22 May 2011


For you guys who Swahili is a foreign language,the happy dude in the middle is a Bishop.Seen in the picture on the left is him preaching the Gospel of Jesus.Joined by the two ladies in a pool,the Bishop couldn't resist flashing a RAPTURous smile...

 The same Bishop,Jamal Ally Hussein,who converted to Christianity from Islam,is seen posing romantically with a young girl...RAPTURE!!!!

Photo credit: Global Publishers

20 May 2011


CCM Arusha kwachafuka

Thursday, 19 May 2011 22:42

CHATANDA ATAKIWA KUNG'OKA, GARI LAKE NUSURA LICHOMWE MOTO NA UVCCM
Moses Mashalla, Arusha
HALI si shwari chama tawala mkoani Arusha mara baada ya gari la Katibu wa CCM hapa, Mary Chatanda kunusurika kuchomwa moto na baadhi ya wanachama wa Umoja wa Vijana wa chama hicho(UVCCM).Wanachama wa umoja huo kutoka wilaya mbalimbali za Mkoa wa Arusha waliandamana katika Jengo la Makao Makuu ya CCM Mkoa wa Arusha, wakishinikiza Chatanda pamoja na Mjumbe wa Baraza la Vijana mkoani Arusha, Mrisho Gambo "wajivue gamba".

Hali hiyo ilijitokeza jana katika jengo la makao makuu ya chama hicho wakati Kikao cha Kamati ya Siasa Mkoa kikiendelea ambapo, hali iliyosababisha dereva wa gari la katibu huyo wa CCM kulitoa nje ya jengo hilo na kisha kulikimbiza mahali kusikojulikana.

Vijana hao walikuwa wameshika mabango yenye ujumbe mbalimbali huku wakipaza sauti zilizokuwa zikimtaka Chatanda kuondoka katika nafasi yake ya uongozi kwa madai kwamba amekuwa akikivuruga CCM mkoani Arusha.

Wakizungumza na waandishi wa habari, wanachama hao kutoka wilaya za Monduli, Longido, Arusha, Arumeru, Karatu na Ngorongoro walisema pamoja na wao kutoa malalamiko mbalimbali juu ya Chatanda na Gambo, lakini uongozi wa CCM taifa umekuwa ukiwakumbatia viongozi hao na kudai sasa wamechoka.

Walisema malaliko yao kuwa Chatanda amekuwa akikivuruga chama chao ikiwa ni pamoja na kusababisha kukosa ushindi wa Jimbo la Arusha Mjini lililoenda kwa Chadema huku wakisema kwamba ikiwa atakataa kung'oka watajua cha kufanya.

“Hatumtaki Chatanda na hatumtaki Mrisho Gambo hawa watu kwanza ni wasaliti, lakini pia wamechangia sisi kushindwa kuchukua jimbo hili kwani walikuwa wanaiunga mkono Chadema tunataka waondoke mara moja hadi kieleweke,” ilisikika sauti ya mmoja wa vijana hao.

Miongoni mwa jumbe ambazo zilikuwa zimeandikwa kwenye mambango hayo ni "Chatanda umehujumu uchaguzi kwa siasa zako za makundi zilizojaa chuki, ubinafsi na ubabe usio na manufaa kwa Chama Cha Mapinduzi", "Chatanda kwa siasa zako za ubabe umetuchonganisha na viongozi wa dini”, na nyingine kadha wa kadha.

Hali hiyo ilisababisha Mwenyekiti wa UVCCM mkoani Arusha, James Ole Millya aliyekuwa kwenye kikao cha kamati ya siasa kutoka nje na kwenda ukumbini kuwatuliza wanachama hao, lakini juhudi zake ziligonga mwamba.

Akizungumza na wanachama hao, Milya aliwataka wapunguze jazba na kusema kuwa yeye ni mjumbe ametumwa kusikiliza madai yao hivyo wampatie na kisha taufikisha ujumbe huo.

“Jamani ninawaomba mtulie sidhani kama mtafanya fujo ninaomba mnipatie ujumbe mnitume niufikishe jamani nami nitaufikisha tulieni jamani,” alisema Milya

Hata hivyo, ushawishi wa Milya haukuzaa matunda na kuamua kurudi kikaoni kwani wanachama hao waliendelea kupaza sauti zao kwa wakidai kuwa wanamtaka katibu huyo aondolewe mkoani Arusha kwa kuwa amekuwa akiingilia uamuzi wa umoja wao na kuendelea kumkubatia Gambo.

“Mheshimiwa tunakipenda sana chama chetu na tunakuheshimu sana, tunaomba Chatanda aondoke la sivyo tutachoma gari lake, tukikutana nalo tutamondoa kwa nguvu,” alisema kwa jazba mmoja wa vijana hao.

Vijana wavamia kikao cha kamati ya siasa
Wakati hayo yakiendelea wanachama hao walikosa uvumilivu na kisha kuvamia ofisi ambapo Kikao cha Kamati ya Siasa mkoa kilipokuwa kikifanyika huku wakitishia kubomoa mlango kitendo kilichosababisha viongozi mbalimbali wa CCM mkoani hapa kuhaha kutuliza tafrani hiyo.

Maafisa usalama wakiwemo askari kanzu walikuwa wametanda katika maeneo ya jengo hilo huku wengine wakionekana wakizungumza na viongozi wa UVCCM kujua chanzo cha vurugu hizo.

Chatanda ajifungia ukumbini
Hadi tunakwenda mitamboni, Chatanda alikuwa bado amejifungia ndani ya ukumbi wa mkutano na hakuna taarifa yoyote ya CCM Mkoa aliyotolewa kuhusiana na tukio hilo.

Tuhuma dhidi ya Chatanda kutoka ndani ya chama chake zimekuja siku chache tangu ashutumiwe kuwa mmoja wa waliosababisha mgogoro mkubwa wa kisiasa mkoani Arusha baina ya vyama vya CCM na Chadema.

Mgogoro huo unafuatia Chadema kupinga katibu huyo wa CCM wa Mkoa wa Arusha kushiriki katika vikao vya Baraza la Madiwani na kupiga kura ya kumchagua meya wa Jiji la Arusha, hali Iliyosababisha maandamano makubwa ambayo yalisababisha vifo vya watu watatu.

Wakati CCM wakidai kuwa Chatanda ni mjumbe halali wa vikao vya baraza hilo, Chadema wamekuwa wakipinga kwa maeleo kwamba mwanamama huyo ni mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Tanga hivyo hana sifa ya kushiriki vikao vya Arusha.
CHANZO: Mwananchi



Mauaji Tarime yalikoroga taifa
• Mbunge Lema apambana na kamishna wa polisi

na Mwandishi wetu

MAUAJI ya watu watano waliouawa na polisi, Tarime mkoani Mara kwa madai walikuwa ni wahalifu waliotaka kuvamia mgodi wa North Mara Barrick sasa ni dhahiri yameikoroga serikali na taifa kwa ujumla.

Jana Jeshi la Polisi pamoja na kutuma timu ya maofisa waandamizi kutoka makao Makuu ya Jeshi hilo, lilishindwa kuwashawishi ndugu wa marehemu hao ambao walikataa kusitisha mgomo kususia miili hiyo hadi serikali itoe tamko la kukomeshwa mauaji hayo na wahusika kuchukuliwa hatua.

Timu ya maofisa waandamizi kutoka makao makuu ya jeshi hilo ikiongozwa na Mkuu wa Mafunzo na Operesheni wa Jeshi la Polisi, Kamishna Paul Chagonja walilazimika kuondoka pasipo kufikia muafaka katika eneo la chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali ya wilaya baada ya mamia ya waombolezaji waliopiga kambi tangu Jumatatu kukataa mapendekezo yao.

Awali Kamishna Chagonja aliwahutubia wananchi hao akiwataka waridhie miili hiyo ifanyiwe uchunguzi na kuchukuliwa kwa ajili ya mazishi yatakayogharamiwa na serikali lakini juhudi zake ziligonga mwamba baada ya ndugu wa marehemu kukataa mapendekezo hayo, kwanza wakitaka taarifa ya serikali kulaani mauaji hayo.

“Sisi tumekuja hapa kushirikiana nanyi kwa lengo la kutafuta ufumbuzi sasa tunawaomba mridhie kufanyika uchunguzi halafu taratibu nyingine za mazishi zifuatwe ambapo pia tumejitolea kama jeshi la polisi kushiriki kwa kutoa msaada wa hali na mali ili tufanikishe zoezi hili, tunaomba mkubali kufanyika uchunguzi na tume huru itaundwa kuchunguza tukio hilo,” alisema Changonja.

Kauli yake hiyo ilipingwa vikali na waombolezaji hao ambao walishikilia kuwa kwa vyovyote vile ilivyotokea hakukuwa na sababu ya kuhalalisha vifo hivyo kwa sababu polisi ndio wahusika na walitumia nguvu nyingi kupita kiasi kukabiliana na raia wasiokuwa na silaha za moto.

Wakiongozwa na mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema (CHADEMA) aliyepiga kambi katika eneo hilo, wana ndugu hao walidai ingawa hawakupinga kuendelea na zoezi la mazishi lakini wasiwasi wao ulitokana na uharaka wa jeshi hilo kutaka kupoteza ushahidi kwa kulazimisha kufanyika mazishi.

Lema apambana na kamishna wa polisi

Katika eneo la chumba cha kuhifadhia maiti, mbunge wa Arusha mjini, ambaye pia ni Waziri Kivuli wa Mambo ya Ndani, Lema alilazimika kumhoji Kamishna Changoja kwa maswali mazito akitaka kujua uharaka wa Jeshi la Polisi kufanya maziko tena ya watu waliowaita kuwa ni wahalifu.

“Kwa nini mnaharakisha maziko bila kuwepo kwa mtu anayewafanyia postmotem? Wewe unasema umetumwa na serikali umetoka makao makuu kuja kuiwakilisha serikali ni serikali ipi unayoiwakilisha?

“Asubuhi Waziri Kagasheki amesema waliouawa ni wahalifu… umekuja hapa huna mkuu wa mkoa, wilaya wala mbunge unamwakilisha nani kwenye serikali iliyokutuma? Ninatilia mashaka uharaka wa serikali kuwazika watu hawa. Ina maana serikali inazika majambazi? Umeanza lini utaratibu huu?” alihoji Lema.

Alisema polisi na serikali yao kuamua kutoa sh milioni tatu kwa kila marehemu kwa ajili ya maziko haijawahi kutokea.

Akizungumza na gazeti hili Lema alisema; “Wakati namuuliza chagonja anasema nisilete siasa kwenye jambo hilo hivi nani sio mwanasiasa? Huyo waziri aliyesema waliokufa ni wavamizi naye mwanasiasa.

“Kwa niaba ya chama changu tumefanikiwa kushwawishi ndugu wote wa marehemu na wameshawishika tukaondoka kwa pamoja pale chumba cha kuhifadhi maiti tukamuacha Chagonja na polisi wenzake, tumemwambia tunaahirisha maziko haya hadi postmotem itakayosema marehemu waliuawa kwa kupigwa risasi wapi kama ni mguuni au kichwani tujue,” alisema Lema.

Kauli nyingine ya Kagasheki

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamis Kagasheki, amemtuhumu mbunge mmojawapo wa chama fulani cha siasa (hakukitaja) kuhusika katika tukio la kushambuliwa kwa Mbunge wa Tarime, Nyambari Nyangwile (CCM), aliyedai kufika katika eneo la Nyamongo kwa ajili ya kuwafariji ndugu wa marehemu waliouawa.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, katika uzinduzi wa sera ya ukimwi eneo la kazi kwa jeshi la polisi nchini, Waziri Kagasheki alisema mbunge wa chama hicho cha siasa alitoka jimboni kwake na kufika kwenye jimbo lingine kwa lengo la kuwahamasisha wananchi kufanya fujo.

“Suala la Nyamongo sitaki kulizungumzia kwa kina, ila niseme kwamba kuna mbunge mmoja wa chama fulani cha siasa, alisafiri kutoka jimboni kwake na kwenda jimbo hilo kwa lengo la kuwahamasisha wananchi kufanya fujo….

“Kitendo kama hicho na vingine vinavyowiana kamwe haviwezi kuvumiliwa ndani ya nchi…,” alisema Waziri Kagasheki.

Alipoulizwa ni hatua gani serikali itazichukuliwa dhidi ya mbunge huyo, Waziri alishindwa kuweka wazi.

“Nimeshasema sitaki kulizungumzia kwa kina suala hilo, na kuliweka wazi mbele ya umma….” alimaliza na kuondoka.

Ngeleja naye azungumza

WAZIRI wa Nishati na Madini, William Ngeleja, ameeleza kusikitishwa na vurugu zilizotokea katika mgodi wa dhahabu wa North Mara. Ngeleja alieleza hayo jana alipokuwa akijibu maswali ya waandishi wa habari waliotaka kujua tamko la wizara yake kuhusu vurugu hizo mgodini.

“Tumesikitishwa na taarifa hizo pamoja na vifo vilivyotokea tunatoa salamu za pole kwa wafiwa, kwa sasa vyombo vya usalama vinashughulikia hali hiyo,” alisema Waziri Ngeleja baada ya kuzindua bodi ya wakala wa ukaguzi wa madini.

Alisema pamoja na mambo mengine, serikali kupitia wizara yake imekuwa ikifanya juhudi kuhakikisha katika eneo hilo kunakuwa na mahusiano mazuri kati ya wawekezaji na wananchi wa eneo hilo.

Alieleza pamoja na changamoto mbalimbali zilizopo katika eneo hilo tayari serikali na wawekezaji wamebuni mradi wa uchimbaji mdogo wa madini ambao utaanza baadaye mwaka huu ili kuwawezesha wananchi kujikwamua kiuchumi.

Takwimu zinaonyesha kuwa zaidi ya watu 23 wameuawa kwa vipindi tofauti kwenye mgodi huo. Hata Barrick wenyewe wanasema nia yao si kuua raia hivyo hawakubaliani na kitendo kilichofanywa na polisi.

CHANZO: Tanzania Daima

19 May 2011


JINA LA BLOG: KONA YA MATUKIO

Tunapenda kulitambulisha wadau wote libeneke jipya la KONA YA MATUKIO ambapo nia na lengo kubwa ni kuleta matukio yanayotokea kila siku katika Jamii yetu na Duniani kwa Ujumla..pia kutakuwa na Matukio ya papo kwa hapo yani Breaking News Endelea kuwepo kila muda kujua nini kitatokea

Kama unatukio la aina yoyote tutumie kupitia [email protected] 
Karibuni nyote na asanteni kwa kututembelea.

Pamoja Tunaweza



Alfajiri ya leo nilikutana na comment ya msomaji mmoja aliyejitambulisha kama Andrew Blasio.Msomaji huyo alianza kwa kuhoji kama sijawahi kuona zuri lililofanywa na CCM.Mie nikamjibu kwa kifupi, "You tell me,sir" kwa maana kama yeye anayajua mema ya CCM basi anieleze badala ya kutegemea mie niyataje.

Akanijibu kuwa yeye haamini kuwa hakuna jema la CCM.HAAMINI.So what?Kwa vile yeye haamini kuwa hakuna jema la chama hicho basi imekuwa nongwa kwa mie kuandika yasiyo mema ya CCM.Akaendelea kunishutumu kuwa eti niko biased katika uandishi wangu,na pengine ni propaganda.Akadai mwandishi sharti awe fair na balanced,na kuhitimisha kuwa hajaona mwandishi anayehubiri uvumilivu wa kisiasa.KWA VILE YEYE HAJAONA BASI INAMAANISHA HAKUNA KITU KAMA HICHO!!!

Nikamjibu

 Sasa mbona wewe unayejua mema ya CCM hutaki kuyaweka hadharani?Na hiyo political tolerance kwako unaitafsiri vipi?Mafisadi wasikemewe?

Nikaongeza 

Unakosoa kuwa niko biased kwa vile hujaona nikiandika "mema" ya CCM.Je bado utaniona biased nikikwambia sijaona jema la kuandika?Na kwanini wewe mwenyewe usijione uko biased kwa kutarajia mema hata kama hayapo?Kukosoa ni rahisi kuliko kutenda jambo.Why not start writing objective,unbiased articles preaching all the good stuff CCM wanafanya?

Naye akanijibu 

Usinishambulie bosi! I'm trying to read " black and white"! kama huoni jema lolote lililofanywa na serikali ya CCM then that is your problem maana "Mwenye macho haambiwi tazama!". Being fair and balanced comes from "journalistic ethics & standard". it doesn't matter whether you are reporting news or you are penning opinions!

Nikahitimisha mjadala kwa kumwambia, 

To be honest with you,I dont write to please whoever reads my articles.I speak my mind supported with facts.As for "journalistics ethics&standards",I'm not a journalist by profession.Tell you what my friend,if you dont like what I write,or it's contrary to what you believe,best I could advise you is to avoid reading them.I dont take issues with constructive criticism,but I hardly pay attention to "people who are not happy with what I wrote just because it's contary to their points of view

Kimsingi,Bwana Blasio hapendezwi na msimamo wa makala zangu kuikosoa CCM,na angependa kuona ikipongezwa.Lakini kama ulivyoona kwenye malumbano yetu hapo juu,yeye mwenyewe hajaongea japo suala moja ambalo lingeweza kuifanya CCM ipongezwe.It doesnt make any sense kumshutumu mtu anayekemea jambo flani lakini wakati huohuo mtoa shutuma anashindwa kutoa japo mfano mmoja wa kuonyesha kuwa kukemea huko sio kwa haki.

Kwa Bwana Blasio na watu wengine wenye mtizamo kama wake,napenda kuwafahamisha kuwa siandiki makala kwa minajili ya kujikomba au kumpendeza mtu.Ninachoandika ni mawazo yangu binafsi,ambayo kama kawaida yangu hayatoki tu pasipo utafiti wa kutosha na wa kusapoti nisemacho.

Lakini la msingi zaidi ni hili.Kama kuna mtu anaona ninachoandika hakimpendezi,kwanini basi apoteze muda wake kukisoma?Si kwamba sipendi kukosolewa bali ninachoafiki ni constructive criticism na sio baseless and unfounded criticism.

Ni rahisi kulaumu makala ninazoandika lakini si rahisi kuandika makala mbadala.Na pengine njia mwafaka ya kupambana na hoja "potofu" kama zangu (kwa mujibu wa Bwana Blasio) ni kuandika makala inayoweza sio tu kujibu au kupinga hoja zangu bali pia kukata mzizi wa fitina kwa kuorodhesha mema ya CCM ambayo hayapatikani kwenye maandiko yangu.

NAREJEA TENA.SIANDIKI KUMFURAHISHA MTU BALI NINA-EXPRESS MAWAZO YANGU NILIYOYAFANYIA KAZI KWA UMAKINI KABLA YA KUYAWEKA HADHARANI.ASIYERIDHISHWA NAYO ANAWEZA KUYAPUUZA KWA KUKAA KIMYA AU KUTOYASOMA.MAWAZO MBADALA RUKSA LAKINI SHUTUMA ZISIZO NA KICHWA WALA MIGUU HAZINA FURSA.


Makala yangu katika toleo la wiki hii la gazeti la Raia Mwema inazungumzia "usanii" wa CCM kujivua magamba,na kuwaingiza mkenge watu kama Nape Nnauye walioamini kuwa chama hicho kimeamua kufanya kweli,kabla ya "moto wa karatasi" haujazimika wenyewe.

Kadhalika,katika makala hiyo nimejaribu kuwashauri CCM watambue kuwa kamwe ugonjwa hautibiki kwa kuukwepa bali kuutambua na kuutibu.Kwa chama hicho,tatizo la msingi ni mwenyekiti wake wa taifa,Rais Jakaya Kikwete,ambaye aliletwa madarakani kwa nguvu za "magamba" na aliposhika hatamu za madaraka akayalea "magamba" hayo.The so-called magamba ni sehemu muhimu ya uhai wa kisiasa wa Kikwete.Kwahiyo kama CCM ina dhamira ya kweli ya kuondokana na ufisadi (magamba) hawana budi kuanza na Kikwete.

Pamoja na makala hiyo ni habari moto moto na makala nyingine zilizokwenda shule ndani ya jarida hili mwanana la Raia Mwema.BONYEZA PICHA HAPO JUU KUSOMA MAKALA HIYO.

18 May 2011


He has been enjoying his freedom to travel back to the UK of late.

And upon his return to London Snoop Dogg looked right at home, conducting a press conference from a gold throne and surrounded by scantily-clad pole dancers.

The rapper played host to the UK media in a strip club yesterday to promote his new album Doggumentary during his second trip to the UK since the ban was lifted.

Snoop Dogg strolled in to the press conference in a sky blue Adidas tracksuit and sipped on tea from a Union Jack mug.



'I'm grateful for being here and proving to the authorities that I deserve to be here. I have had so much love and support from the UK,' The 39-year-old said told the Daily Star.

'When I was a young rapper I would dream of coming here, and when I came I didn't want it to end.'
Snoop Dogg, real name Calvin Cordozar Broadus Jr, was banned from entering the UK following a brawl between his entourage and security at Heathrow airport in 2006.

The following year the Home Office prevented him from obtaining a visa to enter the country with fellow rapper P Diddy, claiming allowing him in the UK could inspire violence and crime amongst fans, despite that his intention was to hold a seminar for youths against gun crime and gang violence.

A judge ruled in 2008 that Snoop had not been at fault during the incident and that he had actually cooperated fully with immigration officials - the ban was fully overturned last year in time for Snoop to play Glastonbury over the summer.

The What's My Name hitmaker is looking forward though, and yesterday announced plans to create his own X Factor-style show.

'X Factor is great but I need to do a show that goes straight to the hood,' he told reporters.

I want to find that raw untamed talent that hasn't been dressed up all nice for the TV. 'Any TV companies want to help me, then they know where I am,' he added.

The competition would feature artists 'with no money, just raw talent and natural ability.'
Snoop Dogg received a warm welcome from fans at a gig later that night before heading to Madame JoJo's and then The Box in Soho.

Earlier this week Snoop performed in Brighton as part of his promotional tour for Doggumentary.


The album features guest performances by Kanye West, David Guetta and also Willie Nelson. At the press conference the rapper named Sade as his ultimate collaborator.

He also defended a more controversial collaboration - his recent record with Charlie Sheen, 'Winning' which was released earlier this month.

'Sheen was my friend before all this happened so I do not judge him,' Snoop Dogg insisted. 'He called on me and I came through for him.

'He is conducting his business, living and functioning. But if the station (CBS, the network behind Two And A Half Men) wanted to put him in a box, then what would have been crazy is staying in that situation.'



Hasheem Thabeet afanya.....

Na Brighton Masalu

STAA wa mpira wa kikapu, duniani akicheza katika Ligi ya NBA nchini Marekani, Hasheem Thabeet Manka ‘Super Tall’ (pichani) amefanya kufuru ya fedha baada ya kumwaga fedha ukumbini na kuwaacha watu wagombanie, twende mstari kwa mstari.

Paparazi wa gazeti hili lenye heshima ya nyota tano kwa habari za mastaa Bongo, alishuhudia tukio hilo live wikiendi iliyopita katika Ukumbi wa Bilicanas uliopo Posta, jijini Dar es Salaam ambapo handsome boy anayecharaza fimbo katika muziki wa kizazi kipya, Abdul Sykes ‘Dully Sykes’ alikuwa akipiga shoo babkubwa.

Awali kasuku wa gazeti hili alimshuhudia Hasheem akikatiza kwa madaha ukumbini humo, akiwa ameongozana na wapambe wake waliokuwa wakimuandalia njia, kisha kukaa sehemu moja na kuanza kula bata kwa mtindo wa ‘tingisha kama imeisha, leta nyingine’.

Wakati shoo ikiendelea Hasheem aliinuka na wapambe wake kuongoza mbele kama kawa, kisha wakaelekea jukwaani alipochomoa burungutu moja la ‘nyekundu nyekundu’ tupu na kumkabidhi Dully Sykes ambaye aliongeza manjonjo baada ya kutuzwa na supastaa huyo.

Hakuishia hapo, aliposhuka jukwaani, alizama mfukoni na kutoa burungutu lingine kisha akalirusha juu na mashabiki kuanza kugombania.

Wakati watu wakiendelea kukanyagana wakigombea mkwanja huo wa ‘sadakalawe’ Hasheem na wapambe wake walitoka nje na kuingia kwenye gari aina ya Hummer na kuondoka kiwanjani hapo.

“Duh! Ebwana ee, jamaa huyu ni noma yaani minoti yote hiyo kaiachia watu wanyang’anyane? Hii ni kufuru, kweli mshkaji fedha imemkubali,” alisika jamaa mmoja akisema ukumbini hapo.

Hasheem Thabeet amerejea nchini hivi karibuni akitokea Marekani anapoishi, yupo kwa mapumziko mafupi. Ni Mtanzania pekee anayeipeperusha bendera ya Tanzania kwenye ligi ya NBA ya mpira wa kikapu nchini humo.

Na yafuatayo ni maoni ya wasomaji wa gazeti hilo

Comment by Eddie Mourice Junior 1 hour ago
Kwa hili umechemka hasheem even if ur money!
Comment by KUU LA MAADUI 7 hours ago
Dogo pesa ni zako lakini kwa hii ya leo umetimba ,sikujua kama na wewe bado mgeni na pesa aise kwa nini unafanya hivyo hujui kama anaweza kufa mtu katika kugombania minoti halafu wewe ukastakiwa kwa kusababisha vifo ,aise umeniuthi unakuwa mrefuuu 22222222 nje ndani mfupi acha ulimbukeni najua hata ndugu zako hawata fuhia upuuzi huo,kama unapesa unakuwasha utumie katika mambo mazuri mungu atakubariki sio kurushia walevi.
Comment by Minja Frank 7 hours ago
Ona mwenzio mwenye kipaji cha mpira wa kikapu kama wewe Dikembe Mutombo wa DRC kajenga Hospital kubwa tu Kinshasa. Wewe wamwaga pesa yako kwenye masanga. Saidia nchi yako!!!
Comment by Alphoncene Gerald 8 hours ago
Sina hata cha kuchangia
Nachoka kabisa
Comment by Miriam John Mndolanga 8 hours ago
Ulivyofanya ndivyo nafsi yako ilivyokutuma, kwa upande wako ni sawa tu ila ni vema hela unayoitolea jasho na kusumbuka sana hadi kuipata ungeiwekeza kwa makundi yenye mahitaji maalum na Mungu atakubarikia zaidi ya ulichotoa. Jifunze kupitie kwa waliofanya kama hivyo wameishia wapi?
Badilika Hasheem, usijijengee sifa mbaya kwa jamii yako.
Comment by julius manning 8 hours ago
huo ni ulimbukeni mkubwa akumbuke akina Tyson walikuwa na hela kuliko yeye lakini leo je
Comment by swalih/waziri 8 hours ago
huo niulimbukieni wakati familia nyengine pesa yakula mtihani wewe pesa unazigawa kwa walevi inshlwa mungu akulaani uje kuzikumbuka sikatowe misaada makanisani msikitini na mashuleni wewe unagawa kwa walevi ili upate jina kuwa umegawa pesa<.
Comment by Matu 8 hours ago
Pesa ni sabuni ya roho lakini pesa nazo zina upepo wake...wakati ukuta...pesa ni kama maua..huchanua na kusinyaaa kwa mtoto wa manka sasa zimechanua...!
Comment by anna [email protected] 8 hours ago
Ama kweli masikini akipata matako huria mbwata, hivi wewe umesahau tabu zote ulizopita, haya baba wakati wako hivi humuoni mwenzio yule modo anaitwa matata kila mwaka anatoa msaada kwa yatima wewe unagawa pesa kwa walevi, una akili nyingi sana mtoto wewe, ina maana hata kule kijijini kwenu huna wanaohitaji msaada, utakuja juta baadae na hao wapambe huta waona sana watakucheka, wapi nice??? unalewa sina
Comment by ikk 8 hours ago
Kweli minoti unaigawa kwa watu wenye ziada tele, tena Klabu? Wakati kuna watoto yatima huko makete wanalea wadogo zao, tena kwa kupika pombe za kienyeji?
Laana huanza polepole!
Comment by Sebastian Salatiel Shemhilu 9 hours ago
DUUH!! HII NI DHARAU YA FEDHA AU JEURI YA FEDHA? HASHEEM TOA PESA ZAKO KWA YATIMA KULIKO KUWAPA PESA WALEVI NAMNA HIYO.MUNGU ATAKUPA ZAIDI.

Comment by Mapresha Getebariadi 9 hours ago
Hela iko wapi wenye fedha hawafanyi hivyo hapo alikuwa anawachanganya warembo waanze kujimwaga kwake. Kama anahela si asomeshe hata yatima 2 tu.
Comment by edmas 9 hours ago

Haya bana, wakati wako huu. Alikuwepo Mr. Nice naye alifanya kufuru ya pesa, sasa yupo apeche alolo, kushnei.
Comment by furaha Tausi 9 hours ago
WEE HASHEEM WEWE KWANINI HIYO HELA USIWASAIDIE HATA WATOTO WA MITAANI JAMANI HATA WALE WATOTO WALIOKO OCEAN ROAD HOSPITAL WANAUMWA KANSA?? MUNGU ATAKULAANI SHAURI YAKO

16 May 2011



Wasaidizi wana nafuu kuliko rais?

Ansbert Ngurumo

BAADHI yetu hatujaelewa ari, nguvu na kasi ya Rais Jakaya Kikwete. Nina hakika naye ameiimba, lakini hajaielewa barabara.

Kaulimbiu hii iliyoasisiwa na kina Samuel Sitta mwaka 2005, ilitumika kumtafutia urais mgombea wa CCM, Jakaya Kikwete, kwa ari mpya, kasi mpya na nguvu mpya.

Waliomjua vema uwezo na udhaifu wake walidokeza mapema kwamba maisha ya Watanzania chini ya CCM ya Kikwete yangedorora na kuwa magumu zaidi - kwa ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya.

Baadaye, sisi na baadhi ya watani wa CCM tuliifupisha kaulimbiu hiyo, tukaiita ANGUKA. Ni kweli! Miaka mitano baadaye, wameangukia pua.

CCM imeanguka. Rais Kikwete ameanguka. Mtandao wake umeanguka. Na kwa bahati mbaya, hata serikali yake imeanguka, ikaishia kuwa serikali kopa-kopa – hata mishahara ya watumishi – licha ya kodi kubwa tunazolipa.

Kuanguka huku, ndiko kumekuwa chanzo cha kura chache za mgombea urais wa CCM katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010. Kuanguka huku ndiko kumekuwa kichocheo cha vilio vya wananchi dhidi ya ufisadi. Kuanguka huku ndiko kumesababisha hata usanii mpya wa CCM wa ‘kujivua gamba.’

Kuanguka huku ndiko kumemkosanisha Rais Kikwete na maswahiba wake wa siku nyingi. Kuanguka huku ndiko kumemfanya Rais Kikwete aogope maandamano ya wananchi yanayoratibiwa na CHADEMA hata akalialia kwamba “wanataka kuniondoa kabla ya wakati.”

Kuanguka huku ndiko kumemwondoa Yusuf Makamba katika ukatibu mkuu wa CCM, yeye na sekretariati na Kamati Kuu. Kuanguka huku ndiko kumerutubisha na kukuza fitina na vita ya makundi ndani ya CCM.

Kuanguka huku ndiko kumewafanya Watanzania kuikataa CCM waziwazi kuliko wakati wote katika historia, na ndiko kumemwingiza Nape Nnauye (Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM) katika migogoro mipya ndani ya makundi ya CCM na kumwandalia anguko lake huko tunakokwenda, hasa baada ya Rais Kikwete kuondoka madarakani.

Anguko hili la ari mpya, kasi mpya na nguvu mpya limewagusa wananchi wenyewe. Sasa wanakabiliwa na ukali wa maisha usiofanana kabisa na ahadi kemkemu walizopewa na CCM mwaka 2005 na 2010.

Bahati mbaya waliosababisha anguko hili, bado wanajitapa kwamba wameleta maendeleo. Vipofu!

Na kwa sababu ya upofu huu, wanakosa mikakati mipya ya kujikwamua. Wanarudiarudia yale yale yaliyoshindwa kuwanusuru miaka mitano iliyopita.

Kwa mfano, mwaka 2006 mwanzoni, Rais Kikwete aliingia na mbinu ya kutembelea wizara moja moja, kutoa maelekezo na kupiga picha na watumishi wa wizara hizo. Ilikuwa propaganda na mapambo ya magazeti na televisheni.

Baadaye, aliwaita mawaziri na watumishi waandamizi wa serikali (mara mbili) katika semina elekezi kwenye Hoteli ya kifahari, Ngurdoto, Arusha.

Leo tunapotazama nyuma, ni nani anaweza kujivunia semina elekezi za Ngurdoto?

Lakini watu wasiojifunza hawafichiki. Mwaka jana, rais yule yule akagombea kwa kaulimbiu ya ari zaidi, kasi zaidi na nguvu zaidi. Yaani, hawa jamaa hawakuridhika na ’anguko jipya’ la 2006. Waliona hilo halitoshi, wakatuandaa “kuanguka zaidi” mwaka 2010!

Haikumwongezea kura mgombea wao. Haikuvuta hisia za vijana wala kina mama. Ili kupata watu wa kuhutubia ilibidi CCM itumie pesa nyingi kuchapisha na kugawa sare, kuwagawia watu na kuwapakia kwenye magari kuwapeleka kwenye mikutano ya mbali.

Haikuwaunganisha watawala wawe na sauti moja, hata baada ya kurejea madarakani. Haikuwasaidia kupata hekima ya kumaliza matatizo ya muda mrefu, kama ukosefu wa umeme ambao umezungumzwa tena na tena bila ufumbuzi.

Sasa kwa ari zaidi, nguvu zaidi na kasi zaidi, watawala wamerudi tena katika semina elekezi, chini ya mwelekezaji yule yule.

Walidhani zile zilishindikana kwa sababu zilifanyika Arusha. Sasa wamekimbilia Dodoma. Kwa wiki nzima, serikali iko Dodoma, imelala; inakula posho. Kazi zinakwama.

Rais naye, badala ya kuwaelekeza kwa hekima na ustadi, “akawananga” wasaidizi wake hadharani, kana kwamba huwa hapati fursa ya kukutana nao – wakati amekuwa akikutana nao kila mwezi katika vikao vya Baraza la Mawaziri. Ndio hao aliowatembelea na kuwasema wizarani kwao miezi miwili iliyopita, hata akawaamuru wengine waache ubabe.

Alitaka kuonewa huruma. Alitaka kuwashitaki kwa wananchi – waonekane wabaya, awe mzuri.

Rais anawasema mawaziri wake kama watoto wadogo wanaohangaika kuelewa kitu kidogo anachowafundisha. Anawaonyesha wananchi kwamba ana mawaziri mizigo, mbumbumbu – ambao kazi pekee wanayofanya ni “kumwangusha” rais.

Anataka turudi kwenye propaganda za kijinga walizoimba miaka mitano iliyopita, kwamba rais pekee ndiye anachapa kazi, bali mawaziri wake wanamwangusha.

Anawaambia mawaziri wake kuwa kama hawawezi kazi “waondoke,” kana kwamba hajui uwezo wao, hajui waliingiaje, wakati ndiye aliyewateua na ndiye ana mamlaka ya kuwaondoa.

Anataka “watoke” waende kwa wananchi kufafanua mafanikio ya serikali yake. Haamini kwamba wananchi wana uwezo wa kuona mazuri na mabaya ya serikali – bila kusubiri taarifa za mawaziri.

Haoni kwamba serikali inayofilisika na kulazimika kukopa hata mishahara ya watumishi wake, inahitaji kubana matumizi na kupunguza ziara na posho nono za viongozi hao waandamizi.

Lakini pia, tunapowatazama watu wenyewe aliokuwa anawapa somo, tunabaki kujiuliza: Rais amepata wapi hekima hii ya kudhani ana uelewa mpana kuliko mawaziri wake?

Amesomea wapi huko wasikojua wao, alikopata hicho cha kuwafunda? Tunapowatazama baadhi yao tunagundua kwamba kama rais angekuwa na busara ya kujifunza kutokana na miaka mitano iliyopita, asingewaita mawaziri kuwafunda, bali angewaita ili wakae kama timu, awaombe ushauri, awasikilize, wampe mang’amuzi yao na mipango mkakati; naye baada ya kuwasikiliza na kuongeza maono yake, awapangie kazi na kuwadai matokeo baada ya muda kadhaa.

Au basi angeunda kikosi kazi cha wasomi waliokubuhu kutoka taasisi mbalimbali zinazoheshimika, akawakutanisha na wasaidizi wake, wote pamoja wakavuna maarifa ya ziada katika kuboresha kazi zao na kukosoa kasoro za huko nyuma.

Angejenga mazingira ya kuambizana ukweli, naye akaambiwa kasoro zake; hasa kwamba serikali imekosa mipango mkakati mbadala na hata hiyo iliyopo imekosa msimamizi makini.

Kitendo cha rais kulialia mbele ya wateule wake na wananchi kupitia vyombo vya habari si ishara ya ushupavu anaostahili kuwa nao kiongozi mkuu wa nchi.

Ndiyo! Tuliona wameinama na kushika tama alipokuwa anafoka. Lakini ana uhakika gani kwamba walikubaliana naye? Ana uhakika gani kwamba walimwona shujaa?

Na kwa kiongozi ambaye ameongoza nchi kwa miaka mitano kwa hotuba na matamko yasiyotekelezeka, anadhani mawaziri wake watamwamini na kumheshimu baada ya kufokewa hadharani Dodoma?

Labda, watamshukuru kwa kuwatengenezea mazingira ya kula posho za safari. Lakini naamini mawaziri wenyewe wanajua fika kwamba hawana sababu ya kusafiri hadi vijijini kila mara, maana huko kuna watendaji wa ngazi za chini wanaopaswa kusimamia kazi na kuleta taarifa kwa ngazi za juu.

Sasa kama rais anaagiza mawaziri waende wenyewe vijijini, hao watendaji wa mikoani, wilayani na vijijini kwenyewe watafanya kazi gani?

Hivi waziri aliyekaa katika wizara ile ile kwa miaka mitatu au zaidi, ana kitu gani cha kujifunza kwa rais aliyekaa madarakani kwa miaka mitano bila maono na mafanikio yanayoshikika?

Rais Kikwete ana mfano gani wa utendaji uliotukuka anaoweza kuutumia kuwasuta mawaziri wake? Aliacha urithi gani katika wizara alizowahi kuongoza kabla hajawa rais?

Ni nani anayejua matatizo, changamoto, na suluhisho la matatizo yake, kati ya waziri aliye kwenye wizara hiyo hiyo, na rais “anayeishi kwenye ndege?”Baadhi yetu tunajua kwamba mkwamo mkubwa wa kiutendaji unatokana na madaraka makubwa ya rais, nidhamu ya woga ya wasaidizi wake na utovu wa uzalendo wa baadhi yao.

Zipo taarifa kwamba siku hizi wasaidizi wa rais wameamua kumwambia yale anayotaka kusikia, kwa sababu anawafokea hovyo hovyo wanapomweleza asiyotaka, au wanapompa mapendekezo magumu.

Wanadai rais hataki kuambiwa asichotaka; nao hawako tayari kupoteza kazi zao.

Kwa mantiki hii, haiwezekani kwamba baadhi ya wasaidizi wa rais wana nafuu kuliko yeye? Kwanini tusiamini, basi, kwamba rais ndiye anawaangusha wasaidizi wake?


Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.