20 May 2010

Nadhani unamfahamu Christina Aguillera,na kama unamfahamu basi ni dhahiri utakuwa unakumbuka 'singo' yake ya kwanza kabisa Genie in a Bottle (Kama huukumbuki basi cheki video hii hapa).

Ushaikumbuka?Well,lengo la makala hii si kumjadili mwanamuziki huyo au wimbo huo uliovuma sana.Nacho-focus hapa ni hiyo ishu ya 'jini kwenye chupa'.

Lakini kabla sijainyambua,ngoja nikupe stori moja fupi.Mwaka 2005 nilipokwenda nyumbani kwenye fieldwork,nilikutana na rafiki yangu mmoja wa zamani ambaye ni mtoto wa Sharifu huko Tanga.Baada ya mahojiano yetu nilimdadisi kuhusu suala la majini.Nae bila hiana akanipa darasa kutoka A mpaka Z.Actually,alikwenda mbali zaidi hadi kunionyesha namna jini linavyotengenezwa.Bila kuingia kwa undani sana,alichovya maandishi flani kwenye chupa na kutengeneza kitu alichokiita kombe,kisha akafunga hiyo chupa.Akaeleza kuwa katika muda aliokusudia,jini litatoka katika hiyo chupa na 'kufanya vitu vyake' (kwa mujibu wa manuizo/dua.Bado nakumbuka jinsi nilivyosisimka baada ya 'kuonyeshwa jini mtarajiwa'

Naamini usemi 'jini ndani/kwenye chupa' unaendana na mantiki ya utengenezaji jini (yaani linawekwa kwenye chupa kisha 'linalipuka' katika muda ulokusudiwa).Kwa mujibu wa yule mtoto wa Sharifu ni kwamba jini likishatengenezwa na kuhifhadhiwa ndani ya chupa tayari kwa 'maangamizi' haliwezi kurejeshwa.Na la zaidi ni kwamba jini likishatoka kwenye chupa haliwezi kurudisha.Kwahiyo basi,usemi 'jini kwenye/ndani ya chupa' unamaanisha kitu ambacho 'kikitoka kimetoka',yaani ni kama maji yakimwagwa ardhini,hayawezi kuzoleka.

Kwanini basi nimeamua kutumia msemo huu katika makala hii?Well,katika uchambuzi wangu kuhusu kauli za/matendo ya Rais wetu (Chaguo la Mungu) Jakaya Kikwete,naanza kupatwa na wasiwasi huohuo wa 'jini ndani/kwenye chupa'.Simaanishi kuwa JK ndio jini.Hapana.Nazungumzia kauli na matendo yake ya hivi karibuni.

Sijawahi kuzungumzia lolote kuhusu hotuba yake kali alotoa kwa wafanyakazi wa serikali waliokuwa wametishia kugoma.Kwa kifupi,baadhi ya kauli zake hazikupaswa kutolewa na kiongozi anayejali utawala wa sheria.Kwa kutaja maneno kama risasi za moto au namna wafanyakazi wangeweza kukumbana na nguvu za polisi ilikuwa ni mithili ya kubariki ukatili.Hata kama wafanyakazi wangegoma bado isingehalalisha matumizi ya nguvu 'to an extent baadhi yao wangeweza kukumbana na makali ya risasi za polisi'.Hivi sio JK huyuhuyu alosema kuwa yeye anathamini haki za binadamu ikiwa ni pamoja na za mafisadi?Tuliache hilo kwa sasa.

Juzijuzi akaibuka tena na kudai suala la takrima ni gumu kukwepeka.Mkuu wa nchi anaposema hivyo ni sawa na kubariki matumizi ya rushwa kwa jina la takrima.Kauli kama hiyo haipaswi kutolewa hata na katibu kata,let alone Mkuu wa nchi.Ugumu wa jambo haumaanishi liachwe kama lilivyo.Yaani kwa vile mapambano dhidi ya ukimwi ni magumu kwahiyo tuache watu 'watembee pekupeku'?Au kwa vile ugonjwa wa malaria umekuwa ukitusumbua miaka nenda miaka rudi basi tuuache kwa vile ni vigumu kupambana nao?Sasa alipohamasisha kampeni ya ZINDUKA na wapambe wake wa bongoflava alikuwa anamaanisha nini?Rais alipaswa kuelewa kuwa kwenye mapambano dhidi ya udhalimu,giving up is not an option.Laiti Nyerere na wapigania uhuru wengine wangekuwa na mtizamo finyu kama huo wa 'jambo hili gumu kwahiyo tuliache kama lilivyo' basi hadi leo tungekuwa bado koloni la Mwingereza.

Kilichonishtua zaidi hadi kufikia hatua hii ya kuleta ulinganifu na 'jini kwenye/ndani ya chupa' ni mkanganyiko uliojitokeza katika sakata la Jumuiya ya Vijana wa CCM (UVCCM).Awali ilielezwa kuwa kuna vipeperushi vilivyosambazwa kumtuhumu aliyekuwa Mwenyekiti ya jumuiya hiyo,Hamad Yusuph Masauni.Baadaye gazeti moja likabainisha kuwa mtoto wa JK,Ridhiwani,anatuhumiwa kuivuruga jumuiya hiyo na kuchochea suala hilo la Masauni.Lakini,akihutubia mkutano wa Jumuiya hiyo huko Iringa,JK aliweka bayana kuwa (namnukuu) "Tulipochunguza ilibainika ni kweli alighushi, wakati wa uchaguzi alisema alizaliwa mwaka 1979, lakini ukweli alizaliwa mwaka 1973 na alianza darasa la kwanza mwaka 1979".Je hii haimaanishi kuwa hata vipeperushi vilivyosambazwa kumhusu Masauni vilikuwa na uhusiano na 'uchunguzi' huo anaozungumzia JK?Kama ni hivyo,je si hatari inapotokea kiongozi wa nchi anaporuhusu michezo michafu kama hiyo kwa minajili tu ya kukidhi matakwa flani?

Kinachokasirisha ni kauli yake kuwa  "kijana huyo (Masauni) mpole na mzito kufanya maamuzi magumu na haraka...ni mkakamavu na mchapakazi atapangiwa kazi nyingine hapo baadaye".Yaleyale ya Mwilima.Mtu anaboronga huku kisha anazawadiwa uongozi.Kama ni kweli Masauni alifoji umri wake,hivi hiyo haimpotezei sifa za kuwa kiongozi mahala kwingine?Sasa JK anapotuambia kuwa aatapangiwa kazi kwingine anamaanisha nini?Au huko atakapopangiwa hakuhitaji uadilifu?Na kama 'kudanganya umri' si big deal kwanini basi wameshinikiza aondolewe UVCCM?Nauliza hiyo kwa vile,kwa mujibu wa 'Chaguo la Mungu',kufoji umri kulikopelekea Masauni kujiuzulu sio big deal ndio maana 'atapewa kazi nyingine baadaye'.

Habari nyingine zinazoweza kuashiria kuwa 'jini lililo ndani/kwenye chupa linaweza kutoka muda wowote ule' ni katika jarida la Raia Mwema kwamba Mawaziri Wakuu wastaafu wanafuatiliwa.Ukisoma habari hiyo utabaini kuwa kwa vyovyovte vile,Mkuu wa Nchi anafahamu kuhusu suala hilo.Lakini sidhani kama tunapaswa kushangaa sana kwa vile kama Masauni alichunguzwa (which is equivalent to kufuatiliwa kwa ex-PMs hao) na hatimaye vipeperushi vikasambazwa,basi katika utawala huu lolote linawezekana,hususan uzandiki na character assassination.

Na hili suala la promotion ya familia kwenye uongozi,japo si kosa,linaweza kutafsiriwa kwa namna ya maandalizi ya udikteta.Baba/mume rais,mama/mke naye mwanasiasa 'kiaina',kaka wa rais naye mwanasiasa,mtoto naye mwanasiasa,na hadi kitinda mimba naye kaingizwa kwenye siasa.Na hapa sizungumzii siasa kwa maana ya hamasa tu bali siasa za mizengwe na kugombea kwa kutumia jina.Hapa tunazalisha mfalme au dikteta?

Kwa Watanzania wengi ni business as usual.Lakini kwa wanaoangalia ishu na kukumbuka kuweka alama za kuuliza,yayumkinika kufananisha suala hili na ' jini ndani/kwenye chupa'.LIKITOKA LIMETOKA,hakutokuwa na jinsi ya kulirejesha kwenye chupa.

Kwa atakayechukizwa na uchambuzi huu (kama yule mjinga alontumia comment ya matusi) all I could tell them is SUCK IT UP!


19 May 2010


Picha kwa Hisani ya Michuzi

Nyuso zao zinasuta nafsi zao.Lakini hii ndio hali halisi ya Tanzania yetu.Pamoja na madudu yooote yanayoendelea kufanywa na CCM lakini Watanzania wengi wanaendelea kuwa usingizini na kuamini kuwa hakuna maisha pasipo CCM.Ungetarajia tabaka la chini (ambalo ndio mtaji mkubwa wa chama tawala) liwe na hasira ya hali ya juu dhidi ya chama kilichowasaliti kwa kukumbatia wafanyabiashara mafisadi huku hali za walalahoi zikizidi kuwa ngumu.Lakini,sijui ni kurogwa au vipi,tabaka hili la chini linaendeleza ndoa yake na CCM kama picha inavyoonyesha hapo juu na hapa chini (wanapozugwa na Kingunge).

Na ni hawahawa utakawasikia wakilalamika baada ya uchaguzi kuwa ahh viongozi wametusahau,na malalamiko mengine kama hayo.CCM ikiwapuuza inaweza kuwa na sababu za msingi kwani haikuwalazimisha waipende,na 'imejitahidi kuwapa sababu kadhaa za kuichukia' lakini wananchi hawa wameendelea kuwa ving'ang'anizi.Yani ni kama mwanamke anayeteswa na mume lakini anaendelea tu kumg'ang'ania licha ya kufahamu kuwa mapenzi ya mume huyo yamehamia nyumba ndogo.Na mfano huu unaweza kulinganisha na ndoa ya CCM na wakulima na wafanyakazi,ambapo kwa mazingira ya sasa ya 'ndoa' hiyo CCM imehamishia mapenzi kwenye nyumba ndogo ambayo ni wafanyabiashara na mafisadi.

Kaaazi kweli kweli

18 May 2010



Watawala wetu waache magari yao ya kifahari wachekwe?Nchi tajiri lakini viongozi wanaishi kawaida,lakini sie masikini na ombaomba wa kutembeza bakuli viongozi wetu wanaishi kifahari kama wafanyabiashara matajiri.

Ofkoz,Mtukufu Rais Jakaya Kikwete alikuwa anatania alipotetea rushwa hadharani kwa kudai takrima haikwepeki.Ndio,Rais alikuwa anatania,na ndo maana,Msajili wa Vyama vya Siasa John Tendwa amekaririwa na magazeti kadhaa akimtetea JK kuwa "kauli yake (JK) kuhusu takrima (rushwa) ilikuwa utani tu".Pengine neno 'utani' kwa mujibu Tendwa linaweza kuwa na maana kubwa zaidi tukilitafsiri katika informal English.Kwenye kamusi,'joke' (informal) inamaanisha An object of amusement or laughter; a laughingstock.Kwa Kiswahili,ni 'kituko', 'kioja' au 'kitu cha kuchekwa'.

Lakini kwa namna siasa zetu zilizvyojaa vituko (jokes) si ajabu Tendwa alikuwa serious kumtetea bosi wake JK.Na inawezekana kabisa Msajili huyo wa Vyma vya Siasa anayepaswa kufanya kazi bila upendeleo anaamini kwa dhati kuwa rais wetu alikuwa anataniana tu na viongozi wa dini.Kama ni hivyo,basi nae ni kituko pia.Haiingii akilini kwa kiongozi wa nchi kukutana na watu muhimu katika jamii yetu (viongozi wa dini) na kufanya 'utani mbaya' kama huo.Kulikuwa na umuhimu gani basi wa rais kuhudhuria mkutano huo kama lengo lilikuwa kutoa utani tu?Si angeweza kuwapigia simu kwa wakati wake kisha akawarushia utani huo!

Kwa bahati mbaya,au makusudi,'utani huo mbaya' ushaanza kusahaulika miongoni mwa Watanzania wengi.Siwezi kuwalaumu walalahoi ambao wako bize na kuhakikisha mkono unaenda kinywani,lakini nashindwa kujizuia kuwashangaa Watanzania wenzetu walio katika 'tabaka la kati' (middle class) kwa kuweka umuhimu zaidi kwenye ishu kama tuzo za Kili,ujio wa Sean Kingston,'kujirusha',nk ilhali tabaka la chini linalohitaji sapoti yao likizidi kuangamia.Wengi wa walio katika tabaka la kati wako bize zaidi 'kuishi kama tabaka tawala' (hata kama hiyo itamaanisha wakope kwa ndugu na marafiki au wajihusishe na ufisadi) kuliko kupambana na 'tabaka tawala' (tabaka la juu) 'kusawazisha uwanja' (to level the ground) kwa minajili ya kujenga jamii yenye kukaribia usawa.


Sijui tunaelekea wapi,lakini lililo bayana ni kwamba hatma ya taifa letu iko mashakani.Ukiona mkuu wa nchi anaongea pasi hofu (na kicheko juu,kama kawaida yake) kuwa takrima (ambayo ni jina la kistaarab la rushwa) haikwepeki.Tafsiri pana ya kauli hiyo ya 'Chaguo la Mungu' ni mithili ya kuhalalisha uhalifu kwa vile rushwa ni kosa la jinai.Lakini binafsi sishangazwi sana na kauli hiyo ya 'mwenye nchi' kwa vile alishawahi kutamka bayana kuwa 'anajali haki za binadamu za mafisadi' alipohutubia Bunge Agosti mwaka 2008



Kusoma habari kamili kuhusu utetezi wa Tendwa kwa Kikwete BONYEZA HAPA na HAPA.

17 May 2010



Haikuweza kufahamika mara moja kuhusu hali za majeruhi.



Picha zaidi kuhusu ajali ya jana.



Jana majira ya saa 2 usiku nilishuhudia mzinga huu katika barabara ya Cumbernauld hapa Glasgow.

16 May 2010



It's been quite a while since our Dear leader Jakaya Mrisho Kikwete last visited the United Kingdom.As a seasoned world traveller,and in the spirit of the Anglo-Tanzania friendship,I suspect JK will be here sooner than later.And in an effort to maintain his record as the first African president to meet Barack Obama,he certainly could be here in a matter of weeks if not days.

Just because you poor souls can't afford to visit other areas in Tanzania either because the fares are too dear,or your intended destinations are inaccesible due to TRL taking a long break from serving walalahoi,or simply because you're scared of dying after looking closely at the growing figures of road accidents (and subsequent deaths) doesn't mean our Dear leader,God's choice,JK should not continue to 'accumulate his international air miles'.

Yes,as Basil Pesambili Mramba once said,a president cannot travel on top of a camel.Of course,he was not really defending that infamous decision to buy a rarely used Presidential jet but rather the dough on its way to his own bank account.

Satiric or not,truth remains that our leaders are so distant from the led that they hardly understand why people keep on complaining about one thing or another.It goes without saying that if Dr Shukuru Kawambwa were to be stranded at a train station for just a couple of hours due to the TRL bullshit,he surely would understand how it affects walalahoi.And if JK trips were to rely on ATC,he certainly would have thought the importance of having a 'living' national carrier (ATC is long dead except for the name and the likes of Mustafa Nyang'anyi who make most of what's left of the corporation).

It's down to such distance that,for instance,our God-sent president came to the decision to order DCs to carry out house house-to-house searches to 'catch' kids who didn't up to schools despite having been selected to join secondary education.Assuming the searches pay dividents,would the militias acting on powers invested to them by the DCs be turning up at the 'truant' kids' homes day in day out to force them to go to schools?Did His Excellency Jakaya do any brainstorming as to why these kids chose to abscond school in the first place?They certainly are not allergic to education,or are they?Would it still chasing these kids deemed necessary had the much-hyped 'secondary school in every ward' corresponded with number of desks for students,housing and salary on time for teachers,and such logistical considerations?Although I truly understand the importance of education,I think this misguided directive should rather target owners of Kagoda and their fellow mafisadi than our innocent kids.

I know the privileged fews whose hands are superglued to the national cake would regard this article as being seditious.Whatever!That's all I can tell them.

15 May 2010

Kwa hakika baadhi ya kauli za Rais wetu Jakaya Kikwete zinachanganya kupita kiasi.Juzijuzi tu alisaini kwa mbwembwe sheria tuliyoambiwa imelenga kudhibiti rushwa katika chaguzi.Tukiweka kando suala la wasaidizi wake kumwingiza mkenge kwa kuchomekea vipengele kinyemela,sambamba na mapungufu lukuki katika utekelezaji wa sheria hiyo (kubwa likiwa uswahiba kati ya CCM ya Kikwete huyohuyo na mafisadi),uamuzi wa kuwa na sheria hiyo ulileta faraja kidogo kwamba angalau mkuu wa nchi sasa anaanza kuikabili rushwa kwa vitendo badala ya maneno na ahadi tupu.

Sasa kabla hata sheria hiyo haijapata nafasi ya kutumika ipasavyo,JK kaja na hadithi mpya.Kwa mujibu wa vyombo vya habari,Rais amewaeleza viongozi wa dini kuwa suala la takrima kwenye chaguzi ni gumu kulidhibiti.Kama huelewi vizuri maana ya takrima basi naomba nikugamishe kuwa hiyo ni jina la kistaarabu (polite name) la rushwa au hongo wanayotoa wagombea kwa kisingizio cha 'ukarimu'.
Kinachonifanya nishindwe kumuelewa JK ni hiki: ina maana wakati anaipigia chapio sheria anayoamini itadhibiti rushwa kwenye chaguzi alikuwa hafahamu kuwa takrima (ambayo ni rushwa) ni ngumu kudhibitiwa? Au tuseme JK haamini kuwa takrima ni rushwa na ndio maana iliharamishwa?Na je kama takrima ni ngumu kudhibitiwa kwahiyo inakuwa halali?Je kiongozi wetu huyu haoni kuwa mkanganyiko anaozua unaweza kupelekea mvurugano baada ya uchaguzi ambapo wagombea watakaoshindwa kutokana na uwezo wao duni kumudu kutoa takrima wakikimbilia mahakamani,watoa rushwa (takrima) watatumia kauli ya JK kuhalalisha kuwa walichofanya ni sehemu ya utamaduni wetu wa ukarimu ("kama alivyobainisha Rais tarehe 14/05/2010)?

Habari kamili kuhusu kauli hiyo ya JK soma HAPA na HAPA.

14 May 2010

Labda na watawala wetu watakuwa na la kujifunza.

Habari kamili bonyeza HAPA.

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.