22 Mar 2009


Na Khamis Mkotya

MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA), imesema orodha ya majina ya watumishi wasio waaminifu kwenye kitengo cha kudhibiti mapato bandarini (TISCAN), bado haijawasilishwa Makao Makuu kama ilivyoahidiwa na Rais Jakaya Kikwete. Akizungumza Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Elimu kwa Walipa Kodi, Protus Mmanda, alisema Menejimenti ya TRA chini ya Kamishna Mkuu, Hary Kitillya, inayasubiri majini hayo kuweza kuchukua hatua stahili.

Mmanda alisema, watumishi wote wa TRA watakaotajwa kwenye orodha hiyo watashughulikiwa kwa mujibu wa sheria na taratibu zote za nidhamu, ikiwa ni pamoja na kufukuzwa kazi kama Rais alivyoagiza. Machi 2, mwaka huu, Rais Kikwete alifanya ziara ya ghafla bandarini kukagua utekelezaji wa maagizo yake kuhusu ufanisi katika utendaji kazi wa bandari ya Dar es Salaam, hasa kuhusu mrundikano wa makontena. Katika ziara hiyo, Rais alionyesha kukerwa na baadhi ya watumishi wa TISCAN ambao wamekuwa wakishirikiana na wafanyabiashara wakubwa kuwaonyesha mbinu za kukwepa kodi, vitendo vinavyolisababishia taifa hasara. Rais Kikwete alisema, orodha ya watumishi wanaoendekeza mchezo huo mchafu anayo na kumtaka Kamishna Mkuu wa TRA, kuwafukuza kazi watumishi hao atakapokabidhiwa majina.

Orodha ya majina hayo bado haijafika kwetu, tunaendelea kusubiri sijui yatakuja lini, maana mimi kwa wadhifa wangu siwezi kwenda Ikulu kuuliza majina hayo yataletwa lini. “Labda kwa kuwa nyinyi waandishi wa habari mnakutana na Salva Rweyemamu, (Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu) muulizeni hayo majini yatakuja lini, lakini sisi huku hatuwezi kuuliza, hadi hapo yatakapoletwa,” alisema. Mmanda alisema kuwa, wakati majina hayo yanasubiriwa, TRA imechukua hatua kadhaa zinazolenga kuweka mfumo mzuri wa utendaji, ikiwa ni pamoja na kufanya mabadiliko kwa baadhi ya maofisa wake.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi huyo, TRA imeshafanya mabadiliko kwa kuwahamisha idara baadhi ya maofisa wake, wanaoonekana kuwa na chembe za ukosefu wa maadili kama hatua za awali za kutekeleza maagizo ya Rais. “Hatuwezi kukaa tu bila kufanya tathimini yoyote juu ya utendaji kazi wetu, kwa sababu tunasubiri majina kutoka kwa Rais. Baadhi ya hatua tulizochukua ni pamoja na kufanya mabadiliko katika baadhi ya idara zetu. “Tumefanya marekebisho pale palipostahili, mahala palipokuwa na watumishi wazembe wasiokuwa waadilifu tumewaondoa na kuweka watumishi wengine,” alisema Mmanda, ingawa hakutaja idara na maofisa wake walioguswa na zoezi hilo.

Mkurugenzi huyo alisema, hatua nyingine zilizochukuliwa ni pamoja na kurahisisha taratibu za usajili wa magari, kuondoa kero ya muda mrefu ambayo imekuwa ikilalamikiwa kuhusu uchelewashaji wa usajili wa magari. Kwa mujibu wa Mmanda, taratibu zote za usajili wa magari yanayoingizwa nchini hivi sasa zitafanywa na ofisi moja, ili kuondoa usumbufu kwa watu, tofauti na zamani ambako taratibu hizo zilikuwa zikishughulikiwa na ofisi zaidi ya moja. Alisema kuwa, utaratibu huo mpya pia utasaidia kuondokana na watu wa ‘kijiweni’ maarufu kwa jina la ‘vishoka’, ambao wamekuwa wakiwatapeli watu kwa kisingizio cha kuwasaidia katika taratibu za usajili wa magari.

CHANZO: Mtanzania


21 Mar 2009


THISDAY REPORTER
Dar es Salaam

CONTROVERSY surrounds the mysterious disappearance of a large consignment of local currency notes with a value running into millions of Tanzanian shillings, as it was being airlifted into the country from Germany on a Qatar Airways flight.

Sources within the Bank of Tanzania (BoT) have confirmed the apparent large-scale theft which was discovered on arrival at the Julius Nyerere International Airport in Dar es Salaam early last week.

It has yet to be established exactly at what point the consignment of bank notes got stolen whether it was in Germany, where the notes were manufactured; in Doha, where the flight made a stopover; or at the final JNIA destination in Dar es Salaam.

According to THISDAY findings, the consignment contained crisp new bank notes of 10,000/- denomination. However, the exact number of such notes involved � and hence the total value of the package � could not be immediately verified.

’’The consignment arrived at the airport in Dar es Salaam on the evening of Monday, March 9. But because the following day was a Maulid holiday, it could not be dealt with until Wednesday, March 11. That’s when it was discovered that the notes were gone,’’ said an informed BoT source.

It is understood that besides the new 10,000/- notes, the consignment also contained a substantial amount of old local currency notes that had long been removed from circulation.

Said the source: ’’The old notes were under audit query...during an earlier auditing exercise, the auditors wanted to know why these notes had not been returned for so many years since being sent to the printers overseas because of various technical problems.’’

But it remains unclear of what use the old notes long out of circulation were expected to be at this moment in time, or whether the government or central bank has received or is expecting any compensation from the company manufacturing the notes.

The discovery of a consignment of defective Tanzanian currency notes with a total value of 3.5bn/- back in 2001, led to serious repercussions including the launch of an official investigation by the then Prevention of Corruption Bureau (PCB).

However, no arrests or prosecutions were ever made.

The notes were printed by the German company Glesecke & Devrient Gmbh, on behalf of the Bank of Tanzania (BoT). They were of 1,000-shilling denomination, amounting to a total value of $3,237,492.

Following this scandal, the government vetoed central bank plans to award another print order to the same German firm, while the defective notes were said to have been quietly withdrawn from circulation.


SOURCE: ThisDay

The first black chief executive of a FTSE 100 Index company was appointed when insurer Prudential named Tidjane Thiam as its next boss...MORE

17 Mar 2009


By Mkinga Mkinga

The Government is assessing the impact of the global financial crisis on the Tanzanian economy.

The deputy minister for Finance and Economic Affairs, Mr Omar Yusuf Mzee, told The Citizen yesterday by phone that officials from his ministry had been dispatched to regions to talk to stakeholders on problems facing them as a result of the global financial crisis.

"I am in Kigoma on a similar mission and my colleague [deputy minister Jeremiah Sumari) is in southern regions," he said.

The assessment is aimed at collecting crucial information on the crisis. He said his tour would take him to Kigoma, Tabora, Singida and Dodoma regions while Mr Sumari would visit Lindi and Mtwara regions to gather similar information.

"We need to know the real picture when we call stakeholders to a national meeting to discuss the crisis.During the meeting we will focus on how we can help businesses which have been affected," he said.

He said a national roundtable with chief executive officers of various firms to discuss the situation would be held soon after completing the assessment.

Bank of Tanzania (BoT) Governor Benno Ndulu, did not say what the Government could do to shore up businesses amid the crisis.

"I cannot say that the Government will offer stimulus packages to affected businesses. But we are aware of the situation and we are planning something for our local entrepreneurs," he said. Prof Ndulu said BoT was closely following the developments.

He noted that so far there was no indication that local banks would face difficulties in the near future as a result of the global crunch.

"People should go on with their activities; there is no need to worry as we are closely following the developments here and abroad. In case of any serious problem, we will issue an alert immediately," he said.

Recently, Finance and Economic Affairs minister Mustafa Mkulo did not rule out direct Government intervention, as members of the business community called for a state plan to save them from collapse.

He said during the forthcoming roundtable meeting, the Government would discuss with CEOs and draw up a joint strategy to deal with the problem.

"Our intervention will be within the limitations of the budget and it is my hope, as the Finance minister, that our engagement will be effected as soon as possible. It should be before the conclusion of the budget proposals," he said.

"If employers are thinking of retrenching workers, this will be discussed to see the best way in which the Government could assist," said Mr Mkulo.
Many countries are offering stimulus packages to private companies.

Such countries include the United States where the financial crunch started, sending financial institutions crumbling.The ministry has dispatched its team to regions at a time when businesses are calling for quick plans to remedy the situation.

The Association of Tanzania Employers (ATE) has confirmed that it had received urgent appeals for assistance from three companies. ATE executive secretary Aggrey Mlimuka warned of difficult times ahead unless the Government intervened.

The Tanzania Horticultural Association bemoans a 50 per cent business slump.It has urged the Government to support the small-scale growers and supply chains using a portion of the money that President Jakaya Kikwete pledged to give to agriculture.

It has also asked for the rescheduling of loans through commercial banks with BoT's intervention.
SOURCE: The Citizen

EACH REGION HAS A REGIONAL COMMISSIONER,REGIONAL ADMINISTRATIVE SECRETARY,REGIONAL PLANNING OFFICER,etc,etc,...AND SO ARE THE DISTRICTS.DOES THIS DECISION TO DESPATCH OFFICIALS FROM THE MINISTRY SUGGEST THAT THOSE AT REGIONAL/MUNICIPAL/DISTRICT LEVEL HAVE NO IDEA ABOUT THE GLOBAL FINANCIAL CRISIS THAT THEY CAN'T FURNISH THE GOVERNMENT WITH THE DATA NEEDED FOR THE ECONOMIC ASSESSMENT,OR THEY ARE TOO DUMB TO TALK TO STAKEHOLDERS IN THEIR RESPECTIVE ADMINISTRATIVE AREAS, OR IT IS ALL ABOUT THE NOTORIOUS PER DIEM SYNDROME AT THE TIME WHEN WE SERIOUSLY NEED TO KEEP OUR EXPENDITURE IN CHECK...!?

16 Mar 2009












KIPINDI CHA INSIDE AFRICA CHA CNN WIKI HII KINA SEGMENT KUBWA KUHUSU TANZANIA.MOJA YA YALIYONIVUTIA KATIKA KIPINDI HICHO NI MAHOJIANO KATI YA RIPOTA WA CNN,DAVID MCKENZIE, NA MSANII WETU NAKAAYA SUMARI.MWANADADA ALIJIELEZA CONFIDENTLY.I WISH NINGE-RECORD VIDEO LAKINI KWA SABABU ZILIZOKUWA NJE YA UWEZO WANGU NILIAMBULIA PICHA HIZO HAPO JUU.UKIPATA WASAA UNAWEZA KUCHEKI VIDEO YA SEGMENT HIYO KWENYE TOVUTI YA CNN-INSIDE AFRICA PINDI WATAKAPOIWEKA (HADI MUDA HUU BADO HAIJAWEKWA).PENGINE BAADA YA KUANGALIA SEGMENT NZIMA UNAWEZA KUBAKI NA MASWALI,LIKE I DID, KUHUSU ASSESSMENT YA RIPOTA HUYO WA CNN KUHUSU MWENENDO WA UCHUMI WETU.



13 Mar 2009


BARAZA Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA), limeibua upya hoja za kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi na Tanzania kujiunga na Jumuiya ya nchi za Kiislamu Duniani (OIC), kwa kuitaka serikali kutafakari kwa kina na hekima juu ya kuridhia kuanzishwa kwa vyombo hivyo.

Kuibuka tena kwa hoja hizo kumekuja miezi michache baada ya Rais Jakaya Kikwete kufunga mijadala hiyo iliyokuwa ikielekea kuwagawa wananchi kwa misingi ya kidini.

Hoja hizo zimeibuliwa juzi kwenye Baraza la Maulid na Naibu Katibu Mkuu wa Utawala wa Bakwata, Suleiman Lolila, ambaye aliitaka serikali iangalie upya na kwa hekima na kama inawezekana iharakishe masuala hayo mawili.

“Tunaipongeza serikali kwa hekima kubwa na jitihada inayoitumia katika kushughulikia masuala ya Mahakama ya Kadhi na Tanzania kujiunga na OIC, Waislamu wanangoja kwa hamu na shauku kubwa ridhaa ya serikali, Inshallah, tunaiombea serikali ipate wepesi katika masuala haya maridhawa.

“Tunawaomba Waislamu wadhamirie kwa dhati katika suala hili la OIC na mahakama ya kadhi kwa kutokuruhusu mwanya wowote wa mifarakano miongoni mwetu, kwani mifarakano itakaribisha mgawanyiko na utengano miongoni mwa jamii,” alisema Lolila.

Naibu Katibu Mkuu huyo, akisoma risala ya Bakwata mbele ya Rais mstaafu wa Awamu ya Pili, Alhaji Ali Hassan Mwinyi, alisema ili kuridhiwa kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi na OIC kuna hitaji utulivu wa hali ya juu miongoni mwa waumini wa dini zote mbili (Waislamu na Wakristo) ili kuipa serikali nafasi ya kufanya maamuzi ya busara kwa lengo la kuimarisha umoja wa kitaifa miongoni mwa jamii.

Suala la uanzishwaji wa mahakama ya Kadhi na Tanzania kujiunga na OIC, mwishoni mwa mwaka jana lilizua mjadala mpya nchini, baada ya kufika bungeni na kutishia kuwagawa wabunge kwa itikadi za kidini.

Oktoba mwaka jana katika hotuba yake, Rais Kikwete, hakutaka kuweka wazi ni lini Tanzania itaridhia kujiunga na OIC pamoja na uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi, na badala yake aliwatuliza wananchi kwa kuwaambia wavute subira wakati serikali ikilifanyia kazi suala hilo kwa masilahi ya umma.

Rais Kikwete aliweka bayana kuwa ni mapema mno kuanza kutoa uamuzi wa masuala hayo, kwa kuwa bado utafiti haujakamilika pamoja na serikali kutotoa uamuzi wa mwisho, hivyo hakuna sababu kwa wananchi kulumbana.

11 Mar 2009


Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi amepigwa kofi na mmoja wa watu waliohudhuria Baraza la Maulid wakati akihutubia katika ukumbi wa Diamond Jubilee Dar es Salaam jana.Mwinyi, ambaye alimwakilisha Rais Jakaya Kikwete katika Baraza hilo, alikutwa na masaibu hayo baada ya kijana aliyefahamika kwa jina la Ibrahim Said (26) kwenda jukwaani akajifanya fundi na kumpiga kofi la nguvu Rais mstaafu.

Kijana huyo aliyekuwa miongoni mwa umati uliohudhuria baraza hilo, aliinuka wakati Rais mstaafu akizungumzia masuala ya Ukimwi na kwenda hadi jukwaani na kujifanya anarekebisha vyombo vya kupaza sauti vikiwemo na vya televisheni alivyokuwa akitumia kuhutubia.Kijana huyo ambaye alikuwa amevalia suruali ya khaki na shati jeupe, alitumia sekunde kadhaa kujifanya kutengeneza vifaa hivyo akiwa mbele ya Mwinyi na ghafla alimzaba kibao. Kitendo hicho kilisababisha viongozi waliokuwa jukwaani, kusimama ghafla na wanausalama kuingilia kati na kumkata mtama kijana huyo katika juhudi za kumdhibiti asiendelee kuleta madhara.

Miongoni mwa watu waliokuwa katika jukwaa kuu ni pamoja Sheikh Mkuu Mufti Issa Shaaban Simba, Kaimu Mufti Suleiman Gorogosi na Waziri Mkuu mstaafu, Rashidi Kawawa ambao wote walibaki katika mshangao. Baada ya wanausalama kumdhibiti kijana huyo waumini walimwagika na kuanza kumtwanga kwa ngumi na mateke na hivyo wanausalama ikabidi wabadili majukumu na kuanza kumhami. Kutokana na hekaheka hizo shughuli za hotuba zilisimama kwa dakika kama nne.

Pamoja na vurumai hizo, wanausalama walifanikiwa kumuingiza kijana huyo katika gari aina Land Cruiser yenye namba za usajili T 531 AUB na kuondolewa katika viwanja vya Diamond Jubilee na kufikishwa Kituo cha Polisi cha Selander Bridge. Kwa mujibu wa Polisi ambaye hakutaka kutaja jina lake kituoni hapo, alisema katika kumhoji, kijana huyo (Said) alijitambulisha kuwa ni mkazi wa Mabibo Farasi, Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa hizo zilizopatikana kituoni hapo, Said ni mzaliwa wa Mkoa wa Dar es Salaam aliyehitimu kidato cha Sita mwaka juzi katika Shule ya Sekondari ya Wavulana ya Tabora. Kijana huyo katika maelezo yake, amejitambulisha kuwa ni Mwalimu wa masomo ya ziada katika Kituo cha Ngome Kongwe, kilichoko Mabibo. Hata hivyo, haikuweza kufahamika sababu za kijana huyo kufanya kitendo hicho kutokana na waandishi kushindwa kupata nafasi ya kuzungumza naye.

Awali, kabla ya kijana huyo kumpiga kofi kiongozi huyo mstaafu wa kitaifa, Mwinyi alikuwa akiwaasa Waislamu kuepukana na ngono zembe zinazochangia ongezeko la Ukimwi. Alisisitiza kwamba ugonjwa huu umekaa mahali pabaya na kuwasihi waumini kuwa ni jukumu la kila mmoja kujilinda. Akizungumza na waandishi wa habari, Kaimu Mufti Gorogosi, alisema amekuwa akimuona kijana huyo katika mikutano ya dini.

"Hata jana (juzi) katika Maulid usiku alikuwepo, hivyo nashindwa kuelewa kama ana akili nzuri au la," alisema Gorogosi. Alimwomba Rais mstaafu awasamehe Waislamu kwa tukio hilo. Wakati huo huo, Joseph Lugendo anaripoti kwamba Mwinyi amewataka viongozi wa dini nchini kujenga daraja la upendo, baina ya waumini wa dini tofauti badala ya kugeuka kuwa kuta zenye kuwagawa Watanzania katika misingi ya dini.

Aliwataka viongozi hao, wakiwamo masheikh na mapadri, kujenga daraja la upendo na masikilizano baina ya waumini wa dini mbalimbali, ili kuendeleza amani na mshikamano uliopo nchini. Akihutubia mkesha wa Maulid ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (SAW) usiku wa kuamkia jana Dar es Salaam, Mwinyi alionya viongozi hao wasigeuke kuwa kuta zisizopenyeka zitakazogawa Watanzania kwa misingi ya dini zao.

"Tupo hapa Waislamu na wasio Waislamu kwa kuwa ushirikiano Tanzania ni jadi na mila yetu, sisi huungana kusherehekea siku zote, Waislamu husherehekea na Wakristo siku ya Pasaka na Krismasi na wao hutuunga mkono kwenye Idd zote."Hili ni jambo jema linaloondoa chuki baina ya dini na kuleta mshikamano, mimi napendezwa sana na mwenendo huu na ninatoa mwito kwa mapadri na masheikh kuliendeleza," alisema Mwinyi.

Alisema hawezi kuisemea dini ya Kikristo kwa kuwa haifahamu, lakini miongoni mwa mafunzo yao ni kuwa na subira na kusamehe na kuongeza kwamba mafundisho yao (Wakristo), yamewataka anayepigwa kofi shavu moja ageuze na lingine lipokee kofi la pili. "Huu ni mfano wa kuepusha shari. Lakini na sisi Waislamu pia Mungu katutaka kuwatendea mema na uadilifu ambao hawakupigana nasi wala hawakututoa majumbani kwetu, hakika Mungu huwapenda waadilifu," alisema Mzee Mwinyi huku akinukuu baadhi ya aya kuongeza nguvu katika hoja yake hiyo.

Alisema msingi wa kuishi kwa amani, huanzia katika kaya mpaka jamii na ndio uliosababisha Tanzania kuwa kisiwa cha amani kilichozungukwa na nchi zenye vurugu na kutaja kuwa dini zimechangia kuunda msingi huo. Hata hivyo, alisema kauli hiyo haina maana kuwa nchi zisizo na amani hazina dini, bali malezi ya Watanzania yaliyotekelezwa na viongozi waliotangulia, pia yamechangia sehemu ya amani iliyopo. "Wazee wetu walitandika zulia la utamaduni wa kuishi kwa amani, upendo na utulivu ... katika hali hii ya utu uzima wangu, inanituma kuwausia vijana, tutunze utulivu huu.

"Katu tusiruhusu uondoke tusiwape wenzetu sababu ya kutupa majina mabaya, ya mjahidina na magaidi, vijana nakuusieni tena tusitoe mwanya huo, tumekuwa tukipewa majina na maadui wa nje. "Wanasema dini yetu ni ya fujo, ni wakati wa kushikamana na si wa kulumbana na kama mnajadiliana si mbaya ila kuwepo na staha, heshima na pasiwepo kejeli, ubabe wala dharau dhidi ya dini nyingine," alisema Mwinyi.


CHANZO: Habari Leo


AJALI HUTOKEA,LAKINI LINAPOKUJA SUALA LA ULINZI WA VIONGOZI AJALI ZINAPASWA KUZUIWA KWA GHARAMA YOYOTE ILE.TULISIKIA YALIYOJIRI MBEYA HIVI KARIBUNI AMBAPO KUNDI LA WANANCHI WALIURUSHIA MAWE MSAFARA WA RAIS JK.KWA MTAZAMO MPANA,TUKIO HILO LINGEWEZA KUTAFSIRIWA KAMA SEHEMU YA MAPUNGUFU KATIKA ENEO ZIMA LA ULINZI WA VIONGOZI WETU.NASEMA HIVYO KWA VILE KUNA WATU WENYE JUKUMU LA KUHAKIKISHA USALAMA WA NJIA AU ENEO ATAKALOPITA KIONGOZI,NA NI KWA UHAKIKA KUTOKA KWAO ONLY,NDIPO MSAFARA AU ZIARA YA KIONGOZI ITAENDELEA KAMA ILIVYOPANGWA.THANKS GOD,HAYO MAWE HAYAKUMDHURU YEYOTE,NA PENGINE LA KUSHUKURU ZAIDI NI KWAMBA YALIKUWA MAWE TU NA SIO SILAHA.
SASA TUNASIKIA MZEE MWINYI NAE AMEKUMBWA NA ZAHAMA KAMA INAVYOELEZWA KATIKA HABARI YA HAPO JUU NA PICHANI HAPO CHINI.INAFAHAMIKA KWAMBA ULINZI WA VIONGOZI HUWA MGUMU ZAIDI KWENYE MIKUSANYIKO AU MIKUTANO YA HADHARA LAKINI KWA KAWAIDA UGUMU HUO UNAPASWA KUWA CHANGAMOTO YA MAFANIKIO YA SHUGHULI NZIMA YA KIONGOZI HUSIKA.TUNAPASWA KUMSHUKURU MUNGU KWAMBA ALICHOPIGWA NACHO MZEE MWINYI NI KIBAO TU,LAKINI KAMA TUKIENDELEA NA "BUSINESS AS USUAL" KUNA SIKU ITAKUWA TINDIKALI AU KITU KINGINE CHENYE MADHARA.KAMA MTU HUYO ALIWEZA KUPIGA KIBAO,NI DHAHIRI KWAMBA ANGEWEZA HATA KUCHOMA KISU AU KURUSHA RISASI.KUMKATA MTAMA MHUSIKA WAKATI AMESHAFANYA MADHARA NI SAWA NA KUSOMA RAMBIRAMBI YENYE MANENO MAZURI WAKATI MTU AMESHAPOTEZA UHAI:INALIWAZA LAKINI HAISAIDII.

(Aliyemzaba kibao Mzee Mwinyi akidhibitiwa baada ya tukio.Wajuzi wa mambo ya ulinzi wa viongozi wanaweza kuafikiana nami-kutokana na picha hii-kwamba kuna mapungufu LUKUKI.Picha ya tukio kwa hisani ya MICHUZI Jr)

NI ISHARA NYINGINE KWAMBA KUNA MAPUNGUFU MAHALA FLANI.YAYUMKINIKA KUHISI KWAMBA MAPUNGUFU HAYO NI MATOKEO YA MAZOWEA.KUNA WATU WANATEKELEZA MAJUKUMU YAO KWA MAZOWEA,KWAMBA KWA VILE JANA ILIFANYIKA HIVI BASI HATA LEO ITAFANYIKA HIVYOHIVYO.DHANA YA "HOPE FOR THE BEST EXPECT THE WORST" INAONEKANA KAMA POROJO TU KWA WANAOENDEKEZA MAZOWEA.

TUSIFIKE MAHALA TUKALEWESHWA NA "AMANI NA UTULIVU".KUNA MENGI YANAYOJIRI HUKO MITAANI YANAYOASHIRIA KWAMBA KIWANGO CHA FRUSTRATIONS KWENYE UMMA KINAONGEZEKA.FOR THAT MATTER,KUNA UMUHIMU MKUBWA WA KUENDESHA MAMBO KULINGANA NA HALI HALISI BADALA YA KUONGOZWA NA HISIA AU IMANI ZISIZOZINGATIA REALITY.

IT CAN BE DONE...BUT IF AND ONLY IF SOMEONE OUT THERE PLAYS THEIR PART.



10 Mar 2009

The winner of a pancake-eating contest has dropped dead while accepting his prize for gorging on 43 of the banana and cream stuffed desserts. Boris Isayev, 48, from west Russia died on stage moments after winning the competition to mark the end of Butter Week.

The contest, which took place in the town of Chernyakhovsk, was part of festivities to celebrate Maslenitsa, the last week before the period of Lent starts. According to local traditions, meat, fish, dairy products and eggs are forbidden during Lent, as well as dancing and parties.Witnesses described Mr Isayev as "the most active participant in the contest" adding that he "ate all the types of pancakes on offer and won fairly".

The witness added: "He had really enjoyed the pancakes but then he started foaming at the mouth and went down like a sack of stones.

"People have fainted during the contests before."

Medics tried to revive Mr Isayev after he collapsed while collecting his prize on stage. The exact cause of death is not clear but doctors believe he choked after a piece of pancake got lodged in his throat. Celebrations are said to have continued after Mr Isayev's body was taken away in an ambulance.


SOURCE: Sky News

8 Mar 2009

Bonyeza HAPA kwa habari na video.

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.