24 Jul 2011


Nimepokea kwa masikitiko kifo cha Mhadhiri wangu wa zamani Profesa Samuel Mushi.Nilikuwa mwanafunzi wa Profesa Mushi tangu nilipojiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Septemba 1996 hadi nilipomaliza mwaka wa kwanza July 1997.Profesa Mushi alinifundisha Utangulizi kwa Stadi ya Sayansi ya Siasa (PS100: Introduction to the Study of Political Science).Marehemu ni miongoni mwa wanataaluma wa mwanzo walionipa uelewa na mwamko wa stadi za siasa,japokuwa mwaka wa pili na wa tatu nilichukua mchepuo wa Sosholojia.

Bwana Ametoa Bwana Ametwaa.
Jina la Bwana Lihimidiwe Milele,
Amen 

23 Jul 2011


FAMILIA YA TULLY NGONYA(MAMA MARIA) NA IKUPA NGONYA WANASIKITIKA KUWAARIFU MSIBA WA BABA YAO MPENZI MZEE J.D. NGONYA ALIEFARIKI LEO ASUBUHI 23.7.11.
KAMA ILIVYOKUWA DESTURI YETU TUNAWAOMBA WOTE TUKUTANE TUWAFARIJI WAFIWA WAKATI WA KIPINDI HIKI KIGUMU.
MSIBA UPO 38 TRELLECK ROAD, READING RG1 6EN. 
BWANA AMETOA, BWANA AMETWAA JINA LAKE LITUKUZWE MILELE. AMEN.
TAFADHALI MJULISHE NA MWENZAKO

Imetumwa na Urban Pulse Creative


Hili sio ombwe tena bali mkusanyiko wa wababaishaji walioteuliwa na mtu asiyejua kwanini aliwateua,na ndio maana wanaendesha mambo kama kwenye mchezo maarufu wa watoto ujulikanao kama kombolela.Watu wazima ovyoo!Lakini ni wazi wanapata jeuri ya kufanya ubabaishaji huo kwa vile wanafahamu fika kuwa aliyewateua hana jeuri ya japo kuwawajibisha,let alone kuwakemea.

Anyway,hebu soma madudu yao hapa chini:

DPP amkana Hoseah  
Friday, 22 July 2011 20:27

ASEMA HAJAPATA JALADA LA CHENGE, AAMBIWA AKAANGALIE MASJAJA
Nora Damian
SIKU moja baada ya Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk Edward Hoseah, kusema kwamba ofisi yake imekamilisha uchunguzi wa madai ya kumiliki Dola za Marekani 1.2 milioni katika Kisiwa cha Jersey, Uingereza yanayomkabili Mbunge wa Bariadi Magharibi (CCM), Andrew Chenge na kwamba imekabidhi faili lake kwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP) kwa ajili ya kumfungulia mashtaka, kiongozi wake, Eliezer Feleshi amejitokeza na kusema kwamba hawahi kuliona jalada hilo.

"Niko safarini subiri hadi wiki ijayo… kwanza ashtakiwe kwa kosa gani? Acheni siasa nyie,” alisema DPP alipotakiwa kuthibitisha kama jalada hilo limefika mezani kwake na lini Mwanasheria huyo Mkuu wa zamani wa Serikali atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili... “Aseme ni tarehe gani alileta jalada hilo kwangu?”

Kutokana na majibu hayo ya DPP, Mwananchi lilimtafuta Dk Hoseah kupata ukweli juu ya kauli yake hiyo aliyoitoa juzi huko Arusha na kusisitiza kuwa jalada hilo limepelekwa katika Ofisi ya DPP na kumtaka mkuu huyo wa Mashitaka nchini asiharakishe kusema hajaliona, kwani siyo lazima kila kitu akabidhiwe mikononi... “Kwani kila kitu kinachopelekwa kwake lazima akione? Ameangalia registry (masjala)?. Suala hili nimeshaliongea nanyi vya kutosha hivyo muulizeni zaidi DPP.”

Juzi, Dk Hoseah alisema taasisi yake imekamilisha uchunguzi dhidi ya tuhuma zinazomkabili Chenge na kwamba jalada lake limepelekwa kwa DPP kwa hatua zaidi. Alisema Chenge atashtakiwa chini ya Kifungu cha 27 cha Sheria ya Takukuru ya mwaka 2007. Kwa mujibu wa kifungu hicho, mtu akiwa na mali ambazo hazilingani na kipato chake alichokipata akiwa madarakani au baada ya kuondoka ni kosa kisheria.

Chenge anadaiwa kukutwa na kiasi hicho cha fedha mwaka 2008 baada ya uchunguzi wa kashfa ya ununuzi wa rada uliofanywa na Taasisi ya Makosa Makubwa ya Jinai ya Uingereza (SFO). Tuhuma hizo ndizo zilizomfanya alazimike kujiuzulu wadhifa wa Waziri wa Miundombinu mwaka huo.

Malumbano kati ya Dk Hoseah na Feleshi siyo ya kwanza. Mwaka jana waliwahi kulumbana baada ya mkuu huyo wa Takukuru kusema kuna majalada takriban 50 ya kesi za rushwa ambayo yamekaliwa na DPP.

Pia Dk Hoseah aliwahi kumshutumu DPP mbele ya wabunge wakati wa semina elekezi mapema mwaka huu akidai kwamba amekuwa kikwazo cha kesi kubwa za ufisadi kupelekwa mahakamani kwa kukwamisha majalada.

CHANZO: Mwananchi 



Kalapina on politics, Freemasons, war, peace, Rostam, Drugs etc.
More from Kalapina and kikosi http://www.reverbnation.com/tunepak/3387426

Click the banner titled CHEUSI DAWA TV (FID-Q) (see the sidebar) for previous episodes of Fridstyle Friday and much more!


Tunasikitika kuwatangazia kifo cha
Machira  NYITAMBE

Kilichotokea mchana leo huko  MUSOMA-TANZANIA

Mazishi yatafanyika huko Kirongwe, Shirati, katika mkoa wa Mara.


Marehemu ni baba mzazi wa:

Mrs Veronica Dibogo Nyitambe
Mrs Beatrice Nyitambe(Baba Mdogo)
Mr Soni Nyitambe (Baba Mdogo) ,


ambao wote wapo hapa Uingereza.

Msiba upo
14 Rothwell Walk
Caversham
Reading

RG4 5DB

Kwa mawasiliano zaidi tumia simu zifuatazo:
Bernard Chisumo
Mob: (0) 787 612 6862
Home: (0) 118 954 5890 
---------------------------------------------------------------- 

POLENI SANA WAFIWA.SIE TULIMPENDA MAREHEMU LAKINI BWANA ALIMPENDA ZAIDI

22 Jul 2011

Samuel Sitta mwenyewe anayepigwa mkwara na Guninita yupo hoi kwa usingizi.Labda hapo anaota yeye bado Spika

Guninita ‘amvaa’ Sitta
Posted By admin On July 22, 2011 @ 7:59 am In Habari kuu,Mtanzania |

• Adai ni mzigo, anawadanganya na kuwapotosha wananchi
• Asisitiza ni sehemu ya tatizo la mgawo wa umeme
• Asema si mgeni serikalini, ni mchochezi, mnafiki na mfitini
• Aonya anaigawa, anaitumbukiza CCM kwenye shimo
• Asema mambo yakiendelea hicho mwaka 2015 CCM itaambulia patupu

Na Habakuki Urio

MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dar es Salaam, John Guninita amemlaumu Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samwel Sitta akidai ni mnafiki na mchochezi anayetumika kuigawa CCM na kukitumbukiza chama hicho kwenye shimo.

“Sitta ni sehemu ya serikali na si mgeni serikalini. Alikuwapo tangu kipindi cha Mwalimu Nyerere, na pia alikuwa Spika wa Bunge. Kwa nafasi hizi yeye ni sehemu ya tatizo na siyo kuwadanganya wananchi na kuwapotosha kwa kuirushia serikali lawama.

‘Anaudanganya umma. Anataka kujenga umaarufu ambao siyo wa kwake. Kama ni kuharibu waliharibu wote na siyo kusema tatizo ni la serikali.
‘Sitta amekuwa mchawi wa CCM… chama kinajimaliza chenyewe tena kwa kutumia viongozi wa nafasi za juu.,” alisema Guninita.

Guninita alikuwa akizungumza katika mkutano wa hadhara Mbezi na Mbezi kwa Msigani katika jana, katika ziara ya kutekeleza agizo la Mwenyekiti wa CCM, Rais Kikwete la kuleta mageuzi ndani ya chama hicho na ‘kujivua gamba’.

Alisema hali ya siasa ndani ya chama hicho si shwari kutokana na mgawanyiko mkubwa wa baadhi ya viongozi ambao wanazungumza wanavyojisikia bila kujali maslahi na ukweli ndani ya Chama hicho.

“Kilichotufikisha hapa tulipo leo ni unafiki na fitina za viongozi kama Sitta ambao hawaeleweki wanafanya nini ndani ya chama chetu. Ndiyo maana viongozi wanajiuzulu ovyo, kitu ambacho siyo sahihi, chama kinapoteza makada muhimu na kuwaacha watu mizigo na wafitini.

“Namshangaa Waziri Sitta, ana uwezo wa kwenda kwa Rais muda anaojisikia na pia alikuwa na nafasi ya kuyasema mambo yale katika vikao vya chana “party caucus”, na pia kwenye vikao vya Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) lakini anaropoka mambo kama hayo mbele ya umma wa watanzania na kuwapa umaarufu wapinzani.

“Amekosa busara kwa kuwa amekiuka maagizo ya Rais. Tunajua hakutumwa na Rais, bali alikurupuka tu, na bila kujijua anaiponda Ilani ya Uchaguzi ya CCM ambayo ndiyo muongozo wa kutekeleza majukumu yetu.
‘Mawaziri na wabunge wanasema tofauti na Rais anavyosema kuhusu matatizo ya umeme kwa sasa,” alisema Guninita

Alisema kauli mbovu za baadhi ya viongozi ambazo hazina ukweli zinabomoa chama, na kama CCM haitakauwa makini na kuwaonya wapotoshaji hao katika uchaguzi mkuu wa 2015 chama hicho kitaambulia patupu.

“Upinzani wanajipanga vizuri katika kuhakikisha mwaka 2015 wanachukua nchi, na kwa hali hii tulio nayo … kwa kauli za akina Sitta watafanikiwa kwa kuwa chama kitakuwa kimeyumba na kukosa imani kwa wapigakura wake.

“Haya siyo maneno ya Waziri, huyu jamaa ana mambo yake anayotekeleza… haiwezekani Sitta leo kuyasema haya, labda ana hasira za kukosa Uspika wakati yalikuwa makubaliano ya CCM kumuondoa kwa mafanikio ya chama na kutimiza sera ya 50 kwa 50.

‘Nilimsikia akisema kuwa atatembea mikoa yote kulisema hilo, lakini nawahakikishia kuwa hatafika Dar es Salaam labda aje na barua ya Mwenyekiti au Katibu Mkuu wa CCM kuwa wamemruhusu kupotosha jamii. Nasema kuwa hatutakubaliana na uongo wake,” alisisitiza Guninita.

Hivi karibuni, katika mkutano wa hadharani mjini Mbeya, Sitta pamoja na mambo mengine, alikaririwa akishauri serikali iwaombe radhi wananchi kutokana na tatizo la mgawo wa umeme unaoendelea nchini hivi sasa.

Guninita alisema mkutano wa jana ni matunda ya makubaliano ya kujivua gamba kama alivyoagiza Mwenyekiti Kikwete na kuwataka viongozi wote wa CCM kutembelea matawi na mashina katika maeneo yao kuyajua matatizo ya wapiga kura wao na kuimarisha mizizi ya chama ambayo ipo katika mashina na matawi.


 
Who Needs Humans?
As if American workers don’t have it rough enough, with unemployment skyrocketing and jobs moving overseas, now there’s another threat: robots.
by Daniel Lyons, July 18, 2011
Amid all the job losses of the Great Recession, there is one category of worker that the economic disruption has been good for: nonhumans.
From self-service checkout lines at the supermarket to industrial robots armed with saws and taught to carve up animal carcasses in slaughter-houses, these ever-more-intelligent machines are now not just assisting workers but actually kicking them out of their jobs.
Automation isn’t just affecting factory workers, either. Some law firms now use artificial intelligence software to scan and read mountains of legal documents, work that previously was performed by highly paid human lawyers.
“Robots continue to have an impact on blue-collar jobs, and white-collar jobs are under attack by microprocessors,” says Edward Leamer, an economics professor at UCLA’s Anderson School of Management and director of the UCLA Anderson Forecast, a survey of the U.S. and California economies. Leamer says the recession permanently wiped out 2.5 million jobs. U.S. gross domestic product has climbed back to pre-recession levels, meaning we’re producing as much as before, only with 6 percent fewer workers. To be sure, robotics are not the only job killers out there, with outsourcing stealing far more gigs than automation.
Jeff Burnstein, president of the Robotics Industry Association, a trade group in Ann Arbor, Mich., argues that robots actually save U.S. jobs. His logic: companies that embrace automation might use fewer workers, but that’s still better than firing everyone and moving the work overseas.
It’s not that robots are cheaper than humans, though often they are. It’s that they are better. “In some cases the quality requirements are so stringent that even if you wanted to have a human do the job, you couldn’t,” Burnstein says. He cites General Motors, which uses robots to lay a bead of sealant on windshields, because humans can’t do the job as precisely.
Same goes for surgeons, who are using robotic systems to perform an ever-growing list of operations—not because the machines save money but because, thanks to the greater precision of robots, the patients recover in less time and have fewer complications, says Dr. Myriam Curet, chief medical adviser at Intuitive Surgical in Sunnyvale, Calif. The surgery bots don’t replace surgeons—you still need a surgeon to drive the robot. And they’re not cheap. Prices go as high as $2.2 million. Nevertheless, Intuitive sold 400 of them just last year. If you’ve had a prostatectomy recently, chances are a robot was involved.

Surgeons may survive the robot invasion, but others at the hospital might not be so lucky, as iRobot, maker of the Roomba, a robot vacuum cleaner, has been showing off Ava, a three-foot-tall droid on wheels that carries a tablet computer. iRobot reckons Ava could be used as a courier in a hospital. And once you’re home, recovering, Ava could let you talk to your doctor, so there’s no need to send someone to your house. That “mobile telepresence” could be useful at the office. If you’re away on a trip, you can still attend a meeting. Just connect via videoconferencing software, so your face appears on Ava’s screen.

Is any job safe? I was hoping to say “journalist,” but researchers are already developing algorithms that can gather facts and write a news story. Which means that a few years from now, a robot could be writing this column. And who will read it? Well, there might be a lot of us hanging around with lots of free time on our hands.

SOURCE: Newsweek 


















Picha zote hizo kwa hisani ya gazeti la Daily Mail zilidakwa na kamera dakika ambapo waogeleaji (pichani) walipokuwa wanajirusha kutoka jukwaani.Ashakum si matusi,hutolaumiwa ukidhani baadhi yao wanajikakamua msalani kushusha "kubwa".

Appeal for Support How to Register


Moja ya matatizo mengi yanayomkabili mtu tuliyemchagua kuwa Rais wetu,Jakaya Kikwete,ni kutokuwa serious.Yeye ni mwepesi wa kuchekacheka hata kwenye mambo yanayohitaji kuwa serious.Anyway,kwanini nimesema hatuna rais?Sio siri,nimepatwa na kichwa kuuma baada ya kusoma mahojiano yafuatayo kati ya Kikwete na mwandishi wa BBC.Angalia majibu yake,angalia vicheko vyake...na kwa hakika unaweza kuafikiana nami kuwa huyu mtu sio tu mbabaishaji bali yawezekana hajui kwanini ni Rais wetu.Anyway,soma mwenyewe

BBC: Suala la Umeme Mheshimiwa Rais Kikwete ungependa kulizungumzia nini?

Rais Kikwete: Tatizo la umeme kimsingi ni suala la ukame tu. Kwa sababu mabwawa yetu ya kuzalisha umeme yanayotoa umeme karibu MW600 sasa hivi yanatoa umeme kidogo sana. Maji pungufu ndio maana kuna tatizo hilo.

BBC:Mheshimiwa, hili suala si la leo wala si la jana limekuwepo kwa muda mrefu, kwanini serikali haina njia mbadala ya kuweza kutatua suala hili? Tanzania ina raslimali nyingi mheshimiwa Kikwete!

Rais Kikwete: Kwanza serikali haina uwezo wa kufanya mvua inyeshe, unajua unajua hivyo, Kwa sababu (kicheko) ingekuwa na uwezo wa kufanya mvua inyeshe mabwawa yale yangejaa. Ni kweli kuwa Tanzania inazo raslimali za kutosha na katika kipindi hiki - toka wakati ule - sisi tulipoingia tumekuta suala la Ukame na mwaka 2007 tukapata matatizo ya kwanza.

Baada ya pale tukafanya uamuzi kwamba sasa tuanze kuwekeza katika vyanzo vingine; tuongeze uzalishaji wa umeme kutoka vyanzo vingine. Tuongeze uzalishaji wa umeme kutoka vya vya kutumia gesi asilia twende kwenye makaa ya mawe. Kutoka vyanzo vya gesi asilia tayari tuna mtambo pale Ubungo, na toka mwaka 2009 mpaka sasa tumeshaongeza MW145, itakapofika Disemba tutakuwa tumeongeza MW160 nyingine. Tutakuwa tumeongeza MW300 siyo kidogo.

BBC: Mhe. Kikwete Mmoja katika wabunge Bw. John Mnyika ambaye ni Mbunge wa upinzani ambaye ni Waziri Kivuli wa Nishati amekuwa akilalamika na kwamba amewahi kusema kwamba hili tatizo ni tatizo linalowahusu Watanzania wote na amesema mje pamoja na kuona vipi mtakavyotatua tatizo hili. Na sasa hivi Bungeni wamesimamisha mswada, wa kutoa bajeti ya nishati ya Tanzania. Wewe unachukulia vipi matamshi kama haya kutoka kwa Wabunge?

Rais Kikwete: Mimi nasema hivi yeye si Mbunge atoe maarifa yake tu; anayo maarifa gani na anapendekeza kitu gani. Kwa sababu toka Uhuru mabwawa tuliyotengeneza ni Kidatu MW200, Mtera MW80, Kihansi MW 165 mimi nilipokuwa Waziri wa Nishati, pale Pangani tumeongeza.

Sasa ufikirie kwamba toka Uhuru tumeweza kuzalisha umeme wa MW600, lakini toka 2009 mpaka Disemba mwaka huu tutakuwa tumeongeza MW300! Ni jitihada kubwa. Mimi nasema kwamba usipozitambua hizo ni kwamba wewe mwenyewe siyo mkweli.

Sasa ni hivi, unajua hii mitambo ya umeme si mitambo unaenda kununua kama unavyonunua jaketi lako hili. Ni kwamba ukitaka mitambo ya umeme, lazima uweke order wakutengenezee. Huu mtambo unaofika mwaka huu Disemba order tuliweka mwezi wa Juni mwaka jana. Inachukua muda huo kutengeneza. Sasa ingekuwa mnaenda kutafuta mitumba, mitumba ya mitambo tu ya kununua iko mingi kweli. Tukasema hatuwezi kufanya hivyo.

Mimi nasema hivi, kitu kikubwa ni kuwa na subira. Tumefanya jitihada kubwa. Ni lazima watu watambue kuwa tumefanya jitihada kubwa katika miaka hii toka 2009 mpaka sasa hivi 2011 Disemba tutakuwa tumeongeza MW300 kulinganisha na MW600 ambazo tumeziongeza katika miaka yote hii. Nasema ni lazima watu watambue hivi. Sasa kama kuna mtu ana maarifa ya haraka zaidi nasema mtu atoe maarifa hayo na sisi kama yapo tutayafanyia kazi.

BBC: Kuna njia kama umeme wa jua, umeme wa kutokea ardhini wa mvuke, kwanini serikali haitafuti njia mbadala kuzalisha umeme kwa njia hizo?

Rais Kikwete: Nasema hivi, hata umeme wa jua lazima ujenge, umeme wa mvuke lazima ujenge, si kitu cha mwezi mmoja. Nasema huo ndio ukweli wenyewe na wakati mwingine na nyinyi mjifunze hayo mambo ya kitaalamu kulikoni kuuliza tu hivi hivi. Unajua ungekuwa na wewe unauliza kwa hoja - “unajua kwamba hiki kitu hiki ingekuwa umeme wa jua miezi miwili tu upo” - tungeweza kufanya hivyo.

Sisi sasa hivi kwa mfano tunajiandaa kuzalisha umeme wa kutumia Upepo, pale Singida. Tuna mwaka wa tatu sasa tuna mipango na Wakorea wa Kusini, umeme haujakuwepo. Kwa hiyo nasema hayo ni maelezo rahisi. Wanasema “mbona jua lipo?” katengeneze umeme wa jua kama jua lipo! (kicheko).

BBC: Watanzania wamekuwa wakisema (mwisho kabisa) kwamba Tanesco ingebinafsishwa ili waweze kupata makampuni kufanya kazi hiyo ya umeme?

Rais Kikwete: Aah! Kwani ukitaifisha kesho ndio utapata mitambo kesho? Nasema hivi ni vizuri kuelewa tu - kwanza tatizo la msingi - ni maji kukauka kwenye mabwawa. Maji yasingekauka kwenye mabwawa tatizo hili halipo. Maji yamekauka kwenye mabwawa kwa sababu ya ukame. Hakuna mtu mwenye uwezo wa kuzuia ukame usiwepo. Sasa hiki ndicho kiini cha tatizo. Sasa nasema sisi jitihada ambayo tumeifanya ni kupunguza sasa kutegemea umeme unaotakana na nguvu ya maji.

Toka mwaka 2009 tumewekeza adi Disemba 2011 tutakuwa tumeongeza MW 310, yenyewe hiyo ni hitihada kubwa, ni vizuri ukaitambua jitihada hiyo. Kulikoni kusema kitu tu nasema hata kama huna majawabu rahisi utuambie tu.

MSIKILIZE HAPA

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.