19 Jan 2010


DAILY NEWS Reporter, 18th January 2010 @ 12:13,

IN an interesting twist of events, President Jakaya Kikwete failed to hand over two ambulance vehicles today, after controversy ensued over the rightful identity of the targeted receivers.

The confusion ensued after a representative from Ngorongoro District in Arusha Region turned up instead of an official from Longido, whom documents indicated was supposed to receive the donation.

The twist happened at the State House grounds before officials and journalists, when the president seemed confused after he discovered it was a representative from Ngorongoro and not from the targeted Longido, who had turned up.

A representative from Mbozi District in Mbeya Region who was meant to receive the second vehicle on behalf of his district had not yet arrived, prompting the president to hand it over to someone else who was present.

When he approached the two cars recently donated by CMC Automobiles Limited, Chief Executive Officer, Mr Abdul Haji, President Kikwete was introduced to the receiver as the Executive Director of Ngorongoro District Council, Kayange Jacob when he suddenly stood back.

“You are….. (as he was being introduced by the State House Comptroller), ahh, you are from Loliondo, this car is not yours, I won’t hand it over to you. It’s not yours. It’s for the people of Longido and not Loliondo.

Turning to State House officials, he asked: What is this. This is scandalous. Apologise to those you invited to witness this”, said the president.

“This one car is to cater for the people of Longido, not Loliondo, who sent you here?’

The Executive Director of Ngorongoro District Council who introduced himself as Kayage, explained to the president that he had been sent by his Regional Commissioner, to come and receive the vehicle as a donation to carry sick people in Ngorongoro.

But the president explained that records show that one of the two cars was supposed to go to Engarinaibo Village in Longido District, following his promise to them when he toured Arusha last year.

“I personally promised the villagers I would give them an ambulance, when I receive a donation of vehicles after witnessing their difficulty in transporting their sick people to hospital. Now what is this? This is scandalous,” he repeated.

Efforts by the State House officials to explain to the president that he hands over the car to the Ngorongoro Director, as there was no other were in vain as he (president) walked back to his office.

After the drama that lasted for approximately 20 minutes, the Assistant Director of Communications at the State House, Premy Kibanga, told journalists that there was negligence on the part of some officials who had verified the documents, subsequently messing up issues.

“There has been a problem of communication here at State House, as all documents including the letter to presiding secretary in Arusha, show that those entitled to the donation is Engarinaiko village in Longido and not Loliondo,”said Kibanga.

Ms Kibanga attributed the anomaly to negligence on the part of the State House official, who was supposed to verify the documents of the director before the handing over, also blaming it on the late arrival of the two officials by ten minutes and that of Mbozi by 20 minutes.

She said the letter from State House to the presiding secretary in Arusha, dispatched at the end of last year, was clear that that the donation was for Engarinaiko village in Longido and had asked the official to release a municipal driver, to get a short course on how to use the facility at CMC.

However, it is not clear to this evening as to whether it was the driver of Longido or Ngorongoro who had received the short training prior to yesterday’s event.

The director of Ngorongoro told journalists that he had been sent by the Regional Commissioner to receive the donation, after a phone call came from the State House asking them to send a representative to receive it.

Efforts to reach the Arusha Regional Commissioner, Isidori Shirima, were futile as his phone went unanswered.

But information sent by the Communication Directorate of State House, said the president handed over one vehicle to the Director of Mbozi District, Levison Chilewa, to cater for citizens of Kamsamba as ambulance.

It was part of the president’s pledge to the area when he visited last year. Earlier, Mr Chilewa told journalists that it would support 26 wards in Mbozi with special target at Kamsamba, Ivuna, Chilulumo, Chitete and Msangano wards.

The two vehicles - Land Rover Defender 110 Hard Top - worth 108,000 US dollars (about 130m/-), were donated by CMC in honour of the manager’s wife, who lived in the country for 30 years before passing away.

15 Jan 2010


The US Government has released a new age-enhanced photograph of al-Qaeda leader Osama bin Laden as he may look now without his trademark long beard...MORE

5 Jan 2010


Naomba kuiwasilisha kama ilivyo

Zitto Kabwe: Kumbikumbi huruka na kuliwa na kunguru

TAFAKURI

Mwanahalisi Toleo Na. 168

.
Na Nkwazi Mhango

ZITTO Kabwe mbunge wa Kigoma Kaskazini, amekiri kumpa magari matatu ofisa habari za zamani wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), David Kafulila.

Magari hayo anayatoa kama msaada kwa Kafulila ili aweze kushinda kampeni za ubunge katika jimbo la Kigoma Kusini. Hizi ni habari zinazozua maswali mengi, ikiwamo utajiri na uwezo wa Zitto kiuchumi.

Je, inakuwaje Zitto aweze kumiliki magari matatu wakati kipato chake kinajulikana? Lakini la pili, Kafulila na Zitto wanawezaje kuanza kampeni za ubunge wakati Tume ya Taifa ya Uchaguzi haijatangaza?

Tayari Zitto amekaririwa akisema, “Ni jambo la msingi kupunguza idadi ya wabunge wa CCM…ndiyo maana nimeamua kumsaidia Kafulila katika chama alichopo (NCCR-Mageuzi). Nipo tayari kujitolea kwa kijana mwingine anayegombea, hata kwa chama kingine, isipokuwa CCM.”

Kwa maneno ya Zitto ni kwamba anamuunga mkono Kafulila, ingawa bado anadai yuko CHADEMA. Ni ajabu kidogo. Je, kama CHADEMA wataamua kusimamisha mgombea Kigoma Kusini wakati Zitto ana mtu wake, atamuunga mkono nani kati ya mgombea wa chama anachodai kimemlea na kumkuza na kumfikisha hapo alipo na rafiki yake kipenzi?

Si vizuri kumsemea Zitto wala Kafulila. Kuna haja ya CHADEMA kuuliza swali hili kabla mambo hayajafika huko. Kwa sasa, Zitto ama kwa kujua au vinginevo, anaanza kujiona maarufu kuliko chama, kama Jakaya Kikwete-kwa mujibu wa maneno ya katibu mkuu wa CCM, Yusufu Makamba.

Ifahamike. Kumbikumbi akaribiapo mauti huotesha mbawa na kuruka na kuishia kuliwa na kunguru.

Inapofikia mtu akafikia kujiona bora kuliko chama, huyu bila shaka hakifai chama wala chama hakimfai. Na lazima kuna tatizo, tena kubwa tu. Hivyo, uwezekano wa kukitosa chama wakati mbaya, hasa ule wa uchaguzi, ni mkubwa. CHADEMA wasingoje kufika huko.
Siasa za Tanzania zina bahati mbaya. Chama kinamlea mtu hadi kufikia umaarufu kama alivyo Zitto Kabwe sasa. Halafu mtu huyu aliyefinyangwa na kulelewa na chama, analewa sifa kiasi cha kujiona bora kuliko chama.

Mwisho wake huwa mbaya kwa mhusika na chama. Daniel arap Moi wa Kenya alifikia hatua ya kulewa sifa hizi pale alipoitwa profesa wa siasa. Alifanya ubabe hadi akakikosesha dola chama chake cha KANU.

Kuna haya ya wanasiasa kuchagua kati ya chama na urafiki. Tumekuwa tukimshutumu Kikwete na CCM kwa kuendekeza urafiki na kujuana. Hata wapinzani wanamlaumu kwa hili, hasa kwa kusema anaendesha nchi “kishikaji.” Hili sina mjadala nao wala sitaki kuingia undani wake. Lakini CHADEMA waangalie wasitoe kibanzi kwenye jicho la mwenzao wakaacha boriti kwao.

Zitto kwa watu wa nje ya chama chake anaonekana kuwa mguu mmoja ndani na mwingine nje. Ushahidi ni shaka juu ya msimamo wake. Kwenye mkutano wa Opesheni Sangara kule Tanga watu wanataka kujua kama Zitto bado yumo chamani au la.

Ni rahisi mtu kukanusha, lakini ushahidi wa mazingira unaweza kupaaza sauti kuliko mwenye kukanusha. Ingawa Zitto anasisitiza kuwa yuko CHADEMA, matendo husema zaidi ya maneno matupu.

Inakuwaje Kafulila awe mali kuliko chama? Zitto anapaswa kubanwa ajibu swali hili kwa usahihi na majibu yanayoingia akilini siyo kupiga siasa. Je, kwa kumuunga mkono Kafulila, hata dhidi ya uamuzi wa CHADEMA, Zitto hadhihirishi asivyokubaliana na hukumu aliyopewa Kafulila?

Kama chama kilimuona Kafulila ana makosa na kikafuata taratibu zote za kumtimua, naye akaamua kujitoa na kutoa kashfa nyingi, maana yake ni kwamba kuna mgongano hata kama wahusika hawataki kulikubali hili.

Litakuwa jambo la ajabu kwa mtu wa cheo na elimu ya Zitto kutoliona hili. Wenzake wamekaa chini wakamtimua Kafulila na kutaja makosa yake-kuvujisha siri za CHADEMA.
Yeye bado anamtetea. Je, huku si kutetea madhambi yake au kuonyesha kuwa kipenzi chake kimeonewa? Kwanini asimtetee kwa namna inayoeleweka badala ya kuendelea kukidhoofisha chama?

Ifahamike. Tunaelekea kwenye uchaguzi mwakani. Kwa uzoefu wangu, wanasiasa nyemelezi watavitelekeza vyama vyao, hasa baada ya kuahidiwa vinono na CCM. Nani mara hii amesahau akina Masumbuko Lamwai, Tambwe Hiza, Walid Aman Kabourou, Shaib Akwilombe, Salum Msabaha na wengine wengi? Kwanini uone ubaya wa chama baada ya kutimuliwa?

Ingawa kuhama vyama ni haki ya wahusika, wengi wa wanasiasa, hasa waliojirejesha CCM baada ya kukosa ukuu kwenye vyama vyao, wameonyesha kuwa nyemelezi na “changudoa.”
Ukiwaondoa watu kama Wifred Rwakatare na wengine wachache, wengi wamedhihirisha wanavyosaka madaraka badala ya kutumikia umma. Wamejivua nguo hata kama baadhi yao wanapewa madaraka ya kufinyangwa kama ilivyo sasa ofisi ya propaganda ya CCM, ambayo imegeuka dampo la wanasiasa nyemelezi.

Hivyo basi, CHADEMA wangembana Zitto wajue msimamo wake kwamba ni nani hasa atamuunga mkono kati ya mgombea wa chama chake na rafiki yake Kafulila.
Ni heri CHADEMA wakamkosa Zitto mapema kuliko kuwachenga saa za mwisho. Huu si wakati wa kucheza pata potea.

Bado Zitto ni mdogo kisiasa na kiumri. Ubunge wa kipindi kimoja hauwezi kumfanya awe yote katika yote hadi kuwa maarufu kuliko chama. Na chama kinapozidiwa umaarufu na mtu mmoja, kama CCM, kijue kinaelekea kuzimu. Nisingetaka CHADEMA wafike huko ingawa dalili zinaonyesha ukomavu wa hali ya juu katika kuyakata mawimbi haya na majaribu makubwa.
Zitto kaamua kumuunga mkono Kafulila wazi wazi, hata kabla ya chama chake kuamua kumsimamisha mgombea Kigoma Kusini. Anajiona si mchezaji bali mwamuzi. Je, alitaka kujenga mtandao ndani ya chama ili baadaye apate madaraka?
Na ikumbukwe. Hii si mara ya kwanza kwa Kabwe kupimana misuli na chama. Nani amesahau mvutano uliotokea hivi karibuni kwenye uchaguzi wa mwenyekiti wa chama? Je, Kabwe anatingisha kiberiti kwa ajili ya kuchukua uamuzi katika chaguzi ujao?

Kwa makala zaidi kutoka kwa MPAYUKAJI tembelea blogu yake HAPA


ASEMA SIASA SI CHAGUO LAKE

Salim Said na Fidelis Butahe

NAIBU Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe ameibuka tena na kutonesha majeraha ya mgogoro uliokuwapo ndani ya chama chake, akisema haridhiki na uamuzi wa chama hicho kuwaengua David Kafulila na Danda Juju.

Ingawa Kabwe hakutaja jina, kauli yake kupinga maamuzi ya kuwavua madaraka wanachama hao; imeonyesha kumzungumzia Katibu Mkuu wa Chadema Dk Willibrod Slaa kwa vile ndiye aliyesema Kafulila na Danda si kitu ndani ya chama hicho na kwamba, anaweza kuwashughulikia bila vikao vya chama.

"Mimi sipendi siasa za kinafiki, uamuzi wa kuwavua nyadhifa zao kina Kafulila haukuniridhisha kwa sababu haukuwa mzuri, ingawa ulipitishwa na mamlaka husika, katika vikao husika," alisema Kabwe katika kipindi cha Jambo Tanzania kilichorushwa na Televisheni ya Taifa (TBC1) jana asubuhi na kuongeza:

"Unajua unaweza ukawa na maamuzi yaliyofanywa katika vikao halali, lakini yasikuridhishe, pia unaweza ukawa na maamuzi katika vikao hivyo hivyo yakakuridhisha. Lakini mimi sikuridhishwa na mamuzi ya kina Kafulila kuvuliwa nyadhifa zao."...INAENDELEA HAPA

PAMOJA NA HESHIMA KUBWA NILIYONAYO KWA ZITTO LAKINI NADHANI KUENDELEA KWAKE KUNG'ANG'ANIA ISHU YA AKINA KAFULILA KUNAMPOTEZEA HAIBA YAKE YA KISIASA MIONGONI MWA WAPENDA MABADILIKO YA KISIASA HUKO NYUMBANI NA WANANCHI KWA UJUMLA.

HAYA MALALAMIKO YATAENDELEA HADI LINI?NA YANAENDELEA KWA FAIDA YA NANI?KAFULILA NA NA MWENZIE WALIKUWA WAAJIRIWA WA CHADEMA.MWAJIRI ANAWEZA KUMPANDISHA AU KUMSHUSHA CHEO MWAJIRIWA WAKE KULINGANA NA TARATIBU NA KANUNI ZA AJIRA HUSIKA.NA IWAPO MWAJIRIWA ATASHUSHWA CHEO KINYUME NA KANUNI HUSIKA BASI ANA HAKI YA KUPELEKA MALALAMIKO HAYO SEHEMU HUSIKA KAMA SI KUCHUKUA HATUA YA KUACHA KAZI KAMA WALIVYOFANYA WANASIASA HAO.HADI HAPO TATIZO LIKO WAPI?

JE ZITTO HADHANI KWAMBA KUTOAFIKIANA NA MAAMUZI YA NGAZI ZA JUU KATIKA CHAMA CHAKE NI SAWA NA KUTAFIKIANA NA CHAMA CHENYEWE AMBACHO YEYE NI KIONGOZI PIA?JE ZITTO SI SEHEMU YA UONGOZI ULIOFIKIA MAAMUZI YA KUWASHUSHA VYEO AKINA KAFULILA (HATA KAMA SI YEYE BINAFSI ALIYEFANYA HIVYO)?HIVI HAKUNA COLLECTIVE RESPONSIBILITY NDANI YA CHADEMA?

PENGINE BADALA YA KUENDELEA KULALAMIKA PASIPO DALILI YA MALALAMIKO HAYO KULETA MABADILIKO NI VEMA KWA MH ZITTO KAMA CHADEMA BADO INAFAA KUWA MAKAZI YAKE KISIASA.VINGINEVYO ITAKUWA KAMA KELELE ZA AKINA MWAKYEMBE KULALAMIKIA UFISADI NDANI YA CCM ILHALI WAO NAO NI SEHEMU YA CHAMA KILICHOGEUZA UFISADI KUWA SERA YAKE.IT SIMPLY DOESN'T MAKE SENSE.

NADHANI KUNA UMUHIMU WA KUIGA BUSARA ZA MKE (RASMI) WA TIGER WOODS KATIKA NAMNA ANAVY-HANDLE SKANDALI ZA UZINZI ZINAZOMKABILI MUMEWE.MWANAMAMA HUYO AMEKUWA MAHIRI KUKWEPA VYOMBO VYA HABARI LICHA YA TETESI KUWA ATAMBWAGA MUMEWE.ANAACHA WANAHABARI NA WAMBEYA WENGINE KUENDELEA NA SPECULATIONS ZAO LAKINI MAAMUZI YAKE YA MOYONI ANAYAJUA YEYE.AKIMTALIKI MUMEWE AU AKIENDELEA NAE,SIFA MOJA KUU ITAKAYOMWANDAMA NI UMAHIRI WAKE KATIKA KU-DEAL NA MATUKIO MAZITO KAMA HILO LA MUMEWE.


4 Jan 2010


Je mama Kikwete ameanza kampeni kwa ajili ya mumewe?

na Nkwazi Mhango

Siku hizi mke wa rais, Salma Kikwete, anaonekana kwenye kurasa za mbele za magazeti karibu kila siku akiwa mikoani akihamasisha hili na lile. Wengi wanahoji. Kwanini sasa na si tangu mwanzo mume wake alipoingia ikulu? Na kwanini asiseme wazi kuwa anampigia kampeni mumewe? Maana, inajulikana alivyo mwana CCM damu damu tena mjumbe wa vikao vyake?

Watetezi wake wanaweza kusema anafanya kazi ya shirika lake lisilo la kiserikali la WAMA. Haiwezekani mumewe akawa mkuu wa serikali naye akawa na shirika lisilo la kiserikali kusiwe na mgongano wa kimaslahi kisheria. Uzoefu tulioupata toka kwa Anna Mkapa ungetosha kumsaidia rais Jakaya Kikwete kuondokana na aina hii ya ufisadi sugu na unyemelezi kwa kutumia mgongo wa ikulu kama angekuwa ni mtu wa kujifunza na kudhamiria kutenda haki kwa taifa.

Ngo yake ni ya mashaka-kwanini ianzishwe baada ya mumewe kuwa rais? Kuanzisha NGO baada ya mume kuwa rais ni ishara tosha ya ufisadi na usasi wa ngawira. Mbona hatuoni wake wa viongozi wa vyama vingine wakiwa na NGOs? Hata wakiwa nazo nani atazichangia iwapo wanaochangia NGOs za wake wa marais wanatafuta kuwa karibu na ikulu ili waihujumu nchi kwa kupata upendeleo kama ilivyokuwa kwa EOTF ambayo ilitumiwa na watu wengi kuliibia taifa? Mke wa Kaisari hapaswi kutenda tendo lenye kuweza kutia shaka au doa utawala wa mumewe.

Tuliishi na kumuona baba wa taifa Mwalimu Julius Nyerere. Mkewe-mama Maria-hakuwahi kujihusisha na upuuzi mdogo mdogo wa kutafuta pesa kwa mgongo wa mumewe.

Niliwahi kuwaandikia barua EOTF na WAMA kuwaonya juu ya hatari ya kuitumia ikulu. Hawakuwahi kunijibu zaidi ya kufumba macho na kuendelea kutengeneza pesa kwa mgogo wa ikulu. Ila nafurahi. WAMA wamefanya jambo moja (la maana la kuondoa aibu)-kuondoa maneno yasemayo WAMA Foundation the office of the First Lady of the United Republic of Tanzania kwenye wavuti wao. Niliandika baruapepe ifuatayo kwa WAMA tarehe 3 Septemba 09:

Kama mzalendo, nimejaribu kukusanya baadhi ya maoni kuhusiana jinsi ufisadi unavyoingia ikulu kiasi cha kututatiza. Kwa sasa Anna Mkapa mke wa rais wa zamani na mumwe wako msambweni. Ukiangalia kinachofanywa na WAMA hakina tofauti na Fursa sawa kwa Wote (Wake za wakubwa).
Kuondoa aibu, nimejitolea kuwasiliana nanyi ili angalau mjue tunavyojihisi kwenye wimbi hili la ufisadi wa kutumia madaraka ya waume zenu. Mama Salma NGO yako ni ulaji mtupu kusema ukweli. Acha kuna kesho. Ni uamuzi wako kuamua. Kuna kesho wakati madaraka yatakuwa mikononi mwa wengine. Hasa nikizingatia kilichompata Regina Chiluba ambacho kinapaswa kumpata hata Anna Mkapa, nimeona bora niseme hata kama nitapuuziwa. Ila najua ujumbe utafika. Someni alama za nyakati na mjue kuwa madaraka yana mwisho na yanalevya. Kuna siku mtakumbuka mchango huu.
Kila la heri,

Bahati mbaya sana , hata wavuti wa Kurungenzi ya habari Ikulu unaonekana kutangaza biashara ya WAMA badala ya wizara za serikali! Ajabu hakuna anayestuka wala kupiga kelele!

Kama umma ukishupaa NGO hii inaweza kufutwa hata na mahakama kutokana na mgongano wa maslahi ukiachia mbali kuwa kichaka cha ufisadi kutokana na uwezekano wa kuchangiwa pesa chafu kutokana na kutokuwapo sheria makini ya kuchuja na kutangaza wafadhili wa WAMA.

Hata hivyo nimefarijika kuwa sauti yangu imesikika na fedheha imeondoka. Maana neno Jamhuri ya Muungano, kisheria, halipaswi kutumiwa na mtu au taasisi yoyote isipokuwa mihimili mitatu ya dola yaani Bunge, Mahakama na Utawala. Cheo cha Ofisi ya First lady hakimo katika katiba yetu.

Kwanini mapenzi kwa wanawake na watoto yaanze baada ya kuupata urais kama siyo gea ya kuitumia vibaya ikulu? Ina maana rais na washauri wake hawalioni hili au wameridhia kwa sababu NGO ya mke wa rais inaweza kutumika kama kivuli cha kuanza kampeni hata kabla ya tume kutanganza hivyo? Inabidi tustuke. Ajabu hata wapinzani hawajaliona hili!

Tanzania inaweza kuwa nchi pekee ambapo rais na mkewe wote ni marais. Kikwete ni rais wa jamhuri huku mkewe akiwa rais wa WAMA. Ukitaka kujua hili jikumbushe mapokezi anayopewa na coverage anayopata Salma kwenye vyombo vya habari. Ajabu ukitafuta uhalali wake kikatiba haupo!

Hata kama anajulikana kwa ubabe na upayukaji wake, bado mke wa rais wa Kenya Lucy Kibaki hana mamlaka kama aliyo nayo Salma ambaye anaweza kuingia mkoa wowote kwa kisingizio cha NGO yake na kufanya shughuli za kisiasa kama kulakiwa na viongozi wa mikoa na kukagua miradi ya maendeleo ukiachia mbali kutoa kauli mbiu zinazoonyesha wazi kumpigia debe mumewe.

Salma anchomzidi Lucy ni ile hali ya kufanya kitu waitacho waingereza one woman show. Kwani kila lilipo jina WAMA yupo yeye. Hii maana yake ni kwamba yeye ni dikteta na mpenda madaraka anayetaka kufanya kila kitu peke yake. Kwanini hatuoni makamu wake au hata wasaidizi wengine wakifanya shughuli za WAMA kama kweli ni ya umma kama anavyodai? Kuthitibitisha hili, tembelea tovuti ya WAMA uone ukweli huu. Hii haiwezi ikawa taasisi ya wanawake na watoto wa Tanzania .

Kuonyesha kuna namna ya kampeni na kutumia mamlaka ya mume wake, hivi karibuni, Mama Kikwete amewahi kutoa namba yake ya simu ya mkononi ambayo ni 0754-294450 kwa wanawake mkoani Singida ili waweze kumpigia au kumtumia ujumbe mfupi wa maneno pindi waume zao watakapowanyanyasa kutokana na kitendo cha wao kwenda kupima kwaajili ya kujua afya zao. Japo kwa juu hili linaweza kuonekana ni jambo bora, kwa mtu anayejua mipaka ya mamlaka yake na utaratibu wa utawala kisheria, angeshauri wahusika waelekeze madai yao kunakohusika-polisi, vituo vya kutetea haki za binadamu hata wizarani.
Licha ya kuwa ubabe, hii ni kampeni ya wazi kuonyesha wahusika wanawajali wananchi jambo ambalo si kweli. Kwanini hasira zake zisielekezwe kwenye kumshauri mumewe kupambana na ufisadi kama ana uchungu na nchi hii? Yaani hajui kuwa ujinga na umaskini ndivyo vyanzo vya haya yote? Sijui hata kwenye kupokea misaada anauliza usafi wa mtoaji.

Kwa nijuavyo upenzi wa sifa wa watawala wetu na watu wao, kama utafanyika uchunguzi huru juu ya matumizi ya MAWA, ushingae pesa inayotumiwa kwenye ziara ikawa kubwa kuliko hiyo inayowafikia walengwa. Bahati mbaya sijwahi kusoma popote taarifa ya mahesabu ya mwaka ya si WAMA wala EOTF.

Wengi wanaweza kuona kama tunamuandama mke wa rais au kutotambua umuhimu wa kupigania haki za akina mama. Kwanini mke wa rais wakati tuna wizara yenye watendaji wanaolipwa pesa ya kodi yetu? Kwanini misaada hiyo anayopokea isipelekwe wizarani au kwenye mashirika huru kama kweli ana uchungu na walengwa na si kujipatia umaarufu, pesa na kubwa zaidi kutumia ikulu kwa manufaa binafsi yawe yake au mumewe na marafiki zake?

Je Salma Kikwete ameanza kampeni kwa ajili ya mumewe hata kabla ya kipenga kupulizwa? Je akina mama wa Tanzania wataingia mkenge wake huku waume na kaka zao wakizidi kuteswa na sera za Kikwete za kuvumilia mafisadi? Je atawalainisha wasahau kuwa Kikwete hajatimiza ahadi hata moja? Je watahoji uhalali wa NGO yake na kumwambia ukweli kuwa ni ya mashaka na ulaji?

2 Jan 2010

31 Dec 2009

BLOGU HII INAWATAKIA NYOTE HERI NA BARAKA KWA MWAKA 2010.NAAMINI TUTAENDELEA KUSHIRIKIANA KWA MICHANGO YA MAWAZO NA KUKOSOA PALE INAPOBIDI,NAMI NAAHIDI KUWEKA MABANDIKO ZAIDI KATIKA MWAKA UJAO.

ASANTENI SANA

30 Dec 2009


THE NATION

AND BEYOND

THE Publishers of

MwanaHALISI,

your enviable Kiswahili weekly

in Tanzania,

wish to convey to you, our

warmest Season Greetings

that bring with them

a New Year – 2010.

We have always done

our piece in Investigative

and Public Journalism;

we are now engaged in

marshalling more skills,

improving methods and

producing quality copy

for IMPACT.

We continue to rely

on your readership;

appreciation of our efforts

to produce a copy worthy

your money; attempt at becoming

a real people’s voice;

and your kind and material

support already rendered

and anticipated.

We pledge to do more

to your satisfaction.

Happy New Year!

Hali Halisi Publishers Limited, Tel/Fax 022 - 2760560

Kasaba Street, Plot 57/31A Kinondoni e-mail: [email protected]

P. O. Box 67311 Dar es Salaam, TANZANIA website:www.halihalisi.com.tz

Cel: 0784 440 073/0777 773347


25 Dec 2009


There will always be bad,or even worse,Santas.Look at THIS,for example.

ANYWAYS,WISHING YOU ALL MERRY CHRISTMAS.

19 Dec 2009


Ahadi za urais 2005 zamtesa Kikwete uchaguzi wa mwakani

Rais Jakaya Kikwet, mzigo mzito wa ahadi zake za mwaka 2005 unamkabili uchaguzi ujao 2010.
Na Mwandishi Wetu
MIEZI michache ikiwa imebaki kabla ya kuanza kwenda kwa wananchi kuomba ridhaa ya kuongoza nchi kwa kipindi kingine cha miaka mitano, Rais Jakaya Kikwete anaonekana kukabiliwa na mzigo mzito wa kutekeleza ahadi nyingi alizozitoa wakati wa kampeni za mwaka 2005.

Kikwete alipata ushindi wa kishindo kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2005 baada ya kunyakua takriban asilimia 80 ya kura, akiwa pia ameshinda kwa kishindo dhidi ya wapinzani wake kwenye uteuzi wa mgombea wa CCM.

Lakini kadri muda unavyokwenda ndivyo umaarufu wake unaonekana kupungua huku tafiti mbalimbali zikionyesha kuwa umaarufu aliokuwa nao wakati akiingia madarakani unaendelea kuporomoka, ikiwa ni miezi tisa kabla ya uchaguzi mkuu wa mwakani.

Wakati akizunguka sehemu mbalimbali nchini kuomba kura za wananchi, Kikwete alikuwa akitoa ahadi kem kem ambazo alizielezea kwa kifupi kwenye kauli mbiu yake ya “Naisha Bora kwa Kila Mtanzania” ambayo mkakati wake wa kuitekeleza ulikuwa ni “ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya”.

Mbali na ahadi ambazo alikuwa akizitoa kwa wananchi kila sehemu alipoelezwa tatizo, ikiwa ni pamoja na matatizo sugu ya maji, miundombinu, huduma za afya na pembejeo, Rais Kikwete pia alitoa ahadi za ujumla kabla na baada ya kushinda uchaguzi kumrithi Benjamin Mkapa.

Baadhi ya ahadi hizo za Rais Kikwete kabla na baada ya kuingia madarakani ni pamoja na kuweka kipaumbele katika kilimo, akitumia kaulimbiu ya Kilimo Kwanza, kupitia upya mikataba ya madini ili inufaishe nchi na wawekezaji, na kuhakikisha kuwa hakuna mwanafunzi wa elimu ya juu anayekosa masomo kwa kukosa karo.

Ahadi nyingine ni pamoja na ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule za umma, kuumaliza mgogoro wa Zanzibar, kuimarisha uhusiano wa kimataifa, kukomesha tatizo la ufisadi, kupambana na tatizo la uhalifu, ikiwa ni pamoja na biashara ya dawa za kulevya na ujambazi, kuandaa mdahalo wa kitaifa wa michezo kwa lengo la kuinua michezo na ujenzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma....INAENDELEA HAPA

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.