26 Mar 2010


How do we best deal with bastards who not only keep on screwing our economy but also put their middle fingers up whenever they see us from the windows of their mansions or Range Rover Vogue,all obtained through unlawful conduct?I know this might sound crazy but,well,something gotta be done.We could try what the North Korean authorities did recently: a high ranking official who oversaw last year’s disastrous currency revaluation has been executed by firing squad.Well,crazy as it might sound but we simply can't let a privileged few plunder our economy while enjoying protection by the same people entrusted with the responsibility of emancipating us from the present abject poverty.Does it really make any sense,for instance,to see the DPP and PCCB dilly-dally in dealing with an illusive monster known as Kagoda?Or,is there any reason why Mzee wa Vijisenti is not in prison for his involvement in the radar scandal?Adding salt to a wound,we now learn that the much-hyped stimulus package has eventually ended up in the coffers of some shady firms which seem to have been formed purposefully to skin as alive just like those involved in the EPA scandal.Or,did they take a leaf out of the way our law enforcement institutions "dealt with" the real culprits of such scandals as Richmond,Kiwira,IPTL?

Call me a prophet of doom but the way those in power deal with ufisadi in our country is a total disgrace and has a potential of creating chaos in the very near future.It actually inspires a new breed,or rather a culture, of ufisadi as getting away with screwing the country becomes a norm.

Unfortunately,while the executed official in North Korea had "a privilege" of being dealt with by the State,our mafisadis might not be so "lucky".When people finally come to a realisation that it is useless to expect anything from their government in dealing with white collar criminals,they might resort to vigilantism,meaning people taking law in their own hands by shooting mafisadi at sight.And that would be too late for "justice" to take it course (it always does when walalahoi 'commit offences').

By the way,mlalahoi has got nothing to lose if sent to prison where their daily needs would then be taken care of by the state,something they hardly enjoy in their "normal" life as good citizens.

24 Mar 2010


Kwa muda mrefu sasa Kanisa Katoliki limejikuta likigubikwa na kashfa za ngono.Hivi karibuni pepo mbaya amezidi kulizungukia Kanisa hio baada ya taarifa kwamba kaka wa Baba Mtakatifu,Georg Ratziger, aliwatangwa makofi wanakwaya wake katika miaka ya 1960.Kwa kitambo sasa,inaonekana Kanisa limekumbwa na jukumu kubwa la kuomba msamaha kutokana na tuhuma za unyanyasaji wa kijinsia (na ulawiti) sambamba na jitihada za kusafisha sura yake.Hata hivyo,pamoja na kuendelea kuibuka kwa tuhuma hizo zisizopendeza,Kanisa Katoliki limeendelea kubaki 'safi' barani Afrika.Je hali hiyo inasababishwa na nini?Na je itaendelea kwa muda gani?Binafsi siamini kwamba tuhuma zinazolikabili Kanisa hilo haziligusi Bara la Afrika,na hususan Tanzania.Tofauti iliyopo ni kwamba imani za kiroho katika nchi zilizoendelea zina tofauti ya namna flani na ilivyo katika nchi zinazoendelea.Yayumkinika kusema watumishi wa Bwana katika nchi kama Tanzania wameendelea kunufaika na unyenyekevu uliokubuhu kutoka kwa waumini wao ilhali katika nchi za Magaharibi imani haimaanishikufumbia macho mauvu ya wasimamizi wa imani hiyo (i.e. watumishi wa Bwana).

Nadhani si mie peke yangu ninayefahamu kwamba baadhi ya watumishi wa Bwana wana watoto,kinyume kabisa na kanuni na taratibu za Kanisa Katoliki.Katika jimbo nililozaliwa,suala hilolinaonekana la kawaida sana kiasi kwamba baadhi ya watumishi wa Bwana wanamudu kuhudumia 'familia' zao (wanawake waliowapa ujauzito na kupata watoto wa wachunga kondoo wa Bwana) pasipo kificho.

Utumishi wa Bwana katika nchi yetu hauna tofauti sana na kinachoendelea kwenye siasa zetu.Tunafahamu wanasiasa wabovu lakini kwa vile wanamwaga vijizawadi hivi na vile tunaendelea kuwalea na hatimaye wanaoendelea kuipeleka mrama nchi yetu.Waumini wengi wa Kanisa Katoliki huko nyumbani wanafahamu fika maovu yanayotendwa na BAADHI ya watumishi wa Bwana lakini wanaendelea kufumbia macho.Natambua kuwa Maandiko Matakatifu yanasisitiza kuzingatia zaidi maneno/mafundisho ya viongozi wetu wa dini na sio kutilia mkazo mateno yao,lakini ni dhahiri padre mzinzi hawezi kuwa na mamlaka ya kiroho (moral authority) kukemea uvunjaji wa amri ya sita.

Na kuna imani kwamba kusuasua kwa baadhi ya viongozi wa dini huko nyumbani kukemea ufisadi na maovu mengine ya wanasiasa kunasababishwa na ukweli kwamba baadhi ya viongozi hao wa dini wanatambua kuwa 'hawako safi kihivyo'.Kama ilivyokuwa wakati wa sakata kati ya serikali na madhehebu ya dini kuhusu ushuru katika bidhaa zinazoingizwa nchi na madhehebu hayo,ambapo baadhi ya wanasiasa walidiriki kusema 'wanafahamu mengi kuhusu baadhi ya viongozi hao wa dini' ni dhahiri wachunga kondoo wa Bwana wanafahamu fika kuwa matendo yanayokiuka maadili yao yanafahamika na wanasiasa wangeweza 'kuwaumbua' kwa kuyaweka hadharani.

Hakuna anayefahamu hatma ya pepo huyu mchafu anayelitesa Kanisa letu lakini kilicho bayana ni athari zake kwa kondoo wa Bwana.Tayari kuna taarifa kwamba kuna mtikisiko wa kiimani katika nchi zinazofahamika kama vinara wa Ukatoliki kwa mfano Ujerumani,Austria na Ufaransa.Hali pia si shwari huko Vatican kiasi kwamba 'mpunga mapepo mkuu' (chief exorcist) katika makao makuu ya Kanisa hilo,Father Gabriel Amorth alinukuliwa akisema kuwa shetani ameweka makazi yake sehemu hiyo.

Wakati Kanisa Katoliki barani Afrika,Tanzania included,likiwa shwari katika kipindi hiki cha upepo mbaya wa shetani,ni muhimu kwa wachunga kondoo wa Bwana wanaokiuka mafundisho ya Kanisa hilo kujirudi wakitambua kuwa siri zao haitadumu milele.Pia ni muhimu kwao kufahamu kuwa japo wanasitiriwa kutokana na unyenyekevu uliopitiliza wa waumini wao,Mungu wanayemtumikia anaowaona na anakasirishwa sana.Japo wanaweza kuendelea kusalimika kutokana na waumini kuendelea 'kuwafumbia macho',ni dhahiri kuwa wasipobadilika wataishia kuwa kuni za kuchochea moto unaowachoma wadhambi huko 'motoni'.

Juma Kuu linapaswa kuwa kipindi kizuri kwa Kanisa Katoliki kila mahali kungalia wapi limejikwaa (na sio lilipoangukia) na kisha kufanya marekebisho yanayostahili.Na kwa Nguvu za Bwana,yote yanawezekana.

Tmsifu Yesu Kristo,Milele Amen.

22 Mar 2010


Kiongozi shurti awe na msimamo na kisha asimamie kile anachoamini.Kwa mara nyingine,Rais Barak Obama ameithibitishia dunia kuwa ni 'mwanaume wa shoka' linapokuja sula la kuamini anachosimamia.Hatimaye jana Obama alifanikiwa kupitisha sera yake ya mabadiliko katika mfumo wa afya ya jamii nchini Marekani.Hiyo ni baada ya safari ndefu na ngumu pengine zaidi ya kampeni yake ya kuingia Jumbe Jeupe (White House).Pamoja na kuhatarisha nafasi yake na ya chama chake kisiasa,Obama alipigana kiume kuhakikisha kuwa lazima mabadiliko hayo yafanyike,kwa gharama yoyote ile.Na kama inavyofahamika,mara nyingi maamuzi ya kihistoria huwa na tabia ya kutokuwa maarufu. Ushindi wa Obama katika suala hili unapaswa kuwa fundisho muhimu kwa Rais wetu Jakaya Kikwete ambaye miezi michache ijayo atahitimisha miaka yake mitano tangu aingie madarakani.Sote tunafahamu,with exception ya wale wanaopenda habari nzuri tu hata kama ni za uongo,kwamba kwa kiasi kikubwa ahadi za Kikwete kuikomboa Tanzania kutoka kwenye lindi na umasikini imebaki kuwa hadithi tu huku ufisadi ukishamiri na kuitafuna Tanzania kwa kasi ya ajabu.Yayumkinika kusema kwamba utawala wa Kikwete utakumbukwa zaidi kwa skandali kuliko ufanisi wa kuwatumikia Watanzania.Kibaya zaidi,Kikwete alitoa lundo la ahadi kuhusu namna atakavyoboresha maisha ya Watanzania,hence kauli-mbiu MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA.

Kuna wanaodhani kuwa kilichomsukuma Kikwete kuogmbea urais mwaka 2005 ni kukamilisha ndoto yake ya mwaka 1995 'iliyokwazwa' na Baba wa Tiafa Mwalimu Julius Nyerere.Wenye mtizamo huo wanaamini kuwa Kikwete alitumia miaka 10 iliyofuata akikusanya nguvu,sio katika namna gani atawatumikia Watanzania,bali atakavyoweza kuingia Ikulu.Ni katika 'piga ua' hii ndipo alijikuta akishirikiana na 'viumbe hatari' waliojipenyeza kwa kivuli cha 'wanamtandao' wakiwa na matarajio makubwa kuwa Kikwete akiingia Ikulu basi nao 'wameula'And they were not wrong.Kusuasua kwa Rais wetu katika kuchukua maamuzi mazito kumechangiwa zaidi na ushirika wake na watu hao.Na hii haiwezi kuwa excuse kwake kwa sababu alikuwa na kila sababu na uwezo wa 'kuwasaliti' laiti angekuwa na nia.Angeweza kabisa kuwaita Ikulu na kuwaambia 'nathamini sana mchango wenu kuniingiza madarakani,lakini mimi sasa ni Rais wa Watanzania wote ninayeongozwa kwa misingi ya Katiba.I'm sorry,atakayekwenda kinyume na sheria na taratibu za nchi basi sheria itachukua mkondo wake.Tubaki marafiki lakini sio kwa urafiki wa kukwamisha utawala wangu'.Simple and clear!

Tupo wengine tunaoamini kuwa licha ya ndoto hiyo iliyoanza 1995,Kikwete pia alisukumwa na dhamira ya kuwatumikia Watanzania.Na kututhibitishia kuwa tuko sahihi,alipoingia tu madarakani alitoa hotuba zilizoonyesha kuwa anafahamu kwa kina vikwazo vya maendeleo ya taifa letu.Aliweka wazi kuwa rushwa ni tatizo kubwa na angefanya kila awezalo kupambana nayo.Kama ilivyokuwa kwenye hotuba zake za wakati wa kampeni,Kikwete alipoingia madarakani alirejea kuahidi makubwa kwa Watanzania,na wengi tulimwamini kwa vile alikuwa akiongea lugha tunayoielewa (tofauti na Mkapa aliyezowea kutoa hotuba 'ngumu' kana kwamba ni mihadhara ya kitaaluma chuo kikuu).

Dalili ya kwanza kuwa Kikwete 'hana jipya' ni kauli yake kuwa 'anawafahamu wala rushwa bali anawapa muda wa kujirekebisha'.Nadhani kauli hiyo itaingia kwenye vitabu vya historia kama ya aina yake kwa mkuu wa nchi kutoa deadline kwa wahalifu.Lakini baadhi yetu tulijipa matumaini kwamba labda Rais alikuwa serious katika kauli hiyo,na kwamba baada ya deadline hiyo ku-expire angechukua hatua flani.Miaka mitano baadaye,sote tunafahamu sasa kuwa kauli hiyo ilikuwa mithili ya 'kumtishia mtu mzima nyau'.Na si kwenye kauli hiyo tu,bali tuliambiwa wakati flani kuwa amekabidhiwa orodha ya wauza madawa ya kulevya (na aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani Bakari Mwapachu) na baadaye tena akatuambia kuwa anawafahamu wala rushwa pale Bandari Dar es Salaam,na majina anayo.So far,hajachukua hatua kwa wauza madawa ya kulevya (wa orodha ya Mwapachu) na hajawasilisha majina ya wala rushwa wa Bandari!Sasa kama Rais hataki kutoa majina ya wala rushwa anaodai anawafahamu,tutegemee nini kutoka kwa mwananchi wa kawaida?

Kama nilivyosema mwanzoni mwa makala hii,uongozi ni kusimamia katika kile unachomini hata kama kitakupunguzia umaarufu.Kikwete alipaswa kufahamu kuwa ili urais wake uwe na manufaa kwa Watanzania ni lazima 'akosane' na baadhi ya marafiki zake.Na kwa hakika hilo lingekuwa na maana zaidi kwani ni bora zaidi mara milioni kupendwa na Watanzania walio wengi na 'kuchukiwa na mafisadi wachache' kuliko kupendwa na 'kigenge kidogo cha mafisadi' na kulaumiwa na mamilioni ya Watanzania.Kama Kikwete alikuwa na dhamira ya dhati ya kuwaletea Watanzania maisha bora alipaswa asimame kidete kuhakikisha hilo linatimia kwa udi na uvumba.

Lakini kwa vile bado kuna miezi kadhaa kabla ya uchaguzi,na kwa vile Obama ametioa darasa zuri kwa viongozi ya type ya Kikwete,basi tunabaki with our fingers crossed kuwa huenda rais wetu nae akajitutumua na kurekebisha mambo katika muda huu uliosalia.Uzuri ni kwamba hata kama ufisadi umetuumiza kwa muda wote huu,uamuzi wa kuukalia kooni katika dakika hizi za majeruhi utafanikiwa kufuta machungu yote tuliyopitia.Ni kama katika fainali ya soka ambapo bao la ushindi linapatikana katika dakika za majeruhi.Shamrashamra zitakazoambatana na ushindi huo hazitajali kuwa bao la ushindi limepatikana dakika za lala salama.What matters ni ushindi.

Basi Rais Kikwete tunatarajia sasa utafanya kweli.Utatamka bayana kuwa ile deadline uliyotoa kwa wala rushwa unaowafahamu ime-expire na kuamuru vyombo vya dola viingie ulingoni (yes,vimekuwa vikiwajibika baada ya ruhusa yako).Utakabidhi ile orodha ya mafisadi ya pale Bandarini ambayo watendaji wanaisubiri ili wachukue hatua zinazostahili.Utaifanyia kazi pia ile orodha ya 'wauza unga' ulokabidhiwa na Mwapachu.Utaamuru wamiliki wa Kagoda wawekwe hadharani na kuchukuliwa hatua zinazostahili.Ukiwa mwenyekiti wa CCM,utatambua kuwa uwepo wa Mzee wa Vijisenti kwenye Kamati ya Maadili ya chama hicho licha ya tuhuma zinazomkabili ni mzaha usiokubalika,na utashauri awekwe kando hadi taratibu za kisheria zitapochukua mkondo wake.Utaamua kuwa suala la Richmond haliwezi kumalizwa 'kishkaji' bali wahusika wote watachukuliwa hatua ili iwe funzo kwa wanaotumia madaraka yao vibaya.Na mwisho,utaanza kutafsiri kwa vitendo ahadi zako lukuki ulizotoa wakati wa uchaguzi na kuendelea kuzitoa kwa muda wote uliokuwa madarakani.Rejesha ari,kasi na nguvu mpya katika kuleta MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA.

Kama Obama ameweza,wewe unaweza pia.It's all about kuamini unachosimamia na kusimamia unachoamini.

20 Mar 2010


MNYAMA AUA ZIMBABWE. Andrew Kingamkono, Harare.

MABINGWA wa soka Tanzania Bara Simba wameirarua Lengthens ya Zimbabwe mabao 2-0 katika mechi ya kuwania kombe la Shirikisho la chama cha soka Barani Afrika CAF iliyofanyika kwenye uwanja wa Rufaro,nchini Zimbabwe.

Mpira ulianza kwa kasi ambapo katika dakika ya 3 Lengthens FC 'Happy People' waliwakosa Simba.

Katika kipindi cha kwanza mabeki wa kati wa Simba Joseph Owino na Kelvin Yondani walikuwa wakijichanganya sana na kuonekana kutoelewana,ambapo kuna wakati bado kidogo wasababishe bao ila mshambuliaji wa Lengthens,Uzukamanda alipiga shuti ambalo lilidakwa na kipa wa Simba Juma Kaseja.

Katika dakika ya 32 Simba ilipata bao la kwanza lililofungwa na Mohamed Banka kwa mpira wa adhabu baada ya kupasiwa na Joseph Owino. Mpira huo wa adhabu ulitokea baada ya Ramadhan Chombo kuangushwa nje ya 18.

Simba iliandika bao la pili katika dakika ya 34 ambalo lilifungwa na Mussa Hassan Mgosi kwa kichwa baada ya kuunganisha mpira wa adhabu uliopigwa na Joseph Owino kutoka winga ya kulia.

Joseph Owino alipiga mpira huo wa adhabu baada ya Nico Nyagawa kufanyiwa faulo.

Lengthens ilitawala mchezo kwa muda.lakini Simba walionekana kurudi mchezoni japokuwa Lengthens walionekana kumiliki zaidi soka kwa kucheza soka ya pasi fupi fupi.

Katika dakika ya 44 na 47 Altwell Nyawima wa Lengthens FC alikosa mabao mawili ya wazi.

Mpaka mapumziko Simba ilikuwa ikiongoza kwa mabao 2-0. Lengthens katika kipindi cha kwanza ilikuwa ikipeleka mashambulizi yao katika winga ya kushoto ambapo alikuwepo beki Haruna Shamte aliyechukua nafasi ya Juma Jabu ambaye alikuwa jukwaani akishuhudia pambano,lakini beki Kelvin Yondani alifanya kazi ya ziada kuzuia mashambulizi ya Lengthens.

Kipindi cha pili kilianza ambapo kulikuwa hakuna mabadiliko ya wachezaji kwa pande zote mbili. Lengthens walianza kipindi hicho kwa kasi na walikosa mabao mawili ambapo shuti la Nhamo liligonga mwamba.

Simba ilifanya mabadiliko ambapo iliwatoa Mike Barasa na Nico Nyagawa na nafasi zao kuchukuliwa na Jabil Aziz na Ulimboka Mwakingwe. Pia Lengthens iliwatoa Steven Matsangaise,Nhamo,Mparati na kuwaingiza Mike Mhunsu,Patrick Makuwaza.

Mabadiliko hayo yaliisaidia Lengthens kurudi mchezoni ambapo katika dakika ya 72 bado kidogo Nyawima afumanie nyavu.Pia katika dakika ya 76 Nxawma alikosa bao akiwa na kipa Juma Kaseja.

Simba ilipata Shambulizi la maana katika dakika ya 83,lakini mshambuliaji Mussa Mgosi alipiga shuti ambalo lilipaa juu ya mwamba.

Kiujumla beki ya Simba inastahili pongezi kwa kucheza kwa kujituma na kuzuia kwa hali ya juu.

Katika mechi hiyo mchezaji wa Simba Haruna Shamte alipewa kadi ya njano kwa kumchezea vibaya Dylaan Chiroodza.

Simba ilifanya mabadiliko tena kwa kumtoa Ramadhan Chombo na kumuingiza Jerry Santo.

Mchezo wa Simba dhidi ya Lengthens ulihudhuriwa na mashabiki wachache kwa sababu jana ilikuwa ni siku ya kazi.

Kikosi cha Simba kilikuwa; Juma Kaseja,Haruna Shamte,Salum Kanoni,Kelvin Yondani, Joseph Owino,Mohamed Banka,Nico Nyagawa,Hillary Echesa,Mussa Hassan Mgosi,Mike Baraza na Ramadhan Chombo.

Lengthens:Makuvarara Lovemore, Mteili Richard,Mparati Tawanda,Machoma Casper,Mono Goderey, Bruce Tshuma,Richard Mteki,Patrick Nshamo,Altwell Nyawima,Asmir Ozukakamanda na Tawanda Mparati.

Mbali na mchezo huo, Caps United ya Zimbazwe itacheza na Morroca Swallows kesho wakati mabingwa wa Zimbabwe Gunners wataonyeshana kazi na Al Ahly ya Misri waliowasili hapa juzi.

CHANZO: Mwananchi.

19 Mar 2010


Katika gazeti la Tanzania Daima toleo la jana (mtandaoni) kulikuwa na habari kuhusu Taasisi ya Kimataifa ya Malaria No More kumfungulia mashtaka msanii nguli wa bongofleva,Joseph Mbilinyi a.k.a Sugu.Kwa mujibu wa habari hizo,Malaria No More imefungua kesi hiyo ya madai kfuatia kauli za Sugu kuwa wazo la kufanya tamasha (lililofanyika hivi karibuni na kuhudhuriwa na Rais JK) la kuhamasisha mapambano dhidi ya ugonjwa wa malaria lilikuwa lake.Kwa vile suala hili liko mahakamani,na kwa vile mie si mjuzi wa sheria,sintazungumzia kesi hiyo bali nitaangalia kipenre katika habari husika kuwa tangu mwaka 2006 Malaria No More ikishirikiana na Wizara ya Afya imetoa vyandarua 267Binafsi nimeshtushwa sana na takwimu hiyo.Yaani kwa wastani,taasisi hiyo imekuwa ikitoa vyandarua 66 kwa mwaka.Kama takwimu hizo ni sahihi basi huu utakuwa ni mzaha wa hali ya juu.Pamoja na nia njema ya Malaria No More lakini vyandarua 66 kwa mwaka ni idadi ndogo mno.Kwa mujibu wa PBS Newshour malaria husababisha vifo vya watoto wa Kitanzania kati ya 60,000 na 80,000 kwa mwaka.Sasa huhitaji kuwa mtaalam wa hisabati kutambua kuwa wastani wa vyandarua 66 kwa mwaka ni mithili ya tone kwenye bahari.

Hata hilo tamasha lenyewe la kuhamasisha mapambano dhidi ya malaria lilikuwa na mzaha wa aina flani.Kwa mfano,ilielezwa kuwa "wageni maalum" walipewa zawadi za vyandarua huku "walalahoi" ambao kimsingi ndio waathiriwa wakubwa wa malaria walisahaulika.Sasa kama tunaamua kufanya hamasa ya kitaifa dhidi ya janga halafu tunaleta "ubaguzi" kati ya waheshimiwa na walalahoi,hiyo malaria itatokomezwa kweli?

Kama ambavyo blogu hii imekuwa ikiandika mara kadhaa,tatizo letu kama nchi haliko kwenye mipango bali usimamizi na utekelezaji wa mipango hiyo.Matamasha yanaweza kuwepo kila wikiendi lakini pasipo usimamizi mzuri na utekelezaji wenye lengo la kuzaa matunda itakuwa ni kazi bure.

Na kwa waungwana wa Malaria No More,pamoja na nia njema mliyonayo ya kutusaidia kutokomeza ugonjwa huu hatari,ni dhahiri kuwa kasi yenu ni ya kutia shaka.Nimerejea kusoma habari husika mara mbili mbili nikidhani labda ni makosa ya kiuchapishaji lakini inaelekea takwimu zenu ni sahihi.Kwa mwenendo mlionao (wa kutoa vyandarua 267 tu tangu mwaka 2006) mtaendelea kubaki "wadau muhimu" katika mapambano dhidi ya malaria lakini ni wazi kuwa mafanikio ya harakati zenu yatabaki kuwa kiduchu.

Mwisho,nadhani kuna umuhimu wa pande zote husika katika sakata hili la nani mmiliki wa wazo la tamasha la kuhamasisha vita dhidi ya malaria kukaa pamoja na kutafuta mwafaka.

18 Mar 2010


Vigogo watajwa kujipa fedha zilizotolewa BoT
Ni Zile za Kunusuru Uchumi (Stimulus Package)

MATUMIZI ya Sh trilioni 1.7 kuhami uchumi dhidi ya mtikisiko wa kiuchumi duniani ulioathiri kampuni za ununuzi pamba mikoa ya kanda ya ziwa na hatimaye kampuni hizo kumegewa sehemu ya fedha hizo sasa yamezua utata, na sasa baadhi ya wakubwa wanatajwa kuwa sehemu ya walionufaika na fedha hizo, Raia Mwema imeelezwa.

Fedha hizo kupitia mfuko maalumu, maarufu kwa jina la ‘Stimulus Package’ , zilipitishwa na Bunge wakati wa bajeti lakini Kambi ya Upinzani Bungeni, kupitia kwa kiongozi wake Hamad Rashid Mohamed ilionya fedha hizo kuibua kile kilichoitwa kashfa ya EPA namba mbili, na kupendekeza fungu hilo liundiwe sheria ili kuwabana wahusika lakini serikali ilipuuza, ikitumia wingi wa wabunge kutoka CCM.Takriban miezi sita sasa tangu fedha hizo kuanza kutolewa, uchunguzi wa Raia Mwema katika kipindi hicho umebaini kuwa baadhi ya fedha zimekwenda katika kampuni zisizofahamika ama ambazo wahusika halisi hawajulikani na badala yake wamewatanguliza watu wengine.

Imeelezwa kwamba sehemu ya kampuni zilizochotewa mamilioni kutoka kitita hicho cha Sh bilioni 1.7 zina uhusiano na vigogo serikalini na wanasiasa na kwamba fedha hizo hazikukidhi matarajio ya serikali kwa wakulima wa pamba.

Kampuni ambazo zinaonekana katika orodha ya zilizopendekezwa ama zilizopata fedha hizo ni pamoja na S & C Ginning Co.Ltd (yenye makao yake Bulamba), Simon Agency Ltd (Mwanza), Fresho Investment Co. Ltd (Shinyanga), Gaki Investment Co. Ltd (ya Shinyanga), Bedugu Ginning Co. Ltd (ya Musoma), Intergrated Cotton Fields Ltd ( ya Mwanza), Igunga Cotton Company (makao yake yako Dar es Salaam), Robasika-Agroproducts Ltd yenye makao yake Kaliua, Tabora na Chesano Cotton Ginnery yenye makao yake Bariadi, Shinyanga.

Kampuni nyingine kwenye orodha hiyo ni Copcot Cotton Trading (Geita), Allanoe Ginneries Ltd (Mwanza), Shinyanga Region Co-op Union (Shinganya), Vsarrian Tanzania Ltd (Bunda), Birchand Oil Mill (Mwanza), Jambo Oil Mill (Shinyanga), Afrisian Ginning Company (Dar es Salaam) na S.M Holdings Ltd (Mwanza).

Nyingine ni Nida Textile Mills Ltd, Hassanal R. Waiji (Maswa), Blore Tanzania Ltd (Mwanhuzi, Shinyanga), Al-Adawi Co.Ltd (Mwanza), Olam Tanzania Ltd (Mwanza), Kahama Oil Mill (Kahama), Kahama Cotton Co. Ltd (Kahama), NGS Investment Co. Ltd (Bariadi), Roko Investment Co Ltd, Cotton Agency & Ginners Ltd na Aham Investment Co. Ltd (Dar es Salaam).

Nyingine ni New Sam Trust Co Ltd (Bariadi), Busangwa Organic Farming Association (Shinyanga), BioSustain Tanzania Ltd (Dar es Salaam), MSK Solutions (Mwanza), Mass Trading (Tabora), Sibuka Co Ltd (Maswa), Nsagali Co. Ltd (Bariadi) na Vitrecs Oil Mill ya Mwanza.

Haikuweza kufahamika mara moja kama kampuni zinazoelezwa kuwa na uhusiano na wakubwa ndizo zilizoorodheshwa ama ni zile ambazo zinatajwa kupokea fedha bila majina ya kampuni hizo kuwa hadharani, lakini Raia Mwema, limethibitishiwa kuwapo wakubwa walionufaika na mamilioni kutoka kwenye “stimulus package.”

Katika hali inayothibitisha kuwa mambo si shwari kati ya wakulima wa pamba na wanunuzi ambao wengi wamepata mgawo wa stimulus package, Bodi ya Pamba Tanzania imejikuta katika lawama kali si tu kutoka kwa wananchi bali hata baadhi ya viongozi wa CCM, akiwamo Mwenyekiti wa Mkoa wa Shinyanga, kukiibuka shinikizo kwa Rais Jakaya Kikwete kuifuta bodi hiyo kwa madai kuwa, imeacha shughuli za ununuzi pamba kufanyika holela kupitia kwa mawakala ambao wanawaumiza wakulima.

Kwa upande mwingine, taarifa zaidi zinabainisha kuwa licha ya Bunge kupitisha Sh trilioni 1.7 kwa ajili ya stimulus package, ni sh bilioni 870.8 pekee hadi sasa, ndizo zimekwishatolewa na Benki Kuu (BoT), chombo ambacho kimepewa mamlaka ya kutoa fedha hizo.

Mpango huo wa stimulus package ilitiliwa shaka na Kambi ya Upinzani Bungeni kupitia kwa kiongozi wake, Hamad Rashid Mohamed na kupendekeza utungiwe sheria maalumu ya udhibiti kwa kurejea uzoefu wa baadhi ya nchi za Asia.

Mapendekezo hayo ya kambi hiyo yalilenga kuinusuru nchi na “EPA namba mbili.” Katika hotuba yake bungeni wakati wa kujadili stimulus package mwaka jana, , mjini Dodoma , Hamad Rashid Mohamed, kwa niaba ya wabunge wenzake kutoka vyama vya CUF, CHADEMA na UDP, alihoji masuala mbalimbali kuhusu matumizi ya fedha hizo Sh. trilioni 1.7, zilizotangazwa na Rais Kikwete.

“Tunataka sheria ya Appropriation Act iwe na Schedule maalumu ya Stimulus Package na iseme waziwazi nani atapata nini, kamati ya Fedha na Uchumi ya Bunge iwe inapata taarifa kila miezi 3 ya utekelezaji wa hiyo stimulus package.

“Ni ukweli uliowazi kuwa stimulus package inazinufaisha benki tu, kwa kuzipa mwanya wa kufanya biashara nzuri na Serikali kwa kutumia fedha za Serikali yenyewe, na ndio maana katika nchi nyingine serikali imelazimika kuwa na hisa ili kuhakikisha kuwa fedha iliyotolewa ambayo inatokana na kodi za wananchi inadhibitiwa na kurudi kwa walipa kodi na wapiga kura.”

Hamadi alisema katika bajeti ya mwaka 2007/08 na ile ya 2008/09 serikali ilijizuia kukopa kwenye mabenki, kwa kigezo kikubwa kuwa mabenki yaweze kufanya biashara ya kukopesha sekta binafsi na kuwa zuio hilo liliongeza ufanisi kwa mabenki kukopesha sekta binafsi kwani mikopo kwa sekta binafsi ilipanda hadi kufikia asilimia 40.

Stimulus Package itapunguza mikopo ya benki kwenda kwenye sekta binafsi, na yale mafanikio yaliyokwishafikiwa yatayeyuka, vinginevyo mabenki yawekewe viwango vya kufikia katika kutoa mikopo nje ya stimulus package.

“Kwa mujibu wa taarifa ya Sera ya Fedha ya BoT serikali itazikopesha benki Sh bilioni 270 kwa ajili ya kuzikopesha sekta binafsi. Itatoa Sh bilioni 205 ili kukopa kwenye benki hizo.

Je, benki hizo zikishindwa kutumia fedha zile ambazo serikali imeziweka ili kukopesha sekta binafsi kutumia fedha hizo kufanya biashara na serikali kwa fedha za serikali? Hili litadhibitiwa vipi? Waziri atueleze,”, alihoji Hamad na kuongeza kuwa;

“Mwaka huu wa bajeti ni ya kuongeza matumizi na madhara yake ni mpango huo wa kuhami uchumi kuongeza mfumuko wa bei.

“Serikali imeamua kufidia vyama vya ushirika na kampuni zinazonunua mazao ya wakulima na kuyauza kwa hasara. Katika soko huria kuna kupata faida na kupata hasara. Wafanyabiashara makini wa mazao hupanga bei zao za kununulia mazao kwa kuzingatia bei walioipata katika soko la baadaye.

“Hata hivyo wengine hawapendi kuchukua tahadhari kwa kutegemea kwamba bei itapanda na kwa hiyo watapata faida kubwa. Bei imeshuka kwa hiyo wamepata hasara.” Alihoji akisema; Je, hakuna wafanyabiashara wa mazao waliolipa mikopo waliokopa kwa kujibana. Serikali ina uhakika gani kuwa mikopo hii ilitumiwa vizuri?”

Pia alipendekeza Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kukagua kampuni zitakazopewa fedha kutoka katika mpango wa kuhami uchuni.

Alitaka CAG kwanza kuthibitisha kuwa hasara waliopata haikutokana na matumizi mabaya ya mikopo na kwamba, gharama ya ukaguzi huu ilipwe na benki zilizokopesha. Alionya kuwa, la sivyo serikali inaweza kuliingiza taifa katika EPA namba mbili.

CHANZO:Raia Mwema.

17 Mar 2010


KLABU ya soka ya Real Madrid ya nchini Hispania jana imemkabidhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Kikwete tuzo ya Jezi ya kiungo mshambuliaji wa timu hiyo Critiano Ronaldo. Akizungumza katika hafura hiyo iliyofanyika Ikuru jana Meya wa jiji la Dar es Salaam, Adam Kimbisa ambaye alimukabidhi Rais jezi hiyo kwa niaba ya viongozi wa klabu ya Real Madrid kutokana kutambua mchango wake katika mchezo wa soka.

"Kwa heshima hiyo Klabu hiyo imetoa tuzo Jezi namba tisa inayovaliwa na mchezaji mahiri wa timu hiyo Cristano Ronado," alisema Kimbisa.

Naye Rais Kikweta mara baada ya kupokea tuzo hiyo ameshukuru klabu hiyo ya Real Madrid kwa zawadi hiyo ambayo alisema kuwa ni hesima kubwa kwa Watanzania.

"Nashukuru sana kwa zawadi hii, Madrid ni timu kubwa duniani kutukumbuka sisi Watanzania ni faraja kubwa kwetu.

"Itabidi tutafute sababu mpya ya kuwaalika upya kuja hapa nchini kufutia ili ya awali kushindikana, ni matumani yetu pia tutapata watu ambao watatusaidia kuwaleta," alisema.

Klabu hiyo ya Real Madrid itarajia kufanya ziara yake hapa nchini kwa ajili ya uzinduzi wa Uwanja wa Taifa mwanzoni mwa mwaka juzi lakini kutokana kuchelewa kukamilika kwa ujenzi wa uwanja huo timu hiyo hakuweza kufanya hivyo.

CHANZO: Mwananchi.

16 Mar 2010


RAIS Jakaya Kikwete ameweka hadharani mambo yanayomchefua katika utendaji wake kuwa ni viongozi wa mashirika ya umma na taasisi zilizo katika hali mbaya kifedha, kumghilibu ili awaongezee mitaji wakati historia inaonyesha kuwa kufilisika kwa mashirika hayo kumetokana na utendaji mbovu.

Rais Kikwete alisema anajisikia vizuri na hata moyo wa kuongeza msukumo katika kuitaka serikali itoe fedha kwa taasisi zinazojiendesha kwa faida ili ziendelee kufanya vizuri kuliko taasisi hizo zinazofilisika.

Rais Kikwete alisema hayo jana alipokuwa akibadilishana mawazo na watendaji wakuu wa tume mpya ya mipango mara baada ya kuwaapisha Ikulu jana.

. Utakuta shirika lilikuwa na ndege tisa. Sasa lina ndege mbili. Anakuja mtu anasema, Mheshimiwa tungeweza kufanya vizuri iwapo tungeongezewa ndege saba,? alisema Rais Kikwete wakati akipata kinywaji na watendaji hao watano, akiwemo Waziri Mkuu Mizengo Pinda.

?Ebu fikiria, walikuwa na ndege tisa sasa zimepungua hadi mbili, lakini wao wanaona sasa waongezewe nyingine. Hii inaingia akilini!

?Ingekuwa sasa wanazo 13 halafu wakaja na maelezo kwamba wangefanya vizuri zaidi iwapo wangeongezewa, hapo inaweza kuingia akilini.?

Rais Kikwete aliwaonya watendaji hao wakuu wa chombo hicho ambacho kitategemewa kufanya mapinduzi ya kiuchumi nchini kwamba viongozi wa mashirika na taasisi wa namna hiyo watafika kwao, hivyo wawe makini katika kuamua kulingana na matakwa yao.

Ingawa Rais Kikwete alionekana kueleza hilo kama mfano tu, mazingira yalionyesha kuwa ni moja ya mambo makuu aliyotaka kuwausia katika utendaji wao, kwenye majukumu waliyopewa watekeleze.

Hali hiyo alidhihirisha kutokana na kurudia mara tatu, kusisitiza juu ya ghiliba za viongozi hao wabovu aliosema kuwa licha ya kufanya vibaya kiutendaji, huishawishi serikali izidi kutoa fedha.

Ingawa Rais Kikwete hakutaja shirika lenye tabia hiyo, kauli yake inaweza kuhusishwa na kuyumba kwa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) ambalo hivi sasa limebakiwa na ndege mbili tu baada ya kuyumba kiutendaji.

ATCL, ambayo ilikuwa ikitamba katika miaka ya themanini kutokana na kuwa na ukiritimba katika usafiri wa anga, iliingia mkataba na Shirika la Ndege la Afrika Kusini (SAA) kwa ajili ya kuboresha huduma zake, lakini likajikuta likiporomoka zaidi hadi mkataba ulipovunjwa mwaka 2006.

Mwaka jana, shirika hilo lilizuiwa kufanya safari za anga baada ya kunyang'anywa leseni ya kupaa angani, hatua ambayo ililidhoofisha zaidi shirika hilo. Baada ya kurejeshewa leseni hiyo, bado ATCL imeshindwa kurudi katika hali yake ya kawaida licha ya serikali kutumbukiza fedha nyingi kujaribu kulinasua.

Takribani wiki mbili zilizopita, ndege ya ATCL ilipata hitilafu wakati ikitua mkoani Mwanza na kusababisha shirika hilo kusimamisha tena huduma zake kutokana na kukwama kwa ndege hiyo.

Awali kabla ya mazungumzo hayo ya chai, Rais Kikwete alimwapisha Dk Philipo Mpango kuwa katibu mtendaji wa Tume ya Mipango, akisaidiwa na manaibu katibu wanne; Maduka Kessy, Happiness Mgalula, Florence Mwandri na Cliphod Tandale.

Tume hiyo ya Mipango imeundwa ikiwa ni utekelezaji wa ahadi ya Rais Kikwete baada ya kuivunja iliyokuwa Wizara ya Mipango na Uchumi, alipokuwa anaunda baraza jipya la mawaziri mwaka 2007.

Mara baada ya kuvunja wizara hiyo, idara ya uchumi iliunganishwa na iliyokuwa Wizara ya Fedha na kuifanya iwe na jina jipya la Wizara ya Fedha na Uchumi.

Akizungumza katika hafla hiyo, Dk Mpango alisema tume hiyo itakuwa chombo muhimu cha serikali katika kuweka mipango yenye tija kiuchumi kwa taifa.

Lakini alisema kwamba anakabiliwa na changamoto kubwa ya kupanga mipango mizuri ya nchi ambayo itasababisha mapinduzi ya kiuchumi, hasa ikizingatiwa kwamba kwa kipindi kirefu mikakati imekuwa ikiwekwa lakini bado Tanzania inaendelea kuorodheshwa kwenye nchi maskini.

?Kinachoniumiza ni kuona taifa linaendelea kuwa maskini hata baada ya miaka 40 ya uhuru,? alieleza Dk Mpango.

Miongoni mwa mambo ambayo yamekuwa yakikwamisha nchi kuendelea, alisema, ni taifa kuwa na vipaumbele vingi kuliko rasilimali yake ya kiuchumi.

Katika mazingira hayo, alisema mikakati mingi imekuwa haikamiliki kutokana na kile kidogo kinachopatikana.

Dk Mpango akasema pamoja na kwamba mawazo ya tume yake yatatokana na ushauri wa wataalamu wake, binafsi anaona watatilia mkazo vipaumbele vichache ili suala la maendeleo liwe la hatua kwa hatua.

Alitoa mfano wa Bandari ya Dar es Salaam kwamba inaweza kuwa kichocheo kikubwa cha maendeleo nchini iwapo itaimarishwa pamoja na miundombinu ya reli ili nchi za Uganda, Rwanda, Burundi na Jamhuri ya Demokrasia ya Congo (DRC), zitegemee kupitisha bidhaa zake Tanzania.

CHANZO:Mwananchi.


Bananas may hold the key to powerful new treatments that protect against the Aids virus.In laboratory tests, scientists found that a banana ingredient called BanLec was as potent as two existing anti-HIV drugs.

They believe cheap therapies based on BanLec have the potential to save millions of lives. The ingredient is a lectin, a naturally occurring chemical in plants which fights infection.

Researchers in the US found that the lectin found in bananas can inhibit HIV infection by blocking the virus's entry into the body. BanLec acts on the protein "envelope" that encloses HIV's genetic material.

Lead author Michael Swanson, from the University of Michigan, said: "The problem with some HIV drugs is that the virus can mutate and become resistant, but that's much harder to do in the presence of lectins.

"Lectins can bind to the sugars found on different spots of the HIV-1 envelope, and presumably it will take multiple mutations for the virus to get around them."

The research is reported in the Journal of Biological Chemistry.
SOURCE: Yahoo! News

14 Mar 2010


Wana-Msimbazi mmeweka rekodi nzuri na inayostahili pongezi.Tunataraji mtatafsiri rekodi hiyo kwa kufanya vema katika michuano ya kimataifa.Penye nia pana njia.
POINTI za Simba sasa zimetosha na imeibuka bingwa wa soka Ligi Kuu Tanzania Bara kwa mwaka 2009/2010, lakini ikiwa ni mara ya 17 kwa klabu hiyo kutwaa ubingwa huo.

Hatua hiyo inatokana na ushindi wa mabao 2-0 iliyoupata jana dhidi ya Azam kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam katika mchezo wa ligi hiyo uliokuwa mkali na wa kusisimua ambao ni wa raundi ya 20.

Kutokana na matokeo hayo, Simba imefikisha pointi 56 ambazo haziwezi kufikiwa na timu yoyote katika ligi hiyo, ambapo Yanga iliyofikisha pointi 45 ikishika nafasi ya pili ikishinda michezo yake mitatu iliyosalia itafikisha pointi 54.

Chereko, nderemo na vifijo vya mashabiki wa Simba vilitawala Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam mara baada ya filimbi ya mwisho ya mwamuzi Ibrahim Kidiwa ambayo iliashiria mwisho wa mechi kati yao na Azam.

Baada ya mpira kumalizika wachezaji wa Simba walizunguka uwanja wakiwapungia mikono mashabiki wao, ambao wengi wao walikuwa wamevalia fulana zenye maneno Simba Bingwa 2009/2011, huku wakiwa wanaonekana wenye furaha isiyo kifani baada ya kutwaa ubingwa huo, huku wakiwa na rekodi safi ya kutopeza mechi yoyote kwenye ligi hiyo na ikiwa imetoka sare mara mbili tu kati ya mechi 20 ilizocheza.

Mabao mawili yaliyofungwa moja katika kila kipindi na mshambuliaji Mkenya wa timu hiyo, Mike Barasa ndio yaliyoiwezesha Simba kuwavua rasmi ubingwa watani zao wa jadi, Yanga, huku ikiwa imesaliwa na mechi mbili mkononi ikiwemo ile dhidi ya watani zao hao itakayochezwa Aprili 11 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Bao la kwanza la Simba lilifungwa dakika ya saba kwa kichwa na Barasa ambaye aliunganisha krosi ya Mkenya mwenzie Hillary Echesa na kuwafanya mashabiki wa Simba kushangilia baada ya kuenea kwa maneno ya uzushi kuwa mnajimu mmoja alitabiri Simba ingepoteza mchezo na isingeweza kutwaa ubingwa.

Baada ya bao hilo Simba ambao walionekana kupania, walilisakama lango la Azam na dakika mbili baada ya bao hilo, Ulimboka Mwakingwe alipiga krosi ndani ya eneo la hatari lakini Musa Hassan ‘Mgosi’ akiwa katika nafasi nzuri ya kufunga alishindwa kumiliki mpira huo, hivyo kupoteza nafasi hiyo. Huku Simba wakionekana kutandaza kandanda safi na kufanya washangiliwe na mashabiki wao waliofurika uwanjani hapo kushuhudia timu yao ikitwaa ubingwa baada ya kuukosa kwa takribani miaka mitatu, walianza kupooza mashambulizi na hivyo kuanza kutoa nafasi kwa Azam ambao walionekana kutawala sehemu ya kiungo kipindi cha kwanza.

Kutokana na udhaifu huo Azam walipeleka mashambulizi kadhaa, langoni mwa Simba na katika dakika 35 washambuliaji John Bocco, Danny Wagaluka walishindwa kupachika bao kufuatia krosi ya Malika Ndeule, baada ya Bocco kuikosa na kipa Juma Kaseja kuuwahi kabla ya kumfikia Wagaluka.

Bocco alikosa bao pale shuti lake alilopiga akiwa kwenye ukingo wa eneo la hatari na kudakwa na Kaseja, dakika mbili baadaye mshambuliaji huyo alijaribu tena shuti kali ambalo lilimtoka Kaseja kabla hajaliwahi na kulidaka tena.

Kipindi cha pili kilianza kwa Azam kufanya mabadiliko ya kuwaingiza Ally Manzi na Mau Ally badala ya Said Sued na Wagaluka.

Mabadiliko ambayo yalionekana kuongeza uhai katika safu ya ushambuliaji ya Azam na kuleta sekeseke kadhaa kwenye safu ya ulinzi ya Simba ambayo ilikuwa ikiongozwa na Kelvin Yondani na Juma Nyosso, kwani Manzi alionekana kumsumbua beki wa kushoto, Juma Jabu.

Simba ilifanya mabadiliko yake ya kwanza dakika ya 55 kwa kumtoa Ulimboka Mwakingwe na nafasi yake kuchukuliwa na Uhuru Selemani na dakika ya 57 nusura Mohamed Banka apachike bao la pili baada ya kupiga shuti kali la adhabu ambalo liligonga mwamba wa juu na kurejea uwanjani huku, kipa Vladimir Niyonkuru akiwa ameshapoteza hesabu, lakini walinzi wake waliokoa.

Dakika ya 60 Azam walijibu shambulio hilo pale Manzi alipomtoka Jabu na kupiga krosi safi ambayo Bocco alichelewa kuinganisha wavuni, dakika mbili baada ya Azam kukosa bao hilo, Uhuru Seleman alitoa pasi ya kubetua kwa Barasa aliyekuwa kwenye eneo la hatari ambaye bila ajizi aliukwamisha mpira wavuni na kuipatia Simba bao la pili.

Yanga iliyokuwa ikitetea ubingwa huo, yenyewe imetwaa kombe hilo mara 21.

CHANZO: Habari Leo.

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.