22 Jan 2011


Imagine wale vibaka wanaowanyima raha pale mtaani wasingekuwepo!

Imagine baba au mama mwenye nyumba angeheshimu mkataba mlowekeana kuhusu jengo unalopanga kwake,na kutambua kuwa kodi unayolipa ina-cover uhuru na haki zako kama mpangaji!

Imagine waandaaji wa filamu za kibongo wangezingatia zaidi uwezo na vipaji vya waigizaji badala ya maumbile au "jina kubwa" (kama sio rushwa za ngono)!

Imagine vituo vya redio vinavyojigamba kuwa vinawalenga vijana vingeachana na watangazaji vilaza wanaojifanya kuifahamu siasa (na hivyo kujipachika wadhifa wa political analysts/commentators) japo wanatambua uwezo wao ni zero,zilch,nada,sifuri,kaput!

Imagine ajira na promosheni makazini vingezingatia ujuzi na uwezo badala ya kujuana plus undugunazesheni (not forgetting rushwa za ngono)!

Imagine baadhi ya wachunga kondoo wa Bwana wangetambua kuwa wanamkasirisha Muumba kwa "kugeuza kondoo wake kuwa vitoweo vya bure" japo wakiwa madhabahuni wanakemea kwa nguvu zote ubanjuaji wa Amri ya Sita!

Imagine na sie mabloga tungejifunza kutoka kwa kampeni ya Rais Obama na,kwa hivi karibuni kabisa,Tunisia,na kuwekeza nguvu zetu katika matumizi ya social media ku-address matatizo yanayoikabili nchi badala ya hali ilivyo sasa ambapo baadhi yetu wako bize zaidi kujikomba kama sio kuripoti tu matukio (na hapa tunaweka kando wenzetu ambao wako bize zaidi na "flani kafanya hili au lile" badala ya nini kifanyike kuikomboa jamii yetu)!

Imagine vyombo vya habari vinavyoendeshwa kwa fedha za walipa kodi vingetambua kuwa kazi ya kupigia debe CCM inapaswa kuachwa kwa Uhuru,Mzalendo na Redio Uhuru pekee!

Imagine Kamati Kuu ya CCM ingekuwa na wazalendo wa kutambua kuwa hata kichaa akiporwa hawezi kumlipa aliyempora,sembuse wao watu wenye akili timamu na wenye dhamana ya kutuongoza lakini wanaendekeza ufisadi na kuhalalisha malipo kwa majambazi wa Dowans!

Imagine....Imagine...Imagine...Too much imagination

And imagine,fani ya siasa Tanzania ingeachwa kwa wenye wito,uwezo na uzalendo badala ya hali ilivyo sasa ambapo kila Tom,Dick and Harry anayeweza kununua wapiga kura anaweza kulala jambazi akaamka mbunge,kama sio waziri au mkurugenzi wa hovyo hovyo!

Na imagine ulimwengu wa siasa za Tanzania ungekuwaje laiti baadhi ya viumbe wangetambua umuhimu wa co-ordinationa kati ya ubongo na mdomo kabla ya kuropoka lolote hadharani.Kwa hakika dunia ingekuwa mahala bora sana pa kuishi laiti baadhi ya wanasiasa wasemaovyo,vichwa maji,vichwa makabati matupu,nk wasingepewa fursa ya kuongoza hata kundi la mifugo,let alone kuongoza wananchi.

Yes,dunia ingekuwa mahala bora kabisa laiti watu kama Yusuph Makamba na Tambwe Hiza wasingeruhusiwa kutamka lolote hadharani hadi itakapothibitika kuwa watakachoongea hakitazidi kuisogeza Tanzania yetu kuelekea kwenye mshikemshike kama wa huko Ivory Coast, au mahala kwingine kwenye mapigano ya wenyewe kwa wenyewe.

Talking of Tambwe Hiza,nimeshindwa kujizuwia kupaliwa na kicheko baada ya kukutana na habari ifuatayo:

Tambwe Hiza alazwa

na Betty Kangonga

SIKU moja baada ya kumshambulia Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, kaimu katibu mkuu wa kitengo cha propaganda wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Richard Hiza, amelazwa katika Hospitali ya Regency akisumbuliwa na maradhi ya pumu.

Akizungumza na Tanzania Daima jana kwa njia ya simu mmoja wa ndugu wa karibu ambaye hakupenda jina lake litajwe kwa kuwa si msemaji wa familia, alisema Hiza alilazwa kwa mara ya kwanza katika Hospitali ya Mbagala Kizuiani akisumbuliwa na maradhi hayo.

Alisema Hiza alizidiwa usiku wa juzi muda mfupi baada ya kurejea kutoka kazini na kukimbizwa katika hospitali hiyo kwa ajili ya kupatiwa matibabu.

Alisema baada ya vipimo vya kiuchunguzi Hiza alibainika kusumbuliwa pia na shinikizo la damu hivyo kulazimu kumhamishia Hospitali ya Regency kwa matibabu zaidi.

“Kwa kweli hali yake haikuwa nzuri na alikuwa hawezi kuzungumza; maana tatizo lake limemuanza ghafla sana ingawa ana tatizo la pumu kwa muda mrefu lakini tumeshangaa hali yake kuwa hivi,” alisema.

Hiza ameugua ikiwa ni siku moja tu baada ya kukaririwa na gazeti moja la kila siku siyo Tanzania Daima akidai Dk. Slaa ana wazimu, amebakiza kuvua nguo na kwamba ni mfa maji anayetapatapa.

Hiza alitoa kauli hiyo akidai kwamba Dk. Slaa ana hofu ya kufungwa kwani serikali ya CCM imepania kufanya hivyo ili kumnyamazisha.

Akitumia lugha ya matusi, Hiza alinukuliwa akisema, “Ninachoweza kusema kwa sasa ni kwamba kiongozi huyo amepandwa na wazimu, alichobakiza ni kuvua nguo tu…amechanganyikiwa na ndiyo maana anatapatapa kutafuta lolote la kusema.

CHANZO: Tanzania Daima
Lol!Mchimba kisima katumbukia mwenyewe kisimani.Jitu zima ovyooo!Linaropoka tu,na kujipachika udaktari wa magonjwa akili to an extent of kum-diagnose Dkt Slaa na maradhi ya akili,kumbe lenyewe lina matatizo makubwa ya afya.Msomaji mpendwa,huhitaji hata dakika moja ya kozi ya utabibu kumaizi kuwa kichaa cha kuzuzshiwa hakifui dafu kwa gonjwa la hatari kama PUMU na SHINIKIZO LA DAMU.

Naomba nisiwe mnafiki kumwombea Tambwe apate nafuu.Ndio,Biblia inatuasa kuwapenda maadui zetu lakini busara katika jamii zinatuasa pia kuwa ADUI YAKO MWOMBEE NJAA (njaa hapo symbolises mambo mabaya kama hayo yalomkuta Msema Ovyo Tambwe Hiza).

Kufungika kwa mdomo mmoja mchafu kunaifanya dunia kuwa mahala bora kabisa kuishi.Sio siri kwamba laiti maradhi yanayomkabili Tambwe yakipelekea kupunguza,kama sio kumaliza,tatizo lake la kuutumia ubongo wake kama matope,kisha kuunyima ubongo huo ushirikiano na mdomo wake,and therefore kupelekea uropokaji usiosahili hata kwenye vilabu vya gongo,siasa za Tanzania zinaweza kuchukua sura mpya.Yaani,siasa minus mbwatukaji mmoja ambaye kauli zake za ovyo ovyo ni maarufu zaidi kuliko madaraka yake.

Ndio maana nimeandika hapo juu kuwa MUNGU SI TAMBWE HIZA.Yeye anajifanya kumsemea ovyo Dokta Slaa,na kumhukumu kuwa ana kichaa,ilhali yeye Tambwe ndiye mwenye matatizo makubwa ya kiafya yanayoweza kabisa kuwa na uhusiano na tabia yake ya kuropokaropoka.

IMAGINE SIASA ZA TANZANIA MINUS UROPOKAJI WA TAMBWE HIZZA!SURELY,THAT WOULD MAKE THE WORLD SUCH A WONDERFUL PLACE TO LIVE...Lol!

21 Jan 2011





Tamko La Umoja wa Vijana Mafisadi

ONLY REASON SOME BASTARDS ARE STILL ALIVE IS BECAUSE SHOOTING THEM IS ILLEGAL.SERIOUSLY.

18 Jan 2011









SAKATA LA DOWANS: Sitta afungwa mdomo

BARAZA LA MAWAZIRI CHINI YA JK LAMSHAMBULIA YEYE NA MWAKYEMBE

na Mwandishi wetu

RAIS Jakaya Kikwete amemfunga mdomo Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Samuel Sitta aliyeingia katika mzozo na waziri mwenzake wa Nishati na Madini, William Ngeleja.

Mzozo huo uliibuka baada ya Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi (ICC), kuamua Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) iilipe Dowans fidia ya sh bilioni 94 kutokana na TANESCO kuvunja mkataba nayo.

Uamuzi wa kumziba mdomo Sitta, ulifikiwa jana katika kikao cha Baraza la Mawaziri, kilichofanyika Ikulu, jijini Dar es Salaam, chini ya Rais Kikwete, ambapo pamoja na mambo mengine, mjadala wa malipo ya Dowans ulitawala kikao hicho.

Mwingine aliyepigwa kufuli katika kikao hicho ni Naibu Waziri wa Miundombinu, Dk. Harrisson Mwakyembe, ambaye naye aliungana na Sitta kumpinga Ngeleja kuilipa Dowans.

Vyanzo vyetu vya habari vilisema Sitta na Mwakyembe walikuwa na wakati mgumu kutetea hoja ya kutaka serikali isiilipe Dowans na kwamba hata Rais alisema hafurahishwi na hukumu ya malipo hayo.

“Kikao bado kinaendelea, lakini Sitta na Mwakyembe walibanwa sana na mawaziri na hata Bwana mkubwa (Rais) aliungana na mawaziri wengine kuwalaumu kwa kupeleka mjadala huo hadharani,” kilisema chanzo chetu cha habari.

Kwa mujibu wa habari hizo, kuanzia sasa Sitta na Dk. Mwakyembe, wamefungwa mdomo kuzungumzia suala la malipo ya Dowans hadharani na kwamba wanapaswa kuwa kitu kimoja kuhakikisha mipango ya serikali inatekelezwa kama ilivyopangwa.

Kabla ya kibano hicho jana, wiki iliyopita katika kikao cha kamati ndogo ya mawaziri uliibuka msuguano wa hoja kati ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Jaji Frederick Werema na Waziri Sitta.

Habari kutoka ndani ya kikao hicho ambacho kilifanyika chini ya uenyekiti wa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, zinaeleza kuwa Jaji Werema alieleza kusikitishwa na matamshi ya Sitta katika vyombo vya habari.

Taarifa kutoka ndani ya kikao hicho zimemkariri Werema akieleza kushangazwa na hatua ya Sitta kuwashambulia yeye na Ngeleja huku akijua kuwa walichokifanya na kuamua kilikuwa kinagusa moja kwa moja mamlaka yao ya kiwajibu na kimamlaka.

Jaji Werema amekaririwa akimweleza Waziri Sitta kwamba iwapo kweli alikuwa ana uchungu na suala la Dowans, basi wakati kesi ikiendelea alipaswa kuisaidia serikali katika kuwasilisha utetezi dhidi ya malalamiko 17 yaliyokuwa yamewasilishwa na kampuni hiyo.

Habari zinaeleza kwamba hatua ya Sitta ambaye alikuwa akitambua fika namna kesi hiyo ilivyokuwa ikiendelea kutochangia jambo lolote wakati shauri hilo likiwa ICC na badala yake kusubiri hadi serikali ishindwe ndipo aanze kutoa matamshi katika vyombo vya habari ilikuwa ni ya kuchochea hasira za wananchi dhidi ya viongozi pasipo sababu zozote.

Wakati Jaji Werema akimshushia lawama Sitta kwa muda usiopungua dakika 15, Waziri Mkuu Pinda alikuwa kimya muda wote.

Baada ya kumaliza hoja yake, Waziri Mkuu aliwataka wajumbe wa kamati hiyo ya mawaziri iliyokuwa ikijadili kuhusu Muswada wa Mabadiliko ya Sheria ya Manunuzi unaotarajiwa kuwasilishwa katika Bunge lijalo kuendelea na mjadala.

Awali kabla ya Werema kuzungumza, Sitta alichangia kuhusu muswada huo na akaeleza haja ya kuwekwa kwa masharti magumu zaidi ili kuzuia uwezekano wa makampuni ya kitapeli kujipenyeza nchini na kuigharimu serikali mamilioni ya fedha kauli ambayo ilionekana kumkera Werema.

Awali hofu ilitawala kwamba Sitta na Mwakyembe, wangeweza kupoteza nafasi zao za uwaziri kutokana na hatua yao ya kuibua mjadala dhidi ya mawaziri wenzao nje ya Baraza la Mawaziri kuhusu uamuzi wa serikali kukubali kuilipa Kampuni ya Dowans Holdings SA.

Mkanganyiko wa kauli ya Sitta na Mwakyembe, ulisababisha Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora), Mathias Chikawe, kutoa matamshi makali ya karipio kwa mawaziri hao wawili.

Ukali wa matamshi hayo ya Chikawe ambaye anadaiwa kupata baraka za Rais Kikwete, uliongezwa na tamko lake la kuwataka Sitta na Mwakyembe iwapo wanataka kuendeleza malumbano hayo nje ya utaratibu wa kawaida wa mawasiliano wa mawaziri, wajiondoe serikalini.

Chikawe amekaririwa akisema kitendo cha Sitta kumtuhumu Ngeleja kwamba alitangaza kulipwa kwa Dowans kabla suala hilo halijafikishwa katika Baraza la Mawaziri kinakwenda kinyume cha miiko ya uwaziri kinachomtaka kutotoa siri za baraza.

Kwa mujibu wa Chikawe, Waziri Ngeleja kwa mamlaka aliyonayo kama waziri mwenye dhamana na masuala ya nishati alikuwa na mamlaka ya kutoa tamko alilotoa baada ya kufanya mashauriano na wataalamu mbalimbali wa masuala ya sheria serikalini.

Chikawe alisema iwapo Sitta na Mwakyembe walikuwa hawajaridhishwa na uamuzi wa Waziri Ngeleja walikuwa na njia za kuwasilisha hoja zao pasipo kutumia vyombo vya habari.

Kwa upande wake, Mwakyembe ameingia matatani kutokana na kunukuliwa na gazeti la Uhuru linalomilikiwa na Chama cha Mapinduzi (CCM) akieleza kushangazwa na hukumu ya Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Migogoro ya Uwekezaji (ICC) iliyoipa ushindi Dowans dhidi ya serikali na kutakiwa kulipwa fidia ya shilingi bilioni 94.

ICC iliamua katika hukumu yake Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) iilipe Dowans fidia ya sh bilioni 94 kutokana na TANESCO kuvunja mkataba nayo.


HAIHITAJI UTAFITI KUBAINI KUWA KIKWETE SIO TU ANASAPOTI DOWANS ILIPWE MABILIONI KAMA ZAWADI KWA KAMPUNI HIYO KUFANIKISHA WIZI HUO MKUBWA WA FEDHA ZA UMMA,BALI PIA YEYE NDIYE ALIYERIDHIA MCHAKATO MZIMA KUANZIA ENZI ZA MAJAMBAZI WA RICHMOND HADI KWA MRITHI WAKE DOWANS.

KWA NAMNA MWENENDO WA MAMBO ULIVYO,WE ARE ALREADY SCREWED (NIKITUMIA SENTENSI YA KISWAHILI ITAKUWA MATUSI).DOWANS WATALIPWA KWA VILE MWENYE NCHI (YES,WAMEIBINAFSISHA TANZANIA NA KUWA KAMA MALI YAO BINAFSI).

LAKINI WAKATI KIKWETE ANAFANYA BIDII KUHAKIKISHA MABILIONI HAYO YANALIPWA KWA MASWAHIBA ZAKE,ASIJIFANYE HAONI KINACHOJIRI HUKO TUNISIA.NA KAMA WASHAURI WAKE WANAMDANGANYA KUWA WATANZANIA WA 2011 NI WALEWALE WA 2005 WAKATI ANAINGIA MADARAKANI BASI HAWAMTAKII MEMA.

ASITOKEE MPUUZI WA KUSEMA TUNAHAMASISHA VURUGU WAKATI WANATUFANYA WATANZANIA KAMA MAHAYAWANI.HAIWEZEKANI KABISA KUWALIPA WEZI NA MAJAMBAZI HATA KAMA TUNGEKUWA NA UTAJIRI WA KUPINDUKIA.

KIKWETE,YOU HAVE BEEN WARNED.JUST REMEMBER THAT ALTHOUGH YOUR SWAHIBAs DID ALL IT TOOK TO MAKE SURE YOU BECAME OUR PRESIDENT (SO THAT YOU WOULD REMAIN INDEBTED TO THEM THROUGHOUT YOUR TERMS OF LEADERSHIP), THEY CERTAINLY WONT BE ABLE TO STOP A TUNISIA-LIKE PEOPLE'S POWER MOVEMENT NOR WOULD THEY CARE ABOUT YOU WHEN THE MASSES SAY "NO MORE SCREWING,ENOUGH IS ENOUGH"


Kilichonisukuma kuandika post hii ni habari niliyoiona kwenye runinga katika kipindi cha Anderson Cooper 360 (katika kituo cha CNN) kwamba mwanabodi wa taasisi moja ya elimu huko Marekani amekuwa akimshambulia mwanaharakati Dkt Martin Luther Jr,ambaye jana ilikuwa siku ya kumbukumbu yake (Martin Luther King Jr Day).

Mashambulizi hayo dhidi ya Dkt King yalijumuisha madai kama "mwanaharakati huyo hakuwa Dokta"-ikimaanisha si sahihi kuweka kitangulizi hicho kabla ya jina lake,na "alikuwa mkomunisti"- na kwa wahafidhina nchini Marekani,ukomunisti unachukuliwa kama Unazi.

Tukio hilo ni mwendelezo tu wa mashambulizi dhidi ya Dkt King hususan kutoka kwa wanaokumbatia hisia za ubaguzi wa rangi.Lakini kama kuna mtu aliyekuwa "obsessed" zaidi na jitihada za kumuumbua Dkt King basi si mwingine bali Mkrugunzi wa zamani wa Shirika la Upelelezi la Marekani (FBI) J.Edgar Hoover.Inaelezwa kuwa shushushu huyo alijitahidi kadri alivyoweza kufanikisha azma yake hiyo muflis,ikiwa ni pamoja na kurekodi (bugging) maongezi ya Dk King anayetambulika kama chachu ya mapambano (ya amani) na mafanikio ya Wamarekani Weusi kukubalika katika nchi hiyo (kwa kiasi kikubwa).Hata mafanikio ya  Barack Obama,Mweusi wa kwanza kushika nafasi ya urais wa Marekani yanahusishwa kwa kiasi kikubwa na harakati na changamoto zilizoanzishwa na Dkt King.

Tanzania yetu ya leo inaweza kabisa kulinganishwa na hali ilivyokuwa katika Marekani ya enzi za akina Dkt King ambapo ubaguzi wa rangi ulikuwa umeshamiri vilivyo.Huko nyumbani,na hasa baada ya kifo cha Baba wa Taifa-aliyekuwa muumini mkubwa wa usawa wa binadamu-wengi wa wanasiasa wetu wamekuwa bize kutengeneza mgawanyiko katika jamii kati ya wenye nacho na wasio nacho,vigogo na walalahoi,na katika zama hizi za Kikwete,tumeshuhudia mgawanyiko mkubwa zaidi katika jamii; mafisadi dhidi ya wananchi wa kawaida,na hivi karibuni CCM,Serikali yake na vyombo vyake vya dola dhidi ya wananchi na wapinzani (hususan Chadema) na haki zao.

Lakini pengine la kutisha zaidi ni vuguvugu linalochochewa na CCM ya Kikwete na mafisadi anaowalea la kuwagawanya Watanzania kwa misingi ya imani zao za kidini.Kila mwenye macho na masikio ameona na kusikia kauli mbalimbali za msigishano kati ya viongozi wa CCM na baadhi ya viongozi wa Kanisa kwa upande mmoja,na kwa upande mwingine ni msuguano (unaoelekea kukua) wa kimtizamo kati ya baadhi ya viongozi wa Kanisa na baadhi ya viongozi wa dini ya Kiislam.

Kama ambavyo nimerejea kwenye posts na makala zangu kadhaa huko nyuma,suala hili tofauti za kidini kutumika kwa maslahi ya kisiasa linanigusa sana,kitaaluma kama mwanafunzi wa utafiti katika mahusiano ya siasa na dini,na kama raia wa Tanzania-nchi ambayo licha ya kuwa na viungo (recipes) vinavyoweza kupelekea mgogoro wa kijami kwa misingi ya kidini,angalau hali kwa ujumla imekuwa salama (kwa maana ya kutokuwepo vurugu za aina hiyo).

Inapofikia mahala vyombo vya habari vya umma,kama TBC1,Habari Leo na Daily News,vinatumika kusambaza ujumbe wa kuchochea mvurugano katika jamii badala ya kuhamasisha maelewano,ni dhahiri kuwa tunakoelekea si kwema.Vyombo hivi vya habari vinavyoendeshwa kwa fedha za walipakodi pasipo kujali itikadi zao za kisiasa vinaanza kuchukua mwelekeo wa gazeti la Kangura na vituo vya radio vya Radio Rwanda na Radio Télévision Libre des Mille Collines (RTLM) ambavyo vilichangia sana kuhamaisha propaganda za chuki dhidi ya Watutsi zilizopelekea mauaji ya kimari nchini Rwanda kati ya mwaka 1994-95.

                                                                                    



Hivi kama blogu binafsi  ya Ze Utamu ilipigwa kufuli kwa vile tu ilionyesha picha isiyofaa ya Rais Kikwete,kwanini basi vyombo hivyo vya habari vya umma vinaruhusiwa kuchochea chuki miongoni mwa Watanzania ambapo madhara yake ni makubwa zaidi ya namna picha za Ze Utamu zingeweza kumdhalilisha Kikwete?Hapa sio kama naitetea blogu hiyo bali ninachojaribu kupigia mstari ni ukweli kuwa amani ya Watanzania inayowekwa rehani na TBC1,Habari Leo na Daily News ina umuhimu na thamani kubwa pengine zaidi hadhi ya Kikwete pekee.Ikumbukwe kuwa wakati jitihada za Serikali kuitia kufuli Ze Utamu zilipelekea picha hizo kutoonekana tena,sumu inayomwagwa na vyombo hivyo vya habari vya umma ikishasambaa hakutakuwa na namna ya kuizuwia.

Nirejee kwa Dkt King na funzo linaloweza kusaidia katika harakati za mapambano dhidi ya udhalimu wa Kikwete na CCM yake inayoendeshwa kishkaji.Pamoja na jitihada na nguvu kubwa iliyotumika kumdhibiti,na hatimaye kuuawa,mbegu alizopanda mwanaharakati huyo zimefanikiwa kuzalisha watu kama Obama,Oprah,Condoleeza Rice,Collin Powell,nk ambao kwa hakika wasingeweza kujichomoza katika mfumo wa kibaguzi uliowabagua Weusi katika kila nyanja ya maisha nchini Marekani.

Kama ambavyo Dk King aliandamwa na FBI na J.Edgar Hoover ndivyo wazalendo kama Dkt Wilbroad Slaa walivyojikuta wakiandamwa na taasisi za serikali katika kila wanalofanya,huku baadhi ya waendaji wa taasisi hizo wakidiriki hata kuvunja "miiko" waliyojiwekea ili waweze kumshamshambulia Dkt Slaa (rejea kauli ya Naibu Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa, Jack Zoka).Na kama ambavyo wabaguzi wa rangi wanavyoendelea kubomoa misingi iliyowekwa na Dkt King,ndivyo Kikwete akisaidiwa na mafisadi anaowalea-plus vyombo vyao vya habari-wanavyofanya kila wawezalo kudhoofisha harakati za kuwakomboa Watanzania kutoka katika himaya ya ufisadi,ukiukwaji haki za binadamu na umasikini wa kupindukia.

Usihadaike na kauli za watu kama Lowassa wanajifanya kutahadharisha kuwa mjadala wa Katiba mpya usiwe chanzo cha kuhaarisha amani kwani yayumkinika kuamini kuwa wale wote wanaohusishwa na ufisadi wasingependelea kuona tunakuwa na Katiba mpya inayompa mamlaka mwananchi wa kawaida kuwa mwenye nchi halisi badala ya hali ilivyo sasa ambapo nchi yetu imekuwa kama kampuni binafsi ya mafisadi,wakiipelekesha watakavyo na sheria zikibaki sheria tu isipokuwa katika kukandamiza maandamano ya amani na kuminya haki za binadamu.


Licha ya kuuawa kwake,wengi wa Wamarekani Weusi sasa wanafaidi matunda ya harakati za Dkt Martin Luther King Jr.Vikwazo na upinzani wa kila hali dhidi ya harakati hizo hakukumvunja moyo Dkt King,na hata kifo chake hakiwazuia washirika na watangulizi wake kuendeleza harakati hizo za kudai usawa wa binadamu.Damu ya mashujaa iliyomwagika huko Arusha kutokana na unyama waliofanyiwa na polisi wa Kikwete na IGP Mwema isipotee bure bali iwe chemuchemu ya kudumu kuhakikisha kuwa hatimaye udhalimu na ufisadi wa CCM na serikali yake unakomeshwa completely.

Kama Dkt Martin Luther King Jr aliweza,na Nelson Mandela akaweza pia-bila kusahau kuwa nasi pia tuliweza kumwondoa mkoloni na kumfurumisha nduli Idi Amin-basi kwa hakika harakati hizi za sasa zinaweza pia kufanikisha ndoto na malengo yetu ya kuwa na Tanzania tunayostahili kuwa nayo,na sio hii ya sasa inayoendeshwa kwa remote control na mafisadi huku wakiwatuza majambazi wa Dowans kwa mabilioni na "kuwazawadia" waandamaji wa amani risasi za kuwaua na kuwajeruhi.



Jana niliona mahala flani kuwa nyota (star signs) zimebadilika.Sikujali.Lakini leo katika pitapita zangu mtandaoni,nimebaini kuwa sio tu kuwa nyota zimebadilika bali pia nyota yangu imekumbwa na mabadiliko.Nilizaliwa Desemba 9,hivyo nyota yangu ilikuwa Mshale au Sagittarius,kama inavyojulikana.Sasa baada ya kuongezeka alama nyingine ya nyota,nimejikuta nikiwa katika alama nyingine ya nyota,OPHIUCHUS.Grrrrr!!!!

Najua imani yangu ya dini inakemea mambo ya unajimu.Lakini,siku za nyuma nili-develop interest kwenye masuala ya nyota baada ya kuanzisha safu kwenye lililokuwa  gazeti maarufu la SANIFU,kabla sijahamishia safu hiyo kwenye gazeti la KASHESHE.Naamini kwa walikuwa wafuatiliaji wa magazeti ya "manyang'unyang'u" waakuwa wanakumbuka tangazo la Anko J Julius Nyaisanga akiwaasa wasomaji kutokosa safu ya USTAADH BONGE.Hiyo ilikuwa mika ya 1997-2000.

Naam,Ustaadh Bonge huyo ndiye mie,truly yours Evarist Chahali.Kuna waliokuwa wanaamini nyota hizo za "kizushi".Nakumbuka wakati huo ambapo nilikuwa mwanafunzi hapo Mlimani (UDSM) kuna baadhi ya watu walifikia hatua ya kuomba "msaada" wangu kuhusu fate zao kinyota.

Na safu hiyo ikaniacha na monikers kama "Ustaadh", "Bonge" au "Ustaadh Bonge",ambayo kwa baadhi ya marafiki zangu,ndio pekee wanayofahamu kuhusu mie.

Looking back,I can't help but just laugh.Good old days za "Kijiweni" nyuma ya ATB "tulipokuwa tunahudhuria masomo kwa kile tulichokiita correspondence" ie mtu mmoja atakaeingingia kwenye mhadhara (lecture) ndiye atakayesambaza contents za kilichofundishwa"!!!However,when the UEs came,we all managed to smash them.
"KIJIWENI" ni kulia kwa picha hii ie nyuma ya ATB

Missing you guys,Ghetto Boy (sasa ni bosi mahala flani), "Dogo" Baraka (naye pia ni bosi katika kampuni moja ya kigeni),Adam Mkula,Busa Musika,Aden,Iku, "Sospiere",Chrisant, Swedi Mlanzi, Bitebo,Manzi,Eric (wape hi Skandinavia), "Queen Latifa",Faith Msina,Belinda,Leila,Kassim,na wengineo.You made our days at the uni one experience that I will never ever forget!!!!

17 Jan 2011


Katika siku za hivi karibuni,jina la Edward Lowassa limekuwa likisikika sana.Blogu hii inahisi kuwa kelele hizi za Lowassa ni sehemu ya jiihada za kuweka jina lake machoni na masikioni mwa Waanzania ili hatimae amrithi swahiba wake,Jakaya Kikwete, hapo 2015.Hebu msikie tena hapa chini,kisha tumjadili kiduchu


Lowassa: Mjadala wa Katiba usivuruge amani

na Betty Kangonga

MBUNGE wa Monduli, Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, ametahadharisha mjadala kuhusu Katiba nchini kuwa chanzo cha kuharibu wa amani iliyoko nchini.

Lowassa alitoa tahadhari hiyo jana wakati akifungua studio ya muziki ya FLEM, jijini Dar es Salaam na kuongeza kuwa hivi sasa inaoneka kuwapo kwa mashindano ya kuharibu amani kutokana na mjadala huo kupamba moto.

Alisema kuwa kadri siku zinavyozidi kusonga mbele ndivyo moyo wa kuharibika kwa amani unavyozidi kuongezeka.

Alisisitiza kuwa hata katika mijadala mbalimbali inayoendelea nchini hasa ya Katiba, wananchi wanatakiwa kupingana kwa hoja na si kwa kuhatarisha amani.

“Tunatakiwa kutunza amani yetu kama mboni ya jicho maana hata nchi jirani za wenzetu ikiwamo Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi hawajawahi kuwa na amani kama tuliyonayo sisi, hivyo tunatakiwa kuhakikisha tunaitunza kwa uwezo wetu wote,” alisema Lowassa.

Katika kusisitizia hilo, aliwashauri waimbaji wa Injili kuamka la kutunga nyimbo zinazohamasisha na kuchochea utunzaji wa amani, ili iendelee kudumu.

“Waimbaji wa Injili wanafanya kazi nzuri sana ingawa katika maisha kuna mahali unayumba, unaanguka na kupanda, lakini yote hayo ni kwa uwezo wa Mungu.

“Hakikisheni mnatunga nyimbo za kutetea amani maana kwa sasa kila mtu ana lake analosema, vyombo vya habari vinachochea kwa njia yake, hivyo tuilinde hii amani,” alisema.

Alisema kuwa bila kuwa na amani hakuna taifa linaloweza kufikia maendeleo, hivyo jamii inapaswa kupingana bila kusababisha mvurugano.

Alisema amani ni tunu pekee aliyotuachia Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, hivyo tunatakiwa kuitetea kwa nguvu zetu zote.


Alisema kuwa ni kipindi cha ajabu sasa, kwani kila mtu amekuwa akiamka na jambo lake linaloonekana kuhatarisha amani.

Kwa upande wake, mchungaji wa kanisa la FPCT la Mtoni Kijichi, Joseph Malundo, aliwataka wamiliki wa studio hiyo kuacha kubweteka na mafanikio hayo bali wazidi kumuomba Mungi ili azidi kuwapandisha juu zaidi.

Alisema hatua hiyo itawezesha vijana wengi kupata ajira hasa kwa kumtumikia Mungu.

CHANZO: Tanzania Daima

Tatizo la Lowassa,na watu wenye mawazo kama yake,ni kuwaona Watanzania ni wajinga,wasio na kumbukumbu,na ambao wako radhi kufisadiwa milele.Pengine mawazo hayo yanatokana na ukweli kuwa licha ya mtu kama yeye kulazimika kujiuzulu uwaziri mkuu kutokana na kuhusishwa na ujambazi wa Richmond (mtangulizi wa Dowans) bado yupo huru,anapeta na licha ya kufanikiwa kurejea Bungeni,ameendelea kupewa heshima ya "Waziri Mkuu Mstaafu".Na si yeye tu,bali hata washirika wake Ibrahim Msabaha na Nazir Karamagi.

Laiti sheria ingefuata mkondo wake,tusingesikia matusi haya ya Lowassa.Ni dhahiri kuwa anafahamu fika kuwa tishio kubwa la amani ya Tanzania na Watanzania ni UFISADI na MAFISADI.Hawezi kuzungumzia hilo kwa vile linamgusa.Na ni wazi kuwa japo anajifanya kuguswa na umuhimu wa Katiba mpya,ni wazi kuwa yeye,rafiki yake Rostam Aziz,na mlinzi wao hapo Ikulu,Kikwete,wasingependa kuona Katiba mpya itakayompa nguvu Mtanzania kupambana na wezi,majambazi,wadhalimu na wabaka uchumi kama hao walioleta Richmond,na sasa wanataka kujizawadia mabilioni kwa usanii wa "fidia kwa wanaharamu wa Dowans".

Na nyie viongozi wa dini mnaoendekeza njaa zenu mnapaswa kuelewa sio kila sadaka inampendeza Mungu.Kwani Bwana Yesu alifanya kazi zake kwa kutegemea michango,achilia mbali michango ya wanafiki,wezi,majambazi au wapinzani wa Amri za Mungu?Njaa zenu ndio zinawapa watu kama Lowassa nafasi ya kujiosha machoni mwa jamii ilhali tunafahamu fika wasingepaa madaraka kuwa laiti Baba wa Taifa angekuwa hai-kwani alishawaona kuwa ni viumbe hatari kabisa kwa Tanzania yetu.



16 Jan 2011

Maji yamezidi unga au afya mbovu?Rais Jakaya Kikwete anaonekana pichani (wa tatu kulia) akiwa hoi bin taaban.Na Lowassa (wa kwanza kulia mstari wa nyuma) anaonekana kama ameguswa na hali ya rafiki yake
Chanzo: Jamii Forums

15 Jan 2011


Hivi kuna uwezekano kwamba Mwenyekiti wa CCM,ambaye pia ni Rais wa Tanzania,Jakaya Kikwete,hamtakii mema Katibu Mkuu wa chama hicho,Yusuph Makamba,na ndio maana (Kikwete) hamshauri Makamba achunge kauli zake.Kwa vile wengi tunafahamu 'upole' (uzembe?) wa Kikwete katika kuwajibisha watendaji fyongo,labda anasubiri Makamba akutane na tukio la 'mchimba kisima kazama kisimani' ie kauli zake za ovyo ovyo zije kumlipukia mwenyewe.

Hebu soma kwanza stori ifuatayo,kisha tutaijadili kidogo.

Makamba amjibu Askofu Laizer
Thursday, 13 January 2011 21:07

Raymond Kaminyoge


KATIBU Mkuu wa CCM, Yusuph Makamba, amesema kuwa na uelewa finyu wa biblia si jambo la ajabu kwake kwa sababu yeye siyo askofu.

Makamba aliliambia Mwananchi jana kwa simu, kuwa licha ya uelewa finyu wa biblia, lakini amekuwa akitoa vifungu hivyo kwenye biblia.
Makamba alisema hayo kufuatia, Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Thomas Laizer kusema Makamba ana uelewa finyu wa biblia.

Laizer alisema hayo juzi mjini Arusha wakati wa kuwaaga watu wawili waliofariki kwa kupigwa risasi na polisi katika maandamano na Chadema yaliyofanyika Januari 5 mwaka huu.

“ Ni kweli ninauelewa finyu wa biblia kwa sababu mimi siyo askofu, hata Qurani naweza kuwa siifahamu vizuri kwa sababu mimi siyo Sheikh, ndiyo maana kila ninachozungumza kuhusu dini hizo nakariri vifungu kutoka katika vitabu hivyo,” alisema. Makamba alisema alimweleza Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, kutoandamana kwa sababu serikali ilipiga marufuku maandamano hayo, wao wakapuuza.

Alimtaka Laizer kutoa tafsiri ya kitabu cha Warumi 13 sehemu ya kwanza hadi ya saba, inayosema kuwa kila mtu hana budi kutii serikali inayotawala kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu.
Alisema kwa hiyo anayepinga mamlaka inayotawala anapinga chombo kilichowekwa na Mungu na watu wanaoasi hujiletea hukumu.

“ Kwa maana watawala hawatishi watu wanaotenda mema bali wale wanaotenda maovu, kama hupendi kuishi kwa kumwogopa mwenye mamlaka basi tenda mema naye atakusifu,” alisema.

“ Laizer anieleze ufinyu wangu katika uelewa wa biblia upo wapi ikilinganisha na tukio lililotokea mkoani Arusha,” alisema.

CHANZO: Mwananchi

Sasa Makamba anaelekea kubaya.Na kama kuna watu wanamtakia mema (angalau ndani ya familia yake) ni vema wakamdhibiti mapema.

Kutumia Maandiko Matakatifu kuhalalisha maovu ni mithili ya matusi kwa waumini wa dini husika.Makamba si Mkristo,na amekiri kuwa uelewa wake wa Biblia Takatifu ni mdogo.Sasa kama ni hivyo,iweje basi aanzishe malumbano na kiongozi wa madehehebu ya Kikristo,achilia mbali kiongozi huyo kuwa ni Askofu Mkuu wa KKKT?

Makamba anaelewa vyema kuwa Maandiko Matakatifu,hayawezi kunukuliwa kwa vipande vipande.Kadhalika,uwezo wa kunukuu haumaanishi uelewa wa nukuu husika.Pia naamini Makamba anafahamu fika kuwa aya aliyotumia kuhalalisha udikteta wa CCM na polisi wake (uliopelekea mauaji ya raia wasio na hatia)haimaanishi kuwa hata mamlaka inayokandamiza watu wasio na hatia iendelee kunyenyekewa.

Kama suala la kutii mamlaka iliyo madarakani,kwanini basi hapo 1979 tulimng'oa Nduli Idi Amini ambaye wakati huo alikuwa Rais halali wa Uganda?Au kwanini basi Hitler nae alivurumishwa ilhali alikuwa kiongozi halali wa Ujerumani?Au kwanini tulisapoti harakati za mapambano dhidi ya makaburu ilhali wabaguzi hao wa rangi walitengeneza "serikali halali"?

Kwa wanaompenda Makamba,ni vema wakamshauri kuwa madaraka aliyonayo,sambamba na kuwa chini ya bosi mwenye huruma kwa wanaoboronga (ie Kikwete),visimfanye apate jeuri ya kuanzisha bifu na Watumishi wa Mungu.Ni vema pia akatambua unyeti wa kutumia Biblia kuhalalisha maovu ilhali yeye ni Muislam.Kiongozi mwenye akili timamu anapaswa kutambua hatari na madhara ya KUDHARAU MAANDIKO MATAKATIFU (kama ambavyo Makamba anavyoichezea Biblia Takatifu mithili ya Manifesto ya Uchaguzi ya CCM-iliyosheheni kila ahadi ya uongo).

Na kama Makamba mwenyewe ameshawahi kusoma blogu hii (which I doubt) basi ushauri wangu mwepesi kwake ni AACHAE KUMCHEZEA MUNGU,hata kama haamini kuwa Mungu ambaye Askofu Mkuu Lazier ni mtumishi wake,ni Mungu wake yeye Makamba.

Na kwa Kikwete,hivi lini utajaribu angalau kuwaonyesha Watanzania kuwa una uwezo japo haba wa kukemea mambo hatari?Ah,yani umekuwa hapo Ikulu kama pambo huku watendaji wako wakizidi kuhangaika kusaka moto na petroli ya kuiunguza Tanzania?

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.