30 Apr 2010

Mtakatifu au mzushi?

Raia mmoja wa India amegusa hisia za jeshi la nchi hiyo kutokana na madai yake kwamba haitaji chakula wala maji kumudu kuishi.Prahlad Jani anadai yeye ni 'breatharia',yaani mtu anayeweza kuishi kwa kutumia nguvu za asili za kiimani.Anadai anapata nguvu hizo za asili kutoka kwa 'mungu wa kike' anayemmwagia kimiminika (elixir)cha miujiza katika paa la chini la mdomo wake (palate),kwa mujibu wa gazeti la Telegraph la London. 


Wakati baadhi ya watu wanamwona kama 'mzushi' flani,taasisi ya maendeleo ya utafiti wa ulinzi inasema Prahlad anaweza kutoa mwangaza katika kuwasaidia wanajeshi kumudu kukaa muda mrefu bila kula,au hata wahanga wa majanga mbalimbali.Hadi sasa amekaa siku sita bila kula au kunywa chochote katika hospitali iliyopo Hyderabad,na madaktari wanasema haonyeshi dalili yoyote ya kuathiriwa na njaa.

"Ikithibitika kuwa madai yakni sahihi,basi itakuwa hatua kubwa sana kwenye sayansi ya tiba",anasema Dkt G.Ilavazhagan,Mkurugenzi wa Taasisi ya Ulinzi ya Fiziolojia na Stadi Shiriki."Itatuwezesha kuokoa maisha ya wanadamu katika nyakati za majanga,kimo cha juu,safari za majini,na mazingira mengine magumu ya kibinadamu na ya asili.Tutaweza kuwaelimisha watu kuhusu namna ya kustahimili (surviving) mazingira magumu pasipo chakula na maji au chochote kile".

Madaktari wataendelea kumchunguza kwa siku 15 kipindi ambacho wanataraji kuona misuli yake ikisinyaa,upungufu mkubwa wa maji mwilini,kupungua uzito wa mwili na baadhi ya viungo vya mwili kushindwa kufanya kazi.

Binadamu wengi hawawezi kustahimili zaidi ya siku 3 hadi 5 pasipo kunywa maji.

Imetafsiriwa kutoka gazeti la Daily News la India.

29 Apr 2010

NEWSWEEK: Black blogs cover a far more diverse range of stories than the rest of the media. Just ask Sandra Bullock. While Sandra Bullock's post-Oscar split from husband Jesse James may be the biggest celebrity news in the last month (or two), it's probably not surprising it's the adopted brown baby that really got the African-American blog sites going. The funny thing is, black Web sites such as MediaTakeOut.com, Bossip, and Young, Black and Fabulous have been following Bullock for years. Part of the reason is her connection to the black community. "They know about her support for victims of Katrina and Haiti so they care about what happens to her, which we thought about when we gave her coverage," says Fred Mwangaguhunga, owner of the black entertainment site MediaTakeOut.com. But part of it is that black blogs look at the world differently than the often segregated mainstream.
. CLICK HERE TO READ THE FULL STORY

The US Army says that it is it is wasting far too much time preparing Powerpoint presentations and not enough time killing people.

For a while now the Army has been concerned that its officers are missing entire wars preparing Powerpoint slides and making presentations.

. TechEye has got its paws on the sort of slide they mean (see above). 

Last summer Gen Stanley McChrystal, the leader of US and Nato forces in Afghanistan, said when we understand that slide that “we’ll have won the war’.

Gen James Mattis of the Marine Corps, said: "Powerpoint makes us stupid". The Marines are not renowned for being that bright in the first place, which makes them some of the US's best soldiers, but Powerpoint sucks about the direction you want to point them.

Sam Nuxoll, a platoon leader in Iraq, seems to have shaken the Pentagon with a quote that said he was spending most of the war making Powerpoint slides. Instead of spending his time dodging bullets, he was making bullet points.

What is the problem is the fact that rather than encouraging making decisions PowerPoint sucks up the time of junior officers. The idea is that they can get crappy decisions blessed if it looks good in Powerpoint. However really good tactics which are dull on screen are being mothballed.

This has been noticed in business too with some companies thinking that Powerpoint presentations are a waste of time too.

.SOURCE: Tech Eye

JIJI la Tanga limfeunikwa na simamzi kuu kufatia wanafunzi 18 wa Chuo cha Kiislamu cha Shamsil-Maariff kufa papo hapo na wengine 125 kujeruhiwa vibaya, baada ya lori walilokuwa wakisafiria kutoka kwenye sherehe za maulidi kupinduka.

. Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Adolphina Kapufi aliliambia gazeti hli jana kuwa ajali hiyo ilitokea saa 5:30 usiku wa kuamkia jana katika eneo la njiapanda kuu ya Mabanda ya Papa jijini hapa.

Kapufi aliwataja baadhi ya waliokufa katika ajali hiyo kuwa ni Twalib Kunemu, Juma Idd, Faraji Habib, Jahshi Rashid, Hussein Bakari, Hajji Athumani naYussuph Hussein na kwamba, kazi ya kuwatambua maiti wengine bado inaendelea.

Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Paschal Kanyinyi alisema kazi ya kuwatambua waliokufa na majeruhi waliolazwa katika hospitali hiyo wodi ya Galanosi inaendelea.

Kanyinyi aliwataja majeruhi waliotambuliwa kuwa ni Jumaa Salim ambaye ameumia mbavu, Makame Ahmed, Ahmed Shehe, Selemani Said na Juma Akida.

Aliwataja majeruhi ambao hali zao ni mbaya, hivyo waliokimbizwa katika Hospitali Taifa ya Muhimbili, jijini Dar essalaam kuwa ni Hemed Shaaban na Hassan Adam.

Kanyinyi alifahamisha kuwa kati majeruhi 125 walifikishwa katika hospitali hiyo usiku wa kuamkia jana baada ya kupata ajali, 70 walipata matibabu na kuruhusiwa kurejea chuoni kwao.

Kwa mujibu wa Kaimu Mganga Mkuu huyo, majeruhi 55 wanaendelea kupata matibabu katika hospitali hiyo kwa msaada wa timu maalumu ya waganga na wauguzi waliokusanywa kutoka hospitali na vituo mbalimbali vya afya mkoani Tanga kwa ajili ya kutoa huduma hiyo.

Mwananchi ilifika katika Hospitali hiyo ya Bombo na kukuta idadi kubwa ya wananchi waliokusanyika katika hospitali hiyo kwa lengo la kutambua miili ya waliokufa na majeruhi.

Mwalimu wa zamu wa Chuo hicho, Ustaadh Ajali Ramadhan, alisema kuwa wanafunzi hao walikuwa wakitokea Kijiji cha Kibafuta ambako walikwenda
kuhudhuria sherehe za kuzaliwa kwa Mtume Mohamad S.A.W.

Hata hivyo, Ustaadhi Ramadhan alisema anashangaa kuona idadi kubwa ya wanafunzi waliopata ajali, kwani aliowaruhusu kutoka chuoni hapo walikuwa 60 tu.

“Nashangaa sijui ni nini kimetokea, kwani niliowaruhusu kuondoka na gari
hilo ni wanachuo 60 tu, lakini idadi ya waliopata ajali imekuwa kubwa. Sijui walipandia wapi…,” alisema mwalimu huyo wa zamu.

Kanyinyi alimshukuru Mkurugenzi wa Kampuni ya Raha Leo, Seleman Abdallah kwa kutoa dawa kwa ajili ya kuwatibu majeruhi wa ajali hiyo.

“Tunashukuru Mkurugenzi wa Raha leo, ametusaidia sana kwa kutoa dawa za
kuwatibu majeruhi na pia vifaa kwa ajili ya kusaidia kuhifadhia miili ya waliokufa,” alisema Kanyinyi.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Meja Jenerali Mstaafu Said Kalembo alifika hospitalini hapo saa 5 .30 asubuhi na kuwapa pole ndugu wa wanafunzi waliokufa katika ajali hiyo.

Akiwa, akiwa katika wodi ya Galanosi Mkuu wa Mkoa huyo alimuagiza Kaimu Mganga Mkuu kuwaita waganga na wauguzi kutoka vituo vyote vya afya vya jijini hapa ili kuongeza nguvu, kwa vile waliopo katika Hospitali ya Bombo walikuwa wmezidiwa na kazi ya kuwahudumia majeruhi.

Katibu wa Bakwata wa Mkoa wa Tanga, Mohamed Riami alisema huo ni msiba
mkubwa uliwakumba Waislamu na Watanzania kwa ujumla, hivyo akaomba msaada wa hali na mali kuokoa maisha ya majeruhi waliopata ajali hiyo.

Ajali hii ni muendelezo wa ajali mbaya za barabarani zinazoendelea kutokea na kuua watu sehemu mbalimbali nchini hivi sasa.

Moja ya ajali hizo mbaya ni iliyotokea jijini Dar es Salaam mwezi uliopita na kuua watu zaidi ya 10 papo hapo baada ya lori la mafuta ya taa kuigonga na kulalia daladala maneo ya Kibamba katika Barabara ya Morogoro.

Katika ajali hiyo iliyotokea alfajiri, daladala ilisagawa na kuwa kama chapati; na miongoni mwa waliokufa ni mama mjazito aliyekuwa anakwenda kujifungua hospitalini akiwa pamoja na mumewe.

CHANZO: Mwananchi
.

British National Party (BNP),chama cha kibaguzi cha hapa Uingereza,kimetangaza kwamba kitatoa paundi 50,000 kwa kila atakayeafiki kuhama Uingereza.Akiongea katika kipindi cha 'Today' cha kituo cha redio cha BBC4,mwenyekiti wa chama hicho,Nick Griffin (pichani) alisema kuwa mpango huo ni mahsusi kwa Waingereza wasio Weupe (non-White British) na wahamiaji wengine wasio weupe (non-White migrants).

Griffin alieleza kuwa kwa mujibu wa sera ya uhamiaji ya chama chake 'milango ya Uingereza itafungwa' kwa wageni isipokuwa tu kwa wale wenye ujuzi au taaluma maalum."Aidha unazungumzia fundi bomba wa ki-Polish au mkimbizi kutoka Afghanistan,milango ya Uingereza itafungwa kwa sababu nchi hii imejaa",aliongeza kiongozi huyo mbaguzi wa rangi.

Kiongozi huyo wa BNP alitanabaisha kuwa "Idadi ya watakaozuiwa kuingia nchi hii itakuwa yoyote na kutoka popote.Milango itafunguliwa tu pale itapokidhi mahitaji wa Waingereza na Uingereza".Akitolea mfano wa utekelezaji wa sera hiyo,Griffin alisema laiti Uingereza ikiwa na mahitaji ya wataalam wa nyukia basi chama hicho kitaruhusu,kwa mfano,mwanafikizia kutoka Japan.

Alipoulizwa kama sera hiyo itaambatana na kuvunja mikataba ya kimataifa,mbaguzi huyo alijibu: "Kabisa.Mikataba ya kimataifa haikidhi mahitaji ya Uingereza na watu wake.U-kimataifa (internationalism) ni miradi ya tabaka la wanasiasa".

Kuhusu kuwataka wasio weupe kuondoka Uingereza,Griffin alisema:"Tunasema tutatoa posho ya kuhama makazi (resettlement grants) na hili ni suala la hiari .Tunazungumzia takriban pauni 50,000 kwa kwa mtu".Alipoulizwa ni watu wangapi wanaotarajiwa kuhama Uingereza kwa mujibu wa sera hiyo alisema: "180,000 kwa mwaka,kama wataondoka katika nchi hii iliyojaa kupindukia".

Imetafsiriwa kutoka Yahoo! News


Judges are set to rule whether to remove the story of the intrepid explorer's first African adventure after a Congolese man claimed it is racist.

. Bienvenu Mbutu Mondondo wants Tintin in the Congo - the second in the celebrated children's series - to be axed for its ignorant depiction of native Africans.


Creator Hergé defended his book, first published in 1930, in later life and said any stereotypes merely reflected contemporary colonialist views.

The Belgian courts may follow a recent compromise decision in Britain and place a sticker warning of offensive content instead.

That was the result when the UK's Commission for Racial Equality called for the comic to be banned in 2007.

Mr Mondondo has put his case to Belgian and French judges before, but his latest legal challenge faces some scepticism.

Online comic magazine actubd.com accused him of lying about his profession, amid other doubts that he will be unable to pay his own lawyers.

SOURCE: Skynews

28 Apr 2010

China has revoked a ban on people with HIV/AIDS entering the country, softening a decades-old policy that drew sharp criticism this year when an Australian writer was blocked after declaring himself HIV-positive. Until now, China's regulations formally banned foreigners entering the country with "psychiatric illness, leprosy, AIDS, sexually-transmitted diseases, active pulmonary tuberculosis or other infectious diseases."


The State Council, China's cabinet, issued amended rules late Tuesday removing the explicit ban on people who have developed AIDS or are infected with the HIV retrovirus, as well as anyone with leprosy, while leaving authorities leeway to decide which diseases could trigger an entry ban.

The United Nations welcomed the decision as an important step towards ending discrimination against people living with HIV.

"I commend President Hu Jintao for China's decision to remove travel restrictions based on HIV status," U.N. Secretary-General Ban Ki-moon said in a statement.

"Punitive policies and practices only hamper the global AIDS response. I urge all other countries with such restrictions to remove them as a matter of priority and urgency."

Travel restrictions, which are imposed in some form by dozens of countries worldwide, do not prevent transmission of the disease or protect public health, the statement added.

China's new rules, posted on the central government website (www.gov.cn), still block foreigners "with serious psychiatric illness, infectious pulmonary tuberculosis or other infectious diseases that may constitute a major threat to public health."

The amended regulations did not say whether AIDS/HIV would be among the infectious diseases that people seeking Chinese visas must declare when applying, possibly leaving officials some leeway on how to apply the rule.

But an unnamed legal affairs official for the State Council indicated that AIDS/HIV would not be a bar to entry.

"Restricting foreigners with these diseases from entering the country has played an extremely limited role in our country's disease prevention and control work, and instead has repeatedly become an impediment to our hosting a variety of international events," the official told the Legal Daily.

In March, more than 90 Australian authors signed a letter decrying China's refusal to grant a visa to one of the country's most celebrated writers, Robert Dessaix, who is HIV-positive.

Friday, Shanghai opens its World Expo, a multi-billion dollar exhibition that is China's latest effort to promote an image as a forward-looking and open country.

The HIV virus can be spread through unprotected sex, sharing of infected needles and blood, and -- without preventive drugs -- to children in the womb of infected mothers or who take milk from an infected woman.

If untreated, the virus attacks the immune system, leading to full-blown AIDS, a deadly condition.

China has 560,000 to 920,000 people infected with the HIV virus and 97,000 to 112,000 AIDS patients, according to 2009 Ministry of Health and United Nations estimates.

SOURCE: Reuters

.

Matokeo ya utafiti uliofanywa na Mradi wa Utafiti na Elimu na Demokrasia Tanzania (REDET) yanaonyesha kuwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda ni mchapakazi zaidi ya 'bosi' zake,Rais Jakaya Kikwete na Makamu wa Rais Dkt Ali Mohammed Shein. Kwa mujibu wa habari zilizochapishwa katika gazeti la Mwananchi,asilimia 61.2 ya wananchi waliohojiwa wameonyesha kuridhishwa na utendaji wa Pinda huku Kikwete akipata asilimia 58.8 na Dkt Shein akiwa na asilimia 46.8Kwa habari kamili soma HAPA.

27 Apr 2010

Tarehe 6 ya mwezi ujao,Waingereza watapiga kura katika Uchaguzi Mkuu.Kura za maoni zinaonyesha kuwa hakuna chama kitakachopata ushindi wa kutosha kuunda serikali peke yake (hung parliament).Vyovyote itakavyokuwa,kuna mambo kadhaa mbayo Watanzania wanaweza kujifunza katika uchaguzi huu hasa kwa vile nasi tutakuwa na uchaguzi hapo Oktoba mwaka huu. 


Kubwa zaidi ni namna wagombea wanavyohangaika kuwabembeleza wapiga kura.Unajua kuna kijitabia cha baadhi ya wanasiasa huko nyumbani ambao sijui ni ulevi wa madaraka au dharau kwa wapiga kura,hawajihangaishi hata kidogo kuwaonyesha wapiga kura kuwa ajira zao zinategemea ridhaa za wapiga kura hao.Pengine ni jeuri ya uwezo wao wa kununua kura katika jina la takrima au kudumisha chama.

Yani hapa ukiangalia kwenye runinga namna Waziri Mkuu wa sasa,Gordon Brown,anavyopelekeshwa na wapiga kura kwa maswali mazito kana kwamba utawala wake ulikuwa mbovu kupindukia,unapata picha kuwa kwa hawa wenzetu GOOD IS NOT ENOUGH,THEY WANT EVEN BETTER (Ubora tu hautoshi,wanataka ubora zaidi).Na si kwamba Brown na Labour yake hawajafanya mambo ya maana kwa Waingereza bali watu hawa hawapendi 'kuangushwa' kwa aina yoyote ile.

Na jingine linalovutia katika kampeni hizi ni namna wapiga kura wanavyozipa manifesto za vyama umuhimu mkubwa na pengine mwelekeo wa nani watampigia kura.Kwetu,manifesto ni sawa na waraka unaokumbukwa wakati wa chaguzi na 'kinga' ya kujitetea pale mambo yanapokwenda mrama.Wengi tunafahamu namna akina Makamba wanavyotumia manifesto ya CCM kujibu shutuma mbalimbali zinazoelekezwa kwa chama hicho tawala.Hilo sio kosa bali tatizo ni kwamba utetezi huo mara nyingi hauendani na hali halisi.Kwa mfano haitoshi kusema manifesto ya CCM inatamka bayana kuhusu 'chuki' yake dhidi ya rushwa huku in practice hadi leo hatufahamu Kagoda ni mdudu gani.Matendo hukidhi haja maridhawa kuliko maneno,so Waswahili say.

Manifesto ya CCM kwenye uchaguzi wa mwaka 2005 iliweka bayana dhamira yake ya kupata ufumbuzi wa suala la mahakama ya kadhi lakini hadi leo suala hilo linapigwa danadana.Utafiti wangu wa shahada ya uzamili kuhusu harakati za vikundi vya waislam nchini Tanzania (unaoelekea ukingoni) ambao umegusia kwa undani suala hilo unaashiria kuwa 'kupuuzia' kero (grievances) kama hiyo ya mahakama ya kadhi na suala la OIC yana potential ya kusababisha matatizo huko mbeleni.Tatizo haliwezi kutatuliwa kwa kuliepuka bali kulikabili.We have to solve difficulties before they become problems (tunapaswa kutatua ugumu kabla haujawa tatizo).

Ni matumaini ya wapiga kura wa Tanzania kuwa watatumia haki zao za kidemokrasia kwa busara zaidi kuchagua wagombea wanaoweza kuwatumikia kwa dhati.Zama za ushabiki wa vyama zimepitwa na wakati hasa kwa vile kitakachowakomboa Watanzania kutoka kwenye lindi la umaskini na ufisadi sio ushabiki bali ufanisi wa chama.

26 Apr 2010

Ujumbe kutoka kwa Executive Producer Baraka Baraka (na video ya interview hapo chini)


Kwa mara nyingine tena ningependa kuwatolea Intavyu siku tuliyotembelea rasmi na world service radio katika studio zetu za Urban Pulse hapa Mjini kusoma UK tukiwa na Presenter Fred Ili kujadili Movie ya £ovely Gamble.




Pia aliweza kukutana na baadhi ya wanatimu wa lovely gamble na pia utapata comments za Steve Kanumba mwenyewe jinsi anaitwa siku hizi.


Pia unaweza kuangalia trailer ya movie inayosubiriwa kwa hamu sana Tanzania 28.4.10 club Billcanaz na hapa mji wa kusoma UK 29.5.10


BARAKA BARAKA
EXECUTIVE PRODUCER
BUZZIE PRODUCTION UK.



Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.