27 Jul 2011



From: Andrew Bomani
Subject: TAMKO LA KIHISTORIA NA HALI YA KUHUZUNISHA NCHINI!
Date: Monday, July 25, 2011, 3:26 AM

Ndugu msomaji,

Kufuatia ombwe la uongozi la kutisha nchini ambalo karibu kila Mtanzania anakiri ndiyo tatizo mama, baadhi yetu tumeona ni vyema tukawafikishia tamko ambalo liliwahi kutolewa mwaka 1995 na Jaji Bomani. Ni jambo la kusikitisha kwamba wananchi wengi wanadhani kwamba viongozi waliokuwepo wakati huo na waliopo sasa pengine ndiyo waliokuwa bora. Jambo hili ni hatari. Haiwezekani nchi yoyote ikakosa watu makini. Soma na tafakari namna mizengwe katika kupata viongozi makini inavyoweza kulifikisha taifa lolote mahali pabaya.

Mungu Ibariki Tanzania.

Tamko la Kihistoria



Barua ya UVCCM Kwa Jaji Bomani Kumwomba Agombee Urais 2005

25 Jul 2011


Nchi ipo kizani,Rais Kikwete yupo bize kuzurura nje ya nchi,na akirejea ni kama hayupo.Binafsi sielewi kwanini huyu mtu aligombea urais mwaka 2005 na baadaye 2010.Je ni kuweka historia tu hata kama historia yenyewe ni ya kukinai?Je ni kutopima kina kabla ya kujitosa bwawani?

Kitu kimoja cha wazi ni kwamba kama kuna mtu anayetegemea Kikwete na CCM yake wataleta ufumbuzi wa matatizo ya Tanzania,basi anaweza pia kutarajia kugema damu kwenye jiwe.Kulalamika peke yake hakuwezi kuleta ufumbuzi wa matatizo.Mkoloni,Makaburu,Nduli Idi Amini hawakuondoka kwa vile tuliwatukana au kuwalalamikia,bali tulijiunga kwa umoja wetu na kupambana nao (hata kwa nguvu ilipobidi).

Anyway,soma habari hii hapa chini inayodhihirisha kuwa wababaishaji hawa (Kikwete na chama chake cha Magamba) wapo too busy katika vita vyao vya kimaslahi to care about matatizo ya Watanzania 

Gamba laivuruga CCM 
Monday, 25 July 2011 08:47


Makamu Mwenyekiti wa UVCCM Benno Malisa

WENYEVITI MIKOA WALIPINGA, BARAZA KUU UVCCM LAUNGA MKONO ZIARA ZA KINA NAPE
Waandishi Wetu
MPANGO mkakati wa kujivua gamba kwa lengo la kurejesha uhai ndani ya CCM unaelekea kuwa bomu la maangamizo kwa chama hicho, baada ya baadhi ya wenyeviti wa mikoa kuupinga huku wakiagiza wafuasi wao kuwashusha majukwaani makada wanaoupigia debe.
Wakati wenyeviti hao wakiupinga, Baraza Kuu la Umoja wa Vijana CCM (UVCCM), jana limetoa tamko rasmi la kuunga mkono ziara hizo zinazofanywa na Katibu wa Itikadi na Uenezi Taifa wa chama hicho, Nape Nnauye za kutekeleza mkakati huo.

Mpango huo wa kujivua gamba ulitangazwa na Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete katika maadhimisho ya miaka 34 ya kuzaliwa chama hicho kikongwe barani Afrika, lakini jana baadhi ya wenyeviti wake wa mikoa akiwamo, John Guninita wa Dar es Salaam na Hamis Mgeja wa Shinyanga, waliupinga wakisema unamwaga sumu kali dhidi ya chama.

Msimamo wa UVCCM
Baraza Kuu la UVCCM limetoa msimamo wake kuunga mkono ziara za mikoani zinazoongozwa na Nnauye za kujivua gamba huku likiweka bayana kuwa huo ni msimamo wa Halmashauri Kuu (Nec) ya chama na si wa Katibu huyo wa Itikadi na Uenezi.

Mbali na Nape, Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk Harrison Mwakyembe na Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka wamekuwa wakifanya ziara mikoani hasa katika mwisho wa wiki ambazo pamoja na mambo mengine, wamekuwa wakifanya mikutano ya kukipa uhai chama huku wakitangaza uvuaji gamba.

Kaimu Mwenyekiti wa UVCCM, Benno Malisa alisema UVCCM ilipongeza uamuzi wote wa NEC: "Kila kinachofanyika ni sahihi na sisi tunaunga mkono kabisa."

Guninita awatangazia vita
Wakati vijana wakiuunga mkono ziara hizo, juzi Guninita aliwaambia wanaCCM wa Tawi la Sinza kwamba watakapomuona kiongozi yeyote mkubwa wa chama hicho anakikiponda katika wasisite kumshusha jukwaani.
Guninita alitoa kauli hiyo alipokuwa akizungumza na wanachama hao kuhusu matatizo mbalimbali ya chama hicho na kusisitiza kwamba Waziri Sitta asipojibiwa kauli zake atajiona kuwa ni mkubwa zaidi.

Wiki iliyopita Mwenyekiti huyo alimtupia kijembe Sitta akidai kwamba waziri huyo ana mpango wa kuhakikisha kuwa Serikali ya chama hicho inaondolewa madarakani kwa kuwa bado ana hasira za kupoteza wadhifa wa Spika wa Bunge.

“Chama chetu kinazidi kupoteza sifa, hii ndiyo sababu ya mimi kufanya ziara katika majimbo ambayo yalishindwa katika ngazi zote kukipatia chama ushindi wakati wa uchaguzi. Kumekuwa na viongozi wakubwa wa chama hicho wanaozunguka nchi nzima na kuchochea ili Serikali iondolewe madarakani, nawaambieni mkiwaona viongozi hao wanakiponda chama washusheni majukwaani, wanataka kujiona wao ndiyo wakubwa zaidi ya wengine.”

Alisema chama hicho kinajipanga kikamilifu ili kuhakikisha uchaguziwa mwaka 2015, kinashinda kwa kishindo ikiwa ni pamoja na kupambana na tatizo la rushwa lililokitawala.

Guninita ambaye amekuwa akipingana hadharani na wapambanaji hao wa ufisadi ndani ya CCM, alisema katika uchaguzi huo hawatahitaji ushahidi kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana Rushwa (Takukuru) na kuwa mtu atakapobainika anajihusisha na rushwa atachukuliwa hatua hapohapo.

“Tatizo la rushwa katika chama lipo hasa wakati wa uchaguzi. Ninachotaka kuwahakikishia ni kwamba tunajipanga na katika uchaguzi ujao hatutahitaji ushahidi wa PCCB (Takukuru), tutakapombaini mtu tutampeleka mahakamani wenyewe. Hatutaki aibu ya mwaka huu itukumbe tena.”

Alisema tayari chama kimewabainisha viongozi wote walioingia madarakani kwa rushwa na kuwa wanaendelea kujadiliana hatua za kinidhamu dhidi yao.

Guninita alisema katika uchaguzi wa mwaka 2015, chama hicho hakitapeleka majina ya watu watakaobainika kutoa rushwa kwa ngazi za juu ili wakubalike katika kura za maoni.

Mgeja atoa tahadhari
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa CCM, Mkoa wa Shinyanga, Hamis Mgeja alisema juzi kwamba licha ya kuwakaribisha wapambanaji hao na mkakatio wao wa kujivua gamba katika mkoa wake, waende na majibu ya kero za wananchi.

Alisema viongozi wa chama chake wanatakiwa kwenda na majibu ya kero zilizopo katika mkoa huo za wakulima kuuziwa dawa feki za pembejeo, rushwa, umasikini na rasilimali kama madini kushindwa kuwanufaisha, badala ya kutumia ziara hiyo kuwapaka matope wenzao.

“Ziara za kusafisha chama siyo mbaya, kama zitatumika vyema, lakini hali ambayo imeanza kujitokeza ni wazi haijengi chama, bali inaendelea kumwaga sumu,” alisema.

Millya, Porokwa waponda ziara hizo
Mbali ya Guninita na Mgeja, Mwenyekiti wa UVCCM, mkoani Arusha, James Ole Millya naye ameziponda ziara hizo za kujivua gamba akisema hazina tija kwa chama na Serikali kwa kuwa Sitta, ni waziri ndani ya Serikali hiyohiyo anayoituhumu na kueleza kwamba anaona kuna uchafu ndani yake ni vyema akatoka.

Millya aliwatuhumu Sitta, Nape, Ole Sendeka na Dk Mwakyembe kuwa wamekuwa wakitumia mwanya wa ziara hizo kuichafua Serikali na chama tawala huku akisisitiza: "Kama wanaona Serikali hiyo haifai ni bora wangeondoka. Sitta ni waziri, Mwakyembe ni waziri na wengine wako ndani ya Serikali na chama hawa wote ni viongozi, sasa kitendo cha wao kuzunguka na kuisema vibaya Serikali na chama tawala hakifai.”

Alisema viongozi hao wameamua kuanza mashambulizi dhidi ya Serikali kwa kuwa ni wabinafsi, huku akikitahadharisha chama hicho kuwa makini na ziara hizo kwa kuwa huenda zikakiingiza katika hatua mbaya.

Naibu Katibu wa CCM Wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro, Daniel Porokwa naye aliziponda ziara za viongozi hao akisema zimejaa unafiki kwa kuwa Sitta na Nape walikuwa waanzilishi wa Chama cha Jamii (CCJ) na kuwaita wasaliti ndani ya CCM.

Alisema pamoja na kutoa tuhuma mbalimbali dhidi ya viongozi hao kuwa ni waasisi wa CCJ, anashangaa hadi leo uongozi wa chama chake haujawahi kumwita au kumwomba udhibitisho juu ya madai aliyoyasema.


Katibu wa Itikadi na Uenezi Chama Cha Mapinduzi (CCM)

Nape akutana na mabango Moshi
Ziara ya Nape, juzi mkoani Kilimanjaro ilikumbana na upinzani mara baada ya kiongozi huyo kupokewa kwa mabango mbalimbali wakati akishuka kwenye gari lake katika Kituo cha Mabasi Moshi Mjini tayari kwa kuhutubia mkutano wa hadhara katika eneo hilo.

Hata hivyo, tofauti na mikutano mingine kama ule wa mkoani Mbeya, huo ulihudhuriwa na watu wachache huku wengine walionekana wakishuka kutoka kwenye mabasi uwanjani hapo.

Nape aliyefika kituoni hapo mnamo a saa 9:00 mchana akitokea Mwika katika ufunguzi wa Tawi la CCM Chuo Kikuu cha Tumaini (Smmuco), alikutana na mabango yaliyokuwa yameshikiliwa na vijana wa CCM wilayani Moshi ambayo yalikuwa yamebeba ujumbe mbalimbali.

Baadhi ya mbango hayo yalikuwa yakisomeka: ”CCJ nao wajivue gamba,” “Hatutaki makundi ndani ya CCM,” ”Vijana tumechoka na wana CCJ, wana CCJ ondokeni mtuachie CCM yetu.”.

Wakati vijana hao wakibeba mabango hayo mbalimbali yaliyolenga kufikisha ujumbe kwa Nape, vijana wa ulinzi wa CCM maarufu kama “Green Guard,” iliwabidi kutumia nguvu za ziada kuzima juhudi za vijana hao waliobeba mabango hayo na waliyakamata na kisha kuyachana baadhi yao huku mengine yakiwasilishwa katika Ofisi ya Katibu wa CCM wilayani Moshi.

Akimkaribisha Nape jukwaani, Katibu wa CCM Wilaya ya Moshi Mjini, Amos Shimba aliyaponda vikali mabango hayo huku akisema vijana walioyabeba siyo wakazi wa Mji wa Moshi, bali wanatoka mkoani Arusha huku akiwaonya, kamwe wasithubutu kuleta mambo hayo mkoani Kilimanjaro.

“Kuna vijana wanaotaka kutuletea vurugu na tunajua wanatoka tu Arusha, tunawaambia tafadhali sana msituletee mambo yenu ya vurugu za Arusha hapa mkoani kwetu,” alionya Shimba.

Akihutubia mkutano huo, Nape alisema lengo la ziara yake mkoani Kilimanjaro ni kuleta matumaini kwa wanachama wa CCM sanjari na kufafanua falsafa ya kujivua gamba ambayo alidai inapotoshwa na watu wachache hapa nchini.

Alikishambulia Chama cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema) hususan viongozi wake kwamba wanapenda vurugu na maandamano huku akionya kwa kutumia mifano na nahau mbalimbali ya kuwa kamwe Serikali ya CCM haitakubali amani ya nchi ichezewe.

Aliendelea kumshambulia vikali Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa akidai kuwa ameamua kukishinikiza chama chake kumlipa kiasi cha Sh7 milioni ihali alikuwa kinara wa kupinga mishahara minono na marupurupu ya wabunge.

“Namtaka Dk Slaa aishi kama anavyoongea, alinituhumu nahusika na EPA mkiniangalia mimi sura yangu inafanania na EPA? Mbona yeye amekishinikiza chama chake kimlipe Sh7milioni wakati alikuwa akipinga mishahara na marupurupu ya wabunge? Huyu ni mnafiki,” alisema Nape.

Alisema falsafa ya kujivua gamba ndani ya CCM imekuwa ikipotoshwa na baadhi ya watu hususan wapinzani na kuuita kuwa ni dhana ya kishetani kwa kuwa imetumia mfano wa nyoka na kuwabeza watu hao kwa kuwataka wasome biblia na msaafu na kuwaeleza kuwa nyoka ametajwa ndani ya vitabu hivyo.

Akizungumzia kauli za wanaCCM wanaoipinga dhana hityo, alisema asingependa kujibizana na watu wanaouzungumza barabarani kwani chama kina vikao ambavyo vitawahukumu.

Alichokisema Sitta
Akizungumza Dar es Salaam juzi, Sitta alisema Serikali makini lazima ikiri mapungufu kutokana na makosa yake: "Nilichokisema Mbeya ni kuwaambia Watanzania ukweli na nitaendelea kuwaambia ukweli."

Alisema serikali makini haiwezi kuwadanganya wananchi wake na kusisitiza, "Watanzania wa leo ni watu wenye akili huwezi kuwambia habari nzuri za umeme wakati umeme ni tatizo."

"Kule Mbeya nilieleza ule umati ukweli kuhusu upungufu wetu serikalini na wananchi walituelewa. Kuna upungufu tumeukiri na tunajipanga kuupatia ufumbuzi. Umeme ni tatizo kubwa huwezi kueleza uongo kwa Watanzania wakakuelewa, waambie wananchi ukweli watakuelewa. Sasa huu ndiyo upungufu wetu, lakini wanatokea baadhi ya watu wenye upeo mdogo ndani ya CCM wanaoendekeza siasa za ufuasi, wanakaa na kuzungumza mambo ya hovyo."

Imeandaliwa na Ramadha Semtawa, Minael Msuya, Dar, Habiel Chidawali, Dodoma, , Moses Mashalla, Moshi

Chanzo: Mwananchi 


CLICK THE PICTURE TO ZOOM

SOURCE: The Economist

24 Jul 2011


Nimepokea kwa masikitiko kifo cha Mhadhiri wangu wa zamani Profesa Samuel Mushi.Nilikuwa mwanafunzi wa Profesa Mushi tangu nilipojiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Septemba 1996 hadi nilipomaliza mwaka wa kwanza July 1997.Profesa Mushi alinifundisha Utangulizi kwa Stadi ya Sayansi ya Siasa (PS100: Introduction to the Study of Political Science).Marehemu ni miongoni mwa wanataaluma wa mwanzo walionipa uelewa na mwamko wa stadi za siasa,japokuwa mwaka wa pili na wa tatu nilichukua mchepuo wa Sosholojia.

Bwana Ametoa Bwana Ametwaa.
Jina la Bwana Lihimidiwe Milele,
Amen 

23 Jul 2011


FAMILIA YA TULLY NGONYA(MAMA MARIA) NA IKUPA NGONYA WANASIKITIKA KUWAARIFU MSIBA WA BABA YAO MPENZI MZEE J.D. NGONYA ALIEFARIKI LEO ASUBUHI 23.7.11.
KAMA ILIVYOKUWA DESTURI YETU TUNAWAOMBA WOTE TUKUTANE TUWAFARIJI WAFIWA WAKATI WA KIPINDI HIKI KIGUMU.
MSIBA UPO 38 TRELLECK ROAD, READING RG1 6EN. 
BWANA AMETOA, BWANA AMETWAA JINA LAKE LITUKUZWE MILELE. AMEN.
TAFADHALI MJULISHE NA MWENZAKO

Imetumwa na Urban Pulse Creative


Hili sio ombwe tena bali mkusanyiko wa wababaishaji walioteuliwa na mtu asiyejua kwanini aliwateua,na ndio maana wanaendesha mambo kama kwenye mchezo maarufu wa watoto ujulikanao kama kombolela.Watu wazima ovyoo!Lakini ni wazi wanapata jeuri ya kufanya ubabaishaji huo kwa vile wanafahamu fika kuwa aliyewateua hana jeuri ya japo kuwawajibisha,let alone kuwakemea.

Anyway,hebu soma madudu yao hapa chini:

DPP amkana Hoseah  
Friday, 22 July 2011 20:27

ASEMA HAJAPATA JALADA LA CHENGE, AAMBIWA AKAANGALIE MASJAJA
Nora Damian
SIKU moja baada ya Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk Edward Hoseah, kusema kwamba ofisi yake imekamilisha uchunguzi wa madai ya kumiliki Dola za Marekani 1.2 milioni katika Kisiwa cha Jersey, Uingereza yanayomkabili Mbunge wa Bariadi Magharibi (CCM), Andrew Chenge na kwamba imekabidhi faili lake kwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP) kwa ajili ya kumfungulia mashtaka, kiongozi wake, Eliezer Feleshi amejitokeza na kusema kwamba hawahi kuliona jalada hilo.

"Niko safarini subiri hadi wiki ijayo… kwanza ashtakiwe kwa kosa gani? Acheni siasa nyie,” alisema DPP alipotakiwa kuthibitisha kama jalada hilo limefika mezani kwake na lini Mwanasheria huyo Mkuu wa zamani wa Serikali atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili... “Aseme ni tarehe gani alileta jalada hilo kwangu?”

Kutokana na majibu hayo ya DPP, Mwananchi lilimtafuta Dk Hoseah kupata ukweli juu ya kauli yake hiyo aliyoitoa juzi huko Arusha na kusisitiza kuwa jalada hilo limepelekwa katika Ofisi ya DPP na kumtaka mkuu huyo wa Mashitaka nchini asiharakishe kusema hajaliona, kwani siyo lazima kila kitu akabidhiwe mikononi... “Kwani kila kitu kinachopelekwa kwake lazima akione? Ameangalia registry (masjala)?. Suala hili nimeshaliongea nanyi vya kutosha hivyo muulizeni zaidi DPP.”

Juzi, Dk Hoseah alisema taasisi yake imekamilisha uchunguzi dhidi ya tuhuma zinazomkabili Chenge na kwamba jalada lake limepelekwa kwa DPP kwa hatua zaidi. Alisema Chenge atashtakiwa chini ya Kifungu cha 27 cha Sheria ya Takukuru ya mwaka 2007. Kwa mujibu wa kifungu hicho, mtu akiwa na mali ambazo hazilingani na kipato chake alichokipata akiwa madarakani au baada ya kuondoka ni kosa kisheria.

Chenge anadaiwa kukutwa na kiasi hicho cha fedha mwaka 2008 baada ya uchunguzi wa kashfa ya ununuzi wa rada uliofanywa na Taasisi ya Makosa Makubwa ya Jinai ya Uingereza (SFO). Tuhuma hizo ndizo zilizomfanya alazimike kujiuzulu wadhifa wa Waziri wa Miundombinu mwaka huo.

Malumbano kati ya Dk Hoseah na Feleshi siyo ya kwanza. Mwaka jana waliwahi kulumbana baada ya mkuu huyo wa Takukuru kusema kuna majalada takriban 50 ya kesi za rushwa ambayo yamekaliwa na DPP.

Pia Dk Hoseah aliwahi kumshutumu DPP mbele ya wabunge wakati wa semina elekezi mapema mwaka huu akidai kwamba amekuwa kikwazo cha kesi kubwa za ufisadi kupelekwa mahakamani kwa kukwamisha majalada.

CHANZO: Mwananchi 



Kalapina on politics, Freemasons, war, peace, Rostam, Drugs etc.
More from Kalapina and kikosi http://www.reverbnation.com/tunepak/3387426

Click the banner titled CHEUSI DAWA TV (FID-Q) (see the sidebar) for previous episodes of Fridstyle Friday and much more!


Tunasikitika kuwatangazia kifo cha
Machira  NYITAMBE

Kilichotokea mchana leo huko  MUSOMA-TANZANIA

Mazishi yatafanyika huko Kirongwe, Shirati, katika mkoa wa Mara.


Marehemu ni baba mzazi wa:

Mrs Veronica Dibogo Nyitambe
Mrs Beatrice Nyitambe(Baba Mdogo)
Mr Soni Nyitambe (Baba Mdogo) ,


ambao wote wapo hapa Uingereza.

Msiba upo
14 Rothwell Walk
Caversham
Reading

RG4 5DB

Kwa mawasiliano zaidi tumia simu zifuatazo:
Bernard Chisumo
Mob: (0) 787 612 6862
Home: (0) 118 954 5890 
---------------------------------------------------------------- 

POLENI SANA WAFIWA.SIE TULIMPENDA MAREHEMU LAKINI BWANA ALIMPENDA ZAIDI

22 Jul 2011

Samuel Sitta mwenyewe anayepigwa mkwara na Guninita yupo hoi kwa usingizi.Labda hapo anaota yeye bado Spika

Guninita ‘amvaa’ Sitta
Posted By admin On July 22, 2011 @ 7:59 am In Habari kuu,Mtanzania |

• Adai ni mzigo, anawadanganya na kuwapotosha wananchi
• Asisitiza ni sehemu ya tatizo la mgawo wa umeme
• Asema si mgeni serikalini, ni mchochezi, mnafiki na mfitini
• Aonya anaigawa, anaitumbukiza CCM kwenye shimo
• Asema mambo yakiendelea hicho mwaka 2015 CCM itaambulia patupu

Na Habakuki Urio

MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dar es Salaam, John Guninita amemlaumu Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samwel Sitta akidai ni mnafiki na mchochezi anayetumika kuigawa CCM na kukitumbukiza chama hicho kwenye shimo.

“Sitta ni sehemu ya serikali na si mgeni serikalini. Alikuwapo tangu kipindi cha Mwalimu Nyerere, na pia alikuwa Spika wa Bunge. Kwa nafasi hizi yeye ni sehemu ya tatizo na siyo kuwadanganya wananchi na kuwapotosha kwa kuirushia serikali lawama.

‘Anaudanganya umma. Anataka kujenga umaarufu ambao siyo wa kwake. Kama ni kuharibu waliharibu wote na siyo kusema tatizo ni la serikali.
‘Sitta amekuwa mchawi wa CCM… chama kinajimaliza chenyewe tena kwa kutumia viongozi wa nafasi za juu.,” alisema Guninita.

Guninita alikuwa akizungumza katika mkutano wa hadhara Mbezi na Mbezi kwa Msigani katika jana, katika ziara ya kutekeleza agizo la Mwenyekiti wa CCM, Rais Kikwete la kuleta mageuzi ndani ya chama hicho na ‘kujivua gamba’.

Alisema hali ya siasa ndani ya chama hicho si shwari kutokana na mgawanyiko mkubwa wa baadhi ya viongozi ambao wanazungumza wanavyojisikia bila kujali maslahi na ukweli ndani ya Chama hicho.

“Kilichotufikisha hapa tulipo leo ni unafiki na fitina za viongozi kama Sitta ambao hawaeleweki wanafanya nini ndani ya chama chetu. Ndiyo maana viongozi wanajiuzulu ovyo, kitu ambacho siyo sahihi, chama kinapoteza makada muhimu na kuwaacha watu mizigo na wafitini.

“Namshangaa Waziri Sitta, ana uwezo wa kwenda kwa Rais muda anaojisikia na pia alikuwa na nafasi ya kuyasema mambo yale katika vikao vya chana “party caucus”, na pia kwenye vikao vya Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) lakini anaropoka mambo kama hayo mbele ya umma wa watanzania na kuwapa umaarufu wapinzani.

“Amekosa busara kwa kuwa amekiuka maagizo ya Rais. Tunajua hakutumwa na Rais, bali alikurupuka tu, na bila kujijua anaiponda Ilani ya Uchaguzi ya CCM ambayo ndiyo muongozo wa kutekeleza majukumu yetu.
‘Mawaziri na wabunge wanasema tofauti na Rais anavyosema kuhusu matatizo ya umeme kwa sasa,” alisema Guninita

Alisema kauli mbovu za baadhi ya viongozi ambazo hazina ukweli zinabomoa chama, na kama CCM haitakauwa makini na kuwaonya wapotoshaji hao katika uchaguzi mkuu wa 2015 chama hicho kitaambulia patupu.

“Upinzani wanajipanga vizuri katika kuhakikisha mwaka 2015 wanachukua nchi, na kwa hali hii tulio nayo … kwa kauli za akina Sitta watafanikiwa kwa kuwa chama kitakuwa kimeyumba na kukosa imani kwa wapigakura wake.

“Haya siyo maneno ya Waziri, huyu jamaa ana mambo yake anayotekeleza… haiwezekani Sitta leo kuyasema haya, labda ana hasira za kukosa Uspika wakati yalikuwa makubaliano ya CCM kumuondoa kwa mafanikio ya chama na kutimiza sera ya 50 kwa 50.

‘Nilimsikia akisema kuwa atatembea mikoa yote kulisema hilo, lakini nawahakikishia kuwa hatafika Dar es Salaam labda aje na barua ya Mwenyekiti au Katibu Mkuu wa CCM kuwa wamemruhusu kupotosha jamii. Nasema kuwa hatutakubaliana na uongo wake,” alisisitiza Guninita.

Hivi karibuni, katika mkutano wa hadharani mjini Mbeya, Sitta pamoja na mambo mengine, alikaririwa akishauri serikali iwaombe radhi wananchi kutokana na tatizo la mgawo wa umeme unaoendelea nchini hivi sasa.

Guninita alisema mkutano wa jana ni matunda ya makubaliano ya kujivua gamba kama alivyoagiza Mwenyekiti Kikwete na kuwataka viongozi wote wa CCM kutembelea matawi na mashina katika maeneo yao kuyajua matatizo ya wapiga kura wao na kuimarisha mizizi ya chama ambayo ipo katika mashina na matawi.


 
Who Needs Humans?
As if American workers don’t have it rough enough, with unemployment skyrocketing and jobs moving overseas, now there’s another threat: robots.
by Daniel Lyons, July 18, 2011
Amid all the job losses of the Great Recession, there is one category of worker that the economic disruption has been good for: nonhumans.
From self-service checkout lines at the supermarket to industrial robots armed with saws and taught to carve up animal carcasses in slaughter-houses, these ever-more-intelligent machines are now not just assisting workers but actually kicking them out of their jobs.
Automation isn’t just affecting factory workers, either. Some law firms now use artificial intelligence software to scan and read mountains of legal documents, work that previously was performed by highly paid human lawyers.
“Robots continue to have an impact on blue-collar jobs, and white-collar jobs are under attack by microprocessors,” says Edward Leamer, an economics professor at UCLA’s Anderson School of Management and director of the UCLA Anderson Forecast, a survey of the U.S. and California economies. Leamer says the recession permanently wiped out 2.5 million jobs. U.S. gross domestic product has climbed back to pre-recession levels, meaning we’re producing as much as before, only with 6 percent fewer workers. To be sure, robotics are not the only job killers out there, with outsourcing stealing far more gigs than automation.
Jeff Burnstein, president of the Robotics Industry Association, a trade group in Ann Arbor, Mich., argues that robots actually save U.S. jobs. His logic: companies that embrace automation might use fewer workers, but that’s still better than firing everyone and moving the work overseas.
It’s not that robots are cheaper than humans, though often they are. It’s that they are better. “In some cases the quality requirements are so stringent that even if you wanted to have a human do the job, you couldn’t,” Burnstein says. He cites General Motors, which uses robots to lay a bead of sealant on windshields, because humans can’t do the job as precisely.
Same goes for surgeons, who are using robotic systems to perform an ever-growing list of operations—not because the machines save money but because, thanks to the greater precision of robots, the patients recover in less time and have fewer complications, says Dr. Myriam Curet, chief medical adviser at Intuitive Surgical in Sunnyvale, Calif. The surgery bots don’t replace surgeons—you still need a surgeon to drive the robot. And they’re not cheap. Prices go as high as $2.2 million. Nevertheless, Intuitive sold 400 of them just last year. If you’ve had a prostatectomy recently, chances are a robot was involved.

Surgeons may survive the robot invasion, but others at the hospital might not be so lucky, as iRobot, maker of the Roomba, a robot vacuum cleaner, has been showing off Ava, a three-foot-tall droid on wheels that carries a tablet computer. iRobot reckons Ava could be used as a courier in a hospital. And once you’re home, recovering, Ava could let you talk to your doctor, so there’s no need to send someone to your house. That “mobile telepresence” could be useful at the office. If you’re away on a trip, you can still attend a meeting. Just connect via videoconferencing software, so your face appears on Ava’s screen.

Is any job safe? I was hoping to say “journalist,” but researchers are already developing algorithms that can gather facts and write a news story. Which means that a few years from now, a robot could be writing this column. And who will read it? Well, there might be a lot of us hanging around with lots of free time on our hands.

SOURCE: Newsweek 

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.