15 Apr 2010


Nimefarijika sana kuona mahojiano niliyofanya na msanii mahiri wa Bongoflava,Hamis Mwinjuma a.k.a Mwana FA,yamechapishwa katika tovuti ya kimataifa ya muziki wa hip-hop,
Hip-Hop-Dance.Net.Pamoja na kuwapatia wasomaji wa blogu hii nafasi ya kuwafahamu Watanzania wenzetu wanaotangaza jina la nchi yetu kwa namna moja au nyingine,dhumuni jingine la mahojiano hayo lilikuwa kutangaza vipaji vinavypatikana nchini kwetu. Japo mahojiano hayo yanaelekea kuzua mjadala mwingine ambao binafsi nautafsiri kama uhuru wa mawazo,ninaishukuru sana tovuti ya Hip-Hop-Dance kwa "kutoa shavu" kwa mahojiano hayo hasa kwa vile Mtanzania mwenzetu mmoja aliamua kuyabania licha ya kumpa ombi ayaweke "kiwanjani" kwake.Again,naamini alifanya hivyo kwa kutumia uhuru wake kuchagua nini kinastahili kuwepo hapo kwake.


Kuhusu suala la elimu ya Mwana FA,ninaomba kumtetea,sio kwa vile nilimhoji,bali kwa sababu naamini anastahili zaidi pongezi kuliko criticism.Naomba niweke wazi kuwa Mwana FA hakuomba mahojiano hayo bali ni mimi niliyemwomba (na namshukuru sana kwa kukubali ombi hilo).Pili,kama alivyosema mwenyewe,mtu haihitaji kuwa na Masters ili aweze kufanya vizuri kwenye bongoflava.Alichukua uamuzi wa kujiendeleza kimasomo kwa vile,kwa mujibu wa maeleoz yake nayoafikiana nayo,fani ya muziki (hasa wetu) haitoi mwamana wa mafanikio katika maisha.Kwa amaan nyingine,alimua kuongeza elimu yake kama hatua ya kimaendeleo mbali na mafanikio yake katika Bongoflava.

Na hata kama angekuwa anadanganya kuhusu elimu yake (which he absolutely doesn't) ingemsaidia nini wakati tayari ana jina kubwa ndani na nje ya nchi yetu?Nadhani baadhi ya wasomaji wanaomtaka "aeleze ukweli" wanapaswa kwanza "kueleza uongo wake" kabla ya kumtaka aseme "ukweli".Nasema hivyo kwa maana kama nasema jina langu ni Evarist,halafu mtu anasema hilo sio jina langu ,basi ni muhimu kwake kuthibitisha jina langu halisi ni nani.

Binafsi,kama mwanafunzi,nimekumbana na zahma kama hiyo ya Mwana FA.Nimekuwa napokea barua pepe na hata SMS za watu wanaoulizia lini namaliza shule.By the way,shule huwa haimalizwi bali mtu anahitimu hatua moja na anaweza kuendelea na hatua nyingine.Kadhalika,katika mfumo wa elimu ya juu hapa,mwanafunzi anaweza kuahirisha kozi yake pale atapoona umuhimu wa kufanya hivyo.In my case,majibu yangu kwa watu wanaoniuliza kistaarabu ni kuwa kuchelewa kumaliza kozi yangu kumesababishwa na A,B,C na kadhalika kisha nawafahamisha hatua niliyofikia.Kwa wale wanaouliza kwa minajili ya "kudhani nauhadaa umma kuhusu elimu yangu" jibu langu huwa jepesi: Mind your own damn business.

Kuna wanaojiuliza inakuwaje mtu atoke IFM na kuja kufanya Masters University of Coventry,nawasihi wafanye utafiti kidogo kwenye mfumo wa elimu ya Uingereza,na pengine hata huko nyumbani.Inawezekana kabisa kupata admission kwenye vyuo vya hapa kwa kigezo cha "sifa linganifu" (equivalent qualifications).Ni kama ambavyo baadhi ya wanafunzi wanavyojiunga na MBA pale Mzumbe au kwingineko baada ya kumaliza masomo ya stashahada kutoka IFM,Nyegezi,Ustawi wa Jamii (pale Sayansi),nk.Kwa kifupi,mifumo mingi ya elimu duniani iko so "accommodating" kwa watu wenye nia ya dhati ya kujiendeleza kitaaluma.

Nimalizie kwa kutoa shukrani kwa wote wanaoendelea kutoa mawazo yao kuhusu mahojiano hayo.Sipingani na mawazo yoyote bali huu ni mchango na mtazamo wangu binafsi (ambao pia unaweza kuwa si sahihi kwa mujibu wa mitizamo mingine).Huo ndio uhuru wa mawazo,alimradi tunatumia lugha za kiungwana na "hatutiani vidole machoni".Kwa Mwana FA,hizi ndio changamoto za Tanzania yetu.

Stay tuned for the next interview na Mtanzania mwingine anayetuwakilisha vilivyo.Can you make a wild guess?Au una pendekezo lolote?

Nimekuletea habari sita zilizopelekea nijiulize swali hilo hapo juu:TUNAELEKEA WAPI kama Taifa?Tutafakari pamoja...

Mwananchi: Polisi waibiana Sh3 bilioni za posho

Salim Said
SIRI ya kuchelewa kwa posho za askari polisi mwezi Febuari mwaka huu imefichuka baada ya kudaiwa kuwa maafisa watatu wa jeshi hilo walitoweka na hundi ya malipo hayo yanayofikia Sh3 bilioni.

Baadhi ya maofisa wa polisi waliozungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti wiki hii, walielezea mazingira ya wizi huo na kusisitiza kuwa ngazi ya juu ya jeshi hilo imekuwa ikificha taarifa hizo, kwa hofu ya kuchafua sifa ya chombo hicho cha dola.

Wakizungumza kwa sharti la kutotajwa majina yao gazetini, walisema fedha hizo ziliibwa na maofisa hao watatu baada ya kubadili maelezo kwenye hati ya malipo na kuielekeza katika akaunti za mmoja wao.
MwananchiTanesco yapoteza umeme wa Sh 100 bilioni kwa mwaka



Sadick Mtulya
MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (Cag), Ludovick Utouh amesema kuwa upo uwezekano wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kufilisika baada ya kubaini kuwa kila mwaka linakabiliwa na upotevu wa Sh 100 bilioni.
Alisema fedha hizo zinapotea wakati wa kusambaza nishati hiyo kutoka kwenye vyanzo vyake hadi kwa watumiaji.
Utouh alieleza kwenye ripoti yake, ambayo gazeti hili lina nakala yake amebaini shirika hilo limepata hasara ya Sh Sh48 bilioni mwaka uliopita kutokana na ununuzi wa umeme kutoka katika kampuni binafsi, ikiwemo IPTL kufuatia mgawo mkubwa uliojitokeza Septemba na Oktoba, mwaka jana.

Ripoti hiyo ya Cag iliyowasilishwa Aprili 6, mwaka huu katika kikao baina ya watendaji wakuu wa Tanesco na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Masharika ya Umma (Poac) kilichofanyika katika ofisi ndogo za Bunge jijini Dar es Salaam.

Kutokana na hali hiyo, Poac iliiagiza Tanesco kuhakikisha inafanya jitihada za kujinasua katika hali hiyo.



Tanzania Daima: Mitambo jengo jipya la Bunge yakwama


na Kulwa Karedia, Dodoma

SPIKA wa Bunge, Samuel Sitta, jana alilazimika kuahirisha kikao cha Bunge kwa muda wa dakika 45 kutokana na hitilafu ya mitambo ya mawasiliano ndani ya jengo hilo jipya la Bunge.
Spika Sitta alifikia hatua hiyo baada ya kuingia ukumbini, majira ya saa 2.59 na kuanza kusoma dua kama kawaida, ingawa alilazimika kukatisha tena baada ya kipaza sauti chake kutofanya kazi.

Jambo hilo lilisababisha Spika kuendesha dua kwa sauti ya chini huku baadhi ya wabunge wakipigwa na butwaa.

Habarileo: Wagombea watarajiwa wadaiwa kuhonga majeneza 

WATU kadhaa waliotangaza au kuonesha nia ya kugombea nafasi mbalimbali za uongozi ukiwemo ubunge wanadaiwa kutoa rushwa yakiwemo majeneza.

Kisheria kipenga cha kuanza kampeni za kuwania urais, ubunge na udiwani hakijapulizwa na hata kampeni za ndani ya vyama hazijaruhusiwa.

Kampeni hizo haramu zimekuwa zikifanyika hadharani katika mikusanyiko ya watu inayohusu mambo ya kijamii zaidi kuliko siasa na mbaya zaidi imebainika kuwa wagombea hao wamekuwa wakivizia misiba, wakati jamii ikiomboleza kuondokewa na ndugu au jamaa, wao wanafikiria kura za waombolezaji.

Kutokana na hali hiyo ambayo imeonekana kwa wanaotangaza nia za kugombea ubunge kupitia vyama mbalimbali, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) imebainisha mwishoni mwa wiki kwamba inafahamu kuwepo kwa vitendo hivyo na imeanza kuwafuatilia wanasiasa hao.

Mkurugenzi wa Idara ya Elimu kwa Umma wa Takukuru, Mary Mosha alibainisha hayo alipokuwa anatoa mada kwenye semina ya kujadili mbinu sahihi za kuripoti habari za uchaguzi mkuu, inayowashirikisha waandishi waandamizi na wahariri wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) inayochapisha magazeti ya Daily News, Sunday News, HabariLeo na HabariLeo Jumapili.

Raia Mwema: Utata mpya waibuka 'EPA namba mbili'

Mwandishi Wetu
Aprili 14, 2010
Ni fedha za stimulus package alizozitetea Kikwete bungeni
Gavana BoT aruka kiunzi, amtupia mpira msaidizi wake




SAKATA la matumizi yenye kutia shaka ya fungu la fedha lililopitishwa na Bunge kwa ajili ya kuhami uchumi, maarufu kama stimulus package , sasa limemrudia Gavana wa Benki Kuu (BoT), Profesa Beno Ndulu, ambaye baada ya baadhi ya kampuni za ununuzi wa pamba kukosa mgawo huo katika mazingira yanayozua maswali zilimtaarifu naye akawajibu kuwa Serikali haina fedha.

Hata hivyo, wakati Gavana akitoa majibu hayo kuwa “Serikali haina fedha” si fedha zote Sh. trilioni 1.7 zilizoidhinishwa na Bunge la Tanzania ndizo zilizotumika katika mpango huo wa kunusuru uchumi uliotikiswa baada ya uchumi wa dunia kuyumba.

Wiki hii Gavana Ndulu amekwepa kuzungumzia suala hilo, akidai kwamba kwa sasa linashughulikiwa na mtu maalumu chini yake anayepaswa kutafutwa kuzungumzia suala hilo.

Raia Mwema ilipozungumza na Profesa Ndulu, ambaye alieleza kuwa yuko mkoani Mwanza kwa ajili ya mkutano, alisema masuala ya ‘‘stimulus package’’ yamekabidhiwa mtu maalumu ndani ya benki hiyo, na kwamba si yeye anayeweza kuyazumngumzia.

“Haya masuala ya stimulus package tumempa mtu maalumu ambaye ni mkuu wa kitengo cha sera na utafiti, mimi siwezi kuyazungumzia,” alijibu Ndulu hata alipotakiwa kujibu yale yanayomhusu moja kwa moja katika sakata hilo pia hakuwa tayari kuzungumzia.

Uchunguzi wa Raia Mwema umebaini kuwa fedha zilizokwishakutumika ni sehemu tu ya Sh trilioni 1.7 zilizopitishwa na Bunge, ambazo ni takriban Sh bilioni 870.8. Fedha hizo Sh bilioni 870.8 kwa mujibu wa taarifa zilizopo ndizo zilizokwishakutolewa na Benki Kuu (BoT), chombo ambacho kimepewa mamlaka ya kutoa fedha hizo.

Kwa mujibu wa utaratibu wa BoT, fedha hizo hutolewa kutoka benki hiyo kwenda katika benki ambazo zilikopesha kampuni zinazostahili kufidiwa, ambazo zimeathiriwa na mtikisiko wa uchumi duniani.
Nipashe: Sungusungu wawavua nguo walimu na kuwachapa viboko



NA ANCETH NYAHORE



14th April 2010

Walimu watatu wa kike na mke mmoja wa mwalimu wa kijiji cha Sakasaka, tarafa ya Kisesa wilayani Meatu, wamevuliwa nguo na kucharazwa viboko na walinzi wa jadi sungusungu wa kijiji hicho kwa madai ya kutohudhuria mkutano uliokuwa umeitishwa na jeshi hilo.

Imedaiwa kuwa walimu hao walishindwa kwenda kwenye mkutano huo kwa sababu ni wajawazito jambo ambalo sungusungu hao walipinga na kuwalazimisha wavue nguo kuthibitisha kama kweli ni wajawazito mbele ya mkutano huo.

Tukio hilo la aina yake na udhalilishaji kijinsia, lilitokea AprilI 7, mwaka huu kati ya saa na 4:00 na 5:00 asubuhi kijijini hapo.Katibu wa Chama cha Walimu (CWT) wa wilaya ya Meatu, Baraka Owawa, aliiambia Nipashe kuwa walimu hao walikamatwa na sungusungu hao na kuanza kuwapiga, kuwavua nguo kwa madai ya kutohudhuria mkutano.Owawa alisema walimu hao hawakuwa na jinsi yoyote ya kukabiliana na sungusungu hao bali walitii amri hiyo ya askari hao wa jadi kunusuru maisha yao.

Mara baada ya walimu hao kufanyiwa unyama huo, Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Julius Mtuli, alitoa taarifa kwa uongozi wa juu wilayani hapa ikiwemo polisi na ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Meatu na timu maalum kuundwa kwenda kijijini hapo kufuatilia suala hilo.

12 Apr 2010



Kama nilivyoahidi jana, leo nawaletea mahojiano maalum (exclusive interview) na msanii mahiri wa Bongoflava,Hamis Mwinjuma,almaaruf Mwana F.A.Pamoja na mambo mengine,blogu hii ilionelea umuhimu wa kufanya mahojiano na msanii huyo kwa sababu kuu mbili.Kwanza,yayumkinika kum-describe MwanaFA kama mmoja wa wasanii wenye elimu ya hali ya juu baada ya kuhitimu masomo yake hapa Uingereza.Pili,ilitarajiwa kwamba kwa kuwa kwake nje ya nchi kwa muda mrefu kimasomo atakuwa katika nafasi nzuri ya kutupa mwanga kuhusu nafasi ya bongoflava ndani na nje ya Tanzania.Basi nisimalize ladha bali tiririka na mahojianio hayo hapa chini. 









KULIKONI UGHAIBUNI (K.U.):Kwanza,blogu hii inatoa shukrani kwa kukubali ombi la kufanya mahojiano nawe.Pili ni pongezi kwa kuhitimu masomo yako ya Shahada ya Uzamili nchini Uingereza.


Umekuwa ukifahamika zaidi kwa jina la Mwanafalsafa,na wakati mwingine Binamu.Je nini asili au maana ya majina hayo?


MwanaF.A: Nashukuru ndugu yangu.



Mwanafalsafa nilipewa na producer wangu wa kwanza,Dj Boniluv..nilikuwa na wimbo unaitwa ‘mwanafalsafa’(upo kwenye album yangu ya kwanza) na Boni akadhani itakuwa busara nikilitumia jina hilo sababu ya aina ya uandishi wa mashairi nnaoufanya(kujaribu kuzungumzia vitu kwa uzito)..Binamu lilikuja baadae,na linaelezea mahusiano yangu na hadhira nnayoongea nayo,kwamba nawaambia watu vitu ambavyo kaka na dada zao wangeshindwa kuwaambia,pengine sababu ya heshima za kindugu walizonazo,lakini mimi kwa ukaribu na urafiki wa ki’binamu naweza kuwawasilishia.




K.U:Ukiwa mmoja wa wasanii wakongwe wa bongoflava,je ni kipi kinachokuwezesha kubaki kwenye form kwa muda mrefu kiasi hiki?


MwanaF.A:ah,kitu cha kwanza najua nimekuwa mwenye bahati,na namshukuru Mungu kwa hilo..sababu naamini kuna wengi walikuwa na vipawa vya kuweza kubaki lakini hawapo kwa sababu moja ama nyingine..huwa najaribu kusema vitu watu wanavyotaka kuvisikia,na pengine hawakuvitegemea,natafuta namna ya kuzunguka na ideas na kuzijengea hoja..then kilichobaki ni siasa za mziki.

K.U:Tuje kwenye maisha yako nje ya Tanzania.Kama msanii unaonaje nafasi ya bongoflava kwenye anga za kimataifa?:


MwanaF.A:sio kubwa kwa kweli,ina safari ndefu SANA..kuna mambo ambayo kimsingi tunatakiwa kuanza kwa kuyakubali kwanza,mathalani mipaka ya lugha..hili sio suala dogo,na nasema hivyo sababu ili kufanya vizuri nyumbani itakubidi kufanya kwa Kiswahili,ambapo nje ya nyumbani ni shida kukivusha..ubora wa mziki wetu na kukosa kwake uhalisi(kuna hiphop,r&b,afro pop,zouk,kwaito,lingala nk kwenye bongo flava) vinaiweka kwenye hali ngumu sana wakati wa kuutafutia nafasi.Pengine,tungeanza kwa kufanyia kazi vitu viwili hivi,lugha na uhalisi.







K.U: Je katika kipindi ulichokuwa nje ya Tanzania ulifanya kazi zozote za kisanii kushirikiana na wasanii wa nje au una mpango wa aina hiyo?:


MwanaF.A:sikuweza kwa kweli..nilikaribia kufanya kazi na producer Amit,lakini ratiba zangu na zake zikawa zinapishana mno so sikuweza tena..nna mpango wa kufanya kazi na wasanii wan je ndio lakini bado naifikiria Africa kwanza..so nawaza Nigeria na South Africa kwa kuanzia.




K.U: Umaarufu unaambatana na usumbufu.Je wakati uko masomoni Uingereza,ulimudu vipi kukabiliana na hali hiyo (i.e. muingiliano wa umaarufu wako katika masomo yako)?


MwanaF.A:nimekuwa nikisoma kwa muda sasa wakati najulikana julikana na watu(siuiti umaarufu)..see,nimekuwa nafanya mziki wa kusikika na kuonekana kwa takriban miaka 9 sasa na nimezoea kukabiliana na vikwazo nnapotaka langu liwe..nilisoma IFM kwa miaka kadhaa na bado niliweza kukabana na mazingira ya kujulikana na shule,so nje ilikuwa rahisi zaidi,sababu watu wachache zaidi wananijua kulingana na nyumbani.

K.U: Ni dhahiri kuwa kutokana na kiwango chako cha juu kitaaluma,utakabiliwa na majukumu mengine kama kikazi,nk.Je unataraji kubalansi vipi maisha yako kama msanii na majukumu mengine ya kimaisha (mfano kikazi)?:


MwanaF.A:kwa kuanzia nimempa AY majukumu ya kusimamia sehemu kubwa ya kazi zangu za mziki ili nipate nafasi ya kumudu kufanya mambo mengine kwa kuwa yeye ana kampuni inayojihusisha na masuala ya mziki(Unity Entertainment)..hii inanibakisha na kufanya mziki na shows tu ambapo ni maisha niliyoyazoea..bado naendelea kufikiri namna bora zaidi ya kutogonganisha majukumu..najaribu kutoweka mipaka kwenye idadi ya vitu nnavyoweza kuvifanya,napigana na haya maisha na najaribu kunyoosha mambo kwa kadri nnavyoweza.





K.U:Je unadhani hatua uliyopiga kitaaluma inaweza kuzaa matarajio mapya kwa washabiki wako hususan kwenye ujumbe uliomo kwenye tungo zako?


MwanaF.A:yeah,naishi najifunza..kila hatua ya maisha nnayopitia ni somo kwangu na nadhamiria kuwaambia watu wangu vingi nnavyojifunza..so hata hatua za kitaaluma nnazopiga zinaniongeza uelewa wa vitu na nimepanga kushiriki na hadhira yangu,sio kwa namna ya kishule,bali kwa namna ambayo mitaa itaelewana nayo.








K.U:Swali linaloshabihiana na hilo lililotangulia.Je kwa hatua uliyopiga kitaaluma,jamii itarajie mtazamo mpya kwenye tungo zako?


MwanaF.A:jibu lake ni exactly kama lililopita.


Nnachoweza kuking’arisha hapa ni kuwa sitaki kuchanganya sana shule yangu na huu mziki isipokuwa kwenye namna ya biashara na vitu vichache vitakavyohitaji mawili matatu nnayojifunza kila kukicha...huhitaji masters degree kutengeza mziki mzuri....huu ni wa mtaa na ntaendelea kuufanya kwa ajili ya mitaa,kama unanielewa vizuri..mara nyingi nyumbani unaweza kuhukumiwa kwa kujua.



K.U:Kama msanii msomi kabisa una ushauri gani kwa wasanii wengine kuhusu suala la kujiendeleza kielimu?


MwanaF.A:namna pekee ya kuliangalia hili kwa wasanii ni kuwa,tusiache maisha yetu yakawa sehemu ya mziki tunaoufanya,bali mziki wetu uwe sehemu ya maisha tunayoishi..niliamua kurudi shule sababu nilikuwa nataka kubaki kuwa mtoto wa mama Hamis,na kwa kufanya kile ambacho ningekifanya kama nisingekuwa mwanamuziki...mziki,HASA HUU WETU, una siasa nyingi na hautoi ahadi ya kukupa uwezo wa kuyamudu maisha yako yote yaliyobaki na familia yako,hivyo ni busara kuwa na mipango ya ziada.





K.U: Kwa uzoefu wako baada ya kuwa nje ya Tanzania kwa muda mrefu,una ushauri gani kwa wasanii wenzio kuhusu uwezekano wao kuvusha kazi zao za sanaa nje ya mipaka ya Tanzania?




MwanaF.A:ni kama nilishajibu na hili mkuu..tunapaswa kuondoka kwenye denial state kwanza..tukubali kuufanyia marekebisho ya kimsingi mziki wetu then tukimbizane na chochoro za kuuvusha..vinginevyo tutaendelea kuimbia wa’Tz 200-300 kwenye maonyesho yetu ya nje kila wakati.




K.U: Mwisho,una ujumbe gani kwa mashabiki wako.Je wategemee vitu vipya hivi karibuni?


MwanaF.A:yeah,maskio yakae wazi..nawadondokea punde tu.








Blogu hii inakutakia kila la heri katika shughuli zako.


MwanaFA: Ahsante sana,nashukuru..na pole kwa kuchukua muda mwingi kujibu..mbio za maisha tena..na naamini wewe na watembeleaji wa blogu mtanielewa.


.

11 Apr 2010

Kama nilivyoahidi awali,blogu yako itakuwa ikikuletea mahojiano na Watanzania 'wanaowakilisha' (representing) nchi yetu kwa namna moja au nyingine.Na sasa nafurahi kukujulisha kuwa blogu imekamilisha mahojiano na supastaa big name wa bongoflava.Could you make a guess?Hint: Ni msanii mwenye kipaji cha hali ya juu katika kupangilia verses na lyrics zake,sambamba na uwezo mkubwa wa 'kucheza na maneno' na kwa sasa ni mwana bongofleva mwenye elimu ya kiwango cha juu kabisa. Na hapa chini (video) inakupa hint zkubwa zaidi.
Mahojiano kamili yatawekwa hapa kesho katika versions mbili:Kiingereza na Kiswahili.USIKOSE

10 Apr 2010

Kama Mtanzania mzalendo na mwenye kupenda nchi yangu nawajibika kuwa na heshima kubwa kwa Rais wangu Jakaya Kikwete.Hata hivyo,heshima inapaswa kuendana na matendo ya mheshimiwa.Kwa maana hiyo,naamini simkosei heshima Rais wangu nikihoji baadhi ya busara zake.Mpaka muda huu sielewi nini kinaendelea kati ya JK,Husna Mwilima na Sophia Simba!Awali,Sophia Simba kama Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa CCM alisimama kidete kuhakikisha Mwilima 'anapigwa chini'.Tuhuma zilizotolewa dhidi yake ni 'mapungufu katika utendaji wake wa kazi.'Sasa kama tukiamini kuwa ni kweli Mwilima alishindwa kumudu majukumu ya uongozi huko UWT,how come JK ameamua kumpa ukuu wa Wilaya? Na kwa kuonyesha kuwa mambo yanaendeshwa kienyeji,Mwilima hakuchelewa 'kutoa mipasho kwa wabaya wake' pale alipotamka bayana kuwa kuteuliwa kwake na JK kuwa DC wa Tandahimba ni 'majibu ya JK kwa akina Sophia Simba'.Huwezi kumlaumu kuwa 'ameropoka' kwa vile hakujiteua.

Lakini swali la msingi ni kwamba je ni kweli JK ameamua kumteua Mwilima kumwonyesha Sophia Simba na UWT yake kuwa mwanamama huyo (Mwilima)aliondolewa katika wadhifa wake huko UWT kwa mizengwe na si mapungufu ya utendaji kazi?Lakini kama jibu la swali hilo ni ndio,hivi JK si ndio Mwenyekiti wa CCM ambayo UWT ni jumuiya yake,na kwa maana hiyo alikuwa na uwezo wa kusimamia mtizamo wake kuwa Mwilima ni mtendaji kazi hodari?Kwanini aliacha mwanamama huyo adhalilishwe huko UWT kabla ya kuamua 'kumsafisha' kwa kumpa u-DC?

Katika picha kubwa zaidi,je inawezekana utoaji wa baadhi ya vyeo unafanyika sio kwa maslahi ya wananchi bali kusafishana na 'kupunguza maumivu ya kisiasa'?Nauliza hivyo kwa vile naamini kwamba kama Mwilima alikuwa ameonewa huko UWT,JK alikuwa na uwezo mkubwa wa 'kumlinda' kama alivyoamua 'kumlinda sasa' kwa kumpa u-DC.Kwa kukaa kwake kimya wakati Mwilima 'anapelekeshwa' huko UWT,inatafsiriwa kuwa alikuwa anaafikiana na maamuzi ya akina Sophia Simba.Lakini kwa uamuzi huu 'mpya' wa kumpa Mwilima u-DC,inatafsiriwa (kama anavyosema Mwilima) kuwa anafikisha ujumbe kwa akina Sophia Simba kuwa Mwilima 'alionewa tu huko UWT kwani bado ana sifa za kuongoza wananchi huko Tandahimba kama DC'!

Nilisema mwanzoni kuwa namheshimu Rais wangu JK lakini nadhani aidha ana washauri wabovu au yeye mwenyewe maamuzi yake ni dhaifu.Na bahati yake ni kwamba Watanzania wengi hawana muda wa kuhoji au 'kukomalia' baadhi ya maamuzi yake.Ni aibu kwa Rais wetu kugeuka sehemu ya mipasho ya akinamama hao (Mwilima na Sophia Simba).Ni dhahiri kinachofanyika hapo ni kupoza pande zote mbili,yaani JK kama Mwenyekiti wa Taifa wa CCM aliamua kukaa kimya pale Sophia Simba na wenzake walipomtimua Mwilima,lakini katika kumpoza Mwilima akaamua kumpatia 'zawadi' ya u-DC.

Halafu kwa mtindo huu tutarajie Maisha Bora kwa Kila Mtanzania?

9 Apr 2010

Yea,I know,it's none of my business but,man,this story left me quite perplexed.Lots of stuff's already been said about what you might call 'the foreign arms of our ruling party CCM.And much of it isn't funny to read,but I personally don't have any issues with people exercising their democratic rights by forming or joining 'matawi ya CCM nje ya Tanzania'.However,as I once wrote,these branches and their members could surely be so instrumental in reforming the old party especially at times when it's perceived by many as the godfather of 'ufisadi'.Our bothers and sisters in the form of 'wanachama wa CCM nje ya nchi' could use their foreign experience to make CCM return to its root as a party of peasants and workers instead of leaving it being hijacked by and put in control of some unscrupulous tycoons (mafisadi). All I could ask our CCM friends in Russia is to settle their differences amicably and avoid tarnishing their party's and own images by the on-going infighting.I sincerely understand that this is a private party affair but wisdom could easily prevail by keeping this matter private instead of making it public.That's,however, not suggesting that the Moscow Branch of CCM should not make use of the web to keep the public informed of whatever they are up to.We have had enough of the thuggery of our local politics,and surely we wouldn't wish to see the same be replicated in the party's 'overseas branches'.The best thing to do with private problems is to see them stay private

A discovery about the way HIV attacks the immune system could pave the way for the development of new treatments. Researchers have identified a new method in which the human immunodeficiency virus, which causes Aids, is able to prevent tetherin - a protein found naturally in human cells - from doing its job of blocking the invaders.

This highly-skilled study has been carried out by a team based in Montreal in Canada.

The hope now is that this information will help scientists to target certain aspects of the virus and therefore develop new anti-HIV drugs.

At the moment, there is no way of knowing how much of a difference this discovery will make to HIV therapy and any such developments could take decades.

Almost 33 million people around the world are thought to be living with HIV and AIDS.

SOURCE: ITN

JK alisaini sheria hiyo kwa mbwembe kama alivyoahidi.Siku chache baadaye,Dkt Wilboard Slaa akaibua hoja kuhusu 'usanii' uliofanyika kuongeza vipengere katika Sheria hiyo.Spika na Mwanasheria Mkuu wa Serikali wakatetea 'usanii' huo.Licha ya mlolongo wa matukio hayo kuashiria kuwa sheria hii yenye nia njema itabaki kuwa maandishi tu,walengwa wakuu wa sheria hiyo wameamua kuipuuza na 'misaada' inatolewa kama kawaida katika kujitengenezea mazingira ya ushindi kwenye uchaguzi. Dk. Nkya kujitosa ubunge Morogoro Kusini Mashariki

na Joseph Malembeka, Morogoro

NAIBU Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Dk. Lucy Nkya, ametangaza nia ya kuwania ubunge katika jimbo la Morogoro Kusini Mashariki.
Dk. Nkya alitangaza nia hiyo akiwa katika ziara ya kukagua maenndeleo na utekelezaji wa ahadi alizotoa baada ya kuchanguliwa kuwa mbunge wa Viti Maalum.

“Nawatakeni wanachama wenzangu ndani ya CCM muelewe kuwa na mimi nakuja huku mbali na kuwa kuna wenzangu waliotangaza nia hii,” alisema Dk.Nkya.

Dk. Nkya ambaye kwa nyakati tofauti alikabidhi vitu mbalimbali yakiwemo mabati, vipaza sauti, saruji, vyerehani, misumari, baiskeli na fedha taslimu sh 1,500,000 kwa wananchi na wana CCM katika kata mbalimbali aliwataka wana CCM kukiimarisha chama na wao kiuchumi.

“Sasa hivi tunakwenda kwenye hekaheka za uchaguzi ila nawatakeni mbali na siasa jiimarisheni kiuchumi kwa kulima mazao yanayokomaa kwa muda mfupi na yanayostahimili ukame tuepukane na janga la njaa,” alitahadharisha Dk. Nkya.

Dk. Lucy Nkya anakuwa miongoni mwa watu saba walioonyesha nia ya kuwania ubunge katika jimbo hilo. Wengine ni mbunge wa sasa wa jimbo hilo (Samir Lotto), Jamira Mohamed, Amani Mwenigoha, Gabriel Mkwawe, Semindu Pawa na Salumu Salum Mkangala.

CHANZO: Tanzania Daima.

Takriban nusu karne tangu tupate uhuru tunakutana na takwimu zinazopaswa kuchochea mjadala wa umuhimu wa kumuondoa mkoloni.Kwa mujibu wa gazeti la Mwananchi,zaidi ya asilimia 90 ya uchumi wa Tanzania unamilikiwa na wageni.Kwa bahati mbaya (au makusudi) habari hiyo haikuingia kwa undani kujadili impacts zinazosababishwa na hali hiyo lakini kilicho wazi ni kwamba uhuru wetu uko mashakani.Katika zama hizi ambapo nguvu za kiuchumi zina athari kubwa kwenye siasa,ni dhahiri kuwa hata huo uhuru wetu wa kisiasa unabaki kuwa wa kinadharia zaidi kuliko uhalisia..Habari husika ni hii hapa
Na Ramadhan Semtawa
ZAIDI ya asilimia 90 ya uchumi wa Tanzania unaendelea kumilikiwa watu wenye asili ya Asia na Ulaya, takwimu zinaonyesha.

Takwimu hizo zimetolewa huku kukiwa na kilio kikubwa cha Watanzania wazawa, kutaka wajengewe mazingira mazuri ya uwezeshaji ili kumiliki uchumi wa nchi kupitia migodi mikubwa ya madini na maeneo nyeti ya kiuchumi.

Lakini wakati kilio hicho kikiwa hakijapata ufumbuzi, Taarifa ya Utendaji ya Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi, iliyowasilishwa katika kikao cha Kamati ya Bunge ya Fedha na Uchumi jana, ilisema watu wenye asili ya mabara ya nje wanaomiliki uchumi wa Tanzania ni sawa na asilimia moja ya Watanzania.

Takwimu hizo zilifafanua kwamba, asilimia hiyo 90 ya uchumi wa nchi umeshikwa na watu wenye asili ya Asia na Ulaya, wakati asilimia 99 ya Watanzania wazawa, hawana kitu.

Kwa mujibu wa takwimu hizo zilizowasilishwa katika kikao hicho kilichohudhuriwa pia na Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi, Omar Yusuph Mzee, tatizo la Watanzania weupe kumiliki uchumi, lilianza tangu wakati wa ukoloni.

"Wakati wa enzi za ukoloni na hata baada ya uhuru Watanzania wengi hawakuwa wakishiriki kikamilifu katika kumiliki uchumi wa nchi yao. Uchumi wa nchi umeendelea kutawaliwa na wageni wakishirikiana na Watanzania wachache," inasema sehemu ya ripoti hiyo.

Ripoti hiyo inasema "asilimia 99 ya wananchi ni Watanzania weusi na asilimia 1 iliyobaki inajumuisha Waasia na Wazungu ambao wana miliki zaidi ya asilimia 90 ya uchumi wa nchi hii (Msambichaka, 2008).

"Hii ina maana asilimia 99 ya Watanzania halisi wanamiliki asilimia 10 tu ya uchumi wa taifa lao," inasisitiza ripoti.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo, serikali imekuwa ikifanya juhudi mbalimbali za kurekebisha kasoro zilizoko, ikiwa ni pamoja na kuanzisha (lililokuwa) Azimio la Arusha, Vijiji vya Ujamaa, Elimu ya Kujitegemea, Serikali za Mitaa, Vyama vya Ushirika, Sera ya Uwekezaji na Sera ya Ubinafsishaji wa Mashirika ya Umma.

Inasema hata hivyo,juhudi hizo hazijazaa matunda yaliyotarajiwa na kwamba na kwamba kushindikana kwa juhudi za kuwawezesha Watanzania kushiriki kikamilifu katika kujenga uchumi wa nchi yao, ndilo chimbuko la kubuniwa kwa mkakati wa kuwawezesha wananchi kiuchumi, katika ilani ya CCM ya mwaka 2000."

CHANZO: Mwananchi

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.