11 Sept 2008

Wakati Waamerika na wapenda amani wengine duniani wanakumbuka mashambulizi ya kigaidi yaliyotokea siku kama leo mwaka 2001,kibosile wa polisi wa Devon&Cornwal hapa Uingereza,Colin Terry,ameadhimisha siku hiyo kiaina kwa kuvaa sanamu la Osama bin Laden.Kitendo hicho kimezua kimbembe na tayari wapo wanaotaka awajibishwe pengine kwa vile afande huyo pia ni mwandamizikatika eneo lake  kwenye mapambano dhidi ya ugaidi.Habari zaidi iko HAPA


10 Sept 2008

Jana niliongelea kidogo kuhusu The Big Bang Theory,na hofu zilizojitokeza kwamba huenda leo,Jumatano,ingekuwa mwisho wa dunia.Well,experiment hiyo inaendelea huko kwenye underground tunnel lililosambaa mpakani mwa Uswisi na Ufaransa na hakuna dalili kwamba dunia itafikia tamati leo!Hata hivyo,hofu ya Big Bang imepelekea mwisho wa dunia huko India.Well,sio kwa nchi nzima bali kwa binti mmoja ambaye aliamua kujitoa uhai wake baada ya kuwa traumatized na taarifa za vyombo vya habari kuhusu uwezekano wa mwisho wa dunia kutokana na experiment ya Big Bang.Pengine tutasikia mengi pindi experiment hiyo itapomalizika.Habari kamili kuhusu binti wa India ni hii HAPA

Pamoja na kuchukua sabbatical leave ya lazima katika uandishi wa makala katika gazeti la Raia Mwema,blogu hii itaendelea kuwaletea kinachojiri kila wiki katika jarida hilo mahiri huko nyumbani.Miongoni mwa habari zilizochukua uzito wa juu katika toleo la wiki hii ni pamoja na kauli ya Spika wa Bunge la Muungano,Samuel Sitta,kwamba amejiandaa vya kutosha kufuatia taarifa kwamba watuhumiwa wa ufisadi wameingiza sumu huko Bongo kwa lengo la kuwadhuru Sitta na Mbunge wa Kyela,Dr Harrison Mwakyembe.Sidhani kama inahitaji kujumlisha mbili na mbili kupata jawaba as to akina nani watakuwa the usual suspects wa unyama wa aina hii.Zaidi BONYEZA HAPA kusoma habari hiyo na nyingine motomoto.

Kuna hii kitu wanaita The Big Bang Theory inaelekea kuwachanganya watu wengi wakiwamo wanasayansi wenyewe.Kwa vile mie sio mzuri sana kwenye maeneo hayo,BONYEZA HAPA kupata undani zaidi wa hii kitu.

Kwa upande wa siasa za Marekani,kuna wanaomuona Sarah Palin kuwa hana tofauti na Islamic fundamentalists ambao mgombea-mwenza wake,John McCain,amefanya kuwa moja ya ajenda zake kuu za kushinda uchaguzi.Habari nzima iko HAPA

Na burudani kidogo kutoka kwa John Legend ft Andre 3000 katika Green Light.

Matatizo ya kidunia yalinifanya nishindwe ku-update blog hii kwa takriban miezi miwili hivi.Kupoteza mzazi inaweza kuwa tukio la kawaida iwapo litatokea kwa mtu mwingine.Lakini ukweli mchungu ni kwamba once ikitokea kwako ni vigumu mno kuhimili matokeo yake.Inaumiza zaidi pale mmoja wa watu aliyekuwa inspirational katika kufikia malengo yake flani (kwa upande wangu,suala la shule) anapoondoka duniani miezi michache kabla ya wewe kufikia lengo hilo.Lakini kwa sie tunaoamini katika mapenzi ya Mungu na usahihi wa maamuzi yake inalazimu kufika mahala kukubali kuwa yote,hata kama machungu kiasi gani,ni MAPENZI YA BWANA.

Blogu hii itaendelea kuwaletea uchambuzi wa masuala mbalimbali,hususan ya kisiasa.Kwa vile tunaelekea kwenye uchaguzi wa rais huko U.S.A,blogu hii itajitahidi kuleta mkusanyiko wa habari mbalimbali.Pamoja na hayo ni picha mbalimbali kutoka Tanzania zilizopigwa katika kipindi cha takriban miezi mitano niliyokuwa huko.

Karibuni tena

Kwa kuanza,kuna hapa chini ni picha kadhaa kutoka angani.Picha ya kwanza ni Addis Ababa kutoka angani,ya pili ni Dar kutoka angani,ya tatu ni Schiphol Airport,Amsterdam na ya mwisho ni Aberdeen Airport.









18 Jul 2008

The family of the late Hon. Richard Mwakasege (MP) of Mbeya Town would like to inform you:

Hon./Rev./Prof./Mr 7Mrs./Mr./Miss.

...............................................................................

That their beloved son Leonard Richard (Ghetto) intend to wed on october 2008. Being a close relative or friend, we kindly ask you to donate to this event.

Please submit your donation to the one who gave you this card before 30th September 2008.



we thank you in advance.



Familia ya Marehemu Mhe: Richard Mwakasege (MB) wa Mbeya Mjini wanayofuraha kukujulisha/kuwajulisha

Mhe./Mch./Prof./Bw & Bi./Bw./Bi.

...............................................

kuwa kijana wao mpendwa

Leonard Richard (Ghetto) anatarajia kubariki ndoa mwezi wa oktoba 2008. Ukiwa kama ndugu, jamaa au rafiki wa karibu tunaomba mchango hali na mali ili kufanikisha shughuli hii.

tafadhali wasilisha mchango wako kwa aliyekupa kadi hii kabla ya tarehe 30/09/2008.

tunatanguliza shukrani zetu.



wasiliana na

Mhe. Salehe Ramadhani Njaa (Advocate) simu 0784-333375

Shaibu Buzohera 0713-333375

Lwitiko Mwalukasa 0754 520353

Everly Mwakyulu 0716 303808

Leonard Richard (Ghetto) 0754 286157.




7 Jul 2008

Binti aitwaye MAGDALENA THOMAS KATIMAKAMU (alias NJEA) anawatafuta Baba yake THOMAS KATIMAKAMU na Mama yake SELINA NDIMINI,ambao inasemekana wanaishi NAIROBI,nchini KENYA.Magdalena,ambaye kwa sasa anaishi Ifakara, alipoteana na wazazi wake mwaka 1989 walipokuja Tanzania mara ya mwisho.Yeyote anayewfahamu wazazi hao anaombwa kufikisha salamu hizo.Kwa mawasiliano zaidi,waweza kutuma barua-pepe kwa [email protected] au sms/simu kwa +255773957709/+255783957709 au +447814843356.Asanteni

Jamaa yangu mmoja mkazi wa Kwa Jongwe (Zimbabwe) kanitumia fedha hii kama rambirambi rambi yake kwa msiba ulionikumba hivi karibuni.

27 Jun 2008

Katika toleo la wiki hii la jarida la Raia Mwema nazungumzia dalili zakutimia kwa utabiri wa Mwalimu Nyerere kwamba upinzani wa kweli unaweza kutoka ndani ya CCM.Kwa namna mambo yanavyokwenda mramba ndani ya chama hicho nidhahiri kwamba kuna tofauti kubwa za kiimani na kimtazamo miongoni mwa viongozi wake.Ili kutokukunyima uhondo zaidi,bingirika na makala hiyo,pamoja na nyinginezo zilizopanda vidato,kwa KUBONYEZA HAPA

19 Jun 2008

Makala yangu katika toleo la wiki hii la gazeti la Raia Mwema inaanza kwa kuwashutumu watangazaji wa radio na runinga za Bongo ambao wanafanya mzaha kwenye shughuli muhimu.Makala inawalenga watangaza taarifa za habari ambao aidha hawajiandai vya kutosha kabla ya news bulletins kiasi cha kuchapia maneno,especially majina ya watu na sehemu,au wanaokuwa too obsessed na sauti za akina Jacob Tesha,Ahmed Kipozi,Ahmed Jongo,Abubakari Liongo,Charles Hillary,nk to an extent wanaishia kusoma madudu badala ya habari.Kuiga sauti sio uhaini lakini kwa kufanya hivyo isiwe sababu ya kusoma vitu vya ajabu.


Pia makala yangu inazungumzia suala zima la ushirikina hapa nyumbani ambapo nimejaribu kulitazama kwa upande mmoja kama mwanafunzi wa zamani wa sosholojia ya dini (sociology of religion) na kwa upande mwingine kama mwanajamii ninayeelewa nini kinanizunguka,hata kama tunaona aibu kukiongelea.Sio siri kwamba mambo ya ushirikina yameshika hatamu sana katika jamii mbalimbali za Kiafrika,lakini hii ya Fisadi Mzee wa Vijisenti kumwaga ndumba ndani ya Bunge inaonyesha jinsi gani mambo yanakwenda mrama sana katika nchi hii tuliyoahidiwa kuwa maisha bora kwa kila aliyezaliwa hapa yanawezekana.Nisikunyime uhodno,bingirika na makala hiyo pamoja na nyingine zilizokwenda shule ya kutosha KWA KUBONYEZA HAPA

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.