23 May 2012




WEDNESDAY, MAY 23, 2012


Hukumu kesho itakuwa mahakama kuu kivukoni na sio mahakama ya kazi akiba

Nimepokea taarifa kwamba hukumu ya kesi ya uchaguzi dhidi ya ushindi wetu Jimbo la Ubungo kesho tarehe 24 Mei 2012 itatolewa katika Jengo la Mahakama Kuu (Kivukoni- Court No. 1) badala ya jengo ilipo mahakama ya kazi (akiba) ambapo kesi iliendeshwa. Kama tulivyotafuta kura pamoja, tukapanga mstari kupiga kura pamoja na tukakesha kuzilinda pamoja tujumuike pamoja kujua hatma ya kura zetu. Hukumu ya kesi inatarajiwa kuanza kusomwa saa nne asubuhi hata hivyo ni muhimu kuwahi mapema zaidi asubuhi kwa ajili ya itifaki za kuingia mahakamani. Maslahi ya Umma kwanza

22 May 2012

Kwanza ninawashukuru wote walionipatia mchango wao wa mawazo kuhusu idea hii ya Makala za Sauti.Ninasema ASANTENI SANA.Pili,wengi wa mlionitumia maoni yenu mmezungumzia uhafifu wa sauti.Nimelifanyia kazi hilo na ndio iliyopelekea kutengeneza makal nyingine leo ili kupata mawazo kama kiwango na ubora wa sauti vinaridhisha.

Kwahiyo,makala ya leo imelenga zaidi kutoa shukrani kwa mapokezi niliyopewa kuhusiana na makala za sauti,na kidogo nimejaribu kuongelea jinsi kila mmoja wetu anavyoweza ku-play role yake katika kuifanya Tanzania yetu kuwa bora zaidi.

Basi naomba nikuache unisikilize hapa chini

Ninafanya majaribio ya kuwaletea makala zilizorekodiwa (za sauti) ambapo kama ilivyo hapa bloguni na katika makala zangu gazetini,nitakuwa nikijadili masuala mbalimbali.Ninaanza na sekta ya huduma ambapo mlengwa mkuu ni TANESCO.Nakuomba sana msomaji na msikilizaji unipatie mawazo na ushauri kuhusu wazo hili (hata kuniambia kuwa ni wazo baya ni ushauri pia).

Toleo la kwanza (nataraji kufanya audio hizi angalau mara moja kwa wiki) ni hili hapa Natambua kuwa kiwango cha audio sio cha hali ya juu lakini toleo hili la kwanza ni la majaribio,na iwapo wasomaji mtaafiki wazo hili basi nitajitahidi kupata nyenzo bora ya kurekodia ujumbe husika.

19 May 2012



Timu ya soka ya watoto ya Biafra Kids inashiriki katikamichuano ya soka ya watoto wenye umri wa chini ya miaka 17 kanda ya Kinondoni.




WADOGO ZETU HAWA WANAOMBA MSAADA WA HALI NA MALI KUWAWEZESHA WAFANIKIWE KATIKA NDOTO ZAO KISOKA.UNAWEZA KUANZA KWA KUWATEMBELEA KWENYE UKURASA WAO WA Google+ UNAOPATIKANA KATIKA ANUANI IFUATAYO 



15 May 2012


BONYEZA PICHA KUINGIA KWENYE BLOGU YA

14 May 2012

Let's party! Manchester City's jubilant players lift the Premier League trophy after the late drama
Baada ya miaka 44,Manchester City ni mabingwa wapya wa Ligi Kuu ya England

Ice cool: Aguero blasts home to seal the 3-2 victory that made City champions after a 44-year wait
GOOOOOAL: Bao la tatu na la ubingwa kutoka kwa Muajentina Sergio Aguero

Incredible: Goal hero Sergio Aguero celebrates winning the title at the final whistle
Kama ndoto vile,wakati kila mshabiki akidhani Man City wamepoteza nafasi ya kutwaa ubingwa,Aguero akapachika bao la tatu

Striking at the death: Aguero wheels away after his magical late goal sealed the title for City
Aguero,ambaye ni mkwe wa gwiji la soka duniani Diego Maradona,akiwa amevua jezi kushangilia bao lililopatikana muda wa nyongeza na lililoipa ubingwa Man City baada ya kusubiri miaka 44


Amazing: Aguero is mobbed as the City fans struggle to believe what they are seeing
Mario Balotelli na Edin Dzeko wakimkimbilia Aguero kumpongeza kwa kufunga bao la tatu

Can you believe it? City players go wild after Sergio Aguero's last-gasp heroics against QPR
Wachezaji wa Man City wakimzonga Aguero baada ya kufunga bao la tatu lililowapa ubingwa

Roberto Mancini celebrates with the trophy
Kocha Mtaliano Roberto Mancini akiwa na kombe la ubingwa wa Ligi Kuu ya England

Vincent Kompany the captain of Manchester City poses with the trophy
Nahodha Vincent Kompany akiwa na kombe

Beautiful moment: Mancini and Carlos Tevez hold the trophy after putting their troubles behind them
Uhasama kando: Mancini na Carlos Tevez wakiteta huku wameshikilia kombe

Star showing: Liam Gallagher (top middle) celebrates with the City fans at the end of the match
Shabiki mkubwa wa Man City,mwanamuziki mkongwe Liam Ghallagher (ex-Osias) akisherehekea

Never forget: City fans party on the pitch after their epic comeback against QPR
Furaha isiyoelezeka

Our moment: City supporters pour on to the pitch at the final whistle at the Etihad Stadium
Shangwe kubwa

Now we rule the city: Manchester City fans celebrate with a banner aimed at their rivals
Furaha tupu

Top of the tree: City's players throw their arms in the air after securing their long-awaited title
Furaha kubwa ya kutwaa ubingwa baada ya kusubiri kwa miaka 44

Smiles better: Mario Balotelli (centre) shares a joke with manager Roberto Mancini as they wear Italian flags
Kocha wa Man City Roberto Mancini akifurahi na wachezaji wake

Show us your medal: Joe Hart holds team-mate David Silva as they enjoy their moment
Kipa wa Man City Joe Hart akiwa amembeba mchezaji mwenzie David Silva

Shocked: Sir Alex Ferguson looks visibly stunned by the late news coming in from City
Kocha wa Man United Sir Alex Ferguson akiwa haamini macho na masikio yake kuwa timu yake imepoteza ubingwa kwa wapinzani wao wa Manchester City

Nightmare: United's players are helpless as they absorb the news coming in from the Etihad Stadium
Wachezaji waManchester United wakipokea habari za ushindi wa Manchester City kwa bumbuwazi
Chanzo: Daily Mail


13 May 2012


MSANII mahiri katika medani ya muziki wa kizazi kipya nchini Abbas Hamisi ‘20 Pacent’ ameamua kujikita kwenye ujasiriamali ambapo sasa amejikita kwenye kilimo huko mkoani Morogoro.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi juzi, 20 Percent ambaye alitamba kwa kuzoa tuzo tano kwa mpigo za Wimbo Bora wa Afro-pop, Mtunzi bora wa nyimbo, Mwimbaji bora wa kiume, Wimbo Bora wa Mwaka na Msanii Bora wa Muziki wa Kiume, katika tuzo za Kili Music Awards kwa mwaka 2010 alisema ameamua kuanza kujipanga kwa maisha ya baadaye.

Nyota huyo aliyetamba na nyimbo kama vile ‘Money Money’, ‘Yanini Malumbano’ na nyinginezo kibao alisema kuwa amehamasika kujikita katika kilimo kama ilivyo kwa mkongwe wa muziki huo nchini Selemani Msindi ‘Afande Sele’.

“Kaka hivi sasa mimi nimeamua kujikita pia kwenye kilimo kwa sababu huwezi kutegemea kazi za muziki tu, kuna kila sababu za kuwa mjasiriamali,” alisema 20 Percent.

CHANZO: Tanzania Daima





Unga unavyouzwa nje nje Kinondoni
Saturday, 12 May 2012 10:08

Mwandishi Wetu
KATIKA manispaa ya Kinondoni jijini Dar es Salaam yapo maeneo kadhaa ambayo mbali na kukaliwa na watu, yamebeba siri kubwa ambazo ni uihalifu wenye athari kubwa kwa maisha ya watu hasa vijana.

Kinondoni ni eneo maarufu ambalo si tu kwamba ni kubwa kwa wingi wa vitongoji vyake au wingi wa watu pekee, lakini hata kwa nyumba za starehe, maduka ya urembo na mavazi.

Kila unapotembea hatua kadhaa, utakutana na ama duka la nguo au baa.  Lakini si hivyo tu, bali katika hatua hizo inawezekana ni tano, kumi, ishirini au zaidi ya hizo, aghalabu utakutana na mtu ambaye ana dalili za ulevi.

Wengi  wa watu wanaoonekana kuwa wamelewa si kwa kunywa pombe, la hasha, bali ni ulivi wa dawa za kulevya. Huu ndio uhalifu ambao tunauzungumzia, kwani unaharibu sana maisha ya vijana kiasi cha kutisha.

Vyombo vya dola vipo na vinaona, viongozi wapo na wanaona, lakini hakuna kinachofanyika ni kama uhalifu huu umehalalishwa. Kutoka na hali hii gazeti hili lilisukumwa kufanya utafiti mdogo tu katika eneo la Kinondoni , kujua wapi kilipo chanzo cha umaarufu wa dawa hizi haramu.

Haikuwa kazi rahisi kwani kwa siku tatu mfululizo ilikuwa ni kazi ya kusoma mazingira ya baadhi ya maeneo yanayotajwa kutumika kuendesha biashara hiyo. Ilibidi zitumike mbinu mbalimbali kwani tuliambiwa kwamba ni hatari sana kufuatilia uhalifu huu.

Ni maeneo yapi?
Eneo la kwanza kugundulika lilikuwa ni lile lililoko maeneo ya karibu na hospitali ya Mwananyamala, nyumbani kwa maarufu, ambaye hata hivyo kwa sasa ni marehemu.

Watu wanavyoingia na kutoka ndani ya nyumba hiyo ni mithili ya nyuki wanavyoingia na kutoka kwenye mzinga wao. Hali hii inatupa ishara kwamba lazima kuna kinachofanyika ndani. 

Nje ya nyumba hiyo, kuna miti kadhaa aina ya mwarobaini, magurudumu ya magari ambayo hutumiwa na wavutaji wa dawa za kulevya kujipumzisha nyakati zote na duka ndogo. 

Ubavuni mwake zipo ofisi za Chama cha Mapinduzi (CCM) na mbele yake kuna soko dogo la wauzaji wa viazi mviringo na mikokoteni ya maji. Mpango wa kuingia ndani ya nyumba hiyo ulikamilika baada ya wiki moja, lakini tulipofanikiwa kuingia, tulibaini kuwa ina vyumba sita, vitatu kulia na vitatu kushoto.

Hata hivyo kuna baadhi ya vyumba vya uani ambavyo vinaonekana kuwa vimepangishwa. Ni vigumu kutambua nani anaishi chumba kipi kutokana na muingiliano, pia wingi wa watu.

Mara unapoingia unakaribishwa, maana wenyeji wanajua kwamba kila anayefika ni mteja wa bidhaa hiyo haramu. Hivyo baada ya kuketi, muuzaji anaitwa,  anatoka ndani ya chumba cha pili kulia, kisha anauliza, “Unahitaji wa shilingi ngapi?”

Mwananchi linatoa noti ya Sh10,000 na yeye anahoji tena, “wa hela yote?.”
Muuzaji anatokomea na kurudi na karatasi lililosokotwa na kulikabidhi kwa mnunuzi.

Tunatoka nje ili kuondoka katika weneo hilo maana tumejawa na hofu kwamba huenda tukagundulika kwamba sisi siyo wateja, mara mmoja wa watu ambaye anaonekana kuwa mtumiaji aliyekubuhu wa dawa hizo anatutahadharisha kwamba  tuwe makini kwani wakati mwingine tunaweza kuuziwa dawa ambazo si ‘kokaine au heroin.’

Tunapohoji ni dawa zipi ambazo zinaweza kuwa za kuchakachua, anatueleza kuwa, wakati mwingine wauzaji husaga mchanganyiko wa tembe za valium, fenegan, hamoxylin au piliton na kuziuza kama dawa za kulevya!.

“Wanachanganya na kusaga hizo dawa na wakikupa kama huujui unga halisi … utaingia mkenge, lakini unapata ‘stimu’ (unalewa) kama kawaida,” anasema.

Kazi nyingine
Katika nyumba hii si uuzaji wa dawa za kulevya pekee unaofanyika, bali pia zinafanyika shughuli za upakiaji na ufungaji wake tayari kwa kuuza.

Chanzo chetu cha habari  kinaeleza kuwa, kila mara mzigo unapowasili,  wapo vibarua ambao hutumiwa kufunga na kwamba wafungaji hawa mara nyingi ni watumiaji. 

Anabainisha kuwa mfungaji hulipwa Sh200,000 kwa kufunga kete 50 na Sh400,000 kwa wanaoweza kufunga kete 100 za dawa hizo.

“Kufunga kwake ni kazi, ndiyo maana wanalipa bei ndefu (kubwa), kwa sababu, ule unga hauji kama unga, bali huja kama donge, kwa hiyo unatakiwa ulisage ili uuingize katika pakiti zake,” kilisema chanzo hicho.

Alisema, kuweka unga katika pakiti 50, huweza kumchukua zaidi ya saa sita.  Chanzo hiki, bila kufahamu kinazungumza na nani, kilitoboa kuwa:
“Juzi nilitumwa nipeleke mzigo wa zaidi ya milioni sita kwa mzee anayeishi Mbezi, nilienda kwa pikipiki, nikalipwa laki moja na nusu,” alisema.

 Akifafanua ni kwa namna gani yeye anaepuka kutumia dawa hizo, hasa wakati wa ufungashaji, alisema, huvaa gloves na kuufunika uso wake kwa kitambaa ili unga usiingie puani mwake.

Kikosi kazi Manyanya
Mwananchi lilibaini kuwa, kikosi kazi chenye mtandao mkubwa hufanya kazi katika kituo cha basi cha Manyanya kinachotumiwa na mabasi yanayoelekea Posta mpya.

Katika baadhi ya vibaraza vya maduka ya eneo hili, ndimo wanamoketi wauzaji. Ni vigumu kuwagundua wauzaji, lakini wanunuzi au watumiaji wanaonekana kwa macho kutokana na kulewa. 

Kituo cha daladala cha Manyanya, kina idadi kubwa ya walioathirika na dawa hizi pengine kuliko kituo chochote hapa Dar es Salaam.

Utafiti wa Mwananchi ulibaini kuwa, baadhi ya maduka yaliyo pembezoni mwa kituo hiki ndimo zinapohifadhiwa dawa hizo. Ilibainika kuwa, dawa hizo huhifadhiwa katika maduka hayo, ili kurahisisha ununuzi kwa watumiaji.

Chanzo kingine kilibainisha kuwa: “Hapa wanafika watu wengi. Usifikiri wanakuja hawa wapiga debe tu. Hata wazee wenye heshima zao na magari yao, akina mama wenye familia, na watu wenye hadhi katika jamii,”  anasema.

Wakati akieleza hayo, anatokea mwanamke wa makamo, anashuka katika gari. Chanzo chetu kinatupasha kuwa, huyo naye ni mtumiaji na aliwahi kuwa mke wa raia wa Uingereza.

Mwananchi liliendelea kuangaza na kuwaona baadhi ya vijana wakisaga dawa hizo kwa kutumia moto, vibati na kigae. Wengine wakiuvuta katika sigara na baadhi, wakinusa katika karatasi. 

Aina mpya ya uvutaji 
Mtoa habari mwingine aliliambia  Mwananchi juu ya uvutaji mpya wa dawa za kulevya, ambao pengine waweza kuwa ni wa hatari zaidi kiafya.

Alisema, mtumiaji huchukua chupa tupu ya maji, kisha hujaza maji aidha nusu au robo ya chupa ile kisha hutumbukiza unga ndani ya maji yale.

Baada ya hapo, huchukua bomba la kalamu na kutoboa chupa, juu kidogo ya yalipoishia maji.Karatasi la foili au nailoni hufungwa katika mdomo wa chupa,  bomba jingine la kalamu huchomekwa juu ya foili au nailoni.

“Ukimaliza unachoma moto bomba la kalamu, moto ukishika kasi na  moshi ukianza kuingia ndani ya chupa, unavuta kwa kupitia bomba la chini,” alisema. Aliutaja mtindo huo kuwa unaitwa "wa kidosi/kitajiri' na wanaovuta dawa za kulevya kwa mtindo huo, hulewa kiasi cha kutojitambua na hujisaidia haja kubwa na ndogo.

“Siku hizi watu hawajichomi sindano, wanatumia njia hiyo, kunusa au kulamba,” alisema na kuongeza: "Huu mtindo unaleta raha ya ajabu, kiasi kwamba mtumiaji huweza kutumia hadi Sh 100,000 kwa siku moja tu."

Halikadhalika chanzo hicho kilikubali kutuuzia kete za dawa za kulevya kwa kutuahidi kutuletea hadi tulipoahidiana kukutana.
Wamiliki wa nyumba 
Kwa mujibu wa chanzo chetu cha habari, mwenye nyumba hiyo alifariki miaka ya 80, aliacha wake wawili na watoto tisa, ingawa baadha wamekwishafariki. 

 “Mke mmoja wa yule mzee amefariki, lakini mwingine sijui habari zake,” kilisema chanzo hicho. Chanzo hicho kiliongeza kuwa, baada ya mzee huyo kufariki, nyumba hiyo ilibaki mikononi mwa watoto hao.

Miaka ya 90 hadi mwanzoni mwa miaka ya 2000, watoto hawa  walijikita zaidi katika biashara ya pombe haramu ya gongo, baadaye bangi.Chanzo hicho kiliongeza kuwa, baadaye waliamua kuachana na uuzaji wa pombe na wakahamia katika uuzaji wa dawa za kulevya pamoja na bangi.

“Kaka yao mkubwa mwanzoni alikuwa analetewa kama msambazaji  na kisha kuwauzia mateja, lakini baadaye akaanza kusafiri yeye mwenyewe,” kilisema chanzo hicho. Vyanzo hivyo vilidai kuwa, ndugu wote zaidi ya 10, wanafanya biashara hiyo, wakiwa na familia zao, na baadhi wakiwa ni watumiaji wakubwa.

Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Minazini, Juma Katogolo alikiri kuifahamu nyumba na familia hiyo ingawa alikana kufahamu biashara hiyo.

"Ninawafahamu, baadhi yao nimesoma nao, kwa mfano, huyo kijana mkubwa, (anamtaja jina) nimesoma naye darasa moja, lakini kujua biashara wanayofanya, siwezi kuthibitisha hilo," alisema Katogolo.

"Unajua hizi biashara hufanyika kwa usiri wa hali ya juu, siwezi kusema nina uhakika na hilo." Katogolo alisema amekuwa hapandezwi na tabia na vitendo vya vijana wa Wilaya ya Kinondoni kujitumbukiza katika utumiaji wa dawa hizo.
Kamanda wa polisi mkoa wa Kinondoni, Charles Kenyella alisema hana taarifa na nyumba hiyo, isipokuwa polisi imekuwa ikifuatilia na kukamata dawa za kulevya kila siku.

“Ni ngumu kusema naifahamu nyumba hiyo lakini nisema tu kwamba Kinondoni kuwa sehemu ya jiji la Dar es 
Salaam, tatizo la dawa za kulevya lipo kwa kuasi kikubwa,” alisema Kenyella.

Kamanda huyo aliendelea kueleza:”Polisi imekuwa ikifanya uchunguzi wake wa kiintelijensia na kwa kutumia msako wa kawaida na kufanikiwa kukamata aina mbalimbali za dawa kila siku.”Cocaine, “Tumekuwa tukikamata bangi, mirungi, heroine na cocaine kwa nyakati tofauti na kuzipeleka kesi hizo mahakamani.”

Hata hivyo Kamanda Kenyella alisema jitihada hizo zinarudishwa nyuma na baadhi ya watu ambao hawataki kushirikiana na polisi katika kuwafichua wahalifu hao.

“Wito wangu kwa jamii ni kwamba mjenga nchi ni mwananchi na mharibu nchi ni mwananchi mwenyewe. Naomba watu watusaidie kupata taarifa na sisi polisi tumekula viapo, tutazifanya taarifa hizo kuwa siri kabisa,” alisema

CHANZO: Mwananchi


LIBENEKE MPYA TOWN...LIBENEKE LINALISIMAMIWA NA PRESETER MKALI TOKA SUPER
BRAND RADIO CLOUDS FM ADAM MCHOMVU AKA BABA JONII SASA INAPATIKANA ONLINE
MASAA 24 IKIWA NA HABARI MOTOMOTO,BEAKIN NEWS,JONII ZOTE NA U HEEEEARD ZA
KILA SIKU ZINAPATIKANA KILA SIKU NA KILA UTAPOIFUNGUA UTASIKIA SAUTI YA
JONII IKIWA NA GRAPHICZ ZA HATARI ZIKIWA ZINASIMAMIWA NA KINGKAPITA KAMA
ADMINISTRATOR MKUU,
NYIMBO MPYA,VIDEO MPYA,MATUKIO YOTE MAKALI,PICHA YA WEEK,NA MATANGAZO KIBAO
YA SHOW ZINAZOENDELEA TOWN...
...TUNAOMBA MSAADA WAKO MDAU LUTANGAZA LIBENEKE HILI JIPYA TOWN
TUNATANGULUZA SHUKRANI ZETU..
LIBENEKE INAITWA

Preposterous spectacle: David Haye and Dereck Chisora announce their dust up at Upton Park

Ni nadra kuona press conference kuhusu pambano la ndondi ikiambatana na uzio wa kutenganiha mabondia husika.Lakini hivyo ndivyo ilivyokuwa Upton Park,jijini London wakati wa Press Conference kuhusu mpambano kati yamahasimu wakubwa David Haye na Dereck Chisora.Mabondia hawa wana uhasama mkubwa.

Face to face: David Haye (left) and Dereck Chisora at Upton Park

Line up: Haye and Chisora were kept apart by a metal fence
CHANZO: Daily Mail

12 May 2012

8 May 2012


3 May 2012



RAIA MWEMA UGHAIBUNI
Wana usalama na nguvu yao kwa viongozi
Evarist Chahali
Toleo la 237
2 May 2012
MAKALA katika safu hii ya Novemba 2 mwaka jana ilianzisha uchambuzi wa nafasi za vyama mbalimbali vya siasa huko nyumbani katika Uchaguzi Mkuu ujao.
Habari zilizotawala nchini Marekani hivi karibuni (na ambazo zinaendelea kuvuma japo si kwa kasi kubwa kama ilivyokuwa awali) ni kuhusu skandali iliyokikumba kitengo cha ulinzi wa Rais wa nchi hiyo, kinachofahamika kama Secret Service.
Kwa kawaida ya taratibu za kikazi, wanausalama hutangulia kukagua usalama wa sehemu inayotarajiwa kutembelewa na kiongozi wa juu wa nchi.
Msafara wa wanausalama hao unaweza kuweka makazi katika sehemu hiyo angalau mwezi mmoja kabla ya ziara husika kutegemea na hali ya usalama katika sehemu hiyo.
Sasa, kabla ya Rais Barack Obama kufanya ziara huko Amerika ya Kusini, jamaa wa Secret Service walishatangulia mapema kuhakikisha kwamba usalama wa kiongozi huyo muhimu si kwa Marekani bali dunia kwa ujumla, hauna mushkeli.
Pamoja na mashushushu waliotoka Marekani, walikuwako wenzao ambao kituo chao cha kazi ni eneo hilo la Amerika ya Kusini. Lakini katika mazingira yaliyosababisha mshtuko mkubwa, baadhi ya maafisa usalama hao walikumbwa na skandali ya kujihusisha na makahaba nchini Colombia.
Pengine skandali hiyo isingeibuka laiti mmoja wa mashushushu hao asingempunja ujira kahaba mmoja, ambaye katika harakati za kudai ‘haki yake’ alisababisha kuibuka kwa kashfa kubwa pengine kuliko zote kwa taasisi za usalama nchini Marekani.
Kwa mujibu wa taarifa, kingine kilichochangia sakata hiyo kufichuka ni ushupavu wa mmoja wa viongozi wa Secret Service, mwanamama Mmarekani Mweusi, Paula Reid ambaye baada ya kupata taarifa za ‘madudu’ ya baadhi ya maafisa anaoongoza alimfahamisha Mkuu wa taasisi hiyo Mark Sullivan kuomba ruhusa ya kuwaondoa walioshiriki kwenye tukio hilo la aibu.
Duru za kisiasa, kiusalama na habari zimemwagia sifa lukuki mwanamama huyo ambaye amekuwa mtumishi wa Secret Service kwa miaka 21 sasa. Reid ni mmoja ya wanawake wachache kabisa Weusi kuwa viongozi kwenye taasisi hiyo nyeti.
Licha ya kulazimika kuchukua hatua alizochukua  kama kiongozi, ni wazi kuwa shushushu huyo wa kike alitambua bayana kuwa laiti ‘lingetokea la kutokea’, yeye kama kiongozi angebeba mzigo wote wa lawama.
Nimesimulia habari hii si tu kwa vile nimevutiwa sana na ujasiri wa Paula Reid bali pia ningependa kuitumia kama mfano katika kujadili mada ya leo: nafasi ya watendaji kazi katika kumjenga au kumbomoa kiongozi.
Nikiri kwamba kwa mara ya kwanza kabisa, katika siku chache zilizopita nimejikuta nikishawishika kuafikiana na kauli inayosikika mara kwa mara kumhusu Rais Jakaya Kikwete, kwamba ‘anaangushwa na wasaidizi wake.’
Labda kabla ya kuingia kwa undani kwenye mada hii ni muhimu kuwafahamu japo ‘kiduchu’ hao wanaoitwa wasaidizi wa Rais. Wakati kuna watumishi kadhaa walioteuliwa na Rais kufanya kazi naye kama wasaidizi wake, kuna idadi kubwa zaidi ya ‘wasaidizi wasioonekana’ na ambao kwa kiasi kikubwa hata Rais mwenyewe hawafahamu lakini wanawajibika zaidi ya hao wateuliwa wake kumpatia ushauri sahihi kila siku kuhakikisha kuwa nchi inakwenda vizuri. Hapa ninawazungumzia ndugu zetu wa Idara ya Usalama wa Taifa.
Wakati mara nyingi watu walioteuliwa na Rais kuwa wasaidizi wake huwa ‘waliobobea’ kwenye fani moja, wanausalama wetu ni watumishi wa umma ambao kwa mafunzo yao na utendaji kazi wao hubobea kwenye takriban kila eneo.
Kwa hiyo hadi hapo unaweza kubaini kuwa ‘wasaidizi’ muhimu wa Rais si mshauri wa uchumi, au siasa, nk bali ni Maafisa wa Idara ya Usalama wa Taifa, ambao kimsingi wanawajibika moja kwa moja kwa Rais.
Naomba ieleweke kuwa simaanishi kuwa ikitokea mshauri wa Rais ameboronga basi hilo litakuwa kosa la Maafisa Usalama. Hapana. Hapa ninajenga ‘picha pana zaidi’ kwa maana ya tija kutoka kwa watu wenye uelewa na ujuzi wa takriban kila eneo la maisha ya Mtanzania.
Turejee kwenye hoja ya kuwa Rais Kikwete anaangushwa na wasaidizi wake (ila hapa nitaangalia hao wasaidizi muhimu zaidi, yaani watu wa Idara ya Usalama wa Taifa).
Kwa mujibu wa taratibu, Idara hiyo ni wasaidizi wa Rais kwa njia ya ushauri tu. Japo wana namna ya kulazimisha ushauri huo utekelezwe, mazingira yetu yanafanya suala hilo kubaki la kinadharia zaidi kuliko vitendo.
Nitoe mfano. Kabla ya uvamizi wa Marekani nchini Iraki, wanasiasa wenye mrengo mkali wa kihafidhina wanaojulikana kama neo-conservatives au kwa kifupi neo-cons, walifanikiwa kuzishawishi taasisi za usalama za Marekani kufukua kila aina ya matishio ‘yaliyosababishwa na kuwapo kwa Saddam Hussein madarakani.
Japo Rais wa wakati huo, George Bush (mtoto) naye alikuwa muumini wa itikadi hiyo ya mrengo wa kulia kabisa wa uhafidhina, kwa kiasi kikubwa kilichompa nguvu ya kuamuru uvamizi wa nchi hiyo huko Iraki ni ‘uthibitisho’ (ambao baadaye ulibainika kuwa fyongo) kuwa Saddam ana silaha za maangamizi ya umma (weapons of mass destruction).
Kwa wanaofuatilia siasa za kimataifa watakumbuka kauli ‘maarufu’ ya mkuu wa Shirika la Kijasusi la nchi hiyo George Tenet  kuwa ‘ushahidi kuwa Saddam ana silaha za maangamizi ya umma ni sawa na 'kuchumpa' na mpira wa kikapu (slam dunk), yaani ni ushahidi wa wazi kabisa, japo baadaye ilibainika kuwa ushahidi huo ulikuwa na mushkeli mkubwa.
Nimetoa mfano huo kuonyesha jinsi gani taasisi ya usalama wa taifa inaweza ‘kulazimisha’ ushauri wake ufuatwe, hasa ikizingatiwa kuwa kimsingi uhai wa taasisi ya urais unategemea mno ufanisi wa idara ya usalama ya nchi husika.
Sasa, tukiangalia-kwa mfano-sakata la mawaziri wanaotuhumiwa kwa ufisadi na kutakuwa wajiuzulu (hadi wakati ninaandaa makala hii walikuwa hawajajiuzulu) tunaweza ‘kumhurumia’ Rais Kikwete kwa kutopewa usaidizi wa kutosha na watendaji wenye dhamana ya kufukua na kuweka wazi ‘madudu’ yote yanayodaiwa kufanywa na mawaziri hao.
Kwa kawaida, Idara ya Usalama wa Taifa hupenyeza watumishi wake katika taasisi mbalimbali kwa minajili ya kupata taarifa sahihi za kiusalama, ambazo hutengeneza msingi wa ushauri wao kwa Rais baada ya kuzichambua.
Je, inawezekana taasisi hiyo nyeti imeshindwa kupata taarifa hizo kiasi kwamba ikashindwa kumfahamisha Rais yanayofanywa na mawaziri wake? Je, inawezekana kuwa taasisi hiyo ilifanikiwa kukusanya taarifa hizo na kutoa ushauri mwafaka lakini ukapuuzwa? Nisingependa kubaishiri jibu kwani ukweli unafahamika kwa wahusika.
Lakini katika mazingira ya kawaida si rahisi kwa kiongozi wa nchi kuamua kupuuzia ushauri wa wasaidizi wake muhimu ambao si tu ‘wana macho kila eneo’ bali pia wanawezesha taasisi ya urais kufanya kazi zake kwa ufanisi na kwa ujumla kuiwezesha nchi kuwa salama.
Katika namna fulani, wanausalama huhusika katika mchakato wa teuzi anazofanya  kiongozi mkuu wa nchi. Japo nisingependa kuingia kwa undani katika hilo, kwa kifupi ushauri wao ni muhimu sana (na pengine huzingatiwa) kabla Rais hajatangaza jina la anayemteua kushika wadhifa fulani.
Sasa, inapotokea baadhi ya wanaoteuliwa na Rais kuwa na walakini, inatubidi kujiuliza iwapo washauri walipotoka au aliyeshauriwa hakuzingatia ushauri husika.
Nimeshawishika kuafikiana na wanaodai kuwa Rais anaangushwa na wasaidizi wake kwa sababu, kwa uelewa wangu, tofauti na washauri wanaoteuliwa na Rais kwenye eneo moja, washauri muhimu kama wa Idara ya Usalama wenye uelewa wa takriban kila eneo wana namna wanayoweza kuitumia ‘kulazimisha ushauri wao ufuatwe kwa maslahi ya taasisi ya urais na taifa kwa ujumla.
Ikumbukwe kuwa Rais ni binadamu kama wengine, na si rahisi kufahamu kila kinachoendelea wizarani au mtaani. Wenye jukumu la kumsaidia kufahamu ni hao wasaidizi wake. Sasa kama hawatekelezi jukumu hilo ipasavyo itamwia vigumu Rais kufahamu kama ‘waziri fulani anafadhiliwa na mafisadi fulani’ au huko mtaani wananchi wanalalamikia hiki au kile.
Sawa, baadhi ya maamuzi yanapewa baraka na Rais kwenye vikao vya Baraza la Mawaziri. Lakini katika mazingira ya kawaida tu ya kibinadamu, atawezaje kufahamu iwapo taarifa zinazowasilishwa kwenye vikao hivyo ni sahihi au la, pasipo wasaidizi wake wenye jukumu la ‘kusaka ukweli’ kumfahamisha mapema?
Nimalizie kwa kusisitiza kuwa ninapoizungumzia Idara ya Usalama wa Taifa katika namna yoyote ile ninasukumwa na imani yangu kwa taasisi hiyo na kutaka kuiona ikizifanyia kazi changamoto mbalimbali inazozikabili ili si tu iwe na msaada mkubwa kwa Rais na taasisi ya urais bali pia kwa Taifa kwa ujumla.
Taasisi hiyo ni uti wa mgongo wa kila nchi duniani, na kila mzalendo anapaswa kuisapoti kwa namna mbalimbali ikiwa ni pamoja na ‘kuishtua pale inapoonekana imesinzia’ kama ninavyofanya katika safu hii.

25 Apr 2012


Predict the 2012 election with our interactive tool!

 at 09:17 AM ET, 04/24/2012

Predict Obama's odds in the 2012 election

Click the image to use the interactive tool.



“To see what’s in front of one’s nose requires a constant struggle,” George Orwell wrote. But the problem for those of us paying attention to the 2012 election is rather the opposite: To ignore what keeps being thrust in front of one’s face requires its own sort of struggle.
Here is a partial list of “scandals” that have grabbed hold of the news cycle in past weeks: “Rosengate,” in which a Democratic operative and CNN contributor named Hilary Rosen said something dismissive about Ann Romney’s work history; “Dog-gate,” in which conservatives pretended to be outraged that President Obama, as a 7-year-old living in Indonesia, had been fed dog meat; and “Cookiegate,” in which Mitt Romney asked if cookies he was offered were from 7-Eleven and inadvertently insulted a local baker.
I could go on. But I won’t. It’s too depressing. The good news, however, is that the tornado of idiocy that seems to accompany modern presidential campaigns — remember “lipstick on a pig”? — doesn’t much matter.
Political scientists have long known that you can predict most of what will happen in a presidential election with just a few key pieces of information: how the economy does, for instance, and the incumbent’s approval ratings in the summer. If you have those two numbers — even before you know the opponent, the campaign strategies or the issues — you can usually call the winner.
What these models suggest, in other words, is that the ephemera of elections aren’t that important. Not that this stuff doesn’t matter at all: Elections are often close, and a few percentage points can mean the difference between defeat and victory. But these micro-scandals mostly serve to distract us from the things that really do matter. And I don’t want to spend the next seven months distracted.
So I asked three political scientists — Seth Hill of Yale, John Sides of George Washington University and Lynn Vavreck of UCLA — to help me create an election forecasting model. And when I say “help me,” I mean that they did all the work and then sat me down and explained, slowly and using small words, what they had done.
The final model uses just three pieces of information that have been found to be particularly predictive: economic growth in the year of the election, as measured by the change in gross domestic product during the first three quarters; the president’s approval rating in June; and whether one of the candidates is the incumbent.
That may seem a bit thin. But it calls 12 of the past 16 elections right. The average error in its prediction of the two-party vote share is less than three percentage points.
Then I started playing with the model. And frankly, it just looked wrong. If GDP is flat — that is to say, if the economy doesn’t grow at all this year — and Obama’s approval rating is 45 percent, he wins 49 percent of the time. If you boost growth to a still-anemic 1.5 percentage points, he wins 74 percent of the time. That seems a little unlikely.
That, the political scientists said, is the point of a model such as this one.
“There’s this moment where you go, ‘Whoa, that’s a high number,’ ” Vavreck says. “ ‘Something must be wrong.’ But what it forces you to do is . . . to divorce yourself from contemporary context. You can’t go in thinking, ‘But, oh, this president is black,’ or ‘Gas prices are high,’ or ‘We just had the tea party.’ You have to strip all that away and say: ‘Incumbent parties, in growing economies, almost always win in contemporary American history.’ ”
She’s right. Since 1948, only three incumbent presidents have lost reelection campaigns: Gerald Ford, Jimmy Carter and George H.W. Bush. Carter and Bush both ran in very bad economies. Ford was a bit of an odd case, as he took office after Richard Nixon resigned over Watergate, and even so, the election was extremely close. This is the way models discipline your thinking: They force you to see relationships and patterns that conflict with your intuition.
The question is what happens when you add contemporary context back in. The model, for instance, assumes that voters will have the same reaction to slow economic growth in 2012 that they would have had in 1996 or 1964. But the past four years have seen the worst financial crisis since the Great Depression. Voters might be much less willing to forgive slow growth. Or, since many place the bulk of the blame for the crisis on George W. Bush, perhaps they’ll grade Obama on a kind of curve. The model can’t tell us.
And, sadly, neither can the past. Since 1948, there have been only 16 presidential elections. Which is another limit of models like this one: a relatively thin data set spread over a relatively long time. It would be nice to have more examples of presidential elections conducted during once-in-a-generation crises, in the Internet era, with serious third parties, with African American incumbents, with Mormon challengers, etc. And as Nate Silver, a statistician and blogger at the New York Times, points out, these models often do much worse when tested against new elections that are not in the original sample.
The three contests that the model was worst at calling were the 2008 race, where it predicted that Obama would get an additional 3.7 percentage points; the 1992 election, where it forecast that the elder Bush would win easily; and the 1972 election, where it foretold an even larger victory for Nixon. Perhaps race depressed Obama’s numbers, Ross Perot hurt Bush, and Nixon hurt Nixon. But those are just hypotheses. We have no way of knowing whether they’re right. We can’t rerun the elections under different conditions.
So sure, perhaps this year will be different — that’s what my gut tells me, and the model has me thinking about the ways in which that could be true. But the reality is, everyone always thinks “this year” will be different, and they’re usually wrong. That’s what the model tells me.
I am, however, confident that if this year really is different, it won’t be because of “Dog-gate.”
There’s no reason we should have all the fun. So we’ve opened the model for you to play around with athttp://wapo.st/election-predictor. Put in your best guess for economic growth this year and Obama’s approval rating in June. Or rerun previous elections and see how the model performs. At the very least, it’ll be a nice distraction from, well, all the distractions.

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.