The Sporah Show itakuwa hewani leo Jumamosi mnamo saa saba mchana (1300hrs) katika kituo cha televisheni cha Star (STAR TV) huko nyumbani Tanzania. Endelea.
5 Mar 2011
5.3.11
Evarist Chahali
SPORAH SHOW, STAR TV
No comments
The Sporah Show itakuwa hewani leo Jumamosi mnamo saa saba mchana (1300hrs) katika kituo cha televisheni cha Star (STAR TV) huko nyumbani Tanzania. Endelea.
2 Mar 2011
2.3.11
Evarist Chahali
RAIA MWEMA
2 comments
Makala yangu katika toleo la wiki hii la jarida mahiri la habari na uchambuzi la Raia Mwema inazungumzia ombwe la uongozi wa Kikwete,na namna ombwe hilo linavyojidhihirisha katika namna tukio la milipuko ya mambomu huko Gongo la Mboto linavyoshughulikiwa.
BONYEZA HAPA KUSOMA MAKALA HIYO pamoja na habari na makala nyingine zilizokwenda shule.
BONYEZA HAPA KUSOMA MAKALA HIYO pamoja na habari na makala nyingine zilizokwenda shule.
28 Feb 2011
28.2.11
Evarist Chahali
MILIPUKO DAR, Reading, Watanzania UK
1 comment
Baadhi ya Watanzania wanaoishi hapa Uingereza waliendesha harambee ya kuchangia wahanga wa milipuko ya mabomu huko Gongo la Mboto jijini Dar es Salaam. Picha za harambee hiyo katika mji wa Reading.
Left to Right: JJ, Chisumo, Ms Jestina, Gardol na Frank
Frank na Ms Jestina
Mdau akichangia
Mkurugenzi wa Locus Impex Shipping,B. Chisumo akifungua harambee
Mtoto Shanelle akimpa mchango Ms Jestina
Toa ndugu ikiendelea
Left to Right: JJ, Chisumo, Ms Jestina, Gardol na Frank
Frank na Ms Jestina
![]() |
| Ms Jestina |
Mdau akichangia
Mkurugenzi wa Locus Impex Shipping,B. Chisumo akifungua harambee
Mtoto Shanelle akimpa mchango Ms Jestina
Toa ndugu ikiendelea
Shughuli ikiendelea
![]() |
| Wadau |
26 Feb 2011
26.2.11
Evarist Chahali
BERNARD MEMBE
1 comment
Yayumkinika kuhisi kuwa laiti Baba wa Taifa angefufuka leo huenda angeishia kutoa machozi.Taifa alilohangaika na wenzie kulipigania uhuru limegeuka kituko.Upande mmoja tunamwona Rais wetu akijibidiisha kusaka amani Ivory Coast ilhali wakazi wa Gongo la Mboto wanaporwa amani na usalama wao na wazembe wa Jeshi la Wababaishaji Tanzania...ooops,I meant Jeshi la Walipua mabomu...oh,not again.Nilitaka kuandika Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ).Kwa upande mwingine ni ziara ya haramia wa Dowans ambaye licha ya kukimbia ukombozi wa Wazanzibari baada ya Mapinduzi amemudu kututapeli,kabla ya kuja kutuhubiria namna ya kuzalisha umeme,na kukumbushia fidia anayopaswa kulipwa kwa kututapeli!
Huku baadhi yetu tukizidi kusononeshwa na namna ombwe la uongozi linavyozidi kufidiwa kwa vitendo vya ufisadi,tunashuhudia eneo jingine ambalo lilisaidia sana kuifanya Tanzania ya Nyerere iheshimike kwa msimamo wake thabiti.Hapa nazungumzia sera za nje za nchi yetu.
Baada ya Mwalimu kung'atuka na nafasi yake kurithiwa na watu ambao kama Urais ni somo basi kwao halikuwemo kwenye silabasi (maana angalau anayepata zero anakuwa amesoma lakini hakufaulu),nchi yetu imegeuka kichekesho linapokuja suala la msimamo wetu kama taifa huru.
Na ukidhani naandika haya kama uzushi basi soma habari hii inayoeleza kuwa Tanzania imeogopa kutoa msimamo wake kuhusu uanaharamu wa dikteta Muamar Ghaddafi dhidi ya wananchi wake wanaodai mabadiliko nchini Libya.
Kwa mujibu wa habari hiyo,Waziri wa Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa Bernard Membe amedai kuwa
Tanzania kama nchi haiwezi kujitokeza wazi wazi kuunga mkono ama kupinga kinachotokea nchini humo kwa sababu ina raia wake wanaoishi huko hivyo kitendo chochote cha kushabikia kwa kuunga mkono ama kupinga kinahatarisha maisha yao.
Katika habari hiyo,Membe amenukuliwa akisema:
Unajua tuna raia wetu kule sasa siyo vizuri kuonyesha utashi wetu inaweza kuhatarisha maisha ya wananchi wetu kwani hii ilitokea kule Misri kwa wale waliojitokeza kuunga mkono waliweza kushambuliwa na kuharibiwa biashara zao
Ungetegemea Membe angejaribu angalau kuficha ombwe katika sera yetu ya nje kwa angalau kudanganya kama mwanadiplomasia kwamba "tunafuatilia kwa karibu matukio ya nchini Libya na tuko katika mchakato wa kuweka bayana msimamo wetu".
Yaani Membe anataka kutuzuga kwamba laiti Tanzania ikilaani unyama wa Ghaddafi dhidi ya raia wake basi kiongozi huyo wa Libya atalipa kisasi kwa kuwadhuru Watanzania 26 (kwa mujibu wa takwimu zake) waliopo nchini humo?
Kichekesho ni kwamba serikali ya CCM ambayo Membe ni miongoni mwa Waziri wake ilimudu kulaani "vurugu zilizosababishwa na Chadema huko Arusha" (ilhali waliopaswa kulaaniwa ni polisi wanaoamini katika ubabe kama wa Ghaddafi) japokuwa kuna Watanzania waliouawa na kujeruhiwa ni Watanzania pia (pamoja na raia mmoja wa Kenya).
Labda nitoe mfano bora zaidi.Hivi wakati Nyerere alipoweka wazi msimamo wake dhidi ya Makaburu wa Afrika Kusini hakukuwa na maslahi yoyote ya Tanzania katika nchi hiyo?Au,je tulipoamua kukabiliana na nduli Idi Amini hakukuwa na Mtanzania huko Uganda?
Ukweli ulio bayana ni kwamba si Membe wala bosi wake Kikwete wenye uthubutu wa kulaani unyama unaofanywa na Ghaddafi.Na si ajabu wanaombea afanikiwe kuteketeza raia wake na kubaki madarakani kisha wajipendekeze kwa kupitisha bakuli huko.
Lakini kwa upande mwingine kumlaumu Membe katika hili ni sawa na kumtaka mwanafunzi wa chekechea aandike thesis kuhusu mada ngumu kama Quantum Physics.Hivi kwa watu wanaoshindwa japo kumkemea mwarabu Adawi anayeifanya nchi yetu kama darasa la majaribio ya kudalilisha uhuru wa taifa,na badala yake wanampa fursa ya mwaliko hapo Ikulu kukutana na Makamu wa Rais (bila kusahau dokezo lake kuwa asipigwe picha),wataweza vipi kumudu mambo mazito kama uhusiano wa kimataifa?
Unapoona kiongozi wa nchi anashindwa kuwawajibisha Waziri wa Ulinzi Dkt Hussein Mwinyi,Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange,na wazembe wote waliogeuza makazi ya raia yaliyo jirani na kabi za jeshi kuwa viwanja vya mazoezi ya kulipua mabomu,basi ni wazi kumtegemea aongoze vema nchi katika masuala ya kimataifa ni sawa na kutarajia damu kutoka kwenye jiwe.
Mwinyi,Mkapa na sasa Kikwete wamefanikiwa sana kuifuta Tanzania kutoka katika nafasi yake kama taifa lenye msimamo na uongozi dhidi ya tawala dhalimu,mfano wa kupigiwa mstari ukiwa nafasi ya Tanzania katika mapambano ya ukombozi Kusini mwa Afrika.
Katika stadi za siasa tunafundishwa kwamba sera imara ya mambo ya nje inategemea sana uimara katika sera za mbalimbali za ndani ya nchi.Sasa kwa mwenendo huu ambapo Taifa letu lipo katika hatari ya kugeuzwa koloni binafsi la mafisadi ambao wanarahisishiwa azma hiyo na uongozi dhaifu wa Kikwete (anayechelea kuwaudhi maswahiba zake wanaoliingiza mkenge taifa letu),itakuwa ni njozi za mchana za mtu mwenye njaa kutegemea nchi hii irejee zama za Mwalimu ambapo tulimudu kujitengenezea heshima kubwa kutokana na misimamo thabiti na isiyoendekeza kujikomba,uoga,unafiki au ubabaishaji.
Kwa mwenendo huu,nalazimika kuafikiana na kauli za Sheikh Yahya kuwa nchi yetu inaweza kukumbwa na mabalaa makubwa huko mbeleni (japo nawalaumu waandishi wa habari walioshindwa kumhoji mnajimu huyo kuhusu utabiri wake kwamba mtu yeyote ambaye angejitokeza kugombea dhidi ya Kikwete katika uchaguzi mkuu uliopita angekufa).
24 Feb 2011
24.2.11
Evarist Chahali
ADAWI, KIKWETE
1 comment
Katika harakati zake duni za kujinasua uhusika wake katika suala la ujambazi wa Dowans,Rais Jakaya Kikwete alijaribu kuwahadaa Watanzania kwa kudai,pamoja na mambo mengine,kuwa "hawajui wamiliki wa Dowans".
Na kwa bahati nzuri kwake,vyombo vyetu vya habari vikaishia kumnukuu tu.Lakini kwa minajili ya kufupisha makala hii(na kupunguza maumivu yanayotokanayo) tuweke kando kuangalia namna Kikwete alivyotengeneza mazingira ya ujio wa Dowans kupitia majambazi wengine wa Richmond.Hapa namaanisha kauli yake kuwa tatizo la umeme lingekuwa historia baada ya ujio wa mitambo ya kuzalisha umeme kutoka Marekani (na tukaishia kuletewa mitambo garasa)
Hatimaye mwarabu Adawi aliyekimbia ukombozi wa Mzanzibari,amediriki kuja na kutufanyia kila aina ya vituko (kukataa kupigwa picha,nk) na kutangaza hadharani kuwa yeye ndio mmiliki wa Dowans.Na kama kututukana Watanzania,akadai kuwa anaweza kuangalia uwezekano wa kupunguza FIDIA ANAYOPASWA KULIPWA KWA KUTUIBIA (yale yale ya vibaka wanaomkaba mtu kisha kumpigia ukelele wa "mwizi,mwizi...")
Adawi ambaye Kikwete anadai hamjui (japo anamjua sana kwani wana mahusiano ya "kifamilia")ameweza kutia mguu Ikulu na kuongea na Makamu wa Rais Gharib Bilali (anayekaimu urais katika kipindi hiki ambacho Kikwete yuko kwenye mizunguko yake).
Japo tunajua kuwa Ikulu yetu imegeuzwa kijiwe cha mafisadi ambao wana uhuru wa kutembelea mahala hapo patakatifu kila wanapojisikia lakini kwa Adawi kupewa nafasi ya kukutana na Rais (kwa maana ya anayekaimu nafasi hiyo),na mkutano huo kufanywa siri,inaashiria kuwa Kikwete na serikali yake sio tu anamjua Adawi bali pia anamtumikia.
Sintashangaa kusikia kuwa Kikwete aliamua kwenda Mauritania ili kumwezesha Adawi afanye uhuni wake kisha ahitimishe ziara yake kwa maongezi na kaimu wa Kikwete (Gharib Bilali).Na sintoshangaa kusikia kwamba kabla ya kurejea Tanzania,maswahiba hao wawili (Kikwete na Adawi) wakakutana faragha kujadili kuendeleza ujambazi wa Dowans.
Na hata tukiweka kando ujio wa Adawi,kauli ya Kikwete kuwa hawajui wamiliki wa Dowans ilhali majina ya wamiliki hao yapo BRELA (na Waziri Ngeleja alishayaweka hadharani kabla Kikwete hajatoa utetezi wake feki) inatosha kuwafahamisha Watanzania kuwa Rais wao ameshindwa kazi.How come Waziri ajue kile ambacho Rais hakijui?Je kama anashindwa kujua jambo dogo tu kama rekodi ndogo tu iliyopo BRELA atawezaje kujua na hatimaye kushughulikia matatizo ya Watanzania takriban milioni 50?
Tusipofumbuka macho kama wenzetu wa Tunisia,Misri,Libya na kwingineko wanakopambana na tawala dhalimu tunaweza kuishia kuwa koloni la Adawi,yaani mwarabu huyo kuongoza nchi yetu kwa kutumia remote control in the form of Kikwete.
Na kwa bahati nzuri kwake,vyombo vyetu vya habari vikaishia kumnukuu tu.Lakini kwa minajili ya kufupisha makala hii(na kupunguza maumivu yanayotokanayo) tuweke kando kuangalia namna Kikwete alivyotengeneza mazingira ya ujio wa Dowans kupitia majambazi wengine wa Richmond.Hapa namaanisha kauli yake kuwa tatizo la umeme lingekuwa historia baada ya ujio wa mitambo ya kuzalisha umeme kutoka Marekani (na tukaishia kuletewa mitambo garasa)
Hatimaye mwarabu Adawi aliyekimbia ukombozi wa Mzanzibari,amediriki kuja na kutufanyia kila aina ya vituko (kukataa kupigwa picha,nk) na kutangaza hadharani kuwa yeye ndio mmiliki wa Dowans.Na kama kututukana Watanzania,akadai kuwa anaweza kuangalia uwezekano wa kupunguza FIDIA ANAYOPASWA KULIPWA KWA KUTUIBIA (yale yale ya vibaka wanaomkaba mtu kisha kumpigia ukelele wa "mwizi,mwizi...")
Adawi ambaye Kikwete anadai hamjui (japo anamjua sana kwani wana mahusiano ya "kifamilia")ameweza kutia mguu Ikulu na kuongea na Makamu wa Rais Gharib Bilali (anayekaimu urais katika kipindi hiki ambacho Kikwete yuko kwenye mizunguko yake).
Japo tunajua kuwa Ikulu yetu imegeuzwa kijiwe cha mafisadi ambao wana uhuru wa kutembelea mahala hapo patakatifu kila wanapojisikia lakini kwa Adawi kupewa nafasi ya kukutana na Rais (kwa maana ya anayekaimu nafasi hiyo),na mkutano huo kufanywa siri,inaashiria kuwa Kikwete na serikali yake sio tu anamjua Adawi bali pia anamtumikia.
Sintashangaa kusikia kuwa Kikwete aliamua kwenda Mauritania ili kumwezesha Adawi afanye uhuni wake kisha ahitimishe ziara yake kwa maongezi na kaimu wa Kikwete (Gharib Bilali).Na sintoshangaa kusikia kwamba kabla ya kurejea Tanzania,maswahiba hao wawili (Kikwete na Adawi) wakakutana faragha kujadili kuendeleza ujambazi wa Dowans.
Na hata tukiweka kando ujio wa Adawi,kauli ya Kikwete kuwa hawajui wamiliki wa Dowans ilhali majina ya wamiliki hao yapo BRELA (na Waziri Ngeleja alishayaweka hadharani kabla Kikwete hajatoa utetezi wake feki) inatosha kuwafahamisha Watanzania kuwa Rais wao ameshindwa kazi.How come Waziri ajue kile ambacho Rais hakijui?Je kama anashindwa kujua jambo dogo tu kama rekodi ndogo tu iliyopo BRELA atawezaje kujua na hatimaye kushughulikia matatizo ya Watanzania takriban milioni 50?
Tusipofumbuka macho kama wenzetu wa Tunisia,Misri,Libya na kwingineko wanakopambana na tawala dhalimu tunaweza kuishia kuwa koloni la Adawi,yaani mwarabu huyo kuongoza nchi yetu kwa kutumia remote control in the form of Kikwete.
24.2.11
Evarist Chahali
Mabadiliko
No comments
Maandamano ya kupinga tawala dhalimu,ambayo yamesambaa maeneo kadhaa ya Afrika Kaskazini,yanaanza kuonyesha dalili za kusambaa sehemu nyingine za bara la Afrika hadi Cameroon,Gabon,Zimbabwe na Mauritania.
Nchini Cameroon,kulikuwa na mpango wakufanya maandamano jana kwa lengo la kumwondoa madarakani Rais Paul Biya,kwa mujibu wa kituo cha televisheni cha CNN cha Marekani.Biya amekuwa madarakani kwa miaka 28.Kiongozi wa upinzani,Kah Walla,aliieleza CNN kwamba kundi lake linataka kuona chaguzi huru na za haki.
Mwandishi wa gazeti la New York Times la Marekani,Nick Kristof, aliandika kwenye Twitter kwamba:
Mapambano ya kudai demokrasia yanasambaa maeneo mapya barani Afrika: Cameroon,Gabon,Zimbabwe,Mauritania.
Wanaharakati wakutana Zimbabwe kujadili yaliyojiri Misri na Tunisia na wameishia kukamatwa.Mugabe hajaelewa somo
Kamati ya Kulinda Waandishi wa Habari inaripoti kwamba Eritrea,Guinea ya Ikweta na Zimbabwe wamedhibiti kabisa maendeleo ya mapambano ya kung’oa tawala dhalimu huko Mashariki ya Kati na Afrika Magharibi.
Habari zaidi kutoka CNN zinaeleza kuwa wanaharakati na viongozi kadhaa wa vya vyama vya wafanyakazi nchini Zimbabwe walizingirwa na polisi wiki iliyopita na sasa wanakabiliwa na hukumu ya kifo baada ya waendesha mashtaka wa serikali ya nchi hiyo kuwasomea mashtaka ya kupanga maandamano ya kuung’oa madarakani utawala wa Rais Robert Mugabe.
Katika kesi hiyo iliyoendeshwa jana,washtakiwa 46 wanakabiliwa na shtaka la uhaini .Walikamatwa Jumapili iliyopita baada ya mamlaka kudai kuwa walikutwa wakiangalia mikanda yenye kuonyesha maandamano yaliyopelekea kung’olewa madarakani aliyekuwa Rais wa Tunisia Zine El Abidine Ben Ali na mwenzie wa Misri Hosni Mubarak.
Mtandao wa habari wa Afrol unaripoti kufanyika kwa maandamano ya nchini nzima huko Cameroon kushinikiza Rais Biya aondoke madarakani ,japokuwa maandamano hayo yalidhibitiwas kirahisi na vyombo vya usalama vya nchi hiyo.
Miji mikubwa ya Younde na Douala ilitawaliwa na askari wa kutuliza ghasia huku magari yakisimamishwa na kupekuliwa na mikusanyiko ya watu ikidhibitiwa.Kadhalika,mashuhuda wameeleza kuwa polisi walinyang’anya kamera na simu za mikononi.
Wachambuzi wa mambo wanadai kuwa licha ya maandamano hayo kutofanikiwa kufikia matarajio ya wengi,bado kuna uwezekano wa yaliyojiri sehemu kama Tunisia na Misri kujitokeza nchini Cameroon hivi karibuni.Kilio cha wananchi wengi wa taifa hilo ni rushwa na hali ngumu ya maisha.Harakati za kudai mabadiliko nchini humo zinachochewa zaidi na Wakameruni wanaoishi nje ya nchi hiyo.
22 Feb 2011
22.2.11
Evarist Chahali
DOWANS
2 comments
Kuna taarifa kwamba mtu aliyetambulishwa kama mmiliki wa kampuni ya Dowans, Brigedia Jenerali (Mstaafu) Sulaiman Mohammed Yahya Al Adawi ni kiini macho.
Chanzo cha kuaminika kinaeleza kuwa tukio zima la "mmiliki wa Dowans kuzungumza na baadhi ya wahariri wa vyombo vya habari" ni sehemu tu ya mkakati mahsusi na endelevu kuughilibu umma wa Watanzania katika sakata la malipo ya fidia kwa kampuni hiyo.
Kwa mujibu wa vyanzo hivyo,sababu iliyopelekea "Bilionea huyo wa Dowans" kukataa kupigwa picha mgando wala kurekodiwa na kamera za televisheni ni hofu kuwa "danganya toto" hiyo ingebainika kirahisi pindi Watanzania wangekwenda mbali zaidi kuchimba undani na ukweli.
Lakini hata katika mazingira ya kawaida tu,haiyumkiniki mfanyabiashara anayejitambulisha kuwa amewekeza zaidi ya dola bilioni moja (USD 1,000,000,000,000) nchini India akwepe kupigwa picha kwa madai dhaifu kuwa anaendesha biashara zake kwa "low profile".
Na kama hiyo haitoshi,itakumbukwa kuwa Waziri wa Nishati William Ngeleja aliwahi kutangaza wamiliki wa kampuni ya Dowans (ambao bosi wa Ngeleja,Rasi Jakaya Kikwete,alidai hawajui) ni Brigedia Jenerali Sulaiman Mohamed Yahya Al Adawi ambaye ni raia wa Oman, Guy Arthur Picard raia wa Canada, Stanley Munai raia wa Kenya. Wengine ni Andrew James Tice raia wa Canada, Gopala Krishnan Balachandran kutoka India na Hon Sun Woo kutoka Singapore.Lakini katika mkutano wake na wahariri hao,'Bilionea huyo wa Dowans' alidai kuwa yeye pekee ndio mmiliki wa kampuni hiyo.
Kwa mujibu wa vyanzo hivyo,sababu iliyopelekea "Bilionea huyo wa Dowans" kukataa kupigwa picha mgando wala kurekodiwa na kamera za televisheni ni hofu kuwa "danganya toto" hiyo ingebainika kirahisi pindi Watanzania wangekwenda mbali zaidi kuchimba undani na ukweli.
Lakini hata katika mazingira ya kawaida tu,haiyumkiniki mfanyabiashara anayejitambulisha kuwa amewekeza zaidi ya dola bilioni moja (USD 1,000,000,000,000) nchini India akwepe kupigwa picha kwa madai dhaifu kuwa anaendesha biashara zake kwa "low profile".
Na kama hiyo haitoshi,itakumbukwa kuwa Waziri wa Nishati William Ngeleja aliwahi kutangaza wamiliki wa kampuni ya Dowans (ambao bosi wa Ngeleja,Rasi Jakaya Kikwete,alidai hawajui) ni Brigedia Jenerali Sulaiman Mohamed Yahya Al Adawi ambaye ni raia wa Oman, Guy Arthur Picard raia wa Canada, Stanley Munai raia wa Kenya. Wengine ni Andrew James Tice raia wa Canada, Gopala Krishnan Balachandran kutoka India na Hon Sun Woo kutoka Singapore.Lakini katika mkutano wake na wahariri hao,'Bilionea huyo wa Dowans' alidai kuwa yeye pekee ndio mmiliki wa kampuni hiyo.
Na kama hiyo haitoshi, 'Bilionea huyo wa Dowans' alishawahi "kuruka kimanga" huko nyuma akidai yeye si mmiliki wa kampuni hiyo LAKINI SASA ANADAI SI TU MMILIKI BALI MMILIKI PEKEE.Hizi ni dalili za wazi za ubabaishaji wa "Bilionea" huyu! (And shame on you gazeti la Tanzania Daima kwa habari iliyoonyesha bayana mnalamba miguu ya mtu huyu ambaye laiti ikibainika ni yeye basi mahala panapomfaa ni Segerea kama sio Keko au Ukonga).
Tovuti hii inaendelea na uchunguzi wa kina kuhusu suala hilo na inaahidi kuwafahamisha maendeleo (ya uchunguzi huo).Kwa wakati huu,tunatoa wito kwa waandishi wetu wa habari kuacha uzembe wa kuripoti kinachotamkwa tu badala ya kwenda mbali zaidi na kufukua data mbalimbali.Kadhalika,wahariri walioalikwa na Brigedia huyo walipaswa kuwa na msimamo wa kuhoji kwanini hataki picha zake zionekane kwenye vyombo vya habari.
20 Feb 2011
20.2.11
Evarist Chahali
JWTZ, MILIPUKO DAR
No comments
Picha hizi za kutisha zinajieleza zenyewe.Hakuna maelezo yanayotosheleza kueleza kwa ufasaha kuhusu janga hili.Lakini kwa vile kamwe hatutoelezwa chanzo cha milipuko ya mabomu huko Gongo la Mboto,kama ambavyo hatukuelezwa chanzo cha milipuko iliyotokea mwaka juzi huko Mbagala,ni muhimu kwa kila Mtanzania kudai haki yake ya kikatiba ya usalama wa maisha yake.
Ni wazi kuwa wahusika wanapata jeuri ya kutangaza hadharani kuwa hawatajiuzulu kwa vile wanafahamu bayana kuwa aliyewateua kushika madaraka hayo ni mzembe,dhaifu na asiyejua kinachoendelea.Kwa lugha nyingine,YUPO YUPO TU.
Nilighadhibika sana niliposoma kauli ya Mkuu wa Usalama na Utambuzi wa JWTZ Brigedia Jenerali Paul Meela kuwa hakuna atakayejiuzulu kwa sababu uongozi jeshini sio nafasi za kisiasa.Haya ni matusi kwa Watanzania.Kwani Amatus Liyumba alipohukumiwa kwenda jela kwa ubadhirifu wa fedha za umma hapo Benki Kuu alikuwa mwanasiasa?
Kwa akili finyu ya Brigedia Meela,ni wanasiasa pekee wanaopaswa kuwajibika wanapoboronga.Lakini kwa vile kamanda huyo alikuwa anamwakilisha Mkuu wa Mwajeshi Jenerali Davis Mwamunyange,yayumkinika kuamini kuwa kauli hiyo pia ni msimamo wa mkuu huyo wa majeshi.
Tuliowahi kupitia mambo ya kijeshi tunafahamu kasumba ya jeuri na u-mungu mtu ilivyokomaa vichwani mwa viongozi jeshini.Hii inaimarishwa zaidi na utaratibu wa kawaida jeshini kwamba amri ina mwelekeo mmoja tu: kutoka juu kwenda chini,na haihojiwi.
Kwahiyo,wakati Kamanda Meela anaongea na waandishi wa habari,akilini mwake alikuwa kama anaongea na makuruta ambao ni dhambi kuu kwao kuhoji lolote lile.Na kwa vile Meela alikuwa anawakilisha mabosi wake,mtu pekee ambaye angeweza kumwadabisha ni Amiri Jeshi Mkuu,Rais Jakaya Kikwete.
Lakini takriban miezi mitano tangu baadhi ya Watanzania wenzetu watusaliti kwa kumrejesha Kikwete madarakani (tukiweka kando uchakachuaji wa Tume ya Uchaguzi),naamini kila Mtanzania anafahamu fika kuwa ombwe la uongozi wa taifa lililojiokeza wakati wa awamu ya kwanza ya utawala wa Kikwete,sio tu limezidi kukua bali pia limeifanya Tanzania kuishi kwa kutegemea kudra za Mwenyezi Mungu.Ni kama hatuna Rais wala serikali.
Na taasisi muhimu kwa ustawi wa taifa kama Idara ya Usalama wa Taifa ziko katika usingizi mzito unaosababishwa zaidi na marupurupu makubwa licha ya utendaji kazi duni na wa chini ya kiwango.Sijui kama watu hawa wanasumbuliwa na mwenendo wa nchi yetu,kwani ingekuwa hivyo tusingeshuhudia mazingaombwe ya kuruhusu mtu kama Edward Lowassa kuwa Mwenyekiti wa kamati nyeti ya bunge ya Ulinzi na Usalama,leave alone ishu kama za Dowans,EPA,nk.
Na kwa kuonyesha watu wa Usalama wamegubikwa na usingizi,wameshindwa hata kumshauri bosi wao Kikwete kuwa safari yake kwenda Mauritania kusaka ufumbuzi wa mgogoro huko Ivory Coast,sio mwafaka wakati huu wa majonzi makubwa kwa Watanzania.Kikwete na washauri wake wanajifanya hawajui kuwa janga la Gongo la Mboto linawagusa zaidi Watanzania kuliko matatizo ya wa-Ivory Coast.Ni rahisi kwa baadhi ya watu kuhisi kuwa Kikwete anakwepa majukumu na kuamua kwenda kuzurura huko ng'ambo.
Tukirejea kauli za wanajeshi wetu,Brigedia Jenerali Meela anasema taarifa za milipuko iliyopita ni kwa matumizi ya jeshi.Kwani JWTZ limegeuka jeshi la mtu binafsi?Sote tunafahamu kuwa hilo ni Jeshi la Wananchi wa Tanzania.Sasa iweje madudu wanayofanya na yanayopelekea kuwaathiri wananchi wasio na hatia yaishie kuchungiuzwa na wao wenyewe kisha findings nazo zibaki kuwa siri yao?
Jibu la maswali haya na mengineyo mengi ni rahisi:Rais tuliyenae ni dhaifu na asiye na uwezo wa kuwawajibisha hata wale aliowateua yeye mwenyewe.Sasa kwa wanaotegemea Kikwete anaweza kudili na maharamia kama wa Dowans (ambao hakuwateua,na sanasana wanamdai fadhila) watakuwa wana jibu la msingi kuhusu kusuasua kwake kuwashughulikia mafisadi.
Picha kwa hisani ya Rev Masanilo wa Jamii Forums
20.2.11
Evarist Chahali
MILIPUKO DAR
4 comments
Tunaendelea kuwaletea updates za tukio la milipuko ya mabomu jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali,hadi sasa inakadiriwa zaidi ya watu 20 wamepoteza maisha katika tukio hilo.
Tovuti ya Shirika la Habari la Uingereza (BBC) Idhaa ya Kiswahili inaripoti:
Hali ya taharuki imetanda mji wa Dar Es Salaam, nchini Tanzania, huku wakaazi wakiamka kuomboleza vifo vya zaidi ya watu kumi na zaidi ya wengine 60 kujeruhiwa kufuatia milipuko iliyotokea kwenye ghala la kuhifadhi silaha za kijeshi, lililo karibu na uwanja wa kimataifa wa ndege.
Wakaazi wa eneo la Gongo la Mboto lililo karibu na ghala hilo wamekesha nje baada ya makaazi yao kubomoka kutokana na mtikisiko wa milipuko hiyo iliyodumu kwa saa kadhaa. Milipuko hiyo ilisikika kwa umbali wa zaidi ya kilomita ishirini kutoka kituo hicho cha kijeshi.
Inaarifiwa kuwa milipuko hiyo ilianza mwendo wa saa mbili usiku.
Msemaji mmoja wa jeshi amesema kuwa kuna watu wengi ambao wamepoteza maisha yao lakini idadi kamili haijajulikana.
Kamanda wa polisi jijini Dar-es-Salaam, Suleiman Kova, ametoa wito kwa raia wa mji kuwa huo watulivu huku maafisa wa ulinzi wakiendelea na mikakati ya kurejesha hali ya uthabiti.
Kova amesema uchunguzi wa awali umebainisha kuwa mlipuko huo ni ajali na wala sio shambulio la kigaidi.
Ni hii mara ya pili kwa milipuko kama hiyo kutoka jijini Dar es Saalam katika kipindi cha miaka miwili iliyopita mwaka wa 2009 zaidi ya watu ishirini waliuawa na wengine 300 kujerihiwa
Kadhalika,Rais Jakaya Kikwete amewaasa wananchi kuepuka maelezo ya "redio mbao" na badala yake wasubiri taarifa rasmi kutoka serikalini na Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ).Hata hivyo inawezekana Kikwete hajajiuliza kwanini wananchi wanategemea taarifa za "radio mbao" kwani ni dhahiri kuwa penye ombwe la taarifa rasmi,wananchi wanalazimika kugeukia vyanzo vya habari visivyo rasmi.
Hadi muda huu,hakuna kiongozi yeyote aliyewajibika au kuwajibishwa.Watanzania wanatarajia kuona Waziri wa Ulinzi Dkt Hussein Mwinyi,Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama,Jenerali Davis Mwamunyange na Mnadhimu Mkuu wa Jeshi hilo,Luteni Jenerali Abdulrahman Shimbo,wakiwajibishwa mara moja.Lakini kwa namna tunavyofahamu udhaifu wa Rais Kikwete katika kuwashughulikia watendaji wake,kuna uwezekano mkubwa wa Dkt Mwinyi,Mwamunyange na Shimbo kuendelea na madaraka yao
Kilicho wazi ni kuwa serikali itapoteza fedha za walipa kodi kuunda tume kama ile ya milipuko ya Mbagala mwaka 2009,na kisha ripoti ya tume hiyo kuishia kuwa karatasi za kufungia vitafunio.
Japo hakuna anayetaka kutumia janga hili la milipuko kama mtaji wa kuwahukumu watawala wetu,lakini kuna umuhimu mkubwa wa kuunganisha matukio yaliyopita na tukio hili na uwajibikaji duni wa serikali iliyopo madarakani.
Ni muhimu pia kutafakari dhamira ya serikali kuilipa kampuni ya kitapeli ya Dowans,sambamba na mpango wa kuwapatia wabunge shilingi bilioni 90 kila mmoja,huku mipango endelevu ya kuepusha na kukabiliana na majanga ikipuuzwa.
Ukweli ulio bayana ni kwamba serikali ya Kikwete na CCM yake haisumbuliwi na hali ya kutokuwa na uhakika na usalama wa wananchi.
Endelea kutembelea tovuti hii kwa habari na uchambuzi zaidi kuhusu tukio hili la kusikitisha.
16 Feb 2011
16.2.11
Evarist Chahali
JWTZ, MILIPUKO DAR, SHIMBO
No comments
Habari kutoka Dar es Salaam zinaeleza kuwa milipuko kadhaa imetokea maeneo ya Gongo la Mboto.Hata hivyo habari nyingine zinadai kuwa milipuka hiyo imetokea maeneo ya Kisarawe
Bado hakuna taarifa rasmi kuhusu eneo na chanzo cha milipuko hiyo japokuwa habari zilizopo zinadai milipuko hiyo imetokea kwenye kambi ya Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ).
Mtandao wa Jamii Forums umemnukuu Mnadhimu Mkuu wa JWTZ Brigedia Jenerali Abdulrahman Shimbo akisema "Hali ni mbaya Kikosi namba tano maghala yamelipuka ni hatari, watu wahame, maghala yako karibu karibu sana, tunaomba wananchi wahame sasa hivi, tunajitahidi kuzuia moto unaotokana na hilo unaweza kwenda mbali sana hadi Kilomota kumi, wananchi walioko karibu na maghala ya kikosi Gongo la Mboto wasogee mbali sasa hivi."
Hadi sasa hakuna taarifa kamili kuhusu idadi ya majeruhi japokuwa picha zilizotumwa na baadhi ya watumiaji wa huduma ya mtandaoni ya Twitter zinaonyesha majeruhi wakiwa katika hali mbaya
Tukio hili la kusikitisha linatokea wakati Serikali ikiwa haijaweka hadharani ripoti ya vyanzo vya milipuko iliyotokea kwenye Kambi ya JWTZ Mbagala mwezi Aprili na Mei mwaka juzi.
Wakati huo,aliyekuwa Waziri wa Ulinzi Dokta Hussein Mwinyi aliahidi kuwa angewajibika iwapo ingebainika amezembea.Lakini simulizi hizo ziliishia hapo baada ya vile Serikali kupitia Wizara inayoongozwa na Mwinyi kuamua kuiweka ripoti hiyo 'kapuni'
Wakati tovuti hii inaendelea kukusanya habari za uhakika kuhusiana na milipuko hiyo ni muhimu kwa Watanzania kudai haki zao za msingi za usalama wa maisha yao na mali zao.Haiyumkiniki kuona 'intelijensia' ya vyombo vya dola ikiwa na 'ufanisi mkubwa' katika kukandamiza haki za kikatiba za wananchi lakini ikishindwa kuepusha majanga kama haya.
Upatikanaji wa taarifa sahihi unakuwa mgumu hasa kutokana na vyombo 'rasmi' vya habari nchini Tanzania kutowajibika ipasavyo kuwajulisha wananchi kinachoendelea.Tovuti zote za magazeti 'makubwa' hazina breaking news hadi wakati naweka habari hii.
Bado hakuna taarifa rasmi kuhusu eneo na chanzo cha milipuko hiyo japokuwa habari zilizopo zinadai milipuko hiyo imetokea kwenye kambi ya Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ).
Mtandao wa Jamii Forums umemnukuu Mnadhimu Mkuu wa JWTZ Brigedia Jenerali Abdulrahman Shimbo akisema "Hali ni mbaya Kikosi namba tano maghala yamelipuka ni hatari, watu wahame, maghala yako karibu karibu sana, tunaomba wananchi wahame sasa hivi, tunajitahidi kuzuia moto unaotokana na hilo unaweza kwenda mbali sana hadi Kilomota kumi, wananchi walioko karibu na maghala ya kikosi Gongo la Mboto wasogee mbali sasa hivi."
Hadi sasa hakuna taarifa kamili kuhusu idadi ya majeruhi japokuwa picha zilizotumwa na baadhi ya watumiaji wa huduma ya mtandaoni ya Twitter zinaonyesha majeruhi wakiwa katika hali mbaya
Tukio hili la kusikitisha linatokea wakati Serikali ikiwa haijaweka hadharani ripoti ya vyanzo vya milipuko iliyotokea kwenye Kambi ya JWTZ Mbagala mwezi Aprili na Mei mwaka juzi.
Wakati huo,aliyekuwa Waziri wa Ulinzi Dokta Hussein Mwinyi aliahidi kuwa angewajibika iwapo ingebainika amezembea.Lakini simulizi hizo ziliishia hapo baada ya vile Serikali kupitia Wizara inayoongozwa na Mwinyi kuamua kuiweka ripoti hiyo 'kapuni'
Wakati tovuti hii inaendelea kukusanya habari za uhakika kuhusiana na milipuko hiyo ni muhimu kwa Watanzania kudai haki zao za msingi za usalama wa maisha yao na mali zao.Haiyumkiniki kuona 'intelijensia' ya vyombo vya dola ikiwa na 'ufanisi mkubwa' katika kukandamiza haki za kikatiba za wananchi lakini ikishindwa kuepusha majanga kama haya.
Upatikanaji wa taarifa sahihi unakuwa mgumu hasa kutokana na vyombo 'rasmi' vya habari nchini Tanzania kutowajibika ipasavyo kuwajulisha wananchi kinachoendelea.Tovuti zote za magazeti 'makubwa' hazina breaking news hadi wakati naweka habari hii.
(Video kwa hisani ya Dedichjr na Picha kwa hisani ya Jamii Forums)
Subscribe to:
Comments (Atom)

























