30 Dec 2008

Pichani,Mkurugenzi Mkuu wa ATCL David Mattaka akiteremka kutoka kwenye ndege iliyonunuliwa na shirika hilo mwezi Februari mwaka huu.Picha kwa hisani ya HAKI.

HEBU SOMA KWANZA HABARI IFUATAYO KISHA TUIJADILI PAMOJA.
Mali za ATCL zakamatwa
Benki ya Stanbic Tanzania Limited, Makao Makuu ya Kinondoni, Dar es Salaam, inayashikilia magari sita ya Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL), baada ya kushindwa kulipa deni la Sh bilioni mbili iliyochukua kama mkopo. 

Fedha hizo zinazodaiwa kushindwa kulipwa kwa miezi miwili sasa zilikopwa na wafanyakazi wa kampuni kwa mikopo na kutokana na kushindwa kuwalipa mishahara watumishi wake, makato ya kila mwezi yameshindikana kukatwa. 

Taarifa zilizopatikana kutoka ATCL na katika benki hiyo jana zilithibitisha kushikiliwa kwa magari matano aina ya Toyota Land Cruiser VX, kuanzia Jumanne jioni wiki iliyopita na gari la sita limekamatwa likiwa mjini Moshi, Kilimanjaro na lilipelekwa katika benki hiyo jana na kufanya idadi ya magari hayo kuwa sita. 

Namba za magari hayo ambazo ‘HabariLeo’ jana ilizipata katika eneo la chini la maegesho yalikohifadhiwa magari hayo japo uongozi wa benki uliokuwapo haukuwa tayari kuzungumza kwa madai kuwa msemaji yupo likizo, ni SU 37079, SU 37081, SU 37082, SU 37086, SU 37083 na lililofikishwa jana ni SU 37084. 

Habari zaidi kutoka eneo la benki yalikohifadhiwa magari hayo zilieleza jana kuwa yataendelea kushikiliwa mpaka deni hilo lililipwe na uamuzi huo ulifikiwa baada ya hofu kuwa huenda kampuni hiyo ikafa na hivyo benki hiyo ikakosa kila kitu. 

Gazeti hili lilifika makao makuu ya Stanbic makutano ya barabara za Ali Hassan Mwinyi na Kinondoni, na mhudumu wa mapokezi alieleza kuwa wasemaji waliokuwapo hawakuwa tayari kulizungumzia, na mwenye dhamana ya kutoa taarifa hiyo ni Mkurugenzi Mkuu, Bashir Awale, yuko likizo. 

Hata hivyo, taarifa za ndani ya benki hiyo zililieleza gazeti hili kuwa deni wanaloidai ATCL ni Sh bilioni mbili kwa mwezi huu na kwamba uamuzi wa haraka ulichukuliwa baada ya akaunti ya kampuni hiyo kwa benki hiyo kuonyesha haina fedha za kulipa deni hilo wala haitarajii kuwa nazo kwa siku za karibuni. 

Chanzo chetu cha habari ndani ya ATCL kilieleza kuwa magari hayo yalikamatwa tangu wiki iliyopita isipokuwa la Mkurugenzi Mtendaji ATCL, David Mattaka. Hata hivyo, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya ATCL, Balozi Mustafa Nyang’anyi, alithibitisha jana kupata taarifa ya kukamatwa kwa magari hayo na ameitisha kikao cha dharura kitakachokaa leo makao makuu ya kampuni hiyo. 

Alisema pamoja na suala hilo, pia watajadili mambo mengine likiwamo la kurejeshewa leseni ya kurusha ndege waliyonyang’anywa na Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Desemba 8, mwaka huu. 

ATCL ilinyan’ganywa leseni hiyo baada ya kubainika kuwa na dosari za kiufundi zinazosababisha kutokuwa na viwango stahili vya kiusalama vya kuwaruhusu kurusha ndege; ukaguzi uliowataka warekebishe dosari hizo ulifanywa Oktoba mwaka jana na leseni hiyo iliisha kazi tangu Aprili mwaka huu, lakini walikuwa wakiongezewa muda mpaka iliposhindikana wakanyang’anywa leseni hiyo. 

“Hilo jambo na mimi nimepewa taarifa, lakini kusema ni kiasi gani au ni deni linahusu nini, mimi siyo menejimenti, mpigie Mattaka, ila ninachoweza kusema ni kwamba deni hilo si kitu cha ajabu maana tulikabidhiwa kampuni na deni la shilingi bilioni kumi na tisa,” alisema Balozi Nyang’anyi na kuongeza: “Ufafanuzi zaidi sina. 

Mnashangaa hilo, kuna na la BP, pia waliokuwa wanatusambazia chakula kwenye ndege… na mengine mengi, yote hayo tutayajadili kesho katika kikao cha dharura na menejimenti nilichokiitisha, tutazungumza hayo na mengine mengi.” 

Alisema katika kikao hicho pia watazungumzia mishahara ya wafanyakazi ambayo mpaka jana walikuwa hawajapata na pia kupanga namna ya kurudi tena katika uzalishaji mara watakaporejeshewa leseni ya kurusha ndege tena. 

Mattaka alipoulizwa jana kuhusu kushikiliwa kwa magari, alikanusha kwa kudai taarifa hizo si za kweli, lakini alikiri kuwapo kwa kikao cha Bodi na Menejimenti alichokiita kuwa ni kikao cha kawaida si cha dharura.Hizo habari umetoa wapi? Si kweli, nasema si kweli?” alisema huku mwandishi akiendelea kumhoji. 

“Kuhusu kikao ni kweli kipo, lakini si cha dharura, ni cha kawaida……naomba unitafute kesho baada ya kikao kuhusu hilo unalotaka kujua,” alisema Mattaka. Hivi sasa TCAA inaendelea kupitia nyaraka za ATCL na kuna taarifa kuwa leo w.anaenda kukagua namna ya wafanyakazi wa kitengo cha dharura ndani ya ndege wanavyoweza kuchukua hatua pindi tatizo linapotokea.

NI DHAHIRI KWAMBA UONGOZI WA SASA WA ATCL HAUWEZI KULIREJESHA SHIRIKA HILO KATIKA UHAI WAKE.KINACHOSHANGAZA NI KWANINI HADI LEO HAWAJAWAJIBISHWA.LAST WEEK ZILITOLEWA SIKU 7 ZA KUTOA MAELEZO.BINAFSI SIDHANI HATA KAMA KULIKUWA NA HAJA YA KUFANYA HIVYO KWA SABABU YEYOTE ATAKAYEPEWA NAFASI YA KUELEZEA UDHAIFU WAKE ATAJITETEA KWA VISINGIZIO LUKUKI.TATIZO HAPA SIO KWAMBA KUJITETEA NI KITU KIBAYA BALI UKWELI KUWA WAKATI SIKU 7 ZINATOLEWA (NA SI AJABU ZIKAONGEZWA) ATCL INAZIDI KUJIWEKA KATIKA HALI MBAYA YA KUREJEA TENA KATIKA OPERESHENI ZAKE.IKUMBUKWE KUWA CHANZO PEKEE CHA MAPATO KWA ATCL (NA SABABU YA KUANZISHWA KWAKE) NI BIASHARA YA USAFIRI WA ANGA.SIKU ZINAZIDI KUKATIKA TANGU SHIRIKA HILO LIPIGWE FULL STOP KUSAFIRISHA ABIRIA,NA HIYO INAMAANISHA KWAMBA ATCL INATENGENEZA HASARA KILA SIKU KWA VILE WAKATI HAKUNA MAPATO YANAYOINGIA,MATUMIZI LAZIMA YAFANYIKE KATIKA KILA SIKU YA UHAI WA SHIRIKA HILO.

HIVI HAKUNA WATU WENGINE WANAOWEZA KUTEULIWA KWENYE NYADHIFA ZA UENYEKITI WA BODI YA ATCL NA MKURUGENZI MKUU BADALA YA NYANG'ANYI NA MATTAKA,RESPECTIVELY?JE HAWA NDIO WATU PEKEE WANAOWEZA KUIOKOA ATCL?KUNA USHAHIDI WOWOTE WA WANANCHI HAWA KUWA NA UWEZO HUO?JE KUSUASUA KWA ATCL HAKUNA MAHUSIANO NA MAPUNGUFU KATIKA UWEZO WAO WA KUONGOZA SHIRIKA HILO?

NA BWANA MATAAKA AMEZUA TABIA MBAYA YA KUKANUSHA KILA TAARIFA ZISIZOPENDEZA ZINAZOELEKEZWA KWA ATCL.LAST TIME,ALIKANUSHA TAARIFA KWAMBA MAMLAKA YA MAWASILIANO IMEZUIA SHIRKA HILO KURUSHA NDEGE ZAKE,LAKINI BAADAYE AKALAMBA MATAPISHI YAKE NA KUKIRI HABARI HIYO.SASA TENA ANAKANUSHA HABARI YA KUKAMATWA KWA MAGARI HAYO WAKATI GAZETI HUSIKA LIMESHUHUDIA MAGARI HAYO YAKIWA KWENYE YADI YA BENKI YA STANBIC.AU MATTAKA ANATAKA KUTUAMINISHA KWAMBA PARKING YA MAGARI YA ATCL SASA NI HAPO STANBIC?

HIVI HII SERA YA KULINDANA ITAENDELEA MPAKA LINI?VIONGOZI WETU HAWAJISKII UCHUNGU WANAPOONA WENZETU WA KENYA AU ETHIOPIA,KWA MFANO,WANAVYOPASUA ANGA NA MASHIRIKA YAO YA NDEGE YENYE HADHI YA KIMATAIFA?KWA KWELI INATIA UCHUNGU NA KUUDHI HASA UNAPOONA VIONGOZI WA SHIRIKA LILILOKO A.C.U WAKISHINDWA KUONYESHA UCHUNGU KWA MATATIZO YALIYOPO HADI KUDIRIKI KUONYESHA KUWA "na kuna deni la BP...madeni ni jambo la kawaida".HIVI WAUNGWANA HAWA WANAWEZA KUTUELEZA WANAFANYA NINI HASA KUIKWAMUA ATCL?NA KAMA UTETEZI WAO PEKEE NI KUTOPEWA FEDHA NA SERIKALI,KWANINI BASI WASIACHIE NGAZI KUONYESHA KUTORIDHISHWA KWAO?KUNA MASLAHI WANAYOPATA VINGENEVYO WANGESHAJIUZULU ILI LAWAMA ZISIWAANGUKIE WAO PINDI ATCL IKIFA.

TUSIPOZIBA UFA TUTAJENGA UKUTA.


29 Dec 2008


I wouldn't consider myself as an expert in blogging,but hey,I've been around since 2006 and still kicking.I've seen blogs born and die,with some dying as fast as they were born.When going through some discussions in Jamii Forums I found a thread about January Makamba's blog.Putting aside the usual unpleasantries in a public forum,one notable point in the said discussion was how should bloggers communicate with their audiances.For instance,I'm Tanzanian,my national language is Kiswahili,and most of my blog posts are in that language too.But in so doing,am I not limiting my audiance?Talking of audiance,is it the people you share an expertise with,fellow countrymen and women,or anybody who has access to the internet?And,in blogging,should the top priority be on what I want my audiance expect from me or is it what I want them to hear from me?

Perhaps in finding answers to such questions,it's worth looking at how other bloggers from different countries blog.For instance,are most Chinese bloggers blog in Arabic?The answer is definitely no,though I do not have supporting statistics on that.May be the Chinese example doesn't do enough justice because of the number of Chinese speakers in the world.

Why do some bloggers prefer a foreign,or rather an international language,instead of their own?Is it because they are targetting a wider,global audiance?Is it because they master some languages other than their own?Or is it just a personal choice?

In one of the threads in Jamii forum,I found another discussion about a UK-based Tanzanian scholar,who was being criticised for using "poor" English in one of his articles in the web.While not passing my judgement on the said article or his critics,I was just wondering if anyone would be bothered if the article had been written in "poor Kiswahili".My assumption here is,a foreign langauge could easily become vulnerable to criticism.And this might be ONE of the reasons as to why many Tanzanian bloggers prefer using Kiswahili to English.However,there could also be a cultural factor.That is,Kiswahili is my national language,and it's part of my culture.So why should I not be proud of using it to communicate with my people?Cultural relativists might question,though,about those non-Kiswahili speakers?

Anyway,personally,I will continue using Kiswahili in most of my posts,especially those I deem of interests to my fellow Kiswahili speakers.However,English will also be used particularly when I give my analysis or opinion on news articles written in English.I am one of those who believe that although a personal blog should largely remain personal,in the sense of choices of words,language,pictures and even accepting or rejecting comments,it also attains a public status soon as it published because it could be read by anybody anywhere,and that necessitates being considerate TO and OF others.


Dada yangu  ambaye pia ni Mhariri Mkuu wa Kituo cha Televisheni cha Channel Ten, Bernadina (Dinna) Chahali akiwa kwenye msiba na kuaga mwili wa mfanyakazi mwenzie,Marehemu Henry Makange.Picha kwa hisani ya Mrisho Blog na Father Kidevu.

28 Dec 2008

Haya ni maongezi ya ki-utu uzima,kwahiyo under-18s mnaombwa kutosoma post hii.Well,just saying it bcoz I know ishu ya umri katika dunia ya sasa ni more theoretical than practical.Anyway,"kuvunja bikra" ni ndoto ya wanaume wengi,na japo ni suala lisilozungumzika hadharani,wengi wa wanaodai kuwa wameshawahi kupata "bahati" hiyo huwa si wakweli (wanaongopa) na wale ambao kweli walishaangukiwa na "kismati" hicho huwa hawaaminiwi wanapotoa "ushuhuda" wao,na wakati mwingine kutakiwa watoe uthibitisho!How could they?

Na pengine wapo akina dada ambao wangetamani kutopeteza bikra "kabla ya muda mwafaka" lakini mara nyingi tukio hilo (la kupoteza bikra) hutokea kwenye foolish age.Inadaiwa (japo sina uthibitisho katika dai hilo) kwamba kuna something very special kwa "ungo kuvunjwa" na mume usiku wa kwanza baada ya ndoa.Hata hivyo,jamaa yangu mmoja anayeelekea kuwa specialist wa kitu chochote kinachohusiana na jinsia ya kike anadai kuwa suala la kuvunjishwa ungo siku ya ndoa lilitengenezwa tu na walinzi wa maadili ili kuhakikisha amri ya sita haivunjwi (kwa wasiofahamu,amri ya sita ni USIZINI.Na kidini,kuzini ni tendo la ndoa nje ya ndoa).

Well,sasa kuna product ambayo "inarejesha" bikra.Nimeweka inverted commas kwa vile urejeshaji huo ni more technological than biological. Ni mithili ya ku-hack elimu-viumbe ya sehemu nyeti.

Khalil Islam spent 22 years in prison for the murder of Malcolm X. Now a free man - who used to go by the name of Thomas 15X Johnson and was a ranking lieutenant at Elijah Muhammad’s Temple No. 7 on 116th Street and Lenox Avenue - Islam is ready to tell his story to the world...CONTINUE

Source:BLACKPOWER.COM




SOURCE:WSHH

27 Dec 2008


POSTMORTEM NI MUHIMU HASA KWENYE VIFO VYENYE UTATA.LAKINI POSTMORTEM KWENYE MASUALA YA SIASA NI MBINU INAYOTUMIKA AIDHA KUKWEPA LAWAMA NA KUZIELEKEZA MAHALA KWINGINE AU KUPOOZA MAUMIVU YALIYOSABABISHWA NA MAPUNGUFU KWENYE UWAJIBIKAJI.KATIKA HABARI IFUATAYO,MBUNGE WA HANDENI,DKT ABDALLAH KIGODA, AMETOA POSTMORTEM REPORT YA MPANGO WA "MABILIONI YA JK",KWAMBA HAYAKUWANUFAISHA WATU WA VIJIJINI.PENGINE KABLA YA KUANGALIA VIJIJINI,SWALI KUBWA LILIPASWA KUWA "MABILIONI HAYO YAMEWANUFAISHA WATU WANGAPI REGARDLESS YA LOCATIONS ZAO-MIJINI AU VIJIJINI".LAKINI LA MSINGI ZAIDI,JE POSTMORTEM REPORT KAMA HIYO YA KIGODA INA UMUHIMU GANI KWA WANANCHI AMBAO HAWAKUNUFAIKA NA MPANGO HUO ULIOLENGA KUBORESHA MAISHA YA WATANZANIA?SOMA KWANZA HABARI YENYEWE KISHA TUENDELEE NA MJADALA:
Na Steven William, Handeni
MBUNGE wa Handeni Dkt Abdallah Kigoda, amesema kuwa dhamira ya Rais Jakaya Kikwete kutenga fedha kwa ajili ya kukopeshwa wajasiriamali wadogo alikuwa na dhamira nzuri, lakini fedha hizo zilivamiwa na 'wajanja' wachache waliozikopa na wananchi hasa wa vijiji hazikuwafikia.

Akizungumza katika mikutano ya hadhara kwenye vijiji vya kata ya Ndolwa wilayani hapa juzi kufuatia wananchi kumbana mbunge huyo kuhusu mikopo hiyo maarufu 'mabilioni ya Kikwete', mbunge huyo alisema kuwa fedha hizo zilitengwa na kupitia benki ambako wananchi wengi hasa wa vijijini hawana uelewa mpana wa kutumia benki zilizopo kukopa.

"Ndugu zangu wananchi dhamira ya Rais ilikuwa nzuri kwani alitenga fedha hizo kwa ajili ya kuwasaidia wenye mitajhi midogo wapandishe mauzo ya bidhaa zao lakini fedha zile zilipitia benki na nyie uwezo wa kuzitumia benki hamjui, hivyo wajanja wakajitokeza wakazichota," alisema Dkt Kigoda.

Aliwapa mfano wa mkoa wa Kagera fedha hizo zilizpopelekwa mkoani humo, ni watu watano tu waliopata fedha hizo kutoka katika benki hizo akiwemo meneja wa benki hiyo hali iliyoleta tafsiri mbaya kwamba waliozichukua ni watu wa mjini waliokuwa na fursa nzuri na uzoefu wa kukopa benki.

Hata hivyo, aliwatoa wasiwasi wananchi hao kwamba serikali itatoa tena fedha lakini walishauri kwamba pindi zikitolewa zishirikishe viongozi wa wilaya husika wachama na serikali ambao wamekuwa wakifahamu vikundi mbalimbali vya wajasiriamali katika maeneo husika hivyo fedha hizo zitafika kwa walengwa.

Kufuatia kuingizwa tena fedha hizo kwenye mabenki hayo, mbunge huyo aliwataka wananchi wa wilaya ya handeni kuhakikisha wanajiunga na vikundi vya ujasiriamali ambavyo vitatambulika na serikali ili waweze kuomba na kupata mikopo.

CHANZO:Mwananchi

HIVI DKT KIGODA ALIKUWA WAPI WAKATI FEDHA HIZO ZIKIELEKEZWA KUSIKOSTAHILI?NA WAKATI ANATOA TAKWIMU ZA KAGERA,KWANINI HATAJI IDADI YA WALIONUFAIKA AU KUATHIRIKA KATIKA JIMBO LAKE LA HANDENI?PIA ANAPASWA KUWAOMBA RADHI ALIOKUWA AKIWAHUTUBIA KWA KUSEMA "..na nyie uwezo wa kuzitumia benki hamjui".HIVI NI KWELI WANAKIJIJI WOTE ALIOKUWA AKIWAHUTUBIA,NA WENGINEO AMBAO HAWAKUPATA MABILIONI HAYO HAWANA UWEZO WA KUZITUMIA BENKI?JE YEYE KAMA KIONGOZI NA MWAKILISHI WAO AMEFANYA NINI KUWASAIDIA WAPIGA KURA WAKE KUWA NA UWEZO WA KUJUA NAMNA YA KUZITUMIA BENKI?BY THE WAY,NENO "KUZITUMIA" NI CONTRADICTORY KWANI LINAWEZA PIA KUMAANISHA KUZITUMIA BENKI KAMA ILIVYOKUWA KATIKA UFISADI WA EPA.ANYWAY,NADHANI ALIKUWA ANAMAANISHA WANAKIJIJI HAWAJUI KUZITUMIA HUDUMA ZA BENKI.IF SO,HAWAJUI KWA VILE HAKUNA BENKI,BENKI ZIPO LAKINI HAZITOI ELIMU YA NAMNA YA KUTUMIA HUDUMA ZAKE,WANAKIJIJI HAWATAKI KUELEKEZWA NAMNA YA KUTUMIA HUDUMA HIZO,AU...?

TATIZO KUBWA LINALOKWAMISHA MIPANGO MIZURI NI MIPANGO MIBOVU.WAINGEREZA WANA MSEMO POOR PLANNING PRODUCES POOR PERFORMANCE.UBOVU WA MPANGO WA MAMILIONI YA JK ULIKUWA KWENYE USIMAMIZI.NI DHAHIRI KWAMBA UKIPELEKA MAMILIONI,LET ALONE MABILIONI,PASIPO KUHAKIKISHA KUWA WAJANJA (ISOMEKE MAFISADI) HAWATABUNI MBINU ZA KUTAFUNA FEDHA HIZO,ITAKUWA NI MITHILI YA KUTWANGA MAJI KWENYE KINU.

MPANGO WA KUWAPATIA FEDHA WANANCHI WASIO NA UWEZO ILI ZIWASAIDIE KUJIKWAMUA KIUCHUMI ULIKUWA MZURI LAKINI ULIHITAJI UCHAMBUZI MAKINI KATIKA USIMAMIZI NA UTEKELEZAJI WAKE.KULIKUWA NA HAJA YA KUANGALIA POWER RELATIONS HUKO ZINAKOPELEKWA FEDHA HIZO,HUSUSAN MAHUSIANO KATI YA WASIMAMIZI NA WALENGWA.UDHAIFU KATIKA HILO NDIO UMEPELEKEA KESI KAMA HIYO YA KAGERA AMBAPO MENEJA WA BENKI NAE AKAJIINGIZA MIONGONI MWA WALENGWA JAPO SIDHANI KAMA ILIPASWA KUWA HIVYO.KILICHOPASWA KUFANYIKA KABLA YA KUPELEKA FEDHA HIZO NI KUTAMBUA WANAOZIHITAJI,KUFAHAMU MIPANGO YAO YA NAMNA WATAKAVYOTUMIA FEDHA HIZO AMBAZO KIMSINGI NI MIKOPO,KUTENGENEZA MAZINGIRA AMBAPO MAFISADI HAWATAZITAFUNA NA MWISHO,KUZIWASILISHA KATIKA WAKATI MWAFAKA.

PENGINE KABLA YA KUFIKIRIA KUTOA AWAMU NYINGINE YA MABILIONI NI MUHIMU KUFANYA TATHMINI YA MAFANIKIO NA FAILURES KATIKA AWAMU ZILIZOTANGULIA.SAMBAMBA NA HILO NI KUCHUKUA HATUA KALI KWA WOTE WALIOFUJA FEDHA HIZO.PIA NI MUHIMU KUFAHAMU FEDHA HIZO ZITAREJESHWA VIPI ILI BAADAYE WASIJE WAJANJA WAKAPORA ARDHI NA MALI NYINGINE ZA WALALAHOI KWA VISINGIZIO VYA KUDAI MAREJESHO YA FEDHA HIZO.

MWISHO,VIONGOZI KAMA DKT KIGODA WANAWEZA KUWA NA UMUHIMU ZAIDI KATIKA KULETA UFANISI WA MPANGO HUO WA MABILIONI YA JK SIO KWA KUTULETEA POSTMORTEM PINDI MAMBO YAKIENDA MRAMA BALI KWA KUSHIRIKI KIKAMILIFU KUHAKIKISHA MAFANIKIO YANAPATIKANA.HILO HALIHITAJI SEMINA ELEKEZI KWANI LIKO NDANI YA UWEZO WETU.KINACHOHITAJIKA NI DHAMIRA NA UWAJIBIKAJI.YES WE CAN!

26 Dec 2008

MASTANTA KIBWENA (Picture for illustrative purpose only)
CLICK HERE TO READ FULL STORY.

CHAGUZI NDANI YA CCM HAZIISHIWI VIOJA.RUSHWA IMETAPAKAA MNO NDANI YA CHAMA HICHO KANA KWAMBA NI SEHEMU YA KATIBA YAKE.SIO MATUSI KUAMINI KWAMBA PENGINE INGEKUWA RAHISI ZAIDI KWA CCM KUAHIDI KUENDELEZA LIBENEKE LA RUSHWA KWENYE MANIFESTO YAKE YA 2005 KULIKO AHADI ZA MAISHA BORA,MAHAKAMA YA KADHI,NK MAMBO AMBAYO HADI SASA YAMEENDELEA KUWA AHADI ZISIZOTEKELEZEKA.NI WAZI,RUSHWA HUZAA VIONGOZI WABOVU,MAFISADI NA WABABAISHAJI.HABARI MBAYA NI KWAMBA HAKUNA DALILI ZA KUISHA KWA GONJWA HILO HATARI NDANI YA CHAMA TAWALA.TAASISI ZA UMMA ZA KUKABILIANA NA RUSHWA ZINAISHIA KUALIKWA TU KWENYE CHAGUZI "KUZUIA RUSHWA" NA VIONGOZI WAANDAMIZI WA CHAMA HICHO WAMEISHIA KUPIGA KELELE TU (SINA HAKIKA KAMA NI ZA DHATI) KUHUSU RUSHWA KWENYE CHAGUZI,LAKINI SOTE TUNAJUA KWAMBA KELELE ZA CHURA HAZIMZUII NG'OMBE KUNYWA MAJI.ENEWEI,HEBU CHEKI MKASA HUU HAPA CHINI KISHA SOMA HITIMISHO LANGU BAADA YA HABARI HII:
Zikiwa zimesalia siku 14 kufika siku ya uchaguzi wa viongozi wa ngazi ya taifa wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), mambo si shwari katika mchakato wa kumpata mwenyekiti wake. 

Uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika mjini Dodoma Januari 7, mwakani ambapo nafasi ya uenyekiti itagombewa na Janet Kahama, Sophia Simba na Joyce Masunga. 

Hali hiyo, ambayo inazidi kuipaka matope CCM, imedhihirika baada ya mgombea wa nafasi ya Janeth Kahama kuwasilisha rasmi malalamiko kwa Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete, akimtuhumu mpinzani wake, Sophia Simba kwamba amewahonga wajumbe wote wa Mkutano Mkuu rushwa ya Sh. 100,000 ili wampe kura. 

Mbali na tuhuma za rushwa, Simba, ambaye ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utawala Bora), anatuhumiwa pia na Kahama kuwa yeye na wapambe wake wamekuwa wakiitumia Ikulu kuwaomba kura wajumbe wa Mkutano Mkuu. 

Kahama, ambaye ni Mbunge wa Viti Maalum (CCM), amewasilisha malalamiko hayo kupitia barua yake yenye kumbukumbu Na. JBK/01/08 ya Desemba 20, mwaka huu, iliyopelekwa kwa Rais Kikwete, Ikulu, jijini Dar es Salaam. 

Nakala ya barua hiyo, ambayo Nipashe inayo, imepelekwa kwa Katibu Mkuu wa UWT Taifa na Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba. 

Makamba alipoulizwa na Nipashe juzi jioni kama amepokea nakala ya barua hiyo, alithibitisha kuipokea. 
Simba anadaiwa kutoa hongo hiyo kupitia kadi alizochapisha kwa lengo la kuwatakia heri ya Mwaka Mpya wajumbe wa Mkutano Mkuu wa UWT Taifa. 

Kadi hizo, ambazo zinadaiwa kusambazwa na Diwani wa Kata ya Ilala, Moshi Kondo, zina picha, jina na saini ya Waziri Simba, kalenda ya Mwaka Mpya wa 2009 na nembo ya CCM. 

Barua hiyo yenye kichwa cha habari kisemacho: `Yah: Malalamiko dhidi ya Mhe. Sophia Simba kugawa vipeperushi mikoani`, Kahama anamueleza Mwenyekiti Kikwete kama ifuatavyo: 

``Kwa heshima ya pekee, nakuomba uhusike na mada ya barua hii kama inavyosomeka hapo juu. Mheshimiwa Mwenyekiti, kama unavyofahamu, Jumuiya yetu ya UWT hivi sasa ipo katika mchakato wa uchaguzi wa viongozi wa ngazi ya taifa unaotarajiwa kufanyika mapema mwakani.`` 

``Mimi nikiwa mmoja wa wagombea wa nafasi hiyo ya Mwenyekiti wa Taifa wa UWT, natambua kuwa wagombea wote tulizuiwa na vikao vya UWT Taifa kutoa vipeperushi vya aina yoyote kwa minajili ya kujinadi kwa wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa wa UWT.`` 

``Lakini, ajabu ni kwamba, mgombea mwenzangu, Bi Sophia Simba amechapisha kalenda na kadi za `Heri ya Mwaka Mpya` zenye picha yake na nembo ya CCM na kuzisambaza kwa wajumbe wote wa Mkutano Mkuu wa UWT Taifa nchi nzima, ndani zikiwa na kitita cha Sh. 100,000 (kwa kila kadi).`` 

``Mheshimiwa Mwenyekiti, nalazimika kukuandikia waraka huu ili kukupa angalizo juu ya suala hilo hasa ikizingatiwa kuwa Mheshimiwa Sophia Simba ni Waziri katika ofisi yako mwenye dhamana ya Utawala Bora.`` 

``Hivyo hatua yake na nembo ya CCM, inakwenda kinyume na kanuni za uchaguzi za CCM, kipengele cha Miiko ya Kuzingatiwa wakati wa Shughuli za Uteuzi na Uchaguzi`, ibara ya 33 kifungu kidogo cha 14 kinachosema: `Ni mwiko kutumia makaratasi ya kampeni nje ya utaratibu wa chama au kutumia vishawishi vya aina yoyote ile kwa minajili ya kupata kura.`` 

``Je, hatua hii ya Mheshimiwa Simba kuchapisha nyaraka hizo zenye picha yake na nembo ya CCM na kuzitawanya nchi nzima, si uvunjaji wa makusudi wa kanuni hizo za uchaguzi za CCM tena kipindi hiki cha kuelekea kwenye Uchaguzi Mkuu wa UWT?`` 

``Je hatuoni kwamba hatua yake hiyo ambayo haijakemewa mpaka sasa ni kielelezo kingine cha ubabe na matumizi mabaya ya madaraka yake kama Waziri tena mwenye dhamana ya Utawala Bora? 

Nasisitiza hili kwa sababu Mheshimiwa Simba na wapambe wake wamekuwa wakipita mikoani na kupotosha wapigakura kuwa yeye ndiye chaguo la Ikulu.`` 

``Mheshimiwa Mwenyekiti, nawasilisha kwako waraka huu wenye malalamiko haya ili uweze kujua nini kinaendelea na kuchukua hatua kwani kama kitaachwa, kinaweza kujenga matabaka ndani ya UWT na mpasuko usio wa lazima ndani ya chama chetu, hasa pale hisia za mgombea mmoja kuandaliwa mazingira ya ushindi dhidi ya wenzake zinapoanza kujengwa.`` 

``Naambatanisha moja ya vipeperushi hivyo vya Mheshimiwa Simba vilivyosambazwa mikoani kinyume na utaratibu nilioueleza hapo juu.`` 

Makamba alipoulizwa na Nipashe juzi, licha ya kukiri kupokea nakala ya barua hiyo ya Kahama, alimtaka mwandishi kama ana swali lolote kuhusiana na suala hilo, akamuulize Rais Kikwete kwa vile ndiye aliyeandikiwa barua hiyo. 

``Mtafute Mwenyekiti wa CCM, yeye ndiye aliyeandikiwa barua, aliyeandikiwa ndiye anayejibu. Mimi nimepewa nakala, anayepewa nakala, anaarifiwa tu,`` alisema Makamba. 

Nipashe ilipowasiliana na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Ikulu, Salvatory Rweyemamu, alisema kwa vile malalamiko ya Kahama yanahusiana na Chama, anayepaswa kujibu suala hilo ni Katibu Mkuu. 

Baada ya Makamba kuulizwa tena, alisema: ``Mimi sina cha kusema, sijaisoma (hiyo barua), sijajua maudhui. 

Nitakapoisoma na kujua maudhui, nitatoa maoni yangu.`` 

Kahama alipoulizwa na Nipashe jana kama barua hiyo ndiye aliyeiandika, hakukiri wala kukanusha, badala yake alisema kwa sasa hawezi kuzungumza lolote kwa vile kipindi hiki ni cha sikukuu ya Krismasi, ambayo yeye kama Mkristo anapaswa kuitukuza. 

``Sina comments (maoni) kabisa kabisa, mpaka nionane na Katibu Mkuu. Pia mimi ni Mkristo na kipindi hiki ni cha Krismasi,`` alisema. 

Naye Diwani wa Kata ya Ilala, Moshi Kondo, alipoulizwa juzi, alikataa kuzungumzia suala hilo, badala yake alimtaka mwandishi akamuulize Simba. 

``Kwani Sophia Simba mimi ni nani kwake?`` alihoji Kondo, ambaye alipojibiwa na mwandishi kuwa ``Simba anadaiwa kuwa ni mtu wake wa karibu``, alisema: ``Nenda kamuulize Simba.`` 

Tangu juzi hadi jana jioni Nipashe ilimtafuta Simba bila kumpata na baadaye kuelezwa na mmoja wa wanafamilia yake kuwa yuko safarini Malaysia. 

CHANZO:Nipashe

WAKATI MAMA KAHAMA AMETUMIA HAKI YAKE YA MSINGI KAMA MGOMBEA NA MWANANCHAMA WA UWT/CCM KUWASILISHA MALALAMIKO YAKE KWA MWENYEKITI WA CCM TAIFA (JK),NADHANI ANGEWEZA PIA KUWASILISHA TUHUMA HIZO POLISI AU TAKUKURU.HIVI KUTOA RUSHWA SI NI KOSA LA JINAI?JE MAMA KAHAMA YUKO MORE CONCERNED NA RUSHWA HIYO KUATHIRI NAFASI YAKE YA KUCHAGULIWA KULIKO UKWELI KWAMBA MTUHUMIWA (SOPHIA SIMBA) SIO WAZIRI TU BALI NI WAZIRI MWENYE DHAMANA YA UTAWALA BORA (ISOMEKE MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA)?


The Afghan chieftain looked older than his 60-odd years, and his bearded face bore the creases of a man burdened with duties as tribal patriarch and husband to four younger women. His visitor, a CIA officer, saw an opportunity, and reached into his bag for a small gift.Four blue pills. Viagra...CLICK HERE FOR FULL STORY


25 Dec 2008


Kiongozi wa mapinduzi hayo,Kapteni Moussa Dadis Kamara,aliyejitangaza kiongozi mpya wa Guinea baada ya kifo cha Rais Lansana Conte.Kwa habari zaidi,BONYEZA HAPA.


HIVI TUNA UHABA MKUBWA SANA WA WATENDAJI NA VIONGOZI WAZURI HADI TUENDELEE KUWANG'ANG'ANIA HATA WALE WALIOKWISHAFANYA MADUDU HUKO NYUMA?KUNA STORI KATIKA GAZETI LA MWANANCHI KUHUSU ALIYEKUWA MKURUGENZI WA MANISPAA YA TEMEKE,JOHN LUBUVA,AMBAYE ALISIMAMISHWA KAZI KUTOKANA NA SAKATA LA UBOMOAJI NYUMBA HUKO TABATA DAMPO.CHA AJABU ETI KWA SASA NI MKURUGENZI WA MANISPAA YA SHINYANGA VIJIJINI.HII SIO TU DHARAU KWA WAKAZI WA MANISPAA HIYO ILIYOLETEWA "MTENDAJI MPYA" BALI PIA NI MUENDELEZO WA HAKA KAMTINDO KA KUNG'ANG'ANIA VIONGOZI WALIOPUNGUKIWA NA SIFA.JE,KUMREJESHA KIONGOZI HUYO MADARAKANI HAKUWEZI KUWA KICHOCHEO KWA VIONGOZI WENGINE KUREJEA MADUDU KAMA YA MWENZAO ALIYEBORONGA,AKAPEWA MAPUMZIKO MAFUPI KISHA AKAREJESHWA MADARAKANI?TANGU LINI ADHABU KWA MAKOSA YA UONGOZI IKAWA KUHAMISHWA KUTOKA TEMEKE NA KUPELEKWA SHINYANGA?HIVI AKILIKOROGA TENA HUKO SHINYANGA ITAKUWAJE?THIS IS NOT ONLY UNFAIR BUT INAKERA NA KUCHUKIZA PIA.


Serikali imeridhia Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMA- JKT), liongezewe nguvu kiutendaji na kuwa kampuni ya ulinzi itakayotoa ushindani kwa makampuni binafsi ya ulinzi yanayotoa huduma hiyo kwa kiwango kisichoridhisha. 

Kwa sasa SUMA, imejikita katika ujenzi wa nyumba za serikali, barabara na kutengeneza samani. 

Uamuzi wa JKT kuwa na kampuni ya ulinzi, una lengo la kuajiri vijana wanaohitimu mafunzo ya awali ya kijeshi. 

Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni hiyo, Kanali Ayoub Mwakang’ata, alitoa taarifa hiyo jana wakati akihutubia katika kilele cha mafunzo ya Operesheni Uadilifu yaliyokuwa yakifanyika katika Kambi ya 835 JKT Mgambo wilayani Handeni. 

Katika taarifa yake alisema kuwa serikali kwa kushirikiana na Jeshi hilo wameridhia kampuni hiyo kuanza kazi rasmi mapema mwakani. 

Kampuni hiyo imepanga kuboresha huduma za ulinzi kwa kuajiri askari waliopitia Jeshi hilo pekee na kuwasambaza katika maeneo mbalimbali nchini kote wakichuana na makampuni mengine yaliyoko sasa, lakini bila ya kuathiri utendaji wao. 

``Suma JKT itakuwa kampuni ya ulinzi rasmi kuanzia mwakani na itachukua vijana waliohitimu mafunzo ya awali ya kijeshi na si askari wa akiba wa mgambo, mpango huu ni maalumu kwa ajili ya kuwasaidia vijana kama hawa kupata ajira za uhakika baada ya kuhitimu mafunzo haya… na ukweli ni kwamba hatua hii itakuwa ni changamoto kwa vijana wengi wanaomaliza darasa la saba na kidato cha nne kujiunga JKT,``alisema. 

Awali Ofisa Utumishi wa JKT Makao Makuu, Meja Elvis Massawe alipohojiwa kuhusiana na hatua iliyofikiwa hadi sasa na Kitengo hicho cha SUMA alikiri kwamba Ofisi hiyo imeshapokea maombi zaidi ya robo tatu ya vijana waliohitimu katika Jeshi hilo nchi nzima wakisubiri kuajiriwa rasmi. 

Kwa mujibu wa Ofisa huyo ni kwamba Kampuni hiyo mbadala ya ulinzi itachukua askari wa rika mbalimbali bila kujali umri wao na kwamba bado jeshi hilo linapokea maombi ya yawanaotaka kujiunga na kampuni hiyo...

CHANZO: Nipashe

SINA HAKIKA KAMA UMEFANYIKA UTAFITI WA KUTOSHA KUHUSIANA NA MAAMUZI HAYA MAZITO (IT'S PERSONAL KWANI NAMI NI MMOJA KATI YA WALIOPITIA JKT KWA MUJIBU WA SHERIA MIAKA YA 90).NAAMINI TATIZO KUBWA LINALOKWAZWA KUIREJESHA JKT KUWA KAMA YA ENZI HIZO NI PAMOJA NA MIPANGO DHAIFU ISIYOANGALIA MBALI.SIJUI BABA WA TAIFA HUKO ALIKO AKISIKIA JKT INATAKA KUGEUZWA KAMPUNI YA ULINZI ATAJISIKIAJE LAKINI KWA HAKIKA NI JAMBO LINALOTIA SHAKA SANA HASA IKIAZINGATIWA KWAMBA JESHI SIO TAASISI YA BIASHARA.NI VIGUMU KUTUAMINISHA KWAMBA JKT ITAWEZA KUHIMILI USHINDANI WA KIBIASHARA KATIKA SEKTA YA ULINZI BINAFSI ILHALI UFANISI WA VITENGO VYA KIBIASHARA KATIKA JESHI HILO (KWA MFANO SUMA NA MRADI WA KOKOTO KUNDUCHI) WENYE MUSHKELI.

JKT INGEWEZA KUWA KITUO CHA KUZALISHA AJIRA KWENYE SEKTA YA KILIMO NA HATA UJASIRIAMALI IWAPO KUTAKUWA NA MAANDALIZI SAHIHI.MSISITIZO WA JKT NI KUWAANDAA VIJANA KULITUMIKIA TAIFA LAO KWA UZALENDO NA SIO KWENDA KULINDA MALI ZA WATU (INCLUDING MAFISADI).HATA KAMA WAZO LA BIASHARA YA ULINZI NI ZURI BADO KUNA WASIWASI KUHUSU MASLAHI YA VIJANA HAO,JAMBO AMBALO LISIPOANGALIWA KWA MAKINI LINAWEZA KUZAA MAJAMBAZI BADALA YA WALINZI BINAFSI.ULINZI NI TAALUMA NYETI NA ISIPOTENGENEZEWA SERA MAKINI INAWEZA KUZAA MAYHEM KATIKA JAMII.

24 Dec 2008


SAFARI YA MAPAMBANO DHIDI YA UFISADI BADO NI NDEFU NA YENYE VIKWAZO LUKUKI.KATIBA NA SHERIA ZINAZOWATOFAUTISHA VIONGOZI NA WANANCHI WA KAWAIDA ZINATUMIKA KAMA KINGA DHIDI YA MATENDO AMBAYO KWA NAMNA MOJA AU NYINGINE YANAHUSU UVUNJAJI WA SHERIA.PIA KINGA HIZO ZINAWEZA KUWA KICHOCHEO KIZURI KWA VIONGOZI WAPYA KWANI KAMA WATANGULIZI HAWAKUCHUKULIWA HATUA WALIPOBORONGA (KWA VILE WANA KINGA) THEN KWANINI WALIOPO MADARAKANI WAOGOPE KUBORONGA?HIVI KAMA WENZETU HUKO MAREKANI WANADIRIKI KUMHOJI RAIS MTEULE,IWEJE VIGUMU KWETU KUMHOJI RAIS MSTAAFU?ANYWAY,SOMA STORI HII HAPO CHINI KISHA TUENDELEE NA MJADALA WETU
Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa, hachunguzwi kwa kosa au tuhuma yoyote ya jinai, imeelezwa. Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), katika taarifa yake kwa umma iliyotolewa Dar es Salaam jana, ilisema uvumi kuwa Rais huyo mstaafu anachunguzwa na vyombo vya dola ikiwamo taasisi hiyo, hauna ukweli wowote. 

Tamko la taasisi hiyo limekuja huku kukiwa na uvumi katika baadhi ya vyombo vya habari kuwa kiongozi huyo anachunguzwa na Takukuru, kutokana na vitendo vingi vya ufisadi vinavyodaiwa kufanywa wakati wa uongozi wake. 

Tayari mawaziri wawili Basil Mramba na Daniel Yona waliowahi kushika nyadhifa nyeti katika Serikali ya Awamu ya Tatu ukiwamo uwaziri wa Fedha, wameshafikishwa mahakamani kwa tuhuma za kutumia madaraka yao vibaya na kuisababishia serikali hasara ya Sh bilioni 11.7. 

Lakini pia baadhi ya watuhumiwa katika kesi za kuchota mabilioni ya fedha katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) katika Benki Kuu (BoT), ambao wamefikishwa mahakamani, wanadaiwa kufanya wizi huo kati ya mwaka 2004 na 2005 kipindi ambacho Rais Mkapa alikuwa madarakani. 

Ofisa Uhusiano wa Takukuru, Doreen Kipwani alisema jana kuwa, taasisi yake haina uwezo wa kumchunguza kiongozi huyo kutokana na Katiba ya nchi kutotoa nafasi hiyo katika Ibara ya 46 (3) ya Katiba ya Tanzania. Kapwani alieleza kuwa taasisi yake inaheshimu Katiba na ina wajibu wa kuilinda na kuheshimu matakwa hayo ya Katiba. 

“Takukuru inawafahamisha wananchi kwamba uvumi huu hauna ukweli wowote, hatumchunguzi kiongozi huyu kwa kosa au tuhuma yoyote ya kijinai,” alisema. “Ni kwa msingi huu, Takukuru imeona ni vyema kuwafahamisha wananchi ukweli dhidi ya uvumi huu. 

Tukumbuke wakati wote kwamba taifa letu lina Katiba ya Nchi ambayo imeweka misingi mikuu ya kuendesha nchi yetu, haki na wajibu wa kila Mtanzania. Katiba kama sheria mama imeweka pia mipaka katika kushughulikia mambo mbalimbali ya nchi na kwa mantiki hii, haina budi kuheshimiwa wakati wote.” 

Kifungu hicho cha Katiba kinaeleza kuwa “Ni marufuku kumshitaki au kufungua mahakamani shauri lolote la jinai au la kumdai mtu aliyekuwa anashika madaraka ya Rais baada ya kuacha madaraka hayo kutokana na jambo lolote alilofanya yeye kama Rais wakati alipokuwa bado anashika madaraka ya Rais kwa mujibu wa Katiba hii.” 

Kapwani alisisitiza kuwa Takukuru itaendelea kufanya kazi zake kwa mujibu wa Katiba na sheria ya nchi na sio vinginevyo. Katika siku za karibuni, baadhi ya vyombo vya habari vimekuwa vinaripoti kuwa Mkapa anachunguzwa na Takukuru licha ya kuwa ana kinga ya kutoshitakiwa. 

Vyombo hivyo vimekuwa vikimwandama kwa madai kuwa ufisadi mkubwa umefanyika katika kipindi ambacho alikuwa madarakani. Watu wenye mtazamo huo wamekuwa wanataka kiongozi huyo aondolewe kinga na afikishwe mahakamani kujibu tuhuma mbalimbali za ufisadi. 

Wiki hii, Mbunge wa Moshi Mjini, Philemon Ndesamburo alieleza kusudio la kuwasilisha hoja binafsi katika kikao kijacho cha Bunge kuomba kifungu kinacholinda marais wastaafu kutoshitakiwa kirekebishwe. Mkapa anatajwa katika tuhuma kuhusu ununuzi wa ndege ya Rais, ununuzi wa rada, wizi wa mabilioni ya EPA, uuzaji wa nyumba za serikali, mikataba yenye utata kama ya NetGroup, Alex Stewart na ubinafsishaji wa mgodi wa Kiwira.
CHANZO: Habari Leo

UFAFANUZI HUO WA TAKUKURU HAUWEZI KUZIMA KELELE ZA WANAOTAKA KUMUONA TUHUMA DHIDI YA MKAPA ZINATHIBITISHWA KWENYE VYOMBO VYA SHERIA.PAMOJA NA KUILINDA NA KUIHESHIMU KATIBA,TAKUKURU INA WAJIBU WA KULINDA NA KUTETEA RASLIMALI ZA WATANZANI ZINAZOFUJWA NA MAFISADI.LAKINI TUKIACHANA NA EXCUSE HIYO YA TAKUKURU (WAMESHATOA LUKUKI) THIS IS A WAKE UP CALL KUHUSU HIZI KINGA DHIDI YA VIONGOZI WASTAAFU (NA PENGINE HATA KWA WALIO MADARAKANI).WAKATI WAZO LA KINGA NI ZURI LIKITUMIWA VIZURI,KWA MFANO DHIDI YA WANAOTAKA KUDHALILISHA VIONGOZI KWA SABABU BINAFSI AU KISASI,WAZO HILO NI HATARI KWA VIONGOZI WALIOZITUMIA VIBAYA OFISI ZAO WALIPOKUWA MADARAKANI.MAHALA PEKEE PANAPOWEZA KUMSAFISHA MKAPA NI MAHAKAMANI NA WALA SIO KWA KAULI ZA KULINDANA KAMA HIZO ZA TAKUKURU.

23 Dec 2008


WAKATI Ripoti ya kitaalam ikionyesha namna bora ya kupunguzwa matumizi ya magari ikiwamo ya kifahari maarufu kama mashangingi, serikali imeanza utekelezaji wa mpango mwingine mkubwa wa kuingiza magari mapya 792 kutoka Japan.

Mpango huo mkubwa wa serikali umekuja wakati ripoti ya kitaalamu inayotaka ijipunguzie matumizi yasiyo ya lazima katika ununuzi wa magari ikiwemo ya kifahari ikiwa imewasilishwa mezani kwa Katibu Mkuu Kiongozi Philemon Luhanjo tangu Aprili mwaka huu.

Waziri Mkuu Mizengo Pinda ambaye wiki moja iliyopita alitoa angalizo kwa makatibu na manibu makatibu wakuu wa wizara kuhusu kupunguza matumizi ya magari ya kifahari, alinukuliwa na gazeti dada la The Citizen, akisema serikali haiwezi kupiga marufuku ununuzi wa magari hayo wakati imeshaagiza lakini alisisitiza kuwa hiyo itakuwa mzigo wa mwisho kuagizwa na mashangingi kiasi hicho.

Ingawa Pinda hakufafanua, lakini duru huru zaidi za habari kutoka serikalini zilidokeza gazeti hili jijini Dares Salaam jana kwamba, tayari magari 300 yalishaingizwa chini ya mpango huo. "Sehemu kubwa ya magari hayo ni Toyota Pickup, tayari 300 yameingizwa nchini chini ya mpango huo maalumu wa serikali," zilisema duru hizo za habari.

Kwa ufafanuzi zaidi, duru hizo zilisema katika orodha hiyo pia yapo mashangingi Vx na GX ambayo jumla yao ni kati ya 100.

Chini ya mpango huo, duru za habari zilisema gari nyingine ambazo ni nyingi ni pamoja na Toyota Land Cruiser Hard Top ambazo kwa takwimu za kiserikali moja hugharimu kati ya sh 72 hadi 75 milioni.

"Ukiacha Vx na Gx 100, magari mengine mengi katika orodha hiyo ni Toyota Land Cruiser Hard Top na Pickup ndiyo mengi katika orodha hiyo ya magari 792," kilifafanua zaidi chanzo hicho.

Waziri Mkuu Pinda alikaririwa jana na gazeti dada la Mwananchi, The Citizen, katika mahojiano maalum akisema uamuzi wa kuzuia ununuzi wa magari hayo hauwezi kuchukuliwa kwa sasa, kwa kuwa tayari yameshaagizwa na yataanza kuingia nchini hivi karibuni.

“Uamuzi wa kuzuia ununuzi wa magari hayo hauwezi kufanyika sasa kwa kuwa magari 800 tayari yameshaagizwa kutoka kampuni inayoyatengeneza nchini Japan na yanatarajiwa kuanza kuingia nchini hivi karibuni,” alisema Pinda katika mahojiano hayo.

Hata hivyo, Pinda alieleza kuwa katika mwaka wa fedha ujao mambo yatakuwa tofauti kutokana na kuwataka makatibu wakuu kutoagiza magari hayo na fedha zitazopatikana katika zoezi la kuacha kununua magari hayo zinunue matrekta ambayo yatakuwa na matokeo yanayoonekana katika kilimo.

Hakuna mtu anaweza kufa kwa kutopanda gari la kifahari (Toyota Land Cruiser VX, GX) lakini kwa kukosa chakula itakuwa ni tatizo,” alisema Pinda katika mahojiano hayo.

Alisema uamuzi wake huo umekuwa ukiungwa mkono na Rais Jakaya Kikwete, ukiwa umelenga kumkomboa mkulima ambaye amekuwa anatumia jembe la mkono kwa miaka 47 ya uhuru wa nchi hii.

“Magari haya ya kifahari yamekuwa yananunuliwa kutokana na baadhi ya watumishi (wakurugenzi) kutaka kuendana na wakati wa magari ya kifahari yaliyopo sokoni,” alisema Pinda huku akisema serikali sasa inataka kuondokana na dhana hiyo.

Alipoulizwa mbona serikali imeamua kuendelea kununua magari hayo japokuwa yamekuwa yanasemwa kuwa ni mzigo kwa serikali, Pinda alisema wakati anaingia tayari magari yalikuwa yameshaagizwa na hivyo mpango huo utaanzia kwenye bajeti ijayo ya serikali.

Aliongeza kuwa “Nimeongea na makatibu wakuu wiki iliyopita nimewaambia kuhusu suala hili la uagizaji magari ya kifahari, sasa tuachane nalo na badala yake tujikite kwenye kilimo cha kisasa,”

Duru hizo zikieleza kwa kina mpango huo, Ripoti ambayo iko kwa Luhanjo na gazeti hili kufanikiwa kuona nakala yake, inaonyesha namna bora ya serikali kupunguza ununuzi wa magari hasa ya kifahari.

Katika mpango huo, moja ya jambo lililopendekezwa na watalaamu ni kuhakikisha gari la moja aina ya VX au Gx hubadilishwa na kukunuliwa jingine kila baada ya miaka saba tofauti na sasa, ambapo waziri, naibu au makatibu wakuu hubadili magari hayo kila baada ya miaka miwili.

Ripoti hiyo pia inaonyesha orodha ya viongozi wanaopaswa kutumia magari hayo kwa kupunguza viongozi wanaopaswa kutumia Vx na Gx, ambao wanapaswa kutumia ni mawaziri, manaibu, makatibu wakuu na manaibu wao, huku kuanzia wakurugenzi wakipasawa kutumia magari mengine ikiwemo Land Cruiser za kawaida.

Pia kumekuwa na pendekezo la kufuata utaratibu ambao hutumiwa na serikali kama ya Afrika Kusini, Namibia na Botswana ambazo hutumia Kampuni ya Emperial kwa ajili ya usimamizi wa kiteknolojia kwa ajili ya magari yote ya serikali ili kuyaangalia na kudhibiti yasitumike katika shughuli binafsi.

Emperial kwa kutumia teknolojia hiyo huweza kuonyesha hatua ya kila gari kwa kutumia mfumo maalumu wa usalama na pia kuzuia wizi hata wa mafuta katika magari ya serikali ambayo sasa hivi hakuna mfumo wa kuyadhibiti.

CHANZO:Mwananchi

NANI KASEMA MATREKTA KWA WAKULIMA NI MUHIMU KULIKO NYONGEZA YA MASHANGINGI KWA WAHESHIMIWA?EBO?NYIE MNATAKA WAHESHIMIWA WAKAGUE MAENDELEO WAKIWA KWENYE MATREKTA?UHESHIMIWA NI PAMOJA NA KUWA KWENYE GARI LA KIFAHARI.HIZI NDIZO PRIORITIES ZETU ZITAKAZOMWEZESHA KILA MTANZANIA KUWA NA MAISHA BORA HIVI PUNDE TU!



PICHA HIZI ZINAONYESHA UHARIBIFU ULIOSABABISHWA NA VURUGU ZINAZOENDELEA NCHINI UGIRIKI KUFUATIA POLISI KUMUUA MTOTO MMOJA.BAADA YA KUANGALIAPICHA HIZO,HEBU SOMA HABARI IFUATAYO KUHUSU VIFO VYA WATOTO WATATU HUKO KILIMANJARO.
WATOTO watatu wa jamii ya wafugaji wa Kimasai, wameuawa kwa kupigwa risasi na askari polisi waliopo kwenye mazoezi ya kulenga shabaha katika Kijiji cha Embukoi, wilayani Siha, mkoani Kilimanjaro.

Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Embukoi, Peter Pekasi, alisema jana kuwa tukio hilo lilitokea majira ya saa 10 jioni, ambapo watoto hao walikuwa wakipita eneo kwenda kusaga nafaka katika mashine iliyo jirani na kijiji hicho.

Mtendaji huyo aliwataja watoto wanaodaiwa kuuawa kuwa ni Lyomo Orkwari (7), Laata Mollel (15) na Samwel Josia(8), wote wakazi wa kijiji hicho cha jamii ya Masai.

Pekasi alisema eneo la tukio limekuwa likitumiwa kwa muda mrefu kama kituo cha kulenga shabaha kwa askari waliopo mafunzoni katika Chuo cha Mafunzo ya Polisi Moshi (CCP) na kuhatarisha maisha yao.

Alisema baada ya tukio hilo walitoa taarifa kwa Mkuu wa Wilaya ya Siha, Anarose Nyamubi.

Kamanda wa Polisi mkoani Kilimanjaro, Lucas Ng’hoboko, alipoulizwa kuhusiana na tukio hilo, alisema hana taarifa kamili za tukio hilo na kuongeza kwamba ametuma maafisa wake eneo la tukio.

“Jamani nimepata taarifa hizo muda mfupi kabla hujaja hapa, nimetuma maofisa wangu eneo la tukio, kwa sasa siwezi kuzungumzia chochote, nitatoa taarifa zaidi baada ya kupata maelezo ya kina kutoka kwa askari wangu,” alisema Ng’hoboko.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Siha, Nyamubi, akizungumza kwa njia ya simu jana, alithibitisha kupata taarifa hizo, lakini hakuwa tayari kuzungumzia kwa undani na kwamba ametuma maofisa wake eneo la tukio.



NA HAITOSHANGAZA IWAPO HAKUNA ATAKAYEWAJIBIKA KWA VIFO VYA WATOTO HAO WASIO NA HATIA.


22 Dec 2008

AISEE,ILE ISHU YA KUMTWANGA GEORGE W BUSH NA KIATU INAENDELEA KUVUTA HISIA.LATEST,JAMAA ALOTENGENEZA VIATU VILIVYOTUMIKA KUMTWANGA BUSH AMEJIKUTA AKIPATA DILI KIBAO,YAANI CHATI NDIO IMESHAPANDA.SINTOSHANGAA TUKISKIA NA HUKO HOME SHOE-SHINER FLANI KAPATA DILI BAADA YA KIATU ALICHOKUWA AKIKIHUDUMIA KUTUMIKA KUMRUSHIA FISADI FLANI....NAJUA HIYO NI PIPE-DREAMING KWA VILE MAFISADI WENYEWE WANALETWA MAHAKAMANI NA MASHANGINGI,WAKIWA LUPANGO WANALAZWA VIP KAMA KEMPINSKI,NA WAKIPATA DHAMANA WANACHUKULIWA NA MA-VOGUE YAO!BACK TO STORI YA IRAQI,KONG'OTA HAPA USOME ZAIDI

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.