Showing posts with label January Makamba. Show all posts
Showing posts with label January Makamba. Show all posts

11 Dec 2015

Julai 8 mwaka huu itabaki moja ya siku zenye kumbukumbu chungu maishani mwangu. Ni siku ambayo baba yangu mzazi, Mzee Philemon Chahali alifariki dunia baada ya kuugua kama kwa wiki hivi.  Japo miaka 7 kabla ya hapo nilikumbwa na msiba mwingine ambapo mama yangu mepndwa, Adelina Mapango, alifariki baada ya kupoteza fahamu kwa zaidi ya miezi mitano, na japo hakuna msiba wenye nafuu, lakini angalau marehemu mama alifariki nikiwa huo Tanzania nilikoenda kumuuguza.  Lakini katika kifo cha baba, kilitokea nikiwa mbali na nyumbani. Na kwa hakika, nyakati za misiba, tunahitaji mno sapoti ya wenzetu kutuliwaza na kukabiliana na uchungu wa kufiwa.

Kwanini ninarejea habari hiyo ya kuskitisha? Kwa sababu tukio hilo ndilo lilinipa nafasi ya kumfahamu vema zaidi mmoja wa wanasiasa maarufu nchini Tanzania, January Makamba, Mbunge wa CCM Bumbuli na mmoja wa makada zaidi ya 40 waliojitokeza kuwania Urais kupitia CCM, na alifanikiwa kuingia katika 'Tano Bora.'

Mara baada ya kutangaza kuwa nimefiwa, January alinipigia simu kunipa pole, na kuulizia jinsi ya kuwasilisha rambirambi yake, ambayo baadaye aliiwasilisha. Pengine kwa watu wengine wanaweza kuliona hili kama ni jambo dogo tu na la kawaida. Lakini kimsingi, sote twafahamu viongozi wetu walivyo busy na majukumu yao, ambayo kwa kiasi kikubwa huwafanya waonekane kama binadamu wasiofikika (inaccessible). Kwa Afrika, ni vigumu sana kukuta kiongozi awe wa kisiasa au kwenye sekta nyingine akiwa karibu na raia wa kawaida, au kufuatilia yanayowasibu. Na kwa wanaomfahamu, amekuwa akiwasaidia watu wengi waliofiwa na wenye matatizo mbalimbali, at least ninaowafamu mie mtandaoni. Ni wazi mtu akiwa mwema kwa watu mtandaoni lazima pia ni mwema katika maisha yake nje ya mtandao.

Nimeanza makala hii na suala hilo binafsi kwa sababu ndilo lililonipa fursa ya kumfahamu kwa karibu zaidi. Awali nilimfahamu kama mwanasiasa kijana aliye karibu na watu wengi, hususan mitandaoni, lakini sikujua 'human side' (utu) yake. 

Tukiweka hilo kando, katika siasa za hivi karibuni za Tanzania, January alikuwa mwanasiasa wa kwanza kabisa kutangaza azma yake ya kuwania urais mwaka huu. Alitoa nia yake takriban mwaka mzima kabla ya kuanza rasmi kwa mchakato huo. Wengi walipokea tamko lake hilo, hasa kwa matarajio kuwa lingewashawishi wanasiasa wengine waliokuwa wanawania nafasi hiyo kujitokeza, na hiyo ingesaidia kuwafahamu vizuri. Kwa hiyo, kwa kifupi, January ndiye aliyepuliza rasmi kipenga cha kuwania urais wa awamu ya tano/

Wakati ukaribu wa mwanasiasa huyo kijana na wananchi, hususan katika mitandao ya kijamii ilikuwa ni turufu yake muhimu, moja ya downsides za kufahamiana na watu wengi ni uwezekano wa baadhi ya 'wakorofi' kujipa uhuru wa kusema chochote kile hata isipostahili. Na katika hili, January alikumbana na mengi: wapo waliomdhihaki wakiona dhamira yake ya urais kama ndoto tu, kashfa zisizostahili, nk. Hata hivyo, mara zote alimudu kuwajibu 'wapinzani' wake kwa lugha ya kistaarabu.

Baadaye alichapisha kitabu chake kilichokuwa na visheni yake ya urais. Again, kitabu hicho kilipokelewa kwa mtizamo chanya na Watanzania wengi japo kulikuwa na kundi dogo 'waliokiponda.' Kimsingi, kitabu hicho kilikuwa na masuala mengi ya msingi kuhusu matatizo ya Tanzania yetu na mikakati ya kuyakabili. Kwahiyo, kinaweza kabisa kuwasaidia watu mbalimbali wanaotaka kuifahamu vema nchi yetu.

Mchakato wa CCM kumpata mgombea wake ulipoanza rasmi, January aliibuka kuwa mwanasiasa pekee tishio kwa Edward Lowassa, kada amabye alitajwa kuutaka urais kwa miaka kadhaa. Tofauti na Lowassa ambaye umaarufu wake ulichangiwa zaidi na uwezo wake wa kifedha, mafanikio ya January katika kampeni yake yalichangiwa zaidi na ukaribu wake kwa watu, hususan vijana.

Na japo hakufanikiwa kupitishwa kuwa mgombea urais kwa tiketi ya CCM, kuingia kwake kwenye 'Tano Bora' ni mafaniko makubwa kabisa, hasa ikizingatiwa kuwa bado ni kijana anayeweza kuyatumia mafanikio yake ya mwaka huu katika chaguzi zijazo. Yayumkinika kuhitimisha kuwa mwanasiasa pekee ambaye mpaka muda huu anatajwa kuwa rais ajaye wa Tanzania baada ya Magufuli ni January.

Baada ya Magufuli kushinda urais, zikaanza tetesi kuwa 'January anataka Uwaziri Mkuu.' Ni muhimu kukumbuka kuwa katika muda mwingi wa harakati zake za kisiasa, mwanasiasa huyo amekuwa akiandamwa na 'wasemaji wasio rasmi' wanaojifanya kumjua zaidi ya anavyojijua mwenyewe. Hakuna wakati au mahali popote ambapo January alisema ana matarajio ya kuwa Waziri Mkuu. Ni hisia tu za watu - waliomtakia mema kutokana na mchango wake mkubwa katika kampeni za CCM katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu, na 'wabaya' wake ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakimzushia vitu mbalimbali.

Rais Magufuli alipomtangaza Kassim Majaliwa kuwa Waziri Mkuu, yakazuka maneno kuwa 'January kakosa Uwaziri Mkuu,' kana kwamba alitangaza kuwa anawania au anatarajia nafasi hiyo. 

Baada ya kitendawili cha uwaziri mkuu kuteguliwa, likabaki fumbo la baraza la mawaziri. Hapo napo yakazuka maneno chungu mbovu. January akapangiwa Wizara kadhaa na 'wanaomjua zaidi ya anavyojijua mwenyewe.' Lakini kuna waliodiriki kuweka 'chuki' zao hadharani na kuombea asiwemo kabisa katika baraza jipya la mawaziri. Ukiwauliza 'kwa lipi alilowakosea,' nina hakika hawana jibu.

Jana baraza likatangazwa. Na January akapanda kutoka Unaibu Waziri katika Awamu iliyopita na kuwa Waziri Kamili. Haya ni mafanikio makubwa kwa mwanasiasa kijana kama yeye. Kama kazini, hiyo ni promosheni, kutoka unaibu waziri hadi uwaziri kamili. Lakini kwa vile 'wabaya' wake walishampangia wizara, January kupewa Uwaziri katika ofisi ya Makamu wa Rais - Muungano na Mazingira imetafsiriwa nao kama 'amepewa kitu pungufu.' Jamani, mtendeeni haki mwanasiasa huyu. Pungufu kivipi ilhali kiukweli amepandishwa cheo kutoka unaibu waziri hadi kuwa waziri kamili?

Jana nilitwiti matarajio yangu kwa January katika nafasi hiyo mpya, na ninashukuru mapokeo yalikuwa mzuri. Maeneo mawili ya majukumu yake ya kiuwaziri ni muhimu sana, na nina hakika atawashangaza wengi. Kwa upande wa Muungano, sote twaelewa hali ya kisiasa ilivyo huko Zanzibar. Kwahiyo, kwa nafasi yake, January anatarajiwa ku-play role muhimu katika jitihada za kutafuta suluhisho la mgogoro wa kisiasa visiwani humo. Lakini licha ya mgogoro huo, moja ya vitu vinavyotishia ustawi wa Muungano wake ni kero zake za muda mrefu. Kwa vile Janaury ni msomi katika tasnia ya usuluhishi wa migogoro (confilict resolution), na kutokana na profile yake kubwa kimataifa, ninatarajia kuwa ataweza kuyashughulikia masuala yote mawili kwa ufanisi mkubwa.

Na katika suala la mgogoro wa kisiasa huko Zanzibar, hali ya 'ubinadamu' kwa maana ya utu au 'humani side' ya January itakuwa na umuhimu wa kipekee. Migogoro ya aina hiyo inahitaji mtu mwelewa, mtulivu, na mwenye busara, sifa ambazo January anazo. Kuweza kuwashawishi Wazanzibari waweke maslahi ya taifa mbele ya maslahi ya vyama vyao kunahitaji mtu ambaye anapoongea anaonekana kama ndugu au rafiki na si mwanasiasa au kiongozi flani. Kwa kifupi, human side ya mpatanishi ni muhimu mno katika tasnia ya utatuzi wa migogoro.

Lakini kama kuna eneo ambalo ninatarajia makubwa zaidi kutoka kwa mwanasiasa huyo ni MAZINGIRA. Moja ya masuala muhimu kabisa dunain kwa sasa ni masuala ya mazingira. Japo kwa Afrika, masuala hayo hayazungumziwi sana japo bara hilo ndilo lililo hatarini zaidi kimazingira, hususan kutokana na matatizo ya kiuchumi na umasikini, Mijadala mbalimbali muhimu inayoendelea duniani kwa sasa nipamoja na kuhusu masuala ya mazingira. Kubwa zaidi ni suala la global warming ambalo wanasayansi wanatahadharisha kuwa lisiposhughulikiwa kikamilifu linaweza kupelekea kuangamia kwa sayari yetu.

Kwa nchi masikini kama Tanzania, masuala ya mazingira yana umuhimu wa kipekee (japo hayazungumziwi inavyostahili) kwa sababu kama tunakwama katika kukabiliana na matatizo yaliyo katika uwezo wa kibinadamu, hali inakuwaje tunapokabiliwa na matatizo ya kiasili (natural) yaliyo nje ya uwezo wa kibinadamu?

Kwa upeo mkubwa alionao na uhodari wake wa kuwasilisha hoja, sintoshangaa kuona huko mbeleni January akitokea kuwa mmoja wa watu muhimu duniani katika masuala ya mazingira. Na uzuri ni kwamba ameingia katika wizara inayishughulikia masuala hayo wakati ambapo jina la Tanzania limeanza kuvuma kwa uzuri kutokana na sifa za uchapakazi wa Rais Magufuli.

Ninasema pasi hofu kuwa sintoshangaa miaka michache ijayo tukashuhudia kwa mara ya kwanza Tanzania ikitoa mshindi wa Tuzo ya Nobel aidha katika usuluhishi wa mgogoro wa Zanzibar au masuala ya mazingira, au hata yeye kuchaguliwa kuwa Mtu wa Mwaka wa jarida la kimataifa la TIME la Marekani (TIME's Person of the Year). 

Nimalizie kwa kueleza kuwa lengo la makala hii ni kuweka sawa kumbukumbu kuhusu watu muhimu katika tanzania yetu, kama January, kwa mahitaji ya sasa na huko mbeleni. Kma taifa, tunakabiliwa na mapungufu makubwa ya uhifadhi wa kumbukumbu. Na japo mie si mbashiri, natumaini kuna siku makala hii itatumika kama reference baada ya 'January kuishangaza dunia' katika eneo fulani. 

Mwisho, ninawatakia kila la heri mawaziri wote walioteuliwa na Rais Magufuli katika kabineti yake mpya, nikiwa na matumaini makubwa kuwa wataendana na kasi yake ya uchapakazi na hivyo kutupatia Tanzania tunayostahili. 

Nawatakia siku njema.



21 Oct 2015



Sababu Tisa kwanini CCM itashinda katika Uchaguzi Mkuu Jumapili hii, Oktoba 25

Na January Makamba

Tarehe 25 mwezi huu Oktoba, Watanzania watapiga kura kumchagua rais wao wa tano, wabunge na madiwani. Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu umekuwa na msisimko mkubwa zaidi tangu kuanzishwa kwa mfumo wa siasa za vyama vingi mwaka 1995. Mengi yamendikwa kuhusu uchaguzi huu, hususan kutokana na hisia kwamba safari hii Upinzani una nafasi ya kukiondoa madarakani moja ya vyama vikubwa na vyenye muundo bora barani Afrika, chama tawala, Chama Cha Mapinduzi (CCM). Matukio mbalimbali kuelekea uchaguzi huo yameleta shauku inayoweza kutengeneza hadithi ya kusisimua.

Nikiwa sehemu ya Timu ya Kampeni ya CCM,na kwa manufaa ya wote ambao wangependa kuwa na mtizamo tofauti, ninatoa sababu 9 kwanini tunaamini kuwa CCM itaibuka mshindi na kwanini Dkt John Pombe Magufuli atakuwa Rais ajaye wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

1.    Ugombea ‘fyongo’ (flawed) wa Edward Lowassa

Ilishabainika kuwa uchaguzi huu ungekuwa mgumu kwa CCM bila kujali nani angekuwa mgombea urais kwa tiketi ya Upinzani. Lakini matokeo ya uchaguzi huu yalielemea upande wa CCM pale Upinzani ulipomchagua Lowassa kuwa mgombea wao. Ni rahisi kwa CCM kuchuana na Lowassa kuliko laiti mgombea wa Upinzani angekuwa Dkt Wilbrod Slaa, ambaye ndiye aliandaliwa kuwa mgombea kabla ya ‘ukusukumwa kando’ na nafasi hiyo kupewa Lowassa. Slaa alikuwa na uadilifu katika maeneo mengi, na aliaminika. Kwa Lowassa, ni vigumu na inanyima raha kuchuana na mfumo aliyoshiriki kujenga na ambao ulikuwa sehemu ya maisha yake hadi Agosti mwaka huu alipohamia Upinzani. CCM ilikuwa na nafasi ya kumpitisha Lowassa kuwa mgombea wake wa nafasi ya urais. Hatukufanya hivyo kwa sababu rahisi tu kwamba ingekuwa vigumu mno kumkabidhi kwa wananchi mgombea wa matarajio ya baadaye ambaye ni kiashirio cha yale yasiyowaridhisha wananchi kuhusu CCM. Kuna wanaoamini kuwa uchaguzi huu ni mgumu kwa vile Lowassa ndiye mgombea wa Upinzani. Sisi twaamini kwamba uchaguzi huu ungekuwa mgumu mara kumi zaidi laiti Lowassa angekuwa ndiye mgombea wetu.

2.    Upinzani umesalimisha ajenda yake ya kupinga ufisadi

Kipindi cha miaka 10 iliyopita kimetawaliwa na matukio mbalimbali ya kuwabainisha mafisadi na kuwachukulia hatua. Vyombo vya habari, taasisi za kiraia na Bunge vimefanya kazi nzuri kushughulikia suala hilo. Rais Jakaya Kikwete ameweka historia kwa kuamuru ripoti za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kupatikana kwa wananchi na kujadiliwa kwa uwazi Bungeni. Waziri Mkuu aliyekuwa madarakani, si mwingine bali Lowassa, alijiuzulu kwa sababu ya kashfa ya rushwa. Mawaziri kadhaa walitimuliwa kazi na manaibu waziri wawili wanatumikia vifungo jela. Huu ni uwajibikaji wa hali ya juu japokuwa kuna wanaoweza kudhani ni hatua ndogo. Umma umeamka.

Upinzani ulijenga hadhi yake kwa kuongelewa sana kuhusu ufisadi. Kilele cha Upinzani kilijiri mwaka 2007 katika mikutano mkubwa wa hadhara ambapo walitangaza majina 10 ya watu waliowaita mafisadi wakubwa zaidi, katika kilichokuja kufahamika kama Orodha ya Aibu (List of Shame). Lowassa alikuwa kinara kwenye orodha hiyo.

Ilitarajiwa kuwa Uchaguzi Mkuu huu uwe ‘hukumu’ kwa CCM kuhusu ufisadi. Upinzani ulitarajiwa kuitumia ajenda ya ufisadi ambayo inawagusa watu wengi. Lakini ghafla, kwa kumteua mwanasiasa, ambaye kwa jitihada zao wenyewe Wapinzani,  amefahamika zaidi kwa ufisadi, iliwalazimu kuzika ajenda hiyo. Kilichofuata baada ya hapo ni kituko na kichekesho. Wale mashujaa wa mapambano dhidin ya ufisadi walijikuta wakilazimika ‘kulamba matapishi yao.’ Wengi wao waliokuwa mahiri katika mitandao ya kijamii walilazimika kufuta historia ya baadhi ya waliyoyaandika mtandaoni walipokuwa wakikemea ufisadi, lakini si kabla ya maandiko yao kunaswa kwa ‘screenshots.’ Ulikuwa ni ukweli wa kushangaza. Ni Dkt Slaa na Professa Ibrahmi Lipumba, viongozi muhimu wa Upinzani tangu miaka ya Tisini, walioamua kujiuzulu nyadhifa zao kwa kukerwa na uamuzi wa Upinzani kumpokea Lowassa.Matokeo yake, Upinzani walijikuta wakichana kadi yao turufu- ajenda dhidi ya ufisadi. Ni nadra kwao kuongelewa suala hilo, na wanapojaribu kufanya hivyo, ni kwa kujitetea tu.

Jioni moja mwezi Agosti, nilimwona Mbunge wa Upinzani, Peter Msigwa, katika mdahalo kwenye runinga. Aliongelea kitu ambacho kilijumuisha mtizamo wa Upinzani kwa muda huo, na kiliniacha hoi. Alisema, kabla hawajampokea Lowassa, walifanya utafiti wao, na “ufisadi sio ajenda muhimu kwa taifa letu.” Alidai kwamba wenye ushahidi kuhusu ufisadi wa Lowassa wajitokeze hadharani.Alionekana kusahau kuwa walipomtaja Lowassa katika List of Shame, walitangaza hadharani kuwa wana ushahidi. Muda si mrefu uliopita, CCM ilikuwa ikiwaomba Wapinzani kuleta ushahidi kila yalipojitokeza madai ya ufisadi dhidi ya viongozi wa chama na serikali allegations were leveled against the party and its leaders. Haikupendeza kuingiza hoja za kisheria katika masuala ya kimaadili. Upinzani sasa umeamua kwa hiari yao kuchukua ‘chembemoyo’ wakati ambapo viongozi wa CCM wanaongelea ufisadi kwa ujasiri na msisitizo.

Uchaguzi huu Mkuu ni muhimu sana kwa Upinzani. Kimsingi, unaweza kuwa na madhara makubwa. Endapo watashindwa hapo Jumapili, ‘watapotea’ kwa muongo mzima ujao. Ndio maana inashangaza kuona wamechukua uamuzi wa kukimbia ajenda yao kuu ya kupambana na ufisadi  ambayo iliwatambulisha na kuwaimarisha. Na kuwapa nguvu kukubalika kwa wapigakura. Kuona wanatarajia kushinda ni miujiza mkubwa.

3.    Mabadiliko ambayo kamwe huwezi kuyaamini

Ukizinguka jijini Dar es Salaam utakutana na mabango ya Upinzani yanayodaia “Ni Muda wa Mabadiliko.” Lakini ukisikiliza mikutano yao ya kampeni, ni porojo na hasira tu. Wasemaji wakuu katika mikutano hiyo ni Waziri Mkuu wa zamani na kada wa muda mrefu wa CCM, Frederick Sumaye na Lowassa mwenyewe. Kwa pamoja, wamekuwa wana-CCM na katika nyadhifa  za juu serikalini kwa zaidi ya miaka 50. Kwa hiyo inasikitisha kusikiliza kauli zao – zinazokosa imani na kupalizwa na aibu – wakipambana na mfumo walioshiriki kujenga, uliojenga tabia zao za kisiasa, na ambao walikuwa wakiusifu miezi mwili tu iliyopita.
Kutokuwa wakweli na kuweka mbele maslahi binafsi kwawatuma kudai kuwa CCM haijafanya chochote katika miaka miaka 50 iliyopita. Inapotokea viongozi wawili waandamizi wa chama na serikali  kwa zaidi ya miaka 30, wote wakiwa walioshika Uwaziri Mkuu, kudai kuwa hakuna chochote kilichofanyika katika miaka 50 iliyopita, wajihukumu wenyewe. Si kwa muundo, mwonekano au ukweli, wanasiasa hao wanasimamia mabadiliko. Yayumkinika kuhitimisha kuwa mabadiliko wanayoongelea ni kuhusu kubadili chombo kilichowaingiza madarakani, mabadiliko ya sare tu za chama. Hawana habari na mabadiliko ya maisha ya wananchi wa kawaida. Wapigakura wameanza kushtukia ukweli huo.

4.    Migogoro na mkanganyiko ndani ya UKAWA

Huko nyuma, kila ulipojiri uchaguzi, Upinzani ulijaribu kuunganisha nguvu ili kuing’oa CCM madarakani.Na kila mara jitihada za ushirikiano zilishindikana. Mwaka 2014, mjadala kuhusu Katiba Mpya kuataka serikali tatu uliwapatia ajenda ya kuwaunganisha pamoja. Kisha wakaamua kutafsiri ushirikiano huo kuwa wa kisiasa, wakaafikiana kusimamisha mgombea mmoja katika nafasi ya urais na kugawana majimbo.

Baada ya hapo kukajitokeza unafiki wa wazi. Kuonyesha kuwa matamanio yaliwekwa mbele ya kanuni zilizopatikana kwa jitihada ngumu, chama ambacho jina lake linajumuisha maneno ‘demokrasia’ na ‘maendeleo’ kilitemea mate mchakato wake chenyewe wa kidemokrasia na mshikamano kupata mgombea wake wa urais, na kukurupuka kumpitisha kada wa muda mrefu wa CCM ambaye jitihada zake kuwania urais kwa tiketi ya chama hicho tawala ziligonhga mwamba.

Waliamini kwamba uamuzi wa Lowassa kuhama CCM ungekiathiri chama hicho tawala, wakitarajia vigogo kadhaa wangemfuata huo Upinzani. Badala yake, ujio wake huko ukapelekea kuondoka kwa wanasiasa wawili waliokuwa nguzo muhimu kwa Upinzani, Dkt Slaa na Prof Lipumba.Kadhalika, wanachama wengine muhimu waliohama na kujiunga na chama cha ACT- Wazalendo, ambacho hakikujiunga na UKAWA.
Kana kwamba hiyo haitoshi, makubaliano ya UKAWA kusimamisha mgombea mmoja  kila jimbo yalikumbwa na mushkeli katika majimbo kadhaa na kupelekea malalamiko yaliyosababisha ugumu katika kampeni za Lowassa.

Huko Masasi, mgombea mwenza wa Lowassa, Juma Duni, alilazimika kuokolewa jukwaani baada ya waliohudhuria mikutano wake wa kampeni kupiga kelele kuwa wataipigia kura CCM. Katika jimbo la Nzega, Lowassa alilazimika kuendesha ‘kura ya sauti’ kuwauliza waliohudhuria mikutano wake wa kampeni wanamhitaji mgombea gani kati ya wawili wa UKAWA waliokuwa wanachuana. Mpango mzima wa ushirikiano miongoni mwa vyama vinavyounda UKAWA umekwenda mrama.CCM sasa ipo katika nafasi nzuri ya kujinyakulia majimbo ambayo vinginevyo yangekwenda kwa wagombea wa Upinzani.

Lakini kilele cha unafiki wa UKAWA ni hiki. Umoja huo uliundwa ili kutetea Katiba Pendekezwa iliyoshauri muundo wa Muungano wa serikali tatu. Kanuni hiyo ya msingi iliwekwa kando pale UKAWA walipomchagua mgombea wao wa tiketi ya urais, Lowassa, ambaye alikuwa mtetezi mkubwa wa muundo wa Muungano wa serikali mbili. Kwa wengi wasioendeshwa na propaganda, uamuzi wa kutelekeza suala la msingi lililopelekea umoja wa vyama hivyo, kwa ajili tu ya imani ya kufikirika ya kushinda urais, yaashiria uchu wa madaraka na sio mabadiliko yanayohubiriwa kwa wananchi.


5.    Lowassa kushindwa kufanya kampeni nchi nzima

Lowassa anaonekana kutokuwa na uwezo wa kusafiri kwa urefu na upana wa Tanzania kufanya kampeni. Mara nyingi amekuwa akitumia usafiri wa anga kwenda mikoani ambako hufanya mikutano mikubwa kwenye makao makuu ya mikoa, kutembelea majimbo mawili au matatu ya jirani kwa helikopta, na kurejea jijini Dar es Salaam. Huko Tanga, kwa mfano, alifanya kampeni katika majimbo matatu tu kati ya tisa mkoani humo. Mkoani Ruvuma, alifanya kampeni katika majimbo matatu kati ya tisa, Kigoma majimbo mawili kati ya manane, na Kagera majimbo matatu tu.

Kinyume chake, mgombea wa CCM, Magufuli amekuwa barabarani tangu Agosti 23, huku akipumzika kwa siku tatu. Anatumia usafiri wa gari, akitembelea kijiji baada ya kijiji, na kufanya mikutano kati ya minane hadi 12 kwa siku. Aina hii ya kufanya kampeni ‘kwa rejareja’ inabaki kuwa nguzo pekee ya kujihakikishia ushindi kwenye uchaguzi mkuu nchini Tanzania, hususan katika maeneo ya vijijini ambayo usikivu na kuonekana kwa vyombo vya habari ni mdogo. Wakati Lowassa anavutia wahudhuriaji wengi katika mikutano yake katika miji mikubwa, Magufuli anajipatia wahudhuriaji wengi katika kila kona ya Tanzania. Kama idadi ya wahudhuriaji katika mikutano hiyo ya kampeni inamaanisha wingi wa kura, basi kwa hakika CCM itashinda. Lakini tofauti na Upinzani, CCM haidanganyiki na wingi huo wa wahudhuriaji katika mikutano ya kampeni. Rekodi ya mahudhurio makubwa ilikuwa ikishikiliwa na Agustino Lyatonga Mrema, mgombea maarufu wa kiti cha urais kwa tiketi ya Upinzani mwaka 1995 (ambaye pia alijiunga na Upinzani akitokea CCM). Hata hivyo alishindwa kwenye uchaguzi huo. Sie twategemea kitu kingine.

6.    Mfumo imara wa CCM katika uhamasishaji kuanzia ngazi ya chini kabisa.

Katika Tanzania, vyama vichache mno vinavyoweza kuchuana na uwezo wa CCM kuhamasisha wananchi. Wakati Wapinzani huhadaiwa na ‘mahaba’ wakati wa kampeni za uchaguzi, mahudhurio makubwa kwenye mikutano yao ya kampeni na vichwa vya habari magazetini, CCM hutumika nguvu yake ya kimuundo na kuwasha ‘mashine zake za kisiasa,’ kuanzia ngazi ya mtaa (ujumbe wa nyumba kumi) kwa nchi nzima. Kimuundo, jumiya ya wanawake wa CCM (UWT) pekee ni kubwa kuliko Chadema, chama kikuu cha upinzani. CCM Haihitaji kusafiri ili kufanya kampeni. CCM ipo kila mahala, ikifanya kampeni katika makundi madogo, vijijini na mitaani, kila siku na mbali ya upeo wa vyombo vya habari. Kwa wanaofahamu muundo wa chama hicho, ushindi kwake si jambo la kushangaza.

Kwenye miaka ya 1950s, wakati wa harakati za kusaka uhuru kutoka kwa mkoloni, uwezo wa TANU kuhamasisha ulikuwa nguzo muhimu kwa Tanganyika kupata uhuru wake.CCM imerithi vinasaba vya TANU. Mwalimu Nyerere aliijenga CCM kuwa imara kwa nyakati kama hizi. Mwaka jana, huku umaarufu wake ukiwa umepungua, CCM ilimudu kushinda uchaguzi wa serikali za mitaa kwa asilimia 80 dhidi ya umoja Huohuo wa Upinzani inaokabilina nao katika uchaguzi huu Mkuu.Tofauti haipo kwenye nini kinachoonekana kwenye vyombo vya habari au mitandao ya kijamii bali jinsi gani makada wa chama hicho tawala walivyofanya uhamasishaji katika kila mtaa na kijiji. Uchaguzi huo wa serikali za mitaa, ambao hufanyika mwaka mmoja kabla ya uchaguzi mkuu, hutoa dalili nzuri kuhusu matokeo ya uchaguzi mkuu.

7.    Umahiri wa Dkt Magufuli

Mwaka jana, baadhi ya waandishi wa habari walikiri kwamba ni vigumu mno kumshambulia na kumshinda Dkt Magufuli. Ana rekodi imara ya usafi, uchapakazi na anayetaka kuona matokeo sahihi. Hajawahi kuvutiwa na harakati za kisiasa, na ilikuwa mshangao alipotangaza kuwania urais. Na alipotangaza, hakufanya mbwembwe wala kijitangaza kwenye vyombo vya habari. Alizingatia kanuni za chama kwa ukamilifu. Dkt Magufuli analeta kumbukumbu za mgombea mwingine aliyekuwa hajulikani mwaka 1995 -  Benjamin Mkapa. Wakati umaarufu wa CCM ukiwa chini, huku ikikabiliwa na upinzani kutoka kwa Naibu Waziri Mkuu aliyehama kutoka chama hicho tawala, CCM ilimchagua turufu yake ambayo ilikuwa ngumu kuikabili.Miaka 20 baadaye, ikikabiliwa na upinzani wa Waziri Mkuu maarufu wa zamani aliyehama chama hicho na kujiunga na Upinzani, CCM imefanya tena ‘vitu vyake.’ Siku zote, CCM hujua ‘kufanya pigo la haja.’

8.    Ufanisi wa CCM katika maeneo ya vijijini

Mimi ni Mbunge wa jimbo lisilo mjini, lenye idadi ya wastani ya wapigakura. Mwaka 2010, katika uchaguzi ulionekana kuwa mgumu, CCM ilishinda jimbo langu kwa asilimia 80., na kitaifa kwa asilimia 61. Hivi sasa, tunatarajia ushindi wa CCM kuwa wa asilimia 90 hivi. Tanzania ina  majimbo kadhaa yaliyo kama jimbo langu. Upinzani hupenda kuwapuuza wananchi katika majimbo yasiyo ya mijini, kama jimbo langu, kwa kudai kuwa wanaichagua CCM kutokana na ujinga wao. Wasingeweza kukosea zaidi ya hivyo.

Popote walipo, watu hupiga kura kulingana na mahitaji yao. Mwaka 2000, vijiji vinne tu katika jimbo langu ndivyo vilikuwa na umeme. Leo, vijiji 44 vina umeme. Japo hatujaweza kutoa huduma zote kwa kiwango cha kumfurahisha kila mtu, lakini hali halisi yaonyesha wingi wa wanafunzi mashuleni, walimu zaidi, madaktari na manesi zaidi, zahanati nyingi zaidi zimejengwa, huduma za mawasiliano ya simu zinapatikana kwa wingi, barabara nyingi za lami, nk. Porojo kuwa hakuna kilichofanyika Kwahiyo wapigakura wasiichague CCM haieleweki katika maoneo hayo ambay kimsingi ndiyo yenye wapigakura wengi. Na wagombea wa CCM wanaposema watafanya zaidi ya waliyokwishafanya, kwa kuzingatia mafanikio yaliyokwishapatikana, wananchi wanawaamini. Hotuba za kampeni ni mwonekano na mantiki.

Chaguzi sio kuhusu ahadi tu bali jinsi gani ahadi hizo zitaandaliwa na kutekelezwa. Jukwaa ambalo kila chama kitanadi ajenda zake za uchaguzi hujengwa wakati wa uzinduzi wa kampeni za chama husika. Yahitaji mtu kuangalia tu uzinduzi wa kampeni za za Lowassa na Magufuli. Lowassa aliongea kwa dakika 9 tu  - akiahidi, pamoja na mambo mengine, kuwaachia huru wabakaji (sio kama ninazusha hili) wanaotumikia vifungo vyao na watuhumiwa ugaidi wanaosubiri kesi zao. Bila kujali alikuwa na malengo gani wakati anatoa ahadi hizo, makosa hayo hayastahili msamaha wa rais.  Kwa upande wake, Magufuli aliongea kwa dakika 58, akielezea kwa undani ajenda za maendeleo katika nyanja za elimu, ajira, afya, ufisadi, huduma za maji, na miundombinu. Kuanzia hapo, kwa muda wote wa kampeni, mwenendo umekuwa hivyo, kwa uzito wa ujumbe kwenye hotuba zake na muda wa kuhutubia

Wanaohudhuria mikutano ya Dkt Magufuli huondoka katika mikutano hiyo wakiwa na matumaini na wenye nguvu. Kwa upande mwingine, wahudhuriaji katika mikutano ya Lowassa huondoka wakiwa wamekanganywa. Siku ya kupiga kura, wapigakura wanamkumbuka jinsi mgombea alivyoonekana na alivyoongea, na jinsi walivyojisikia walipomwona jukwaani. Kwa kigezo hiki, ni bora ningekuwa upande wa Magufuli.  

9.    Uongo, uongo na takwimu

Tanzania haina utamaduni wa kura za maoni kupima nafasi za wagombea katika uchaguzi. Tuna utaratibu wa muda mrefu wa kupata maoni ya wananchi katika maamuzi makubwa ya kisera – kuingia mfumo wa vyama vingi vya siasa, marekebisho ya Katiba, na kadhalika. Mwaka 2005, kulifanyika kura ya maoni, iliyobashiri ushindi mkubwa kwa CCM. Na kwa hakika, CCM ilishinda kwa asilimia 80. Mwaka 2010, kura ya maoni iliyoendeshwa na kampuni ya Ipsos-Synovate iliashiria kuwa idadi ya kura za CCM ingepungua hadi kufikia asilimia 61. CCM ilipinga matokeo ya kura hiyo ya maoni ikidani kuwa yalikuwa kiasi kidogo sana. Matokeo ya uchaguzi huo yalikuwa kama yalivyotabiriwa katika kura hiyo ya maoni. CCM ilipata asilimia 61 ya kura zote.

Hivi karibuni, kura mbili za maoni zilichapishwa. Zote zilifanywa na taasisi huru zinazoheshimika. – Twaweza and Synovate-Ipsos tena- zote zikijihusisha na utafiti wa kusaka maoni. Taasisi mbili tofauti, zilizotumia mbinu tofauti za kufanya utafiti, katika nyakati tofauti, matokeo yaleyale. CCM itashinda kwa asilimia 62 ya kura zote.

Inaruhusiwa, na kwa yumkini ni jambo zuri, kupingana na sababu hizi tisa za kwanini CCM itashinda. Lakini namba zina tabia ya ukandamizaji. Ndio mwelekeo wa kura huwezi kubadilika. Lakini kwa kuzingatia yote yaliyokwishaongelewa kuhusu kinachodaiwa kuwa ufuasi mkubwa kwa Upinzani, basi muda huu ingetarajiwa tuwa tunajadiliana kuhusu ufuasi wa wengi kutoka Upinzani kuelekea CCM– na sio kutarajiwa ufuasi wa wengi kutoka CCM kuelekea Upinzani. Na ndiyo, kura za maoni zaweza kukosea, na tusiwekee mkazo sana.Lakini hoja hii sasa ndiyo hupendelewa zaidi na upande unaelekea kushindwa kwenye uchaguzi.


January Makamba ni Mbunge wa Bumbuli (CCM), Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM, na msomaji wa Kampeni za CCM 

10 Jul 2014

HATIMAYE mbio za kuelekea Ikulu hapo mwakani zimeanza rasmi baada ya mwanasiasa kijana, Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia na Mbunge wa Bumbuli (CCM), January Makamba, kutangaza kuwa atagombea urais.
Habari hiyo imetawala mno katika mitandao ya kijamii na ukiweka kando michuano ya Kombe la Soka la Dunia inayoendelea nchini Brazil, tangazo la mwanasiasa huyo limeonekana kuwagusa wengi.
Na kama pongezi ni ishara ya ushindi, basi kwa hakika uamuzi wake wa kugombea nafasi hiyo kubwa kabisa nchini unaonekana kuunngwa mkono japo kwenye mitandao ya kompyuta.
Ninampongeza January kwa ujasiri wa kutamka dhamira yake ya urais hadharani. Huko nyuma nilishawahi kuzungumzia umuhimu wa wanasiasa wanaotaka urais kujitokeza hadharani mapema ili tupate fursa ya kuwaelewa vizuri na pengine kuwapa ‘hukumu’ stahili.
Utaratibu wa kutangaza nia ya kuwania urahisi mapema ni kama jambo la kawaida kwa siasa za nchi za Magharibi, hususan, huko Marekani.
Hata hivyo, pamoja na faida yake kwa wananchi, na pengine kwa mgombea kutambulika na hata kupata kuungwa mkono zaidi, moja ya athari zake ni kwa mtarajiwa kuwapa maadui zake ‘silaha’ za kummaliza mapema.
Kadhalika, kwa kutangaza nia mapema, mtarajiwa anaweza kujikuta amechokwa mapema hata kabla ya uchaguzi, hususan, kama ana mapungufu yaliyofichika.
Ifahamike kuwa kwa kujitangaza kugombea urais mapema, mwanasiasa anawapa fursa wananchi kumchunguza-kwa mema na mabaya- na iwapo kuna kasoro zilizofichika au ambazo hazikuwahi kupewa umuhimu mkubwa, basi anaweza kujitengenezea mazingira ya kushindwa mapema.
Sasa  tuangalie nafasi ya January kufanikiwa kuwa rais ajaye wa Tanzania. Moja ya sifa kubwa ya mwanasiasa huyo inatajwa kuwa ukaribu wake na wananchi wa kawaida. Kwa sisi tunaotumia muda mwingi kwenye mitandao ya kijamii tunaweza kuafikiana na hoja hiyo. Lakini ‘maisha ya mtandaoni’ si lazima yawe ndo maisha ya mtu kihalisia (real life).
Kingine kinachoweza kumsaidia mwanasiasa huyo ni ujana wake. Japo sina takwimu za hakika, yayumkinika kuhitimisha kuwa idadi kubwa ya wapigakura huko nyumbani ni vijana. Kwahiyo kama ujana wa January waweza kutafsiriwa katika sapoti kutoka kwa vijana wenzie basi anaweza kuwa na nafasi nzuri.
Na siku chache baada ya kutangaza nia yake ya kuwania urais hapo mwakani, waziri mkuu mstaafu Jaji Joseph Warioba alinukuliwa na vyombo vya habari akishauri kuwa ni vema kwa wazee kuwaachia vijana nafasi za uongozi. Hiyo ni sapoti kubwa kwa January hasa ikizingatiwa kuwa licha ya kebehi zilizoelekezwa kwake kufuatia uongozi wake katika ‘Tume ya Warioba,’ mwanasiasa huyo bado anaheshimika miongoni mwa Watanzania wengi.
Hata hivyo, moja ya vikwazo vikubwa kwa January kufanikiwa kuwa mrithi wa Rais wa sasa, Jakaya Kikwete, ni utaratibu wa kumpata mgombea urais ndani ya CCM. Binafsi, sitilii sana maanani mizengwe iliyozoeleka ndani ya chama hicho kila linapokuja suala la kupata mgombea (hata wa nafasi ya uenyekiti wa serikali ya mtaa, achilia mbali urais) bali nafasi ya Zanzibar katika suala la mgombea urais kwa tiketi ya CCM.
Inafahamika kuwa awali chama hicho tawala kilikuwa na utaratibu usio rasmi wa ‘uongozi wa kupokezana’ kwa maana baada ya Mtanzania Bara kumaliza awamu zake, ni zamu ya Zanzibar kutupatia rais. Hata hivyo, baada ya Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere (m-Bara) kung’atuka na kumwachia rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi (Mzanzibari), ambaye naye baada ya kustaafu alirithiwa na rais mstaafu Benjamin Mkapa (m-Bara), ilitarajiwa kuwa rais wa Awamu ya nne angetoka Zanzibar.
Wenye uelewa wa siasa za nchi yetu wanadai kuwa kilichovuruga utaratibu huo (angalau kwa muda) ni nguvu ya mtandao uliomwingiza Rais Kikwete madarakani. Inadaiwa kuwa mtandao huo uliojipenyeza kila mahali ulifanikiwa kuzima matakwa ya wana-CCM Zanzibar kuwa “Awamu ya nne ilikuwa zamu yao.”
Je, January ana raslimali za kutosha kisiasa kuweza kuwashawishi Wazanzibari wamruhusu agombee na hivyo kuwanyima fursa nyingine ya urais baada ya miaka 20 ya Mkapa na Kikwete?
Kuna tatizo jingine ambalo japo si kubwa lakini laweza kumkwamisha mwanasiasa huyo kijana. Utaratibu mwingine usio rasmi kuhusu urais ni wa nafasi hiyo kuzunguka kati ya Mkristo na Mwislamu. Nyerere alikuwa Mkristo, Mwinyi Mwislamu, Mkapa Mkristo na Kikwete Mwislamu. Je, uwezekano wa kuwa na rais mwingine Mwislamu hauwezi kuzua manung’uniko? Binafsi sioni kama hoja hiyo ina msingi kwa sababu uongozi bora hauna dini, lakini ni vema kufahamu kuwa japo tunapinga udini lakini hisia hizo zipo na hazikwepeki.
Kikwazo kingine kwa January, angalau kwa wasio wana-CCM, ni u-CCM wake. Yayumkinika kuhitimisha kwamba kuna idadi ya kutosha ya Watanzania wanaokiona chama hicho tawala kama chanzo kikuu cha matatizo yanayoikabili nchi yetu.
Si siri kwamba CCM imegeuka kuwa kichaka cha kuhifadhi mafisadi, na kuna wanaodhani kuwa dhamira ya CCM kubaki madarakani ni si tu ukweli kuwa chama chochote cha siasa kilicho madarakani lazima kitataka kuendelea kutawala bali pia uwepo wake madarakani ni kulinda maslahi binafsi ya viongozi wake na washiriki wao.
Je, January, na wengine watakaokuja,  watawashawishi vipi Watanzania kuwa licha ya kuwa viongozi wa ngazi ya juu katika chama hicho tawala, wapo tofauti kimtizamo au vitendo na viongozi wengine wa CCM? Na katika hilo kuna suala la kumbukumbu.
Kuna uwezekano mwanasiasa huyo akaulizwa “sawa, wewe ni msafi lakini ulishafanya nini kuondoa uchafu unaokikabili chama chako?”
Baadhi yetu tunadhani kuwa uhusiano kati ya CCM na mafisadi ni kama ule unaofahamika kibaiolojia kama ‘symbiotic,’ kwamba ustawi wa mafisadi unategemea uhai wa CCM na wa CCM unaowategemea mafisadi.
Ndiyo maana jitihada fyongo za chama hicho ‘kujivua magamba’ zilikwama kwa sababu, tofauti na nyoka anavyoweza kujivua ‘gamba’ akasalimika, jaribio hilo la CCM lilikuwa kama kobe kujivua gamba; lazima atakufa!
Hapo juu nimetaja kuwa ujana wa January waweza kuwa ‘asset’ katika dhamira yake ya kuingia Ikulu. Hata hivyo, binafsi ninapingana vikali kabisa na mtizamo kwamba ujana (au hata uzee) ni sifa muhimu ya rais tunayemhitaji.
Hivi wakati huu ambapo nchi yetu inabakwa mchana kweupe na mafisadi kupitia skandali kama za EPA, Richmond, ESCROW, nk hatuna viongozi vijana ndani ya CCM? Mbona hatuwasikii wakipiga kelele dhidi ya ufisadi huo?
Majambazi wanaofanya kila jitihada za kufilisi nchi yetu hawana umri maalumu; wauza madawa ya kulevya, matapeli wa kisiasa, na wahalifu wengine ni pamoja na vijana. Na hata uzalendo hauna umri. Mzee au kijana anaweza kuipenda nchi yake na akaitumikia kwa uadilifu kama ambavyo kijana au mzee anavyoweza kuibomoa nchi.
Na kingine kisichonipendeza kuhusu ‘ubaguzi’ dhidi ya wazee ni uwezekano wa ‘domino effect,’ yaani leo itakuwa “wazee hawafai kutuongoza,” kesho itakuwa “wanawake hawafai kushika uongozi,” na katika hali ya hatari kabisa, twaweza kufikia hatua ya “Wakristo/Waislam hawafai kutuongoza.”
Nihitimishe makala hii kwa kurejea pongezi zangu kwa January Makamba kwa kutangaza mapema dhamira yake ya kutaka kuwania uraia hapo mwakani, hatua ambayo angalau imeamsha mjadala muhimu kuhusu rais ajaye.
Ni matarajio yangu kwamba wanasiasa wengine wenye nia ya kuongoza taifa wataiga mfano huo ili kuwasaidia Watanzania wawaelewe kwa undani ili hatimaye wafanye uamuzi sahihi katika sanduku la kura.
Ni muhimu kutambua kwamba uchaguzi huo una umuhimu mkubwa kwa hatma ya kila Mtanzania na uhai wa Tanzania yetu.
Kadhalika, kwa vile inatarajiwa kuwa uamuzi wa January ‘kutangaza nia’ waweza kusababisha ‘wenye nia’ wengine kujitokeza hadharani, ni muhimu kwa Watanzania kujiandaa kuwauliza swali hili: “nchi yetu kamwe haijawahi kuwa na uhaba wa wanasiasa wanaoahidi mambo mazuri lakini wakiingia madarakani ‘wanazisahau ahadi zao’, je una lipi ulilokwishaifanyia Tanzania la kutufanya tukuone tofauti na wapiga porojo wengine?”

24 Jul 2013


WAKATI taifa likiwa katika maombolezo ya vifo vya mashujaa wetu saba waliouawa huko Darfur, Sudan, wakitumikia kikosi cha Umoja wa Mataifa cha kulinda amani nchini humo, Jeshi letu la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) lilifanya tukio linalostahili pongezi nyingi, japo huenda ni wananchi wachache tu wenye taarifa nalo.
Jumapili iliyopita jeshi hilo lilianza kutumia rasmi mtandao wa kijamii wa twitter likitumia ‘handle’ @jw_tz. Hatua hiyo ni ya kimaendeleo na inaonyesha kuwa jeshi letu limedhamiria kwenda na kukumbatia teknolojia ya kisasa ya mawasiliano.
Mtandao wa twitter na pengine mitandao ya jamii kwa ujumla, bado ni suala geni kwa Watanzania wengi. Na licha ya ugeni huo, ukweli kwamba umiliki na upatikanaji wa huduma ya kompyuta bado ni ‘anasa’ wanayomudu watu wachache unafanya matumizi ya twitter (na mitandao mingine ya kijamii) kutokuwa suala muhimu au maarufu kwa jamii yetu.
Hata hivyo, mitandao ya kijamii hivi sasa imekuwa sehemu muhimu ya mawasiliano; huku ikibadili kwa kiasi kikubwa upatikanaji na kupashana habari. Wakati kwa muda mrefu mawasiliano kati ya mtu na mtu yamekuwa yakitegemea aidha neno la mdomo (kwa maana ya watu kukutana au kwa njia ya barua) au magazeti na redio, na kwa kiasi fulani runinga, mitandao ya jamii na teknolojia ya mawasiliano kwa ujumla imetokea kuwa njia ya haraka ya mawasiliano katika jamii.
Ukitaka kupata mfano wa umuhimu wa teknolojia hiyo ya mawasiliano, ni jinsi ziara ya kihistoria ya Rais wa Marekani Barack Obama huko nyumbani Tanzania, hivi karibuni, ilivyoripotiwa in real time (kadri matukio yalivyokuwa yakitokea) badala ya kusubiri gazeti la kesho au ripoti za redioni au kwenye runinga.
Kadhalika, kwa kutumia mtandao wa twitter, wananchi wamekuwa wakiendesha kampeni mbalimbali, na ya hivi karibuni kabisa ni ile inayohamasisha kupinga kodi ya sim card ambapo inatumia hashtag #NoSIMcardTax.
Iwapo Serikali itasikiliza kilio cha wananchi na kusitisha au kufuta kodi hiyo, basi kampeni hiyo ya mtandaoni (hususan huko twitter) itastahili pongezi kubwa.
Pamoja na pongezi zangu kwa hatua hiyo ya JWTZ kujiunga na mtandao wa twitter, bado taasisi hiyo inakabiliwa na changamoto kubwa; hususan kutumia ipasavyo mtandao huo kama nafasi kwa jeshi hilo kuupasha umma habari stahili.
Kwa mfano, juzi Rais Jakaya Kikwete aliwaongoza Watanzania kutoa heshima zao za mwisho kwa miili ya wanajeshi wetu waliouawa Darfur, na katika mazingira mwafaka, tungetegemea akaunti ya twitter ya JWTZ ingetulea tukio hilo ‘live’ lakini haikuwa hivyo. Siwalaumu kwa vile pengine ni ugeni tu katika matumizi ya teknolojia hiyo.
Licha ya ujio huo wa JWTZ huko twitter, mtandao huo wa kijamii unatumiwa pia na baadhi ya viongozi wetu wa serikali na wanasiasa, japo idadi yao ni ndogo. Rais Kikwete ni miongoni mwa viongozi hao; huku akiweka historia ya kuwa mmoja wa marais wachache wa Afrika wanaotumia mitandao ya kijamii.
Miongoni mwa mawaziri wachache wanaotumia mtandao wa twitter ni Mheshimiwa Lazaro Nyalandu (@LazaroNyalandu), Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii. Uwepo wake katika mtandao huo umenisaidia kumfahamu katika namna ambayo pengine Watanzania wengi hawaifahamu.
Nyalandu amekuwa mfano bora wa jinsi inavyostahili na inavyowezekana kuweka maslahi ya nchi mbele ya maslahi ya kiitikadi. Lilipotokea tukio la milipuko ya mabomu jijini Arusha, Waziri Nyalandu alishiriki kikamilifu kuufahamisha umma kuhusu hatua mbalimbali zilizokuwa zikifanyika kuwasaidia majeruhi.
Na japo Nyalandu ni Mbunge wa CCM, kamwe hajawahi ku-tweet mambo ya kiitikadi, na badala yake tweets zake zimekuwa zikihusu masuala ya Tanzania na Watanzania, badala ya masuala ya CCM.
Kingine kinachopendeza kuhusu Naibu Waziri huyo ni usikivu kwa hoja mbalimbali zinazowasilishwa kwake kupitia mtandao huo. Kama ilivyo kwa Naibu Waziri mwingine, Januari Makamba (@JMakamba), Nyalandu huwasiliana na wananchi waliopo twitter kwa heshima na unyenyekevu mkubwa, kiasi yaweza kuwa vigumu kudhani ni mtu mwenye dhamana kubwa serikalini.
Ni kwa sababu hiyo, kupitia mtandao wa twitter Jumapili iliyopita nilimtumia ombi Waziri Nyalandu kumsihi awasilishe kilio cha msanii Johnson Nguza (Papii Kocha) ambaye, pamoja na baba yake Nguza Viking na kaka zake wawili, wanatumikia kifungo kirefu jela kwa kosa la kubaka.
Mwishoni wa wiki, blog mbalimbali zilichapisha barua iliyoandikwa na msanii huyo (Papii Kocha) kwenda kwa Rais Kikwete akiomba msamaha kwa yeye na familia yake, na kumwomba Rais awatoe gerezani.
Nina sababu mbili za msingi za kuguswa na suala la ‘Babu Seya’ na wanae ambao wamekuwa gerezani kwa takriban miaka 10 sasa. Kwanza, japo kuna msemo maarufu kwenye kila jela kuwa ‘kila mfungwa hana hatia’ (yaani amefungwa kwa kuonewa), tangu Nguza na wanae walipokamatwa na hatimaye kufungwa nimebaki na hisia kuwa sheria ilipindishwa dhidi yao.
Mengi yameshasemwa huko mitaani kwamba kesi hiyo ilisababishwa na visasi binafsi dhidi ya msanii huyo na wanae. Ikumbukwe kuwa katika nchi zetu masikini kuna ‘haki za aina mbili,’ kwa wanyonge ambao wanaweza kwenda jela kwa kusingiziwa tu, na kwa vigogo ambao ni kama wana kinga ya kudumu ya kisheria.
Sababu ya pili ya kumwomba Waziri Nyalandu amfikishie Rais Kikwete ujumbe wa Papii Kocha ni ya kibinadamu zaidi. Tuweke kando hisia kuwa kifungo cha Nguza na wanae ni sheria kufuata mkondo au kupindishwa.
Kama binadamu, na hasa katika Mwezi huu Mtukufu wa Ramadhan, unajiskiaje ukisoma barua ya kutoa majonzi kutoka kwa kijana mfungwa anayezeekea jela akiomba msamaha kuhusu hukumu ambayo tangu mwanzo wafungwa hao wamekuwa wakidai ni ya uonevu tu dhidi yao?
Ndio, huko jela ‘kila mfungwa hana hatia’ (yaani wafungwa wengi hudai wamefungwa kwa kuonewa hata kama walikamatwa red-handed wakifanya makosa).Lakini katika mazingira ya kawaida, ni wafungwa wangapi waliopo jela kwa takriban miaka 10 na wanaendelea kusisitiza kuwa walifungwa kwa uonevu na wanaomba hukumu dhidi yao ziangaliwe upya au wasamehewe?
Laiti ukisoma barua hiyo ya Papii Kocha (na amekuwa akiandika barua kama hiyo mara kadhaa) usipolengwa na machozi basi utakuwa na ‘moyo mgumu’ kweli.
Lakini hata tukiweka kando huruma ambayo baadhi yetu tunayo kwa Nguza na wanae, katika ubinadamu tu, msanii huyo na wanae wameshatumikia adhabu ndefu (bila kujali walitenda kosa au la), na adhabu waliyokwishapata inatosha kutoa fundisho kwao na kwa jamii kwa ujumla. Hivi sisi kama jamii tutaathirika vipi iwapo Nguza na wanawe wakisamehewa?
Kama nilivyotarajia, ‘mtu wa watu’ Naibu Waziri Nyalandu alinijibu juzi akisema kwa tweet (namnukuu) “copy that...” akimaanisha amesikia ombi langu na atalifanyia kazi.
Licha ya imani yangu kwa Nyalandu, nina imani pia kuwa Rais Kikwete atasikiliza ujumbe huo kutoka kwa mteuliwa wake. Vilevile ukweli kuwa huu ni Mwezi Mtukufu, na nina hakika Rais amefunga pia, roho ya huruma itamsukuma kusikiliza kilio cha mara kwa mara kutoka kwa Papii Kocha, kaka zake na baba yao.
Mwisho, ninaomba kila Mtanzania mwenye kuamini katika kuwasamehe waliotukosea (ikiwa ni pamoja na wanaotajwa kuwa wahanga wa makosa yaliyofanywa na ‘Babu Seya na wanawe) atajumuika nami kuwaombea msamaha wasanii hao.
Maandiko Matakatifu katika Surat Al I’mran 155 ya Kurani Tukufu na Marko 11:25 ya Biblia Takatifu ni baadhi za aya lukuki zinazotusisitiza kuhusu msamaha.



26 Aug 2012


New Africa: the politician fighting corruption in Tanzania

Government minister January Makamba is full of innovative ideas for harnessing technology to help his country
January Makamba
Tanzanian minister January Makamba on the campaign trail. Photograph courtesy of January Makamba
January Makamba is Tanzania's deputy minister for communication, science and technology. In 2009, President Kikwete introduced him to Barack Obama, who was much taken by his dynamism, observing that he was the sort of politician likely to help transform the fortunes of the continent.
Makamba is an interesting combination of old and new Africa. He attended university in the US, but explains that, although he is the son of a teacher, politician and public servant, it was the time spent in Tanzania's rural areas as a child that most influenced his development. "The most rewarding experience was living with my grandmother. The daily routine was testing – I'd wake at 5am, walk 8km to school, come home at 3pm and go out to herd goats." This gave him, he feels, the "empathy needed for good decision-making".
It was empathy that turned him into a politician when, in his gap year, he was manager of Mtabila refugee camp, overseeing 120,000 Burundi refugees. "Witnessing that misery made me political." It made him "philosophical". But Makamba has emerged as a politician who does more than philosophise. He is an innovator with formidable drive. He is determined to unshackle his country from reliance on aid. He set upBumbuli Development Corporation to borrow $10m from Wall Street philanthropists, invested in bonds with dividends to be spent in his constituency. "We decided not to find an NGO to help us but start our own – and not make it a charity. We have had a flurry of NGOs with little impact. This corporation would be a driver for development and private enterprise. It would be a social business with huge potential." The corporation money is already funding community projects. He gives an example: "Fifty per cent of our fruit and vegetables used to be spoiled before going to market." Now, a "new aggregation centre" is putting this right.
His most exciting innovation, launching next month, is a new text message anti-corruption campaign, a global naming-and-shaming project. "Only 6.9% of corruption cases are currently reported. We want to solve the problem. Almost everyone in Tanzania has a mobile." He sets the scene: "At a hospital you are asked for a bribe. You have a USP code, you enter the location and details of the bribe and send it to a web platform: it will appear as a dot on a map so everyone can see that at a certain hospital a bribe was asked for."
Africans he admires
Fred Swaniker Ghanaian founder of African Leadership Network.
Malusi Gigaba A minister in South Africa, and a voice of reason and reassurance

5 Jul 2012


MOJA ya matokeo yasiyopendeza ya ujio wa mageuzi ya kisiasa katika miaka ya tisini ni ukweli kwamba kwa kiasi kikubwa hayajamsaidia mwananchi wa kawaida mtaani.
Mageuzi hayo - hasa katika nyanja ya siasa na uchumi, yameendelea kuonekana kama ni kwa ajili ya kikundi kidogo katika jamii huku yakitanua pengo kati ya walio nacho na wasio nacho.
Kwenye siasa, ujio wa vyama vingi haujafanikiwa kwa kiwango cha kutosha kuweka mbele maslahi ya wananchi na badala yake umekuwa kama fursa kwa baadhi ya wanasiasa kujinufaisha.
Utitiri wa vyama vya Upinzani umekuwa turufu muhimu kwa chama tawala kutoyumbishwa au kuwajibishwa vya kutosha; hasa kwa vile Upinzani usio na umoja ni rahisi kudhibitiwa na hata kuhujumiwa na chama kimoja imara na chenye uzoefu wa harakati za siasa. Hapa ninaizungumzia CCM.
Tumeshuhudia baadhi ya vyama vikiibuka nyakati za chaguzi tu, na badala ya kutoa upinzani kwa CCM, vyama hivyo vimekuwa vikigawa kura za wapinzani na hivyo kukinufaisha chama tawala.
Kuna hisia kwamba CCM, kwa kutambua kuwa ushirikiano na/au umoja wa wapinzani ni tishio kwa ustawi na uhai wake, imekuwa ikivisaidia vyama hivyo dhaifu katika nyakati za chaguzi kwa minajili ya kugawa kura za wapinzani.
Pengine hoja hiyo inapewa nguvu na namna baadhi ya vyama hivyo vinavyoendesha kampeni zake ambapo badala ya kuelekeza mashambulizi kwa chama tawala, huwageukia wapinzani wenzao.
Lakini hata kama tuhuma hizo dhidi ya CCM hazina ukweli wowote, kilicho wazi ni kwamba vyama vingi vya upinzani nchini havina maslahi yoyote kwa Mtanzania. Baadhi ya vyama vimegeuka kama kampuni za kifamilia ambapo kiongozi ndio chama ilhali hakuna jitihada zozote za ufunguzi wa matawi mapya au kuongeza idadi ya wabunge au/na madiwani.
Yayumkinika kuhitimisha kuwa adui mkubwa wa vyama vya upinzani ni ubinafsi miongoni mwa baadhi ya viongozi wa vyama hivyo; hususan wale ambao wamegeuza vyama hivyo kuwa mali zao binafsi.
Tukiangalia kwa upana zaidi, tatizo la upinzani dhaifu unaotokana na mgawanyiko (badala ya ushirikiano) miongoni mwa wapinzani linachangiwa pia na ukweli kuwa katika mazingira ya Tanzania yetu, hivi sasa siasa imegeuka kuwa ajira.
Kama ambavyo madhehebu mbalimbali yamevamia na walaghai wanaotumia dini kama chanzo cha mapato yao binafsi, siasa nayo imevamiwa na kundi la wahuni ambao wamebaini kuwa sio tu fani hiyo ni chanzo kizuri cha mapato lakini pia inatoa kinga dhidi ya uhalifu wowote wanaojihusisha nao.
Na ndio maana kila kunapofanyika uchaguzi tunashuhudia baadhi ya wanaowania nafasi za uongozi wakimwaga mamilioni ya fedha ili wachaguliwe. Na kwa kutambua udhaifu wa vyombo vya dola katika kuwabana watoa rushwa kwenye chaguzi, baadhi ya matapeli hao wa kisiasa hufanikiwa kushinda chaguzi hasa kutokana na ukweli kuwa wapiga kura wengi “wana njaa” na wapo radhi kunadi kura zao kwa pishi za mchele na doti za kanga.
Tukiangalia kwenye mageuzi ya kiuchumi, manufaa kwa Mtanzania wa kawaida mtaani yameendelea kuwa haba. Kana kwamba itikadi ya Ujamaa na Kujitegemea ilikuwa ikiwafunga mkono baadhi ya viongozi kutekeleza imani yao ya ubepari kwa vitendo, mara baada ya kile kinachofahamika kama Azimio la Zanzibar, nchi yetu imeshuhudia matendo kadhaa maovu pengine zaidi ya mkoloni tuliyemtimua mwaka 1961.
Siku zote huwa natoa ‘excuse’ kwa wakoloni kwamba; angalau wao walikuwa na sababu ya kutoihurumia Tanzania yetu kwani hawakuwa Watanzania, na hata nchi hiyo ingetumbukia mtaroni wao wasingeathirika kwani wana makwao. Sasa sijui tuwaelewe vipi Watanzania wenzetu ambao matendo yao ya kuibaka nchi yetu kiuchumi yanazidi kuipeleka nchi yetu mahali pasipostahili.
Hawa hawana ‘excuse’ hasa kwa sababu wengi wao walizaliwa na kukulia Tanzania, na hata nyadhifa walizonazo zimechangiwa na mzigo uliobebwa na Watanzania wenzao kwa njia ya kodi.
Kibaya zaidi, kiasili takriban kila Mtanzania anahusiana na Mtanzania mwingine (kwa wenye uelewa wa historia wanafahamu asili za makabila yetu hususan ya Kibantu). Mtu anayeruhusu madawa ya kulevya yaingie nchini alimradi akaunti yake inazidi kufurika “vijisenti” anapaswa kufahamu baadhi ya watumiaji wa madawa hayo ni watu wanaohusiana nae kikabila kama si kiukoo.
Lakini hata kama hawahusiani, nguvu kazi inayoathiriwa kutokana na matumizi ya madawa hayo inaweza kumwathiri hata mpokea rushwa huyo; kwani sote tunajua kuwa nchi haiwezi kujengwa na 'jeshi la mateja' (watumia madawa ya kulevya).
Kijamii, japo mageuzi hayakuwa ya moja kwa moja, lakini madhara yaliyojitokeza yanaweza kuonekana zaidi katika nyanja za utamaduni, sambamba na kwenye mila na desturi zetu.
Eneo moja ninaloweza kulitumia kama mfano ni katika matumizi ya lugha yetu ya taifa Kiswahili. Binafsi, katika takriban muongo mmoja nilioishi hapa Uingereza sijawahi kuwaona au kuwasikia Waingereza wakiendesha majadiliano/mazungumzo yao kwa lugha ya kigeni.
Na hiyo si kwa Waingereza pekee. Nchi nyingi duniani zimekuwa zikienzi sana lugha zao kwani ni utambulisho muhimu wa utaifa wao.
Sasa akina sie ambao licha ya kuwa na lugha ya taifa Kiswahili tuna lundo la lugha zetu za asili, tunaendelea kuichukulia lugha ya Kiingereza kama kioo cha elimu au ubora wa mtu.
Juzijuzi, nilitoa changamoto kwa Watanzania wenzangu wanaotumia mtandao wa kijamii wa twitter kwamba ni muhimu kwetu kuenzi lugha yetu ya taifa badala ya kuendeleza mijadala yetu kwa Kiingereza.
Japo ninakiri kuwa nyakati fulani nami nimekuwa nikitumia Kiingereza huko twitter(angalau kwa kisingizio kuwa baadhi ya watu wangu wa karibu hapa hawaelewi Kiswahili), kwa kiwango kikubwa nimekuwa nikijitahidi kuenzi lugha yangu ya taifa Kiswahili.
Na kwa sie tulio mbali na nyumbani, kuna wakati tunatamani tuwe kama wenzetu Wachina au Wahindi (kwa mfano) ambao kila wanapokutana wanawasiliana kwa kutumia lugha zao.
Unaingia mtandaoni ukiwa na hamu ya kuwasiliana na wenzio kwa Kiswahili, lakini wao wanakazania lugha nyingine (huku wengine wakikaza misuli ili waimudu lugha hiyo ya kigeni).
Lakini tatizo si kwenye lugha pekee; bali hata kwenye mila na tamaduni zetu. Ukiangalia baadhi ya zinazoitwa kazi za sanaa unaweza kuhisi kuwa ‘mwisho wa dunia’ unakaribia.
Nilishawahi kuandika katika makala moja huko nyuma kuhusu baadhi ya vikundi vya burudani ambavyo sio tu vinatumia majina yenye maana mbaya (kwa mfano ‘Kitu Tigo’), lakini hiyo burudani yenyewe ni laana tupu.
Na kana kwamba ibilisi anazidi kupata wafuasi, burudani za aina hiyo zimetokea kupata umaarufu mkubwa.
Ukiangalia kwenye eneo ambao pengine lingeweza kuwa mkombozi wetu kisanaa, yaani filamu za Kitanzania, hutolaumiwa ukihitimisha kuwa baadhi ya wanaoingia kwenye fani hiyo wapo ‘kibiashara binafsi’ zaidi kuliko kisanii.
Hivi kuna ugumu gani kuwaiga Waafrika wenzetu wa Nigeria ambao sekta yao ya filamu ya Nollywood inatamba ndani na nje ya Afrika; hususan kwa sababu filamu zao zimeelemea zaidi katika uhalisia wa maisha ya Mwafrika, na wengi wa wasanii wanavuma kwa vipaji vyao na si kutengeneza vichwa vya habari visivyopendeza magazetini.
Lakini kwa wengi wa ‘mastaa’ wetu wa filamu, umaarufu wao unaenda sambamba na taarifa za kufumaniwa, kuvaa nguo nusu-utupu na uhayawani mwingine!
January Makamba
Katika kuelekea kuhitimisha makala hii, ningependa kutoa pongezi za kipekee kwa mwanasiasa kijana, January Makamba, ambaye kwa namna fulani anafanya jitihada binafsi za kuleta matokeo chanya ya mageuzi niliyoongelea katika makala hii.

Mwanasiasa huyu wa CCM ni mmoja ya wachache wanaotumia vyema mitandao ya kijamii kuushirikisha umma.
Wiki hii ameandika makala moja nzuri sana kuhusu u-liberali mamboleo ambapo kimsingi anachoongelea kinashabihiana kwa karibu na dhima ya makala hii.
Katika makala hiyo yenye kichwa cha habari ‘Kubadili Dhana’ (Changing the Paradigm), January anachambua jinsi zaidi ya miaka 30 ya dhana hiyo ya u-liberali mamboleo ilivyoshindwa kuzaa matunda ya maana kwa nchi zinazoendelea na hata zile zilizoendelea.
Anaeleza kuwa kushindwa kwa dhana hiyo kunajidhihirisha katika kuyumba kwa uchumi wa soko, kuendelea kutumia jembe la mkono, utajiri kuendelea kuwa mikononi mwa wachache, uhaba wa kidemokrasia, machafuko, kushindwa kukabiliana na maradhi, nk.
Licha ya kuvutiwa na jitihada zake binafsi za kuushirikisha umma; hususan kupitia mitandao ya kijamii, mwanasiasa huyu analeta picha adimu ya mafanikio ya mageuzi ambapo anachepuka nje ya dhana iliyozoeleka ya u-mungu mtu wa viongozi wetu (yaani kiongozi anaonekana jukwaani tu akihutubia huku akitoa maagizo pasipo kusikia mawazo ya wananchi wa kawaida) na ‘kujichanganya’ na wananchi pasipo kujali kaliba zao.
Ukidhani sifa hizo si stahili kwake, jaribu kujiuliza ‘ukiweka kando ‘undugu’ wakati wa kampeni za kuomba kura’ ni lini ulipata fursa ya kuongea na japo diwani wako-achilia mbali Naibu Waziri kama January-kumfahamisha matatizo mbalimbali yanayoikabili eneo analoongoza?
Viongozi wengi hulea dhana potofu kwamba kuwa karibu na wananchi wa kawaida kunawashushia hadhi. Ni katika mazingira ya aina hii ndio maana matendo na kauli za wengi wa viongozi wetu ni kama wanaishi sayari nyingine - hawajui hali halisi mtaani ikoje.
Wengine wanajijengea ukuta wa mawasiliano kati yao na wanaowaongoza ili kukwepa maswali kuhusu ahadi zao hewa walizotoa wakati wanaomba kura.
Nihitimishe kwa kutoa wito kuwa mageuzi ya kweli yanaweza kuletwa na wananchi wenyewe; kwani wao ndio wanaojua nini wanahitaji kwa ajili yao na jamii/nchi yao.



Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.