5 Jul 2011


Nimekutana nayo huko Jamii Forums.For the time being,taarifa hii inabaki kuwa tuhuma tu hadi hapo itakapothibitishwa.

Wana Jf Mm nimefikia hapa hoteli inayoitwa AFRICA TULIP hapa Arusha mbunge wa CCM Viti maalum kutoka mbeya,Mary Mwanjelwa amekamatwa akiwa ameiba Mataulo,Vikapu vidogo ambavyo huwekwa maua chooni wafanyakazi wa hapa wanadai tukio hili ni la pili baada ya mwezi uliopita kufanya tukio la aina hiyo aliondoka salama wafanyakazi wakakatwa mshahara leo wakati ana check out wafanyakazi waliamua kumsachi na kweli wakakuta ameiba.Hili ni tukio la aibu ameaibisha nchi, bunge na chama chake. Wafanyakazi wa hapa leo wanadai kwamba mabinti wawili mwezi Jana walikatwa kiasi cha shilingi laki 2 nilikua na wazungu wamesikitika sana baada ya kufahamu kuwa huyu ni mbunge.Wanajf nimesikitika nikasema nanyi muipate taarifa hii ni aibu kwa Taifa,Fatilieni ni tukiop la Leo hapa Hotelini ni AIBU NI AIBU NI AIBU DUH Wana Jf nimefatilia Mara ya kwanza alifikia chumba namba 14 akafanya wizi wa soup dish,wizi wa mara ya pili ni room namba 20 miongoni mwa vitu alivoiba ni Pambo la Kitanda,Marekebisho ni kwamba aliiba siku ya Jpili si leo.Naomba kuwasilisha.


DAR PLUS ni Jarida jipya ambalo liko njiani kuingia mtaani mda si mrefu. Jarida hili ni maalum kwa ajili kutoa matangazo na kutangaza biashara ya aina yoyote ikiwepo mitindo, burudani, michezo na matukio mbali mbali kutoka kwenye pande zote za dunia. Vile vile litakuwa likiwaletea habari motomoto pamoja mahojiano ya watu mashuhuri wanaotoa mchango katika jamii yetu.

Kwa maelezo zaidi na gharama za matangazo piga simu namba +255 657 975 747 au +255 655 454 162

Asanteni
DAR PLUS GROUP

4 Jul 2011


Nimekuwa nikipokea shutuma na lawama nyingi kwamba ninaichukia CCM na uongozi wake (sana sana nikituhumiwa kuwa na "chuki binafsi").Kadhalika,nimekuwa nikilaumiwa kuwa ninamchukia Rais Jakaya Kikwete,huku wengine wakidai mimi nia Chadema damu damu.

Kawaida yangu ni kutojihusisha na malumbano na wasomaji wa blogu hii.Hata hivyo,ninapotupiwa shutuma kwa lugha ya kistaarabu huwa najaribu kutoa ufafanuzi kuhusu mtizamo na msimamo wangu.Naomba nirejee position yangu.Kwanza,mimi ni Mtanzania,na japo nimekuwa nje ya nchi yangu kwa takriban muongo (decade) moja sasa,haijanipunguzia japo kwa asilimia 0.0001 utanzania wangu.Baba yangu,kaka na dada zangu,wadogo zangu,marafiki,ndugu na jamaa wengi (zaidi ya asilimia 99.9) bado wapo Tanzania.Kwahiyo uwepo wangu hapa Uingereza haunipunguzii utanzania wangu.Kwa mantiki hiyo,kila kinachowagusa Watanzania wenzangu kinanigusa pia,regardless Watanzania hao wapo huko nyumbani au nje ya nchi.

Pili,mimi ni mwanafunzi wa stadi za siasa (political studies).Japo siwezi kujiita mtaalamu wa siasa au kujimilikisha uelewa wa hali ya juu wa siasa,ukweli ni kwamba angalau ninaielewa siasa at an advanced stage.Sasa kuna faida gani ya kuelimika pasipo kuitumikia jamii?Kwa wasiofahamu definition ya elimu,neno hilo linamaanisha jitihada za binadamu katika kukabiliana na mazingira yake.Sasa kama nimeelimika kwenye fani ya siasa,kisha nikaacha kutumia elimu hiyo kuisaidia jamii yangu kwa namna moja au nyingine,basi sintokuwa na tofauti na mafisadi.Ufisadi wa kitaaluma sio tu kufoji vyeti au kutelekeza taaluma na kukimbilia fedha bali pia kutoitumia taaluma ipasavyo.

Tatu,uwepo wangu nje ya nchi umenisaidia kulinganisha na kutofautisha baadhi ya mambo yanayotokea huko nyumbani.Actually,wakati naanzisha blogu hii niliweka bayana approach yangu katika mambo mbalimbali nitakayokuwa nayaongelea humu.Nilibainisha kuwa napendelea kujadili mambo katika namna ya kukosoa.Natambua kuwa sie waswahili hatupendi kukosolewa (at least wengi wetu).Lakini tatizo sio kukosoa bali kukosoa fyongo,kwa mfano kumkosoa mtu kwa vile tu humpendi.Mara kadhaa nimejaribu kuwaeleza wasomaji wangu kuwa,kwa mfano,sina tatizo na Mtanzania mwenzangu aitwaye Jakaya Kikwete bali nina matatizo na kiongozi wa nchi yetu,Rasi Jakaya Kikwete.Na sina matatizo na naye kwa vile yeye ni Mkwere na mie ni Mndamba (by the way wote ni Watanzania) bali tatizo langu kubwa lipo kwenye udhaifu wa uongozi wake.

Kuhusishwa kwangu na Chadema kunatokana na kushabihiana kimtizamo.Chama hicho kimejidhihirisha kuwa  mahiri katika mapambano dhidi ya ufisadi na maovu mengine katika jamii yetu.Nami pia hilo ndilo jukumu langu kubwa.Kwangu,faida pekee ya elimu yangu ni pale itakapotumika ipasavyo kuitumikia nchi yangu.Kwa kugusia tu,hata kabla ya kuanza uandishi nilikuwa naitumikia nchi yangu katika namna mbayo Watanzania wengi hawajapata fursa kama hiyo.Nisingependa kufafanua kwa sababu za kimaadili na kisheria lakini tu ieleweke kuwa nami ni miongoni mwa Watanzania wachache kabisa waliokuwa wakikesha macho for several nights a week kuifanya Tanzania yetu kuwa nchi stahili ya kuishi.You could feel the blanks by yourself,if you wish to.

Sasa,pamoja na mabaya mengi ya CCM,kuna baadhi ya viongozi wa chama hicho ambao kwa hakika kuna nyakati wanastahili pongezi.Na makala hii inamhusu January Makamba.Najua madhara ya kumsifia kiongozi; watu hawakawii kuhitimisha kuwa "aah anajikomba huyu".Well,let anybody make such a silly conclusion lakini penye ukweli sharti tuseme au tuandike.

Gazeti la Mwananchi toleo la leo lina habari kuwa Wizara ya Nishati na Madini imeingia kwenye kashfa ya kuhonga wajumbe wa kamati ya bunge ya nishati na madini ili "bajeti ya wizara hiyo ipite kiulaini huko bungeni".And guess what,aliyefanikisha kufahamika kwa taarifa hizo za kushtua si mwingine bali mwenyekiti wa kamati hiyo,yaani January.Huu ni uzalendo wa kupigiwa mstari.Ukiweka kanda political rhetorics and sentiments ambazo zimezoeleka kwenye competitive politics,January ana mitizamo inayoshairia kuweka mbele maslahi ya nchi badala ya maslahi ya chama chake.Of course,kama kiongozi wa CCM analazimika kuisifia na kuwarushia madongo wanasiasa wa upinzani,lakini hatuwezi kumhukumu kwa yale tusiyayapenda tu.Ndio maana hata katika makala niliyoandika kwenye jarida la Raia Mwema kumkosoa baba wa taifa Julius Nyerere nilibainisha wazi kuwa wengi tunafahamu mazuri ya Nyerere lakini "mabaya" yake yamebaki kuwa muted au taboo kuyaongelea.Kama kuongelea "mabaya" ya Nyerere hakumaanishi kumchukia,kumsifia January Makamba hakumaanishi kuipenda CCM (at least kwa madudu yake na ulezi wake kwa mafisadi).It simply means giving credit where it's due...au kwa kiswahili ni mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni.

Kwahiyo Mheshimiwa January,natumaini hutoishia tu kwenye kufichua uovu ndani ya kamati yako bali pia utajaribu kusambaza jitihada zako za kizalendo na kwenye maeneo mengine pia.CCM inahitaji viongozi watakaotanguliza maslahi ya nchi mbele ya maslahi ya chama.Haimaanishi msiwe mashabiki wa chama chenu bali nchi yetu ni muhimu zaidi ya chama cha siasa.

Anyway,habari husika ni hii hapa chini

Kashfa nzito Wizara ya Ngeleja  
Monday, 04 July 2011 08:44
MAOFISA WA JUU WATUHUMIWA KUIHONGA KAMATI YA MAKAMBA
Mwandishi Wetu
WIZARA ya Nishati na Madini imeingia katika kashfa nzito ambapo baadhi ya maofisa wa wizara hiyo wanatuhumiwa kuwahonga baadhi ya wabunge katika Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini kwa kile kinachodaiwa kutaka bajeti ya wizara hiyo kupita kwa urahisi, Mwananchi limebaini.
Habari zilizopatikana kutoka Dodoma na Dar es Salaam zimedokeza kuwa taarifa za uovu huo tayari zimefikishwa mezani kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ambaye amesema atalishughulikia baada ya kuwa amewasiliana na Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja.
Kwa mujibu wa habari hizo suala hilo pia tayari limefikishwa kwa Spika wa Bunge, Anne Makinda na kwamba kamati ya uongozi ya bunge anayoiongoza pia imearifiwa kuhusu suala hilo.
Kashfa hiyo imeikumba wizara hiyo katika kipindi kigumu ambacho nchi iko gizani huku wizara hiyo ikilaumiwa kutokana na uhaba wa nishati ya umeme kiasi cha Waziri Ngeleja kutangaza mgawo wa saa 10 wakati wa mchana na saa sita wakati wa usiku "ni janga la kitaifa".
Habari zaidi zinasema miongoni mwa mambo muhimu ambayo kamati hiyo ilikuwa ikitaka maelezo ni mapendekezo ya wizara hiyo kutaka kujenga jeno la makao yake makuu jijini Dar es Salaam kinyume cha ilani ya CCM ambayo inaweka wazi kwamba hakutakuwa na ujenzi wa makao makuu ya wizara jijini humo katika kipindi cha miaka mitano ijayo.
Habari zilizolifikia Mwananchi zilidai kwamba, Mwenyekiti wa Kamati ya Nishati na Madini ya Bunge, January Makamba ndiye aliyewasilisha malalamiko kwa Pinda na Makinda baada ya kubaini 'ulegevu' miongoni mwa wajumbe wa kamati yake wakati wa mchakato wa kujadili mapendekezo ya bajeti ya Wizara hiyo na kwamba mapema alikuwa ameishapokea taarifa kuhusu baadhi ya wajumbe wake kuhongwa.
"Mwenyekiti (January) alipewa taarifa za wajumbe wawili wa kamati yake ambao walikataa hongo hiyo, na baada ya kufanya uchunguzi alibaini kwamba kuna kila dalili kwamba baadhi ya wabunge katika kamati yake walikuwa wamebadili msimamo katika baadhi ya mambo," kilieleza chanzo chetu mjini Dodoma.
Habari zaidi zilidai kuwa kufuatia hali hiyo, January aliitisha kikao cha wabunge ambao ni wajumbe wa kamati yake na kugeuka mbogo, huku akiweka bayana kuchukizwa kwake na taarifa za wajumbe wake kuhongwa na kwamba alikwenda mbali zaidi akitishia kujiuzulu nafasi ya uenyekiti ili kutoa nafasi kwa wabunge hao kuchagua mwenyekiti mwingine ambaye atakuwa tayari kuvumilia uovu huo.
"Yule kijana (January) alikasirika sana, alichukizwa kweli kweli na hali hiyo kwa sababu ni kama wajumbe waliopokea hizo bahasha walikuwa wakimzunguka kwani tayari walikuwa wanajua nini wanachopaswa kufanya ili kuziokoa sekta za nishati na madini,"kilieleza chanzo hicho.
Kadhalika suala hilo la hongo lilijadiliwa katika kikao cha pamoja baina ya wajumbe wa kamati hiyo na viongozi wa Wizara ya Nishati na Madini, ambapo Waziri Ngeleja na Naibu wake, Adam Malima waliomba radhi kutokana na tukio hilo, hivyo kamati hiyo kuagiza maofisa wa wizara waliohusika wachukuliwe hatua.
"Ni kama Ngeleja na Malima walimalizana na kamati, si unajua maana ni kama January alikuwa peke yake, kama kulikuwa na wanaomsapoti (wanaomuunga mkono) walikuwa ni wachache, hivyo kama waziri na naibu wake waliomba radhi hakukuwa jinsi zaidi ya kumalizana nao," zilidai taarifa hizo na kuongeza:
"Hata hivyo Mwenyekiti na baadhi ya wajumbe walimwagiza Ngeleja na Malima kuwachukulia hatua maofisa waliohusika na ugawaji wa fedha hizo kwa baadhi ya wabunge".
Kauli za viongozi
Mwananchi liliwasiliana na January ili kufahamu undani wa suala hilo, lakini mbunge huyo wa Bumbuli hakukanusha wala kukubali kuhusu baadhi ya wajumbe wake kupokea rushwa.
"Nani kakwambia bwana, mimi siwezi kuzungumza lolote, mambo ya kamati jamani si yote tunayoweza kuweka wazi, lakini siku hizi hatufanyi vikao bila kuwaruhusu waandishi wa habari, kama hayo yangetokea si yangeonekana wakati huo?,"alihoji January.
Waziri Ngeleja kama ilivyo kwa January naye hakukubali wala kukanusha kuwepo kwa tuhuma hizo na badala yake alisisitiza kwamba anayeweza kuzizungumzia ni mwenyekiti wa kamati akimaanisha January.
"Unasikia, kama jambo limetokea kwenye kamati mimi sina mamlaka ya kulizungumzia hata kidogo maana nitakuwa navunja kanuni, kama wengine nilivyowaambia maana naona leo wengi wananitafuta kwa habari hii, mpigieni mwenyekiti wa kamati yeye ana mamlaka, mimi kwangu no comment (siwezi kusema chochote),"alisema Ngeleja kwa simu.
Spika wa Bunge, Makinda kwa upande wake pia alikanusha kupokea taarifa hizo. "Mimi ndiyo nazisikia kutoka kwako, pengine kama zimeletwa kwa barua sijaiona, lakini sifahamu kitu kama hicho," alisema Makinda alipozungumza kwa simu na Mwananchi.
Kwa upande wake Naibu Spika Job Ndugai alisema kuwa hana taarifa hizo kwa kuwa yeye alikuwa nje ya nchi kikazi. "Ndugu yangu, pengine ukimpata Spika anaweza kukusaidia, mimi nimerudi jioni hii (jana jioni) ndio naingia hapa Dodoma najiandaa kwa ajili ya kesho,"alisema Ndugai.

Nihitimishe makala hii kwa kutoa wito kuwa it's high time Ngeleja has to go.Sijui afanye madudu yepi ili Rais Kikwete agunude kuwa Waziri huyu hafai kuendelea kuongoza Wizara hiyo nyeti lakini ni matarajio yetu kuwa skandali hili jipya ni kitanzi cha mwisho kwa Ngeleja.He has to go..NOW!

Kadhalika,Spika Anne Makinda sasa anapaswa kuhamishia udikteta wake kwa wabunge wa upinzani  to wajumbe wa kamati waliopokea mlungula.Na jeshi la polisi ambalo ni mahiri kwa kuwabana wapinzani linapaswa kuanza uchunguzi wa mara moja kuhusu suala hili,sambamba na TAKUKURU.

3 Jul 2011


DCI Manumba katika kashfa; Adaiwa kumkingia kifua mbunge asikamatwe
Sunday, July 3, 2011, 12:03
Habari, Mtanzania
*Adaiwa kumkingia kifua mbunge asikamatwe

Na Kulwa Karedia

MKURUGENZI wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai nchini (DCI), Robert Manumba, amedaiwa kumkingia kifua Mbunge wa Busega, Dk. Titus Kamani (CCM) asikamatwe.
Uamuzi wa kukamatwa umekuja baada ya mbunge huyo kuhusishwa na njama za kutaka kumuua aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Dk. Raphael Chegeni.

Habari zinadai kuwa, DCI Manumba amekuwa akimkingia kifua mbunge huyo, licha ya Jeshi la Polisi kutangaza azma ya kumkamata kwa nguvu kutokana na ukaidi wa kutotii amri ya jeshi hilo.

Kwa mujibu wa chanzo hicho cha habari, DCI Manumba amekuwa akimkingia kifua mbunge huyo kwa kuwa wanatoka wilaya moja ya Magu, mkoani Mwanza.

Taarifa hizo ziliendelea kudai kuwa, tayari Dk. Kamani alikwisha jisalimisha polisi mkoani Mwanza mwishoni mwa wiki kwa mahojiano zaidi.

Akizungumza na MTANZANIA Jumapili, Manumba alikanusha shutuma hizo na kueleza kuwa tangu mbunge huyo ahusishwe na sakata hilo, hajawahi kumkingia kifua kwa namna yoyote.

“Kwanza nikwambie ukweli, suala hilo ndilo kwanza nalisikia kwako, sielewi kinachoendelea… kama kuna mambo Dk. Kamani amefanya taratibu zote za kisheria zitafuatwa.

“Sijawahi hata siku moja kumkingia kifua, kesi yao naamini inashughulikiwa kwa mujibu wa sheria za nchi, sasa iweje mimi nijiingize kwenye kitu ambacho sihusiki?” alihoji DCI Manumba.

DCI Manumba alisema yeye hapaswi kuzungumzia kwa undani suala hilo kwa kuwa si msemaji wa polisi na kwamba anayefaa kuhojiwa ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Saimon Sirro.

“Sasa hayo mengine unayosema mimi si msemaji, nakuomba umtafute RPC Sirro yeye ndiye anayeweza kuzungumzia zaidi suala hilo kwa kuwa limetokea kwake,” alisema.

DCI Manumba alikiri kutoka eneo moja na mbunge huyo, ingawa alisema hiyo si sababu ya kumkingia kifua. “Ni kweli huyu ni mbunge wangu na mimi ni mpiga kura wake, lakini hii si sababu ya kufanya nizuie polisi wasifanye kazi yao, hakuna mtu aliye juu ya sheria, hatutoki kijiji kimoja…narudia mimi ni mpiga kura wake, …nawashauri wale wote wanaohusishwa na tukio hili, waendelee na mambo yao, mimi sihusiki hata chembe katika hili,” alisema DCI Manumba.
Alisema upelelezi ndiyo njia pekee itakayomkomboa mbunge huyo kama ana hatia au la.

“Unajua hatufanyi kazi kwa kukurupuka, upelelezi unaoendelea ndiyo njia pekee itakayoamua kama nani ana kesi ya kujibu, tungoje tuone,” alisema.

Mapema wiki hii, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Simon Sirro, aliwaambia waandishi wa habari kuwa mbunge huyo alijisalimisha na kutoa maelezo yake kuhusiana na tuhuma zinazomkabili.

Alisema mbunge huyo alifika na kuhojiwa mwishoni mwa wiki na baada ya hapo aliachiwa, huku polisi wakiendelea na upepelezi zaidi kabla ya kumpandisha kizimbani.

Habari zinasema mbunge huyo, alijisalimisha kituo cha polisi Juni 25, mwaka huu na kuhojiwa usiku kabla ya kuondoka kuelekea Dodoma kuendelea na vikao vya Bunge. Akiwa mkoani Shinyanga, gari lake liligonga mtu na kuua papo hapo.

Mei 31, mwaka huu, inaelezwa kuwa Jeshi la Polisi mkoani Mwanza, liliandika barua Ofisi ya Bunge kutaka Dk. Kamani aende Mwanza kwa ajili ya mahojiano dhidi ya tuhuma zinazomkabili.

Barua hiyo yenye namba MZR/CID/SCR/105/2011/4 ilitumwa kwa Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashilila ikimtaka Dk. Kamani kwenda kujibu kesi yenye namba ya usajili MW/IR/2607/2011-MR-CC.28/2011.

Dk. Kamani atakuwa mshitakiwa wa tano iwapo atafikishwa mahakamani, baada ya watu wanne ambao ni Dismas Zacharia Ndaki, Erasto Kazimili Kombe, Queen Joseph Bogohe na Ellen Joseph Bogohe, ambaye ni Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Mwanza.

CHANZO: Mtanzania



Na Nova Kambota,

Binafsi nimeshtushwa sana na kauli za baadhi ya wana CCM kuwa chama chao kimeshajivua gamba , wanatumia mabadiliko ya safu ya uongozi ndani ya chama hiko yaliyofanyika hivi karibuni huko Dodoma, wakiwa na furaha kubwa wanadai kuwa hatua ya sekretarieti ya chama chao kujiuzulu huku ikimtupa nje katibu mkuu Yusuph Makamba na kumwingiza katibu mkuu mpya Willison Mkama na pia hatua ya kamati kuu ya chama hiko kuvunjika kwa maana nyingine imewatupa nje wajumbe mbalimbali lakini kati ya hao wapo wanasiasa wawili waliotawala vichwa vya magazeti hawa ni Andrew Chenge na Rostam Aziz lakini kujipa matumaini wanaccm wanadai kuwa kuingia kwa sura mpya tena za vijana kama Nappe Nauye na January Makamba ni ushahidi kuwa chama chao kimejivua gamba na sasa kipo safi .

Hata hivyo miezi michache tu baada ya safu mpya ndani ya chama hiko kutangazwa dalili za wazi kabisa zimeonekana kuwa CCM ilikuwa imeshiba sana kiasi kwamba ilikuwa vigumu kwake kupenya kwenye tundu jembamba sana hivyo ilipaswa kujivua gamba ili ipite lakini kwavile gamba la CCM limeshikamana na ngozi basi kikao cha Dodoma kimehofia maumivu ya kuvua gamba na badala yake CCM imejidanganya yenyewe kama sio kufanya mchezo wa kitoto wa kutapika ikidhani kuwa kwa kupunguza ukubwa wa tumbo itaweza kupenya hapo lakini sivyo inapaswa kujivua gamba! Lakini kwanini nasema CCM imetapika tu na sio kujivua gamba kama wengi wadhaniavyo?

Kwanza kabisa wanabiolojia au wataalamu wa elimu ya viumbe wanafahamu kuwa nyoka hajivui gamba kwa lazima la hasha! Bali gamba lenyewe huelegea na kujivua au hulegea sana na wakati nyoka akipita kwenye upenyo Fulani basi gamba huvuka hata pasipo nyoka mwenyewe kufahamu huu ni ukweli wa kisayansi kabisa lakini cha ajabu sana ni kile kinachoitwa kujivua gamba kwa ccm ni kwa kujilazimisha ,hakika nyoka hawezi kujivua gamba kwa kujilazimisha hivyo hata CCM haiwezi kujivua gamba kwa kujilazimisha badala yake inaweza kutapika kwa kujilazimisha labda kwa kuingiza vidole kwenye koromeo au kula kitu Fulani kitakachopelekea tumbo kuvurugika kisha kutapika hivyo kwa mantiki hii ni dhahiri kabisa ilichofanya CCM ni kutapika tu lakini sio kujivua gamba kama wanavyotaka kuuaminisha umma wa watanzania.

Pili ni jinsi CCM ilivyoshindwa kufanya mabadiliko ya kimchakato ndan ya mioyo ya makada wake nasema hivi kwasababu naona kabisa kile kinachoitwa migawanyiko au minyukano ndani ya CCM itaendelea kwa maana mpaka sasa CCM haijafanikiwa kujipambanua kiitikadi na kiimani iwapo ipo pamoja na wafanyabiashara ambao ni wafadhili wa chama hiko huku wengi wao wakihusishwa na tuhuma za ufisadi au wapo pamoja na wakulima na wafanyakazi ambao ndio wenye chama chao lakini sasa wameporwa kiasi kwamba sasa wenye fedha ndio wenye nguvu na ndio wenye uwezo wa kugombea na kushinda ndani ya chama hiko kiasi kwamba katibu mkuu wa zamani wa chama hiko Philip Mangula aliwahi kutamka kuwa CCM itangaze tenda kwenye kuwania uongozi! Hivyo ni wazi kuwa CCM haijaweza kuwaleta meza moja Harrison Mwakyembe na Edward Lowassa, pia haijafaulu kuwakutanisha kimtazamo Samwel Sitta na Rostam Aziz au kuwaimbisha wimbo mmoja Andrew Chenge na Anne Kilango Malecela wala mabadiliko haya hayawezi kuwasemesha lugha moja Yusuph Makamba na Shy-Rose Bhanji, CCM ingejivua gamba haya yasingekuwepo lakini kwavile imejidanganya kwa kutapika tu siiombei mabaya ila nasema isubiri ione nini kitafuata.

Tatu CCM ingejia gamba kweli isingejitosa kwenye maji ya moto tena yanayochemka nasema hivi kwasababu mpaka sasa dalili za wazi zinaonyesha kuwa CCM haiamini kuwa ipo ndani ya mfumo wa vyama vingi chukulia mfano wa hoja ya katiba mpya , naona kabisa ukimtoa Prince Bagenda nadhani wanaccm wengine wote licha ya kutamka kuwa katiba ni hoja ya wananchi ila mioyoni mwao wanaamini katiba ni hoja ya CHADEMA, CUF, NCCR na baadhi ya wanaharakati tu kwasababu iwapo kweli CCM inaamini kuwa ipo kwenye ushindani wa kisiasa kwenye mfumo wa vyama vingi basi kujijenga kwake kungetegemea katika kuipenda na kuikuza demokrasia badala yake inategemea nguvu zake , mimi naamini CCM ilipaswa kuwa ya kwanza kuipinga rasimu ya marekebisho ya katiba kwa jinsi ilivyojaa mapungufu badala yake inaunga mkono licha ya mapungufu hayo hii inatafsiri gani? Je CCM inataka kuvikomoa vyama vya upinzani au uhafidhina unaisumbua CCM? Je CCM ingejivua gamba ingeendeleza uhafidhina wa jinsi hii? au na yenyewe ingepinga rasimu hiyo? Jibu rahisi ingejivua gamba isingekuwa na uchafu wa aina hii ila kwavile imetapika tu ndio maana sasa ina njaa ya kuwakomoa wapinzani lakini niwakumbushe kuwa katiba mpya ni hitaji la watanzania sio CHADEMA wala CUF.

Nne CCM walipaswa kufanya mapinduzi ya kimfumo sio watu kama ilivyofanya, kwangu mimi nilitegemea CCM ingekuja na maazimio ya kukomesha mfumo wa wafanyabiashara kukimbilia ndani ya chamma hiko na vilevile kukomesha mfumo wa viongozi wa chama hiko kupendaz kusifia na kusifiwa tu , mimi nilitegemea kuwa sasa CCM inaandaa mkakati rasmi wa kuwa na tabia ya kujikosoa ili kulinda staha, tunu na falsafa ya mapinduzi ya chama hiko lakini sijaliona hili amini nakwambia ndani ya CCM bado ukiwa msemakweli kama Samwel Sitta,Harrison Mwakyembe na John Magufuli utajikuta unaongeza maadui kuliko marafiki, mambo haya hayawezi kubadilishwa kwa kumwondoa Makamba na kumweka Mkama bali kubadili mfumo wa CCM ndio maana nasisitiza kuwa ilichofanya CCM imetapika tu haijajivua gamba kwa kuhofia maumivu kwa maana gamba limeshikamana na ngozi.

Tano nilitegemea CCM ijisafishe kwa dhati kabisa kwenye kila ngazi na jumuiya zake tena kwa kuwapiga chini viongozi wale wanaoonekana ni mzigo lakini siamini kama hili litafanyika , hapa sidhani kama UVCCM , UWT na Jumuiya ya wazazi zitaguswa, labda nitumie wasaa huu kumpa siri Jakaya Kikwete kuwa hayo anayoita makundi na minyukano ya vigogo wa chama hiko kuelekea uchaguzi mkuu wa 2015 chanzo chake haswa ni huko kwenye jumuia hizi na endapo hatazigusa wala kuzitikisa walau kidogo basi hicho kinachoitwa kujivua gamba litakuwa ni jambo la kufikirika tu kuliko uhalisia ndani ya chama chake hiko.

Mwishowe nihitimishe makala haya kwa kuwaasa wanaaccm kuwa bado wana safari ndefu ya kujivua gamba sio kirahisirahisi hivi kama wanavyodhani tena hakuna ubishi kuwa kwa gamba lilliloshikamana na ngozi kazi kubwa inahitajika kulivua, kwa upande wa vijana wa chama hiko wasishangilie kuingia kwa vijana wenzao January Makamba na Nappe Nauye bali wanapaswa wajikite zaidi katika mapambano ya ndani ya chama yatakayowawezesha kukibadili chama hiko kutoka wazee oriented kuwa vijana oriented kisha wapindue mfumo wa wafanyabiashara na wakirudishe chama mikononi mwa wakulima na wafanyakazi vinginevyo hiko wanachoita kujivua gamba si lolote bali ni kutapika tu na hivyo CCM yao haiwezi kupenya kwenye mioyo miyembamba ya watanzania masikini kwa kujitapisha tu bali inapaswa ijivue gamba hata kama itapata maumivu makali…Tafakari!


Nova Kambota,
+255717 709618
www.novakambota.com
Tanzania, East Africa
Jumamosi, 2 julai 2011

Naomba kura yako kwenye tuzo za blog Tanzania kwenye vipengele vya best collaboration/group blog, best informative political blog na best political blog kunipigia kura nenda www.tanzanianblogawards.com

30 Jun 2011

This is Haika Lawere,Executive Director of Mbezi Garden Hotel. 
I would like to introduce to you our ; 
CONFERENCE PACKAGE which cost only Tsh 30,000 pa pax and it covers the following; 
-Arrival Tea n Coffee 
-Mid morning tea/coffee with snacks 
-Stationaries 
-Buffee Lunch 
-Afternoon Tea/Coffee with snacks 
-LCD projector 
-Wireless Internet 
We have various seminar/seminar/training rooms 
-Selous.................10pax 
- Manyara ..............15 pax 
-Ngorongoro..............50px 
-Ruaha....................80pax 
-Katavi.....................80pax 
-Serengeti hall.........250 pax 
Also we provide MEAL SERVICES/CATERING SERVICES to 
-Corporate Events/cocktail 
-Product launches 
-Opening of new offices 
-Farewell parties 
I am looking forward to hear from you soon, 

Have a nice day! 
Karibu sana. 

Best regards, 

Haika Lawere 
Executive Director 
MBEZI GARDEN HOTEL 
Mob: 0714 750404 /0756 696369 
www.mbezigarden.com 
www.facebook.com/haika





29 Jun 2011


Serikali yafanya kufuru
• Yatumia milioni 50/- kumlipia Waziri Hoteli

na Martin Malera Dar na Dauson Kaijage, Dodoma

SERIKALI inatumia zaidi ya sh milioni 50 kwa mwezi kwa ajili ya kugharimia malazi na chakula kwa ajili ya Waziri wa Mambo ya Ndani, Shamsi Vuai Nahodha, anayeishi katika Hoteli ya New Afrika tangu alipoteuliwa, Tanzania Daima Jumatano, limebaini.

Taarifa ya Waziri Nahodha kuishi hotelini, ziliibuliwa bungeni wiki iliyopita wakati wa kipindi cha maswali na majibu kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.

Ingawa taarifa ya bungeni hazikuwa za kina, uchunguzi uliofanywa na gazeti hili umebaini Nahodha ambaye amepata kuwa Waziri Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), amekuwa akiishi hotelini hapo tangu alipoteuliwa kushika wadhifa huo Novemba mwaka jana.

Habari kutoka ndani ya hoteli hiyo yenye hadhi ya Nyota Nne zilisema waziri huyo amepangishiwa vyumba vitatu ndani ya hoteli hiyo.

Inaelezwa kwamba amepanga kwenye moja ya vyumba maalumu kwa vigogo, (Executive); chumba ambacho kina sehemu mbili, ikiwemo ya kulala na ya kumpumzikia.

Kwa mujibu wa habari hizo, chumba hicho kinalipiwa dola 300 kwa siku, sawa na sh 480,000.

Vyanzo vyetu vya habari vilitonya kuwa chumba cha pili kinatumika kwa ajili ya walinzi na wasaidizi wake na cha tatu ni kwa ajili ya wageni muhimu wanaomtembelea hotoleni hapo hasa familia yake ambayo iko Zanzibar.

Habari hizo zinasema vyumba hivyo vinagharimu dola 220 kila kimoja kwa siku.

“Kwa maana hiyo, serikali kwa siku inalipa dola 740, sawa na sh 1,124,800 kwa ajili malazi tu ya Waziri Nahodha.

“Kwa hiyo ukifanya hesabu kwa mwezi serikali inalipa sh milioni 33.7 kwa ajili ya malazi tu ya Waziri mmoja na hadi sasa ana miezi saba hotelini,” kilisema chanzo chetu cha habari.

Kwa mujibu wa habari hizo, gharama hizo ni mbali ya chakula na huduma zingine hotelini ambazo kwa mwezi ni zaidi ya sh milioni 20, hivyo kufikia kiasi cha sh milioni 50 kwa mwezi.

Sababu kubwa ambayo inadaiwa na serikali kumfanya waziri huyo aishi hotelini ni uhaba wa nyumba za mawaziri.

Inadaiwa kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani aliyepita, Laurence Masha, alikuwa akiishi nyumbani kwake katika kipindi chote alichoshika nafasi hiyo na wala siyo kwenye nyumba ya serikali.

“Kwa hiyo Nahodha alipoteuliwa kushika wadhifa huo, serikali ikajikuta haina nyumba kwa ajili ya Waziri wa Mambo ya Ndani na hicho ndicho chanzo cha Waziri Nahodha kulala hotelini,” kilisema chanzo chetu cha habari.

Mbali ya Nahodha, kuna mawaziri wengine wanne wanaoishi hotelini kutokana na uhaba wa nyumba za serikali.

Uchunguzi zaidi unasema kuwa sababu kubwa ya Waziri Nahodha na wenzake kukosa nyumba, ni serikali kuwaacha baadhi ya mawaziri waliotemwa kuendelea kuishi kwenye nyumba za serikali.

“Kuna waziri alifariki; mjane wake bado anaishi kwenye nyumba za serikali, wapo mawaziri waliotemwa, wameomba wabaki kwa muda kwenye nyumba za serikali, ili wajipange. Hawa wote wameziba nafasi za mawaziri wa sasa,” alisema mmoja wa maofisa wa Wizara ya Ujenzi.

Habari zaidi kutoka ndani ya Wizara ya Ujenzi zimedokeza kuwa Nahodha ilishapata nyumba ya kuishi, lakini alikataa kwa madai kuwa haina ulinzi na samani za ndani.

Mtoa habari huyo alisema mvutano uliopo sasa ni kuwa kiongozi huyo anataka apewe stahiki hizo kama Waziri Kiongozi mstaafu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) wakati Wizara ya Ujenzi ikipinga jambo hilo kwamba anapaswa kugharimiwa sawa na mawaziri wengine.

Chanzo hicho kimedokeza kuwa kilimtaarifa Waziri Shamsi kuwa kama anataka samani za nyumba awasiliane na Wizara ya Mambo ya Ndani anayoiongoza ili kuangalia uwezekano wa kupata vitu anavyovitaka.

Chanzo kingine cha Tanzania Daima Jumatano, kimedokeza kuwa Shamsi, anaweza kupewa huduma hizo kama angeendelea kuwapo Zanzibar na si bara ambako hivi sasa ameteuliwa kuwa waziri.

Kilibainisha kuwa SMZ, haina utaratibu wa kuwapangia nyumba na kuwapa huduma mbalimbali ikiwemo ulinzi na wahudumu wa ndani viongozi wake wanaoishi nje ya Zanzibar.

Kiliongeza kuwa Shamsi, anapata huduma za hadhi ya Waziri Kiongozi kila anapokuwapo visiwani humo lakini anapotoka nje ya mipaka hiyo kwa maana ya kuwa Tanzania Bara, anagharimiwa sawa na mawaziri wengine.

Alipoulizwa na gazeti hili sababu za Waziri Nahodha kuendelea kuishi hotelini na gharama ambazo serikali inazipata, Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Goodluck Ol- Medeye, alisema wizara yake haihusiki na utoaji wa makazi ya viongozi na watendaji wa serikali, bali inahusika kwa Watanzania wote.

“Suala hili sio la wizara yetu, hatuhusiki kabisa na makazi ya mawaziri wala viongozi wengine wa serikali, tunahusika na makazi ya Watanzania wote,” alisema Naibu Waziri huyo.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk. Harrison Mwakyembe, alipoulizwa kuhusiana na suala la makazi la Waziri Nahodha na wengine, alisema hajui chochote kwani yuko mjini Dodoma kuhudhuria vikao vya Bunge la Bajeti.

“Mimi sijui chochote, muulizeni Katibu Mkuu ambaye yuko jijini Dar es Salaam, atawapa ufafanuzi,” alisema kwa kifupi Dk. Mwakyembe.

Sakata la Waziri Nahodha kuishi hotelini, liliibuliwa kwa mara ya kwanza wiki iliyopita wakati wa kipindi cha maswali ya papo kwa hapo kwa Waziri Mkuu na Mbunge wa Chambani, Salim Hemed Khamis (CUF).

Mbubge huyo alitoa taarifa zilizomshtua Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, na wabunge wengine kuwa Waziri Nahodha, anaishi hotelini.

Kabla ya kutoa kauli hiyo, mbunge huyo alihoji dhamira ya serikali katika kupunguza matumizi.

Alisema serikali inakusudia kusitisha ununuzi na matumizi ya mashangingi, kuacha kuagiza fenicha kutoka nje na kupunguza posho kama moja ya njia ya kupunguza gharama za matumizi kwa serikali.

Alisema pamoja na dhamira hiyo ya kubana matumizi, serikali imewaacha baadhi ya mawaziri wake waishi hotelini na hivyo kuongeza gharama za matumizi.

“Kuna mawaziri wanaishi hotelini tangu walipoteuliwa hadi sasa, serikali haioni kama hali hiyo ni kikwazo kwa mafanikio ya Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano tulioupitisha hivi karibuni bungenin?” alihoji mbunge huyo.

Akijibu swali hilo, Waziri Mkuu Pinda kwanza alionekana kushangazwa na taarifa hiyo na baadaye alimtaka ataje majina ya mawaziri anaowajua wanaishi hotelini hadi sasa tangu walipoteuliwa.

“Naomba Mheshimiwa Mbunge nitajie majina ya mawaziri unaowajua kwamba wanaishi hotelini,” alisema Pinda.

Mbunge huyo ambaye alikuwa akisubiri majibu ya Waziri Mkuu kwa hamu, akataja jina la Waziri Nahodha kwamba ni mmoja wa mawaziri wanaoishi hotelini.

Huku akiwa haamini na kumwangalia Waziri Nahodha, Pinda alijibu kwa kifupi tu: “Basi nimesikia.”


28 Jun 2011

Na Luqman Maloto
Kikombe cha Mchungaji Mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Ambilikile Masapile ‘Babu Ambi’ ni janga la kitaifa, hali halisi ni mbaya na madaktari wametahadharisha.

Kitendo cha idadi kubwa ya wagonjwa wa kisukari na ukimwi kuacha kutumia dawa za kurefusha maisha na baadhi yao kuanza kufariki dunia mmoja baada ya mwingine, imeelezwa kuwa hali itakuwa mbaya baadaye.

Kwa mujibu wa madaktari waliozungumza na gazeti hili, watu wengi wanaokunywa kikombe cha Babu Ambi, wanadharau dozi za dawa za kisukari na ukimwi kwa imani kuwa tiba ya Loliondo inaponya.
Mbali na madaktari, ipo ripoti kuwa kila kukicha watu wanapoteza maisha pande mbalimbali za nchi, ikielezwa kwamba sababu ya vifo ni wagonjwa kuacha kutumia dozi za kurefusha maisha walizopewa hospitalini baada ya kunywa kikombe cha Babu Ambi wa Samunge, Loliondo.

“Wanakosea sana, hivi sasa watu wanakufa lakini mbele ya safari watapukutika zaidi. Tunapokea watu wakiwa mahututi, wapo ambao wanakufa lakini wengine tunafanikiwa kuokoa maisha yao na kuwaanzishia dozi,”  alisema daktari mmoja wa Hospitali ya Taifa, Muhimbili (jina tunalo) na kuongeza:

“Taifa litapata msiba mkubwa baadaye kwa sababu watu wengi watakufa. Mamilioni ya watu wameshatibiwa Loliondo. Hivi kati ya hao, watu milioni moja ikiwa wanaumwa kisukari na ukimwi, wakiacha tiba inakuaje?
“Ni ruhusa watu kwenda Loliondo kwa sababu ni ngumu kuingilia imani za watu, lakini ni vizuri watu wakapokea ushauri wa kitaalamu ambao tunawapa. Wasithubutu hata siku moja kupuuza wala kuacha tiba za hospitali.”

Daktari mwingine wa Muhimbili (jina linahifadhiwa) alionya kuwa taifa linakabiliwa na mtihani mkubwa kwa sababu hata baadhi ya viongozi hawataki kuamini wanapoambiwa ukweli kwamba kikombe cha Babu Ambi hakijathibitika kuwa kinaponya.

“Hapa tunamuomba Rais Jakaya Kikwete (pichani) aingilie kati. Tunatakiwa kujua ni watu wangapi wamekwenda Loliondo, waliopimwa baada ya kunywa kikombe tuambiwe hali zao. Hapo tutapata jawabu kama Babu anapaswa kuendelea kuruhusiwa kutoa tiba au afungiwe,” alisema daktari huyo.

Aliendelea kusema: “Leo nazungumza lakini inaweza kuonekana ni mzaha, ukweli ni kuwa tiba ya kikombe cha Babu ni janga zaidi ya ajali ya MV Bukoba. Vifo vingi vinatokea, watu wenye ukimwi watakufa zaidi kwa sababu wameacha dawa za kurefusha maisha.”
MV Bukoba ni meli iliyopata ajali Mei 21, 1996 karibu na Bandari ya Mwanza na kuua watu 900.

Kutokana na takwimu hiyo, daktari huyo alisema: “Mamilioni ya watu wamekwenda Loliondo, wengi wanaacha kutumia dawa, ni matokeo gani yanangojewa? Loliondo ni janga zaidi ya MV Bukoba, ukweli upo hivyo. Tusubiri matokeo, wagonjwa wengi wanakuja kupima, tunawabaini bado hawajapona lakini wanatuambia wametoka Loliondo.

“Mimi ni daktari, kuna kasoro Wizara ya Afya katika kulifanyia kazi suala la Loliondo. Wanalichukulia kawaida wakati linabeba watu wengi. Kuna watu wamejipa matumaini hewa, wanamwaga fedha kwenda kunywa kikombe lakini hakuna kupona. Rais Kikwete aingilie kati.”

Mbali na madaktari hao walioomba hifadhi ya majina yao gazetini, Daktari Leopold Mwinuka wa Munufu Clinic alishauri wagonjwa kutoacha dawa za hospitali, hasa wale wenye kisukari.

Saidi Mohamed ambaye ni daktari mstaafu aliliambia gazeti hili: “Kuna rafiki yangu alitaka kwenda Loliondo nikamshauri asifanye hivyo. Kwenda Loliondo ni kujitafutia matatizo zaidi, wengi wakitoka huko wanaacha kutumia dozi walizoelekezwa hospitali, hivyo wanazidiwa kabisa. Sijaona mtu aliyepona. Nina mifano ya watu watano waliopoteza maisha.”

Kwa upande wa Mchungaji wa Kanisa moja, Kibaha Pwani, Godfrey Mtani alisema kuwa suala la Loliondo wamelitazama kwa maono ya kiroho na kubaini kuwa wote waliokunywa kikombe inawezekana wakafariki dunia baada ya miaka miwili.
Wakati huo huo, Makongoro Oging’, aliyekuwa Kahama mkoani Shinyanga anaripoti kuwa watu tisa waliokunywa kikombe cha Babu Ambi wa Loliondo wameangua kilio baada ya kupima na kugundua kuwa bado wana virusi vya ukimwi.

Dk. Timoth Mhezzi wa Kituo cha Mhezzi kinachojihusisha na ushauri na kupima virusi vya ukimwi kwa hiari, Kijiji cha Kakola, Kahama alisema, wagonjwa hao tisa walifika kituoni hapo mwezi uliopita kupima afya zao lakini walimwaga machozi walipopewa majibu kuwa Loliondo haikuwasaidia kitu.

“Baadhi ya wagonjwa hao walianza kububujikwa machozi baada ya kugundua hawajapona, huku  wengine walidai kwamba walitumia fedha zao nyingi kwenda Loliondo bila mafanikio,” alisema Mhezzi.


CHANZO: Global Publishers

Pichani ni jengo la "Tanesco ya Senegal",Senelec,lililoshambuliwa na waandamanaji wenye hasira kuhusu kukatika umeme mara kwa mara jijini Dakar.Akina sie tunashambulia kwa matusi,lawama,na manung'uniko huko Twitter na Facebook!!!

Sio siri kwamba upole wa Watanzania ni miongoni mwa sababu kuu za mabaya mengi yanayotokea huko nyumbani.Na kama kuna suala linalosikitisha kuhusu mwamko wa Watanzania kudai haki zao ni tatizo la mgao wa umeme sambamba na ubabaishaji wa hali ya juu wa serikali na Tanesco katika kushughulikia tatizo hilo.

Sasa hivi,mitandao ya jamii ya Twitter na Facebook imetawaliwa na malalamiko ya Watanzania wengi kuhusu mgao.Wengine wanaishiwa na uvumilivu na kuishia kuitukana Tanesco,kana kwamba matusi hayo yatarejesha umeme.Wengine wamekuwa wakipeana taarifa kuhusu maeneo ambayo "Tanesco wameshachukua umeme wao".Kwa kifupi,kinachosikika zaidi ni manung'uniko,lawama,vilio na hata matusi.Cha kusikitisha ni kwamba hakuna dalili yoyote kutafsiri malalamiko hayo into vitendo.

Sio kama nawasimanga ndugu zangu.I really feel you lakini ukweli mchungu ni kwamba kelele zenu haziwezi kumaliza tatizo hilo.Kinachohitajika ni kudai haki kwa nguvu.By "nguvu" simaanishi vurugu bali kuchukua hatua za makusudi kuhakikisha serikali na Tanesco wanawajibika.Mgao utaendelea milele iwapo Watanzania wataishia kulalamika tu.Hakuna miujiza katika kuleta mabadiliko.Either watu wajitoe muhanga kudai haki yao kama walipakodi au waendelee kuteswa na mgao.

Bahati nzuri,wenzetu nchini Senegal wanatuonyesha namna gani matatizo yanayoathiri nchi yanavyoshughulikiwa na umma.Nisieleze kwa maneno yangu bali naomba usome habari ifuatayo:

Associated Press

DAKAR,Senegal: Maelfu ya waandamanaji wameingia mitaani katika mji mkuu wa Senegal kupinga kukatika umeme mara kwa mara.Maandamano hayo ni tukio la tatu la vurugu nchini humo ndani ya wiki.

Wananchi wenye hasira walivamia ofisi za shirika la umeme la Senelec,jijini Dakar baada ya maandamano ya kupinga kukatika kwa umeme kwa muda mrefu.

Watu kadhaa walishambulia majengo ya serikali hapo jana.Wanadaia kuwa baadhi ya maeneo yamekuwa yakikosa umeme kwa masaa 24 au zaidi.

Kama ilivyo kawaida kwa vyombo vya dola barani Afrika,askari wa kikosi cha kutuliza ghasia walipambana na waandamanaji kwa kutumia maji na mabomu ya machozi.Msemaji wa polisi hakuweza kuthibitisha idadi ya waliojeruhiwa katika ghasia hizo.

Alhamisi iliyopita,vurugu kubwa ziliibuka kupinga mpango wa mabadiliko ya katiba ya nchi hiyo

Uchaguzi ni wenu Watanzania wenzangu.Mwendelee kulalama huku Serikali na Tanesco wakiendelea kuwasanifu (mgao wa umeme hauwagusi kwa vile aidha wana jenereta zinazojazwa mafuta na hela yako mlipakodi au maeneo wanayoishi hayakatwi umeme kutokana na unyeti wake) AU muige mfano wa wenzetu wa Senegal.Hakuna njia ya mkato katika kutatua matatizo sugu yanayosababishwa na watendaji wasiotimiza wajibu wao.It's now or never!

27 Jun 2011

 Pichani juu ni mwanamuziki mahiri kutoka nchini Jamaika,Shaggy,akisimikwa uchifu wa kabila la Wasukuma.Picha ya chini ni wasanii wawili mahiri kabisa wa Kitanzania,Profesa Jay na MwanaFa "wakikamua" (kama wanasemavyo watoto wa mjini).Na picha ya mwisho chini ni wasanii hao wakiwa na msanii mwingine mahiri Chid Benz.Swali la kichokozi: kwa kumpa Shaggy uchifu badala ya wasanii wetu wa ndani,haimaanishi kasumba ya kuthamini mno vya nje kuliko vya ndani?Nishasema ni swali la kichokozi,nothing serious anyway.And dont get me wrong,I like Shaggy,who I rate as one of the most down-to-earth celebrities.


Mwalimu wangu Profesa Matondo unasemaje kuhusu hili?Na MwanaFA una lolote la kuchangia?

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.