Showing posts with label ADMINISTRATION OF JUSTICE IN TANZANIA. Show all posts
Showing posts with label ADMINISTRATION OF JUSTICE IN TANZANIA. Show all posts

24 Jul 2013


WAKATI taifa likiwa katika maombolezo ya vifo vya mashujaa wetu saba waliouawa huko Darfur, Sudan, wakitumikia kikosi cha Umoja wa Mataifa cha kulinda amani nchini humo, Jeshi letu la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) lilifanya tukio linalostahili pongezi nyingi, japo huenda ni wananchi wachache tu wenye taarifa nalo.
Jumapili iliyopita jeshi hilo lilianza kutumia rasmi mtandao wa kijamii wa twitter likitumia ‘handle’ @jw_tz. Hatua hiyo ni ya kimaendeleo na inaonyesha kuwa jeshi letu limedhamiria kwenda na kukumbatia teknolojia ya kisasa ya mawasiliano.
Mtandao wa twitter na pengine mitandao ya jamii kwa ujumla, bado ni suala geni kwa Watanzania wengi. Na licha ya ugeni huo, ukweli kwamba umiliki na upatikanaji wa huduma ya kompyuta bado ni ‘anasa’ wanayomudu watu wachache unafanya matumizi ya twitter (na mitandao mingine ya kijamii) kutokuwa suala muhimu au maarufu kwa jamii yetu.
Hata hivyo, mitandao ya kijamii hivi sasa imekuwa sehemu muhimu ya mawasiliano; huku ikibadili kwa kiasi kikubwa upatikanaji na kupashana habari. Wakati kwa muda mrefu mawasiliano kati ya mtu na mtu yamekuwa yakitegemea aidha neno la mdomo (kwa maana ya watu kukutana au kwa njia ya barua) au magazeti na redio, na kwa kiasi fulani runinga, mitandao ya jamii na teknolojia ya mawasiliano kwa ujumla imetokea kuwa njia ya haraka ya mawasiliano katika jamii.
Ukitaka kupata mfano wa umuhimu wa teknolojia hiyo ya mawasiliano, ni jinsi ziara ya kihistoria ya Rais wa Marekani Barack Obama huko nyumbani Tanzania, hivi karibuni, ilivyoripotiwa in real time (kadri matukio yalivyokuwa yakitokea) badala ya kusubiri gazeti la kesho au ripoti za redioni au kwenye runinga.
Kadhalika, kwa kutumia mtandao wa twitter, wananchi wamekuwa wakiendesha kampeni mbalimbali, na ya hivi karibuni kabisa ni ile inayohamasisha kupinga kodi ya sim card ambapo inatumia hashtag #NoSIMcardTax.
Iwapo Serikali itasikiliza kilio cha wananchi na kusitisha au kufuta kodi hiyo, basi kampeni hiyo ya mtandaoni (hususan huko twitter) itastahili pongezi kubwa.
Pamoja na pongezi zangu kwa hatua hiyo ya JWTZ kujiunga na mtandao wa twitter, bado taasisi hiyo inakabiliwa na changamoto kubwa; hususan kutumia ipasavyo mtandao huo kama nafasi kwa jeshi hilo kuupasha umma habari stahili.
Kwa mfano, juzi Rais Jakaya Kikwete aliwaongoza Watanzania kutoa heshima zao za mwisho kwa miili ya wanajeshi wetu waliouawa Darfur, na katika mazingira mwafaka, tungetegemea akaunti ya twitter ya JWTZ ingetulea tukio hilo ‘live’ lakini haikuwa hivyo. Siwalaumu kwa vile pengine ni ugeni tu katika matumizi ya teknolojia hiyo.
Licha ya ujio huo wa JWTZ huko twitter, mtandao huo wa kijamii unatumiwa pia na baadhi ya viongozi wetu wa serikali na wanasiasa, japo idadi yao ni ndogo. Rais Kikwete ni miongoni mwa viongozi hao; huku akiweka historia ya kuwa mmoja wa marais wachache wa Afrika wanaotumia mitandao ya kijamii.
Miongoni mwa mawaziri wachache wanaotumia mtandao wa twitter ni Mheshimiwa Lazaro Nyalandu (@LazaroNyalandu), Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii. Uwepo wake katika mtandao huo umenisaidia kumfahamu katika namna ambayo pengine Watanzania wengi hawaifahamu.
Nyalandu amekuwa mfano bora wa jinsi inavyostahili na inavyowezekana kuweka maslahi ya nchi mbele ya maslahi ya kiitikadi. Lilipotokea tukio la milipuko ya mabomu jijini Arusha, Waziri Nyalandu alishiriki kikamilifu kuufahamisha umma kuhusu hatua mbalimbali zilizokuwa zikifanyika kuwasaidia majeruhi.
Na japo Nyalandu ni Mbunge wa CCM, kamwe hajawahi ku-tweet mambo ya kiitikadi, na badala yake tweets zake zimekuwa zikihusu masuala ya Tanzania na Watanzania, badala ya masuala ya CCM.
Kingine kinachopendeza kuhusu Naibu Waziri huyo ni usikivu kwa hoja mbalimbali zinazowasilishwa kwake kupitia mtandao huo. Kama ilivyo kwa Naibu Waziri mwingine, Januari Makamba (@JMakamba), Nyalandu huwasiliana na wananchi waliopo twitter kwa heshima na unyenyekevu mkubwa, kiasi yaweza kuwa vigumu kudhani ni mtu mwenye dhamana kubwa serikalini.
Ni kwa sababu hiyo, kupitia mtandao wa twitter Jumapili iliyopita nilimtumia ombi Waziri Nyalandu kumsihi awasilishe kilio cha msanii Johnson Nguza (Papii Kocha) ambaye, pamoja na baba yake Nguza Viking na kaka zake wawili, wanatumikia kifungo kirefu jela kwa kosa la kubaka.
Mwishoni wa wiki, blog mbalimbali zilichapisha barua iliyoandikwa na msanii huyo (Papii Kocha) kwenda kwa Rais Kikwete akiomba msamaha kwa yeye na familia yake, na kumwomba Rais awatoe gerezani.
Nina sababu mbili za msingi za kuguswa na suala la ‘Babu Seya’ na wanae ambao wamekuwa gerezani kwa takriban miaka 10 sasa. Kwanza, japo kuna msemo maarufu kwenye kila jela kuwa ‘kila mfungwa hana hatia’ (yaani amefungwa kwa kuonewa), tangu Nguza na wanae walipokamatwa na hatimaye kufungwa nimebaki na hisia kuwa sheria ilipindishwa dhidi yao.
Mengi yameshasemwa huko mitaani kwamba kesi hiyo ilisababishwa na visasi binafsi dhidi ya msanii huyo na wanae. Ikumbukwe kuwa katika nchi zetu masikini kuna ‘haki za aina mbili,’ kwa wanyonge ambao wanaweza kwenda jela kwa kusingiziwa tu, na kwa vigogo ambao ni kama wana kinga ya kudumu ya kisheria.
Sababu ya pili ya kumwomba Waziri Nyalandu amfikishie Rais Kikwete ujumbe wa Papii Kocha ni ya kibinadamu zaidi. Tuweke kando hisia kuwa kifungo cha Nguza na wanae ni sheria kufuata mkondo au kupindishwa.
Kama binadamu, na hasa katika Mwezi huu Mtukufu wa Ramadhan, unajiskiaje ukisoma barua ya kutoa majonzi kutoka kwa kijana mfungwa anayezeekea jela akiomba msamaha kuhusu hukumu ambayo tangu mwanzo wafungwa hao wamekuwa wakidai ni ya uonevu tu dhidi yao?
Ndio, huko jela ‘kila mfungwa hana hatia’ (yaani wafungwa wengi hudai wamefungwa kwa kuonewa hata kama walikamatwa red-handed wakifanya makosa).Lakini katika mazingira ya kawaida, ni wafungwa wangapi waliopo jela kwa takriban miaka 10 na wanaendelea kusisitiza kuwa walifungwa kwa uonevu na wanaomba hukumu dhidi yao ziangaliwe upya au wasamehewe?
Laiti ukisoma barua hiyo ya Papii Kocha (na amekuwa akiandika barua kama hiyo mara kadhaa) usipolengwa na machozi basi utakuwa na ‘moyo mgumu’ kweli.
Lakini hata tukiweka kando huruma ambayo baadhi yetu tunayo kwa Nguza na wanae, katika ubinadamu tu, msanii huyo na wanae wameshatumikia adhabu ndefu (bila kujali walitenda kosa au la), na adhabu waliyokwishapata inatosha kutoa fundisho kwao na kwa jamii kwa ujumla. Hivi sisi kama jamii tutaathirika vipi iwapo Nguza na wanawe wakisamehewa?
Kama nilivyotarajia, ‘mtu wa watu’ Naibu Waziri Nyalandu alinijibu juzi akisema kwa tweet (namnukuu) “copy that...” akimaanisha amesikia ombi langu na atalifanyia kazi.
Licha ya imani yangu kwa Nyalandu, nina imani pia kuwa Rais Kikwete atasikiliza ujumbe huo kutoka kwa mteuliwa wake. Vilevile ukweli kuwa huu ni Mwezi Mtukufu, na nina hakika Rais amefunga pia, roho ya huruma itamsukuma kusikiliza kilio cha mara kwa mara kutoka kwa Papii Kocha, kaka zake na baba yao.
Mwisho, ninaomba kila Mtanzania mwenye kuamini katika kuwasamehe waliotukosea (ikiwa ni pamoja na wanaotajwa kuwa wahanga wa makosa yaliyofanywa na ‘Babu Seya na wanawe) atajumuika nami kuwaombea msamaha wasanii hao.
Maandiko Matakatifu katika Surat Al I’mran 155 ya Kurani Tukufu na Marko 11:25 ya Biblia Takatifu ni baadhi za aya lukuki zinazotusisitiza kuhusu msamaha.



19 Aug 2010

I came across an article below in The Moscow Times of today (“Financial Investigator's Son Handles Cash for Aeroflot”) and thought it would be appropriate to rekindle the discussion on Nepotism in Tanzania we had with you a while ago, see my email of Aug. 11th herein under. Before that, in July this year, I made similar comments about the son of the former Russian prime minister {Mr. Mikhail Fradkov - now Head of the Russia’s Foreign Intelligence Service (SVR)}, Mr. Peter Fradkov, who is currently the deputy chairman of Vnesheconombank (Russia’s State Bank for Foreign Economic Relations) and also the deputy chairman of the African Coordinating Committee for Economic Cooperation with African Countries (AfroCom). See in the Aeroflot article mentioned above (read the yellow-shaded part below) on how other senior Russian government officials place their off-springs in honey places, a similar trend currently appearing in Tanzania, albeit at times we see off-springs of our officials involved in fraudulent crimes as you may read in the article below on the son (Tony) of CCM stalwart Kingunge Ngombale Mwiru (“Kingunge relative in the dock for forgery, 242 million/- theft”). As I wrote earlier, I don’t think putting kids and relatives of bigwigs in high places based on kinship only and not merit is a wise thing to do. Indeed, it is very dangerous and speaks a lot of the unhealthy political situation in a country as well as the existence of an incompetent and ineffective government .

Best regards,

Shaaban

Moscow, Russia

1 Jun 2009


NIMEMALIZA KUSOMA RIWAYA YA KWANZA YA MATUKIO YA KWELI (NON-FICTION) KWA MTUNZI MAHIRI WA RIWAYA ULIMWENGUNI,JOHN GRISHAM.BINAFSI,GRISHAM NA SIDNEY SHELDON NDIO WALIOJAZA KIJIMAKTABA CHANGU CHA VITABU MBALIMBALI.NILIANZA KUSOMA RIWAYA ZA LUGHA YA KIINGEREZA NILIPOKUWA SHULE YA MSINGI,NA SHUKRANI ZIMWENDEE BABA MZEE CHAHALI KWA KUTUSIMULIA WANAWE YALIYOMO KWENYE RIWAYA YA JAMES HADLEY CHASE YA COME EASY GO EASY,KISHA NIKAJITUTUMUA KUISOMA MWENYEWE NA KUFANIKIWA KUELEWA.TANGU MUDA HUO,MIE NA NOVELS TUMEKUWA DAM DAM.KWA UJUMLA MIONGONI MWA INTERESTS ZANGU NI PAMOJA NA KUSOMA VITABU PAMOJA NA UANDISHI BUNIFU (CREATIVE WRITING).

RIWAYA HIYO YA GRISHAM INAITWA THE INNOCENT MAN.PASIPO KUINGIA KWA UNDANI ZAIDI,INAHUSU SHERIA INAPOKWENDA MRAMA.MWAKA 1982 YALITOKEA MAUAJI YA BINTI AITWAYE DEBRA CARTER KATIKA MJI MDOGO WA ADA,PONTOTOC COUNTY JIMBONI OKLAHOMA POLISI WAKASUASUA KUMPATA MUUAJI,"KESI IKABAMBIKWA" KWA RON WILLIAMSON (MHUSIKA MKUU KATIKA STORI HIYO) AMBAYE KIMSINGI ALIKUWA NA MATATIZO YA AKILI,HALI AMBAYO ILIPELEKEA "AKIRI KUWA MUUAJI" LAKINI KATIKA SIMULIZI YA NDOTO ALIYOOTA USIKU MMOJA.RAFIKI YAKE WA KARIBU,DENNIS FRITZ NAE AKAFANYWA MTUHUMIWA NAMBARI MBILI,KWA VILE TU "RAMLI YA POLISI" (KAMA HIYO ILIYOPIGWA KWENYE
AJALI YA MWAKYEMBE) ILIONYESHA KUWA ISINGEKUWA RAHISI KWA MAUAJI HUSIKA KUFANYWA NA MTU MMOJA.HATIMAYE,RON ALIHUKUMIWA KIFO NA KUPELEKWA DEATH ROW NA DENIIS ALIHUKUMIWA KIFUNGO CHA MAISHA.KUSALIMIKA KWA "WAUAJI HAO" NI TEKNOLOJIA YA D.N.A AMBAYO ILIONYESHA KUWA HAWAKUHUSIKA NA MAUAJI HAYO.

SI LENGO LANGU KUWASIMULIA SIMULIZI KUTOKA KWENYE RIWAYA BALI THE INNOCENT MAN IMENIFANYA NIJIULIZE KUHUSU HUKUMU YA KWENDA JELA MIAKA 11 ALIYOPEWA ALIYEKUWA HAKIMU WA MAHAKAMA YA WILAYA YA TEMEKE,
JAMILA NZOTA.MWANAMAMA HUYO ALIKUTWA NA HATIA YA KOSA LA KUOMBA NA KUPOKEA RUSHWA YA SHILINGI LAKI 7 (AWALI ALIDAI MLUNGULA WA SHS MILIONI 4).

HAKI IMETENDEKA.LAKINI KWA UPANDE FLANI INAWEZEKANA HAKI HAIJAONEKANA KUTENDEKA,SI KWA HAKIMU NZOTA BALI WALE ALIOWAHI KUWAHUKUMU WAKATI WA UTAWALA WAKE.HIVI HAKUNA UWEZEKANA KWAMBA TUKIO LILOPELEKEA HAKIMU HUYO KUKAMATWA NA MLOLONGO WA MATUKIO KADHAA KATIKA MAISHA YA UHAKIMU WA JAMILA?MAANA WASWAHILI WANAPOSEMA ZA MWIZI NI 40 WANAMAANISHA PIA KUWA MWIZI ANAENDELEA NA WIZI WAKE HADI ITAPOJIRI HIYO 40

KATIKA MANTIKI HIYOHIYO,KUKAMATWA KWA HAKIMU HUYO KULIKUWA NI SAWA NA 40 YA "WIZI" WAKE,LAKINI PIA KULIASHIRIA MWISHO WA SHUGHULI ILIYOANZA AT A CERTAIN POINT OF TIME.MIMI NA WEWE HATUJUI NI LINI LAKINI YAYUMKINIKA KUAMINI KUWA KUNA HUKUMU ZILIZOTOLEWA NA HAKIMU HUYO AMBAZO ZILIKUWA INFLUENCED NA "MCHEZO" WAKE WA KUOMBA NA KUPOKEA RUSHWA.HAPA KUNA MAWILI:KUNA WALITOA RUSHWA ILI WASIKUTWE NA HATIA KATIKA HUKUMU ZA HAKIMU NZOTA,NA KUNA WALIOHUKUMIWA KWENDA JELA LICHA YA KUWA HAWANA HATIA LAKINI WALISHINDWA KUTOA RUSHWA KWA HAKIMU HUYO.

SISHANGAI KWANINI HABARI YA KIFUNGO CHA HAKIMU HUYO IMESHASAHAULIKA.NDIO TANZANIA YETU HIYO.LICHA YA AMANI NA TULIVU,TUNASIFIKA PIA KWA USAHALIFU HATA KATIKA MAMBO YANAYOWEZA KUWA NA MADHARA MAKUBWA MBELENI.TUNGETARAJI VIKUNDI VYA UTETEZI WA HAKI ZA BINADAMU AU TAASISI ZA KISHERIA ZISHIKILIE BANGO KUHUSU MAPITIO (REVIEWS) YA HUKUMU ZILIZOTOLEWA NA HAKIMU HUYO.LAKINI KATIKA UTAMADUNI WA LAISSEZ FAIRE,NDIO "IMETOKA HIYO" KAMA WASEMAVYO WATOTO WA MJINI (ILA SINA HAKIKA KAMA MSEMO HUU BADO UNATUMIKA AS KISWAHILI KINAKUA KWA KASI YA TSUNAMI).

NI UTAMADUNI HUU WA "BORA LIENDE" UNAOIMARISHA UNYONGE WA WATANZANIA NA KUDUMISHA ULAFI WA MAFISADI KATIKA KILA NYANJA.NI UTAMADUNI HUU TUTAKAOUSHUHUDIA TENA MWAKA KESHO WAKATI WA KAMPENI ZA UCHAGUZI AMBAPO WABABAISHAJI WALEWALE WALIOAHIDI BAKULI ZA MAZIWA NA ASALI HAPO 2005 (LAKINI WAKAISHIA KUTUMWAGIA UJI WA MWAROBAINI NA SHUBIRI) WATAKUJA TENA NA AHADI ZILEZILE,ILA ZIKINOGESHWA NA UONGO KUWA TUMEJIPANGA VYA KUTOSHA.BADALA YA BAKULI ZENYE MAZIWA NA ASILI TUMEAMUA KUWAJENGEA MABWAWA KABISA YATAKAYOKUWA YAKITIRIRIKA MAZIWA NA ASALI 24/7.WATAKAPOULIZWA KWANINI AWALI WALIAHIDI HIVYO NA BADALA YAKE WAKATOA MWAROBAINI NA SHUBIRI,WATAJIBU KISIASA KUWA MCHAKATO WA UTEKELEZAJI ENDELEVU WA BLAH BLAH BLAH NDIO ULIPELEKEA HIVYO LAKINI SASA KILA KITU KIKO TAYARI...TUPENI KURA ZENU ILI MFAIDI UHONDO KWENYE ARDHI YA MAZIWA NA ASALI....NA WATAPEWA.

TUMEROGWA?

28 Mar 2009


Aliyekuwa Waziri wa Miundombinu, Andrew Chenge (61), amewekwa chini ya ulinzi katika Kituo cha Polisi cha Oysterbay, Dar es Salaam, kwa zaidi ya saa saba baada ya kuhusishwa na ajali ya gari na bajaj ambayo imeua watu wawili. Waliokufa ni wanawake wawili ambao ndugu amejitokeza na kudai kuwa wote ni wageni, waliwasili juzi Dar es Salaam kutoka Mwanza na mmoja alikuwa njiani kwenda Zanzibar kuolewa. Kwa mujibu wa vyanzo vya habari, ajali hiyo ilitokea saa 10 alfajiri usiku wa kuamkia jana wakati Chenge akiendesha gari namba T 512 ACE aina ya Toyota Hilux na kuigonga bajaj hiyo namba T 736 AXC iliyokuwa na abiria hao wawili wanawake.

Chanzo hicho kilidai kuwa baada ya ajali hiyo, Chenge alikwenda kwanza nyumbani kwake na kuripoti kituoni hapo saa moja asubuhi jana na kuwekwa chini ya ulinzi na kuhojiwa hadi saa saba mchana, huku nje akisubiriwa na ndugu zake. Gazeti hili lilimshuhudia mbunge huyo wa Bariadi Magharibi akiingizwa kwenye gari la Polisi namba PT 0217 na kwenda eneo la tukio karibu na shule ya msingi ya Oysterbay katika makutano ya barabara za Karume na Haile Selassie, ambako alieleza namna ajali hiyo ilivyotokea.

Wakati mbunge huyo akitolewa katika kituo cha Polisi, kulitokea vurugu baina ya ndugu zake na waandishi wa habari, ndugu hao wakitaka kuzuia Chenge kupigwa picha, hali iliyosababisha kusukumana na kurushiana maneno makali. “Ninyi mmezidi kumwonea huyu kwani ni lazima mumpige picha ndio muuze? Hebu tokeni hapa,“ alisikika mwanamke ambaye alikuwa mstari wa mbele kusukuma waandishi, huku akilia na almanusra wapigane na mmoja wa wapigapicha waliokuwa kazini.

Hata hivyo, vurugu hizo zilimalizika baada ya waandishi kuwazidi nguvu ndugu hao na kung’ang’ania kumpiga picha mbunge huyo ambaye awali alikuwa akifunikwa magazeti na nduguze, lakini aliyatoa na kupisha waandishi wampige picha vizuri. Akiwa katika eneo la tukio, Chenge alimwelezea Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, Peter Kivuyo, namna ajali hiyo ilivyotokea na alidai ilitokea baada ya bajaj hiyo kutaka kupita gari jingine kwa kasi.

“Bajaj ile ilikuwa inataka kupita gari jingine lililokuwa likitoka Morogoro Stores, bahati mbaya kukawa na gari lingine linakuja, ile bajaj ikabana upande wangu na mimi nilikuwa katika mwendo wa kati ya kilometa 80 hadi 100 kwa saa,“ alidai Chenge. Alidai kuwa baada ya kuona bajaj ile inakwepa gari la mbele wasigongane uso kwa uso, alirudi upande wa kulia ndipo alipoigonga ubavuni kushoto. "Gari la nyuma lingesimama, dereva wake angeweza kueleza vizuri, ila baada ya ajali nikasikia watu wanaita 'Chenge! Chenge!’ nikajua niko salama, nikashuka,“ alidai.

Aliendelea kudai kuwa aliposhuka, alikuta abiria wawili wanawake wakiwa bado wanapumua ingawa kwa shida, lakini walipofika trafiki hali zao zilizidi kuwa mbaya na katika kipindi hicho chote, dereva wa bajaj alikuwa haonekani. Naye askari wa usalama barabarani aliyefika katika ajali hiyo, Mustafa Salum, alimweleza Kivuyo juu ya tukio hilo, ambapo alisema alipata taarifa za ajali hiyo saa 10.30 alfajiri na alipofika eneo la tukio, alikuta tayari abiria hao wawili wameshafariki dunia. “Niliipeleka miili ya marehemu hospitali ya Mwananyamala, ila kwa mujibu wa watu waliokuwa eneo la tukio, waliowaona marehemu hao wawili katika ukumbi wa Maisha Club,“ alisema.

Naye kaka wa mmoja wa marehemu hao, January Constantine, alisema alipata taarifa za kifo cha dada yake, Beatrice Constantine (34) asubuhi na alikwenda kutambua mwili wake hospitalini, lakini kutokana na alivyopondeka alimtambua kwa alama za mwili. Alisema dada yake ni mfanyabiashara na mkazi wa Mwanza na kwamba aliwasili Dar es Salaam, akiwa na rafiki yake huyo na ilikuwa aondoke jana alfajiri kwenda Zanzibar kwa ajili ya harusi ya rafiki yake huyo. Gazeti hili lilishuhudia gari la Chenge kwa mbele likiwa na damu, nywele na mabaki ya ubongo ambao unasadikiwa kuwa wa mmoja wa marehemu hao. Polisi pia iliokota kipande cha fuvu la mtu katika eneo la tukio.

Gari hilo lilikuwa na stika ya Bima ambayo ilikatwa Juni 6, 2006 na kumaliza muda wake Juni 6, mwaka juzi. Naye Theopista Nsanzugwanko anaripoti kuwa Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu Dar es Salaam, Suleiman Kova, alithibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema mmiliki wa bajaj hiyo ni Zuwena Nassoro na anatakiwa kuripoti katika kituo chochote cha Polisi huku wakiwa wanamshikilia Chenge Oysterbay ili kuisaidia Polisi. Alisema uchunguzi wa tukio hilo unafanywa chini ya Kivuyo na wataalamu mbalimbali ili kuondoa dhana ya upendeleo kwa kuwa Chenge ni mtu maarufu.

Chenge (62) alijiuzulu uwaziri wa miundombinu Aprili 20 mwaka jana, kutokana na kashfa ya rushwa ya dola milioni moja kutoka kampuni kubwa ya uuzaji vifaa vya kijeshi duniani ya BAE Systems. Alijiuzulu baada ya kudaiwa kupokea rushwa ili kuwezesha ununuzi wa rada ya kijeshi ya pauni milioni 20 za Uingereza na kwamba fedha hizo ziliwekwa katika akaunti yake ya kisiwa cha Jersey.

Baada ya kujiuzulu, alikaririwa akisema pamoja na tuhuma hizo, mapenzi kwa nchi yake na chama chake, ndivyo vilimlazimisha achukue uamuzi huo na kuongeza kuwa fedha zilizokutwa katika akaunti yake hiyo hazina uhusiano wowote na BAE Systems. Tuhuma hizo za rushwa zilichochea kelele pale alipohojiwa na waandishi wa habari na kujibu kuwa fedha anazotuhumiwa nazo ni 'vijisenti (fedha kidogo)'.

CHANZO: HabariLeo

I SMELL DITOPILE-LIKE ADMINISTRATION OF JUSTICE......KWA UBINADAMU WA KAWAIDA TU,GARI LAKO LIKIHUSIKA KATIKA AJALI INAYOPELEKEA HATARI YA MAISHA YA MAJERUHI PRIORITY INAKUWA KWENYE KUOKOA MAISHA YA MAJERUHI HAO (KWA MUJIBU WA HABARI HII MZEE WA VIJISENTI ALIKWENDA ZAKE NYUMBANI HADI SAA 1 ASUBUHI ALIPORIPOTI KITUO CHA POLISI NA KUHOJIWA KWA MASAA 7-(DOES IT REALLY MATTER HOW LONG THE INTERROGATION LASTED WHEN TWO PEOPLE HAD ALREADY LOST THEIR LIVES?).

ANYWAY,LET'S GIVE THE POLICE A BENEFIT OF DOUBT HOPING THAT THIS TIME HAKUTAKUWA NA USANII KAMA KATIKA ISHU YA MAREHEMU DITO.

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.