4 Nov 2008

KLHN yaweza kuripoti kwa uhakika kabisa kuwa mpango wa kuanzisha uchafuzi wenye mlengo wa kidini na kikabila nchi umeundwa na sasa umefichuliwa. Mpango huo ambao unawahusisha watu mbalimbali wenye majina makubwa umedhihirika kuanzia siku ya Ijumaa iliyopita. Mpango huo ulianza kusukwa wiki chache zilizopita na hatimaye kuanza kutekelezwa siku ya Ijumaa iliyopita. Kwa wanaokumbuka siku ile (ya Ijumaa) kulikuwa na mkutano wa Waislamu kuelezea masuala mbalimbali ya maslahi yao na hasa suala la OIC. Baadhi ya viongozi wa Waislamu toka mikoani walikuwa jijini pia. 

Ilikuwa ni katika nafasi hii timu iliyokuwa imeanza kukusanywa iliweza kuwakutanisha viongozi mbalimbali hao wa Waislamu kwa kuandaa mkakati kamambe ambao kwa madai yao mipango yake inatoka ndani na juu kwenye serikali. Katika kufanya hivyo viongozi kama 9 hivi wa Kiislamu waliweza kupatikana na kukutanishwa katika hoteli ya Regency siku ya Ijumaa. 

Miongoni mwao ni mashehe na viongozi wengine wa kidini; baadhi yao ni pamoja na Shekhe Mazinge, Mwaipopo, Said Liko, Chifu Msokwa, Ustaadh Twaha, Dr. Salehe, Abubakar Bonde, Sheikh Amour Jongo, Rajabu Jazba, na Ustaadh Ramadhani. Waliokuwemo kwenye mkutano huo pia ni pamoja na Albert Marwa (inadaiwa ni mtoto wa kulelewa wa Generali Marwa) pamoja na mtu mmoja aitwaye Mtawa (huyu yasemekana ni mtumishi wa ngazi ya Juu ikulu). Walikuwepo baadhi ya watu wengine ambao wanadaiwa kuwa ni maafisa wa Usalama wa Taifa ambao kutokana na sheria hatuwezi kuwataja majina yao. 

Mpango huo ambao “vijidudu” vya uchunguzi viliweza kuunasa kwa picha na kwa sauti kimsingi una malengo yafuatayo. 

a. Kuwaonesha waislamu kuwa Bw. Reginald Mengi na Freeman Mbowe ndio maadui wakubwa wa maslahi ya Waislamu nchini.
b. Kwamba Mengi na Mbowe wana mkakati wa kuhakikisha kiongozi anayekuja ni kutoka kabila la Wachagga. Katika hili la dhidi ya “Uchagga” wanamkakati walikuwa wana uhakika wa kutobughudhiwa na polisi kwenye mikutano ambayo waliipanga kuifanya hasa wakiamini kuwa IGP Said Mwema yuko upande wao. Hata hivyo mmoja wao aliapa kuwa aliwahi kuambiwa na Dr. Nchimbi kuwa Mwema ni Mchagga (sijui kwa upande wa mama) na hivyo wasitarajie sana.
c. Walioleta mpango huo wamemhusisha kiongozi wa juu serikalini kuwa ndiye aliyewatuma kutekeleza mpango huo hasa kuonesha kuwa vyombo vya IPP vinatumika kueneza Ukristu, kukandamiza Waislamu, na kuinua Wachagga. Hili litaelezwa ili Waislamu waanze kuvisusisa vyombo vya habari vya IPP. 
d. Kuendelea kuwahusisha Mengi na Mbowe katika vifo vya Chacha Wangwe na Gavana Ballali.

Katika kutekeleza mpango huo timu hiyo ilikuwa ijipange na kuandaa bajeti ya kiasi kisichopungua shilingi milioni 100 ambazo zitagawanywa kati yao na kwa wale ambao watakuwa tayari kutekeleza mpango huo. Kiasi ambacho cha awali ambacho kila mmoja alikuwa agawiwe ni kama milioni tatu tatu huko mmoja wa wanamkakati huo akiahidi uwezekano wa kupata fedha zaidi kutoka kwa Bakhresa. Kiasi cha awali kinadaiwa kutolewa na mfanyabiashara Yusuph Manji wa Quality Group.

Siku ya Jumamosi kundi hilo la wanamkakati lilikutana kwenye hoteli ya Golden Tulip kuendelea na mipango yao ambayo ka nzi ka KLHN kalikuwa kanafuatilia kila hatua tena kwa ukaribu kabisa. 

Wakiwa na magari yenye namba za usajili za T267 ABT na T87 ABG wanamkakati wakiongozwa na Mazinge Mwipopo (spelling yaweza isiwe sahihi) na Chifu Msokwa walihamisha kikao chao kingine kutoka Golden Tulip kuelekea Msikiti wa Mtambani ambapo waliamua kubadilisha na kuelekea Msikiti wa kwa Mtoro. Ka nzi kaliweza kunasa habari za kutosha. 

Siku ya Jumapili kikao chao kiliendelea huko Kinondoni mtaa wa Kazina nyumba (censored) ambapo kuanzia saa tisa hadi majira ya Magharibi waliendelea na mipango yao na maazimio yao ikiwemo la kuhakikisha kuwa viongozi watakaoshiriki katika mkakati huo wa kuitisha mikutano mbalimbali mikoani wahakikishe na wao wanapata watu angalau 20 chini yao. 

Kutoka kwenye vikao hivyo iliazimiwa uitishwe mkutano wa waandishi wa habari ili kuweza kufafanua madai yao dhidi ya Mengi na Mbowe na hivyo kuanzisha mchakato huo wa kueneza propaganda hii ya udini na ukabila. Baadhi ya wajumbe walikuwa wameshaondoka siku ya Jumatatu kuelekea mikoani kuanza kazi hiyo na hilo ndilo lililosababisha vyombo vya ITV kurusha hivyo walivyonavyo. 

KLHN imepata nafasi ya kusikiliza masaa ya kutosha ya mazungumzo ya kundi hili na jambo moja ambalo tunaweza kusema kwa uhakika ni kuwa linatia hofu na kuuliza tumefikaje hapa. 

Hata hivyo mpango huo haujaenda vizuri kama ulivyotarajiwa hasa baada ya kutokea mabishano ya kiasi cha fedha huko baadhi ya wajumbe wakiamini kuwa Bw. Albert Marwa amepewa fedha zaidi kuliko alizowapatia wajumbe hao. Wengine wameanza kudai kuwa Bw. Marwa ndiye aliyeinjinia mpango wa wao kunaswa na vyombo vya kielectroniki. 

Jioni ya leo (jumanne) ka nzi ketu kanaruka ruka mikoani kamethibitisha pasipo shaka kuwa baadhi ya simu za wahusika wakuu zimekuwa ‘tapped’ ili kuweza kujua jinsi operesheni hii ilivyoendesha kikamilifu ikihusisha utaalamu na ujasiri wa hali ya juu kuliko uwezo wowote wa TISS kuwanyemelea mafisadi. 

Msimamizi wa Operesheni hii ardhini ambaye alizungumza na KLHN kwa masharti yale yale mliyoyazoea amesema kuwa hawakuwa na mpango wa kuhusisha vyombo vya usalama kwani kwenye suala zima vyombo hivyo baadhi ya wahusika wake wa kuu wamo ndani mpango huu na hivyo njia pekee ilikuwa ni kuwadokeza tu watu kuwa mpango huo upo, unajulikana, na utakapoanza kutekelezwa Watanzania “wasishtuke”. 

Hata hivyo wameahidi kuwa endapo Mwendesha Mashtaka Mkuu ataamua kuunda "Special Tribunal" ya kufuatilia suala hili ili kuona mashtaka yoyote kuletwa au uchunguzi ushirikiano unaweza kutolewa kwa kadiri ya kwamba vyanzo vyote vya habari hii vitabakia kuwa siri na havitalazimishwa kujitaja isipokuwa kuleta ushahidi kama ulivyo (raw evidence). Nje ya hapo amesema kuwa hawana "imani na Polisi wala Usalama wa taifa kwenye suala hili".

KLHN inaendelea kufuatilia kwa karibu mpango huu na kufichua njama yoyote ile ya kifadi yenye lengo la kuleta mgongano wa kidini au kikabila nchini. Baadhi ya habari zitasahihishwa kwa kadiri wingu linavyozidi kusafishika zaidi.



RAMANI YA OBAMA/MCCAIN BY STATE KWA MUJIBU WA UTABIRI WA KARL ROVE
McCain-Obama 11-3-08 FINAL


I HEREBY ENDORSE YOU (WELL,I KNOW NOBODY CARES,AND IT WONT MAKE ANY DIFFERENCE) AND WISH YOU ALL THE BEST!

Nadhani unakumbuka wasiwasi nilioonyesha katika POST HII.Inaelekea suspicion yangu haiko mbali na ukweli.Zaidi,soma habari hii:
Serikali imesema itakuwa tayari kununua mitambo ya Kampuni ya Dowans Tanzania Ltd endapo Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), litaishauri kufanya hivyo. Dowans Tanzania Ltd jana ilitangaza rasmi zabuni ya kuuza mitambo yake ya kuzalisha umeme ikiwa ni miezi mitatu baada ya serikali kukatisha mkataba wake na Tanesco. 

Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja aliiambia HabariLeo jana kuwa kimsingi serikali haitakuwa na tatizo na mitambo hiyo endapo wataalamu wa Tanesco watashauri hivyo. “Tanesco ndiyo wataalamu wetu, tutawauliza wakisema tununue tutanunua, lakini kwa kufuata taratibu na sheria za manunuzi ya mitambo hiyo,” aliongeza Ngeleja. 

Endapo serikali au Tanesco watanunua mitambo hiyo, itasaidia kupunguza uwezekano wa kutokea mgawo wa umeme mara mitambo mingine ikipata hitilafu. Mwezi uliopita, Tanesco ililazimika kutangaza mgawo wa umeme baada ya mashine moja ya Kampuni ya Songas yenye uwezo wa kuzalisha megawati 40 kuharibika. 

Hata hivyo, Meneja Mawasiliano wa Tanesco, Badra Masoud alisema jana kuwa shirika hilo halijaamua kama watanunua au la. Alisema watatoa taarifa uamuzi ukifikiwa. Dowans Tanzania Limited ilirithi mkataba wa kuiuzia umeme wa megawati 120 Tanesco kutoka kwa Kampuni ya Richmond Development LLC ambayo baadaye iligundulika kuwa ni kampuni hewa. 

Serikali ilifikia uamuzi wa kusitisha mkataba huo Agosti mosi mwaka huu baada ya kuridhika kuwa mkataba huo haukuwa halali wala haukuwa na nguvu kisheria. Tangazo lililotolewa jana na kampuni hiyo lilimtaka mtu yeyote, taasisi, kampuni itakayotaka kununua mitambo hiyo ipange bei inayoona inaweza kutoa kuipata mitambo hiyo.


CHANZO: HabariLeo

3 Nov 2008

Obama's grandmother, Madelyn Dunham,RIGHT,and grandfather, Stanley Dunham.CLICK HERE  for more about her death.

Nyumbani kwa Obama kijijini Kogelo,Kenya.

Kwa mujibu wa ripota wa CNN aliyeko kijiji cha Kogelo huko Kenya,ambacho kinahusiana kwa karibu sana na asili ya Barack Obama,kuna kundi la viumbe-hai wanaoombea mgombea wa urais huyo asishinde kesho ili viumbe hao wasalimike.Hao ni ng'ombe ambao wanaandaliwa kwa ajili ya sherehe kubwa pindi Obama atapotangazwa mshindi.Ni dhahiri kwamba asiposhinda,ng'ombe hao nao watasalimika.Who would you  have felt more sorry for?

Wakati ng'ombe hao wakisubiri hatima yao,sangoma mmoja kijijini hapo ametabiri kuwa Obama atashinda uchaguzi huo wa kesho.Of course,sangoma huyo-John Radima-sio pundit wa major TV networks au pollster kutoka Gallup,lakini ameweza kukamata attention ya vyombo vya habari vya kimataifa.

Kwa upande wa grandmother wa Obama,yeye anasema hawezi ku-take things for granted hadi hapo mshindi atapotangazwa,na anafuatilia kwa karibu maendeleo ya mjukuu wake kwenye runinga inayotumia solar power kwa vile hakuna umeme katika makazi yake.Sarah Onyango Obama,wenye miaka 86,anasema kwamba katika soka huwezi kutabiri ushindi mpaka goli lipatikane.Wakati bibi Sarah (pichani chini) akisubiria kwa hamu matokeo ya kesho,upanuzi wa uwanja wa ndege wa Kisumu umewafanya baadhi ya watu kutania kwamba huenda ni maandalizi ya ujio wa Air Force One ikiwa na Obama.



Kizitto Noya, Kilwa Masoko
WAKATI baadhi ya watu wakiamini kuwa serikali ilitumia busara kuhakikisha fedha zilizochotwa kwenye Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA), zinarejeshwa kabla ya wezi kufikishwa mahakamani, katibu mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad haamini kama fedha hizo zimerejeshwa.

Na badala yake waziri huyo kiongozi wa zamani wa Zanzibar anasema madai ya kurejeshwa kwa Sh69 bilioni kati ya Sh133 ni mwendelezo wa usanii wa chama na serikali yake.

Maalim Seif alisema hayo mwishoni wa wiki alipokuwa akihutubia maelfu ya wakazi wa Mkoa wa Lindi kwenye Uwanja wa Kilwa Masoko, baada ya kupokea maandamano ya CUF ya kupinga ufisadi na kushinikiza wezi hao wa fedha za EPA wafikishwe mahakamani.

Alisema hawezi kuamini kwamba mafisadi hao wamerudisha fedha mpaka aone kwamba wamefikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili za kuiba Sh133bilioni.

"Mimi naamini kwamba, hakuna hata mtuhumiwa mmoja wa ufisadi wa EPA aliyerudisha fedha na kauli ya Rais (Jakaya) Kikwete ni mwendelezo wa usanii wa serikali ya CCM kuwalaghai Watanzania ili waamini kuwa kazi imefanyika," alisema.

Alisema yeye kama Watanzania wengine wenye akili timamu, hataamini kwamba kuna fedha iliyorudishwa na mafisadi wa EPA na kwamba atafanya hivyo ikiwa ataona mafisadi hao wanafunguliwa kesi mahakamani.

Kauli ya Maalim Seif ilifuatia maswali ya waandamanaji hao kumtaka aeleze msimamo wa CUF kuhusu ufisadi wa EPA na mazungumzo ya mwafaka baina ya chama chake na CCM.

Alisema CUF hairidhishwi na namna serikali inavyoshughulikia suala la EPA na ndio maana viongozi wake wakuu wanazunguka nchi nzima kufanya maandamano ya amani kupinga ufisadi huo na kuishinikiza serikali iwafikishe mahakamani.

Rais Kikwete alitaka wezi hao warejeshe fedha kabla ya Oktoba 31 na kwamba wale ambao watashindwa kuzirejesha, wafikishwe mahakamani ifikapo Novemba mosi.

Katika hotuba yake ya mwisho wa mwezi aliyoitoa Oktoba 31, Rais Kikwete alisema jumla ya Sh69 bilioni zimesharejeshwa na kwamba, ametoa ruhusa kwa watuhumiwa kufikishwa mahakamani.

Hata hivyo, hadi jana Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), alikuwa bado hajawasimamisha watuhumiwa hao mahakamani.

Kuhusu mwafaka, Maalim Seif alisema CCM ilianza kutumia nguvu ya ulaghai katika suala hilo kwa kujifanya inataka kumaliza mgogoro wa mpasuko wa Zanzibar wakati ikijua kuwa haina nia hiyo.

Alisema: "CUF tumegundua ulaghai huo na sasa tumewaambia kwamba haturudi tena kwenye mikutano ya mwafaka. Tunataka kama wana nia njema na mwafaka, wasaini makubaliano yaliyofikiwa," alisema.

Alisema CUF pia imefunga mjadala na vikao vya mwafaka baina yake na CCM baada ya kuona kuwa wenzao wa CCM wanawarubuni na kuwahadaa.

Kuhusu nguvu ya utajiri wa kifisadi, Maalim Seif alisema CCM inatumia fedha nyingi kuwarubuni wananchi kwa zawadi ili waendelee kuiamini na kuwachagua, fedha ambazo baadaye wanazirudisha kwa wizi wa mali za umma na ufisadi.

"Pia CCM wanatumia ya nguvu dola kuwatisha wananchi na kuwapiga wananchi ili wasiwe huru kuwachagua vingozi wanaowapenda," alisema.

CHANZO: Mwananchi

PENGINE HOFU YA AINA HII INATOKANA NA UKWELI KWAMBA HAO WANAODAIWA KUREJESHA MABILIONI HAYO WAMEENDELEA KUWA ANONYMOUS.IWAPO MAJORITY YA WATOA SADAKA MAKANISANI NA ZAKA MISIKITINI (SUALA AMBALO NI LA HIARI NA SI LA KISHERIA HUJIWEKA WAZI) HOW COME THEN WADAIWA (SUALA LA KISHERIA) WAHIFADHIWE?NI SIMPLE LOGIC:KAMA MDAIWA NI ANONYMOUS,ITAPOELEZWA KUWA AMELIPA DENI NA KUENDELEA KUBAKIA ANYNYMOUS BASI LAZIMA KUTAKUWA NA STRONG SUSPICION KAMA DENI HILO LIMELIPWA KWELI.

MSIMU WA MVUA,BARABARA YA KWENDA KWETU IFAKARA NI MITHILI YA SWIMMING POOL YA MATOPE.SIJUI NA HII NAYO WAWEKEZAJI WATATAKA IBINAFSISHWE.HOFU YANGU WANAWEZA WAKAICHUKUA KISHA WAKAIGEUZA SHAMBA LA MPUNGA,SASA SIJUI AKINA SIE TUTAENDA HUKO KWA UNGO...

Kwa jinsi baadhi ya wawekezaji wetu huko nyumbani walivyo wasanii (inasemekana wengi wao huja na empty briefs case na vi-credit cards vyenye dola chache tu lakini huondoka na mamilioni ya dola) si ajabu mpango huu wa kubinafsisha baadhi ya barabara za jiji la Dar unaweza kutufikisha mahala tukakuta daraja la Salender limevunjwa na kugeuzwa kibangaluu cha mwekezaji flani!Sijui njia ya mkato itakuwa baharini au vipi!Nina wasiwasi zaidi na eneo la Victoria kwani kutokana na majimaji ya eneo lile si ajabu mwekezaji akaamua kufunga barabara na kuanzisha shamba la maua.Sounds like a joke,doesnt it?Lakini ukisoma habari hii hapa chini unaweza kupata picha kama hiyo inayonijia mie

Dar es Salaam city authority`s $3bn transport crisis rescue plan, which will involve private individuals funding the multibillion-project, has elicited strong resentment from the public. 

A cross-section of motorists and city residents interviewed on Friday said they were completely opposed to the idea terming it as misplaced. Any attempt to carry on with the plan would only show how things have gone awry for the government.

``No, it can`t be! It can�t just happen! That would be completely outrageous! It will be like selling off this country,`` a visibly surprised and thoroughly agitated Rajabu Hassan Mambo, a taxi driver at Mwenge in Dar es Salaam, said.

He was reacting to the recent mooted plan, which aims to revamp the city`s road transport network through private funding that will see individuals own public utility roads.

Mambo likened the idea to giving out one`s plot to a private developer, and then upon assuming residence on the same plot, you go on to pay rent for the rest of your life.

Overwhelmed by ceaseless traffic snarl-ups on most roads heading to, and from the city centre, city authorities have embarked on an expensive and overly ambitious Dar es Salaam Transport Policy and System Development Master Plan to remedy the situation by 2030. Under the arrangement, private individuals are invited to invest in the reconstruction of sections of some roads and widening of the main highways within the city.

According to the Dar es Salaam city mayor Adam Kimbisa, any prospective private investor will be apportioned a section of the road to finance its refurbishment, and then collect toll from motorists to recover expenses incurred.

Mayor Kimbisa justified the plan, stating that it has successfully been carried out in Malaysia`s capital city, Kuala Lumpur.

Several interviewed by The Guardian on Sunday said they were disappointed with the country`s leadership.

Jankar Mbungo for example faulted the government for remaining out of touch with real issues affecting Tanzanians.

``We, ordinary citizens, are burdened with taxes already. Prices of commodities are all time high, and instead of the government making policies that will solve the country`s problems it`s making life more difficult for us.`` Mr Mbungo stated.
SOURCE: Sunday Observer


(MY APOLOGIES FOR THE GRAPHIC IMAGE BUT I HOPE THIS SENDS A STRONG MESSAGE TO THOSE WHO WANT TO DRAG OUR COUNTRY INTO THIS SORT OF CRUELTY)
Mogadishu, Somalia - A 13-year-old girl who said she had been raped was stoned to death in Somalia after being accused of adultery by Islamic militants, a human-rights group said.
Dozens of men stoned Aisha Ibrahim Duhulow to death Oct. 27 in a stadium packed with 1,000 spectators in the southern port city of Kismayo, Amnesty International and Somali media reported, citing witnesses. The Islamic militia in charge of Kismayo had accused her of adultery after she reported that three men had raped her, the rights group said.

Initial local media reports said Duhulow was 23, but her father told Amnesty International she was 13. Some of the Somali journalists who first reported the killing later told Amnesty International that they had reported she was 23 based upon her physical appearance.

Calls to Somali government officials and the local administration in Kismayo rang unanswered Saturday.

"This child suffered a horrendous death at the behest of the armed opposition groups who currently control Kismayo," David Copeman, Amnesty International's Somalia campaigner, said in a statement Friday.

Somalia is among the world's most violent and impoverished countries. The nation of some 8 million people has not had a functioning government since warlords overthrew a dictator in 1991 then turned on each other.

A quarter of Somali children die before age 5; nearly every public institution has collapsed. Fighting is a daily occurrence, with violent deaths reported nearly every day.

SOURCE:AP

Mitambo ya Richmond ikiwasili kwa mbwembwe.Kampuni hiyo ya kitapeli imerithiwa na Dowans.Picha kwa hisani ya MICHUZI

Kampuni ya Dowans Tanzania Ltd imetangaza rasmi zabuni ya kuuza mitambo yake ya kuzalisha umeme ikiwa ni miezi mitatu baada ya serikali kusitisha mkataba wake na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco). 

Dowans Tanzania Limited ilirithi mkataba wa kuiuzia umeme wa megawati 120 Tanesco kutoka kwa Kampuni ya Richmond Development LLC ambayo baadaye iligundulika kuwa ni kampuni hewa. Serikali ilifikia uamuzi wa kusitisha mkataba huo Agosti mosi mwaka huu baada ya kuridhika kuwa mkataba huo haukuwa halali wala haukuwa na nguvu kisheria. 

Serikali pia ilisema ilibaini iwapo mkataba husika ungekuwa halali, uhamishaji wa mkataba kutoka RDVCO badala ya Richmond Development LLC kwenda Dowans Tanzania Ltd, haukufuata msingi wa mkataba.“Hivyo uhamishaji haukuwa halali na ifahamike kwamba mkataba ulikuwa baina ya Richmond Development Company LLC na Tanesco na siyo na REDVCO na Tanesco,” alisema. 

Tangazo ambalo limetolewa na kampuni hiyo leo kwa vyombo vya habari, limesema watu au kampuni makini ambazo zitakuwa na nia ya kununua mitambo hiyo wanakaribishwa kuinunua. Kutolewa kwa tangazo hilo la kuuza mitambo yake, huenda ikawa ni ishara ya kampuni hiyo kufungasha virago baada ya kimya kingi tangu mkataba huo usitishwe. 

Baada ya kusitishwa kwa mkataba huo, Tanesco imekuwa ikitumia pamoja na vyanzo vingine vya umeme, mitambo yake ya megawati 100 iliyojengwa na Kampuni ya Watsilla ya Finland ili kufidia upungufu uliotokana na kuondoka Dowans. Tanesco pia imekuwa ikinunua umeme kutoka kwa kampuni za Songas na IPTL. 

Siku chache baada ya kusitishwa kwa mkataba huo, mmoja wa maofisa wa Dowans aliiambia HabariLeo kuwa walikuwa na njia nyingi za kufanya na mitambo hiyo ikiwa kuikodisha au kuiuza kwa watu wengine. “Kukatishwa kwa mkataba haina maana hatuwezi endelea na kazi, tutatafuta wateja wengine kama kampuni za migodi na kuwauzia umeme au tunaweza kukodisha mitambo yenyewe,” alisema ofisa huyo. 

Kwa mujibu wa tangazo hilo, mitambo hiyo ina mashine tano za uzalishaji wa umeme ambazo mnunuzi atazinunua kwa bei ya hali yake ilivyo kwa wakati wa kununua. “Vifaa vyote ikiwa pamoja na vipuri na vifaa vingine vya pembeni vipo na vitauzwa kwa pamoja kama bidhaa moja,” lilisema tangazo hilo. 

Mkataba kati ya Tanesco na kampuni ya Richmond Development LLC umekuwa ni mmoja wa mikataba ambayo ilivuta hisia za watu wengi kitu ambacho kilisababisha kuundwa kwa Kamati iliyokuwa chini ya uenyekiti wa Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe (CCM), ambako kutokana na ripoti hiyo, aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa alijiuzulu. 

Wengine waliojiuzulu ni aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi na Ibrahim Msabaha ambaye alikuwa Waziri wa Wizara hiyo na kabla ya kuhamishiwa Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Kutokana na mapendekezo ya ripoti hiyo, serikali iliahidi kuyafanyia kazi mapendekezo ya ripoti hiyo, ambapo moja ya hatua iliyochukuliwa ni kusitisha mkataba na Dowans.

 CHANZO : HabariLeo

I SMELL SOMETHING FISHY HERE.HII TENDA YA KUTANGAZWA KWA PRESS RELEASE INAZIDISHA SUSPICION YANGU.KWANINI ISIWE TANGAZO LA ZABUNI GAZETINI BADALA YA KU-SEEK ATTENTION KWENYE MAGAZETI,AMBAYO MENGI YAO HUWA HAYANA MUDA WA KU-READ BETWEEN LINES YANAPOPATA STORIES?I SUSPECT KUNA DILI INATAKA KUCHEZWA HAPA.POTENTIAL BUYER WA MITAMBO HIYO ATAKUWA TANESCO (CLICK HAPA NA HAPA KUPATA HINT). ITANUNULIWA KWA UTARATIBU UNAOONEKANA TRANSPARENT (HIVI TRANSPARENCY INA UMUHIMUWOWOTE  KATIKA KUNUNUA BIDHAA BOMU?) KISHA MITAMBO HIYO (AMBAYO "WAMBEA" WANADAI NI INJINI MBOVU ZA NDEGE) ITAISHIA "KUBUMA".DOWANS WAKATI HUO ISHAKUWA KAMPUNI MFU,KAMA MZAZI WAKE RICHMOND.LET'S WAIT AND SEE!

2 Nov 2008

Lewis Hamiliton made history,a few minutes ago,after becoming the first Black and the youngest  winner of Formula One Championship.And another history could be written day after tomorrow if Obama wins in the U.S. Presidential Election.Where is James Watson?

Pakistani police break up marriage between 4-year-old girl and 7-year-old boy

Mohammad Ismil (C) holds his 7-year old son Mohammad Waseem (R) and his son's 4-year old "bride" Nisha (L) at a police station in Karachi, Pakistan

Pakistani police raided a child marriage ceremony in the city of Karachi and arrested a cleric who was presiding over the wedding of a 4-year-old girl and a 7-year-old boy.

Pakistani law says people must be 18 to marry but some Islamic laws allow girls to marry after puberty.

Yet despite the laws, young girls are often given away in marriage to settle disputes or pay off debts.

Police said they raided a house on Thursday evening following complaints from residents, including a former district government official, who said the girl was being married off by her father for about 500,000 rupees (£3,750).

The official told Reuters: 'We had noticed some gatherings at this house for a couple of days.

'Last night I went there and saw that the little girl was actually getting married. So we called the police.'

Some other residents said the marriage was taking place to resolve a long-standing family dispute. Police said they had arrested the boy's father but the girl's father had run away.

SOURCE: Dailymail



Comedians flani wamemuingiza mkenge Gavana Sarah Palin kumuaminisha kuwa anaongea na Rais wa Ufaransa Nicholas Sarkozy.Sikiliza kichekesho hicho kwa ku-click link ifuatayo hapa chini:


Talking of Gov Palin,kituko kingine ni kwamba katika mkutano wake wa kampeni huko Polk City,Florida jina la mgombea mwenza wake,John McCain,was surprisingly missing kama inavyoonekana katika picha ifuatayo hapo chini.Au ndio ameshaanza kampeni za 2012?


1 Nov 2008

Picha kwa hisani ya SPOTI NA STAREHE

Ubabaishaji unakwamisha sana maendeleo ya taifa letu.Lakini hapa nataka nizungumzie ubabaishaji kwenye uongozi na uendeshaji wa vilabu vya Simba na Yanga.Hebu soma kwanza hapa chini kabla hatujaendelea na mada hii ya kupotezea muda.
MWENYEKITI wa klabu ya Simba Hassan Dalali amemteua Mkurugenzi wa Kampuni ya Aurora Security, Ally Suleiman kuwa mshauri wake atakayesaidia kumshauri kuhusiana na mambo yote yanayohusu masuala ya uongozi wa Simba. 

Akizungumza Dar es Salaam jana, Dalali alisema ameamua kuwa na mshauri ili aweze kuiendesha klabu yake kwa umakini na kufuata mwongozo ambao utaisadia klabu hiyo. 

Dalali alisema Suleiman amekuwa mtu wa karibu, ambaye ametoa mchango mkubwa ndani na nje ya klabu, hivyo ameona ni muhimu na kuwa uteuzi huo ni kujenga Simba yenye umoja na mshikamano.
Alisema klabu yake ipo katika mikakati ya kuhakikisha Simba inakuwa klabu kubwa, huku ikiimarisha timu yake na kuwa mfano wa kuigwa. 

"Uteuzi wa mshauri wangu umezingatia vigezo vingi ikiwemo ukaribu wake katika mambo ya msingi yanayoihusu klabu yetu," alisema Dalali.

Akizungumzia uteuzi huo, Suleiman alisema amefurahi kupata wadhifa huo na kuahidi kuisaidia klabu hiyo kwa hali na mali lengo likiwa ni kujenga Simba imara
CHANZO:Majira
Baada ya kufungwa na Yanga ndio Dalali anakumbuka umuhimu wa kuwa na mshauri!?Kwa tafsiri nyingine ni kwamba kwa muda wote tangu apate uenyekiti wa Simba m-babaishaji huyu amekuwa akiongoza kwa kubahatisha.Ndio!Kama sio hivyo,mshauri wa nini muda huu? Yaani ni ubabaishaji juu ya ubabaishaji.

Mimi ni mpenzi wa Simba.Zamani Simba ikifungwa basi ni majonzi makubwa.Katika familia yetu,watoto wote wanane tunaipenda Simba.Marehemu Mama (Mungu Amlaze Mahali Pema Peponi) alikuwa mpenzi wa Pan Africa,kwa sababu mpwae,Gordian Mapango,alikuwa mchezaji wa timu hiyo.Baba aliamua kuisapoti Yanga,sio kwa vile anaipenda bali kuleta "usawa" ndani ya familia.

Kwa miaka kadhaa sasa,nimebaki kuwa mpenzi-jina tu,it doesnt really make any difference Simba ikishinda au ikifungwa.Sababu kuu ya kupoteza mapenzi kwa Simba,na soka ya Tanzania kwa ujumla,ni ubabaishaji uliopita kiasi wa viongozi wa klabu hiyo kongwe.Ubabaishaji huo umepelekea timu hiyo kukimbiwa na wafadhili kibao na kupoteza udhamini mbalimbali.Nani mwenye akili timamu atawekeza kwenye biashara kichaa?Ukiona mtu anapanda mpunga jangwani basi hicho sio kilimo bali tambiko.Ndo maana nashawishika kuamini kwamba uwepo wa Manji hapo Yanga unaweza kuwa ni "zaidi ya mambo ya soka".

Nirudi kwenye title ya post hii.Nilitegemea Simba ingefungwa na Yanga.Na nilitegemea kipigo kikubwa zaidi ya hilo bao moja.Kama Toto Africa waliweza kutufunga bao 4-1,tungetegemea nini katika mechi na Yanga?Anyway,kipigo ni kipigo.Mategemeo yangu ya kipigo yametimia,japo kwa idadi tofauti na niliyokuwa naitarajia.Kingine nilichadhani kingeandamana na kipigo hicho ni kuutimua uongozi mzima wa Simba.Hilo halijatokea lakini naamini viongozi hao wamekalia kuti kavu.By the way,uongozi wa Simba na Yanga ni zaidi ya kukalia kuti kavu;ni sawa na kibonge cha mtu kuning'inia kwenye utando wa buibui.Mtu mwenye mtizamo makini hawezi kutamani kuongoza timu hizi za kibabaishaji,ambazo lugha wanayoelewa "wanachama" ni ushindi tu.

Of course,timu inatakiwa ishinde kila mechi.Lakini timu itashinda vipi ikiwa haina vyanzo vya mapato zaidi ya kutembeza bakuli kama ombaomba?Hao wachezaji wanakula nini kabla ya kujituma uwanjani?Au ni timu za kiroho ambapo Neno la Mungu linashinda mahitaji ya fedha na vifaa?Kwanini wachezaji wasipokee rushwa iwapo viongozi wanawaibia mishahara yao kiduchu inayopatikana kwa migomo?Wanachama wababaishaji wa klabu hizi wanajua kupiga majungu tu lakini hawana mchango wowote kwa ustawi wa klabu hizi.Ndio maana akiondoka mfadhili mmoja timu inakuwa hohehahe.Na ndio maana Manji amekuwa mungu-mtu hapo Yanga (na mwenyekiti Madega amegeuka kuwa msemaji wa familia ya mfadhili kuhusu ugonjwa wa mfadhili huyo!)

Je kuna ufumbuzi wa tatizo hili la ubabaishaji wa viongozi na wanachama wa Simba na/au Yanga?Kwa mtizamo wangu nadhani ufumbuzi upo lakini unahitaji udikteta wa aina flani.Unajua kuna udikteta kwa ajili ya watu na udikteta dhidi ya watu.Udikteta kwa ajili ya watu ni kama ule wa Sokoine:kwa wahujumu wa uchumi Sokoine alikuwa dikteta,lakini kwa wananchi wengi kiongozi huyo alikuwa ni shujaa na mkombozi.Sihitaji kuelezea dikteta dhidi ya watu ni wa aina gani,lakini anaweza kuwa hata anayethamini haki za binadamu za mafisadi wachache badala ya walalahoi walio wengi.Je udikteta kwa ajili ya watu unawezaje kuokoa vilabu vyetu na soka la Tanzania kwa ujumla?Ni kwa serikali kutumia sheria kali katika kuleta mageuzi ya kudumu katika vilabu vya soka.Najua kuna ishu za watu kwenda mahakamani kupinga maamuzi flani,lakini ukweli unabaki kwamba sheria zikiandaliwa na kusimamiwa vizuri basi wahuni wanaokimbilia mahakamani watafyata mkia.Njia nyepesi ya kuvibana vilabu hivyo ni kutunga sheria inayovitaka kujisajili upya,kwa mfano.Pia sheria hiyo inaweza kutamka bayana aina ya viongozi,namna ya uendeshaji wa vilabu unavyopaswa kuwa na hata aina za wanachama.FIFA itatufungia kwa vile serikali imeingilia mambo ya soka?Why care!kwani sasa hatujafungiwa na tumeendelea kuwa kichekesho kila mwaka?Bora tu tufungiwe ili tuweze kujipanga vyema kuliko kuendeleza ubabaishaji huu.Au msomaji unasemaje?


DEARBORN HEIGHTS/DEARBORN - Illinois Sen. Barack Obama will win Tuesday's election and become the next president of the United States, according to a recent poll conducted by Zogby International, an American market research and opinion-polling firm.

Their Reuters/C-SPAN/-Zogby Poll out Friday morning indicates the support for both candidates had solidified and remained unchanged from the previous several days. Obama was at 50.1 percent among likely voters, while McCain was at 43 percent. That put Obama outside the margin of error five days before the actual vote.

"With less than a week to go, today's numbers are not a good development for McCain," said John Zogby, founder of Zogby International. "There is no momentum for him, and the clock is starting to fun short."

Out of 1, 202 likely voters polled Oct. 27-29, Obama increased his lead among independent voters to 19 points — up from 16 points on Oct. 29 — while McCain's support among his base of Republican voters waned just slightly, dropping two points to 85 percent.

Obama's support among Democratic Party voters remained steady at 84 percent, the poll showed.

According to the Zogby International Web site, www.zogby.com, the poll sampled 1,202 likely voters by phone with approximately 33 questions asked. The margin of error is plus or minus 2.9 percentage points. Interviews were conducted using live telephone interviewers in Zogby's in-house call center in Upstate New York.

A poll released Thursday shows Obama leads by five points among men, 49 percent to 44 percent for McCain. Among women, the Democratic candidate leads by a 10-point margin, 52 percent to 42 percent.

Among liberals, Obama wins 86 percent support, while McCain wins 75 percent of conservatives. Among moderates, Obama wins 65 percent support, compared to 26 percent for McCain.

"But six days, including Election Day, is an eternity and McCain cannot be counted out yet, though he may need a wing and a prayer," Zogby said Thursday.

According to a Zogby poll conducted Oct. 10-15, Arab American voters are expected to have a significant impact on Tuesday's election. The poll sampled 504 likely voters with approximately 41 questions asked. The margin of error is plus or minus 4.5 percentage points.

The poll finds about one-third of Arab Americans live in battleground states — Michigan, Virginia, Ohio, Florida and Pennsylvania. In Michigan, Arab Americans comprise about 5 percent of the state's total population, compared to 1.5 percent in Pennsylvania.

According to the poll, Obama leads McCain by a three-to-one margin among Arab American voters, in both the two-way match-up and the four-way match-ups. This represents the greatest support ever recorded for a Presidential candidate among Arab American voters, the poll finds.

Vice presidential candidate Joe Biden also out-performs Republican candidate Sarah Palin among all groups, including Arab Americans, with Biden's margin being 58/31 and Palin's 58/39.

When asked to name the two most important issued in the election, jobs and the economy were the most frequently mentioned, according to the poll. The second and third most important issues are the Iraq war and health care.

A recent statement issued by Michigan Secretary of State Terri Lynn Land said than an estimated 5 million voters, or approximately 70 percent of registered voters, will case ballots on the Nov. 4 election.

SOURCE: Press&Guide
"Voter enthusiasm is at an all-time high and because of that I expect an unprecedented number of voters to attend the polls on Election Day," Land said. "I encourage you to take time to educate yourself on the candidate and issues, and the cast your ballot on Election Day."


By Dee Dee Myers

Despite George W. Bush's improbable path to the presidency—he was, after all, elected not by the people but by the Supreme Court—neither he nor his chief strategist, Karl Rove, felt compelled to moderate their agendas. In fact, Rove went public with his grand ambition early and often: to use Bush's presidency to build a permanent Republican majority, not just in Washington but across the country. Give Rove credit for always thinking big.

Eight years later, however, the verdict is in. And Rove's plan has been a spectacular failure.

George W. Bush is the most unpopular president in modern times. Barely two in ten voters approve of the job he's done, and the other eight wonder how anyone could still find things about his administration to like. In better days, Bush was in high demand, as candidates across the country sought his endorsement, his energetic presence at their events, and his prodigious ability to raise money. How times have changed. According to NBC News, Bush hasn't made a single public campaign appearance with a G.O.P. candidate this cycle. Not one.

When Bush was elected, Republicans controlled both the House and the Senate. And after the events of September 11, their majorities grew. But as voters soured on the war in Iraq, the administration's endless ethical entanglements, and its abominable response to Hurricane Katrina, they gave Democrats back control of both chambers. And this year, Democrats are poised to make even bigger gains: somewhere north of 20 seats in the House and enough seats in the Senate to put them tantalizingly close to a filibuster-proof majority.

And what about the electorate more broadly? To begin with, Republican registration has fallen, and Democratic registration has grown, particularly among new voters, the ones forming impressions of the political parties that can last a lifetime. First-time voters, who are mostly between 18 and 21 years old—as well as those who haven't voted in recent years—prefer Barack Obama to John McCain by huge margins: 69 to 27 percent, according to one recent poll. These same voters prefer a Democratic controlled Congress by 66 to 31 percent.

So even if Barack Obama doesn't win—an unlikely outcome given the dynamics of this race—the Republican party will be in shreds: divided, demoralized, and long, long way from Karl Rove's erstwhile dream of a permanent governing majority.

SOURCE: Vanity Fair


Wananchi wahoji Rais ametumia sheria gani kusamehe wahalifu?
Na Daniel Mjema,Dodoma
BAADHI ya watu nchini wakiwamo, wanasiasa na wabunge wa Bunge la Jamhuri wamepokea kwa hisia tofauti hotuba ya Rais Jakaya Kikwete kuhusu suala la mafisadi wa fedha zaAkaunti ya Madeni ya nje katika Benki Kuu ya Tanzania ( EPA), huku baadhi wakisema hotuba hiyo imejaa porojo na kuongeza utata zaidi ambao umewakatisha tamaa Watanzania.

Hata hivyo, baadhi ya wabunge waliunga mkono uamuzi huo wa Rais kuwasamehe wale waliorejesha fedha za EPA ingawa pia wapo wengine waliokataa kutoa maoni yao wakisema bado wanatafakari hotuba hiyo.

Mbunge wa Karatu, Dk Wilbroad Slaa(Chadema) ambaye pia ni Naibu Msemaji wa Kambi ya Upinzani bungeni, aliliambia Mwananchi Jumapili jana kuwa hotuba yake imethibitisha hana muda wa kusoma alama za nyakati na kwamba hata wasaidizi wake hawamsaidii.

Dk Slaa alisema matarajio ya watanzania walio wengi ni kwamba Rais angetaja majina ya watu au makampuni yaliyorejesha Sh69 Bilioni na kutoa ufafanuzi ya fedha zilizorejeshwa ni fedha taslimu au zinajumuisha nyumba na magari ya watuhumiwa ambao serikali ilitangaza kuyataifisha.

“Rais amefanya kosa lile lile alilolifanya alipohutubia Bunge kwa sababu tunataka kufahamu ni akina nani hawa waliorudisha fedha hiyo ni moja lakini pili hizi Bilioni 69 zilizorudishwa ni fedha taslimu au zinajumuisha mali wanazodai wamezitaifisha,”alihoji Dk.Slaa.

Dk Slaa aliongeza kusema; "Angetuambia hizo nyumba na magari ziko wapi na zina thamani gani kwa kweli Rais amezidisha utata zaidi kuliko kutoa majibu…binafsi naiona hotuba ya jana kama porojo za alinacha”.

Mbunge huyo alimtaka Rais Kikwete amwambie ni kifungu gani cha sheria kinachomruhusu kumsamehe mtuhumiwa wa kosa la jinai ambaye hajahukumiwa na mahakama akisema kinachoonekana Rais ana safiri zaidi nje ya nchi na wala hana washauri wazuri wa kumsaidia.

Alisema kama Rais angekuwa na wasaidizi makini asingeiongezea muda kamati ya mwanasheria mkuu wa Serikali Johnson Mwanyika kuendelea kutafuna fedha za walipa kodi kuchunguza makampuni tisa kwa kuwa makampuni hayo yalishatangaza hakuna mtu wanayemdai Tanzania.

Hata hivyo Mbunge wa Nungwi, Ame Pandu Ame (CCM) alikataa kusema lolote kwa sasa akisema hilo ni jambo zito linalohitaji tafakuri ya hali ya juu huku Mbunge wa Same Mashariki,Anna Kilango Malecela(CCM) naye akisema kwa sasa bado anaitafakari hotuba hiyo ya Rais.

Mbunge wa Kigoma Kaskazini,Zitto Kabwe(CHADEMA),alisema kitendo cha Rais kuwasamehe watuhumiwa wa EPA waliorejesha fedha kimewagawa watanzania kwamba watuhumiwa wakubwa wanatakiwa kurudisha walichokiiba bali wanyonge ndio wanatakiwa kufungwa.

“Watanzania wanachotaka ni kwamba warudishe wasirudishe fedha lazima washitakiwe lakini hiki alichokifanya Rais ni kibaya sana kwamba wezi wakubwa wanatakiwa kurudisha fedha lakini hawa wadogo wanafungwa magerezani…hii ni mbaya sana”alisema Kabwe.

Kabwe alisema msamaha wa Rais una taratibu zake na huwa unamhusu mtu ambaye tayari amehukumiwa na mahakama lakini alichokifanya Rais si sahihi na kusema angalau basi kamati ya Bunge ya mambo ya sheria ingearifiwa ili ijadili na kuridhia kuwasamehe watuhumiwa hao.

“Tusubiri DPP atasema nini lakini tangu mwanzo tulimshauri Rais kwamba wale wa Bilioni 90 wafikishwe mahakamani na wale wa Bilioni 42 uchunguzi wao uendelee na jana(juzi) kwa mara ya kwanza Rais ametofautisha makundi hayo mawili”alisema Kabwe.

Baadhi ya wabunge ambao hawakupenda majina yao yatajwe walipinga hatua ya Rais kuwasamehe waliorejesha fedha hizo wakisema uamuzi huo unakwenda kinyume na misingi ya utawala wa sheria ambao unatambua kuwepo kwa Mahakama katika kushughulikia wahalifu.

"Hata kama wamerejesha fedha hawa ni wezi wamegushi nyaraka wanasamehewaje? kama ni hivyo tuwaachie pia watoto wetu, ndugu zetu na wajomba zetu wanaoozea magerezani kwa kuiba kuku ni jambo la ajabu na limeleta sura mbaya sana kwa jamii,'' alidai Mbunge mmoja.

Mbunge mwingine wa viti maalumu kutoka CCM alisema alitegemea Rais angezingatia maneno ya Spika wa Bunge,Samwel Sitta aliyemtaka Rais kutowaonea huruma watuhumiwa wa EPA kwa kisingizio cha haki za Binadamu kwa sababu hicho ndicho wananchi wanachokitaka.

''Kama utakumbuka alipokuja hapa Bungeni Spika alimweleza waziwazi suala hili na maneno ya Spika ndio ambayo yaliwapa faraja sana wananchi kuliko yale ya Rais ambaye alionekana kama anaogopa kitu fulani kuhusu hawa mafisadi,” alidai Mbunge huyo.

Mbunge wa Mkwajuni, Mzee Ngwali Zubeir(CCM) alisema binafsi haoni tatizo kwa Rais kuwasamehe watuhumiwa hao kwani walipewa muda wa kujirekebisha na kufanya hivyo lakini akasema anaunga mkono kufikishwa mahakamani kwa wale ambao hawajarejesha fedha hizo.

“Nafahamu wapo wananchi ambao hawajafurahishwa na uamuzi huu wa Rais lakini wapo pia wanaona ni uamuzi wa busara nafikiri ni sahihi kuwasamehe wale waliorejesha kwa sababu walipewa muda wa kujisahihisha na wakafanya hivyo”alisema Mbunge huyo.

Masanja James mmoja kati ya wanafunzi wa chuo kikiu cha SAUT Mwanza amesema kuwa katika hotuba ya Rais amejitahidi katika kuzungumzia matatizo mengine kama yale ya mauji ya Albino, na OIC.

Alisema kuwa kulingana na utata wa sula la OIC hoja ni kuanzisha mjadala kama ambavyo rais ameeleza lakini kueleza masikitiko yake kuhusiana na suala la EPA ambalo alisema kuwa Rais bado ameonekana kuwa hatambui anachokijibu kwa wananchi.

''Amezungumza vizuri sana haya masuala mengine, lakini katika suala la EPA hapa hakutoa maelezo ya kuridhisha, kama Rais wa nchi anaweza kueleza kuwa amekuwa akipokea taarifa vipande vipande?

Kubwa ni kwamba, bado Rais hajaeleza wezi hao watashughulikiwa vipi na serikali yake kwa wizi huo, kwa mtazamo wangu ameonesha kuidhinisha wizi kwa waliolipa kurejesha kwa vile hajatwambia hatua ambayo watachukuliwa,” alieleza James.

Alisema kwa kauli ya rais katika hotuba yake wizi wa fedha za umma umeruhusiwa kwa wale wote wataofanikiwa kuiba, isipokuwa kwa wale ambao watashindwa kurejesha wao hatua zitachukuliwa.

James alieleza kuwa hali hiyo itakuza wizi katika sekta mbalimbali serikali kwa vile inaacha somo kuwa kila anayeiba vizuri akirudisha hakuna kuchukulia hatua kama ilivyo kwa wizi wa mabilioni ya EPA.

Mwajabu Bakari alisema kuwa katika hotuba ya Rais Kikwete ameghazabishwa na kuona jinsi serikali isivyo sikiliza kilio cha wananchi kutaka walioiba na kurejesha fedha za EPA wachukuliwe hatua na kusema kuwa jambo hili litalifikisha taifa mahari pabaya.

?Naye Salim Said anaripoti kuwa Mwenyekiti wa taifa wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba alisema, amesikitishwa na kusononeshwa sana na hotuba ya Rais Jakaya kwa kuamua kufanya kazi isiyomuhusu.

''Nimesononeshwa, nimesikitishwa na nimekasirishwa sana na hotuba ya Rais, kwa kuwasemehe watu waliofanya jinai kabla ya mahakama kufanya kazi yake. Rais anaweza kusamehe, lakini hadi mahakama ifanye kazi yake. Huu ni ufunjifu wa Sheria za nchi,'' alisema Prof. Lipumba.

Alifafanua kuwa, utawala wa Kikwete ni utawala mbovu uliokosa muelekeo na unaongeza ufisadi ndani ya nchi, kwa kukosa nguvu ya kuwashughulikia mafisadi wa EPA.

''Hatuna utawala kabisa, tumekosa uongozi nchini. Hizi fedha zilituimika katika kumuingiza madarakani na ndio mana leo anakosa nguvu ya kuwashughulikia wezi hao,'' alilalamika Profesa Lipumba.

Profesa Lipumba aliwataka Watanzania kujipanga na kujiandaa kwa ajili ya kuing’oa serikali ya CCM madarakani, katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 kabla nchi haijayoyoma.

Naye Katibu Mkuu wa Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislaam Tanzania, sheikh Ramadhan Sanze alisema, ni mfano mbaya sana kwa mamlaka ya kirais nchini kufagilia sheria kutumikia siasa jambo ambalo ni hatari kwa mamlaka nyengine za chini.

Alisema, inaonekana kuna siri nzito katika suala la wizi wa fedha za EPA kwa kuwa kuchukua fedha kinyume na taratibu ni kosa la jinai lakini rais amelichukulia kama la madai.

''Tatizo si kurudisha fedha, hapa tunataka kukomesha huu mchezo mchafu, kwa sababu kuchukua fedha visivyo ni kosa la jinai. Kwa mpango huu wa rais Kikwete kufagilia Sheria kutumikia siasa, basi watu wataendelea kukwepa sheria kwa mlango wa siasa kila siku,'' alitahadhariasha Sheikh Sanze.

Sheikh Sanze alifafanua kwamba, pamoja na juhudi kubwa anazofanya rais Kikwete katika suala la EPA, bado maslahi ya kisheria na utawala bora yamekiukwa.

''Jambo hili litawafanya Watanzania waanze kuhoji ni jinsi gani nguvu na mamlaka ya rais yananavyoshindwa kufanya kazi ya kuwashughulikia mafisadi. Jambo ambalo linatutia wasiwasi mkubwa juu ya mamlaka na nguvu hiyo,'' alisema Sheikh Sanze.

CHANZO: Mwananchi


This dude is angy because T.I. is calling for people to give tips to Crimestoppers.They call it snitching.So,for this fool,he would rather see his brothers and sistas die rather than help the police to make the street safer!Barack Obama could well win come November 4,but I doubt if his victory as the first Black President of US could help change this crazy mentality horbered by majority of these gangtaz.

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.