9 May 2011


Baada ya kifo cha Osama bin Laden,nani anaweza kuchukua nafasi yake?Tuangalie historia na tabia za warithi watarajiwa wa uongozi wa kundi la kigaidi la Al-Qaeda



big-fat-aman-nb04-inline
AFP-Getty Images
Ayman al-Zawahiri
Cheo: "Naibu" wa Osama
Wasifu: Daktari wa macho
Sifa Maalum: Msemaji mahiri wa Al-Qaeda
Maficho: Mara ya mwisho alionekana Khost, Afghanistan, mwaka 2001
Wasifu: "Kichwa" kilichoandaa Mashambulizi ya September 11,2001 nchini Marekani
Anafahamika zaidi kwa: Ushiriki wake katika mashambulizi ya mabomu kwa balozi za Marekani mwaka 1998
"Nembo" (trademark): Miwani ya njano


big-fat-aladel-nb04-inline
FBI-Getty Images
Saif al-Adel
Cheo: Mwandaaji wa operesheni za kigaidi kimataifa
Asili: Vikosi Maalum (special forces) vya Jeshi la Misri
Sifa maalum: "Bwana mipango"
Maficho: Waziristan, kwa mujibu wa ripoti
Wasifu: Aliwekwa kizuizini kwa miaka minane nchini Iran
Anafahamika kwa: Mashambulizi ya mabomu mwaka 1998
"Nembo": Vijinywele kwenye kidevu


big-fat-nb04-allibi-inline
Intel Center
Abu Yahya al-Libi
Cheo: Mwanateolojia
Asili: Mshairi na mwanazuoni
Sifa Maalum: Mwanapropaganda wa Al Qaeda
Maficho: Afghanistan au Pakistan
Wasifu: Alitoroka jula ya Wamarekani huko Bagram, Afghanistan
Anafahamika kwa: kujaribu kumuua Muammar Gaddafi
"Nembo": Hotuba kali


big-fat-nassar-nb04-inline
Intel Center / Polaris
Nasser al-Wuhayshi
Cheo: Kiongozi Peninsula ya Rabia
Asili: Katibu muhtasi wa Osama
Sifa maalum: Alitoroka gerezani Sanaa, Yemen, mwaka 2006
Maficho: Yemen
Wasifu: Alishirikiana bega kwa bega na Osama katika mapambano huko Tora Bora, Afghanistan
Anafahamika zaidi kwa: Kutoroka jela huko Yemen
"Nembo": "Andunje": ni mfupi wa chini ya futi tano



big-fat-adam-nb04-inline
Intel Center / AFP-Getty Images
Adam Gadahn
Cheo: Msemaji
Asili: Anapenda miziki ya sauti kali  yenye ujumbe wa kifo
Sifa maalum: Anamudu kiingereza vizuri,mjuzi wa teknolojia
Maficho: Alihamia Pakistan mwaka 1998, ameoa mkimbizi wa Kiafghanistani
Wasifu: Aliwahi kufungwa kwa kumpa kipigo mwenyekiti wa msikiti aliokuwa akiswali
Anafahamika zaidi kwa: Kumpa elimu Osama kuhusu mtikisiko kwenye sekta ya dhamana ya majengo (mortgage crisis)
"Nembo": Mjukuu wa mtaalam wa Kiyahudi wa elimu ya mkojo (urology)


big-fat-adnan-nb04-inline
FBI-Getty Images
Adnan el-Shukrijumah
Cheo: Afisa mipango ya nje
Asili: alisoma Kemia
Sifa maalum: Aliishi Marekani kwa miaka 15
Maficho: inadhaniwa kuwa Pakistan
Wasifu: Mrithi wa Khalid Sheikh Mohammed
Anafahamika zaidi kwa: Kupanga shambulio lililofeli la mabomu kwenye mfumo wa reli ya chini ya ardhi nchini Marekani mwaka 2009
"Nembo": Kushirikiana na magenge ya majahili wa Honduras


big-fat-nb04-alquso-inline
Fahd al-Quso
Cheo: Kamanda wa operesheni za mashambulizi
Asili: Mbeba mabegi ya bin Laden
Sifa maalum: Kulala fofofo: "alilewa" usingizi hadi akachelewa kazi ya kurekodi shambulio la kigaidi kwa manowari ya  USS Cole.
Maficho: Kaskazini mwa Waziristan
Wasifu: Kuandaa shambulizi la mabomu kwa manowari ya USS Cole.
Anafahamika zaidi kwa : Aliwatambua kwa Shirika la Upelelezi la Marekani (FBI) magaidi wawili waliohusika na mashambulizi ya kigaidi ya Septemba 11,2001 nchini Marekani
"Nembo": Nywele zake kwenye paji lake zimekaa kama herufi V iliyogeuzwa


big-fat-nb04-Droukdel-inline-tease
Sifaouoi Mohamed / SIPA
Abdelmalek Droukdel
Cheo: Kiongozi wa  Islamic Maghreb
Asili: mwanafunzi wa sayansi
Sifa maalum: Mtaalam wa milipuko
Maficho: Aljeria
Wasifu: Idara ya Hazina ya Marekani ilitaifisha mali zake mwaka 2007
Anafahamika zaidi kwa: Kuua watu 70 kwenye kwa shambulizi za bomu jijini Algiers,Aljeria
Trademark: Tambara la kijana kama yale ya mabaniani
Imetafsiriwa (isivyo rasmi) kutoka jarida la Newsweek




Mkutano wa tatu wa Diaspora umemalizika majuzi jijini London huku,kama ilivyokuwa kwa Diapora I na Diaspora II,tumeishia kushuhudia zaidi picha za matukio kuliko maelezo ya mambo muhimu yaliyojiri katika mkutano huo (if there were any).Sina tatizo na watu wanaopenda kupiga picha na viongozi kwani huo ni uhuru wao wa kikatiba.Hata hivyo,nina tatizo kubwa na wale wanaodhani picha na viongozi ni muhimu kuliko kuwabana viongozi hao,hususan wanaposhindwa kutoa maelezo ya kueleweka.

Waziri wa Mambo ya Nje Bernard Membe amekuwa sura iliyozoeleka kwenye mikutano hiyo ya Diaspora.Kwa wadhifa wake,ni mtu mwafaka kuiwakilisha serikali,sambamba na kusikia maoni,ushauri,maswali,nk kutoka kwa Watanzania wanaoshi nje ya nchi.Lakini kwa mwenendo wa ushiriki wake kwenye mikutano hiyo,yayumkinika kusema kuwa Membe amekuwa kama mtalii tu wa kutoa porojo moja baada ya nyingine badala ya kuwaeleza washiriki wa Diaspora Forums mafanikio yaliyokwishapatikana kutokana na uwepo wake au umuhimu wa mikutano hiyo (kama upo).

Usanii wa kwanza wa Membe ni katika kauli yake kuwa moja ya changamoto zinazoikabili serikali anayoitumikia ni kujua idadi ya Watanzania wanaoishi nje ya nchi.Huu ni usanii wa kitoto kwa vile Watanzania hao hajawaanza kuja nje wiki iliyopita,wala balozi za Tanzania nje-ambazo Membe ameziagiza kubuni mikakati ya kuwezesha kupata idadi ya Watanzania wanaoishi nje-hazijafunguliwa mwezi huu.

Badala ya kupachika jina la CHANGAMOTO,Membe alistahili kueleza bayana kuwa kutofahamika kwa idadi ya Watanzania wanaoishi nje ya nchi ni moja tu ya UZEMBE ULIOZOELEKA kwenye balozi zetu.Ni uzembe kwa vile umuhimu wa kufahamu idadi hiyo ya wana-diaspora umekuwepo tangu zamani hizo na sio mwaka huu tu au kwenye Diaspora Forums pekee.

Laiti washiriki wa Disapora hiyo wangekuwa serious,wangemkalia kooni Membe kumhoji kwanini zoezi hilo la kufahamu Watanzania waliopo nje ya nchi halijafanyika huko nyuma,na kwanini tuamini kuwa sasa litafanyika?Ikumbukwe Membe amekuwa Waziri wa Nje kwa miaka sita sasa,hivyo kukurupuka wiki iliyopita kukumbuka umuhimu wa kuwa na idadi ya Watanzania nje ya nchi ni sehemu tu ya ubabaishaji wake.

Membe anadai kuwa sababu ya yeye kuja London kuhudhuria mkutano huo ni kukusanya hoja kutoka kwa wadau ili ziweze kusaidia tatizo la Diaspora kupelekwa Bungeni na hatimaye kuingizwa kwenye Katiba.Come on,Membe!That's too cheap politicking even in your own standards.Yaani kukusanya hoja za Watanzania wanaoishi ughaibuni ni lazima kufanywe na waziri ilhali tuna balozi zetu na vyama mbalimbali vya Watanzania?

Na hata tukimpa Membe benefit of a doubt,kwanini asituambie namna alivyokwisha shughulikia hoja alizokusanya kwenye Diaspora I na Diaspora II kabla ya kukurupuka na usanii mwingine kwenye Diaspora III?Kama hoja za nyuma hazijafanyiwa kazi,how come hizo mpya au mwendelezo wa zile za zamani zitashughulikiwa sasa?

Japo Membe anastahili lawama,lakini washiriki wa Diapora Forums nao wanapaswa kulaumiwa kwa kuruhusu cheap lies kutoka kwa same crooked politicians year in year out.Yayumkinika kuamini kuwa udhaifu wa wahudhuriaji wa Diaspora Forums kuuliza maswali magumu yanayostahili majibu ya msingi unachangia sana kumfanya Membe awe "MGENI RASMI WA KUDUMU" kwenye mikutano hiyo kwani anajua he would easily get away with usanii wake.Unadhani angejua kuwa atakaliwa kooni kuhusu ubabaishaji wake,kwa mfano kwenye suala la dual nationality,angetia mguu kwenye Diaspora Forum iliyopita majuzi?

Lakini kilichonikera zaidi katika usanii wa Membe ni kauli yake ya kitoto kuwa eti changamoto nyingine inayoikabili Diaspora ni "WATU WENGI HAWAFAHAMU VIZURI MAANA YA DIASPORA".Utterly rubbish!Hivi Membe anaweza kutueleza amejuaje kuwa watu wengi hawafahamu maana ya Diaspora?Au,je anaweza kutuambia kwanini hawafahamu maana ya neno hilo ambalo lipo kwenye kamusi?Ungetarajia waliohudhuria mkutanio huo wamzomee Membe kwa kauli hiyo isiyo na kichwa wala miguu.Na Membe ana lipi la kutuambia katika madai yake kuwa neno Diaspora halifahamiki kwa wengi,i.e. kutofahamu maana ya neno hilo kunakwamishaje maazimio ya Diaspora Forums zilizopita?

Haya ndio matatizo ya kualika wageni rasmi wanaokuja kutalii badala ya kuzungumza mambo ya msingi.Ni dhahiri kuwa laiti waandaaji wa Diaspora Forums wangetaka mkutano huo uwe na maana wangeandaa mazingira ya kuepuka wababaishaji kama Waziri Membe ambao ni mahiri sana katika kutoa hotuba za kuleta matumaini lakini hotuba hizo zinabaki kuwa hotuba tu,na kusahaulika mara baada ya kumalizika kwa shughuli husika.

Kama kupiga konzi kwenye kidonda kibichi,Membe pasi aibu aligusia suala la uraia pacha (dual nationality).Akaanza kwa kueleza umuhimu wa uraia pacha,na kusema kuwa nchi zilizoruhusu uraia pacha zimewafanya watu wao kupata kazi nzuri zenye mishahara mikubwa na hivyo kuwawezesha kutuma fedha nyingi katika nchi wanazotoka.Huu ndio uelewa wa Waziri wa Mambo ya Nje kuhusu umuhimu wa Diaspora!!!

Labda hakupitia speech notes zake vizuri,labda hakufanya brainstorming ya kutosha kabla ya kutoa hotuba yake kwa wana-Diaspora,lakini ni wazi Membe anafahamu fika kuwa umuhimu zaidi wa uraia pacha ni suala la haki za binadamu kuliko mishahara mikubwa au kazi nzuri.Nani aliyemwambia Membe kuwa wana-Diaspora wana kazi za ovyo ovyo zisizolipa mishahara mizuri kwa vile tu hawana uraia pacha?

Kwa hoja hizi mfu,ni wazi kuwa Membe si mwakilishi mzuri wa wana-Diaspora katika kilio chao cha muda mrefu cha uraia pacha.Membe amegeuza Diaspora Forums kuwa sehemu ya kuwapa matumaini kuhusu suala hili ilhali hafanyi jitihada zozote kuhakikisha suala hilo linahama kutoka kuwa ahadi hewa na kuwa sheria kamili inayotekelezeka.

Kuhusu changamoto ya kuwawezesha Watanzania walio nje ya nchi kuchangia maendeleo ya Tanzania,Membe anapswa kufahamu kuwa kila Mtanzania aliye nje ya nchi ana connection na Tanzania.Wengine tuna wazazi,kaka,dada,wadogo,nk huko nyumbani na licha ya nchi yetu kujifanya haitambua umuhimu wa Watanzania walio nje,wameendelea kupunguza makala ya ufisadi kwa ndugu na jamaa zao huko nyumbani kwa kuwatumia fedha za matumizi na misaada mingineyo.

Katika mkutano huo,mmoja wa wajumbe alipendekeza uanzishaji wa kumbukumbu mkeka ya ujuzi na fani wazizonazo Watanzania waishio nje.Wazo zuri lakini nadhani mtoa hoja amesahau umuhimu wa data protection,na namna taarifa hizo binafsi za Watanzania walio nje zinavyoweza kuishia mtaa wa Mkwepu kwa wanaotengeneza vitambulisho feki.I would never trust fisadi awe na taarifa zangu binafsi ilhali nafahamu fika kuwa zitaozea tu kwenye mafaili kama sio kufungiuwa vitumbua na maandazi.

Kama taafira zilizokusanywa kufahamu chanzo cha milipuko ya mabomu huko Mbagala na Gongo la Mboto zimepuuzwa,mtoa hoja anataraji mijuiza gani  kwa taarifa za Watanzania walio nje kutumiwa ipasavyo?Nadhani kuna baadhi ya Watanzania wenzetu walio nje hawajishughulishi kufahamu uharamia,ufisadi,ubabaishaji,uzembe na utapeli wa kisiasa unaendelea huko nyumbani kiasi kwamba wanaweza kupoteza muda wao kuwasikiliza akina Membe "wakiuza sura" kwenye Diaspora Forums.

Unajua kwanini nasema Membe anafanya usanii kwenye suala la uraia pacha?Ameshatoa kauli kadhaa za kibabaishaji kuhusu suala hilo,moja ikiwa aliyoitoa Januari mwaka huu kwenye mkutano wa IOM ambapo alidai kuwa utafiti uliofanyika umehitimisha umuhimu wa uraia pacha,Wizara yake imeanzisha kitengo cha kushughulikia suala la Diaspora,na sheria ipo mbioni kuanzishwa.

Lakini kwenye mkutano wa Diaspora uliomalizika wiki iliyopita,Membe wala hakugusia ni lini sheria hiyo itaanza kufanya kazi.Katika mkutano huohuo wa IOM,Membe aliwazuga wajumbe kwa kuahidi kuwa sheria ya uraia pacha ingekuwa tayari kufikia mwisho wa mwaka jana.Amekuja London miezi mitano baadaye na kuendelea ngonjera hizo hizo.

Hebu sikiliza porojo za Membe kwenye Diaspora Forum II iliyofanyika mwaka jana



Na hapa pamoja na kuongelea mambo mengine,mwishoni mwa clip ifuatayo anajibu swali na Freddy  Macha kwa kuahidi tena "MWISHO WA MWAKA HUU" kama alivyoahidi mwaka jana kuwa "MWISHO WA MWAKA HUO 2010".



Enewei,kulikuwa Diaspora Forum I,ikamalizika na picha tukaona.Ikaja Diaspora Forum II,ikamalizika na picha tukaonyeshwa.Na majuzi imemekuja Diaspora Forum III,imemalizika wiki iliyopita na picha tumeziona.Tusubiri Diaspora Forum IV...bila shaka tutaendelea kushuhudia picha nyingine na usanii mwingine unaohanikizwa na maneno kama "mchakato","changamoto","vipaumbele" na usanii mwingine kama huo.Blogu hii inatoa wito kwa wana-Diaspora kujaribu kuwaonyesha Watanzania wenzatu walio nyumbani kuwa licha ya kutopendezwa na ubabaishaji wa baadhi ya viongozi wetu huko nyumbani,hatuwezi kutoa fursa kwa ubabaishaji huo kuwa exported hadi huku ughaibuni.Ili Diaspora Forums ziwe na manufaa,they need to go beyond being just another photo-ops.

7 May 2011


Nilipofika hapa Uingereza kwa mara ya kwanza,takriban muongo mmoja uliopita,nilishangazwa na jinsi wengi wa watu hawa waliotuletea dini huko nyumbani wakiwa hawana habari kabisa na dini.Ilinishangaza kuona baadhi ya majengo yaliyokuwa yakitumika kama nyumba za ibada huko nyuma yakiwa yamegeuzwa klabu za usiku au baa.

Kwa ujumla,idadi kubwa ya wanaohudhuria makanisani kwa hapa ni raia wa kigeni au wale wenye asili ya nje ya nchi hii.Hata hivyo,kuna idadi ya wastani ya Waingereza wanaojitambulisha kama wenye imani ya kidini japo haimaanishi kuwa wanakwenda makanisani.

Pamoja na kuzorota kwa dini miongoni mwa wengi,kwa kiasi kikubwa wananchi hapa wana uadilifu mkubwa hususan katika kutoa huduma.Unajua,kibarua sio suala la mshahara tu bali pia kujali yule unayemhudumia.Kadhalika,kutoa au kupokea rushwa sio tu suala la kukosekana kwa sheria madhubuti bali pia ni suala la kiroho,namna nafsi inavyomsuta mtu kutoa,kudai au kupokea rushwa.

Binafsi nadhani dini ya kweli ni upendo.Na hata katika Biblia Takatifu tunafundishwa kuwa ni vigumu mtu kumpenda Mungu ambaye hamuoni ilhali anamchukia jirani yake anayemwona kila mara.

Japo ni muhimu kuhudhuria nyumba za ibada,lakini binafsi naona ni bora kuwa mtu asiyekwenda kanisani au msikitini lakini anaishi katika namna anayompendeza Mungu (na wanadamu wenzie) kuliko hao wasiokosekana makanisani au misikitini lakini ndio wanaodumisha uzinzi,ufisadi,unafiki,na kila aina ya baya.Hapa simaanishi kuwa kila aendaye kanisani au msikitini hafanyi anayopaswa kufanya,bali napigia mstari umuhimu wa matendo mema.

Kwa hapa Uingereza kumekuwa na mfumuko mkubwa wa makanisa "mapya" (new Christian movements).Makanisa haya yanazidi kupata waumini wengi na kukua aidha kwa sababu madhehebu makuu (Katoliki,Waluteri,Waanglika,nk) yameshindwa kukidhi matarajio ya waumini hao wanaokimbilia makanisa mapya,au kwa upande mwingine ni ukweli kuwa licha ya majukumu ya kiroho,makanisa hayo ambayo waumini wake wengi ni wageni (hususan Waafrika) yamekuwa kama sehemu ya watu wanaotoka eneo moja kujumuika.Mnaijeria akienda kanisa la Kinaijeria anajikuta kama yupo nyumbani,na hivyo hivyo kwa Mtanzania akienda kanisa linaloendesha ibada kwa kiswahili.

Lakini,baadhi ya makanisa hayo yamekuwa yakishutumiwa kuwa ni miradi ya kitapeli ya wajanja flani.Kwa mfano,kituo cha runinga cha Channel 4 kiliwahi kuonyesha documentary ya namna baadhi ya makanisa ya Waafrika jijini London yalivyokuwa yakisababisha kuvunjika kwa ndoa (kwa mfano pale mchungaji anapomwambia mume kuwa mkewe ana majini) na hata kupelekea vifo,hususan vya watoto wadogo wanaotuhumiwa kuwa wana majini.Kibaya zaidi,baadhi ya maaskofu wa makanisa hayo walidiriki kudanganya mabinti kuwa matatizo waliyokuwa nayo yalihitaji maombi maalumu nyakati za usiku,na hatimaye mabinti hao wakaishi kufanyiwa tendo la ndoa.

Utafiti mdogo tuliofanya mie na wanafunzi wenzangu Faith Msina,Latifa Almasi (Queen Latifa) na Baraka Msemwa,mwaka 1999 (kama sehemu ya kozi ya Mwaka wa Tatu Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika Sosholojia ya Dini) ulionyesha matokeo kwamba wengi wa watu wanaoamua kujiunga na "madhehebu mapya" ni pamoja na wale wenye matatizo ya kibinadamu ambayo "dini kuu" zimeshindwa kuyatatua.Tulifanya utafiti wetu kwenye Kanisa "la Kakobe" (Full Gospel Bible Fellowship),Mwenge jijini Dar,na asilimia kubwa ya wahojiwa walikiri kuwa kilichowavutia kujiunga na kanisa hilo ni "miujiza" mbalimbali,kwa mfano kwenye uponyaji,ajira,nk.

Lakini jambo la kusikitisha ni tabia inayozidi kushamiri ya matapeli kuanzisha makanisa kama ajira.Hawa ni wajanja wanaofahamu fika kuwa masuala ya imani hayahitaji udadisi,na laiti tapeli husika akifanikiwa kutangaza "miujiza yake",basi muda si mrefu kijikanisa chake kitageuka hekalu kubwa la "maombezi na miujiza".Simaanishi kuwa wote wanaoanzisha makanisa ni matapeli,lakini ni ukweli usiopingika kuwa kuna matapeli kadhaa wanaotumia jina la Bwana kutapeli waumini wenye mahitaji ya kimwili na kiroho.

Ni kwa mantiki hiyo basi,siafikiani na msimamo wa baadhi ya wachunga kondoo wanaopinga dhamira ya serikali kukagua mapato na matumizi yao.Pengine ni kukosa ufahamu tu,uamuzi wa serikali kutotoza kodi au kutoangalia mapato na matumizi ya taasisi za dini ni suala la upendeleo (privilege) zaidi kuliko stahili.Kama waumini wa taasisi hizo za kidini wanawajibika kwa mamlaka za mapato,kwanini isiwe kwa viongozi wa dini na/au taasisi zao?

Je wachunga kondoo hao wa Bwana wanahofia nini kuhusu dhamira hiyo nzuri ya serikali?Ieleweke kuwa kama wana kipato juu ya kiwango cha msamaha wa kodi basi ni lazima walipe kodi.Lakini hata kama suala hapa si ulipaji wa kodi,ni muhimu kwa mamlaka za mapato kufahamu mapato na matumizi ya taasisi hizo kama ilivyo kwa taasisi nyingine za umma na za binafsi.Dini si kigezo cha kutofuata sheria,na hata Maandiko Matakatifu yanakumbusha kuwa "ya Musa apewe Musa,na ya Kaizari apewe Kaizari",or something like that.

Enewei,soma habari husika hapa chini

Maaskofu wapinga serikali kudai taarifa za mapato

na Betty Kangonga

BAADHI ya makanisa ya Kipentekoste yamesema si haki kwa serikali kudai taarifa ya mapato na matumizi ya fedha za makanisa wakati yenyewe haitoi hata ruzuku kwa taasisi hizo za dini.

Kauli hiyo ilitolewa jana jijini Dar es Salaam na Mchungaji wa Kanisa la Maombezi la Ubungo Kibangu (GRC), maarufu kama Mzee wa Upako, Anthony Lusekelo, wakati wa hafla ya chakula cha usiku kwa wachungaji 100 wa makanisa ya Kipentekoste.

“Huu ni uonevu usio na mfano, wachungaji lazima tusimame imara kuhakikisha tunatetea haki zetu, tena tunatakiwa kuacha woga. Kwa nini serikali inahitaji mapato na matumizi wakati hawajui fedha hiyo tunapopata? Tunahitaji serikali ijenge heshima na kazi inayofanywa na viongozi wa dini ndani ya nchi,” alieleza.

CHANZO:Tanzania Daima

6 May 2011


KESI YA BALOZI MAHALU: Mkapa akunjua makucha

na Happiness Katabazi

HATIMAYE utetezi wa Rais mstaafu Benjamin Mkapa katika kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia, Profesa Costa Mahalu, umetua rasmi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi, Kisutu jijini Dar es Salaam.

Mkapa ambaye ni shahidi wa pili wa kesi hiyo alitoa utetezi huo ambao unaweza kuandika historia mpya katika mwenendo wa kesi nchini, kupitia kiapo chake ambacho kimewasilishwa mahakamani na wakili wa mshtakiwa huyo, Mabere Marando.

Katika moja ya vipengele 13 vya kiapo hicho, pasipo kutaja jina, maelezo ya kiongozi huyo mstaafu yanamgusa Rais Jakaya Kikwete ambaye wakati Mkapa akiwa madarakani alikuwa ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Hiyo inakuwa ni mara ya kwanza kwa rais mstaafu, kutoa utetezi mahakamani kwa kesi inayomgusa mmoja wa waliokuwa wateule wake wakati akiwa madarakani.

Kesi hiyo Namba 1/2007 ambayo Mahalu anashtakiwa pamoja na Grace Martin inasikilizwa na Hakimu Mkuu Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Ilivin Mugeta.

Katika kesi hiyo, Mahalu na Martin wanatuhumiwa kwa wizi wa shilingi bilioni tatu katika ununuzi wa jengo la ubalozi mjini Rome.

Katika hati ya kiapo chake cha Machi 31 mwaka huu, ambayo imeandaliwa kwa mujibu wa Sheria ya Usajili wa Nyaraka (The Registration of Documents Act, Cap. 117 of 2002), Mkapa anaeleza kuwa kila kilichofanywa na Mahalu kilikuwa sahihi na kilikuwa na baraka ya serikali aliyokuwa akiingoza toka mwaka 1995-2005.

Ushahidi huo wa rais Mkapa ambao Tanzania Daima inayo nakala yake, umeorodhesha maelezo yake yaliyoainishwa katika vipengele 13.

Mkapa katika utetezi wake huo anadai kuwa mchakato mzima wa ununuzi wa jengo hilo la ubalozi lililoko katika mtaa wa Vialle Cortina d’Ampezzo 185 mjini Rome ulizingatia sera ya serikali ya upatikanaji au ujenzi wa majengo ya kudumu ya ofisi na makazi na kwamba ulizingatia maslahi ya taifa.

Hati hiyo ya kiapo ambayo tayari wakili Marando amesema ameishaiwasilisha pia Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) Eliezer Feleshi, inaanza kwa kusema, “Mimi Benjamin Mkapa, mtu mzima, Mkristo, mkazi wa Dar es Salaam, ninaapa kama ifuatavyo, ’nilikuwa Rais mtendaji wa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa vipindi viliwili mwaka 1995-2005 na nina uhakika wa yote haya nitakayosema ndani ya kiapo hiki.’

Katika kiapo hicho Mkapa anadai pia kuwa alifahamishwa na watendaji wa serikali aliyokuwa akiingoza jinsi mchakato uliofanyika na ripoti za uthamini wa serikali zilizotumika katika kufikia hatua ya kununua jengo hilo la ubalozi.

Anadai kuwa tathmini ya jengo hilo ambalo Mahalu anadaiwa kufanya udanganyifu na wizi kwa kulipa fedha kinyume na ilivyotajwa katika mkataba ambayo ilifanywa na serikali ya awamu ya tatu kupitia wizara mbili tofauti, Wizara ya Ujenzi na Wizara ya Ardhi na Maendeleo Mijini.

Anaendelea kudai kuwa, anatambua kuwa ripoti ya serikali ya uthamini wa jengo hilo iliandaliwa na Wizara ya Ujenzi kwa kiwango cha dola za Marekani milioni tatu na Wizara ya Ardhi kwa thamani ya euro milioni 5.5.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo kupitia mchakato wa ununuzi wa jengo hilo ulikuwa wa aina mbili, mmoja ni rasmi na mwingine wa kibiashara na kuongeza kuwa kwa mujibu wa taratibu ya serikali ya Italia na kuwa hilo lilifanyika kwa baraka za serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

“Utaratibu kama huo wa mikataba miwili ushawahi kufanywa na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pale ambapo ilionekana haja kwa kuzingatia maslahi ya taifa kwanza....na kuwa ni mimi ndiye niliyezindua jengo hilo la ubalozi Februari 23 mwaka 2003,” anadai Mkapa.

Shahidi huyo wa Mahalu anadai pia kuwa kwa mujibu wa kiapo chake anakumbuka vyema taarifa ya serikali iliyotolewa bungeni Agosti 3 mwaka 2004 iliyosema na kuthibitisha kuwa taratibu zote zinazohusiana na manunuzi ya jengo kwa mujibu wa maelekezo ya serikali, zilifuatwa na kwamba muuzaji wa jengo hiilo alilipwa fedha zote.

Kumbukumbu ambazo gazeti hili linazo zinaonyesha kwamba, Agosti 3, 2004, Kikwete alitoa maelezo bungeni kuhusu utata uliokuwapo awali kuhusu ununuzi wa jengo hilo la ubalozi.

Kikwete katika maelezo yake hayo ambayo yako pia katika kumbukumbu rasmi za Bunge (Hansard) anaeleza, “Mheshimiwa Naibu Spika mwaka 2001/02 wizara ilinunua jengo la ubalozi counsel katika ubalozi wa Rome katika jitihada za kuondokana na tatizo la kupanga majumba ya watu huko nje na pia kupunguza gharama za kuendelea kulipa pango la nyumba kila mwaka.

“Ununuzi wa jengo hili ulifuata taratibu zote za manunuzi ya majengo ya serikali kwa kuzishirikisha wizara za ujenzi, ardhi na maendeleo ya makazi pamoja na Wizara ya Fedha.

“...Jengo lilifanyiwa tathmini na wataalamu wetu na kukubaliana na ununuzi wa Euro 3,098,781.40 tarehe 6 Machi 2002 fedha za awamu ya kwanza katika ubalozi wa Rome zilipelekwa nazo zilikuwa shilingi 700,000,000 tarehe 28 Juni 2002 zilipelekwa shilingi 120, 000,000.

“Mwishoni mwa tarehe 26 Agosti mwaka 2002 zilipelekwa shilingi 1,000,000,000 jumla ya fedha zilizokuwa zimepelekwa zikafikia shilingi 2,900,000,000 na baada ya hapo ubalozi wetu ulitekeleza taratibu zote za ununuzi wa jengo na kumlipa mwenye nyuma kiasi hicho cha fedha,” alieleza Kikwete.

Akimwelezea Mahalu katika utetezi wake, Mkapa alidai katika kipindi chote alichokuwa rais wa nchi alifanya kazi na mshtakiwa huyo katika nyadhifa mbalimbali za utumishi wa umma na kwamba mshtakiwa huyo ni mtu wa tabia njema, mkweli, mwaminifu na mchapaji kazi.

Mkapa anahitimisha utetezi wake kwa kueleza kuwa, kutokana na mwenendo huo wa kutukuka, Rais wa Italia alimpatia moja ya tuzo za heshima yenye hadhi ya juu kabisa ya taifa hilo Profesa Mahalu, muda mrefu baada ya balozi huyo kuwa ameshaondoka nchini humo.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kuwasilisha mahakamani ushahidi huo wa Mkapa jana, wakili Marando alisema mteja wake anakusudia kupeleka jumla ya mashahidi 10.

Mashahidi hao ni mteja wake (Mahalu), Mkapa, Rais Jakaya Kikwete, kwani wakati akinunua jengo hilo ndiye alikuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ambaye ndiye alimpa mteja wake nguvu ya kisheria ya kuendelea na ununuzi wa jengo hilo, aliyekuwa waziri wa Ujenzi wa John Magufuli na mashahidi wengine na aliyekuwa Waziri wa Fedha, Basil Mramba ambaye pia anakabiliwa na kesi ya matumizi mabaya ya ofisi ya umma na kuisababishia serikali hasara ya sh bil. 11.7.

Kuwasilishwa kwa hati ya kiapo cha Mkapa mahakamani hapo, kumekuja baada ya Hakimu Mkuu Mfawidhi Ilvin Mugeta kusema kuwa yeye ndiye amejipangia kusikiliza utetezi wa washtakiwa hao Aprili 28 mwaka huu.

Hatua ya Hakimu Mugeta kusikiliza utetezi huo inakuja baada ya Machi 28 mwaka huu, Jaji Sivangilwa Mwangesi ambaye ndiye aliyekuwa akisikiliza kesi hiyo tangu awali kujitoa baada ya mawakili wa washtakiwa kuwasilisha sababu sita za kumwomba ajitoe kwa sababu kukosa imani naye Machi 25 mwaka huu.

Mapema mwaka 2007, Jamhuri kupitia mawakili wake toka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Ben Lincoln na Ponsian Lukosi iliwafikisha mahakamani hapo kwa mara ya kwanza washtakiwa hao kwa makosa ya uhujumu uchumi, wizi wa zaidi ya euro milioni mbili wakati wakisimamia ununuzi wa jengo la ubalozi mjini Rome nchini Italia.

CHANZO: Tanzania Daima











CHANZO: Jamii Forums

5 May 2011


Makala yangu katika toleo la wiki hii la jarida maridhawa la Raia Mwema inafanya uchambuzi linganifu kuhusu,kwa upande mmoja,tuhuma zilizomwandama Rais Obama kuwa sio raia wa Marekani,na hatimaye uamuzi wake kutoa cheti chake cha kuzaliwa,na kwa upande mwingine ni tuhuma za ufisadi zinazomwandama Rais Kikwete,na jinsi kutochukua hatua kadhaa kunazifanya tuhuma hizo kuwa na uzito.

Kadhalika,makala hiyo inawagusa jamaa zangu wa Usalama wa Taifa,kwa kuangalia wnavyofanikisha upatikanaji wa taarifa zinazowahusu wanasiasa wa CCM wanaotajwa kama magamba.Lakini ninaibua maswali kadhaa huku nikiwatahadharisha kuhusu uwezekano wa kuzua skandali kama ile ya Watergate ya nchini Marekani ambapo Rais Nixon,pamoja na mambo mengine alitumia nafasi yake kuamrisha ukusanyaji wa taarifa za kiintelijensia dhidi ya wapinzani wake wa kisiasa.

Pamoja na makala hiyo unayowaza kuisoma kwa KUBONYEZA HAPA,jarida hili la Raia Mwema limesheheni habari na chambuzi za kiwango cha juu kabisa. 


4 May 2011






When Osama bin Laden was killed earlier this week,US officials said DNA testing and facial recognition software proved they had got their man.

However, the lack of actual documentation released to the public (so far), and the fact he was buried at sea so quickly, has predictably seen an explosion of conspiracy theories dreamt up by doubters, or ‘deathers’ – as they’ve have now been dubbed. Here are just a few of them.



SOURCE: Yahoo! News

Osama bin Laden conspiracy theories


1. He must be still alive because there’s no proof

The lack of photos, videos and other evidence, plus inconsistencies in accounts of the raid that killed him, apparently shows the US government made the whole thing up.

Taliban spokesman Zabiullah Mujahid is one doubter. He released a statement to journalists saying: “This news is only coming from one side, from Obama’s office, and America has not shown any evidence or proof to support this claim.” Iranian State television also declared: "the mystery [of his death] has increased”.

Anti-war activist Cindy Sheehan, whose son was killed in the Iraq war, also disputed the news on Facebook. She said: "I am sorry, but if you believe the newest death of OBL, you're stupid. Just think to yourself - they paraded Saddam's dead sons around to prove they were dead - why do you suppose they hastily buried this version of OBL at sea? This lying, murderous Empire can only exist with your brainwashed consent - just put your flags away and THINK!"

Naturally, several other Facebook pages made by skeptics have been set up, while searches for "osama bin laden not dead," "osama bin laden still alive" and "bin laden not dead" on Yahoo! spiked off the charts on Monday.

Our figures show most of the searchers of "bin laden conspiracy" were from the US states of Oregon, Wisconsin, North Carolina, Indiana and New Jersey.

2. He’s already dead

Ever since the September 11 attacks there have been numerous reports of bin Laden’s death. Back in 2001 Fox News reported he’d died of lung complications in Tora Bora. In 2005 Senator Harry Reid suggested bin Laden was killed in the Pakistan earthquake, while in 2007 Benazir Bhutto said the al-Qaeda boss was murdered by Pakistani militant Omar Sheikh.

Conspiracy theorists reckon official news of his death was kept from the public to continue justifying the war on terror, with the US government periodically releasing fake videos of the terror leader to keep the world convinced. The theory is that because the powers that be didn’t need bin Laden as a terrorist ‘boogieman’ anymore, they finally announced his death.

3. He was taken alive

Controversial Fox News talk show host Glenn Beck is famous for his conspiracy theories and gave a couple of suggestions about bin Laden’s death on his radio show. Firstly, he speculated that Obama ‘ghosted out’ the al-Qaeda leader - which means the Navy SEALs made it look like he was killed when actually he was taken alive, presumably to be interrogated.

4. He knew about a nuclear bomb

Beck’s other theory was that bin Laden was captured to stop him revealing the location of al-Qaeda’s nuclear bomb. This is reference to WikiLeaks documents that show US security officials briefed other countries on the possibility the terror group had a dirty bomb. Beck didn’t explain why the US government would do this.

5. He’s been ‘on ice’ for years

Another controversial US radio host Alex Jones said the US concocted the story to justify a security crackdown. He reckons bin Laden was killed back in 2002 and his body has been “literally frozen” to be rolled out at a later date.

6. He was given up by Pakistan

Website Maggie’s Farm quotes ‘speculation’ (though they don’t name sources) that, contrary to the reports the US acted alone, Pakistan actually knew all all about Osama’s location and offered up the al-Qaeda leader as a “sweetener” to speed US withdrawal from Afghanistan.

7. He was killed as a pretext for war in Pakistan

David Icke doesn’t agree though. No round-up of conspiracy theories would be complete without a contribution from Icke, who has written extensively about the event on his website. One of his theories is that the killing was fabricated to give the US a reason to actually invade Pakistan because they were harbouring the terror chief. War with China, he suggests, then Russia, will follow. Let’s hope he’s wrong.

8. He was killed to revive Obama’s poll ratings

Barack Obama’s presidency has been a difficult one. Universal healthcare, the budget deficit, high unemployment and fuel costs have resulted in low poll ratings and defeat for the Democrats at last year’s mid-terms, when the Republicans took the House of Representatives.

What better way then, some bloggers have argued, to get those poll ratings up than by suddenly killing America’s most wanted man? Writing on a Tea Party website, one conspiracy theorist said: "Don't you think Obama needs something to assure his re-election?"

9. He was killed to trump Trump

There’s no love lost between Donald Trump and Obama, with the property tycoon reviving the issue of the president’s birth certificate last week. Obama responded by first mocking Trump at the White House correspondents’ annual dinner. Then, when the time came for the bin Laden announcement, ‘Celebrity Apprentice’ had to be interrupted on NBC. The host? Donald Trump.

10. His killing was delayed for the Royal Wedding

The close proximity of the Royal Wedding and the death of bin Laden inevitably means some conspiracy theorists have linked the two events.

Firstly, a security expert told The Daily Express that the reason Wills and Kate postponed their honeymoon - possibly to Jordan – was because they had a tip-off on Friday about the upcoming events in Pakistan.

There’s also been speculation that the White House, who could have killed bin Laden on Friday, delayed pulling the trigger for two days in order for the two events not to clash.

11. His date of death is spooky

Osama bin Laden’s death was announced exactly eight years after George W Bush made his now infamous ‘Mission Accomplished’ announcement. Even spookier, it happened 66 years and 6 hours after the world learned about the death of Hitler. That’s 666.


CCM yamvua gamba Azzan
Wednesday, 04 May 2011 19:34 newsroom

NA SELINA WILSON

KAMATI ya Siasa ya CCM Mkoa wa Dar es Salaam, imemfungia kwa miezi 18 Mbunge wa Kinondoni Idd Azzan, kutogombea nafasi yoyote ndani ya Chama. Pia, imempa onyo kali kwa kosa la kutumia vibaya madaraka yake na kuzichafua mamlaka za CCM Mkoa. Adhabu hiyo imekuja kufuatia Azzan kuwatuhumu wajumbe wa Kamati ya Siasa na Sekretarieti ya Mkoa kuwa ni mafisadi na wala rushwa, hivyo kutaka wajivue gamba. Kwa mujibu wa taarifa, adhabu hiyo imetolewa kwa kujibu Kanuni za Uongozi na Maadili toleo la Februari, Ibara ya 8 (iii).

Katibu wa Itikadi na Uenezi ya CCM Mkoa Dar es Salaam, Juma Simba, alisema jana kuwa uamuzi huo ulitolewa jana baada ya kupokea taarifa ya kamati ya maadili na kuijadili. “Kamati ya Siasa imeona shutuma nzito kama vile ufisadi, rushwa na kushindwa kutekeleza wajibu kwenye vyombo vya habari kwa mamlaka za vikao, Sekretarieti na Kamati ya Siasa ni kukipaka matope Chama, hivyo imetoa adhabu ya karipio,” alisema. Hata hivyo, alisema kuwa baada ya Kamati ya Siasa kujadili tuhuma hizo, ilimpa nafasi Azzan kujitetea kwa mujibu wa Katiba ya CCM, Ibara ya 14 (4), ambapo ilionekana kuwa amefanya makosa kwa makusudi kuzichafua mamlaka za Chama. Azzan alidaiwa kutoa maneno hayo, ambayo yaliripotiwa kwenye vyombo mbalimbali vya habari matoleo ya Aprili 13, mwaka huu.

Simba alisema kuwa baada ya kuchapishwa kwa taarifa hizo, Chama kilimuandikia barua Azzan kikimtaka kufuata taratibu kwa kuwasilisha malalamiko yake badala ya kutumia vyombo vya habari. Hata hivyo, Simba aliongeza adhabu hiyo haina lengo la kumfunga mdomo Azzan wala kumsafisha kiongozi yeyote wa CCM Mkoa, na kwamba anapaswa kuwasilisha tuhuma zake kwa kufuata utaratibu. Hivi karibuni Azzan alikaririwa na vyombo vya habari akiipa siku 30 Kamati ya Siasa na Sekretarieti ya CCM Mkoa, kujivua gamba kutokana na kukithiri kwa rushwa na ufisadi.

CHANZO: Uhuru

Osama (kushoto) na Zawahiri
Ayman al-Zawahiri,daktari mwenye umri wa miaka 59 aliyezaliwa Misri,anatarajia kuwa kiongozi wa kundi la kigaidi la Al-Qaeda baada ya kuuawa kwa Osama Bin Laden.

Gazeti la Wall Street Journal la Marekani linamwelezea Zawahiri kuwa ni mwenye msimamo mkali kuliko Osama,japo ana mapungufu wa mvuto (charisma) na utajiri wa Osama.

Taarifa za kwenye kompyuta Zililopatikana katika eneo alilokuwa akiishi Osama,kama zinavyoelezwa HAPA na mtandao wa Politico,zinaweza kuwasaidia mashushushu wa Marekani kufahamu mengi zaidi kuhusu Al-Qaeda na kupelekea uwezekano wa kufahamu alipo Zawahiri.Hadi itapokuwa hivyo,gaidi huyo aliyekuwa namba 2 (Osama akiwa namba 1) katika kundi la Al-Qaeda anaendela kubaki kwenye orodha ya Shirika la Upelelezi la Marekani (FBI) ya watu wanaosakwa kwa udi na uvumba,na tishio kubwa.

Shirika la Ujasusi la Marekani (CIA) limeshawahi kukaribia kumkamata Zawahiri.Huku akiwa mafichoni,gaidi huyo alitoa mkanda wa video kuhusu vuguvugu la mageuzi nchini Misri mwanzoni mwaka huu,akisema demokrasia inawezekana tu katika ukafiri.Pia alimtukana Rais Obama akitumia neno la ki-baguzi wa rangi (racial epithet).


CHANZO: Huffington Post

3 May 2011


Sakata linalomhusu Ridhiwani Kikwete,mtoto wa Rais Jakaya Kikwete-kwa upande mmoja,na Katibu Mkuu wa Chadema Dkt Willibroad Slaa na Mwenyekiti wa chama cha DP,Mchungaji Christopher Mtikila-kwa upande mwingine,linaanza kupamba moto baada ya wanasiasa hao kumjibu Ridhiwani.Kimbembe hicho kilianza kwa kauli zilizotolewa na Dkt Slaa na Mtikila ambao katika nyakati tofauti walimtuhumu Ridhiwani kuwa bilionea aliyepata fedha isivyo kihalali akitumia mgongo wa baba yake,Rais Kikwete.

Tuhuma hizo zilipelekea Ridhiwani kuitisha mkutano na waandishi wa habari ambapo licha ya kukanusha kuwa sio bilionea-na kudai kuwa magari ya kifahari anayoonekana akiendesha mara kwa mara ni ya kuazima kutoka kwa marafiki zake-alitoa siku saba kwa Dkt Slaa na Mtikila kuthibitisha madai yake vinginevyo atawafikisha mahakamani.

Sasa,kama habari ifuatayo inavyoonyesha,wanasiasa hao wamemtaka Ridhiwani awahi kwenda huko mahakamani,na wao watatumia fursa hiyo kuthibtisha madai yao.Nisikumalizie uhondo,soma mwenyewe hapa chini

Slaa, Mtikila wamtega mtoto JK

Tuesday, 03 May 2011 21:50
Leon Bahati na Raymond Kaminyoge

KATIBU Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa, amemtega mtoto wa Rais Jakaya Kikwete, Ridhiwani, akisema akifanikiwa kukifikisha chama hicho mahakamani atakuwa amefanikiwa kula mfupa ambao uliwashinda vigogo waliowatangazwa hadharani kuwa ni mafisadi nchini.

Dk Slaa alitoa kauli hiyo jana alipotakiwa kutoa msimamo wake kuhusu kauli ya Ridhiwani aliyoitaoa Dar es Salaam juzi, kuwa atamfikisha mahakamani ili kuthibitisha kauli yake kwamba mtoto huyo wa rais ni bilionea aliyepata utajiri wa kutisha kipindi kifupi.

Ridhiwani alimpa siku saba Dk Slaa, kuanzia jana awe amekanusha kauli hiyo ya kumtuhumu kuwa fisadi, vinginevyo atamfikisha mahakamani.
"Sisi tunasema atangulie huko mahakamani sisi tutakuja nyuma," alisema Dk Slaa.

Dk Slaa ambaye katika uchaguzi uliopita aligombea urais na kutoa upinzani mkubwa kwa Rais Kikwete aliyetangazwa kuwa mshindi, alisema kauli za kushtakiwa wanapotangaza taarifa za ufisadi hadharani zimekuwa za kawaida.

Alisema wengi waliwahi kutoa kauli kama hiyo kupitia vyombo vya habari baada ya kuwatuhumu hadharani kuwa ni mafisadi, lakini wakashindwa kwenda mahakamani.

"Chadema tuna uzoefu tulipotaja orodha ya mafisadi walitutishia kuwa watatushtaki mahakamani tukawaambia watangulie sisi tutakuja nyuma, lakini walishindwa kutekeleza ahadi yao," alisema Dk Slaa na kuongeza kuwa, iwapo Ridhiwani atafanya hivyo atakuwa amevunja rekodi ambayo imewashinda watu wazito.

Katibu huyo ambaye umaarufu wake ulikuja kwa kasi kipindi cha miaka 15 aliyokuwa Mbunge wa Karatu, Arusha, alijigamba kuwa hawazungumzi jambo bila vielelezo ndio maana wanajiamini kwa kila wanachokisema hadharani.

Dk Slaa alitupia lawama Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), kwamba amekuwa akisisitiza ifutwe kwa sababu inashindwa kufanya kazi yake, ikiwamo kufanya uchunguzi kwa watu wanaotuhumiwa kupata utajiri katika mazingira yenye utata.

Katika mkutano na waandishi wa habari, Ridhiwani alikanusha kuwa kijana bilionea kama Dk Slaa anavyomtuhumu.Alisema anamiliki shamba mkoani Pwani, lenye ukubwa wa ekari 1.5, gari ndogo na akaunti kwenye benki ya CRDB, NBC na Stanbic, ambazo hakutaja kiasi cha fedha.

Dk Slaa alipinga vikali kauli hiyo na kwamba, alimaliza shule miaka michache iliyopita, lakini sasa ni bilionea na utajiri huo aliupata kwenye mazingira ya utata.

Wakati huohuo, Mwenyekiti wa DP, Mchungaji Christopher Mtikila, alisema atatoa uthibitisho mahakamani kuhusu mali alizozitaja kuwa zinamilikiwa na Ridhiwani.“Siwezi kumuomba radhi mtu, nina uhakika wa kuwa kijana yule anamiliki mali ambazo hajazipata kwa njia halali, itakuwa vizuri ikiwa atanipeleka mahakamani, kwani huko ndiko nitakakoonyesha uthibitisho wangu,” alisema Mchungaji Mtikila.

Jumamosi iliyopita, Mtikila alikaririwa na vyombo vya habari akisema, Ridhiwani ni bilionea anayemiliki nyumba za ghorofa, malori, kampuni za ujenzi wa barabara na ardhi.
CHANZO: Mwananchi

Uzuri wa sakata hili upo katika pembe nyingi.Kwanza,Ridhiwani ni mwanasheria kitaaluma,kwahiyo yayumkinika kuamini kuwa tishio lake (la kuwapeleka Dkt Slaa na Mtikila mahakamani iwapo watashindwa kuthibitisha tuhuma dhidi yake) lilikuwa sio danganya toto.Pili,Ridhiwani ni mtoto wa Rais Kikwete,na kwa vile tuhuma hizo zinamhusisha pia baba yake (kwa maana ya kutumia fursa ya urais kumnufaisha mwanaye) inatarajiwa kuwa suala hapa sio kujisafisha yeye tu bali pia baba yake.

Lakini kwa upande wa pili ni wasifu wa Dkt Slaa,na pengine Mtikila.Wengi tunafahamu kuwa Mtikila na mahakama ni kama mtu na nyumbani kwake.Japokuwa siku za karibuni amekuwa na msimamo unaoyumba lakini bado anatambulika kuwa anapoamua kupigania haki basi atakwenda umbali wowote ule pasipo kuchelea madhara ya kufanya hivyo.

Kwa Dokta Slaa,wengi tunamfahamu kama mmoja wa wanasiasa adimu kabisa ambao ni nadra kutoma matamshi pasipo kuyafanyia utafiti wa kutosha na kuwa na uthibitisho.Yayumkinika kuamini kuwa Dkt Slaa alikuwa akifahamu vema kuwa kwa vile Ridhiwani ni mwanasheria,na pia asingependa kuona jina lake na la baba yake yanahusishwa na ufisadi hadharani,ni lazima angetishia kwenda mahakamani kama sio kwenda kabisa huko mahakamani kufungua kesi ya madai.Kwa mantiki hiyo,na kwa kurejea historia ya Dkt Slaa,inawezekana kuamini kuwa alikuwa na uhakika na alichosema,sambamba na kuwa na ushahidi mzito kuhusu madai hayo.

Enewei,siku saba si nyingi.Leo ni siku ya pili,tumebakiwa na siku tano.Tusubiri kusikia kauli kutoka kwa Ridhiwani Jumatatu ijayo ambapo siku saba alizotoa zitakuwa zimekwisha muda wake.

Ngoma inogire!


The United States Naval Special Warfare Development Group (NSWDG), commonly known as DEVGRU and informally by its former name SEAL Team Six (ST6), is one of the United States' two secretive Tier One counter-terrorism and Special Mission Units (SMUs); the other such group is 1st SFOD-D (Delta Force).

The vast majority of information surrounding DEVGRU is highly classified and details of its activities are not commented on by either the White House or the Department of Defense. While DEVGRU is administratively supported by the Naval Special Warfare Command like the other SEAL Teams, it is operationally commanded by the Joint Special Operations Command.

History

The origins of ST6 can be traced to the aftermath of Operation Eagle Claw, the failed 1980 attempt to rescue American hostages at the U.S. Embassy in Iran.During the Iran Hostage Crisis in 1979, Richard Marcinko was one of two Navy representatives for a Joint Chiefs of Staff task force known as the TAT (Terrorist Action Team). The purpose of the TAT was to develop a plan to free the American hostages held in Iran, which culminated in Operation Eagle Claw. In the wake of the operation's disaster at Desert One, the U.S. Navy saw the need for a full-time dedicated Counter-Terrorist Team and tasked Marcinko with its design and development.

Marcinko was the first commanding officer of this new unit that he named SEAL Team Six. At the time, the US Navy had only two SEAL teams. Marcinko purportedly named the unit Team Six in order to confuse the Soviet intelligence as to the number of SEAL Teams in operation. It became officially operational in 1981.The men in the unit were handpicked by Marcinko himself from across the U.S. Navy's Special Operations personnel. SEAL Team Six would be known as the U.S. Navy's premier counter-terrorist unit. It has also been compared to the US Army's Delta Force.Marcinko held the command of SEAL Team Six for three years from 1980–1983 instead of what was typically a two-year command in the Navy at the time.SEAL Team Six was formally created in October 1980, and an intense, progressive work-up training program made the unit mission-ready six months later. Prior to this, the existing SEAL teams had already begun counter-terrorism training, including 12 platoons in SEAL Team One on the West Coast. On the West Coast, elements of the SEAL Team One had taken the issue one step further. They formed a dedicated two-platoon group known as "MOB Six" (Mobility Six) in anticipation of a maritime scenario requiring a counter-terrorism response and had begun training to that end.
Richard Marcinko, founder of SEAL Team Six, and its first C.O.

In 1987, a new unit was formed, given the official title of "Naval Special Warfare Development Group" (abbreviated to NAVSPECWARDEVGRU, or DEVGRU) after SEAL Team Six was dissolved. Reasons for the disbanding are varied.But the name SEAL Team Six is often used in reference to DEVGRU because of their similarities as a maritime counter-terrorism unit.
[edit] Recent renaming

In a recent article, Marc Ambinder wrote that DEVGRU's designation had been changed by the Defense Department to a new name. However, the new name is currently classified. This has also been the case for Delta Force, which was originally designated 1st Special Forces Operational Detachment-Delta, and is now known as Army Compartmented Elements," or "ACE."

Recruitment, selection, and training

In the early stages of creating SEAL Team Six, Marcinko had been given only six months to get ST6 up and running. This meant that there was a timing issue and Marcinko had little time to create a proper selection course, similar to that of Delta Force, and as a result hand-picked the first plankowners of the unit himself after assessing their Navy records and personally interviewing each man. It has been said that Marcinko regretted not having enough time to set up a proper selection process/course. All applicants came from the UDTs and East and West Coast SEAL teams. Marcinko's criteria for recruiting applicants was combat experience due to the fact that he would know they could perform under fire; language skills were vital, as the unit would have a worldwide mandate to be able to communicate with the local population if needed; union skills, in order to be able to blend in as civilians during an operation; and finally SEAL skills. Each member of SEAL Team Six was selected in part because of the different specialty skills each man brought with him to the unit.

The training schedule was intense. The claim had been made by one former Team member that in one year SEAL Team Six fired more rounds of ammunition than the entire U.S. Marine Corps.The emphasis was on shooting skills, range firing, close-quarters battle (CQB), and stress shooting in a variety of conditions.

As with most aspects of the unit being highly classified, information regarding the process of recruitment and selection for the NSWDG ("DEVGRU") is also scarce, but what is speculated and is known is that the selection and training for the unit hasn't changed dramatically since its creation. All applicants come from the "regular" SEAL teams and the Navy's Explosive Ordnance Disposal units, unless applying for support positions (in which there have been open advertisements on the web for support personnel).

It can be inferred from the quality of their pool of applicants that those considered are in peak physical condition, maintain an excellent reputation as an operator within the Naval Special Warfare community, and have done operational deployments with a SEAL Team where an operator will have picked up invaluable experience. As a result, the candidate will usually be in his 30s. As ST6 was recruiting the best and brightest SEALs/UDTs from the regular teams, this created animosity between the unit and the "regular" teams that their best SEALs were being poached for the unit.

Those who pass the stringent recruitment and selection process will be selected to attend a six- to seven-month Operators Training Course. Candidates will join the unit's training wing known as "Green Team." The training course attrition rate is extremely high; at least half the class will fail the course. During one selection course, out of the original 20 candidates, only 12 completed the course. All candidates are watched closely by DEVGRU instructors and evaluated on whether they were suitable to join the individual squadrons.

Like all Special Operations Forces units that have an extremely intensive and high-risk training schedule, serious injuries or death among operators can result. SEAL Team Six/DEVGRU has lost several operators during training, including parachute accidents and close-quarters battle training accidents. It is presumed that the unit's assessment process for potential new recruits is different from what a SEAL operator experienced in his previous career, and much of the training tests the candidate's mental capacity rather than his physical condition, as he will have already completed Basic Underwater Demolitions/SEAL training.

Candidates will be put through a variety of advanced training courses that can include courses led by civilian and/or military instructors. These can include free-climbing, advanced unarmed combat techniques, defensive and offensive driving, advanced diving, and "survival, evasion, resistance, and escape" (SERE) training. All candidates must perform at the top level during selection, and the unit instructors evaluate the candidate during the training process. Any candidate not performing to the highest level will be returned to his previous unit.

Once a candidate has been selected, he will be assigned to one of the Tactical Development and Evaluation Squadrons.

Roles and responsibilities

When SEAL Team Six was first created it was devoted exclusively to counter-terrorism with a worldwide maritime responsibility; its objectives typically included targets such as ships, oil rigs, naval bases, or other civilian or military bases that were accessible from the sea or inland waterways.

SEAL Team Six was originally also tasked with covertly infiltrating international hot spots in order to carry out reconnaissance or security assessments of U.S. military bases and U.S. Embassies.

Although the unit was created as a maritime counter-terrorism unit, it has become a multi-functional Special Operations unit with multiple roles that include high-risk personnel/hostage extractions. Such operations include the failed rescue of Linda Norgrove, the successful rescue of an American businessman, and in 1991 the successful recovery of Haitian President Jean-Bertrand Aristide and his family during a coup that deposed him.

After SEAL Team Six was disbanded and renamed, the official mission of the currently operating NSWDG is to test, evaluate, and develop technology and maritime, ground, and airborne tactics applicable to Naval Special Warfare forces such as Navy SEALs; however, this is presumed this is only a small part of the group's work assignment.

DEVGRU's full mission is classified but is thought to include preemptive, pro-active counterterrorist operations, counter-proliferation (efforts to prevent the spread of both conventional weapons and weapons of mass destruction), as well as assassination or recovery of high-value targets (HVTs) from unfriendly nations.DEVGRU is one of only a handful of U.S. special mission units authorized to use preemptive actions against terrorists and their facilities.

DEVGRU and the Army's Delta Force train together and deploy together on counter-terrorist missions usually as part of a joint special operations task force (JSOTF).

The CIA's highly secretive Special Activities Division (SAD) and more specifically its elite Special Operations Group (SOG) recruits operators from SEAL Team Six. Joint Navy SEALs and CIA operations go back to the famed MACV-SOG group during the Vietnam War. This cooperation still exists today and is seen in the wars in Iraq and Afghanistan.

SOURCE: Wikipedia







A little-known spy agency in Washington helped track the hour-by-hour movements of the al Qaeda courier who inadvertently led a Navy SEALs assault team directly to Osama bin Laden on Sunday, where they killed the terrorist mastermind with two precision shots to the head.

For eight months, after analysts tentatively identified a spacious walled compound near Islamabad, Pakistan, as a possible bin Laden hideout, an array of satellites and unmanned drones kept an unblinking, day-night “staring eye’’ watch, tracking individuals’ movements in and out, and following “individuals of interest’’ as they traveled across the region.

The data was continuously downloaded to an Air Force ground station housed in a nondescript hangar at Langley Air Force Base in Virginia, where teams of analysts pored over the “take’’ and streamed it live to intelligence analysis cells at the CIA, the National Security Agency and the National Counterterrorism Center.

The NCTC, housed in an innocuous office building in Rosslyn, Va., just across the Potomac River from Washington proper, operates far from the spotlight that illuminates even the secretive CIA, but it played a pivotal role in the bin Laden manhunt.

Working with the military’s Joint Special Operations Command Targeting and Analysis Center, located at Langley, and with the National Geospatial-Intelligence Agency up the river in Bethesda, Md., the NCTC analysts helped develop what the military calls a “common operating picture.’’ In layman’s terms, that amounted to a detailed four-dimensional “map’’ of the bin Laden compound and its occupants and their patterns of living and working.

The data enabled JSOC’s commandos to build, in a remote section of the U.S. air base at Bagram, Afghanistan, a full-scale replica of the al Qaeda compound at Abbottabad, an hour’s drive north of Islamabad. In constant rehearsals at the mock-up, they perfected the timing and the tactics used in Sunday’s raid.

NCTC officials declined to comment publicly on the agency’s operations or the work that led to bin Laden’s death on Sunday.

But a senior intelligence official, who briefed reporters anonymously because much of the information is classified, said the breadth and depth of the information was critical. After the compound was initially discovered last summer, he said, officials “developed good information on how life at the compound was carried out.’’

The information was so complete, he added, that “the operators who assaulted the compound felt they had all the intelligence they needed.’’ Such assessments are unusual because the military, and commandos in particular, rarely acknowledge they have “enough’’ intelligence.

In a statement, James R. Clapper, the director of national intelligence who presides over all 16 of the country’s intelligence agencies, said that in his nearly 50-year career “never have I seen a more remarkable example of focused integration, seamless collaboration and sheer professional magnificence’’ as was evident in the final hunt for bin Laden.

As impressive as it is, the elimination of the al Qaeda founder, after nearly a decade of effort, won’t have nearly the impact on global terrorism that it might have several years ago, counterterrorism officials say. Thanks to the “franchising’’ of extremist Islamist terror cells to Yemen, Somalia and elsewhere, the danger -- and the action -- has shifted away from bin Laden’s core al Qaeda group, according to NCTC director Michael Leiter.

None of the recent terrorist operations against the United States, including the 2009 Fort Hood shootings that killed 13 Americans and the drive-by shooting later that year that killed a soldier at a Little Rock, Ark., recruiting station, were directed or inspired by bin Laden. Rather, these two attacks, together with the three failed but potentially deadly attacks -- the attempted Times Square bombing, the bungled Christmas 2009 airliner bombing, and the parcel bombs hidden in printer cartridges last fall -- all were inspired or directed by a the Yemeni-based cleric, Anwar al-Awlaki, and the al Qaeda offshoot, al Qaeda in the Arabian Peninsula, also based in Yemen.

Leiter and other counterterrorism officials say that AQAP and other “franchises’’ have surpassed the original Pakistan-based al Qaeda in terms of speedy planning and imaginative attacks. They cite a further threat: the emergence of homegrown Islamist terrorists in the United States, such as the alleged Little Rock shooter, Abdulhakim Mujahid Muhammad, a 24-year-old Muslim convert formerly known as Carlos Bledsoe.

“Bin Laden personally, al Qaeda’s terrorist tradecraft, all of that is becoming less popular in most places in the world,’’ Leiter said in a December speech at the Center for Strategic and International Studies in Washington.

The affiliates, he added, “no longer simply rely upon their linkages to al Qaeda senior leadership in Pakistan but they have in fact emerged more as self-sustaining, independent movements and organizations.”

Leiter also noted that the affiliates maintain “important tentacles back to al Qaeda senior leadership” but operate with a high degree of independence.

“And, frankly, they operate at a different pace and with a different level of complexity than does al Qaeda senior leadership, and that has complicated our task significantly,’’ Leiter added.

The NCTC’s role in the killing of bin Laden is payback of sorts for the U.S. intelligence community, which was criticized for its failure to prevent the 9/11 attacks -- when a lack of coordination kept intelligence officers from fitting together known pieces of the al Qaeda plot. In the aftermath of the attacks, a presidential commission urgently recommended the establishment of a new agency to unify “strategic intelligence and operational planning against Islamic terrorists.’’

The NCTC was operational by 2004.

This time, by all accounts, the intelligence agencies and the military operational headquarters worked together smoothly and swiftly, justifying the effort put into breaking down institutional walls and separate data bases, said counterterrorism officials who requested anonymity because their operations are classified.

A former Navy pilot who flew EA6B Prowler jamming and attack planes over the Balkans and Iraq, Leiter, 42, is a cum laude graduate of Harvard Law School and clerked for Supreme Court Justice Stephen G. Breyer before starting work in counterterrorism. He was appointed as NCTC director by President George W. Bush -- and asked to stay on by President Barack Obama. He was married Saturday evening in Washington; the honeymoon was postponed.

SOURCE: Huffington Post



Hapana,leo sio April 1-Siku ya Wajinga- bali habari ifuatayo ni ya kweli na wala si kanyaboya flani.Baada ya usanii uliodumu kwa takriban mwezi mzima,hatimaye CCM imerejea kwenye asili yake.Wengine tulishashtukia mapema usanii uliobeba jina la "kujivua magamba".Tangu lini nyoka akageuka mjusi baada ya kujivua magamba?Na tangu lini mchawi akageuka mtu mwema kwa vile tu kavua tunguri?

Enewei,habari kamili ni hii:

CCM yatoa msimamo

*Mukama asema maazimio ya NEC yamepotoshwa
*Ataka chama kiheshimu taratibu, aisulubu Chadema
Na Mwandishi Wetu

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wilson Mukama, amesema Halmashauri Kuu (NEC) ya CCM, haijawahi kutoa maazimio ya kuwataka watuhumiwa wa ufisadi kujiuzulu nyadhifa zao ndani ya siku 90, ila wenye kutoa kauli hizo wanapotosha.

Mukama alikuwa akizungumza na wahariri wa vyombo vya habari vyote nchini, walipokutana jijini Dar es Salaam jana. Alitoa kauli hiyo baada ya kuhojiwa ataje majina ya mafisadi ni akina nani, na kwamba barua wanazosema watapewa zitakabidhiwa lini kwa wanachama hao wa CCM.

Akizungumza kwa tahadhari kubwa, Mukama alisema NEC ilitoa maazimio 26, na kati ya hayo, azimio namba 15 lilikuwa likiwataka watuhumiwa wa ufisadi, “kupima, kutafakari na kuchukua hatua wenyewe,” ila akaongeza kuwa wakati Mwenyekiti, Rais Jakaya Kikwete anafunga kikao cha NEC, alisema watuhumiwa wasipochukua hatua wenyewe chama kitawachukulia hatua.

“Kwa maana hiyo, kuna watu wame-hype information (wamepotosha taarifa kwa propaganda)… sijui hizi siku 90 zimetoka wapi? Kwanza NEC haikutani kila baada ya siku 90. NEC inakutana kila baada ya siku 120, yaani miezi minne au mara tatu kwa mwaka… Mimi nasema maamuzi ya NEC hayakutaja majina ya watu. Kitu hiki hakipo. Mtuache kama Chama tuna taratibu zetu, wala hatuhitaji mashinikizo kutoka popote,” alisema Mukama.

Mukama alisema yeye anaamini katika utaratibu wa kuendesha chama kama taasisi, hivyo kauli za watu zinazotoa siku 90 si za chama, bali chama kinasimamia maamuzi yanayotokana na kumbukumbu rasmi ambazo ni maazimio 26 ya NEC na hotuba rasmi ya Mwenyekiti wao wakati anafunga kikao cha NEC.

Msimamo huu wa Katibu Mkuu Mukama, umekuwa tofauti na kauli zilizotolewa na Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara), Pius Msekwa, Naibu Katibu Mkuu (Bara), John Chiligati na Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, ambao wamekuwa wakitamba kuwa baada ya siku 90 chama kitawafukuza kwenye chama watuhumiwa wa ufisadi ikiwa wao watashindwa kujiondoa sasa.

Hata hivyo, Mukama alisema watu wanaotuhumiwa wanapaswa kufikiri na kuchukua hatua wenyewe wanazoona zinafaa kwa nia ya kujenga chama chao upya. Alisema falsafa ya kujivua gamba imefanyiwa kazi kwa Kamati Kuu na sekretarieti ya chama kujiuzulu, hivyo hakuna sababu ya watu kupotosha falsafa hiyo na kukilazimisha chama kufanya maamuzi ya kujiua.

Wakati huo huo, Mukama alikishambulia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kuwa kitakufa kabla ya CCM, kwani chama hicho kimeanzishwa kwa shinikizo la Shirika la Fedha Ulimwenguni (IMF). “You can quote me on this (nikariri katika hili) Chadema kilianzishwa kwa shinikizo la IMF. Yule aliyetofautiana na Nyerere ndiye aliyekwenda kukianzisha,” alisema Mukama bila kufafanua.

Katika mkutano huo, Mukama aliambatana na Katibu wa Idara ya Siasa na Mambo ya Nje, January Makamba, Katibu wa Fedha na Uchumi, Mwigulu Mchemba na Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye.

Mukama alisema CCM haijapoteza mwelekeo, na itaendelea kujijenga upya kwa nia ya kutumikia vyema wananchi, huku akisisitiza kuwa mabadiliko yaliyofanywa yalikuwa ya lazima kukipa uhai mpya chama hicho.

CHANZO: New Habari

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.