18 May 2011


He has been enjoying his freedom to travel back to the UK of late.

And upon his return to London Snoop Dogg looked right at home, conducting a press conference from a gold throne and surrounded by scantily-clad pole dancers.

The rapper played host to the UK media in a strip club yesterday to promote his new album Doggumentary during his second trip to the UK since the ban was lifted.

Snoop Dogg strolled in to the press conference in a sky blue Adidas tracksuit and sipped on tea from a Union Jack mug.



'I'm grateful for being here and proving to the authorities that I deserve to be here. I have had so much love and support from the UK,' The 39-year-old said told the Daily Star.

'When I was a young rapper I would dream of coming here, and when I came I didn't want it to end.'
Snoop Dogg, real name Calvin Cordozar Broadus Jr, was banned from entering the UK following a brawl between his entourage and security at Heathrow airport in 2006.

The following year the Home Office prevented him from obtaining a visa to enter the country with fellow rapper P Diddy, claiming allowing him in the UK could inspire violence and crime amongst fans, despite that his intention was to hold a seminar for youths against gun crime and gang violence.

A judge ruled in 2008 that Snoop had not been at fault during the incident and that he had actually cooperated fully with immigration officials - the ban was fully overturned last year in time for Snoop to play Glastonbury over the summer.

The What's My Name hitmaker is looking forward though, and yesterday announced plans to create his own X Factor-style show.

'X Factor is great but I need to do a show that goes straight to the hood,' he told reporters.

I want to find that raw untamed talent that hasn't been dressed up all nice for the TV. 'Any TV companies want to help me, then they know where I am,' he added.

The competition would feature artists 'with no money, just raw talent and natural ability.'
Snoop Dogg received a warm welcome from fans at a gig later that night before heading to Madame JoJo's and then The Box in Soho.

Earlier this week Snoop performed in Brighton as part of his promotional tour for Doggumentary.


The album features guest performances by Kanye West, David Guetta and also Willie Nelson. At the press conference the rapper named Sade as his ultimate collaborator.

He also defended a more controversial collaboration - his recent record with Charlie Sheen, 'Winning' which was released earlier this month.

'Sheen was my friend before all this happened so I do not judge him,' Snoop Dogg insisted. 'He called on me and I came through for him.

'He is conducting his business, living and functioning. But if the station (CBS, the network behind Two And A Half Men) wanted to put him in a box, then what would have been crazy is staying in that situation.'



Hasheem Thabeet afanya.....

Na Brighton Masalu

STAA wa mpira wa kikapu, duniani akicheza katika Ligi ya NBA nchini Marekani, Hasheem Thabeet Manka ‘Super Tall’ (pichani) amefanya kufuru ya fedha baada ya kumwaga fedha ukumbini na kuwaacha watu wagombanie, twende mstari kwa mstari.

Paparazi wa gazeti hili lenye heshima ya nyota tano kwa habari za mastaa Bongo, alishuhudia tukio hilo live wikiendi iliyopita katika Ukumbi wa Bilicanas uliopo Posta, jijini Dar es Salaam ambapo handsome boy anayecharaza fimbo katika muziki wa kizazi kipya, Abdul Sykes ‘Dully Sykes’ alikuwa akipiga shoo babkubwa.

Awali kasuku wa gazeti hili alimshuhudia Hasheem akikatiza kwa madaha ukumbini humo, akiwa ameongozana na wapambe wake waliokuwa wakimuandalia njia, kisha kukaa sehemu moja na kuanza kula bata kwa mtindo wa ‘tingisha kama imeisha, leta nyingine’.

Wakati shoo ikiendelea Hasheem aliinuka na wapambe wake kuongoza mbele kama kawa, kisha wakaelekea jukwaani alipochomoa burungutu moja la ‘nyekundu nyekundu’ tupu na kumkabidhi Dully Sykes ambaye aliongeza manjonjo baada ya kutuzwa na supastaa huyo.

Hakuishia hapo, aliposhuka jukwaani, alizama mfukoni na kutoa burungutu lingine kisha akalirusha juu na mashabiki kuanza kugombania.

Wakati watu wakiendelea kukanyagana wakigombea mkwanja huo wa ‘sadakalawe’ Hasheem na wapambe wake walitoka nje na kuingia kwenye gari aina ya Hummer na kuondoka kiwanjani hapo.

“Duh! Ebwana ee, jamaa huyu ni noma yaani minoti yote hiyo kaiachia watu wanyang’anyane? Hii ni kufuru, kweli mshkaji fedha imemkubali,” alisika jamaa mmoja akisema ukumbini hapo.

Hasheem Thabeet amerejea nchini hivi karibuni akitokea Marekani anapoishi, yupo kwa mapumziko mafupi. Ni Mtanzania pekee anayeipeperusha bendera ya Tanzania kwenye ligi ya NBA ya mpira wa kikapu nchini humo.

Na yafuatayo ni maoni ya wasomaji wa gazeti hilo

Comment by Eddie Mourice Junior 1 hour ago
Kwa hili umechemka hasheem even if ur money!
Comment by KUU LA MAADUI 7 hours ago
Dogo pesa ni zako lakini kwa hii ya leo umetimba ,sikujua kama na wewe bado mgeni na pesa aise kwa nini unafanya hivyo hujui kama anaweza kufa mtu katika kugombania minoti halafu wewe ukastakiwa kwa kusababisha vifo ,aise umeniuthi unakuwa mrefuuu 22222222 nje ndani mfupi acha ulimbukeni najua hata ndugu zako hawata fuhia upuuzi huo,kama unapesa unakuwasha utumie katika mambo mazuri mungu atakubariki sio kurushia walevi.
Comment by Minja Frank 7 hours ago
Ona mwenzio mwenye kipaji cha mpira wa kikapu kama wewe Dikembe Mutombo wa DRC kajenga Hospital kubwa tu Kinshasa. Wewe wamwaga pesa yako kwenye masanga. Saidia nchi yako!!!
Comment by Alphoncene Gerald 8 hours ago
Sina hata cha kuchangia
Nachoka kabisa
Comment by Miriam John Mndolanga 8 hours ago
Ulivyofanya ndivyo nafsi yako ilivyokutuma, kwa upande wako ni sawa tu ila ni vema hela unayoitolea jasho na kusumbuka sana hadi kuipata ungeiwekeza kwa makundi yenye mahitaji maalum na Mungu atakubarikia zaidi ya ulichotoa. Jifunze kupitie kwa waliofanya kama hivyo wameishia wapi?
Badilika Hasheem, usijijengee sifa mbaya kwa jamii yako.
Comment by julius manning 8 hours ago
huo ni ulimbukeni mkubwa akumbuke akina Tyson walikuwa na hela kuliko yeye lakini leo je
Comment by swalih/waziri 8 hours ago
huo niulimbukieni wakati familia nyengine pesa yakula mtihani wewe pesa unazigawa kwa walevi inshlwa mungu akulaani uje kuzikumbuka sikatowe misaada makanisani msikitini na mashuleni wewe unagawa kwa walevi ili upate jina kuwa umegawa pesa<.
Comment by Matu 8 hours ago
Pesa ni sabuni ya roho lakini pesa nazo zina upepo wake...wakati ukuta...pesa ni kama maua..huchanua na kusinyaaa kwa mtoto wa manka sasa zimechanua...!
Comment by anna [email protected] 8 hours ago
Ama kweli masikini akipata matako huria mbwata, hivi wewe umesahau tabu zote ulizopita, haya baba wakati wako hivi humuoni mwenzio yule modo anaitwa matata kila mwaka anatoa msaada kwa yatima wewe unagawa pesa kwa walevi, una akili nyingi sana mtoto wewe, ina maana hata kule kijijini kwenu huna wanaohitaji msaada, utakuja juta baadae na hao wapambe huta waona sana watakucheka, wapi nice??? unalewa sina
Comment by ikk 8 hours ago
Kweli minoti unaigawa kwa watu wenye ziada tele, tena Klabu? Wakati kuna watoto yatima huko makete wanalea wadogo zao, tena kwa kupika pombe za kienyeji?
Laana huanza polepole!
Comment by Sebastian Salatiel Shemhilu 9 hours ago
DUUH!! HII NI DHARAU YA FEDHA AU JEURI YA FEDHA? HASHEEM TOA PESA ZAKO KWA YATIMA KULIKO KUWAPA PESA WALEVI NAMNA HIYO.MUNGU ATAKUPA ZAIDI.

Comment by Mapresha Getebariadi 9 hours ago
Hela iko wapi wenye fedha hawafanyi hivyo hapo alikuwa anawachanganya warembo waanze kujimwaga kwake. Kama anahela si asomeshe hata yatima 2 tu.
Comment by edmas 9 hours ago

Haya bana, wakati wako huu. Alikuwepo Mr. Nice naye alifanya kufuru ya pesa, sasa yupo apeche alolo, kushnei.
Comment by furaha Tausi 9 hours ago
WEE HASHEEM WEWE KWANINI HIYO HELA USIWASAIDIE HATA WATOTO WA MITAANI JAMANI HATA WALE WATOTO WALIOKO OCEAN ROAD HOSPITAL WANAUMWA KANSA?? MUNGU ATAKULAANI SHAURI YAKO

16 May 2011



Wasaidizi wana nafuu kuliko rais?

Ansbert Ngurumo

BAADHI yetu hatujaelewa ari, nguvu na kasi ya Rais Jakaya Kikwete. Nina hakika naye ameiimba, lakini hajaielewa barabara.

Kaulimbiu hii iliyoasisiwa na kina Samuel Sitta mwaka 2005, ilitumika kumtafutia urais mgombea wa CCM, Jakaya Kikwete, kwa ari mpya, kasi mpya na nguvu mpya.

Waliomjua vema uwezo na udhaifu wake walidokeza mapema kwamba maisha ya Watanzania chini ya CCM ya Kikwete yangedorora na kuwa magumu zaidi - kwa ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya.

Baadaye, sisi na baadhi ya watani wa CCM tuliifupisha kaulimbiu hiyo, tukaiita ANGUKA. Ni kweli! Miaka mitano baadaye, wameangukia pua.

CCM imeanguka. Rais Kikwete ameanguka. Mtandao wake umeanguka. Na kwa bahati mbaya, hata serikali yake imeanguka, ikaishia kuwa serikali kopa-kopa – hata mishahara ya watumishi – licha ya kodi kubwa tunazolipa.

Kuanguka huku, ndiko kumekuwa chanzo cha kura chache za mgombea urais wa CCM katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010. Kuanguka huku ndiko kumekuwa kichocheo cha vilio vya wananchi dhidi ya ufisadi. Kuanguka huku ndiko kumesababisha hata usanii mpya wa CCM wa ‘kujivua gamba.’

Kuanguka huku ndiko kumemkosanisha Rais Kikwete na maswahiba wake wa siku nyingi. Kuanguka huku ndiko kumemfanya Rais Kikwete aogope maandamano ya wananchi yanayoratibiwa na CHADEMA hata akalialia kwamba “wanataka kuniondoa kabla ya wakati.”

Kuanguka huku ndiko kumemwondoa Yusuf Makamba katika ukatibu mkuu wa CCM, yeye na sekretariati na Kamati Kuu. Kuanguka huku ndiko kumerutubisha na kukuza fitina na vita ya makundi ndani ya CCM.

Kuanguka huku ndiko kumewafanya Watanzania kuikataa CCM waziwazi kuliko wakati wote katika historia, na ndiko kumemwingiza Nape Nnauye (Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM) katika migogoro mipya ndani ya makundi ya CCM na kumwandalia anguko lake huko tunakokwenda, hasa baada ya Rais Kikwete kuondoka madarakani.

Anguko hili la ari mpya, kasi mpya na nguvu mpya limewagusa wananchi wenyewe. Sasa wanakabiliwa na ukali wa maisha usiofanana kabisa na ahadi kemkemu walizopewa na CCM mwaka 2005 na 2010.

Bahati mbaya waliosababisha anguko hili, bado wanajitapa kwamba wameleta maendeleo. Vipofu!

Na kwa sababu ya upofu huu, wanakosa mikakati mipya ya kujikwamua. Wanarudiarudia yale yale yaliyoshindwa kuwanusuru miaka mitano iliyopita.

Kwa mfano, mwaka 2006 mwanzoni, Rais Kikwete aliingia na mbinu ya kutembelea wizara moja moja, kutoa maelekezo na kupiga picha na watumishi wa wizara hizo. Ilikuwa propaganda na mapambo ya magazeti na televisheni.

Baadaye, aliwaita mawaziri na watumishi waandamizi wa serikali (mara mbili) katika semina elekezi kwenye Hoteli ya kifahari, Ngurdoto, Arusha.

Leo tunapotazama nyuma, ni nani anaweza kujivunia semina elekezi za Ngurdoto?

Lakini watu wasiojifunza hawafichiki. Mwaka jana, rais yule yule akagombea kwa kaulimbiu ya ari zaidi, kasi zaidi na nguvu zaidi. Yaani, hawa jamaa hawakuridhika na ’anguko jipya’ la 2006. Waliona hilo halitoshi, wakatuandaa “kuanguka zaidi” mwaka 2010!

Haikumwongezea kura mgombea wao. Haikuvuta hisia za vijana wala kina mama. Ili kupata watu wa kuhutubia ilibidi CCM itumie pesa nyingi kuchapisha na kugawa sare, kuwagawia watu na kuwapakia kwenye magari kuwapeleka kwenye mikutano ya mbali.

Haikuwaunganisha watawala wawe na sauti moja, hata baada ya kurejea madarakani. Haikuwasaidia kupata hekima ya kumaliza matatizo ya muda mrefu, kama ukosefu wa umeme ambao umezungumzwa tena na tena bila ufumbuzi.

Sasa kwa ari zaidi, nguvu zaidi na kasi zaidi, watawala wamerudi tena katika semina elekezi, chini ya mwelekezaji yule yule.

Walidhani zile zilishindikana kwa sababu zilifanyika Arusha. Sasa wamekimbilia Dodoma. Kwa wiki nzima, serikali iko Dodoma, imelala; inakula posho. Kazi zinakwama.

Rais naye, badala ya kuwaelekeza kwa hekima na ustadi, “akawananga” wasaidizi wake hadharani, kana kwamba huwa hapati fursa ya kukutana nao – wakati amekuwa akikutana nao kila mwezi katika vikao vya Baraza la Mawaziri. Ndio hao aliowatembelea na kuwasema wizarani kwao miezi miwili iliyopita, hata akawaamuru wengine waache ubabe.

Alitaka kuonewa huruma. Alitaka kuwashitaki kwa wananchi – waonekane wabaya, awe mzuri.

Rais anawasema mawaziri wake kama watoto wadogo wanaohangaika kuelewa kitu kidogo anachowafundisha. Anawaonyesha wananchi kwamba ana mawaziri mizigo, mbumbumbu – ambao kazi pekee wanayofanya ni “kumwangusha” rais.

Anataka turudi kwenye propaganda za kijinga walizoimba miaka mitano iliyopita, kwamba rais pekee ndiye anachapa kazi, bali mawaziri wake wanamwangusha.

Anawaambia mawaziri wake kuwa kama hawawezi kazi “waondoke,” kana kwamba hajui uwezo wao, hajui waliingiaje, wakati ndiye aliyewateua na ndiye ana mamlaka ya kuwaondoa.

Anataka “watoke” waende kwa wananchi kufafanua mafanikio ya serikali yake. Haamini kwamba wananchi wana uwezo wa kuona mazuri na mabaya ya serikali – bila kusubiri taarifa za mawaziri.

Haoni kwamba serikali inayofilisika na kulazimika kukopa hata mishahara ya watumishi wake, inahitaji kubana matumizi na kupunguza ziara na posho nono za viongozi hao waandamizi.

Lakini pia, tunapowatazama watu wenyewe aliokuwa anawapa somo, tunabaki kujiuliza: Rais amepata wapi hekima hii ya kudhani ana uelewa mpana kuliko mawaziri wake?

Amesomea wapi huko wasikojua wao, alikopata hicho cha kuwafunda? Tunapowatazama baadhi yao tunagundua kwamba kama rais angekuwa na busara ya kujifunza kutokana na miaka mitano iliyopita, asingewaita mawaziri kuwafunda, bali angewaita ili wakae kama timu, awaombe ushauri, awasikilize, wampe mang’amuzi yao na mipango mkakati; naye baada ya kuwasikiliza na kuongeza maono yake, awapangie kazi na kuwadai matokeo baada ya muda kadhaa.

Au basi angeunda kikosi kazi cha wasomi waliokubuhu kutoka taasisi mbalimbali zinazoheshimika, akawakutanisha na wasaidizi wake, wote pamoja wakavuna maarifa ya ziada katika kuboresha kazi zao na kukosoa kasoro za huko nyuma.

Angejenga mazingira ya kuambizana ukweli, naye akaambiwa kasoro zake; hasa kwamba serikali imekosa mipango mkakati mbadala na hata hiyo iliyopo imekosa msimamizi makini.

Kitendo cha rais kulialia mbele ya wateule wake na wananchi kupitia vyombo vya habari si ishara ya ushupavu anaostahili kuwa nao kiongozi mkuu wa nchi.

Ndiyo! Tuliona wameinama na kushika tama alipokuwa anafoka. Lakini ana uhakika gani kwamba walikubaliana naye? Ana uhakika gani kwamba walimwona shujaa?

Na kwa kiongozi ambaye ameongoza nchi kwa miaka mitano kwa hotuba na matamko yasiyotekelezeka, anadhani mawaziri wake watamwamini na kumheshimu baada ya kufokewa hadharani Dodoma?

Labda, watamshukuru kwa kuwatengenezea mazingira ya kula posho za safari. Lakini naamini mawaziri wenyewe wanajua fika kwamba hawana sababu ya kusafiri hadi vijijini kila mara, maana huko kuna watendaji wa ngazi za chini wanaopaswa kusimamia kazi na kuleta taarifa kwa ngazi za juu.

Sasa kama rais anaagiza mawaziri waende wenyewe vijijini, hao watendaji wa mikoani, wilayani na vijijini kwenyewe watafanya kazi gani?

Hivi waziri aliyekaa katika wizara ile ile kwa miaka mitatu au zaidi, ana kitu gani cha kujifunza kwa rais aliyekaa madarakani kwa miaka mitano bila maono na mafanikio yanayoshikika?

Rais Kikwete ana mfano gani wa utendaji uliotukuka anaoweza kuutumia kuwasuta mawaziri wake? Aliacha urithi gani katika wizara alizowahi kuongoza kabla hajawa rais?

Ni nani anayejua matatizo, changamoto, na suluhisho la matatizo yake, kati ya waziri aliye kwenye wizara hiyo hiyo, na rais “anayeishi kwenye ndege?”Baadhi yetu tunajua kwamba mkwamo mkubwa wa kiutendaji unatokana na madaraka makubwa ya rais, nidhamu ya woga ya wasaidizi wake na utovu wa uzalendo wa baadhi yao.

Zipo taarifa kwamba siku hizi wasaidizi wa rais wameamua kumwambia yale anayotaka kusikia, kwa sababu anawafokea hovyo hovyo wanapomweleza asiyotaka, au wanapompa mapendekezo magumu.

Wanadai rais hataki kuambiwa asichotaka; nao hawako tayari kupoteza kazi zao.

Kwa mantiki hii, haiwezekani kwamba baadhi ya wasaidizi wa rais wana nafuu kuliko yeye? Kwanini tusiamini, basi, kwamba rais ndiye anawaangusha wasaidizi wake?





Yanga wampa uchifu Manji 
Sunday, 15 May 2011 20:54

Clara Alponce
WAZEE wa klabu ya Yanga jana walimkabidhi Mkuki, Ngao na Kigoda kama alama ya cheo cha uchifu kwa aliyekuwa mfadhili wao Yussuf Manji.Manji alikabidhiwa heshima hiyo na kamati ya wazee ya muafaka wa Yanga chini ya kiongozi wake Mzee Yahaya Akilimali.

Akizungumza kwenye hafla hiyo mama Shadia Karume alisema Manji amejifunza mengi Yanga na amerejea rasmi kwa ajili ya kufanya kazi ya kuijenga Yanga mpya.Mama Karume alisema," Manji anatakiwa kujua hasira, jazba hazifai namtaka asahau yote yaliyopita."

Mama Karume aliongeza kuwa kuna watu wengi waliofanya mambo makubwa na mazuri Yanga huko nyuma na Manji ni moja wao."Mume wangu ndiye aliyejenga jengo la Yanga hapa Dar es Salaam, lakini angejisikia vibaya kama lingeachwa na kuharibika bila ya kufanyiwa ukarabati kama aliousimamia Manji,"alisema Mama Karume ambaye pia alimtaka Manji kujenga jengo lingine la Yanga huko Zanzibar kwa sababu uwanja umeshapatikana.

Tukio hilo lilishuhudiwa na viongozi wa serikali akiwemo Jamal Rwambo, Mbunge Mussa Zungu, Mudhihir Mudhihir pamoja na wachezaji wa Yanga huku burudani ikitolewa na bendi za Msondo, Sikinde na Tanzanite

CHANZO: Mwananchi.


Rais wetu mpendwa Jakaya Mrisho Kikwete kwa kushangaa hajambo.Sasa anashangaa kwanini kuna utitiri wa mabango yenye ujumbe dhidi ya rushwa lakini rushwa inaendelea kutawala katika wizara mbalimbali bila uoga.

Tell you what Mr President,jibu la kinachokushangaza ni rahisi sana.Kama wewe mwenye kila nyenzo ya kukabiliana na rushwa,na ambaye ulitangaza hadharani kuwajua wala rushwa ila uliwapa muda wa kujirekebisha-na wakagoma kujirekebisha,lakini unaogopa kuwachukulia hatua-unasuasua katika kutekeleza ahadi uliztoa mwenyewe,unatarajia nini kutoka kwa watu wasio na uwezo wala mamlaka ya kupambana na rushwa?

Wewe unashangaa na sie tunakushangaa pia.One thing for sure,rushwa haiwezi kumalizwa kwa Rais kushangaa.Kinachohitajika ni vitendo na sio kubembelezana katika semina elekezi zinazozidi kuwatwisha mzigo walipa kodi masikini.

Jaribu kuwa mkali kidogo,punguza kushangaa,fanya vitendo.

Habari kamili ni hii hapa chini

Kikwete ataka vita vya rushwa kwa vitendo

na Danson Kaijage, Dodoma

RAIS Jakaya Kikwete, ameagiza mabango yote ya kupambana na rushwa yanayobandikwa katika wizara na taasisi za serikali na za umma yaendane na matendo yanayofanywa na maofisa katika ofisi husika.

Alitoa agizo hilo jana alipokuwa akifunga semina elekezi kwa viongozi na watendaji wakuu wa serikali iliyofanyika mjini Dodoma kwa siku saba.

Alisema wananchi wangependa kuona ukusanyaji wa mapato unaimarika na nidhamu ya matumizi ya fedha na mali za umma inakuwa bora zaidi badala ya kujaza mabango mengi yasiyokuwa na faida.

Alisema wananchi wanatarajia kuona juhudi za mapambano ya kweli kwa kudhibiti mianya ya rushwa badala ya kuona mabango mengi bila kuwepo na juhudi za makusudi.

Rais Kikwete alisema kinachoshangaza ni kuona wingi wa mabago katika kila kona wakati rushwa inaendelea kutawala ndani ya wizara mbalimbali bila woga.

Aidha, alisema kutokana na kuwepo kwa rushwa kuanzia ngazi ya juu ni wazi kuwa rushwa itaendelea kutendeka hadi ngazi ya chini kwa kuwa misingi ya rushwa inaanzia ngazi ya juu na kushuka ngazi ya chini.

Aliwataka vingozi na watendaji wakuu hao, kuonyesha ujasiri mkubwa juu ya kupiga vita masuala ya rushwa badala ya kuoneana aibu na kufichiana siri.

Rias Kikwete alisema semina hiyo ambayo ilikuwa na mikakati ya kuimarisha utendaji ndani ya serikali inapaswa kuzaa matunda hasa katika mapambano dhidi ya rushwa.

Hata hivyo, alisema wananchi wanatazamia kuona viongozi wa ngazi ya juu wakiwa mfano mzuri wa utawala bora, kuheshimu Katiba, utawala wa sheria na nidhamu ya kazi na uwajibikaji.

Naye Katibu Mkuu Kiongozi, Philimon Luhanjo, alisema waliazimia mazimio 14 ambayo viongozi hao wanatakiwa kuyatekeleza na kuyawasilisha katika ofisi yake kila baada ya miezi mitatu.

Semina hiyo iliwashirikisha mawaziri, makatibu wakuu, manaibu makatibu wakuu na wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama.





Hongera sana kwa mdau Godwin Habibu Meghji kwa kuhitimu Shahada ya Uzamili ya Sayansi Katika Mawasiliano ya Teknolojia iliyobobea katika uongozi wa miradi,aliyotunikiwa na Bodi ya wadhamini wa vyo vikuu vya Maryland,nchini Marekani.Kwa niaba ya wasomaji wa tovuti hii nakutakia kila la heri nikiamini kuwa shahada hiyo itakuwa chachu katika jitihada zetu za kizalendo za kuitumikia Tanzania yetu mahala popote pale (yes,nchi yetu inajengwa ndani na nje ya nchi)

15 May 2011



Mbele is a docudrama film about the journey of a music artist "Albino Fulani" as he links up with his fellow Tanzanian artist LBT for a USA benefit concert tour (S.A.P - Save Albinos Project). Being an Albino person himself, this show will take you behind the scenes where you will see dramatic episodes on how Albino Fulani associate and interrelate

The benefit concert takes place yearly to help raise funds which help children with albinism in Tanzania and also to raise awareness. The docudrama will show you how the two artists face and overcome professional and personal struggles and obstacles to raise funds and make the benefit concert a success.

The first season consists of 10 episodes which is expected to air in major Television Networks in Tanzania, Kenya and Uganda. Please join and “like” us on our Facebook page http://www.facebook.com/pages/Mbele/128019230601306 where as a member you will receive inside information and you will be able to watch the previews, behind the scene photographs and updates before the public does.

Stay tuned for the official trailer to be released on May 20th 2011. Please join the above facebook page to be the 1st to watch and comment.

Your support is very much needed and appreciated.

Sponsors and media please contact [email protected]

Thank you.

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.