2 May 2011



Breaking news kwenye vyombo mbalimbali vya habari vya kimataifa ni kuhusu kuuawa kwa gaidi wa kimataifa Osama Bin Laden.Rais Barack Obama ametangaza taarifa hizo ambazo zitakuwa ahueni kubwa kwa Wamarekani baada ya kumwinda Osama kwa muongo mzima tangu mashambulizi ya September 11,2001 ambayo inaaminika yalipangwa na Osama.

Taarifa zaidi baadaye


Canada’s lacklustre federal election campaign has finally ignited after claims the man many tip to be the country’s next prime minister was found naked by police in a suspected illegal brothel.

Jack Layton, the leader of the New Democratic Party (NDP), was discovered lying on a bed in a room with a 5ft 10in Asian woman in her mid-20s during a police search for underage prostitutes in 1996.

The married Layton, who was a Toronto city councillor at the time, was cautioned and released without charge, a retired Asian crime unit officer told the Sun News Network.

In a campaign that has been overshadowed by the royal wedding and hockey playoffs the report comes a critical time - just one day before Canadians go to the polls for the fourth time in seven years.

Mr Layton’s popularity surge is unprecedented in recent Canadian political history with polls and political analysts even tipping him to become the country’s first NDP Prime Minister.

The genial 60-year-old, nicknamed ‘Gentleman Jack’, uses a cane after undergoing hip surgery in March and is recovering from a recent battle with prostate cancer.

The left-leaning NDP currently sits in fourth position on Canada’s political map with just 49 seats. It is well behind Prime Minister Stephen Harper’s ruling Conservatives (143 seats), the Liberal Party (77) and the nationalist Bloc Quebecois (49).

But Mr Layton has been riding an extraordinary wave of popularity, seemingly spurred on by an electorate desperate to break the political stalemate which has delivered a series of Liberal and Conservative minority governments.

Olivia Chow, Mr Layton's wife and a New Democratic Party MP seeking re-election in Toronto, issued a statement saying Mr Layton told her about the incident at the time it happened.

‘No one was more surprised than my husband when the police informed him of allegations of potential wrongdoing at this establishment,’ Mrs Chow said. ‘Any insinuation of wrongdoing on the part of my husband is completely and utterly false.’

Married: Jack Layton and his wife Olivia Chow wave to his political supporters

Mrs Chow described the business as a ’massage clinic’ that was registered with the City of Toronto.

The notebook of the officer who questioned Mr Layton details how the NDP leader was asked whether he received any services of a sexual nature, to which he replied: ‘No sir, I was just getting a shiatsu.’

The officer then asked Mr Layton if he knew that sex acts were being carried out in the building, to which he replied: ‘No sir.’

The policeman’s notes also detail how the woman, from China, denied carrying out a sex act on Mr Layton.

During an unscheduled press call in Vancouver Mr Layton claimed he was being smeared in the final hours of a campaign just as opinion polls have his party poised to make a historic breakthrough.

‘It's unfortunate to see the smear campaign starting in these last few days of the campaign. Absolutely nothing wrong was done,’ he said.

‘There was no wrongdoing here, yet the smears start. And you know, this is why a lot of people get turned off politics and don't even want to get involved.’

Mr Layton did not address the allegations specifically but a lawyer for the New Democratic Party issued a stern warning about the reports.

‘The facts are that Mr Layton had obtained a massage from a massage therapist, but had no knowledge whatsoever that the therapist’s location may have been used for illicit purposes,’ Brian Iler said.

‘Any statement or inference that Mr Layton’s actions or behaviour was other than the facts stated above would be without any factual basis, would clearly (be) made with malice, and ought not to be published.’

Mr Iler added that Mr Layton was told by police he did nothing wrong but that the location was questionable. He said Mr Layton gave police his name and address and nothing further happened.

Prostitution is legal in Canada but brothels are outlawed.

SOURCE: Dailymail

Francia ambaye alikuwa akisherehekea birthday yake na meneja wake Shelami

Jambo Band wakitumbuiza

Kawelee mzigoni

Kiondo kutoka ubalozini na familia yake

Abubakar Faraji na Chris Love

Maofisa ubalozi

Balozi akifungua sherehe

Balozi na mkewe wakifungua muziki

Balozi na Urban Pulse

Balozi na mkewe wakijiandaa kufungua dansi


Mkurugenzi wa ASET,Asha Baraka,akiongea na mke wa Balozi.

Miss Jestina na Jesse Malongo

Wadau kwenye pozi

Wakati wa kusakata rumba

1 May 2011



Ansbert Ngurumo

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kinajitapa kwamba kinajivua gamba. Lakini sasa imeanza kudhihirika kwamba badala ya kujivua gamba kinajichuna ngozi. Kitakufa!

Bahati mbaya, kama baadhi yetu tulivyowahi kuandika huko nyuma, CCM kinashindwa kuwaaminisha watu wenye akili timamu kwamba kikiwafukuza ujumbe wa Kamati Kuu na Halmashauri Kuu watu watatu – Andrew Chenge, Edward Lowassa na Rostam Azizi – kitakuwa safi. Kinajidanganya!

Taarifa zinaonyesha kuwa wanaoshabikia igizo hili la kujivua gamba ni Mwenyekiti wao, Rais Jakaya Kikwete, Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, na kundi linalofuata mkumbo kwa unafiki na woga.

Lakini wapo wana CCM wengi wenye akili timamu, na wananchi wengine, wanaosema wazi kwamba hata hao watatu wakiondoka, CCM haiwezi kuwa safi tena. Wala haitamsaidia Rais Kikwete kuonekana mwema kwa Watanzania. Na haitakifanya chama hicho kirejeshe mng’aro wake kwa umma.

Ni wazi, jitihada za Rais Kikwete na wenzake zinatokana na ukweli unaomuuma yeye binafsi kutokana na CCM kufanya vibaya katika uchaguzi mkuu uliopita.

Na ingawa kuna ukweli kwamba ufisadi umechangia kukifanya CCM kichukiwe na wananchi, hoja hiyo haiishii kwa watatu hawa. Mafisadi CCM ni wengi. Nimesema huko nyuma, kwamba hata Rais Kikwete mwenyewe, alitajwa kuwa miongoni mwao.

Hata jana alitajwa upya katika mkutano wa Mchungaji Christopher Mtikila na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, akimhusisha rais na utajiri wa ghafla wa mtoto wake.

Ufisadi huu wa rais unamnyima makali ya kuwashughulikia mafisadi wenzake. Na zaidi ya hayo unapanua wigo wa adui zake, maana sasa anagombana na watu wanaomfahamu vema; waliomsaidia na kumjenga, wakambeba hadi Ikulu.

Woga wake ni kwamba baadhi ya hawa waliombeba hadi Ikulu wana uwezo wa kutumia nguvu zile zile kumwondoa ama Ikulu au kwenye chama. Anachofanya sasa ni kuwashughulikia mapema ili kujinusuru.

Lakini nina hakika jitihada hizi hazitakinusuru chama chake. Na ingawa ameaminishwa kwamba mafisadi hawa ndio waliokifanya chama chake “kishindwe” uchaguzi mwaka jana, wapo wanaosema yale asiyotaka kusikia.

Anajiuliza zilikokwenda kura zake mwaka 2010, anapolinganisha na mwamko wa 2005. Anatafuta wachawi, lakini anasahau mambo kadhaa.

Kwa mfano, serikali imeshindwa kukidhi matakwa ya wananchi kama ilivyoahidi mwaka 2005. Kwa nini waipe CCM kura nyingi hata kama inawahonga mashati, kanga, kofia, pesa na pombe?

Wananchi walimsikia Rais Kikwete mwenyewe akiwaambia wafanyakazi ”sitaki kura zenu!” Wengi walikuwa waaminifu kwa kauli yake; wakamnyima. Si wao tu, bali hata rafiki zao, ndugu zao na wajuani wao, walikaa upande wa wafanyakazi. Kwa nini atarajie kura za CCM ziongezeke?

Mara kadhaa, Rais Kikwete alijikuta akigombana na baadhi ya viongozi wa dini kubwa zenye ushawishi kwa umma. Aliwadanganya Waislamu kuhusu Ofisi ya Kadhi Mkuu. Wamedai hadi wakakata tamaa. Hatimaye akawapatia ufumbuzi usioendana na ahadi yake. Wana sababu ya kumwamini na kumpa kura nyingi?

Serikali yake, kupitia kwa wasaidizi na washauri wake kadhaa, na hata yeye binafsi, ilijiingiza katika mzozo usio wa lazima na madhehebu kadhaa ya Wakristo, ikikerwa na jitihada zao za kukuza elimu ya uraia, na kuwahamasisha kuchagua viongozi waadilifu.

Sasa kama alikerwa na kampeni ya kuchagua viongozi waadilifu, tutamwaminije leo katika vita dhidi ya ufisadi? Na anapata wapi ujasiri wa kupiga vita mafisadi wale wale ambao alifika kwenye majimbo yao akawamwagia sifa na kuwanyanyua mikono kuwaombea kura?

Na kumbukumbu zinaonyesha kwamba katika wote, kama tunarejea ile orodha ya mafisadi ya awali (ambamo naye yumo), walishinda wote isipokuwa mmoja – Basil Mramba.

Zaidi ya hayo, walishinda wa kura nyingi. Maana yake ni kwamba wanakubalika katika majimbo yao, na hata nguvu yao inapenya katika vikao vya juu vya chama.

Ndiyo maana baadhi yao (kwa mfano Lowassa) wamefanikiwa hata kupata uongozi katika kamati za Bunge. Anajua nguvu yao ya ushawishi. Ndiyo inayomtisha.

Zaidi ya hayo, CCM kimetumia mabilioni ya shilingi kwa ajili ya “kununulia kura,” kinyume kabisa cha sheria ya gharama za uchaguzi. Ni mbunge gani wa CCM anaweza kujitapa kuwa amepita bila nguvu za ufisadi? Sasa rais na wenzake wanapiga vita ufisadi gani wakati wenyewe wamepita kifisadi, na chama kimejaa wabunge waliopita kifisadi?

Ndiyo maana sisi wengine tunakwenda mbali. Tunasema katika igizo la sasa la kujivua gamba, Rais Kikwete na wenzake, kama wana ujasiri wa kutosha, wasiishie tu kuwafukuza kwenye vikao vya Kamati Kuu na Halmashauri Kuu.

Wawavue na ubunge. Wapoteze kila kitu. Tuanze upya. CCM igombee majimbo hayo bila nguvu ya rushwa. Je, CCM ina ujasiri huo?

Wapo wanaodokeza pia kwamba hata udhaifu binafsi wa rais kiafya ulichangia kupunguza imani na matumaini ya watu. Kwa mfano, madaktari wake walijaribu kufunika funika kwa taarifa zenye utata, lakini walishindwa kumzuia kuanguka hadharani mara kadhaa. Wanadhani hiyo ilikuwa mbinu ya kumwongezea kura?

Hizi ni chache tu, lakini zipo sababu nyingi za kuanguka kwa CCM katika uchaguzi uliopita. Hata maisha magumu yanayowakabili wananchi sasa hivi, ni kigezo kingine cha kuwahamasisha wananchi waichukie serikali na chama chake.

Ndiyo maana wenye akili wanapotazama kampeni hii ya kuvuana magamba wanasema bila woga kwamba tatizo la CCM si watu fulani, bali mfumo. Chama kimejikita katika mfumo wa ufisadi, kinaongoza kwa mazoea, kinakumbatia udikteta wa rais na mwenyekiti, na kinaogopa mabadiliko.

Mtu mmoja amenidokeza kwamba haikuwa kwa bahati mbaya Pius Msekwa kuteuliwa makamu mwenyekiti wa CCM. Ni Msekwa huyu aliyekuwa Katibu Mtendaji Mkuu wa CCM mwaka 1977.

CCM haina muono mpya, au damu mpya za kushika nafasi ya Msekwa katika chama? Maana yake ni kwamba CCM iko nyuma ya wakati kwa miaka 34.

Hii ndiyo CCM inayoshabikiwa na kina Nape waliozaliwa ndani ya kipindi cha u-CCM wa Msekwa?

Ndiyo maana wanashindwa kujivua gamba, maana wao wenyewe ni magamba manene yaliyoshikamana na nyama za chama. Wakidiriki kuyavua, wataondoka na mnofu wa CCM.

Lakini hili haliwezekani kwa sababu CCM bila ufisadi, haiwezi kudumu. Ninachoona ni kwamba, ingawa wanaogopa kujichuna ngozi ili wasife, jitihada wanazofanya sasa ni sawa na kunywa sumu kali ambayo haiwezi kuwaepusha na mauti ya kisiasa. Wanalijua hilo?



Wanasema "kisasi ni sawa na chakula ambacho ladha yake inaongezeka kinapokuwa kimepoa".Maana ya msemo huo ni kwamba kisasi kinamuumiza zaidi mkosaji pale mkosewa anapomvutia muda mkosaji hadi anasahau kuwa alishawahi kumkosea mtu,kisha mkosewa analipiza kisasi.Inakuwa kama kuchonokoa kidonda kilichokwishapona.

Lakini inaelekea Rais Barack Obama hakutaka kusubiri hadi Donald Trump asahau kuwa alikuwa kinara wa fitna kwamba Obama si raia wa Marekani.Na jana alipata fursa mwanana ya "kumfanyizia" tajiri huyo wa uwekezaji kwenye majengo.

Katika hafla ya kila mwaka ya Waandishi wa Habari wanaoripoti habari kutoka Ikulu ya Marekani ambapo mgeni rasmi huwa Rais,Obama alimrushia Trump vijembe vikali lakini katika hali ya utani,kama ilivyo desturi ya halfa hiyo.

Hikuwa siku nzuri kwa Trump aliyehudhuria hafla hiyo kwa mwaliko wa gazeti la Wahington Post.Alipowasili tu alikumbana na sauti za kuzomewa.Lakini alikuwa Obama aliyemnyong'onyeza tajiri huyo kwa vijembe vikali vya utani wenye ukweli.

Obama alimkebehi Trump kwa kijembe kwamba ana furaha suala la wanaodadisi uraia wake sasa limekwisha kwahiyo Trump atapata wasaa wa kuchunguza kama kweli wataalamu wa anga walifika kweli mwezini,na iwapo Tupac na Biggie (Notorious B.I.G) kweli waliuawa.

Lakini kimbembe kwa tajiri huyo hakikuishia kwa vijembe vya Obama pekee kwani mchekeshaji maarufu Seth Meyer hakubaki nyuma katika "kummaliza" Trump.Alimgalagaza kwa kutanabaisha kuwa "Donald Trump amekuwa akieleza kuwa atagombea urais kwa tiketi ya chama cha Republican,jambo ambalo ni la kushangaza...nilidhani jambo pekee analoweza kugombea ni kuwa kituko".

Kadhalika,Obama aliwatania pia baadhi ya wagombea urais watarajiwa wa Republicans kwa kusema tetesi zinaonyesha kuwa Michelle Buchmann,mwanamama kipenzi cha wahafidhana wa Tea Party Movement,alizaliwa Canada na sio Marekani (na kumkumbusha kuwa majungu huwa yanaanza kihivyo).Pia alimtania mgombea mwingine mtarajiwa Tim Pawlenty kwa kudai amesikia kwamba jina kamili la mwanasiasa huyo ni Tim HOSNI Pawlenty (akimaanisha pengine ana asili ya Misri kwa akina HOSNI Mubarak).

Sio siri.Kwa mara ya kwanza kabisa nilimwonea huruma Trump alipokuwa akipigwa vijembe na Obama na Meyer huku ukumbi ukilipuka kwa mayowe.Lakini ndio hivyo,mkuki mtamu kwa nguruwe lakini kwa binadamu mchungu.

Angalia clip ifuatayo kisha jiburudishe kwa video za Tupac na Biggie (kwa vile walitajwa katika hafla hiyo)




Mimi ni Rais wenu,na huyu ndiye mwanangu mpendwa ninayependezwa na ufisadi,oops..ujasiriamali wake

na Mwandishi wetu

RAIS Jakaya Kikwete anakabiliwa na kashfa nzito kutokana na utajiri wa mtoto wake, Ridhiwani. Sasa anatuhumiwa kuitumia Ikulu kumtajirisha mwanawe, ambaye anasemekana ni bilionea.

Kwa nyakati mbalimbali, ukwasi wa mtoto huyo wa rais uliibuliwa na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa na Mwenyekiti wa Chama cha Democratic (DP), Mchungaji Christopher Mtikila.

Katika moja ya mikutano yake ya hadhara hivi karibuni mkoani Tabora, Dk. Slaa alisema Ridhiwani amemaliza shule miaka michache iliyopita, lakini hivi sasa ni tajiri bilionea na kwamba ameupata utajiri huo katika mazingira ya kutatanisha.

Jana Mtikila alizungumza na waandishi wa habari katika Hoteli ya Travertine, akidai Ridhiwani amegeuka bilionea kwa muda mfupi “kwa mgongo wa baba yake.”
Akibainisha zaidi uwezo wa kifedha wa kijana huyo, Mtikila alisema hivi karibuni mtoto huyo ambaye ni Mjumbe wa Baraza Kuu la Umoja wa Vijana (UVCCM), aliingiza magari makubwa ya mizigo aina ya “semi trailer” zaidi ya 100 na kudai kuwa yanafanya kazi ya kusomba mizigo DRC na mengine ameyauza.

Alidai pia mtoto huyo wa rais anamiliki makampuni ya ujenzi wa barabara na maeneo mengi ya ardhi kwa lengo la kujenga maghorofa ya kupangisha.

“Huyu ni mtoto mdogo, kamaliza shule juzi, pesa za utajiri wote huu kazipata wapi?” alihoji Mtikila.

Hata hivyo, wiki iliyopita, Ridhiwani alikaririwa na moja ya vyombo vya habari akisema kuwa yuko tayari kutoa ushirikiano kwa Dk. Slaa kuonyesha kila anachomiliki.

Kutokana na tuhuma hizo, Mtikila alimtaka Rais Kikwete naye ajivue gamba kwa kuonyesha mfano, vinginevyo ni uendawazimu kujivua gamba bila mkuu huyo wa nchi kujiuzulu urais na uenyekiti wa CCM.

Huku akionekana kuwatetea Edward Lowassa (Monduli), Andrew Chenge (Bariadi Magharibi) na Rostam Aziz (Igunga), Mtikila alisema Kikwete anawachezea wana CCM na Watanzania kwamba ana nia ya kuwatimua makada hao kwa madai kuwa ni mafisadi wakati yeye ni mshirika wao.

“Kikwete aanze kutoka yeye ndipo awanyoshee vidole hawa Mapacha Watatu alioshirikiana nao kwenye ufisadi wa EPA, Richmond na Dowans, vinginevyo anawadanganya Watanzania. Aanze yeye,” alisema Mtikila.

Alisema anashangazwa na Kikwete kuibuka na dhana ya kujivua gamba kwa kuwatosa marafiki zake watatu wakati chama hicho kina mafisadi lukuki.

Mchungaji Mtikila pia aliorodhesha miradi ya ufisadi aliyomhusisha nayo Kikwete na watendaji wengine serikalini kuwa ni pamoja na IPTL, uuzaji wa iliyokuwa Benki ya NBC, Meremeta, Richmond, Dowans, EPA na nyingine, kwamba zinawahusu watendaji wengi na si mapacha watatu pekee.

”Kikwete aliunda tume kubaini waliochota fedha za EPA na kutakiwa warudishe, lakini hadi sasa hatujui kina nani wamehusika, na kiasi gani cha fedha kilichorudishwa. Kama rais hahusiki na ufisadi huu, usiri wa nini?” alihoji Mtikila.

Alisisitiza kuwa hana maana kuwa Lowassa, Rostam na Chenge ni wasafi, bali anataka orodha ya kuwatimua mafisadi wa CCM iwe kubwa, akiwamo Rais Kikwete kwani ndilo gamba kubwa kuliko yote.

Kuhusu hatima ya CCM na kile alichokiita usanii wa kujivua gamba, Mchungaji Mtikila alisema chama hicho kina ugonjwa wa ‘Nambulila’ ambao mgonjwa hufa na kuzikwa akijiona.

“Wapangwa wana ugonjwa unaitwa Nambulila. Ni ugonjwa unaotokana na tego la mke. Mtu akitembea na mke wa mtu anaupata na anapokufa, anawaona watu wanavyomlilia, wanavyomuingiza kwenye kaburi, lakini hana uwezo wa kusema, hivyo anazikwa akiwa hai, akiona kila kitu. Ndivyo ilivyo CCM, inakufa ikijiona. Hii ndiyo Nambulila,” alisema Mtikila.

Alisema usanii wa kujivua gamba hauwezi kuinusuru CCM kwani ni dhana ya uendawazimu yenye lengo la kuwaghilibu Watanzania.

Sambamba na hilo, Mtikila aliwataja mawaziri wakuu wastaafu, Frederick Sumaye, Joseph Warioba na Cleopa Msuya, kuwa ni miongoni mwa watu wachache wasafi ndani ya CCM.

Alipobanwa kueleza usafi wa Sumaye wakati miaka sita iliyopita alipata kumtaja kwamba ni fisadi namba moja, Mtikila alikiri kutoa kauli hiyo na kuongeza kwamba baada ya kufuatilia walibaini kashfa dhidi yake zilikuwa za uongo na zilipikwa ili kumrahisishia Kikwete njia ya kuwa rais.

“Kweli niliwahi kumtaja kama fisadi namba moja, tulipofuatilia tulibaini kwamba haikuwa sahihi na ndiyo maana leo namtaja kama mmoja ya viongozi wachache wasafi,” alisema.

Aliwataka wana CCM kutobeza ushauri wa viongozi hao wachache wasafi na kutolea mfano wa Warioba na Sumaye walivyoshambuliwa na UVCCM walipotoa mawazo yao.




Opinion by Jerome McCollom
(8 Hours Ago) in Society

President Obama, in far beyond what he is legally required to do, released his long-form birth certifiate from the state of Hawaii. He had already released the short-form certificate, the one that Hawaii gives to those born there, and which was already good enough to get issued a U.S. passport.

Who takes credit, well Donald Trump. See, Trump wants attention, and he says he is going to run for the presidency, and to do so he is trying to attract birther support. Well, Trump had stated before Obama released the long form in an interview with Meredith Vieira.

DONALD TRUMP:

" …You are not allowed to be a President if you are not born in this country. He may not have been born in this country, and I tell you what: three weeks ago I thought he was born in this country — right now I have some real doubts. I have people that actually have been studying it, and they cannot believe what they’re finding."

MEREDITH VIEIRA:
"You have people now, down there, searching, I mean in Hawaii?"

DONALD TRUMP:
"Absolutely. Absolutely, and they cannot believe what they’re finding."

When George Stephanopoulos asked him about these supposed investigators, after Obama's release of the original birth certificate, The Donald responded, "That’s none of your business right now.”

What?! The Donald runs for the presidency by saying he has investigators who "cannot believe what they are finding', and now that isn't a concern? Who are these incompetent investigators on Trump's payroll? Because he sure needs to say you're fired to them, if anyone. Look at the ego on a man who gets angry that anyone dare question or point out that either he has incompetents/liars on his payroll or that he was lying himsef. Actually, it is pretty clear that Trump lied about this.

Or, maybe he was just believing the blather of one of those birthers writing books attacking Obama as a non-citizen, the Jerome Corsis and Joseph Farahs of the birther movement The Donald is actually taking credit for his absurd crusade to get Obama to release a certificate that wasn't necessary to prove he was a citizen, because Obama already released the short form version that the state of Hawaii releases to everyone. We don't need an energy solution in America, we need just to power our electronics and lights from the hot air that is Donald Trump.



Donald Trump -- star of NBC's birther movement "Celebrity Apprentice" -- decided to show his hair, er, face at the White House Correspondents' Association Dinner on Saturday.

Trump, who began the week taking credit for the White House's decision to release President Obama's birth certificate, was promptly booed on arrival.

Trump arrived on the red carpet at Washington’s Hilton Hotel with his wife, Melania, shortly at 7:00 p.m. (ET). After giving a brief interview with a group of several of media outlets, Trump -- who was invited to the event as a guest of the Washington Post -- walked away to a chorus of audible boos from the media members on the press line. (And it wasn't because they wanted to hear Trump talk more.)

Trump's entrance briefly took the spotlight away from the other celebrity arrivals, including Mila Kunis, Scarlett Johansson, Sean Penn, David Arquette, Elizabeth Banks, Erin Andrews, Mira Sorvino, Jeremy Piven and at least one of the Wayans Brothers.

Obama and his wife are scheduled to arrive at the 8 p.m. (ET).

I didn't see New Yorker editor David Remnick -- who earlier this week called Trump a "race-baiting, irrepressible jackass" [4] -- but Zach Galifianakis, Jon Hamm and the Coen Brothers were among the guests invited to sit alongside him at the magazine's table.

There was some question whether Trump would attend the dinner at all -- though not because of the "birther" controversy. Trump was also scheduled to attend the wedding of fellow real estate mogul (and noted Obama hater) Steve Wynn in Las Vegas on Saturday, and delivered an expletive-filled speech [5] there on Thursday.

Guessing there may be more than a few of those muttered at tonight's so-called "nerd prom" -- and plenty of firesworks in store.




VATICAN CITY — Pope John Paul II moves a step closer to sainthood on Sunday when his successor beatifies him before an expected crowd of several hundred thousand people. Pilgrims from all over the world, many from the pope's native Poland, have flocked to Rome to witness the beatification mass and take part in the biggest event in the Italian capital since the late pope's funeral in 2005.

Groups carrying national flags and singing songs have gathered over the weekend where the ceremony will take place, in St Peter's Square, which is bedecked with posters and photos of the late pope.

Up to 200,000 people attended a prayer vigil on Saturday evening in the Circus Maximus, the huge oval once used by the ancient Romans for chariot races. Some Rome churches threw their doors open all night to give pilgrims a space to pray.

John Paul's successor Pope Benedict XVI will pronounce a Latin formula on Sunday declaring one of the most popular popes in history a "blessed" of the Church.

A place of honor is reserved for Sister Marie Simon-Pierre Normand, a French nun who suffered from Parkinson's disease but whose inexplicable cure has been attributed to John Paul's intercession with God to perform a miracle, thus permitting the beatification to go ahead.

The Vatican will have to attribute another miracle to John Paul's intercession after the beatification in order for him to be declared a saint.

Some 90 official delegations from around the world, including members of five European royal families and 16 heads of state, will attend the beatification.

They include Zimbabwean President Robert Mugabe, who has been widely criticized for human rights abuses in his country. Mugabe is banned from traveling to the European Union, but the Vatican – a sovereign state – is not a member of the bloc.

Coffin on display

Pope John Paul's coffin was exhumed on Friday from the crypts below St Peter's Basilica and will be placed in front of the main altar. After Sunday's beatification mass, it will remain there and the basilica will remain open until all visitors who want to view it have done so.

It will then be moved to a new crypt under an altar in a side chapel near Michelangelo's statue of the Pieta. The marble slab that covered his first burial place will be sent to Poland.

John Paul's beatification has set a new speed record for modern times, taking place six years and one month after his death on April 2, 2005.

While the overwhelming number of Catholics welcome it, a minority are opposed, with some saying it happened too fast.

Liberals in the church say John Paul was too harsh with theological dissenters who wanted to help the poor, particularly in Latin America. Some say John Paul should be held ultimately responsible for the sexual abuse scandals because they occurred or came to light when he was in charge.

Ultra-Conservatives say he was too open toward other religions and that he allowed the liturgy to be "infected" by local cultures, such as African dancing, on his trips abroad.

The pope is being beatified on the day the Church celebrates the movable Feast of Divine Mercy, which this year happens to fall on May 1, the most important feast in the communist world.

The coincidence is ironic, given that many believe the pope played a key role in the fall of communism in Eastern Europe. 

 SOURCE: GMA News

30 Apr 2011



Kuna wapuuzi wanajaribu kutuminisha usanii unaoitwa "kujivua magamba" kwa chama tawala CCM kilichozaa serikali iliyopo madarakani.Lakini hata tukiweka kando ukweli kwamba nyoka anayejivua magamba anakuwa hatari zaidi kuliko awali,porojo hizi za kuchefua za CCM ni miongoni tu mwa jitihada zake kuwapumbaza Watanzania kuhusu matatizo ya msingi yanayotishia uhai wa taifa letu.

Wakati akili za Watanzania zimeelekezwa Samunge "kwa Babu wa Loliondo" na "magamba" ya akina Lowassa,Chenge na Rostam,mafisadi wanaitumia vizuri nafasi hiyo kubaka uchumi wetu kwa kasi ya kimbunga.Hebu angalia habari zifuatazo ambazo ni mwendelezo tu wa mkakati wa kuiflisi Tanzania yetu.

CAG abaini ufisadi wa Sh50 bilioni serikalini

Saturday, 30 April 2011 10:00

Boniface Meena

MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), amebaini ufisadi wa Sh50.6 bilioni serikalini ukiwamo wa malipo yanayotia shaka ya Sh15.7 bilioni katika kipindi cha mwaka wa fedha 2009/2010.

Katika ripoti yake ya ukaguzi iliyoishia Juni, 30, 2010, CAG amesema fedha nyingi zilitumika kufanya ununuzi bila kufuata taratibu.

Katika ripoti yake, amesema wizara, idara, wakala na sekretarieti za mikoa, zilitumia fedha katika kipindi cha mwaka 2009/2010 kufanya ununuzi ambao haukuwa kwenye mpango wa mwaka.

Alisema matumizi hayo ni kinyume cha kifungu cha 45 cha Sheria ya Ununuzi ya Umma ya mwaka 2004 kinachozitaka taasisi za ununuzi kuweka mpango wa mwaka kwa lengo la kuepuka ununuzi wa dharura, kupata thamani ya fedha, kupunguza gharama za matumizi na kufanya ununuzi sahihi kwa njia ya kandarasi.

"Ukaguzi umebainisha kwamba katika mwaka wa fedha 2009/2010, taasisi zilizoonyeshwa hapa chini zilifanya ununuzi yenye thamani ya Sh50.6 bila kufuata kifungu cha sheria," imeeleza sehemu ya ripoti hiyo.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo, kati ya fedha hizo, Sh650.7 milioni zilitumika katika Ofisi ya Makamu wa Rais, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto, kununulia samani kwa maofisa wanaoishi katika nyumba binafsi

Wizara nyingine ni Nishati na Madini, Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Maliasili na Utalii, Habari, Vijana na Michezo na Tume ya kurekebisha Sheria.

"Ununuzi wa samani kwa maofisa hao ulikuwa si sawa kwa kuwa hawana stahili ya kununuliwa vitu hivyo na ni kinyume cha waraka wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma (Utumishi) Na. C/CA/134/213/01/G/69 wa Januari 30, 2006, unaohusu malipo ya posho ya nyumba na ununuzi wa samani kwa nyumba za Serikali kwa maofisa wenye stahili," imesema ripoti hiyo.

CAG ameeleza pia kuwa eneo jingine ambalo fedha hizo zimetumika vibaya ni matengenezo ya magari ya serikali na taasisi zake ambako Jumla ya Sh176.7 milioni zimeliwa.

Alisema wakati kanuni ya 5 ya Kanuni za Ununuzi wa Umma (mali, kazi, huduma zisizo za ushauri na uuzaji wa mali ya umma kwa zabuni) ya mwaka 2005, ikitaka wizara, idara, wakala na sekretarieti za mikoa kutengeneza magari yake Temesa (Wakala wa Ufundi na Umeme), au kupeleka katika karakana zilizoidhinishwa na wakala huyo, magari mengi yalikuwa yanatengenezwa kwenye karakana binafsi.

"Magari hayo yametengezwa kwenye karakana hizo bila kuwa na kibali kutoka Temesa kama sheria inavyotaka."

CAG amebaini pia kuwa serikali na taasisi zake imetumia Sh13.8 bilioni kulipia mali na vifaa ambavyo hata hivyo, havikupokewa au vilipokewa pungufu.

"Hii ni kinyume na kanuni ya 122 ya kanuni za Ununuzi ya Umma (mali, kazi, huduma zisizo za ushauri na uuzaji wa mali ya umma kwa zabuni) ya mwaka 2005," alisema.

Taarifa hiyo ilisema katika kipindi cha mwaka wa fedha 2009/2010, wizara, idara, sekretarieti za mikoa mitatu zilifanya malipo yenye shaka yanayofikia Sh15.7 bilioni.

Malipo hayo yalikosa viambatanisho ambavyo vingeonyesha taarifa za kina pasipo kuacha shaka yoyote kuhusiana na usahihi wa malipo hayo.

CHANZO: Mwananchi

Mamilioni yafujwa Mambo ya Nje

na Mwandishi wetu

WIZARA Ya Mambo ya Nje na Ushirikinao wa Kimataifa imegumbikwa na ufisadi mkubwa wa upotevu wa mamilioni ya dola katika ubalozi wake wa heshima nchini Israel na ubalozi wa Marekani.

Imebainika kuwa dola za Marekani milioni 615 zimeyeyuka katika ubalozi wake Israel na hivyo jana kuifanya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali kumuweka kiti moto Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Hayo yalibainika jana katika kikao cha pamoja cha Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC), kilichoketi chini ya mwenyekiti wake, John Cheyo, ambaye alihoji matumizi ya fedha hizo ambayo yalipingana na ripoti ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).

Cheyo, alisema mwaka 2008/2009 imeonekana katika ubalozi huo kupotea kwa kiasi hicho cha fedha hasa katika utoaji wa viza na kutotolewa risiti kwa wahusika.

“Hapa inaonyesha Balozi wa heshima Madam Rinit Hershkovity wa Israel alitumia fedha za serikali vibaya na kamati yetu inahitaji kupata maelezo ya kina inakuaje kiasi cha dola milioni 615 za Marekani kupotea katika mazingira ya kutatanisha.”

“Hii kamati si ya kuchezea hasa katika kudai matumizi ya fedha za walipa kodi wa nchi hii sasa tunahitaji majibu mazuri na hatua zilizochukuliwa juu ya mtu huyu aliyefanya ufisadi wa aina hii,” alisema Cheyo.

Akijibu maswali hayo Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya nje na ushirikiano wa Kimataifa, John Haule, alisema serikali ilipogundua ubadhirifu huo ililazimika kuufunga ubalozi huo toka Februari 2, mwaka 2009 na kumtaka balozi huyo kurejesha fedha hizo.

Haule, alisema kwa kuwa yeye ni mgeni katika wizara hiyo amegundua kukabiliwa na changamoto ya kuweka mahesabu sawa ikiwemo kupambana na matumizi mabaya ya fedha za umma.

“Mwenyekiti mimi ni mgeni toka niripoti wizarani; nina siku 21, lakini hivi sasa tumefanikiwa kuufunga ubalozi wa heshima wa Israel; hata hivyo bado ninakiri kuwa nina kazi ya kurekebisha mifumo ya fedha na utendaji wa kazi,” alisema Haule.

Majibu hayo ya Katibu Mkuu Haule, yalimuinua Mbunge wa Kibiti, Abdul Marombwa (CCM), ambaye alitaka kufahamua matumizi ya kiasi cha cha dola za Marekani 7,600,000 zilizotolewa kwa ajili ya kununua jengo la ghorofa sita nchini Marekani kwa kiasi cha dola 10.4 milioni.

Alisema ripoti ya watalaamu ilionyesha kuwa badala ya kufanya kazi hiyo wizara iliagiza kutumika kiasi cha dola milioni 151.0 huku kukiwa hakuna haja ya kufanya hivyo.

“Ripoti hiyo ilibainisha kazi iliyofanyika sio ukarabati bali ni kukata vyumba… sasa kwa hili tunahitaji maelezo ya kina, na hatua zote hizo hakuna kibali kilichothibitisha matumizi ya fedha hizo wala uhalali wa matumizi hayo,” alisema Marombwa.

Hata hivyo hali hiyo ilimfanya katibu mkuu wa wizara ya mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa kumwachia naibu katibu Mkuu wake kutoa maelezo ya kina kwa kamati hiyo ambaye alisema kuwa hivi sasa wanalazimika kuzifunga balozi nyingi za heshima kutokana kutokuwepo udhibiti.

Kwa mujibu wa ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), inaonyesha kuwa zaidi ya euro 144,202 hazijalipwa kwa mujibu wa jalada namba TZBR/A.20/11 la Agosti 26, 2009 na kuonyesha kuwa deni hilo bado halijalipwa hadi sasa.

Balozi ambazo zimekumbwa na upotevu wa fedha na kuthibitishwa na CAG ambazo hadi sasa hazijatoa maelezo ya kina kuhusu matumizi yake ni pamoja na Italia waliotakiwa kurejesha kiasi cha sh 6,060,519.00 ambapo wahusika walitakiwa kufanya hivyo.

Mbali na upotevu wa fedha hizo kati ya mwaka 2007/2008 ubalozi ulitakiwa kuwasilisha kibali cha ukaguzi na kufanya matuzi ya sh 517,741,802 zilizotumika kinyume cha sheria


Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.