4 May 2010

Wiki moja baada ya kusherehekea mwaka wake wa 115 tangu azaliwe,binadamu mwenye umri mkubwa zaidi duniani amefariki katika kisiwa cha kaskazini mwa Japan cha Okinawa.Kama Chinen alizaliwa tarehe 10 ya mwezi Mei mwaka 1895 na kubahatika kushuhudia karne tatu tofauti,kwa mujibu wa wa taasisi ya utafiti wa vipengele (aspects) vya kijamii,saikolojia na baiolojia vya ukuaji wa binadamu (Gerontology Research Group)


Kikongwe huyo alifariki Jumapili iliyopita kwenye nyumba ya kutunza wazee/wagonjwa (care home)japokuwa taarifa za kifo chake hazijatolewa kwa nduguze ambao wamekuwa wakilinda faragha ya bibi hiyo kwa makini.

Kisiwa cha Okinawa kina sifa ya kuwa na wakazi wenye maisha marefu hali inayohusishwa na mlo wa asili wa mchaichai (green tea),supu ya 'miso',mbogamboga,wali na samaki.

Kama ameshikilia rekodi ya umri mkubwa duniani tangu mwezi Sptemba mwaka jana,baada ya kikongwe Gertrude Baines kufariki akiwa na umri wa miaka 115 huko Los Angeles nchini Marekani.Baada ya kifo cha Kama,rekodi yake sasa inabaki kwa bibi wa Kifaransa,Eugenie Blanchard,aliyezaliwa mwezi Februari mwaka 1896.Mwingereza Florence Emily Baldwin,wa Leeds,anashikilia nafasi ya pili akiwa na umri wa miaka 114 pia.Japo bibi huyo anasema kuwa kula sandiwichi ya mayai (egg sandwich)ndio siri ya kuishi kwake miaka yote hiyo,wataalam wanahisi maisha yasiyohusisha uvutaji sigara,unywaji pombe na kufanya kazi kwa bidii kumechangia zaidi.

Imetafsiriwa kutoka kituo cha runinga cha Sky


3 May 2010

Video courtesy of Michuzi Blog

Americans worry that illegal immigrants are putting a strain on schools, hospitals and the depressed job market but still are sympathetic to their plight.

Eight in 10 Americans, 84%, are very or somewhat concerned that illegal immigrants are burdening government services, and 77% worry that they are driving down wages, a USA TODAY/Gallup Poll finds.

Yet 77% are concerned that stricter immigration laws would mean illegal immigrants and their families who have lived productively in the United States for years would be forced to leave



"People seem to be more concerned about that than the hypothetical things like civil rights," Gallup pollster Jeffrey Jones said.

The seemingly contradictory sentiments reflect the difficulty in grappling with the immigration issue, said Tomas Jimenez, a fellow at the New America Foundation think tank and a sociology professor at Stanford University.

"On the one hand, they don't like the idea that people are breaking our immigration laws, that it appears we have a Southern border that is out of control," Jimenez said. "On the other hand, they think the people coming here who work hard, who have dreams of a better life, are really participating in an American tradition that is as old as this country."

The poll of 1,049 adults Saturday and Sunday has a margin of error of +/- 4 percentage points.

SOURCE: USAToday


.


Waziri Mkuu wa Australia,Kevin Rudd,amekuwa akifuatilia tovuti za ngono (porn sites),kwa mujibu wa kituo cha runinga cha Sky. 


Rudd,hata hivyo,amekuwa 'mfuatiliaji' wa tovuti hizo kutokana na mapungufu katika nyenzo za usalama/udhibiti (setting) katika akaunti yake ya Twitter.Kutokana na mapungufu hayo,kiongozi huyo amekuwa akifuatilia watu kama bloga wa mambo ya ngono,duka linalouza bidhaa za ngono,mwanamama aliye kifua wazi huku amjifunga pingu,na kadhalika.

Msemaji wa Waziri Mkuu ameeleza kuwa tatizo hilo lilitokana na akaunti ya Twitter ya Rudd kufuata wale wote wanaomfuata (auto-follow those who follow him)."Japo Waziri Mkuu anajitahidi kutoa majibu kwa wale wanaosema chochote kwake,kazi hiyo ni ngumu ukizingatia idadi ya watu ni 900,000", alieleza msemaji huyo.

Japo inamhitaji mtumiaji wa Twitter kuangalia kwanza wasifu wa mtu anayeomba kukufuata,kuna kipengele kinachoiwezesha akaunti imkubali moja kwa moja mtu anayeomba kumfuata pasipo haja ya mwenye akaunti kufanya hivyo.Uwezo huo unaonekana kuwa muhimu kwa watumiaji wa Twitter wenye wafuasi (followers) wengi.Katika akaunti yake KevinRuddPM,Waziri Mkuu huyo ni mfuasi wa wana-twitter wengine 200,000.

Wataalam wa teknolojia wanatahadharisha kuwa nyenzo za habari kwa jamii (social media)zinaweza kuhatarisha usalama wa mtuamiaji kama hataokuwa makini."Kuna imani kwamba kwenye vitu kama Twitter unaweza tu kufungua akaunti na mambo yakaenda mwanana",anasema Handsley,makamu mwenyekiti wa kampuni ya Young Media Australia."Tunapaswa kufahamu kwa undani kuhusu usalama wa chanzo husika cha habari kwa jamii kabla ya kuamua kukitumia",aliongeza alipoongea na gazeti la Herald Sun.

Kwa mujibu wa gazeti hilo,baadhi ya wengine 'waliofuatiliwa' na Waziri Mkuu Rudd ni pamoja na tovuti ya kamera-mtandao (webcams) za ngono na mmiliki wa kiota cha watenda ngono wa jinsia moja (gay resort) cha Phuket,Thailand.

Rudd amekuwa mtumiaji mzuri wa teknolojia ya habari huku nyakati nyingine akitumia nyenzo kama Twitter kubainisha sera zake.

Imetafsiriwa kutoka Sky News

1 May 2010




Message from JESTINAI will be hosting a brand new talk show ALL ABOUT WOMEN.It explores issues and the progress made by women of Black origin who work and live in and outside London. The show is presented by Jestina George and Kayisha.On this show, the girls talk about everything from fashion to music and general gossip. The show will start showing on Sky Channel 184 BEN TV every monday 10:30 PM. The first show goes out on Monday the 3rd of May 2010. Also the show can be watched on AILTV just log on http://www.ailtv.com or you can purchase a set top box and watch the show and many other programs on a normal television set. For more info Please contact us [email protected] or call us on 07595040952

30 Apr 2010

Mtakatifu au mzushi?

Raia mmoja wa India amegusa hisia za jeshi la nchi hiyo kutokana na madai yake kwamba haitaji chakula wala maji kumudu kuishi.Prahlad Jani anadai yeye ni 'breatharia',yaani mtu anayeweza kuishi kwa kutumia nguvu za asili za kiimani.Anadai anapata nguvu hizo za asili kutoka kwa 'mungu wa kike' anayemmwagia kimiminika (elixir)cha miujiza katika paa la chini la mdomo wake (palate),kwa mujibu wa gazeti la Telegraph la London. 


Wakati baadhi ya watu wanamwona kama 'mzushi' flani,taasisi ya maendeleo ya utafiti wa ulinzi inasema Prahlad anaweza kutoa mwangaza katika kuwasaidia wanajeshi kumudu kukaa muda mrefu bila kula,au hata wahanga wa majanga mbalimbali.Hadi sasa amekaa siku sita bila kula au kunywa chochote katika hospitali iliyopo Hyderabad,na madaktari wanasema haonyeshi dalili yoyote ya kuathiriwa na njaa.

"Ikithibitika kuwa madai yakni sahihi,basi itakuwa hatua kubwa sana kwenye sayansi ya tiba",anasema Dkt G.Ilavazhagan,Mkurugenzi wa Taasisi ya Ulinzi ya Fiziolojia na Stadi Shiriki."Itatuwezesha kuokoa maisha ya wanadamu katika nyakati za majanga,kimo cha juu,safari za majini,na mazingira mengine magumu ya kibinadamu na ya asili.Tutaweza kuwaelimisha watu kuhusu namna ya kustahimili (surviving) mazingira magumu pasipo chakula na maji au chochote kile".

Madaktari wataendelea kumchunguza kwa siku 15 kipindi ambacho wanataraji kuona misuli yake ikisinyaa,upungufu mkubwa wa maji mwilini,kupungua uzito wa mwili na baadhi ya viungo vya mwili kushindwa kufanya kazi.

Binadamu wengi hawawezi kustahimili zaidi ya siku 3 hadi 5 pasipo kunywa maji.

Imetafsiriwa kutoka gazeti la Daily News la India.

29 Apr 2010

NEWSWEEK: Black blogs cover a far more diverse range of stories than the rest of the media. Just ask Sandra Bullock. While Sandra Bullock's post-Oscar split from husband Jesse James may be the biggest celebrity news in the last month (or two), it's probably not surprising it's the adopted brown baby that really got the African-American blog sites going. The funny thing is, black Web sites such as MediaTakeOut.com, Bossip, and Young, Black and Fabulous have been following Bullock for years. Part of the reason is her connection to the black community. "They know about her support for victims of Katrina and Haiti so they care about what happens to her, which we thought about when we gave her coverage," says Fred Mwangaguhunga, owner of the black entertainment site MediaTakeOut.com. But part of it is that black blogs look at the world differently than the often segregated mainstream.
. CLICK HERE TO READ THE FULL STORY

The US Army says that it is it is wasting far too much time preparing Powerpoint presentations and not enough time killing people.

For a while now the Army has been concerned that its officers are missing entire wars preparing Powerpoint slides and making presentations.

. TechEye has got its paws on the sort of slide they mean (see above). 

Last summer Gen Stanley McChrystal, the leader of US and Nato forces in Afghanistan, said when we understand that slide that “we’ll have won the war’.

Gen James Mattis of the Marine Corps, said: "Powerpoint makes us stupid". The Marines are not renowned for being that bright in the first place, which makes them some of the US's best soldiers, but Powerpoint sucks about the direction you want to point them.

Sam Nuxoll, a platoon leader in Iraq, seems to have shaken the Pentagon with a quote that said he was spending most of the war making Powerpoint slides. Instead of spending his time dodging bullets, he was making bullet points.

What is the problem is the fact that rather than encouraging making decisions PowerPoint sucks up the time of junior officers. The idea is that they can get crappy decisions blessed if it looks good in Powerpoint. However really good tactics which are dull on screen are being mothballed.

This has been noticed in business too with some companies thinking that Powerpoint presentations are a waste of time too.

.SOURCE: Tech Eye

JIJI la Tanga limfeunikwa na simamzi kuu kufatia wanafunzi 18 wa Chuo cha Kiislamu cha Shamsil-Maariff kufa papo hapo na wengine 125 kujeruhiwa vibaya, baada ya lori walilokuwa wakisafiria kutoka kwenye sherehe za maulidi kupinduka.

. Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Adolphina Kapufi aliliambia gazeti hli jana kuwa ajali hiyo ilitokea saa 5:30 usiku wa kuamkia jana katika eneo la njiapanda kuu ya Mabanda ya Papa jijini hapa.

Kapufi aliwataja baadhi ya waliokufa katika ajali hiyo kuwa ni Twalib Kunemu, Juma Idd, Faraji Habib, Jahshi Rashid, Hussein Bakari, Hajji Athumani naYussuph Hussein na kwamba, kazi ya kuwatambua maiti wengine bado inaendelea.

Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Paschal Kanyinyi alisema kazi ya kuwatambua waliokufa na majeruhi waliolazwa katika hospitali hiyo wodi ya Galanosi inaendelea.

Kanyinyi aliwataja majeruhi waliotambuliwa kuwa ni Jumaa Salim ambaye ameumia mbavu, Makame Ahmed, Ahmed Shehe, Selemani Said na Juma Akida.

Aliwataja majeruhi ambao hali zao ni mbaya, hivyo waliokimbizwa katika Hospitali Taifa ya Muhimbili, jijini Dar essalaam kuwa ni Hemed Shaaban na Hassan Adam.

Kanyinyi alifahamisha kuwa kati majeruhi 125 walifikishwa katika hospitali hiyo usiku wa kuamkia jana baada ya kupata ajali, 70 walipata matibabu na kuruhusiwa kurejea chuoni kwao.

Kwa mujibu wa Kaimu Mganga Mkuu huyo, majeruhi 55 wanaendelea kupata matibabu katika hospitali hiyo kwa msaada wa timu maalumu ya waganga na wauguzi waliokusanywa kutoka hospitali na vituo mbalimbali vya afya mkoani Tanga kwa ajili ya kutoa huduma hiyo.

Mwananchi ilifika katika Hospitali hiyo ya Bombo na kukuta idadi kubwa ya wananchi waliokusanyika katika hospitali hiyo kwa lengo la kutambua miili ya waliokufa na majeruhi.

Mwalimu wa zamu wa Chuo hicho, Ustaadh Ajali Ramadhan, alisema kuwa wanafunzi hao walikuwa wakitokea Kijiji cha Kibafuta ambako walikwenda
kuhudhuria sherehe za kuzaliwa kwa Mtume Mohamad S.A.W.

Hata hivyo, Ustaadhi Ramadhan alisema anashangaa kuona idadi kubwa ya wanafunzi waliopata ajali, kwani aliowaruhusu kutoka chuoni hapo walikuwa 60 tu.

“Nashangaa sijui ni nini kimetokea, kwani niliowaruhusu kuondoka na gari
hilo ni wanachuo 60 tu, lakini idadi ya waliopata ajali imekuwa kubwa. Sijui walipandia wapi…,” alisema mwalimu huyo wa zamu.

Kanyinyi alimshukuru Mkurugenzi wa Kampuni ya Raha Leo, Seleman Abdallah kwa kutoa dawa kwa ajili ya kuwatibu majeruhi wa ajali hiyo.

“Tunashukuru Mkurugenzi wa Raha leo, ametusaidia sana kwa kutoa dawa za
kuwatibu majeruhi na pia vifaa kwa ajili ya kusaidia kuhifadhia miili ya waliokufa,” alisema Kanyinyi.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Meja Jenerali Mstaafu Said Kalembo alifika hospitalini hapo saa 5 .30 asubuhi na kuwapa pole ndugu wa wanafunzi waliokufa katika ajali hiyo.

Akiwa, akiwa katika wodi ya Galanosi Mkuu wa Mkoa huyo alimuagiza Kaimu Mganga Mkuu kuwaita waganga na wauguzi kutoka vituo vyote vya afya vya jijini hapa ili kuongeza nguvu, kwa vile waliopo katika Hospitali ya Bombo walikuwa wmezidiwa na kazi ya kuwahudumia majeruhi.

Katibu wa Bakwata wa Mkoa wa Tanga, Mohamed Riami alisema huo ni msiba
mkubwa uliwakumba Waislamu na Watanzania kwa ujumla, hivyo akaomba msaada wa hali na mali kuokoa maisha ya majeruhi waliopata ajali hiyo.

Ajali hii ni muendelezo wa ajali mbaya za barabarani zinazoendelea kutokea na kuua watu sehemu mbalimbali nchini hivi sasa.

Moja ya ajali hizo mbaya ni iliyotokea jijini Dar es Salaam mwezi uliopita na kuua watu zaidi ya 10 papo hapo baada ya lori la mafuta ya taa kuigonga na kulalia daladala maneo ya Kibamba katika Barabara ya Morogoro.

Katika ajali hiyo iliyotokea alfajiri, daladala ilisagawa na kuwa kama chapati; na miongoni mwa waliokufa ni mama mjazito aliyekuwa anakwenda kujifungua hospitalini akiwa pamoja na mumewe.

CHANZO: Mwananchi
.

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.