13 Oct 2009


Hivi mwenzangu unapoiangalia CCM kwa mtazamo wa kawaida tu (yaani usiohisha uchambuzi wa kitaaluma) unaielezeaje?Pengine huafikiani na mtizamo wangu wa “kawaida” na kitaaluma kwamba pamoja na hadi lukuki za kuwakomboa Watanzania kutoka kwenye lindi la umasikini,chama hicho hakijaonyesha dhamira ya dhati kutimiza ahadi hizo.

Naamini kuwa baadhi ya ahadi hizo zilikuwa za dhati,hususani ile ya kuleta maisha bora kwa kila Mtanzania.Naamini hivyo kwa vile ni dhahiri kwamba chama hicho kilikuwa kinatambua hali ngumu inayowakabili Watanzania baada ya miongo kadhaa ya utawala wake.Kwa kutambua tatizo,CCM ilileta dalili za matumaini kwamba sio tu inataka kuendelea kutawala lakini pia inataka kuwa chachu ya mabadiliko.Japo chama hicho kinafahamika kwa usugu wa kukiri mapungufu ya utendaji wake,uamuzi wake kugusia maeneo yanayowakera wananchi ilikuwa ishara ya kutambua mapungufu katika awamu zilizotangulia na kudhamiri kufanya marekebisho.

Binafsi nilitarajia kwamba kama ilivyokuwa mwaka 2005 ambapo CCM “ilikiri mapungufu yake kiaina” kwa kuahidi kuboresha maisha sambamba na kukabili chanzo kikuu cha kuzorota/kudidimia kwa maendeleo (rushwa),basi safari hii pia kingepata ujasiri wa kutueleza bayana kwamba kumekuwa na mapungufu makubwa zaidi katika utekelezaji wa ahadi hizo.

Ni nani asiyejua kuwa kiwango cha rushwa kinazidi kupaa siku hadi siku?Ni nani asiyejua kuwa rushwa na uhujumu mwingine wa uchumi umechukua sura mpya kwa kuzaa tabaka “jipya” la mafisadi?Ni nani pia asiyejua kuwa kwa kiasi kikubwa ahadi ya maisha bora kwa kila Mtanzania imekuwa na maana zaidi kwa mafisadi kuliko walalahoi?Ni dhahiri kwamba Watanzania wenzetu kama wamiliki wa kampuni ya Kagoda wanaishukuru CCM kwa ukarimu na huruma yake to an extent that inaona aibu kuwataja hadharani.Matapeli wa Richmond (achana na yule Mhindi aliyegeuzwa mbuzi wa kafara mahakamani) wanaishukuru sana CCM kwa huruma yake kwao ambapo kila kikao cha bunge kinazugwa kuwa “taarifa ya utekelezaji wa mapendekezo ya kamati ya Mwakyembe itatolewa katika kikao kijacho”,na porojo nyingine kama hizo.

Kinachokera sasa sio tu madudu yanayoendelea kufanywa na CCM bali hizi kauli za kukera kwamba eti chama hicho kimeweka rekodi ya mapambano ya rushwa kuliko nyakati yoyote ile.Hii ni sawa na kuwasanifu Watanzania.Ni mithili ya kuwafanya wajinga,wasioona madudu yanayoendelea,wasiosikia maumivu ya vibano wanavyopewa na mafisadi,na wasiofahamu kuwa watuhumiwa kadhaa wa ufisadi hawajaguswa hadi leo (na hakuna dalili kuwa wataguswa licha ya ahadi kuwa kuna kesi tatu kubwa zitafunguliwa hivi karibuni....na kila mara tunaambiwa “hivi karibuni).”

Ni kweli kwamba hatua dhidi ya watuhumiwa wa ufisadi hazipaswi kuchukuliwa kutokana na utashi wa watu flani bali kwa kuzingatia sheria na kanuni.Lakini utashi ni muhimu katika kuchukua hatua,na hapa hatuzungumzii utashi wa wananchi wasio na uwezo wa kuuamua,kwa mfano “Chenge na tuhuma za vijisenti vyake huko Jersey hastahili kuwa kwenye kamati ya maadili ya CCM.”Kwanza kuwa na utashi wa kufanya jambo jema si dhambi,kama CCM inavyotaka kutuaminisha.Kuwa na utashi wa kuchukua hatua dhidi ya mafisadi ndio itapelekea chama hicho kuwatenga mafisadi inaowakumbatia,na hivyo kuwa rahisi kwake kuchukua hatua dhidi yao.Utashi unapaswa kuepukwa ni kama ule wa wanamtandao unaoendelea kuwaangalia wana-CCM wasio wanamtandao kuwa mithili ya wahaini.

Mamlaka husika zinapozembea kuchukua hatua sahihi halafu tunaishia kuambiwa kuwa hatua haziwezi kuchukuliwa kwa utashi wa watu flani...jibu jepesi ni kwamba matatizo yetu hayawagusi wanaotuongoza.Wanaona tunapiga kelele zisizo na msingi,ndio maana kwao haki za binadamu za mafisadi ni muhimu zaidi kuliko za walalahoi walio wengi.

Hivi kweli CCM inataka kutuzuga kuwa haifahamu kwamba Watanzania wengi wangependa kuona wahusika “halisi” wa utapeli wa Richmond wakifikishwa mahakamani badala ya kile tunachoelezwa kuwa “walijiuzulu kwa maslahi ya taifa”?CCM haijui kwamba kwa kuendelea kuminya taarifa kuwa nani anamiliki Kagoda ni mithili ya kuwapuuza Watanzania?Au CCM haifahamu kuwa kuwaachia mzigo Waingereza kudili na vijisenti vya ujambazi wa rada ni kukwepa majukumu?

Au chama hicho kinapotulaghai kwamba tumwache mhusika mkuu wa ufisadi katika mgodi wa Kiwira apumzike kwa amani ni sawa na kuruhusu kila mtu aibe kisha aachwe apumzike kwa amani?Kwanini basi vibaka wanajazana magerezani ilhali wezi wakubwa wanatetewa kwa nguvu zote?

Watanzania wana kila sababu ya kuiadhibu CCM hapo mwakani.Kinachofanywa na chama hicho kinapodai kuwa “kimeweka rekodi ya kupambana na rushwa” ni mithili ya vibaka wanaokuibia kisha wanakupigia ukelele wa mwizi na kupelekea wewe mwathiriwa wa uporaji huo kushushiwa kipigo kitakatifu huku kibaka “akiyeyuka kiulaini.”Badala ya kukiri kwamba kasi yao ya kupambana na ufisadi ni ndogo, wao wanatukejeli kuwa wameweka rekodi!Halafu bado tutegemee lolote kutoka kwa wababaishaji hawa?

Hakuna haja ya kubishana au kupigiana kelele nao.Dawa yao ni hapo mwakani.Kama unataka kuendelea kuona mafisadi wakitetewa huku wanaowapinga wakikemewa basi irejeshe CCM madarakani hapo mwakani.Kama unadhani maisha bora yaliyoahidiwa 2005 yamepatikana zaidi ya matarajio yako basi hutofanya kosa kutoa kura ya ndio kwa chama hicho.

Tukiendeleza mazowea tutazidi kuumia.Kuna wanaodhani kwamba Tanzania haiwezi kuwa kisiwa cha amani pasipo utawala wa CCM.Wanachosahau kuwa hata hao CCM ni Watanzania wenzetu japo wanawathamini zaidi wageni (wawekezaji) kuliko sie wenye nchi.Wanasahau pia kuwa wingi wa wabunge wa CCM unakwaza jitihada wa wapambanaji kama akina Dokta Slaa kuwakalia kooni wababaishaji waliojazana chini ya utawala wa CCM.

Atakayenuna na anune lakini nchi hii ni yetu sote na kila Mtanzania ana haki ya kudai haki yake.Tukiruhusu kuendelea kwa ngojera za “tunaendelea na mchakato wa blah blah blah” au “kesi kadhaa zkubwa zitapelekwa mahakamani hivi karibuni...” na hadithi nyingine kama hizo basi tutaendelea kuwa watu wa kulalamika kila siku japo ni sie wenyewe tunaoweza kukomesha usanii wa kisiasa wa aina hiyo.Kama imewezekana Ghana basi hata kwetu inawezekana.Si kweli kwamba chama mbadala kitashindwa kutupeleka tunakostahili kwenda hasa ikizingatiwa kuwa hakuna uwezekano wa chama hicho mbadala kupata idadi kubwa ya wabunge zaidi ya CCM,which means itakuwa rahisi kukidhibiti iwapo kitaonyesha dalili za kurejea madudu ya CCM.

Kusanya hasira zako lakini usipigane bali pugie kura ya kujiletea maisha yako bora wewe mwenyewe kwa kuwaondoa wanaokwaza uwezekano huo.Ifike wakati tusema tumechoshwa na ahadi na maneno matamu (na mengine si matamu bali ya dharau kama hayo ya kudai wameweka historia ya kupambana na rushwa wakati wanajua waziwazi kuwa wamekuza rushwa kupindukia).

It can be done if you play your part.

Inawezekana ukiamua kutimiza wajibu wako.


10 Oct 2009


SOMA KAULI ZA BABU HUYU HAPA CHINI KISHA UELEWE KWANINI NATOA WITO AONEWE HURUMA KWA KUPUMZISHWA.

Ahofia wabunge wengi CCM kutorudi Bungeni
Na Keneth Goliama, Mbeya

MBUNGE wa kuteuliwa wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Kingunge Ngombale Mwiru, amewashutumu viongozi wanaounda makundi ndani ya chama hicho na kuwaita waliochanganyikiwa.

Mbunge huyo aliapa kuwa matajiri wasipewe kipaumbele katika uongozi, kwani watu wakishakuwa na fedha wanajiingiza katika siasa kufanikisha malengo yao ya kibiashara.

Kingunge ambaye pia ni Naibu Kamanda UVCCM Taifa,aliyasema jana wakati akiwaapisha Makamanda wa Mkoa wa Mbeya kwenye ukumbi wa Mkapa.

Aliwataka makamanda hao kufanya kazi ya kuwashauri vijana na sio kuwaingiza vijana katika makundi yaliyopo ndani ya chama hicho.

Kingunge alisema kauli za baadhi ya viongozi kuwa, wabunge wengi wa CCM hawatarudi katika ubunge mwaka 2010 ni kweli kwa sababu kunahitajika mabadiliko katika uongozi ndani ya chama.

Hata hivyo, alisema wabunge hao wapya ni faraja kwa CCM kwa sababu watakuwa ni wakutoka ndani ya chama hicho.

Aliongeza licha ya Mkoa wa Mbeya ni mingoni mwa mikoa ambayo ilitoa watu waliokuwa mstari wa mbele kugombea uhuru , lakini sifa hiyo imeharibiwa na viongozi wachache.

Kingunge alisema baadhi ya viongozi mkoani hapa wanauhasama wa kugombea madaraka na kwamba sasa ugomvi huo unakiharibia chama.

Akiunga mkono jitihada za vijana wa mkoa huo kupambana na mafisadi, Kingunge aliwataka wasiache kutetea haki yao kwa sababu vijana ndio wenye nguvu katika maendeleo ya jamii na siasa.

Kingunge aliwaasa wanachama hao kukataa kurubuniwa na watu wenye fedha kwani kukubali kufanya hivyo ni kuua chama.

Baadhi ya viongozi wamefanikiwa kuwarubuni vijana kwa fedha ili waweze kujinufaisha wenyewe na kuharibu siasa mkoani hapa, alisema Kingunge

Alikionya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuwa, hakijui siasa ndio maanakimejaa matatizo matupu na uchaguzi wao ni ovyo na kwamba hakina uwezo wa kupewa kuongoza dola.

CHANZO: Mwananchi

HIVI ALIYECHANGANYKIWA NI NANI KATI YA KINGUNGE NA HAO ANAOWAITA "WAMECHANGANYIKIWA."MAJUZI,MTETEZI MAHIRI WA MAFISADI,YUSUPH MAKAMBA NAE ALITOA TAMKO LINALOSHOBIHIANA NA HILI LA KINGUNGE,MWANASIASA ALIYETUZUGA ENZI ZA MWALIMU KUWA NI MFUASI MAHIRI WA UJAMAA ONLY KUIBUKA MTETEZI MAHIRI WA MAFISADI.LEO,MIEZI MICHACHE KABLA YA UCHAGUZI MKUU,NAE ANAJITUTUMUA KUKEMEA MAFISADI!?HUKU NI KUCHANGANYIKIWA KUNAKONASIBISHWA NA KUZEEKA VIBAYA.

9 Oct 2009


From its politics to its economy to its environment and way of life, California is like a patient on life support. At the start of summer the state government was so deeply in debt that it began to issue IOUs instead of wages. Its unemployment rate has soared to more than 12%, the highest figure in 70 years. Desperate to pay off a crippling budget deficit, California is slashing spending in education and healthcare, laying off vast numbers of workers and forcing others to take unpaid leave. In a state made up of sprawling suburbs the collapse of the housing bubble has impoverished millions and kicked tens of thousands of families out of their homes. Its political system is locked in paralysis and the two-term rule of former movie star Arnold Schwarzenegger is seen as a disaster – his approval ratings having sunk to levels that would make George W Bush blush. The crisis is so deep that Professor Kevin Starr, who has written an acclaimed history of the state, recently declared: "California is on the verge of becoming the first failed state in America." WRITES The Observer's Paul Harris.



Na Ramadhan Semtawa

RAIS Jakaya Kikwete aliweka hadharani matokeo ya uchunguzi wa vipimo vya afya yake, yanayoonyesha kuwa kiongozi huyo wa nchi ana afya njema baada ya tatizo la kuishiwa nguvu akiwa jukwaani mjini Mwanza Oktoba 4, kuibua mjadala.

Lakini vipimo hivyo vinaonyesha kuwa tatizo pekee linalomsumbua Rais Kikwete ni maumivu ya shingo ambayo yanatokana na kuumia nyakati za ujana au utoto.

Afya ya Rais Kikwete ilizuia mjadala baada ya kuishiwa nguvu akihutubia kwenye Uwanja wa Kirumba mjini Mwanza na kulazimika kubebwa na wasaidizi wake hadi chumba kidogo cha uwanjani hapo na ilielezwa baada ya rais kuzinduka kuwa tatizo hilo lilitokana na uchovu baada ya safari ndefu kati ya New York, Marekani na Dar es salaam na baadaye Arusha na Mwanza.

Pamoja na uchovu huo kuhusishwa na safari ndefu ya Rais Kikwete taarifa iliyopokelewa kutoka Radio Jamaica jana jioni zinasema kuwa rais atakwenda nchini Jamaica kwa ziara ya kikazi itakayoanza Novemba 24 na kumalizika Novemba 26.

Na jana daktari wa rais, Peter Mfisi alirejea tena kauli hiyo akisema uchovu, hasa wa safari, ndio uliosababisha kiongozi huyo wa nchi kuishiwa nguvu jukwaani, huku kukiwa na habari kuwa ataenda Jamaica mwezi ujao kwa safari ya kikazi.

Hii ni mara ya kwanza kwa Ikulu kuweka hadharani vipimo vya uchunguzi wa afya ya Rais Kikwete, ambaye pia aliwahi kuishiwa nguvu siku ya mwisho ya kampeni zilizomuingiza Ikulu, na kuanguka akiwa jukwaani.

Daktari wa rais, Peter Mfisi aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa vipimo hivyo ni pamoja na cha damu kwa ajili ya kuangalia virusi vya Ukimwi ambacho huchukuliwa kila baada ya miezi sita.

"Nimekuja kufafanua afya ya mheshimiwa rais kutokana na tukio la Oktoba 4, 2009 (la kuishiwa nguvu jukwaani) pale Mwanza. Tukio hilo limesababisha mshtuko kwa watu wengi na kuendelea kuwa jambo linalozua mjadala kuhusu hali ya afya ya mheshimiwa," alisema daktari huyo.

"Naelewa sababu ya wananchi kuwa na hofu na kuwepo kwa mjadala miongoni mwao. Tatizo pekee ambalo limekuwa likimsumbua rais mara kwa mara ni maumivu ya shingo yanayotokana na kuumia utotoni na wakati wa ujana.

"Baadhi ya pingili za uti wa mgongo sehemu ya shingoni ziliathirika kutokana na kuumia huko na humsababishia maumivu. Mara nyingi matatizo hayo huwapata wanamichezo na wanajeshi."

Dk Mfisi aliongeza kusema: "Tumekuwa tunamfanyia mheshimiwa rais uchunguzi wa damu yake kwa vipimo mbalimbali vinavyotumika kutambua maradhi mbalimbali yanayohusu damu yenyewe na mwili mzima wa mwanadamu. Tumekuwa tunafanya hivyo hapa nchini na hata nje kwa nia ya kulinganisha matokeo yetu na kwa vipimo ambavyo sisi tunavyo.

"Matokeo ya uchunguzi wetu yameonyesha mheshimiwa rais yuko salama, hana maradhi ya damu au kisukari, wala Ukimwi au wingi wa mafuta (Cholestrol), kiwango cha madini, tezi la kibofu wala shingo, au ya ini, au ya homoni mbalimbali zilizoko mwilini na mengine."

Dk Mfisi alifafanua kwamba, uamuzi huo wa kutoa vipimo hivyo umetokana na ridhaa ya rais mwenyewe.

"Ni ridhaa ya mheshimiwa rais mwenyewe... kutokana na kiapo changu cha udaktari na maadili yangu ya kazi, siruhusiwi kutoa hadharani undani wa habari yoyote inayohusu mgonjwa ninayemtibu bila ridhaa yake," alisema Dk Mfisi.

Kwa mujibu wa daktari huyo, baada ya Rais Kikwete kuishiwa nguvu jukwaani, alichukua vipimo muhimu wakati akiwa kwenye chumba maalumu uwanjani hapo kama ilivyo kawaida na kwamba vipimo hivyo vimeshafanyiwa uchunguzi.

Alifafanua kwamba matokeo ya vipimo vilivyochukuliwa siku ya tukio la Mwanza yalionyesha shinikizo la damu (BP) lilikuwa kati ya 130 kwa 85 (vipimo vya kitaalamu), kitu ambacho ni cha kawaida kwa mtu mwenye umri kama wa Rais Kikwete.

"Mapigo ya moyo wake yalikuwa ni 76 kwa dakika ambayo pia ni ya kawaida; sukari kwenye damu ilikuwa 5.5 ambayo nayo ilikuwa ya kiwango cha kawaida; joto la mwili lilikuwa nyuzi 37.5 ambalo ni la kawaida," alifafanua Dk Mfisi.

"Mheshimiwa Rais pia hakuwa na kiungo chochote kilichoonekana kutetereka, jambo ambalo lilithibitisha kuwa hakupata kiharusi. Mheshimiwa Rais hakuwa na matatizo yoyote ya kiafya ambayo yangeweza kuhusishwa kuwa chanzo cha tukio lile (la Mwanza)."

Hata hivyo, Dk Mfisi alisema baada ya kurejea Dar es Salaam alijaribu kuwasiliana na madaktari wenzake wa ndani na nje ya nchi ambao wamekuwa wakishirikiana nao katika kuchunguza na kufuatilia afya ya Rais Kikwete.

"Wote hao baada ya kuwasimulia kilichotokea na matokeo ya vipimo nilivyomfanyia mheshimiwa rais, kwa tafakuri zao hawakuwa na wasiwasi wowote kuwa tukio hilo lilisababishwa na jambo jingine lolote isipokuwa uchovu," alisisitiza daktari huyo wa rais.

Aliongeza kwamba mmoja wao alimuona rais siku moja kabla ya kuondoka New York ambako alipata nafasi ya kumchunguza afya ya mkuu huyo wa nchi.

Dk Mfisi, akitoa mtiririko huo wa vipimo mbalimbali na matokeo alisema: " Blood Pressure (shinikizo la damu), tunafuatilia kwa karibu sana msukumo wa damu, mwenyewe tunampa mashine ya kujipima kila siku na anafanya hivyo, kwa jumla presha yake iko kwenye viwango vya kawaida.

"Aidha, uzito wake wa mwili unaendana ipasavyo na urefu wake, mheshimiwa Rais ni mtu mwenye mazoea ya kufanya mazoezi na yuko makini katika chakula anachokula."

Daktari huyo wa rais aliweka bayana kwamba, wanahusika kwa ukamilifu na kuelekeza kuhusu chakula anachokula na kuongeza kwamba "ana nidhamu ya kujipima pamoja na mazoezi na chakula."

Kuhusu moyo, Dk Mfisi alisema tayari walishamfanyia rais vipimo vya kitaalamu vinavyofahamika kama ECHO na ECG na vingine, na kwamba matokeo yameonyesha hakuna tatizo lolote.

Akizungumzia ubongo, alisema mwaka jana Rais Kikwete alifanyiwa uchunguzi wa afya ya ubongo wake katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa kutumia kipimo cha CT-Scan na matokeo yake yalionyesha kwamba, hakuwa na tatizo pia.

Dk Mfisi alisema Rais Kikwete aliwahi kufanyiwa uchunguzi wa ini, figo, bandama na kongosho kwa kutumia kipimo cha mionzi (ultra sound), uchunguzi ambao ulibaini viungo vyote hivyo viko salama.

"Kila mwaka tunapomfanyia uchunguzi wa afya ya mheshimiwa rais, tumekuwa tunafanyia uchunguzi wa viungo vyake muhimu vya tumboni kama vile ini, figo, bandama na kongosho na kwa kupima damu yake kwa vipimo vyote muhimu," aliongeza Dk Mfisi.

Kuhusu mfumo wa njia ya chakula, ambayo huhusisha koromeo la chakula, tumbo, utumbo mdogo, Dk Mfisi aliweka bayana kwamba matokeo ya uchunguzi yameonyesha hakuna tatizo lolote.

Alisema mwaka 2007 walimfanyia kipimo cha kitaalamu cha colonoscopy mjini Paris, Ufaransa, kuchunguza hali ya afya ya utumbo mkubwa na kwamba matokeo ya uchunguzi yalionyesha kuwa hana matatizo yoyote.

Alisema daktari aliyemfanyia rais kipimo hicho aliwaambia kuwa mkuu huyo wa nchi hahitaji kufanyiwa kipimo kama hicho tena mpaka baada ya miaka saba na kwamba daktari huyo alimtania rais kwa kusema kuwa "angefurahi kuazima utumbo" wake.

Kuhusu tezi la shingo, Dk Mfisi alisema kuwa akiwa mjini New York katika safari yake ya juzi, Rais Kikwete alifanyiwa uchunguzi wa afya ya tezi la shingo pamoja na kiwango chake cha utoaji wa homoni, matokeo yaliyoonyesha hakuna tatizo, hali kadhalika uchunguzi wa tezi la kibofu ulionyesha hana tatizo.

Dk Mfisi alisema rais hana tatizo la macho, masikio na pua na kwamba uvaaji miwani wa Kikwete haumaanishi kuwa ni maradhi.

"Tunapofanya uchunguzi wa macho ukiacha ile ya kuchunguza uwezo wa kuona, tunaangalia presha ya macho na hali ya viungo vya nje na ndani, mheshimiwa Rais hana matatizo yoyote," alisema.

CHANZO: Mwananchi

WAKATI DR MFISI AKITOA MAELEZO HAYO,MHADHIRI MWANDAMIZI KATIKA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM DR HAJI SEMBOJA AMENUKULIWA NA JARIDA LA RAIA MWEMA AKIELEZA KUWA URAIS NI ASASI NA SI MTU BINAFSI.

Urais si Kikwete binafsi, ni mfumo wa kitaasisi. Ni wazi kuwa Rais amesema yeye ndiye hakuzingatia ushauri wa wataalamu wake kutokana na kuwaondolea lawama. Ameamua kuwalinda kwa kubeba lawama, lakini ukitazama jambo hili kwa upana wake wasaidizi wake walipaswa kutambua tangu awali kuwa urais ni system nzima Ikulu hata mlinzi wa getini. Kwa hiyo, wasaidizi ndiyo wenye kuamua na si kila kitu kifanywe na Rais kama ambavyo wanasema sasa watajaribu kumpunguzia ratiba,” ALISEMA DR SEMBOJA NA KUSISITIZA KWAMBA“Sidhani kama ni sahihi kukubali kuwa Rais ndiye alikataa ushauri, kwa taratibu za kimfumo Rais anapangiwa kila kitu ni kama anaamriwa hivi. Kwa tukio hili ameamua tu kuwa na nidhamu ya kuwalinda wasaidizi wake, namwombea afya njema lakini ni muhimu tuzingatie kuwa wengi walioamua kufanya kila kitu wenyewe walipata matatizo, Ikulu sasa ifanye kazi kama Ikulu.”

BINAFSI NAAMINI TATIZO NI LA KIMFUMO ZAIDI.KUNA TAASISI ZENYE MAMLAKA NA WAJIBU WA KUPANGA RATIBA ZA RAIS SAMBAMBA KWA KUZINGATIA UHALISIA,USALAMA NA MAMBO MENGINE KAMA HAYO.KWA WENZETU WANAOZINGATIA KANUNI NA TARATIBU ZA KITAASISI,SI RAHISI KWA RAIS KUJIAMULIA MAMBO YAKE MWENYEWE PASIPO KUZINGATIA USHAURI WA KITAALAM.SI RAHISI,KWA MFANO,BARACK OBAMA KUJIAMULIA KWENDA MAHALA FLANI KINYUME NA USHAURI WA U.S. SECRET SERVICE.UBISHI WA RAIS KAMA BINADAMU HAUNA NAFASI KATIKA UFANISI WA TAASISI INAYOZINGATIA TAALUMA NA MAADILI.IKUMBUKWE KWAMBA LAITI RAIS AKING'ANG'ANIA KUFANYA ZIARA MAHALA FLANI KINYUME NA USHAURI WA WASAIDIZI WAKE KISHA AKAPATWA NA JANGA,WATAKAOBEBA LAWAMA NI WASAIDIZI HAO NA SI RAIS.LAKINI PIA KUNA SUALA LA FEDHA ZA WALIPA KODI ZINAZOTUMIWA NA TAASISI HUSIKA KUILINDA ASASI YA URAIS NA BINADAMU ALIYEKABIDHIWA DHAMANA YA URAIS.NI DHAHIRI KWAMBA RAIS AKIPUUZA USHAURI WA WA TAASISI HUSIKA INAMAANISHA PIA UPOTEVU WA FEDHA ZA WALIPA KODI.



UTENDAJI WA AINA YA ZIMAMOTO,AU VIBAYA ZAIDI,KULENGA SHABAHA BAADA YA RISASI KUFYATUKA,UTATUGHARIMU HUKO MBELENI.LEO HII TUSINGEHITAJI DAKTARI WA RAIA KUWEKA HADHARANI TAARIFA NYETI ZA AFYA YA JK LAITI TAASISI HUSIKA ZINGEMLAZIMISHA JK KUFUATA USHAURI WA KITAALAMU KUHUSIANA NA RATIBA AU ZIARA ZAKE.TUSISUBIRI JAMBO LITOKEE NDIPO TUANZE KUTOA MAELEZO YA KITAALAMU. BY THE WAY,TAARIFA HIYO YA DAKTARI WA RAIS INAWEZA KUZUA MJADALA USIO NA TIJA KUHUSU MANTIKI YAKE.JAPO NI VEMA KUTOA UFAFANUZI KATIKA MASUALA YANAYOZUA UTATA (I WISH NA KWELI ISHU YA KAGODA INGEKUWA HIVYO) LAKINI KUNA UWEZEKANO WA "WABISHI" KUHOJI KAMA DAKTARI WA RAIS WA AFRIKA ANAWEZA KUTOA TAARIFA "MBAYA" DHIDI YA BOSI WAKE!

KWA SASA,MAMLAKA HUSIKA ZINAWEZA KUFARIJIKA BAADA YA KUPATA UTETEZI KUTOKA KWA JK.LAKINI NI VEMA ZIKATAMBUA KUWA JUKUMU LAO SI KUMWOGOPA MHESHIMIWA BALI KUFANYA KAZI ZAO KWA KUZINGATIA MAADILI NA TAALUMA.JK KAMA MTU ANAWEZA KUTOZINGATIA USHAURI WA MAMLAKA HIZO,LAKINI JK KAMA RAIS HARUHUSIWI KUJIAMULIA MAMBO YANAYOWEZA KUATHIRI ASASI YA URAIS.UOGA NA KUJIKOMBA NI MAMBO YASIYO NA NAFASI KATIKA PROFESSIONALISM.


8 Oct 2009

Mambo mengine huku Ughaibuni ni vituko vitupu.Kuna watu wanafuga majoka makubwa na kuyalea kama watoto wao,kuna wanaofuga panya mithili ya paka,na wengine wamegeuza tumbili kuwa watoto wa kambo.Na matunzo wanayopewa mbwa na paka hayatofautiani sana na anasa wanazofaidi watoto wa wabaka-uchumi wetu (mafisadi).

Kuna vijibwa flani vimekuwa kwenye chati kwa muda mrefu kutokana na kushebedukiwa na watu maarufu.Nadhani ushakiona ki-chihuahua cha Paris Hilton,kijibwa kidogo mithili ya paka.Sasa imeibuka fasheni mpya ya “kitimoto pimbi”,yaani nguruwe wadogo kupindukia.

Jioni hii kipindi cha Live From Studio Five katika kituo cha runinga cha Channel Five kimezungumzia fasheni hiyo mpya ambayo kwa hakika inaweza kuzua songombingo na maustaadhi pindi ikitua Bongo,almaaruf kwa ku-copy na ku-paste mengi ya yanayojiri anga hizi.






Manji, Jeetu wagombea matrekta

• Homa ya Kilimo Kwanza

na Mwandishi Wetu

WAFANYABIASHARA wawili maarufu hapa nchini wenye asili ya Kiasia, Yusuf Manji na Jayantkumar Chandubhai Patel, maarufu kwa jina la Jeetu Patel, wanadaiwa kuingia katika mzozo mkubwa wa kibiashara wakati wakigombea kupata zabuni ya mradi wa kuingiza nchini na kusambaza matrekta, wenye thamani ya zaidi ya sh bilioni 50.

Habari ambazo Tanzania Daima Jumatano limezipata kutoka vyanzo vyake vya habari vya kuaminika zimeeleza kuwa, Manji na Patel ambao wanadaiwa kuhusika kwa namna moja au nyingine katika kuomba zabuni hiyo, sasa wanawindana huku wakitishana kumalizana kibiashara.

Baadhi ya watu wa karibu na wafanyabiashara hao mabilionea waliozungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti katika siku za karibuni walieleza kuwa, kumekuwa na jitihada za chini kwa chini zinazofanywa na wapambe wao kuvujisha katika vyombo vya habari mbinu zao wanazotumia kupata zabuni kubwa za serikali.

Mfanyabiashara mmoja maarufu ambaye yuko karibu na wafanyabiashara hao, alilieleza gazeti hili kuwa, mabilionea hao sasa wamekuwa mahasimu baada ya kuzidiana ujanja katika zabuni hiyo ambapo kila mmoja anatishia kutoa siri za kibiashara za mwenzake.

“Sasa wanatishana, kila mmoja anatishia kutoa siri za mwenzake kibiashara. Wote wanapata tenda kubwa kutoka serikalini, wanavyozipata wanajua wao. Kinachotushangaza kila mmoja anasema atamuanika mwenzake,” alisema mfanyabiashara huyo aliyeomba jina lake lisitajwe.

Taarifa za ndani kutoka kwa watu walio karibu na Manji, zinadai kuwa mfanyabiashara huyo hakufurahishwa na jinsi mchakato wa upatikanaji zabuni hiyo ulivyoendeshwa, na sasa anakusudia kuvujisha katika vyombo vya habari taratibu zilizokiukwa katika mchakato wa utoaji wa zabuni hiyo.

Zinadai kuwa, Manji anajiandaa kuweka wazi jinsi sheria ya manunuzi ya umma ya mwaka 2004 ilivyokiukwa wakati wa mchakato wa utoaji zabuni hiyo.

Katika mradi huo, Jeetu ambaye anatajwa kuwa mwakilishi wa Kampuni ya Escort hapa nchini, yenye makao makuu yake nchini India, ambayo imeshinda zabuni hiyo, anadaiwa kuwashawishi maofisa wa juu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) ambalo limekabidhiwa jukumu la kuutekeleza mradi huo na serikali, kuipatia kampuni hiyo.

Habari hizo zimedai kuwa, Jeetu alifanikisha mpango huo baada ya kuwaunganisha maofisa kadhaa wa ngazi za juu wa JKT na watendaji wakuu wa Escort walioko India, ambao baada ya kuhakikishiwa kupewa zabuni hiyo, waliwaalika maofisa kadhaa wa JKT kwenda nchini humo kwa ajili ya kusaini mkataba wa utekelezaji wa kazi ya kusambaza matrekta hapa nchini.

Taarifa zaidi zilidai kuwa, tayari baadhi ya viongozi wa juu wa JKT wamekwisha safiri hadi India kusaini mkataba huo.

Hata hivyo, inadaiwa kuwa, Manji anapinga hatua ya viongozi wa JKT kwenda kusaini mkataba huo nchini India, ikizingatiwa kuwa baadhi ya watendaji wa serikali wamekwishalalamikiwa kwa kusaini mikataba inayohusu miradi ya kitaifa nje ya nchi.

Aidha, inadaiwa kuwa, baadhi ya habari zinazotarajiwa kusambazwa zitakuwa zinahoji ukiukwaji wa taratibu kwa kutoa zabuni hiyo pasipo kuitangaza kama sheria ya manunuzi ya umma inavyoelekeza, licha ya Baraza la Mawaziri kuujadili mradi huo na kutoa baraka kwa JKT kuutekeleza.

Kwa upande wa Jeetu, taarifa zinadai kuwa, anajiandaa kujibu tuhuma za aina yoyote zitakazotolewa katika vyombo vya habari, zikiwa na lengo la kuichafua Kampuni ya Escort au zinazohusu upatikanaji wa zabuni hiyo.

Baadhi ya maofisa wa serikali waliozungumza na Tanzania Daima Jumatano kuhusu suala hilo walieleza kuwa, serikali ina taarifa kuhusu jambo hilo na inalifuatilia kwa karibu ili kuhahakisha hakuna taratibu zinazokiukwa katika utekelezaji wa mradi huo.

Mmoja wa maofisa wa ngazi za juu serikalini aliyezungumza kwa sharti la kutotajwa jina lake alieleza kuwa, anafahamu kuwa Serikali ya India ilitoa mkopo usiokuwa na riba, wa zaidi ya sh bilioni 50 kwa Serikali ya Tanzania kwa ajili ya kununulia matrekta, wakati Makamu wa Rais, Dk. Ali Mohamed Shein, alipofanya ziara nchini humo mapema mwaka huu, kwa sharti la kulipwa katika kipindi cha miaka 10.

Alisema sharti jingine lililotolewa katika kutoa mkopo huo, linaitaka Serikali ya Tanzania kuhakikisha inanunua matrekta hayo kutoka kampuni za India na si vinginevyo.

Ofisa huyo alisema, serikali iliamua kuikabidhi JKT jukumu la kusimamia utekelezaji wa mradi huo ili kuondoa mazingira yoyote ya kutokea udanganyifu katika kuutekeleza.

Hata hivyo, alieleza wasiwasi wake iwapo kuna taarifa za baadhi ya maofisa wa JKT waliokabidhiwa jukumu la kusimamia utekelezaji huo, kuzungumza na mwakilishi wa Kampuni ya Escort hapa nchini (Jeetu), kisha wakaipa kampuni anayoiwakilisha zabuni hiyo bila kufuata taratibu.

“Hili jambo linaweza kuharibu kabisa sifa ya JKT kama litakuwa kweli, kwa sababu itakuwa ni kashfa kubwa kwa jeshi kukiuka taratibu za manunuzi ya umma. Ingawa kuna imani kuwa si rahisi mambo ya kijeshi kuchunguzwa, lakini hili liko wazi mno kwa sababu ni zabuni iliyo wazi iliyokuwa ikifuatiliwa na wafanyabiashara wengi, hivyo hao hao wanaweza kuwa wametoa siri za taratibu kukiukwa,” alisema ofisa huyo.

Waziri mmoja aliyezungumza na gazeti hili hivi karibuni, alisema suala hilo lilizungumzwa katika Baraza la Mawaziri na kupatiwa baraka zote za kulitekeleza. Aliongeza kuwa, anaamini hakuna taratibu zilizokiukwa.

Hata hivyo, alionya kuwa Baraza la Mawaziri linazo taarifa za mfanyabiashara mmoja maarufu kufanya mpango wa kutoa taarifa za uongo kuhusu mchakato wa upatikanaji zabuni hiyo kwa sababu ya kisasi cha kukosa zabuni hiyo.

Tanzania Daima Jumatano lilipowasiliana na Ofisa Habari wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Nadhifa Omary, ili kupata ufafanuzi wa suala hilo, alisema jambo hilo linaweza kuzungumziwa na waziri tu kwa sababu ya unyeti wake.

Alieleza zaidi kuwa, hawezi kulizungumzia kwa sababu yuko nje ya ofisi kwa mapumziko, hivyo hana maelezo ya kina ya kulitolea ufafanuzi.

Alipoulizwa, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga, Dk. Hussein Mwinyi, alisema analifahamu vizuri suala hilo na alilihakikishia gazeti hili kuwa, hakuna utata wowote katika utekelezaji wa mradi huo, isipokuwa linaweza kufanywa ajenda ya kuchafuana na watu ambao wana malengo binafsi na mradi huo.

“Ninalijua vizuri jambo hilo, tenda zilitangazwa na zikafunguliwa, nakuhakikishia. Mimi mwenyewe niliona kampuni kama 11 hivi zilizoomba zabuni hiyo, sasa kama kuna mtu anasema kulikuwa na kasoro, ni mambo ya wafanyabiashara kutaka kuchafuana tu kwa malengo binafsi waliyonayo katika mradi huo,” alisema.

Naye Manji alipotafutwa kupitia simu yake ya kiganjani ili kuzungumzia suala hilo, kwa mara kadhaa ilikuwa ikipokelewa na wasaidizi wake na kueleza ameweka utaratibu wa kutoongea na waandishi wa habari mpaka inapobidi.

CHANZO: Tanzania Daima

NILIWAHI KUANDIKA HUKO NYUMA KWANZA HUU WIMBO WA "KILIMO KWANZA" HAUNA TOFAUTI NA USANII WA "MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA."NGONJERA ZA KISIASA ZINAZOHANIKIZWA NA KAULI-MBIU MWANANA HAZIWEZI KUMKOMBOA MTANZANIA KATIKA LINDI LA UMASIKINI UNAOMKABILI.BADALA YAKE,JITIHADA KUBWA ZINAHITAJIKA KATIKA KUPAMBANA NA UFISADI NA MAFISADI,VIKWAZO VIWILI VIKUU VYA MAENDELEO YETU.HILO HALIWEZEKANI CHINI YA UTAWALA WA CCM KWA VILE CHAMA HICHO NI KITALU MWAFAKA KWA MAZALISHO NA HIFADHI YA UFISADI NA UFISADI.

HAWA WAHINDI WAMEGEUZA TANZANIA KAMA SEHEMU YA MAJARIBIO YA KILA MADUDU YANAYOWAJIA KICHWANI.WAMENABAKA UCHUMI WETU HUKU TULIOWAKABIDHI DHAMANA YA KUULINDA WANAENDELEA KUWANYENYEKEA KUTOKANA NA NJAA YAOYA TENI PASENTI.

MWAKA WA HUKUMU 2010 UNAKARIBIA.USIREJEE MAKOSA YA 2005,PLEEEEEZ!

6 Oct 2009


NILIWAHI KUBASHIRI HUKO NYUMA KWAMBA KADRI 2010 INAVYOSOGEA NDIVYO TUTAVYOZIDI KUSHUHUDIA VITUKO.LEO HII MAKAMBA NAE AMEJIUNGA KATIKA VITA DHIDI YA UFISADI!HIVI SI BINADAMU HUYU ALIYEWATAKA WATANZANIA KUACHANA NA MIJADALA YA UFISADI KWA VILE BAADHI YA WAHUSIKA WAMEFIKISHWA MAHAKAMANI?

HEBU MSIKIE ALIVYOGEUKA KINYONGA KATIKA HABARI HII HAPA CHINI:

Makamba ahimiza mapambano dhidi ya ufisadi

na Jacob Ruvilo, Kigoma

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Yusufu Makamba, amesema ufisadi unapaswa kupigwa vita na kila Mtanzania mzalendo, kwani umechangia kwa kiasi kikubwa kudidimia maendeleo ya nchi.

Makamba alisema hayo juzi kwenye semina ya viongozi wa CCM Jimbo la Kigoma Mjini iliyofanyika katika viwanja vya Lake Tanganyika.

Alisema suala la watu kujipatia mali kinyume cha utaratibu na kuhujumu nchi havina uhusiano wowote na CCM, kwani watuhumiwa wote hawakuagizwa na chama kufanya hivyo, bali ni hulka zao binafsi.

Makamba alifafanua kuwa suala la muumini wa dhehebu fulani kwenda kinyume na maadili au amri ya vitabu vya dini, hapaswi kulaumiwa sheikh au mchungaji, badala yake ni muumini husika ambaye mwisho wa siku ndiye atakayepata adhabu kwa Mungu.

Aidha, Makamba alisema suala la vyama vya upinzani kushika bango na kuidhihaki CCM kuwa ni mafisadi kutokana na viongozi wachache wasio waaminifu, halina maana, bali suala la umoja na mshikamano katika kupinga mafisadi hao ni jukumu la watu wote, ikiwamo CCM.

Mbali na hilo, Makamba alikemea baadhi ya viongozi wa chama hicho kutumia uwezo wao wa fedha kutoa rushwa ili kupita katika chaguzi mbalimbali kuwa ni moja ya upatikana wa viongozi mafisadi na wasiofaa kwa jamii.

Alisema Tanzania haikuandaliwa kutawaliwa na wenye nacho na kwamba hali hiyo inaweka tabaka la mwenye nacho na asiyenacho, hali ambayo isipoangaliwa kwa umakini suala la rushwa litabaki kuwa ndoto.


TATIZO LETU WATANZANIA NI UWEPESI WETU KUAMINI KILA KINACHOAHIDIWA.MWAKA 2005 MAKAMBA NA CCM YAKE WALITAMBUA HILO NA KUJA NA AHADI LUKUKI IKIWEMO ILE MAARUFU YA KULETA MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA.SASA WANASEMA KWAMBA SUALA LA MAISHA BORA LILIANZA ZAMA ZA MWALIMU NYERERE,PENGINE KATIKA KUKWEPA KUTUELEZA HAYO MAISHA BORA WALIYOAHIDI ILIKUWA NI KWA MAFISADI PEKEE AU...?MAANA KAMA SUALA HILO LILIASISIWA NA NYERERE BASI WANGETAMKA BAYANA WAKATI ZA KAMPENI ZA 2005 BADALA YA KUIFANYA KAULI-MBIU MUHIMU ILIYOWAZUGA WATANZANIA NA KUTOA USHINDI MKUBWA KWA CCM.

NI MUHIMU KWA WAPIGA KURA KUTAMBUA KUWA WANASIASA WETU WANAWEZA KUAHIDI LOLOTE ILI WAPATE KURA KAMA ILIVYOSANIFISHWA KWENYE WIMBO WA "NDIO MZEE" WA PROFESA JAY.

TUSIREJEE MAKOSA YA 2005,PLEEEEZ!


The media as the source of information has the power influence public opinion. But before getting into how it might, it is important to know what my understanding of public opinion. I would define public opinion as the opinion shared by the majority of the public. Majority because it is almost impossible to find an absolutely agreed opinion among people with different social and economic background, racial differences, age, gender, etc. Gauging public opinion is normally done by using opinion polls, which as we all know, are merely representative of opinions shared by different groups in a given society, or in research terms, population.

If a study that is measuring public opinion on the impact of global warming finds 75% of respondents thinks that global warming possess a major threat to the future of mankind, it would then be concluded as “the study found that global warming is actually a threat to the future of mankind.”Public opinion is more about what many, and not necessarily all, think about something rather than what each of us think.

Take an example of the Loch Lomond “myth.” Majority of those who believe about the Loch Lomond monster have not even been to Scotland, let alone Loch Lomond itself. One of the reasons for the publicity of the myth has been the stories we frequently hear of read, or hear from, the media. The publicity has led to many us believing the existence of the Loch Lomond monster. If there were an opinion poll on whether people believe there is actually a monster there, the results could very likely be “yes” mainly because a larger section of the media has led us to believe that way.

As the public is made of individuals, it is difficult for each of them to make their opinions known, hence the usefulness of the media in giving a medium for a rather general collection of what each of us think about something. If manipulated, the media could as well lead us into believing that majority of us something is the way it is because many think so. Neglecting deviants, many people tend to be conformists in the sense that they normally do not want to look different from what the majority’s position. Therefore, as the Americans were led to believe by a section of the US media that the Saddam Hussein’s regime was actually linked for the 9/11 atrocities, rather than a neo-con agenda spearheaded by the likes of Donald Rumsfield, Richard Perle and Paul Wolfowitz,so does a section of the British public becomes influenced in their opinion by The Sun, The Daily Express, The Daily Telegraph and The Daily Mail that asylum seekers and refugees as actually among the causes of the country’s economic problems.

A biased media could in short or long run effectively influences public opinion because it communicates what “A” thinks in Derbyshire and “B” thinks in Lanarkshire. Or in an international perspective, what Maggie thinks in Glasgow and Evarist thinks in Dar es Salaam, Tanzania. It is even more effective in shaping public opinion in the less educated or less informed section of society that normally takes what is said by the media for granted.

During the 2005 general election campaigns in Tanzania, the ruling party courted the media to publicise a story that a neighbouring country’s army was planning to invade Tanzania. The ruling party then went on urging reminding the voters how the country emerged victorious in the 1978-79 war against Uganda under its (the ruling party’s) leadership. Some analysts believe that although the gimmick did not directly determine the outcomes of the election it all the same helped the ruling party to identify itself to voters as one they could rely on during uncertain times.

Exploiting the ineffectiveness of the Kenyan political situation in which a coalition of opposition parties successfully broke an “African political taboo” that a ruling party never loses an election, CCM-Tanzania’s ruling party-has frequently used the media during elections to tell voters that bringing an opposition into power could not solve the country’s problems, referring to the Kenyan situation. The pro-CCM media has also been telling Tanzanians that regardless of how bad they think of CCM, it still is the “devil they know”, and therefore should never try a political experience of voting an opposition party into power. Many would agree despite proving wrong in some African countries such as Ghana the trick has been very successful.

The pro-government media in Sudan has also been effective in swaying public opinion in favour of President Al-Bashir when he a warrant was made by the International Criminal Court in The Hague accusing him of being responsible for genocide in the Darfur region. The media working under the directives of the Sudanese government portrayed the warrant as an attempt by the West to re-colonise Africa.

Although public opinion could also shape opinion in the media, it is rather for commercial purposes than public interest. When The Daily Mail ran an exclusive story about an “illegal immigrant” employed by Baroness Scotland, it fair to believe that based on its strong anti-immigration stance, it did not do so to sympathise with the plight faced by those who make a choice of being in the UK illegally but rather to amass pressure to force the peer out of office.

If we agree that although the media the primary source of information broadcasted or published by the media comes from the public, and therefore a need to see the media serves the interest of the public, it still remains true that the flow information has usually been from the media to the public in terms of news consumption. The point here is that the media collects information from the public not for final consumption but rather for the public consumption. It is on such views that I argue that it is the media which shapes public opinion, and not vice versa.


5 Oct 2009


KWANGU,MISINGI MIKUU YA NYERERE ILIKUWA UJENZI WA JAMII YENYE USAWA NA INAYOTHAMINI UTU WA BINADAMU.UHURU BILA USAWA NI POROJO.UMOJA KATIKA LINDI LA UMASIKINI NI SAWA NA USINGIZI WA PONO KWENYE UTANDO WA BUIBUI.NA MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA HAYAWEZI KUPATIKANA KATIKA SIASA ZA KUKUMBATIA MAFISADI SAMBAMBA KUKEMEA WAPAMBANAO NA UFISADI,KUTOJUA VIPAUMBELE VYA NCHI,NA KUENDELEZA AHADI ZA MAENDELEO ILHALI ZILE ZA AWALI HAZIJATEKELEZWA.

JK AMEKUMBUKA MISINGI YA MWALIMU.MSOME KATIKA HABARI IFUATAYO:

Mwandishi Maalum, Mwanza

RAIS Jakaya Kikwete ametaja misingi mikuu mitatu iliyowekwa na Baba wa Taifa, Hayati Julius Nyerere katika kulijenga taifa la Tanzania, misingi ambayo rais alisema ni kumbukumbu yao kuu kwa kiongozi huyo wa harakati za Uhuru wa Tanganyika.

Rais Kikwete aliwashangaa Watanzania ambao wanabeza Uhuru wa Tanzania na kufurahia wakati jina la Tanzania linaposhambuliwa na wageni.

Aliitaja misingi hiyo mikuu kuwa ni uhuru, umoja wa taifa la Tanzania, na safari ya kujenga maisha bora kwa kila Mtanzania iliyoanza hata kabla ya Tanganyika kupata uhuru wake rasmi Desemba 9, 1961.

Rais Kikwete alisema hayo mjini Mwanza juzi alipozungumza na vijana wa CCM ambao wanaanza safari ya kuelekea kijijini Butiama mkoani Mara, ikiwa ni matembezi ya kumuezi Mwalimu Nyerere ambaye alifariki miaka 10 iliyopita baada ya kuugua saratani ya damu.

Mwalimu Nyerere alifariki Oktoba 14, 1999 akiwa amelazwa hospitali ya St Thomas jijini London, Uingereza.

Vijana 166 kutoka mikoa yote ya Tanzania wanashiriki katika matembezi hayo ya siku 10 ambayo yatapitia njia ambayo Mwalimu Nyerere alitembea mwaka 1967 katika kuunga mkono na kuhamasisha Azimio la Arusha.

Kauli mbiu ya matembezi hayo ni “Uhuru na Kazi” na miongoni mwa mambo ambayo vijana hao watafanya njiani ni kukarabati Shule ya Msingi ya Mwisenge ambako Mwalimu Nyerere alipata elimu yake ya msingi.

Rais Kikwete alisema kuwa urithi mkuu ambao Mwalimu aliwaachia Watanzania ni misingi hiyo mikuu ambayo imeendelea kulifanya Taifa la Tanzania kuwapo na kuwa imara.

Rais Kikwete alisema kuwa kila taifa duniani lina waasisi wake ambao wanastahili kuendelea kukumbukwa siyo tu kwa uasisi pekee, bali pia kwa mambo ambayo waliyasimamia, waliyaamini na waliyajenga.

"Wamarekani wanaye George Washington… sisi tunaye Mwalimu Julius Kambarage Nyerere… na kila nchi ina muasisi wake ambaye anakumbukwa kwa aliyoyasimamia," alisema JK.

"La kwanza la kumkumbuka Mwalimu ni uhuru wa nchi yetu. Huyu alikuwa ni kiongozi aliyeambiwa achague kati ya siasa ama kazi ya ualimu… huyu mzee wetu akachagua siasa na utumishi wa umma bila hata kujua atakula nini.

"Akachagua kupigania uhuru wa nchi yetu. Kama mnavyojua nyote hii kazi ya siasa ni kamari... unakwenda kugombea ukijua kuna kupata ama kukosa... lakini yeye alifanya uamuzi sahihi wa kupigania uhuru,"

Rais Kikwete alisema kuwa uhuru siyo mipaka bali ni heshima ya nchi na ndiyo maana Tanzania haitasita kumkabili yoyote ambaye atajaribu kuchezea uhuru huo.

Alisisitiza: "Mwaka 1978 yule msanii na profesa wa historia na jiografia, Idi Amin alivamia nchi yetu… na sisi tukamfurumusha ili kulinda uhuru wetu na wako wenzetu ambao walipoteza maisha yao kwa ajili ya kulinda uhuru wetu. Wamelala Kaboya (mkoani Kagera) na tutaendelea kuwaenzi kwa sababu walijitolea kulinda uhuru wetu."

Rais Kikwete pia aliwashangaa watu wote ambao wanafurahia wakati heshima ya Tanzania inapobezwa na wageni.

"Uhuru siyo mipaka kama nilivyosema. Uhuru ni heshima ya taifa letu. Wako wale wenzetu wanaofurahi wakati wageni wanaposhambulia nchi yetu. Ni wajibu wetu sote kuhakikisha kuwa uhuru wetu hauchezewi na mtu yoyote,"alisema.

Kuhusu umoja wa taifa, Rais Kikwete alisema Mwalimu alihakikisha kuwa uhuru wa nchi unazaa umoja ili nchi iwe moja na isigawanyike vipande vipande kwa sababu yoyote ile.

"Aliondoa viashiria vyote vya kuvunja umoja wa taifa tokea mwanzo kabisa. Aliondoa uchifu ili kuondoa nguvu za ukabila. Alitambua hatari ya dini na akataifisha shule zote za dini ili vijana wetu waelimishwe na kulelewa kama vijana wa taifa moja na siyo vijana wa dini tofauti,"alisema Kikwete.

Rais Kikwete alisema kuwa hata kabla ya uhuru, Mwalimu alitambua kuwa ili uhuru na umoja viweze kudumishwa ni lazima wananchi wake wapate maisha bora na ndiyo maana akawatambua maadui wakuu watatu – ujinga, maradhi na umasikini- na njia za kukabiliana na maadui hao.

CHANZO:
Mwananchi

BAADHI WANAHOJI KUHUSU MANTIKI YA UHURU ALIOPIGANIA BABA WA TAIFA NA WENZAKE.TULIMKIMBIZA MKOLONI ILI TUJITAWALE NA KUFAIDI RASLIMALI ZETU KWA HAKI NA USAWA.JAPO SIO EXCUSE,LAKINI MKOLONI HAKUTUJALI KWA VILE HAKUWA MTANZANIA.LEO HII WANAOTUTENDA VIBAYA ZAIDI YA WAKOLONI NI WATANZANIA WENZETU,WENGI WAO WAKIWA WALIOSOMOSHWA KWA SHIDA NA FEDHA ZA WATANZANIA WENZAO.KUNDI JINGINE NI LA MABWANYENYE WALIOPTA URAIA KWA VIJISENTI VYAO NA WAKOLONI -MAMBOLEO WALIOREJEA KWA JINA LA WAWEKEZAJI.NYERERE HAKUPIGANIA UHURU ILI WAGENI WAJE NA DOLA MOJA NA KUONDOKA NA MAMILIONI YA DOLA,AU AKINA LOWASSA KUTUINGIZA MKENGE KWENYE RICHMOND,NA USANII MWINGINE WA KISIASA.

UHURU PASIPO UONGOZI BORA NI SAWA NA KUWA NA VOGUE LENYE DEREVA MLEVI AU KIPOFU;LITATUMBUKIA MTARONI KAMA SI KUPORWA NA MAJAMBAZI.UHURU ILHALI TUMEBANWA NA NIRA ZA MAFISADI NI UTANI MBAYA KWA WALIOPIGANIA UHURU WA NCHI YETU.WEZI WA KAGODA WAMEHIFADHIWA HADI LEO,MASHIRIKA YA UMMA YAMEGEUKA KICHAKA CHA WATU KUHUJUMU KISHA WABADILISHIWE (REJEA MATTAKA NA ATCL),WAZEMBE WANAENDELEA KULINDWA KWA VILE TU KUWABADILISHA KTATHIBITISHA MAPUNGUFU YA ALIYEWATEUA IN THE FIRST PLACE,NA HADITHI NYINGINE ZA KUSIKITISHA.

HATUKUPIGANIA UHURU KUPATA HESHIMA FEKI MACHONI MWA JUMUIYA YA KIMATAIFA BALI AMANI NAFSINI NA MIILINI MWETU KAMA WATANZANIA.

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.