11 May 2009


AH,HAPA SIJUI NISEMEJE.HEBU SOMA KWANZA HABARI KAMILI HAPA CHINI KISHA TUJADILI.

Kompyuta za IGP, Mkemia Mkuu zaibwa
• Ni katika mazingira ya kutatanisha

na Deogratius Temba

WAKATI kesi ya watuhumiwa 11, walioiba kompyuta katika ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP), ikiendelea imebainika Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP), Said Mwema, naye ameibiwa kompyuta ndogo (Laptop).

Wiki mbili baada ya tukio la wizi wa kompyuta za IGP Mwema, Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali, nayo iliibiwa kompyuta ya mezani ambayo inasadikika ilikuwa na kumbukumbu nyingi ambazo hazijabainishwa zinahusiana na mambo gani.

Uchunguzi uliofanywa na Tanzania Daima Jumapili, kwa wiki kadhaa sasa umebaini kuwa kumekuwapo kwa wasiwasi mkubwa wa kuibwa kwa nyaraka na vifaa mbalimbali katika ofisi za viongozi wakubwa wa serikali akiwemo Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Mwanasheria Mkuu wa serikali (AG).

Chanzo kimoja kimelidokeza Tanzania Daima Jumapili, uchunguzi wa wizi wa kompyuta hizo mpaka sasa unaendelea ili kuwabaini wahalifu waliotenda tukio hilo na kujua walikuwa na lengo gani.

Chanzo hicho kimebainisha kuwa kikosi maalum kimeundwa kufuatilia wizi huo ambao umeonekana kuanza kushamiri katika ofisi nyeti za serikali hasa katika kipindi hiki ambacho kumekuwa na tuhuma nyingi za ufisadi na matumizi mabaya ya madaraka yanayofanywa na viongozi.

Taarifa za ndani zinadai kuwa kompyuta ya IGP iliibwa mezani kwake majira ya mchana siku ya Ijumaa wakati mkuu huyo akiwa amekwenda msikitini kuswali. Katika meza hiyo kulikuwapo na simu za mkononi na kiasi cha fedha kinachodaiwa kuwa sh milioni saba, lakini ni kompyuta pekee ndiyo iliyoibwa.

Habari zaidi zinabainisha kuwa IGP aliporudi alishangaa kutoikuta kompyuta hiyo ilhali simu na fedha vilikuwapo kama alivyoviacha, baada ya kubaini wizi huo zilichukuliwa alama maalumu za vidole zikaonekana ni za mlinzi wake wa karibu (Board guard), ambaye inadaiwa huwa na kawaida ya kuingia mara kwa mara katika ofisi pasi na kutiliwa shaka.

Chanzo chetu cha habari kilieleza kuwa uchunguzi ulipofanyika ndani ya jeshi la polisi ilibainika kuwa kuna afisa wa jeshi hilo, mwenye cheo cha mkaguzi, ndiye aliyeichukua kompyuta hiyo, ambaye hadi sasa anahojiwa ili kulisaidia jeshi hilo liweze kupata chanzo cha uhalifu huo.

Aidha, taarifa zinasema kuwa aliyeichukua kompyuta hiyo, inadaiwa, amelipwa sh mil. 10 kama ujira wake kwa kazi hiyo. Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai nchini (DCI), Robert Manumba, alipoulizwa juu ya hatua ambazo jeshi hilo linazichukua dhidi ya wizi huo ambao unaonekana wazi kulenga kuiba nyaraka muhimu za serikali, alisema huo ni wizi kama mwingine kwani wezi hao hawakulenga kuiba kompyuta hizo kwa lengo maalumu.

“ Siyo kwamba wizi haufanyiki, unafanyika sana; mara hii umetokea katika ofisi nyeti inayomhusisha mkuu wa jeshi la polisi, wizi huo umefanyika tu kama unavyoweza kufanyika nyumbani kwako, haukulenga ofisi hizi tu,” alisema DCI Manumba.

Pamoja na kusema hivyo, alilithibitishia Tanzania Daima Jumapili kuwa hatua za uchunguzi zinaendelea ili kuwabaini wahalifu hao ambao wamefikia hatua mbaya.

“Tanzania hatuna wizi wa kulenga ofisi maalumu za serikali, ndiyo maana unapotokea unawashangaza watu wengi lakini tumejipanga vilivyo katika uchunguzi kuhakikisha tunawakamata wale wote waliohusika,” alisema Manumba na kuongeza:

“Nakwambia ukweli, wewe umekuja kuniuliza kwa sababu wizi umetokea katika ofisi hii, lakini matukio kama haya yanatokea pia katika nyumba za watu binafsi, hata siwezi kukuhesabia idadi ya kesi hizo, tusiwashtue watu waamini kuwa ulilengwa kwa kazi hiyo.”

Manumba alizidi kusisitiza kuwa wizi upo dunia nzima na wanaweza kuiba mahali popote kama wataona kuna kitu, lakini hakuna wizi uliopangwa kulenga katika ofisi hizo za IGP, DPP , au kwa Mkemia Mkuu wa Serikali.

Taarifa zimeeleza kuwa kompyuta iliyoibwa katika Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali ilikuwa kubwa ya mezani (PC), ambayo ilichukuliwa kupitia dirishani katika mazingira ya kutatanisha wakati milango ikiwa imefungwa.

Chanzo chetu kutoka ndani ya ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali, kimeeleza kuwa kompyuta hiyo ilikuwa ikitumika ndani ya ofisi ya Mkemia Mkuu, ambapo bado haijajulikana na nyaraka gani muhimu zilikuwa zimehifadhiwa humo.

“Ni kweli kompyuta iliibwa hapa, milango imefungwa tumefika tukaelezwa kuwa kompyuta ya msaidizi wa bosi wetu haionekani wakati milango ilikuwa imefungwa,” alisema mmoja wa watumishi wa ofisi hiyo ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini.

Aidha kuhusu tukio hilo lililotokea katika ofisi hizo zilizoko karibu na Taasisi ya Saratani, Ocean Road, imeelezwa kuwa bado uchunguzi unaendelea ili kubaini mtu aliyehusika kuiba kompyuta hiyo kama ni mmoja wa wafanyakazi au la.

Kutokea kwa wizi huo kunawafanya baadhi ya watu kuwa na wasiwasi kuwa kuna njama zimepangwa na baadhi ya watu kupoteza vielelezo au ushahidi wa tuhuma au kesi mbalimbali zinazowakabili.

Wasiwasi huo umechangiwa zaidi na matukio ya hivi karibuni ya kupandishwa mahakamani kwa baadhi ya vigogo wa serikali, wafanyabiashara na watu binafsi kwa wizi au matumizi mabaya ya madaraka.

Mpaka sasa watu 11 wameshapandishwa katika Mahakama ya Kisutu jijini Dar es salaam kujibu tuhuma za kuiba kompyuta katika ofisi ya Mkurugeni wa Mashtaka Nchini (DPP).

JANA NILIWEKA HABARI YA KIBAKA ALIYEFANIKIWA KUIBA UA IKULU.JUZIJUZI,USTAADH MMOJA ALIDIRIKI KUMZABA KIBAO RAIS MSTAAFU ALI HASSAN MWINYI.SIKU KADHAA ZILIZOPITA,TULISIKIA KUWA DPP AMEIBIWA LAPTOP YAKE.LEO TENA TUNASIKIA IGP NAE KALAMBWA KOMPYUTA.MATUKIO YOTE HAYA YANAASHIRIA KWAMBA TUNARUKARUKA KWENYE UTANDO WA BUIBUI ILHALI CHINI YA UTANDO HUO KUNA BWAWA LA TINDIKALI.

SWALI LA MSINGI KUJIULIZA KUHUSIANA NA WIZI HUO WA LAPTOP YA IGP NI KWANINI HABARI HIYO IMEVUJA KIRAHISI HIVYO?NI HABARI YA FEDHEHA AMBAYO KWA MAZOWEA TULIYONAYO YA "WAKUBWA HUWA HAWAKOSEI" INGEDHIBITIWA KWA NGUVU ZOTE.NIITE CONSPIRANCY THEORIST,LAKINI I STRONGLY SMELL SOMETHING FISHY.IT'S EITHER KUNA MTU (HUYO ANAYEDAIWA KULIPA MILIONI 10 BAADA YA KUFANIKIWA "WIZI" HUO) ANAYETAFUTWA ILI AWE IMPLICATED AU KUNA EVIDENCE INAPOTEZWA KWA EXCUSE YA "ILIKUWA NDANI YA LAPTOP ILIYOIBIWA."KATIKA ZAMA HIZI ZA UFISADI,LOLOTE KATI YA HIZO CONSPIRANCY THEORIES ZANGU INAWEZA KUWA SAHIHI.


Na Frederick Katulanda, Busanda

WAZIRI wa Nishati na Madini, William Ngeleja jana alijikuta kwenye wakati mgumu baada ya kuzongwa na kundi la wananchi waliomuhoji juu ya ahadi zake za umeme alipowasili katika mji wa Katoro wilayani Geita.

Tukio hilo mithili ya mdahalo lilitokea kati ya majira ya ya saa 9:30 hadi saa 10:15 muda mfupi tu baada ya Ngeleja kuwasili Busanda akitokea Mwanza.

Maswali yalianza baada ya Waziri Ngeleja kusalimiana na wananchi hao na akajibiwa kwa kuonyeshwa alama za vidole viwili.

Hali hiyo ilimfanya waziri huyo kuwauliza wananchi hao sababu za kuichukia CCM wakati imekuwa ikijitahidi kuwaletea maendeleo na ndipo walipoanza kumuuliza maswali huku akiyajibu wakati fulani kugeuka mabishano.

"Hatuwezi kuwashangilia nyinyi... mmetuahidi umeme siku nyingi na hatuuoni, leo mnakuja kutuambia nini. Alikuja hapa sijui (Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Adam) Malima akasema umeme utakuja, lakini wapi hatujaona lolote mpaka leo," alisema mwananchi mmoja.

Ngeleja alipotaka kujibu, mwananchi mwingine alidakia kusema: "Hata kwenye machimbo mmekuwa mkitunyang'anya maeneo yetu na kuwapa wawekezaji. Sisi mnatuona hatufai kama vile ni wakimbizi ndani ya nchi yetu."

Ngeleja alilazimika kuwatuliza na kuwaomba wapunguze maswali ili ajibu swali moja baada ya jingine, lakini kila mtu akataka kumuuliza swali na kukawa na msuguano kati yake na wananchi.

Alianza kujibu kwa kusema kuwa serikali ipo mbioni na kwamba kinachofanyika sasa ni kufuata taratibu kwa sababu mchakato wa suala hilo hauwezi kumalizika siku moja, hivyo akawaomba wawe watulivu wakati mchakato ukiendelea.

Ngeleja alidai kuwa suala lao kuhusu umeme liko katika hatua ya kuridhisha na kwamba wanapaswa kutambua utaratibu wa kushughulikia miradi ya serikali umekuwa ukifanyika kwa hatua.

Majibu hayo yalipingwa na wananchi ambao walimwambia wamekuwa wakidanganywa kama watoto kwa sababu ya kutaka kura na wakishapata, hutoweka.

"Sikiliza basi nikujibu, wewe naona umetanguliza ushabiki tuu. Naomba unisikilize. Ni kweli tulipowaahidi umeme tulidhani mchakato ungekamilika mapema, lakini kuna mambo yametukwamisha, tunaomba mtuvumulie," alisema huku wananchi hao wakiendeleza maswali.

Wakati wakiendelea na mjadala huo, lilipita gari la mgombea CCM wa kiti cha ubunge cha Busanda, Lolensia Bukwimba na mara moja wananchi hao wakageuka na kuanza kuzomea msafara.

Wakati wakiendelea kuzomea ndipo Ngeleja alipopata mwanya na dereva wake akawasha gari na kuondoka.

Waziri Ngeleja alitaja mlolongo wa maeneo ambayo alisema mengi yatapata umeme kabla ya kumalizika kwa mwaka huu, lakini mkakati wao wa umeme ulitibuliwa baada ya Bunge kukataa kuinunua mitambo ya umeme wa dharura ya Dowans Tanzania Limited.

CCM imekuwa na wakati mgumu tangu kuanza kwa kampeni za ubunge wa jimbo hilo lililoachwa wazi na Faustin Kabuzi Rwilomba ambaye alifariki akiwa nchini India alikoenda kutibiwa
.

CHANZO: Mwananchi

IWAPO KUNA LOLOTE LA KUJIFUNZA KATIKA KAMPENI HIZI ZA UCHAGUZI MDOGO WA JIMBO LA BUSANDA BASI NI NAMNA CCM ILIVYO KICHWA NGUMU KUELEWA SOMO.THING IS,WAMESHAHADAA WAPIGA KURA KIASI CHA KUTOSHA KWA AHADI HEWA,HIVYO KUREJEA TENA AHADI HIZOHIZO AMBAZO HAWAJAZITEKELEZA NI MITHILI YA,ASHAKUM SI MATUSI,KUMTONGOZA MTALAKA WAKO.

PENGINE JINGINE NI NAMNA CHAMA HIVYO KISIVYO SERIOUS NA USTAWI WA WANANCHI.WHY?BADALA YA KUREJEA AHADI HIZO AMBAZO HAZIJATEKELEZWA,CHAMA HICHO KWANZA KILIPASWA KUWAOMBA RADHI WAPIGA KURA KWA KUSHINDWA KUTEKELEZA AHADI HIZO HADI SASA,NA ANGALAU BAADA YA HAPO KINGEWEZA KUJARIBU KETE YA KUREJEA AHADI HIZO.NASEMA THAT IS INDICATIVE OF LACK OF SERIOUSNESS KWA VILE CCM INAAMINI KUWA KAMA ILIKUWA IKITOA LOTS OF EMPTY PROMISES FOR AGES NA WAGOMBEA WAKE WAMEENDELEA KUCHAGULIWA,BADO KUNA IMANI KUWA SUCH A RISKY STRATEGY COULD WORK AGAIN AND AGAIN.

CCM HAIDHANI KUWA IMAGE YAKE IKO SEVERELY TARNISHED NA USWAHIBA WAKE NA UFISADI/MAFISADI.INAENDELEA KUAMINI KUWA SHUTUMA DHIDI YAKE KWAMBA NI KICHAKA NA HIFADHI YA MAFISADI NA ZA WATOVU WA NIDHAMU WACHACHE KAMA SIE LAKINI SIO KWAMBA KELELE ZETU NI UWAKILISHI TU WA VILIO VYA MAMILIONI YA WATANZANIA WALIOCHOKA KUFANYWA WAJINGA.

HIVI KIONGOZI MWENYE BUSARA ANAWEZA KUDIRIKI KU-BRING UP ISHU ZA DOWANS KWENYE BY-ELECTION KAMA YA BUSANDA?CAN'T BLAME NGELEJA KWA KUWA KWA YEYE NA VIGOGO WENZIE WA CCM,EQUATION YA DOWANS=RICHMOND HAIJAMWINGIA KICHWANI.

10 May 2009

PICHANI,NI MBUNGE WA IGUNGA,ROSTAM AZIZ,AKIKABIDHI KINACHODAIWA KUWA DOSSIER LENYE TUHUMA DHIDI YA MFANYABIASHARA RAGINALDMENGI.ANAYEKABIDHIWA NI AFISA UCHUNGUZI WA TAKUKURU GWAKISA.Picha hii ni kwa mujibu wa gazeti la The African.

HUU NI NI UPUUZI.YAANI HAINGII AKILINI HATA KIDOGO.JAMANI,HIVI LINI MMEWAHI KUONA TAKUKURU WAKIKABIDHIWA USHAHIDI/TUHUMA MBELE YA VYOMBO VYA HABARI AS SEEN IN THE PICTURE ABOVE?

HUYU ROSTAM AMEKUWA MITHILI YA MUNGU MTU: ALIPOTAJWA TU NA MENGI,MAWAZIRI WAZIMA NA BUSARA ZAO (SOPHIA SIMBA NA KAPTENI MKUCHIKA) WAKALIPUKA KUMTETEA (JAPO SASA WAMEKAA KIMYA ROSTAM ALIPORUDIA KILEKILE ALICHOFANYA MENGI).KISHA TAKUKURU NAO KATIKA HALI INAYOONYESHA NAMNA GANI TAASISI HIYO NI WABABAISHAJI WA DARAJA LA JUU WAKAANDAA MITHILI YA PRESS CONFERENCE YA KUMPOKEA ROSTAM NA KINACHODAIWA KUWA NI USHAHIDI WAKE DHIDI YA MENGI (JAPO KUNA MADAI KUWA WAJANJA WAMEMWINGIZA MJINI KWA KUMUUZIA "CHENI BANDIA"-ISOMEKE DATA FEKI).

HAWA TAKUKURU NI WAZEMBE ZAIDI YA WAZEMBE.HIVI UBABAIKAJI KAMA HUO WALIOFANYA KWA ROSTAM WANGEUELEKEZA KWA KAGODA SI TUNGEPIGA HATUA FLANI?AU WANGEKUWA "FASTA" NAMNA HIYO KATIKA,SIO KUITETEA BALI KUICHUNGUZA IPASAVYO KAMPUNI YA RICHMOND,KWA HAKIKA TUSINGEKUWA HAPA TULIPO SASA.

MBONA WENZETU MNAJIDHALILISHA KIASI HICHO?NI HIZO FEDHA ZA ROSTAM AU NJAA ZENU?THIS IS MORE THAN TOO MUCH.IT'S ABSURD,CRAZY AND UTTERLY NONSENSE.


A woman accused of tormenting her neighbours with her noisy love-making has appeared in court. Skip related content

Caroline Cartwright, 48, was remanded in custody until May 5 charged with three breaches of her Asbo in ten days.

Magistrates in Sunderland slapped her with a four-year order on April 17, banning her from "making excessive noise" anywhere in England.

But Houghton le Spring Magistrates' Court heard that police arrested her on April 18, April 22 and April 26 after neighbours complained she was flouting the ban with the help of husband Steve.

Prosecutor Claire Ward said there were complaints of early morning shouting, moaning, groaning and the sound of a bed banging against the wall. Cartwright was arrested on Sunday and charged with three counts of breaching her Asbo.

Cartwright, of Hall Road, Concord, Washington, Tyne and Wear, whose husband sat in the public gallery, elected trial by jury and her case will be transferred to Newcastle Crown Court.

A bail application from defence solicitor Peter Lothian was refused.

Cartwright was remanded in custody and ordered to appear via video link before Sunderland Magistrates' Court on May 5.

On April 17, she was convicted for five breaches of an abatement notice and fined a total of £515.
Magistrates also imposed the Asbo, banning her from making excessive noise, knocking, shouting, screaming or vocalisation that can be heard in neighbouring properties or outside the house, and playing loud music.


SOURCE: ITN

9 May 2009




Kibaka aduwaza walinzi Ikulu

2009-05-08 13:51:35
Na Jacqueline Mosha

Mfanyabiashara wa Kariakoo jijini Dar es Salaam, Ally Nasoro (41) amefikishwa mahakamani kujibu shitaka la kuingia Ikulu ya Rais Jakaya Kikwete na kuiba ua moja lenye thamani ya Sh. 5,000, mali ya Ikulu hiyo.

Mshitakiwa huyo alifikishwa mbele ya Hakimu Mwajuma Diwani wa Mahakama ya Mwanzo Kariakoo jijini Dar es Salaam jana, na kusomewa shitaka hilo.

Akisoma hati ya mashitaka, karani wa mahakama hiyo, Caphren Maduhu, alidai mbele ya hakimu Diwani kuwa mshtakiwa alifanya kitendo hicho Mei 2 mwaka huu.

Mahojiano mahakamani hapo yalikuwa kama ifuatavyo:

Karani: Kesi hii ni ya wizi na imefunguliwa na mlalamikaji ambaye ni askari mwenye namba E 4716 Koplo Mnyaga.

Mshitakiwa katika shitaka hili ni Ally Nasoro, anaishi eneo la Mabibo jijini Dar es Salaam na anakabiliwa na kosa wizi alilofanya Mei 2, mwaka huu, saa 4:24 usiku huko Ikulu ya Rais.

Hakimu: Mshitakiwa umesikia mashitaka ya kosa lako, unajibu nini?

Mshitakiwa: Mimi nilikuwa napima uwezo wa akili wa walinzi waliowekwa Ikulu ili kumlinda Rais wa nchi, maana isije ikawa wako wako tu kumbe hawana hata uwezo wa kumlinda.

Hakimu: Ile ni sehemu ya heshima na inalindwa iweje wewe upate wazo la kutaka kuingia ndani, ulikuwa na nia gani?

Mshitakiwa: Nilichokigundua siku hiyo ni kwamba kumbe naweza kuingia Ikulu kiulaini bila hata ya kuguswa na mtu. Kwanza nilipofika pale getini nilitaka kufahamu kama naweza kufanikiwa kuingia, hivyo, nilisimama kwa saa nne nje ya geti bila hata kuulizwa chochote na walinzi. Baadaye nilifanikiwa kupata mwanya wa kuingia ndani na kweli niliingia kiulaini bila hata 'shobo'.

Hakimu: Ilikuwaje mpaka ukaiba hilo ua?

Mshitakiwa: Nilipolichukua lile ua na kulibeba ndipo walinzi waliniona na baada ya kuniona walinzi hao walibaki wakitetemeka huku mimi nikiwa nimeshikilia ua na ndipo waliponikamata na kunichukulia hatua. Kama naweza kuchukua ua si ningeweza hata kuingia ndani kwa Rais kiulaini? Yaani walinzi wamelala pale. Hawako makini kama nilivyodhani.

Hakimu: Unajibu nini kuhusu shitaka la wizi huo?

Mshitakiwa: Si kweli, sijaiba ua.

Hakimu Diwani aliahirisha kesi hiyo mpaka itakapotajwa tena mahakamani hapo Mei 11 mwaka huu. Mshitakiwa alipelekwa mahabusu baada ya kushindwa kutimiza masharti ambayo ni kuwa na wadhamini wawili.

CHANZO: Nipashe

SOMEONE SOMEWHERE IS NOT UP TO THE TASK.AWALI,RAIS MSTAAFU MWINYI ALIZABWA KIBAO HADHARANI,A COUPLE OF WEEKS AFTER MSAFARA WA JK KURUSHIWA MAWE HUKO MBEYA.SUPPOSE HUYU KIBAKA HAD INTENDED TO,NOT TEASE THE GUARDS WITH A STOLEN FLOWER BUT, CAUSE HARM TO THE PRESIDENT.....

SECURITY SLACKNESS

8 May 2009


Venance George, Kilombero

BAADHI ya wadau katika Wilaya ya Kilombero, wameitahadharisha serikali kuhusu uanzishwaji wa taasisi zenye mtazamo kama wa Deci ili kuwanusuru wananchi wasipoteze mali zao.

Tahadhari hiyo inafuatia kuanzishwa kwa PUFDIA, katika mji mdogo wa Ifakara ambayo watu wanaifananisha na Deci. Wakizungumza na gazeti hili baadhi ya wadau hao, Ibrahim Madon na Kenedy Haule waliishauri serikali kudhibiti uanzishwaji wa taasisi kama hizo. Walisema kama serikali haitakuwa makini, baadhi ya watu wachache wanaojali maslahi yao, watakuwa wanaanzisha taasisi hizo na kuendelea kuwakamua wananchi maskini.

Walitolea mfano wa Deci ambayo ilipigwa marufuku na serikali hivi karibuni, baada ya kuanzisha kwa mchezo wa upatu ambao baadaye ungesababisha hasara kubwa kwa wateja wengi wao wakiwa ni wananchi maskini. Taasisi ya PUFDIA imeingia wilayani humo hivi karibuni na kujinadi kwamba ni taasisi mpya inayotoa huduma za miradi mitano endelevu kwa ajili ya maendeleo ya watu wa nchi nzima.

Miradi inayoshughulika na taasisi hiyo ni pamoja na udhamini wa masomo ya sekondari hadi chuo kikuu kwa kwa mtoto wa mtu yeyote. Katika mchakato wake taasisi hiyo inaeleza kuwa chini ya mradi wa elimu, itatoa fedha za kulipia gharama zote za masomo na bajeti inayotolewa kwa kila mtoto ni Sh 570,000 kwa wale wanaosoma shule za msingi wakati wale wanaosoma shule za sekondari watapewa Sh980,000 na Sh 2.64 milioni kwa vyuo vikuu.Gharama hizo ni kwa kila muhula.

Mradi mwingine ni wa kujengewa nyumba za thamani ya Sh 6 milioni kama msaada kwa mwananchi yeyote mwenye shida ya nyumba wakati wanaotaka kujengewa shule wanatakiwa kwenda katika ofisi hiyo kujaza fomu yenye uwezo wa kujengewa shule yenye thamani ya Sh 46.2 milioni

Taasisi hiyo pia imesema itasaidia wananchi kwa kuwapa mikopo isiyo na riba yenye thamani ya Sh 2,470,000. Mwandishi wa habari hizi alikwenda katika ofisi za PUFDIA na kuwahoji maofisa wake ambao hata hivyo, hawakutaka kutaja majina yao. Maafisa hao walidai kuwa huduma wanazotoa ni halali na kwamba wanalipia kodi.

Kwa mujibu wa maelezo yao, taasisi hiyo inafadhiliwa na taasisi kubwa ya kidini iliyoko nje ya nchi. Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, alikiri kuwepo kwa taasisi hiyo na kwamba maafisa wake, walikwenda ofisini kwake kuomba kutoa huduma hiyo.

Alisema hata hivyo atalipitia upya jalada la taasisi hiyo na kuelezea mustakhabali wake.


CHANZO: Mwananchi


ASHANTI ft CROOKED I "Baby-Remix"

Featured by FAT JOE in What's Love

Foolish (TERRENCE HOWARD cameo)


Ja Rule ft. Ashanti & Rkelly - Wonderful
by Shameek


MTV NEWS reports that Ashanti and Murder Inc will soon be partying company.

It's weekend,let's have some fun.How about this?




That's according to ThisIs50.Com

Pakistan's army declared a "full-scale" offensive against Taliban insurgents holed up in the Swat valley today as warplanes pounded militant bunkers and caused thousands more residents to flee.The fighting was concentrated in the main town, Mingora, where an estimated 4,000 Taliban fighters are heavily dug in. Artillery and helicopter gunships battered militant-held buildings, while the Taliban planted mines across the city in expectation of a major ground offensive... continue


KUNA JAMAA YANGU,MMOJA MWINGEREZA LAKINI AMEKAA TANZANIA KWA MUDA KIASI.KWAHIYO LUGHA YA TAIFA INAPANDA,NA ANACHUNGULIA MAGAZETI YETU MTANDAONI.KAUNIULIZA SWALI "LA KIZUSHI": HIVI MBONA MUDA MWINGI VIONGOZI WENU WAKO ZIARANI?KAMA SIO RAIS YUKO NJE YA NCHI AU ZIARANI MKOA FLANI,BASI MAKAMU WA RAIS YUKO ZIARANI SEHEMU FLANI,AU WAZIRI MKUU YUKO ZIARANI MKOA FLANI!JE MAENEO HAYO WANAYOZURU HAYANA VIONGOZI?KAMA WAPO,HAWAWEZI KUWAPELEKEA RIPOTI ZA MAENDELEO WAKUU WAO PASIPO UMUHIMU WA WAKUU HAO KUZURU?

NIMEKOSA JIBU,SO FAR.MAANA SIKUMBUKI MARA YA MWISHO NI LINI WAZIRI MKUU WA HAPA,GORDON BROWN ALIKUWA KATIKA ZIARA YA BANDIKA BANDUA.SIJUI YUKO BUSY SANA!?
SIJUI MWENZANGU UNGEJIBU NINI!


Dar es Salaam, Tanzania (PANA) 16/09/2005- Tanzania's controversial opposition leader, the Reverend Christopher Mtikila alleged Friday that ruling Chama cha Mapinduzi (CCM) presidential candidate Jakaya Kikwete had used funds from Iran to defeat his opponents at the party's recent convention.

The Chairman of the Democratic Party claimed at a press conference that the Iranian government through Tanzanian MP Rostam Aziz, had funded Kikwete's campaign for over 10 years.

The press conference was held ahead of a meeting by eight opposition parties to plan a common strategy against the CCM in Tanzania's October elections.

Mtikila alleged that the Iranian government had set aside a substantial amount to prop presidential candidates in countries where the Asian country has economic interests.

Aziz, a Tanzanian of Iranian extraction is representing Igunga constituency in Tanzania's Union Parliament on the platform of the CCM.

Mtikila did not say how much Aziz had allegedly received from the Iranian government for Kikwete's presidential campaign, but cited Tanzania's uranium deposit as possible motivation for the alleged assistance.

He said the Iranian government could not have given Aziz money for nothing: "they must be harbouring interests in Tanzania."

This is the second time that Aziz, Kikwete's campaign manager, would be accused of securing foreign funds for Kikwete's presidential campaign.

Last April, London-based journal, Africa Confidential claimed that he had been given two million US dollars by the Oman government as campaign funds for Kikwete.

Kikwete, Tanzania's Foreign Affairs and International Co-operation Minister had vowed to sue the journal over the report, but since his nomination as CCM presidential candidate in May, he has said nothing about the report.

The London journal has challenged him to go to court insisting it has overwhelming evidence to back its claims.

There was no immediate reaction to Mtikila's allegations from either Aziz or Kikwete.


SOURCE: PANAPRESS

NA KUNA MJADALA UNAENDELEA HUKO JAMII FORUMS KUHUSU URAIA WA BWANA ROSTAM AZIZ.



Na Frederick Katulanda, Busanda

KAMPENI za uchaguzi za CCM katika uchaguzi mdogo wa jimbo la Busanda jana zilizidi kukumbana na upinzani mkali baada ya makamu mwenyekiti wa chama hicho, Pius Msekwa na makamu mwenyekiti wa zamani, John Malecela, kujikuta wakizomewa wakati walipokuwa wakijinadi katika mkutano uliofanyika Nyarugusu wilayani Geita.

Mbali na vigogo hao wa CCM, mgombea wa chama hicho katika uchaguzi huo mdogo, Lolencia Maselle Bukwimba na mumewe, Maselle Buziku walizomewa wakati walipotambulishwa kwenye mkutano huo wa kampeni.

Tukio hilo limetokea siku moja baada ya chama hicho kujikuta kikiwa na watu wachache wakati wa kuzindua kampeni zake kwenye kata ya Kaseme, tofauti na mikutano ya vyama pinzani vya Chadema na CUF.

Dalili za hali mbaya katika mkutano huo zilianza wakati viongozi hao wakiingia eneo la Nyarugusu ambalo ni maalumu kwa wachimbaji wa dhahabu. Viongozi hao walipokelewa na alama ya vidole viwili kila walikopita. Alama ya vidole viwili hutumiwa na Chadema.

Zomea zomea hizo ziliwakabili viongozi hao wa CCM wakati walipokuwa wakimnadi mgombea wao. Hali mbaya ilianza kwa katibu mwenezi na uhamasishaji, Simon Mangelepa wakati aliposimama jukwaani na kuanza kuwatambulisha wageni walioambatana nao na kufuatiwa na mbunge wa viti maalum mkoani Mwanza, Maria Hewa ambaye alizomewa baada ya kuwaeleza wananchi kuwa wanapaswa kutulia.

Kutokana na hali hiyo mwenyekiti wa CCM mkoani Mwanza, Clement Mabina alisimama jukwaani kabla ya kumkaribisha Malecela ili amnadi mgombea wa chama hicho na kuwaeleza kuwa anazo taarifa kuwa kuna watu ambao wamepangwa hapo kwa ajili ya kuzomea, naye kuzomewa.

Baadaye ikawa zamu ya Malecela ambaye baada ya kusimama jukwaani aliwaeleza wananchi kuwa shutuma za ufisadi hazina nafasi katika kampeni kwa sasa na kuwataka wenye ushahidi wa ufisadi kuupeleka polisi, kauli ambayo iliwafanya wananchi ambao walikuwa wametulia, kuanza kuzomea wakimtaka aondoke huku wakionyesha vidole viwili.

Hata hivyo, Malecela aliwatuliza na kuwaeleza kuwa hiyo ndio njia sahihi ya kushughulikia mafisadi na kuendelea kuwaeleza wananchi kuwa iwapo wataichagua CCM katika uchaguzi huo watapatiwa umeme pamoja na kutengewa maeneo kwa ajili ya wachimbaji wadogo.


Nataka kuwaeleza iwapo mtamchagua mgombea huyu, basi serikali italeta umeme eneo hili….na kutenga maeneo kwa ajili ya wachimbaji wadogo," alisema lakini akakatwa kauli na kelele za wananchi ambao walisema miaka yote wameichagua CCM na kuahidiwa mambo hayo bila ya kufanikiwa.

Kutokana na hali hiyo Malecela aliamua kuwatuliza na kuomba Busanda isigeuke kama Tarime na kwamba wao CCM wanataka kampeni za amani na utulivu.

Ndipo ilipofika zamu ya Msekwa kumnadi mgombea na baada ya kupanda jukwaani alimkaribisha mgombea aliyemsimamisha mumuwe, Maselle Buziku, ambaye naye alipoeleza kuwa iwapo watamchagua mkewe atatumia nafasi yake SEDA kuhakikisha wanapata mikopo, lakini akazomewa na wananchi hao.


Hata hivyo zomea zomea hizo hazikuweza kuhatarisha amani katika mkutano huo na mgombea huyo alijieleza bila ya matatizo na kupiga magoti lakini alipoomba kura, naye akajikuta anazomewa.

Katibu mkuu wa CCM, Yusuf Makamba amekiri kuwa kuna hali ngumu kwenye Jimbo la Busanda na kuwataka viongozi wa chama hicho kupigana kufa au kupona ili kuhakikisha jimbo haliangukii mikononi mwa upinzani kwa kuwa machungu ya kushindwa Tarime anayajua.

Kauli hiyo ilitolewa na Makamba juzi mchana wakati alipokuwa akizungumza na viongozi mbalimbali wa chama hicho katika mkutano wa ndani kwenye ofisi za CCM wilayani Geita baada ya kuwasili kwa ajili ya uzinduzi wa kampeni wa chama chake zilizofanyika juzi katika kata ya Kaseme.

Makamba alikiri kuwa hali ni ngumu na hivyo kuwaomba kila mmoja kuhakikisha mgombea wa CCM anashinda, akilalamika kuwa makali ya kushindwa alishayaonja Tarime.

Habari zilizopatikana kutoka ndani ya kikao hicho na kuthibitishwa na mmoja wa viongozi wa chama wilayani humo zimeeleza kuwa Makamba aliamua kufanya mkutano huo kwa lengo la kuwekana sawa kutokana na CCM kukabiliwa na upinzani mkali kutoka kwa wale walioenguliwa katika kura za maoni za kuwania kuteuliwa kuwa mgombea wa chama hicho.

Makamba amesema "jamani kushindwa ni kubaya, mwenzenu Tarime nilionja ubaya wake mpaka ilibidi nitoroshwe na Green Guard ili kuepuka kuzomewa, sasa tusiposhikamana mambo yatakuwa magumu tutoe tofauti zetu,'” alisema mmoja wa wajumbe waliokuwa kwenye kikao hicho akimnukuu Makamba.

Hata hivyo, baada ya kauli hiyo Makamba alishtuka na kuhoji iwapo walikuwemo waandishi wa habari ukumbini humo na kuonya utoaji wa taarifa hizo baada ya kujibiwa hawakuwemo.

Aidha baada ya kujibiwa kuwa hakuna waandishi Makamba alishtuka baada ya kubaini kuwa kulikuwa na mpiga picha wa chama na kumuagiza kuhakikisha mkanda huo anaukabidhi kwa katibu wa CCM wa mkoa.

Makamba alipoulizwa kuhusu suala hilo alijibu kuwa hajawahi kukiri kuwepo kwa hali ngumu kwa vile hana wasiwasi na uchaguzi huo na kusema alikuwa akieleza masuala ya kushikamana.

“Wewe unataka nikueleze mikakati yangu, kama nilikuwa nawahimiza watoto wangu kulima we unakutakia nini,” alihoji katibu huyo wa CCM alipoulizwa na Mwananchi kuhusu kikao hicho.

Sambamba na hatua hiyo Makamba alimtaka mjumbe wa halmshauri kuu ya chama hicho mkoani Mwanza, Anthony Diallo kutumia uwezo wake kuhakikisha kampeni hizo zinakuwa na hamasa ya kutosha ikiwa ni pamoja na kurusha taarifa zake katika vyombo vya habari.

Uchaguzi katika jimbo la uchaguzi la Busanda umepangwa kufanyika Mei 24 kwa lengo la kujaza nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, marehemu Faustine Kabuzi Rwilombe.

Vyama vingine vinavyowania kiti hicho ni Chadema, CUF na UDP.

CHANZO: Mwananchi

WANACHOHITAJI CCM NI BUSARA ZA KI-UTU UZIMA,YAANI KUKIRI PALE WALIPOKOSEA,NA KUAHIDI KUJIREKEBISHA BADALA YA KUENDELEZA AHADI HUKU ZILE WALIZOTOA MWANZO ZIMEENDELEA KUBAKI AHADI TU PASIPO KUZITEKELEZA.WAINGEREZA WANASEMA " A PROMISE MEANS NOTHING UNTIL DELIVERED."
HALAFU HIZI KAULI ZA KIBAGUZI KUWA "ICHAGUENI CCM IWALETEE HIKI AU KILE" (AS IF AWALI ILIYOCHAGULIWA ILIKUWA CHADEMA AU CUF) NI KUWAFANYA WAPIGA KURA WAJINGA AU WASAHAULIFU.KAMA WALIKUWA NA NIA YA KULETA HUO UMEME,SI WANGEFANYA HIVYO WAKATI WAPIGA KURA WALISHAWAPA HESHIMA YA KUMCHAGUA MGOMBEA WA CCM KWENYE UCHAGUZI ULIOPITA?SASA HIZI HABARI KUWA MKITUCHAGUA TENA NDIO TUTAFANYA HIKI AU KILE NI MITHILI YA KUWAHADAA WANANCHI.
I HOPE WAPIGAKURA WA BUSANDA HAWATAISHIA KUFIKISHA UJUMBE KWA CCM KWA KUZOMEA TU BALI PIA KUINYIMA KURA ILI IKIAMSHE CHAMA HICHO KUTOKA USINGIZINI KWAMBA THIS IS 2009,AND SO FAR THE ASSESSMENT OF HOW THE PARTY HAS IMPLEMENTED ITS ELECTION MANIFESTO LEAVES A LOT TO BE DESIRED.KAMA TARIME WALIWEZA,BUSANDA PIA WANAWEZA.NA KAMA WOTE WASIORIDHIKA NA MWENENDO WA CCM WATAAMUA KUWA ENOUGH IS ENOUGH,NO MORE FALSE PROMISES,THEN CHANGE IS NOT ONLY COMING BUT WILL EVENTUALLY BE ACHIEVED.
AS OBAMA SAID,YES WE CAN IF WE BELIEVE IN CHANGE.

7 May 2009

PENGINE KUNA CHA ZIADA KINACHONIFANYA NISIAMINI MACHO YANGU KUONA JACOB ZUMA NDIO HIVYOOO ANAELEKEA KUKABIDHIWA URAIS WA AFRIKA KUSINI.NCHI ZA MAGHARIBI ZINAFUATILIA KWA KARIBU YANAYOENDELEA HUKO SAUZI,LAKINI HOFU YA WENGI NI KUWA HUENDA ZUMA NI POPULIST FLANI AMBAYE AMEFANIKIWA SANA KUKONGA NYOYO ZA WENGI NCHINI HUMO LAKINI ANAYEWEZA PIA KULIINGIZA TAIFA HILO TAJIRI MATATIZONI.BINAFSI HUWA SINA IMANI YA KUTOSHA NA WANASIASA WANAOSHINDWA KUONYESHA UDILIFU KWENYE NDOA ZAO KISHA UWATARAJIE WAWE WAADILIFU KWA TAIFA.INAELEKEA WASAUZI WAMELIPUUZA HILO.


NADHANI TAFSIRI SAHIHI YA "WORLD'S MOST INFLUENTIAL PEOPLE" INAWEZA KUWA NGUMU KWA LUGHA YETU YA TAIFA.SIJUI TUITE "WATU MAARUFU ZAIDI DUNIANI" AU "WENYE MVUTO ZAIDI" AU...?SINA HAKIKA KAMA INFLUENCE NI UMAARUFU AU MVUTO.ANYWAY,KWA MUJIBU WA ORODHA YA WATU 100 INFLUENTIAL KABISA DUNIANI KWA MWAKA 2009 INAYOANDALIWA KILA MWAKA NA JARIDA LA TIME LA MAREKANI,RAIS PAUL KAGAME AMESHIKA NAFASI YA 13.MARA NYINGI ORODHA HIYO HUPATA PIA UPINZANI NA KEJELI HUSUSAN KUTOKA KWA WAHAFIDHINA WANAOTAFSIRI JARIDA LA TIME NA ORODHA HIYO KUWA NA MRENGO WA KUSHOTO AU KILIBERALI ZAIDI.

"NDANI YA NYUMBA" PAMOJA NA KAGAME,NI MCHANYATO WA WANASIASA KAMA SENETA TED KENNEDY NA WAZIRI MKUU WA UINGEREZA GORDON BROWN,KIONGOZI WA KIYAHUDI MWENYE MSIMAMO MKALI KABISA AVIGDOR LIEBERMAN (Pichani Chini)
NA "MFALME WA UNGA" (COCAINE), JOAQUIN GUZMAN,"PABLO ESCOBAR MPYA" AMBAYE PIA NI MIONGONI MWA WATU MATAJIRI KABISA DUNIANI NA AMBAYE KICHWA CHAKE KIMEWEKWA REHANI YA US$ 5MILLION NA VYOMBO VYA DOLA VYA MAREKANI (Pichani Chini),MCHEZA SINEMA MWENYE MVUTO BRAD PITT,TAPELI LA PONZI BERNIE MADOFF,GWIJI LA "KUSEMA OVYO" RUSH LIMBAUGH,MWANAMUZIKI JOHN LEGEND(Pichani Chini),MWANADADA WA KIZAMBIA DAMISA MOYO (Pichani Chini)
BILA KUMSAHAU RAIS OBAMA NA MKEWE MICHELLE (Pichani chini na Oprah)
NA USUAL SUSPECTS KAMA TOM HANKS,GEORGE CLOONEY,TIGER WOODS NA WENGINEO.

BONYEZA HAPA KUANGALIA ORODHA KAMILI.HONGERA RAIS KAGAME.WANYARWANDA WANA KILA SABABU YA KUJIVUNIA UONGOZI WAKO HASA KWA TAIFA LILILOWEZA KUSIMAMA KIDETE KUTOKA KWENYE MAUAJI YA KIMBARI HADI KUWA HADITHI YA KUPIGIWA MFANO BARANI AFRIKA.ANYWAY,SIE TWAENDELEA KUJIVUNIA AMANI NA UTULIVU WETU UFISADI STYLE!!!

6 May 2009

ANGALIA HAPA .KAMA INAZINGUA TAFUTA STREAM NYINGINE HAPA

5 May 2009








CHANZO: Jamii Forums


CLICK HERE for more about the match.


Sarah Baxter

A COMEDIAN who had a walk-on part in the Rutles film spoof of the Beatles is poised to deliver a 60-seat super-majority to the Democrats in the Senate as President Barack Obama consolidates his grip on the levers of power.

Al Franken, 57, a satirist turned Democrat politician, is expected to be proclaimed the winner of the protracted race for the US Senate in Minnesota, in time to give Obama a free hand to appoint a Supreme Court replacement for retiring Justice David Souter without fear of Republican blocking tactics.

If Franken wins, Obama will hold an unassailable majority after Senator Arlen Specter’s sudden defection from the Republicans to the Democrats last week. A 60-seat majority would deprive the Republicans of the ability to scupper appointments and legislation by filibustering...
continue


SOURCE: The Times

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.