6 Mar 2020


Coronavirus phishing attacks just won’t go away. As the novel coronavirus (COVID-19) outbreak continues to spread, cybercriminals have intensified their phishing attacks, adding fuel to the global crisis.
Beyond the devastating effects of the coronavirus, the outbreak is producing a perfect storm for cybercriminals. Cybercriminals are feeding on public anxiety and preying on victims using scare tactics and urgent calls to action to entice an ill-advised click. And to make matters worse, the global reach of the coronavirus means virtually everyone is a relevant target for a coronavirus scam.
We collected seven coronavirus phishing attack examples to shed light on the top tactics cybercriminals are using so you can prepare your employees for the threats they are facing now and in the foreseeable future.
Is your organization susceptible to phishing attacks? Find out today with a free Phishing Risk Test!
RUN FREE TEST

1. Safety measures turned malicious

This phishing attack impersonates a coronavirus specialist from the World Health Organization to trick victims with two malicious options. The email urges the victim to download a malicious file disguised as a safety document.
coronavirus phishing email
Image courtesy of Sophos
The same attack was spotted without the World Health Organization branding, but instead targeted to the victim’s region.
coronavirus phishing email
Image courtesy of Wired
The attack also gives the victim the option to click a “Safety Measures” button. If the victim clicks the link, they are redirected to a spoofed World Health Organization site and prompted to provide their email address and password.
coronavirus phishing email
Image courtesy of Sophos

2. Internal organization alert

This phishing attack takes a corporate approach by impersonating a company’s president to deliver an attachment disguised as tips to prevent infection. The attachment is designed to infect an employee’s machine with malware.
coronavirus phishing email
Image courtesy of Trustwave

3. New cases in your area

This attack preys on the fears of Coronavirus spreading near the victims’ location. Disguised as a CDC alert, this phishing email tricks victims into clicking a malicious link by offering an updated list of new cases of the virus documented near them.
coronavirus phishing email
Image courtesy of Trustwave

4. The donation scam

Like the tried-and-true donation scams used after natural disasters, this phishing attack solicits donations to fight the spread of the coronavirus. The attack imitates a CDC emergency outreach email and asks victims to deposit money into a Bitcoin account.
coronavirus phishing email
Image courtesy of Kaspersky

5. Information from the source

In this coronavirus phishing attack, the cybercriminal impersonates a doctor from The Central Hospital of Wuhan to play on victims’ fears, lend credibility to the email and convince the victim to download a malicious attachment.
coronavirus phishing email
Image courtesy of Mailguard

6. Coronavirus domains

Along with the phishing tactics above, one of the largest concerns facing cybersecurity researchers is the massive increase in coronavirus-themed domain registrations. Many suspect that these coronavirus-related domains will be used for phishing attempts like those listed above.
coronavirus phishing domains
Image courtesy of Checkpoint

7. Fake product scam

Beyond the coronavirus phishing threats listed above, the SEC is warning consumers of investment scams related to products claiming to prevent, detect or cure coronavirus. Future phishing attacks may leverage this same tactic.

Prepare your employees for coronavirus phishing attacks

Coronavirus phishing attacks show no signs of slowing down. We’ve already seen a wide range of tactics cybercriminals are using to scam victims, infect their devices and steal information. By providing your employees with simulated phishing training, you can not only help them detect these phishing attacks at work to keep your organization secure, but also help them develop more secure habits to stay secure at home.
Security awareness and simulated phishing platforms like Infosec IQ come loaded with topical phishing templates (including templates for the attacks above) to help you prepare your workforce and keep your organization secure.
Run a free phishing risk test to see how it works!
RUN FREE TESTSource: INFOSECINSTITUTE

4 Mar 2020



Kuna njia mbalimbali za kufanya uchambuzi wa kiintelijensia, njia zinazotegemea vigezo mbalimbali, kigezo muhimu zaidi kikiwa tukio husika na/au "key players" (kwenye ushushushu tunawaita "subjects") katika tukio hilo.

Katika kufanya uchambuzi wa kiintelijensia kuhusu tukio la jana ambapo Rais Magufuli alikutana na viongozi wakuu watatu wa upinzani, Maalim Seif Sharif Hamad wa ACT-Wazalendo, James Mbatia wa NCCR-Mageuzi, na Ibrahim Lipumba wa CUF, nitatumia kanuni ijulikanayo kama 'Linchpin,' ambayo ni mwafaka zaidi pale ambapo "ukweli mzima" upo bayana (au "vipande vya ukweli).



Kanuni hii ya Linchpin ilibuniwa na Naibu Mkurugenzi wa zamani wa Shirika la Ujasusi la Marekani (CIA), Douglas MacEachin, na inahusu "matukio ya ghafla/ya kushangaza," ambapo aliitumia kanuni hiyo kueleza tukio la ghafla na Iraki kuivamia Kuwait mwaka 1990. 

Katika kanuni hii, uchambuzi wa kiintelijensia unatathmini tukio/matukio husika kwa kuzingatia "ukweli uliopo/unaofahamika," kitu tofauti kidogo na mbinu nyingine za uchambuzi wa kiintelijensia zinazoanza na hisia au dhana (kama ile ya ACH -Dhana Zinazoshindana -nilioutumia majuzi kuchambua tukio la Membe kufukuzwa uanachama wa CCM)

Kwa vile lengo la makala hii sio kutoa darasa la "mbinu za uchambuzi wa kiintelijensia," bali kutumia kanuni ya Linchpin kueleza "tukio la ghafla," la Jiwe kukutana na Maalim Seif, Mbatia na Lipumba, ni vema nikahamia kwenye uchambuzi husika.

Kwa kutumia kanuni hiyo, kuna "ukweli " (facts) kadhaa ambao ni msingi wa uchambuzi huu. Ukweli mkubwa zaidi ni kitu nilichokiongea wiki iliyopita baada ya mwandishi Erick Kabendera kuachiwa baada ya kuwekwa jela kwa uonevu kwa zaidi ya miezi sita.



Awali nilieleza kuhusu hilo la "Jiwe kukaliwa kooni na mabeberu" katika chapisho langu hili


Kwahiyo ukweli mmoja - na muhimu zaidi - uliopelekea "tukio hilo la ghafla" ni shinikizo la mabeberu. Shinikizo ambalo wiki iliyopita lilipelekea mwandishi Kabendera kuachiwa, na wiki hii limepelekea Jiwe kukutana na viongozi hao watatu wa upinzani.

Nimetanabaisha kuwa huo ni "ukweli muhimu zaidi" kwa sababu kuna ukweli mwingine japo sio wenye uzito sana. 

Uamuzi wa Jiwe kukutana na akina Maalim Seif jana ni sawa na "kuua ndege wawili kwa JIWE moja." Kwa upande mmoja amefanikiwa kutuliza shinikizo la mabeberu ambao wameweka bayana msimamo wao kuwa wanaweza kutochangia bajeti ijayo endapo ukandamizwaji wa demokrasia na haki za binadamu utaendelea. Amewatuliza mabeberu kwa kuwaonyesha kuwa "demokrasia ipo" na ndio maana ameweza kukutana na sio kiongozi mmoja tu wa upinzani bali watatu kwa mkupuo.

Nimesema "ameua ndege wawili kwa jiwe moja." Na "ndege" wa pili ni Membe. Mkutano wake huo na akina Maalim Seif unafikisha salamu muhimu kwa Membe aliyefukuzwa uanachama wa CCM wiki iliyopita, kwamba "hao unaotaka kujiunga nao ndo hawa niko nao hapa Ikulu kwangu."

Kama nilivyoeleza katika uchambuzi kuhusu tukio hilo la Membe kufukuzwa uanachama wa CCM, kuna uwezekano mkubwa wa mwanasiasa huyo kujiunga na ACT-Wazalendo. Na kwa vilekufukuzwa kwake CCM ni matokeo ya uoga wa Jiwe kuhusu upinzani kwenye nafasi ya urais, Membe "kuwa mgombea wa urais kwa tiketi ya ACT-Wazalendo" ni worst nightmare kwa Jiwe. 

Naomba nirudie kusisitiza kuwa uoga huo wa Jiwe hauna msingi kwa sababu Membe hana uwezo wa kumwangusha Jiwe kwa sababu nilizowahi kutanabaisha katika makala hii.



Kwahiyo Jiwe akiweza kumzuwia Membe kisaikolojia asiwaamini Wapinzani itakuwa ni nafuu kubwa kwake na uoga wake.

Ukweli mwingine kuhusu mkutano huo kati ya Jiwe na viongozi hao wa upinzani ni "busara ya kisiasa" inayosema "kuwa karibu na marafiki zako, lakini kuwa karibu zaidi na maadui zako."

Ukweli mchungu kuhusu wanasiasa wetu - wa CCM na hao wa upinzani - ni huu: wote wapo katika "tabaka tawala" (ruling class). Hapana, simaanishi kuwa akina Seif, Mbatia na Lipumba ni sehemu ya utawala wa Jiwe bali ukiangalia kwa undani wasifu wa viongozi mbalimbali wa vyama vya siasa, unaweza kubaini kuwa "wote ni wale wale."

Na ukiangalia wasifu wa Maalim Seif, Mbatia na Lipumba hutoshindwa kubaini kuwa ni watu ambao tumekuwa tukiwasikia "miaka nenda miaka rudi" lakini "wakiwa upande wa pili," kwa maana "sio upande wetu" watu wa tabaka la chini. Kwa kuazima neno la mtaani, hawa ni "vigogo."

Ukweli mwingine ni kwamba mkutano huo wa Jiwe na akina Maalim Seif "ndio siasa ilivyo." Kuna kitu kwenye siasa kinaitwa "realpolitik" ambacho kwa tafsiri isiyo rasmi ni "siasa ilivyo kimatendo kuliko kinadharia/kiitikadi." 

Sasa kwenye "siasa halisi" iwe ya kitaifa au ya kimataifa, "hakuna marafiki au maadui wa kudumu bali maslahi tu." Na ndio maana licha ya msimamo wake msimamo wake mkali dhidi ya vikundi vya kigaidi, na kauli maarufu kuwa "we don't negotiate with terrorists," majuzi Marekani ilifikia makubaliano na kundi la kigaidi la Taliban.

Na jana ilifahamika kuwa Rais wa nchi hiyo Donald Trump aliwapigia simu viongozi wa kundi hilo, kitu ambacho kabla ya tukio hilo kilikuwa sio rahisi kukifikiria.



Baada ya kuangalia "ukweli"(facts) huo unaojenga msingi wa uchambuzi huu, kanuni ya Linchpin inawezesha kujenga picha ya matarajio yanayohusiana na tukio/watu husika. Hapa ninamaanisha kuwa hadi kufikia hapa, yawezekana kueleza nini kinaweza kujirihivi karibuni au huko mbeleni.

Moja ni hiyo sintofahamu inayoweza kumkumba Membe baada ya kumuona Maalim Seif akiwa Ikulu na Jiwe. Ikumbukwe tu Lowassa alipoonekana Ikulu bila kutarajiwa "waumini"wake walimtetea na kuamini porojo zake kuwa kaambiwa arudi CCM lakini amegoma. Baadaye ukweli ukadhihirika baada ya Waziri Mkuu huyo wa zamani kurejea CCM.

Simaanishi kuwa Maalim Seif atakubali kurudi CCM. La hasha. Kinachoweza kutokea ni Jiwe kujaribu tena "kuua ndege wawili kwa JIWE moja." Anaweza kumfarakanisha Maalim Seif na Zitto na hapohapo kupunguza tishio kubwa kwake kutoka kwa Zitto kama Zitto, na Zitto akiwa na Maalim Seif.

Ikumbukwe tu kuwa japo Lowassa alikuwa kama 'mungu-mtu' huko Chadema, kitendo chake cha kuonekana Ikulu na Jiwe kiliwafanya hata baadhi ya "waumini" wake waanze kuwa na hofu nae.

Sina uhakika hali ikoje huko ACT-Wazalendo baada ya Maalim Seif kukutana na Jiwe, lakini ni siri ya wazi kuwa Jiwe na Zitto "picha haziivi," na wala sio jambo la kushangaza kuona Zitto hakualikwa kwenye mkutano huo.Na wala  sina hakika kama angekubali mwaliko wa Jiwe.

Kuhusu Mbatia na Lipumba, hakuna haja ya kupoteza muda kuwajadili maana "wapo kama hawapo." 

Moja ya maswali muhimu kuhusu Malim Seif kwenda Ikulu kukutana na Jiwe ni je alipata ridhaa ya Zitto na chama kwa ujumla? Na je tukio hili linaweza kuzua mpasuko huko ACT-Wazalendo? Pengine kukusaidia kuelewa vema "siasa za ACT-Wazalendo," pitia uchambuzi wangu huu nilioufanya mara baada ya Maalim Seif kujiunga ACT-Wazalendo.

Huhitaji kuwa na uelewa mkubwa wa siasa za Tanzania yetu kubaini kuwa mnufaika mkubwa wa mkutano huo kati ya Jiwe na viongozi hao watatu wa upinzani ni Jiwe mwenyewe. 

Hilo lipo wazi. Lisilo wazi ni "yanayoweza kujiri" kutokana na mkutano huo. Je Maalim Seif anaweza kuangaliwa kama "msaliti" kwa kukubali "kukutana na dikteta ambaye majuzi tu akiwa Zanzibar alikuwa anamwaga sumu kwa Dkt Shein kuhusu jinsi ya kumdhibiti Maalim Seif?"

Kwa upande mwingine, kama kweli Jiwe alikuwa na nia njema ya kukutana na viongozi wa upinzani basi pengine wa kwanza kabisa kupewa kipaumbele cha kukutana nae angekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, ambaye majuzi tu alimuomba Jiwe kuwe na MARIDHIANO. Lakini ni vema "kuweka akiba ya maneno" kwani haitokuwa jambo la kushangaza tukimuona Mbowe Ikulu kama alivyoongozana na timu yake Mwanza kwenye sherehe za Uhuru Desemba 9 mwaka jana. 

Nihitimishe uchambuzi huu kwa kutahadharisha kuwa intelijensia sio sayansi timilifu (intelligence is not exact science) licha ya uchambuzi huu kuongozwa na kanuni ya Linchpin ambayo ina ufanisi mkubwa penye uwepo wa ukweli kuhusu tukio/mtu husika.


29 Feb 2020


Somo: Kuvuliwa uanachama Bernard Membe, Waziri Wa Zamani wa Mambo ya Nje, Mbunge wa zamani, kada mkongwe na mmoja wa wana CCM walioingia "tano bora" ya kutafuta mgombea urais kwa tiketi ya CCM katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015

Key subject(s)

  1. Bernard Kamilius Membe
  2. John Pombe Magufuli
  3. Jakaya Mrisho Kikwete
  4. Modestus Kipilimba
Dhana ya kwanza: Membe "anakubali matokeo," anaamua kuachana na siasa. 

Dhana ya pili: Membe "anafanyiziwa."

Dhana ya tatu: Membe "anakubali matokeo," anaamua kujiunga na chama cha upinzani

Dhana ya nne: Membe hakubali matokeo, anaamua "kutafuta haki yake" CCM.

Dhana ya tano: Membe hakubali matokeo, anaamua "kutafuta haki yake" nje ya CCM

Ushahidi: Hadi muda huu Membe hajatoa tamko rasmi kuhusu mustakabali wake. Kwahiyo dhana zote nne zinasimama kama zilivyo kwa vile hakuna ushahidi wa kupelekea kuziondoa.

Kipimo/Vipimo: Haipo muda huu mpaka Membe atoe tamko rasmi. Dhana zote zinaendelea kubaki hai.

Mchujo: Kwa kuzingatia kuwa Membe hakuomba msamaha alipoitwa kwenye vikao husika, na kwa kuzingatia "damu mbaya" (bad blood)kati yake na Rais John Pombe Magufuli, tangu mwanzo wa Awamu ya Tano, yayumkinika kuamini kuwa uwezekano wa Membe "kutafuta haki yake" CCM ni hafifu.
Vigezo hivyo vinafanya uwezekano wa Dhana Ya Nne kutimia kuwa ni hafifu. Kwa mantiki hiyo, dhana hiyo inaondoshwa (yaweza kurejeshwa huko mbeleni)

Walakini: Hakuna

Unyeti: upo katika maeneo yafuatayo
  1. Membe ni mmoja wa makada zaidi ya 40 wa CCM waliojitokeza kuwania kupitishwa na chama hicho kwenye nafasi ya urais wa JMT.
  2. Membe alikuwa mpinzani mkuu wa Edward Lowassa kada aliyekuwa anapewa nafasi kubwa ya kuwa mrithi wa Rais Jakaya Mrisho Kikwete, na ambaye baada ya kutopitishwa CCM alihamia Chadema, japo baadaye alirudi tena CCM.
  3. Membe alikuwa miongoni mwa "tano bora" pamoja na Magufuli, January Makamba, Amina Ali na Asha Rose Migiro
    Migiro
  4. Membe ni swahiba mkubwa wa Rais mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete
  5. Membe ni mwanachama wa kwanza wa CCM "mwenye hadhi ya kitaifa"kufukuzwa uanachama.
Uchambuzi:

Uzito wa dhana ya kwanza kwamba Membe atakubali matokeo na kuachana na siasa upo kwenye hoja kwamba kutokana na uzoefu wake ndani ya CCM, anafahamu kuwa jaribio lolote la kuendelea na "maisha ya kisiasa" litakumbwa na upinzani na vikwazo vingi kutoka kwa Magufuli na CCM kwa ujumla.

Kadhalika, kama shushushu wa zamani, Membe anafahamu kuwa yeye sasa ni "high value target" huko Idara ya Usalama wa Taifa, ambapo kila nyendo yake sio tu itafuatiliwa kwa karibu bali pia anaweza "kuchanganywa akili" kwa kufanyiwa "overt surveillance" (kumfuatilia mlengwa bila kificho, lengo likiwa kumjulisha kuwa anafuatiliwa. Mbinu hii hutumika zaidi "kumchanganya akili" mlengwa).

Mapungufu ya dhana ni ukweli kwamba Membe ni "high value target" pia kwa vyama vya upinzani, na kwa kuzingatia kuwa huu ni mwaka wa uchaguzi, anaweza kupewa fursa ya "kulipa kisasi dhidi ya Magufuli kwa kupitishwa kuwa mgombea wa chama cha upinzani."

Mapungufu mengine katika dhana ya kwanza  ni "dalili za awali" kuwa "huu sio mwisho wa Membe kisiasa."

Uzito wa dhana ya pili upo katika ukweli kwamba Magufuli " hana mshipa wa aibu." Kama aliweza "kuamuru Lissu afanyiziwe," hashindwi kutoa maagizo kama hayo dhidi ya Membe.

Uzito mwingine upo kwenye ukweli kwamba shushushu wa zamani Membe nje ya CCM anabaki kuwa tishio kuliko alipokuwa mwanachama "anayebanwa na taratibu za chama."

Uzito mwingine ni ukweli kwamba Membe ni swahiba na watu wawili muhimu kwenye siasa za Tanzania, na ambao huenda wakawa na influence kwenye uchaguzi mkuu ujao, Rais Mstaafu Kikwete na Mkurugenzi wa zamani wa Idara ya Usalama wa Taifa, na sasa balozi wa Tanzania Namibia, Dkt Modestus Kipilimba. Japo watu hawa wawili, kama ilivyo kwa Membe sasa, nao ni "high value targets" ambao sio tu wanafuatiliwa na mawasiliano yao kusikilizwa (uwepo wa walinzi unarahisisha zoezi hilo), lakini wanaweza kuwa nguzo muhimu kwaMembe "kulipa kisasi."

Kwa vile Kipilimba yupo nje ya nchi, na Kikwete huwa safarini mara kwa mara, kuwafuatilia kwa utimilifu wa asilimia 100 ni kugumu, na ikizingatiwa kuwa Membe ni shushushu wa zamani, anaweza kufanikisha mawasiliano nao na kuepa "surveillance" (kufuatiliwa) na "bugging" (kunasa mawasiliano).

Mapungufu ya dhana yapo kwenye ukweli kuwa japo "Magufuli hana mshipa wa aibu," na hivyo anaweza "kumfanyizia" Membe, lolote litakalomtokea Membe kati ya sasa na Oktoba litatafsiriwa moja kwa moja kuwa ni "mkono wa Magufuli." Na hilo linaweza kuwafanya "mabeberu kumrukia kama mwewe."

Na ikumbukwe kama Waziri wa Mambo ya Nje kwa miongo miwili, Membe atakuwa na "connections" kubwana nzito huku ughaibuni. Akidhuriwa na Magufuli, yawezekana kabisa "mabeberu" wakaamua kuharakisha utekelezaji wa mkakati wa kumng'oa kiongozi huyo.

Uzito wa dhana ya tatu ni ukweli kwamba kujiunga na chama cha upinzani sio tu kunaweza kumpatia fursa ya "kulipa kisasi kwa Magufuli, kwa kuwa mpinzani wake kwenye uchaguzi mkuu ujao (kwa kuamini kuwa atapitishwa kuwa mgombea urais katika chama chochote atakachohamia)," pia itakuwa nafasi adimu kwake kufanya jaribio jingine la kuwania urais wa Tanzania.

Uzito mwingine wa dhana hii ni kauli za Kiongozi Mkuu wa chama cha Wazalendo (ACT),Zitto Kabwe baada ya tangazo kuhusu kufukuzwa kwa Membe huko CCM, Kauli hizo zilikuwa na harufu ya "karibu kwetu."




Mapungufu ya dhana hii yapo kwenye ukweli kwamba hata kama Membe ataamua kujiunga na chamacha upinzani, vikwazo na usumbufu kutoka kwa Magufuli kupitia Idara ya Usalama wa Taifa vinaweza kumfanya "atamani ardhi immeze."

Kingine ni ukweli kwamba "Membe sio msafi kihivyo," na hiyo inaweza kumrahisishia Magufuli "kumzulia kesi ya utakatishaji fedha na/au uhujumu uchumi." 

Vivilevile, Idara ya Usalama wa Taifa inaweza kumshurutisha Membe asijiunge na chama kingine, hasa ikizingatiwa kuwa Magufuli amekuwa akiitumia taasisi hiyo kuwatisha na kuwahujumu wapinzani wake au/na wakosoaji/wanaharakati.

Kadhalika, licha ya Zitto kuonyesha dalili za awali za uwezekano wa "Membe kuhamia ACT-Wazalendo," kwa kuwa hatujui Maalim Seif na "ACT-Zanzibar" wana mtazamo gani kuhusu "ujio wa Membe," na ukweli kuwa wanaweza kumkataa, yawezekana Membe kuhamia chama hicho kusitokee.

Uzito kwenye dhana ya tano upo kwenye ukweli kwamba endapo atatumia vema ujuzi wake kama shushushu mstaafu, na endapo atapata sapoti kutoka kwa Kikwete na Kipilimba, Membe anaweza kuwa tishio nje ya CCM bila hata kujiunga na chama kingine cha siasa. 

Ukweli kwamba kuna wana-CCM wengi tu wanaotamani Magufuli aondoke hata kesho unaweza kumsaidia Membe kupata "marafiki" wengine muhimu ndani ya chama hicho, ambao pamoja nao wanaweza kuanzisha harakati za kumng'oa Magufuli.

Mapungufu ya dhana hii ukweli kwamba kwa nchi ambayo "ili nguvu za kisiasa shurti uwe mwanasiasa," uwezekano wa Membe kuwa na "nguvu" nje ya mfumo wa kisiasa ni mdogo.

Mchanganuo: Kwa upande mmoja, uamuzi wa Magufuli kumfukuza Membe unaelezea zaidi kuhusu yeye kuliko kilichompata Membe. Ukweli kwamba jina la Membe limekuwa likitajwa mara kadhaa kuhusiana na kinyang'anyiro cha urais mwaka huu, uamuzi huo wa Magufuli unatafsiriwa kuwa ni UOGA. Kwa kifupi, Magufuli amemuogopa Membe akiwa ndani ya CCM na ndio maana akashinikiza afukuzwe chamani.

Hofu ya Magufuli kwa Membe haina mashiko. Membe hakupaswa kushika nafasi ya tano kwenye "tano bora" ya kumtafuta mgombea urais kwa tiketi ya CCM, huku akiambulia kura 120 tu, nyuma ya JanuaryMakamba (124), Migiro (280),Amina Ali  (284) na Magufuli (290). Hakupaswa kushika nafasi hiyo kwa sababu kuu mbili. Kwanza, yeye ndiye alikuwa "front runner," kwa kuzingatia kuwa ndiye alikuwa mpinzani mkuu wa Lowassa.Na pili ni uswahiba wake na Kikwete na familia yake. Kingine cha kuongezea hapo ni ukaribu wake na maafisa mbalimbali wa Idara ya Usalama wa Taifa ambayo aliwahi kuitumikia huko nyuma.

Membe hakuwa na sababu moja ya msingi ya kutoibuka mshindi kwenye kinyang'anyiro hicho. Sasa sijui hiyo hofu ya Magufuli inatoka wapi. 

Ubashiri: Endapo Magufuli "hatomfanyizia" Membe, kuna uwezekano mwanasiasa huyo akajiunga na ACT- Wazalendo. Lakini kujiunga huko kutategemea endapo Maalim Seif na "ACT - Zanzibar) wataridhia. Hata hivyo, intelijensia sio sayansi timilifu, na matokeo ya ubashiri huu yanaweza kuwa tofauti.

Hitimisho: Suala hili lina sura mbili. Moja ni ukweli kwamba udikteta wa Magufuli sasa umepiga hodi ndani kabisa ya CCM.Pili, mpira upo mikononi mwa Membe. Akipanga karata zake vizuri, anaweza kutoa upinzani japo kidogo kwa Magufuli hapo Oktoba. Anaweza kuwa Rais ajaye wa Tanzania? Uwezekano huo ni hafifu japo wanasema "never say never in politics."

Uchambuzi huu ni endelevu. Utakuwa updated kadri kunapotokea maendeleo mapya.









28 Feb 2020


Kabla hujanitolea jicho kwa kutanabaisha kuwa "hatuna uhaba wa viongozi wapumbavu," na kunituhumu kuwa nimekosa heshima kwa viongozi wetu, naomba tu kukukumbusha kauli maarufu ya Rais wetu John Magufuli 

Image


Sasa kama Mheshimiwa sana Magufuli anaweza kutumia neno hilo kwanini sie watawaliwa wake iwe dhambi? 😝

Naam taifa letu halina uhaba wa viongozi wapumbavu, na ndio maana baadhi yao wamefikia hatua ya kuaminiwa na Rais wetu hadi kupewa dhamana ya kuongoza wizara muhimu. 

Jana nilikutana na clip moja inaeleza kuhusu ujio wa lundo la watalii kutoka CHINA. Yes, China hii hii ambayo kwa sasa ndio kama "makao makuu" ya maambukizi ya virusi vya Corona.


Huku nchi za Magharibi, ambako wana teknolojia za hali ya juu kutambua maradhi mbalimbali ikiwa ni pamoja na maambukizi ya virusi vya Corona, wanafanya udhibiti mkali kwa kila mtu anayetoka China, ikiwa ni pamoja na raia wa nchi hizi za Magharibi. Muda huu ninapoandika makala hii, kuna raia kadhaa wa Uingereza "waliozuiliwa" sehemu mbalimbali kufuatia tishio la maambukizi ya virusi hivyo.

Sasa sijui sie ni kiburi tu au kutojali uhai wa Watanzania wenzetu au ndio huo upumbavu wa kupindukia, bila hofu wala aibu tuna viongozi wanaoruhusu ujio wa lundo la Wachina katika kipindi hiki hatari.

Kibaya zaidi, nimemsikia daktari mmoja anaongelea suala hilo kwa kuwakejeli walioapatwa na taharuki kutokana na ujio wa Wachina hao, akidai kuwa Wachina hao wamefanyiwa vipimo vyote. 

Huu ni zaidi ya upumbavu, kwa sababu pindi jana la virusi hivyo likiingia katika Tanzania yetu itakuwa balaa kubwa. Huu sio ugonjwa wa "watu masikini" kwa sababu moja ya njia za kusambaa kwake ni pamoja na msongamano, kitu kilichozeleka kwenye daladala zetu, maeneo kama Kariakoo, mashuleni na vyuoni, nk. 

Nihitimishe makala hii kwa kukuambatanishia ujumbe huu muhimu pichani


26 Feb 2020


Kuna mdau ameniomba nimtangazie kiwanja chake anachokiuza. Namnukuu

Mkuu naomba nami unisaidie kunitangazia kiwanja changu kilichopo Kata ya kimbiji mtaa wa kijaka wilaya ya kigamboni.
Block : E
SQ. : 1104 
Price : 5M tuu 
Nauzia shida tu na matatizo
Pia naweza kubadilishana na gari ndogo






Nawasilisha

1 Jan 2020




Kwa zaidi ya miaka 10 sasa nimekuwa na utaratibu wa kufanya ubashiri kuhusu yanayotarajiwa kutokea katika mwaka mpya, zoezi ninalolifanya siku ya kwanza ya mwaka mpya husika.

Mwaka huu 2020 unatarajiwa kuwa mgumu sana kwa Tanzania. Na bila kuumauma maneno, ugumu wa mwaka huo utachangiwa na "utawala wa mkono wa chuma" - unaozidi kuota mizizi -wa Rais John Magufuli. 

Moja ya matukio yatakayotawala vichwa vya habari mwaka huu ni pamoja na watu kadhaa maarufu kutoka kada mbalimbali "kupotea." Wahanga wakubwa wanatarajiwa kuwa wanaharakati wanaodiriki kukemea maovu mbalimbaliyanayofanywa na utawala wa Rais Magufuli.

"Kupotea" huko kutaendelea kufanya tishio la "Watu Wasiojulikana" liendelee kuwasumbua Watanzania kama ilivyokuwa mwaka jana 2019.

Kinachotarajiwa kufanya hali kutokuwa nzuri ni pamoja na hofu isiyo na msingi aliyonayo Rais Magufuli kuhusu uwezekano wa yeye kuchaguliwa kuwa mgombea urais kwa tiketi ya CCM na uwezekano wa yeye kushinda nafasi hiyo. 

Hofu hiyo inachangiwa na kile Waingereza wanasema "the guilty are always afraid." Sio siri kwamba Rais Magufuli amejitahidi sana kuwavunja moyo watu wengi tu ambao sio tu walikuwa na matarajio makubwa kwake bali baadhi yao  - ikiwa ni pamoja na mie -walishiriki kumnadi kwa nguvu zote katika kampeni za uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

Kubwa zaidi lililowavunja moyo watu hao ni "valid excuse" ya Rais Magufuli kuwa Watanzania waelekeze nguvu zao kwenye kuchapa kazi ilivyogeuka kuwa excuse ya kuwanyima raia haki zao za msingi. Kukandamiza haki ya kikatiba ya vyama vya upinzani kufanya shughuli zao za kisiasa, kukandamiza uhuru wa vyombo vya habari, kuwabambikiziawatumbalimbali kesi zisizo na kichwa wala miguu, kuendeleza siasa za chuki, ubaguzi na ukanda wa mchana kweupe, matusi ya hadharani dhidi ya watendaji mbalimbali wa serikali, na mlolongo wa vitu visivyopendeza. 

Kwa vile Rais Magufuli anafahamu kuwa "amewageuka" wengi wa waliomnadi na kumuunga mkono, anajikuta akiwa kwenye kundi la "the guilty are always afraid." Gulity for what? Well, hadi muda huu serikali yake inabaki suspect number one katika "kupotea" kwakda maarufu wa Chadema Ben Saanane ambaye alikuwa critic mkubwa wa Rais Magufuli; suspect number one katika jaribio la kumuua Tundu Lissu; suspect number one katika "kupotea" kwa mwanahabari Azory Gwanda; suspect number one katika yanayodaiwa kuwa "mauaji ya mamia" huko Mkuranga, Kibiti na Rufiji (MKIRU), suspect number one katika kifo cha afisa wa hazina kitengo cha EU, Marehemu Leopold Lwajabe ambaye kabla ya kuuawa alitekwa, akateswa na kubakwa. Unyama usiomithilika.

Serikali ya Rais Magufuli ni suspect number one katika kinachodaiwa kuwa ufisadi wa kihistoria wa fedha za umma, jambo lililopelekea kuondolewa kwa CAG Prof Assad ili ufisadi huo uendelee kufichwa.

In short tema, Rais Magufuli anaishi na hofu ya kitakachomtokea pindi akiwa sio rais, iwe kwa kushindwa uchaguzi, kung'olewa madarakani au kumaliza muhula wake. Kilicho wazi ni kwamba kwa aliyokwishatenda katika miaka hii minne kuelekea mitano, sio rahisi kwake japo kufikiria kuhusu kuwa nje ya nafasi ya urais. 

Na kwa vile mbinu yake kuu ya utawala - UBABE - inaelekea kuwa na ufanisi, kwa maana ya kwamba hakuna jitihada zozote zilizofanyika kupambana na mengi yasiyopendeza yanayofanywa na utawala wake, mwaka huu unatarajiwa kushuhudia ubabe maradufu. Kwa upande mmoja ubabe huo utakuwa mwendelezo tu wa yanayojiri muda huu lakini kwa upande mwingine utakuwa ni mkakati wa kuhakikisha anarudi Ikulu baada ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba.

Talking of uchaguzi mkuu, inatarajiwa kuwa uchaguzi huo mkuu utatawaliwa na hila na vituko na hujuma na mbinu chafu maradufu ya ilivyokuwa kwenye mzaha wa kisiasa uliopewa jina la "uchaguzi wa serikali za mitaa," ambapo pasi haya, chama tawala CCM kilijitangaza mshindi kwa asilimia 99.

Wakati endapo kila kitu kitabaki "constant" (yaani endapo hakutokuwa na mabadiliko), Rais Magufuli na CCM yake watajitangaza washindi wa kishindo kwenye uchaguzi huo mkuu ambapo kura zake na za CCM zitakuwa zaidi ya asilimia 90.

Kadhalika, endapo kila kitu ktabaki "constant," vyama vya upinzani vitaambulia kati ya viti 10 hadi 20 tu (yawezekana vikawa hata pungufu ya 10) vya ubunge kwenye uchaguzi huo mkuu.

Kadhalika, kadri uchaguzi huo mkuu utakavyozidi kujongea ndivyo Rais Magufuli na CCM yake watakavyozidi kuongeza jitihada za kuwanunua wabunge na madiwani wa vyama vya upinzani ili wajiondoe kwenye vyama vyao na kutangaza kujiunga na CCM. Mkakati huo ni sehemu ya jithada za kukomboa majimbo yaliyo chini ya wabunge wa upinzani.

Sambamba na hilo ni kukua kwa "uhasama" kati ya Chadema na ACT-Wazalendo, kitu kitakachochochewa na jitihada endelevu za CCM kuhujumu vyama vyaupinzani sambamba na jitihada za mapandikizi waliomo kwenye vyama hivyo vya upinzani wakiwana jukumu moja tu- kuvikwamisha.

Ukandamizwaji dhidi ya wanasiasa utawakumba pia baadhi ya wana-CCM hususan wanaohisiwa kuwa karibu na Bernard Membe, mwanasiasa anayemnyima usingizi Rais Magufuli kwa kudhani kuwa anataka kuchuana nae kwenye kinyang'anyiro cha kuwania urais kwa tiketi ya CCM.

Kuna uwezekano mkubwa kwa wana-CCM kadhaa wenye majina makubwa kufukuzwa uanachama. Licha ya hatua hiyo, wana-CCM hao watafunguliwa kesi za uhujumu uchumi.

Kwa upande mwingine, mwaka huu utashuhudia angalau mabadiliko mawili ya baraza la mawaziri. Sambamba na hilo, endapo Rais Magufuli atafanikiwa kuwa mgombea pekee wa CCM, inatarajiwa atashinikiza kuteuliwa kwa mgombea mwenza mwingine badala ya Mama Samia. 

Kuna uwezekano wa kujitokeza matishio ya mashambulizi ya kigaidi yatakayohusiana na hali tete iliyopo kwenye mpaka wa Tanzania na Msumbiji. 

Kuhusu Idara ya Usalama wa Taifa, nabashiri kutokea kwa mabadiliko makubwa yanayoweza kupelekea Mkurugenzi Mkuu wa sasa, Diwani Rajabu kuondolewa kwenye wadhifa ho na nafasi yake kuchukuliwa na aliyewahi kuwa Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Idara hiyo, Robert Makungu ambaye awali alitumbuliwa na kuwa RAS huko Tabora. 

Kiuchumi, vyuma vitaendelea kukaza. Na hali inatarajiwa kuwa ngumu zaidi mwaka huu kwa sababu CCM itaongeza jitihada za kukusanya fedha kwa ajili ya uchaguzi mkuu. Neno "jitihada" hapa linamaanisha mbinu chafu na za kifisadi kama ilivyokuwa kwenye skandali ya EPA/Kagoda.

Uchumi pia unatarajiwa kuwa mgumu kwa sababu kuna uwezekano wa baadhi ya nchi wahisani kusitisha misaada yao kufuatia ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu nchini Tanzania. 

Jambo jingine linalotarajiwa kuathiri uchumi na matumizi holela yanayofanywa na serikali ya Rais Magufuli bila kuzingatia idhini yabunge au/na kanuni za bajeti. 

Moja ya matukio ya nje ya Tanzania yanayoweza kuigusa Tanzania ni uhasama endelevu kati ya Rais Museveni na Kagame. Unfortunately, Tanzania ni eneo muhimu kimkakati kwa nchi zote mbili hasa kwa vile ndipo kunapotokea "vita ya kijasusi" kati ya Uganda na Rwanda. Kwamba nchi hizo mbili zinaweza kuingia vitani sio jambo lisilowezekana japo sio rahisi sana.

Kabla ya kuhitimisha makala hii, naomba kusisitiza kuwa ubashiri huu sio exact science bali ni matokeo ya mie mtumishi wako kumudu kusoma mwenendo wa mambo (trends) huko Tanzania. Japo ni rahisi kuhisi kwamba MATAGA na Praise Teram watatafsiri ubashiri huu kuwa ni "kazi ya kibaraka wa mabeberu kuiombea mabaya Tanzania," ukweli ni kwamba ubashiri huu umefanyika objectively.

Mwisho, haitokuwa jambo la kushangaza endapo mgombea urais wa CCM katika uchaguzi mkuu ujao hatokuwa Rais Magufuli. Si kwamba jina lake litakatwa lakini "laweza kutokea la kutokea."

Nimalizie kwa kuwatakia nyote heri ya mwaka mpya 2020.



14 Apr 2019

[Uchambuzi wa ACT Wazalendo Kuhusu Maeneo Kumi (10) Muhimu Kwenye Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa Mwaka wa Fedha wa 2017/18].

- Ikulu Yatumika Kuficha Ukaguzi wa Manunuzi ya Ndege

- Bilioni 800 Hazikutolewa kwa Ukaguzi
- Trilioni 4.8 Zimetumika Bila Kupita Mfuko Mkuu wa Hazina
- Mikopo ya Ndani Yashindwa Kulipa Madeni Kikamilifu
- 40% ya Bajeti yategemea Mikopo na Misaada Kutoka Nje



Ndugu Wanahabari



A: Utangulizi 



Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Prof. Mussa Juma Assad ametoa taarifa yake ya Ukaguzi wa Mapato na Matumizi ya Fedha za Umma kwa mwaka wa fedha wa 2017/18. Licha ya changamoto mbalimbali zilizotokea kabla ya CAG kukamilisha wajibu wake huu wa kikatiba, taarifa hiyo sasa iko wazi kwa umma, baada ya kuwa imekabidhiwa rasmi bungeni. 



Sisi ACT Wazalendo, tumeisoma, kuipitia na kuichambua taarifa husika, kwa lengo la kuitumia ili itusaidie kutimiza wajibu wetu wa kuisimamia Serikali kama chama mbadala nchini na kama Chama cha Upinzani Bungeni. Tunafurahi kupata fursa ya kuwa nanyi hapa ili kuzungumza na umma, kupitia nyinyi, juu ya maeneo Kumi (10) muhimu kwenye ripoti ya CAG kwa mwaka wa fedha wa 2017/18.



B: Maeneo Kumi (10) Muhimu Katika Ripoti ya CAG



1. Bajeti ya Serikali Sio Halisia, Mapato Yasiyokusanywa ni Tarakimu Mbili



Kwenye bajeti ya mwaka wa fedha wa 2016/17, ambayo ni bajeti ya kwanza ya Serikali ya Awamu ya Tano, mipango ya Serikali ilikuwa ni kukusanya shilingi 29.5 trilioni, kwa mujibu wa ripoti ya CAG ya 2016/17, kati ya fedha hizo, Serikali ilikusanya shilingi 25.3 trilioni. Na hivyo, kutokufikia lengo la makusanyo kwa 14.33%. Kwenye uchambuzi wetu wa mwaka jana tulieleza kuwa bajeti za Serikali si halisia.



Kwenye ripoti hii ya mwaka 2017/18, kwa mara nyengine, CAG amelithibitishia Taifa kuwa Serikali ya awamu ya tano inatunga Bajeti ambayo sio halisia. Katika Bajeti ya Serikali ya mwaka wa fedha wa 2017/18 jumla ya shilingi 31.7 trilioni zilitarajiwa kukusanywa na zilipitishwa kutumika na Bunge. Hata hivyo, kwa mujibu wa ripoti hii ya CAG, Serikali iliweza kukusanya kutoka vyanzo vyake vyote shilingi 27.7 trilioni tu, na kutumia shilingi 26.9 trilioni. Hivyo ikikosa makusanyo kwa 12.66% na ikikosa matumizi kwa 15.2%.



Kwa miaka mitatu ya mwisho ya Serikali ya awamu ya nne, wastani wa lengo lisilofikiwa na Serikali katika ukusanyaji wa mapato ya Bajeti ni tarakimu moja, 6.3% tu, ambapo kwa mwaka 2013/14 lengo halikufikiwa kwa 9%, kwa mwaka 2014/15 nako lengo halikufikiwa kwa 4%, na kwa mwaka wa fedha wa 2015/16 lengo halikufikiwa kwa 6% tu.



Hii inadhihirisha Kwa mara nyengine tena kuwa Serikali ya Awamu ya Tano hutangaza viwango vikubwa vya Bajeti ili kufurahisha umma ilhali uhalisia ni kuwa Bajeti ni ndogo zaidi. Kwa miaka 2 mfululizo CAG ametuonyesha kuwa Serikali inashindwa kufikia makadirio ya Bajeti Kwa zaidi ya shilingi Trilioni 4 kutoka Bajeti inayopitishwa na Bunge.



2. 40% ya Bajeti Inategemea Misaada na Mikopo



Ripoti ya CAG imetuonyesha kuwa ndani ya miaka miwili ya Serikali ya awamu ya tano uwezo wetu wa kujitegemea kibajeti umezidi kuzorota. Kwa mwaka wa fedha wa 2016/17 nchi yetu ilijitegemea Kibajeti kwa 65% kwa mapato ya ndani ya nchi, na 35% iliyobaki ndiyo iliyotokana na mikopo pamoja na misaada ya Wahisani. Hali Hiyo ni tofauti kwa mwaka wa Fedha wa 2017/18, tumedidimia zaidi.



CAG ameonyesha katika uchambuzi wake kuwa, nanukuu “Uchambuzi unaonyesha kwamba bila Mikopo na misaada kutoka kwa wahisani wa maendeleo, makusanyo ya ndani ya nchi yetu yangeweza kugharamia matumizi yote ya Serikali kwa asilimia 60 tu” (Chanzo: Ripoti ya Ukaguzi-Serikali Kuu-2017/18: Ukurasa wa 89).



Hii inaonyesha kuwa Bajeti yetu ya Tanzania ni tegemezi kwa 40% tofauti na tunavyoelezwa na Serikali kila wakati kuwa nchi yetu inaondoa utegemezi kwenye bajeti. Kwa mwaka 2016/17 utegemezi wetu uliongezeka kwa 27%, na kwa mwaka 2017/18 utegemezi wetu umeongozeka kwa 22%.



CAG ameonyesha kuwa Serikali ilikusanya shilingi 27.7 trilioni tu (makusanyo yote, ikiwemo misaada na mikopo kutoka ndani na nje) kwa mwaka wa fedha wa 2017/18. Makusanyo ya ndani yakiwa ni shilingi 16.7 trilioni, sawa na 60% ya makusanyo yote, na kwamba matumizi ya kawaida yaliyofanyika mwaka huo ni shilingi 15.3 trilioni, ambayo ni sawa na asilimia 55% ya makusanyo yote lakini ni 93% ya mapato ya ndani. Utegemezi huu utaathiri sana nchi yetu kwani gharama za kulipia mikopo (riba) zitakuwa kubwa kuliko hata uwezo wetu wa kuongeza mapato ya ndani.



3. Shilingi 800 Bilioni Hazikutolewa kwa Ukaguzi



Katika Uchambuzi wetu wa mwaka jana tulionyesha kuwa 6% ya fedha zilizokuwa zimekusanywa na Serikali hazijulikani zilipokwenda. Hizi zilikuwa ni shilingi 1.5 trilioni ambazo mjadala wake ulichukua mwaka mzima. Hoja yetu hiyo ilipelekea kufanyika kwa uhakiki maalumu na CAG, na ambapo bado Serikali ilishindwa kuonyesha zilipokwenda fedha hizo, zaidi ya kudai kuwa ilihamishia Ikulu matumizi ya shilingi 976 bilioni kati ya hizo 1.5 trilioni bila kumpa CAG uthibitisho wa uhamishaji huo wala kuonyesha fedha hizo zimefumikaje huko Ikulu.



Katika ukaguzi wa CAG wa Bajeti ya mwaka 2017/18, ambayo ni Bajeti ya Pili ya Serikali ya awamu ya 5, ameonyesha kuwa katika Bajeti ya shilingi 31.7 trilioni iliyoidhinishwa na Bunge, Serikali iliweza kukusanya shilingi 27.7 trilioni tu kutoka kwenye vyanzo vyote vya kodi, vyanzo visivyo vya kodi, mikopo ya ndani na nje, na misaada ya wahisani na washirika wa maendeleo. 



Serikali ilishindwa kukusanya kiasi cha shilingi 4 trilioni kama ilivyokuwa mwaka uliopita ingawa sasa ni sawa na 13% ya Bajeti yote ya mwaka 2016/17. Hata hivyo CAG anaonyesha kuwa shilingi 26.9 trilioni tu ndio zilitolewa kutoka Mfuko Mkuu wa Serikali na kwenda kutumika, hivyo shilingi 800 bilioni kati ya shilingi 27.7 trilioni zilizokusanywa kutokujulikana ziliko na hazikutolewa kwa ukaguzi.



4. Shilingi 4.8 Trilioni Zimetumika Bila Kupita Kwenye Mfuko Mkuu



Katika Ukurasa wa 91 wa ripoti yake yam waka wa fedha wa 2017/18, CAG anasema, nanukuu “Ikilinganishwa taarifa ya kutoa fedha (exchequer issue report) na taarifa ya Fedha zilizopokelewa na kuripotiwa katika taarifa za fedha za Mafungu husika pamoja na barua za kukiri mapokezi ya fedha kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, imebaini utofauti wa taarifa zilizoripotiwa…”. 



CAG ameeleza kuwa tofauti hiyo imesababishwa na kutokuwepo kwa mifumo thabiti ya usuluhishi kati ya fedha zilizotolewa na hazina na fedha zilizotolewa na wahisani wa maendeleo moja kwa moja kwenye miradi ya maendeleo katika Wizara. Ni muhimu sana kusisitiza hapa kuwa kwa mujibu wa CAG kuna fedha shilingi trilioni 4.8 ambazo makusanyo yake hayakuingizwa mfuko mkuu wa Serikali (tazama uk 91 wa Taarifa, tanbihi namba 15).



Suala la udhaifu wa Mifumo Katika Hazina pia limeelezwa kwa kina Katika Taarifa ya CAG ya Uhakiki wa Tofauti ya shilingi 1.5 Trilioni Katika mwaka wa Fedha 2016/17. Bado udhaifu huu unaendelea na madhara yake Katika usimamizi wa Fedha za Umma ni makubwa sana.



5. Bilioni 678 za Mamlaka Nyengine Ziliporwa na Mlipaji Mkuu wa Serikali



Kwenye ripoti ya CAG ya 2017/18 imeonyeshwa kuwa bado Serikali inatumia fedha ambazo sio zake (ring fenced) kama ilivyoonyeshwa kwenye ripoti ya mwaka 2016/17. Kwa mwaka 2017/18 CAG amebaini jumla ya shilingi 678 bilioni zilizokusanywa na Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) kwa niaba ya taasisi nyengine hazikuhamishwa kwenda kwenye taasisi husika, na badala yake zilihamishiwa kwa Katibu Mkuu Hazina ambapo huko hazikuonekana kwenye ukaguzi kama sheria inavyotaka. 



Fedha zilizoporwa na Hazina ni pamoja na shilingi 169 bilioni za Shirika la Reli, shilingi 168 bilioni za Wadau wa Korosho nchini na shilingi bilioni 16 za Wakala wa Umeme Vijijini (REA). CAG kwa mara nyengine tena amependekeza sheria iheshimiwa kuhusu matumizi ya fedha hizi za Taasisi mbalimbali. Kwenye ripoti ya CAG ya mwaka 2016/17 kiasi cha shilingi 2.2 trilioni za mamlaka mbalimbali nchini hazikurejeshwa kwenye mamlaka husika mara baada ya fedha hizo kukusanywa na TRA. Tabia hii ya kupora Fedha za Mamlaka nyengine licha ya Kwamba Fedha hizo zimewekwa kisheria na kikatiba inaua misingi ya matumizi bora ya Fedha za Umma.



Kwa Upande wa TRA Bado kuna changamoto kubwa ambazo zinahitaji kutatuliwa. Makusanyo yetu ya kodi Bado ni kidogo sana (tax yield) tukiwa wa mwisho Katika Jumuiya ya Afrika Mashariki, uwiano wa makusanyo ukiwa ni 12% tu ya Pato la Taifa. Hii inatokana tax base kuwa ndogo na mifumo sio rafiki kwa walipa kodi. Inawezekana TRA huchukua Fedha za Taasisi kupeleka Hazina ili kuonyesha makusanyo zaidi ilhali hali sio hiyo. Serikali inapaswa kukaa na sekta Binafsi kujadili kwa unyoofu (honestly) njia bora ya kupanua wigo wa Kodi ili nchi iweze kujitegemea. Katika uchambuzi wetu tumeacha mambo Mengi ikiwemo upotevu mkubwa wa mizigo ya transit ambao CAG ameuonyesha.



6. Kushuka kwa Thamani ya Shilingi Kunakuza Zaidi Deni la Taifa



Ripoti ya CAG ya 2017/18 imetuonyesha kuwa Deni la Taifa (Deni la Serikali) limefikia shilingi 50 trilioni mpaka Juni 30, 2018 likiwa na ongezeka la shiingi 4.85 trilioni, sawa na 10% kutoka shilingi 46 trilioni za Juni 30, 2017, deni hili likikua kwa shilingi 9.8 trilioni kwa muda wa miaka miwili tu kutoka Juni 30, 2016 mpaka Juni 30, 2018. CAG ameeleza kwamba kushuka kwa thamani ya shilingi ya Tanzania dhidi ya fedha za kigeni kumechangia kuongezeka kwa Deni kwa 20% kwa mwaka wa fedha wa 2017/18 (ongezeko kubwa zaidi ukilinganisha na 9% za mwaka wa fedha wa 2016/17). 



Hii inatokana na Deni letu la Nje kuwa kwenye Fedha za Kigeni na hivyo kuathirika sana kutokana na thamani ya shilingi kutetereka. Baada ya makosa ya kimaamuzi kwenye suala la Zao la Korosho, ni dhahiri kuwa Deni letu la Nje litaongezeka zaidi baada ya shilingi ya Tanzania kutetereka zaidi kwa kukosa Mapato ya Fedha za Kigeni. MAARIFA makubwa yanahitajika kuhami nchi kutokana na janga la Deni la Taifa.



7. Mikopo ya Ndani Yashindwa Kulipa Madeni Kikamilifu 



Lakini pia CAG ameeleza kuwa sababu Kuu zaidi ya kukua kwa deni la Taifa ni kwa kuwa tunaendelea kukopa zaidi. Kwa miaka mitatu iliyopita kukopa zaidi kulichangia ukuaji wa deni letu kwa 70%, ambapo kwa mwaka 2016/17 ilikuwa juu zaidi na kufikia 88%.



Zaidi CAG ameonyesha pia kuwa tulikopa mikopo ya ndani ya shilingi 5.7 trilioni kwa mwaka 2017/18 ambayo pamoja na kuwa na athari mbaya kwenye mikopo ya sekta binafsi nchini (maana inapunguza fursa ya wafanyabiashara wetu kukopeshwa na taasisi za ndani za fedha), lakini pia mikopo hiyo imeshindwa kulipa riba za mwaka za shilingi 6.1 trilioni. Na hivyo ilibidi Serikali kutafuta shilingi 448 bilioni kutoka kwenye vyanzo vingine ili kuweza kulipa riba hizo. 



Ripoti ya CAG imeeleza, nanukuu “Deni la Ndani halikuchangia kwenye miradi ya Maendeleo”. Hivyo tulikopa ndani ya nchi si kwaajili ya kufanya shughuli za maendeleo, bali kulipa deni la nyuma, na bado hata hiyo mikopo haikutosheleza ulipaji wa hayo madeni ya nyuma. Hali hii si afya kwa taifa letu.



Mfano kwa mwaka 2017/18 Kiwango cha kuhudumia Deni la nchi ni 108% ya fedha zilizopatikana kutoka kwenye mikopo ya ndani, na CAG ameonya kuwa jambo hilo lina athari kubwa. Ukurasa wa 141 wa Ripoti ya Ukaguzi wa Serikali Kuu CAG ameeleza, nanukuu “kuna uwezekano wa kuwa na madhara kwa uchumi (hali ya kuhudumia deni kwa 108%) isipotafutiwa ufumbuzi”. 



CAG pia ameonyesha kuwa kasi ya kukua kwa mikopo ya nje ni 38%, hali ambayo inaongeza gharama za kuhudumia madeni. Na jambo baya zaidi ni kuwa tunakopa zaidi mikopo ya kibiashara. CAG ameshauri watunga sera kuwa na busara wakati wa kuchagua miradi ya kupewa fedha za mikopo ya kibiashara, akishauri maamuzi yazingatie uzalishaji wa miradi husika. Vinginevyo Bajeti ya Taifa itakwenda kuhudumia deni tu.



Kwenye eneo hilo la Deni la Taifa pia ripoti ya CAG imeonyesha kuwa kuna upotoshwaji mkubwa wa mapokezi ya mikopo kutokana na mapungufu ya udhibiti wa ndani. Pia CAG ameonyesha kuwa mifumo wa kutunza madeni ni kianalojia (ya kizamani), jambo ambalo linaathiri kumbukumbu za madeni. 



8. Serikali Imeanza Kushindwa Kulipa Madeni (Defaulting)



Ripoti ya CAG imeonyesha kuwa Serikali imeshaanza kushindwa kulipa baadhi ya madeni yake (Defaulting). Tayari kuna fedha kiasi cha shilingi 212.7 bilioni Serikali imeshindwa kuzilipa kwa Benki Kuu nchini (BOT), zikiwa shilingi 199.79 bilioni ni riba ya nakisi ya Serikali, na shilingi 12.9 bilioni ni sehemu ya Serikali ya gharama za kudhibiti ukwasi kuanzia mwaka 2015/16 hadi 2017/18.



Serikali ilisaini Mkataba wa Makubaliano (MoU) na BOT, ambao unaitaka kulipa kila robo mwaka sehemu yake ya gharama ya kudhibiti ukwasi pindi hati ya madai inapotolewa. Ucheleweshwaji huu wa malipo utaongeza uwepo wa mali za BOT zisizo na tija, na ni dalili ya Serikali kushindwa majukumu yake kifedha.



9. Ikulu Yatumika Kuficha Ukaguzi wa Manunuzi ya Ndege



Hatujafanikiwa kuona Ukaguzi wa Manunuzi ya Ndege ikiwemo Ununuzi wa Ndege za Shirika la Ndege Nchini, ATCL ambao kwa sehemu umefanyika mwaka wa fedha 2016/17 na 2017/18.



Katika uchambuzi wetu wa ripoti ya CAG ya mwaka jana (ripoti ya mwaka wa fedha wa 2016/17) tuliwaeleza kuwa katika ripoti ile licha ya kuwa ni taarifa bora sana kwa maudhui na uchambuzi, kuna mambo muhimu kadhaa ambayo CAG aliyaacha. Na tukamtaka kwenye ripoti yake ya mwaka 2017/18 ayafanyie kazi, mojawapo ni ukaguzi wa Ununuzi wa Ndege Sita (6) zinazoendeshwa na Kampuni ya Ndege nchini, ATCL.



Mpaka sasa Serikali imeshatumia jumla ya Shilingi Trilioni1 kununua ndege sita (6) na katika makadirio ya Bajeti ya mwaka 2019/20 yanayoendelea sasa bungeni Serikali imeomba Bunge liidhinishe shilingi Bilioni 500 kwa ajili ya kulipia ndege mpya nyengine. Ufuatiliaji wetu umegundua kuwa Serikali imekuwa ikichukua Fedha za Umma kupitia Fungu 62 (Wizara ya Uchukuzi) na kufanya manunuzi ya ndege. Ndege hizo wanakabidhiwa Wakala wa Ndege za Serikali kama wamiliki na shirika la ATCL inakodishiwa ndege hizo kwa Mkataba maalumu (ambao haujawekwa wazi popote, hata kwa Bunge).



Tulitarajia kuwa ripoti hii ya CAG ya mwaka 2017/18 kwenye ukaguzi wa fungu Namba 62 tungeweza kuona ukaguzi wa manunuzi ya ndege hizi. Lakini Serikali kwa lengo la kuficha taarifa imeamua kuhamishia kwenye Ofisi ya Rais (fungu 20) Wakala wa Ndege za Serikali kupitia tangazo la Serikali namba 252 la Juni 2018.



Tumetafuta taarifa ya ukaguzi wa fedha hizo za umma zilizofanya manunuzi ya ndege bila mafanikio. Tunamwomba CAG;
- Afanye Ukaguzi Maalumu wa Fedha za Umma Shilingi Trilioni 1 zilizotumika kununua ndege.
- Afanye Ukaguzi wa usimamizi wa mkataba wa ukodishwaji wa ndege hizo kati ya Wakala wa ndege za Serikali na Shirika la Ndege la ATCL ili Watanzania wajue matumizi sahihi ya Fedha zao za Kodi.



Jambo hili ni muhimu sana, kwa sababu uzoefu unaonyesha kuwa kila jambo lenye harufu ya wizi au matumizi yenye mashaka basi Serikali huliamishia jambo hilo ikulu (Kwa kuwa inajua ukaguzi wake hautawekwa wazi). Hata kwenye fedha shilingi 1.5 trilioni ambazo tulizianisha kuwa hazijulikani ziliko kutokana na uchambuzi wetu wa ripoti ya CAG ya mwaka 2016/17, baada ya kuibana Serikali na kumtaka CAG afanye uchunguzi maalum, mwishowe Serikali ilihamishia Ikulu matumizi ya Shilingi 976 bilioni kati ya hizo shilingi 1.5 trilioni ili isihojiwe.



Mafungu mawili, Fungu 20 (Ofisi ya Rais Ikulu) na Fungu 30 (Sekretariati ya Baraza la Mawaziri) yanapaswa kumulikwa sana katika matumizi ya Fedha za Umma. Tumeona mwaka huu Serikali inaomba Bunge litenge shilingi Bilioni 302 kwa Fungu 30 kwa kile kinachoitwa ‘matumizi mbalimbali ya kitaifa’. Mwaka ujao, Mungu akituweka hai, tutafuatilia kwa kina kaguzi za mafungu Haya kwani inaonyesha ndimo inakuwa kichaka Cha kuficha Taarifa za namna Fedha za Umma zinatumika.



10. Hoja za Ukaguzi za Shilingi Bilioni 225 hazina majibu kabisa
Kwa ujumla, na kwa Serikali Kuu peke yake, Hoja zote za Ukaguzi zilizoibuliwa na CAG kwenye Hesabu za Mwaka 2017/18 ukiachana na hoja kubwa nilizoeleza hapo juu, zina thamani ya shilingi 225 bilioni kati ya Fedha zote zilizokusanywa kwenye mwaka wa Fedha husika. Hii inaonyesha kuwa bado Serikali haijaweza kufanyia kazi Hoja za CAG kwa wakati na kwamba mifumo ya Serikali bado inavujisha Fedha za Umma.



C: Mapendekezo ya ACT Wazalendo 



Baada ya kusoma taarifa hiyo ya CAG na kuyaanisha maeneo Kumi (10) muhimu, sisi ACT Wazalendo tuna mapendekezo yafuatayo:



1. ACT Wazalendo tunawasihi Wabunge wote bila kujali vyama vyao kutekeleza wajibu wao wa kuisimamia Serikali. Wabunge wasipotekeleza wajibu wao huo basi nchi yetu itaangushwa na matumizi mabovu na ya kinyume na Sheria kama tulivyoaina kwenye Uchambuzi wetu.



2. Serikali iwe inatunga Bajeti Halisia ambayo inatekelezeka, tofauti na inavyofanya kwa miaka minne mfululilo sasa, ambapo inataja namba kubwa ambayo Bajeti husika huwa haipatikani kwa ukamilifu wake na hivyo kuathiri sana miradi ya Maendeleo ambayo inakuwa imepangiwa mafungu ya Fedha. Ni bora kuwa na Bajeti ndogo ambayo inatekelezwa badala ya kuwa na Bajeti kubwa ambayo haitekelezwi ipasavyo.



3. Serikali itazame upya utekelezaji wa Sera zake za kiuchumi kwani dalili zinadhihirisha kuwa Uchumi wetu unaanguka. Ikibidi Kuwe na Mjadala wa Kitaifa juu ya hali ya uchumi wa nchi yetu, mjadala huo usaidie kupata uhalisia wa hali mbaya ya uchumi wetu, mbinu za kuunasua, na mawazo ya kuinasua nchi kutoka kwenye utegemezi wa misaaada pamoja na mikopo inayoongeza ukuaji wa deni la Taifa.



4. Serikali ionyeshe ilipo shilingi 800 bilioni isiyoonekana matumizi yake katika ripoti ya CAG yam waka wa fedha 2017/18.



5. Serikali ileze ni kwa nini Fedha Jumla ya shilingi Trilioni 4.8 hazikupita kwenye Mfuko Mkuu wa Hazina ili utolewaji wake uweze kufuata masharti ya Katiba na Sheria za nchi. Fedha hizi za Wafadhili zinaonekana Katika Vitabu vya Bajeti Lakini CAG hazioni kuingia mfuko Mkuu na hivyo kutoka kwake kunaweza kuwa ni kinyume Cha Sheria. Menejimenti ya Wizara ya Fedha na Mipango ihakikishe inafanya usuluhishi sahihi wa taarifa za fedha zilizotolewa kwa Wizara mbalimbali na fedha zilizopokelewa moja kwa moja na wahisani wa maendeleo katika miradi. Hazina ifanyiwe usafi maalumu ili kuhakikisha ‘credibility’ ya Taarifa zake.



6. Serikali izingatie Sheria na Katiba Kuhusu Fedha za Taasisi ambazo zimetengwa kisheria Lakini Hazina inazitumia bila kujali Sheria. Hazina ihakikishe inazirejesha kwa wenyewe Ada, Tozo na mapato hayo ambayo TRA ilikusanya kwa niaba ya Idara, Wakala na Taasisi nyengine.



7. Wabunge, kama sehemu ya wenye wajibu wa kutunga sera tunayo nafasi ya kuisimamia Serikali kwenye suala la kushuka kwa thamani ya shilingi, kwanza kwa kuwawajibisha wote waliosababisha sintofahamu ya zao la korosho ambalo kama tungeuza basi kungepatikana unafuu kwenye deni la Taifa.



8. Ili kudhibiti kasi ya ukuaji wa Deni la Taifa, haswa Deni la Nje, kutokana na kushuka kwa thamani ya shilingi yetu, tunapendekeza kuwa Serikali ifanye hedging ya Deni la Nje ili kuwa na uhakika wa thamani ya fedha itakayotumika muda wote kuhudumia Deni hilo. Serikali ya Awamu ya Tano imeonyesha kutegemea sana mikopo ya kibiashara kutoka Mabenki ya Nje na hivyo kuweka nchi kwenye hatari kubwa ya Mtego wa Madeni (Debt Trap). Hedging inaweza kusaidia kudhibiti kasi ya ukuaji wa Deni la Nje.



9. Tunamsihi ndugu Rais atambue kuwa njia ya bora ya kupambana na rushwa na ufisadi ni kuwezesha mifumo kufanya kazi. Mtu mmoja hawezi kamwe kuwa dawa ya ufisadi ulioota mizizi nchini kwetu. Ripoti za CAG na madudu yaliyoibuliwa kila kona inaonyesha dhahiri kuwa silaha ya uhakika ni kujenga Taasisi imara za Uwajibikaji ili kudhibiti Fedha za Umma. Miaka 4 aliyepo madarakani imethibitisha kuwa nguvu ya Mtu mmoja haitoshi kukomesha ubadhirifu bali Mifumo Imara.



Ni matarijio yetu kuwa Watanzania wataendelea kuisoma na kuichambua Taarifa ya CAG na kuwaomba Wabunge watimize wajibu wao wa kuisimamia Serikali ili kujibu hoja zote za Ukaguzi. Bila Bunge kutimiza wajibu wake ipasavyo mzunguko wa uwajibikaji unakuwa haufungi. Tumeona Katika Taarifa ya CAG kuwa Hoja hazijibiwi na hivyo hazifungwi na madhara yake ni kuwa kila mwaka hoja zinaongezeka tu.


Ahsanteni Sana.

Kabwe Z. Ruyagwa Zitto
Mbunge, Kigoma Mjini
Kiongozi wa Chama, ACT W
azalendo
Aprili 14, 2019
Dodoma

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.