14 Oct 2009


Na Fredy Azzah

MAKAMU Mwenyekiti wa CCM, Pius Msekwa, amesema kashfa za ufisadi zinazowakabili baadhi ya viongozi wake, zimekiumbua chama hicho pamoja na serikali yake.

Akiwahutubia wanafunzi wa matawi ya CCM ya vyuo vikuu vilivyopo jijini Dar es Salaam, wakati wa maadhimisho ya kumbukumbu ya miaka 10 ya kifo cha Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere jana, alisema ufisadi ambao umewakumba wengi umesababishwa na tabia ya viongozi kulindana na kutosimamia kikamilifu maadili ya uongozi yaliyoainishwa ndani ya katiba ya CCM.

Alisisitiza kuwa tabia hiyo ni kinyume na misingi ambayo Baba wa Taifa, aliwaachia Watanzania....ENDELEA

WAKATI HUOHUO

WASOMI na wanazuoni nchini, wamesema nchi haina dira na kwamba kuna mpasuko mkubwa ambao usiposhughulikiwa mapema, nchi inaweza kuingia kwenye machafuko.

Wakizungumza juzi katika baraza lililopewa jina la Mbongi, lililoandaliwa na Kigoda cha Taaluma cha Mwalimu Julius Nyerere, walisema mpasuko hiyo ni pamoja na ya udini, ukabila, ukanda, matatizo ya vitambulisho Zanzibar pamoja na hofu ya kuvunjika muungano...ENDELEA

CHANZO: Mwananchi


Police recoup £1.4m from criminals in last two weeks as war on crime profits gathers pace



Oct 12 2009 by Rebekah Oruye, Birmingham Mail



WEST Midlands Police is driving home the message that crime does not pay after confiscating £1.4 million from criminals in the past two weeks.

In addition, nearly £100,000 in cash was seized from a car on the M6 in Birmingham, believed to have been intended for criminal use.

Det Chief Insp Simon Wallis, head of the force’s economic crime team, said: “This money has been taken from those who think crime is an easy way to make money.

“It brings West Midlands Police to a total of £15 million seized from criminals in the last 18 months.

“On many of these occasions through financial investigation and the confiscation process we are able to trace monies and give them back to victims. In cases where money is transferred abroad, it still is able to be retrieved. Crime does not pay. We will investigate those involved in criminality to ensure that they do not enjoy their ill gotten gains.”

Among the success stories for the police is the near £900,000 seized from Walsall conman Mponjoli Malakasuka, who had been stealing and exporting high powered luxury cars.

Malakasuka, aged 36, from the Yew Tree estate, was ordered to pay back the money in one month or face an additional four years in jail. He was originally sentenced to three-and-a-half years in July 2008 for conspiracy to steal.

Malakasuka had used a variety of sophisticated methods to steal prestige vehicles which he then exported out of the UK to Tanzania and Kenya. The cars were stolen both through car key burglaries and a variety of identity fraud and fake hire purchase agreements.

The cars included Mercedes Benz S320 CDi and Porsche Cayenne cars. In all over £300,000-worth of vehicles were stolen.

At the time of his arrest police discovered Malakasuka to be living a life of luxury in his four-bed house. At his address were pictures of luxury houses in Tanzania into which officers believed he had invested his fraudulent cash.

The court accepted the houses in Tanzania were proceeds of his criminality. Financial investigators were also able to show thousands of pounds passing through in excess of 70 bank accounts in the UK and Tanzania including one account which alone had £350,000. Det Sgt Jonathan Jones, who led the investigation for the Economic Crime Team, said: “This has been a great investigation, as not only have we stopped fraud and theft, but we have now recovered the profit that this man made from his criminality.”

In a separate case a money launderer from Birmingham was ordered to pay back more than £450,000 of his criminal profit.

Barrington Fulcott, aged 48, from Kingstanding, was told to pay £450,386 at the hearing in Birmingham Crown Court.

He was given six months to return the cash, or face an extra four years in prison. Fulcott was originally sentenced to 42 months in prison in February 2008 in relation to three counts of money laundering.

He had gathered considerable wealth from his criminal activity which had allowed him to purchase five properties in the West Midlands and begin the development of a large home in St Annes, Jamaica.


13 Oct 2009


WAKATI TUNAADHIMISHA KIFO CHA MWASISI WA TAIFA LA TANZANIA,MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE,TUNAPASWA PIA KUTAFAKARI MAMBO KADHAA AMBAYO KWA KIASI KIKUBWA HAYAKUPATA FURSA YA KUJADILIWA WAKATI WA UHAI WA NYERERE,NA KUYAJADILI BAADA YA KIFO CHAKE INAWEZA KUTOA TAFSIRI POTOFU YA UTOVU WA NIDHAMU.

MENGI YAMEONGELEWA KUHUSU MCHANGO WA NYERERE KATIKA HARAKATI ZA UHURU WA TANGANYIKA,NA NDOTO YAKE YA UMOJA ILIYOZAA TAIFA LA TANZANIA KWA KUUNGANA NA ZANZIBAR,PAMOJA NA MCHANGO WA TANZANIA KATIKA MAPAMBANO YA UHURU KUSINI MWA BARA LA AFRIKA.

BAADHI YA MISINGI ALIYOJENGA NYERERE BADO IPO LICHA YA JITIHADA KUBWA ZA "WANAFUNZI WAKE" KUIBOMOA.WATANZANIA BADO TUNASIFIKA KWA NAMNA TUNAVYOTHAMINI UNDUGU WETU (USHAHIDI UKIWA NENO "NDUGU" KABLA YA MAJINA YETU JAPO WAWAKILISHI WETU BUNGENI WANAITWA WAHESHIMIWA).

KAMA KATUNI YA KIPANYA INAVYOONYESHA HAPO JUU,NYERERE PIA ALITUFANYA TUWE WAPOLE KUPITA KIASI.UPOLE HUO ZAMA ZA CHAMA KIMOJA ULIIMARISHWA NA SHERIA ZILIZOTULAZIMISHA KUAMINI KUWA KIONGOZI YUKO SAHIHI WAKATI WOTE.MADHARA YA IMANI HIYO NI HUJUMA INAYOFANYA NA BAADHI YA WANASIASA KUAHIDI MAMBO WASIYOWEZA KUTEKELEZA LAKINI KWA VILE WATANZANIA NI WAPOLE,NA WANAOAMINI KILA ASEMACHO KIONGOZI,WAMEENDELEA KUTUTAWALA NA SI AJABU WAKAENDELEA KUTUTAWALA ZAIDI.WANAFAHAMU KUWA WANAOWATAWALA HAWANA JEURI YA KUHOJI AHADI ZISIZOTEKELEZEKA ACHIULIA MBALI VITENDO VYA UFISADI VINAVYOFANYWA NA WATEULE WA VIONGOZI HAO.

PAMOJA NA HESHIMA YANGU KUBWA NILIYONAYO KWA BABA WA TAIFA,NALAZIMIKA KUMLAUMU KWA UZAZI NA KULEA TABAKA AMBALO LEO HII TUNALIITA MAFISADI.SIAMINI KABISA KUWA BAADHI YA WANAFUNZI WA MWALIMU WALIKURUPUKA GHAFLA KUWA MATAJIRI KUPINDUKIA HUKUN WAKIKUMBATIA WAGENI NA MARAFIKI ZAO.NAAMINI KUWA WATU HAWA HAWAKUWAHI KUWA WAJAMAA JAPO WALIIMBA NA KUCHEZA UJAMAA MAJUKWAANI WAKIWA NA MWALIMU.

TUMWANGALIE MTU KAMA KINGUNGE NGOMBALE MWIRU.HUYU ALIKUWA SWAHIBA WA MWALIMU NA TULIAMBIWA KUWA DINI YAKE NI UJAMAA.HIVI KWELI KINGUNGE AMEBADILIKA GHAFLA KUWA MTETEZI WA MAFISADI AU ALIKUWA ANAMZUGA TU MWALIMU ZAMA ZA UTAWALA WAKE?

BAADHI YA MADUDU TUNAYOSHUHUDIA LEO YALIANZA ZAMA ZA MWALIMU.KULIKUWA NA KIJITABIA CHA MTU AKIHARIBU HAPA ANAHAMISHIWA PALE,KAMA AMBAVYO AKINA MATTAKA WALIVYOSHINDWA KUIOKOA TRC LAKINI WAKAPELEKWA BIMA.SI KWELI KWAMBA NYERERE HAKUENDEKEZA URAFIKI,MAANA ISINGEKUWA HIVYO BASI ASINGEMPIGIA DEBE MKAPA,RAIS AMBAYE BAADA YA KUTOKA IKULU AMEACHA WATANZANIA WENGI WAKISHANGAA KWA NAMNA ALIVYOTUMIA FURSA HIYO KUJITAJIRISHA (REJEA ISHU YA KIWIRA).

BAADHI YA WACHAMBUZI WA SIASA ZA AFRIKA WANAMTUHUMU MWALIMU KUWA WAKATI ANASTAAFU MWAKA 1985 ALIACHA TAIFA LIKIWA KATIKA HALI MBAYA SANA KIUCHUMI.KUNA WANAODAI KWAMBA UAMUZI WA KUNG'ATUKA UNAOPIGIWA MSTARI KAMA MFANO WA KUIGWA ULIKUWA MATOKEO YA KUKWEPA MAJUKUMU.WAPO WANAOKWENDA MBALI ZAIDI NA KUDAI KWAMBA MWALIMU ALIPASWA KUWAOMBA MSAMAHA WATANZANIA KWA KULIFIKISHA TAIFA LILIPOFIKA WAKATI ANASTAAFU.

HATA SIASA YA UJAMAA NAYO IMEZUA MJADALA KWA BAADHI YA WACHAMBUZI WA SIASA.KUNA WANAOONA KUWA NYERERE ALIKUWA MUUMINI PEKEE WA ITIKADI HIYO HUKU AKIWA AMEZUNGUKWA NA KUNDI LENYE BAADHI YA MATAPELI WA KISIASA WALIOKUWA WANAMUUNGA MKONO JAPO NAFSINI MWAO WALIKUWA NA MAWAZO TOFAUTI.NA MFANO UNAOREJEWA MARA NYINGI NI UAMUZI WA KUUA AZIMIO LA ARUSHA MARA BAADA YA MWALIMU KUTOKA MADARAKANI NA KULETA AZIMIO LA ZANZIBAR.

TATIZO JINGINE LA UJAMAA LIKO KWENYE UKWELI KWAMBA ULIKUWA MITHILI YA JARIBIO,AMBALO KWA KIASI KIKUBWA HALIKUFANIKIWA HADI MWALIMU ANAONDOKA MADARAKANI.KUTOKUFANIKIWA HUKO KULICHANGIWA NA NAMNA UJAMAA ULIVYOSAMBAZWA,AMBAPO MATUMIZI YA NGUVU YALIKUWA JAMBO LA KAWAIDA.REJEA NAMNA OPERESHENI VIJIJI VYA UJAMAA ILIVYOWAATHIRI BAADHI YA WATANZANIA KWA KUONDOLEWA MAHALA WALIPOJIJENGA NA KUPAZOWEA NA KUPELEKWA "UGENINI."HOJA HAPA SI KWAMBA WAZO LA UJAMAA LILIKUWA ZURI AU BAYA BALI KAMA LILIKUWA LINATEKELEZEKA HASA IKIZINGATIWA KWAMBA TANZANIA ILIKUWA TEGEMEZI KIUCHUMI TANGU ILIPOPATA UHURU WAKE 1961.

KUDHANI KWAMBA MAFISADI WALIIBUKA GHAFLA NI KUKWEPA KUDADISI CHANZO CHA TATIZO.MAFISADI WENGI NI TABAKA LILILOIBUKA MIAKA YA MWISHO WA HARAKATI ZA UHURU NA BAADA YA KUPATIKANA UHURU.NI KIKUNDI CHA WARASIMU WALIOTUELEKEZA NAMNA YA KUFANYA JAPO WAO WENYEWE HAWAKUFANYA HIVYO.TABAKA HILI LILIKUWA LINASUBIRI MWALIMU AONDOKE MADARAKANI LIANZE "KUFANYA VITU VYAKE",AND SURE THEY DID!

NYERERE ALIZUNGUKWA NA LUNDO LA WANAFIKI.KISICHO NA HAKIKA NI KAMA ALIFAHAMU UNAFIKI WAO NA KUWAVUMILIA AU WALIMZIDI AKILI.YOTE MAWILI HAYAMTOI LAWAMANI KWA VILE PINDI KIONGOZI ANAPOCHAGUA WASAIDIZI WENYE MAPUNGUFU,AIDHA KWA KUTOJUA AU KWA MAKUSUDI,NI LAZIMA ABEBE LAWAMA KWA UTEUZI MBOVU.

UJAMAA,REGARDLESS YA KUWA ITIKADI YA MAJARIBIO,UNGEWEZA KUZAA MATUNDA MEMA IWAPO UNGEGUSA KILA MTANZANIA PASIPO KUJALI NAFASI YAKE KATIKA JAMII.NI DHAHIRI KUWA LAITI HILO LINGETIMIA BASI TUSINGESHUHUDIA AWAMU YA PILI (BAADA YA NYERERE) IKIENDESHA TAIFA KWA MTINDO WA LAISSEZ FAIRE (BORA LIENDE) NA AWAMU YA TATU IKITUAMINISHA UJIO WA ZAMA ZA UWAZI NA UKWELI HUKU WATU WANAUZIANA MGODI WA KIWIRA KWA BEI YA KISHKAJI.YA UFISADI KILA MMOJA WETU ANAFAHAMU HALI ILIVYO.

KWA VILE MIE NI MKRISTO,NA KWA VILE MILA ZETU ZINAKATAZA KUWASEMA VIBAYA MAREHEMU,BASI NAUNGANA NA WATANZANIA WENZANGU KUMTAKIA MWALIMU PUMZIKO LA MILELE NA MWANGA WA MILELE,APUMZIKE KWA AMANI,AMINA.HATA HIVYO,KAMA SIE WAKATOLIKI TUNAVYOAMINI KUWA ROHO ZA MAREHEMU ZIKO "HAI" TUKIZIKUMBUKA KWA SALA,BILA SHAKA MWALIMU ANAJUTA KUCHAGUA "MARAFIKI" AMBAO BAADA YA KUONDOKA KWAKE WAMEGEUZA TANZANIA KUWA SHMBA LA BIBI,WANACHUMA WATAKAVYO,WANAKWIBA WATAKAVYO,LAKINI KWA VILE ALITUGEYUZA WAPOLE NA WAGUMU KUDAI HAKI ZETU,TUNAENDELEA KUVUMILIA MACHUNGU.

MWISHO,KWA VILE LAWAMA PEKEE HAZIWEZI KUSAIDIA KUTUFIKISHA TUENDAKO,JUST LIKE MAKALA NDEFU ZA KUMBUKUMBU YA MWALIMU ZISIVYOWEZA KUWAKWAMUA WALALAHOI,NI MUHIMU KUITUMIA SIKU HII KUJIULIZA SWALI HILI MUHIMU.JE NYERERE NA WAPIGANIA UHURU WENZAKE WALIPAMBANA NA MKOLONI KWA MINAJILI YA KUMUONDOA MTU MWEUPE NA KUMUWEKA MKOLONI MWEUSI (MAFISADI,et al)?

ANGALAU MKOLONI ALIKUWA NA EXCUSE YA KUTUNYONYA NA KUTUPELEKESHA.HAKUWA MTANZANIA,HAKUWA NA UCHUNGU NA NCHI HII,NA HAKUFIKISHWA ALIPOFIKIA KWA JITIHADA ZA WATANZANIA.LAKINI MAFISADI NI WATANZANIA WENZETU,WANALAZIMIKA KUWA NA UCHUNGU NA NCHI YETU KWA VILE KWA VYOVYOTE VILE BAADHI YA WAATHIRIKA WA UFISADI WAO NI NDUGU ZAO WA MBALI (WA KARIBU WAMESHATENGENEZEWA ULAJI SOMEWHERE).

NJIA BORA YA KUMUENZI MWALIMU NI KUREKEBISHA PALE ALIPOKOSEA (KWA MFANO KUWALEA VIONGOZI WALIOMZUGA KUWA NI WAJAMAA LAKINI WAKAGEUKA MAFISADI MARA BAADA YA KUONDOKA KWAKE) NA KUIANGALIA TANZANIA KAMA NCHI YETU SOTE NA SI YA WATEULE WACHACHE (AMBAO MARA NYINGI HAWATAKI KUSIKIA SAUTI TOFAUTI NA YAO UNLESS IWE NI VIGEREGERE AU MAKOFI YA PONGEZI).TUMUENZI MWALIMU KWA KUKATAA NCHI YETU KUWA SHAMBA LA BIBI HUKU WAWEKEZAJI UCHWARA WAKIJA NA BRIEF CASES TUPU NA KUONDOKA WAKIWA MAMILIONEA.TUKATAE WEZI KAMA WA KAMPUNI YA KAGODA NA MATAPELI KAMA WA RICHMOND,NA UJAMBAZI KAMA WA MEREMETA,TANGOLD,NK KUENDELEA HUKU WAHUSIKA WAKITUPUUZA KWA KUGOMA KUTUELEZA UKWELI.


BONYEZA PICHA KUIKUZA NA KUSOMA STORI



Hivi karibuni niliandika makala flani kuhusu milipuko ya mabomu huko Mbagala, jijini Dar es Salaam. Kwa kutambua kuwa blogu yangu haina idadi kubwa ya wasomaji (japo nawathamini sana wachache wanaotumia muda wao kuitembelea) niliamua kuisambaza makala hiyo kwa bloga wenzangu wawili ambao “nyumba” zao hupata “wageni” wa kutosha kila siku.

Kwa bahati mbaya, bloga hao waliamua kuiweka makala hiyo kapuni.Siwalaumu,kwa sababu kadhaa. Kwanza, blogu ni mali ya mmiliki, na hilo linampa haki ya kuchagua nini kiwepo kwenye blogu yake na nini kisiwepo.Pili, kila bloga ana mtazamo wake kuhusu mambo mbalimbali yanayotuzunguka, iwe siasa, dini au nyanja nyingine za maisha ya binadamu. Kwa maana hiyo, kama ataletewa makala inayokinzana na mtazamo huo, ana haki ya kuipuuza. Kuna sababu nyingine za kibinafsi lakini sidhani kama zina umuhimu sana.

Makala husika (isome hapa) haikuwa ya matusi, kashfa au utovu wa nidhamu kwa watawala japo ilikuwa ikizungumzia uzembe na kutowajibika kwa baadhi ya viongozi wetu unavyohusika na janga hilo la milipuko ya mabomu.Nilishauri katika makala hiyo kwamba wakati umefika kwa Watanzania kudai haki zao hasa pale zinapopuuzwa makusudi. Kwamba ripoti ya milipuko ya kwanza inaozea katika makabrasha ya Wizara husika, kisha mlipuko mwingine unatokea lakini hakuna anayewajibika, jambo linalohitaji shinikizo la kudai haki na uwajibikaji.

Naamini kwamba laiti makala hiyo ingechapishwa laiti ingekuwa ya kumsifia kiongozi flani au kukumbushia tarehe yake ya kuzaliwa. Au laiti ingekuwa ni tangazo binafsi. Yote hayo ni mazuri kwa vile ni huduma kwa umma. Hata hivyo, harakati tunazohangaika nazo wengine kuboresha future ya nchi yetu ni muhimu pia na hazipaswi kupuuzwa.

Ni rahisi kwangu kuhitimisha kwamba kinachokwanza makala za aina hiyo kuchapishwa ni uoga wa mabloga husika wakihofia kuwaudhi watawala. Japo huo ni uhuru wao kibinadamu, madhara yake kwa jamii ni makubwa kwa vile historia inaonyesha kwamba uoga ni kitalu mwafaka kwa ushamiri wa tawala dhalimu.

Lengo langu si kulaumu bali kushauriana.Kukimbilia kuweka picha za kiongozi akihutubia au akirejea Dar akiwa bukheri wa afya lakini kuchelea kujumuisha maelezo kwamba pia alikumbwa na dhahama ya kiafya ni kutowatendea haki wasomaji wetu. Hapa narejea tukio lililotokea jijini Mwanza hivi karibuni ambapo baadhi ya wenzetu walitonyesha “picha nzuri” za JK lakini “wakabania” maelezo kuhusu mkasa uliomkumba wa kushindwa kuendelea na hotuba yake katika kile kilichoelezwa kuwa “uchovu wa safari.”

Ushirikiano wetu jumuiya iliyojibebesha dhamana ya kuujulisha umma kuhusu mambo mbalimbali usiishie kwenye yanayopendeza machoni pekee bali pia yale yanayoudhi au kukera.


Hivi mwenzangu unapoiangalia CCM kwa mtazamo wa kawaida tu (yaani usiohisha uchambuzi wa kitaaluma) unaielezeaje?Pengine huafikiani na mtizamo wangu wa “kawaida” na kitaaluma kwamba pamoja na hadi lukuki za kuwakomboa Watanzania kutoka kwenye lindi la umasikini,chama hicho hakijaonyesha dhamira ya dhati kutimiza ahadi hizo.

Naamini kuwa baadhi ya ahadi hizo zilikuwa za dhati,hususani ile ya kuleta maisha bora kwa kila Mtanzania.Naamini hivyo kwa vile ni dhahiri kwamba chama hicho kilikuwa kinatambua hali ngumu inayowakabili Watanzania baada ya miongo kadhaa ya utawala wake.Kwa kutambua tatizo,CCM ilileta dalili za matumaini kwamba sio tu inataka kuendelea kutawala lakini pia inataka kuwa chachu ya mabadiliko.Japo chama hicho kinafahamika kwa usugu wa kukiri mapungufu ya utendaji wake,uamuzi wake kugusia maeneo yanayowakera wananchi ilikuwa ishara ya kutambua mapungufu katika awamu zilizotangulia na kudhamiri kufanya marekebisho.

Binafsi nilitarajia kwamba kama ilivyokuwa mwaka 2005 ambapo CCM “ilikiri mapungufu yake kiaina” kwa kuahidi kuboresha maisha sambamba na kukabili chanzo kikuu cha kuzorota/kudidimia kwa maendeleo (rushwa),basi safari hii pia kingepata ujasiri wa kutueleza bayana kwamba kumekuwa na mapungufu makubwa zaidi katika utekelezaji wa ahadi hizo.

Ni nani asiyejua kuwa kiwango cha rushwa kinazidi kupaa siku hadi siku?Ni nani asiyejua kuwa rushwa na uhujumu mwingine wa uchumi umechukua sura mpya kwa kuzaa tabaka “jipya” la mafisadi?Ni nani pia asiyejua kuwa kwa kiasi kikubwa ahadi ya maisha bora kwa kila Mtanzania imekuwa na maana zaidi kwa mafisadi kuliko walalahoi?Ni dhahiri kwamba Watanzania wenzetu kama wamiliki wa kampuni ya Kagoda wanaishukuru CCM kwa ukarimu na huruma yake to an extent that inaona aibu kuwataja hadharani.Matapeli wa Richmond (achana na yule Mhindi aliyegeuzwa mbuzi wa kafara mahakamani) wanaishukuru sana CCM kwa huruma yake kwao ambapo kila kikao cha bunge kinazugwa kuwa “taarifa ya utekelezaji wa mapendekezo ya kamati ya Mwakyembe itatolewa katika kikao kijacho”,na porojo nyingine kama hizo.

Kinachokera sasa sio tu madudu yanayoendelea kufanywa na CCM bali hizi kauli za kukera kwamba eti chama hicho kimeweka rekodi ya mapambano ya rushwa kuliko nyakati yoyote ile.Hii ni sawa na kuwasanifu Watanzania.Ni mithili ya kuwafanya wajinga,wasioona madudu yanayoendelea,wasiosikia maumivu ya vibano wanavyopewa na mafisadi,na wasiofahamu kuwa watuhumiwa kadhaa wa ufisadi hawajaguswa hadi leo (na hakuna dalili kuwa wataguswa licha ya ahadi kuwa kuna kesi tatu kubwa zitafunguliwa hivi karibuni....na kila mara tunaambiwa “hivi karibuni).”

Ni kweli kwamba hatua dhidi ya watuhumiwa wa ufisadi hazipaswi kuchukuliwa kutokana na utashi wa watu flani bali kwa kuzingatia sheria na kanuni.Lakini utashi ni muhimu katika kuchukua hatua,na hapa hatuzungumzii utashi wa wananchi wasio na uwezo wa kuuamua,kwa mfano “Chenge na tuhuma za vijisenti vyake huko Jersey hastahili kuwa kwenye kamati ya maadili ya CCM.”Kwanza kuwa na utashi wa kufanya jambo jema si dhambi,kama CCM inavyotaka kutuaminisha.Kuwa na utashi wa kuchukua hatua dhidi ya mafisadi ndio itapelekea chama hicho kuwatenga mafisadi inaowakumbatia,na hivyo kuwa rahisi kwake kuchukua hatua dhidi yao.Utashi unapaswa kuepukwa ni kama ule wa wanamtandao unaoendelea kuwaangalia wana-CCM wasio wanamtandao kuwa mithili ya wahaini.

Mamlaka husika zinapozembea kuchukua hatua sahihi halafu tunaishia kuambiwa kuwa hatua haziwezi kuchukuliwa kwa utashi wa watu flani...jibu jepesi ni kwamba matatizo yetu hayawagusi wanaotuongoza.Wanaona tunapiga kelele zisizo na msingi,ndio maana kwao haki za binadamu za mafisadi ni muhimu zaidi kuliko za walalahoi walio wengi.

Hivi kweli CCM inataka kutuzuga kuwa haifahamu kwamba Watanzania wengi wangependa kuona wahusika “halisi” wa utapeli wa Richmond wakifikishwa mahakamani badala ya kile tunachoelezwa kuwa “walijiuzulu kwa maslahi ya taifa”?CCM haijui kwamba kwa kuendelea kuminya taarifa kuwa nani anamiliki Kagoda ni mithili ya kuwapuuza Watanzania?Au CCM haifahamu kuwa kuwaachia mzigo Waingereza kudili na vijisenti vya ujambazi wa rada ni kukwepa majukumu?

Au chama hicho kinapotulaghai kwamba tumwache mhusika mkuu wa ufisadi katika mgodi wa Kiwira apumzike kwa amani ni sawa na kuruhusu kila mtu aibe kisha aachwe apumzike kwa amani?Kwanini basi vibaka wanajazana magerezani ilhali wezi wakubwa wanatetewa kwa nguvu zote?

Watanzania wana kila sababu ya kuiadhibu CCM hapo mwakani.Kinachofanywa na chama hicho kinapodai kuwa “kimeweka rekodi ya kupambana na rushwa” ni mithili ya vibaka wanaokuibia kisha wanakupigia ukelele wa mwizi na kupelekea wewe mwathiriwa wa uporaji huo kushushiwa kipigo kitakatifu huku kibaka “akiyeyuka kiulaini.”Badala ya kukiri kwamba kasi yao ya kupambana na ufisadi ni ndogo, wao wanatukejeli kuwa wameweka rekodi!Halafu bado tutegemee lolote kutoka kwa wababaishaji hawa?

Hakuna haja ya kubishana au kupigiana kelele nao.Dawa yao ni hapo mwakani.Kama unataka kuendelea kuona mafisadi wakitetewa huku wanaowapinga wakikemewa basi irejeshe CCM madarakani hapo mwakani.Kama unadhani maisha bora yaliyoahidiwa 2005 yamepatikana zaidi ya matarajio yako basi hutofanya kosa kutoa kura ya ndio kwa chama hicho.

Tukiendeleza mazowea tutazidi kuumia.Kuna wanaodhani kwamba Tanzania haiwezi kuwa kisiwa cha amani pasipo utawala wa CCM.Wanachosahau kuwa hata hao CCM ni Watanzania wenzetu japo wanawathamini zaidi wageni (wawekezaji) kuliko sie wenye nchi.Wanasahau pia kuwa wingi wa wabunge wa CCM unakwaza jitihada wa wapambanaji kama akina Dokta Slaa kuwakalia kooni wababaishaji waliojazana chini ya utawala wa CCM.

Atakayenuna na anune lakini nchi hii ni yetu sote na kila Mtanzania ana haki ya kudai haki yake.Tukiruhusu kuendelea kwa ngojera za “tunaendelea na mchakato wa blah blah blah” au “kesi kadhaa zkubwa zitapelekwa mahakamani hivi karibuni...” na hadithi nyingine kama hizo basi tutaendelea kuwa watu wa kulalamika kila siku japo ni sie wenyewe tunaoweza kukomesha usanii wa kisiasa wa aina hiyo.Kama imewezekana Ghana basi hata kwetu inawezekana.Si kweli kwamba chama mbadala kitashindwa kutupeleka tunakostahili kwenda hasa ikizingatiwa kuwa hakuna uwezekano wa chama hicho mbadala kupata idadi kubwa ya wabunge zaidi ya CCM,which means itakuwa rahisi kukidhibiti iwapo kitaonyesha dalili za kurejea madudu ya CCM.

Kusanya hasira zako lakini usipigane bali pugie kura ya kujiletea maisha yako bora wewe mwenyewe kwa kuwaondoa wanaokwaza uwezekano huo.Ifike wakati tusema tumechoshwa na ahadi na maneno matamu (na mengine si matamu bali ya dharau kama hayo ya kudai wameweka historia ya kupambana na rushwa wakati wanajua waziwazi kuwa wamekuza rushwa kupindukia).

It can be done if you play your part.

Inawezekana ukiamua kutimiza wajibu wako.


10 Oct 2009


SOMA KAULI ZA BABU HUYU HAPA CHINI KISHA UELEWE KWANINI NATOA WITO AONEWE HURUMA KWA KUPUMZISHWA.

Ahofia wabunge wengi CCM kutorudi Bungeni
Na Keneth Goliama, Mbeya

MBUNGE wa kuteuliwa wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Kingunge Ngombale Mwiru, amewashutumu viongozi wanaounda makundi ndani ya chama hicho na kuwaita waliochanganyikiwa.

Mbunge huyo aliapa kuwa matajiri wasipewe kipaumbele katika uongozi, kwani watu wakishakuwa na fedha wanajiingiza katika siasa kufanikisha malengo yao ya kibiashara.

Kingunge ambaye pia ni Naibu Kamanda UVCCM Taifa,aliyasema jana wakati akiwaapisha Makamanda wa Mkoa wa Mbeya kwenye ukumbi wa Mkapa.

Aliwataka makamanda hao kufanya kazi ya kuwashauri vijana na sio kuwaingiza vijana katika makundi yaliyopo ndani ya chama hicho.

Kingunge alisema kauli za baadhi ya viongozi kuwa, wabunge wengi wa CCM hawatarudi katika ubunge mwaka 2010 ni kweli kwa sababu kunahitajika mabadiliko katika uongozi ndani ya chama.

Hata hivyo, alisema wabunge hao wapya ni faraja kwa CCM kwa sababu watakuwa ni wakutoka ndani ya chama hicho.

Aliongeza licha ya Mkoa wa Mbeya ni mingoni mwa mikoa ambayo ilitoa watu waliokuwa mstari wa mbele kugombea uhuru , lakini sifa hiyo imeharibiwa na viongozi wachache.

Kingunge alisema baadhi ya viongozi mkoani hapa wanauhasama wa kugombea madaraka na kwamba sasa ugomvi huo unakiharibia chama.

Akiunga mkono jitihada za vijana wa mkoa huo kupambana na mafisadi, Kingunge aliwataka wasiache kutetea haki yao kwa sababu vijana ndio wenye nguvu katika maendeleo ya jamii na siasa.

Kingunge aliwaasa wanachama hao kukataa kurubuniwa na watu wenye fedha kwani kukubali kufanya hivyo ni kuua chama.

Baadhi ya viongozi wamefanikiwa kuwarubuni vijana kwa fedha ili waweze kujinufaisha wenyewe na kuharibu siasa mkoani hapa, alisema Kingunge

Alikionya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuwa, hakijui siasa ndio maanakimejaa matatizo matupu na uchaguzi wao ni ovyo na kwamba hakina uwezo wa kupewa kuongoza dola.

CHANZO: Mwananchi

HIVI ALIYECHANGANYKIWA NI NANI KATI YA KINGUNGE NA HAO ANAOWAITA "WAMECHANGANYIKIWA."MAJUZI,MTETEZI MAHIRI WA MAFISADI,YUSUPH MAKAMBA NAE ALITOA TAMKO LINALOSHOBIHIANA NA HILI LA KINGUNGE,MWANASIASA ALIYETUZUGA ENZI ZA MWALIMU KUWA NI MFUASI MAHIRI WA UJAMAA ONLY KUIBUKA MTETEZI MAHIRI WA MAFISADI.LEO,MIEZI MICHACHE KABLA YA UCHAGUZI MKUU,NAE ANAJITUTUMUA KUKEMEA MAFISADI!?HUKU NI KUCHANGANYIKIWA KUNAKONASIBISHWA NA KUZEEKA VIBAYA.

9 Oct 2009


From its politics to its economy to its environment and way of life, California is like a patient on life support. At the start of summer the state government was so deeply in debt that it began to issue IOUs instead of wages. Its unemployment rate has soared to more than 12%, the highest figure in 70 years. Desperate to pay off a crippling budget deficit, California is slashing spending in education and healthcare, laying off vast numbers of workers and forcing others to take unpaid leave. In a state made up of sprawling suburbs the collapse of the housing bubble has impoverished millions and kicked tens of thousands of families out of their homes. Its political system is locked in paralysis and the two-term rule of former movie star Arnold Schwarzenegger is seen as a disaster – his approval ratings having sunk to levels that would make George W Bush blush. The crisis is so deep that Professor Kevin Starr, who has written an acclaimed history of the state, recently declared: "California is on the verge of becoming the first failed state in America." WRITES The Observer's Paul Harris.



Na Ramadhan Semtawa

RAIS Jakaya Kikwete aliweka hadharani matokeo ya uchunguzi wa vipimo vya afya yake, yanayoonyesha kuwa kiongozi huyo wa nchi ana afya njema baada ya tatizo la kuishiwa nguvu akiwa jukwaani mjini Mwanza Oktoba 4, kuibua mjadala.

Lakini vipimo hivyo vinaonyesha kuwa tatizo pekee linalomsumbua Rais Kikwete ni maumivu ya shingo ambayo yanatokana na kuumia nyakati za ujana au utoto.

Afya ya Rais Kikwete ilizuia mjadala baada ya kuishiwa nguvu akihutubia kwenye Uwanja wa Kirumba mjini Mwanza na kulazimika kubebwa na wasaidizi wake hadi chumba kidogo cha uwanjani hapo na ilielezwa baada ya rais kuzinduka kuwa tatizo hilo lilitokana na uchovu baada ya safari ndefu kati ya New York, Marekani na Dar es salaam na baadaye Arusha na Mwanza.

Pamoja na uchovu huo kuhusishwa na safari ndefu ya Rais Kikwete taarifa iliyopokelewa kutoka Radio Jamaica jana jioni zinasema kuwa rais atakwenda nchini Jamaica kwa ziara ya kikazi itakayoanza Novemba 24 na kumalizika Novemba 26.

Na jana daktari wa rais, Peter Mfisi alirejea tena kauli hiyo akisema uchovu, hasa wa safari, ndio uliosababisha kiongozi huyo wa nchi kuishiwa nguvu jukwaani, huku kukiwa na habari kuwa ataenda Jamaica mwezi ujao kwa safari ya kikazi.

Hii ni mara ya kwanza kwa Ikulu kuweka hadharani vipimo vya uchunguzi wa afya ya Rais Kikwete, ambaye pia aliwahi kuishiwa nguvu siku ya mwisho ya kampeni zilizomuingiza Ikulu, na kuanguka akiwa jukwaani.

Daktari wa rais, Peter Mfisi aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa vipimo hivyo ni pamoja na cha damu kwa ajili ya kuangalia virusi vya Ukimwi ambacho huchukuliwa kila baada ya miezi sita.

"Nimekuja kufafanua afya ya mheshimiwa rais kutokana na tukio la Oktoba 4, 2009 (la kuishiwa nguvu jukwaani) pale Mwanza. Tukio hilo limesababisha mshtuko kwa watu wengi na kuendelea kuwa jambo linalozua mjadala kuhusu hali ya afya ya mheshimiwa," alisema daktari huyo.

"Naelewa sababu ya wananchi kuwa na hofu na kuwepo kwa mjadala miongoni mwao. Tatizo pekee ambalo limekuwa likimsumbua rais mara kwa mara ni maumivu ya shingo yanayotokana na kuumia utotoni na wakati wa ujana.

"Baadhi ya pingili za uti wa mgongo sehemu ya shingoni ziliathirika kutokana na kuumia huko na humsababishia maumivu. Mara nyingi matatizo hayo huwapata wanamichezo na wanajeshi."

Dk Mfisi aliongeza kusema: "Tumekuwa tunamfanyia mheshimiwa rais uchunguzi wa damu yake kwa vipimo mbalimbali vinavyotumika kutambua maradhi mbalimbali yanayohusu damu yenyewe na mwili mzima wa mwanadamu. Tumekuwa tunafanya hivyo hapa nchini na hata nje kwa nia ya kulinganisha matokeo yetu na kwa vipimo ambavyo sisi tunavyo.

"Matokeo ya uchunguzi wetu yameonyesha mheshimiwa rais yuko salama, hana maradhi ya damu au kisukari, wala Ukimwi au wingi wa mafuta (Cholestrol), kiwango cha madini, tezi la kibofu wala shingo, au ya ini, au ya homoni mbalimbali zilizoko mwilini na mengine."

Dk Mfisi alifafanua kwamba, uamuzi huo wa kutoa vipimo hivyo umetokana na ridhaa ya rais mwenyewe.

"Ni ridhaa ya mheshimiwa rais mwenyewe... kutokana na kiapo changu cha udaktari na maadili yangu ya kazi, siruhusiwi kutoa hadharani undani wa habari yoyote inayohusu mgonjwa ninayemtibu bila ridhaa yake," alisema Dk Mfisi.

Kwa mujibu wa daktari huyo, baada ya Rais Kikwete kuishiwa nguvu jukwaani, alichukua vipimo muhimu wakati akiwa kwenye chumba maalumu uwanjani hapo kama ilivyo kawaida na kwamba vipimo hivyo vimeshafanyiwa uchunguzi.

Alifafanua kwamba matokeo ya vipimo vilivyochukuliwa siku ya tukio la Mwanza yalionyesha shinikizo la damu (BP) lilikuwa kati ya 130 kwa 85 (vipimo vya kitaalamu), kitu ambacho ni cha kawaida kwa mtu mwenye umri kama wa Rais Kikwete.

"Mapigo ya moyo wake yalikuwa ni 76 kwa dakika ambayo pia ni ya kawaida; sukari kwenye damu ilikuwa 5.5 ambayo nayo ilikuwa ya kiwango cha kawaida; joto la mwili lilikuwa nyuzi 37.5 ambalo ni la kawaida," alifafanua Dk Mfisi.

"Mheshimiwa Rais pia hakuwa na kiungo chochote kilichoonekana kutetereka, jambo ambalo lilithibitisha kuwa hakupata kiharusi. Mheshimiwa Rais hakuwa na matatizo yoyote ya kiafya ambayo yangeweza kuhusishwa kuwa chanzo cha tukio lile (la Mwanza)."

Hata hivyo, Dk Mfisi alisema baada ya kurejea Dar es Salaam alijaribu kuwasiliana na madaktari wenzake wa ndani na nje ya nchi ambao wamekuwa wakishirikiana nao katika kuchunguza na kufuatilia afya ya Rais Kikwete.

"Wote hao baada ya kuwasimulia kilichotokea na matokeo ya vipimo nilivyomfanyia mheshimiwa rais, kwa tafakuri zao hawakuwa na wasiwasi wowote kuwa tukio hilo lilisababishwa na jambo jingine lolote isipokuwa uchovu," alisisitiza daktari huyo wa rais.

Aliongeza kwamba mmoja wao alimuona rais siku moja kabla ya kuondoka New York ambako alipata nafasi ya kumchunguza afya ya mkuu huyo wa nchi.

Dk Mfisi, akitoa mtiririko huo wa vipimo mbalimbali na matokeo alisema: " Blood Pressure (shinikizo la damu), tunafuatilia kwa karibu sana msukumo wa damu, mwenyewe tunampa mashine ya kujipima kila siku na anafanya hivyo, kwa jumla presha yake iko kwenye viwango vya kawaida.

"Aidha, uzito wake wa mwili unaendana ipasavyo na urefu wake, mheshimiwa Rais ni mtu mwenye mazoea ya kufanya mazoezi na yuko makini katika chakula anachokula."

Daktari huyo wa rais aliweka bayana kwamba, wanahusika kwa ukamilifu na kuelekeza kuhusu chakula anachokula na kuongeza kwamba "ana nidhamu ya kujipima pamoja na mazoezi na chakula."

Kuhusu moyo, Dk Mfisi alisema tayari walishamfanyia rais vipimo vya kitaalamu vinavyofahamika kama ECHO na ECG na vingine, na kwamba matokeo yameonyesha hakuna tatizo lolote.

Akizungumzia ubongo, alisema mwaka jana Rais Kikwete alifanyiwa uchunguzi wa afya ya ubongo wake katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa kutumia kipimo cha CT-Scan na matokeo yake yalionyesha kwamba, hakuwa na tatizo pia.

Dk Mfisi alisema Rais Kikwete aliwahi kufanyiwa uchunguzi wa ini, figo, bandama na kongosho kwa kutumia kipimo cha mionzi (ultra sound), uchunguzi ambao ulibaini viungo vyote hivyo viko salama.

"Kila mwaka tunapomfanyia uchunguzi wa afya ya mheshimiwa rais, tumekuwa tunafanyia uchunguzi wa viungo vyake muhimu vya tumboni kama vile ini, figo, bandama na kongosho na kwa kupima damu yake kwa vipimo vyote muhimu," aliongeza Dk Mfisi.

Kuhusu mfumo wa njia ya chakula, ambayo huhusisha koromeo la chakula, tumbo, utumbo mdogo, Dk Mfisi aliweka bayana kwamba matokeo ya uchunguzi yameonyesha hakuna tatizo lolote.

Alisema mwaka 2007 walimfanyia kipimo cha kitaalamu cha colonoscopy mjini Paris, Ufaransa, kuchunguza hali ya afya ya utumbo mkubwa na kwamba matokeo ya uchunguzi yalionyesha kuwa hana matatizo yoyote.

Alisema daktari aliyemfanyia rais kipimo hicho aliwaambia kuwa mkuu huyo wa nchi hahitaji kufanyiwa kipimo kama hicho tena mpaka baada ya miaka saba na kwamba daktari huyo alimtania rais kwa kusema kuwa "angefurahi kuazima utumbo" wake.

Kuhusu tezi la shingo, Dk Mfisi alisema kuwa akiwa mjini New York katika safari yake ya juzi, Rais Kikwete alifanyiwa uchunguzi wa afya ya tezi la shingo pamoja na kiwango chake cha utoaji wa homoni, matokeo yaliyoonyesha hakuna tatizo, hali kadhalika uchunguzi wa tezi la kibofu ulionyesha hana tatizo.

Dk Mfisi alisema rais hana tatizo la macho, masikio na pua na kwamba uvaaji miwani wa Kikwete haumaanishi kuwa ni maradhi.

"Tunapofanya uchunguzi wa macho ukiacha ile ya kuchunguza uwezo wa kuona, tunaangalia presha ya macho na hali ya viungo vya nje na ndani, mheshimiwa Rais hana matatizo yoyote," alisema.

CHANZO: Mwananchi

WAKATI DR MFISI AKITOA MAELEZO HAYO,MHADHIRI MWANDAMIZI KATIKA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM DR HAJI SEMBOJA AMENUKULIWA NA JARIDA LA RAIA MWEMA AKIELEZA KUWA URAIS NI ASASI NA SI MTU BINAFSI.

Urais si Kikwete binafsi, ni mfumo wa kitaasisi. Ni wazi kuwa Rais amesema yeye ndiye hakuzingatia ushauri wa wataalamu wake kutokana na kuwaondolea lawama. Ameamua kuwalinda kwa kubeba lawama, lakini ukitazama jambo hili kwa upana wake wasaidizi wake walipaswa kutambua tangu awali kuwa urais ni system nzima Ikulu hata mlinzi wa getini. Kwa hiyo, wasaidizi ndiyo wenye kuamua na si kila kitu kifanywe na Rais kama ambavyo wanasema sasa watajaribu kumpunguzia ratiba,” ALISEMA DR SEMBOJA NA KUSISITIZA KWAMBA“Sidhani kama ni sahihi kukubali kuwa Rais ndiye alikataa ushauri, kwa taratibu za kimfumo Rais anapangiwa kila kitu ni kama anaamriwa hivi. Kwa tukio hili ameamua tu kuwa na nidhamu ya kuwalinda wasaidizi wake, namwombea afya njema lakini ni muhimu tuzingatie kuwa wengi walioamua kufanya kila kitu wenyewe walipata matatizo, Ikulu sasa ifanye kazi kama Ikulu.”

BINAFSI NAAMINI TATIZO NI LA KIMFUMO ZAIDI.KUNA TAASISI ZENYE MAMLAKA NA WAJIBU WA KUPANGA RATIBA ZA RAIS SAMBAMBA KWA KUZINGATIA UHALISIA,USALAMA NA MAMBO MENGINE KAMA HAYO.KWA WENZETU WANAOZINGATIA KANUNI NA TARATIBU ZA KITAASISI,SI RAHISI KWA RAIS KUJIAMULIA MAMBO YAKE MWENYEWE PASIPO KUZINGATIA USHAURI WA KITAALAM.SI RAHISI,KWA MFANO,BARACK OBAMA KUJIAMULIA KWENDA MAHALA FLANI KINYUME NA USHAURI WA U.S. SECRET SERVICE.UBISHI WA RAIS KAMA BINADAMU HAUNA NAFASI KATIKA UFANISI WA TAASISI INAYOZINGATIA TAALUMA NA MAADILI.IKUMBUKWE KWAMBA LAITI RAIS AKING'ANG'ANIA KUFANYA ZIARA MAHALA FLANI KINYUME NA USHAURI WA WASAIDIZI WAKE KISHA AKAPATWA NA JANGA,WATAKAOBEBA LAWAMA NI WASAIDIZI HAO NA SI RAIS.LAKINI PIA KUNA SUALA LA FEDHA ZA WALIPA KODI ZINAZOTUMIWA NA TAASISI HUSIKA KUILINDA ASASI YA URAIS NA BINADAMU ALIYEKABIDHIWA DHAMANA YA URAIS.NI DHAHIRI KWAMBA RAIS AKIPUUZA USHAURI WA WA TAASISI HUSIKA INAMAANISHA PIA UPOTEVU WA FEDHA ZA WALIPA KODI.



UTENDAJI WA AINA YA ZIMAMOTO,AU VIBAYA ZAIDI,KULENGA SHABAHA BAADA YA RISASI KUFYATUKA,UTATUGHARIMU HUKO MBELENI.LEO HII TUSINGEHITAJI DAKTARI WA RAIA KUWEKA HADHARANI TAARIFA NYETI ZA AFYA YA JK LAITI TAASISI HUSIKA ZINGEMLAZIMISHA JK KUFUATA USHAURI WA KITAALAMU KUHUSIANA NA RATIBA AU ZIARA ZAKE.TUSISUBIRI JAMBO LITOKEE NDIPO TUANZE KUTOA MAELEZO YA KITAALAMU. BY THE WAY,TAARIFA HIYO YA DAKTARI WA RAIS INAWEZA KUZUA MJADALA USIO NA TIJA KUHUSU MANTIKI YAKE.JAPO NI VEMA KUTOA UFAFANUZI KATIKA MASUALA YANAYOZUA UTATA (I WISH NA KWELI ISHU YA KAGODA INGEKUWA HIVYO) LAKINI KUNA UWEZEKANO WA "WABISHI" KUHOJI KAMA DAKTARI WA RAIS WA AFRIKA ANAWEZA KUTOA TAARIFA "MBAYA" DHIDI YA BOSI WAKE!

KWA SASA,MAMLAKA HUSIKA ZINAWEZA KUFARIJIKA BAADA YA KUPATA UTETEZI KUTOKA KWA JK.LAKINI NI VEMA ZIKATAMBUA KUWA JUKUMU LAO SI KUMWOGOPA MHESHIMIWA BALI KUFANYA KAZI ZAO KWA KUZINGATIA MAADILI NA TAALUMA.JK KAMA MTU ANAWEZA KUTOZINGATIA USHAURI WA MAMLAKA HIZO,LAKINI JK KAMA RAIS HARUHUSIWI KUJIAMULIA MAMBO YANAYOWEZA KUATHIRI ASASI YA URAIS.UOGA NA KUJIKOMBA NI MAMBO YASIYO NA NAFASI KATIKA PROFESSIONALISM.


Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.