Blogger.