30 Sept 2011



Nimetumiwa na mdau Tluway Tsere,nami naiwasilisha kama ilivyo



Habari za asubuhi Ndg. zangu
Tutafakari hii hadithi fupi, kwani mimi sikulala usingizi
jana baada ya kusikia kuwa Tuzo ya Rostam Aziz imekubaliwae
na mahakama kuu. Watakaolipa si Tanesco bali ni sisi watumiaji
wa umeme.
"tutafakari"
.
An airplane was about to crash; there were 5 passengers on board but only 4 parachutes. The first passenger said, " I'm Kobe Bryant, the best NBA basketball player, the Lakers need me, I can't afford to die.... So he took the first pack and left the plane. The second passenger, Hillary Clinton, said, "I am the wife of the former president of the United States, I am also the most ambitious woman in the world and I am a New York Senator and a potential future president." She just took the second parachute and jumped out of the plane. The third passenger, J.K, said: "I'm President of Tanzania, I have a great responsibility being the leader of a nation. And above all I'm the cleverest President in Tanzania's history, so Tanzania's people won't let me die." So he put on the pack next to him and jumped out of the plane. The fourth passenger, the Pope, says to the fifth passenger, a 10 year-old school boy, "I am old and frail and I don't have many years left, as a Catholic I will sacrifice my life and let you have the last parachute." The boy said, "It's OK, there's a parachute left for you. Tanzania's cleverest President has taken my schoolbag."

27 Sept 2011



Natumaini baada ya kuisoma tunaweza kuelewana kwanini ninatofautiana na uchambuzi wa Bwana Ilyas.Katika paragrafu ya kwanza tu,mwandishi ameshahitimisha kuwa Chadema ina safari ndefu ya kushinda kuwa mtawala mbadala.Anaandika "...ili CHADEMA kushinda katika safari ndefu iliyonayo kama mtawala mbadala kinapaswa kushindwa sasa." Hata hivyo,katika makala hiyo hakuna mahala ambapo mwandishi ameweka sababu za kwanini safari hiyo ya Chadema iwe ndefu,au kwanini anaona hivyo.

Pengine jingine linaloweza kuzua taswira tofauti ya mtizamo wa Bwana Ilyas kwa Chadema ni ukweli kwamba kwa ujumla 'uhuni waliofanya Chadema' unaweza kabisa kufunikwa na 'uhuni mwingine mkubwa' uliofanywa na kiongozi wa CCM,Mbunge Ismail Aden Rage kupanda jukwaani akiwa na bastola.Kwa hakika alichofanya Rage ni zaidi ya uhuni,kwani hata kama anamiliki silaha hiyo kihalali,haiingia akilini kwa mbunge huyo kupanda jukwaani akiwa na silaha-na hakufanya jitihada yoyote kuificha.

Na 'uhuni' mwingine wa kuchefua ni ukweli kwamba hadi sasa hatua pekee iliyochukuliwa dhidi ya Rage ni tamko la Waziri wa Mambo ya Ndani kwamba mbunge huyu anastahili kuhojiwa.Hebu pata picha aliyepanda jukwaani angekuwa Mbunge wa Chadema au CUF!Ni dhahiri muda huu angekuwa lupango,na uchunguzi wa kama anamiliki silaha kihalali au la ungefanyika wakati akiwa rumande.

Tukibaki kwenye hoja hiyo hiyo ya 'uhuni' hivi kuna uhuni mkubwa na mchafu zaidi ya ule wa kiongozi mwandamizi wa CCM (na de facto mratibu wa kampeni za chama hicho huko Igunga),Mwigulu Mchemba kutembea na mke wa kada mwenzie wa CCM?Huu sio tu uhuni bali ni ukosefu wa maadili usioelezeka.

Angalau Chadema wanaweza kutoa excuse (ambayo inaweza isikubalike) kuwa chama hicho na viongozi wake si wakomavu wa kisiasa (kwa maana ya uzoefu) lakini tunawezaje kuelezea uhuni wa viongozi wa chama ambacho si tu ni chama tawala lakini pia kina uzoefu unaoweza kuzidi jumla ya umri wa vyama vyote vinavyoshiriki kampeni hizo?

Japo Bwana Ilyas amebainisha kuwa hawezi kutaja "mlolongo wa matukio ambayo yamepelekea baadhi ya watu kuiangalia Chadema kwa jicho la tahadhari badala ya matumaini" kwa hakika shutuma nzito anazoelekeza dhidi ya chama hicho zilipaswa kuambatana na mlolongo huo wa matukio,japo in a point form (yaani kwa kutaja pasipo kufafanua).

Naomba kuweka bayana kwamba two wrongs do not make a right.Hapa ninamaanisha kuwa 'uhuni' wa Rage na wa Waziri (katika kudili na uhuni wa Rage) haupunguzi 'uhuni' wa Chadema.


Lakini pia Bwana Ilyas anakosea kuchukulia tukio hilo lililofanywa na wafuasi wa Chadema wakiongozwa na wabunge wawili tu kuwa ni taswira nzima ya 'uhuni' wa Chadema.Mchambuzi yeyote makini hawezi kuhitimisha kuwa kitendo cha Rage kupanda na silaha jukwaani au kitendo cha Mchemba kutembea na mke wa kada mwenzie wa CCM kuwa ni picha halisi ya nidhamu mbovu ya CCM.

Lakini pia naomba ifahamike kuwa Chadema wanatambua fika mwenendo wa mambo ambapo sheria huonekana zimevunjwa pale tu wapinzani (au walalahoi) wanapokwenda kinyume na taratibu.Bwana Ilyas anafahamu fika kuwa laiti Chadema wangeamua kutoa taarifa kwa vyombo husika kuhusu 'uhuni' wa Mkuu wa Wilaya 'aliyekwidwa' kwa kukiuka taratibu za uchaguzi kusingefanyika lolote.Ushuhuda wa hili ni namna tuhuma za waziwazi za vitendo vya rushwa kwenye mchakato wa ndani wa CCM kupata wagombea wake kwenye nafasi za udiwani na ubunge katika uchaguzi mkuu uliopita ambapo tulishuhudia TAKUKURU ikichezeshwa sandakarawe,na wananchi kumwagiwa mchanga wa macho kwa baadhi ya wahusika kukamatwa.Labda Bwana Ilyas anaweza kutupa takwimu ni watuhumiwa wangapi walikwisha adhibiwa kisheria kutokana na vitendo hivyo.

Siungi mkono matumizi ya nguvu katika kudai haki,lakini ni ukweli usiopingika kuwa mara nyingi tawala dhalimu hazitowi haki pasipo kutumia msuli.Diplomasia ni njia bora zaidi ya kudai haki au kuendesha majadiliano.Lakini kwa  bahati mbaya- na naamini Bwana Ilyas anajua hilo-mara kadhaa diplomasia imekuwa kikwazo katika upatikanaji wa haki kwa haraka.Ndio maana hata Wapalestina walipowasilisha ombi lao la uanachama wa umoja wa mataifa waliweka bayana kuwa WAMECHOSHWA na danadana za haki yao kuchezewa kama privilege flani.

Laiti sheria,kanuni na taratibu zingezingatiwa,Mkuu wa Wilaya mhusika katika tukio hilo asingezifinyanga,na kwa maana hiyo asingekutana na hasira za wana-Chadema wanaodai haki yao.Marehemu Kighoma Ali Malima aliweka wazi mtazamo wake kuhusu namna haki inavyoapaswa kudaiwa.Alisema: "HAKI HAITOLEWI KAMA ZAWADI.INACHUKULIWA AU KUDAIWA,HATA KWA NGUVU INAPOBIDI."

Maandiko Matakatifu ya Waislamu (dini ambayo naamini Bwana Ilyas ni muumini wake yanasema hivi (roughly)  kuhusu jambo baya: "lisemewe vibaya...lichukiwe...na ikibidi liondolewe hata kwa nguvu." (Ninasistiza kuwa nukuu hiyo ni roughly).Sijui kwa Bwana Ilyas kama kuna jambo baya na amelichukia lakini bado lipo,amelikemea lakini linazidi kukua,hatofikia hatua ya kuliondosha hata kwa nguvu ikibidi?

Hicho ndicho kilichofanywa na Chadema.Wlilazimika kumkwida Mkuu wa Wilaya kwa vile aliamua kwa makusudi kupuuza sheria za uchaguzi na haki za vyama vingine vinavyoshiriki kwenye uchaguzi huo mdogo.Ni kweli ingependeza iwapo diplomasia ingetumika,lakini huwezi kuwa na fair play kwenye soka katika mechi ambayo timu pinzani ina wachezaji 15,yaani licha ya wale 11 wa kawaida,pia yumo refa,washika vibendera wawili na kamisaa.Au hakuna haki itakayopatikana katika kesi ambapo mshtaki au mshtakiwa pia anafanya kazi ya uendesha mashtaka,yeye huyhuyo ni mzee wa baraza,na pia ni hakimu/jaji.

Pasipo kuitihumu waziwazi,Bwana Ilyas anaihusisha Chadema na ukabila-yaani Uchagga.Amemtaja Mzee Edwin Mtei na mwenyekiti wa sasa Freeman Mbowe.Kwa makusudi kabisa,amekwepa kutaja safu nzima ya uongozi wa juu wa Chadema unaojumuisha (pasipo kufuatilia mpangilio maalum) Mchaga (Mbowe),Muha (Zitto Kabwe) na Mmbulu (Dkt Slaa).

Busara ndogo tu ingeweza kumsaidia Bwana Ilyas kubaini kuwa ushindi walioupata Chadema katika majimbo mbalimbali kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka jana haukutokana na ukabila.Je John Mnyika alishinda ubunge huko Ubongo kwa vile kuna Wachagga wengi?Vipi kuhusu Halima Mdee huko Kawe?

Pengine katika kuonyesha chuki yake kwa Chadema,Bwana Ilyas anaituhumu Chadema kuwa iliwezesha Mbowe (Mchagga na Mkristo) kupata uenyekiti kwa kutumia mbinu (ambazo hata hivyo ameshindwa kuzibainisha).Kwani ndugu yangu huyu ambaye ninamheshimu vya kutosha hataki kumwangalia Mbowe kama MTANZANIA na badala yake anaangalia kabila lake (UCHAGGA na dini yake UKRISTO).Huu ni ubaguzi wa waziwazi.Ni sawa kwake kuinyooshea kidole Chadema kwa kujaza Wachagga na Wakristo lakini haoni tatizo kwa kwa CUF au CCM kuwa na idadi kubwa ya Waislam kwenye ngazi za juu za uongozi wa vyama hivyo.

Bwana Ilyas,hivi hata katika karne hii bado unajadili wasifu wa watu kwa vigezo vya dini na kabila,badala ya kuangalia sifa walizonazo kiuongozi?Na kuna ubaya gani kwa chama kujaza watu wa kabila au dini moja ilhali kinawatumika wananchi ipasavyo?Je msukumo wa Chadema uliopelekea serikali ya Rais Jakaya Kikwete kushughulikia bei ya sukari kuna uhusiano gani na ukristo au uchagga?

Bwana Ilyas anaendeleza tuhuma zake dhidi ya Chadema na kudurufu madai kuwa chama hicho kinalea udini.Anadai (nanukuu)"...Kama vile hilo halitoshi, tukielekea katika uchaguzi wa rais na wabunge wa mwaka 2010 ambao CHADEMA ilionyesha muamko mkubwa katika medani za siasa nchini, CHADEMA ama kwa kudhamiria, kutokudhamiria au kwa kulazimika, wakafanya kosa jingine ambalo badala ya kuwanasua katika kiwingu cha ukabila na udini wakajikuta wanajisimika ndani ya wingu la Udini."

Katika uchambuzi fyongo,Bwana Ilyas anadai kuwa Chadema imekuwa ikitafuta uungwaji mono na Kanisa Katoliki.Lakini anajikanganya pale anapoweka wazi kwanini inawezekana kuhisi Chadema na Kanisa Katoliki ni "damu damu" anaposema, "Hili lilikuja ama kutokana na kanisa hilo kama watanzania wengine kuchukizwa na maovu na usaliti wa Chama cha Mapinduzi (CCM)..." Kwa hiyo ni wazi kuwa chuki ya Kanisa Katoliki dhidi ya maovu yaliyokuwa yanafanywa na CCM ilishabihiana na ajenda za kupinga maovu zilizotawala kampeni za Chadema.Huu nao ni udini?

Lakini anageuka tena na kuirushia kombora Chadema kwa kudai "...au kutokana na dalili za uwezekano wa ushindi wa uhakika wa mgombea Urais wa CHADEMA ambaye ni kiongozi wa kiroho na aliyekuwa mtumishi wa ngazi za juu wa chombo nyeti cha kanisa hilo." Hivi Bwana Ilyas anataka kutuambia kuwa hadi leo hafahamu kuwa Dkt Willbrod Slaa si kiongozi wa kiroho?Aua ameamua wka makusudi kuwaiga Daily News na Habari Leo walioamua kumtambulisha Dkt Slaa kama PADRE?

Ni kweli,kiongozi huyo wa Chadema aliwahi kuwa Padre (na upadre si uhalifu kiasi cha kujenga negative connotation) lakini aliamua kuacha nafasi hiyo na kujikitka kwenye siasda.Kuendelea kumwita kiongozi wa kiroho ni sawa na kumtambulisha Kikwete kama kiongozi wa jeshi japo alishaacha uanajeshi zamani hizo.

Bwana Ilyasa anafanikiwa vizuri kuweka tatizo lake la UDINI (ambao ironically anautumia kuishutumu Chadema) anapodai "Kitendo cha viongozi wa kanisa la Katoliki kuanzisha na kuendeleza mpambano mkali wa majukwaani na katika alteri za kanisa kuwashutumu viongozi wa chama tawala cha CCM na serikali yake inayoongozwa na Rais na Mwenyekiti Muislamu, kabla na hata wakati wa uchaguzi huo kilijenga mtazamo wa kuwa kanisa hilo na hivyo wafuasi wake walipaswa kuiepuka CCM na wagombea wake na hivyo kuashiria kuwa CHADEMA ndio chaguo lao."

Naomba kumfahamisha Bwana Ilyas kuwa mtazamo huo ni wa makengeza.Kanisa lilikuwa na linaendelea kukemea maovu bila kujali yanafanywa na muumini wa dini gani.Kwani wakati Kanisa linaikemea CCM kuhusu ufisadi,Waziri Mkuu wa serikali ya CCM hakuna Mkristo?Ina maana Bwana Ilyas anataka kutuaminisha kuwa Kikwete (Muislam) ndio CCM?Au kwa lugha nyingine,tunaposhutumu ufisadi ndani ya CCM tunaushutumu Uislam kwa vile tu mwenyekiti wa chama hicho ni Muislam?Na Bwana Ilyas anasemaje kuhusu Muislam Zitto Kabwe anapokemea ufisadi akiwa ndani ya 'chama cha Wachagga na Wakristo Chadema'?

Bwana Ilyas anaendelea kuuthibtishia umma jinsi udini unavyomkwaza kufanya uchambuzi usio wa kibaguzi kwa kuwashutumu Chadema kumdhalilisha "mwanamama wa Kiislam na hijabu yake." Hapati shida kuepuka kuzungumzia wadhifa wa mwanamama huyo bali inakuwa rahisi kwake kumtambulisha kwa dini yake na vazi lake la kidini.Ni hivi,si Uislam au hijab itakayompendeza Laah pasipo kutenda yale atakayo kama ambavyo si upadre au kutembea na Rozari Takatifu kutakakomfanya Mkristo afikie uzima wa milele.Kama DC huyo alikuwa mcha Mungu halisi basi angefuata maagizo ya kidini ya kutii mamlaka za dunia.Angezingatia taratibu za uchaguzi zinasemaje badala ya kukurupuka na vikao vya kizushi ambavyo kimsingi vililenga kuitengenezea CCM mazingira ya ushindi.

Pamoja na mazingaombe yanayoendelea kuhusu dhana ya kujivua gamba ndani ya CCM, Bwana Ilyas anadiriki kukisifu chama hich akidai kuwa hiyo ni hatua ya kwenda mbele kufuatia matokeo yasiyoridhisha sana katika uchaguzi mkuu uliopita.Ninapenda kuamini kuwa ndugu yangu huyu ana uwezo kubwa wa kujenga hoja lakini amnakwazwa na hisia binafsi.Hilo gamba lililowishavuliwa na CCM ni lipi?Kujiuzulu kwa Rostam Aziz?Ni Rostam huyuhuyu aliyesafishwa na Kikwete kwenye kampeni za uchaguzi mkuu mwaka jana na ambaye leo anatumika kuipigia debe CCM huko Igunga?

Na kama kujivua gamba,vipi mbona Mzee wa Vijisenti Chenge na mwenzie Lowassa bado wapo madarakani huku tukiendelea kusikia kauli za kujikanganya kuhusu suala zima la CCM kujivua gamba?

Nimalizie makala hii kwa kumsihi Bwana Ilyas kwamba ili aweze kuiangalia Chadema vizuri anapaswa kuweka kando hisia zake za udini.Na kama anataka kutumia hoja za udini basi asichelee kuzungumzia pia namna CCM inavyowatumia baadhi ya Waislam kwa manufaa ya kisiasa (na hapa wa kulaumiwa ni Waislam haohao ambao mwaka 2005 waliingizwa mkenge na akina Kikwete kwa kuwaahidi Mahakama ya Kadhi huku dandana zikiendelea hadi leo).

Ushindi wa Chadema ni ushindi kwa kile asiyependa kuona Tanzania ikiendelea kuwa shamba la bibi kwa mafisadi.Chadema,pamoja na Bwana Ilyas kuituhumu kuwa inakumbatia udini na ukabili,imewatumikia vyema Watanzania katika muda mfupi tu ambapo imeweza kuibua ujambazi mkubwa dhidi ya taifa letu (EPA,Richmond,Buzwagi,Deep Green,Meremeta,nk).

Bwana Ilyas anapaswa kutambua pia kuwa laiti Chadema ingekuwa chama cha udini isingepiga kelel kuhusu umafia wa Richmond ambao mhusika mkuu alikuwa Edward Lowassa,mkristo ambaye amekuwa akimwaga mamilioni ya shilingi makanisani.Kadhalika,Chadema ingekalia kimya ufisadi wa Kiwira au namna Ikulu ilivyogeuzwa sehemu ya biashara na Rais Mstaafu Benjamin Mkapa,Mkatoliki ambaye hakosekani kanisani kila Jumapili.

Na kelele za Chadema kuhusu umuhimu wa marekebisho ya Katiba hazikuangalia maslahi ya Wakristo bali Watanzania kwa ujumla.Kuihukumu kwa hoja mfu za udini,ukabila na uhuni hakuna tofauti na harakati za makusudi za mafisadi kumhukumu kila anayepigania haki ya Mtnzania kuwa ni mhaini,anayetaka kuvuruga amani na utulivu (wa mafisadi kufanya ulafi wa kuifilisi Tanzania,I suppose) na kukwaza harakati za kumpatia Mtanzania ukombozi wa pili.

Kama alivyoniambia msahiliwa mmoja kwenye utafiti vitendo wa kozi yangu kimasomo, "haya mambo ya Ukristo na Uislamu sana sana ni huko mijini tu,ambako napo watu wanatumia dini kama mbinu ya kumudu maisha.Huku vijijini uhaba wa maji haubagui Mkristoa au Muislam.Mgao wa umeme pia hauchagui madhehebu.Kisima cha maji kilichopom msikitini kinahudumia wanakijiji wote pasipo kuuliza kama huyu ni Hamisi au John.Vyama vya ushirika vinapotukopa mazao yetu haviangalii kama flani ni Mkristo au Muislam.Pengne matokeo ya darasa la saba au sekondari yakitoka na Waktisto wengi wamefaulu na watoto wetu wa Kiislam wamefeli ndio kidogo unaweza kusikia watu wanahoji,lakini kimsingi watoto hao,paspo kuangalia madhehebu yao wanasoma katika mazingira magumu kabisa-sakafuni na walimu wao-pasipo kuangalia madhehebu yao-wametawaliwa na manung'uniko."

Tusiwape excuse mafisadi kwa vile tu wanaongozwa na Muislam au Mkristo.Tunaweza kutofautiana katika jinsi tunavyopiga kelele kuhusu ufisadi lakini kimsingi waathirika wa dhambi hiyo ni sote.Lakini kwa vile mafisadi hawana tofauti na wakoloni waliotubagua kwa misingi ya rangi na dini,wataendelea kutumia kete za ukabila na udini kutufarakanisha ili wazidi kutufisadi.Hata hivyo sote tunajua kuwa fedha wanazotufisadi haziendi misikitini au makanisani bali zipo kwenye akaunti zao za vijisenti huku Ughaibuni,huku nyingine zikitumika kuongeza idadi ya mahekalu yao na misururu ya magari yao ya kifahari pamoja na kukuza idadi ya nyumba ndogo zao.Wahanga wao ni mimi na wewe,regardless ya tofauti zetu za kidini au kikabila.

Let's agree to disagree!

26 Sept 2011


Wajuzi wa mambo wanadai kuwa moja ya mambo yanayopunguza ufanisi wa Idara yetu ya Usalama wa Taifa ni tabia iliyoota mizizi ambapo kila kigogo anataka kumpatia mwanae,mpwae,mtoto wa rafiki yake,nk katika ajira ya taasisi hiyo nyeti.Haina ubaya kutoa ajira iwapo mwajiriwa mtarajiwa atakuwa na sifa husika.Lakini uzoefu umeonyesha kuwa kanuni na taratibu zinabemendwa makusudi ili ajira hizo ziende kwa watu wa karibu wa vigogo hao.

Kibaya zaidi ni ukweli kwamba wengi wa watoto wa vigogo wanapopata ajira kwenye taasisi kama hii ambayo msingi wake mkubwa ni uzalendo wa mtumishi husika hujiona kama 'untouchables' flani,wanafanya mambo wapendavyo,usumbufu mtaani kwa zile 'unajua mimi ni nani/nafanya kazi wapi' huku bastola zikiachwa zionekane waziwazi kama Aden Rage.Wengi wa hawa vijana hawafahamu jukumu kubwa walilonalo kwenye kila sekunde ya uhai wa Mtanzania.Don't get me wrong kuwa ninajifanya kuelewa sana mambo haya lakini ukweli ni kwamba taaluma ya ushushushu ni uti wa mgongo wa uhai wa taifa lolote lile duniani.Idara ya Usalama ya nchi ikiyumba,nchi nayo inayumba.Watu wengi hawaelewi umuhimu wa chombo hiki kwa vile kimaadili kinapaswa kufanya kazi zake kwa siri,japo watoto wa vigogo wanaona usiri huo kama kero.

Anyway,nimekutana na tangazo la ajira za ushushusu katika 'Idara ya Usalama' (wa ndani-yaani ya kuzuia ujasusi) ya Uingereza-MI5 au kwa kirefu Military Inteligence,Section 5)-ambalo limewekwa kwenye gazeti la bure la kila siku la METRO.Utaratibu huu ambao sitarajii kuuona ukiigwa na taasisi nyingi za usalama duniani,achilia mbali yetu,unaweza kusaidia sana kufanya zoezi zima la kuajiri (recruitment process) kuwa ya huru,wazi na inayowekea mkazo uwezo,ujuzi na sifa za mwombaji kazi (based on merit(s)).

Hii ni mada nyeti kwahiyo naomba niishie hapa.Ukiwa na swali,usisite kuniuliza (majibu yatategemea swali limeulizwaje).

25 Sept 2011


Mchungaji aliyetibuana na kanisa lake ameanzisha kanisa la Facebook.Mchungaji Mark Townsend (44),ameanzisha kanisa analoliita The Hedge-Church baada ya kuhitilafiana na wazee wa Church of England.

Katika kuchangisha fedha,mchungaji huyo  pia anamiliki tovuti ya kukodisha mchungaji,ijulikanayo kama Rent-a-Rev ambayo inachaji kati ya pauni 40 (Shs 102,029.40) na 150 (shs 382,610.25) kwa ajili ya kufungisha ndoa za wandandoa wa jinsia moja au wa jinsia tofauti,ibada za mazishi na ubatizo,shughuli ambazo zinafanyikia aidha msituni,majumbani au hata kwenye baa.

Kanisa hilo tayari lina waumini 416 na inaaminika kuwa ni la aina yek duniani.Misa na huduma za maombi zinafanyikia mtandaoni na waumini wanatumia ujmumbe wa baraka kila siku kutoka kwa Mchungaji Townsend.

Mwezi ujao,Mchungaji huyo ataendesha ibada ya komunio itakayoonyeshwa moja kwa moja mtandaoni (live streaming).Mark,kutoka eneo la Leominster,Herefordshire,anasema: "Niliamua mwaka jana kuachana na Church of England.Kwa miaka 10 iliyopita nimelitumikia kanisa hilo katika mahusiano ya upendo-chuki (love-hate relationship).Nililazimika kufanya mambo ambayo nilikuwa siyaamini na nilitamani sana mabadiliko.Imechukua mwongo mzima  (kipindi cha miaka 10) kwa dhamira yangu kutimia."

CHANZO: Habari hii imetafsiriwa kutoka gazeti la Daily Recond la hapa Scotland toleo la jana (Jumamosi,Oktoba 24,2011)

24 Sept 2011


Huwa ninapenda kuwasilisha habari nyingi za kimataifa katika lugha yetu ya taifa Kiswahili.Unajua,tusipokienzi Kiswahili sie wenye lugha sijui nani atakayejihangaisha nacho.Ukienda Twitter ni kimombo kwenda mbele,japo angalau kwenye Facebook Kiswahili bado kinatawala.

Sasa habari ifuatayo ni ya kisayansi zaidi na kuna vitu havitafsiriki Kiswahili (au kama kuna tafsiri basi ni TUKI na BAKITA pekee wanaoweza kutafsiri kwa usahihi).Hivi unaweza kweli kutafsiri kwa Kiswahili maneno haya: Particle physicist,Neutrinos,Theory of Special Relativity,au bricks" of photographic emulsion films interleaved with lead plates?


Habari husika kwa kimombo ni hii



Faster than light particles found, claim scientists

Particle physicists detect neutrinos travelling faster than light, a feat forbidden by Einstein's theory of special relativity
Subatomic Neutrino Tracks
Neutrinos, like the ones above, have been detected travelling faster than light, say particle physicists. Photograph: Dan Mccoy /Corbis
It is a concept that forms a cornerstone of our understanding of the universe and the concept of time – nothing can travel faster than the speed of light.
But now it seems that researchers working in one of the world's largest physicslaboratories, under a mountain in central Italy, have recorded particles travelling at a speed that is supposedly forbidden by Einstein's theory of special relativity.
Scientists at the Gran Sasso facility will unveil evidence on Friday that raises the troubling possibility of a way to send information back in time, blurring the line between past and present and wreaking havoc with the fundamental principle of cause and effect.
They will announce the result at a special seminar at Cern – the European particle physics laboratory – timed to coincide with the publication of a research paper (pdf) describing the experiment.
Researchers on the Opera (Oscillation Project with Emulsion-tRacking Apparatus) experiment recorded the arrival times of ghostly subatomic particles called neutrinos sent from Cern on a 730km journey through the Earth to the Gran Sasso lab.
The trip would take a beam of light 2.4 milliseconds to complete, but after running the experiment for three years and timing the arrival of 15,000 neutrinos, the scientists discovered that the particles arrived at Gran Sasso sixty billionths of a second earlier, with an error margin of plus or minus 10 billionths of a second.
The measurement amounts to the neutrinos travelling faster than the speed of light by a fraction of 20 parts per million. Since the speed of light is 299,792,458 metres per second, the neutrinos were evidently travelling at 299,798,454 metres per second.
The result is so unlikely that even the research team is being cautious with its interpretation. Physicists said they would be sceptical of the finding until other laboratories confirmed the result.
Antonio Ereditato, coordinator of the Opera collaboration, told the Guardian: "We are very much astonished by this result, but a result is never a discovery until other people confirm it.
"When you get such a result you want to make sure you made no mistakes, that there are no nasty things going on you didn't think of. We spent months and months doing checks and we have not been able to find any errors.
"If there is a problem, it must be a tough, nasty effect, because trivial things we are clever enough to rule out."
The Opera group said it hoped the physics community would scrutinise the result and help uncover any flaws in the measurement, or verify it with their own experiments.
Subir Sarkar, head of particle theory at Oxford University, said: "If this is proved to be true it would be a massive, massive event. It is something nobody was expecting.
"The constancy of the speed of light essentially underpins our understanding of space and time and causality, which is the fact that cause comes before effect."
The key point underlying causality is that the laws of physics as we know them dictate that information cannot be communicated faster than the speed of light in a vacuum, added Sarkar.
"Cause cannot come after effect and that is absolutely fundamental to our construction of the physical universe. If we do not have causality, we are buggered."
The Opera experiment detects neutrinos as they strike 150,000 "bricks" of photographic emulsion films interleaved with lead plates. The detector weighs a total of 1300 tonnes.
Despite the marginal increase on the speed of light observed by Ereditato's team, the result is intriguing because its statistical significance, the measure by which particle physics discoveries stand and fall, is so strong.
Physicists can claim a discovery if the chances of their result being a fluke of statistics are greater than five standard deviations, or less than one in a few million. The Gran Sasso team's result is six standard deviations.
Ereditato said the team would not claim a discovery because the result was so radical. "Whenever you touch something so fundamental, you have to be much more prudent," he said.
Alan Kostelecky, an expert in the possibility of faster-than-light processes at Indiana University, said that while physicists would await confirmation of the result, it was none the less exciting.
"It's such a dramatic result it would be difficult to accept without others replicating it, but there will be enormous interest in this," he told the Guardian.
One theory Kostelecky and his colleagues put forward in 1985 predicted that neutrinos could travel faster than the speed of light by interacting with an unknown field that lurks in the vacuum.
"With this kind of background, it is not necessarily the case that the limiting speed in nature is the speed of light," he said. "It might actually be the speed of neutrinos and light goes more slowly."
Neutrinos are mysterious particles. They have a minuscule mass, no electric charge, and pass through almost any material as though it was not there.
Kostelecky said that if the result was verified – a big if – it might pave the way to a grand theory that marries gravity with quantum mechanics, a puzzle that has defied physicists for nearly a century.
"If this is confirmed, this is the first evidence for a crack in the structure of physics as we know it that could provide a clue to constructing such a unified theory," Kostelecky said.
Heinrich Paes, a physicist at Dortmund University, has developed another theory that could explain the result. The neutrinos may be taking a shortcut through space-time, by travelling from Cern to Gran Sasso through extra dimensions. "That can make it look like a particle has gone faster than the speed of light when it hasn't," he said.
But Susan Cartwright, senior lecturer in particle astrophysics at Sheffield University, said: "Neutrino experimental results are not historically all that reliable, so the words 'don't hold your breath' do spring to mind when you hear very counter-intuitive results like this."
Teams at two experiments known as T2K in Japan and MINOS near Chicago in the US will now attempt to replicate the finding. The MINOS experiment saw hints of neutrinos moving at faster than the speed of light in 2007 but has yet to confirm them.
• This article was amended on 23 September 2011 to clarify the relevance of the speed of light to causality.
CHANZO: The Guardian


Setalaiti 'chakavu' yenye ukubwa unaolingana na basi la abiria inatarajiwa kuanguka duniani kutoka angani muda wowote hivi sasa.Awali setalaiti hiyo ya Shirika la Mambo na Anga la Marekani (NASA) ilitarajiwa kuanguka duniani usiku huu (kwa saa za hapa Uingereza ambazo ni masaa mawili mbele huko nyumbani Tanzania) lakini inaelekea itachelewa kutokana na kasi mwendo wake kupungua.

Inaonekana kuwa vumbi linalotoka kwenye setalaiti hiyo linatarajia kuangukia Amerika ya Kaskazini japokuwa bado uwezekano huo ni mdogo.Setalaiti hiyo 'chakavu' ina uzito wa zaidi ya nusu tani (tani moja ni kilo 1000).Awali NASA walieleza kuwa setalaiti hiyo isingeweza kuangukia Amerika ya Kaskazini lakini taarifa zilizopatikana baadaye zimeonyesha kuwa hadi sasa haifahamiki chombo hicho kitaangukia sehemu gani duniani.

"Kuingia (kwa chombo hicho) duniani kunatarajiwa kutokea Ijumaa ya tarehe 23 Septemba (jana kwa saa za hapa), au mapema Jumamosi tarehe 24,mchana kwa saa za Mashariki ya Marekani (masaa matano mbele kwa saa za hapa au masaa saba mbele kwa saa za huko nyumbani)" ilieleza taarifa ya NASA.

NASA inatarajia vipande 26 vya chombo hicho,vyenye jumla ya kilo 532 vitabaki vimefungamana na kuanguka duniani.Vipande vidogo vidogo vya chombo hicho vinatarajiwa kusambaa kwa umbali wa maili 500 katika uso wa dunia.Kutegemea ukubwa wake,vipande hivyo vinatajiwa kuanguka duniani  kwa kasi ya kati ya maili 55 (kilometa 90) kwa saa  na maili 240 (kilometa 385) kwa saa.

Vituo vya rada sehemu mbalimbali duniani vinafuatilia safari ya chombo hicho lakini kuna uwezekano mdogo wa kutabiri vipande vipande vyake vitaangukia wapi.Matarajio ya wanaanga ni kuona vipande vipande vya chombo hicho vikiangukia baharini (na hivyo kuepusha madhara yoyote kwa wanadamu na mali zao).

Habari njema ni kwamba uwezekano wa vipande vipande vya chombo hicho kukuangukia ni takriban 1 kwa trilioni 20 (1:20,000,000,000,000)

NASA wanashauri mtu yeyote atakayeona vipande kutoka katika chombo hicho kutovigusa bali awasiliane na mamlaka husika (polisi kwa Marekani).Kwa mujibu wa mikataba ya kimataifa inayosimamiwa na Umoja wa Mataifa,kila kipande kitakachoanguka popote pale kinapaswa kurekjeshwa kwa mmiliki wake,yaani NASA.

Sasa kwa wale wanaofanya biashara za chuma chakavu wakiona vipande hivyo na kuvifanya dili watakuwa wanajitafutia kesi za bure na NASA na Wamarekani kwa ujumla.Well,hiyo ni changamsha-baraza,lakini ni matumaini yetu sote kuwa kuanguka kwa setalaiti hiyo hakutakuwa na madhara yeyote kwa wanadamu popote pale walipo.

Habari hii imetafsiriwa kwa ufupi kutoka gazeti la Guardian la hapa Uingereza

23 Sept 2011


Hatimaye mfungwa maarufu kuliko wote nchini Tanzania kwa miaka ya hivi karibuni,Bwana Amatus Liyumba ameachiwa huru leo.Haijafahamika kama amemaliza kifungo,au amepewa msamaha wa Rais au muda wa kipindi cha maigizo umekwisha.

Na kwa vile fisadi huyu ameachiwa,je wewe mlipakodi umenufaika vipi na kifungo chake?Sikuwahi kusikia kuwa fedha alizokwiba zilitaifishwa,ikimaanisha kwamba anaweza kabisa kutumia jeuri ya fedha hizo kwa kufuru ya kukufanya utamani angeendelea kuzeekea jela.

Na kwa vile habari za kifungo chake huko jela zilikuwa za siri,hatuna uhakika kuwa alikuwa mfungwa wa kawaida-kwa maana ya kutopewa huduma za ki-V.I.P au hata kuwa analala nyumbani kisha asubuhi anarejea jela.

Anyway,kwa sasa habari ndio hiyo.

22 Sept 2011


Raia Mwema Ughaibuni
Ya Usalama wa Taifa na teuzi za Rais Kikwete!
Evarist Chahali
USKOCHI
21 Sep 2011
Toleo na 204
“KATIKA kupambana na uhalifu, hakuna njia ambayo - kama inaweza kuleta ufanisi - haitotumika. Kama inazingatia sheria, maadili, na inafanywa kwa nia nzuri, nipo tayari kuifanyia kazi...tumeajiriwa na tunalipwa kupambana na uhalifu, na hicho ndicho nitakachofanya...” .
Nukuu hii inapatikana katika hotuba ya kwanza ya Mkuu mpya wa ‘kanda kuu’ ya kipolisi ya London (Metropolitan Police) Bernard Hogan-Howe.
Hogan-Howe alishinda nafasi hiyo baada ya kuwabwaga makamanda wengine watatu kujaza nafasi iliyoachwa na Sir Paul Stephenson aliyejiuzulu kufuatia kuhusishwa kwake na skandali ya kunasa kwa siri maongezi ya simu (phone hacking) kulikofanywa na baadhi ya magazeti ya Uingereza yanayomilikiwa na tajiri mkubwa kabisa wa vyombo vya habari duniani, Rupert Murdoch.
Mkuu huyo wa Metropolitan Police alitamka bayana kuwa jukumu kuu alilonalo mbele yake ni kupambana na uhalifu na kuwahudumia waathirika wa uhalifu. Na rekodi yake kiutendaji ni ya kuvutia sana.
Akiwa Mkuu wa Polisi wa kanda ya kipolisi ya Merseyside (inayojumuisha jiji lililokuwa likisifika kwa uhalifu la Liverpool), alifanikiwa kuifanya kanda hiyo itoke kwenye nafasi ya 42 kati ya 43 ya ‘ligi ya uhalifu’ hadi kufikia nafasi ya kwanza alipotoka kwenye nafasi hiyo.
Kadhalika alifanikiwa kupunguza uhalifu kwa asilimia 29 na vitendo visivyoendana na maadili ya jamii (anti-social behaviour) kwa asilimia 25 katika kile alichokiita upolisi timilifu (total policing) na vita kamili dhidi ya uhalifu (total war on crime).
Dhamira hiyo ya Hogan-Howe inashabihiana na kauli aliyotoa Mkurugenzi Mkuu wa Usalama wa Taifa, Rashid Othman alipoteuliwa na Rais Jakaya Kikwete kushika nafasi hiyo mwezi Agosti mwaka 2006.
Othman, shushushu mzoefu, alitoa ole kwa majambazi akisema moja ya kazi zake kuu ni kuhakikisha kuwa anaendeleaza mapambano dhidi ya ujambazi na majambazi, kazi ambayo alisema ilikuwa imeasisiwa na Rais Kikwete.
Kadhalika, aliahidi kuwa angehakikisha anaweka utaratibu mzuri wa kukutana na vyombo vya habari ili kuwapa wananchi taarifa za kiusalama ambazo wanastahili kuzipata, na wana haki ya msingi kujua serikali yao inafanya nini katika suala zima la usalama, na hiyo ingeongeza ufanisi wa katika utendaji kazi.
Wakati sina hakika ya mafanikio katika dhamira hizo za Mkuu huyo wa Usalama wa Taifa kupambana na ujambazi ‘wa asili’ (yaani ule wa kuvunja majumba au ofisi, kupora kwa kutumia silaha, nk), yayumkinika kuhitimisha kuwa hajafanikiwa kabisa kupambana na ujambazi dhidi ya mali ya umma au kwa neno maarufu “ufisadi”.
Tangu alipotoa kauli hiyo hadi sasa, tumeshuhudia mlolongo wa matukio ya ujambazi unaofahamika kwa kimombo kama ‘uhalifu wa kola nyeupe’ (white collar crime) ambapo wahusika hawatumii silaha; bali ujuzi na madaraka yao kuliibia taifa.
Sote tunakumbuka kuhusu ujambazi wa EPA, utapeli wa kampuni ya Richmond, dili za ufisadi kwenye makampuni ya Meremeta, TANGOLD, Deep Green Finance, na uhalifu mwingineo ambao umelisababishia taifa hasara ya mabilioni ya shilingi.
Ni ukweli usiopingika kuwa baadhi ya watu wanahoji Idara ya Usalama wa Taifa iko wapi wakati haya yote yanatokea. Kuvuruga mambo kabisa, taasisi hiyo nyeti ilijikuta ikihusishwa na ufisadi wa EPA ambapo mmoja wa maafisa wake waandamizi alitajwa kuwa mnufaika wa wizi huo mkubwa.
Na hapa ndipo inapofika mahala pa kuangalia ahadi za Othman wakati anateuliwa ambapo aliahidi kuandaa utaratibu mzuri wa kukutana na vyombo vya habari ili kuwapa wananchi taarifa za kiusalama.
Kwa kumbukumbu zangu, wakati pekee ambapo Idara hiyo ilizungumza na waandishi wa habari, ni pale Naibu Mkurugenzi Mkuu wake, Jack Zoka alipokanusha madai ya mgombea kiti cha urais kwa tiketi ya CHADEMA, Dkt.Willibrod Slaa, kuwa taasisi hiyo ilikuwa ikiisaidia CCM kwenye kampeni za uchaguzi mkuu wa mwaka jana.
Hadi leo, hakuna maelezo yoyote yaliyotolewa na idara hiyo kuhusu namna ilivyohusishwa na skandali ya fedha za EPA. Ilipaswa aidha wajitenganishe na afisa huyo mwanadamizi na kubainisha kuwa kampuni zilizodaiwa kumilikiwa naye hazikuwa na mahusiano na taasisi hiyo, na kutajwa kwake hakuhusiani kabisa na idara hiyo nyeti.
Kadhalika, haingekuwa vibaya kwa taasisi hiyo kuufahamisha umma ilikuwaje ikashindwa kubaini ufisadi huo, na pengine kuweka bayana mikakati yake ya baadaye ya namna ya kuzuia kurejea kwa matendo ya kihalifu kama hayo.
Naanika haya nikitambua kuwa kazi za taasisi hiyo zinafanywa kwa siri (kwa nia njema kabisa), lakini tatizo linakuja pale mambo yanapokwenda fyongo ambapo ni rahisi kwa wananchi kupata hisia kuwa utendaji kazi huo wa siri unatumika kuficha mapungufu au hata kufunika ushiriki wa taasisi hiyo katika ufisadi.
Si lengo la makala hii kumhoji kiongozi huyo mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa bali, kama nilivyobainisha mwanzoni, kauli yake siku alipoteuliwa inashabihiana na iliyotolewa na mkuu huyu mpya wa Metropolitan Police.
Na kwa vile ni nia ya kila Mtanzania kuona nchi yetu ikielekea kule inakopaswa kwenda, hakuna ubaya katika kukumbushana yale yote yanayoweza kutufikisha tuendako kwa usalama.
Lengo kuu la makala hii ni kuangalia namna teuzi zinavyofanywa na Rais, na pengine watendaji wengine wa serikali pasipo kuangalia iwapo teuzi hizo zitaleta ufanisi.
Wiki iliyopita, Rais Kikwete alitangaza wakuu wa mikoa wapya na waliobadilishiwa vituo vya kazi. Kadhalika, tulifahamishwa majina ya wakuu wa mikoa waliostaafu na ‘waliopumzishwa kwa muda’ (kwa matarajio ya kupangiwa kazi nyingine).
Kabla hata ya kujadili iwapo walioteuliwa walipaswa kupewa nafasi hizo, sijui inaleta picha gani pale Rais anapoamua kumteua mtu ambaye wapiga kura walimkataa katika ngazi ya jimbo. Hapa nazungumzia baadhi ya walioteuliwa kuwa wakuu wa mikoa lakini waliangushwa katika uchaguzi wa wabunge katika majimbo yao.
Tuwe wakweli: Hivi kama idadi ndogo tu ya wananchi katika jimbo imekosa imani na mgombea, na hivyo kutompa kura za kutosha za kumfanya awe mbunge, inawezekanaje kwa mtu huyo kukabidhiwa ‘urais wa mkoa’? Ndio, ukuu wa mkoa ni kama urais wa mkoa; kwani anayepewa dhamana hiyo ni mwakilishi wa Rais katika mkoa husika.
Sijui lengo ni kuwakebehi wapigakura waliomnyima ubunge kiongozi wa aina hiyo au ndio hadithi zile zile za kuteuana ‘kishkaji’ (kirafiki) lakini sidhani kama kuna maelezo stahili ya kuelezea teuzi za aina hii; hasa ikizingatiwa kuwa nchi yetu haina uhaba wa wazalendo wenye uwezo wa kushika nyadhifa.
Katika baadhi ya teuzi hizo zilizofanywa na Kikwete baada ya ya takriban mwaka mzima wa ‘upembuzi yakinifu’ zina walakini uliozoeleka wa watendaji ambao rekodi zao zina walakini. Hili halihitaji kutajwa majina; kwani mikoa iliyoboronga kimaendeleo inafahamika.
Kuwazawadia waharibifu wa maendeleo nafasi za ‘kujaribu tena mkoa mwingine’, ni sawa kabisa na kutothamini maslahi ya wananchi katika maeneo husika.
Lakini pia katika walioteuliwa kuna mbunge ambaye anaungana na baadhi ya wabunge wenye kofia zaidi ya moja -kwa maana ya kuwa mbunge na mkuu wa mikoa. Kitendo hiki ni kuwanyima kwa makusudi wananchi nafasi ya kuwa na kiongozi atakayeelekeza nguvu zake kwa jukumu moja.
Katika mazingira yakawaida, mbunge ana majukumu ya kuwatumikia wapiga kura wake. Kumpa jukumu jingine la kuongoza mkoa ni kumbembesha mzigo mzito wa ziada pasipo kujali matokeo yatakuwaje.
Kukosoa na kumlaumu pasipo kutoa ushauri si jambo jema. Nimalizie makala hii kwa kushauri kuangalia madaraka ya Rais katika kufanya teuzi mbalimbali, na kwa vile tupo kwenye mchakato wa marekebisho ya Katiba, basi, ni muhimu pia kuangalia  uwezekano wa ulazima wa teuzi zinazofanywa na Rais kuidhinishwa na Bunge.
Rais kama binadamu anaweza kufanya teuzi zisizo na maslahi kwa taifa. Bunge likifanya kazi yake zaidi ya kuwa ‘mhuri wa kuidhinisha kila kinacholetwa na serikali’, linaweza kabisa kuepusha teuzi fyongo au zile zinazozidi kudidimiza nchi yetu kwenye lindi la umasikini unaochochewa na ufisadi.


21 Sept 2011

Kama kuna hoja inayotawala zaidi kuliko nyingine kwenye blogu na maandiko mengi ya wengi wa mabloga wa kike wa Kitanzania ni hii ya hisia kwamba WANAUME WA KITANZANIA SI WAAMINIFU KWENYE MAHUSIANO.Ninaposema inatawala simaanishi kuwa huo ndio mtizamo wa mabloga hao bali ni kitu kinachojitokeza mara nyingi pengne zaidi ya vitu vingine,hususan kwenye sehemu za kutolea maoni (comments).

Utakuta dada mmoja anaomba ushauri kwa wenzie kuhusu mwenza wake ambaye aidha anamhisi kuwa si mwaminifu au amemsaliti kwenye uhusiano wao.Ukiweka kando ushauri atakaopewa,wengi wa wachangiaji wa kike hukimbilia kuhitimisha kuwa tatizo la msingi ni "ukweli kwamba wanaume wa Kibongo si waaminifu",huku wengine wakienda mbali zaidi na kudai "wanaume wetu wa Kibongo wanatembea wakiwa na zipu zao wazi-kwa maana ya kuwa tayari kukamata chochote kile kitakachokatiza mbele yao".

Katika hatua hii siwezi kusema hisia hizo ni sahihi au la ila nisichokubaliana na hitimisho la jumla (blanket conclusion) kwamba WANAUME WOTE WA KITANZANIA SI WAAMINIFU.Sijui kama wanaohitimisha hivi huwa wanajaribu angalau kutafakari kidogo kuhusu baba zao,maana nao pia ni wanaume wa Kitanzania.Hatari kubwa ya kuhitimisha jambo jumla jumla ni kuwaingiza hata wale wasiohusika.Wengi wetu tunafahamu jinsi baba zetu walivyo waadilifu kwa mama zetu hadi kufanikiwa kutufikisha hapa tulipo.Japo si wote lakini kwa kiasi kikubwa baba zetu-hususan wale waliokula chumvi nyingi-wamejitahidi kadri wawezavyo kuwa waaminifu kwa mama zetu.

Kwa vile mada hii ni ndefu na ili kuijadili kwa ukamilifu inahitaji kitabu kizima basi niifupishe kwa,kwanza,kuangalia sababu za kitaaluma kwanini watu wana-cheat.Naomba ieleweke kuwa hata kwenye kusaka sababu kwenye masuala mengine ni nadra kupata sababu timilifu kabisa kwa sababu kuna vigezo vingine vinavyoathiri kila sababu,kwa mfano mazingira,umri,uchumi,malezi,nk

Hata hivyo,tafiti mbalimbali za mahusiano ya kimapenzi zinataja sababu zifuatazo kuwa 'maarufu' zaidi katika kuelezea kwanini watu wana-cheat

KULIPIZA KISASI:

Sie Wakristo tunafundishwa kwenye Agano Jipya kuwa ukipigwa kofi shavu la kushoto basi geuza na shavu la kulia.Hii inapigia mstari umuhimu wa kutolipiza kisasi.Lakini hata kwenye Maandiko hayo Matakatifu haikuwa hivyo siku zote.Katika Agano la Kale,mafundisho yalikuwa ni JICHO KWA JICHO na JINO KWA JINO.Kwenye stadi za dini inafahamika kama 'sheria ya kulipiza kisasi' (law of retaliation) na 'sheria ya mapatano' (law of reconciliation).Katika poetic justice 'jino kwa jino' inaweza kulinganishwa na kile kiitwacho adhabu ya kioo (mirror punishment),yaani-kwa kifupi-malipizi kwa kutenda kosa.Msingi hapa ni kwamba tendo jema huzawadiwa na tendo baya huadhibiwa.

Kwa hiyo,kwa vile mwenza wa kiume au wa kike ame-cheat basi yule aliyekuwa cheated anaamua kulipiza kisasi kwa ku-cheat pia.Jino kwa jino,au tit-for-tat.Lakini hitimisho la kisomi ni kwamba mara nyingi kulipiza kisasi hakusaidii sio tu kuleta ufumbuzi wa tatizo bali pia hata kuondoa maumivu ya kusalitiwa kwenye penzi.

Unajua kuna tofauti kati ya kufanya jambo pasipo msukumo wowote na kufanya jambo kwa vile kuna msukumo flani.Mwanaume au mwanamke anayeamua tu ku-cheat kwa vile anajiskia kufanya hivyo ana tofauti na yule aliyelazimika ku-cheat kwa sababu tu anataka kumkomoa flani.Tofauti hii ni sawa na ile ya binti anayefanya ukahaba kama hobby na yule anayefanya kwa vile anahitaji fedha au hana njia nyingine ya kipato zaidi ya kuuza mwili/utu wake.Kufanya jambo kwa uhuru ni,well,kuwa huru (hata kama ni makosa) wakati kufanya jambo kutokana na kusukumwa ni sawa na utumwa.

Anyway,hapa tunataja sababu za ku-cheat na sio kuhukumu kuwa anaye-cheat kwa sababu flani yuko sahihi au la.Twende sababu ya pili

KAMA KIPO KITUMIE

Kuna wenzetu wanaoamini kwamba kama nyama iliyopo kwingineko ni ya kupendeza,tamu,isiyo na sumu,na inapatikana,then kwanini isiliwe?Watu wa aina hii wanaamini kuwa wanachofanya ni kula kilicho bora,na ambacho kinapatikanika (available/accessible).Hawana uchungu kwa kufanya hivyo kwa vile wanaamini kuwa maridhio ya nafsi ni muhimu zaidi kuliko uhalali au ukosefu wa uhalali wa tendo husika.

Nadhani ushaskia misemo kama 'cha muhimu ni kupata fedha,jinsi ilivyopatikana sio muhimu'.Au wengine wanakwenda mbali zaidi na kudai kuwa watu wenye kuifaidi zaidi dunia ni wale waisoongozwa na 'hiki ni halali na hiki si halali'.Ishu kama uadilifu,uaminifu,nk sio muhimu kwao.

Katika kundi hili kuna wale tunaoweza kuwaita waathirika wa Columbus Syndrome (tafsiri ya Kiswahili ni ngumu lakini turahishishe kwa kuita 'ugonjwa wa kiu ya uvumbuzi kama Christopher Columbus.Yaani tamaa ya kujua mambo zaidi ya maelezo sahihi yanavyoelezea mambo hayo).Unakuta mwanaume 'anafukuzia sketi' kwa vile tu anataka kuonja sehemu za siri za mwanamke huyo.Haijalishi kama ana mwenza au hana,bali la muhimu kwake ni kwamba A sio B,na nyama ya mbuzi si ya ng'ombe,na japo maharage na kunde zote ni mboga lakini maharage si kunde.Hawa wapo katika kile kinachoitwa kwa kimombo kama taste-testing (kujaribu ladha).

Kwenye kundi hili pia kuna wale wanaotaka kupima kama ujuzi wao wa kufukuzia sketi bado upo,licha ya ukweli tayari wana wenza nyumbani.Kwa akina dada,inawezekana ni kupima kama "kama nilimudu kum-cheat yule bwege mwaka juzi na hakujua mpaka tunaachana kwanini nisijaribu tena safari hii?"Ni sababu zinazoweza kuonekana kama za kupuuzi lakini kumbuka kuwa mara nyingi wanaofanya upuuzi hawana muda wa kutafuta sababu.Na hata ukiwahoji wakupe sababu basi majibu watakayokupa yanaweza kukutibua kuliko upuuzi waliofanya.

Kufupisha maelezo,wanao-cheat kwa mujibu wa sababu hii wanafanya hivyo kwa vile,well,kama kipo kitumie.

WASIOTOSHEKA

Unakumbuka ule wimbo wa zamani wenye maneno "ee jamani mwanadamu hatosheki,hata ukimpa nini milele hataridhika...ukimpa kumi atataka mia..."Well,si kweli kwamba kila mwanadamu hatosheki bali ukweli ni kwamba kama ilivyo kuna wenzetu ni wepesi kutosheka,wenzetu wengine kamwe hawatosheki.Tuchukulie mifano halisi.Katika kusaka ufumbuzi watatizo la rushwa katika Mamlaka ya Mapato Tanzania ikashauriwa mishahara minono na marupurupu mazuri inaweza kusaidia kuondoa vishwawisho vya watumishi wa taasisi hiyo kudai na kupokea rushwa.Seriakli ikaridhia kufanya marekebisho katika muundo wa mishahara ya watumishi wa taasisi hiyo.Sihitaji kukwambia kuwa TRA ni miongoni mwa taasisi zilizobobea kwa rushwa,pengine mara dufu ya ilivyoluwa zama za mishahara kiduchu.

Kwanini watu hawa waendelee kudai na kupokea rushwa ilhali wanalipwa mishahara minono kabisa?Well,jibu rahisi ni tamaa.Lakini jibu jingine linaweza kuwa mazowea.Kuna msemo wa Kiingereza usemao "vyovyote utakavyomtunza,mbwa mwitu hawezi kuwa mbwa".Nenda porini,kamata mbwa mwitu,mpe kila aina ya matunzo kama mbwa wa kawaida,lakini kama hatoishi kukung'ata basi atatoroka na kurejea porini.Wanasema kunguru hafugiki,na samaki yake maji.Ukimtoa samaki majini,basi umemuua.Period.

Kwahiyo kama ambavyo kuna watu hawatosheki na fedha wanazopata (kwa mfano mafisadi serikalini ambao wanalipwa mishahara mikubwa kuliko mahitaji yao) basi pia kuna watu hawatosheki na tendo la ndoa.Hata mkewe/mwenza wake ampe uroda kiasi gani bado atahitaji nyongeza.Na kuna akinadada hata apewe-ashakum si matusi- 'mabao' mangapi bado atahitaji zaidi.

Katika sababu hii kuna marejeo ya sababu iliyopita ya 'kama kipo tumia' kwa maana ya kama una njaa na chakula kipo basi kula,na kama ukienda kwingine na bado unajiskia hamu ya kula endelea kula.Ma-Tiger Woods hawa wa kike na kiume wanahitaji zaidi na zaidi just like wale wala rushwa wa TRA.

Kwa wengine hili ni kama tatizo la kiafya linalohitaji tiba za kisayansi.Kabla ya tiba hiyo,dawa pekee ya kukabiliana na 'hamu isyoisha ya kula au kuliwa uroda' ni 'kula au kuliwa uroda' zaidi na zaidi.Ni mithili ya walevi ambao njia pekee ya kumudu maisha ni pombe.

Kwa bahati mbaya,watu wa kundi hili wanaweza kujikuta matatizoni zaidi ya kuharibu mahusiano na wenza wao.Yaleyale ya simba akikosa nyama anaweza kula majani,basi si ajabu kwa watu wa kundi hili kujikuta wakiamua liwalo na liwe na kudiriki hata kufanya tendo la ndoa na watoto wadogo,watu wa jinsia moja na wao,kubaka aua hata kufanya tendo la ndoa na midoli.Kwao,tendo la ndoa ni sawa na oksijeni,pasipo hiyo ni kama wanaelekea kukata roho.

Namkumbuka kijana mmoja enzi hizo za ujana,mitaa ya Kinondoni.Kila wikiendi alikuwa anakwenda Ambassador Plaza (Gogo Hotel) 'kukamatia',na kwa vile sehemu hiyo ilikuwa inapendelewa na mashoga basi alipokuwa akikosa binti wa kulala naye basi 'anakamatia' shoga.Na huyu kijana alikuwa na girlfriend mrembo kupita maelezo.

Na kuna mama mmoja niliyewahi kufanya nae kazi sehemu fulani ambayo mshahara,posho na fedha kwa ujumla ilikuwa sio tatizo.Lakini licha ya kuwa na mume mwenye uwezo wa kifedha na mwenye haiba ya kutamanisha mwanamke yeyote yule,mama huyo alikuwa yuko radhi kulala hata na wafagizi hapo ofisini,baada ya kuwamaliza mabosi wenzie na wafanyakazi wa kada ya kati.Wambeya walikuwa wanadai kuwa mama huyo 'alipokuwa kwenye siku zake' alilazimika kufanya tendo la ndoa kinyume cha maumbile alimradi akidhi addiction yake.

KITULIZA ROHO

Wakati mwingine mwenza hujikuta anashawishika ku-cheat kutokana na mapungufu yanayozidi kuathiri mahusiano yake na mwenzie.Naomba tuelewane hapa.Sio kama nahalalisha ku-cheat bali natoa moja ya sababu zinazoweza kumfanya mtu a-cheat.Ikumbukwe kuwa wizi ni wizi tu,hakuna wizi halali.Mtu anayekutwa na hai ya kuua,kwa mujibu wa sheria zetu,adhabu yake ni kunyongwa hadi afe.Hakuna tofauti kati ya aliyeua mtu mmoja na aliyeuwa watu 10,wote ni wauaji.

Kadhalika,anaye-cheat kwa vile mumewe/mkewe hamridhishi,hana tofauti na yule wa kundi la kwanza au la pili au la tatu hapo juu.Wote wame-cheat,na kama kuna adhabu dhidi ya ku-cheat,wote wataadhibiwa kama cheaters,period!

Inaelezwa kuwa baadhi ya wanawake wanapoolewa wanaweza kujikuta wanajisahau kuhusu vitu vilivyofanya waume zao watamani kuwaoa in the first place.Matokeo yake ndoa inakuwa dull,tendo landoa linakuwa kama kutimiza wajibu tu kama sio kutokuwepo kabisa.Nasisitiza kuwa ku-cheat sio ufumbuzi lakini kwa mhusika hiyo ni excuse tosha ya kwenda nje ya uhusiano.

Wanaume pia,iwe kwenye ndoa au mahusiano tu kati ya boyfriend na girlfriend,wanadaiwa kuwa wakati mwingine wakishapata wanachohitaji wanawachulia wenza wao for granted.Zawadi za 'enzi za kutongozana'-maua,perfume,kadi,sim/sms mfululizo,nkzinaanza kufifia kadri umri wa uhusiano unavyozidi kuongezeka.

Again,naomba kusisitiza kuwa hii sio kwenye kila uhusiano bali hutokea,wewe na mimi tumeshaskia simulizi za aina hii mara kadhaa.

Mwenza anajikuta yupo kwenye uhusiano ambao ni 'uhusiano jina',hakuna mahaba,hakuna msisimko,na pengine kibaya zaidi,hakuna tendo la ndoa,au hata kama likiwepo ni la 'kizushi' tu.Kuna wanaoanza kwa kutishia ku-cheat-si kwa maneno bali vitendo.Kwa mfano,binti ambaye baada ya kuwa na mwenza wake alianza kubadilisha uvaaji wake 'wa utatanishi' (kwa lengo la kuepusha wasumbufu mtaani) anaamua kurejea kwenye uvaaji huo ili kumpelekea ujumbe mwenza wake kuwa 'kama ulinitamani uliponiona katika mavazi haya siku hizo,basi hata sasa naweza kutamaniwa na wengine'.Kwa bahati mbaya,'tisha toto' hii inaweza kupelekea madhara yasiyokusudiwa.Kwamba akajitokeza mdau akaonyesha interest ya kutosha na hatimaye mwanadada akashawishika kutembea naye 'mara moja tu' (na hatimaye mara moja hiyo kuzaa mara ya pili na kadhalika na kadhalika).

Kuna wengine hawana hata muda huo wa kufikisha ujumbe na huamua kuingia kwenye hatua ya ku-cheat moja kwa moja.Hoja ya msingi kwao ni kwamba kama huwezi kunipa ninachohitaji basi kuna wengine w3anaweza kunipa.Na kwa vile mie na wewe sio dada na kaka basi sioni umuhimu wa kuishi na mwanaume au mwanamke ambaye hanitimizii mahitaji yangu ya kimahusiano.

Kama nilivyaondika awali,ningependa sana kuingia kwa undani na kujadili njia mwafaka za kusaka suluhisho kwa kila sababu ya ku-cheat niliyotaja hapa lakini kwa leo naomba niishie kwenye kutaja sababu tu,kabla ya kuhamia kwenye mada ya msingi ambayo ni hoja ya wanawake wengi kuwa Wanaume wa Kitanzania si waaminifu.

UCHAMBUZI

Kwa kifupi kabisa,naomba nikuachie msomaji uondoe MWANAUME WA KITANZANIA kwenye kila sababu niliotaja hapo juu na uweke MWANAUME WA KIKENYA,KIMAREKANI,KIINGEREZA au MWANAUME WA NCHI YOYOTE ILE.Kisha angalia kama kuna mwanaume wa uraia flani hawezi ku-fit kwenye sababu hizo hapo juu.

Kisha jaribu tena kuondoa MWANAUME (awe wa KITANZANIA au wa nchi nyingine) na uweke MWANAMKE WA KITANZANIA.Je hakuna mwanamke wa Kitanzania anayeweza ku-cheat kwa sababu tu ANALIPIZA KISASI (at least according to her)?Je hakuna mwanamke wa Kitanzania anayeweza ku-cheat kwa sababu tu anaamini KAMA KIPO KITUMIE?Au je hakuna mwanamke wa Kitanzania anayeweza ku-cheat kwa vile tu HATOSHEKI na anachopewa na mwenza wake?Na mwisho,je hakuna wanawake wa Kitanzania wanaoweza ku-cheat kwa minajili ya KUTULIZA ROHO kutokana na mapungufu yanayokabili mahusiano na wenza wao?

HITIMISHO:

Kwa kuangalia sababu hizo za kitaaluma as to kwanini wenza wanaweza ku-cheat,ni wazi kuwa,kwanza si mwanaume tu anayeweza kuwa na sababu (hata kama haikubaliki) ya ku-cheat.Na pili,si wanaume wa Kitanzania tu wanaoweza ku-apply sababu hizo wanapo-cheat,au kwa lugha nyingine,si wanaume wa Kitanzania tu wanao-fit explanations/sababu nilizobainisha hapo juu kuhusu kwanini watu wana-cheat.

Kwahiyo basi,natumaini makala hii inaweza kutoa jibu kwa niaba ya Wanaume wote wa Kitanzania wanaotuhumiwa kuwa si waaminifu katika mahusiano.Jibu ni kwamba si wanaume wa Kitanzania pekee,na si wanaume pekee,wanaoweza kuwa nasababu moja au nyingine ya ku-cheat.Makala hii haijaribu kwa namna yoyote kuhalalisha cheating kwa vile kama nilivyobainisha hapo mwanzo,ku-cheat si ufumbuzi wa tatizo lililopelekea mtu a-cheat.Faraja ya muda mfupi-iwe ni kulipa kisasi,kukidhi utafutaji ladha mbadala nje,kutibu kiu ya ngono au kujiliwaza-haiwezi kuwa ufumbuzi wa kukarabati uhusiano unaokwenda mrama.

Siku ya siku nitajadili njia mwafaka za kuboresha uhusiano na kuondoa fursa ya ku-cheat.

Inatosha kwa leo

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.