22 Oct 2010


Kama ilivyo ada,toleo la wiki hii la jarida la Raia Mwema limesheheni habari moto moto na makala zilizokwenda shule.

Makala yangu katika toleo hili inazungumzia kuhusu Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Jumapili wiki ijayo.Nimejaribu kujenga hoja kwanini miaka mingine mitano kwa Jakaya Kikwete ni hatari kwa ustawi wa taifa letu.

Nisikupunje uhondo bali bingirika na makala hiyo kwa KUOBONYEZA HAPA.


Mke wa Balozi

Mheshimiwa Balozi Peter Kallaghe

Kushoto kwenda Kulia: Mariam Kilumanga (Mwenyekiti wa TAWA), Mama Balozi Joyce Kallaghe na Mariam Mungula (Katibu wa TAWA)























Picha zimeletwa na Miss Jestina

20 Oct 2010



Serikali sasa yatishia kulifuta Mwananchi
Wednesday, 20 October 2010 07:52

Mwandishi Wetu
SERIKALI imetishia kulifunga au kulifutia usajili gazeti la Mwananchi kwa madai kwamba linaandika habari za uchochezi dhidi ya serikali ya awamu ya nne.Barua ya serikali yenye kumbukumbu namba ISC/N.100/1/VOL.V/76 iliyoandikwa kwa mhariri mtendaji wa gazeti la Mwananchi, inaonya kwamba kama gazeti hili litaendelea kuandika habari ambazo imeziita za uchochezi dhidi yake, haitasita kuchukua hatua stahiki kwa mujibu wa sheria za nchi.

Hata hivyo, barua hiyo haijaweka bayana habari hizo ilizozielezea kuwa ni za mtazamo hasi dhidi ya serikali na ambazo imedai kuwa ni za uchochezi.

“Kwa barua hii unatakiwa kuacha mara moja tabia ya kuandika habari za uchochezi na kuidhalilisha nchi na serikali kwa kisingizio cha uhuru wa habari na uhuru wa kutoa mawazo ulioanishwa katika katiba ya nchi yetu," inaeleza barua hiyo ya Oktoba 11 iliyosainiwa na Raphael Hokororo kwa niaba ya Msajili wa Magazeti.

"Aidha ukiendeleza tabia hiyo, serikali haitasita kuchukua hatua stahiki za kulifungia gazeti lako au kulifutia usajili kwa mujibu wa sheria za nchi.”

Barua hiyo, ambayo imebeba kichwa cha habari kisemacho "Karipio kali kwa kuandika habari zenye mwelekeo wa uchochezi wa kudhalilisha", ni mwendelezo wa barua nyingine iliyoandikwa na mkurugenzi wa Idara ya Habari, Clement Mshana kwenda kwa mhariri wa gazeti hili Septemba 24, 2010.

Katika barua hiyo ya Mshana, serikali imedai kuwa gazeti la Mwananchi limekuwa na mtazamo hasi dhidi ya serikali na ikamtaka mhariri ajieleze.

Barua hiyo yenye kumbukumbu namba ISC/N.100/1/VOL.V/70, bila ya kutoa mifano, inadai kuwa Mwananchi imekuwa ikiandika habari hasi tu kana kwamba serikali haina zuri linalofanywa kwa wananchi wake na kutaka maelezo.

“Katika kipindi kirefu sasa, na zaidi wakati huu wa kampeni za uchaguzi, gazeti lako limekuwa likiandika habari zenye mtazamo hasi dhidi ya serikali. Habari hizo zimekuwa zikidhalilisha serikali iliyo madarakani ya awamu nne,” inasema sehemu ya barua hiyo.

Katika majibu ya barua hiyo ya kwanza, Mwananchi Communications Ltd (MCL), ilieleza kuwa baada ya kutafakari kwa kina ilishindwa kuelewa msingi wa tuhuma hizo ambazo hazina mifano yoyote ya habari inayodaiwa kuwa ni hasi kwa serikali.

“Baada ya kupitia barua yako na kuitafakari, imetuwia vigumu kuelewa msingi wa tuhuma zako kwa gazeti hili kuhusu mtazamo hasi dhidi ya serikali bila hata kutoa mifano ya habari ambazo zinabeba tuhuma zako kwa gazeti hili hasa unaposema kuwa kwa kipindi kirefu sasa, hasa wakati huu wa kampeni za uchaguzi,” inasema barua hiyo yenye kumbukumbu namba MCL/RN/09/VOL.1.27 iliyoandikwa na mhariri mtendaji wa MCL, Theophil Makunga.

Barua hiyo ya MCL inaeleza kuwa kimsingi habari za kampeni za uchaguzi katika kipindi hiki zinahusu vyama vya siasa na kuhoji sababu za serikali kujiona inaandikwa vibaya na Mwananchi wakati ni vyama ndivyo vinavyoshiriki kwenye kampeni.

Mhariri wa Mwananchi anaeleza katika barua hiyo kuwa kwa sasa gazeti lake linaandika habari za wagombea uongozi kutoka vyama mbalimbali na sera zao ili wananchi wafanye uamuzi siku ya kupiga kura na hakuna chama kilichoandika barua ya malalamiko.

“Kwa taarifa yako tangu kuanza kwa kampeni za uchaguzi Agosti 21, 2010, gazeti la Mwananchi halijawahi kupata malalamiko kutoka chama chochote cha siasa kinachoshiriki katika kampeni hizo juu ya kuandikwa vibaya. Kimsingi Mwananchi linachofanya ni kuripoti wanachosema wagombea wa vyama mbalimbali au kufanyiwa katika mikutano ya kampeni,” inasema barua hiyo ya MCL kwenda kwa Msajili wa Magazeti.

Katika barua hiyo, MCL inaiomba serikali kutoa ufafanuzi zaidi kuhusu kuhusika kwa serikali katika kampeni za uchaguzi hadi gazeti hili lionekane lina mtazamo hasi.

“Kwa msingi huo, tunaomba ufafanuzi zaidi hapa; serikali inahusika vipi katika kampeni mpaka Mwananchi ionekane ina mtazamo hasi kwa serikali wakati vinavyoshiriki katika kampeni ni vyama vya siasa na wagombea wake,” inasema barua hiyo.

Baada ya barua hiyo, Msajili wa Magazeti alijibu kwamba majibu yaliyotolewa na MCL hayaridhishi na hivyo ofisi yake haikuridhika na utetezi huo.

“Kama tulivyoeleza kwenye barua yetu kwako kuwa katika kipindi kirefu sasa na zaidi wakati huu wa kampeni za uchaguzi, gazeti lako limekuwa likiandika habari zenye mtazamo hasi dhidi ya serikali. Gazeti lako sasa limeamua kufanya ‘house style’ yake ya kuandika habari zenye uchochezi na kudhalilisha nchi na serikali iliyopo madarakani,” inasema barua hiyo.

Katika onyo lake, serikali inasema kwamba picha, habari zinazopewa kipaumbele katika ukurasa wa kwanza wa gazeti zinatiwa chumvi kwa lengo la kuchochea wananchi waione serikali yao haijafanya chochote kwa maendeleo yao.

Akiongelea hatua hiyo ya serikali, Makunga alisema kwamba MCL imeshtushwa na karipio hilo ambalo halikuonyesha ni habari ipi ambayo gazeti la Mwananchi limekosea.

“Msajili hakunukuu hata sheria moja ya vyombo vya habari kuonyesha jinsi gani gazeti limekosea wala habari au kichwa cha habari chenye mtazamo hasi kwa serikali,” alisema Makunga.

Alisema Mwananchi imechukulia hatua hiyo ya msajili kuwa inatishia uhuru wa vyombo vya habari hasa katika kipindi hiki cha kampeni za uchaguzi ambacho kinahitaji uvumulivu baina ya taasisi mbalimbali katika jamii.

Makunga alisema kwa kuwa Mwananchi na msajili inaonekana kutokubaliana katika suala hilo, wameamua kupeleka taarifa Baraza la Habari Tanzania (MCT) liweze kufanya uchunguzi kwa mujibu wa katiba yao.

Alisema msimamo wa sera ya uhariri ya MCL inasimamia kwenye ukweli na weledi pasipo kushurutishwa na vikundi vyovyote vya nje na ndani.Makunga alisema Mwananchi itaendelea kuandika habari za ukweli bila ya kumuonea mtu au taasisi yoyote kwa maslahi ya Tanzania.

CHANZO: Mwananchi


Baadhi ya wazazi wa watoto wanaugua ungonjwa wa malaria wakiwa nje ya Kituo cha Afya Nyamongo Wilayani Tarime

Anthony Mayunga, Tarime

KITUO cha Afya Nyamongo wilayani Tarime hakijapata dawa ya mseto inayotibu malaria kwa kipindi cha miezi mitatu hadi sasa.

Tatizo hilo linakwenda kinyume na kampeni za kupambana na malaria kwa kuwatibu wagonjwa ambayo inasisitiza kwamba Watanzania watapata vyandarua na dawa sahihi za kutibu malaria.

Uchunguzi wa uliofanywa na Mwananchi katika kituo hicho kilichoko katikati ya eneo la mgodi wa dhahabu wa North Mara ,ulibaini ukubwa wa tatizo hilo na wananchi kuonyesha kukata tamaa juu ya
mikakati inayonadiwa na viongozi kutokomeza malaria nchini. Marwa Ryoba mkazi wa Nyangoto alisema wanalazimika kutumia dawa za krolokwini,metakefilini na SP ambazo zilikwishapigwa marufuku na serikali kwa kushindwa kutibu ugonjwa huo.

“Tunashangaa ahadi na tambo nyingi za serikali kuwa watatokomeza malaria wakati hatupati dawa , hivi kupewa vyandarua na Wamarekani bila dawa inatusaidia?”alihoji kwa uchungu.

Mganga mfawidhi wa kituo hicho Dk George Marwa alikiri kuwa hawajapata
dawa mseto licha ya kutoa taarifa kwa zaidi ya miezi mitatu. “Hapa tunapambana na matatizo makubwa maana jamii haijui tatizo la Msd badala yake lawama zinaelekezwa kwetu,maana kama hakuna Alu unadhani huko wanatumia nini,”alisema. Kuhusu kadi za kiliniki hakuna na wajawazito na wenye watoto
wanalazimika kununua mitaani inadaiwa wananunua Sh2,000= maana hatuna,na hilo linawakatisha tamaa wasiokuwa na fedha kuhudhuria
kiliniki.
“Hapa tunahudumia zaidi ya watu laki moja kutoka kata zaidi ya nne za Tarime na Serengeti, glovu unapewa pc 50 kwa miezi mitatu ,wakati hizo ni kwa wiki moja,wanalazimika kununua, na ni tatizo la mfumo.

Awali mwanamke aliyekutwa katika kituo hicho akisubiri huduma jina tunao ,alisema kuwa wanachofanya ni kwenda kuandikiwa tu kisha wanakwenda kununua dawa kwenye maduka ya watu ambao pia si wataalam.
“Wengi tunatumia panadol wakati unaumwa malaria na hata kwa watoto
,matokeo yake panapotokea vifo inakuwa vigumu kujua nini tatizo ,maana wapo wanaoishiwa damu, lakini tunashindwa watibiwe na nini,”alisema.

Alikwenda mbali na kudai kuwa matatizo ya wananchi kwa huduma za afya yamegeuka kuwa mtaji kwa wanasiasa wanafiki,kwa kutoa ahadi ambazo hazitekelezeki,”suala la dawa limeshindikana sasa wanadai malaria
itakuwa historia kwa kuua ama nini?”alihoji kwa masikitiko.Baadhi ya wajawazito na wenye watoto waliokuwa hapo kituo
cha afya walisema mbali na dawa ya malaria pia wanalazimika kununua kadi na glovu kwa kuwa hazipatikani hapo kituoni .

“Pembeni wanasema huduma kwa wajawazito na watoto chini ya miaka mitano bure ,lakini hapa tunanunua dawa,mipira ya mikononi(Gloves)na kadi za kiliniki,wengi wanajifungulia majumbani na hawaleti watoto
kiliniki akiugua malaria wananunua panadol na dawa za kienyeji,”walisema.

CHANZO: Mwananchi

NAAMINI TATIZO LA KUDAIWA MALIPO KWA HUDUMA ZINAZOPASWA KUTOLEWA BURE NI KARIBU KILA MAHALI NCHINI.NDIO MAANA CCM HAWATAKI KUSIKIA AHADI YA CHADEMA KUHUSU  ELIMU BURE.

17 Oct 2010

Moja ya mambo yaliyokuwa yakiwaumiza vichwa wafuasi wa Barack Obama wakati wa kinyang'anyiro kati yake na Hillary Clinton kupata mgombea urais wa Marekani kwa tiketi ya chama cha Democrats mwaka 2008 ni theory inayofahamika kama Bradley Effect.Kwa kifupi kabisa,Bradley Effect (au Wilder Effect) ni hali inayoweza kutokea kwenye kura za maoni katika chaguzi nchini Marekani panapokuwa na mgombea Mweupe (White) na asiye mweupe (non-White).Pengine ili wasionekane wabaguzi wa rangi,wahojiwa Weupe katika kura za maoni hueleza kuwa chaguo lao ni mgombea asiye Mweupe au husema kuwa hawajafanya uamuzi kuhusu chaguo lao (Undecided).

Kwahiyo,matokeo ya kura ya maoni yanaweza kuonyesha mgombea asiye Mweupe anapendwa zaidi kuliko mgombea Mweupe lakini inapofika kwenye hatua ya kupiga kura (ambapo mpiga kura anakuwa peke yake),wapiga kura Weupe wanampigia Mweupe mwenzao.

Asili ya Bradley Effect ni katika kinyang'anyiro cha uchaguzi wa uchaguzi wa gavana wa jimbo la California mwaka 1982 ambapo licha ya mgombea Mweusi,Meya wa Jiji la Los Angeles Tom Bradley kuongoza kura za maoni,aliishia kushindwa uchaguzi huo kwa mgombea Mweupe George Deukmejian.

Baadhi ya wachambuzi wa chaguzi nchini Marekani wanaamini pia kuwa Bradley Effect ilijitokeza tena kwenye mchakato wa kumpata mgombea wa chama cha Democrats kwenye jimbo la New Hampshire ambapo licha ya Obama kuongoza katika kura za maoni,Hillary Clinton aliibuka mshindi kwenye jimbo hilo (japokuwa baadaye Obama alifanikiwa kuibuka mshindi wa jumla,na kupitishwa kuwa mgombea urais kwa tiketi ya Democrats,na hatimaye kushinda nafasi ya urais).

Katika post hii najaribu kubashiri (hypothesize) namna Bradley Effect inavyoweza kuwa sababu ya mgombea wa CCM,Jakaya Kikwete,kuongoza katika tafiti za  taasisi za Redet na Synovate kuhusu nafasi za wagombea urais katika uchaguzi mkuu wa Tanzania hapo Oktoba 31.Hapa ntawazungumzia wagombea wawili tu,Kikwete na mgombea urais kwa tiketi ya Chadema,Dokta Wilbroad Slaa.

Japo Bradley Effect 'halisi' inahusu mgombea Mweupe na asiye Mweupe,sababu inayopelekea matokeo ya kura kutorandana na mwelekeo wa kura za maoni inaweza kutumika kuelezea kwanini kura za maoni za Redet na Synovate zilimpa Kikwete ushindi na sio Dokta Slaa.Kama ilivyo kwenye chambuzi mbalimbali,kuna mambo flani inabidi 'kupuuzwa' ili kufikia matokeo yanayokusudiwa.Katika uchambuzi huu,naomba 'nipuuze' urafiki kati ya taasisi hizo na CCM na badala yake nikazanie kwenye uwezekano wa Bradley Effect pekee.

Inawezekana kabisa kuwa wahojiwa kwenye tafiti za Redet na Synovate ni wananchi waliotoa majibu 'kuwaridhisha watafiti',yaani walisema wanampenda zaidi Kikwete kuliko Dokta Slaa.Moja ya sababu za kutoa majibu ya aina hiyo ni mazingira halisi ya Tanzania ambapo licha ya 'siasa za mkono wa chuma' za zama za chama kimoja kuonekana kama historia,ukweli unabaki kuwa baadhi ya wananchi wanaamini kuwa kusema lolote lisilowapendeza watawala ni kujitafutia matatizo.

Naomba kufafanua kidogo katika hilo.Nilipokwenda Tanzania mwaka 2005 kufanya fieldwork ya utafiti wangu wa shahada ya uzamifu (PhD) nilikumbana na wakati mgumu kuwahoji baadhi ya maustaadh (mada yangu inahusu masuala ya Waislam na Uislam nchini Tanzania) kwa vile baadhi yao walidhani mie ni wakala wa serikali niliyetumwa kuwachunguza ili 'serikali iweze kuwadhibiti zaidi'.Bahati mbaya,fieldwork hiyo ilifanyika wakati jeshi la polisi lilikuwa linamsaka mwanaharakati wa Kiislam,Sheikh Issa Ponda.Ilichukua kitambo kujenga uaminifu kati yangu na maustaadh hao.

Kuna wanaoilaumu Redet na Synovate kuhusu aina ya watu waliohojiwa wakidai kuwa huenda wahojiwa walikuwa watu walio karibu na CCM (kwa mfano mabalozi wa nyumba kumi).Uwezekano wa Bradley Effect  'yetu' (yaani isiyohusiana na ishu za ubaguzi wa rangi) ni mkubwa kwa vile wahojiwa wanaweza kutoa majibu yasiyoonyesha 'wanambagua mgombea wao' na hivyo kusema huyo ndio chaguo lao japo mioyoni wana dhamira na/au chaguo tofauti.

Of course,inawezekana tafiti hizo za Redet na Synovate 'zilipikwa' ili kuendana na matakwa ya CCM.Inawezekana pia kuwa aina ya watu waliohojiwa ni ambayo isingetoa majibu tofauti na 'ushindi kwa Kikwete'.Lakini,kama makala hii inavyojaribu kubashiri,inawezekana kabisa kuwa wahojiwa 'waliwazuga' jamaa wa Redet na Synivate 'ili isiwe shida'.Nani yuko tayari kuona genge lake au kibanda cha biashara kinabomolewa kwa vile tu amechoshwa na namna CCM inavyozidi kuahidi maisha bora lakini wanaonufaika ni mafisadi pekee?Mtu wa aina hii haoni shida 'kudanganya leo' kisha 'akaungama siku ya kupiga kura' kwa 'kumwadhibu Kikwete na CCM kwenye sanduku la kura ambapo hakutokuwa na wa kumtoa mimacho kwanini hajampigia kura Kikwete au CCM'.

Huu ni ubashiri tu.Unaweza kuwa sio sahihi lakini kama zilivyo bashiri nyingine-hususan zinazoambatana na mifano hai-unaweza kuwa na ukweli ndani yake.Kadhalika,Bradley Effect 'yetu' inaweza kutoa matokeo ya kuwashangaza wote wenye imani kuwa CCM na Kikwete watarudia kupata ushindi wa kishindo kama wa mwaka 2005.

Pengine kuna watakaohoji kwanini Bradley Effect 'yetu' haiwezi kutumika kwenye utafiti mwingine (wa TCIB) unaoonyesha kuwa Dokta Slaa anaongoza.Jibu langu ni kwamba watoa maoni hawana cha kupata (nothing to gain) kuwadanganya watafiti kuwa wanampenda Dokta Slaa wakati ukweli wanayempenda ni Kikwete.Likewise,kwenye tafiti za Redet na Synovate,inawezekana baadhi ya wahojiwa walikuwa na cha kupoteza laiti wangesema hawampendi Kikwete (si unajua kuhusu umoja na mshikamano ndani ya chama?).Vilevile,yawezekana wahojiwa hawakuwa na cha kupoteza (nothing to lose) kwa kudanganya kuwa wanampenda Kikwete (kwa minajili ya kuwaridhishwa watafiti na 'kulinda ugali wao') kisha wakamnyima kura katika usiri wa chumba cha kupigia kura.

Mwisho,naomba kusisitiza tena kuwa hypothesis hii imejaribu kupuuza sababu za 'wazi' kama vile upendeleo wa watafiti,uoga wa wahojiwa,na kubwa zaidi,UCHAKACHUAJI.

16 Oct 2010


Senegal welcomed 163 Haitian university students to Dakar Wednesday. Senegalese president Abdoulaye Wade, offered them free education after an earthquake devastated their island nation in January.

Sanogier Genevieve Julbertha arrived in Senegal Wednesday, less than a year after a catastrophic earthquake in her country killed about 200,000 people and caused widespread structural damage.

The 20-year-old law student is one of the more than 160 Haitians who will enroll in a Senegalese university this fall free of charge.

She says she does not have the words to describe how good it is to be in Senegal. She says we are the same people. We share the same roots. She says life is still difficult for many Haitians. Many universities collapsed, she says, and many families are still homeless.

The Senegalese government was swift to offer aid to Haiti in the earthquake's aftermath this January, committing $1 million in emergency relief as well as offering land to Haitians who wanted to relocate to Senegal.

Senegalese President Abdoulaye Wade addressed the students Wednesday at a ceremony at the foot of his recently-inaugurated Monument to the African Renaissance. He called the students' arrival an act of "panafrican solidarity."

Mr. Wade says today marks the return of young Haitians to the land of their ancestors and a resounding victory for Africa. Others before us have tried, he says, only to return to a land still dominated by outside forces, but these students are returning freely to an independent Africa in control of its destiny.

The students will attend one of three Senegalese universities on full scholarships from the Senegalese government.

Mardoche Fontilus, 20, says he will study psychology in Senegal. The opportunity is a "dream come true," he says, but it cannot erase the memories of this past year.

He says the earthquake impacted the lives of everyone in Haiti, and it was our brothers, sisters, aunts and cousins under the rubble. He says he is grateful for the international aid they have received, but January 12 was a sad day they will never be able to forget.

Fontilus said he hopes the education he receives in Senegal will allow him to return to Haiti and help rebuild his country.

SOURCE: VoA

15 Oct 2010


Na Mwandishi wetu

Shirika lisilo la kiserikali linalojishughulisha na kutoa utafiti wa taarifa mbalimbali kwa lengo la kuwawezesha wananchi maamuzi kwa uelewa la Tanzania Citizens Information Bureau (TCIB) limetoa taarifa ya matokeo ya utafiti wa kura ya maoni kuhusu wagombea urais 2010.

Akizungumza na waadishi wa habari Mhadhiri Chuo Kikuu cha Dar es salaam idara ya Uchumi Dr. Vicent Leyaro amesma malengo ya TCIB ni kutoa msukumo kwa wananchi kushiriki katika harakati za kulinda na kendeleza misingi ya Demokrasia, Kutoa fursa kwa wananchi katika kutoa maoni yao juu ya mambo mbalimbali katika maisha na kujenga uwezo wa wananchi kwa njia ya tafiti na elimu katika nyanja za serikali, siasa, Mambo ya Kimataifa, ulinzi, elimu na maadili.
Kutoka kushoto ni Mhadhini kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Idara ya Uchumi Dr.Vicent Leyaro akizungumza na waandishi wa habari katika Hotel ya Courtyard juu ya utafiti wa (TCIB) akiwa na mwakilishi wa Mkurugenzi wa (TCIB) Bw. Steven Msechu.

Aidha Dr. Vicent Leyaro amesema washiriki katika kura hii ya maoni ni 3047 wenye wasifu wa aina mbalimbali ikiwa ni pamoja na watoto chini ya darasa la saba, elimu ya sekondari na elimu iliyo juu ya sekondari ambapo katika utafiti huo silimia kubwa ya vijana wamonekana kuunga mkono mgombea urais wa CHADEMA Wllbrod Slaa na asilimia kubwa ya wazee wameonyesha kumuunga mkono mgombea urais wa CCM Jakaya Kikwete.

Amesema Dr. Willbod Slaa ameongoza kwa asilimia kubwa katika mikoa ya Kilimanjaro 71%, Arusha 60.4%, Manyara79.8%, Iringa58.2% na Dar es salaam 42% ambapo Jakaya Kikwete ameongoza kwa asilimia kubwa katika mikoa Dodoma 59.3%, Morogoro 56%, Mbeya50%, Rukwa 54.3% na Ruvuma 55%.

Akihitimisha wakati akijibu maswali kwaa waandishi wa habari Dr. Vicent Reyaro amesema utafiti haukuangalia wala kupendelea sehemu ambazo mtu anapendwa sana kuliko sehemu nyingine na uchambuzi wa matokea kimkoa yanaonyesha kuwa wagombea wawili Jakaya Kikwete na Dr. Willbrod Slaa wanachuana vikali baadhi ya mikoa na mikoa mingine kufanya vibaya.

Hata hivyo utafiti huu wa kura ya maoni kuhusu wagombea urais hauukufanyika kwa upande wa Zanzibar japokuwa wananchi wa Zanzibar wanashiriki katika kupiga kura ya kuchagua rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Chanzo: Changamoto

Habari kwa hisani ya Jamii Forums


Makala yangu katika toleo la wiki hii la jarida maridhawa la Raia Mwema inazungungumzia madai ya mgombea Urais kwa tiketi ya Chadema,Dkt Wilbroad Slaa,kuwa serikali ya Rais Jakaya Kikwete imesambaza maafisa usalama nchi nzima ili kuhujumu uchaguzi (kumsaidia Kikwete ashinde).Kwa kutumia taaluma na utaalam wa kutosha kuhusu masuala ya intelijensia,makala inajaribu kumpa mwangaza msomaji iwapo Idara yetu ya Usalama wa Taifa inaweza kutumiwa visivyo katika mazingira tuliyonayo sasa.

BONYEZA HAPA KUSOMA MAKALA HIYO Pamoja na habari na makala nyingine zilizokwenda shule katika jarida hili mahiri la Raia Mwema


Mimi si mwanasheria japo nasaka uhitimu wa kiwango cha kati (katika Sheria) kwa njia ya masafa.Kwahiyo nina uelewa wa wastani kuhusu masuala ya jumla-jumla kuhusiana na taaluma ya Sheria.Na ni katika hilo ndipo nafahamu kuhusu CLASS ACTION.Kwa uelewa wangu wa wastani,Class Action ni aina ya kesi ya madai inayofunguliwa na kundi (mara nyingi kundi kubwa) dhidi ya taasisi au kundi flani.

Kwa mfano,kundi la wavuta sigara linaweza kufungua class action dhidi ya kiwanda cha tumbaku au cha sigara kulingana na madai yao dhidi ya wadaiwa.Aina hii ya kesi ni maarufu zaidi huko Marekani,na sina ufahamu kama imeshawahi kutokea huko nyumbani.

Naamini tuna Watanzania wazalendo katika kila fani.Naamini pia tuna Watanzania wazalendo wenye taaluma ya sheria hususan kesi za madai au kwenye sheria za mawasiliano.Lengo la makala hii ni kuuliza kama wazalendo hao hawawezi kutoa fundisho kwa makampuni mbalimbali ya simu huko nyumbani ambayo yayumkinika kuyatuhumu kuwa yanakiuka haki za usiri (privacy) wa wateja wao.

Kuna hayawani flani amekuwa akisambaza SMS za kumchafua mgombea urais kwa tiketi ya Chadema,Dokta Wilbroad Slaa.Haihitaji uchambuzi wa aina yoyote kufahamu uhuni huo wa SMS usingekuwepo laiti Dokta Slaa asingekuwa tishio.

Na japo CCM wamekanusha kuhusika na uhuni huo lakini kama waliweza kuchafuana wenyewe kwenye mchakachuo wa kura za maoni watashindwaje katika mpambano huu wa kufa na kupona hapo Oktoba 31?Unajua tatizo la CCM ya Jakaya Kikwete ukilinganisha na ile ya Mwalimu,Mwinyi au hata Mkapa,ni ombwe kuuuuubwa la uongozi katika chama hicho.Kama ambavyo Kikwete amemudu kutengeneza ombwe la uongozi wa kitaifa akiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano,ndivyo ambavyo ameshindwa kwa kiasi kikubwa kumudu nidhamu ndani ya CCM.Tatizo kubwa linalomkabiri Kikwete ni kujazana kwa viumbe kadhaa waliofadhili kampeni zake za kupata urais mwaka 2005.Hana jeuri ya kuwadhibiti (japo angeweza kufanya hivyo kama angemudu kuweka ushkaji pembeni).

Katika mazingira ya sasa ambapo CCM imekuwa kama povu linaloelea angani likisubiri japo pini litoboke,chizi yoyote yule anaweza kukurupuka na mkakati wa kihuni wa kusambaza SMS dhidi ya Dokta Slaa.Baadhi ya taarifa zinamhusisha mhuni huyo na familia ya fisadi mmoja mwenye wadhifa mkubwa ndani ya CCM (Like Father Like Son).Au inawezekana kabisa kuwa SMS zina baraka zote za CCM na Kikwete mwenyewe.Katika siasa za kichakachuaji lolote linawezekana.

Back to my point kuhusu uwezekano wa Class Action.Makampuni ya simu yanayoruhusu wateja wao kubughudhiwa na SMS hizo hayawezi kukwepa lawama kuhusu uhuni huu.CCM wanakiri kuwa wao wanatuma SMS njema tu.Je nani anawapa namba za kutuma SMS hizo njema?Jibu ni makampuni yetu ya simu.

Sasa,iwe ni SMS njema au za kihuni kama hizo za dhidi ya Dokta Slaa,lililo dhahiri ni kuwa makampuni hayo yanavunja haki za wateja wao kutobughudhiwa.Na hapo ndipo napojaribu kuwahamasisha wanasheria wazalendo kuangalia uwezekano wa Class Action dhidi ya makampuni hayo.

Nilishawahi kuandika kwenye makala zangu kwenye jarida la Raia Mwema kuhusu upole wa Watanzania hata pale wanaponyimwa haki zao za msingi.Kwa mfano,ni Watanzania wangapi ambao nyumba na mali zao zimeshawahi kuungua kutokana na uzembe wa Shirika la Umeme (TANESCO) lakini wahanga hao wameishia kunung'unika tu badala ya kuwashikisha adabu wana-umeme hao?Ni dhahiri kuwa laiti TANESCO wangefikishwa mahakamani kwa kusababisha shoti japo ya pasi ya umeme tu wangekuwa makini kabla ya kukurupuka kuzima umeme kila wanapojiskia.

Au ni Watanzania wangapi wamepoteza wapendwa wao (kama sio wao wenyewe kupoteza viungo vyao) kutokana na ajali zinazochangiwa na mchanyato wa ufisadi wa matrafiki na wamiliki wa vyombo vya usafiri,lakini wahanga hao wameishia kuomba msaada wa Mungu badala ya kudai fidia?Of course,hakuna fidia inayotosheleza kifo cha mtu lakini tunafundishwa kwenye sosholojia kuwa negative sanctions (kwa mfano adhabu kama faini,kifungo,nk) zinaweza kuzuia wakosaji kurejea tena makosa yao.

Pengine hakuna mwanasheria mzalendo anayepita kwenye blogu hii.Lakini pengine unamfahamu mwanasheria wa aina hiyo.Basi ombi langu ni kumfikishia ujumbe huu wa kuangalia uwezekano wa Class Action dhidi ya makampuni ya simu yanayopuuza haki za wateja wao kwa kuruhusu SMS za kihuni.

TUSIPOZIBA UFA TUNAWEZA KUJENGA UKUTA.LEO SMS NI DHIDI YA DOKTA SLAA KWA VILE MAFISADI HAWATAKI AINGIE IKULU.KESHO KUNAWEZA KUWA NA SMS ZA KUHAMASISHA YALEYALE YA WAHUTU DHIDI YA WATUTSI AU WAISLAMU DHIDI YA WAKRISTO.NA HAYO YANAWEZEKANA ZAIDI KATIKA MAZINGIRA HAYA YA OMBWE LISILOELEZEKA (INCONCEIVABLE) KATIKA MEDANI YA UONGOZI WA TAIFA LETU "CHANGA".



Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.