5 Apr 2010

Ukifuatilia kwa karibu namna nchi yetu ilivyogeuzwa 'shamba la bibi' unaweza kupata shinikizo la damu siku si zako.However,shinikizo la damu or not,tutaendelea kufahamishana namna ufisadi unavyoiteketeza nchi kwa kasi,ari na nguvu kubwa.Na haya yanatokea wakati kuna watu wanalipwa mishahara kuhakikisha hayatokei. Nimekutana na habari moja kwenye gazeti la Mwananchi ikieleza kwamba Jeshi la Magereza limekumbwa na kashfa ya ufisadi wa shilingi milioni 300.Ufisadi huo umewekwa hadharani na Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali kwa Kamati Ya Bunge ya Hesabu za Serikali.Yaani taasisi iliyopewa jukumu la kuwahifadhi na kuwarekebisha tabia wafungwa nayo inafanya yaleyale yaliyopelekea wengi wa wafungwa kuwa jela in the first place.Well,namaanisha wale waliofanya uhalifu lakini hawakuwa na majina ya kuwalinda au hawakuwa na uwezo wa kuhonga ili kesi zao zife kienyeji.

Kichekesho ni kwamba wezi wa mamilioni hayo walifikishwa mahakamani (pengine katika kutuzuga kuwa sheria inachukua mkondo wake) lakini wakaachiwa huru katika kile kinachofahamika kisheria kama want of prosecution.Kichekesho kingine ni kwamba licha ufisadi huo,Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi imelipa jeshi la magareza 'hati safi'.Yani ni kama wanapongwezwa kwa kuiba mamilioni badala ya mabilioni kaka wenzao huko Benki Kuu,TRA,nk.Na kikubwa zaidi ya kichekesho ni kauli ya Mbunge Mudhihir Mudhihir,ambaye ni mjumbe wa Kamati hiyo ya Bunge,kwamba "Pamoja na kwamba mna hati safi, lakini upotevu huu wa fedha unasikitisha sana..."Hivi kusikitika sana kunasaidia nini?Kwanini badala ya kupoteza muda kusikitika,Mbunge huyo na Kamati yake wakaagiza hatua zaidi za kisheria?Rais anasikitika,mawaziri wanasikitika,wabunge wanasikitika!Yani utadhani kwa kusikitika kwao mafisadi watapatwa na huruma na kusitisha ujambazi wao.

Well,makala hii inauliza Mdhibiti na Mkaguzi wa nini nikimaanisha ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali inavyofanya kazi ya kujaza maji kwenye gunia.Ikumbukwe kuwa uandaaji wa ripoti za ofisi hiyo unahisisha matumizi ya fedha za walipakodi.Kinachokasirisha ni ukweli kwamba taarifa za ofisi hiyo zimeendelea kuwa kama utaratibu tu wa kusukuma siku kwani wenye mamlaka ya kuzifanyia kazi hawaonekani kuguswa kwa namna yoyote na wingi wa tarakimu katika fedha zilizofisadiwa.

Picha hapo juu inamwonyesha Rais Kikwete akipokea ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu,Ludovic Utouh.Unaweza kupata matumaini kuwa labda ripoti hiyoi inaweza kufanyiwa kazi mwaka huu kwa vile kuna uchaguzi,au kwa vile CCJ imezaliwa...kalagabaho,huo ni utaratibu tu.Utouh katimiza wajibu wake,na JK nae katimiza wajibu wake wa kupokea taarifa,na kupigwa picha inayoashiria kuwa tuna Tanzania ina uongozi unaoguswa sana na matumizi ya fedha za umma!

2 Apr 2010

Jana ilikuwa Siku ya Wajinga Duniani.Binafsi niliiadhimisha kwa matendo mawili.Kwanza niliweka 'breaking news ya kizushi' kuwa Baba Mtakatifu Benedikti wa 16 ametangaza kujiuzulu kufuatia skandali ya ngono na ulawiti inayolikabili Kanisa Katoliki.Pili,kwenye ukurasa wangu wa Facebook niweka tahadhari kuwa 'pranks' kama kuwapigia simu polisi na kudai wewe ni gaidi wa kujilipua bomu la kujitoa mhanga (suicide bomber)zinaweza kumwingiza mtu matatani hata kama zilikuwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Wajinga.Vitendo au kauli za utani katika Siku ya Wajinga zina mipaka yake. Nimekutana na habari katika gazeti la Mwananchi kuwa Kamati ya Bunge ya Miundombinu imetoa ushauri wa kununuliwa ndege nyingine ya rais kwa madai kuwa zilizopo zimechoka.Naamini kuwa kauli hiyo ilikuwa sio serious bali ni sehemu tu ya maadhimisho ya Siku ya Wajinga Duniani.Kama kauli ya Mwenyekiti wa Kamati hiyo,Mohammed Missanga ilikuwa ya dhati basi yayumkinika kusema kwamba baadhi ya wanasiasa wetu wana upeo finyu kupindukia linapokuja suala la vipaumbele vyetu kama taifa.

Of course,rais kama mheshimiwa hawezi kusafiri kwa miguu au kwa punda,japo wengi wa anaowatawala ni masikini wa kutupwa ambao hawawezi kumudu hata gharama ya mlo wa siku.Lakini pamoja na uheshimiwa huo wa rais,na umuhimu wa yeye kusafiri kwa ndege yake maalum,wazo la kumnunulia ndege mpya ni mufilisi na linalopaswa kukemewa kwa nguvu zote.Kama hoja ni uzamani wa ndege zilizopo basi kuna haja gani ya kupuuzia malalamiko ya wafanyakazi wa serikali wanaotoshia kugoma kwa madai ya mishahara kiduchu?Maana nao pia mishahara yao ni ya zamani kama zilivyo ndege za rais.

Missanga na Kamati yake wanapendekeza pia kununuliwa helikopta zitakazowezesha viongozi kufika maeneo yanayokumbwa na majanga.Hivi la muhimu ni kufika kwa viongozi katika maeneo hayo au first responders (eg zimamoto)?Kwanini kipaumbele kisiwe katika kuboresha vitendea kazi vya first responders badala ya nyenzo za usafiri wa viongozi?Kwahiyo kiongozi akishafika eneo la janga atasaidia kuokoa maisha ya wahanga wa janga husika?Au Missanga na wenzake anajaribu kutueleza kuwa mara nyingi hakuna jambo linalofanyika hadi kiongozi afike mahala husika?Kama ni hivyo,la muhimu si ndege au helikopta mpya bali uongozi na usimamizi mzuri wa nguvu kazi,sambamba na kukomesha tabia ya kusubiri maagizo ya rais au viongozi wengine wakuu katika kuutumikia umma.

Na kichekesho cha mwaka,na kilichonifanya niamini kuwa kauli ya Missanga na wenzie ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Wajinga,ni ukweli kuwa ndege za rais zimetumika kwa asilimia 37 tu hadi kufikia mwezi Machi mwaka huu.Kwa lugha sahihi,ndege hizo zimetumika chini ya nusu ya mahitaji yake.Je hiyo si sababu tosha kuonyesha kuwa ndege hazina umuhimu na ndio maana zinatumika 'kwa bahati mbaya'?

Leo ni Ijumaa Kuu.Kwa Wakristo,hii ni siku ambapo mkombozi wetu Yesu Kristo alitoa maisha yake msalabani kuwakomboa wanadamu.Japo natambua kuwa uongozi wa kisiasa ni tofauti na wa kidini lakini mfano wa Bwana Yesu kutoa maisha yake kwa ajili ya wanadamu unapaswa kuigwa na viongozi wetu kwa maana ya kujitoa mhanga kwa ajili ya wanaowaongoza.Na mhanga ninaozungumzia hapa sio wa kujitoa maisha kama alivyofanya Bwana Yesu bali kuangalia kuwatumikia wananchi kwa uadilifu na ufanisi.

1 Apr 2010

Katika hali isiyotarajiwa,Baba Mtakatifu Benediktini wa 16 ametangaza kujiuzulu wadhifa huo kufuatia tuhuma zinazoliandama Kanisa Katoliki kuhusu kashfa za ngono na ulawiti. Uzushi tu wala hajajiuzulu.Leo ni Siku ya Wajinga Duniani.Je wewe ni miongoni mwao (at least kwa leo)?

31 Mar 2010

Picha kwa Hisani ya Blogu ya Dina Marios
Mie kama Mkatoliki,siafikiani na ushoga au usagaji.Lakini kutoafikiana na kitu ni jambo moja na kukizuia ni jambo jingine.Ni ukweli usiofichika kuwa vitendo vya ushoga na usagaji vinaanza kuonekana kuwa vya kawaida katika jamii ya Kitanzania,hususan jijini Dar es Salaam.Je wakati umefika sasa kuhalalisha ushoga na usagaji?Na je kwa sheria za nchi ku-criminalise homosexuality inakiuka haki za binadamu?Na pengine swali la ziada,kuufanya ushoga na usagaji kuwa mithili ya laana kumesaidia chochote kuukomesha? Ni mjadala wa miaka nenda miaka rudi,karne baada ya karne.Je ushoga na usagaji ni tabia tu ya mwanadamu au ni asili?Ukitafuta jibu la mkato,unaweza kutotenda haki kwa upande mwingine wa mjadala.Kwa ufahamu wangu mdogo,kuna maelezo ya takriban aina mbili.Hoja ya kwanza,ushoga na usagaji ni suala la kimaumbile/kibaiolojia zaidi kuliko ridhaa ya mwanadamu.Maelezo haya yanazingatia wingi wa homini za jinsia tofauti kwatika mwili.Kwa maana kwamba mwanamke mwenye homoni nyingi za kiume ana uwezekano wa kuwa msagaji,na mwanaume mwenye homoni nyingi za kike anaweza kuwa shoga.Ni ishu complicated lakini nimejaribu kuieleza kwa kifupi.

Hoja ya Pili,ushoga na usagaji ni tabia tu ya mwanadamu kama zilivyo tabia nyingine.Yaani ni kama mtu anapoamua kuwa mvuta sigara au mtumia kilevi.Namna mhusika anavyoangukia kwenye tabia ya ushoga au usagaji nayo inaweza kuangalia kwa namna kadhaa.Kwa mfano,mwanadamu anaweza kuangukia kwenye ushoga au usagaji kwa tamaa.Au anaweza kuingia kwenye vitu hivyo kutokana na kuiga.Au pia anaweza kuwa 'majeruhi wa mchezo mchafu' i.e. alilawitiwa jela akaishia kupenda,alijaribu akanogewa,nk.La muhimu hapa ni kwamba uamuzi wa kuwa shoga au msagaji ni katika kile wanasosholojia wanakiita rational choice.Mtu anapima faida na hasara (cost and benefit analysis) kisha anachukua uamuzi anaoona unafaa.Pia hapa kuna suala la makuzi (socialisation) ambapo zawadi na adhabu (rewards and punishment),au tuseme sanctions,zinachangia kukua au kusinyaa kwa tabia husika.Kama familia,kwa mfano,haikemei tabia flani basi kuna uwezekano wa tabia hiyo kuonekana inakubalika.Lakini pia kuna vitu kama fedha ambapo mtoto analawitiwa kisha anapewa fedha inayoweza kumwaminisha kuwa alichofanya ni sahihi.Again,ni maelezo complicated sana na ni ya kitaaluma zaidi kuliko kimtaani.

Yote katika yote,ushoga na usagaji unazidi kushamiri katika jamii yetu licha ya 'jicho kali' la jamii.Je hiyo inamaanisha kuwa ukali huo dhidi ya tabia hiyo umeshindwa kuleta ufanisi?Tukiangalia suala hilo kwa mtazamo wa kisosholojia,inawezekana jibu lisiwe kuwa jamii imeshindwa bali ni ukweli kwamba katika jamii yoyote kuna uwezekano wa kuwepo tabia zisizokubalika.Hiyo ni katika kile wanasosholojia wanakiita deviance.Kila jamii ina walevi,wazinzi,vibaka,mafisadi,nk.Ni makundi yanayokwenda kinyume na kanuni na taratibu zinazoiongoza jamii husika.

Kwa huku nchi za Magharibi,ushoga na usagaji unazidi kuwa jambo la kawaida katika jamii.Lakini sio kirahisi hivyo kwani bado mashoga na wasagaji wanaangaliwa kwa 'jicho la shaka'.Na wao ni miongoni mwa makundi yanayolalamikia kubaguliwa.Hata hivyo,sheria zinawalinda na katika baadhi ya nchi hata ndoa zao zinatambulika kuwa ni ndoa halali.Lakini tena,kuwa na sheria ni kitu kimoja,na jamii kuiheshimu ni kitu kingine.Ni katika minajili hiyo,mashambulizi au uonevu dhidi ya mashoga na wasagaji si jambo geni katika nchi hizo.

Hawa wenzetu wanaamini kuwa mashoga na wasagaji hawastahili kubaguliwa,pasipo kujali kwanini mtu amekuwa shoga au msagaji.Na kinachoangaliwa hapo ni haki za binadamu.Wanasema ushoga au usagaji haumuondolei mtu haki zake kama mwanadamu.Je,kwa mtizamo huo wa Kimagharibi,ina maana jamii yetu huko nyumbani inawanyima haki wanajamii wenzao wanaojihusisha na ushoga na usagaji?Well,kuna wanaosema mila na desturi zetu zinapinga vitendo kama hivyo.Je mila hizo ziendelee kudumu hata kama zinawabagua baadhi ya wanajamii?Binafsi sina jibu sahihi bali nadhani swali hilo linabaki mikononi mwa jamii yetu.

Sijui wewe msomaji unaonaje lakini mie binafsi,nikiweka kando imani yangu ya Kikatoliki,sijali sana namna gani mtu anatumia uhuru wake wa kijinsia alimradi hanikwazi kwa namna yoyote.Naweza kutamka bayana kuwa namchukia zaidi fisadi anayekwaza maendeleo ya nchi yangu kuliko shoga au msagaji anayefanya anachoamini ni sahihi kwake.Lakini hiyo sio kusema naunga mkono vitendo hivyo hasa kwa vile imani yangu kiroho haiafiki.


Mwaka 1996 nikiwa mwanafunzi wa mwaka wa kwanza pale Mlimani nilipata 'somo' moja muhimu kuhusu wanasiasa wa Tanzania.Ilikuwa ni kwenye mhadhara (lecture) ya Dr (Profesa kwa sasa) Max Mmuya katika somo Siasa na Serikali Tanzania na Nchi Nyingine za Afrika Mashariki (PS 102),ambapo mhadhiri huyo alitupatia wasifu wa wagombea urais wanne walioshiriki Uchaguzi Mkuu wa mwaka 1995.Pasipo kuingia sana kiundani,wagombea hao wote walikuwa 'wawakilishi wa tabaka tawala'.Hakuna mmoja kati yao ambaye tungeweza kumtambua kama 'mlalahoi'.Ni katika minajili hiyo ndipo makala hii inajaribu kuangalia kama ujio wa CCJ utakuwa na lolote jipya kwa 'mlalahoi' (mtu wa kawaida mtaani)Binafsi,tafsiri yangu ya kwanza ya ujio wa CCJ katika kipindi hiki tunachoelekea uchaguzi mkuu hauna tofauti sana na wanasiasa wanaobadili vyama pindi wakiona hawana nafasi ya kupitishwa na vyama vyao kugombea nafasi flani au wale ambao hawakupitishwa na vyama hivyo.Japo hiyo ni haki yao ya kikatiba,jamii inapaswa kuwaangalia wanasiasa hao kwa jicho la shaka pia.Je wanafanya hivyo kwa minajili ya kupata fursa ya kuutumikia umma au ni maslahi binafsi?Historia inaweza kutusaidia katika kupata jibu la swali hili.Mara nyingi tumesikia wanasiasa wakipita huku na kule wakijaribu kutuaminisha kuwa bila wao hatuwezi kupata maendeleo.Cha kuchekesha ni kwamba baadhi ya wanaotueleza hivyo,wamekuwa madarakani miaka nenda miaka rudi na badala ya kusonga mbele maendeleo yetu yanazidi kudorora.

Ni vigumu kuamini kuwa CCJ italeta mabadiliko yoyote ya maana kwa vile kimsingi chama hicho hakina tofauti na CCM,Chadema,CUF au chama kingine cha siasa.Labda tofauti kubwa ni kuwa CCJ si chama tawala,lakini kama ni hilo basi hata Chadema au NCCR Mageuzi navyo si vyama tawala.Labda tofauti nyingine ni upya wake.Lakini historia pia inatuusia kuwa si kila kipya ni kinyemi.Upya wa chama si jambo la muhimu kwa wananchi bali ufanisi wake katika kuwatumikia.Je katika mazingira tuliyonayo,CCJ inaweza kweli kuwa mkombozi wa Watanzania?Jibu linaweza kupatikana kutoka kwa waasisi wa CCJ na sie wananchi wenyewe.Kwa viongozi wa chama hicho,so far hawajatuthibitishia kuwa ujio wa chama chao utaleta lolote jipya zaidi ya maneno mataaaamu just like ilivyo kwenye miongozo mbalimbali ya CCM.Kama nilivyowahi kuandika mara kadhaa,tatizo la Tanzania (na pengine Afrika kwa ujumla) halijawahi kuwa katika kuunda mawazo au mipango mizuri.Siku zote kikwazo chetu ni usimamizi na utekelezaji wa mawazo/mipango hiyo.

Ni katika minajili hiyo ndipo wananchi wanapaswa kuhoji kama CCJ sio CCM kwenye jezi nyingine.Yani mvinyo wa zamani kwenye chupa mpya.Na kibaya zaidi,kwa kuzingati tukio la jana ambapo mmoja wa wabunge wa CCM Fred Mpendazoe ametangaza kujiunga na CCJ,chama hicho kipya kina kila dalili ya kuwa CCM-B.Hilo halina ubaya iwapo wanaotoka CCM na kujiunga na CCJ watakuwa wanasiasa wenye uchungu wa dhati kwa nchi yetu na wenye nia ya kuutumikia umma kwa uadilifu.Lakini miaka arobaini na ushee ya uhuru wetu imeshatupa darasa zuri kuhusu wanasiasa wetu.Wengi wao wametawaliwa na ubinafsi huku wakiamini kuwa ni wao pekee ndio wenye ujuzi,nguvu,mamlaka na haki ya kutuongoza.Kibaya zaidi,kwa kiasi kikubwa wengi wao wamechangia mno kutufikisha hapa tulipo:hohehahe wa kutupwa huku raslimali za nchi yetu zikiibiwa kana kwamba hazina mwenyewe.

Pengine siitendei haki CCJ kwa kuiona kama shati chakavu lililopigwa pasi na kunyunyiziwa uturi.Lakini nina kila sababu ya kuhofia ujio wake.Japo natambua kuwa katika siasa timing is everything,lakini kwa muda huu mchache uliosalia kabla ya uchaguzi mkuu,yayumkinika kuamini kuwa chama hicho kitakuwa washiriki tu badala ya kuwa serious contenders.Hilo si baya sana iwapo matokeo mabaya kwenye uchaguzi ujao hayatopelekea hadithi kama za NCCR Mageuzi mwaka 1995.Tatizo la vyama vinavyofikiria uongozi tu badala ya utumishi kwa umma ni kwamba vikishindwa uchaguzi basi ndio inakuwa mwisho wa safari.Yani vinakuwa kama mapenzi ya pesa,ukiwa nazo utaonekana mfalme,'ukifulia' unabwagwa.

Nimalizie kwa hitimisho lisilopendeza kwa wale wanaotaka kuiona CCM ikidondoka kwenye uchaguzi mkuu ujao.Kinyume na fikra zinazoelekea kupata umaarufu kuwa ujio wa CCJ ni kilio kwa CCM,ukweli ni kwamba chama hicho kimekuja kugawa kura za wapinzani.Hilo linaweza tu kuepukika iwapo CCJ itaamua kushirikiana na chama kingine/vingine kwenye uchaguzi mkuu ujao.Lakini kinachokwaza ushirikiano wa vyama vyetu vya upinzani sio kutofautiana kwa sera zao bali ubinafsi.Wapinzani wataendelea kuwa wapinzani kwa muda mrefu huku CCM 'ikipeta' licha ya kulea ufisadi na kuipeleka nchi kusikoeleweka.Kwa wapiga kura,CCM inabaki kuwa the devil they know.Ni uamuzi mbovu lakini at the end of the day unaendelea kuiweka CM madarakani.

Na nisisahau.CCJ ina kazi ya ziada ya kukabiliana na 'nguvu za giza' zinazotumia pesa za walipa kodi kuhakikisha CCM inatawala milele.Na si ajabu miongoni mwa wanaopigia debe CCJ,au watakaojiunga hivi karibuni, ni wawakilishi wa nguvu hizo za giza.

30 Mar 2010

Your blog-Kulikoni Ughaibuni-is always striving to come up with spanking new ideas,the latest being an introduction of "THE WEEK IN BULLSHIT".It's all about the weirdest,craziest and even funniest stuffs that happened during a given week. Siku zote Blogu yako ya Kulikoni Ughaibuni imekuwa ikijitahidi kuja na mawazo mapya,na lililojiri sasa ni UPUUZI/UBABAISHAJI KATIKA WIKI.Hii itahusu habari za vimbembe,uzushi na vichekesho vilivyojiri katika wiki husika.

Kimbembe cha kwanza katika safu hii ni taarifa kwamba mwanamama mmoja aliyetinga nyumbani kwa Inspekta Jenerali mstaafu wa Polisi (IGP),Omari Mahita,"kujitambulisha" kuwa ni mtoto wa afannde huyo,ameishia kuswekwa lupango kwa kosa la "kuingia kwa jinai".

Wakati blogu hii haina mamlaka ya kuhukumu iwapo ni kweli mwanamama huyo,Sophia Mahita (45) ni mtoto halali wa Afande Omari,kitendo cha jeshi la polisi kumswekwa rumande mwanamke huyo ni cha uonevu usiposwa kulelewa.Kwanini,kwa mfano,badala ya kumsweka ndani wasingefikia uamuzi wa kuitisha vipimo vya DNA?Ikumbukwe kuwa Afande Mahita ana historia ya kuwa na mtoto nje,na kukana,kama ilivyothibitika kwenye kesi ya mwaka 2006 iliyofunguliwa na ex-mtumishi wa ndani wa Mahita,Rehema Shabani .Katika kesi hiyo Rehema alidai alitungwa ujauzito na Mahita na alikuwa anahitaji msaada katika matunzo ya kijana wao.Afande alikanusha 'mzigo' huo,lakini hatimaye mahakama ilitoa hukumu kuwa 'ngunguli' huyo ni baba halisi wa mtoto husika.

Jeshi letu la polisi ni miongoni mwa taasisi zinazoongoza kwa ubabe na ukiukaji wa haki za binadamu.Lakini jeuri walioyonayo inachangiwa zaidi na udhaifu mkubwa katika taasisi za kiserikali na zisizo za kiserikali zinazohusika na uangalizi na kuhakikisha haki za binadamu nchini.Ni katika mazingira hayo ndipo tunakuta wanyonge wakihofia kuwaripoti vigogo au wenye nazo kwa vile si ajabu wanyonge hao wakaishia kugeuziwa vibao.

A mini-bullshit of the week ni uamuzi wa CCM kumteua Zakia Menghji kuongoza kamati ya usimamizi wa fedha na vifaa kwa ajili ya uchaguzi mkuu ujao.Hivi huyo mama si ndiye aliyeingizwa mkenge na mafisadi wa EPA na kuidhinisha mabilioni yaliyokwibwa na majambazi hao?Labda,nasisitiza LABDA,uteuzi huo umezingatia uzoefu wake katika namna ya kudili na mafisadi kutoa chochote kwa chama hicho tawala.

See you next time

28 Mar 2010


Kwa mara nyingine,baadhi ya Watanzania waishio Uingereza walipata nafasi ya kuhudhuria mkutano uliobeba jina la Diaspora Forum 2.Binafsi sikuhudhuria,sio kwa vile sikuona umuhimu wa kufanya hivyo bali nilitingwa na majukumu binafsi.Hata hivyo,laiti ningehudhuria ningejaribu kutoa mchango wa kwanini uhamasishaji kwa Watanzania walio nje kurejea nyumbani au kuchangia maendeleo ya taifa unaweza kuendelea milele pasipo kupatikana mafanikio yanayokusudiwa. Pamoja na nia nzuri ya kuwepo forums kama hiyo ya Diaspora,lakini ni muhimu kutambua kuwa kikwazo kikubwa cha maendeleo yetu kama taifa hakijawahi kuwa kwenye mipango mizuri.Tanzania tumebahatika kuwa na viongozi wenye uwezo wa hali ya juu katika kuongea na kubuni mipango mizuri.Lakini,kwa bahati mbaya au makusudi,wengi wa viongozi hao ni wazembe wa daraja la kwanza linapokuja suala la utekelezaji mipango including waliyoibuni wao wenyewe.Unajua kuna tofauti kati ya uzembe katika kutekeleza mawazo ya mwenzako na uzembe katika kutekeleza mawazo yako binafsi.Kwa mfano,hakuna mtu aliyeishauri CCM kuja na kauli-mbiu ya "ARI MPYA,KASI MPYA NA NGUVU MPYA" au ile ya "MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA".Uamuzi wa kuja na kauli-mbiu hiyo ulikuwa wa CCM binafsi pasipo shinikizo kutoka kwa wafadhili,viongozi wa dini,wananchi au kikundi chochote kile.Nafahamu wapo watakaobisha kuwa kauli-mbiu zote hizo zimeishia kuwa kauli-mbiu tu pasipo matokeo kuonekana,lakini ukweli ndio huo,na shurti uwekwe wazi.

Back to the Diaspora thing.Kwanza,katika mazingira ya kawaida,haihitajiki kumhamasisha mwananchi kurudi nyumbani kwake au kuchangia maendeleo ya alikotoka.Wengi wa Watanzania walioko ughaibuni hawahamasishwi kusaidia ndugu na jamaa zao walio Tanzania bali wanafanya hivyo kwa vile wanatambua kuwa ni wajibu wao.Naamini kuwa wengi wa wanaokumbuka ndugu na jamaa nyumbani wanasukumwa zaidi na namna misaada yao inavyosaidia walengwa huko nyumbani.Sidhani kama kuna mtu ambaye kila wiki au mwezi anakwenda Western Union,Moneygram au "Kwa Wapemba" kutuma pauni zake alizopata "kwa mbinde" only for watumiwa huko Tanzania kuendeleza libeneke la anasa.

Ninajaribu kutumia mfano wa ndugu na jamaa kama mahala pa kuanzia kabla ya kuangalia namna Watanzania walio nje wanavyoweza kufanya the same kwa nchi yao.Kwa bahati mbaya,forums kama Diapora 2 hazitoi sura ya pili ya hali ilivyo huko nyumbani.I wish miongoni mwa waalikwa wangekuwa taasisi zinazohamasisha Watanzania walio nje kuchangia kuleta mabadiliko ya haraka kwenye mwendendo na hatma ya taifa letu.Yah,Diaspora forums zinaweza kuhamasisha Watanzania wote walio ughaibuni kurejea nyumbani au kuchangia asilimia kadhaa ya vipato vya kujenga taifa letu "changa" (sijui lini litakua),lakini kwa hali ilivyo sasa,watakaoendelea kunufaika ni wateule wachache wafahamikao kama MAFISADI.

Na tatizo jingine linalotukabili Watanzania wengi ni usikivu uliotukuka pasipo udadisi.I hoped mshiriki mmoja angemuuliza Waziri Membe kuhusu commitment ya watwala wetu katika kupambana na ufisadi underlining mifano kama dilly-dallying za kuwachukulia hatua majambazi wa Kagoda au hili skandali jipya la trilioni za stimulus package ambapo tunaambiwa kuwa mafisadi came up with some phony companies to create another EPA-like swindle.

Binafsi napenda kuamini kuwa moja ya negative legacy za itikadi ya Ujamaa ni kwa wananchi kupenda kunyenyekea viongozi "kikasuku".Utaona wananchi wakihangaika kupata nafasi za kupiga picha na kiongozi badala ya kumkalia kooni kumuuliza kwanini mamabo yanaenda mrama.Unadhani laiti Mugabe au Waziri wake akija UK na kukutana na Wazimbabwe waishio hapa "patatosha"?And I don't mean kufanyiwa vurugu bali kubanwa na mwaswali ya msingi kwanini mambo yanakwenda mrama.Lakini kwa akina sie,mdau akishapata picha na kigogo kisha akaipenyeza bloguni basi anakuwa ame-achive lengo kubwa kabisa.

Naamini,hata kama ntapingwa,kuwa Watanzania walio nchi zinazojitahidi kuwatumikia wananchi kwa namna inavyostahili (kama hapa Uingereza,though it couldn't always be absolutely perfect) hawawezi kukwepa lawama za michango yao hafifu katika kuboresha hali ilivyo huko nyumbani.Siamini kama ni ubinafsi au imani kwamba "hata tukisema haitobadilisha kitu" bali ni kasumba ileile inayokwaza mabadiliko huko nyumbani kwamba kwa namna ya miujiza,watu walewale wanaokwaza maendeleo yetu wataamua kwa hiari yao kubadilika na kisha kuutumikia umma kwa ufanisi.Hivi,kwa Watanzania walio Uingereza,hatuoni namna Labour wanavyobanwa mbavu katika jitihada zao za kurejea madarakani?Na si kwamba wame-perform vibaya kihivyo-compared to our CCM-lakini taxpayers wa Uingereza wanaamini kuwa good is not good enough,they want better if not the best from Labour.

Juzijuzi,Makamu Mwenyekiti wa CCM,Pius Msekwa,alifanya ziara hapa UK lakini akanusurika pasipo kubanwa na wana-CCM wenzake kwamba,kwa mfano,kwanini chama hicho kinashindwa kuwachukulia hatua viongozi wanaotuhumiwa kuhusika na ufisadi.Mimi si mmoja wa wanaobeza uanachama wa CCM nje ya nchi kwa vile natambua kuwa hiyo ni haki ya kikatiba ya kila Mtanzania.By the way,kuna Democrats Abroad na Republicans Abroad which are more or less the same as na matawi ya CCM nje ya nchi.Nadhani wanaopinga uanzishwaji wa matawi ya CCM nje ya nchi au unachama wa matawi hayo wanasukumwa zaidi na ukweli kwamba kuna madudu mengi yanayolelewa na CCM huko nyumbani.Sasa inatarajiwa kuwa wana-CCM walio nje ya nchi wakisaidie chama hicho tawala kutambua kuwa mwenendo wake unawaangusha Watanzania.Na wanatarajiwa kufanya hivyo kwa vile wana advantage ya ku-compare and contrast as to kwanini,kwa mfano,Labour inaweza lakini CCM inashindwa.Yaani,kama Labour inaweza kuwakalia kooni wabunge wake kwenye expenses scandal kwanini basi CCM ishindwe kumbana mtu kama Mzee wa Vijisenti ambaye hadi muda huu ni Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ndani ya chama hicho?

Nimaelizie kwa kupongeza waandaaji wa Diaspora Forums kwani naamini kuwa wanachofanya kina umuhimu mkubwa.Hata hivyo,umuhimu huo unakwamishwa na ukweli kwamba mazingira ya nchi yetu kwa sasa yanakwaza wengi wa Watanzania walio nje kuchangia jitihada za ujenzi wa taifa.Hakuna anayetaka kuona fedha anazochuma kwa mbinde zinaishia kunufaisha nyumba ndogo za mafisadi huko nyumbani au kuongeza idadi ya mahekalu yao.Diaspora forums zinaweza kufanywa hata kila baada ya wiki lakini hazitazaa matunda yanayokusudiwa-au kubaki photo ops tu-laiti mwenendo wa mambo huko nyumbani hautarekebishwa.

26 Mar 2010


How do we best deal with bastards who not only keep on screwing our economy but also put their middle fingers up whenever they see us from the windows of their mansions or Range Rover Vogue,all obtained through unlawful conduct?I know this might sound crazy but,well,something gotta be done.We could try what the North Korean authorities did recently: a high ranking official who oversaw last year’s disastrous currency revaluation has been executed by firing squad.Well,crazy as it might sound but we simply can't let a privileged few plunder our economy while enjoying protection by the same people entrusted with the responsibility of emancipating us from the present abject poverty.Does it really make any sense,for instance,to see the DPP and PCCB dilly-dally in dealing with an illusive monster known as Kagoda?Or,is there any reason why Mzee wa Vijisenti is not in prison for his involvement in the radar scandal?Adding salt to a wound,we now learn that the much-hyped stimulus package has eventually ended up in the coffers of some shady firms which seem to have been formed purposefully to skin as alive just like those involved in the EPA scandal.Or,did they take a leaf out of the way our law enforcement institutions "dealt with" the real culprits of such scandals as Richmond,Kiwira,IPTL?

Call me a prophet of doom but the way those in power deal with ufisadi in our country is a total disgrace and has a potential of creating chaos in the very near future.It actually inspires a new breed,or rather a culture, of ufisadi as getting away with screwing the country becomes a norm.

Unfortunately,while the executed official in North Korea had "a privilege" of being dealt with by the State,our mafisadis might not be so "lucky".When people finally come to a realisation that it is useless to expect anything from their government in dealing with white collar criminals,they might resort to vigilantism,meaning people taking law in their own hands by shooting mafisadi at sight.And that would be too late for "justice" to take it course (it always does when walalahoi 'commit offences').

By the way,mlalahoi has got nothing to lose if sent to prison where their daily needs would then be taken care of by the state,something they hardly enjoy in their "normal" life as good citizens.

24 Mar 2010


Kwa muda mrefu sasa Kanisa Katoliki limejikuta likigubikwa na kashfa za ngono.Hivi karibuni pepo mbaya amezidi kulizungukia Kanisa hio baada ya taarifa kwamba kaka wa Baba Mtakatifu,Georg Ratziger, aliwatangwa makofi wanakwaya wake katika miaka ya 1960.Kwa kitambo sasa,inaonekana Kanisa limekumbwa na jukumu kubwa la kuomba msamaha kutokana na tuhuma za unyanyasaji wa kijinsia (na ulawiti) sambamba na jitihada za kusafisha sura yake.Hata hivyo,pamoja na kuendelea kuibuka kwa tuhuma hizo zisizopendeza,Kanisa Katoliki limeendelea kubaki 'safi' barani Afrika.Je hali hiyo inasababishwa na nini?Na je itaendelea kwa muda gani?Binafsi siamini kwamba tuhuma zinazolikabili Kanisa hilo haziligusi Bara la Afrika,na hususan Tanzania.Tofauti iliyopo ni kwamba imani za kiroho katika nchi zilizoendelea zina tofauti ya namna flani na ilivyo katika nchi zinazoendelea.Yayumkinika kusema watumishi wa Bwana katika nchi kama Tanzania wameendelea kunufaika na unyenyekevu uliokubuhu kutoka kwa waumini wao ilhali katika nchi za Magaharibi imani haimaanishikufumbia macho mauvu ya wasimamizi wa imani hiyo (i.e. watumishi wa Bwana).

Nadhani si mie peke yangu ninayefahamu kwamba baadhi ya watumishi wa Bwana wana watoto,kinyume kabisa na kanuni na taratibu za Kanisa Katoliki.Katika jimbo nililozaliwa,suala hilolinaonekana la kawaida sana kiasi kwamba baadhi ya watumishi wa Bwana wanamudu kuhudumia 'familia' zao (wanawake waliowapa ujauzito na kupata watoto wa wachunga kondoo wa Bwana) pasipo kificho.

Utumishi wa Bwana katika nchi yetu hauna tofauti sana na kinachoendelea kwenye siasa zetu.Tunafahamu wanasiasa wabovu lakini kwa vile wanamwaga vijizawadi hivi na vile tunaendelea kuwalea na hatimaye wanaoendelea kuipeleka mrama nchi yetu.Waumini wengi wa Kanisa Katoliki huko nyumbani wanafahamu fika maovu yanayotendwa na BAADHI ya watumishi wa Bwana lakini wanaendelea kufumbia macho.Natambua kuwa Maandiko Matakatifu yanasisitiza kuzingatia zaidi maneno/mafundisho ya viongozi wetu wa dini na sio kutilia mkazo mateno yao,lakini ni dhahiri padre mzinzi hawezi kuwa na mamlaka ya kiroho (moral authority) kukemea uvunjaji wa amri ya sita.

Na kuna imani kwamba kusuasua kwa baadhi ya viongozi wa dini huko nyumbani kukemea ufisadi na maovu mengine ya wanasiasa kunasababishwa na ukweli kwamba baadhi ya viongozi hao wa dini wanatambua kuwa 'hawako safi kihivyo'.Kama ilivyokuwa wakati wa sakata kati ya serikali na madhehebu ya dini kuhusu ushuru katika bidhaa zinazoingizwa nchi na madhehebu hayo,ambapo baadhi ya wanasiasa walidiriki kusema 'wanafahamu mengi kuhusu baadhi ya viongozi hao wa dini' ni dhahiri wachunga kondoo wa Bwana wanafahamu fika kuwa matendo yanayokiuka maadili yao yanafahamika na wanasiasa wangeweza 'kuwaumbua' kwa kuyaweka hadharani.

Hakuna anayefahamu hatma ya pepo huyu mchafu anayelitesa Kanisa letu lakini kilicho bayana ni athari zake kwa kondoo wa Bwana.Tayari kuna taarifa kwamba kuna mtikisiko wa kiimani katika nchi zinazofahamika kama vinara wa Ukatoliki kwa mfano Ujerumani,Austria na Ufaransa.Hali pia si shwari huko Vatican kiasi kwamba 'mpunga mapepo mkuu' (chief exorcist) katika makao makuu ya Kanisa hilo,Father Gabriel Amorth alinukuliwa akisema kuwa shetani ameweka makazi yake sehemu hiyo.

Wakati Kanisa Katoliki barani Afrika,Tanzania included,likiwa shwari katika kipindi hiki cha upepo mbaya wa shetani,ni muhimu kwa wachunga kondoo wa Bwana wanaokiuka mafundisho ya Kanisa hilo kujirudi wakitambua kuwa siri zao haitadumu milele.Pia ni muhimu kwao kufahamu kuwa japo wanasitiriwa kutokana na unyenyekevu uliopitiliza wa waumini wao,Mungu wanayemtumikia anaowaona na anakasirishwa sana.Japo wanaweza kuendelea kusalimika kutokana na waumini kuendelea 'kuwafumbia macho',ni dhahiri kuwa wasipobadilika wataishia kuwa kuni za kuchochea moto unaowachoma wadhambi huko 'motoni'.

Juma Kuu linapaswa kuwa kipindi kizuri kwa Kanisa Katoliki kila mahali kungalia wapi limejikwaa (na sio lilipoangukia) na kisha kufanya marekebisho yanayostahili.Na kwa Nguvu za Bwana,yote yanawezekana.

Tmsifu Yesu Kristo,Milele Amen.

22 Mar 2010


Kiongozi shurti awe na msimamo na kisha asimamie kile anachoamini.Kwa mara nyingine,Rais Barak Obama ameithibitishia dunia kuwa ni 'mwanaume wa shoka' linapokuja sula la kuamini anachosimamia.Hatimaye jana Obama alifanikiwa kupitisha sera yake ya mabadiliko katika mfumo wa afya ya jamii nchini Marekani.Hiyo ni baada ya safari ndefu na ngumu pengine zaidi ya kampeni yake ya kuingia Jumbe Jeupe (White House).Pamoja na kuhatarisha nafasi yake na ya chama chake kisiasa,Obama alipigana kiume kuhakikisha kuwa lazima mabadiliko hayo yafanyike,kwa gharama yoyote ile.Na kama inavyofahamika,mara nyingi maamuzi ya kihistoria huwa na tabia ya kutokuwa maarufu. Ushindi wa Obama katika suala hili unapaswa kuwa fundisho muhimu kwa Rais wetu Jakaya Kikwete ambaye miezi michache ijayo atahitimisha miaka yake mitano tangu aingie madarakani.Sote tunafahamu,with exception ya wale wanaopenda habari nzuri tu hata kama ni za uongo,kwamba kwa kiasi kikubwa ahadi za Kikwete kuikomboa Tanzania kutoka kwenye lindi na umasikini imebaki kuwa hadithi tu huku ufisadi ukishamiri na kuitafuna Tanzania kwa kasi ya ajabu.Yayumkinika kusema kwamba utawala wa Kikwete utakumbukwa zaidi kwa skandali kuliko ufanisi wa kuwatumikia Watanzania.Kibaya zaidi,Kikwete alitoa lundo la ahadi kuhusu namna atakavyoboresha maisha ya Watanzania,hence kauli-mbiu MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA.

Kuna wanaodhani kuwa kilichomsukuma Kikwete kuogmbea urais mwaka 2005 ni kukamilisha ndoto yake ya mwaka 1995 'iliyokwazwa' na Baba wa Tiafa Mwalimu Julius Nyerere.Wenye mtizamo huo wanaamini kuwa Kikwete alitumia miaka 10 iliyofuata akikusanya nguvu,sio katika namna gani atawatumikia Watanzania,bali atakavyoweza kuingia Ikulu.Ni katika 'piga ua' hii ndipo alijikuta akishirikiana na 'viumbe hatari' waliojipenyeza kwa kivuli cha 'wanamtandao' wakiwa na matarajio makubwa kuwa Kikwete akiingia Ikulu basi nao 'wameula'And they were not wrong.Kusuasua kwa Rais wetu katika kuchukua maamuzi mazito kumechangiwa zaidi na ushirika wake na watu hao.Na hii haiwezi kuwa excuse kwake kwa sababu alikuwa na kila sababu na uwezo wa 'kuwasaliti' laiti angekuwa na nia.Angeweza kabisa kuwaita Ikulu na kuwaambia 'nathamini sana mchango wenu kuniingiza madarakani,lakini mimi sasa ni Rais wa Watanzania wote ninayeongozwa kwa misingi ya Katiba.I'm sorry,atakayekwenda kinyume na sheria na taratibu za nchi basi sheria itachukua mkondo wake.Tubaki marafiki lakini sio kwa urafiki wa kukwamisha utawala wangu'.Simple and clear!

Tupo wengine tunaoamini kuwa licha ya ndoto hiyo iliyoanza 1995,Kikwete pia alisukumwa na dhamira ya kuwatumikia Watanzania.Na kututhibitishia kuwa tuko sahihi,alipoingia tu madarakani alitoa hotuba zilizoonyesha kuwa anafahamu kwa kina vikwazo vya maendeleo ya taifa letu.Aliweka wazi kuwa rushwa ni tatizo kubwa na angefanya kila awezalo kupambana nayo.Kama ilivyokuwa kwenye hotuba zake za wakati wa kampeni,Kikwete alipoingia madarakani alirejea kuahidi makubwa kwa Watanzania,na wengi tulimwamini kwa vile alikuwa akiongea lugha tunayoielewa (tofauti na Mkapa aliyezowea kutoa hotuba 'ngumu' kana kwamba ni mihadhara ya kitaaluma chuo kikuu).

Dalili ya kwanza kuwa Kikwete 'hana jipya' ni kauli yake kuwa 'anawafahamu wala rushwa bali anawapa muda wa kujirekebisha'.Nadhani kauli hiyo itaingia kwenye vitabu vya historia kama ya aina yake kwa mkuu wa nchi kutoa deadline kwa wahalifu.Lakini baadhi yetu tulijipa matumaini kwamba labda Rais alikuwa serious katika kauli hiyo,na kwamba baada ya deadline hiyo ku-expire angechukua hatua flani.Miaka mitano baadaye,sote tunafahamu sasa kuwa kauli hiyo ilikuwa mithili ya 'kumtishia mtu mzima nyau'.Na si kwenye kauli hiyo tu,bali tuliambiwa wakati flani kuwa amekabidhiwa orodha ya wauza madawa ya kulevya (na aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani Bakari Mwapachu) na baadaye tena akatuambia kuwa anawafahamu wala rushwa pale Bandari Dar es Salaam,na majina anayo.So far,hajachukua hatua kwa wauza madawa ya kulevya (wa orodha ya Mwapachu) na hajawasilisha majina ya wala rushwa wa Bandari!Sasa kama Rais hataki kutoa majina ya wala rushwa anaodai anawafahamu,tutegemee nini kutoka kwa mwananchi wa kawaida?

Kama nilivyosema mwanzoni mwa makala hii,uongozi ni kusimamia katika kile unachomini hata kama kitakupunguzia umaarufu.Kikwete alipaswa kufahamu kuwa ili urais wake uwe na manufaa kwa Watanzania ni lazima 'akosane' na baadhi ya marafiki zake.Na kwa hakika hilo lingekuwa na maana zaidi kwani ni bora zaidi mara milioni kupendwa na Watanzania walio wengi na 'kuchukiwa na mafisadi wachache' kuliko kupendwa na 'kigenge kidogo cha mafisadi' na kulaumiwa na mamilioni ya Watanzania.Kama Kikwete alikuwa na dhamira ya dhati ya kuwaletea Watanzania maisha bora alipaswa asimame kidete kuhakikisha hilo linatimia kwa udi na uvumba.

Lakini kwa vile bado kuna miezi kadhaa kabla ya uchaguzi,na kwa vile Obama ametioa darasa zuri kwa viongozi ya type ya Kikwete,basi tunabaki with our fingers crossed kuwa huenda rais wetu nae akajitutumua na kurekebisha mambo katika muda huu uliosalia.Uzuri ni kwamba hata kama ufisadi umetuumiza kwa muda wote huu,uamuzi wa kuukalia kooni katika dakika hizi za majeruhi utafanikiwa kufuta machungu yote tuliyopitia.Ni kama katika fainali ya soka ambapo bao la ushindi linapatikana katika dakika za majeruhi.Shamrashamra zitakazoambatana na ushindi huo hazitajali kuwa bao la ushindi limepatikana dakika za lala salama.What matters ni ushindi.

Basi Rais Kikwete tunatarajia sasa utafanya kweli.Utatamka bayana kuwa ile deadline uliyotoa kwa wala rushwa unaowafahamu ime-expire na kuamuru vyombo vya dola viingie ulingoni (yes,vimekuwa vikiwajibika baada ya ruhusa yako).Utakabidhi ile orodha ya mafisadi ya pale Bandarini ambayo watendaji wanaisubiri ili wachukue hatua zinazostahili.Utaifanyia kazi pia ile orodha ya 'wauza unga' ulokabidhiwa na Mwapachu.Utaamuru wamiliki wa Kagoda wawekwe hadharani na kuchukuliwa hatua zinazostahili.Ukiwa mwenyekiti wa CCM,utatambua kuwa uwepo wa Mzee wa Vijisenti kwenye Kamati ya Maadili ya chama hicho licha ya tuhuma zinazomkabili ni mzaha usiokubalika,na utashauri awekwe kando hadi taratibu za kisheria zitapochukua mkondo wake.Utaamua kuwa suala la Richmond haliwezi kumalizwa 'kishkaji' bali wahusika wote watachukuliwa hatua ili iwe funzo kwa wanaotumia madaraka yao vibaya.Na mwisho,utaanza kutafsiri kwa vitendo ahadi zako lukuki ulizotoa wakati wa uchaguzi na kuendelea kuzitoa kwa muda wote uliokuwa madarakani.Rejesha ari,kasi na nguvu mpya katika kuleta MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA.

Kama Obama ameweza,wewe unaweza pia.It's all about kuamini unachosimamia na kusimamia unachoamini.

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.