8 Oct 2009

Mambo mengine huku Ughaibuni ni vituko vitupu.Kuna watu wanafuga majoka makubwa na kuyalea kama watoto wao,kuna wanaofuga panya mithili ya paka,na wengine wamegeuza tumbili kuwa watoto wa kambo.Na matunzo wanayopewa mbwa na paka hayatofautiani sana na anasa wanazofaidi watoto wa wabaka-uchumi wetu (mafisadi).

Kuna vijibwa flani vimekuwa kwenye chati kwa muda mrefu kutokana na kushebedukiwa na watu maarufu.Nadhani ushakiona ki-chihuahua cha Paris Hilton,kijibwa kidogo mithili ya paka.Sasa imeibuka fasheni mpya ya “kitimoto pimbi”,yaani nguruwe wadogo kupindukia.

Jioni hii kipindi cha Live From Studio Five katika kituo cha runinga cha Channel Five kimezungumzia fasheni hiyo mpya ambayo kwa hakika inaweza kuzua songombingo na maustaadhi pindi ikitua Bongo,almaaruf kwa ku-copy na ku-paste mengi ya yanayojiri anga hizi.






Manji, Jeetu wagombea matrekta

• Homa ya Kilimo Kwanza

na Mwandishi Wetu

WAFANYABIASHARA wawili maarufu hapa nchini wenye asili ya Kiasia, Yusuf Manji na Jayantkumar Chandubhai Patel, maarufu kwa jina la Jeetu Patel, wanadaiwa kuingia katika mzozo mkubwa wa kibiashara wakati wakigombea kupata zabuni ya mradi wa kuingiza nchini na kusambaza matrekta, wenye thamani ya zaidi ya sh bilioni 50.

Habari ambazo Tanzania Daima Jumatano limezipata kutoka vyanzo vyake vya habari vya kuaminika zimeeleza kuwa, Manji na Patel ambao wanadaiwa kuhusika kwa namna moja au nyingine katika kuomba zabuni hiyo, sasa wanawindana huku wakitishana kumalizana kibiashara.

Baadhi ya watu wa karibu na wafanyabiashara hao mabilionea waliozungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti katika siku za karibuni walieleza kuwa, kumekuwa na jitihada za chini kwa chini zinazofanywa na wapambe wao kuvujisha katika vyombo vya habari mbinu zao wanazotumia kupata zabuni kubwa za serikali.

Mfanyabiashara mmoja maarufu ambaye yuko karibu na wafanyabiashara hao, alilieleza gazeti hili kuwa, mabilionea hao sasa wamekuwa mahasimu baada ya kuzidiana ujanja katika zabuni hiyo ambapo kila mmoja anatishia kutoa siri za kibiashara za mwenzake.

“Sasa wanatishana, kila mmoja anatishia kutoa siri za mwenzake kibiashara. Wote wanapata tenda kubwa kutoka serikalini, wanavyozipata wanajua wao. Kinachotushangaza kila mmoja anasema atamuanika mwenzake,” alisema mfanyabiashara huyo aliyeomba jina lake lisitajwe.

Taarifa za ndani kutoka kwa watu walio karibu na Manji, zinadai kuwa mfanyabiashara huyo hakufurahishwa na jinsi mchakato wa upatikanaji zabuni hiyo ulivyoendeshwa, na sasa anakusudia kuvujisha katika vyombo vya habari taratibu zilizokiukwa katika mchakato wa utoaji wa zabuni hiyo.

Zinadai kuwa, Manji anajiandaa kuweka wazi jinsi sheria ya manunuzi ya umma ya mwaka 2004 ilivyokiukwa wakati wa mchakato wa utoaji zabuni hiyo.

Katika mradi huo, Jeetu ambaye anatajwa kuwa mwakilishi wa Kampuni ya Escort hapa nchini, yenye makao makuu yake nchini India, ambayo imeshinda zabuni hiyo, anadaiwa kuwashawishi maofisa wa juu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) ambalo limekabidhiwa jukumu la kuutekeleza mradi huo na serikali, kuipatia kampuni hiyo.

Habari hizo zimedai kuwa, Jeetu alifanikisha mpango huo baada ya kuwaunganisha maofisa kadhaa wa ngazi za juu wa JKT na watendaji wakuu wa Escort walioko India, ambao baada ya kuhakikishiwa kupewa zabuni hiyo, waliwaalika maofisa kadhaa wa JKT kwenda nchini humo kwa ajili ya kusaini mkataba wa utekelezaji wa kazi ya kusambaza matrekta hapa nchini.

Taarifa zaidi zilidai kuwa, tayari baadhi ya viongozi wa juu wa JKT wamekwisha safiri hadi India kusaini mkataba huo.

Hata hivyo, inadaiwa kuwa, Manji anapinga hatua ya viongozi wa JKT kwenda kusaini mkataba huo nchini India, ikizingatiwa kuwa baadhi ya watendaji wa serikali wamekwishalalamikiwa kwa kusaini mikataba inayohusu miradi ya kitaifa nje ya nchi.

Aidha, inadaiwa kuwa, baadhi ya habari zinazotarajiwa kusambazwa zitakuwa zinahoji ukiukwaji wa taratibu kwa kutoa zabuni hiyo pasipo kuitangaza kama sheria ya manunuzi ya umma inavyoelekeza, licha ya Baraza la Mawaziri kuujadili mradi huo na kutoa baraka kwa JKT kuutekeleza.

Kwa upande wa Jeetu, taarifa zinadai kuwa, anajiandaa kujibu tuhuma za aina yoyote zitakazotolewa katika vyombo vya habari, zikiwa na lengo la kuichafua Kampuni ya Escort au zinazohusu upatikanaji wa zabuni hiyo.

Baadhi ya maofisa wa serikali waliozungumza na Tanzania Daima Jumatano kuhusu suala hilo walieleza kuwa, serikali ina taarifa kuhusu jambo hilo na inalifuatilia kwa karibu ili kuhahakisha hakuna taratibu zinazokiukwa katika utekelezaji wa mradi huo.

Mmoja wa maofisa wa ngazi za juu serikalini aliyezungumza kwa sharti la kutotajwa jina lake alieleza kuwa, anafahamu kuwa Serikali ya India ilitoa mkopo usiokuwa na riba, wa zaidi ya sh bilioni 50 kwa Serikali ya Tanzania kwa ajili ya kununulia matrekta, wakati Makamu wa Rais, Dk. Ali Mohamed Shein, alipofanya ziara nchini humo mapema mwaka huu, kwa sharti la kulipwa katika kipindi cha miaka 10.

Alisema sharti jingine lililotolewa katika kutoa mkopo huo, linaitaka Serikali ya Tanzania kuhakikisha inanunua matrekta hayo kutoka kampuni za India na si vinginevyo.

Ofisa huyo alisema, serikali iliamua kuikabidhi JKT jukumu la kusimamia utekelezaji wa mradi huo ili kuondoa mazingira yoyote ya kutokea udanganyifu katika kuutekeleza.

Hata hivyo, alieleza wasiwasi wake iwapo kuna taarifa za baadhi ya maofisa wa JKT waliokabidhiwa jukumu la kusimamia utekelezaji huo, kuzungumza na mwakilishi wa Kampuni ya Escort hapa nchini (Jeetu), kisha wakaipa kampuni anayoiwakilisha zabuni hiyo bila kufuata taratibu.

“Hili jambo linaweza kuharibu kabisa sifa ya JKT kama litakuwa kweli, kwa sababu itakuwa ni kashfa kubwa kwa jeshi kukiuka taratibu za manunuzi ya umma. Ingawa kuna imani kuwa si rahisi mambo ya kijeshi kuchunguzwa, lakini hili liko wazi mno kwa sababu ni zabuni iliyo wazi iliyokuwa ikifuatiliwa na wafanyabiashara wengi, hivyo hao hao wanaweza kuwa wametoa siri za taratibu kukiukwa,” alisema ofisa huyo.

Waziri mmoja aliyezungumza na gazeti hili hivi karibuni, alisema suala hilo lilizungumzwa katika Baraza la Mawaziri na kupatiwa baraka zote za kulitekeleza. Aliongeza kuwa, anaamini hakuna taratibu zilizokiukwa.

Hata hivyo, alionya kuwa Baraza la Mawaziri linazo taarifa za mfanyabiashara mmoja maarufu kufanya mpango wa kutoa taarifa za uongo kuhusu mchakato wa upatikanaji zabuni hiyo kwa sababu ya kisasi cha kukosa zabuni hiyo.

Tanzania Daima Jumatano lilipowasiliana na Ofisa Habari wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Nadhifa Omary, ili kupata ufafanuzi wa suala hilo, alisema jambo hilo linaweza kuzungumziwa na waziri tu kwa sababu ya unyeti wake.

Alieleza zaidi kuwa, hawezi kulizungumzia kwa sababu yuko nje ya ofisi kwa mapumziko, hivyo hana maelezo ya kina ya kulitolea ufafanuzi.

Alipoulizwa, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga, Dk. Hussein Mwinyi, alisema analifahamu vizuri suala hilo na alilihakikishia gazeti hili kuwa, hakuna utata wowote katika utekelezaji wa mradi huo, isipokuwa linaweza kufanywa ajenda ya kuchafuana na watu ambao wana malengo binafsi na mradi huo.

“Ninalijua vizuri jambo hilo, tenda zilitangazwa na zikafunguliwa, nakuhakikishia. Mimi mwenyewe niliona kampuni kama 11 hivi zilizoomba zabuni hiyo, sasa kama kuna mtu anasema kulikuwa na kasoro, ni mambo ya wafanyabiashara kutaka kuchafuana tu kwa malengo binafsi waliyonayo katika mradi huo,” alisema.

Naye Manji alipotafutwa kupitia simu yake ya kiganjani ili kuzungumzia suala hilo, kwa mara kadhaa ilikuwa ikipokelewa na wasaidizi wake na kueleza ameweka utaratibu wa kutoongea na waandishi wa habari mpaka inapobidi.

CHANZO: Tanzania Daima

NILIWAHI KUANDIKA HUKO NYUMA KWANZA HUU WIMBO WA "KILIMO KWANZA" HAUNA TOFAUTI NA USANII WA "MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA."NGONJERA ZA KISIASA ZINAZOHANIKIZWA NA KAULI-MBIU MWANANA HAZIWEZI KUMKOMBOA MTANZANIA KATIKA LINDI LA UMASIKINI UNAOMKABILI.BADALA YAKE,JITIHADA KUBWA ZINAHITAJIKA KATIKA KUPAMBANA NA UFISADI NA MAFISADI,VIKWAZO VIWILI VIKUU VYA MAENDELEO YETU.HILO HALIWEZEKANI CHINI YA UTAWALA WA CCM KWA VILE CHAMA HICHO NI KITALU MWAFAKA KWA MAZALISHO NA HIFADHI YA UFISADI NA UFISADI.

HAWA WAHINDI WAMEGEUZA TANZANIA KAMA SEHEMU YA MAJARIBIO YA KILA MADUDU YANAYOWAJIA KICHWANI.WAMENABAKA UCHUMI WETU HUKU TULIOWAKABIDHI DHAMANA YA KUULINDA WANAENDELEA KUWANYENYEKEA KUTOKANA NA NJAA YAOYA TENI PASENTI.

MWAKA WA HUKUMU 2010 UNAKARIBIA.USIREJEE MAKOSA YA 2005,PLEEEEEZ!

6 Oct 2009


NILIWAHI KUBASHIRI HUKO NYUMA KWAMBA KADRI 2010 INAVYOSOGEA NDIVYO TUTAVYOZIDI KUSHUHUDIA VITUKO.LEO HII MAKAMBA NAE AMEJIUNGA KATIKA VITA DHIDI YA UFISADI!HIVI SI BINADAMU HUYU ALIYEWATAKA WATANZANIA KUACHANA NA MIJADALA YA UFISADI KWA VILE BAADHI YA WAHUSIKA WAMEFIKISHWA MAHAKAMANI?

HEBU MSIKIE ALIVYOGEUKA KINYONGA KATIKA HABARI HII HAPA CHINI:

Makamba ahimiza mapambano dhidi ya ufisadi

na Jacob Ruvilo, Kigoma

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Yusufu Makamba, amesema ufisadi unapaswa kupigwa vita na kila Mtanzania mzalendo, kwani umechangia kwa kiasi kikubwa kudidimia maendeleo ya nchi.

Makamba alisema hayo juzi kwenye semina ya viongozi wa CCM Jimbo la Kigoma Mjini iliyofanyika katika viwanja vya Lake Tanganyika.

Alisema suala la watu kujipatia mali kinyume cha utaratibu na kuhujumu nchi havina uhusiano wowote na CCM, kwani watuhumiwa wote hawakuagizwa na chama kufanya hivyo, bali ni hulka zao binafsi.

Makamba alifafanua kuwa suala la muumini wa dhehebu fulani kwenda kinyume na maadili au amri ya vitabu vya dini, hapaswi kulaumiwa sheikh au mchungaji, badala yake ni muumini husika ambaye mwisho wa siku ndiye atakayepata adhabu kwa Mungu.

Aidha, Makamba alisema suala la vyama vya upinzani kushika bango na kuidhihaki CCM kuwa ni mafisadi kutokana na viongozi wachache wasio waaminifu, halina maana, bali suala la umoja na mshikamano katika kupinga mafisadi hao ni jukumu la watu wote, ikiwamo CCM.

Mbali na hilo, Makamba alikemea baadhi ya viongozi wa chama hicho kutumia uwezo wao wa fedha kutoa rushwa ili kupita katika chaguzi mbalimbali kuwa ni moja ya upatikana wa viongozi mafisadi na wasiofaa kwa jamii.

Alisema Tanzania haikuandaliwa kutawaliwa na wenye nacho na kwamba hali hiyo inaweka tabaka la mwenye nacho na asiyenacho, hali ambayo isipoangaliwa kwa umakini suala la rushwa litabaki kuwa ndoto.


TATIZO LETU WATANZANIA NI UWEPESI WETU KUAMINI KILA KINACHOAHIDIWA.MWAKA 2005 MAKAMBA NA CCM YAKE WALITAMBUA HILO NA KUJA NA AHADI LUKUKI IKIWEMO ILE MAARUFU YA KULETA MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA.SASA WANASEMA KWAMBA SUALA LA MAISHA BORA LILIANZA ZAMA ZA MWALIMU NYERERE,PENGINE KATIKA KUKWEPA KUTUELEZA HAYO MAISHA BORA WALIYOAHIDI ILIKUWA NI KWA MAFISADI PEKEE AU...?MAANA KAMA SUALA HILO LILIASISIWA NA NYERERE BASI WANGETAMKA BAYANA WAKATI ZA KAMPENI ZA 2005 BADALA YA KUIFANYA KAULI-MBIU MUHIMU ILIYOWAZUGA WATANZANIA NA KUTOA USHINDI MKUBWA KWA CCM.

NI MUHIMU KWA WAPIGA KURA KUTAMBUA KUWA WANASIASA WETU WANAWEZA KUAHIDI LOLOTE ILI WAPATE KURA KAMA ILIVYOSANIFISHWA KWENYE WIMBO WA "NDIO MZEE" WA PROFESA JAY.

TUSIREJEE MAKOSA YA 2005,PLEEEEZ!


The media as the source of information has the power influence public opinion. But before getting into how it might, it is important to know what my understanding of public opinion. I would define public opinion as the opinion shared by the majority of the public. Majority because it is almost impossible to find an absolutely agreed opinion among people with different social and economic background, racial differences, age, gender, etc. Gauging public opinion is normally done by using opinion polls, which as we all know, are merely representative of opinions shared by different groups in a given society, or in research terms, population.

If a study that is measuring public opinion on the impact of global warming finds 75% of respondents thinks that global warming possess a major threat to the future of mankind, it would then be concluded as “the study found that global warming is actually a threat to the future of mankind.”Public opinion is more about what many, and not necessarily all, think about something rather than what each of us think.

Take an example of the Loch Lomond “myth.” Majority of those who believe about the Loch Lomond monster have not even been to Scotland, let alone Loch Lomond itself. One of the reasons for the publicity of the myth has been the stories we frequently hear of read, or hear from, the media. The publicity has led to many us believing the existence of the Loch Lomond monster. If there were an opinion poll on whether people believe there is actually a monster there, the results could very likely be “yes” mainly because a larger section of the media has led us to believe that way.

As the public is made of individuals, it is difficult for each of them to make their opinions known, hence the usefulness of the media in giving a medium for a rather general collection of what each of us think about something. If manipulated, the media could as well lead us into believing that majority of us something is the way it is because many think so. Neglecting deviants, many people tend to be conformists in the sense that they normally do not want to look different from what the majority’s position. Therefore, as the Americans were led to believe by a section of the US media that the Saddam Hussein’s regime was actually linked for the 9/11 atrocities, rather than a neo-con agenda spearheaded by the likes of Donald Rumsfield, Richard Perle and Paul Wolfowitz,so does a section of the British public becomes influenced in their opinion by The Sun, The Daily Express, The Daily Telegraph and The Daily Mail that asylum seekers and refugees as actually among the causes of the country’s economic problems.

A biased media could in short or long run effectively influences public opinion because it communicates what “A” thinks in Derbyshire and “B” thinks in Lanarkshire. Or in an international perspective, what Maggie thinks in Glasgow and Evarist thinks in Dar es Salaam, Tanzania. It is even more effective in shaping public opinion in the less educated or less informed section of society that normally takes what is said by the media for granted.

During the 2005 general election campaigns in Tanzania, the ruling party courted the media to publicise a story that a neighbouring country’s army was planning to invade Tanzania. The ruling party then went on urging reminding the voters how the country emerged victorious in the 1978-79 war against Uganda under its (the ruling party’s) leadership. Some analysts believe that although the gimmick did not directly determine the outcomes of the election it all the same helped the ruling party to identify itself to voters as one they could rely on during uncertain times.

Exploiting the ineffectiveness of the Kenyan political situation in which a coalition of opposition parties successfully broke an “African political taboo” that a ruling party never loses an election, CCM-Tanzania’s ruling party-has frequently used the media during elections to tell voters that bringing an opposition into power could not solve the country’s problems, referring to the Kenyan situation. The pro-CCM media has also been telling Tanzanians that regardless of how bad they think of CCM, it still is the “devil they know”, and therefore should never try a political experience of voting an opposition party into power. Many would agree despite proving wrong in some African countries such as Ghana the trick has been very successful.

The pro-government media in Sudan has also been effective in swaying public opinion in favour of President Al-Bashir when he a warrant was made by the International Criminal Court in The Hague accusing him of being responsible for genocide in the Darfur region. The media working under the directives of the Sudanese government portrayed the warrant as an attempt by the West to re-colonise Africa.

Although public opinion could also shape opinion in the media, it is rather for commercial purposes than public interest. When The Daily Mail ran an exclusive story about an “illegal immigrant” employed by Baroness Scotland, it fair to believe that based on its strong anti-immigration stance, it did not do so to sympathise with the plight faced by those who make a choice of being in the UK illegally but rather to amass pressure to force the peer out of office.

If we agree that although the media the primary source of information broadcasted or published by the media comes from the public, and therefore a need to see the media serves the interest of the public, it still remains true that the flow information has usually been from the media to the public in terms of news consumption. The point here is that the media collects information from the public not for final consumption but rather for the public consumption. It is on such views that I argue that it is the media which shapes public opinion, and not vice versa.


5 Oct 2009


KWANGU,MISINGI MIKUU YA NYERERE ILIKUWA UJENZI WA JAMII YENYE USAWA NA INAYOTHAMINI UTU WA BINADAMU.UHURU BILA USAWA NI POROJO.UMOJA KATIKA LINDI LA UMASIKINI NI SAWA NA USINGIZI WA PONO KWENYE UTANDO WA BUIBUI.NA MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA HAYAWEZI KUPATIKANA KATIKA SIASA ZA KUKUMBATIA MAFISADI SAMBAMBA KUKEMEA WAPAMBANAO NA UFISADI,KUTOJUA VIPAUMBELE VYA NCHI,NA KUENDELEZA AHADI ZA MAENDELEO ILHALI ZILE ZA AWALI HAZIJATEKELEZWA.

JK AMEKUMBUKA MISINGI YA MWALIMU.MSOME KATIKA HABARI IFUATAYO:

Mwandishi Maalum, Mwanza

RAIS Jakaya Kikwete ametaja misingi mikuu mitatu iliyowekwa na Baba wa Taifa, Hayati Julius Nyerere katika kulijenga taifa la Tanzania, misingi ambayo rais alisema ni kumbukumbu yao kuu kwa kiongozi huyo wa harakati za Uhuru wa Tanganyika.

Rais Kikwete aliwashangaa Watanzania ambao wanabeza Uhuru wa Tanzania na kufurahia wakati jina la Tanzania linaposhambuliwa na wageni.

Aliitaja misingi hiyo mikuu kuwa ni uhuru, umoja wa taifa la Tanzania, na safari ya kujenga maisha bora kwa kila Mtanzania iliyoanza hata kabla ya Tanganyika kupata uhuru wake rasmi Desemba 9, 1961.

Rais Kikwete alisema hayo mjini Mwanza juzi alipozungumza na vijana wa CCM ambao wanaanza safari ya kuelekea kijijini Butiama mkoani Mara, ikiwa ni matembezi ya kumuezi Mwalimu Nyerere ambaye alifariki miaka 10 iliyopita baada ya kuugua saratani ya damu.

Mwalimu Nyerere alifariki Oktoba 14, 1999 akiwa amelazwa hospitali ya St Thomas jijini London, Uingereza.

Vijana 166 kutoka mikoa yote ya Tanzania wanashiriki katika matembezi hayo ya siku 10 ambayo yatapitia njia ambayo Mwalimu Nyerere alitembea mwaka 1967 katika kuunga mkono na kuhamasisha Azimio la Arusha.

Kauli mbiu ya matembezi hayo ni “Uhuru na Kazi” na miongoni mwa mambo ambayo vijana hao watafanya njiani ni kukarabati Shule ya Msingi ya Mwisenge ambako Mwalimu Nyerere alipata elimu yake ya msingi.

Rais Kikwete alisema kuwa urithi mkuu ambao Mwalimu aliwaachia Watanzania ni misingi hiyo mikuu ambayo imeendelea kulifanya Taifa la Tanzania kuwapo na kuwa imara.

Rais Kikwete alisema kuwa kila taifa duniani lina waasisi wake ambao wanastahili kuendelea kukumbukwa siyo tu kwa uasisi pekee, bali pia kwa mambo ambayo waliyasimamia, waliyaamini na waliyajenga.

"Wamarekani wanaye George Washington… sisi tunaye Mwalimu Julius Kambarage Nyerere… na kila nchi ina muasisi wake ambaye anakumbukwa kwa aliyoyasimamia," alisema JK.

"La kwanza la kumkumbuka Mwalimu ni uhuru wa nchi yetu. Huyu alikuwa ni kiongozi aliyeambiwa achague kati ya siasa ama kazi ya ualimu… huyu mzee wetu akachagua siasa na utumishi wa umma bila hata kujua atakula nini.

"Akachagua kupigania uhuru wa nchi yetu. Kama mnavyojua nyote hii kazi ya siasa ni kamari... unakwenda kugombea ukijua kuna kupata ama kukosa... lakini yeye alifanya uamuzi sahihi wa kupigania uhuru,"

Rais Kikwete alisema kuwa uhuru siyo mipaka bali ni heshima ya nchi na ndiyo maana Tanzania haitasita kumkabili yoyote ambaye atajaribu kuchezea uhuru huo.

Alisisitiza: "Mwaka 1978 yule msanii na profesa wa historia na jiografia, Idi Amin alivamia nchi yetu… na sisi tukamfurumusha ili kulinda uhuru wetu na wako wenzetu ambao walipoteza maisha yao kwa ajili ya kulinda uhuru wetu. Wamelala Kaboya (mkoani Kagera) na tutaendelea kuwaenzi kwa sababu walijitolea kulinda uhuru wetu."

Rais Kikwete pia aliwashangaa watu wote ambao wanafurahia wakati heshima ya Tanzania inapobezwa na wageni.

"Uhuru siyo mipaka kama nilivyosema. Uhuru ni heshima ya taifa letu. Wako wale wenzetu wanaofurahi wakati wageni wanaposhambulia nchi yetu. Ni wajibu wetu sote kuhakikisha kuwa uhuru wetu hauchezewi na mtu yoyote,"alisema.

Kuhusu umoja wa taifa, Rais Kikwete alisema Mwalimu alihakikisha kuwa uhuru wa nchi unazaa umoja ili nchi iwe moja na isigawanyike vipande vipande kwa sababu yoyote ile.

"Aliondoa viashiria vyote vya kuvunja umoja wa taifa tokea mwanzo kabisa. Aliondoa uchifu ili kuondoa nguvu za ukabila. Alitambua hatari ya dini na akataifisha shule zote za dini ili vijana wetu waelimishwe na kulelewa kama vijana wa taifa moja na siyo vijana wa dini tofauti,"alisema Kikwete.

Rais Kikwete alisema kuwa hata kabla ya uhuru, Mwalimu alitambua kuwa ili uhuru na umoja viweze kudumishwa ni lazima wananchi wake wapate maisha bora na ndiyo maana akawatambua maadui wakuu watatu – ujinga, maradhi na umasikini- na njia za kukabiliana na maadui hao.

CHANZO:
Mwananchi

BAADHI WANAHOJI KUHUSU MANTIKI YA UHURU ALIOPIGANIA BABA WA TAIFA NA WENZAKE.TULIMKIMBIZA MKOLONI ILI TUJITAWALE NA KUFAIDI RASLIMALI ZETU KWA HAKI NA USAWA.JAPO SIO EXCUSE,LAKINI MKOLONI HAKUTUJALI KWA VILE HAKUWA MTANZANIA.LEO HII WANAOTUTENDA VIBAYA ZAIDI YA WAKOLONI NI WATANZANIA WENZETU,WENGI WAO WAKIWA WALIOSOMOSHWA KWA SHIDA NA FEDHA ZA WATANZANIA WENZAO.KUNDI JINGINE NI LA MABWANYENYE WALIOPTA URAIA KWA VIJISENTI VYAO NA WAKOLONI -MAMBOLEO WALIOREJEA KWA JINA LA WAWEKEZAJI.NYERERE HAKUPIGANIA UHURU ILI WAGENI WAJE NA DOLA MOJA NA KUONDOKA NA MAMILIONI YA DOLA,AU AKINA LOWASSA KUTUINGIZA MKENGE KWENYE RICHMOND,NA USANII MWINGINE WA KISIASA.

UHURU PASIPO UONGOZI BORA NI SAWA NA KUWA NA VOGUE LENYE DEREVA MLEVI AU KIPOFU;LITATUMBUKIA MTARONI KAMA SI KUPORWA NA MAJAMBAZI.UHURU ILHALI TUMEBANWA NA NIRA ZA MAFISADI NI UTANI MBAYA KWA WALIOPIGANIA UHURU WA NCHI YETU.WEZI WA KAGODA WAMEHIFADHIWA HADI LEO,MASHIRIKA YA UMMA YAMEGEUKA KICHAKA CHA WATU KUHUJUMU KISHA WABADILISHIWE (REJEA MATTAKA NA ATCL),WAZEMBE WANAENDELEA KULINDWA KWA VILE TU KUWABADILISHA KTATHIBITISHA MAPUNGUFU YA ALIYEWATEUA IN THE FIRST PLACE,NA HADITHI NYINGINE ZA KUSIKITISHA.

HATUKUPIGANIA UHURU KUPATA HESHIMA FEKI MACHONI MWA JUMUIYA YA KIMATAIFA BALI AMANI NAFSINI NA MIILINI MWETU KAMA WATANZANIA.


AONDOLEWA JUKWAANI, ASEMA NI UCHOVU WA SAFARI

Frederick Katulanda, Mwanza na Exuper Kachenje, Dar

RAIS Jakaya Kikwete jana alizidiwa ghafla wakati akihutubiwa waumini wa Kanisa la African Inland (AICT) kwenye Uwanja wa CCM Kirumba na kulazimika kukatisha hotuba yake na baadaye kuondolewa uwanjani akiwa amebebwa na walinzi wake kabla ya kiongozi huyo kurejea jukwaani muda mfupi baadaye.

Rais Kikwete, ambaye alifika mkoani hapa akitokea Arusha ambako alifungua mkutano wa Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola, ikiwa ni siku chache tangu atoke Marekani kuhudhuria mkutano wa Baraza la Umoja wa Mataifa, alikumbwa na mkasa huo majira ya saa 6:29 mchana.

Rais Kikwete alikatisha hotuba yake wakati akianza kuelezea suala la kudumisha amani upendo na mshikamano, akisema:"Wakati nilipokuwa nikipita kuomba ridhaa yenu kuongoza nchi hii, kote nilikopita niliomba kudumishwa kwa amani upendo na mshikamano…"

Ghafla alinyamaza na baadaye ikasikika sauti kutoka kwenye kipaza sauti chake ambayo inaonekana kuwa ya mlinzi wake, iliyosema "Kakae".

Baadaye Rais Kikwete aliuliza kwa sauti akisema "naweza kuhutubia nikiwa nimekaa"na kujibiwa na mwenyeji wake, Askoku Mkuu wa AICT, Daniel Nungwana kuwa "unaweza kukaa", jibu ambalo lilifanya aondoke kwenye eneo ambalo alikuwa akitumia kuhutubia jukwaani na kwenda kukaa meza kuu ambayo ilikuwa umbali wa takriban mita mbili.

Mara baada ya kukaa na vipaza sauti kurekebishwa ili aendelee na hotuba, Rais Kikwete alitamka kwa sauti ya juu iliyoonyesha kuwa afya yake si nzuri wakati alipoeleza kuwa “nimechoka sana kwa sababu ya safari” na kisha kuendelea na hotuba yake, lakini sauti yake ilizidi kubadilika na kuwa inayokwaruza na akakatisha hotuba yake, akiacha waumini wakinong’ona.

Baadaye Rais Kikwete, ambaye aliwahi kupoteza nguvu jukwaani wakati akihitimisha kampeni zake za uchaguzi kwenye viwanja vya Jangwani jijini Dar es salaam, alinyamaza na kutulia huku akiwa anaangalia upande wa mashariki, shingo yake ikilalia bega la kushoto na kichwa kuegemea kwa mkuu wa mkoa wa Mwanza, Abbas Kandoro.

Dakika chache baadaye (saa 6: 35), mlinzi wake ambaye alisimama nyuma ya kiti chake, alimtikisa kwa muda, lakini rais hakuonekana kujibu kitu na ndipo walinzi wake na maofisa wengine wa usalama walipomzunguka kumkinga kuzuia watu wasimuone na baadaye kumbeba juu na kumpeleka kwenye chumba maalumu kilicho eneo la jukwaa kubwa la Uwanja wa CCM Kirumba.

Wakati akiingizwa chumbani humo, magari yote ya msafara wake yalielekea nje ya uwanja huo na kuegeshwa nje ambako kuna mlango, jambo lililoashiria kuwa iwapo afya yake isingetengemaa, angetolewa kupitia mlango huo na kukimbizwa hospitali.

Wakati harakati hizo zikiendelea, Kandoro alirejea jukwaani na kuelekea kwenye kipaza sauti. Kandoro aliwataka wananchi kutulia kwa maelezo kuwa hali ya rais ni nzuri na kwamba amepumzika kwa muda kutokana na uchovu.

"Nawaomba mtulie, Rais wetu amepumzika tu kwa muda kutokana na uchovu wa safari na yuko salama. Nawahakikishia kuwa yuko salama na huu ni uchovu tu kwani amesafiri sana kutoka nje ya nchi hadi Arusha na baadaye kuja hapa Mwanza. Hivi sasa amepumzika na atarudi hapa," alieleza Kandoro.

Kikwete alirejea jukwaani majira ya saa 6: 45 akitembea bila ya msaada wa walinzi ambao walikuwa nyuma yake na kwenda kukaa kwenye meza kuu ambako aliomba kipaza sauti na kusema maneno machache.

"Ndugu wachungaji na waumini, nguvu imerudi; nataka kutumia fursa hii kuzindua mfuko wenu maalumu; nami nachangia shilingi milioni moja,"alisema Kikwete na kuamsha kelele za shangwe na vigelegele.

Baadaye ratiba ya sherehe hizo iliendelea kwa harambee ya kuchangia mfuko maalumu wa watu wenye ulemavu wa ngozi ambao aliombwa na Askofu Nungwana kuchangia kwa kuuzindua kabla ya hotuba yake.

Askofu Musa Mwagwesela aliwatangazia wananchi kuwataka wajitokeze kuchangia mfuko huo kwa kipindi cha dakika tano, ili wamruhusu rais aondoke uwanjani hapo. Alisema ameombwa kufanya hivyo na watu wa usalama.

Zoezi hilo la wananchi na watu mbalimbali kuchangia mfuko huo liliendelea na majira ya saa 7:08 mchana Rais Kikwete aliombwa na mwenyeji wake Askofu Daniel Nungwana kuwashukuru wananchi kabla ya kuondoka.

Aliposimama Rais Kikwete alisema: "Kwanza nawaombeni radhi kwa mshtuko niliopata. Lakini umenitokea kwa ubishi wangu; ni kwa ajili ya uchovu wa safari."

Kikwete aliendelea kusema: "Nimerudi juzi saa 7:00 usiku. Nilikuwa Arusha kwenye mkutano wa bunge, walinishauri nipumzike nikasema ahaa hawa nao ngoja niende tu; waliniambia tunaona uchovu mwingi, nikasema hawa nao ahaa… nitaweza tu; nimekuja hapa… siku nyingine nitawasikiliza wanaonishauri."

Hii si mara ya kwanza kwa Rais Kikwete kukumbwa na mikasa hadharani. Aliishiwa nguvu ghafla wakati akihutubia mkutano wa mwisho wa kampeni kwenye uchaguzi mkuu mwaka 2005. Alitolewa viwanja vya Jangwani na kwenda kupatiwa matibabu.

Lakini saa chache baadaye CCM ilitoa taarifa kuwa afya ya mgombea wake wa kiti cha urais ni nzuri na kwamba, mkasa huo ulitokana na rais kuwa alifunga na uchovu wa safari nyingi za kampeni hizo.

Alikumbana na mkasa mwingine mjini Mwanza Oktoba 15, 2005 wakati akiwa kwenye kampeni za kuwania kuingia Ikulu. Alikuwa akisimikwa kuwa mtemi wa kabila la Wasukuma kabla ya mtu mmoja, Lucas Omahe Garani, 34, ambaye ni mganga wa jadi, kujipenyeza hadi jukwaani na kujaribu kumvuta miguu, lakini akawahiwa na watu waliomzunguka Kikwete.

Alikuwa akisimikwa utemi na kikundi cha waganga kutoka Kituo cha Utamaduni wa Kisukuma cha Bujora ambacho kinamilikiwa na Kanisa Katoliki, Jimbo Kuu la Mwanza.

Garani, ambaye kwa sasa anatumikia kifungo cha miaka 13 jela kutokana na kosa hilo, alidai kuwa alifanya kitendo hicho kupinga uamuzi wa kikundi hicho cha waganga kumsimika chifu hadharani na mchana, kitu ambacho alidai kinakiuka mila za kisukuma.

Garani mkazi wa Mtaa wa Nyakabungo jijini Mwanza alikuwa anafanya kazi ya kutunza bustani ya ofisi za Dayosisi ya Victoria Nyanza ya Kanisa la Anglikana.

Kabla ya kuzidiwa na kukatisha hotuba yake jana, Rais Kikwete alilipongeza kanisa hilo kwa kutimiza miaka 100 na kwa kutoa huduma mbalimbali katika sekta ya afya na elimu.

Alisema serikali inatambua mchango wa mashirika ya dini na kusisitiza kuwa unapotaja maendeleo ya nchi hii, huwezi kukwepa mchango huu wa mashirika ya dini.

Hali haikuwa shwari kwa wananchi waliokuwa kwenye uwanja huo licha ya matangazo ya Kandoro kuwa afya ya rais ni nzuri. Kulikuwa na minong'ono mingi kutokana na kila mmoja kuuliza nini kimetokea kabla ya Askofu Mussa Magwesela kuwaambia waumini kuanza maombi maalumu kumuombea rais kutokana na hali iliyomkumba ghafla.

"Waumini wote naomba tumuombee mpendwa rais wetu; tumuombee Mungu amrejeshee afya yake,"alisema na mara moja waumini wakaanza maombi ya mmoja mmoja.

Hata hivyo, taarifa iliyotolewa baadaye na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu ilidai kuwa Rais Kikwete alilazimika kupumzika kwa dakika chache "baada ya kumaliza hotuba yake” katika sherehe hizo kutokana na kuzidiwa na uchovu.

"Nguvu imerudi…napenda sasa kuchukua nafasi hii kuzindua rasmi uchangiaji wa shughuli za kanisa lenu na mimi naanza na mchango wa Sh 1,000,000," taarifa hiyo ya Ikulu ilimkariri Rais Kikwete ikieleza kuwa baada ya mapumziko mafupi alirejea na kuendelea kushiriki shughuli hiyo.

Ilieleza kuwa Kikwete alianza kusikia uchovu wakati akisoma hotuba yake mbele ya maelfu ya waumini wa Kanisa hilo.

Taarifa hiyo inaeleza: "Mheshimiwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete leo, Jumapili, Oktoba 4, 2009, amelazimika kupumzika kwa dakika chache katika chumba cha mapumziko kwenye Uwanja wa Kirumba mjini Mwanza mara tu baada ya kumaliza hotuba yake wakati wa sherehe za miaka 100 tokea kuanzishwa kwa Kanisa la African Inland (AICT) nchini Tanzania.

"Mhe. Rais amelazimika kupumzika kutokana na kuzidiwa na uchovu kufuatia shughuli nyingi mfululizo katika siku za karibuni. Baada ya mapumziko hayo, Mhe. Rais aliendelea kushiriki katika shughuli hizo hadi mwisho wa shughuli hiyo ya AICT."

Taarifa hiyo inaeleza kuwa Kikwete alikiri kupata matatizo hayo, akisema kuwa yalitokana na kutofuata ushauri wa wasaidizi wake waliomtaka apumzike baada ya kurejea kutoka Marekani. Taarifa hiyo imeeleza kuwa washauri walimtaka asiende Arusha kufungua mkutano huo wa mabunge na baadaye kumzuia asiende Mwanza.

Taarifa hiyo ya Ikulu inasema: "Kwa kweli mshtuko huu wa leo ni matokeo ya ubishi wangu. Nilishauriwa na wasaidizi wangu nipumzike baada ya kurejea nyumbani kutoka Marekani. Niliambiwa nisiende Arusha ama kuja hapa. Lakini nikakataa. Siku nyingine nitawasikiliza zaidi."

Taarifa hiyo ya Ikulu imeeleza kuwa rais amekuwa na shughuli nyingi katika miezi kadhaa iliyopita na kwamba hakuwahi kupumzika kutokana na ratiba ya shughuli hizo kufuatana.

Ilisema ndani ya siku 15 zilizopita Kikwete alikuwa New York, Marekani kuhudhuria Mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UN), juzi na jana alikuwa mjini Arusha na jana na leo mjini Mwanza alipokutwa na tukio hilo.

Taarifa hiyo ilikumbusha kuwa Septemba 20 Rais Kikwete aliondoka kwenda nchini Marekani kuhudhuria Mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UNGA) na tangu hapo hajapumzika.

Kwa mujibu wa Ikulu Kikwete alirejea nchini kutoka Marekani saa 7:00 usiku wa kuamkia Ijumaa baada ya kusafiri kwa zaidi ya saa 19 na Ijumaa asubuhi alisafiri kwenda Arusha kufungua mkutano huo wa 55 wa Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola.

Wakati huohuo, Ofisi Binafsi ya Rais (OBR) imetangaza kuwa itaangalia upya ratiba ya rais kwa namna ya kumpunguzia mlundiko wa shughuli hata kama yeye binafsi ni “mpenzi mkubwa wa kuchapa kazi na kutumikia wananchi”.

OBR ndiyo husimamia upangaji ratiba za rais.

CHANZO: Mwananchi

4 Oct 2009


The Sun. Not the celestial near the earth, round which the earth and other planets revolve. I am talking about the UK’s bestselling newspaper. Its popularity is partly due to its normally informal journalistic style, with its “news in brief” on page 3 depicting semi-nude models being one of its main distinguishing features. It is also known for its strong nationalistic views, anti-European Union and anti-immigration stances. The Sun could as well be described as a right-leaning paper together with The Daily Express, The Daily Telegraph and The Daily Mail.

On its front page last Wednesday, the newspaper declared that Gordon Brown, the incumbent British Prime Minister, and his Labour Party have already lost the next British election. In its editorial, the paper announced that it switches sides, and would support The Conservative Party in the election. However, its Scottish version, The Scottish Sun, while withdrawing its support for Labour, has distanced itself from its English by not endorsing any Scottish political party.

Apart from selling reportedly 1 million copies a day, The Sun is also famous for its supposed reputation of backing British election winners. It is argued that the paper was responsible for Neil Kinnock’s defeat and it was a driving force for Tony Blair to become the Prime Minister after successive Labour defeats.


But is The Sun really a paper that makes election winners? Some observers doubts that popular claim, especially in this age when the internet has emerged as the most powerful in almost every sphere of our lives. Remember how Obama won the last US Elections?

Some analysts argue that in its decision to switch sides The Sun has just followed what many of the recent polls indicate about the coming British elections that the Conservatives would defeat Labour. They also claim that the newspaper is just representing opinions of most of its readers who seem to be disgruntled by the Labour Party.

However, The Sun might get it wrong this time because despite Labour’s poor performance, the Conservatives have so far not actually proved how they would be a better alternative to Labour. I first came to the UK in 2002 when Labour was already in power, so I wouldn’t pretend to know how good or bad the Conservatives were. However, their CV doesn’t look impressive from what I have heard. It is even bad news to non-Whites as the Tory still looks a Whites party despite its recent efforts to become all-inclusive. Of course, it is not as evil as the racist British National Party but there is still a sense of uncertainty among such groups as the ethnic minorities.

I still think Labour deserves another term. British voters should be sympathetic to Gordon Brown & Co in the way they have handled the credit crunch, particularly by looking beyond the UK’s borders. They should also not forget what The Tories did to this country prior to Labour getting into power.

As for The Sun’s decision to back potential election winners...well,if its US “sisters”- Fox News and The Ney York Post-couldn’t make John McCain win or Barack Obama lose the election, then even The Sun could have got it wrong come the next British elections. And didn’t the same newspaper campaign against Alec Salmond and his Scottish National Party in the previous elections, and he still managed to win?

After all, it is the British voters, not The Sun, who would be the real winners or losers regardless of the paper’s position.



A long die fan of the Scottish Premier League side, Motherwell Football Club, has changed his name to, guess what! Motherwell Football Club. Formerly known as Fraser Boyle, Mr Motherwell Football Club expressed his excitement on the prospects of his new name. “It’s more recognizable,” he told a BBC Scotland reporter. However, Mr Motherwell Football Club’s idea has not won her mom’s heart. She said she couldn’t understand why her son decided to change his name.

Well, if a child born on Sunday could be named Sunday, why not a die-hard Motherwell fan adopts his club’s name!But imagine someone had decided to change their name to Kajumulo Football Club...!!!


HATIMAYE Shirika la Ugavi wa Umeme Tanzania (TANESCO) limetangaza mgawo wa umeme nchi nzima kutokana na upungufu wa maji kwenye vituo vya kuzalisha umeme vya Kihansi na Pangani.

Hatua hiyo ya TANESCO imekuja miezi michache tu baada ya Mkurugenzi Mkuu wa shirika hilo, Dk. Idris Rashid, kuonya kuwa taifa litaingia gizani iwapo mitambo ya Kampuni ya Dowans yenye uwezo wa kuzalisha megawati 100 haitanunuliwa.

TANESCO ilikuwa na mpango wa kununua mitambo ya Dowans ambayo ilirithi mkataba kutoka Kampuni ya kuzalisha umeme wa dharura ya Richmond iliyobainika kutokuwa na uwezo wa kuzalisha nishati hiyo...ENDELEA

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.