10 Jan 2011



Tanzania tuna tatizo kubwa.Hakuna haja ya kunyoosheana vidole as to nani amechangia tatizo hilo bali cha muhimu na haraka ni namna tutakavyoweza kutatua tatizo hili.Nisimung'unye maneno: tatizo kubwa linaloikabili ni kuwa na Rais ambaye takriban miaka sita tangu aingie Ikulu haelewi wajibu wake.

Hivi msomaji mpendwa wa blogu hii utamuelezeaje Jakaya Kikwete,Rais wetu,baada ya kumsikia akijitetea kwa mabalozi wanaowakilisha nchi zao Tanzania kuwa "unyama wa hali ya juu uliofanywa na polisi huko Arusha,na kusababisha vifo vya Watanzania wasio hatia,ni BAHATI MBAYA"!!!

Yani Kikwete aliishiwa kabisa na cha kudanganya mpaka akakurupuka na excuse dhaifu kiasi hiki!Bahati mbaya kwa maana gani?Bahati mbaya IGP Said Mwema kutengua dakika za majeruhi ruhusa ya maandamano iliyotolewa na RPC wa Arusha?Bahati mbaya polisi kuachana na jukumu la kusindikiza maandamano ya amani na badala yake kuanza kuwaadhibu wananchi wasio na hatia ambao "kosa" lao lilikuwa kutumia haki yao ya kikatiba kuandamana kwa amani?Bahati mbaya kupuuza miito kutoka kada mbalimbali juu ya umuhimu wa kutafuta ufumbuzi wa mgogoro wa umeya wa Arusha?Au bahati mbaya kwa risasi kutoka kwenye mitutu ya bunduki na hatimaye kutoa uhai wa Watanzania wasio na hatia?

Au Kikwete alikuwa anamaanisha kwamba unyama wa polisi wake dhidi ya wafuasi wa CUF walipoandamana,au vitendo vya udhalilishaji vya polisi hao dhidi ya wastaafu wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki,au unyanyasaji uliozoeleka dhidi wa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kila wanapoandamana,ni BAHATI NZURI kwa vile hakuna aliyeuawa?

Nashindwa hata kuhisi mabalozi walipatwa na mawazo gani walipomsikia mkuu wa nchi anatoa kauli ya ajabu kiasi hicho.Nahisi kuna waliomhurumia kwa kijibebesha jukumu asiloweza.Hii inanikumbusha wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005 (ambazo zilinikuta nikiwa huko nyumbani kwa miezi kadhaa).Kuna baadhi ya wajuzi wa siasa za Tanzania waliniambia kuwa Kikwete anaweza kushinda urais kwa vile ana timu ambayo iko tayari kufanya lolote kuhakikisha anapata ushindi LAKINI urais wake utakuwa kituko.Na kituko amekuwa.

Kuna watakaosema wa kulaumiwa ni washauri wake.Lakini hao watakuwa wamesahau kuwa alipoanguka Mwanza alitanabaisha kuwa huwa anapuuza ushauri wa washauri wake (ambapo tulielezwa walimshauri apumzike kabla ya kukumbwa na zahma hiyo).Sasa inawezekana kabisa kuwa hata kabla ya kuongea na mabalozi hao,washauri wake walimshauri kitu sensible cha kuongea lakini akapuuza.Au pengine waliona hakuna haja ya kumshauri mtu ambaye ni "haambiliki".

Lakini tukiweka kando excuse hiyo ya kitoto iliyotolewa na mtu tuliyemkabidhi jukumu la kutuongoza Watanzania takriban milioni 50,ukweli kwamba Kikwete amediriki kujiumauma kwa mabalozi unapigia mstari ushauri niliotoa kwenye makala yangu iliyopita.Katika makala hiyo niliwashauri Watanzania wanaoishi katika nchi wafadhili wa Tanzania kuwasiliana na wabunge/wawakilishi wao na kuwafahamisha udikteta wa Kikwete,kisha kuwaomba wafikishe kilio cha Watanzania kwa serikali za wafadhili hao.Kikwete amelazimika kuokoteza excuses kwa vile anatambua bayana kuwa ni lazima awapoze wafadhili kwani mchango wa wafadhili hao ni muhimu sana kwa ustawi wa taifa letu.Ni muhimu zaidi kwa ustawi wa Kikwete na serikali yake inayosifika kwa matumizi ya anasa yanayozidi mapato.Wafadhili wakiamua kusitisha misaada,serikali itaanguka within months if not weeks.Lakini idea yangu ya kufikisha ujumbe kwa nchi wafadhili haikulenga kuwashawishi wasitishe misaada bali naamini wao wanaweza kumbana dikteta huyu aanze kuheshimu haki za binadamu.

Na kuthibitisha kuwa Kikwete alikuwa anawazuga mabalozi hao,gazeti la Tanzania Daima lina habari kuwa jeshi la polisi limezuia maandamano ya amani huko Songea yaliyoandaliwa na Chadema kupinga ufisadi katika sekta ya kilimo. Huu ni uthibitisho tosha kuwa unyanyasaji wa raia wasio na hatia na ukiukwaji wa haki za binadamu unaofanywa na polisi sio suala la BAHATI MBAYA kama anavyozuga Kikwete.Ni utekelezaji wa maagizo ya serikali iliyopo madarakani inayoongozwa na Kikwete huyohuyo.

Hivi Kikwete ameshindwa angalau kuwatosa Waziri wa Mambo ya Ndani Shamsi Vuai Nahodha,IGP Mwema na RPC wa Arusha kuwa "mbuzi wa kafara" ali mradi imsaidie kudanganya kuwa yeye hahusiki na maagizo yaliyopeleka polisi kuua.Hawezi kuwatosa kwa vile ni kiongozi anayeendekeza ushkaji.Sasa kama familia haiwezi kuongozwa kishkaji,nchi ikiongozwa kwa mtindo huo inakuwaje?

Na kuna kila dalili kuwa hivi sasa Kikwete anaongoza nchi na CCM yake kwa mtindo wa "bora liende".Hebu angalia jinsi ishu ya fidia kwa Dowans inavyoonyesha mparaganyiko kwenye kabineti ya Kikwete.Wakati Waziri William Ngeleja anatweta kuwakikishia mafisadi wa Dowans kuwa lazima walipwe kwa utapeli wao,Waziri Samuel Sitta anatangaza hadharani kuwa kuwalipa Dowans ni jambo la hatari.Uwajibikaji wa pamoja Kikwete's cabinet style!Huko CCM,Katibu wa chama hicho mkoani Arusha,Mary Chatanda anawawakia viongozi wa dini akiwataka wavue majoho yao wajiunge na siasa badala ya kukemea maovu (mpuuzi huyu anakosa adabu hata kwa Watumishi wa Mungu!).Kwa upande mwingine,Katibu Mkuu wa chama hicho,Yusuph Makamba,anadai kila mtu ana uhuru wa kutoa mawazo yake including viongozi wa dini.Na yote hayo yanatokea huku yakiweka kivuli kwenye tukio la kihistoria la diwani wa CCM kujiunga na Chadema.Tukio hili linapaswa kuchukuliwa kama ugonjwa nyemelezi kwa mwathirika wa ukimwi: linaashiria mwanzo wa mwisho wa CCM.

NIMALIZIE KWA KUKUMBUSHIA WITO WANGU KWA WATANZANIA WENZANGU WANAOISHI NCHI ZA WAFADHILI WA TANZANIA.KUWA MBALI NA NYUMBANI ISIWE SABABU KWETU KUSHINDWA KUSAIDIA UPATIKANAJI WA UHURU WA PILI WA TANZANIA (wa kwanza ulikuwa wa kumwondoa mkoloni,wa pili ni wa kuondoa udhalimu,ufisadi,ubabaishaji,unyanyasaji,ukiukwaji haki za binadamu,udikteta na kila baya unalofahamu).TUWASILIANE NA WABUNGE/WAWAKILISHI KATIKA MAENEO TUNAYOISHI NA KUWAOMBA WATUFIKISHIE KWA SERIKALI ZAO VILIO VYA WATANZANIA WENZETU WANAONYANYASIKA KWA KILA HALI CHINI YA UTAWALA WA KIKWETE NA CCM YAKE

8 Jan 2011







Mbunge wa zamani kutoka chama cha Labour hapa Uingereza,David Chaytor (pichani juu),leo amelala usiku wa kwanza akiwa jela kama mfungwa baada ya kuhukumiwa kifungo cha miezi 18 kutokana na kukutwa na hatia ya ubadhirifu wa fedha za umma takriban pauni 20,000 (takriban shilingi 45 milioni za Tanzania).Ubadhirifu wa fedha hizo za umma ni kutokana na matumizi mabaya ya fedha za posho kwa wabunge.


Wakati hayo yakijiri hapa,huko nyumbani Waziri wa Nishati na Madini,William Ngeleja alivunja mzizi wa fitina kwa kutangaza hadharani kuwa hatimaye serikali italipa shilingi 95,000,000,000 (bilioni tisini na tano) kwa kampuni ya kifisadi ya Dowans kufuatia hukumu ya kiini macho iliyotoa ushindi kwa kampuni hiyo licha ya rundo la utata linaloendelea kuizunguka.



Ngeleja,bila haya wala uoga,alieleza kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali (Frederick Werema) ameridhia hukumu hiyo ya miujiza kabisa na ushauri wake wa kitaalam (ya sheria) ni kuilipa kampuni hiyo.

Wote,Ngeleja na Werema ni wateuliwa wa Rais Jakaya Kikwete,ambaye kwa makusudi kabisa aliepuka kuzungumzia suala la Dowans katika hotuba yake ya kukaribisha mwaka mpya 2011.Ni dhahiri kuwa Kikwete ameridhia Dowans ilipwe na ndio maana Ngeleja na Werema wanatoa maamuzi yao bila hofu wala aibu. Na kama umesahau,ni Kikwete huyuhuyu aliyeahidi wakati wa kampeni zake kuwa ana dhamira ya kuboresha maisha ya Watanzania.Nadhani labda alichomaanisha ni kuboresha akaunti za mafisadi kwa mgongo wa walalahoi.

Napata shida kutumia lugha ya kistaarabu kushangazwa na uwendawazimu huu!Hivi hawa viongozi wetu wamerogwa na mafisadi au ni matokeo ya kupokea fadhila za mafisadi kupita kiasi kwamba sasa wanalazimika kulipa fadhila hizo kwa gharama yoyote ile?Hizi sio tamaa za kawaida tulizozowea kuziona kwa watawala wetu.Hiki ni kichaa hatari ambacho pasipo hatua za haraka kinaweza kupelekea nchi nzima kuuzwa,kisha akina Werema wakaja kutuambia gharama za kuzuia kuuzwa kwa nchi yetu ni kubwa kuliko uamuzi wa kukubali nchi iuzwe.

Blogu hii ilifanya kila ilichoweza kuhamasisha wapiga kura waiepuke CCM na mgombea wake Kikwete.Sio kwamba blogu hii ilifanya utafiti wa kina kubaini athari za kuirejesha CCM madarakani bali taarifa kuhusu uhuni wa chama hicho,sambamba na kilivyojipa jukumu la kuwa kichaka cha kuhifadhi mafisadi,zilikuwa bayana kwa kila mwenye macho.Hivi kuna Mtanzania asiyefahamu kuwa ujio wa kampuni ya kijambazi ya Richmond (iliyopelekea ujambazi mwingine wa Dowans) ulikuwa na baraka za Kikwete pamoja na swahiba wake Lowassa na "kubwa la maadui" Rostam Aziz?





Ndio maana majuzi baada ya aliyekuwa mgombea urais kwa tiketi ya Chadema,Dkt Wilbroad Slaa,kurejea kauli yake kuwa Kikwete ni mmiliki wa Dowans,hasira za mkuu huyo zikaishia kwa kuamuru polisi wake kutoa kipigo kwa raia wasio na hatia huko Arusha na kupelekea vifo kadhaa (Polisi wanadai wameua watu watatu tu lakini tangu lini wauaji wakaaminika?).


Na kama adhabu ya Kikwete kwa Chadema na wana-Arusha haijatosha,kaamua kuwadhihaki Watanzania wote kwa kuidhinisha Dowans ilipwe mabilioni hayo,huku swahiba wake Rostam akidhihaki Watanzania kwa kudai hizo bilioni kadhaa ni fedha kiduchu tu kwake.Huwezi kumlaumu kwani kaiweka serikali mfukoni na anaendesha nchi kwa remote control.

Blogu hii iliwaasa wapiga kura kuhusu madhara ya kumpatia Kikwete miaka mitano mingine baada ya awamu yake ya kwanza kugubikwa na ufisadi wa kutisha.Lakini hata kwa viwango vilivyozoeleka vya ufisadi hakuna aliyetarajia kuwa hata kabla miezi mitatu haijapita tangu arejee madarakani,Kikwete angediriki kuruhusu Watanzania wenzie wabakwe kiuchumi kwa mtindo huu wa Dowans.Lakini kwa vile Katiba tuliyonayo inampa madaraka mithili ya mungu-mtu,na kwa vile anafahamu fika kuwa Watanzania ni wepesi wa kusahau na ndio maana wengi wao wakampigia kura licha ya maumivu aliyowasababishia tangu aingie madarakani Desemba 2005,ameruhusu ujambazi huu wa mabilioni ya fedha za walipa kodi pasi soni.

Tusipochukua hatua za haraka tutashtukia tumefikishwa mahala ambapo hatutokuwa na namna ya kurekebisha mambo.Kama less than three months tangu Kikwete arejee madarakani tumeshashuhudia Dowans ikizawadiwa mabilioni kama asante ya kututapeli,na tumeona hasira za Kikwete kwa ukatili na mauaji yaliyofanywa na polisi wake (kisa kasutwa kuwa analea ufisadi),ni wazi kuwa hali itazidi kuwa mbaya na yawezekana ikawa ya kutisha kabla Kikwete hajamaliza muda wake hapo 2015 (assuming hatachakachua Katiba kutaka aongezewe muda).

Moja ya hatua inayoweza kuzaa matunda ni kufikisha kilio chetu kwa nchi wahisani.In addition to malezi anayotoa Kikwete kwa mafisadi,sasa tuna jambo jingine zito ambalo linaweza kuvuta hisia za wahisani,nalo ni ukiukwaji wa haki za binadamu kama ilivyodhihirika huko Arusha.



Kwa kuanzia,blogu hii inamwomba kila mzalendo anayeishi katika nchi mfadhili kwa Tanzania,kuwasiliana na mbunge wake na kumwomba afikishe kilio cha wanyonge wa Tanzania.Toa chapa ya picha za matukio ya Arusha pamoja na habari zinazobainisha ukiukwaji wa haki za binadamu,na ufisadi,kisha mfahamishe mbunge huyo kuwa hii ndio hali halisi ya Tanzania chini ya utawala wa Kikwete.Kama utahitaji maelezo zaidi ya namna ya kuwasilisha ujumbe wako kwa mbunge wa sehemu unayoishi,usisite kuwasiliana nami.

KWA USHIRIKIANO WETU,TUNAWEZA KUPAMBANA NA UTAWALA DHALIMU AMBAO LICHA YA KUUA RAIA WASIO NA HATIA HUKO ARUSHA,UNATOA ZAWADI YA SHILINGI BILIONI 95 KWA DOWANS KANA KWAMBA HIYO NDIO RAMBIRAMBI KWA WALIOUAWA NA POLISI HUKO ARUSHA.

7 Jan 2011













PICHA KWA HISANI YA VYANZO MBALIMBALI MTANDAONI.
INTELIJENSIA YA KUBASHIRI KUWA MAANDAMANO YA AMANI YATAISHIA KUVUNJA AMANI-IPO.INTELIJENSIA YA KUMJUA MMILIKI WA KAGODA HAIPO.INTELIJENSIA YA KUMTAMBULISHA MMILIKI WA DOWANS HAIPO!

BINAFSI NACHUKULIA AMRI YA KIKWETE ILIYOPELEKEA MAUAJI YA WATANZANIA WASIO NA HATIA ILITOKANA NA HASIRA YA YEYE KUTAJWA KUWA NI MMILIKI WA KAMPUNI YA KIJAMBAZI YA DOWANS.

LAKINI KWA VILE KIKWETE-NA DOLA YAKE ANAYOJIVUNIA KUWADHIBITI WANAOMTAKA AWAJIBIKE- AMEINGILIA JUKUMU LA MWENYEZI MUNGU KWA KUKATISHA UHAI WA WATANZANIA WASIO NA HATIA HUKO ARUSHA (HATUWEZI KUJUA KWA HAKIKA NI WANGAPI WAMEUAWA KWA VILE WATOA TAARIFA NI POLISI HAOHAO WALIOUA) BASI AMIN NAWAAMBIA MUNGU MTOA HAKI YA KWELI ATATENDA HAKI.HAKUNA MAHAKAMA YA TANZANIA INAYOWEZA KUMHUKUMU KIKWETE AU SAID MWEMA LAKINI TAYARI MAHAKAMA YA UMMA (COURT OF PUBLIC OPINION) IMESHATOA HUKUMU,NA TUNACHUSUBIRI NI HUKUMU KUBWA ZAIDI KUTOKA KWA MUUMBA WETU (MAANA KIKWETE KALEWA MADARAKA MPAKA KUINGILIA KAZI ZA MUNGU ALIYEMUUMBA).

KWA WAZALENDO WALIOUAWA-"KOSA" LAO LIKIWA KUTUMIA HAKI YAO YA KIKATIBA KUANDAMANA KWA AMANI-DAMU YENU HAIJAMWAGIKA BURE.KIKWETE NA WAPAMBE WAKE WATAJITAHIDI KUWAPACHIKA KILA MAJINA ILI KUHALALISHA KUWA MLISTAHILI KUUAWA.HATUWEZI KUMZUWIA KWA SASA.LAKINI KAMA DOLA ZA KIKOMUNISTI ZA ULAYA YA MASHARIKI ZILISAMBARATIKA LICHA YA MATUMIZI MAKUBWA YA NGUVU ZA DOLA,BASI IPO SIKU UBABE,UNYAMA,UUAJI NA USHENZI WA CCM UTAFIKA KIKOMO.

TUNAKUOMBA MUNGU MWENYE HURUMA NA UPENDO UZIREHEMU ROHO ZA MASHUJAA WETU WALIONYANG'ANYWA UHAI NA SERIKALI YA KIKWETE,NA TUNAKUOMBA UTOE ADHABU KALI KWA WAHUSIKA,HUSUSAN RAIS JAKAYA KIKWETE NA VYOMBO VYAKE VYA DOLA.KWA MUNGU YOTE YANAWEZEKANA. 

6 Jan 2011

10 wauwawa kwenye ghasia mjini Arusha

Dr Wilbroad Slaa naye pia amekamatwa
Watu wasiopungua kumi wameripotiwa kuuwawa na wengine wengi kujeruhiwa katika mji wa Arusha Tanzania, kwenye makabiliano baina ya Polisi na wafuasi wa chama cha upinzani cha CHADEMA.

Ghasia zilianza baada ya Polisi kumkamata mwenyekiti wa kitaifa wa chama hicho Freeman Mbowe na mbunge wa Arusha mjini Godbless Jonathan Lema, wakiwa wanaelekea kuhutubia mkutano wa kisiasa.

Baadaye polisi pia walimkamata aliyekuwa mgombea wa chama hicho cha CHADEMA kwenye uchaguzi wa Urais uliofanyika mwezi Oktoba Dr Wilbroad Slaa.

Taarifa zinasema biashara kadhaa zilichomwa moto kwenye vurugu hizo.

Kwa mujibu wa waandishi wa habari mjini Arusha, Polisi walikuwa wamewakataza viongozi wa CHADEMA na wafuasi wao kufanya maandamanao kabla ya mkutano wa kisiasa wa Jumatano, lakini mamia ya wafuasi wa chama hicho wakawafuata viongozi hao walipokuwa wanaelekea eneo la mkutano.

Bwana Slaa amenukuliwa akisema maandamano hayo yalikuwa ya kupinga ufisadi katika serikali mpya ya Rais Jakaya Kikwete.

Polisi walifyatua risasi hewani mara kadhaa kutoa tahadhari kwa maelfu ya wafuasi waliokwenda kutaka viongozi wao waachiwe huru, na baadaye wakafyatua gesi ya kutoa machozi ili kuwatawanya.

Walioshuhudia wanasema Polisi waliendelea kufyatua risasi mchana kutwa, huku wafuasi wa CHADEMA wakiendelea kukabiliana na askari Polisi katika maeneo mbali mbali ya mji wa Arusha.

Kwenye mkutano huo wa kisiasa, Dr Slaa aliwataka Polisi kumwachilia huru Bwana Mbowe na wengine, na pia akamtaka Rais Kikwete kujiuzulu.

Hadi kufikia Jumatano jioni hakuna taarifa iliyokuwa imetolewa na serikali kuhusu mzozo huo.

Kumekuwa na mvutano wa kisiasa nchini Tanzania tangu kumalizika kwa uchaguzi mkuu wa Urais ambao vyama vya upinzani vinadai ulikuwa na udanganyifu.

Kufuatia uchaguzi huo shinikizo zinaendelea za kutaka Tanzania iwe na katiba mpya tofauti na iliyopo sasa, ambayo hairuhusu matokeo ya uchaguzi wa urais kupingwa mahakamani yanapotangazwa na tume ya uchaguzi.

CHANZO: BBC Swahili

5 Jan 2011


Kwa niaba ya wasomaji wapendwa wa blogu hii,na kwa niaba ya familia ya Chahali (na vijimatawi vyake),naomba kumtakia heri ya siku ya kuzaliwa rafiki yangu wa karibu na bloga mahiri Haki Ngowi.Licha ya urafiki na ushirikiano wetu kwenye fani ya kublogu,Haki ni mdau mwenzangu kwenye michakato flani (partner-in-crime).

HAPPY BIRTHDAY MKURUGENZI

Picha Hii Inatoa Maelezo Alfu Kidogo.Ukiangalia kwa Makini Utamwona Rostam Kama Kalizimishwa Kuinua Mkono,huku Kikwete Akiwa as if Anampigia Debe Bosi Wake...na Tabasamu Juu!Lol,Ama Kweli Rais Tunaye,Si Mchezo

Dk. Slaa: Kikwete ajiuzulu
• Asisitiza anahusika na Dowans, aahidi kutoboa siri
na Janet Josiah

KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Wilibrod Slaa, sasa amekuja na hoja mpya ya kumtaka Rais Jakaya Kikwete ajiuzulu kutokana na kuhusika moja kwa moja na sakata la Dowans iliyorithi mikoba ya Richmond.

Dk. Slaa ametoa kauli hiyo nzito jana katika mahojiano maalumu na Tanzania Daima Jumatano, ikiwa ni siku moja baada ya Ikulu kutoa taarifa ya kejeli na vijembe vya mitaani dhidi yake kuhusu sakata hilo.

Akizungumza kwa utulivu na umakini mkubwa, Dk. Slaa alisema Rais Kikwete alipaswa kujiuzulu kabla ya aliyekuwa Waziri Mkuu na swahiba wake mkubwa, Edward Lowasa, kuchukua hatua hiyo Februari 7, mwaka 2008, mjini Dodoma.

Yaani Kikwete Mpaka Kaikamata Mic Kuhakikisha Kuwa Debe Analompigia Swahiba Wake ni La Nguvu Kweli Kweli!Kama Alivyowahi Kusema Lowassa,Wawili Hawa Hawakufahamiana Mtaani.Wametoka Mbali.BIRDS OF A FEATHER..
Mawaziri wengine waliojiuzulu kutokana na sakata la Richmond lililozua mjadala mkali nchini ni pamoja na aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini wakati huo, Nazir Karamagi na Ibrahim Msabaha ambaye alikuwa waziri wa wizara hiyo kabla ya kuhamishiwa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki (EAC).

Akitoa ufafanuzi wa taarifa ya Ikulu iliyotolewa juzi na Kurugenzi ya Mawasiliano, Dk. Slaa alisema mkuu huyo wa nchi hawezi kukwepa kuhusishwa na sakata la Dowans, kwani alilijua hata kabla mitambo yake haijaingizwa nchini.

"Nataka niwatoe Watanzania wasiwasi kwamba ingawa kurugenzi ya mawasiliano imetoa taarifa ya kumsafisha Rais Kikwete na kunikashifu mimi kwa lugha ya mtaani, nawaambia alipaswa kujiuzulu kabla na anatakiwa ajiuzulu sasa, kwani anahusika moja kwa moja na uingiaji wa mkataba wa Kampuni ya Richmond na baadaye na Dowans" alisema Dk. Slaa.

Alimtaka Rais Kikwete kutambua kuwa hawezi kukaa kimya kwa kisingizio cha kuhatarisha amani na utulivu wakati wananchi wanaibiwa mabilioni ya fedha na mafisadi wachache kupitia kampuni feki ya Dowans.

Akirejea historia ya vita dhidi ya ufisadi aliyoiasisi bungeni, Dk. Slaa aliwataka wananchi wakumbuke kuwa taifa lilipokumbwa na tatizo la umeme kabla ya mitambo ya Richmond kuingia nchini, Rais Kikwete alikwenda Marekani kwa ziara ya kikazi.

Alisema aliporejea nchini, alizungumza na waandishi wa habari kuhusu tatizo hilo na kuahidi kuwa serikali yake inalifanyia kazi na siku chache baadaye, rafiki yake wa karibu, Rostam Azizi, Mbunge wa Igunga (CCM), naye alikwenda Marekani.

"Rostam aliporejea kutoka Marekani baada ya siku chache tukaanza kusikia mitambo ya kuzalisha umeme wa dharura kutoka Kampuni ya Richmond inatarajiwa kuwasili. Kweli ilitua nchini katika Uwanja wa Mwalimu Nyerere na shughuli nyingine zilifungwa uwanjani hapo kupisha ushushaji wa mitambo ya Richmond" alisema Dk. Slaa.

Kwanini Rostam Asiwe na Furaha?Kuendesha Nchi ya Watu Takriban Milioni 50 kwa Kutumia Remote Control si Jambo Dogo Ati!

Huku akisisitiza kuwa ana ushahidi wa anachokisema, Dk. Slaa alisema hata baada ya Richmond kushindwa kuzalisha umeme na kusababisha mawaziri kujiuzulu, serikali ya Kikwete iliamua kuingia mkataba na Dowans iliyorithi shughuli za Richmond na hatua hiyo Rais Kikwete pia aliijua.

"Dowans nayo ikashindwa kuzalisha umeme, mwisho Bunge katika moja ya maazimio yake liliridhia uamuzi wa kuvunja mkataba huo, lakini leo Serikali inadaiwa fidia ya sh bilioni 185, je, Rais Kikwete anaweza kukwepa kwamba hana mkono wake hapo?" alihoji.

Kutokana na hayo, Dk. Slaa alimtaka Rais Kikwete amtaje mmiliki halali wa Dowans ili kuwatoa kiu Watanzania wanaohitaji kumjua.

"Sitaacha kuzungumzia masuala yanayowagusa Watanzania na mali, hasa katika kipindi hiki ambacho Watanzania wanataka kuibiwa fedha zao, wakati wa kukaa kimya umekwisha" alisema Dk. Slaa.

Alisema hashangazwi na kejeli za Ikulu na kuwataka Watanzania kukumbuka alipoanza kuwalipua mafisadi, Rais Kikwete aliwahi kutamka kwamba kelele za mlango haziwezi kumnyima mwenye nyumba usingizi na kamwe kelele za chura hazimzuii ng ombe kunywa maji.

Kaaazi Kweli Kweli
"Lakini baada ya sisi kuamua kupambana na Richmond, Rais Kikwete alikiri linamnyima usingizi na hili la Dowans litamnyima usingizi zaidi katika kipindi hiki cha mwisho cha uongozi wake" alisema Dk. Slaa.

Ili kumaliza kelele za Dowans, Dk. Slaa alimtaka Rais Kikwete kumtaja mmiliki wake ambaye anataka kuwaibia Watanzania mabilioni ya fedha.


 
Wakati Dk. Slaa akimkaba koo Rais Kikwete, mjadala wa Dowans hivi sasa umewavuruga hata viongozi wa serikali tangu ilipoamriwa ilipwe sh bilioni 185.

Aliyekuwa Spika wa Bunge lililopita, Samuel Sitta, hivi karibuni alikaririwa akiitaka serikali iache kuilipa Dowans kwa madai kuwa ni mradi wa mafisadi watatu.

Kauli hiyo ilipingwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, ambaye alisema kuwa suala la malipo ya Dowans lipo kisheria na ikithibitika serikali haiwezi kukata rufaa, italazimika kulipa mabilioni hayo.

Juzi Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu imeelezea kukerwa kwake na hatua ya Dk. Slaa kumtaja Rais Kikwete kuwa alihusika katika uzembe uliosababisha taifa kutakiwa kuilipa Kampuni ya Dowans sh bilioni 185 kama fidia.

Taarifa hiyo kali ya Ikulu iliyobeba ujumbe wenye maneno ya kebehi na ya mitaani ya kumwita Dk. Slaa mtu aliyechanganyikiwa na mzabinazabina ilisainiwa na Salvatory Rweyemamu, ambaye kabla ya kwenda Ikulu alikuwa mmoja wa wahariri watendaji, aliyekuwa akiheshimika kwa kutumia lugha fasaha na ya staha.

Rweyemamu katika taarifa yake hiyo iliyoonyesha waziwazi kuandikwa na mtu mwenye hasira, chuki na dharau ama kwa Dk. Slaa, CHADEMA na Tanzania Daima, alikwenda mbali na kumwita kiongozi huyo wa kisiasa kuwa ni mtu hatari.

Katika mahojiano maalumu na gazeti la Tanzania Daima Jumapili, mwishoni mwa wiki, Dk. Slaa alikaririwa akisema chanzo cha suala la Dowans kutakiwa kulipwa fidia limetokana na uzembe wa serikali na Rais Kikwete mwenyewe anahusika kuileta Kampuni ya Richmond ambayo baada ya kuonekana ya kitapeli iliamua kurithisha kazi zake kwa Dowans.

VYANZO: Habari kwa Mujibu wa Tanzania Daima.Picha Kutoka Vyanzo Mbalimbali Mtandaoni.


Lowassa awaonya vigogo wanaojali matumbo yao

na Violet Tillya, Arusha

WAZIRI Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, ametoa wito kwa wabunge na madiwani waliochaguliwa katika uchaguzi mkuu uliopita kuhakikisha wanafanya kila liwezekanalo kubadilisha hali ya maisha ya wananchi wao kiuchumi.
Kadhalika amewataka viongozi hao kuweka kipaumbele katika kujali matumbo ya wapigakura wao ikiwa ni pamoja na kuweka utaratibu mzuri wa kuwakopesha ili waweze kuanzisha miradi ya kujikwamua kiuchumi kutokana na ugumu wa maisha unaowakabili wananchi wengi hapa nchini.

Lowassa aliyasema hayo mwishoni mwa wiki katika kijiji cha Manyire, Kata ya Mlangarini, wilayani Arumeru alipokuwa akizungumza katika sherehe za kuwapongeza na kuwashukuru wananchi wa kata hiyo kwa kumchagua diwani wao Mathias Manga (CCM).

"Wakati umefika kwa viongozi katika maeneo mbalimbali hapa nchini kubadilika na kuacha tabia na mazoea ya kujinufaisha wao wenyewe na familia na jamaa zao na kuhakikisha kuwa wanajikita zaidi kuwatumikia wananchi hususan kujali wanakula nini" alisema Lowassa.

Pia alitumia fursa hiyo kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa uamuzi wake wa kukubali mabadiliko ya Katiba na kutoa wito kwa wananchi kuhakikisha kuwa wakati ukifika wajitokeze kwa wingi kutoa maoni yao.


MBONA MAMBO!YAANI MPAKA KUFIKIA 2015 TUTASIKIA MENGI


Sijui ni ulevi wa madaraka,au ulevi wa kilevi,lakini kauli za baadhi ya watendaji ni za kihuni,usizorarajia kabisa kuzisikia kutoka kwa watu wenye nyadhifa muhimu kwa Taifa.

Nadhani wengi wetu bado tunakumbuka taarifa iliyotolewa na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa,Jack Zoka (pichani chini),ambapo ilikuwa na "kauli za mtaani" kinyume na wadhifa wake nyeti katika taasisi hiyo na Taifa kwa ujumla.

Baadaye tukapewa dozi ya kauli zilizojaa ngebe na kichwa ngumu kutoka kwa Frederick Werema,mtu aliyewahi kushika wadhifa wa Jaji wa Mahakama Kuu,na kwa sasa ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali.Mtu huyu ni kama ana "bifu" na jamii anayopaswa kuitumikia.Ukisikia kauli zake kuhusu suala la Katiba na ishu ya Dowans,utabaki mdomo wazi kama sio kufura kwa hasira.

Kikwete Akimkabidhi Werema "RUNGU" linalompa jeuri ya kusema ovyo

Kana kwamba kuna mashindano ya kauli za ovyo ovyo,Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Ikulu,Salva Rweyemamu,nae hajataka kuachwa nyuma.Japo ana rekodi nzuri ya kusema ovyo,safari hii nadhani amevuka mpaka.Anyway,hebu soma taarifa yake ifuatayo:

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUTOKA KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS, IKULU.


KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Dkt. Wilboard Slaa, leo, Jumapili, Januari 2, 2011, amekaririwa na Gazeti la Tanzania Daima, linalomikiwa na chama chake hicho, akidai kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ni mmoja wa wamiliki wa Kampuni ya Kuzalisha Umeme ya Dowans.

Huu ni uongo wa mchana, ni uzushi wa karne na propaganda ya hatari. Kwa hakika na kwa namna isiyoweza kuelezeka kwa ufasaha, tumeshtushwa sana na kauli hii ya Dkt. Slaa na hatutaki kuamini kabisa wala kukubali kuwa ni kweli kauli hii imetolewa na mtu ambaye majuzi tu alikuwa akiwania kuwa kiongozi wa juu wa taifa letu, yaani Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Na kama kweli Dkt. Slaa ametoa kauli hii na kusema maneno ya namna hii basi sasa Watanzania wanayo kila sababu na haki ya kuamini kuliko wakati mwingine wowote kuwa mzee huyu sasa amechanganyikiwa na ni mtu wa hatari sana kwa utulivu wa nchi hii. Kwa nini?

Sababu ni rahisi sana. Mheshimiwa Rais Kikwete siyo mmiliki wa Kampuni ya Kuzalisha Umeme ya Dowans. Hakupata kuwa mmiliki, siyo mmiliki na wala hatakuwa, hata siku moja, mmiliki wa Kampuni hii.

Kama Dkt. Slaa anataka kweli kujua wamiliki wa Kampuni ya Dowans, basi atafute ukweli huo na aachae tabia ya kutapatapa na udhabinadhabina yenye lengo la kuwapaka watu watope. Tabia ya kuwasingizia na kusema uongo kuhusu viongozi wa taifa letu ni tabia ya hatari.

Mheshimiwa Rais Kikwete hahusiki na Kampuni ya Dowans wala na kampuni nyingine yoyote ya kibiashara. Yeye ni kiongozi wa juu kabisa wa siasa wa nchi yetu na siyo heshima wala haki kumhusisha na jambo la kutunga na kuzua na lisilokuwa la ukweli wowote.

Kiongozi huyo wa upinzani ametoa shutuma zake dhidi ya Rais Kikwete kufuatia Kampuni ya Dowans kulishitaki Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) katika Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Migogoro ya Kibiashara (ICC) na Mahakama hiyo ikaamua kuwa Dowans ilipwe kiasi cha sh bilioni 185.

Dkt. Slaa amezomoko na kumshutumu Rais Kikwete eti kwa sababu Mheshimiwa Rais hakuzungumzia suala hilo katika salamu zake za Mwaka Mpya kwa wananchi Ijumaa iliyopita.

Mwaka huu, Dkt Slaa aliwania urais wa Tanzania kupitia CHADEMA na akashindwa vibaya sana. Tokea wakati huo amekuwa mtu wa kutunga na kuzua stori za kila aina ya uongo na umbea kuwachanganya Watanzania kwa sababu ya kinyongo chake cha kushindwa.

Tunapenda kuwataka na kuwaomba Watanzania, kama ambavyo wamekuwa wanapuuza uongo na uzushi mwingine wa mara kwa mara wa Dkt. Slaa, waupuuze uzushi na uongo wa sasa kuhusu miliki ya Dowans. Ni sehemu ya tabia iliyoanza kuzoeleka sasa ya Mzee huyo kutapatapa kisiasa.

Imetolewa na Salva Rweyemamu – Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais - Ikulu

Unajua watu hawa wanapata wapi jeuri ya kusema ovyo?Well,ni huyo aliyewateua.Heshima ni mithili ya barabara ya kwenda na kurudi (two-way).Ukijiheshimu utaheshimiwa.Na pia,heshima kwa aliyekuteua inaweza kuonekana kwa namna unavyomwakilisha katika jamii.Wateuliwa wa Rais ni sawa na taswira ya Rais kwa jamii.Kauli za kihuni za wateuliwa hao zinaweza kutoa picha kuwa Rais kateua wahuni au wababaishaji.

KWA KIFUPI,NA PASIPO KUUMAUMA MANENO,KAULI ZA WATENDAJI HAO MUHIMU WA RAIS KIKWETE NI TASWIRA YA KIKWETE MWENYEWE NA UONGOZI WAKE.

3 Jan 2011



Summary Boeing executives, at times, are pressed by foreign government officials and airline executives to hire “agents” or other intermediaries to help deliver a sale. Typically, these agents ask for some kind of a commission to make introductions to officials running the competition. Boeing faced such a request in Tanzania in 2007, as it was bidding on a relatively small contract to modernize the Air Tanzania fleet. It was already concerned, as the bidding began, that AirBus had an inside track. Boeing officials refused to hire the agent and reported the request to the State Department. Air Tanzania was shut down by aviation safety authorities about a year after this exchange.


Date 2007-09-13 11:25:00


Source Embassy Dar Es Salaam

Classification CONFIDENTIAL

C O N F I D E N T I A L SECTION 01 OF 02 DAR ES SALAAM 001249

SIPDIS

SIPDIS

DEPT FOR AF/E RMEYERS, SHAMILTON

AF/EPS FOR THASTINGS, AF/EB

PASS TO DEPARTMENT OF COMMERCE FOR ITA ALSO PASS TO MCC FOR MKAVANAGH, GBREVNOV NAIROBI FOR FCS

E.O. 12958: DECL: 09/13/2017

TAGS: ETRD, ECON, PGOV, BEXP, TZ


SUBJECT: BOEING AND AIR TANZANIA: THE STRUGGLE TO ENSURE TRANSPARENCY AND A LEVEL PLAYING FIELD

REF: DAR ES SALAAM 1074

Classified By: Deputy Chief of Mission D. Purnell Delly for reasons 1.4 b and d.


SUMMARY

--------

1. (C) As Air Tanzania shops for new airplanes for its aging fleet, we remain troubled by separate press reports, quoting Air Tanzania leadership and most recently the Minister of Infrastructure, that a decision has been made in favor of Airbus. This decision would have been made without any serious negotiations with Boeing. We have actively engaged at the highest reaches of this government, and for the moment halted the rush to Airbus and opened a window that Boeing intends to exploit. Air Tanzania now seems to be seriously evaluating the leasing and sale options offered by Boeing.


But we do not believe we are out of the woods, in view of early efforts to pressure Boeing to hire an "agent," and subsequent rumors that China is tying aid to purchase of

Airbuses in order to give business to the joint manufacturing facility being built in China. Ambassador Green raised MCC, the importance of transparency to the investment climate, and a level playing field for Boeing in his presentation of credentials to President Kikwete on September 12. Earlier the DCM had called on the Infrastructure Minister and spoken with a close advisor to the President underscoring the same points. We will continue to press hard not only on behalf of Boeing, but the importance of transparency and a level playing field to the positive investment climate Kikwete is working to create.


END SUMMARY.


2. (SBU) Air Tanzania plans to replace its aging fleet with newer, more efficient aircraft, and has solicited proposals from Boeing and Airbus. In June 2007, Boeing submitted a request for advocacy through the Department of Commerce's International Trade Administration, and Ambassador Retzer, the DCM, and EconCouns met with Rob Faye, Regional Director of Sales for Boeing Commercial Airplanes, on several occasions.


Boeing's early dealings with top officials of the airline beginning in June suggested to Post that the company's fear of outside influence or corruption might be legitimate (reftel).


3. (C) Subsequent to meetings with Faye, the DCM raised the issue of Air Tanzania's dealings with Boeing and Airbus in conversations with a close advisor to President Jakaya Kikwete. The DCM specifically noted Air Tanzania Managing Director and CEO, David Mattaka's unusual "suggestion" that Faye should contact a wealthy South Asian hotelier, who subsequently suggested to Faye that he would need his services to open the right doors in government. Faye flatly refused, responding that Boeing does not use "agents" in Tanzania or elsewhere. (Comment: "Agents" and steep "commissions" have been at the heart of several corruption scandals here, including a BAE radar deal in which the GOT paid a 31 percent commission to a Tanzanian agent, much of which ended up in Swiss bank accounts, according to a UK Parliamentary investigation. Despite the fact that the UK shared this evidence with Tanzania's corruption board, no evident action has been taken. End Comment.) The presidential advisor later got back to the DCM, telling him that President Kikwete was "incensed" upon learning that senior Air Tanzania officials might be intending to profit personally from the deal.


4. (SBU) On August 9, Boeing's Faye met with Maua Daftari, Deputy Minister of Infrastructure, and Dr. Bartholomew Rufunjo, Director of Transport and Communications in the Ministry of Infrastructure (the Ministry that makes all financial decisions regarding Air Tanzania). Faye reported his meetings with both Daftari and Rufunjo were promising.


Both officials mentioned more than once the importance of a fair and level acquisition process for Air Tanzania's development. David Mattaka, CEO of Air Tanzania, went out of his way to tell Faye on August 10 that Air Tanzania did not use agents. Mattaka repeated this statement during a meeting between Faye and the Air Tanzania board of directors. Faye reported that it was apparent that there had been some communication with the Ministry, presumably from State House, to ensure there would be no "go-betweens" in Air Tanzania's dealings with Boeing. On the sidelines, Mattaka mentioned to Faye that he thought the pressure was originating with the U.S. Embassy.


DAR ES SAL 00001249 002 OF 002


5. (U) Ambassador Retzer forcefully raised the issue of combating corruption in his last public speech beforebdeparting Post on August 31. On September 2, forty-eight hours after Retzer departed country, the Tanzanian press reported for the second time that Air Tanzania was in the process of procuring eight Airbus planes, and extensively quoted Tanzanian Minister of Infrastructure, Andrew Chenge.

We did not view the timing of the second announcement -- on the heels of Retzer's departure and before Ambassador Green had arrived and been credentialed -- as a coincidence.


6. (C) On September 7, the DCM and EconOff met with Minister Chenge. The DCM began by raising President Kikwete's upcoming trip to the United States and his plan to take a large business delegation. Kikwete would be marketing Tanzania as a prime location to trade and invest. It was important, therefore, that a major U.S. corporation like Boeing compete on a level playing field with Airbus, so its message to the U.S. business community would echo Kikwete's message. The DCM said Boeing and the Embassy had been confused by recent press reports regarding Air Tanzania's acquisition of new aircraft, and asked Chenge to clarify the status of negotiations.


7. (C) Chenge said contrary to his purported statements to the Tanzanian press, no final decision had been made on whether Air Tanzania would acquire Airbus or Boeing airplanes. The first decision was what type of airplanes to buy, and Boeing was the obvious choice since Air Tanzania already owned and maintained several Boeing airplanes.


However, the issue of financing was also a primary concern due to a lack of government funding for the new aircraft. He stated that he could say "with certainty" that no decision has been made, but his Ministry was "very cautious on how to proceed because (they) don,t have the money." He said he understood Boeing could help open doors to financing possibilities, but "certain deadlines" needed to be met. The

DCM stressed that regardless of the outcome, the Embassy wants to see that Air Tanzania is engaged in fair and transparent negotiations. He pointed out that Tanzania would benefit from giving Boeing the chance to underbid Airbus.


8. (C) The DCM ended the meeting by mentioning the upcoming vote on the Millennium Challenge Corporation (MCC) Compact for Tanzania, and the importance of transparency to sustaining any Compact that eventually would be signed. On the way out, Chenge,s staffer told the DCM that he was aware that Chenge had "misspoken" and been "misquoted" in the press, and that his office had already received several calls for clarification. (Comment: We think one of the calls to Chenge's office may have come from State House. End Comment)


-------


9. (C) Although Air Tanzania is a small airline, looking to expand its fleet of two Boeing 737's to a fleet of about 10 planes, this deal has the potential to result in USD 537 million in sales for Boeing. Boeing is ready to offer Air Tanzania a number of capacity-building services to enable the airline to better serve the Tanzanian public. More broadly, if done right, the deal can reinforce the impression that Tanzania is a promising place to invest. Done wrongly, it can reinforce impressions that have been building here for

the past 18 months that this is a government without the political will to tackle senior-level corruption. To us, reinforcing the view that Tanzania is a positive place to invest is almost as important as ensuring one of America's premier private sector "champions" is accorded the transparency and level playing field it is due. We remain concerned, however, in part due to rumors that the Chinese have tied aid to buying Airbus. We will continue to monitor this case closely, intervening decisively with the government when necessary.


Destination

VZCZCXRO6390

PP RUEHDBU RUEHDT RUEHKN RUEHLMC RUEHMJ RUEHMR RUEHPB

DE RUEHDR #1249/01 2561125

ZNY CCCCC ZZH

P 131125Z SEP 07

FM AMEMBASSY DAR ES SALAAM

TO RUEHC/SECSTATE WASHDC PRIORITY 6752

INFO RUCNCLM/MCC CANDIDATE COUNTRY COLLECTIVE PRIORITY

RUEHNR/AMEMBASSY NAIROBI PRIORITY 0780



RUCPDOC/DEPT OF COMMERCE WASHDC PRIORITY
---------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
SOURCE: New York Times



Smiling happily as she teaches medicine in Africa, this is the young doctor who was ‘betrayed’ by Britain’s healthcare postcode lottery.
Becky Smith, 30, was told she could be dead within 18 months after her breast cancer was missed four times and health chiefs refused to fund a breakthrough treatment.
The Daily Mail told in May how her local NHS trust had denied funding for the £23,000 treatment, despite it being freely available from 40 other trusts across Britain.

Dr Smith won a funding U-turn after the Mail highlighted her case, and has now had the drug therapy, which she hopes will help to prolong her life. Together with months of chemotherapy and other treatment, it has stabilised her condition and left her well enough to realise her dream of teaching her skills to doctors in Africa.

Dr Smith flew to Tanzania within days of finishing her latest round of chemotherapy, and has just completed a two-week stint of voluntary work at a hospital there.

She said: ‘I am so grateful that I have had this chance – I have no symptoms at the moment, I’m not ill and I don’t feel ill.
‘For the first time in months, I don’t feel like a cancer patient. It goes to show what is possible, even with a terminal diagnosis.
‘But it’s only possible if you’re given the treatment you need to give you a fighting chance.’

Dr Smith found a pea-sized lump in her left breast in April 2008, when she was 28 and working at High Wycombe Hospital in Buckinghamshire.

She went to her GP but was told to wait a month because she was considered too young to have breast cancer and it was more likely to be a cyst.

She returned to her doctor in June and was referred to a specialist cancer clinic at the John Radcliffe Hospital in Oxford. She was given an ultrasound scan and examination but was told the lump was a benign cyst which posed no risk to her health.
But by December 2008 the lump had grown to the size of a golf ball and she returned to see a third GP at her local practice. Again, her fears were dismissed.

Dr Smith, a urologist, then asked a cancer care nurse at her own hospital for help. A scan revealed three lumps in her breast and she was diagnosed with cancer the day after her 29th birthday.

Worse still, further scans found it had spread to her liver and her spine, where it was inoperable.

She had a mastectomy to remove the breast cancer, and doctors believe she could live for ten to 20 years with the tumours in her spine, if they can treat her liver cancer. Specialists recommended she receive Selective Internal Radiation Therapy, but her local primary care trust in Ryde, on the Isle of Wight, refused to fund it.

It said there was not enough evidence that it was cost-effective, or that it would be successful.
Dr Smith was faced with having to cancel her wedding to childhood sweetheart Simon Morton to pay for the treatment, or allowing her retired parents to remortgage their house.

Within days of the Mail reporting her plight, generous readers had pledged more than £12,000 to help her. But she won an appeal against the funding decision, and completed her last round of treatment in November.

It is too early to know if it has successfully shrunk the tumours in her liver enough for them to be removed or destroyed, but preliminary scans have shown an improvement.

Meanwhile, Dr Smith married her fiance, a chartered engineer, in July and was able to carry out charity work on the Tanzanian island of Zanzibar, where average life expectancy is just 47.

Before her cancer diagnosis, she had been due to do a year’s voluntary work at the Makunduchi Hospital on the island, but was forced to cancel it while she had treatment.

Dr Smith said: ‘It’s been wonderful to be back in a hospital and working alongside doctors again.’

SOURCE: Daily Mail

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.