24 Oct 2008


Na Peter Edson
JUMUIYA ya Kikristo Tanzania (CCT) imemuonya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe kuwa kauli zake kuhusu kujiunga na Jumuiya ya Kimataifa ya Nchi za Kiislamu (OIC) zinaweza kusababisha mgawanyiko wa kitaifa na kumtaka aachane nazo au ajiuzulu wadhifa wake.

Tamko hilo la maaskofu wa makanisa ya Kikristo imekuja baada ya Waziri Membe kukaririwa akisema kuwa hakuna athari zozote kwa Tanzania kujiunga na taasisi hiyo, ambayo madhumuni yake ni kutetea binadamu na hasa Waislamu na sehemu takatifu.

Membe alisema hakuna haja ya kuwa na woga wa kujiunga na taasisi hiyo wakati katika mchakato wake wakristo na waislamu watanufaika na miradi itakayokuwa ikisimamiwa na OIC, na akashangaa ujasiri wa Watanzania wa kupambana na matatizo umekwenda wapi kiasi cha kuogopa nchi kujiunga na jumuiya hiyo.

Suala hilo liliwahi kuibuka mwishoni mwa utawala wa Rais Ali Hassan Mwinyi wakati vyombo vya habari vilipofichua kuwa serikali ilijiunga kinyemela na jumuiya hiyo. Baadaye viongozi wa serikali walikiri kufanya hivyo kabla ya kujiondoa, lakini safari hii upinzani umekuwa mkubwa zaidi.

Wakitoa tamko lao kwa waandishi wa habari jana, maaskofu hao kutokana makanisa ya kiprotestanti walisema kauli ya Waziri Membe ina lengo la kutetea maslahi ya watu wachache.

Maaskofu hao walisema kwa kuwa katiba ya OIC hiyo inaeleza bayana kuwa italinda mila, desturi na tamaduni za kiislamu, kujiunga na jumuiya hiyo itakuwa ni kukiuka katiba ya nchi inayoeleza kuwa dini ni huru na jambo la hiari la mtu binafsi, na kwamba shughuli ya uendeshaji wa jumuiya za dini zitakuwa nje ya shughuli za mamlaka ya nchini.

"Kama serikali ikikubali, kutakuwa ni mwanzo wa kuruhusu kubomoka na kuvunjika kwa amani ya nchi kwa sababu yanagusa hisia na itikadi za wananchi," alisema Askofu Peter Kitula, ambaye ni makamu mwenyekiti wa kwanza wa CCT.

Askofu Kitula, ambaye alisoma tamko hilo la maaskofu, alisema baada ya kutafakari kwa roho ya kiutume na kinabii wameamua kupinga kuanzishwa kwa mahakama ya kadhi pamoja na mchakato wa kujiunga na OIC.

Alisema katiba ya Tanzania ibara ya 19 kifungu cha 2 inaeleza wazi kuwa kazi ya kutangaza dini, kufanya ibada na kueneza dini itakuwa ni huru na jambo la hiari la mtu binafsi, na shughuli ya uendeshaji wa jumuiya za dini zitakuwa nje ya shughuli za mamlaka ya nchini.

"Ibara hii ni muhimu sana kwa ajili ya kusimamia na kuhakikisha kwamba mambo ya dini yanatenganishwa kabisa na shughuli za uendeshaji wa nchi," alisema.

Alisema sehemu hiyo ya katiba inapingana na ibara ya 1 kifungu cha 11 ya katiba ya OIC kinachosema kuwa jumuiya hiyo inatetea mila, tamaduni na desturi za kiislamu, kuwalinda na kuwaelimisha wananchi kuhusu uislamu nchini, jambo ambalo askofi huyo alisema linaonyesha wazi kuwa kujiunga na IOC itakuwa ni ukiukwaji wa katiba.

Alisema siku za hivi karibuni Bunge la Jamuhuri ya Muungano limekuwa likijadili miswada ya sheria ya kuanzisha au kujihusisha na vyombo hivyo viwili, lakini akasema kuwa kushinikiza kukubalika kwake ndani ya bunge ni kwenda kinyume na katiba.

Naye Owdernburg Mdegela, askofu wa dayosisi ya Iringa ya Kanisa la Kiinjili la Kilutherani Tanzania (KKKT), alisema kitendo cha Waziri Membe kulizungumza jambo hilo bila kulionea haya ni kutetea maslahi ya watu wachache na kuvunja katiba.

Alisema Tanzania ina rasilimali za kutosha hivyo kujiunga na umoja huo kwa lengo la kutafuta misaada ama kutafuta kula na baadaye kupoteza mwelekao wa taifa, ni kujiingiza katika mtego ambao kujinasua kwake kunahitaji gharama ambayo ni kumwaga damu.

"Sisi tunasimama kama viongozi wa kanisa tukimwambia Membe kuwa hafai wadhifa huo, hivyo ni vema akaacha mara moja kutoa kauli zake zisizo na mantiki. Lakini kama hawezi, basi inampasa ajiuzulu," alisema Askofu Mdegela.

Naye askofu wa kanisa pentekoste, Sylivester Gamanywa alisema Waziri Membe anatoa kauli ambazo zina lengo la kuweka hisia binafsi na mgawanyiko wa kitaifa pamoja na kuvunjika kwa amani.

Alisema kitendo cha waziri huyo kusema kuwa serikali inaruhusu fedha chafu na kwamba kama mtu akikuta fedha za shetani inampasa kuzichukuwa, ni kuwadhalilisha Watanzania na taifa lao kwa ujumla.

Naye askofu wa Anglikana, Dk. Stephen Munga alisema kuwa waziri Membe hafai katika kushughulikia masuala ya kitaifa kwani hakuna mamalaka yoyote iliyomuagiza aende kuzungumzia suala la kuaanzishwa kwa OIC.

"Inampasa Waziri Membe afahamu kuwa sisi ni Tanzania na tutafuata mambo yetu na si kuiga masuala ya nje. Anavyosema tuwaige Waganda si jambo sahihi," alisema Dk. Munga.

Alisema kama kanisa msimamo wao ni kuyakataa mambo hayo mawili na kuitaka Serikali na mamlaka zake zote kuacha kuendelea kukaribisha mijadala ya mambo hayo kwani kufanya hivyo ni kupoteza muda wa wenye dhamana ya mamlaka ya nchi hii na rasilimali zake.

"Tunauhakika kuwa yaliyomo ndani ya OIC ni hatari kabisa, kwani endapo yakikubalika katiba ya nchi itakuwa imevunjwa na Watanzania watakuwa wameingia katika migogoro itakayoua maridhiano, mshikamano, utengemano na umoja wa kitaifa," alisema Askofu Kitula.

"Kwa kuzingatia wajibu wetu wa kinabii na kiutume, tunatoa wito kwa bunge kutoruhusu kamwe uanzishwaji wa mahakama ya kadhi kwa kupitia mchakato wa utendaji wa mamlaka ya nchi, pia kutoridhia uanachama wa Tanzania katika OIC."

Akizungumzia tamko la maaskofu, mwenyekiti wa kamati ya msikiti wa Idrissa, Sheikh Ally Basaleh alisema kuwa awali kabla ya kuanza kwa mchakato wa masuala hayo serikali ilishafanya uchambuzi wa kina na kugundua umuhimu wa kuanzishwa kwa vyombo hivyo.

"Kauli za maaskofu hawa na viongozi wa kanisa zinadhihirisha kuwa wanakataa maamuzi yao ya awali kwamba Rais Jakaya Kikwete ni mteule wa Mungu, kwani ndiye anayesimamia masuala haya yote," alisema Basaleh.

Alisema waislamu ni sehemu ya jamii hivyo wao kama viongozi wa dini wanaandaa mchakato wa kutoa tamko litakalokuwa likitoa mchanganuo kuhusu uhalali wa kuanzishwa kwa vyombo vyote hivyo viwili nchini.
CHANZO: Mwananchi


HERE is the story.



CLICK HERE for the story.


SERIKALI ipo katika hatua za mwisho za kuingia ubia na Kampuni ya Sonangol kutoka nchini China kwa ajili ya kuendesha Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL).

Nia hiyo ya serikali ilitangazwa jana kwenye ofisi ndogo za Bunge jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Miundombinu, Mohamed Misanga, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari baada ya kupokea taarifa ya utendaji kazi wa ATCL.

Alisema ATCL, hivi sasa ipo katika hali mbaya kiuchumi kutokana na kuelemewa na madeni sambamba na kutokuwa na mtaji ambao utawezesha kuingia katika soko la ushindani.

Alisema awali serikali ilipozindua upya kampuni hiyo iliahidi kuchukua madeni yote na kutoa mtaji kwa kampuni hiyo, ili iweze kufanya biashara ya ushindani, lakini imeshindwa kutekeleza ahadi yake.

“Hali ya kiuchumi kwa ATCL ni mbaya, serikali imeamua kuinusuru kwa kuingia ubia na Kampuni ya Sonangol International ambayo wakati wowote kuanzia sasa watasaini mkataba,” alisema Misanga.

Alisema wabunge wameionya serikali kuwa makini na mwekezaji huyo, ili ubia huo usije ukawa kama wa kampuni ya SAA ambayo kwa kiasi kikubwa ndiyo iliyosababisha ATCL iwe hoi na kuidai madeni makubwa.

Alisema lengo la wabunge ni kuona serikali haiingi tena katika uingiaji mikataba mibovu ambayo imekuwa isainiwe na wataalamu wa serikali kila kukicha,” alisema Misanga.

Alisema ni jambo la kusikitisha kuwa hivi sasa ATCL imekuwa ikinunua mafuta kwa siku kila ndege inapotaka kufanya safari badala ya kununua mafuta ya muda wa miezi mitatu au minne.

Aliongeza kuwa shirika hilo halikopesheki na kila kinachopatikana hutumika kwa madeni na shughuli za uendeshaji, jambo ambalo hulidhoofisha shirika hilo kununua na kukodisha ndege.

Alibainisha kuwa Serikali tayari imeamua kuiandikia barua Kampuni ya SAA kuitaka iache kuidai ATCL na badala yake iidai serikali ambayo ndiyo iliyoyachukua madeni.

Aidha, alisema ATCL ipo katika mchakato wa kuuza ndege yake aina ya Boeing 737-200 ambayo inadaiwa kutumia mafuta mengi sambamba na kupitwa na wakati.

“Uamuzi huu utasaidia kupunguza gharama zisizo za lazima kwa shirika lakini pia itasidia kupatikana kwa fedha kidogo zitakazotumika kwa mambo mengine,” alisema Misanga.

Aidha, alikanusha kuwa ATCL hakuna ndege mbovu zilizoletwa hivi sasa kwani kuna Mamlaka mbalimbali ambazo huzithibitisha ndege hizo kabla ya kuanza kazi.

CHANZO: Tanzania Daima

Hivi hatuwezi kuwauliza wenzetu Wakenya au Waethiopia kwanini wao wameweza lakini sie tunashindwa?Well,pengine Kenya na Ethiopia ni mbali,if so kwanini tusiwadadisi wazalendo wenzetu wa Precision Air?


Soma kwa makini stori hizi kisha make your own conclusion

STORI YA KWANZA:
Waziri Membe akana kuubeba msalaba OIC
Na Ramadhan Semtawa
WAZIRI wa Mambo Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bernad Membe, amekuja juu akisema baadhi ya watu wamekuwa wakimtwisha mzigo kwamba, ameingiza Tanzania katika Jumuiya ya nchi za Kiislam Duniani (OIC), kitu ambacho si kweli.

Kauli hiyo ya Membe ni ya kwanza kuitoa hadharani tangu kuibuka kwa kasi kwa mjadala huo, ambao unaonekana kuigawa nchi katika misingi ya kiitikadi.

Akizungumzia hilo jijini Dar es Salaam jana, Membe alisema si kweli kwamba Tanzania imekwishajiunga na OIC na wala yeye hajasema lazima ijiunge.

Membe akifafanua huku akionekana kuguswa na tuhuma hizo dhidi yake kutokana na kutamka hilo bunge katika hotuba ya bajeti ya wizara yake, alisema uamuzi wa kujiunga au la, uko kwa wananchi.

"Nimekuwa kimya, kuachia na kusikiliza watu waseme, jamani, Tanzania haijajiunga na OIC wala sijasema lazima ijiunge," alisema na kuongeza:

"Uamuzi wa kujiunga au kutojiunga utakuwa chini ya wananchi, wasomi, NGOs na ninyi waandishi wa habari, ndiyo mtakaoamua."

Membe alikuwa akifafanua kuhusu uhusiano kati ya Tanzania na Iran, ambao unaonekana na baadhi ya watu kama wenye nia ya kuingiza nchi OIC.

Akifafanua zaidi, alisema watu wasiingize vitu visivyokuwa na msingi kwa ajili ya kutunga na kuzungumzia hisia, na kushauri wasome historia kufahamu uhusiano kati ya nchi hizo mbili.

Membe huku akionekana kuchukizwa na fikra mbovu za kupandikiza udini katika nchi, alisema Watanzania ni watu wanaoheshimika duniani kwa umakini wao, ni aibu na haipendezi kujadili udini.

Alisema kama ni kujiunga na OIC ni jambo la kuamua, kwani Uganda ambako kuna Waislam asilimia 10 imeweza kujiunga huku Wakristo wakiwa ni asilimia 66 na wengine wapagani.

"Sasa jamani, msitake kunichinganisha na watu wangu, nawaambieni tena na tena, Tanzania haijajiunga na OIC na haitaweza kujiunga uamuzi huo ni ridhaa ya wananchi," alisisitiza.
CHANZO: Mwananchi

STORI YA PILI KUHUSU SUALA HILOHILO:
Waziri: Tanzania kujiunga OIC ni dhahiri
23 Oct 2008
By Muhibu Said

Tanzania inatarajia kujiunga na Jumuiya ya Kimataifa ya Nchi za Kiislamu (OIC) wakati wowote katika siku zijazo baada ya serikali kuweka bayana azma hiyo jana.

Azma hiyo ya serikali iliwekwa bayana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Seif Ali Iddi, alipozungumza na Nipashe jana, ikiwa ni wiki chache tangu Waziri wa Wizara hiyo, Bernard Membe, aliambie Bunge kwamba, hakuna madhara yoyote kwa Tanzania kujiunga na jumuiya hiyo.


Balozi Iddi alisema mchakato kwa Tanzania kujiunga na OIC, unatarajiwa kuanza wakati wowote na kwamba, hatua ya mwanzo ya mchakato huo, viongozi wa serikali ya Jamhuri ya Muungano watakutana na wenzao wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) kwa ajili ya kupata msimamo wa pamoja kuhusu suala hilo.

Naibu Waziri huyo alisema hayo alipoulizwa na Nipashe kama mchakato kwa Tanzania kujiunga na OIC umeshaanza au la tangu Waziri Membe atoe kauli hiyo bungeni, mjini Dodoma, Agosti 22, mwaka huu.

``Bado hatujaanza mchakato. Kuna kikao tunachotaka kwanza kufanya kwa ajili ya kushauriana na wenzetu wa Zanzibar ili tuwe na msimamo mmoja kuhusu hilo. Ilikuwa tuanze sasa, lakini Mheshimiwa Waziri (Membe) hayupo na Bunge linatarajiwa kuanza,`` alisema Balozi Iddi.

Alisema mchakato kwa Tanzania kujiunga na OIC ni mrefu, ambao unatarajiwa pia kulishirikisha Baraza la Mawaziri kufikia maamuzi.

Balozi Iddi alisema hatua nyingine ya mchakato, ambayo serikali inatarajia kuichukua, ni kutoa elimu kwa umma ili kuwaondoa uoga wote walioonyesha hofu iwapo Tanzania itajiunga na jumuiya hiyo.

``Hao wanaopinga, ni waoga tu, hawajaeleweshwa kwani haina maana Tanzania itakuwa nchi ya Kiislamu. Zipo nchi kama vile Uganda zimejiunga na OIC, lakini hazijabadilika kuwa nchi za Kiislamu. Tutawaelewesha wakati ukifika, tunavyo vyombo vya kuelimisha hilo,`` alisema Balozi Iddi.

Agosti 22, mwaka huu Waziri Membe wakati akifunga mjadala wa hotuba ya makadirio ya mapato na matumizi ya wizara yake, alisema hakuna madhara yoyote kwa Tanzania kujiunga na IOC.

Waziri Membe alisema serikali mwaka huu, ilifanya kikao na Baraza la Wawakilishi kuhusu suala hilo na kugundua kuwa nchi 21 zimejiunga na jumuiya hiyo.

Alisema kati ya nchi hizo, zimo pia nchi za Wakristo ambazo zimejiunga na hazijapata madhara yoyote.
``Tumeshakusanya takwimu za nje na kuona hakuna madhara yoyote ya kujiunga na IOC, bora tu kufuata taratibu,`` alisisitiza Waziri Membe.

Alisema suala hilo lilileta utata awali kwa sababu aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje wakati huo, marehemu Ahmed Hassan Diria, alipeleka ombi la Zanzibar kujiunga kwenye jumuiya hiyo bila kuishirikisha Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Hata hivyo, alisema suala hilo limefanyiwa kazi na serikali na kuona kuwa hakuna madhara kujiunga na IOC.

Siku chache baada ya Waziri Membe kutoa kauli hiyo bungeni, viongozi wa makanisa na baadhi ya wasomi, akiwamo Askofu Msaidizi wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Dk. Methodius Kilaini, walipinga vikali kauli hiyo ya serikali.

Wengine waliopinga suala hilo, ni Askofu Stefano Msangi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Pare, Askofu Mkuu wa Kanisa la KKKT Tanzania, Dk. Alex Malasusa, Mhadhiri Mwandamizi wa Sheria wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Sengodo Mvungi.

Hata hivyo, Imamu Mkuu wa Msikiti wa Mnyamani, Buguruni, jijini Dar es Salaam, Sheikh Mohammed Iddi, amekuwa akijitokeza kuwapinga maaskofu kuhusu kauli zao za kupinga suala hilo.
CHANZO:Nipashe

23 Oct 2008


BATAVIA, Ohio (AdAge.com) -- Conventional polls this year are fraught with doubts -- from the "Bradley Effect" to the elusive cellphone-only households. But one poll based in the all-important swing state of Ohio has never failed since its inception in 1984, and it has Barack Obama with an almost insurmountable lead over John McCain. 

The Busken Cookie Poll, in which the chain of Cincinnati-area retail bakeries sells cookies bearing cartoon images of each candidate, as of Thursday morning had Mr. Obama ahead 6,477 to 3,090 -- a 68% to 32% margin. Daily updates can be found at www.busken.com. 

Unscientific? Perhaps. But Brian Busken, VP-marketing of the family business, said that since the poll's inception in 1984, it has accurately predicted the winner of the presidential election every four years and never been further than 4 percentage points from the final popular vote tally nationwide. (Note: While the website shows a smiling Obama cookie and a frowning McCain cookie, the cookies sold in stores have both smiling.) 

"We've never seen a spread like this before in the numbers," Mr. Busken said. "I don't know if there's going to be a crumbslide or not. ... We may still predict the winner, but probably by way too many cookies." 

Already there are allegations of irregularities. Commenters on a story at the website of the Cincinnati Business Courier allege some bookstores have Obama cookies up front, McCain cookies in the back, and that Remke stores in Northern Kentucky had run out of the McCain cookies. 

Mr. Busken said wholesale sales such as those referenced in the comments don't count. Nor does a recent bulk purchase of 400 McCain cookies by Rob Portman, former Republican congressman and White House budget director. If Acorn buys cookies online for the Dallas Cowboys and their cheerleaders, those don't count either. Only cookies sold in the 11 Ohio stores tracked by the poll count. 

Busken milks the poll, of course, for all the publicity it can get, and has incorporated it into outdoor ads from the Creative Department, Cincinnati. The chain will advertise cookie-poll results on the Norton Digital Network in the area during the four days leading up to the election.




Zaidi kuhusu kioja hiki BONYEZA HAPA.


Serikali imeionya Taasisi ya HakiElimu kuacha kutumia matangazo yake katika vyombo vya habari, kueneza chuki miongoni mwa watoto na vijana nchini na badala yake ingetumia nafasi iliyonayo katika kuwafundisha utawala bora. 

Aidha, imewatahadharisha wote wanaoanzisha taasisi za elimu kwa minajili ya kupata fedha bila kuchangia lolote katika sekta ya elimu, ikiwa ni pamoja na shule zinazotoza wazazi fedha nyingi ambazo hazilingani na mazingira na kiwango cha elimu kinachotolewa. 

Akizungumza wakati wa ziara ya Kamati ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii katika ofisi za Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET), Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Dk. Lucy Nkya, alisema HakiElimu pamoja na kuonywa na kusimamishwa hivi karibuni kutokana na utendaji wake, bado imeendelea kutoa matangazo ambayo yanaeneza chuki kwa vijana. 

Hili tangazo tena linalorushwa hata televisheni ya TBC1 la watoto wa sekondari wanazungumzia EPA, wanafanyiwa hesabu na kisha wanaambiwa waseme hizi hela zingefanyia hili na lile, kumbukeni samaki mkunje angali mbichi, huku ni kueneza chuki kwa watoto hawa,” alisema Dk. Nkya. 

Alisema taasisi hiyo ya HakiElimu inakosea kutumia matangazo hayo kwa upande mmoja tu wa kukosoa. “Mimi nimesomea saikolojia, huu mtindo wa kukosoa serikali kwa namna hii, kunawajengea vijana wetu chuki, badala ya kuwafundisha utawala bora, sasa watoto wanafikiri serikali yote ni mafisadi,” alisema. 

Alisema kutokana na matangazo na vitendo hivyo kwa sasa, hata watoto wa baadhi ya viongozi wamelazimika kuhamishwa katika shule za kawaida na kupelekwa shule nyingine kwa vile wanaitwa watoto wa mafisadi na wenzao. 

Aliitaka taasisi ya TEN/MET kufikisha ujumbe kwa HakiElimu kuwa wanayo nafasi nzuri kuelimisha jamii juu ya masuala ya sekta ya elimu na si kueneza chuki pekee, kwani serikali itafika mahala italazimika kutumia meno yake. 

“Msiisingizie serikali haina demokrasia pindi itakapotumia meno yake, haitokuwa kibogoyo tena,” alionya. Naye Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali wa Zanzibar, Haroun Ali Suleiman, alitaka kufahamu uwezo wa kiutendaji wa mtandao huo wa elimu kwa kuwa haujitangazi, kwani pamoja na yeye kuwa Waziri wa Elimu ndio anausikia. 

Kwa upande wake, Mratibu wa TEN/MET, Joseph Kisanji, alikiri kuwa mtandao huo umejificha na kwamba wanajitahidi kwa sasa kuutangaza kwa kutumia mtindo wao bila kuiga HakiElimu. 

Alisema awali wakati HakiElimu ilipokabiliwa na serikali, takribani asasi nyingi za elimu ziliwatetea ukiwamo mtandao huo. “Hata hivyo, kuna mipaka yake katika kutumia media (vyombo vya habari) kwani zina nguvu na tuliwaambia wenzetu juu ya hilo ila hatuna maamuzi, kazi yetu ni kushauri,” alisema. 

Alisema kama suala la tangazo la EPA limeleta athari hadi kufikia watoto wa viongozi kuhamishwa shule ni jambo hatari, hivyo aliahidi kulifikisha katika Bodi ya Mtandao huo ili walijadili na kulifikisha kwa taasisi hiyo ya HakiElimu. 

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya TEN/MET, Antoine Gizenga, alisema watalivalia njuga suala la HakiElimu kwani mtandao wao unaitazama taasisi hiyo kama asasi inayosaidia kuibua yaliyojificha. 

Mwaka jana, Ofisi ya Waziri Mkuu ilipiga marufuku machapisho na matangazo yanayotolewa na HakiElimu kupitia vyombo vya habari na kutishia kulichukulia hatua kali za kisheria iwapo itakiuka amri hiyo.

CHANZO: HabariLeo




By Samuel Kamndaya 

Annual inflation surged to a 10-year high point of 11.6 percent in September owing to soaring food prices, official data from the National Bureau of Statistics show. 

The inflation rate hit the double digit for the first time in a decade due to skyrocketing food prices in the Holy month of Ramadhan. 

In August this year, the inflation rate was 9.8 percent. The recent surge indicates a 1.8-point increase within a month. In February this year, inflation was 8.9 percent. 

Analysts say the Government would not be able to bring down the inflation rate to seven percent by the end of the current financial year. 

"The seven per cent goal is now unrealistic since, under the current system, Tanzania has nothing in place to control food and fuel prices, the two most dominant factors in the country's inflation basket," said Dr Honest Ngowi who lectures at Mzumbe University. 

He said since the inflationary spiral was mainly on food, fuel and other production factors, it would be very difficult for the country to control it in the short-term. 

"It could be easily contained if it was caused by excess money supply on the market. However, this is due to production factors," he said. 
He said this could worsen considering that the holiday season was just around the corner. 

Dr Semboja Haji of the University of Dar es Salaam's Economic Research Bureau (ERB) also said: "Inflation will now be fluctuating between 10 and 12 percent. It requires magic for the government to bring it back to seven per cent," he said. 

He criticised the government for having no mechanism in place to protect the country from the negative effects of economic developments outside. 

Food makes over 55 percent of Tanzania's inflation basket. But Dr Semboja suggested that the development was due to bad policies. 
"I find no reason why food prices in Tanzania should be going up while we have a capacity of producing enough to meet the local demand as well for exports," he said. 

He urged the government to have price mechanisms for sensitive products like food and fuel. 

He cited the Energy and Water Utilities Regulatory Authority (Ewura), saying it should understand that local companies were colluding to increase prices even when there was nothing to force them to increase the prices. 

In that respect, the don said, there was no reason to stick to the concept of market pricing while companies were conspiring among themselves to increase prices willy-nilly.


SOURCE: The Citizen

22 Oct 2008


Barack Obama akifanikiwa kushinda urais hapo Novemba 4 atakuwa ameweka historia kwa kuwa Mweusi wa kwanza kuwa rais wa Marekani.Lakini mafanikio ya Obama yanawasumbua wachambuzi wa siasa (hususan za tabia za uchaguzi wa Marekani).Hayawasumbui kwa vile Obama na wao ni wabaguzi.La hasha,bali ni namna hisia kwamba Bradley effect ingemwangusha zinavyoelekea kuwa wrong.

Nilishakiri katika post yangu moja huko nyuma kwamba awali nilitamani Hillary Clinton apitishwe kuwa mgombea wa Democrats.Sababu yangu kuu ilikuwa ni katika hofu kwamba Obama angeshinda nomination basi Weupe wangeungana bila kujali itikadi zao kuhakikisha mtu mweusi haingii White House.Baada ya kumbwaga Hillary,nililazimika kukubaliana na busara za stadi za siasa kwamba lolote linawezekana katika fani hiyo.

Tukirejea kwenye kinachowasumbua wachambuzi wa siasa ni namna Bradley effect inavyoelekea kushindwa kuwa na impact kwa Obama,hasa kipindi hiki ambacho sio tu anapambana na Mweupe bali Mweupe kutoka chama cha weupe wahafidhina (Republican).Kuna wanaoamini kwamba Bradley effect ni uzushi (myth) wa aina flani.I dont.Lakini kama sio myth basi kwanini Obama anazidi kupaa kwenye opinion polls?

Binafsi nadhani hii ni REVERSE BRADLEY EFFECT.Yaani,wapiga kura Weusi hawaonyeshi dhamira zao hadharani (kwa wanaochukua opinion polls) kwamba watamsapoti Mweusi mwenzao.Kwa lugha nyingine,wanashusha matarajio ya support ya Weusi kwa Mweusi mwenzao.Lakini kwa vile Weusi ni wachache Marekani,na hata kama wangefanya nacho-hypothesize hapo juu bado wasingeweza kuifanya hali kuwa kama ilivyo sasa,nachoamini zaidi ni tabia "mpya" ya Weupe kudai hadharani kuwa hawajaamua wampigie kura nani (undecided) au Weupe (hasa wa Republicans) kuongopa hadharani kwamba wanamsapoti McCain ilhali dhamira na sapoti yao ni kwa Obama.

Weusi wa Obama ni issue kwenye uchaguzi huu,nami ni muumini wa hoja kwamba kama Obama angekuwa Mweupe basi muda huu tungeshafuta uwezekano wa McCain kuwa rais hapo Novemba.Kwanini nasema hivyo?Wamarekani wengi wamechoshwa na Republicans na uhafidhina kwa ujumla.Bush ameendelea kuwa one of the most unpopular US presidents ever,na Democrats wanaonekana kama ndio watakaoleta ufumbuzi wa matatizo ya Marekani.Sababu zote hizo ni tosha kumfanya mgombea anayekubalika wa Democrats kuwa mbali sana kwenye kura za maoni.Kwanini Obama anamwacha McCain kwa wastani wa kura 10 tu?Jibu la haraka ni Weusi wake.

Whether Bredley effect ni hype au ndio ujio wa Reverse Bredley effect itajulikana baada ya exit polls hapo Novemba 4.However,no matter what happens to Obama,alipofika ni historia tosha,japo itanoga zaidi akishinda kiti hicho.

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.