Showing posts with label BONGOFLAVA. Show all posts
Showing posts with label BONGOFLAVA. Show all posts

4 Nov 2013



Makala hii iliandikwa kwa minajili ya kuchapishwa katika jarida la Raia Mwema toleo la Oktoba 23. Hata hivyo haikuchapishwa kwa madai kuwa ilikuwa inapromoti msanii Fid Q na wimbo wake mpya wa Siri ya Mchezo. Whether uamuzi wa jarida hilo ni sahihi au la, nimeonelea ni vema kuichapisha makala hiyo hapa bloguni

MAKALA YA RAIA MWEMA TOLEO LA OKTOBA 23, 2013

Nianze makala hii kwa kuomba radhi kutokana na kuadimika kwangu katika toleo lililopita. Hali hiyo ilitokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo wangu.

Uandishi wa makala zangu umekuwa sehemu muhimu ya maisha yangu, na pindi ikipita wiki pasi kuandika chochote (kama ilivyokuwa wiki iliyopita) huwa najisikia kama nimepungukiwa na kitu flani.

Pamoja na kiu yangu kubwa ya kuhamasisha mijadala mbalimbali, kukemea maovu na hata kuhabarishana tu, moja ya hamasa kubwa zinazonifanya niendelee na jukumu hili ni mapokeo ya wasomaji mbalimbali.

Na wiki iliyopita nilipata hamasa kubwa kutoka kwa msanii maarufu wa muziki wa Bongofleva, Fareed Kubanda, au 'Fid Q' kwa jina la kisanii.
Msanii huyo ametoa kibao chake kipya kinachofahamika kama ‘Siri ya Mchezo’ (unaweza kukisikiliza na kusoma mashairi yake hapa). Kilichonivutia kuhusu wimbo huo ni ujumbe mzito wa kisiasa, ambapo ni kitu adimu kwa wasanii wetu kuzungumzia masuala ya kisiasa kwenye tungo zao.

Niliongea na Fid Q kwa kutumia mtandao wa kijamii wa Twitter, ambapo pamoja na mambo mengine alinieleza kitu kimoja kilichonigusa sana. Namnukuu, “Believe or not, nilijaribu kujivisha viatu vyako wakati ninaandika hii track.”

Ni nani hatofarijika kuambiwa na msanii mwenye jina kubwa kama Fid Q kuwa alipata hamasa kutoka kwao wakati anaandika mashairi ya wimbo ambao kwa hakika utavuma?

Lakini licha ya hamasa, furaha na heshima hiyo kutoka kwa msanii huyo, kuna kitu cha ziada ambacho kimsingi ndicho kinabeba dhima ya makala hii: nafasi ya wasanii wetu katika kuhamasisha mabadiliko chanya kwa jamii.

Kwa muda mrefu wasanii wetu, hususan wa muziki ‘wa kizazi kipya’ (Bongofleva) wamekuwa wakilaumiwa kwa aidha kutumika vibaya na wanasiasa au kutotilia maanani matatizo mbalimbali yanayoikabili Tanzania yetu.

Imezoeleka kwamba ukifika wakati wa uchaguzi ndipo wanasiasa wetu hukumbuka kuwa kuna vijana wanaendesha maisha kwa kujishughulisha na sanaa ya muziki. Kama ilivyo kwa makundi mengine ya jamii, wanasiasa hao pasi haya huwavuta karibu wasanii na kisha kuwatumia kwenye kampeni zao. Wakishapata madaraka, wanawatelekeza kama inavyotokea kwa wengi wa wapigakura majimboni.

Lakini wakati ni rahisi kuwalaumu wasanii kwa kile kinachotafsiriwa na wengi kama ‘kutojali matatizo yanayoikabili Tanzania yetu,’ Fid Q alinieleza kuwa tatizo mojawapo ni ukiritimba wa vyombo vya habari ‘vya asili’ (yaani traditional media, kwa maana ya radio, televisheni na magazeti). Sio siri kwamba wamiliki wa vyombo hivyo huchelea sana kuwaudhi watawala kiasi kwamba si ajabu kwa wimbo unaokemea maovu flani yanayowahusu watawala ukanyimwa fursa radioni au kwenye runinga.

Tukirejea kwenye wimbo huo wa Siri ya Mchezo, yayumkinika kubashiri kuwa Fid Q anafungua mlango wa kile kinachofahamika kimuziki kama ‘political rap’ yaani muziki wa kufokafoka uliobeba ujumbe wa kisiasa. Aina hiyo ya muziki ilikuwa maarufu sana huko Marekani kwenye miaka ya 1970 hadi 1980, ambapo ulilenga kuzungumzia masuala mbalimbali ya kisiasa na kijamii. Kimsingi, muziki huo ulikuwa ni kama nyenzo ya wasanii kupambana na udhalimu, sambamba na kuhamasisha jamii, hususan vijana, kushiriki katika harakati za kujenga jamii bora.

Katika wimbo huo, Fid Q anamkumbuka mmoja wa wasomi lulu kwa taifa letu, marehemu Profesa Chachage Chachage ambaye wakati wa uhai wake alijitahidi sana kutuelimisha kuhusu soko huria na athari zake. Kadhalika, msanii huyo anasononeka kuhusu hatma ya taifa letu akidadisi “tutarithi nini...” katika zama hizi ambapo utajiri wetu unanufaisha wachache (hususan wageni na vibaraka wao) huku mamilioni ya Watanzania wakibaki masikini.

Kadhalika, msanii huyo anawanyooshea kidole wahujumu wa uchumi, kabla ya kutoa angalizo muhimu kuwa “taifa la kondoo huendeshwa na serikali ya dubu/mbwa mwitu wenye siri...

Vilevile, Fid Q anatahadharisha kuhusu siasa inavyotumika kama kitega uchumi, na kusikitishwa na jinsi ukoloni mamboleo ulivyotupatia uhuru wa bendera huku ukituonyesha “kufuru za wenye hela.”

Katika lugha ya kisanii, msanii huyo analalamika kuwa Tanzania imegeuka kama mwanamke asiyefuata maadili, ‘anayetembea’ na kila mtu, mpaka wanamwita “cha wote,” na ambaye anatumia pombe kama njia ya kukimbiza matatizo yake. Kimsingi, hapa anazungumzia jinsi nchi yetu ilivyogeuka ‘shamba la bibi’ ambapo kila mwenye ‘fursa’ anajichumia.

Msanii huyo anakwenda mbali zaidi na kukemea dhana kuwa wawekezaji wa kigeni watatuletea maendeleo, na anasema “maendeleo ni ndoto, ile mwekezaji ashaipuuza,” na kutahadharisha kwamba uwepo wa wawekezaji hautufanyi tufikie viwango vya maendeleo katika nchi zao, akihoji “je kukaa karibu na moto ni kuota au kujiunguza?”

Fid Q pia anazilaumu taasisi za kisiasa kwa ‘kuwafelisha’ wananchi, kama ambavyo tunashuhudia vyama vyetu vya kisiasa vikiwa ‘bize’ kulumbana huku walalahoi wakizidi kutaabika.

Pia anakumbusha kuwa “hakuna utumwa mbaya kama kujiona uko huru” na kutahadharisha kuwa jitihada za kusaka ukweli zitakumbwa na vizingiti, akisema, “Kuusaka ukweli  ni  sawa na kumenya kitunguu/
kila ganda litakutoa machozi na utabaki macho juu/
Ukishafika kwenye kiini  niambie nini utagundua.
.?”

Anahitimisha tungo hiyo aliyomshirikisha msanii mwingine maarufu Juma Nature kwa kutahadharisha kuhusu wanasiasa matapeli ambao “wamejivisha u-Noah, safina zao zikatoboka; wakajivisha u-Mussa, fimbo zao hazikugeuka nyoka; sasa wamejivisha u-Mungu mtu...” Kadri tunavyoelekea kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 tutashuhudia kila aina ya utapeli wa kisiasa ambapo baadhi ya wanaosaka urais wataahidi mambo ambayo hata wenyewe hawayaamini.

Lengo la makala hii sio kuchambua wimbo huo bali kupigia mstari umuhimu wa alichofanya msanii Fid Q kutumia kipaji chake cha muziki kuuzindua umma hasa katika kipindi hiki cha mchakato wa kupata Katiba mpya, sambamba na hekaheka za uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2015.

Nimalizie makala hii kwa kumpongeza msanii huyo, na kutoa wito kwa kila Mtanzania kutumia nafasi aliyonayo kuwa chachu ya mabadiliko stahili kwa nchi yetu. Hatuwezi kuendelea kuwa watu wa kulalamika tu ilhali tuna uwezo wa kubadilisha yote yanayokwaza ustawi wa taifa letu.


Inawezekana, timiza wajibu wako

9 Jun 2013


Huiwezi kuuzungumzia muziki wa Bongoflava pasi kumtaja Mike Mhagama. Huyu alikuwa mtangazaji wa kituo cha kwanza binafsi cha redio nchini Tanzania, Radio One. Mike,ambaye kwa sasa anaishi nchini Marekani, alitoa mchango mkubwa sana kuutambulisha muziki wa Bongoflava- na kama sijakosea ni miongoni mwa waasisi wa neno 'Bongoflava' (sina hakika sana).

Ninakumbuka enzi hizo, kukosa kipindi cha DJ Show (kama sijakosea) ilikuwa kama dhambi flani kwa mtu anayependa muziki. Ama kwa hakika zama hizo kulikuwa na raha ya kuskiza redio, burudani iliyokuwa ikitolewa licha ya kuwa na ladha nzuri lakini pia iliendeshwa ki-professional.

Kama ambavyo wengi tumeguswa na kinachoonekana kama 'bifu' (uhasama) wa wasanii wawili nguli wa Bongofleva, Hamisi Mwinjuma a.k.a @MwanaFA na Judith Wambura a.k.a @LadyJaydee, Mike nae ameonyesha kuguswa na suala hilo japo yupo mbali na nyumbani.

Katika 'Timeline' yake huko Twitter, mtangazaji (@MikeMhagama) huyo wa zamani ameandika (ninamnukuu)

Screenshot_2013-06-09-21-09-01-1.png

Mike alikuwa anajibu rai yangu kwa wasanii Fareed Kubanda a.k.a @FidQ Ambwene Yesaya a.k.a AY (@AyTanzania) na Joseph Haule a.k.a @Profesa_Jay wafanye jithada za upatanishi kati ya Mwana FA na Jide. Kadhalika nilipendekza kuwa kikao hicho kinaweza pia kuhudhuriwa na watangazaji walio-present Kilimanjaro Tanzania Music Awards 2013 Jokate (@JokateM) na Millard Ayo (@MillardAyo)

Hadi wakati ninaandika makala hii raia hiyo ilikuwa haijajibiwa.Hata hivyo,ninapenda kumpongeza Mike Mhagama kwa angalau kuonyesha kuguswa na 'bifu' hiyo na kutamani kuisuluhisha. Si vigumu kuelea kwanini Mike ameguswa. Kama miongoni mwa waasisi na waliopromoti Bongoflava tangu inazaliwa hadi ilipofikia, lazima atakuwa anahuzunishwa na ugomvi huu.

Kwa upande mwingine, mhariri na mmiliki wa tovuti ya Bongo Celebrity, ambayo maarufu zaidi ya burudani kuliko zote za Watanzania,  Jeff Msangi, naye ameandika makala nzuri inayohusu suala hilo la bifu ya FA na JIDE. 

Makala hiyo ni hii hapa chini 

LADY JAYDEE Vs MwanaFA: BEEF,BIASHARA, PERSONAL AU?

Yapo mambo ambayo mara nyingi sisi hapa BC huwa tunayaacha yapite. Miongoni mwa mambo hayo ni pamoja na Beef baina ya watu fulani fulani hususani wale ambao BC inawachukulia kama Celebrities na hivyo kuleta maana halisi ya BongoCelebrity.
Nakumbuka wakati BC inaanza (miaka mingi sasa) nia ilikuwa ni kuyatizama maisha ya watu wetu maarufu (celebrities) katika jicho chanya zaidi. Tulielewa kwamba watu wanapenda zaidi kusikia umbea. Tulifahamu kwamba habari mbaya huenea kwa kasi ya aina yake kulinganisha na habari njema. Pamoja na kuelewa hivyo,tumejikita kwenye nia. To stay positive and ask everyone to stay positive and pay attention to more positives than negatives.
Sasa kama wewe ni mtumiaji au mtembeleaji mzuri wa mitandao ya kijamii kama vile Twitter,Facebook, Instagram etc, bila shaka leo umekumbana na maendeleo ya mpambano wa maneno kati ya Lady Jaydee na MwanaFA.Kuna kashfa, kuna kuitana majina. Kuna ushabiki ambao naamini mwisho wake sio mzuri….
Hawa wote ni wasanii wakongwe. Ni mifano ya kutizamwa na wengi hususani wasanii wachanga ambao wanataka kufikia mafanikio ambayo hawa tayari wameyafikia. Kinachoendelea, ingawa ni kweli kinaleta msisimko fulani (hususani kwa watu wanaofurahia wakati wengine wakiumizana), hakina mantiki yenye mlengo chanya. Ni ushindani wa siku moja (June 14-siku ambayo wote wana show). Tarehe 15 June kutakuwa na nini?
Kuna njia kadhaa za kuangalia kitu kinachoendelea. Ni beef? Ni biashara? Au ni mambo binafsi? Kama ni beef la ukweli,basi kuna haja ya mtu kuingilia kati na kuwapatanisha. Kama wasanii naamini issues zao zinafanana. Matatizo ya kudhulumiwa au kutolipwa ipasavyo, ni matatizo yao wote. Sio tatizo la JayDee au MwanaFA peke yake. Hakuna haja ya beef. Kuna haja ya kuungana na kupigania kitu kimoja; Haki.
Kama malumbano haya ni kibiashara zaidi, basi tutaona tarehe 14 June kama njia inayotumiwa ni sahihi au la. Kuna tofauti kubwa kati ya beef za kupromote biashara katika nchi za wenzetu kama Marekani (50Cent na Kanye West) na Tanzania yetu.Mazingira yanatofautiana…
Kama kinachoendelea ni masuala binafsi…then we don’t have a business to be into other people’s businesses. Wanaweza kuyamaliza…



CHANZO: BONGOCELEBRITY.COM Ni matumaini yangu-na pengine yenu wasomaji- kuwa hatimaye wasanii wetu, Mwana FA na Jide, watakaa pamoja na kufikia mwafaka wa kumaliza tofauti zao.Labda baadhi ya video hizi walioshirikiana zinaweza kuwakumbusha kuwa wamtoka mbali
Katika wimbo huu 'Nangoja Ageuke' wa FA a AY kuna cameo ya Lady Jaydee



22 Oct 2012



                                                    ALCOHOLISM AND EFFECTS
            POMBE NA MADHARA
                Lets check why many people change characters baada ya kulewa pombe na pombe hufanya nini mwilini mwa binadamu anapozitumia? mili yetu iliumbwa kwa ajiri ya kujiponya yenyewe endapo tu utakuwa unakula vizuri na nikisema kula vizuri haimaanishi ule ushibe hapana bali ninamaanisha ule chakula bora chenye lishe bora,rutuba ambazo ni vitamins na minerals zinazoweza kulinda na kurutubisha mwili na automatically or kujiponya naturally na upungufu wa rutuba mbali mbali mwilini ndo huleta matokeo ya watu kuumwa pasipo kupona ama kuumwa magonjwa kama presha, kisukari cancer,donda ndugu,kumea vinyama usoni malaria na typhoid za mara kwa mara,liver and kidney failure n.k na kuyaita haya magonjwa kama ni magonjwa yasiyo tibika ama magonjwa sugu kwa mimi i agree to dis agre na kwa uwezo tulio nao wa kufikiri je huwa unauhudumia mwili kama linavyohudumiwa gari?

            kwa kuwa endapo ingekuwa hivyo binadamu wote wangeweza kuishi hadi miaka 85 ndo waanze kuzeeka kama jinsi ilivyo kwa wajapani lakini tunaenda kinyume na haya yote, hebu jiulize je utaweza kuweka maji kwenye engine ya gari ama chumvi badala ya petroli? haiwezekani na hii ni kwa kuwa gari halina uwezo wa kujisafisha lenyewe na kujiponya na ndo maana huwa tunalipeleka service je sisi huwa tunajifanyia service ama body detoxination? (kuodoa sumu mwilini na uchafu usiohitajika mwilini?)

         So look at how our amazing bodies does mara nyingi huwa hatuwezi kuona emediet effects za pombe,sumu mwilini au effects za vyakula na aina ya madawa tunayotumia kwa kuwa miili yetu ili unbwa kwa ajiri ya kujiponya na kujiendesha yenyewe na ndo maana sumu haziwezi kuathiri mwili kama ambavyo ungeweka chumvi kwenye gari badala ya mafuta huwa effects zake zinajijenga taratibu na kufikia kikomo ama viungo vya kuchujia na kusambazia vitamins sahihi na minerals kukwama ambavyo mara nyingi viungo hivi viki collapse huwa very dangerous na viungo hivi ni ini na figo ambapo si tu hutumika kuchuja vilivyo vibaya na visivyo hitajika mwilini pia hutumika kwa kuvisambaza na kuvipeleka mahala husika panapohitaji certain type of vitamins and minerals so just imagine hivi viwili vikipata damage tge body suply inakuwa je?

          kwa leo nitaishia hapo juu ya vungo hivi viwili as we go on nitaendelea kuwafahamisha zaidi but today ninazungumzia pombe huwa inafanya nini mwilini hadi wengine huonekana kama wanamatusi,wakorofi na wakati mwingine kutojitambua na ni kwa sababu gani watu dini mbali mbali huzikemea! the thing is pombe si mbaya but kilicho kibaya ni vile pombe inavyo damage mwili wako na kutake control of everything when ever your drunk your life,dignity, behaviour and how you think and make desicions na hata waelimishaji wa masuala ya VVU/Ukimwi husisitiza sana watu kutokuwa walevi kwa kuwa pombe yaweza sababisha ulewe na kuamua kuwa na mwanamke au mwanaume na kufanya ngono zembe ama ngono pasipo kutumia kinga, na pia waweza kumchukua  mtu ambaye laiti ungekuwa mzima usingeweza hata kuongozana nae katika hali ya kawaida lakini kwa kuwa umekunywa pombe it was easy hadi kwenda kufanya naye mchezo mbaya kwa maana hiyo pombe hupunguza kudhoofisha ama kuua uwezo wako wa kufikiri na unakuwa poor decision maker.
               MADHARA KWA MWANAMKE MJAMZITO
     Kwa mwanamke mjamzito anayekunywa mara kwa mara pombe inaweza kumsababishia mtoto kuzaliwa taahira,inaweza ikasababisha kutoka kwa ujauzito (miscarriage) ama ikasababisha kudmaa kwa mtoto na asiweze kukua hata akiwa tumboni na baadae ikasababisha hyperactivity and irritability in the child, if a pregnant woman consumes alcohol on a regular basis (as well as drugs) the fetus can become addicted to these substances,
         Pia alcohol ni substance ambayo hutumia vitamins na minerals nyingi mno toka mwilini kwa ajiri ya kujiendesha ama umeng'enyukaji wake na kama pombe ikikuta hakuna vitamins na madini ya kutosha mwilini huwa inatabia ya kwenda kuchukua zile vitamins zilimo kwenye Tissue mwilini ambazo tissue hizi huwa katika damu na ndo husababisha kasoro nyingi za mwilini na kuleta matokeo ya kudhoofu kwa mwili na kuanza kuumwa ovyo ovyo.

               Mazingira sababishi juu ya wanywa pombe ni
Stress,Kazi,Kula bata na washkaji ama kunywa tu na marafiki pombe kwa kuwa compan yako yote wanakunywa,depression(mawazo) kujitenga, immaturity/foolish age kwa kudhani usipokunywa utaonekana haujakua bado ama hutoonekana ni kijana wa kisasa zaidi, loneliness (upweke) and Heredity
               Madhara mengine ya matumizi ya pombe ni
1.In the Pancreas (acute Pancreatistis)
2.In the liver (cirrcohosis) kwenye Ini kupunguza ufanis wa
kufanya kazi laweza pia kuvimba ama kujaa maji

3.In the Heart (kwenye moyo) kuvimba,kujaa maji, n.k

4.In the urinary system( kwenye njia ya mkojo na ndo maana huona wakati mwingine walevi huwa wanajikojolea kwa kuwa hata nerves zao huwa kama disconnected na mtu wa namna hii anaweza ahisi kitu ama kwa wanaume anaweza akashindwa kufanya tendo la ndoa kwa kuwa hakuna hisia tena ama mzunguko wa damu haui mzuri na kupeleka taarifa kwenye ubongo kwa kuwa pombe huua oksijen inayosaidia mzunguko huo wa damu na kuzidisha ufanisi wa nerves sytem

5.In the skin kudhoofisha ngozi
6.In the sexual organs (causing impotence) kupunguza uwezo wa tendo la ndoa haswa kwa wanaume
7.In the gastrointestinal and digestive tracts, kupunguza uwezo wa usagaji chakula na kusababisha gesi nyingi kila wakati hata kama hujala chakula huwa kama umeshiba na kukata hamu ya kula.

8.In the nervous sytem which can become completely unsettled by the death of cells,hii ni kwa kuwa pombe huwa inaondoa maji kwenye these cells producing a series of nervous disoders  which are frequently reflected in a sign depression and anxiety which in extreme cases can lead to delirium trements causing hallucinations ama kuweweseka,


So kwa wale wanaopata tatizo la  hang over baada ya kunywa ama kama unataka kukata pombe na unawahi meeting ama ofisini waweza call 0753 32 0009 ili kupata kujua jinsi ya kuepukana ama kudhibiti hali hiyo.

Na kwa wale wanaotaka kufanya detoxination ama kufanya miili yao service na kuondoa sumu mwilini Tafadhari call 0753 32 00 09 Mtu ni afya

4 Sept 2012


Brooklyn Hip hop Festival




Wes Jackson, President and executive director of Brooklyn Hip hop festival in the middle Witnesz the Fitnes mkewe Ebonie Jackson ambaye yupo kwenye kitengo cha mahesabu ya shughuli kadhaa za mumewe ikiwemo Hip Hop Festival and Brooklyn Bodega





Brooklyn Bodega a complicated animal, creators of  BHF, Top notch blogazine (blog meets magazine) cultural programmers, Hip Hop Advocacy Group.

The bodega was founded in 2006 by Wes Jackson as the online home of the BHF , under the guidance of Bodega’s initial creative director and administrator James Blagden and Alma Geddy-Romeo.

The bodega grew into one of the most respected online destinations in the Hip Hop community Editorially, the Bodega  strives to add a more academic voice to the world of Hip Hop Journalism, It Derives deep into issue facing the Hip Hop community from music business to politics to technology and they offer a professional and intellectual voice.

Wes Jackson has over 15years experience as an entrepreneur and innovator in music business. His carrier began with producing concerts for Nas, The Roots, The Dave Mathews, band and de La Soul etc. He went on and started his own promotions company by the name seven Heads Promotions, seven Heads was instrumental in launching the career of MOs Def. ,Talib Kweli and others under Wes’ Leadership. Seven Heads expanded into a Record label and a management company, The record company that spun into the room Service Group (RSG) one of the leading digital marketing, RSG has worked with Def. Jam, Capitol, Warner Bros, Interscope, vivendi, and converse the list is endless.

 In addition to his successful business ventures Wes also serves as lecture at city University of New York (CUNY) Wes’s entrepreneurship spirit endure as he continues to grow the BHF into a world class event also as the Brooklyn Bodega Brand with the pop-up store Bbeats at DeKalb market in Downtown Brooklyn,

Wes aliweza eleza kiurefu zaidi juu ya biashara mjini New York kama mmiliki halisi wa hiyo Festival iitwayo Brooklyn Bodega na record label na mengineyo ambayo yote yanahusika na harakati za kihip hop zenye mafanikio makubwa up to date na kufafanua kibiashara zaidi mambo mbali mbali ikiwemo ujasiriamali na sababu za festival hiyo kutohusisha sana au kabisa wasanii kutoka nje wa Hip Hop,alisema wes kuwa wasanii wa hip hop Nchini New York wapo wengi mno mfano wa mafuriko na wote ni wa kali na kusbabisha eneo hilo kuwa hapatoshi hata kwa wakazi wenyewe so mtu yeyote akitoka nje ya nchi akitaka kuingia kwenye soko hilo ni lazima awe extra special, multitalented, unique na awe ni mchapa kazi mara tatu ya wasanii wa New York na ndivyo ilivyo kwa wanawake wanao fanya Hip Hop pia the half to beat men ambao they are flooded with extra energy has to be used In order to stay on the top of the game.
                                                                                                 
                                                                                                  
       Pia nilipata kujua maana ya neno Bodega kama ambapo iliwahi sikika kwenye moja ya nyimbo za Big punisher alipo sema my father’s Bodega kwenye intro na kufafanua ya kwamba neno Bodega ni la kispanish likimaanisha panapo tengenezwa wine, ama corner store mjini new york ambapo huuzwa wine,vilevi mbali mbali na vitu vyote vihusuvyo starehe ikiwemo urahisi wa kupata condoms hata nyakati za usiku huwa pako wazi masaa 24 siku saba za wiki 24/7 kwenye hiyo corner store  wanapatania ya kuwa ni an organized mess place,nikmrahisishia kwa kusema an organized place in a disorganized manner? akasema thats whats up kwa kuwa ukienda kwenye a corner store kulikuwa kuna taka taka karibia za aina zote anazohitaji mtu kwa nyakati za usiku na mchana na hutumika kama maskani na kupanga kuhusu mitikasi pamoja na kupeana mistari ma dj,rappers watu wa aina zote kwenye harakati walikuwa wakitia maguuhapo hata mkiwa hampatani mtaani mkifika hapo kila mtu huwa peacefull ni kiduka kona ambacho watu wa jinsia zote na kutoka pande zote kupata huduma,kwa upande wangu nilipata picha ya gengeni ambapo mara nyingi vijana hukaa hapo ndani ya bong na kuganga njaa ama wakihesabu magari ama kwa kuwalaghai mabinti hahahahaa!


 
                          So a lot of things happening at a bodega store you name it as the aim of the Brooklyn Bodega ambapo ndiye mama wa Hip Hop festival tamasha ambalo hufanyika kila mwaka mjini New York tangu lianze limekwisha fanya matamasha nane mpaka sasa na mwaka huu limekwisha fanyika ,ambapo watumbuizaji wa kuu walikuwa Buster Rhymes na Tribe called Quest na host Mkuu wa tamasha hilo miaka nenda miaka rudi akiwa ni Uncle Ralph.
                                                                                                                     Heshima Zizidi Kuendelea










8 Aug 2012

9 Jul 2012




Naomba nivamie eneo ambalo ninaweza kujiita 'mgeni' (foreign territoty).Hili ni uchambuzi wa muziki,au kwa usahihi zaidi,uchambuzi wa video za muziki.

Nikurejeshe nyuma kidogo.Zamani hizooo,niliwahi 'kuota' kuwa mshiriki wa muziki.Well,sio kuwa mwanamuziki per se bali kujishughulisha na utengenezaji muziki.Nilipokuwa sekondari nilimudu kutunga nyimbo kadhaa kwa kwaya ya shule.Niliweza kutunga aya na sauti lakini tatizo lilikuwa kwenye namna ya uchezaji.Hadi leo,mie na kucheza ni kama kibaka na polisi.Kwa kifupi sijui ku-dance.

Ndoto za kuwa mtengeneza muziki (prodyuza) zilichangiwa zaidi na jinsi ninavyothamini 'michango isiyoonekana.' Hapa ninamaanisha kazi za watu kama watengeneza filamu, watengeneza muziki au hata mashushushu.Hawa ni watu wanaowezesha mengi na pengine laiti wangekuwa wanaonekana na 'products' zilizokwishakamilika basi sifa nyingi zingewaendea wao kuliko ilivyo sasa.

Tunapoona filamu nzuri,sifa nyingi huenda kwa actor au actress.Lakini kimsingi kazi kubwa inayoweza kupelekea filamu ikapata umaarufu hufanywa na mtengenezaji filamu.Kwenye filamu,uzuri wa filamu husika ni mkusanyiko wa jitihada za mwongozaji filamu (yaani director) na mtengenezaji filamu (yaani producer).

Nimeutaja ushushushu.Jamaa hawa ndio kila kitu.Ukiona nchi inakwenda vyema ujue wanafanya kazi yao kwa ufanisi.Ukiona mambo yanayumba basi ujue ndugu zetu hawa wana mushkeli mahala flani.Lakini kimsingi ni kuwa hawaonekani.Kama ilivyo kwa director au prodcuer wa filamu,sifa za kazi husika hulekezwa kwa wengine (kwenye filamu ni actors/actresses) na kwenye mwenendo wa nchi sifa huelekezwa kwa askari au taasisi nyingine za serikali.

Tofauti na filamu na ushushushu ambapo ni mara nyingi ni mkusanyiko wa wengi,kwenye muziki mara nyingi ni jithada za mtu mmoja au wawili. Mara nyingi producer wa muziki ndiye anayebuni ladha ya wimbo kwa maana ya kuunda beatsjapo jukumu la mwisho la ku-flow linabaki kwa msanii husika.Pia inawezekana wimbo ukawa umetungwa na mtu mwingine kisha kumpatia msanii au producer.La msingi hapa ni kuwa producer au mtunzi wa wimbo (kama si msanii mwenyewe) ni watu ambao hawapati sifa za kutosha ukilinganisha na msanii husika.

Kwahiyo moja ya ndoto zangu udogoni ilikuwa kuwa music producer...lakini kama tujuavyo katika maisha sio kila tutakacho ndio tupatacho.Ndoto hiyo 'ilikufa kifo cha asili' baada ya kuelekeza nguvu zangu kwenye  maeneo mengine ya maisha.Lakini hadi leo nina mapenzi ya dhati na muziki hususan wa kufokafoka.

Lengo la makala hii ni kuchambua kazi mbili za wasanii mahiri wa Bongoflava,Fid-Q na Solo Thang,ambao hivi karibuni wametambulisha video zao mpya.

Naomba nisisitize kuwa licha ya mapenzi yangu kwa muziki,mie si mtaalam (expert) wa eneo hilo.Uchambuzi wangu huu ni wa ki-layman (i.e. wa mtu asiye na upeo wa kutosha katika mada husika).

Jingine la kupigia mstari ni desturi iliyojengeka miongoni mwetu kuwa pindi ukionyesha mapungufu ya kitu flani basi wewe ni HATER.Binafsi,nimefika nilipofika kwa sababu siku zote nimekuwa nikipokea na kufanyia kazi maoni mbalimbali hata yale yanayokinzana na imani au mtazamo wangu.Kupewa sifa kuna tatizo moja: hakuwezi kukusaidia kutambua wapi umekwenda kombo.Ofkoz, kazi nzuri lazima isifiwe lakini pengine ili kumsaidia aliyefanya kazi hiyo ni vema kumfahamisha wapi arekebishe au penye mapungufu.Na hiki ndio nitakachofanya katika makala hii.

Video za muziki ninazozichambia ni ile ya SIHITAJI MARAFIKI ya FID-Q na MISS TANZANIA ya SOLO THANG.Kwa kifupi,video zote ni za ubora wa hali ya juu.Wasanii wote wawili wamechagua location za kuvutia wakati wanarekodi video zao.Kadhalika,ubora wa picha ni wa kiwango cha juu.


Wasanii hawa wana sifa moja inayolingana: ni mahiri mno katika uwasilishaji wa ujumbe uliomo kwenye wimbo husika.Wote wana uwezo wa hali ya juu wa kucheza na maneno, neno pekee la Kiingereza unaloweza kulitumia kuwaelezea ni LYRICAL ASSASSINS (Usitishwe na hiyo 'assassins' kwani ni neno tu linalotumiwa kutanabaisha namna msanii anavyoweza 'kucheza na maneno' kwenye tungo husika).

Wakati Solo Thang anamzungumzia Miss Tanzania,Fid-Q anazungumzia marafiki.Ujumbe katika tungo zote mbili haupo wazi sana na inambidi msikilizaji 'asome kati ya mistari' (reading between the lines) kuelewa kinachoongelewa.Usipokuwa makini unaweza kudhani Solo 'anawapaka' warembo lakini kimsingi MISS TANZANIA imebeba ujumbe mzito hususan kwa mabinti warembo wenye kuendekeza tabia zisizopendeza machoni kwa jamii.

Ujumbe wa Solo unapigia mstari mtizamo wa wengi kuhusu urembo kama fani (iwe u-Miss au uanamitindo).Yayumkinika kusema kuwa machoni wa wengi fani hizo mbili hutizamwa 'kwa jicho baya' hasa kutokana na tabia kama za huyo 'Miss Tanzania anayezungumziw na Solo.' Huu ni ukweli i.e. ni mtazamo wa wengi japo si kila Miss au mwanamitindo ana tabia zisizopendeza katika jamii.Inawezekana Solo anamzungumzia Miss Tanzania flani?Jibu la swali hili analo yeye mwenyewe lakini kwa vile ni mahiri mno wa 'kucheza na maneno' yayumkinika kuamini kuwa kuna ujumbe mpana pengine zaidi ya uelewa wetu.

Kwa upande wake Fid-Q, SITAKI MARAFIKI haimaanishi marafiki si muhimu bali kwa kutumia kipaji chake kikubwa cha kuwasilisha ujumbe kwa namna inayohitaji tafakuri,msanii huyo anaweka wazi mtazamo wake kuhusu mahusiano katika jamii,kwa kutumia mfano mwafaka wa marafiki.Nadhani ushaskia msemo  'MARAFIKI WA NINI KAMA MAADUI WANANISAIDIA.' Mara nyingi,marafiki zetu hupenda kututendea mazuri tu tunayotarajia kutoka kwao na pengine kuepuka kutueleza 'hapa umechemka.' Lakini maadui zetu huwa mahiri wa kuonyesha kasoro zetu (hata kama ni kwa uchache) japo kimsingi matarajio yao huwa ni kuonyesha mabaya yetu.Kwa hiyo pasipo kukusudia,maadui zetu wanaweza kuwa na mchango flani chanya katika maisha yetu kwa sababu hawana unafiki katika kunyooshe akidole mapungufu yetu.

Kwa anayezifahamu vema kazi za Fid-Q na Solo Thang ni wazi hatokuwa na wasiwasi kuhusu namna watakavyouwasilisha ujumbe kwenye tungo mpya.Kama nilivyoeleza hapo juu,wasanii hawa wana uwezo wa hali ya juu wa 'kucheza na lugha na maneno.' Uwezo huo unawasiaidia sana katika kuwasilisha ujumbe katika namna inayomwacha msikilizaji 'ameterazika' (ameridhika)

Sasa nigeukia eneo linaloweza kuniingiza matatizoni: mapungufu katika kazi hizo za wasanii hao.Kimsingi si mapungufu bali ni pungufu kwani ni moja tu,na si kubwa sana.Ukiangalia video zote mbili utabaini jambo hili: katika video ya Fid-Q,tangu mwanzo hadi mwisho wa video yake amevaa vazi lilelile.Kwa Solo,kwa kiwango kikubwa katika video hiyo yupo katika T-shirt ileile japo kuna vipande ambapo anaonekana amevaa shati.

Kama nilivyotanabaisha,hii ni kasoro ndogo inayoweza kabisa kufunikwa na ladha ( flavour) ya muziki, ujumbe uliomo katika wimbo,na kiwango cha video.Hata hivyo,kama inavyotanabaishwa kwenye na Andrew Goodwin kwenye Kanuni ya Video ya Muziki (Music Video Theory) vinavyoonekana katika video ya muziki (visuals) vinaweza kuwa na mchango mkubwa sio tu kuiboresha video husika bali pia kuiunganisha na hadhira.

Pengine ili uelewe ninachoelezea hapa nitolee mfano msanii kama Lady Gaga.Mavazi yake ni burudani tosha-japo sio aina ya mavazi unayoweza kumwambia fundi cherahani akutengenezee.Msanii kama Michael Jackson alifahamika sio tu kwa miziki yake bali pia mavazi yake.Kwa sanii wa hip-hop wa Marekani,mavazi ni moja ya vitu muhimu mno,na baadhi ya mapendezeo yao katika mavazi yamepelekea mwamko wa fasheni,kwa mfano mashati ya 'DOGI DOGI' yaliyokuwa yanapendelewa na wasanii wa rap/hiphop wa pwani ya magharibi ya Marekani (West Coast rappers) kwa mfano Snoop Dogg na Ice Cube



Nadhani sababu pekee iliyowafanya Fid-Q na Solo wasionekane katika mavazi tofaut tofauti katika video zao ni MUDA.Hapa ninabashiri kuwa hawakuwa na muda wa kutosha kurekodi video zao kwa muda mrefu ambao ungewapa nafasi za kubadili mavazi mara kadhaa.Naomba nisistize kuwa kasoro hiyo ndogo haijapoteza hata chembe ladha ya kazi zao bora kabisa.Nimeipigia mstari kasoro hii kwa minajili ya kuwasaidia wasanii hao huko mbeleni wajaribu kutumia muda zaidi katika kurekodi video zao.Kanuni nyepesi ya kurekodi kitu chochote kile ni hii: kadri unavyojipa muda wa kutosha ndivyo unavyomudu kurekodi vitu vingi zaidi ambavyo wakati wa kuhariri utaondoa vile usivyovitaka na kuacha vile unavyovitaka.

Lakini kasoro hiyo ndogo inarekebishika.Ninaamini tulichoshuhudia katika video ya SIHITAJI MARAFIKI na MISSI TANZANIA ni matoleo ya mwanzo tu (iwapo Fid na Solo wana mtizamo kama wangu).Si ajabu kwa msanii kutoa video ya mwanzo kisha kutoa video nyingine rasmi kwa ajili ya wimbo husika.Mfano mzuri ni huu wa kundi la TOK katika wimbo wao Footprints Hii ni version ya awali

Hii ni version rasmi

Pengine kitawachowarahisishia Solo na Fid-Q kutengeneza video 'r(kama wataona kuna haja ya kufanya hivyo) ni ukweli kwamba tayari wana video nzima ya asili,ambapo wakiamua kuongeza chochote inakuwa ni suala la kuongeza tu vipande vipya katika original version.Hili si lazima,as long as wao wameridhika na versions walizoweka hadharani.

Ukiweka kando kasoro hiyo ndogo,Solo Thang ameendelea kuwa mithili ya balozi wetu wa Bongoflava katika anga za kimataifa ambapo anafanyia kazi zake kutoka nchini Ireland.Lakini licha ya kuwa nguli (legend) wa bongoflava na 'wadhifa' huo wa ubalozi wa kimataifa,msanii huyu ni miongoni mwa wachache ambao ni down-to-earth sana na anayejali sana kuishirikisha hadhira,hususan kupitia Twitter na Facebook.Kadhalika,ana blogu yake anayotumia kuwafahamisha wapenzi wa muziki wake kuhusu kazi zake.

Kwa upande wa Fid-Q, mkongwe huyu wa muziki wa kufokafoka huko nyumbani amekuwa mahiri sana katika matumizi ya mitandao ya kijamii kutangaza kazi zake na kuishirikisha hadhira.Huko Twitter ana utaratibu wa kujibu maswali angalau mara moja kwa wiki kwa kutumia hashtag #AskFidQ. Hii inatoa fursa kwa wengi kumuuliza maswali mbalimbali.Kadhalika,anaendesha kitu kinachofahamika kama Hip-Hop Darasa,ambapo pamoja na mambo mengine anatoa elimu kwa kizazi kipya cha Hip-hop huko nyumbani.Taarifa za hivi karibuni zinaonyesha kuwa kipindi chake maarufu mtandaoni cha Fidstyle Friday kitaanza kuonyeshwa kwenye runinga katika kituo cha East Africa Television (EATV).Haya ni maendeleo makubwa.

Basi nimalizie kwa kuwapongeza Fid-Q na Solo Thang kwa kazi zao bora kabisa.Naomba wasitafsiri kasoro ndogo niliyobainisha hapo juu kuwa ni HATING. Sote tunapenda kuona wasanii wetu wakifanikiwa na kuteka anga sio huko nyumbani tu bali Afrika na duniani kwa ujumla.Natambua kuna wataosema "huyu nae,anajifanya anajua kila kitu" lakini lengo langu si kujifanya mjuaji bali kutoa mchango wangu kwa wasanii wetu.

Nimalizie makala hii na video zifuatazo za wasanii hao



13 May 2012


MSANII mahiri katika medani ya muziki wa kizazi kipya nchini Abbas Hamisi ‘20 Pacent’ ameamua kujikita kwenye ujasiriamali ambapo sasa amejikita kwenye kilimo huko mkoani Morogoro.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi juzi, 20 Percent ambaye alitamba kwa kuzoa tuzo tano kwa mpigo za Wimbo Bora wa Afro-pop, Mtunzi bora wa nyimbo, Mwimbaji bora wa kiume, Wimbo Bora wa Mwaka na Msanii Bora wa Muziki wa Kiume, katika tuzo za Kili Music Awards kwa mwaka 2010 alisema ameamua kuanza kujipanga kwa maisha ya baadaye.

Nyota huyo aliyetamba na nyimbo kama vile ‘Money Money’, ‘Yanini Malumbano’ na nyinginezo kibao alisema kuwa amehamasika kujikita katika kilimo kama ilivyo kwa mkongwe wa muziki huo nchini Selemani Msindi ‘Afande Sele’.

“Kaka hivi sasa mimi nimeamua kujikita pia kwenye kilimo kwa sababu huwezi kutegemea kazi za muziki tu, kuna kila sababu za kuwa mjasiriamali,” alisema 20 Percent.

CHANZO: Tanzania Daima




23 Feb 2012


Chuck D,mwanzilishi na kiongozi wa lilikouwa kundi maarufu la rap huko Marekani,Public Enemy,aliwahi kusema muziki wa rap ndio CNN ya mtaa.Tangu awali,muziki wa rap umekuwa ukizungumzia masuala mbalimbali yanayoikabbili jamii-kutoka ukimwi,mihadarati,ubaguzi wa rangi hadi sera za ndani na za nje.Na sasa tunashuhudia baadhi ya wasanii wetu wakipata mwamko kama huo wa Public Enemy.Ushuhuda ni huu hapa chini.Sahau kidogo kuhusu video na sikiliza ujumbe kwa makini



CHANZO: Dj Choka's Blog

23 Jul 2011



Kalapina on politics, Freemasons, war, peace, Rostam, Drugs etc.
More from Kalapina and kikosi http://www.reverbnation.com/tunepak/3387426

Click the banner titled CHEUSI DAWA TV (FID-Q) (see the sidebar) for previous episodes of Fridstyle Friday and much more!

8 Oct 2010

Image and video hosting by TinyPic


Urban Pulse Creative ikishirikiana na Aset Inapenda kuwataarifu wadau wote wa Music wa bongo Flava na Hip Hop kuwa imeandaa tamasha maalum linaloitwa URBAN TOUR ambapo msanii Diamond kutoka bongo anayetamba na kibao chake cha Mbagala atakuwepo hapa ukerewere kuanzia mwezi wa November mwaka huu. Wasanii wengine ni Pamoja na First lady wa Urban Pulse Mish Ze Fyah Sis UK Artist anayetamba na single yake Freedom na I don't give a damn.



Tamasha Hili ni kwa ajili ya kuchangia Vita Dhidi ya Malaria Afrika. Diamond ni ambassador wa Malaria Tanzania na ndiye atakekuwa akiwakilisha.
Shows Hivi zitafanyika tarehe 6th Nov Milton keynes, 12th Nov London and 27th Nov Birmingham.
Stay tune kwa habari zaidi.

Asanteni,

Urban pulse Creative.

29 Jan 2009


29 Sept 2008

Hizi ni miongoni mwa kazi za wanasanii wetu wa nyumbani ambazo zilinigusa nilipokuwa huko hivi karibuni.Nilichopenda kwenye hii ya kwanza,"Nangoja ageuke" ya MwanaF.A. ft AY, ni mchanganyiko wa midundo na video yenyewe.Ushirikishwaji wa mastaa wetu wa Kibongo umeongeza chachandu pia.


Hizi zilizosalia zilinivutia zaidi katika flavour na beats





15 Jan 2008

Hivi msomaji wangu mpendwa ulishaota ndoto ngapi za "ningependa kuwa flani" kabla hujafika hapo ulipo?Kwangu ni 3,moja naendelea kuhangaika nayo,na kwa Mapenzi yake Mola+jitihada zangu,natarajia kuitimiza miezi michache ijayo.Naomba niihifadhi ndoto hiyo kwa sasa.Ndoto yangu kwanza utotoni ilikuwa kuwa daktari.Sehemu ya elimu yangu ya msingi na O'level ilipatikana katika shule zilizokuwa karibu na hospitali flani yenye CV ya kuridhisha (imezaa madaktari wengi kupitia chuo cha udaktari kilichopo hapo).Kutokana na ukaribu kati ya shule na hospitali hiyo,wanafunzi walikuwa wakipendelea kwenda hapo wakati wa mapumziko ya asubuhi na mchana.Taratibu nikajikuta natamani kwamba siku moja nami niwe katika majoho meupe nikiokoa maisha ya binadamu wenzangu.Nadhani kilichonivutia zaidi kuhusu taaluma ya utatibu ni role yao katika maisha ya binadamu (well,at least sio kama wale wazembe "waliochanganya madawa" huko Muhimbili kwa kumpasua mtu kichwa badala ya mguu na vice versa).Ndoto hiyo iliyeyuka kama pande barafu kwenye maji ya moto baada ya kufeli somo la Fizikia (sioni haya kusema nilipata F japo nilikuwa na A ya Kemia).PCB ikawa imegoma hapo (nilikuwa na C ya Baiolojia).Nikapiga mahesabu ya CBG-Kemia,Baiolojia na Jiografia (ambapo "combi" ingekubali kwani nilikuwa nina A,C na B,consecutively).Ndoto ilifutika kabisa baada ya kuwasili shule nilopangiwa kusoma A'level.CBG ilikwepo lakini,kwanza shule ilikuwa haina mwalimu wa Jiografia (hivyo wanafunzi walikuwa wanalazimika kwenda shule jirani kupata mihadhara ya somo hilo).Lakini,to make matter even worse,nikaja kugundua kwamba Kemia ya A'level ni "hadithi tofauti" na ile ya O'level niliyoimudu.Did I mention kwamba niliibuka na D ya kichovu kwenye Hisabati huko O'level?Yeah I did,na Kemia ya A level imejaa "namba" (nadhani Physical Chemistry ndio balaa zaidi).Enewei,nikaamua kukimbilia kwenye HGL-Historia,Jiografia na Lugha ya Mama..Kimombo (ambayo ilikuwa na msingi mzuri wa A,B na A,consecutively huko O'level).Kilichonisaidia kuwa na options mbalimbali ni mchanganyiko wa masomo huko O'level (sayansi,sanaa na biashara) lakini ndoto ya udaktari ndio ikafa kifo cha asili.

Ndoto ya pili ilinijia nilipokuwa jeshi la kujenga taifa (JKT).Did I mention kwamba shule niliyosoma A'level nayo ilikuwa ya mchepuo wa kijeshi?Sorry if I didn't,lakini "jeshi linininoma" kisawasawa kwa miaka miwili ya A'level kijeshi na mmoja wa JKT kijeshi.Let's leave it there.Huko JKT nilikutana na jamaa flani mahiri sana kwa kufokafoka (rapping).Sijui yuko wapi sasa.Yeye alikuwa rafiki na jamaa mmoja ambaye aliwahi kuibuka mshindi wa mashindano ya Yo!Rap Bonanza miaka ileeee...anaitwa Frank Mtui a.k.a Fresh XE (kama sijakosea,maana ni muda mrefu sasa).Urafiki wao ndio uliopelekea jamaa yangu huyo ambaye jina limenitoka kidogo kuwa mahiri kwenye ku-rap.Tofauti na yeye,mie nikagundua mapema kwamba ulimi wangu mzito,hivyo to become a rapper was out of question.Ndoto yangu ikaegemea kwenye u-producer.Baada ya ngarambe na fatiki za kambini,jamaa yangu huyo alikuwa akinisimulia stori mbalimbali kuhusu maprodyuza maarufu wa muziki wakufokafoka,kama vile Dr Dre,Jermaine Dupri,Pete Rock,et cetera (Dre became my most favourite).Baadaye nikakutana na watu wawili waliozidi kuipa uhai ndoto yangu ya uprodyuza,mmoja anaitwa Profesa Ludigo (alikuwa akitajwatajwa sana kwenye bongoflava kadhaa,ila sijui kwa sasa yuko wapi),mwingine anaitwa Sajo (sio wa Daz Nundaz) ambaye aliwa karibu na Saigon wa Diplomatz,moja ya makundi ya awali ya rap huko nyumbani.Mara ya mwisho nilisikia huyu jamaa (Sajo) yuko Wichita.Prof Ludigo ni "kichwa" kwenye music production na Sajo anaijua fani hiyo nje-ndani.Ndoto ya uprodyuza ikapata nguvu za ziada.How I ended not being a producer I,for some time, dreamt of becoming ,only my God and I know...here I am,not "book-worming" a certain medical journal or searching for some new beat producing softwares,but SIASA...yeah,that's what I'm studying.

Let's go to the point.Nimesoma na kusikia habari kwamba "hali ya afya ya Bongoflava sio ya kuridhisha",na kama ni mgonjwa basi yuko chumba cha wagonjwa mahututi.May be hiyo ni kile ambacho kwenye sarufi ya Kiingereza wanaita "hyperbole" au kuzidisha chumvi.Lakini,kwa a producer that never became one (mimi huyo),nadhani mwelekeo wa muziki huo sio wa kuleta matumaini sana.Frankly speaking,baadhi ya nyimbo za bongofleva zinaweza kukupa hisia kwamba mwanamuziki na prodyuza wake waliurekodi wimbo husika wakiwa usingizini.Ladha (flava) duni,ujumbe (message) ni dhaifu au haueleweki,na wakikurupuka na video ndio inakuwa kana kwamba ililengwa kwa ajili ya "youtube" na sio kuonyeshwa kwenye runinga.Of course,kuna exceptions lakini ni chache.

Nadhani tatizo kubwa liko kwa mwanamuziki kuhakikisha anakuwa bora zaidi ya alipotoa single au album iliyompatia umaarufu.Shughuli imekuwa "kujirusha" sana na kuwekeza "chini" (you surely know what I mean.If you dont,namaanisha "ngono").Wengine wakakimbilia kununua vitu vya thamani ambavyo kwa bahati mbaya hawana uwezo wa kuvimudu.Wengine wakajilinganisha na "wazungu wa unga" ambao hutumia fedha kwa kasi wakijua "shamba" lipo pindi "wakichoka" (wakifilisika).Wengine wakawaiga watu wa Mbughuni na Mererani ambao nao,kama "wazungu wa unga" hutumia kwa fujo wakijua "jiwe" bado lipo mgodini.

Hakuna dhambi kula matunda ya jasho lako lakini ni muhimu kuepuka kung'oa kabisa mmea unaotoa matunda hayo.Lakini vijana wengi waliotokea kupata umaarufu kwenye bongofleva wanakabiliwa na tatizo jingine kubwa zaidi ya hilo la kubweteka au kula jasho lao pasipo kufikiria kesho itakuwaje.Hili ni matumizi ya majani haramu yajulikanayo kama bangi.Kuna idadi kubwa ya wasanii wanaoendekeza bangi kupita vipaji vyao.Najua wapo wanaodai wakivuta "weed" ndio wanawezesha verse kushuka kwa kasi ya tsunami,lakini hizo ni crazy excuses.Bangi sio kitu kizuri.Na mbaya zaidi ni kwa wale wanaotengeneza cocktail ya bangi,unga na laga.

Nini kifanyike?Well,nchi ina matatizo makubwa na ya muhimu zaidi kuliko "hali ya afya ya bongoflava".Na kwa vile suala la kulinda au kutelekeza ajira au kipaji ni la mtu binafsi,inaweza kuwa sio rahisi kuwashauri baadhi ya nyota wetu wanaoelekea kufifia.Wanaopenda majibu mepesi kwenye maswali magumu wanahitimisha kwamba "taarabu ilivuma wee baadaye ikafifia,na sasa ni zamu ya bongoflava...".Mie naona chanzo ni kipana zaidi ya suala la kuvuma na kufifia:kubweteka na mafanikio,kuendekeza anasa na kusahau kazi,maprodyuza wanaoigana wanaopelekea msikilizaji kushindwa kutofautisha wimbo wa msanii mpya na wa zamani-sambamba na productions nyingi "zisizokwenda shule" ni mlolongo wa sababu zinazowakwaza vijana hawa.You have been warned....

Talking of Dr Dre,he cautions in Been There Done That, that "...a fool and his dough soon split..." in the 3rd line of the 2nd verse.Here is the video (caution: explicit lyrics).


Na hapa ni Jay-Z katika Girls,Girls,Girls (dedicated kwa "wanaoendekeza vimwana")


And finally,nadhani utakubaliana nami kwamba some flavaz seem to last forever in your ears,kwa mfano hii I Got 5 on It ya Luniz (japo wenyewe "wamepotea")





Au hii soundtrack ya Friday, You Can Do It ya Ice Cube (Caution: explicit lyrics)


Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.