16 May 2009


Na Leon Bahati

MAKAMU wa Rais wa Kenya, Kalonzo Musyoka amekiri kuwa mlima Kilimanjaro umekuwa ukiisaidia nchi yake kukuza sekta ya utalii kutokana na Wakenya wengi kuutumia katika kujitangaza hasa wawapo kwenye nchi za ulaya.

Pamoja na kufaidika huko, alisema kuwa hiyo haifuti ukweli kwamba mlima huo mrefu kuliko yote Afrika, upo Tanzania, ingawa pia huweza kuonekana kutokea Kenya.

Musyoka alisema hayo kwenye hafla fupi ya chakula cha mchana alichoandaliwa na mwenyeji wake, Makamu wa Rais wa Tanzania, Dk Ali Mohamed Shein.

“Wakenya wanapoenda Ulaya wanawaambia wazungu: Njooni Kenya ili muone mlima Kilimanjaro,” alisema Musyoka katika ziara hiyo ya kiserikali kwa mwaliko wa Tanzania...
endelea

CHANZO: Mwananchi


WELL,HUWEZI KUWALAUMU IWAPO SIE "WENYE MLIMA HUO" TUNAENDEKEZA ZAIDI POLITIKI KULIKO KUTANGAZA VIVUTIO VYETU.WANAOPEWA DHAMANA YA KUTANGAZA RASLIMALI ZETU WAKO BIZE ZAIDI NA "TENI PASENTI" YA MIKATABA YA MATANGAZO KULIKO UFANISI WA MATANGAZO HAYO.


MSIKIE MATTAKA ANAVYOONGEA KWA KUJIAMINI KANA KWAMBA ALIJITEUA MWENYEWE KUWA MKURUGENZI WA ATCL NA KUJIPA UJUMBE WA NIC.


Mattaka ajiweka kando ATCL
Imeandikwa na Mwandishi Wetu; Tarehe: 16th May 2009

Mkurugenzi Mtendaji na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL),
David Mattaka ametangaza kutoiongoza kampuni hiyo kwa miezi sita kutokana na kuteuliwa kuwamiongoni mwa wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Bima la Taifa (NIC).

Katika taarifa ya barua hiyo iliyotolewa na ofisi yake kwa wafanyakazi Mei 11, mwaka huu, inaonyesha kuwa Mattaka amelazimikakutofanya kazi ATCL kwa kipindi hicho kutokana na nafasi yake hiyo aliyoteuliwa naWaziri wa Fedha na Uchumi, Aprili 23, mwaka huu kuwamo katika Bodi ya Wakurugenzi ya NIC kazi ambayo zinamtaka awapo wakati wote kazini.

Uteuzi huo sambamba na wa Rais Jakaya Kikwete wa Februari 23, mwaka huu wa kuwamo katika kikosikazi cha kulifufua shirika hilo, Mattaka alisema “Katika nafasi zote nilizoteuliwa zinanitaka nifanye kazi muda wote kuanzia Mei mosi.” Kutokana na nafasi hizo mpya, kwa kipindi cha miezi sita ambayo hatakuwao ATCL, Bodi ya Wakurugenzi imemteua William Haji kukaimu nafasi yake.

“Bodi ya Wakurugenzi imemteua William Haji kukaimu nafasi ya Mkurugenzi Mkuu na CEO kuanzia Mei 8 na wakati huohuo kuendelea na nafasi yake ya Mkurugenzi wa Fedha,” alisema Mattaka. Bodi ya Wakurugenzi ya NIC iliyoanza kazi Mei mosi, inaongozwa na Mwenyekiti Balozi Charles Mutalemwa na wajumbe ni Michael Mhando kutoka Bima ya Afya, Msajili wa Hazina Agnes Bukuku, Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) Kate Bandawe na Charles Kilasile.

CHANZO: Habari Leo

KWA UPANDE FLANI,HATUWEZI KUMLAUMU KWANI KWA HAKIKA ALIYEMTEUA AMEONEKANA KURIDHISHWA NA UTENDAJI WAKE.USHKAJI KATIKA TEUZI NI MIONGONI MWA VYANZO VIKUU VYA KUSUASUA NA HATIMAYE VIFO VYA TAASISI MBALIMBALI ZA UAMMA,BILA KUSAHAU KUSHAMIRI KWA UFISADI.KWANI HAKUNA WATU WENYE UWEZO ZAIDI YA MATTAKA?KAMA AMECHEMSHA ATCL,ATALETA MIUJIZA GANI HUKO BIMA?


YANI TUNAVYOENDESHA MAMBO KIHOLELA UTADHANI TUSHAPIGA HATUA KUJIKWAMUA KIUCHUMI KUMBE WAPI.VICHWA VILIVYOISHIWA MAWAZO NA MBINU ZA KUNUSURU TAASISI ZA UMMA HAVIWEZI KULETA MAPYA YOYOTE VINAVYOZUNGUSHWA KIUSHKAJI KUTOKA TAASIS MOJA KWENDA NYINGINE KANA KWAMBA NI ZA KIFAMILIA.



UMASIKINI WA WATANZANIA (KAMA UNAVYOONYESHWA KATIKA PICHA YA JUU kwa hisani ya Dr Faustine) UNACHANGIWA ZAIDI NA MAFISADI WACHACHE WASIONYIMWA USINGIZI NA MISHANGAO KAMA HIYO YA BALOZI WA SAUZI.HAWANA MUDA WA KUJALI NANI ANASEMA NINI,ALIMRADI VOGUE ZAO (kama katika picha ya mfano hapo chini) ZINAENDELEA KUWAPA UJIKO MTAANI!YALEYALE YA MTU ANAKUPORA MKEO KISHA ANAMPTISHA MBELE YAKO MAKUSUDI KUKURUSHA ROHO!
Na Claud Mshana

BALOZI wa Afrika Kusini nchini amesema anashangazwa kuona nchi iliyojaliwa rasilimali nyingi kama Tanzania kujiendesha kwa kutegemea misaada kutoka nchi wahisani na marafiki.

Balozi huyo, Sindiso Mfenyana alisema rasilimali zilizo nchini zinaweza kugeuzwa na kuwa tegemeo la misaada kwa nchi nyingine.

Mfenyana alisema hayo wakati akizungumza na wahariri mbalimbali wa vyombo vya habari jijini Dar es salaam. Mfenyana alisema inashangaza kuona Tanzania ambayo imebarikiwa kuwa na rasilimali za kila aina ikiendelea kutegemea misaada katika uchumi wake.

"Kama rasilimali zilizopo zitatumiwa vizuri kwa maendeleo ya nchi hii na pia kukawa na usawa katika matumizi ya rasilimali hizo, nchi hii ingekimbiliwa na watu wengine kwa misaada," alisema balozi huyo.

Mfenyana alisisitiza kuwa Tanzania haina haja kuhofia wawekezaji kutoka Afrika Kusini, hasa wazungu kwa sababu zama za ubaguzi wa rangi zimeshapita na kwamba kilichopo sasa ni kuona nchi inakuwa na ushirikiano wenye manufaa bila kujali rangi wala historia baina ya nchi za Afrika.

"Ni ajabu kuona mtu anakuwa na wasiwasi kuingia ubia wa kiuchumi na 'Mzungu', pengine ni kutokana na historia iliyokuwepo kabla… inawezekana kuwa vyombo vya habari havikutangaza vya kutosha kuwa vita vya ubaguzi wa rangi vimekwisha," alisema.

"Leo hii mtu mweusi wa Afrika Kusini anakuwa na chuki na mtu mweusi mwenzake kuliko hata Mzungu, jambo hili linaonyesha kuwa enzi za kuchukiana kwa misingi ya rangi imeshapita.

Ni lazima tuendeleze uhusiano wetu kwa manufaa ya nchi zetu." Kwa upande wake, Meneja wa Jukwaa la Wafanyabishara wa Tanzania na Afrika Kusini, ambaye pia ni meneja wa hoteli ya Southern Sun, Adam Fuller alisema kumekuwa na maendeleo chanya ya ushirikiano wa kibiashara kwa nchi hizi mbili.

Alifafanua kuwa tofauti na zamani, Tanzania ilikuwa ikijitenga kiushirikiano na nchi nyingine labda kwa kuhofia ushindani, hivi sasa kuna tofauti kubwa na kuongeza kuwa wataendelea kushirikiana zaidi kwa kutumia fursa zilizopo kibiashara.

Kuhusu tatizo la umasikini nchini humo ambalo linachangia kwa kiasi kikubwa kuwepo na wimbi la uhalifu, Mfenyana alisema serikali ya nchi yake imejipanga kukabiliana na hali hiyo na tayari hatua madhubuti zimeshachukuliwa kukabiliana na
tatizo hilo.

CHANZO: Mwananchi

INA MAANA BALOZI HUYU HAJUI KUWA RASILIMALI ZETU TAYARI NI MSAADA KWA MAFISADI?NCHI YETU IMEGEUZWA SHAMBA LISILO NA MWENYEWE,WATU WANAJICHUMIA WEE MPAKA WANAKINAI NA KULETA NYODO!INATIA UCHUNGU LAKINI NDIO HIVYO TENA.


15 May 2009

Pombe bwana!Huyu si "shoga",ni mwanaume ila tu kinywaji kimemkolea kaamua atinge gauni.Na sijui hiyo pozi kajifunzia wapi!

Huyu "Beyonce Mweupe" anaonyesha ufundi wa kunengua.

Hao si watoto wa shule,na huo "upole" ni sehemu ya kinywaji pia!

"Kwanini Mungu aliwapendelea ng'ombe kuwa na miguu minne na sie wanadamu miguu miwili?"Yaelekea ndio "malalamiko ya muungwana huyo anayetambaa.Au anakumbukia alivyokuwa akitambaa wakati wa utoto?Katika pombe,lolote linawezekana!

Kilio tena!?

Pombe huwafanya wanyonge wajione majabali,only kinywaji kinapoyeyuka kichwani hujikuta wakiwa wanyonge vilevile PLUS majeraha.
"Yes!Nimeweza.Si mlisema siwezi kulibalansi hilo boksi la take-away eti nimelewa?Mbona nimeweza.Watu tumeanza pombe zamani,in fact kabla ya kunyonya maziwa ya mama...teh teh teh"
"Basi nikwambie shoga,mwaka 1978 nili....halafu kabla ya hapo mwaka 1749 nilikuwa....na mwaka huu 2004 nita....".Stori za kilevi hazihitaji kuwa makini na tarehe au muda.Na zinaweza kuendelea milele.Kimsingi huwa haziishi,na mada hubadilika kama bendera na upepo.

" Nahisi kama niko 'leba' mtoto najifungua.Hee nimezaa mtoto wa kiume".Si ajabu huyu akiamka asubuhi anamaizi kuwa kweli "alizaa" lakini mtoto ni "pooh" (ile kitu inayotupeleka msalani).
Duh.Hapa ni ujenzi wa mahekalu hewani
Huyu ashukuru ufanisi wa polisi wa doria wanaosaidiwa na CCTV.Ukaaji huo mitaa ya uswahilini ingeweza kumfanya huyo jamaa kwa siku kadhaa asitoke nyumbani kutokana na aibu.Ni mkao hatari sana!
Hoi!

Ah,nani kasema kitanda lazima kiwe chumbani.Hapa napata 'nepu' ya bure buleshi.
" Hee hawa vipi tena?",dada wa kushoto haamini anachokiona."Ahaaa,ndio mana wanaume wa kiskotishi wanapenda hizo kilt zao wanapokwenda out..." Anazidi kutafakari mdada wa watu.

"Kuanzia leo mto wangu utakuwa tairi..."Chapombe afanya uvumbuzi usiku wa manane.
Huy kibonge sijui anatoa nasaha gani kwa wenzake.Pombe huleta "busara" za ajabu kabisa.
Oh dear dear....
Picha hizi zimepigwa na mwanafunzi wa KiPolish jijini Cardiff,Wales.Habari zaidi kuhusu picha hizo na utamaduni wa chapombe (binge culture) BONYEZA HAPA.





Hiyo ni kwa mujibu wa The Guardian




Now, most footballers are partial to a flash motor or two as an ultimate status symbol.But to say this show-stopping chrome Mercedes-Benz SLR McLaren is just slightly attention-seeking would be something of an understatement.The garish £420,000 supercar belongs to proud owner Blackburn Rovers' striker El Hadji Diouf (below)....CONTINUE
SOURCE: The Daily Mail


SOMA HABARI HII KISHA UNGANA NAMI MWISHONI KATIKA KUHOJI LOGIC YA TCRA.


Kusajili simu lazima
:: Ambazo hazitasajiliwa hadi kufikia Desemba kufungwa
:: Serikali, kampuni zote za simu kushirikiana pamoja
:: Usajili kuanza rasmi Julai mosi, lengo kuthibiti uhalifu

Na Debora Sanja

MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), imewataka watumiaji wa simu za mikononi kusajili simu zao kabla ya Desemba, mwaka huu.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Connie Shirima kwa niaba ya Mhandisi wa mamlaka hayo James Kilaba, wakati akiwasilisha mada ya usajili wa kadi za simu kwa wahariri wa vyombo vya habari.

Shirima alisema, kwa wale wote ambao hawatasajili kadi zao za simu, ifikapo Desemba zitafungwa na hawatakuwa na uwezo wa kuzitumia
tena.

“Kazi ya kusajili kadi za simu za mikononi itaanza rasmi Julai mosi, mwaka huu, kwa kuwa wajumbe wote wa mamlaka husika wameshakaa na kujadili ni jinsi gani kadi hizo zitasajiliwa,” alisema Shirima.

Alisema wajumbe wa kamati hiyo ya usajili ni kampuni zote za simu nchini, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka, Idara ya Uhamiaji na TCRA
wenyewe.

Shirima alisema wameamua kushirikisha idara hizo zote, ili kuhakikisha zoezi hilo halikwami kutokana na kuacha kushirikisha idara ambayo ni
muhimu katika usajili huo.

Alisema Tanzania bado haijawa na vitambulisho vya uraia kwa watu wake, lakini vitambulisho mbalimbali vitatumika wakati wa kusajili simu hizo.

“Vitambulisho ambavyo vitatumika katika usajili huo ni kitambulisho cha kazi, leseni ya gari, kitambulisho cha benki, kitambulisho cha kupiga kura, kitambulisho cha bima ya afya, hati ya kusafiria, vitambulisho vya vyuo, vitambulisha vya umoja wa kikundi, na kadi za magari,” alisema Shirima.

Alisema vitambulisho ambavyo vitakuwa havina picha, mteja atatakiwa kupiga picha na kuipeleka kwa ajili ya usajili. Shirima alisema zoezi hilo linawezekana, kwa kuwa kuna nchi nyingi kama vile Afrika ya Kusini na Ufilipino ambako Serikali zimeweza kusajili simu zao za mikononi, japokuwa hawana vitambulisho vya uraia.

Alisema vitendo vya uhalifu wa kutumia simu za mkononi havitakuwapo tena kwa kuwa kila mwenye kadi ya simu atajulikana kutokana na taarifa zake ambazo atakuwa amejaza kabla ya kusajiliwa.

Akizungumzia tatizo la uuzaji wa kadi za simu kiholela, alisema wamiliki wote wa mitandao ya simu watatakiwa kuwasajili wachuuzi wanaouza kadi za simu kwa kuwapa namba maalumu, ambazo zitawezesha kujua mteja amenunua wapi kadi hiyo.

Wale wote watakaokuwa wanauza line za simu barabarani watapewa namba maalumu na fomu ambazo zitamuwezesha mteja kujaza taarifa zake muhimu kabla ya kununua kadi ya simu,” alisema.

Alisema kamati ya usajili imeamua fomu zote atakazojaza mteja kabla ya kununua kadi ya simu zitakuwa zinafanana, ili kuondoa utata ambao unaweza kujitokeza.

Katika fomu hizo, mteja atatakiwa kujaza jina lake kamili, namba yake ya simu, mkoa na wilaya anayotoka, kabila, namba ya kadi ya simu yake na namba ya sehemu ambapo amenunua kadi hiyo.

Vile vile alisema kuna sheria ambayo inaandaliwa kwa ajili ya kuboresha usajili wa simu za mikononi.

Akizungumzia suala la utumiaji wa namba za siri katika kupiga simu, amesema TCRA walishapiga marufuku tangu Machi mosi, mwaka huu.

TCRA imeanza jana kuadhimisha wiki ya Mawasiliano na Habari Jamii Tanzania (WTSD), ambapo jana imeanza na semina kwa wahariri wa vyombo vya habari nchini.

Miongoni mwa mada zilizojadiliwa, ni ujumbe wa mwaka huu wa kuwalinda watoto na utumiaji wa mtandao, shughuli za TCRA na nafasi iliyonayo ya udhibiti, jinsi ya kutumia teknolojia ya kisasa(digital) na usajili wa simu na kadi za simu.

Uzinduzi rasmi wa siku hiyo unafanyika leo katika hoteli ya Ubungo Plaza, ambako mada mbalimbali zitatolewa kujadili jinsi gani ya kumlinda mtoto na matumizi ya mtandao, na mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri wa Sayansi, Mawasiliano na Teknolojia, Profesa Peter Msolla.

CHANZO:
Mtanzania


HII IMEKAA MKAO WA KURA ZA MAONI YA WAUAJI WA ALBINO.KAMA HUJANIELEWA,NAMAANISHA UTARATIBU ULIOZOELEKA WA KUJA NA MAAGIZO YASIYO PRACTICAL.MAMLAKA YA MAWASILIANO (TCRA) INALETA HADITHI ZA KULAZIMISHA KUSAJILI SIMU ZA MIKONONI.SABABU WANAYOONA YA MSINGI KUTOA AMRI HIYO NI KUPUNGUZA UHALIFU.HII NI SABABU DHAIFU KWA VILE KWANZA,UHALIFU ULIKUWAPO HATA KABLA YA UJIO WA MOBILE PHONES MWISHONI MWA MIAKA YA 90,NA TCRA HAWAJAELEZA LINI WALIFANYA UTAFITI ULIOONYESHA KUWA USAJILI WA SIMU ZA MIKONONI UTASAIDIA KUPUNGUZA UHALIFU. WANASEMA ZOEZI KAMA HILO LIMEWEZEKANA AFRIKA KUSINI NA UFILIPINO (SIO KWAMBA LIMEKOMESHA UHALIFU BALI LIMEWEZEKANA PASIPO VITAMBULISHO VYA URAIA)

ETI WANASEMA BAADA YA USAJILI HUO UHALIFU WA KUTUMIA SIMU UTAKOMA?KWA MIFANO IPI HAI?WHAT IF MTU ATANIOMBA SIMU YANGU,KISHA AKAITUMIA KWA SHUGHULI YA UHALIFU PASIPO RIDHAA YANGU?SI YANAKUJA YALEYALE YA KURA ZA MAONI KUHUSU MAUAJI YA ALBINO AMBAPO BAADHI YETU TULIONYA HATARI YA KURA ZA CHUKI?

LAKINI KUNA SUALA LA MUHIMU ZAIDI YA WHETHER MPANGO HUO UTAFANIKIA AU LA,NALO NI RIGHT TO PRIVACY.NASHANGAA MAKUNDI YA HAKI ZA BINADAMU YAMEKUWA KIMYA KUHUSU SUALA HILI.KAMA SUALA NI KUPUNGUZA ( AU KUTOKOMEZA UHALIFU) TAYARI TUNA MAMLAKA KAMA POLISI LENYE JUKUMU HILO NA SIJAWAHI KUSIKIA LIKIDAI KUWA UHALIFU UNAONGEZEKA KWA VILE SIMU HAZIJASAJILIWA.VILEVILE,JESHI HILO LINAPASWA KUWA NA TEKNOLOJIA YA KU-TRACE SIMU SIMU ZINAZOSHUKIWA KUHUSIKA NA UHALIFU.

HII NI VICTIMIZATION OF WATUMIAJI WOTE WA SIMU IN THE SENSE KUWA KILA MTUMIAJI SIMU NI POTENTIAL CRIMINAL.TUKIRUHUSU SUCH ABUSE OF OUR HUMAN RIGHTS INAWEZA KUPELEKEA FURTHER ABUSES KWENYE MAENEO MENGINE KAMA VILE INTERNET.KWA VILE KUNA TOVUTI ZINATUMIA TEKNOHAMA KUFANYA MAMBO YASIYOSTAHILI SIO EXCUSE KWA MAMLAKA HUSIKA KUZI-CRIMINALIZE TOVUTI ZOTE.IN THE SAME LINE OF THINKING,KWA VILE BAADHI YA WAHALIFU HUTUMIA SIMU KATIKA KUTENDA UHALIFU SIO SABABU YA KU-CRIMINALIZE KILA MTUMIAJI WA SIMU.

NA PENGINE CHA MUHIMU ZAIDI NI USALAMA WA HIZO PERSONAL DETAILS ZITAKAZOHITAJIKA WAKATI WA KUKAMILISHA USAJILI WA SIMU.KAMA MITIHANI INAVUJA HUKO NECTA,FEDHA ZINAIBIWA BENKI KUU (NOT MENTIONING KUIBIWA KWA LAPTOP YA IGP OFISINI KWAKE),KWANINI TUSIHOFU KUWA SIKU YA SIKU PERSONAL DETAILS HIZO ZINAWEZA AIDHA KUIBIWA AU KUUZWA? HIVI KWANINI TCRA HAIZUNGUMZII USALAMA WA DATA HIZO,ITAZIHIFADHI KWA MUDA GANI,NA HATUA ZIPI ZITACHUKULIWA PINDI DATA HIZO ZITAKAPOTUMIKA NDIVYO SIVYO?

HIVI TAASISI ZA HAKI ZA BINADAMU HUKO NYUMBANI ZIKO WAPI?AU ZIKO BUSY NA KUOMBA POSHO KWA WAFADHILI FOR PERSONAL PURPOSES?

14 May 2009


From Ms Mariam Savimbi,
Ouagadougou,Burkina Faso.

Dearest one,

Good day,my name is Mariam.J.Savimbi the only daughter of Mr. JANTORE K.SAVIMBI a licensed solid mineral (gold, diamond and cocoa)exporter during his days.

Before the death of my father, he apparently married a woman who became my stepmother because my mother died when i was six years and since then my father took me special than any other person till his point of death, but I discovered that there was some ill-feeling from my stepmother towards me since after the death of my late Dad, since after then I have been badly treated; being forced to undertake work befitting like a servant in my own father's house. When my father died instead of her being in the state of mourns as custom and traditional demanded, she went as much as desired and claimed my father's house properties etc which in future regarded as a possible danger to my live.

Before my father passed away recently, he called to informed me privately that he had a deposit
valued Seven million three hundred thousand USD ($7,300.000.00usd)and a deposit of 350 kilos of 22 carat annuval gold dust for safe keeping in a security company here , he further told me that he intended to move the said funds and gold dust abroad to his foreign associate for investment on my behalf, this properties was acquired from the diamond/gold export contract he secured and executed under the umbrella of the government.

Truly i don't know you but considering my situation and security, couple with an uncontrollable
crisis between me and my stepmother, I discover my life is no more safe here.I therefore confided on your assistance and write with due respect and ask for your kind assistance to please help me and get the funds and the gold moved to your country on my behalf for investment.

Meanwhile I am willing to offer you 15% of the total funds/gold dust as a compensation towards
your assistance.And 5% will also be set aside should in case of any income expenses handled by you during the depositing of the funds into your bank account while the remaining 80 % will be for me and the investment under your care.I have plans to do investment in your country, like real estate, industrial production or any other lucrative investment you bring to my notice in your country.

Please if you are willing to assist me, indicate your interest by sending your response so that I can communicate with you for more details and immediate procedure.

Thanks and waiting for your urgent response.

Yours sincerely.

Mariam Savimbi.


Former Tanzanian beauty queen Mona Lewis, who was dumped from The Apprentice, has admitted that it may have been because she was too boring.The 28-year-old from Kent also defended claims that she had not enjoyed this week's task - to revitalise Margate's tourist industry - because her team chose to attract gay people...continue



TOLEOJIPYA39 TOLEOJIPYA39 JIMMY PHILEMON

12 May 2009


11 May 2009






Read it HERE.


HIVI KARIBUNI,WAZIRI WA NCHI OFISI YA RAIS (MENEJIMENTI NA UTUMISHI WA UMMA),USTAADHA HAWA GHASIA,ALITOA ONYO KALI DHIDI YA WATU WANAOJIHUSISHA NA KILE ALICHOKIITA "WIZI WA NYARAKA ZA SERIKALI".NISINGEPENDA KUREJEA REACTIONS MBALIMBALI ZILIZOTOKANA NA KAULI HIYO LAKINI MMOJA YA SAUTI ZILIZOPINGA VIKALI TAMK HILO LA GHASIA NI MBUNGE WA KARATU NA KATIBU MKUU WA CHADEMA,DR WILBROAD SLAA.MWANASIASA HUYO NGULI WA MAPAMBANO DHIDI YA UFISADI ALIELEZA WAZIWAZI KWAMBA NYARAKA ZINAZOFICHA UFISADI HAZIPASWI KUWEKWA KWENYE KUNDI LA NYARAKA ZA SIRI ZA SERIKALI.DR SLAA ALIELEZA BAYANA KWAMBA PINDI AKILETEWA NYARAKA ZA AINA HIYO ATAZIMIA PASI UOGA KWA VILE NI KWA NJIA HIYO NDIO TUMEFANIKIWA KUBAINI SKANDALI KAMA ZA EPA,RICHMOND NA NYINGINEZO.


NI DHAHIRI TAMKO LA WAZIRI GHASIA LILENGA KUWATISHA WATU KAMA DR SLAA.LAKINI PIA WAZIRI HUYO ALIFANYA HIVYO KWA VILE NI MIONGONI MWA VIONGOZI WA SERIKALI WENYE DHAMANA NA MASUALA YANAYOHUSU IDARA MBALIMBALI ZA SERIKALI.


BILA KUUMAUMA MANENO,HEBU TUJIULIZE: HIVI ROSTAM AZIZ ALIPOITISHA PRESS CONFERENCE YAKE NA KUTOA "USHAHIDI" MBALIMBALI KUPIGILIA MSUMARI HOJA YAKE KUWA REGINALD MENGI (MWENYEKITI MTENDAJI WA MAKAMPUNI YA IPP) NI FISADI NYANGUMI,ALIZIPATAJE NYARAKA MBALIMBALI ZINAZOPASWA KUWA KATIKA HIFADHI YA TAASISI HUSIKA ZA SERIKALI?

ROSTAM SI MTUMISHI WA MAMLAKA YA MAPATO AU MWAJIRIWA KATIKA WIZARA YA FEDHA KIASI CHA KUWA NA "DATA" ALIZOTOA KUHUSU MENGI.NA KWA VILE MAMLAKA HUSIKA ZIMEKUWA KIMYA KUHUSU WAPI MBUNGE HUYO WA IGUNGA ALIPATA NYARAKA HIZO NI WAZI KWAMBA ALIPATIWA KWA RIDHAA YA WAHUSIKA.

WATETEZI WA ROSTAM,KUANZIA WAZIRI SOPHIA SIMBA NA KAPTENI GEORGE MKUCHIKA WAMEKUWA KIMYA KABISA KUKEMEA "HUKUMU" ALIYOTOA ROSTAM DHIDI YA MENGI TOFAUTI NA WALIVYOKURUPUKA MARA BAADA YA KIPENZI CHAO KUTAJWA KUWA NA MENGI KUWA NI FISADI PAPA.BY THE WAY,MENGI SI MTU WA KWANZA KUMTUHUMU ROSTAM KUWA NI FISADI.HIYO NI OPEN SECRET,NA KINACHOKWAZA WATU HAWA KUCHUKULIWA HATUA NI NJAA TU ZA HAO WENYE WAJIBU WA KUFANYA HIVYO ZINAZOKIDHIWA NA JEURI YA FEDHA ZA MAFISADI HAO.

SASA,SIJUI WAZIRI GHASIA ANAWEZA KUTUELEZA NINI KUHUSU WIZI WA NYARAKA ZA SERIKALI ULIOFANYWA NA ROSTAM.NAUITA WIZI KWA VILE ROSTAM SIO TRA,DPP,MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI AU TAASISI YOYOTE YA SERIKALI YENYE DHAMANA YA KUWA NA NYARAKA ZILIZOTUMIWA NA MFANYABIASHARA HUYO KWENYE "KUJENGA KESI" YAKE DHIDI YA MENGI.

SASA NAELEWA KWANINI ROSTAM ANAWEZA KU-WISH ASINGEJIBU HOJA ZA MENGI KWANI WATAPOFIKA MAHAKAMANI ANAPASWA KUULIZWA YEYE ALIKUWA NA NYARAKA HIZO KAMA NANI?ALIZIPATAJE?NA JE KUWA NAZO SIO KOSA (KWA KUREJEA "MKWARA" WA WAZIRI GHASIA?

NA HIYO NI NJE YA TAARIFA ZA KUAMINIKA KUWA NYINGI YA DATA ALIZOTUMIA ROSTAM NI "MAKANJANJA" (FAKE DATA) AMBAPO WAJANJA WA MJINI WALIPOSIKIA KUNA TENDA YA FEDHA NYINGI YA KUWEZESHA KUPATIKANA KWA INCRIMINATING EVIDENCE DHIDI YA MENGI WAKACHANGAMKIA TENDA HIYO LAKINI KATIKA HALI YA UFISADI.WHY NOT,KUMFISADI FISADI NI SAWA KABISA NA KULIPA KWA NOTI BANDIA MANUNUZI YA CHENI ILIYOTENGENEZWA KWA DHAHABU FEKI.


MWISHO,NAPENDA KUSISITIZA KWAMBA SINA CHUKI NA ROSTAM AU MTANZANIA YEYOTE MWENYE ASILI YA NJE YA NCHI.ILA SIFICHI UKWELI KWAMBA NINA ZAIDI YA CHUKI,HASIRA,DUA BAYA (NA MENGINE NISIYOWEZA KUTAJA HAPA) DHIDI MAFISADI.UTETEZI WA KIPUUZI WA MAFISADI UMEKUWA KWENYE VITU KAMA RANGI,DINI,KABILA,NK.MTAKUMBUKA MKURUGENZI WA IPC,EMMANUEL OLE NAIKO ALIZONGWA KUHUSU KWANINI ALITOA KIBALI CHA UWEKEZAJI KWA KAMPUNI YA KITAPELI YA RCHMOND,KIMBILIO LAKE KUU LILIKUWA UKABILA.ETI "NAANDAMWA KWA VILE NATOKA ENEO MOJA NA LOWASSA"!

LEO HII AKINA ROSTAM,MANJI,SOMAIYA,JEETU NA SUBASH WANATAKA KUTUAMINISHA KUWA TUHUMA DHIDI YAO ZINACHANGIWA NA "UTANZANIA" WAO WENYE ASILI YA NJE YA NCHI.HUU NI UTETEZI MUFILIS NA NI WA KIFISADI KAMA WANAVYOTUHUMIWA.HIVI WANATAKA KUTUAMBIA KUWA TULIPOPAMBANA NA MKOLONI,MJERUMANI NA MWINGEREZA TULIKUWA WABAGUZI WA RANGI?


AH,HAPA SIJUI NISEMEJE.HEBU SOMA KWANZA HABARI KAMILI HAPA CHINI KISHA TUJADILI.

Kompyuta za IGP, Mkemia Mkuu zaibwa
• Ni katika mazingira ya kutatanisha

na Deogratius Temba

WAKATI kesi ya watuhumiwa 11, walioiba kompyuta katika ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP), ikiendelea imebainika Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP), Said Mwema, naye ameibiwa kompyuta ndogo (Laptop).

Wiki mbili baada ya tukio la wizi wa kompyuta za IGP Mwema, Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali, nayo iliibiwa kompyuta ya mezani ambayo inasadikika ilikuwa na kumbukumbu nyingi ambazo hazijabainishwa zinahusiana na mambo gani.

Uchunguzi uliofanywa na Tanzania Daima Jumapili, kwa wiki kadhaa sasa umebaini kuwa kumekuwapo kwa wasiwasi mkubwa wa kuibwa kwa nyaraka na vifaa mbalimbali katika ofisi za viongozi wakubwa wa serikali akiwemo Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Mwanasheria Mkuu wa serikali (AG).

Chanzo kimoja kimelidokeza Tanzania Daima Jumapili, uchunguzi wa wizi wa kompyuta hizo mpaka sasa unaendelea ili kuwabaini wahalifu waliotenda tukio hilo na kujua walikuwa na lengo gani.

Chanzo hicho kimebainisha kuwa kikosi maalum kimeundwa kufuatilia wizi huo ambao umeonekana kuanza kushamiri katika ofisi nyeti za serikali hasa katika kipindi hiki ambacho kumekuwa na tuhuma nyingi za ufisadi na matumizi mabaya ya madaraka yanayofanywa na viongozi.

Taarifa za ndani zinadai kuwa kompyuta ya IGP iliibwa mezani kwake majira ya mchana siku ya Ijumaa wakati mkuu huyo akiwa amekwenda msikitini kuswali. Katika meza hiyo kulikuwapo na simu za mkononi na kiasi cha fedha kinachodaiwa kuwa sh milioni saba, lakini ni kompyuta pekee ndiyo iliyoibwa.

Habari zaidi zinabainisha kuwa IGP aliporudi alishangaa kutoikuta kompyuta hiyo ilhali simu na fedha vilikuwapo kama alivyoviacha, baada ya kubaini wizi huo zilichukuliwa alama maalumu za vidole zikaonekana ni za mlinzi wake wa karibu (Board guard), ambaye inadaiwa huwa na kawaida ya kuingia mara kwa mara katika ofisi pasi na kutiliwa shaka.

Chanzo chetu cha habari kilieleza kuwa uchunguzi ulipofanyika ndani ya jeshi la polisi ilibainika kuwa kuna afisa wa jeshi hilo, mwenye cheo cha mkaguzi, ndiye aliyeichukua kompyuta hiyo, ambaye hadi sasa anahojiwa ili kulisaidia jeshi hilo liweze kupata chanzo cha uhalifu huo.

Aidha, taarifa zinasema kuwa aliyeichukua kompyuta hiyo, inadaiwa, amelipwa sh mil. 10 kama ujira wake kwa kazi hiyo. Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai nchini (DCI), Robert Manumba, alipoulizwa juu ya hatua ambazo jeshi hilo linazichukua dhidi ya wizi huo ambao unaonekana wazi kulenga kuiba nyaraka muhimu za serikali, alisema huo ni wizi kama mwingine kwani wezi hao hawakulenga kuiba kompyuta hizo kwa lengo maalumu.

“ Siyo kwamba wizi haufanyiki, unafanyika sana; mara hii umetokea katika ofisi nyeti inayomhusisha mkuu wa jeshi la polisi, wizi huo umefanyika tu kama unavyoweza kufanyika nyumbani kwako, haukulenga ofisi hizi tu,” alisema DCI Manumba.

Pamoja na kusema hivyo, alilithibitishia Tanzania Daima Jumapili kuwa hatua za uchunguzi zinaendelea ili kuwabaini wahalifu hao ambao wamefikia hatua mbaya.

“Tanzania hatuna wizi wa kulenga ofisi maalumu za serikali, ndiyo maana unapotokea unawashangaza watu wengi lakini tumejipanga vilivyo katika uchunguzi kuhakikisha tunawakamata wale wote waliohusika,” alisema Manumba na kuongeza:

“Nakwambia ukweli, wewe umekuja kuniuliza kwa sababu wizi umetokea katika ofisi hii, lakini matukio kama haya yanatokea pia katika nyumba za watu binafsi, hata siwezi kukuhesabia idadi ya kesi hizo, tusiwashtue watu waamini kuwa ulilengwa kwa kazi hiyo.”

Manumba alizidi kusisitiza kuwa wizi upo dunia nzima na wanaweza kuiba mahali popote kama wataona kuna kitu, lakini hakuna wizi uliopangwa kulenga katika ofisi hizo za IGP, DPP , au kwa Mkemia Mkuu wa Serikali.

Taarifa zimeeleza kuwa kompyuta iliyoibwa katika Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali ilikuwa kubwa ya mezani (PC), ambayo ilichukuliwa kupitia dirishani katika mazingira ya kutatanisha wakati milango ikiwa imefungwa.

Chanzo chetu kutoka ndani ya ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali, kimeeleza kuwa kompyuta hiyo ilikuwa ikitumika ndani ya ofisi ya Mkemia Mkuu, ambapo bado haijajulikana na nyaraka gani muhimu zilikuwa zimehifadhiwa humo.

“Ni kweli kompyuta iliibwa hapa, milango imefungwa tumefika tukaelezwa kuwa kompyuta ya msaidizi wa bosi wetu haionekani wakati milango ilikuwa imefungwa,” alisema mmoja wa watumishi wa ofisi hiyo ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini.

Aidha kuhusu tukio hilo lililotokea katika ofisi hizo zilizoko karibu na Taasisi ya Saratani, Ocean Road, imeelezwa kuwa bado uchunguzi unaendelea ili kubaini mtu aliyehusika kuiba kompyuta hiyo kama ni mmoja wa wafanyakazi au la.

Kutokea kwa wizi huo kunawafanya baadhi ya watu kuwa na wasiwasi kuwa kuna njama zimepangwa na baadhi ya watu kupoteza vielelezo au ushahidi wa tuhuma au kesi mbalimbali zinazowakabili.

Wasiwasi huo umechangiwa zaidi na matukio ya hivi karibuni ya kupandishwa mahakamani kwa baadhi ya vigogo wa serikali, wafanyabiashara na watu binafsi kwa wizi au matumizi mabaya ya madaraka.

Mpaka sasa watu 11 wameshapandishwa katika Mahakama ya Kisutu jijini Dar es salaam kujibu tuhuma za kuiba kompyuta katika ofisi ya Mkurugeni wa Mashtaka Nchini (DPP).

JANA NILIWEKA HABARI YA KIBAKA ALIYEFANIKIWA KUIBA UA IKULU.JUZIJUZI,USTAADH MMOJA ALIDIRIKI KUMZABA KIBAO RAIS MSTAAFU ALI HASSAN MWINYI.SIKU KADHAA ZILIZOPITA,TULISIKIA KUWA DPP AMEIBIWA LAPTOP YAKE.LEO TENA TUNASIKIA IGP NAE KALAMBWA KOMPYUTA.MATUKIO YOTE HAYA YANAASHIRIA KWAMBA TUNARUKARUKA KWENYE UTANDO WA BUIBUI ILHALI CHINI YA UTANDO HUO KUNA BWAWA LA TINDIKALI.

SWALI LA MSINGI KUJIULIZA KUHUSIANA NA WIZI HUO WA LAPTOP YA IGP NI KWANINI HABARI HIYO IMEVUJA KIRAHISI HIVYO?NI HABARI YA FEDHEHA AMBAYO KWA MAZOWEA TULIYONAYO YA "WAKUBWA HUWA HAWAKOSEI" INGEDHIBITIWA KWA NGUVU ZOTE.NIITE CONSPIRANCY THEORIST,LAKINI I STRONGLY SMELL SOMETHING FISHY.IT'S EITHER KUNA MTU (HUYO ANAYEDAIWA KULIPA MILIONI 10 BAADA YA KUFANIKIWA "WIZI" HUO) ANAYETAFUTWA ILI AWE IMPLICATED AU KUNA EVIDENCE INAPOTEZWA KWA EXCUSE YA "ILIKUWA NDANI YA LAPTOP ILIYOIBIWA."KATIKA ZAMA HIZI ZA UFISADI,LOLOTE KATI YA HIZO CONSPIRANCY THEORIES ZANGU INAWEZA KUWA SAHIHI.


Na Frederick Katulanda, Busanda

WAZIRI wa Nishati na Madini, William Ngeleja jana alijikuta kwenye wakati mgumu baada ya kuzongwa na kundi la wananchi waliomuhoji juu ya ahadi zake za umeme alipowasili katika mji wa Katoro wilayani Geita.

Tukio hilo mithili ya mdahalo lilitokea kati ya majira ya ya saa 9:30 hadi saa 10:15 muda mfupi tu baada ya Ngeleja kuwasili Busanda akitokea Mwanza.

Maswali yalianza baada ya Waziri Ngeleja kusalimiana na wananchi hao na akajibiwa kwa kuonyeshwa alama za vidole viwili.

Hali hiyo ilimfanya waziri huyo kuwauliza wananchi hao sababu za kuichukia CCM wakati imekuwa ikijitahidi kuwaletea maendeleo na ndipo walipoanza kumuuliza maswali huku akiyajibu wakati fulani kugeuka mabishano.

"Hatuwezi kuwashangilia nyinyi... mmetuahidi umeme siku nyingi na hatuuoni, leo mnakuja kutuambia nini. Alikuja hapa sijui (Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Adam) Malima akasema umeme utakuja, lakini wapi hatujaona lolote mpaka leo," alisema mwananchi mmoja.

Ngeleja alipotaka kujibu, mwananchi mwingine alidakia kusema: "Hata kwenye machimbo mmekuwa mkitunyang'anya maeneo yetu na kuwapa wawekezaji. Sisi mnatuona hatufai kama vile ni wakimbizi ndani ya nchi yetu."

Ngeleja alilazimika kuwatuliza na kuwaomba wapunguze maswali ili ajibu swali moja baada ya jingine, lakini kila mtu akataka kumuuliza swali na kukawa na msuguano kati yake na wananchi.

Alianza kujibu kwa kusema kuwa serikali ipo mbioni na kwamba kinachofanyika sasa ni kufuata taratibu kwa sababu mchakato wa suala hilo hauwezi kumalizika siku moja, hivyo akawaomba wawe watulivu wakati mchakato ukiendelea.

Ngeleja alidai kuwa suala lao kuhusu umeme liko katika hatua ya kuridhisha na kwamba wanapaswa kutambua utaratibu wa kushughulikia miradi ya serikali umekuwa ukifanyika kwa hatua.

Majibu hayo yalipingwa na wananchi ambao walimwambia wamekuwa wakidanganywa kama watoto kwa sababu ya kutaka kura na wakishapata, hutoweka.

"Sikiliza basi nikujibu, wewe naona umetanguliza ushabiki tuu. Naomba unisikilize. Ni kweli tulipowaahidi umeme tulidhani mchakato ungekamilika mapema, lakini kuna mambo yametukwamisha, tunaomba mtuvumulie," alisema huku wananchi hao wakiendeleza maswali.

Wakati wakiendelea na mjadala huo, lilipita gari la mgombea CCM wa kiti cha ubunge cha Busanda, Lolensia Bukwimba na mara moja wananchi hao wakageuka na kuanza kuzomea msafara.

Wakati wakiendelea kuzomea ndipo Ngeleja alipopata mwanya na dereva wake akawasha gari na kuondoka.

Waziri Ngeleja alitaja mlolongo wa maeneo ambayo alisema mengi yatapata umeme kabla ya kumalizika kwa mwaka huu, lakini mkakati wao wa umeme ulitibuliwa baada ya Bunge kukataa kuinunua mitambo ya umeme wa dharura ya Dowans Tanzania Limited.

CCM imekuwa na wakati mgumu tangu kuanza kwa kampeni za ubunge wa jimbo hilo lililoachwa wazi na Faustin Kabuzi Rwilomba ambaye alifariki akiwa nchini India alikoenda kutibiwa
.

CHANZO: Mwananchi

IWAPO KUNA LOLOTE LA KUJIFUNZA KATIKA KAMPENI HIZI ZA UCHAGUZI MDOGO WA JIMBO LA BUSANDA BASI NI NAMNA CCM ILIVYO KICHWA NGUMU KUELEWA SOMO.THING IS,WAMESHAHADAA WAPIGA KURA KIASI CHA KUTOSHA KWA AHADI HEWA,HIVYO KUREJEA TENA AHADI HIZOHIZO AMBAZO HAWAJAZITEKELEZA NI MITHILI YA,ASHAKUM SI MATUSI,KUMTONGOZA MTALAKA WAKO.

PENGINE JINGINE NI NAMNA CHAMA HIVYO KISIVYO SERIOUS NA USTAWI WA WANANCHI.WHY?BADALA YA KUREJEA AHADI HIZO AMBAZO HAZIJATEKELEZWA,CHAMA HICHO KWANZA KILIPASWA KUWAOMBA RADHI WAPIGA KURA KWA KUSHINDWA KUTEKELEZA AHADI HIZO HADI SASA,NA ANGALAU BAADA YA HAPO KINGEWEZA KUJARIBU KETE YA KUREJEA AHADI HIZO.NASEMA THAT IS INDICATIVE OF LACK OF SERIOUSNESS KWA VILE CCM INAAMINI KUWA KAMA ILIKUWA IKITOA LOTS OF EMPTY PROMISES FOR AGES NA WAGOMBEA WAKE WAMEENDELEA KUCHAGULIWA,BADO KUNA IMANI KUWA SUCH A RISKY STRATEGY COULD WORK AGAIN AND AGAIN.

CCM HAIDHANI KUWA IMAGE YAKE IKO SEVERELY TARNISHED NA USWAHIBA WAKE NA UFISADI/MAFISADI.INAENDELEA KUAMINI KUWA SHUTUMA DHIDI YAKE KWAMBA NI KICHAKA NA HIFADHI YA MAFISADI NA ZA WATOVU WA NIDHAMU WACHACHE KAMA SIE LAKINI SIO KWAMBA KELELE ZETU NI UWAKILISHI TU WA VILIO VYA MAMILIONI YA WATANZANIA WALIOCHOKA KUFANYWA WAJINGA.

HIVI KIONGOZI MWENYE BUSARA ANAWEZA KUDIRIKI KU-BRING UP ISHU ZA DOWANS KWENYE BY-ELECTION KAMA YA BUSANDA?CAN'T BLAME NGELEJA KWA KUWA KWA YEYE NA VIGOGO WENZIE WA CCM,EQUATION YA DOWANS=RICHMOND HAIJAMWINGIA KICHWANI.

10 May 2009

PICHANI,NI MBUNGE WA IGUNGA,ROSTAM AZIZ,AKIKABIDHI KINACHODAIWA KUWA DOSSIER LENYE TUHUMA DHIDI YA MFANYABIASHARA RAGINALDMENGI.ANAYEKABIDHIWA NI AFISA UCHUNGUZI WA TAKUKURU GWAKISA.Picha hii ni kwa mujibu wa gazeti la The African.

HUU NI NI UPUUZI.YAANI HAINGII AKILINI HATA KIDOGO.JAMANI,HIVI LINI MMEWAHI KUONA TAKUKURU WAKIKABIDHIWA USHAHIDI/TUHUMA MBELE YA VYOMBO VYA HABARI AS SEEN IN THE PICTURE ABOVE?

HUYU ROSTAM AMEKUWA MITHILI YA MUNGU MTU: ALIPOTAJWA TU NA MENGI,MAWAZIRI WAZIMA NA BUSARA ZAO (SOPHIA SIMBA NA KAPTENI MKUCHIKA) WAKALIPUKA KUMTETEA (JAPO SASA WAMEKAA KIMYA ROSTAM ALIPORUDIA KILEKILE ALICHOFANYA MENGI).KISHA TAKUKURU NAO KATIKA HALI INAYOONYESHA NAMNA GANI TAASISI HIYO NI WABABAISHAJI WA DARAJA LA JUU WAKAANDAA MITHILI YA PRESS CONFERENCE YA KUMPOKEA ROSTAM NA KINACHODAIWA KUWA NI USHAHIDI WAKE DHIDI YA MENGI (JAPO KUNA MADAI KUWA WAJANJA WAMEMWINGIZA MJINI KWA KUMUUZIA "CHENI BANDIA"-ISOMEKE DATA FEKI).

HAWA TAKUKURU NI WAZEMBE ZAIDI YA WAZEMBE.HIVI UBABAIKAJI KAMA HUO WALIOFANYA KWA ROSTAM WANGEUELEKEZA KWA KAGODA SI TUNGEPIGA HATUA FLANI?AU WANGEKUWA "FASTA" NAMNA HIYO KATIKA,SIO KUITETEA BALI KUICHUNGUZA IPASAVYO KAMPUNI YA RICHMOND,KWA HAKIKA TUSINGEKUWA HAPA TULIPO SASA.

MBONA WENZETU MNAJIDHALILISHA KIASI HICHO?NI HIZO FEDHA ZA ROSTAM AU NJAA ZENU?THIS IS MORE THAN TOO MUCH.IT'S ABSURD,CRAZY AND UTTERLY NONSENSE.


A woman accused of tormenting her neighbours with her noisy love-making has appeared in court. Skip related content

Caroline Cartwright, 48, was remanded in custody until May 5 charged with three breaches of her Asbo in ten days.

Magistrates in Sunderland slapped her with a four-year order on April 17, banning her from "making excessive noise" anywhere in England.

But Houghton le Spring Magistrates' Court heard that police arrested her on April 18, April 22 and April 26 after neighbours complained she was flouting the ban with the help of husband Steve.

Prosecutor Claire Ward said there were complaints of early morning shouting, moaning, groaning and the sound of a bed banging against the wall. Cartwright was arrested on Sunday and charged with three counts of breaching her Asbo.

Cartwright, of Hall Road, Concord, Washington, Tyne and Wear, whose husband sat in the public gallery, elected trial by jury and her case will be transferred to Newcastle Crown Court.

A bail application from defence solicitor Peter Lothian was refused.

Cartwright was remanded in custody and ordered to appear via video link before Sunderland Magistrates' Court on May 5.

On April 17, she was convicted for five breaches of an abatement notice and fined a total of £515.
Magistrates also imposed the Asbo, banning her from making excessive noise, knocking, shouting, screaming or vocalisation that can be heard in neighbouring properties or outside the house, and playing loud music.


SOURCE: ITN

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.