3 Nov 2008


Kizitto Noya, Kilwa Masoko
WAKATI baadhi ya watu wakiamini kuwa serikali ilitumia busara kuhakikisha fedha zilizochotwa kwenye Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA), zinarejeshwa kabla ya wezi kufikishwa mahakamani, katibu mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad haamini kama fedha hizo zimerejeshwa.

Na badala yake waziri huyo kiongozi wa zamani wa Zanzibar anasema madai ya kurejeshwa kwa Sh69 bilioni kati ya Sh133 ni mwendelezo wa usanii wa chama na serikali yake.

Maalim Seif alisema hayo mwishoni wa wiki alipokuwa akihutubia maelfu ya wakazi wa Mkoa wa Lindi kwenye Uwanja wa Kilwa Masoko, baada ya kupokea maandamano ya CUF ya kupinga ufisadi na kushinikiza wezi hao wa fedha za EPA wafikishwe mahakamani.

Alisema hawezi kuamini kwamba mafisadi hao wamerudisha fedha mpaka aone kwamba wamefikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili za kuiba Sh133bilioni.

"Mimi naamini kwamba, hakuna hata mtuhumiwa mmoja wa ufisadi wa EPA aliyerudisha fedha na kauli ya Rais (Jakaya) Kikwete ni mwendelezo wa usanii wa serikali ya CCM kuwalaghai Watanzania ili waamini kuwa kazi imefanyika," alisema.

Alisema yeye kama Watanzania wengine wenye akili timamu, hataamini kwamba kuna fedha iliyorudishwa na mafisadi wa EPA na kwamba atafanya hivyo ikiwa ataona mafisadi hao wanafunguliwa kesi mahakamani.

Kauli ya Maalim Seif ilifuatia maswali ya waandamanaji hao kumtaka aeleze msimamo wa CUF kuhusu ufisadi wa EPA na mazungumzo ya mwafaka baina ya chama chake na CCM.

Alisema CUF hairidhishwi na namna serikali inavyoshughulikia suala la EPA na ndio maana viongozi wake wakuu wanazunguka nchi nzima kufanya maandamano ya amani kupinga ufisadi huo na kuishinikiza serikali iwafikishe mahakamani.

Rais Kikwete alitaka wezi hao warejeshe fedha kabla ya Oktoba 31 na kwamba wale ambao watashindwa kuzirejesha, wafikishwe mahakamani ifikapo Novemba mosi.

Katika hotuba yake ya mwisho wa mwezi aliyoitoa Oktoba 31, Rais Kikwete alisema jumla ya Sh69 bilioni zimesharejeshwa na kwamba, ametoa ruhusa kwa watuhumiwa kufikishwa mahakamani.

Hata hivyo, hadi jana Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), alikuwa bado hajawasimamisha watuhumiwa hao mahakamani.

Kuhusu mwafaka, Maalim Seif alisema CCM ilianza kutumia nguvu ya ulaghai katika suala hilo kwa kujifanya inataka kumaliza mgogoro wa mpasuko wa Zanzibar wakati ikijua kuwa haina nia hiyo.

Alisema: "CUF tumegundua ulaghai huo na sasa tumewaambia kwamba haturudi tena kwenye mikutano ya mwafaka. Tunataka kama wana nia njema na mwafaka, wasaini makubaliano yaliyofikiwa," alisema.

Alisema CUF pia imefunga mjadala na vikao vya mwafaka baina yake na CCM baada ya kuona kuwa wenzao wa CCM wanawarubuni na kuwahadaa.

Kuhusu nguvu ya utajiri wa kifisadi, Maalim Seif alisema CCM inatumia fedha nyingi kuwarubuni wananchi kwa zawadi ili waendelee kuiamini na kuwachagua, fedha ambazo baadaye wanazirudisha kwa wizi wa mali za umma na ufisadi.

"Pia CCM wanatumia ya nguvu dola kuwatisha wananchi na kuwapiga wananchi ili wasiwe huru kuwachagua vingozi wanaowapenda," alisema.

CHANZO: Mwananchi

PENGINE HOFU YA AINA HII INATOKANA NA UKWELI KWAMBA HAO WANAODAIWA KUREJESHA MABILIONI HAYO WAMEENDELEA KUWA ANONYMOUS.IWAPO MAJORITY YA WATOA SADAKA MAKANISANI NA ZAKA MISIKITINI (SUALA AMBALO NI LA HIARI NA SI LA KISHERIA HUJIWEKA WAZI) HOW COME THEN WADAIWA (SUALA LA KISHERIA) WAHIFADHIWE?NI SIMPLE LOGIC:KAMA MDAIWA NI ANONYMOUS,ITAPOELEZWA KUWA AMELIPA DENI NA KUENDELEA KUBAKIA ANYNYMOUS BASI LAZIMA KUTAKUWA NA STRONG SUSPICION KAMA DENI HILO LIMELIPWA KWELI.

MSIMU WA MVUA,BARABARA YA KWENDA KWETU IFAKARA NI MITHILI YA SWIMMING POOL YA MATOPE.SIJUI NA HII NAYO WAWEKEZAJI WATATAKA IBINAFSISHWE.HOFU YANGU WANAWEZA WAKAICHUKUA KISHA WAKAIGEUZA SHAMBA LA MPUNGA,SASA SIJUI AKINA SIE TUTAENDA HUKO KWA UNGO...

Kwa jinsi baadhi ya wawekezaji wetu huko nyumbani walivyo wasanii (inasemekana wengi wao huja na empty briefs case na vi-credit cards vyenye dola chache tu lakini huondoka na mamilioni ya dola) si ajabu mpango huu wa kubinafsisha baadhi ya barabara za jiji la Dar unaweza kutufikisha mahala tukakuta daraja la Salender limevunjwa na kugeuzwa kibangaluu cha mwekezaji flani!Sijui njia ya mkato itakuwa baharini au vipi!Nina wasiwasi zaidi na eneo la Victoria kwani kutokana na majimaji ya eneo lile si ajabu mwekezaji akaamua kufunga barabara na kuanzisha shamba la maua.Sounds like a joke,doesnt it?Lakini ukisoma habari hii hapa chini unaweza kupata picha kama hiyo inayonijia mie

Dar es Salaam city authority`s $3bn transport crisis rescue plan, which will involve private individuals funding the multibillion-project, has elicited strong resentment from the public. 

A cross-section of motorists and city residents interviewed on Friday said they were completely opposed to the idea terming it as misplaced. Any attempt to carry on with the plan would only show how things have gone awry for the government.

``No, it can`t be! It can�t just happen! That would be completely outrageous! It will be like selling off this country,`` a visibly surprised and thoroughly agitated Rajabu Hassan Mambo, a taxi driver at Mwenge in Dar es Salaam, said.

He was reacting to the recent mooted plan, which aims to revamp the city`s road transport network through private funding that will see individuals own public utility roads.

Mambo likened the idea to giving out one`s plot to a private developer, and then upon assuming residence on the same plot, you go on to pay rent for the rest of your life.

Overwhelmed by ceaseless traffic snarl-ups on most roads heading to, and from the city centre, city authorities have embarked on an expensive and overly ambitious Dar es Salaam Transport Policy and System Development Master Plan to remedy the situation by 2030. Under the arrangement, private individuals are invited to invest in the reconstruction of sections of some roads and widening of the main highways within the city.

According to the Dar es Salaam city mayor Adam Kimbisa, any prospective private investor will be apportioned a section of the road to finance its refurbishment, and then collect toll from motorists to recover expenses incurred.

Mayor Kimbisa justified the plan, stating that it has successfully been carried out in Malaysia`s capital city, Kuala Lumpur.

Several interviewed by The Guardian on Sunday said they were disappointed with the country`s leadership.

Jankar Mbungo for example faulted the government for remaining out of touch with real issues affecting Tanzanians.

``We, ordinary citizens, are burdened with taxes already. Prices of commodities are all time high, and instead of the government making policies that will solve the country`s problems it`s making life more difficult for us.`` Mr Mbungo stated.
SOURCE: Sunday Observer


(MY APOLOGIES FOR THE GRAPHIC IMAGE BUT I HOPE THIS SENDS A STRONG MESSAGE TO THOSE WHO WANT TO DRAG OUR COUNTRY INTO THIS SORT OF CRUELTY)
Mogadishu, Somalia - A 13-year-old girl who said she had been raped was stoned to death in Somalia after being accused of adultery by Islamic militants, a human-rights group said.
Dozens of men stoned Aisha Ibrahim Duhulow to death Oct. 27 in a stadium packed with 1,000 spectators in the southern port city of Kismayo, Amnesty International and Somali media reported, citing witnesses. The Islamic militia in charge of Kismayo had accused her of adultery after she reported that three men had raped her, the rights group said.

Initial local media reports said Duhulow was 23, but her father told Amnesty International she was 13. Some of the Somali journalists who first reported the killing later told Amnesty International that they had reported she was 23 based upon her physical appearance.

Calls to Somali government officials and the local administration in Kismayo rang unanswered Saturday.

"This child suffered a horrendous death at the behest of the armed opposition groups who currently control Kismayo," David Copeman, Amnesty International's Somalia campaigner, said in a statement Friday.

Somalia is among the world's most violent and impoverished countries. The nation of some 8 million people has not had a functioning government since warlords overthrew a dictator in 1991 then turned on each other.

A quarter of Somali children die before age 5; nearly every public institution has collapsed. Fighting is a daily occurrence, with violent deaths reported nearly every day.

SOURCE:AP

Mitambo ya Richmond ikiwasili kwa mbwembwe.Kampuni hiyo ya kitapeli imerithiwa na Dowans.Picha kwa hisani ya MICHUZI

Kampuni ya Dowans Tanzania Ltd imetangaza rasmi zabuni ya kuuza mitambo yake ya kuzalisha umeme ikiwa ni miezi mitatu baada ya serikali kusitisha mkataba wake na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco). 

Dowans Tanzania Limited ilirithi mkataba wa kuiuzia umeme wa megawati 120 Tanesco kutoka kwa Kampuni ya Richmond Development LLC ambayo baadaye iligundulika kuwa ni kampuni hewa. Serikali ilifikia uamuzi wa kusitisha mkataba huo Agosti mosi mwaka huu baada ya kuridhika kuwa mkataba huo haukuwa halali wala haukuwa na nguvu kisheria. 

Serikali pia ilisema ilibaini iwapo mkataba husika ungekuwa halali, uhamishaji wa mkataba kutoka RDVCO badala ya Richmond Development LLC kwenda Dowans Tanzania Ltd, haukufuata msingi wa mkataba.“Hivyo uhamishaji haukuwa halali na ifahamike kwamba mkataba ulikuwa baina ya Richmond Development Company LLC na Tanesco na siyo na REDVCO na Tanesco,” alisema. 

Tangazo ambalo limetolewa na kampuni hiyo leo kwa vyombo vya habari, limesema watu au kampuni makini ambazo zitakuwa na nia ya kununua mitambo hiyo wanakaribishwa kuinunua. Kutolewa kwa tangazo hilo la kuuza mitambo yake, huenda ikawa ni ishara ya kampuni hiyo kufungasha virago baada ya kimya kingi tangu mkataba huo usitishwe. 

Baada ya kusitishwa kwa mkataba huo, Tanesco imekuwa ikitumia pamoja na vyanzo vingine vya umeme, mitambo yake ya megawati 100 iliyojengwa na Kampuni ya Watsilla ya Finland ili kufidia upungufu uliotokana na kuondoka Dowans. Tanesco pia imekuwa ikinunua umeme kutoka kwa kampuni za Songas na IPTL. 

Siku chache baada ya kusitishwa kwa mkataba huo, mmoja wa maofisa wa Dowans aliiambia HabariLeo kuwa walikuwa na njia nyingi za kufanya na mitambo hiyo ikiwa kuikodisha au kuiuza kwa watu wengine. “Kukatishwa kwa mkataba haina maana hatuwezi endelea na kazi, tutatafuta wateja wengine kama kampuni za migodi na kuwauzia umeme au tunaweza kukodisha mitambo yenyewe,” alisema ofisa huyo. 

Kwa mujibu wa tangazo hilo, mitambo hiyo ina mashine tano za uzalishaji wa umeme ambazo mnunuzi atazinunua kwa bei ya hali yake ilivyo kwa wakati wa kununua. “Vifaa vyote ikiwa pamoja na vipuri na vifaa vingine vya pembeni vipo na vitauzwa kwa pamoja kama bidhaa moja,” lilisema tangazo hilo. 

Mkataba kati ya Tanesco na kampuni ya Richmond Development LLC umekuwa ni mmoja wa mikataba ambayo ilivuta hisia za watu wengi kitu ambacho kilisababisha kuundwa kwa Kamati iliyokuwa chini ya uenyekiti wa Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe (CCM), ambako kutokana na ripoti hiyo, aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa alijiuzulu. 

Wengine waliojiuzulu ni aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi na Ibrahim Msabaha ambaye alikuwa Waziri wa Wizara hiyo na kabla ya kuhamishiwa Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Kutokana na mapendekezo ya ripoti hiyo, serikali iliahidi kuyafanyia kazi mapendekezo ya ripoti hiyo, ambapo moja ya hatua iliyochukuliwa ni kusitisha mkataba na Dowans.

 CHANZO : HabariLeo

I SMELL SOMETHING FISHY HERE.HII TENDA YA KUTANGAZWA KWA PRESS RELEASE INAZIDISHA SUSPICION YANGU.KWANINI ISIWE TANGAZO LA ZABUNI GAZETINI BADALA YA KU-SEEK ATTENTION KWENYE MAGAZETI,AMBAYO MENGI YAO HUWA HAYANA MUDA WA KU-READ BETWEEN LINES YANAPOPATA STORIES?I SUSPECT KUNA DILI INATAKA KUCHEZWA HAPA.POTENTIAL BUYER WA MITAMBO HIYO ATAKUWA TANESCO (CLICK HAPA NA HAPA KUPATA HINT). ITANUNULIWA KWA UTARATIBU UNAOONEKANA TRANSPARENT (HIVI TRANSPARENCY INA UMUHIMUWOWOTE  KATIKA KUNUNUA BIDHAA BOMU?) KISHA MITAMBO HIYO (AMBAYO "WAMBEA" WANADAI NI INJINI MBOVU ZA NDEGE) ITAISHIA "KUBUMA".DOWANS WAKATI HUO ISHAKUWA KAMPUNI MFU,KAMA MZAZI WAKE RICHMOND.LET'S WAIT AND SEE!

2 Nov 2008

Lewis Hamiliton made history,a few minutes ago,after becoming the first Black and the youngest  winner of Formula One Championship.And another history could be written day after tomorrow if Obama wins in the U.S. Presidential Election.Where is James Watson?

Pakistani police break up marriage between 4-year-old girl and 7-year-old boy

Mohammad Ismil (C) holds his 7-year old son Mohammad Waseem (R) and his son's 4-year old "bride" Nisha (L) at a police station in Karachi, Pakistan

Pakistani police raided a child marriage ceremony in the city of Karachi and arrested a cleric who was presiding over the wedding of a 4-year-old girl and a 7-year-old boy.

Pakistani law says people must be 18 to marry but some Islamic laws allow girls to marry after puberty.

Yet despite the laws, young girls are often given away in marriage to settle disputes or pay off debts.

Police said they raided a house on Thursday evening following complaints from residents, including a former district government official, who said the girl was being married off by her father for about 500,000 rupees (£3,750).

The official told Reuters: 'We had noticed some gatherings at this house for a couple of days.

'Last night I went there and saw that the little girl was actually getting married. So we called the police.'

Some other residents said the marriage was taking place to resolve a long-standing family dispute. Police said they had arrested the boy's father but the girl's father had run away.

SOURCE: Dailymail



Comedians flani wamemuingiza mkenge Gavana Sarah Palin kumuaminisha kuwa anaongea na Rais wa Ufaransa Nicholas Sarkozy.Sikiliza kichekesho hicho kwa ku-click link ifuatayo hapa chini:


Talking of Gov Palin,kituko kingine ni kwamba katika mkutano wake wa kampeni huko Polk City,Florida jina la mgombea mwenza wake,John McCain,was surprisingly missing kama inavyoonekana katika picha ifuatayo hapo chini.Au ndio ameshaanza kampeni za 2012?


1 Nov 2008

Picha kwa hisani ya SPOTI NA STAREHE

Ubabaishaji unakwamisha sana maendeleo ya taifa letu.Lakini hapa nataka nizungumzie ubabaishaji kwenye uongozi na uendeshaji wa vilabu vya Simba na Yanga.Hebu soma kwanza hapa chini kabla hatujaendelea na mada hii ya kupotezea muda.
MWENYEKITI wa klabu ya Simba Hassan Dalali amemteua Mkurugenzi wa Kampuni ya Aurora Security, Ally Suleiman kuwa mshauri wake atakayesaidia kumshauri kuhusiana na mambo yote yanayohusu masuala ya uongozi wa Simba. 

Akizungumza Dar es Salaam jana, Dalali alisema ameamua kuwa na mshauri ili aweze kuiendesha klabu yake kwa umakini na kufuata mwongozo ambao utaisadia klabu hiyo. 

Dalali alisema Suleiman amekuwa mtu wa karibu, ambaye ametoa mchango mkubwa ndani na nje ya klabu, hivyo ameona ni muhimu na kuwa uteuzi huo ni kujenga Simba yenye umoja na mshikamano.
Alisema klabu yake ipo katika mikakati ya kuhakikisha Simba inakuwa klabu kubwa, huku ikiimarisha timu yake na kuwa mfano wa kuigwa. 

"Uteuzi wa mshauri wangu umezingatia vigezo vingi ikiwemo ukaribu wake katika mambo ya msingi yanayoihusu klabu yetu," alisema Dalali.

Akizungumzia uteuzi huo, Suleiman alisema amefurahi kupata wadhifa huo na kuahidi kuisaidia klabu hiyo kwa hali na mali lengo likiwa ni kujenga Simba imara
CHANZO:Majira
Baada ya kufungwa na Yanga ndio Dalali anakumbuka umuhimu wa kuwa na mshauri!?Kwa tafsiri nyingine ni kwamba kwa muda wote tangu apate uenyekiti wa Simba m-babaishaji huyu amekuwa akiongoza kwa kubahatisha.Ndio!Kama sio hivyo,mshauri wa nini muda huu? Yaani ni ubabaishaji juu ya ubabaishaji.

Mimi ni mpenzi wa Simba.Zamani Simba ikifungwa basi ni majonzi makubwa.Katika familia yetu,watoto wote wanane tunaipenda Simba.Marehemu Mama (Mungu Amlaze Mahali Pema Peponi) alikuwa mpenzi wa Pan Africa,kwa sababu mpwae,Gordian Mapango,alikuwa mchezaji wa timu hiyo.Baba aliamua kuisapoti Yanga,sio kwa vile anaipenda bali kuleta "usawa" ndani ya familia.

Kwa miaka kadhaa sasa,nimebaki kuwa mpenzi-jina tu,it doesnt really make any difference Simba ikishinda au ikifungwa.Sababu kuu ya kupoteza mapenzi kwa Simba,na soka ya Tanzania kwa ujumla,ni ubabaishaji uliopita kiasi wa viongozi wa klabu hiyo kongwe.Ubabaishaji huo umepelekea timu hiyo kukimbiwa na wafadhili kibao na kupoteza udhamini mbalimbali.Nani mwenye akili timamu atawekeza kwenye biashara kichaa?Ukiona mtu anapanda mpunga jangwani basi hicho sio kilimo bali tambiko.Ndo maana nashawishika kuamini kwamba uwepo wa Manji hapo Yanga unaweza kuwa ni "zaidi ya mambo ya soka".

Nirudi kwenye title ya post hii.Nilitegemea Simba ingefungwa na Yanga.Na nilitegemea kipigo kikubwa zaidi ya hilo bao moja.Kama Toto Africa waliweza kutufunga bao 4-1,tungetegemea nini katika mechi na Yanga?Anyway,kipigo ni kipigo.Mategemeo yangu ya kipigo yametimia,japo kwa idadi tofauti na niliyokuwa naitarajia.Kingine nilichadhani kingeandamana na kipigo hicho ni kuutimua uongozi mzima wa Simba.Hilo halijatokea lakini naamini viongozi hao wamekalia kuti kavu.By the way,uongozi wa Simba na Yanga ni zaidi ya kukalia kuti kavu;ni sawa na kibonge cha mtu kuning'inia kwenye utando wa buibui.Mtu mwenye mtizamo makini hawezi kutamani kuongoza timu hizi za kibabaishaji,ambazo lugha wanayoelewa "wanachama" ni ushindi tu.

Of course,timu inatakiwa ishinde kila mechi.Lakini timu itashinda vipi ikiwa haina vyanzo vya mapato zaidi ya kutembeza bakuli kama ombaomba?Hao wachezaji wanakula nini kabla ya kujituma uwanjani?Au ni timu za kiroho ambapo Neno la Mungu linashinda mahitaji ya fedha na vifaa?Kwanini wachezaji wasipokee rushwa iwapo viongozi wanawaibia mishahara yao kiduchu inayopatikana kwa migomo?Wanachama wababaishaji wa klabu hizi wanajua kupiga majungu tu lakini hawana mchango wowote kwa ustawi wa klabu hizi.Ndio maana akiondoka mfadhili mmoja timu inakuwa hohehahe.Na ndio maana Manji amekuwa mungu-mtu hapo Yanga (na mwenyekiti Madega amegeuka kuwa msemaji wa familia ya mfadhili kuhusu ugonjwa wa mfadhili huyo!)

Je kuna ufumbuzi wa tatizo hili la ubabaishaji wa viongozi na wanachama wa Simba na/au Yanga?Kwa mtizamo wangu nadhani ufumbuzi upo lakini unahitaji udikteta wa aina flani.Unajua kuna udikteta kwa ajili ya watu na udikteta dhidi ya watu.Udikteta kwa ajili ya watu ni kama ule wa Sokoine:kwa wahujumu wa uchumi Sokoine alikuwa dikteta,lakini kwa wananchi wengi kiongozi huyo alikuwa ni shujaa na mkombozi.Sihitaji kuelezea dikteta dhidi ya watu ni wa aina gani,lakini anaweza kuwa hata anayethamini haki za binadamu za mafisadi wachache badala ya walalahoi walio wengi.Je udikteta kwa ajili ya watu unawezaje kuokoa vilabu vyetu na soka la Tanzania kwa ujumla?Ni kwa serikali kutumia sheria kali katika kuleta mageuzi ya kudumu katika vilabu vya soka.Najua kuna ishu za watu kwenda mahakamani kupinga maamuzi flani,lakini ukweli unabaki kwamba sheria zikiandaliwa na kusimamiwa vizuri basi wahuni wanaokimbilia mahakamani watafyata mkia.Njia nyepesi ya kuvibana vilabu hivyo ni kutunga sheria inayovitaka kujisajili upya,kwa mfano.Pia sheria hiyo inaweza kutamka bayana aina ya viongozi,namna ya uendeshaji wa vilabu unavyopaswa kuwa na hata aina za wanachama.FIFA itatufungia kwa vile serikali imeingilia mambo ya soka?Why care!kwani sasa hatujafungiwa na tumeendelea kuwa kichekesho kila mwaka?Bora tu tufungiwe ili tuweze kujipanga vyema kuliko kuendeleza ubabaishaji huu.Au msomaji unasemaje?


DEARBORN HEIGHTS/DEARBORN - Illinois Sen. Barack Obama will win Tuesday's election and become the next president of the United States, according to a recent poll conducted by Zogby International, an American market research and opinion-polling firm.

Their Reuters/C-SPAN/-Zogby Poll out Friday morning indicates the support for both candidates had solidified and remained unchanged from the previous several days. Obama was at 50.1 percent among likely voters, while McCain was at 43 percent. That put Obama outside the margin of error five days before the actual vote.

"With less than a week to go, today's numbers are not a good development for McCain," said John Zogby, founder of Zogby International. "There is no momentum for him, and the clock is starting to fun short."

Out of 1, 202 likely voters polled Oct. 27-29, Obama increased his lead among independent voters to 19 points — up from 16 points on Oct. 29 — while McCain's support among his base of Republican voters waned just slightly, dropping two points to 85 percent.

Obama's support among Democratic Party voters remained steady at 84 percent, the poll showed.

According to the Zogby International Web site, www.zogby.com, the poll sampled 1,202 likely voters by phone with approximately 33 questions asked. The margin of error is plus or minus 2.9 percentage points. Interviews were conducted using live telephone interviewers in Zogby's in-house call center in Upstate New York.

A poll released Thursday shows Obama leads by five points among men, 49 percent to 44 percent for McCain. Among women, the Democratic candidate leads by a 10-point margin, 52 percent to 42 percent.

Among liberals, Obama wins 86 percent support, while McCain wins 75 percent of conservatives. Among moderates, Obama wins 65 percent support, compared to 26 percent for McCain.

"But six days, including Election Day, is an eternity and McCain cannot be counted out yet, though he may need a wing and a prayer," Zogby said Thursday.

According to a Zogby poll conducted Oct. 10-15, Arab American voters are expected to have a significant impact on Tuesday's election. The poll sampled 504 likely voters with approximately 41 questions asked. The margin of error is plus or minus 4.5 percentage points.

The poll finds about one-third of Arab Americans live in battleground states — Michigan, Virginia, Ohio, Florida and Pennsylvania. In Michigan, Arab Americans comprise about 5 percent of the state's total population, compared to 1.5 percent in Pennsylvania.

According to the poll, Obama leads McCain by a three-to-one margin among Arab American voters, in both the two-way match-up and the four-way match-ups. This represents the greatest support ever recorded for a Presidential candidate among Arab American voters, the poll finds.

Vice presidential candidate Joe Biden also out-performs Republican candidate Sarah Palin among all groups, including Arab Americans, with Biden's margin being 58/31 and Palin's 58/39.

When asked to name the two most important issued in the election, jobs and the economy were the most frequently mentioned, according to the poll. The second and third most important issues are the Iraq war and health care.

A recent statement issued by Michigan Secretary of State Terri Lynn Land said than an estimated 5 million voters, or approximately 70 percent of registered voters, will case ballots on the Nov. 4 election.

SOURCE: Press&Guide
"Voter enthusiasm is at an all-time high and because of that I expect an unprecedented number of voters to attend the polls on Election Day," Land said. "I encourage you to take time to educate yourself on the candidate and issues, and the cast your ballot on Election Day."

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.