6 Dec 2012
4 Dec 2012
30 Nov 2012
30.11.12
Evarist Chahali
RAIA MWEMA
No comments

NILIPOSIKIA Abdulrahman Kinana ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) hisia zangu zilikwenda kwa Karl Rove, Mmarekani anayeweza kuelezwa kama gwiji la mikakati ya siasa (political strategist) katika duru za siasa za Marekani.
Kwa uelewa wangu wa siasa za Marekani na za huko nyumbani, Rove na Kinana wanafanana kwa karibu katika utendaji kazi wao. Wote wawili ni watu waliopata mafanikio makubwa katika majukumu yao ya kuhakikisha ushindi wa mgombea waliyekuwa wakimuunga mkono; George W. Bush kwa upande wa Rove, na Rais Jakaya Kikwete kwa upande wa Kinana.
Hata hivyo, wakati Kinana amefanikiwa katika chaguzi mbili ‘kumpatia’ ushindi Kikwete, Rove alijaribu na kushindwa kupata ushindi wa mgombea zaidi ya Bush, harakati zake kwa kutumia taasisi za American Crossroads na Crossroads GPS (Grassroots Political Strategy) na mikakati wa ‘kumwaga’ dola bilioni moja kumuunga mkono aliyekuwa mgombea wa Republicans, Mitt Romney, kumwangusha Rais Barack Obama, hazikuzaa matunda.
Kimsingi, baadhi ya wachambuzi wa Uchaguzi Mkuu wa Marekani mwaka huu wanayumkinisha kuwa ukiachilia mbali kushindwa kwa Romney, wahanga wakubwa wa uchaguzi huo ni Rove na baadhi ya wachambuzi wa siasa (political pundits).
Wakati Rove, ambaye pia ni miongoni mwa pundits hao, ‘aliangukia pua’ licha ya matumizi makubwa ya fedha kupitia taasisi alizokuwa akiongoza, wachambuzi wengine wa kisiasa wanatafsiriwa kuwa ‘walipigwa bao’ na magwiji wa takwimu wakiongozwa na Mmarekani nguli wa ubashiri kwa kutumia takwimu, Nate Silver.
Katika ubashiri wake, Silver alisema Obama angepata kura za uchaguzi (electoral college votes) 313 (akapata 332) na Romney 225 (akapata 206). Kwenye uchaguzi wa Seneti, Silver alibashiri Democrats wangepata viti 52.5 (wakapata 53) na Republicans viti 47.5 (wakapata 45). Kitakwimu, ubashiri huo unaweza kuitwa sahihi. Hiyo ni kinyume kabisa na Rove aliyebashiri Romney angeshinda kwa angalau kura za uchaguzi 279 dhidi ya Obama.
Nirejee kwa Kinana. Baada ya kuteuliwa kwa mwanamikakati (strategist) huyo wa CCM kunikumbusha kuhusu Rove, nikakumbana na swali jingine kichwani: baada ya mafanikio makubwa kwa awamu mbili za Kikwete (2005 na 2010), je, uamuzi wa Kinana kuingia kwenye ‘active politics’ utadumisha rekodi yake au ndio political suicide (kujiua mwenyewe kisiasa) yake?
Kimsingi, japo nimemfananisha Kinana na Rove kana kwamba siasa za uchaguzi huko nyumbani ni za uwazi kama za Marekani, lakini pengine tukiingia kwa undani na kuangalia vigezo vingine vilivyosaidia ushindi wa Kikwete - kwa mfano nafasi ya ‘Wanamtandao’ na ‘usaidizi’ wa Idara ya Usalama wa Taifa na Jeshi la Polisi kwa CCM - inawezekana kazi ya Kinana ilikuwa nyepesi tu kwa vile mazingira yalikuwa mwafaka kwa mgombea wa CCM kushinda.
Lakini wakati ninajaribu kumtendea haki Kinana kwa kutoihukumu rekodi yake kwa vitu ambavyo havipo wazi kirekodi (yaani kama vigezo nilivyovitaja hapo juu), Jumapili iliyopita zikapatikana habari na picha zikimwonyesha anagawa leseni 21 za uchimbaji madini kwa wananchi huko Mugusu, Geita.
Kwa kweli sikuamini kwamba Kinana niliyefikia hatua ya kumlinganisha na Rove angeweza ‘kuingia mkenge’ wa kuigeuza CCM kuwa Wizara ya Nishati na Madini. Hivi kweli Kinana hatambui kuwa kusimamia na kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM hakumaanishi kupora majukumu ya Wizara? Kama hatambui hilo basi hapaswi kuwa japo mwenyekiti wa serikali ya mtaa, achilia mbali huo ukatibu mkuu wa CCM.
Kwa upande mmoja kitendo hicho cha Kinana kinarejesha ‘machungu’ ya ufisadi wa Kampuni ya Meremeta ambapo Watanzania walidanganywa kuwa Jeshi la Wananchi wa Tanzania lilijihusisha na biashara ya madini. Ninasema hivi, hili la Kinana kugawa hati za vitalu vya kuchimba madini lina kila dalili ya kuturejesha kwenye skandali kama hiyo ya Meremeta.
Hivi leseni alizotoa Kinana ziliombwa na nani huko wizarani? Yeye Kinana, CCM au hao wananchi waliokabidhiwa leseni? Kama Kinana ana uchungu na wachimbaji wadogo wa madini basi angeanza na hizo kampuni kubwa za madini ambazo kila mmoja wetu anatambua zinavyonufaika kutokana na udhaifu wa serikali yetu katika sera ya madini.
Hivi Kinana atanilaumu nikizua ‘conspiracy theory’ kuwa hao wananchi waliopewa leseni za kuchimba madini ni mwendelezo tu wa ufisadi ambapo walalahoi hutumiwa kwa maslahi ya mafisadi (yaani jina kwenye leseni ni la mlalahoi lakini mnufaika ni kigogo fulani)?
Leo CCM ‘mpya’ ya Kinana inapora jukumu la Wizara ya Nishati na Madini na kugawa leseni za uchimbaji madini, kwa nini kesho isipore jukumu la Ofisi ya Rais na kuiagiza Idara ya Usalama wa Taifa kuangamiza vyama vya upinzani vinavyoonekana tishio kwa CCM?
Naam, Waingereza wana msemo ‘once a cheater always a cheater’ (yaani, ukishawahi kuwa msaliti kwenye uhusiano wa kimapenzi utabaki kuwa msaliti wa mapenzi milele). Kama Kinana na CCM yake wameshaonja ‘utamu wa kuhonga leseni za uchimbaji madini’ (na yayumkinika kuamini kuwa hakuna mwenye uwezo wa kubadilisha kashfa hiyo ya kikatiba) kwa nini ‘asichonge mzinga’ na kupora majukumu ya wizara na idara/taasisi nyingine za serikali?
Laiti ningekuwa ninafahamiana na Kinana ningemshauri hivi: “Kinachoifanya CCM ionekane adui wa maendeleo ya Mtanzania wa kawaida ni uamuzi wa chama hicho kutelekeza msingi wake kama chama cha ‘jembe na nyundo’ (yaani wakulima na wafanyakazi) na kugeuka chama cha ‘bunduki na kisu’ (yaani hifadhi ya mafisadi na waporaji wa rasilimali zetu).”
CCM haiwezi kupendwa na Watanzania kwa kuingilia majukumu ya wizara. Kwamba wizara hizo zipo chini ya serikali ya CCM haimaanishi chama hicho kiingilie utendaji kazi wake.
Nimalizie makala hii kwa utabiri, sio ‘fyongo’ kama wa Rove niliyemlinganisha na Kinana, bali wa Nate Silver: kwa mwenendo huu wa Kinana kupora majukumu ya Wizara ya Nishati na Madini na kutoa leseni za uchimbaji madini kwa wananchi, ninabashiri kuwa anaweza kuishia kukumbukwa zaidi si kwa kuwa mmoja wa wanamikakati wa kisiasa mahiri kabisa katika historia ya Tanzania bali kwa ‘madudu’ (kama ya Karl Rove mwaka huu) ya kuwapa sababu za ziada wapiga kura wa Tanzania ‘kuizika’ CCM ikiwa bado hai hapo mwaka 2015.
27 Nov 2012
26 Nov 2012
26.11.12
Evarist Chahali
Global economy
No comments

The excitement that drove the discovery of "emerging markets" in the 1980s and the easy money that turbocharged growth during the booming 2000s are over. The most hyped countries -- Brazil, Russia, India, and China -- are all slowing sharply, taking the average growth rate in the developing world back to the old normal of about 5 percent. Today's global economy is all about moderate, uneven growth, with stars emerging in previously underappreciated nations. Forget about the BRICs -- these seven countries are the real breakout nations to watch:
1. Philippines: This country's huge wealth in natural resources is still largely untapped, and its long stagnant per capita income is still less than $3,000 -- but that means it has lots of room to grow. Since his election in 2010, President Benigno "Noynoy" Aquino has worked to finally deliver his political dynasty's promise to restore the luster of the Philippines of half a century ago, when it was billed as the next East Asian tiger. Aquino has overseen economic reforms that have made government spending more transparent and pushed for more tax revenue. And thanks tosuccess in the outsourcing industry, the Philippine economy has watched incomes grow and new wealth spread.
2. Turkey: The next two members of the club of trillion-dollar economies will be large Muslim democracies -- Indonesia and Turkey. Turkish Prime Minister Recep Tayyip Erdogan has brought to his country both economic orthodoxy, taming the hyperinflation that raged when he took office in 2003, and normalcy, opening up opportunities for pious Muslims who had been shut out of plum jobs by the previous secular regimes. This was tantamount to welcoming the majority into the commercial mainstream, and Turkey has prospered ever since, riding the success of its surging auto exports and the boom in the financial services sector.
3. Indonesia: Most economies that have thrived mainly by exporting raw materials -- think Brazil and Russia -- have slowed sharply amid the global financial downturn. Indonesia, however, is a commodity-fired economy that has achieved balance: between its export market and its healthy consumer economy, between the national capital and increasingly vibrant provincial generators of growth, and in the form of a leader, Susilo Bambang Yudhoyono, who understands the basics of economic reform. That makes the country the model example of those Southeast Asian tigers that were defanged in the 1997 financial crisis but are roaring once again today.
4. Thailand: Like the rest of its neighbors, Thailand suffered during the late-1990s East Asian financial crisis, when the devaluation of the Chinese currency suddenly made Southeast Asia uncompetitive. But as the renminbi has appreciated over the last few years, while Chinese wages have risen, the region, and Thai manufacturing in particular, is competitive again. Thailand's wild card is the seemingly never-ending political tension between capital and countryside. If Prime Minister Yingluck Shinawatra can contain it, Thailand is in a strong position to prosper as the central trade corridor of the Greater Mekong.
5. Poland: Poland, which entered the European Union in 2004, is a case study of a country in the "sweet spot" -- the period after a member state enters the EU but before it adopts the euro. It is stable, attracting investment, and benefiting from EU subsidies, and it has made required reforms to financial institutions and curbed its deficits to meet EU requirements. At the same time, it suffers none of the instability that comes with adopting the euro (see Portugal and Spain). It continues to grow much faster than the European average and is in no hurry to join the euro. In fact, Poland recently confirmed its status as a model European reformer with a tough pension overhaul that raised the retirement age to 67, at a time when many Europeans still retire in their late 50s.
6. Sri Lanka: The outbreak of war has derailed many high-growth economies, but few for as long as Sri Lanka, where the uprising of Tamil rebels that began in the 1980s did not end until just a few years ago. It was a miracle that the Sri Lankan economy was able to grow at even 4 to 5 percent during the war years, when nearly 30 percent of the landmass and 15 percent of the population had been cut off by the fighting. Now the country is reincorporating the provinces once controlled by the rebels, and, with its strategic location on shipping routes between India and China and a highly literate population, Sri Lanka is poised to grow much more rapidly.
7. Nigeria: In a country plagued for years by corrupt leaders, President Goodluck Jonathan has committed himself to reform, encouraging investment in Nigerian agriculture, oil and natural gas, and, most importantly, electrical power. For now, the whole country generates only as much electricity as some small towns in England, and this lack of a reliable power supply has made Nigeria one of the world's most expensive markets for operating a business. But the key in a place like Nigeria is that it doesn't take much to grow from a very low base, given its per capita income of just $1,500. The landmark change from bad to good leadership, now focused on improving basic infrastructure and boosting investment, may be enough to make Nigeria among the world's fastest-growing economies over the next five years -- and in the process make it the largest economy on the African continent.
SOURCE: Foreign Policy
24 Nov 2012
24.11.12
Evarist Chahali
No comments


Vigogo katika Idara ya Kazi na Pensheni ya hapa Uingereza walikumbwa na taharuki baada ya hackers kubandika tangazo feki la kazi kwenye tovuti ya Idara hiyo kwa nafasi ya 'mtaalam wa kuangamiza watu wasiotakiwa na serikali' Government Elimination Specialist.
Katika tangazo hilo (angalia picha hapo juu) hackers hao walidai kuwa "katika nyakati fulani, serikali ya Uingereza huwa na hitaji la kuwaondoa watu ambao uwepo wao unatishia amani."
Katika tangazo hilo ka 'kuzushi' pia kuliwekwa anwani ya barua pepe ya Shirika la Kijasusi la Uingereza ambalo makao yake makuu yapo jirani na Daraja la Vauxhaul jijini London (pichani chini)

Kwa habari kamili BONYEZA HAPA
23 Nov 2012
23.11.12
Evarist Chahali
RAIA MWEMA
1 comment

NIANZE makala haya na nukuu ya bandiko la Nape Nnauye, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), kuhusu ushindi wa hivi karibuni wa Rais Barack Obama wa Marekani. Nape aliweka bandiko hilo kwenye mtandao wa Jamii Forums, Novemba 7, mwaka huu akisema:
“Ushindi wa Obama dhidi ya Romney, ni fundisho zuri kwa upinzani nchini kwetu kama wataamua kujifunza, mafunzo muhimu sana kwa washindani wa kisiasa ni pamoja na; Mosi, kiwango cha utekelezaji wa ahadi mbalimbali na mipango (Ilani ya Uchaguzi) kwa wananchi ina nguvu kubwa katika kuwafanya wapigakura kuamua nani wa kumpa kura wakati wa kupiga kura...kupigia kura mabadiliko au la...Pili, kelele nyingi na wingi wa wapiga kelele si kigezo cha kupata kura nyingi siku ya kupigiwa kura...mikakati na ukaribu na wapigakura ambao huonyesha ni kiasi gani Chama kiko karibu na kuzijua changamoto zinazowakabili wapigakura, ni moja ya misingi mikubwa...Tatu, kutumia muda mwingi kuponda mafanikio yaliyopatikana kwenye kipindi cha mshindani wako...hasa aliyeko madarakani, hakusaidii kukufanya upate kura, bali wenye akili zao wataona unawadharau na kuwaona wajinga kama vile hawaoni yaliyofanyika...ndicho kilichommaliza Romney...Nne, lakini ushindi kwa Obama ni dalili njema za kukubalika kwa fikra za kijamaa kwa Taifa kubwa na la kibepari duniani...sasa tizameni upya itikadi zenu...”
Katika makala haya, nitamjibu Nape hoja kwa hoja kwa minajili ya kuwafumbua macho Watanzania wenzangu juu ya hatari ya baadhi ya wanasiasa kama Nape kuteka mafanikio ya wanasiasa wa nchi nyingine na kuyalinganisha na ubabaishaji wao ambao wao wanaamini ni mafanikio.
Kimsingi, mwanasiasa huyo amepotoka katika hoja zote nne. Ingawa ni kweli kwamba CCM na Serikali yake wamejaribu kutekeleza baadhi ya ahadi zao (kwa mfano ujenzi wa barabara kadhaa), moja ya ahadi za msingi iliyotolewa na mgombea wa chama hicho mwaka 2005, Rais Jakaya Kikwete, kuhusu maisha bora kwa Watanzania imeendelea kuwa kiini macho.
Kwa mtizamo wangu, kikwazo kikubwa kwa ahadi hiyo ya Rais Kikwete, ni ufisadi ambao yayumkinika kuhitimisha kuwa umeshamiri zaidi tangu Awamu ya Nne iingie madarakani. Na ufisadi usingepaswa kuwa kikwazo kwani moja ya matamko ya awali ya Rais Kikwete baada ya kuingia madarakani ilikuwa kuwapa ‘deadline’ mafisadi, akidai kuwa asingekuwa na huruma nao na kwamba tabasamu lake lisitafsiriwe vibaya.
Hadi leo hakuna fisadi mmoja aliyejali ‘deadline’ hiyo, na badala yake tunashuhudia ufisadi mpya ukiibuka kila kukicha. Kwa makusudi, Nape anajaribu kulinganisha utekelezaji wa ahadi za Obama wakati anaingia madarakani na porojo za CCM.
Wakati Obama amefanikiwa kutekeleza ahadi ya kumteketeza aliyekuwa gaidi wa kimataifa, Osama bin Laden, na pia kutekeleza ahadi yake ya kuyaondoa majeshi ya Marekani huko Iraki, licha ya ‘deadline’ ya Rais Kikwete kwa mafisadi kubaki historia tu, ahadi nyingine kuwa angemaliza kero ya mgao wa umeme, imeendelea kuwa ndoto tu.
Katika hoja ya pili, Nape anadai CCM inazijua changamoto zinazowakabili wapigakura wa Tanzania. Yupo sahihi. CCM inatambua kero za Watanzania, hususan kushamiri kwa rushwa nchini, lakini chama hicho kimetokea kuwa hifadhi ya wala rushwa.
Ushahidi wa karibuni kwamba CCM ni kichaka kinachohifadhi mafisadi ni kusuasua kwa Serikali yake kuwashughulikia majambazi walioficha fedha zetu huko Uswisi. Anachokiita Nape kuwa ni wingi wa kelele, akimaanisha za vyama vya upinzani, kwa hakika ni kilio cha Watanzania walio wengi, ukiondoa mafisadi. Kelele hizo anazozungumzia Nape ndizo zilizopelekea kuibua ufisadi mkubwa kama wa EPA, Richmond na kadhalika na sasa hili suala la fedha zilizoibwa na mafisadi na kufichwa Uswisi.
Katika hoja ya tatu, Katibu Mwenezi huyo wa CCM anadai kuwa kudharau mafanikio ya utawala uliopo madarakani, ni sawa na kuwatusi wapigakura. Kimsingi, sijawahi kuwasikia CHADEMA au chama kingine cha upinzani kikiponda jitihada za Serikali ya CCM katika masuala ya maendeleo ya nchi. Na ndiyo maana Rais Kikwete alipokuwa ziarani mkoani Arusha, alimwagiwa sifa na baadhi ya wapinzani hao hao ambao Nape anadai wanaponda kila kitu.
Kile anachotafsiri Nape kwamba ni kuponda kila kitu, kwa hakika ni usikivu wa vyama vya upinzani kwa kero za wananchi na kisha kuziongelea hadharani. Sawa, ujenzi wa barabara ni moja ya ‘priorities’ zetu, lakini miundombinu bora kwenye jamii iliyogubikwa na ufisadi, ni sawa na kuwa na ndoo inayojazwa maji ilhali imetoboka.
Rais Kikwete anajenga, mafisadi wanabomoa, na pasipo kuwadhibiti mafisadi hao, ni wazi kwamba jitihada zake zitaishia kuwa moto wa karatasi tu.
Hoja ya nne ya Nape inanifanya nijiulize kama alikuwa anafanya utani mbaya au ni uthibitisho kwamba hata Katibu Mwenezi wa Taifa wa CCM haelewi chama chake kinafuata itikadi gani. Nape anaweza kuwa mjamaa, na anaweza kuwa anatamani chama chake kirejee kwenye itikadi hiyo, lakini haihitaji kuwa na uelewa wa siasa za nchi yetu kutambua kuwa CCM iliyokumbatiwa na mafisadi, si tu haifuati siasa za ujamaa, bali haiwezi kurejea kwenye itikadi hiyo kamwe.
Wakati Nape ana haki ya kulinganisha ‘mafanikio’ ya CCM na chama chochote kile (haki hiyo imebainishwa katika Katiba yetu: freedom of expression), ukweli ni kwamba kitakachokimaliza chama hicho tawala ni mitizamo kama hiyo fyongo ya Nape kuwa kelele za wapinzani ni zao binafsi na si vilio vya Watanzania.
Wakati niliweza kubashiri kwa usahihi ushindi wa Obama, ninachelea kufanya hivyo kwa uchaguzi wetu mkuu wa mwaka 2015 kuhusu nafasi ya wapinzani kuing’oa CCM. Hiyo si kwa sababu CCM ina mafanikio kama Obama na chama chake cha Democrats (yaliyopelekea kumbwaga Romney na Republicans kwa ujumla), bali ukweli kwamba upinzani una kazi kubwa ya kujiimarisha kati ya sasa na 2015 kama kweli una nia ya kuing’oa CCM, ambayo kimsingi inafanya kila jitihada kung’olewa madarakani haraka iwezekanavyo.
15 Nov 2012
15.11.12
Evarist Chahali
DINI TANZANIA
No comments
Nianze makala hii kwa kujipongeza kutokana na ‘ubashiri wangu sahihi’ kuhusu Uchaguzi wa Rais wa Marekani. Kama mnakumbuka, katika makala ya kwanza kwa mwaka huu nilijaribu kubashiri mwenendo wa masuala mbalimbali kwa ‘mwaka mpya’ 2012, na moja ya ubashiri huo ulikuwa huu:
“Kwa kuzingatia uchambuzi wa watu mbalimbali na kwa kadri ninavyofuatilia siasa za Marekani, dau (bet) langu ni ushindi ‘kiduchu’ kwa Obama dhidi ya Mitt Romney, mgombea ninayetabiri atapitishwa na Republican (iwapo upepo wa kisiasa hautobadilika.)”
Well, Romney alifanikiwa kushinda kuwa mgombea wa Republican na hatimaye kuchuana na Obama kwenye uchaguzi moja ya chaguzi zilizokuwa na ushindani mkali kabisa, na hatimaye Obama akafanikiwa kutetea kiti chake cha Urais (nami nikafarijika kuona ‘utabiri’ wangu umetimia.)
Tukiachana na hilo, makala hii anahitimisha mfululizo wa makala zangu kuhusu vurugu za kidini huko nyumbani. Katika kuhitimisha, nitazungumzia maeneo manne: vikwazo vya ndani ya Uislam kupata ufumbuzi wa manung’uniko yao; baadhi ya migongano ya kiimani kati ya Waislam na Wakristo, na ‘utata’ wa Kikatiba kuhusu migongano hiyo; na mwisho, mapendekezo ya nini kifanyike kukabiliana na vurugu za kidini huko nyumbani.
Vikwazo vya ndani ya Uislam kupata ufumbuzi wa manung’uniko yao:
Maeneo mawili yanayothibitika kitaaluma kuwa ni msingi wa manung’uniko ya Waislamu wengi ni upatikanaji (access) wa nafasi ya elimu na ajira. Sote twatambua kuwa ukimnyima mtu elimu unamnyima fursa ya ajira (angalau kwa ajira zinazohitaji ujuzi.)
Tukiweka kando ‘lawama’ kuhusu ‘mfumo wa kibaguzi, ni muhimu kwa Waislam wenyewe kutambua kuwa lawama pekee haziwezi kuleta ufumbuzi utakaoleta angalau usawa katika fursa za ajira na elimu. Tukumbuke kuwa hata mkoloni hakuamua kutupa uhuru kwa kumchukia au kumlaumu tu.
Kadhalika Nduli Idd Amin (ambaye hivi karibuni baadhi ya ‘Waislam wenye msimamo mkali’ walibadili mtizamo wao na kumwona kama shujaa katika namna ileile ya kifo cha gaidi la Kimataifa Osama bin Laden kiliombolezwa na watu hao kama shujaa wao) hakuondoka kwa vile tulimwita kila aina ya jina baya.
Kama Waislam wanaafikiana kuwa mfumo ‘wa kibaguzi’ uliwanyima fursa ya elimu na hivyo kuwatengenezea mazingira magumu ya kupata ajira zinazohitaji elimu, basi ni muhimu kwao kuwekeza vya kutosha kwenye elimu.
Na moja ya njia bora inaweza kuwa kuziwezesha shule za kidini (pengine kuanzia madrasa) zitoe pia elimu ‘ya kidunia.’ Nilishaeleza huko nyuma kwenye mfululizo wa makala hizi jinsi shule za seminari za Kikristo zilivyochangia kuzalisha wasomi Wakristo.
Huu ni ‘ukweli mchungu’: kama mtoto wa Kikristo akitoka shule anaenda twisheni kuongeza maarifa ya ‘elimu ya kidunia’ ilhali mwenzie wa Kiislam akitoka shule anaenda madrasa kuongeza elimu ya kidini, ni wazi mmoja wao anajitengenezea mazingira mazuri ya kufaulu huku mwingine anajikwaza. Hapa simaanishi watoto wasiende madrasa bali ikiwezekana, shule za kidini (ikibidi hata kuanzia madrasa) zijumuishe pia elimu ya kidunia.
Kwa uelewa wangu, misikiti si mahala pa ibada pekee bali pia sehemu ya kumpatia muumini elimu itakayomwezesha kumtumikia Muumba wake ipasavyo. Pengine kuna umuhimu kwa kasi ya ujenzi wa misikiti kuendana na kasi ya ujenzi/uanzishwaji wa taasisi za kielimu, au ikibidi kutumia misikiti hiyo kama sehemu za ‘mapambano ya kuziba pengo la kielimu linalowakabili Waislam wengi.’
Pendekezo jingine ambalo lipo nje ya uwezo wa Waislamu ni kwa serikali kuangalia uwezekano wa kile kinachofahamika katika lugha ya Kiingereza kama ‘affirmative action’ (yaani upendeleo wenye lengo la kuleta uwiano kwa kundi flani katika jamii katika eneo flani.) Sitaki kuamini kuwa kama takwimu zikiwekwa wazi kuonyesha pengo lililopo kielimu na kiajira kati ya Wakristo na Waislamu, kisha serikali ikaridhia kutaka kupunguza pengo hilo kwa njia za uwazi, Wakristo watapinga hatua hiyo. Cha muhimu ni kufanya jitihada hizo kwa uwazi. Affirmative action imeweza kufanikiwa kwa kiasi fulani katika nchi za Magharibi kuleta uwiano kati ya, kwa mfano, ‘wazungu’ (Whites) na makundi madogo katika jamii (minorities), kwa mfano Watu Weusi (Blacks).
Baadhi ya migongano ya kiimani kati ya Waislamu na Wakristo, na utata wa Kikatiba unaotokana na migongano hiyo:
Kuna migongano kadhaa ya kiimani kati ya Waislamu na Wakristo lakini nafsi hainiruhusu kuitaja/kuizungumzia yote. Hapa nitazungumzia eneo moja tu, ambalo binafsi ninalitafsiri kama ‘nyeti’ zaidi.
Kwa Wakristo, Yesu ni Mungu na pia mwana wa Mungu (yaani Utatu Mtakatifu wa Mungu.) Kwa Waislamu, ile kusema tu Mungu ana mtoto (achilia mbali mtoto huyo ni Nabii Issa bin Mariam, yaani Yesu) ni kufr. Hakuna njia ya mkato katika migongano huu, hasa kwa vile dini hizi mbili zinaongozwa na Maandiko Matukufu/Matakatifu tofauti, yaani Kuran Tukufu kwa Waislam na Biblia Takatifu kwa Wakristo. Laiti Waislam wangekuwa wanatumia Biblia kuchunguza imani ya Wakristo kuwa Yesu ni Mwana wa Mungu, na laiti Wakristo wangekuwa wanatumia Kuran kuchunguza kwanini kusema Mungu ana mtoto ni kufr, labda kungepatikana mwafaka wa namna flani.
Lakini kama ilivyo kwa sie wanafunzi wa stadi za siasa kuwekea mkazo zaidi kwenye siasa na sio Fizikia, ndivyo ambavyo Waislam wanawekea mkazo kwenye Kuran na Wakristo kwenye Biblia. Na huo ni wajibu kwa kila muumini.
Hata hivyo, kama ambavyo sie wanafunzi wa siasa kuna nyakati tunalazimika kuyaelewa maeneo mengine ya kitaaluma in relation to siasa, ndivyo ambavyo baadhi ya Waislam wanafanya jitihada ya kuuelewa Ukristo in relation to Uislam, na baadhi ya Wakristo kuuelewa Uislam in relation to Ukristo. Hata hivyo hao ni wachache.
Na kwa bahati mbaya (au makusudi), jitihada hizo za kusaka uelewa wa dini nyingine ‘zimetekwa’ na dhamira ‘mbaya’ ya ‘kutaka kumwelewa adui vizuri ili kumkabili vizuri pia.’ Kwa wanaofuatilia mihadhara ya ‘kashfa’ ya kidini watakuwa wameshuhudia namna wengi wa wahubiri wanavyotumia Biblia au Kuran kuonyesha kwanini Ukristo au Uislam sio dini sahihi.
Lakini ili kuepusha ‘overgeneralization’ (kuhitimisha mambo jumla jumla) ni muhimu kufahamisha kuwa wapo wanazuoni wachache wa Kiislamu wanaoisoma Biblia kwa minajili ya uelewa tu wa kidini (na si kupambana na Ukristo).Kadhalika, katika stadi za kidini za Kikristo kuna wachache wanaoisoma Kuran kwa minajili ya uelewa tu wa kidini.
Mgongano wa kiimani kati ya Waislam na Wakristo kuhusu “Yesu ni Mungu na pia Mwana wa Mungu” ulijidhihirisha zaidi katika kesi iliyomkabili mhadhiri mmoja wa Kiislam, Ustaadh Khamis Dibagula, ambaye mwaka 2000 alihukumiwa kwenda jela huko Morogoro kwa ‘kashfa’ ya kudai “Yesu si Mungu” kama wanavyoamini Wakristo.
Kipengele cha 19 cha Katiba yetu kinatoa uhuru wa kuamini dini yoyote (japo kinakumbushia umuhimu wa kufanya hivyo bila kuathiri sheria za nchi). Na kipengele cha 18 kinatoa uhuru wa kutoa maoni (pasipo kuathiri sheria za nchi.) Kwahiyo basi Kipengele cha 19 cha Katiba kilimruhusu Dibagula kuamini “Yesu si Mungu/Mwana wa Mungu”, na kipengele cha 18 kilimruhusu kueleza imani yake hiyo waziwazi.
Kwahiyo, kwa upande mmoja Katiba iliruhusu kutoa maoni ambayo kwa upande mwingine ni kashfa. Hili ni eneo hatari ambalo ninachelea kuingia kwa undani zaidi kwani hata huo migongano wa kisheria uliopelekea Dibagula kufungwa na hatimaye kuachiwa huru ni suala ambalo Waingereza wanaliita legal minefield (yaani uwanja wa kisheria uliotegwa mabomu).
Kwa kifupi, ufanisi wa Katiba katika suala hilo unategemea zaidi busara za waumini, hususan utashi kuwa “nikasema hili-japo ni sahihi katika imani yangu-nitakuwa ninamkwaza flani.” Lakini, kusema ni jambo moja na kuamini ni jambo jingine. Katiba inaweza kuzuwia kusema hadharani kuwa “Yesu si Mungu/Mwana wa Mungu” lakini haiwezi kuzuwia wanaoamini kuwa “Yesu si Mungu/Mwana wa Mungu.”
Na kwa vile sheria zinazotokana na Katiba yetu ndizo zilizomfunga Dibagula kwa ‘kashfa’ lakini baadaye zikamwachia huru, hatua hiyo inajenga taswira gani kuhusu Katiba yetu kama chombo kinachopaswa kulinda uhuru wa kuabudu na wa maoni?
Nini kifanyike?
- Tuukabili ukweli kuwa tuna matatizo. Badala ya kuwa na sensa zinazokwepa kutupa ufahamu wa uwiano wa kielimu na ajira kati ya Wakristo na Waislam, ni muhimu kuwa na njia za wazi za kufahamu ukubwa wa tatizo la inequality katika maeneo mbalimbali, na hili si kwa Waislam pekee bali hata makundi mengine ya jamii.
- Jitihada za makusudi zinahitajika kushughulikia matatizo hayo. Ugonjwa hauponi kwa kujidanganya kuwa haupo. Badala ya kuruhusu wanasiasa watumie manung’uniko ya Waislam kama mtaji wao wa kura (mfano ahadi feki za CCM kwa Waislamu kuhusu Mahakama za Kadhi na kujiunga na OIC), harakati za kiraia zikiongozwa na wanazuoni na wanataaluma wenye mtizamo wa kuleta maelewano badala ya mifarakano ziimarishwe.
- Jitihada za ndani na nje ya Uislam zinahitajika katika kuhamasisha maendeleo ya kielimu kwa Waislam. Malalamiko pekee hayawezi kuleta ufumbuzi. Kadhalika, ushirikiano kati ya Waislam na serikali na taasisi nyingine za kidini na kijamii ni muhimu iwapo itakubalika kuwa na affirmative action.
Adui yetu mkubwa ni umasikini unaotishia uhai wa nchi yetu bila kujali huyu ni Hamisi na yule ni John. Mafisadi wanaotafuna raslimali zetu na kuficha mabilioni huko Uswisi, visiwa vya Jersey, nk hawafanyi hivyo kwa vile wanawapenda Wakristo na kuwachukia Waislam (au kinyume chake), bali wanamnyonga kila Mtanzania pasi kujali dini yake.
Kama ambavyo umasikini wetu ni mtaji mzuri kwa maharamia wa kisiasa kununua kura ndivyo ambavyo utengano wetu wa kidini unavyokuwa turufu kubwa kwa wanasiasa mufilisi ambao kimsingi dini zao si Uislam au Ukristo bali ulafi wa kuifilisi nchi yetu hadi tone la mwisho.
UMOJA NI NGUVU UTENGANO NI UDHAIFU
11 Nov 2012
11.11.12
Evarist Chahali
DINI TANZANIA, WAISLAM
No comments
KATIKA matoleo mawili yaliyopita ya jarida hili maridhawa, safu hii imekuwa ikijadili vurugu za kidini zilizojitokeza hivi karibuni nchini.
Katika makala hii, nitaanza sehemu ya kwanza ya kuhitimisha mjadala huo (na sehemu ya pili ya hitimisho itakuwa katika toleo lijalo).Ni matarajio yangu kuwa mfululizo huu wa makala hizi utafungua mjadala mpana zaidi kuhusu hali ya dini nchini Tanzania, nafasi ya dini katika kujenga au kubomoa amani, na hatimaye mapendekezo ya nini kifanyike kudumisha umoja, upendo, amani na mshikamano miongoni mwetu.
Mwamko ulioonyeshwa na makundi mbalimbali ya kijamii katika kulaani na kuzungumzia suala hili unatoa picha chanya kuwa wengi wetu tunatamani kuiona Tanzania yetu ikiendelea kuwa “kisiwa cha amani” (japo neno ‘amani’ lina tafsiri pana, na linaweza kuzua mjadala mwingine mpya. Lakini kwa minajili ya mada hii, tuitafsiri amani kama hali ya utulivu na maelewano miongoni mwa jamii).
Katika makala zilizotangulia, nilijikita zaidi kubainisha sababu ambazo kwa uelewa wangu zilichangia kuleta vurugu hizo za kidini. Nimejaribu kurejea historia ya nchi yetu, kabla na baada ya uhuru, na kuonyesha sababu zilizozalisha manung’uniko ya Waislam, hususan katika maeneo makuu mawili ya upatikanaji (access) wa fursa ya elimu na ajira.
Kwa kuangalia michango mbalimbali ya wanajamii katika mjadala kuhusu vurugu hizo, moja ya hoja inayoonekana kupewa uzito mkubwa ni ile inayodai kuwa chanzo cha vurugu hizo si dini.
Naomba niweke bayana msimamo wangu kuwa binafsi ninazitafsiri vurugu hizo ZINA SABABU ZA KIDINI japokuwa si DINI PEKEE bali pia kuna mwingiliano wa sababu nyingine.
Ninachomaanisha hapa ni kwamba si kweli kuwa vurugu hizo hazihusiani kabisa na dini bali dini ni moja ya sababu za vurugu hizo.
Kwa kuwa katika makala zilizotangulia nimeelemea zaidi katika sababu hizo ‘zisizo za kidini kwa asilimia 100,’ katika makala hii ya mwanzo wa hitimisho nitajaribu kujadili ‘eneo hatari’ la dini kama moja ya chanzo cha vurugu hizo.
Ninasema ‘eneo hatari’ kwa sababu yayumkinika kuhisi kuwa baadhi ya wasomaji hawatopendezwa na uthibitisho nitakaoweka wazi, na ambazo ni lazima tuziongelee ili si tu tuweze kuwa na mjadala wa maana kuhusu suala hili, bali pia tuweze kuwa katika nafasi ya kusaka ufumbuzi.
Kama ilivyo mahala kwingineko (kwa maana ya si Tanzania pekee), uchambuzi kuhusu dini si tu unaweza kuzua hisia hasi (kama vile kuhisi mwandishi Mkristo haruhusiwi kukosoa Uislam, au kinyume chake), lakini pia unakabiliwa na tatizo la msingi la vigezo vingine vinavyoathiri dini husika, kama vile tofauti kati ya mjini na vijijini, idadi ya wakazi katika sehemu husika, historia ya sehemu husika, nk.
Kwa kifupi-na huu ni mfano tu-inaweza kuwa na ugumu wa namna fulani kuuchambua Ukristo kwa kutumia mikoa miwili ya Kilimanjaro na Kaskazini Pemba kama maeneo ya kupata takwimu za kuwezesha uchambuzi husika.
Wakati Kilimanjaro ina idadi kubwa ya Wakristo, Kaskazini Pemba ina idadi kubwa ya Waislamu. Tofauti hizo ‘zisipolindwa vema kwa kuzingatia kanuni za tafiti’ zinaweza kuzua matokeo ‘fyongo.’
Na suala hili la ‘vigezo vingine’ ni moja ya mambo yaliyojitokeza katika utafiti wangu kuhusu harakati za vikundi vya Kiislamu huko nyumbani.
Kwa mfano, baadhi ya wahojiwa wa Kiislamu katika jiji la Dar es Salaam walionekana kuwa na hamasa kubwa kuzungumzia ‘ubaguzi wanaofanyiwa na kile walichokieleza kama Mfumo Kristo,’ wengi wa wahojiwa katika ‘maeneo yasiyo ya mijini (rural areas) walionekana kuelemea zaidi kwenye kero zinazowakabili kila siku katika nyanja kama za afya, elimu na kilimo.
Hata mwanazuoni mmoja wa Kiislamu niliyefanya naye mahojiano alikiri kwamba, (namnukuu) “…kwa huko vijijini haya masuala ya udini hayana uzito kulinganisha na adha zinazowakabili wananchi katika maeneo hayo ambazo kimsingi hazibagui kuwa huyu ni Juma au Petro…”
Tukiweka kando ‘kikwazo’ hicho kinacholeta ugumu fulani katika kuchambua dini, moja ya mifumo (models) ya kuchambua vurugu (ziwe za kidini, kikabila, kisiasa, nk) unaonyesha hali hii (kwa mchanganuo wa jumla): ubaguzi huzua manung’uniko; manung’uniko huzua hamasa; hamasa huzua upinzani ambao waweza kuzua vurugu.
Na moja ya sababu za msingi zinazoelezwa katika model hiyo kuwa zinaweza kujenga hisia ya kubaguliwa ni kupotea kwa hali ya kujiendeshea mambo pasi kuingiliwa (autonomy).
Kufutwa kwa Mahakama za Kadhi kunaweza kuwa mfano mwafaka.
Japo mahakama hizo zilikuwa za kidini lakini kimsingi zilijitosheleza kushughulikia ‘kesi za kidini’ miongoni mwa Waislamu (yaani masuala kama mirathi, nk).
Lakini eneo jingine linaloweza kuingia katika kundi hili ni ushiriki wa baadhi ya Waislamu katika harakati za uhuru. Ushiriki huo haukuwa wa kisiasa tu bali wa kidini kwani moja ya mafundisho ya Uislamu katika kushughulikia jambo baya (kama udhalimu wa mfumo wa ukoloni) ni “kulikemea, kulichukia au kuliondoa” jambo hilo.
Kwa kutafsiri ushiriki wa Waislamu hao ulikuwa na msingi wa kidini (licha ya siasa), kujumuika kwao kuliwapa autonomy ya aina fulani, yaani kuweza kuitumia imani yao ya kidini kukabiliana na jambo baya (ukoloni).
Kama nilivyobainisha katika makala zilizotangulia, hisia kuwa “tulikuwa mstari wa mbele kupambana na mkoloni lakini uhuru ulipopatikana tumeishia kuwa chini ya wenzetu waliomsapoti mkoloni (kwa maana ya ukaribu kati ya ukoloni na Kanisa/ Ukristo)” zinaweza kutafsiriwa kama kupoteza autonomy hiyo.
Lakini pia ni muhimu kuelewa kuwa Uislamu si suala la imani pekee bali ni mfumo kamili wa maisha. Stadi zinaonyesha kuwa pindi mfumo wa kimaisha unapoonekana kuwa hatarini (kwa sababu moja au nyingine) inaweza kuleta mwamko wa kukabili tishio husika.
Kimsingi, dini hutoa mwongozo kwa muumini kuhusu maisha yake kibinafsi na katika jamii. Sasa tukiafikiana kuwa Uislamu kama dini na kama mfumo kamili wa maisha hauridhii aina yoyote ya uonevu, ni wazi hisia kuwa “Waislamu wanabaguliwa” zinaweza kufuata ile model ya ubaguzi – manung’uniko – hamasa – upinzani.
Pengine hili halitowapendeza baadhi ya wasomaji: katika utafiti wangu (na katika baadhi ya stadi nyingine) kuna uthibitisho wa kuwapo kwa vikundi vya Kiislamu vyenye mrengo mkali wa kiimani (Islamic extremists). Naomba ieleweke kuwa uwepo wa vikundi hivyo katika Uislamu haimaanishi kuwa mrengo mkali katika dini ni kwa Uislamu pekee.
Israel kuna Wayahudi wenye mrengo mkali kabisa ambao hawataki kabisa kusikia lolote kuhusu Wapalestina. Huko Marekani kuna Wakristo wenye msimamo mkali kabisa ambao kwa kiasi fulani wanachangia ‘uhasama’ kati ya taifa hilo na Waislamu na Uislamu kwa ujumla (kwa mfano Pasta Terry Jones aliyezua sokomoko duniani kwa kuchoma Kuran Tukufu).
Sasa kwa huko nyumbani, vikundi hivyo vya Waislam wenye msimamo mkali si tu ‘wameteka’ ajenda ya msingi ya manung’uniko (tunayoweza kuafikiana kuwa ni halali) ya Waislamu bali pia wamegeuza ajenda hiyo kuwa nguzo muhimu ya kupambana na wale wote wasioafikiana na mtizamo wao.
Wahanga wa ‘wana-msimamo mkali’ hawa si Wakristo pekee bali hata Waislamu wenzao wanaoonekana ‘kutokuwa na msimamo kama wao.’
Uthibitisho wa hii ni pamoja na vurugu zilizojitokeza nyakati fulani za uporaji wa misikiti. Japo wateka misikiti hao walidai kuwa wanairejesha kwa Waislamu misikiti iliyokuwa chini ya BAKWATA, kuna uthibitisho kuwa lengo lilikuwa kuigeuza misikiti hiyo kuwa ya ‘msimamo mkali.’
Badala ya hoja ya msingi inayohusu manung’uniko ya Waislamu dhidi ya mfumo wanauona kuwa unawakandamiza, vikundi vya Kiislamu vyenye msimamo mkali vinakwenda mbali zaidi kiasi cha kutaka kulazimisha kila mtu afuate imani yao (pasipo kujali ni Muislamu au la).
Uchambuzi wa wasifu wa baadhi ya viongozi wa vikundi hivyo unatoa picha ya waumini ambao ‘si washika dini kihivyo’ lakini ‘wenye hasira kali dhidi ya yeyote asiyeshika dini inavyostahili.’
Kwao, ‘kafir’ si asiye Muislamu tu bali hata Muislamu anayeshirikiana na wasio Waislamu (hata pale ambapo ushirikiano huo hauna madhara kwa Waislamu na dini yao).
Kuna tatizo jingine la msingi. Wakati kumekuwa na jitihada kubwa kwa Wakristo kutafsiri Biblia Takatifu kwa Kiswahili, yayumkinika kusema kuwa jitihada za kuitafsiri Kuran Tukufu kwa Kiswahili hazijaendelezwa vya kutosha.
Sasa, kwa vile ni rahisi kutumia Maandiko Matukufu/Matakatifu kuhalalisha au kuharamisha kitu fulani, kutoa fursa kwa watu wasio na uelewa wa kutosha wa maandiko hayo kuwa viongozi wa dini kunaweza kuwa na madhara.
Kwa uelewa wangu, ijtihad ni jukumu la wanazuoni wa Kiislamu, lakini kuna uthibitisho wa kitaaluma kuwa baadhi ya viongozi wa vikundi vya Kiislamu vyenye msimamo mkali wamejipachika jukumu hilo na kufanya tafsir (exegesis au tafsiri) katika minajili inayoendana na ajenda/matakwa yao (ya ‘msimamo mkali.’)
Japo katika Uislamu ni vigumu kuchora mstari unaotenganisha dini na siasa, tofauti na kwenye siasa ambapo mwananchi yeyote yule anaweza kuwa mwanasiasa, kwenye dini ni tofauti, kwani uelewa wa dini (kwa maana ya maandiko, sheria, nk) ni kigezo muhimu cha kuwa na mamlaka ya kuwaongoza waumini wengine.
Katika toleo lijalo, makala ya mwisho wa mfululizo huu itaangalia vikwazo vya ndani ya Uislamu kupata ufumbuzi wa manung’uniko yao; baadhi ya migongano ya kiimani kati ya Waislamu na Wakristo, na ‘utata’ katika Katiba kuhusu migongano hiyo; mapendekezo ya nini kifanyike kukabiliana na vurugu za kidini huko nyumbani.
ITAENDELEA
10 Nov 2012
4 Nov 2012
28 Oct 2012
28.10.12
Evarist Chahali
DINI TANZANIA, RAIA MWEMA
No comments
KABLA ya kuingia kwa undani katika makala hii ambayo ni mwendelezo wa makala iliyochapishwa katika toleo la wiki iliyopita, naomba niwasimulie wasomaji mkasa ambao unaweza kuwa “funga kazi” katika utitiri wa vimbwanga vya watawala wetu.
Wiki iliyopita, Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo, aliwatia aibu Watanzania akiwa Afrika Kusini alipodai kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaundwa kwa Muungano kati ya kisiwa cha Bahari ya Hindi cha Pemba na Zimbabwe. Ukidhani ninamsingizia, basi angalia video hii kupitia kiunganishi hiki; http://goo.gl/uW6H2
Na licha ya kufanya madudu hayo, Mulugo ‘alilikoroga’ zaidi alipodai kuwa Muungano huo wa ‘Zimbabwe na Pemba’
ulitokea mwaka, (namnukuu) “one nineteen sixty-four.” Mwaka huo hauleti maana yoyote, iwe kwa Kiingereza au kwa Kiswahili, kwani 1-19-64 inaweza tu kuleta maana kwa mfumo wa tarehe wa Marekani (yaani tarehe 19 mwezi wa kwanza mwaka 64).
Ninaomba nitamke bayana kuwa Naibu Waziri Mulugo ni mzembe wa hali ya juu. Yawezekana aliandaliwa hotuba hiyo, lakini haihitaji busara japo kidogo kuwa huwezi kukurupuka kutoa hotuba kabla hujaipitia. Sijui Rais Jakaya Kikwete alijisikiaje baada ya kuona video hiyo yenye hotuba ya Mulugo, lakini kwa kosa hilo la ajabu kabisa, Naibu Waziri Mulugo sio tu anapaswa kutuomba radhi Watanzania kwa kupotosha historia ya taifa letu bali pia ingefaa aondolewe katika wadhifa wake unaoshughulikia elimu (elimu gani hiyo ambayo wakati Tanzania ‘haijamalizana’ na Malawi kuhusu mpaka kwenye Ziwa Nyasa, yeye ‘anaihamasisha Zimbabwe ‘idai Pemba ni sehemu ya nchi hiyo?’)
Nisiongelee sana suala hilo bali ninawaachiwa Watanzania wenzangu kuhitimisha wenyewe kuhusu madudu haya ‘ya karne.’
Kama nilivyoahidi katika toleo lililopita, wiki hii ninaendelea na mjadala kuhusu vurugu za kidini ambazo kwa siku za karibuni zinaonekana kushika kasi.
Katika makala iliyopita, nilijaribu kuonyesha sababu zilizojenga msingi wa manung’uniko ya Waislamu katika masuala ya elimu na ajira. Mwishoni mwa makala hiyo niliuliza maswali yafuatayo (ninajinukuu)
“Je; kilichotokea Mbagala ni hasira tu za baadhi ya Waislamu waliochukizwa na kitendo cha ‘mtoto wa Kikristo’ kukojolea Kuran Tukufu?
Je; udini ni tatizo kubwa katika Tanzania yetu ingawa halizingumzwi vya kutosha? Binafsi, ninaamini jibu la swali hilo, ni ndiyo. Kama ni ndiyo, kwa nini tunalikwepa tatizo hili?
Je; yawezekana udini ni turufu muhimu kwa baadhi ya wanasiasa mufilisi?”
Kwa swali la kwanza, nilishabainisha kwenye makala hiyo kuwa kwa mtizamo wangu, vurugu hizo za Mbagala zilisababishwa na zaidi ya hasira za baadhi ya Waislamu waliokasirishwa na kitendo cha mtoto kuikojolea Kuran Tukufu.
Yayumkinika kusema kuwa hasira za baadhi (na pengine ni wengi) ya Waislamu huko nyumbani (Tanzania) ni dhidi ya kile kinachotajwa kama ‘Mfumo Kristo.’ Kwa kifupi, wanaoamini hivyo wanauona mfumo huo unawapendelea Wakristo sambamba na kuwabagua Waislamu, hususan katika sekta za elimu na ajira, ambazo kimsingi zinahusiana kwa karibu.
Japo, kama nilivyobainisha katika makala yangu iliyopita kuwa Ukristo kwa kushirikiana na ukoloni ulichangia kutengeneza hali ya kutokuwa na usawa katika elimu na ajira, haimaanishi moja kwa moja kuwa Wakristo wanawabagua Waislamu. Naomba nieleweke hapa: kuna tofauti kati ya mfumo na watu wanaonufaika au kuathiriwa na mfumo huo.
Ninasema hivyo kwa sababu, wakati hoja ya kuwa Wakristo wanawabagua Waislamu ingeweza kuwa na mashiko wakati wa utawala wa Awamu ya Kwanza chini ya uongozi wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, na Awamu ya Tatu ya Rais Benjamin Mkapa, ambao wote ni Wakristo, ni vigumu kwa hoja hiyo kuwa na uzito kwenye Awamu ya Pili na hii ya sasa (ya Nne) za marais Waislamu Ali Hassan Mwinyi na Jakaya Kikwete.
Hata hivyo, kwa mtizamo wangu, viongozi hao wote wanne, hawawezi kukwepa lawama kuwa kwa kiasi kikubwa hawajafanikiwa sio tu kuyatupia macho kwa makini malalamiko ya Waislamu bali pia wamekuwa wakikwepa kuyashughulikia kwa uzito unaostahili.
Angalau kwa upande wa Baba wa Taifa tunaweza kukubaliana kuwa sio tu kwamba alishakiri kuwa kukosekana kwa usawa katika elimu na ajira kwa Waislamu ni tatizo, lakini pia alikwenda mbali zaidi na kujaribu kuukarabati mfumo wa elimu ili uweze kutoa fursa kwa Watanzania wote bila kujali imani zao.
Ni muhimu kukumbuka kuwa licha ya ukweli kuwa Mwalimu alikuwa Mkristo na mshika dini, mafanikio yake katika harakati za kupigania uhuru yalichangiwa zaidi na Waislamu.
Lawama ‘kubwa’ inayoweza kuelekezwa kwa Mwalimu ni jinsi serikali yake ilivyoshughulikia suala ‘nyeti’ la uundwaji Baraza la Waislamu Tanzania (BAKWATA) na kupigwa marufuku Jumuiya ya Ustawi wa Waislamu wa Afrika Mashariki (East African Muslim Welfare Society- EAMWS).
Kwa kifupi, tangu kuundwa kwake, kwa kiasi kikubwa BAKWATA imeshindwa kujitenganisha na serikali, na pia imeshindwa kufuta hisia kuwa ‘ni chombo kinachotumiwa na serikali kuwagawanya na kuwakandamiza Waislamu.’
Japo EAMWS ilikuwa taasisi ya kidini lakini ilionekana kama ‘mkombozi wa Waislamu’ hususan kwenye sekta ya elimu, na yayumkinika kusema kuwa laiti kuundwa kwa BAKWATA kungeibua taasisi yenye ufanisi kama EAMWS, basi pengine pengo lililopo kwenye maeneo ya elimu na ajira kati ya Waislamu na Wakristo lingekuwa limepungua kwa kiasi kikubwa.
Ufinyu wa nafasi unaninyima fursa ya kuingia kwa undani kujadili hoja za kuifungia EAMWS na hatimaye kuanzisha BAKWATA, lakini ukweli kwamba serikali hiyo hiyo iliyoipiga marufuku EAMWS ilishiriki kikamilifu katika uundwaji wa BAKWATA umechangia kudumu kwa hisia kuwa ‘BAKWATA iliundwa kama chombo cha serikali dhidi ya Waislamu.’
Na katika utafiti wangu, matokeo ya awali yanaonyesha Waislamu wengi hawaridhishwi na mwenendo wa BAKWATA katika kutetea maslahi yao. Kimsingi, moja ya jambo lilionekana ‘kuwaunganisha’ wahojiwa wangu wa Kiislamu (ambao nilieleza katika makala iliyopita kuwa niliwagawanya katika makundi mawili ya ‘walio na msimamo mkali’ na ‘wa kawaida’- kwa minajili ya kiutafiti- ni suala hilo la BAKWATA.
Sasa katika mazingira haya ambacho chombo pekee kikuu kinachotarajiwa kuwaunganisha Waislamu kinaonekana kuwa kinawakandamiza, na-kuwanukuu baadhi ya wahojiwa- ni sehemu ya ‘Mfumo Kristo’ ni wazi kuwa baadhi (na pengine wengi) ya Waislamu wanajiona kama ‘mateka wa mfumo,’ kwa maana ya hisia za kubaguliwa na Wakristo na kubaguliwa na chombo kinachopaswa kutetea maslahi yao (BAKWATA).
Kwa mtizamo wangu, kuwa ‘mateka wa mfumo usiokubalika’ kunasababisha kuuchukia, na kama tujuavyo, chuki huzaa hasira. Hasira hizo zinasubiri mazingira ‘mwafaka’ ili zichomoze hadharani. Na tukio kama la Mbagala lilitoa ‘fursa mwafaka’ kwa hasira hizo.
Na ‘hasira’ hizo zinatoa jibu la swali la pili kuhusu udini. Kwamba Waislamu wanawachukia Wakristo, sitaki kuamini hivyo. Kwamba Waislamu (baadhi au wengi) wanachukizwa na mfumo wanauona kuwa unawabagua na kuwapendelea Wakristo, binafsi jibu langu ni ndio.
Na kwa vile ni vigumu kutofautisha ‘Mfumo Kristo’ na Wakristo kama waumini wa dini, ni muhimu kutambua kuwa kwa namna fulani-kubwa au ndogo- kuna uhasama wa kisaikolojia au kihisia kati ya madhehebu haya mawili. Kinachosaidia ‘kuficha’ uhasama huo ni misingi iliyojengwa huko nyuma ambayo ilisisitiza zaidi Utanzania wetu kuliko Uislamu au Ukristo wetu.
Kwa bahati mbaya-au makusudi-misingi hiyo inavunjwa kwa nguvu na wanasiasa waliokuja baada ya Mwalimu Nyerere. Kwa kifupi, wakati siasa ya Ujamaa na Kujitegemea ilijenga misingi ya kutuunganisha Watanzania tuwe kitu kimoja, ‘ubabaishaji’ uliofuatwa-kwa mfano kinachoitwa Azimio la Zanzibar- umechangia sana kukuza ombwe lililotokana na ‘kifo cha Ujamaa,’ na wakati huo huo kutoa fursa kwa wenye ‘hasira’ zao kuziweka hadharani.
Kama nilivyowahi kuandika katika makala moja huko nyuma kuhusu unafiki wetu kuhusu suala la ushoga (hoja kubwa ikiwa ni imani zetu za kidini na mila na desturi zetu), kuna unafiki unaoendelea katika sio tu kuzungumzia suala la udini kwa uwazi zaidi bali pia hakuna utashi wa kisiasa (na hata kijamii) kukabili tatizo hili.
Ni nani asiyejua kuwa wakati wa utawala wa Mwinyi kulikuwa na baadhi ya Wakristo waliokuwa wakinung’unika chini chini kuwa teuzi za Mwinyi zilikuwa zinapendelea Waislamu? Ni nani pia asiyejua kuwa alipokuja Mkapa lawama kama hizo ziliendelea kuwapo chini chini kuwa Mkapa alikuwa akiwapendelea Wakristo? Na ni nani atakayejifanya hajui kuwa utawala wa Rais Kikwete umekuwa ukilaumiwa chini chini kuwa unawapendelea Waislamu?
Ninafahamu kuna watakaosema hizi ni hisia zangu tu. Hawa ndio ninaowaita wanafiki. Na unafiki huu ndio miongoni mwa vikwazo vikubwa vya kujadili tatizo la udini, na vurugu zinazohusishwa na tatizo hilo, kwa hofu ya kuitwa mdini. Niseme hivi, bora niitwe mdini kwa kujitoa mhanga kuanzisha mjadala wa suala hili kuliko ‘nionekane mwema’ ilhali tunalipeleka taifa letu mahali kusikofaa.
Nitajitahidi kuhitimisha mfululizo wa makala hizi kuhusu vurugu za kidini kwenye toleo lijalo, au pengine makala mbili zijazo. Hata hivyo, nihitimishe makala hii kwa jibu fupi kwa swali la tatu kuhusu udini unavyotumiwa na wanasiasa mufilisi kwa minajili yao binafsi.
Ninaamini sote tunakumbuka jinsi kampeni za uchaguzi mkuu uliopita zilivyogubikwa na tuhuma za udini. Na hapa nisiume maneno: chama tawala CCM kilifanya kila jitihada kuufanya ‘upadri’ wa mgombea wa CHADEMA, Dk. Willibrod Slaa, kuwa turufu muhimu ya kumnyima kura za Waislamu. Hili nitalijadili kwa kirefu katika makala ijayo, lakini kwa namna fulani, CCM haiwezi kukwepa lawama kuwa ni miongoni mwa vyanzo vya vurugu za kidini tunazoshuhudia hivi sasa.
Chama cha siasa kinapoamua kwa makusudi kuwagawa wapiga kura kwa misingi ya imani zao za kidini, kinaandaa ‘viungo’ kwa ajili ya vurugu za kidini. Na ikumbukwe kuwa ni CCM hii hii iliyowahadaa Waislamu kuhusu kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi (huku ikitambua kuwa haina dhamira ya dhati ya utekelezaji wa ahadi hiyo) na hadi sasa inaendelea kucheza danadana katika suala hilo.
Nimalizie makala hii kwa kuwakumbusha Watanzania wenzangu kuwa tuna kila kitu cha kupoteza (everything to lose) kwa kutengana kwa misingi ya kidini na hatuna cha kupoteza (nothing to lose) tukiendelea kuwa wamoja, kama majeruhi wa ufisadi, umasikini, magonjwa na dhahma nyingine zinazotukabili ambazo hazijali imani zetu za kidini. Ili Tanzania yetu ifike mahala tunapotamani ifike, au inapostahili kuwa, ni lazima tuwe kitu kimoja. Tukumbuke, UMOJA NI NGUVU NA UTENGANO NI UDHAIFU
Makala hii itaendelea toleo lijalo
22 Oct 2012
22.10.12
Evarist Chahali
BONGOFLAVA, Witnesz
No comments
ALCOHOLISM AND EFFECTS
POMBE NA MADHARA
Lets check why many people change characters baada ya kulewa pombe na pombe hufanya nini mwilini mwa binadamu anapozitumia? mili yetu iliumbwa kwa ajiri ya kujiponya yenyewe endapo tu utakuwa unakula vizuri na nikisema kula vizuri haimaanishi ule ushibe hapana bali ninamaanisha ule chakula bora chenye lishe bora,rutuba ambazo ni vitamins na minerals zinazoweza kulinda na kurutubisha mwili na automatically or kujiponya naturally na upungufu wa rutuba mbali mbali mwilini ndo huleta matokeo ya watu kuumwa pasipo kupona ama kuumwa magonjwa kama presha, kisukari cancer,donda ndugu,kumea vinyama usoni malaria na typhoid za mara kwa mara,liver and kidney failure n.k na kuyaita haya magonjwa kama ni magonjwa yasiyo tibika ama magonjwa sugu kwa mimi i agree to dis agre na kwa uwezo tulio nao wa kufikiri je huwa unauhudumia mwili kama linavyohudumiwa gari?POMBE NA MADHARA
kwa kuwa endapo ingekuwa hivyo binadamu wote wangeweza kuishi hadi miaka 85 ndo waanze kuzeeka kama jinsi ilivyo kwa wajapani lakini tunaenda kinyume na haya yote, hebu jiulize je utaweza kuweka maji kwenye engine ya gari ama chumvi badala ya petroli? haiwezekani na hii ni kwa kuwa gari halina uwezo wa kujisafisha lenyewe na kujiponya na ndo maana huwa tunalipeleka service je sisi huwa tunajifanyia service ama body detoxination? (kuodoa sumu mwilini na uchafu usiohitajika mwilini?)
So look at how our amazing bodies does mara nyingi huwa hatuwezi kuona emediet effects za pombe,sumu mwilini au effects za vyakula na aina ya madawa tunayotumia kwa kuwa miili yetu ili unbwa kwa ajiri ya kujiponya na kujiendesha yenyewe na ndo maana sumu haziwezi kuathiri mwili kama ambavyo ungeweka chumvi kwenye gari badala ya mafuta huwa effects zake zinajijenga taratibu na kufikia kikomo ama viungo vya kuchujia na kusambazia vitamins sahihi na minerals kukwama ambavyo mara nyingi viungo hivi viki collapse huwa very dangerous na viungo hivi ni ini na figo ambapo si tu hutumika kuchuja vilivyo vibaya na visivyo hitajika mwilini pia hutumika kwa kuvisambaza na kuvipeleka mahala husika panapohitaji certain type of vitamins and minerals so just imagine hivi viwili vikipata damage tge body suply inakuwa je?
kwa leo nitaishia hapo juu ya vungo hivi viwili as we go on nitaendelea kuwafahamisha zaidi but today ninazungumzia pombe huwa inafanya nini mwilini hadi wengine huonekana kama wanamatusi,wakorofi na wakati mwingine kutojitambua na ni kwa sababu gani watu dini mbali mbali huzikemea! the thing is pombe si mbaya but kilicho kibaya ni vile pombe inavyo damage mwili wako na kutake control of everything when ever your drunk your life,dignity, behaviour and how you think and make desicions na hata waelimishaji wa masuala ya VVU/Ukimwi husisitiza sana watu kutokuwa walevi kwa kuwa pombe yaweza sababisha ulewe na kuamua kuwa na mwanamke au mwanaume na kufanya ngono zembe ama ngono pasipo kutumia kinga, na pia waweza kumchukua mtu ambaye laiti ungekuwa mzima usingeweza hata kuongozana nae katika hali ya kawaida lakini kwa kuwa umekunywa pombe it was easy hadi kwenda kufanya naye mchezo mbaya kwa maana hiyo pombe hupunguza kudhoofisha ama kuua uwezo wako wa kufikiri na unakuwa poor decision maker.
MADHARA KWA MWANAMKE MJAMZITO
Kwa mwanamke mjamzito anayekunywa mara kwa mara pombe inaweza kumsababishia mtoto kuzaliwa taahira,inaweza ikasababisha kutoka kwa ujauzito (miscarriage) ama ikasababisha kudmaa kwa mtoto na asiweze kukua hata akiwa tumboni na baadae ikasababisha hyperactivity and irritability in the child, if a pregnant woman consumes alcohol on a regular basis (as well as drugs) the fetus can become addicted to these substances,
Pia alcohol ni substance ambayo hutumia vitamins na minerals nyingi mno toka mwilini kwa ajiri ya kujiendesha ama umeng'enyukaji wake na kama pombe ikikuta hakuna vitamins na madini ya kutosha mwilini huwa inatabia ya kwenda kuchukua zile vitamins zilimo kwenye Tissue mwilini ambazo tissue hizi huwa katika damu na ndo husababisha kasoro nyingi za mwilini na kuleta matokeo ya kudhoofu kwa mwili na kuanza kuumwa ovyo ovyo.
Mazingira sababishi juu ya wanywa pombe ni
Stress,Kazi,Kula bata na washkaji ama kunywa tu na marafiki pombe kwa kuwa compan yako yote wanakunywa,depression(mawazo) kujitenga, immaturity/foolish age kwa kudhani usipokunywa utaonekana haujakua bado ama hutoonekana ni kijana wa kisasa zaidi, loneliness (upweke) and Heredity
Madhara mengine ya matumizi ya pombe ni
1.In the Pancreas (acute Pancreatistis)
2.In the liver (cirrcohosis) kwenye Ini kupunguza ufanis wa
kufanya kazi laweza pia kuvimba ama kujaa maji
3.In the Heart (kwenye moyo) kuvimba,kujaa maji, n.k
4.In the urinary system( kwenye njia ya mkojo na ndo maana huona wakati mwingine walevi huwa wanajikojolea kwa kuwa hata nerves zao huwa kama disconnected na mtu wa namna hii anaweza ahisi kitu ama kwa wanaume anaweza akashindwa kufanya tendo la ndoa kwa kuwa hakuna hisia tena ama mzunguko wa damu haui mzuri na kupeleka taarifa kwenye ubongo kwa kuwa pombe huua oksijen inayosaidia mzunguko huo wa damu na kuzidisha ufanisi wa nerves sytem
5.In the skin kudhoofisha ngozi
6.In the sexual organs (causing impotence) kupunguza uwezo wa tendo la ndoa haswa kwa wanaume
7.In the gastrointestinal and digestive tracts, kupunguza uwezo wa usagaji chakula na kusababisha gesi nyingi kila wakati hata kama hujala chakula huwa kama umeshiba na kukata hamu ya kula.
8.In the nervous sytem which can become completely unsettled by the death of cells,hii ni kwa kuwa pombe huwa inaondoa maji kwenye these cells producing a series of nervous disoders which are frequently reflected in a sign depression and anxiety which in extreme cases can lead to delirium trements causing hallucinations ama kuweweseka,
So kwa wale wanaopata tatizo la hang over baada ya kunywa ama kama unataka kukata pombe na unawahi meeting ama ofisini waweza call 0753 32 0009 ili kupata kujua jinsi ya kuepukana ama kudhibiti hali hiyo.
Na kwa wale wanaotaka kufanya detoxination ama kufanya miili yao service na kuondoa sumu mwilini Tafadhari call 0753 32 00 09 Mtu ni afya
19 Oct 2012
Subscribe to:
Posts (Atom)