28 Feb 2012

Nigerian state governor funded international playboy lifestyle with £50million fraud as he rose from humble roots working in London DIY store

  • James Ibori bought a portfolio of luxury London homes and a fleet of armoured Range Rovers
  • Fraudster may have stolen $250million from Nigerian coffers as he rose through the ranks
  • He spent £15,000 in two-day stay at London's The lanesborough hotel
  • He owned SEVEN properties in Britain
  • Ibori, 49, siphoned off millions by inflating state contracts
Last updated at 11:28 PM on 27th February 2012

His rise from DIY store worker to international playboy with a £250million fortune is the stuff of dreams.
A few years after quitting his £5,000-a-year job as a cashier for Wickes, James Ibori had become one of Nigeria's most influential and richest politicians.
He wasted no time spending his new-found wealth on luxury homes, top-of-the-range cars, five-star travel and fees at exclusive boarding schools.
Playboy lifestyle: James Ibori, 49, admitted a fraud totalling more than £50million. The former Nigerian state governor had a fleet of cars and six luxury properties in Britain
Playboy lifestyle: James Ibori, 49, admitted a fraud totalling more than £50million. The former Nigerian state governor had a fleet of cars and six luxury properties in Britain
But yesterday the 49-year-old stood shame-faced in the dock of London's Southwark Court as he admitted stealing tens of millions of pounds from the oil-rich state he governed in Nigeria. Scotland Yard detectives believe his fraud could exceed £250million.
He was on trial in the UK because much of the stolen money was laundered through his London office.
Ibori moved from Nigeria to West London in the late 1980s and was found guilty of stealing goods from the Wickes store he worked at in Ruislip in 1990.
 


A year later he was convicted of handling a stolen credit card. He moved back to Nigeria and worked for its president, Sani Abacha, as a policy consultant.
Rising quickly through the ranks of the ruling People's Democratic Party, he was voted governor of Delta State in 1999, winning re-election four years later.
In power, he systematically stole from the public purse, taking kickbacks and transferring state funds to his own bank accounts around the world.
Luxury: Property in Hampstead bought by Ibori for £2.2million in cash in 2001
Luxury: Exclusive home that Ibori bought in Hampstead, north London, with £2.2million in cash in 2001
He was helped by family members, including his wife Theresa, sister Christine Ibori-Ibie, his mistress Udoamaka Oniugbo, and Mayfair lawyer Bhadresh Gohil.
A massive police investigation into Ibori's activities revealed he had bought six properties in London, including a six-bedroom house with indoor pool in Hampstead for £2.2million and a flat opposite the nearby Abbey Road recording studios.
There was also a property in Dorset, a £3.2million mansion in South Africa and further real estate in Nigeria.
Extravagant: Ibori, 49, owned an apartment in this block on Abbey Road, London, opposite the famous music studios
Extravagant: Ibori, 49, owned an apartment in this block on Abbey Road, London, opposite the famous music studios
Fleet of cars: The former Nigerian state governor owned a number of cars including this Bentley Continental worth in the region of £150,000
Fleet of cars: The former Nigerian state governor owned a number of cars including this Bentley Continental worth in the region of £150,000
He owned a fleet of armoured Range Rovers costing £600,000 and a £120,000 Bentley. On one of his trips to London he bought a Mercedes Maybach for more than £300,000 at a dealer on Park Lane and immediately shipped it to South Africa.
He bought a private jet for £12million, spent £126,000 a month on his credit cards and ran up a £15,000 bill for a two-day stay at the Lanesborough hotel in London.
Prosecutor Sasha Wass told the court Ibori concealed his UK criminal record, which would have excluded him from office in Nigeria.
Extraordinary extravagance: James Ibori owned a fleet of armoured Range Rovers - including this one - bought with the proceeds of his £50million fraud
Extraordinary extravagance: James Ibori owned a fleet of armoured Range Rovers - including this one - bought with the proceeds of his £50million fraud
Large home: James Ibori's home in Abuja, Nigeria. Today he was facing a jail sentence after admitting a £50million fraud
Large home: James Ibori's home in Abuja, Nigeria. Today he was facing a jail sentence after admitting a £50million fraud
'He was never the legitimate governor and there was effectively a thief in government house,' Miss Wass said. 'As the pretender of that public office, he was able to plunder Delta State's wealth and hand out patronage.'
The court heard Ibori abused his position to award contracts to his associates including his sister and his mistress.
Scotland Yard began its investigation into Ibori after officers found two computer hard drives in his London office that revealed his criminality.
Fraudsters: Solicitor Bhadresh Gohil and James Ibori's wife Theresa who have already been convicted of money laundering
Fraudsters: Solicitor Bhadresh Gohil and James Ibori's wife Theresa who have already been convicted of money laundering
Guilty: Ibori's sister Christine Ibori-Idie and his mistress Udoamaka Okoronkwo who have both being found guilty of money laundering
Guilty: Ibori's sister Christine Ibori-Idie and his mistress Udoamaka Okoronkwo who have both being found guilty of money laundering
He was arrested by the Nigerian Economic and Financial Crimes Commission in December 2007, but two years later a court in his home town, Asaba, dismissed the charges saying there was not enough evidence.
When the case was reopened by Nigerian authorities in April 2010, Ibori fled to Dubai where he was detained at the request of the Metropolitan Police and extradited to the UK last April.
In a packed courtroom Ibori, dressed in a dark grey suit and black shirt, appeared in the dock to enter ten guilty pleas to fraud, money laundering and conspiracy on what was due to be the first day of a 12-week trial.
Luxury: Property in Lagos
Property: Kenton, north-west London
Luxury: Homes he owned in Lagos, Nigeria, and Kenton, north-west London
One of Christine Ibori-Ibie's London properties
One of Udoamaka Onuigbo's London properties
Homes: An apartment owned by Ibori's sister Christine Ibori-Ibie in Brent, north-west London (left) and a London property (right) owned by his mistress Udoamaka Onuigbo
His wife, his mistress and his sister were all jailed for five years each for money laundering offences following earlier trials.
Last March, Gohil, 46, and described as Ibori's London-based lawyer, was jailed for seven years for his role in the scam.
Attempts will be made to confiscate as much of Ibori's money and assets as possible so that they can be returned to Nigeria.
The Met's Detective Inspector Paul Whatmore said: 'It is always rewarding for anyone working on a proceeds of corruption case to know that the stolen funds they identify will eventually be returned to some of the poorest and most vulnerable people in the world.'
Ibori will be sentenced on April 16 and 17.
Luxury: One of Udoamaka Onuigbo's London properties
James Ibori's property in the West Country Bought in 2005 for £311,000
Fraud: A flat owned by Udoamaka Onuigbo, Ibori's mistress, in central London (left) and a property he bought in Shaftesbury, Dorset, for £311,000 in 2005 (right)


SOURCE: Daily Mail

27 Feb 2012


kATUNI KWA HISANI YA kING kINYA NA gLOBAL PUBLISHERS.

26 Feb 2012




Song Push Dem
Artist:Jahson
Producer:Washingtone in Uganda


Kwa Waafrika wengi,na pengine kwingineko ulimwenguni,Wanigeria wanatamba kwa sifa kuu mbili;moja mbaya  na nyingine nzuri.Mbaya ni tabia yao ya utapeli ambapo ni bora kulala na chatu mwinye njaa kuliko kumwamini Mpopo.Wenye uzoefu nao wanajua ninamaanisha nini.Sifa yao nzuri-hasa kwa wanaume ni kutamba katika soka takriban kila kona ya dunia.Inayoambatana na hiyo ni mfaniko makubwa waliyonayo wengi wao-hasa nje ya nchi (usiulize wameyapataje).

Katika hili la mafanikio,juzi juzi tu tumesikia wanamuziki kadhaa wa Kipopo wakivamia anga za muziki nchini Marekani ambapo tayari majina makubwa kama Snoop Dogg na Akon wameshafanya kazi nao.D'Banj kwa sasa anafanya kazi kwenye lebo ya G.O.O.D Music ya Kanye West



Kwa upande mwingine,wanamuziki maarufu wa Kinigeria P.Square, 2Face Idibia na Whizkid wamesaini kwenye lebo ya Konvict ya Akon.



Na wiki hii,gazeti maarufu la nchini Marekani la New York Times lina makala ndefu kuhusu kiwanda cha filamu za Nigeria kinachojulikana kama Nollywood.Unaweza kusoma makala hiyo ndefu HAPA.

Maendeleo haya ya wasanii wa kipopo yanaweza kuwa changamoto kubwa kwa wasanii wetu huko nyumbani.Japo kuna dalili kidogo za kutia matumaini baada ya wasanii AY na Jay Mo kushirikiana na wasanii wa kimataifa,kimsingi wengi wa wasanii wetu wanaendelea kutafsiri mafanikio kwa kigezo cha umaarufu ndani ya Tanzania (na kidogo kwa Afika Mashariki) na kuendekeza zaidi shoo za hapa na pale.




Ifuatayo ni taarifa niliyotumiwa kutoka kundi la VINEGA kuhusu maafikiano yalifikiwa hivi karibuni kati ya Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi (a.k.a SUGU) na mmoja wa Wakurugenzi wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba.Ninaomba kuiwasilisha kama ilivyo:


Tamko La Vinega Juu Ya Makubaliano Ya Sugu Na Ruge

25 Feb 2012

24 Feb 2012

First Man of Finland caught gawping at Danish princess's breasts

The husband of Finland's president was caught on camera casting an admiring glance at the cleavage of Princess Mary of Denmark.






Pentti Arajarvi, Finland's "first gentleman", cast a glance as he sat next to the princess during a state dinner hosted by her mother-in-law, Queen Margrethe of Denmark.
As all eyes turned towards one of the evening's many speeches, Mr Arajavi's roamed down the neckline of the 43-year-old princess.
When she turned to face him, his gaze jerked upward and for a few awkward moments he pretended to be admiring the ceiling of the Amalienborg Palace in Copenhagen.
An alarmed Princess Mary raised a protective hand over her neckline as Mr Arajavi, 63, continued to squint upwards.
The incident provoked a scathing reaction in the Danish press and is unlikely to do much for the country's relationship with neighbouring Finland, which is governed by Mr Arajavi's wife, Tarja Halonen.
It carries echoes of the 2009 G8 summit in Italy when Nicolas Sarkozy was accused of leering at the figure of a shapely Brazilian woman.


SOURCE: Daily Telegraph

23 Feb 2012


Tamko la Mbunge wa Ubungo kupitia Chadema,Mheshimiwa John Mnyika kuhusu tatizo za upatikanaji wa maji jijini Dares Salaam na ubabaishaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka (Dawasco):


THURSDAY, FEBRUARY 23, 2012


DAWASCO imekiuka mikataba; hatua za haraka zinahitajika kuboresha upatikanaji wa maji DSM

Kampuni ya Maji Safi na Maji Taka (DAWASCO) imekiuka mikataba miwili muhimu inayoongoza kazi zake na kusababisha matatizo ya maji katika Jiji la Dar es Salaam ikiwemo maeneo mbalimbali ya Jimbo la Ubungo.


Imenibidi nitoe taarifa hii kwa umma kwa nilitumia taratibu za kawaida za kiofisi tarehe 14 Februari 2012 kuiandikia barua DAWASCO kuchukua hatua kuhusu tatizo la kutozingatiwa kwa ratiba ya mgawo wa maji katika Jiji la Dar es salaam hali ambayo imesababisha kero ya maji katika maeneo mbalimbali ya jimbo la Ubungo.


Hata hivyo DAWASCO haikujibu barua husika kueleza hatua ambazo imechukua, hivyo natoa mwito wa wazi wa siku tatu kwa DAWASCO kufanya ukaguzi wa mtandao wa maji na kurekebisha kasoro zilizopo na kutoa taarifa kwa umma kuhusu matitizo ya maji yanayoendelea katika maeneo mengi ya Jiji la Dar es salaam ikiwemo katika Jimbo la Ubungo. 


Kazi ya mbunge kwa mujibu wa katiba ni kuwawakilisha wananchi, kutunga sheria na kuisimamia serikali hivyo nakusudia kuchukua hatua zaidi za kibunge dhidi ya DAWASCO iwapo haitazingatia masharti ya mikataba husika na kushughulikia matatizo ya maji yanayoendelea hivi sasa katika jiji la Dar es salaam ikiwemo katika Jimbo la Ubungo.


Ikumbukwe kuwa DAWASCO ni shirika la umma lililoundwa kwa tangazo la Serikali nambari 139 la tarehe 20 Mei 2005 kwa mujibu wa Sheria ya Mashirika ya Umma ya mwaka 1992.


Tarehe 1 Julai 2005 DAWASCO ilipewa mkataba wa ukodishaji (lease agreement) na DAWASA ambao unaitaka DAWASCO kuendesha miundombinu ya maji na kuhakikisha matengenezo ya mtandao wa maji katika jiji la Dar es salaam.


Aidha, katika kutekeleza mkataba huo DAWASCO inapaswa kuzingatia mkataba wa huduma kwa wateja (Client Service Charter) ambao unaitaka DAWASCO kushughulikia kwa muda maalum malalamiko ya wateja na kutoa taarifa kwa umma kila panapokuwa na matatizo ya maji.


Kwa mujibu wa mkataba wa huduma kwa wateja DAWASCO inapaswa kushughulia malalamiko ya wateja na kuyajibu ndani ya siku tano na iwapo matatizo yaliyopo yanahitaji hatua za kiufundi; DAWASCO inatakiwa kushughulikia matatizo hayo ndani ya siku 30.


Kuanzia mwishoni mwa mwezi Disemba 2011 mara baada ya maafa ya mafuriko katika Mkoa wa Dar es salaam mpaka leo tarehe 22 Februari 2012 nimepokea malalamiko mbalimbali toka kwa wananchi kuwa hali ya upatikanaji wa maji katika kata mbalimbali za Jimbo la Ubungo sio nzuri kama ilivyokuwa baada ya hatua ambazo tulichukua kwa nyakati mbalimbali kuanzia Januari 2011 mpaka Septemba 2011.


Itakumbukwa kwamba tarehe 5 mwezi Septemba 2011 nilifanya maandamano ya kwenda DAWASCO nikiwa na wawakilishi wa wananchi wa kata mbalimbali za Jimbo la Ubungo ambapo tulifanya mkutano na Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASCO. 


Kufuatia mkutano huo DAWASCO ilichukua hatua mbalimbali ambazo ziliboresha mgawo wa maji katika maeneo kadhaa ya Jimbo la Ubungo kabla ya ratiba ya mgawo kuvurugika kufuatia mafuriko yaliyokumba mkoa wa Dar es salaam.


Hata hivyo, baada ya mafuriko hayo DAWASCO haikuchukua hatua zinazostahili kwa wakati na kuachia kurejea tena kwa mtandao haramu wa biashara ya maji wenye kuhujumu wananchi hususan wa kipato cha chini katika Jiji la Dar es salaam ikiwemo katika maeneo mbalimbali ya Jimbo la Ubungo.


Hivyo, bodi ya wakurugenzi ya DAWASCO chini ya uenyekiti wa Mhandisi Suleiman Said Suleiman na Mtendaji Mkuu wa kampuni Jackson Midala wanapaswa kurekebisha kwa haraka mfumo mzima wa ufuatiliaji wa DAWASCO kuwezesha ukaguzi wa ufanisi wa mtandao mzima wa maji.


Katika kipindi hiki cha matatizo makubwa ya maji katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es salaam ikiwemo katika kata mbalimbali za Jimbo la Ubungo DAWASCO iache kuwatumia wafanyakazi wanaohusika na ukaguzi kufanya kazi tofauti za kusoma mita na kugawa Ankara badala yake wafanyakazi tajwa wafanye ufuatiliaji wa dharura wa ufanisi wa mtandao mzima wa maji katika maeneo mbalimbali.


Baadhi ya maeneo ambayo yanapaswa kutembelewa ni kata za Makuburi, Kimara, Saranga, Mbezi Luis, Msigani, Kwembe, Goba, Kibamba, Sinza, Makurumla, Mabibo, Manzese, Ubungo na Mburahati. 


Kwa upande mwingine, kwa kuwa mkataba wa huduma kwa wateja unatoa haki kwa wateja wa DAWASCO lakini pia unaeleza wajibu; natoa mwito kwa wananchi katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es salaam kutimiza wajibu wa kuwaelekeza wakaguzi husika mitaa yenye matatizo katika mtandao wa maji ili hatua ziweze kuchukuliwa.


Mkataba huo unawataka wateja wa DAWASCO kutoa taarifa kuhusu uharibifu wa miundombinu, wizi wa maji na kuhusu matatizo ya maji hivyo wananchi watoe taarifa husika na kufuatilia wakaguzi kufika maeneo yao kwa kupiga nambari ya bure 0225500240 au 0762979627 za DAWASCO makao makuu.


Pia, wananchi wanaweza kuwasilisha kero za maji kwa ofisi ya DAWASCO zilizo katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es salaam na kupitia nambari zifuatazo: Temeke +255 775016184, Ilala +255 775048556, Magomeni +255 775016179, Boko/Tegeta +255 775048553, Tabata +255 775016181, Kawe +255 775016185, Kinondoni +255 775016180 na Kimara +255 775048554. 


Wananchi watumie pia nafasi hii kuwasilisha kwa DAWASCO maelezo na vielelezo kuhusu maeneo ambayo hakuna miundombinu ya maji kabisa au miundombinu iliyopo haijawahi kutoa maji kwa kipindi kirefu kwa ajili ya kutaka hatua za ziada. 


Matatizo ya maji katika maeneo mengi ya jiji la Dar es salaam ikiwemo katika Jimbo la Ubungo yamedumu kwa miaka mingi, wananchi wametupa wajibu wa kuwawakilisha kuisimamia serikali na mamlaka zake kupunguza kero husika kwa haraka hivyo wananchi watarajie vitendo zaidi vya kushinikiza uwajibikaji kwenye sekta ya maji katika kipindi cha karibuni.


Imetolewa tarehe 22 Februari 2011 na:


John Mnyika (Mb) 


DCI Manumba amewasiliana na Wizara ya Afya ya nchi gani?

Sumu ya Dk. Mwakyembe
Mwakyembe, Sitta wajiuzulu kutumikia Serikali wanayoituhumu
MIONGONI mwa matukio ya kukumbukwa ya Bunge lililokuwa chini ya Spika wa zamani, Samuel Sitta ni tuhuma kwamba mmoja wa wabunge alifanya vitendo vya ushirikina.
Japo suala hilo lilimalizwa kimya kimya, ukweli unabaki kuwa lilikuwa ni la kuaibisha na pengine kudhihirisha upungufu mkubwa kwa baadhi ya watu tuliowakabidhi jukumu la kutuongoza.
Na kama ilivyozoeleka kwenye masuala mengi yenye utata, Watanzania hawakuwa na jinsi ya kudai ukweli kuhusu suala hilo. Kwa upande mmoja huwezi kuwalaumu hasa ikizingatiwa kuwa, wengi wao wanahangaika tangu mawio hadi machweo kuhakikisha ‘mkono unakwenda kinywani.’ Kwa upande mwingine, watawala wetu wamejitengenezea mazingira ambayo mwananchi wa kawaida hawawezi kudadisi ‘upuuzi’ wao (kama huo wa madai ya ushirikina bungeni).
Lakini pengine kikubwa zaidi ni ukweli kwamba kama hadi leo hii watawala wetu wamegoma kabisa kutuambia kuhusu wahusika wakuu wa ujambazi wa mchana kweupe (daylight robbery) katika skandali za EPA (hasa nani anayemiliki kampuni iliyoiba fedha nyingi ya Kagoda), Richmond, Meremeta, Tangold na nyinginezo, basi ni dhahiri hawakuona haja ya kujihangaisha na ‘jambo dogo’ kama hilo la tuhuma za ushirikina bungeni .
Busara zinatukumbusha kuwa ‘usipoziba ufa utajenga ukuta.’ Tabia ya kuyapuuza masuala yanayopaswa kushughulikiwa ipasavyo sasa imeanza kuzua sokomoko mpya ambayo imeendelea kutawala vichwa vya habari kwa siku kadhaa sasa. Ninazungumzia sakata linalowahusu Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk. Harrison Mwakyembe, kwa upande mmoja, na Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, Robert Manumba, kwa upande mwingine.
Unaweza kulipanua sakata hilo na kumjumuisha Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta (ambaye amejitokeza kuwa mtetezi mkuu wa Mwakyembe) na Jeshi zima la Polisi chini ya uongozi wa IGP, Said Mwema.
Tuhuma kwamba Mwakyembe amenyweshwa sumu zilianza kama mzaha. Kadri siku zilivyozidi kwenda, suala hilo lilianza kupata uzito hasa baada ya tamko la wazi lililodai kwamba Idara ya Usalama wa Taifa ilikuwa na mpango wa kumuua.
Sijui nchi yetu imefika mahali gani kiasi naibu waziri na mbunge anaituhumu taasisi muhimu na nyeti ya dola kuwa ina njama za kuondoa uhai wake lakini wahusika waliipuzia. Lakini kama nilivyobainisha hapo awali kuwa, masuala mengi yenye kugusa hisia za umma yamekuwa yakimalizwa kienyeji, hazikufanyika jitihada zozote aidha kukanusha madai hayo ya Mwakyembe wala hatua madhubuti za kuyachunguza.
Mwananchi wa kawaida anaweza kujiuliza, “Hivi kama mashushushu wanaweza kupanga njama za kumuua kiongozi wa kitaifa anayetoka chama tawala CCM; je, hali ikoje kwa viongozi wa vyama vya upinzani? Na je, kama usalama wa vigogo unatishiwa na chombo kinachopaswa kulinda usalama wa nchi, hivi kuna usalama kweli kwa walalahoi?
Pengine suala hilo lilipuuzwa kwa matarajio lingekufa kifo cha asili na kusahaulika akilini mwa Watanzania. Hali ya Mwakyembe ikazidi kuwa mbaya na swahiba wake, Waziri Sitta, akapita huku na kule kuukumbusha umma kuwa mafisadi wakishirikiana na vyombo vya dola ndio waliomdhuru naibu waziri huyo ambaye pia ni mbunge wa Kyela (CCM).
Kama mchezo wa kuigiza vile, Waziri wa Mambo ya Ndani, Shamsi Vuai Nahodha, akaingizwa kwenye sakata hilo pale alipomtaka Waziri Sitta kuwasilisha ushahidi wa madai yake kuwa Mwakyembe amenyweshwa sumu.
Lakini katika kile kinachoweza kuashiria kuwa nchi yetu inaendeshwa kwa mtindo wa ‘bora liende,’ Nahodha pia alidai kuwa hajawahi kusikia suala hilo (japo yeye ndiye mwenye dhamana ya jeshi la polisi na usalama wa raia), na kuwataka waandishi wa habari wamuulize Sitta aliyetoa tuhuma hizo.
Hatimaye Sitta naye akamjibu Waziri mwenzake (Nahodha) kwa kubainisha kuwa hatapeleka ushahidi wa madai aliyotoa kuwa Mwakyembe alilishwa sumu kwa kuwa polisi tayari wanao ushahidi.
Awali, Nahodha alidai kuwa “...masuala yote yanayohusu uchunguzi hayawezi kuzungumzwa katika vyombo vya habari...ni mambo ambayo hufanyika kwa umakini mkubwa...” na hatimaye DCI Manumba akathibitisha kauli hiyo ya bosi wake (kufanya mambo kwa umakini) kwa kukurupuka na kudai Mwakyembe hajalishwa sumu. Pia, aliwataka wananchi kupuuza madai ya Sitta, akidai kuwa Jeshi la Polisi liliwasiliana na Wizara ya Afya ambayo ilithibitisha ilitoa taarifa kuwa Mwakyembe hakulishwa sumu.
Kauli hiyo ya Manumba ikawaibua Mwakyembe na Sitta ambao walishusha tuhuma nzito dhidi ya Manumba na Jeshi la Polisi kwa ujumla. Mwakyembe alikwenda mbali zaidi na kudai jeshi hilo lilimtuma ‘askari mtuhumiwa wa dawa za kulevya na ujambazi’ kufuatilia taarifa za (Mwakyembe) kutishiwa maisha yake.
Katika kile kinachoashiria kuwa ‘sinema’ hii inaweza kuendelea kwa muda mrefu, muda mfupi kabla sijaandika makala hii Waziri wa Afya, Dk. Hadji Mponda, ameikana kauli ya Manumba kuwa wizara hiyo ilitoa uthibitisho kwa polisi kuwa, Mwakyembe hajalishwa sumu.
Ni vigumu kuwasilisha sakata hili katika mtiririko unaoleta maana kwa sababu staili inayotumiwa na wahusika ni mithili ya ‘piga nikupige.’ Lakini kilicho wazi ni ombwe kubwa kabisa la uongozi kuanzia kwa Rais Jakaya Kikwete mwenyewe.
Kwa vyovyote vile Kikwete anashuhudia mtifuano huu unaoweza kabisa kupoteza imani ya wananchi kwa Serikali yake na taasisi kama Jeshi la Polisi na Idara ya Usalama wa Taifa, lakini amekaa kimya kana kwamba mambo hayo yanatokea Somalia na si Tanzania anayoiongoza.
Yeye ndiye aliyewateua Mwakyembe na Sitta, japo uteuzi huo ulionekana na baadhi ya wachambuzi wa siasa za nchi yetu kama mbinu ya ‘kuwadhibiti wanasiasa hao wanaotajwa kuwa ni makamanda wa vita dhidi ya ufisadi.’ Wanaodai hivyo wanapigia mstari kanuni ya uwajibikaji wa pamoja ambayo kama inazingatiwa, haitarajiwi mawaziri wanaotumikia ‘kabineti’ moja kupingana hadharani.
Kama Mwakyembe aliituhumu Idara ya Usalama wa Taifa kuwa ilikuwa na njama za kumuua, na kimsingi kiongozi mkuu wa taasisi hiyo nyeti (sponsor) ni Rais mwenyewe, hiyo inaweza kuzaa tafsiri kuwa Rais ni sehemu ya njama hizo. Kwa hiyo ni wazi kwamba laiti umakini ungetumika tangu mwanzoni mwa sakata hii, Rais Kikwete angeweza kuchukua hatua za aidha kumwajibisha Mwakyembe (kwa vile haiwezekani waziri anayeituhumu taasisi inayoongozwa na Rais kufanya kazi kwa ufanisi na Rais huyo) au kuitisha uchunguzi wa kina wa ili suala hilo kupatiwa majibu sahihi na hatimaye kulimaliza kabisa.
Lakini kwa upande mwingine, ninashindwa kabisa kuwaelewa Mwakyembe na Sitta. Japo ninaguswa na maradhi yanayomsibu Mwakyembe lakini sielewi kwa nini yeye na Sitta wanaendelea kuitumikia Serikali ambayo kimsingi wanaituhumu kuhusika na suala hilo la kulishwa sumu. Idara ya Usalama na Jeshi la Polisi si tu ni taasisi muhimu za Serikali bali pia zote zipo chini ya Rais ambaye ni Amiri Jeshi Mkuu.
Na kama Mwakyembe alikuwa na uhakika kwamba Idara ya Usalama ina mpango wa kumuua kwa nini hakumwomba Rais aingilie kati, hasa baada ya kubaini (kwa mujibu wa maelezo yake) kuwa Jeshi la Polisi lilikuwa linachukulia tuhuma zake kama mzaha?
Kwa upande wa Idara ya Usalama wa Taifa, ninaamini ukimya wao unachangia kulikuza suala hili. Tuhuma kutoka kwa naibu waziri kuwa taasisi hiyo ina njama za kumuua si ndogo. Sasa kama walidiriki kukana madai yaliyowahi kutolewa na aliyekuwa mgombea urais kwa tiketi ya CHADEMA, Dk. Willbrod Slaa kuwa Idara hiyo ilishiriki kumhujumu katika Uchaguzi Mkuu uliopita, kwa nini ikalie kimya tuhuma kuwa inataka kumuua kiongozi asiye na hatia?
Ikumbukwe kuwa kuna nyakati taasisi za intelijensia katika nchi mbalimbali hulazimika ‘kummaliza mlengwa’ (termination) alimradi kufanya hivyo ni kwa maslahi ya nchi. Hilo lipo ndani ya mamlaka wanayokabidhiwa na taifa husika. Naomba ieleweke kuwa hapa simaanishi kuwa Idara yetu ya Usalama wa Taifa nayo inajihusisha na vitendo vya aina hiyo, lakini kwa vile mbinu hiyo ‘inakubalika katika mazingira ya utendaji kazi wa taasisi za aina hiyo,’ kunyamazia tuhuma za Mwakyembe kunaweza kusababisha hisia kuwa ni za kweli.
Jeshi la Polisi nalo lina maswali kadhaa ya kujibu. Kwanza, lini watatoa matokeo ya uchunguzi wao kuhusu tuhuma za Mwakyembe kuwa Idara ya Usalama ilikuwa na njama za kumuua? Pili, kama jeshi hilo limeshatamka bayana kuwa wananchi wapuuze madai ya Waziri Sitta kuwa Mwakyembe amelishwa sumu, kwa nini halijamchukulia hatua ‘kwa kutoa tuhuma nzito kama hizo’? Na tatu, DCI Manumba alipata taarifa kutoka ‘Wizara ya Afya ya nchi gani kuwa Mwakyembe hajalishwa sumu’ (kwani Waziri Mponda ameshang’aka wizara yake kuhusika na hilo)?
Nimalizie makala hii kwa kutoa hadhari kwamba hiki kinachoonekana kama ‘mchezo wa kuigiza’ kinaweza kuwa na madhara makubwa huko mbele.
Wanaozembea kwa kukaa kimya kwa matarajio kuwa suala hili litapotea tu kama masuala ya Kagoda, Meremeta na Tangold wanajidanganya na hatma yake inaweza kuwa mbaya na isiyoweza kurekebishika.


By Joyce Joliga
The Citizen Correspondent
Songea. Police in Songea allegedly shot dead four civilians yesterday, during a fracas associated with a public demonstration against a reported string of murders over the past four months, that the law enforcement organ is accused of neither curbing nor resolving.In a quick rejoinder, however, Ruvuma Regional Police Commander Michael Kamuhanda put the figure of those who had died at two.  

Several other people were injured when police officers used tear gas and live ammunition to quell angry demonstrators, some of whom had stormed the town’s main police station.The Ruvuma regional hospital chief medical officer, Dr Benedicto Ngaiza, confirmed that the hospital  had received four bodies and about 20 injured persons. 

He said two of the bodies had bullet wounds, and  two of the injured persons had bullet injuries  as well, and were rushed to the theatre for operations. All the bodies were delivered by the police,  he explained, adding that, one of them was that of a motorcyclist who had  accidentally hit a tree while speeding  away from the fracas.
Since November last year, nine people have been murdered in the town – a roughly monthly average of two –  some of whose bodies had been mutilated.

The trend has triggered much panic and anger amongst wananchi, who are in the dark over whether the crime is the work of a serial killer or a gang. Worrisome, too, is that, so  long as  the motives of the murders are not known, anyone was a potential next victim.

Chaos  and confusion reigned in Songea for a couple of hours yesterday, as most of the normal  official, business and social activities came to a standstill, as  much attention was  focused on the drama featuring chanting and stone-throwing demonstrators and law enforces who strived to restrain them.

Government offices,  the regional hospital, shops,  and the main bus stand, were among the  sensitive facilities that were temporarily closed and reopened only after relative calm had been restored.

The closures were  prompted by fears by  many people over  being caught in the cross-fire,  or falling victim to looters and petty thieves, since amongst the presumed demonstrators were  people who wielded crude weapons like iron bars.

Many people scattered in various directions towards safer places away from  the procession route, including crew  and passengers awaiting long distance  bus trips. Guards at the regional hospital closed the gates  of the facility as a precaution, as they couldn’t  establish whether  all the people in the huge crowd  that pleaded to be  allowed in were seeking protective shelter, or whether some  were thugs.

 The procession towards the police station  that started early in the morning, attracted hundreds of people marching on foot as well as motorcyclists in slow motion. The crowd swelled as word spread to various parts of the town and more people joined in.

Reports say that  the police fired live ammunition in the air and lobed teargas canisters into the crowds in a bid to restrain them, but, some amongst them continued pushing relentlessly into the police  station compound.

It was at that juncture that the police fired directly  into the crowd, killing two of the protestors, according to RPC Kamuhanda,  who explained that they had refusing to heed orders aimed at preventing a breach of peace. Mr Kamuhanda said investigations had been launched, but  hinted that initial indications pointed to  superstitious beliefs and politicking as causes of the chaos.

The Ruvuma Regional Commissioner, Mr Said Mwambungu,  expressed  dismay over the incident, and appealed to wananchi to remain calm while the Police was continuing with efforts to track down the  perpetrators  of the murders that had fuelled their anger.

He appealed  to Songea residents to avoid walking alone at night, especially if they didn’t have important engagements  that warranted taking risks.

In the evening, Mr Mwambungu chaired a crisis meeting of the regional peace and security committee, to chart  strategies  for containing the mysterious killings.

SOURCE: The Citizen


Chuck D,mwanzilishi na kiongozi wa lilikouwa kundi maarufu la rap huko Marekani,Public Enemy,aliwahi kusema muziki wa rap ndio CNN ya mtaa.Tangu awali,muziki wa rap umekuwa ukizungumzia masuala mbalimbali yanayoikabbili jamii-kutoka ukimwi,mihadarati,ubaguzi wa rangi hadi sera za ndani na za nje.Na sasa tunashuhudia baadhi ya wasanii wetu wakipata mwamko kama huo wa Public Enemy.Ushuhuda ni huu hapa chini.Sahau kidogo kuhusu video na sikiliza ujumbe kwa makini



CHANZO: Dj Choka's Blog

21 Feb 2012


Kwa maelezo zaidi BONYEZA HAPA


It's your birthday and I can't be there
But I'll send you a special birthday wish and a little prayer
Have a happy birthday
I hope that all of your birthday wishes come true
May you have a great time today and find happiness in everything you do.










CHANZO: Jamii Forums

KWA MWENDENO HUU NDIO MAANA TUNASHUHUDIA "MAFURIKO YA WAWEKEZAJI" WANAOISHIA KUPORA AJIRA ZA WAMACHINA (KWA MFANO WACHINA).UKILINGANISHA FOMU HIYO HAPO JUU NA FOMU ZA KUOMBEA VIZA ZA KUINGIA NCHI KAMA UINGEREZA AU MAREKANI UTABAINI JINSI GANI HATUPO SERIOUS KATIKA MAMBO NYETI.

20 Feb 2012


WAPENDWA WATAZAMAJI WA TMTV.
 
TUNAPENDA KUWATANGAZIA KUWA KUTOKANA NA MATATIZO YA KIUFUNDI.
KUMEKUWA NA TATIZO LA KUINGIA KTK TV KATIKA SIKU CHACHE ZILIZOPITA.TATIZO HILO LINAENDELEA KUFANYIWA KAZI.
KWA SASA UNAWEZAENDELEA KUBURUDIKA NA TMTV KWA LINK HII  http://tmtv.eightzerodigital.com/player.php
TUNAWAAHIDI MAMBO MAZURI YANAKUJA,VIDEO KIBAO MPYA ZITAONGEZEKA KWA RAHA ZAIDI KAMA KAWAIDA 24/7 NON-STOP.


Familia ya JK yamkana aliyetoweka na mamilioni UVCCM 
Monday, 20 February 2012 07:38

Rais Jakaya Kikwete
Peter Saramba, Arusha
FAMILIA ya Rais Jakaya Kikwete imekana kuwa na nasaba na aliyekuwa Katibu wa Jumuiya ya Umoja wa vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), wilayani Simanjiro, Alhaj Omar Yufus Kariaki, anayetuhumiwa kutokomea na zaidi Sh26 milioni, mali ya jumuiya hiyo.

Dada wa Rais Kikwete aliyehudhuria harambee ya kuchangisha fedha hizo kwa mwaliko wa Alhaj Kariaki, Tausi Kikwete aliliambia gazeti hili mwishoni mwa wiki iliyopita kuwa kitendo cha kijana huyo kujinasibu kuwa na undugu na familia yao, kililenga katika kujinufaisha isivyo halali.

“Ukweli ni kwamba kijana huyo siyo ndugu yetu hata kwa mbali. Kwanza yeye anatoka Kondoa, wapi na wapi na sisi Wakwere wa Bagamoyo, mkoani Pwani, Hatumfahamu kabisa kwenye ukoo wetu zaidi ya kufahamiana naye tulipokutana Hija,” alisema Tausi.

Alisema yeye na ndugu yake Mwanaisha Kikwete, walikutana na mtuhumiwa walipokwenda kuhiji Mecca, Saudi Arabia na baadaye kupeana mawasiliano yaliyowawezesha kuendelea kuwa karibu hata baada ya kurejea nchini.

Alisema baada ya kurejea, yeye na Mwanaisha waliendelea kuwasiliana na Alhaj Kariaki aliyeonyesha kuwa kijana mwenye upendo na busara zilizowavutia wao kutembelea nyumbani kwao, Kondoa kwa mwaliko wake.
“Ukaribu wetu ulifikia hatua ya sisi kutembelea nyumbani kwao Kondoa baada ya yeye kutualika. Lakini ukweli unabaki pale pale kwamba kijana huyo si ndugu yetu wala hana nasaba yoyote na kina Kikwete.” alisisitiza Tausi.

Alisema ilipofika wakati wa  harambee ya kutunisha Mfuko wa Mradi wa Maendeleo ya Vijana wa Wilaya ya Simanjiro, kijana huyo akiwa Katibu wa UVCCM wilayani humo, aliwaalika yeye na Mwanaisha kwenda kutoa semina kwa vijana kuhusu mbinu za ujasiriamali na miradi midogo.

Kwa mujibu wa Tausi, semina hiyo ilifanyika katika ukumbi wa mikutano ya Hoteli ya Manyara Inn, iliyoko Mererani siku mbili kabla ya harambee iliyoongozwa na aliyekuwa Waziri Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), Shamsi Vuai Nahodha, ambaye sasa ni Waziri wa Mambo ya Ndani katika Serikali ya Muungano.
Hata hivyo kauli hiyo ya Tausi inapinga na kauli yake ya awali kupitia simu mwaka jana, ambapo licha ya kukiri kumfahamu Alhaj Kariaki, pia alisema wana unasaba naye.

“Ni kweli mimi na Mwanaisha ni dada wa mheshimiwa Rais (Kikwete) pia ni ndugu wa karibu wa kijana huyo (Alhaj Kariaki). Lakini binafsi sina mawasiliano naye tangu awe diwani huko kwako Kondoa. Kwa kifupi sijawasiliana naye tangu tuachane Mererani,” alisema Tausi mwaka jana alipoulizwa kuhusu mtuhumiwa huyo.

Katika harambee hiyo iliyohudhuriwa na viongozi na watu kadhaa maarufu kutoka Mikoa ya Manyara na Arusha, Nahodha alichangia Sh2 milioni fedha taslimu  wakati aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Manyara Henry Shekifu akichangia 500,000.
Kwa sasa Shekifu ni Mbunge wa Lushoto.

Mwenyekiti wa UVCCM wa Wilaya ya Simanjiro, Kiria Laizer, alisema baada ya yeye kukabidhiwa mfuko wenye fedha mara baada ya harambee ambayo mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka naye alichangia Sh1.5 milioni, alikabidhi mfuko huo kwa katibu wake Alhaj Kariaki ambaye hadi juzi alipojitokeza baada ya gazeti hili kuripoti suala hilo.

Mwenyekiti huyo aliwataja wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya UVCCM wilaya walioshuhudia makabidhiano kati yake na katibu wake  kuwa ni Bonny Shongo na Paul Sipitet.

Laizer aliyetoa pongezi na shukrani kwa mwandishi na gazeti la Mwananchi kwa kufanikisha mtuhumiwa kujitokeza, alisema awali walikuwa wakihofia kufuatilia suala hilo kwa karibu kwa hofu kwamba mtuhumiwa ana undugu na familia ya Rais.

Alhaj Kariaki ambaye sasa ni Diwani wa Kata ya Kwa Delo wilayani Kondoa, aliibuka wiki iliyopita baada ya habari zake kuripotiwa katika gazeti hili.

Alikiri kutokabidhi fedha zilizopatikana kwenye harambee hiyo iliyofanyika Mei 9 mwaka juzi akidai sehemu ya fedha hizo amezitunza kwenye akaunti yake, akisubiri kumalizika kwa kile alichodai kuwa mgogoro baina ya viongozi wa CCM mkoani Arusha ili azikabidhi

CHANZO: Mwananchi

16 Feb 2012


Wafuateni kina Zitto, Januari Makamba

MAKALA katika toleo lililopita la jarida hili ilizua mjadala mrefu kwenye mtandao wa kijamii wa twitter kutokana na kunukuu matamshi ya Rais Jakaya Kikwete na utata kama wasifu uliopo kwenye mtandao huo ni wa Rais mwenyewe.
Katika makala hiyo niliandika kuwa “nilifanya mazungumzo yasiyo rasmi na Rais kuhusu mkanganyiko uliojitokeza kufuatia kauli ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda juu ya nyongeza ya posho za wabunge.”
Baadhi ya wananchi hawakupendezwa na matumizi ya maneno ‘nilifanya maongezi na Rais...’ wakidai huko ni kupotosha ukweli. Pengine hali hiyo ilisababishwa na kasumba iliyozoeleka kuwa ni nadra mno kwa kiongozi (achilia mbali Rais) kufanya maongezi (hata yasiyo rasmi) na ‘mtu wa kawaida’ kama mimi.
Kwa upande mwingine, imezoeleka kuwa ‘maongezi’ ni pale tu mtu anapozungumza nawe uso kwa uso, kukuandikia barua, kukupigia simu au kukutumia SMS.
Maendeleo ya teknolojia yanayowezesha mazungumzo kufanyika kupitia mitandao ya kijamii kama twitter, facebook, google+, nk, bado ni kitu kigeni kwa wengi. Na si tu ni jambo geni kwa vile watumiaji ni wachache bali pia mazoea ya wengi wetu yanapeleka kuyaona mawasiliano ya aina hiyo kutostahili kuitwa maongezi.
Kimsingi, maendeleo katika teknolojia yamebadili kwa kiwango kikubwa jinsi habari zinavyokusanywa au/na kupatikana. Wakati kabla ya kuja kwa radio, runinga, simu, nk njia pekee ya kupata habari ilikuwa kwa kukutana uso kwa uso na chanzo cha habari, hali sasa ni tofauti kabisa.
Wakati kauli mbalimbali za viongozi wetu zinaendelea kupatikana kupitia mikutano yao na wanahabari au/na press releases, waandishi wengi wamekuwa wakifuatilia ‘kurasa’ za viongozi (na watu wengine maarufu) kwenye mitandao ya kijamii kwa minajili ya kupata habari.
Kadhalika, kuna nyakati viongozi hufanya maongezi na watumiaji wengine wa mitandao hiyo. Kwa mfano, huko twitter unaweza kumuuliza kiongozi swali (ili kufanya hivyo unapaswa kuandika jina analotumia kwenye wasifu wake likianza na tarakimu @) na yeye akakujibu.
Na hivyo ndivyo ilivyotokea kwangu. Nilimuuliza swali Rais Kikwete naye akanijibu. Sikuona ubaya wa kutumia ‘maongezi’ hayo (yasiyo rasmi) kwenye makala husika hususan kwa kuchelea kuonekana nimepandikiza maneno yangu binafsi kwenye habari hiyo.
Jambo la pili lililozua mjadala ni uhalali wa akaunti ya Rais Kikwete huko twitter. Kwa upande mmoja, baadhi ya watu walidai kuwa yote yanayoandikwa kwenye ‘ukurasa’ wa Rais hufanywa na timu yake ya mitandao ya kijamii (social media team).
Hoja hiyo inaingia akilini kwa sababu sote tunafahamu jinsi Mkuu wa Nchi anavyokuwa na majukumu mengi yanayoweza kumkwaza kufuatilia kila kinachoendelea kwenye mitandao ya kijamii, magazetini, nk. Hata hivyo, yayumkinika kuamini kuwa wasaidizi wa Rais waliokabidhiwa jukumu hilo (kama wapo) wanafanya hivyo kwa ridhaa ya Rais mwenyewe.
Hiyo ni kama jinsi taarifa mbalimbali zinapotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu au Mwandishi wa Habari wa Rais. Japo anayeandika na/au kusambaza taarifa hizo si Rais mwenyewe, ridhaa yake na ukweli kwamba kinachoongelewa kinamhusu yeye kunapelekea taarifa za aina hiyo kupokewa na umma kama kauli (au msimamo) ya Rais.
Mkanganyiko kuhusu akaunti ya Rais huko twitter unachangiwa pia na kukosekana na alama inayoashiria kuwa akaunti husika imehakikiwa na wamiliki wa mtandao huo wa kijamii (yaani kuwa verified).
Wakati Rais Kikwete anatajwa kuwa miongoni mwa viongozi wachache barani Afrika wanaoitumia mitandao ya jamii mara kwa mara, si yeye pekee ambaye akaunti yake ya twitter haijahakikiwa (kwa mfano, ya Rais Jacob Zuma na Yoweri Museveni pia zipo katika hali hiyo).
Lakini japo pengine ingependeza akaunti rasmi ya Rais inaonyesha alama ya verified na hivyo kuondoa ‘sintofahamu’ kuhusu mmiliki wake, ukweli kwamba licha ya Ikulu kutoikana, na miongoni mwa followers wake ni watu na taasisi zenye hadhi kwenye jamii (kwa mfano CCM, CHADEMA, na familia ya Kikwete mwenyewe) basi kwa sasa tunaweza kuamini kuwa akaunti hiyo ni yake.
Lengo la makala hii si kuendeleza mjadala huo ambao kwa hakika si wa muhimu kulinganisha na masuala mbalimbali muhimu kwa Taifa. Hata hivyo, unaweza kutupa fursa nzuri kutathmini nafasi ya teknolojia ya mawasiliano katika mwingiliano (interactions) kati ya watawala na watawaliwa au viongozi na wananchi.
Kuna ugumu mkubwa katika kupata taarifa rasmi kutoka taasisi za umma. Wahanga wakubwa wa tatizo hilo si waandishi wa habari tu bali pia watafiti wanaosaka takwimu kwa ajili ya tafiti zao na wananchi kwa ujumla.
Uzuri wa namna ya kutumia teknolojia kama ya mitandao ya jamii upo kwenye urahisi wa namna ya kuitumia. Mitandao kama twitter na facebook inafikika kirahisi kwa kutumia hata simu (ili mradi iwe na huduma ya intaneti).
Pasipo kujali ni kiongozi mwenyewe au wasaidizi wake wanaosimamia ukurasa husika mtandaoni, uwepo wa ukurasa huo unaweza kutoa nafasi nzuri kwa wananchi kuwasiliana na kiongozi husika, sambamba na kuepusha mkanganyiko unaoweza kujitokeza pindi kauli ya kiongozi inapowasilishwa na mtu mwingine.
Mfano hai katika hilo ni mkanganyiko uliojitokeza siku chache kuhusiana taarifa zilizohusu ongezeko la posho za wabunge.
Ninatambua kuwa kwa mwananchi wa kawaida kule kijijini (ambako uhaba wa huduma muhimu za jamii unaumiza kichwa zaidi ya suala kama intaneti) anaweza asione umuhimu wa kuhamasisha viongozi wetu kuitumia mitandao ya kijamii, ukweli ni kwamba njia yoyote itakayowezesha kuwaweka viongozi hao karibu na wananchi inapaswa kutiliwa mkazo.
Wenzetu katika nchi zilizoendelea wana sheria zinazolazimisha upatikanaji wa habari zenye maslahi kwa umma, kwa mfano, sheria ya uhuru wa kupata habari (Freedom of Information Act).
Kwa huko nyumbani, tatizo si kuwapo (au kutokuwapo) kwa sheria ya aina hiyo, bali utashi kwa upande wa watawala kuona habari zenye maslahi ya umma zinapatikana kwa wananchi pasipo vikwazo.
Sasa katika mazingira ambapo habari kutoka taasisi za umma au viongozi zinapatikana kama fadhila (badala ya kuwa haki ya msingi), kuwa na viongozi kwenye mitandao ya kijamii kunaweza kusaidia sana kupunguza ombwe hilo.
Kwa kuwa Rais Kikwete (bila kujali ni yeye mwenyewe au wasaidizi wake) anaonekana kuwa ‘muumini mzuri’ wa matumizi ya mitandao ya kijamii, anaweza kuhamasisha watendaji wake na taasisi kuiga mfano wake.
Lakini kwa vile ‘mtoto hazaliwi akatambaa’ (kwa maana itachukua muda kabla mwingiliano wa viongozi wa/taasisi za umma na wananchi kwa kutumia mitandao ya kijamii haujaenea kwa kiwango kikubwa) bado kuna nafasi ya kutumia vyombo kama blogu za Kitanzania (ambazo idadi yake inaongezeka kwa kasi) kutimiza jukumu hilo.
Kwa sasa, njia pekee ya blogu kuwasilisha habari kutoka kwa viongozi au taasisi mbalimbali ni kwa kunukuu habari kutoka vyombo ‘vya asili’ vya habari (yaani magazeti, radio na runinga).
Kibaya zaidi ni ukweli kuwa tovuti za taasisi chache za umma (zilizoona umuhimu wa kuwa na tovuti) aidha haziwekwi habari mpya mara kwa mara au zimebaki kuwa anwani tu (kwa maana hazipatikani mtandaoni).
Ukienda kwenye blogu ya Ikulu (inayoendeshwa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Ikulu) utaona habari ‘mpya’ ni mwanzoni mwa mwezi uliopita. Wakati viungo (links) ni kwa Wizara pekee, kuna video moja tu kwenye ukurasa wa video. Blogu hii ingeweza kabisa kuwa na kipengele cha maandiko ya Rais na/au Ikulu kwenye mitandao mingine ya kijamii (kama twitter na facebook), hiyo ingesaidia kuondoa mkanganyiko kama nilioubainisha awali.
Nimalizie makala hii kwa kuwapa changamoto viongozi wetu kuiga mfano wa baadhi ya wanasiasa kama Zitto Kabwe, Januari Makamba, Dk. Faustine Ndugulile, Dk. Hamisi Kigwangalla, Mo Dewji na John Mnyika (na wengineo wachache) ambao kama Rais Kikwete mwenyewe, wamekuwa mahiri katika matumizi ya teknolojia ya mawasiliano kwa kutumia mitandao ya jamii.
Licha ya kuwa nyenzo muhimu katika shughuli zao za kisiasa, mitandao hiyo inawaweka karibu zaidi na wananchi na kurahisisha upatikanaji wa habari zinazowahusu au zenye maslahi kwa umma.


14 Feb 2012

13 Feb 2012


Katuni kwa hisani ya KING KINYA na Global Publishers

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.