12 Oct 2011


Hello to all you lovely people,

Miss Jestina George Blog has been nominated for the Blog of the Year category at the 2011 (BEFFTA) Black Entertainment Film Fashion Television and Arts Awards. Please show your support by voting through this link, http://www.beffta.com/voting, under category select News 4. Blog Of the Year & Under Nominee select Miss Jestina George then submit your vote. Voting closes on 14th October and your vote would be very much appreciated. If you have any questions please feel free to contact this email.

Thank you for your time,


--
Jestina George
CEO & Founder - MISS JESTINA GEORGE BLOG
Telephone: +447404332910
Facebook: JestinaGeorge


MSIBA WA MTANZANIA MWENZETU MZEE SAID MUHAMMAD SIKAMKONO

Tunaskitika kuwataarifu kuhusu kifo cha Mtanzania mwenzetu Mzee Said Muhammad Sikamkono kilichotokea jana tarehe 11/10/2011 mchana katika hospitali ya Queen Elizabeth, Woolwich, London.
Mipango ya mazishi inaendelea na mtaendelea kujulishwa. Kwa wakati huu ambao tutakuwa tunasubiri kupata taarifa ya mazishi, mwenye kuweza kuchangia chochote au mwenye kuhitaji kujua zaidi kuhusu msiba huu, tunaomba awasiliane na;
Sheikh Ayub kwa namba; 07944930708
AU
 Said Surur kwa namba; 07538063536
AU
Mr. Haruna Mbeyu kwa namba; 07813539025.

“MWENYEZI MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU SAID MUHAMMAD SIKAMKONO MAHALI PEMA.  MUNGU AMETOA NA MUNGU AMETWAA, JINA LAKE LIBARIKIWE”

11 Oct 2011


Nyakati za Ujamaa na Kujitegemea tulifundishwa kuwa maadui wakubwa wa maendeleo ni ujinga,maradhi na umasikini.Na tuliaswa kuhakikisha tunapambana nao kwa nguvu zote.Lakini mambo haya matatu si binadamu bali ni hali ya kimaisha.

Kibinadamu,tulifundishwa kuwa maadui wakubwa ni wanyonyaji-makupe,makabaila,mamwinyi,ma-mangi meza,na viumbe wengine kama hao.

Baada ya itikadi ya Ujamaa kuzikwa hai na aliyekuwa Rais wa Awamu ya Pili,Ali Hassan Mwingi na kundi lake,utambulisho wa maadui zetu ulibaki wa kusuasua.Lakini tulipoingia kwenye siasa za vyama vingi,wakazuka maadui wapya.Kundi moja-ambalo na akina sie (waropokaji au vimbelembele-kama wanavyotuita watawala) lilikuwepo hata zama za Ujamaa.Uzuri au ubaya ni kwamba nyakati hizo haikuwa rahisi kupingana au kuwa na mawazo tofauti na watawala.Na 'vimbelembele' na 'waropokaji' waliishia jela kama si kusumbuliwa kwa muda wao wote wa uhai wao.

Baada ya mageuzi ya kisiasa na kiuchumi,kundi hili limeendelea kunyanyaswa japo kwa wakati huu sio waziwazi.Akina Marehemu Katabalo,Kolimba na wengineo ni majeruhi wa hasira za watawala na washirika wao dhidi ya kundi hili.Na hadi leo wapo wenzetu wengi tu ambao wananyanyaswa na vyombo vya dokla kwa kosa la kusema ukweli ambao watawala na washirika wao hawataki usemwe.

Lakini kundi jipya la maadui baada ya ujio wa mageuzi ni vyama vya upinzani.Pamoja na CCM kuridhia kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi,wapinzani wameendelea kujengewa picha kwenye jamii kama watu wa kuogopwa kama ukoma.Wanahujumiwa kwa fedha za walipa kodi,wanasemwa vibaya na kupachikwa majina mabaya kuliko makupe,makabaila,nk.

'Kosa' kubwa  la wapinzani ni kutaka kuwanyang'anya watawala na washirika wao fursa ya kuendelea kutukandamiza.Wanaonekana kama walafi na waroho wa madaraka (watakuwaje waroho wakati wameingia juzi tu ilhali kuna watu wanazeekea madarakani?).Hoja inayojengwa ni kwamba walikimbia CCM na kujiunga na upinzani si kwa minajili ya kuutumikia umma kwa siasa bali kutokana na tamaa,ulafi na uroho wao wa madaraka.

Ukimsikia mtu kama Nape Nnauye akiwazungumzia wapinzani unaweza kabisa kuhisi kuwa anawazungumzia Taliban au Al-Shabaab.Picha inayojengwa ni ya viumbe hatari kuliko virusi vya ukimwi.

Kwa muda mrefu CCM imekosa sauti za kusisitiza mshikamano wa kitaifa (ambapo hata wapinzani wana jukumu hilo) na badala yake nguvu nyingi zimeelekezwa katika kupanda mbegu ya chuki.Wapinzani wanaonyeshwa kama sio Watanzania,na pale inapobidi kuwakubali kuwa ni Watanzania wenzetu basi jitihada zinafanywa kujenga picha kuwa wenzetu hao wanataka kuitumbukiza nchi yetu kwenye shimo lenye kina kirefu.

'Kosa' jignine la wapinzani ni kutumia nafasi waliyonayo kupigania maslahi ya wananchi,ambao kwa kiasi kikubwa wanaendelea kutapeliwa na watu wanaolipwa mshahara kwa kazi ya kuwawakilisha-I mean Wabunge wetu.Hatuhitaji kuingia kwa undani kuhitimisha kuwa wengi wa wabunge wetu ni sawa na majambazi tu ambao wanalipwa mishahara minono pasipo kuwatumikia wapiga kura wao ipasavyo.Nasisitiza,NI BAADHI TU ya wabunge.

Sasa katika pitapita zangu mtandaoni nimekutasna na habari ifuatayo ambayo kwa hakika imenitia nguvu sana.Kaimu Mwenyekiti wa UVCCM, Benno Malisa ameonyesha ukomavu wa hali ya juu kisiasa kwa kuongea masuala ambayo kwa hakika ni kwa maslahi ya taifa na si ya kichama.

Najua kuna watakaomsema vibaya-hususan ndani ya chama chake-lakini uzuri wa ukweli ni kwamba ukishawekwa hadharani,atakayeumia na aumie lakini hakuna wa kuufuta.Wapo watakaodai Malisa ameanza kumpigia debe mmoja wa wanaotajwa kutaka Urais 2015 (nadhani itakuwa ni Lowassa) na wengine wanaweza kumtuhumu kuwa huenda hata yeye (Malisa) ana nia ya kugombea urais.

Sijawahi kumsifia Malisa lakini kwa hili NINAMPA TANO.Namsihi apuuze tuhuma zote zitakazoelekezwa kwake kwa 'kosa' la kusema 'yasiyopaswa kusemwa.' Laiti tukiwa na viongozi wanaodiriki kueleza hisia zao pasi kuhofia kuwachukiza watu fulani (na wanachokiongea kuwa chenye maslahi kwa umma) basi kwa hakika tunaweza kufanya mijadala muhimu kuhusu taifa letu na kuzika chuki zisizo za msingi dhidi ya wale wanaoongea tusiyopendezwa nayo.

Nisiandike mengi,hebu soma habari ifuatayo:

UVCCM yataka CCM isiifuatefuate Chadema
Monday, 10 October 2011 22:27
Waandishi wetu, Arusha 
KAIMU Mwenyekiti wa Umoja Vijana wa CCM (UVCCM), Benno Malisa amewataka vigogo ndani ya chama hicho tawala kuacha kuingilia mambo ya chama kikuu cha upinzani nchini, Chadema hasa mgogoro wake na madiwani wa Arusha Mjini na badala yake watafute suluhu ya matatizo ya msingi yanayoikabili nchi kama mfumuko wa bei na tatizo la ajira.Akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika katika eneo la Hospitali ya Mtakatifu Thomas, Malisa alisema wapo baadhi ya watu ndani ya CCM ambao siyo wana Chadema lakini wamekuwa wakijihusisha na mgogoro wa chama hicho pinzani. 
Alisema wana CCM hao wamekuwa wakiingilia mgogoro kati ya Chadema na madiwani wake ambao tayari chama hicho kilikwishaamua kuwafukuza na kusisitiza kuwa mambo ya chama hicho pinzani yaachwe yasiingiliwe. 
Kauli hiyo ya Malisa inakuja kipindi ambacho Chadema kimekuwa kikilalamikia baadhi ya mawaziri wa Serikali kupuuza uamuzi wake wa kuwatimua madiwani wake.
Chadema imewahi kumnyooshea kidole Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Tamisemi,) George Mkuchika kwamba alikuwa na ajenda ya siri baada ya kuendelea kuwatambua madiwani hao.
Pia Chadema kimekuwa kikituhumu baadhi ya makada wa CCM mkoa wa Arusha na taifa, kujaribu kuingilia uamuzi huo wa Chadema wa kutimua madiwani hao kutokana na uamuzi wao wa kuingia muafaka wa Umeya wa Arusha. 
Kaimu Mwenyekiti huyo wa UVCCM, alisema si sahihi kwa CCM kutumia hata vyombo vya serikali kudhoofisha demokrasia kwa vyama vya upinzani akionya kwamba
mwisho wa siku matokeo yake hayatakuwa mazuri kwa taifa. 
Alisema demokrasia inapaswa kuachwa ichanue kwa vyama vya upinzani ili kujenga ustawi mzuri wa nchi.

“Nitumie nafasi hii kumuomba Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), kaka yangu (Godbless) Lema kuwa mstari wa mbele katika kuleta umoja na mshikamano hapa mjini na kumaliza tofauti za UCCM na UCDM (U - Chadema) ili wakazi wa Arusha wapate maendeleo. Sasa uchaguzi umekwisha tujenge nchi yetu.” 
Alisema CCM kinapitia katika wakati mgumu hivi sasa na kuonya kwamba badala ya kuisimamia Serikali wapo wanaohangaika kutafuta wachawi na kutuhumu watu. 
“Tuache kabisa. Hili jambo halisaidii chama wala taifa letu, kumekua na dhana na fikra potofu juu ya ushindi wetu wa 2010 matokeo yale na tuliyoyaona Igunga ni funzo kwetu na hasa vijana,” na kuongeza kuwa vijana wengi wameanza kukosa imani na CCM kwa sababu: 
“Tunashindwa kuwaonyesha kuwa tuna majibu ya matatizo yao. Tumebaki tunaimba historia na kumtaja Baba wa Taifa na kutumia nukuu zake bila kuwapa matumaini vijana kuwa Tanzania yao itakua njema, watapata elimu nzuri, afya na itakua ya uhakika.” 
Alisema vijana wanataka kusikia uchumi umekua, ajira zinapatikana, fursa za kujiajiri zipo, mikopo inapatikana na kusisitiza: “Tusipotoa matumaini haya na kuyafikia 2015, wapiga kura milioni sita wapya watatukataa, uelewa wa vijana wa Kitanzania sasa umekua mkubwa. Wanajua haki na wajibu wao tuache kufanyia siasa maisha ya Watanzania.” 
Wanaotaka urais 2015
Akizungumzia mbio za urais kwa mwaka 2015 ndani ya CCM, Malisa aliwataka makada wa chama hicho wanaotaka kuwania nafasi hiyo kuacha kuwagawa vijana na kuvuruga chama akisema kufanya hivyo ni hatari kwa uhai wa chama. 
“Wapo baadhi ya watu wanaopita wenzangu msiishi kwa kutarajia madaraka ya kupewa wapo wengine wanapita wanakusanya CV za vijana na kuwaahidi vyeo vya U-DC. Msipotoshwe na wala msifungwe fikra kwa sababu mmepewa ahadi ya kuteuliwa U DC. Tuna bahati mbaya wapo ambao mpaka leo wanaishi kwa kusubiri U DC wamegeuka kuwa ndiyo mzee na watumwa kifikra, tuukatae utumwa huu UVCCM.” 
“Tusiwe ndiyo mzee. Nawaagiza wenyeviti na makatibu wa mikoa na wilaya zote Tanzania, wafuatilie katika halmashauri zao kujua mipango ya maendeleo inayohusu vijana na kufuatilia utekelezaji wake wakiona hakuna utekelezaji, watumie kamati za siasa za wilaya kuwabana wenyeviti wa halmashauri. Nazitaka wilaya zote zifuatilie zituletee taarifa juu hili jambo. Tusikubali kuwa ndiyo mzee lazima tusimamie maslahi ya Vijana.” 
Alisema huu si wakati Serikali ya CCM kukaa likizo badala yake ifikirie namna ya kufikia matarajio ya Watanzania. 
Dowans
Akizungumzia suala la mitambo ya Dowans Malisa alisema: “Watu waliosababisha hasara wawajibike, walitudanganya. Kama taifa leo tumeshindwa kesi mitambo ile waliyosema haifai leo inatumika na kampuni ya Symbion. Wanatufanya Watanzania mazuzu. Walisema heri tukae giza wakati wao wanatumia majenereta na wanalipiwa na Serikali huku wakinunua aspirini kwa mamilioni.” 
“Leo wanajifanya wazalendo. Nilitarajia wawajibike walidanganya taifa, Serikali ikavunja mkataba. Wakasema mitambo haifai mibovu leo imenunuliwa na Wamarekani na wanatuuzia umeme... wanafiki wametufikisha hapa niwaombe UVCCM na vijana wa vyama vyote tuungane hawa wawajibike.” 
Watunishiana misuli na polisi
Kabla ya kuhutubia, Malisa na msafara wake waliingia katika mgogoro na vyombo vya dola, baada ya kufanya maandamano na mikutano ya uzinduzi wa matawi mapya ya UVCCM ambayo awali, yalizuiwa na polisi kabla ya kuruhusiwa baadaye. 
Mamia ya vijana wa CCM walianza kukutana kuanzia asubuhi katika Ofisi za UVCCM mkoani hapa, lakini walipoanza matembezi walizuiwa na polisi mbele ya Jengo la CCM Mkoa. 
Sababu ya kuzuiwa inaelezwa kuwa ni mgogoro ndani ya chama hicho katika Wilaya ya Arusha. Viongozi wa umoja huo wanadaiwa kupinga ziara ya viongozi hao wa kitaifa. Hata hivyo, maandamano hayo yaliendelea baada ya mazungumzo baina ya polisi na viongozi hao wa UVCCM huku wakikubaliana njia za kupita. 
Lakini, mara baada ya kukamilika kwa uzinduzi wa matawi hayo viongozi wa umoja huo walionyesha kukerwa kwao na hatua ya polisi na baadhi ya viongozi wa chama hicho kutaka kuzuia kazi hiyo. 
Habari hii imeandikwa na Mussa Juma,Peter Saramba na Moses Mashalla


CHANZO: Mwananchi



Ubinafsi hauwezi kukusaidia kutengeneza marafiki wengi lakini inaelekea utakusaidia kupata mafanikio kazini.

Utafiti mpya umebaini kwamba watu wasio wabinafsi na wenye roho nzuri ndio wanaopendwa zaidi lakini wakati huohuo wameonekana kama wasiofaa kufukiriwa kwa ajili ya kupandishwa vyeo makazini.

Utafiti huo umeonyesha kuwa ujeuri na kiburi ni ishara za uwezo (nguvu) ilhali upole na wema unachukuliwa kama dalili za udhaifu.

Utafiti uliofanywa na Chuo cha Utawala ya Kellogg,Chuo cha Masomo ya ngazi ya juu ya Biashara cha Stanford na Chuo cha Biashara cha Tapper katika Chuo Kikuu cha Carnegie Mellon ulilenga kuchunguza aina ya maisha ya mtu tunayoihusisha na uongozi.

Katika mlolongo wa majaribio matatu,watafitiwa waliwekwa kwenye makundi,kisha watafiti walichambua tabia zao katika matumizi ya ishara zilizotumika kama fedha; jinsi gani baadhi waliamua kubaki na ishara hizo kwa ajili yao binafsi huku wengine wakiziingiza ishara hizo kwenye hazina ya kundi.

Wale wenye tabia za kibabe walionekana kama wenye tabia 'alpha' (alpha personalities).

Mhariri mwenza wa ripoti ya utafiti huo, Rober Livingston wa Chuo cha Biashara cha Kellog alieleza, "Kuwa mbinafsi kunafanya mtu aonekane anatawala,na kuonekana unatawala kunakufanya uonekana unafaa kuwa kiongozi,hususan pale penye ushindani."

"Akilini,watu wanalinganisha wema kuwa sawa udhaifu."

Dr Livingston anaamini kwamba tabia hii ya kuhusisha ubabe na uongozi inaweza kutoa maelezo kwani tunakuwa na rushwa.

"Watu wenye maadili,wema na wapenda watu wana nafiasi finyu ya kuteuliwa kushika majukumu ya uongozi," alisema msomi huyo.

"Hiyo inaongeza uwezekano wa rushwa na utendaji kazi kinyume cha sheria kwa sababu tunakuwa na watu wasiofaa kwenye nafasi za uongozi."

Lakini Bob Kaplan,Makamu Mwenyekiti wa Zamani wa taasisi ya fedha ya Goldman Sachs,na sasa Profesa wa kanuni za utawala katika Chuo Kikuu cha Harvard haafikiani na hoja ya utafiti huo.

Aliieleza tovuti ya Today.com kwamba maadili mema ndio kigezo kinachoweza kushauri kuhusu kiongozi anayefaa.

"Sisemi kwamba ili kuwa bosi lazima uwe mtu 'poa' lakini nadhani inabidi uwe na maadili,uadilifu na kushirikiana vema na watu, na kuwajenga watu," alisema.

CHANZO: Tafsiri isiyo rasmi kutoka gazeti la Daily Mail


9 Oct 2011


Tuipende,tuichukie lakini ukweli unabaki kuwa CCM ndio chama tawala.Kwa mantiki hiyo kila Mtanzania,including sie tusiokuwa wananchama wa chama chochote kile cha siasa tunalazimika kuwa na interest na hali ya mambo ndani ya chama hicho.Afterall,tofauti zetu za kiitikadi hazimaanishi uadui kama unavyohubiriwa na akina Nape.Sote ni Watanzania,na iwe CCM,Chadema,CUF,nk vyote ni vyombo tu vya kutushirikisha katika siasa za nchi yetu kwa namna moja au nyingine.

Anyway,niende kwenye mada.CCM inakabiliwa na changamoto kubwa katika kumpata mgombea wake anayetarajiwa kumrithi Rais Jakaya Kikwete atakapomaliza muda wake mwaka 2015.Naomba kuorodhesha changamoto hizo kama ifuatavyo

MGOMBEA KUTOKA ZANZIBAR

Japo Katiba ya Jamhuri ya Muungano na ile ya CCM hailazimishi utamaduni usio rasmi wa kupokezana nafasi ya mgombea urais kati ya CCM Bara na Zanzibar,yayumkinika kuamini kuwa baada ya miaka 20 (1995-2015) ya CCM Zanzibar kutotoa mgombea kwenye nafasi ya Urais wa Muungano upande huo utakuwa unatarajia kuwa sasa ni zamu yao.Baada ya Rais Mzanzibari Ali Hassan Mwinyi,alikuja M-Bara Benjamin Mkapa aliyetawala kwa miaka 10 kabla ya kurithiwa na M-Bara mwingine Jakaya Kikwete ambaye kufikia mwaka 2015 atakuwa ametawala kwa miaka 10.

Kwa vile katika utamaduni mwingine usio rasmi ndani ya CCM mgombea atakayepitishwa mwaka 2015 (na ikitokea akashinda) anaweza kuwa madarakani kwa miaka 10 (kwa maana kuwa anatarajiwa kupitishwa tena mwaka 2020-kama ilivyokuwa kwa Mwinyi,Mkapa na sasa Kikwete), Wazanzibari wakikubali mgombea ajaye wa CCM atoke Bara itamaanisha wakose nafasi kwa miaka 30 mfululizo.

Tofauti na ccm Bara ambapo uongozi wake una sauti kuliko wanachama,kwa Zanzibar wanachama na viongozi wa kawaida wana influence kubwa ndani ya chama hicho.Wakati uongozi wa CCM Zanzibar unaweza kuridhia mgombea ajaye ataoke Bara,ni vigumu kuhisi wanachama na viongozi wa kawaida wakakubali miaka mingine 10 pasipo Mzanzibari mwenzao kushika urais kupitia CCM.

Iwapo CCM Bara watashinikiza lazima mgombea atoke Bara basi Wazanzinari wanaweza kutumia turufu ya "tunatoka nje ya Muungano" na hili linaweza kuzua sokomoko kubwa.

MGOMBEA/RAIS MUISLAM KISHA MKRISTO (na vice versa)

Utamaduni mwingine ndani ya CCM ni kuzungusha nafasi ya urais (au mgombea wa urais) kati ya Waislam na Wakristo.Baada ya miaka kadhaa ya utawala wa Mwalimu Nyerere ikaja zamu ya Muislam Mwinyi,ambaye naye alirithiwa na Mkristo Mkapa,kabla ya ujio wa Muislam Kikwete.Katika mambo ambayo CCM inapaswa sifa nyingi ni pamoja na umakini wake katika kudili na ishu nyeti ya dini (japo wanasiasa mufilisi wameanza kutumia udini kwa minajili ya kusaka mafaniko yao binafsi kisiasa).Chama hicho kimejitahidi sana kuzingatia ukweli wa mgawanyo wa kiimani miongoni mwa Watanzania ambapo Waislam na Wakristo wanatengeneza takriban robo mbili za wakazi wote wa nchi yetu (robo nyingine ni wanaofuata imani nyingine pamoja na wapagani)..

Sasa,kwa kuzingatia ukweli kuwa Kikwete ni Muislam,inatarajiwa mgombea urais wa CCM mwaka 2015 awe Mkristo ili kudumisha utamaduni huo usio rasmi.Iwapo mgombea huyo atatoka Bara,haitokuwa vigumu kumpata.Tatizo ni iwapo mgombea atatakiwa kutoka Zanzibar.Kama tujuavyo,takriban asilimia 99 ya Wazanzibari ni Waislam,na hali ni kama hiyo kwenye uongozi wa CCM visiwani humo.Uwezekano wa kumpata mgombea urais kutoka Zanzibar ambaye ni Mkristo ni mgumu pengine kuliko uwezekano wa Gaddafi kuwa mgombea urais wa Marekani kuchuana na Rais Barack Obama hapo mwakani.

Kwa mantiki hiyo,kama changamoto ya kwanza itapatiwa ufumbuzi,yaani CCM kufanikiwa kupata mgombea wake kutoka Zanzibar,tatizo litabaki kwenye changamoto ya pili,yaani kupata mgombea Mkristo kutoka visiwani humo.

CHAGUO LA KIKWETE

Ni wazi Rais Kikwete angependa kupata mrithi atakayeweza kumpa amani baada ya kustaafu.Baada ya kuonjesha ladha ya 'ujeuri' pale baadhi ya vigogo wa chama hicho wanapodaiwa kutaka kumng'oa kwenye kiti cha uenyekiti wa chama hicho kwa kigezo cha kutenganisha kofia ya urais na uenyekiti wa CCM,yayumkinika kuamini kuwa asipokuwa makini kumpata mrithi atakayehakikisha anakula pensheni yake bila usumbufu wala hofu ya kukumbana na yaliyomkuta Chiluba...

Lakini Kikwete kulazimisha chaguo lake kutategemea namna atakavyoweza kumpromoti kuanzia sasa.Wachambuzi wengi wa siasa zetu wanafahamu kuwa Kikwete hana sauti kubwa ndani ya chama hicho.Kimsingi,mtu kama Edward Lowassa ana nguvu takriban mara mbili ya alizonazo Kikwete ndani ya chama hicho.Nguvu pekee ya mwenyekiti huyo ni kutoka kwa watu wa Idara ya Usalama wa Taifa ambao licha ya kumpatia dossiers zenye "machafu" ya viongozi wenzie wa CCM,pia wanaweza kulazimisha matakwa ya Kikwete yakatimia kwa mbinu chafu za kiintelijensia.Hilo linafanyika sehemu nyingi tu duniani ambapo siasa na intelijensia zimefunga ndoa isiyo rasmi.

Lakini hili la mashushushu kuingilia siasa za ndani ya CCM linategemea zaidi siasa za ndani za Idara ya Usalama wa Taifa.Wajuzi wa mambo wanafahamu mgogoro wa chini chini ndani ya Idara hiyo kuelekea mchakato wa CCM kumpata mgombea wake mwaka 2005.Tofauti za kimaslahi miongoni mwa viongozi waandamizi wa Idara hiyo zilitishia kwa kiasi kikubwa jina la Kikwete kupitishwa,na hata alipofanikiwa kupitishwa na hatimaye kushinda urais baadhi ya viongozi waandamizi wa Idara hiyo walijikuta majeruhi.

LOWASSA NA 'PIGA UA' YAKE

Mpende au mchukie, lakini Edward Lowassa ameendelea kuwa mwanasiasa mwenye nguvu na ushawishi mkubwa ndani na nje ya CCM.Licha ya uwezo wake mkubwa wa kifedha,Lowassa amewasaidia viongozi wengi wa CCM kuwepo madarakani,iwe kwa misaada ya kifedha au kimkakati.

Japo hajaweka msimamo wake hadharani,wachunguzi wengi wa siasa wanaamini kuwa ndoto za mwanasiasa huyo kumrithi Kikwete bado zipo hai.Inaaminika kuwa chanzo cha ndoto hizo ni mkataba usio rasmi kuwa Kikwete angemwachia Lowassa jahazi la kuongoza Tanzania baada ya kumaliza miaka yake 10 ya Urais.Mahesabu yalikwenda vizuri hadi pale ilipoibuka skandali ya Richmond iliyopelekea Lowassa kuachia ngazi.Laiti hilo lisingetokea basi muda huu wala nisingeandika makala hii kwa vile ingekuwa wazi kuwa Lowassa ndiye Rais ajaye baada ya Kikwete.

Kinachomsaidia Lowassa ni jinsi anavyotumia kila nafasi ipasavyo kuhakikisha jina lake linaendelea kuwa masikioni mwa Watanzania.Mwanasiasa huyo yupo radhi hata kuwaunga mono wanasiasa wa vyama vya upinzani alimradi kufanya hivyo kunamweka karibu zaidi na wapiga kura.

Kadhalika,pamoja na kuhusishwa na ufisadi,Lowassa anakubalika kama mtu anayemudu kufanya anachoamini,jambo linalomtofautisha na Rais Kikwete ambaye anaelemewa zaidi na kutaka kuwafurahisha watu wake wa karibu.Lowassa yupo tayari aonekane mbaya ndani ya CCM lakini aishie kuonekana mkombozi kwa Watanzania.

Na katika kumtendea haki,Lowassa ana 'u-Sokoine' wa namna flani.Hasiti kutoa maamuzi na anaweza kusimamia maamuzi yake.Laiti mwanasiasa huyu asingekuwa na mawaa ya ufisadi basi Tanzania ingeweza kupata carbon copy ya Sokoine.

Kuna wanaomwona Lowassa kama mwanasiasa anayeweza kubadilika kwa sababu kuu mbili.Kwanza,utajiri mkubwa alionao unaweza kabisa kumshawishi asitumie madaraka yake kuendeleza utaratibu wa kuifanya Tanzania kuwa shamba la bibi.Japo utajiri sio kigezo cha fisadi kutotamani fedha zaidi lakini madaraka kama ya Urais yanaweza kumfanya mtu apate huruma kwa anaowaongoza.Kikwete ana huruma lakini tatizo ni kwamba huruma yake kwa mafisadi ni kubwa ziadi ya ile aliyonayo kwa walalahoi.Hilo halina mjdala na mwenyewe anajua hilo.

Kingine kinachoweza kumpa faida Lowassa ni network yake ambayo inaweza kabisa kupenya Zanzibar kuwashawishi wamuunge mkono.Ukichanganya na advantage nyingine kwamba yeye ni Mkristo (ambayo inamfanya awe eligible kwa mujibu wa changamoto ya pili hapo juu),

Lakini pengine faida nyingine aliyonayo mwanasiasa huyu ni ukaribu wake na Idara ya Usalama wa Taifa,ambayo penda usipende itacheza nafasi muhimu kwa mgombea mwana-CCM yeyote anayetaka kumrithi Kikwete.Japo sina hakika kwa sasa ukaribu huo upo katika hali gani lakini unaweza kuwa na faida kubwa kwake.

Kubwa zaidi ya yote ni ukweli kwamba Lowaasa anamfahamu Kikwete in and out.Kwa mantiki hiyo,anaweza kumwandama Kikwete hata atakapomaliza muda wake wa Urais.Na kwa vile by then Kikwete hatokuwa na nguvu za kutosha ukilinganisha na hali ilivyo sasa ambapo yeye ni mkuu wa nchi, yayumkinika kuamini kuwa angependa kuwa na maadui wachache wenye nguvu na uwezo wa kumwangamiza.Kikwete anaweza kujikuta anakabiliwa na mzimu uleule ambao yeye na wanamtandao wenzake walimsababishia Rais Mkapa.

Inafahamika kuwa Kikwete na timu yake waliweka wazi kwa Mkapa kuwa laiti asingepitishwa basi aidha angegombea (na pengine kushinda) kupitia tiketi ya chama cha upinzani.Sasa ukizingatia Kikwete hakuwa karibu kihivyo na vyama vya upinzani kwa wakati huo,ukaribu wa Lowasaa kwa wapinzani unaweza kulifanya tishio la aina hiyo kuchukuliwa kwa uzito mkubwa.Ikumbukwe kuwa nafuu pekee kwa Kikwete atakapostaafu ni kwa CCM kubaki madarakani kwani kuna kila dalili kuwa kama chama cha upinzani kikishinda basi anaweza kabisa kupandishwa kizimbani kujibu tuhuma lukuki za ufisadi.

Je CCM wanawezaje kukabiliana na changamoto hizi?Moja ya njia mwafaka ni kujaribu kuiga utaratibu wa siasa za uchaguzi nchini Marekani ambapo wananchama wenye nia ya kuwania kupitishwa kugombea urais wanatangaza dhamira zao mapema.Pamoja na faida ya kumfanya mwanachama mwenye dhamira hiyo kufahamika vema kwa wapiga kura,utaratibu huo unaambatana na hatari zake.Kwa mwananchama kujitambulisha hadharani mapema anaweza kuwapatia maadui zake wa kisiasa ammunition ya kutosha kumteketeza mapema,na ikifika wakati wa kupiga kura za kumpitisha mgombea anaweza kuwa amekwisha kabisa.

Anyway,kwa leo naomba kuishia hapa.Nitaendelea na mada hii wakati mwingine



Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete,

Kwanza naomba kukupa salamu za heri kwa siku yako ya kuzaliwa uliyoadhimisha jana.Mungu akuzidishie uhai,afya njema na nguvu ya kuendelea kututumikia Watanzania wenzako.

Baada ya salamu hizo,naomba niende kwenye mjadala usio rasmi ulioanzia juzi huko Twitter.Katika majibu yako kwa swali langu tunawezaje kuuelezea umasikini unaowakabili wakazi wa wilaya Kilombero (ambapo ulizuru majuzi) licha ya utajiri mkubwa wa raslimali-hususan ardhi yenye rutuba ambayo imelifanya eneo hilo kuwa maarufu kwa kilimo cha mpunga na nafaka ya mchele-ulieleza, naomba nikunukuu, "In Kilombero we've extension officers,SACCOS,market facilitation and mechanization initiatives.Some are using these opportunities" (kwa Kiswahili,Kilombero tuna maafisa ugani,vyama vya ushirika wa kuweka na kukopa,uwezeshaji masoko,jitihada za matumizi ya mashine.Baadhi ya watu wanatumia fursa hizi."

Labda nikuulize,Mheshimiwa Rais,je uliona umasikini usiofichika unaowagubika wakazi wengi wa wilaya ya Kilombero?Ninatumai uliouna japo watendaji wengi wana tabia ya kuificha taswira zisizopendeza ili waonekane wanatekeleza wajibu wao ipasavyo.Hapa ninamaanisha si ajabu iwapo watendaji wa serikali wilayani Kilombero wangeamua kukupa picha ya "kila kitu ni shwari" ili uridhishwe na utendaji kazi wao.

Tuje kwenye jibu lako with an assumption kwamba uliona umasikini unaowakabili "matajiri" wa Kilombero (in the sense of kuwa wakazi kwenye sehemu yenye utajiri lukuki).Mheshimiwa Rais,tatizo la Tanzainia yetu halipo kwenye uwepo wa maafisa wenye majukumu fulani bali ni iwapo maafisa hao wanatekeleza majukumu yao ipasavyo.Mara kadhaa,Mheshimiwa Rais,umelazimika kutumia madaraka yako kuwasaidia wananchi licha ya uwepo wa waziri husika,naibu wake,katibu mkuu,naibu katibu mkuu,mkurugenzi wa idara husika,mkuu wa mkoa,mkuu wa wilaya na pengine diwani kama si mwenyekiti wa serikali ya mtaa.

Mheshimiwa Rais,kama ilivyo kwenye sheria zetu nzuri na ambazo kwa hakika zingesimamiwa ipasavyo tungemedu kukabiliana na matatizo kama ufisadi kwa ufanisi (kwa mfano kwa kiutumia ipasavyo Sheria ya Uhujumu Uchumi) ni wazi pia kuwa laiti wengi wa watendaji unaoamini kuwa wanaweza kuwasaidia wananchi kufikia malengo yao ya kimaendeleo wangetimiza wajibu wao ipasavyo basi tusingeendelea kuwa moja ya nchi masikini kabisa duniani licha ya utajiri lukuki wa raslimali tulionao.

Ni wazi,Mheshimiwa Rais,kuwa laiti maofisa ugani unaowazungumzia huko Kilombero wangekuwa wanatimiza wajibu wao ipasavyo sio tu baadhi ya wakazi au wazawa wa neo hilo kama mie tusingekuwa na cha kulalamikia bali pia eneo hilo lingeweza kabisa kuwa mithili ya Saudi Arabia ya Tanzania (kwa kulinganisha uzalishaji mafuta wa Saudi na mchele wa wilaya ya Kilombero).Wnachofanya maofisa ugani unaosifia uwepo wao ni kukupatia ripoti nzuri zenye kutia matumaini lakini kimsingi wao ni miongoni mwa vikwazo vinavyokwamisha maendeleo ya eneo hilo.

Mheshimiwa Rais,ninaomba kuafikiana nawe kuwa uwepo wa SACCOs umelta ukombozi mkubwa kwa wananchi hususan wa vijijini.Masikini hawa ambao hawana amana za kuwawezesha kukupa benki wamepata ukombozi mkubwa kupitia SACCOs.Hata hivyo,nyingi ya taasisi hizo zimekuwa zikikabiliwa na na tatizo sugu la mtaji mdogo ambao unapelekea kuhudumia wananchi wachache kuliko ilivyopaswa.

Mhehimiwa Rais,utakumbuka jinsi wajanja (polite word for mafisadi) walivyo-misuse "Mamilioni ya Kikwete" na sehemu ya fedha hizo kuishia mifukoni mwao badala ya kuwafikia walengwa.Moja ya taasisi ambazo zingenufaika sana na mpango huo ni SACCOs mbalimbali nchini.

Lakini pia,Mheshimiwa Rais,katika kuonyesha namna serikali yako isivyotoa kipaumbele cha kutosha kwa wakulima waodogo wadogo,fedha za stimulus package zilielekezwa zaidi kwa viwanda na kampuni (ikiwa pamoja na zilizo hewa) badala ya kuwatupia macho wakulima hawa.

Kwa hakika inapendeza kumwona mwekezaji wa kigeni akiwekeza katika kilimo cha mpunga.Lakini ni wazi,Mheshimiwa Rais,ingependeza zaidi iwapo uwekezaji huo ungefanywa na wakulima hao masikini.Sio tu uwekezaji huo ungeinua hali za maisha za walalahoi hawa lakini pia ungeweza kutoa ajira za kutosha na kusaidia harakati za maendeleo ya eneo hilo na nchi kwa ujumla.

Mheshimiwa Rais,kuhusu kuwezesha upatikanaji wa soko,ninaamini kuwa laiti ungepeata wasaa wa kusikia kilio cha wakazi wa eneo hilo (na pengine maeneo mengine ya uzalishaji) ungebaini kuwa licha ya utajiri wa mpunga/mchele,wakazi wa eneo hilo wanakabiliwa na tatizo sugu la masoko.Kimbilio kubwa limekuwa kwa walanguzi ambao hujazana huko kila unapojiri msimu wa mavuno.

Cha kusikitisha zaidi ni kwamba wakati tunaadhimisha mika 50 ya uhuru wetu,baadhi ya wakazi wa Kilombero hullazimika kurejea njia za kale za uuzaji wa mazao yao ambapo barter trade hutumika kuwawezesha baadhi ya wakulima kumudu kupata bidhaa kama mitumba ya nguo,sukari na hata chumvi.Hivi Waziri husika ana mpango gani mahsusi ya kusaidia wakulima wa aina hii?Tumesikia kuhusu Kilimo Kwanza na Mapinduzi ya Kijani lakini kama ilivyokuwa katika zama za Ujamaa na Kujitegemea kauli mbiu hizo zimesihia kuwa matamko tu yenye malengo mazuri lakini utekelezaji sio wa kuridhisha.

Kuhusu sapoti katika matumizi ya teknolojia kwa maana ya mashine za kilimo,laiti Mheshimiwa Rais ungeongea na wananchi wa eneo hilo wangekufahamisha kuwa wanakabiliwa na tatizo sugu la uhaba wa matrekta.Machache yaliyopo ni mabovu na gharama zake ni kubwa mno kiasi kwamba wakulima wanalazimika kutegemea jembe la kono.Miaka 50 ya uhuru lakini mkulima wa Kitanzania bado anategemea zaidi jembe la mkono badala ya mashine za kisasa.

Mheshimiwa Rais,moja ya sababu zilizowashawishi Watanzania kukupa kura nyingi mwaka 2005 (na baadaye mwaka 2010) ni dhamira uliyoonyesha mwanzoni kuwa unataka kupunguza (kama si kumaliza kabisa) matatiao yanayowakabili Watanzania.Kihistoria,unafahamika kama miongoni mwa viongozi wachache walio karibu sana na wananchi (hata kabla hujaingia Ikulu).Uelewa wako kuhusu matatizo ya Watanzania ulitarajiwa kutoa suluhisho la tatizo la umasikini wa kutupa unaowakabili Watanzania wengi.

Binafsi siamini kuwa wewe binafsi ndio pekee wa kulaumiwa bali baadhi ya watendaji wako.Sasa,Mheshimiwa Rais,mwaka 2006 ulionya watendaji wabovu wasitafsiri vibaya upole wako kwani usingesita kuwawajibisha.Lakini ukweli ni kwamba wengi wa watendaji wako hao wameendela kuwa kikwazo kikubwa kwa maendeleo ya wananchi.

Mheshimiwa Rais,mwezi huu wa Oktoba utakuwa unatimiza mwaka mmoja mzima tangu uingie madarakani kwa awamu nyingine ya Urais.Lakini kama unakumbuka vyema,nyingi ya hadi ulizotoa mwaka 2005 hazijatekelezwa,na ukichanganya na za mwaka 2010 utaona kuwa una kazi ya ziada kumaliza utekelezaji wa ahadi hizo kabla hujang;atuka rasmi mwaka 2015.

Mwalimu Nyerere alitufundisha kuwa ili tuendelee tunahitaji WATU,ARDHI,SIASA SAFI na UONGOZI BORA.Sasa Mheshimiwa Rais,sio tu kwamba watu wapo bali pia   wana nia na kiu ya maendekleo yao binafsi na ya jamii zao.Ardhi ipo ya kutosha ikama ulivyoona huko Kilombero.Nadhani kinachokosekana na SIASA SAFI na UONGOZI BORA.

Mheshimiwa Rais,umebakiwa na miaka minne tu kabla hujamaliza muda wako kwa mujibu wa sheria.Hivi  ungependa umalize muda wako ukiwa na legacy isiyopendeza kuhusu masikini wa kutupa ambao hawana mbele wala nyuma.

Mwaka 2005 uliahidi maisha bora kwa kila Mtanzania lakini baadhi yetu sasa tumekuwa tukitafsiri kama Mauisha Bora kwa kila fisadi.Ninaamini kabisa,Mheshimiwa Rais uliota ahadi hizo ukiamini kuwa zinatekelezeka.Lakini kwa bahati mbaya-au makusudi- hali yetu ni mbaya sana.Maendeleo tunayodaiwa kuyafikia yameendelea kubaki ndoto ya mbali.

Sasa Mheshimiwa kwa vile umebakiwa na miaka minne tu na rundo la ahadi zinazosubiri utekelezaji basi ninaomba utumie muda huu ulisailia kufanya jtihada za makusudi kuhakikisha unakumbukwa kwa jambo moja au jingine la msingi.

Basi Mheshimiwa Rais naomba nisikuchoshe sana na makala hii ndefu.Ninaamini una kila SABABU,na UWEZO lakini kiachokosekana ni NIA ya kuifikisha Tanzania mahala inapostahili kuwepo kimaendeleo.Kama Rwanda wamemudu kupiga hatua licha ya mauaji ya kimbari huko nyuma kuathri umoja wao kitaifa,na kama Botswana na Sychelles zinamudu kuwa majabali ya uchumi barani japo tunaweza kuwa na utajiri mkubwa wa raslimali kuliko nchi hizo,hivi tuna sababu gani ya kuendelea kusuasua kiuchumi na kimaendeleo kiujumla?

UKIAMUA,INAWEZEKANA

7 Oct 2011


Raia Mwema Ughaibuni
Kama hali ni hii, ustaarabu wa kisiasa tuusahau 2015!
Evarist Chahali
Uskochi
5 Oct 2011
Toleo na 206
HATIMAYE uchaguzi mdogo wa jimbo la Igunga umefanyika. Kama zilivyo chaguzi mbalimbali nchini tumeshuhudia kila aina ya vituko.
Kama kuna lolote la kujifunza, basi ,ni ukweli kwamba safari yetu ya kidemokrasia bado ni ndefu. Waingereza wana msemo kuwa katika jambo lililofanyika muda mrefu uzoefu una umuhimu wake (tafsiri isiyo rasmi ya in long run experience counts).
Lakini inapokuja kwenye masuala ya siasa zetu, uzoefu wa muda mrefu wa chama tawala CCM unageuka kuwa mithili ya kikwazo cha demokrasia.
Kwa vyovyote vile; matokeo ya uchaguzi huo mdogo wa jimbo la Igunga, yamezidi kudhihirisha kuwa CCM ipo tayari kufanya lolote lile ili mradi ibaki madarakani.
Haihitaji kuwa mchambuzi mzuri wa siasa kupata picha kwamba kama chama hicho tawala kimeweza kutumia kila mbinu katika kampeni zake kwenye uchaguzi huo wa jimbo tu, basi, ni dhahiri kuwa kama ilivyo kwenye chaguzi kuu zilizotangulia, mwaka 2015 tutashuhudia tena mambo yasiyoendana kabisa na ustaarabu wa kisiasa.
Pengine kabla ya kuendelea zaidi na makala hii niweke wazi msimamo wangu kisiasa. Mara kadhaa nimekuwa nikihusishwa na CHADEMA; huku wengine wakinituhumu kuwa kujiweka kwangu karibu na chama hicho ni kwa matarajio ya kupata madaraka iwapo kitafanikiwa kukamata dola.
Ni kweli kuwa maandiko yangu mengi yameonyesha kuiunga mkono CHADEMA; lakini hiyo haimaanishi kuwa mimi ni mfuasi au mwanachama wake. Msimamo wangu kisiasa ni kutofungamana na chama chochote cha siasa.
Kwa vile dhamira yangu ni kuwa mchambuzi ‘halisi’ wa siasa, kufungamana na chama fulani kunaweza kuathiri utekelezaji wa majukumu yangu.
Itikadi yangu kisiasa ni uzalendo. Japo kwa mujibu wa Katiba yetu yenye mapungufu ni vigumu kwa mwananchi kushiriki katika siasa kwa ukamilifu pasipo kuwa mwanachama wa chama cha siasa, binafsi ninaamini njia bora ya kuutumikia umma ni kutanguliza maslahi ya taifa bila kujali uanachama wa chama cha siasa.
Katika siasa tunafundishwa kuwa nchi ni lazima iendelee kuwepo; ilhali vyama vya siasa vinazaliwa na vinaweza kabisa kufa kwa sababu moja au nyingine. Lakini linapokuja suala la uhai wa nchi, kila mwananchi anapaswa kufanya kila jitihada kuhakikisha kuwa sio tu inaendelea kuwepo bali pia inakuwepo katika hali inayostahili.
Sasa, kwa muda mrefu CHADEMA imejitambulisha kwa umma kama mtetezi wa kweli wa wanyonge na maslahi ya nchi yetu. Chama hicho kumekuwa mstari wa mbele katika vita dhidi ya ufisadi na mafisadi.
Kwa namna fulani, harakati za chama hicho zimeweza hata kuifanya CCM ijiangalie kama kweli ipo madarakani kuwatumikia Watanzania na si mafisadi pekee.
Kwa mantiki hiyo, kuna uwezekano mkubwa wa kila anayeipenda Tanzania yetu kwa dhati kuungana na harakati za CHADEMA katika safari yake ya kuhamasisha na hatimaye kufikia ‘uhuru wa pili.’
Naam, vita ya uhuru ‘wa kwanza’ ilikuwa ya kumwondoa mkoloni, mgeni aliyetunyanyasa kwa vile -pamoja na sababu nyingine - hakuwa na uchungu na nchi hii.
Vita hii ya sasa ni dhidi ya Watanzania wenzetu ambao kwa tamaa na ulafi wao wameweka mbele maslahi yao pasipo kujali wanalipeleka wapi taifa letu.
Kama nilivyoandika katika makala yangu katika toleo la wiki iliyopita mazingira ya chaguzi zetu, na kama ilivyoshuhudiwa huko Igunga, hayatoi fursa kwa vyama vya upinzani kuchuana na CCM kwa haki.
Uhuni uleule wa kila siku ambapo timu moja ya soka yenye wachezaji 11 inalazimika kuchuana na timu pinzani yenye wachezaji 15 (kwa maana ya wachezaji 11 wa kawaida wakisaidiwa na refa, washika vibendera wawili na kamisaa).
Watendaji wa serikali wanaopaswa kusimamia chaguzi pasipo upendeleo wanalazimika (aidha kwa uoga wao au kwa kufuata maelekezo ya serikali) kuipendelea CCM waziwazi.
Na chanzo kikubwa cha tatizo hili ni kufeli vibaya kwa harakati za kuondoa itikadi za kisiasa kwenye utumishi wa umma serikalini.
Katika mazingira ya kawaida, huwezi kumzuia Mkuu wa Wilaya asiipendelee CCM; ilhali anajua bayana kuwa iwapo chama hicho tawala kitashindwa kwenye uchaguzi unaofanyika kwenye jimbo lililopo kwenye wilaya ya DC huyo, basi naye atakuwa matatani.
Ni vigumu kwa Mkuu wa Mkoa ambaye amezawadiwa u-RC kutokana na ushiriki wake ndani ya CCM kumudu kusimamia uchaguzi kwa uhuru na haki na hatimaye kuruhusu CCM ishindwe kihalali.
Hali ni hivyo hivyo kwa Tume ya Uchaguzi na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa ambapo utendaji kazi wa taasisi hizo ni kama kwa njia ya ‘remote control’ kwa matakwa ya chama tawala, kiasi kwamba malalamiko yoyote ya vyama vya upinzani huchukuliwa kama ‘kelele za mpangaji ambazo hazimnyimi usingizi mwenye nyumba’.
Ni kweli kwamba mawaziri wote tulionao ni wana CCM, lakini jukumu la waziri na wizara, kama ilivyo serikali, ni kuwatumikia Watanzania wote pasipo kujali itikadi zao.
Sasa waziri anapokwenda kwenye kampeni za uchaguzi na kuwatisha wapiga kura kwamba wakidiriki kuchagua mbunge wa chama cha upinzani watanyimwa maendeleo, ni uhuni wa hali ya juu wa kisiasa.
Katika kampeni huko Igunga tulisikia ‘hadithi’ kwamba CHADEMA wameingiza magaidi kutoka nje ya nchi kwa minajili ya kufanya vurugu kwenye uchaguzi huo. Hizi si tuhuma ndogo na zinaweza kuwa na madhara makubwa kwa taifa letu.
Wanasema, moja ya athari za ugomvi kati ya wanafamilia ni uwezekano wa watu walio nje ya familia hiyo na ambao wana chuki na familia husika kutumia migongano huo wa kifamilia kuihujumu; huku wakijua fika itakapofika hatua ya ‘kusaka mchawi’ macho yataelekezwa kwa miongoni mwa wanafamilia wanaokorogana.
Kwa kutumia mfano huo wa kinadharia, iwapo kuna magaidi wanaotaka kuidhuru Tanzania wanaweza kutumia propaganda hizo mufilisi za CCM kuja kutudhuru; huku wakielewa fika uwepo wa imani fyongo kuwa ‘magaidi tishio kabisa kwa Tanzania wanalelewa na CHADEMA.’
Tunafanya yote hayo kwa faida ya nani? Sote tunawajua wabunge wetu na utendaji wa bunge lenyewe. Hivi kweli tunakubali kufarakanishwa kwa ajili ya watu ambao wengi wao wakishaingia bungeni wanakuwa bize zaidi na kutafakari namna ya kutumia mamilioni wanayolipiwa kama posho na mishahara?
Hivi kweli wapiga kura wanakuwa radhi kusikia porojo za Rais Mstaafu Benjamin Mkapa ambaye alikuwepo madarakani kwa miaka 10 na kumbukumbu kubwa aliyotuachia ni tuhuma dhidi yake kuwa aliigeuza Ikulu kuwa sehemu ya kufanyia biashara?
Kwa vyovyote vile; matokeo ya uchaguzi huo mdogo wa Igunga yanamaanisha kuwa waathirika wakubwa ni wana Igunga wenyewe. Rushwa mbalimbali zilizoambatana na burudani kutoka ‘mjini’ hazitadumu muda mrefu, na busara au ukosefu wa busara kwa kumchagua mbunge asiyeweza kulitumikia jimbo kwa manufaa, zitaanza kuonekana muda si mrefu.
Kwa CHADEMA, uchaguzi huu mdogo unapaswa kuendelea kuwa darasa zuri kwao kujiimarisha kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.
Kilicho wazi kwa kila aliyefuatilia mwenendo wa uchaguzi huo ni ukweli kwamba chama hicho kilikuwa kinapambana na CCM, CUF na serikali kwa ujumla.
Idadi ya kura ambazo CHADEMA imepata ni ‘mithili ya ushindi’; kwani upinzani dhidi yao ulikuwa mkubwa kuliko umri wa chama chenyewe.
Kwa ndugu zangu wa CUF, ninachoweza kuwatahadharisha ni kwamba pasipo umakini wa kujua kwa nini chama hicho kilianzishwa, kuna hatari ya sio tu kupoteza nafasi yake kama wapinzani nambari mbili nyuma ya CHADEMA, bali pia kinaweza kujichimbia kaburi.
Siasa za Zanzibar zinakiweka chama hicho katika nafasi ngumu ya kupambana kwa dhati dhidi ya CCM, na badala yake kinaelekeza mapambano yake dhidi ya wapinzani wenzao wa CHADEMA.
Lakini CUF wanafahamu fika kuwa CHADEMA si chama tawala, na kuiandama kunaweza kuzua hisia kuwa CUF ipo ipo tu na ‘inatumia uhasama usiokuwepo na CHADEMA kwa minajili ya umaarufu tu na kuinufaisha CCM.
Nimalizie kwa kuwakumbusha tena Watanzania wenzangu kuwa kamwe tusikubali kufarakanishwa kwa ajili ya maslahi ya chama au mtu binafsi. Maendeleo na ustawi wa Tanzania yetu ni jukumu letu kama wananchi na sio kuliacha mikononi mwa wanasiasa wasioishiwa na ahadi ambazo hata wasipozitekeleza bado wana uhakika wa kuingiza mamilioni kwenye akaunti zao.
Inawezekana, timiza wajibu wako


6 Oct 2011



1. Apple I (1976): Home computing

The Apple-1 had only 8k of memory and was sold by the Apple boss from his parents garage in California in 1976. The machine sold for $666 then - an early model sold recently for £133,000 at Christies in London
The Apple-1 had only 8k of memory and was sold by the Apple boss from his parents garage in California in 1976. The machine sold for $666 then - an early model sold recently for £133,000 at Christies in London

2. Apple II (1977): Mass-market PC

Apple co-founder Steve Jobs introduces the new Apple II in Cupertino
Apple co-founder Steve Jobs introduces the new Apple II in Cupertino

3. Apple 1984: The 'graphical' PC 

The 1984 Apple MacIntosh launched with a Superbowl commercial directed by Ridley Scott. The hit 'graphical' computer continued to sell well into the Eighties
The 1984 Apple MacIntosh launched with a Superbowl commercial directed by Ridley Scott. The hit 'graphical' computer continued to sell well into the Eighties


4. Pixar (1986): Digital Effects

After leaving Apple, Jobs founded Pixar - and helped launch the era of digital effects in films. Jobs had left by the time hits such as Toy Story came out, but was behind the early successes of the company
After leaving Apple, Jobs founded Pixar - and helped launch the era of digital effects in films. Jobs had left by the time hits such as Toy Story came out, but was behind the early successes of the company


5. NEXT (1989): Dawn of the web

After being pushed aside in 1985 by Apple's board of directors, Jobs founded NeXT, a computer platform development company - its computers offered the first web browsers
After being pushed aside in 1985 by Apple's board of directors, Jobs founded NeXT, a computer platform development company - its computers offered the first web browsers


During the low point of the NEXT years, Fortune magazine described Jobs as either a 'visionary' or 'a snake oil salesman'
During the low point of the NEXT years, Fortune magazine described Jobs as either a 'visionary' or 'a snake oil salesman'

6. Apple iMac (1998): 'Lifestyle PCs' 

The colourful iMac - the design team 'got inspiration' by going to a sweet factory - heralded Jobs's return to Apple
The colourful iMac - the design team 'got inspiration' by going to a sweet factory - heralded Jobs's return to Apple


7. iPod (2001): Digital music

The first-generation iPod offered a mere 5Gb of memory - smaller than even the cheapest iPhone model today
The first-generation iPod offered a mere 5Gb of memory - smaller than even the cheapest iPhone model today


8. iTunes Store (2003): The download era

The launch of iTunes store was a new era for media - turning Apple into the biggest music company on Earth
The launch of iTunes store was a new era for media - turning Apple into the biggest music company on Earth

9. iPhone (2007): Smartphones

Companies such as Sony Ericsson had touchscreen phones on the market before the 2007 launch of iPhone - but iPhone conquered the market
Companies such as Sony Ericsson had touchscreen phones on the market before the 2007 launch of iPhone - but iPhone conquered the market


10. iPad (2010): The post-PC era

Apple's iPad ushered in a new era of slim touchscreen devices - now being copied by every computer manufacturer on Earth
Apple's iPad ushered in a new era of slim touchscreen devices - now being copied by every computer manufacturer on Earth
 
Apple computers - a timeline
Apple computers - a timeline

Some that didn't work quite so well...


Every genius has his 'off' days - and some of Steve Jobs's most recognisable products weren't QUITE as successful as the others... 


The 'puck' mouse
G4 cube
The puck mouse for Apple's iMac computer looked pretty, but was almost unusable - and the G4 Cube was prone to overheating and unpopular with fans, despite walking off with design awards


Few people know this, but iPhone was not the first 'iTunes phone' - this monstrosity was. A partnership with Motorola, the ROKR worked with iTunes, but was far too fiddly
Few people know this, but iPhone was not the first 'iTunes phone' - this monstrosity was. A partnership with Motorola, the ROKR worked with iTunes, but was far too fiddly


SOURCE: Daily Mail

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.