Showing posts with label KENYA. Show all posts
Showing posts with label KENYA. Show all posts

3 Apr 2015

Takriban watu 150 wameuawa katika shambulizi lililofanywa na kikundi cha kigaidi cha Al-Shabaab, katika eneo la Garisa, nchini Kenya. Katika tukio hilo la kinyama lililotokea saa 11 asubuhi kwenye Chuo Kikuu cha Garisa, magaidi hao waliwapiga risasi na kuwachinja wanafunzi Wakristo.baada ya kuwazidi nguvu walinzi.
Masked gunmen stormed the Garissa University College campus, in Kenya's north-east, yesterday
Kwa mujibu wa gazeti la Daily Mail la hapa Uingereza, idadi ya waliouawa inafikia 147 na majeruhi ni 79 huku watu 500 wakiokolewa. Wengi wa waliouawa na wanafunzi wa chuo hicho, pamoja na polisi wawili,mwanajeshi mmoja na walinzi wawili.



Kenyan soldiers and police officers pictured at Garissa University College in Kenya where 147 people were murdered by terrorists yesterday

Waziri wa Mambo ya Ndani wa Kenya, Joseph Nkaissery , alieleza kuwa magaidi wanne walijifunga mabomu, na polisi walipowapiga risasi, walilipuka kama mabomu ambapo vipande vya mabomu hayo viliwahjeruhi polisi.
Kenyan police officers, pictured, take cover across from the university during the terrorist gun attack

Maafisa wa usalama katika eneo la tukio walieleza kwamba mateka kadhaa waliokolewa, na magaidi wanne waliokuwa na bunduki aina ya AK-47 waliuawa.
Kenyan security officials at the scene said dozens of hostages were freed and four of the gunmen were killed
Jana usiku, Kituo cha Operesheni ya Uokoaji Kitaifa kilieleza kwamba idadi ya wanafunzi wote, wazima na waliouawa sasa inafahamika.
Students fled the area, some of them without shoes, after the al-Shabaab terrorists launched their attack

Just last week, the Chief Security Officer at the University of Nairobi feared an attack was imminent and issued a security warning - but it is unclear whether the same information was relayed to Garissa officials 

Students ran for their lives as the terrorists launched their attack on the college campus in Kenya yesterday

Escape: Students pictured fleeing from the university. The death toll rose to 147 as the siege ended last night

Some of the students did not have time to dress as they fled for their lives when faced by the gunmen

Distraught: Paramedics help a woman injured during the attack on the Garissa University College campus

Shambulizi hilo linaelezwa kuwa baya zaidi nchini humo katika miaka 17 baada ya shambulizi jingine kubwa la kigaidi  mwaka 1998 kwenye Ubalozi wa Marekani nchini humo ambalo lilipelekea vifo zaidi ya 200.
Heavily armed soldiers pictured outside the Garissa University College campus where 147 people were murdered

Safety: A student hostage is escorted out of Garissa University College after Kenya Defence Forces ended a siege by terrorist gunmen

A Kenyan soldier runs for cover near Garissa University College's perimeter wall where 147 people have been killed

Rescued: A woman is led to safety from the building where she was held hostage by al-Shabaab terrorists





An injured man on a stretcher is taken to Kenyatta National Hospital following the attack by al-Shabaab terrorists

Medical treatment: An injured man arrived at Kenyatta National Hospital in Kenya's capital, Nairobi following the raid by terrorists



Tukio hilo la jana limetokea katika Juma Kuu, kipindi cha majonzi katika kalenda ya Wakristo. Jana ilikuwa Alhamisi Kuu ambayo kwa mujibu wa taratibu za baadhi ya madhehebu ya Kikristo, ni siku ya maungamo. Leo, Ijumaa Kuu, ni siku ya maadhimisho ya kusulubiwa kwa Yesu Kristo msalabani na hatimaye kufa. Jumapili ijayo ni Pasaka ambapo Wakaristo wanaadhimisha ufufuo wa Yesu Kristo.
A Kenya Defence Forces soldier carries a machine gun outside Garissa University College on April 2 2015

Captured: The Kenyan military launched a major security operation and detained one terrorist trying to escape

A Kenya Defence Forces tank driven outside Garissa University College. Al-Shabaab terrorists raided the campus shortly after 5am local time yesterday, overwhelming guards and killing anyone they suspected of being a Christian

Kenyan police managed to arrest one of the terror suspects, right, after he tried to flee from the campus

The death toll rose to 147 tonight and the siege ended, according to the country's disaster response agency. A total of 79 were injured, 587 were led to safety


Most of those killed were students but two police officers, one soldier and two watchmen are among the dead

Tragedy: Last night, officials confirmed the security operation is now over but the death toll has reached 147

Gunfire: A Kenya Defense Force soldier takes cover near the perimeter wall of Garissa University College

Kenyan soldiers took cover as heavy gunfire continued at Garissa University College in Kenya yesterday

Kenyan security officials at the scene said dozens of hostages were freed and four of the gunmen were killed

A Kenyan soldier takes cover as shots are fired in front of Garissa University College in Garissa town, located near the border with Somalia

Maafisa usalama wa Kenya walieleza kuwa gaidi mmoja alikamatwa wakati anajaribu kutoroka. Kadhalika, serikali ya nchi hiyo imetangaza zawadi ya Shilingi za Kenya Milioni  20 kwa atakayewezesha kukamatwa kwa Mohammed Mohamud, anayejulikana pia kama Dulyadin, au Gamadhere, ambaye anatuhumiwa kupanga shambulizi hilo.

A £145,000 reward has been offered for information leading to the capture of Mohamed Mohamud, who is believed to have masterminded the attack

Wanausalama nchini humo wanaamini kuwa gaidi huyo ni mkuu wa operesheni za kigaidi wa kundi la Al-Shaabab.Inaaminika kuwa gaidi huyo ametumia muda mwingi kuwafunza magaidi watarajiwa kwenye madrasa mbalimbali.Pia anatuhumiwa kuhususika na shambulizi jingine la kigaidi lililotokea Novemba 22 mwaka jana huko Mkka, nchini humo, ambapo watu 28 waliuawa.
A Kenyan soldier takes cover as shots are fired in front of Garissa University College in Garissa town, located near the border with Somalia
Mkuu wa Polisi, Joseph Boinet, alitangaza amri ya kutotembea ovyo kuanzia saa 12 unusu jioni hadi saa 12 unusu asubuhi.katika mikoa minne inayopakana na Somalia kama tahadhari ya kiusalama.

Chuo kilichokumbwa na shambulizi hilo kina takriban wanafunzi 887 wanaoishi katika mabweni sita



Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo, Collin Wetangula, Makamu Mwenyekiti wa Serikali ya Wanafunzi chuni hapo, alieleza kuwa yeye na wenzake waliposikia milio ya bunduki walijificha kwa kujifungia chumbani.

"Nilisikia milio ya bunduki, lakini hakuna mtu aliyepiga kelele, kwa hofu ya kuwashtua wanaofanya shambulio hilo."

"Watu hao waliokuwa wakifyatua risasi walikuwa wanasema 'sisi ni Al-Shabaab'"

Wetangula alieleza zaidi alisikia magaidi hao wakihoji wanachuo kuhusu dini zao (kama ni Waislam au Wakristo). Alisema, "Ukiwaambia wewe ni Mkristo, walikupiga risasi hapohapo. Kila mlio wa bunduki ulinifanya nijisikie kama nakufa."

"Baadaye tulipochungulia dirishani tuliwaona watu wenye sare za jeshi ambao baadaye walijitambulisha kuwa ni maafisa wa jeshi la Kenya."
Kenyan authorities have airlifted some of the wounded to Nairobi for treatment following the attack yesterday morning

Msemaji wa magaidi wa Al-Shbaab alitangaza kuwa kundi lake linahusika na shambulizi hilo. Sheikh Abdiasis Abu Musab, 'msemaji wa operesheni za kijeshi za Al-Shabaab,' alisema, "Tuliwachambua watu, na kuwaachia huru Waislam.Kuna miili mingi ya Wakristo, na tunawashikilia wengine kadhaa."

Rais Uhuru Kenyatta alieleza baadaye kuwa anaharakisha ajira ya askari 10000 ili kukabiliana na tishio la magaidi hao.
Treatment: Paramedics attend to an injured Kenyan student as she is wheeled into Kenyatta National Hospital in Nairobi
Wiki iliyopita, Afisa Mkuu wa Usalama katika Chuo Kikuu cha Nairobi alitoa tahadhari ya uwezekano wa shambulio la kigaidi lakini bado haijafahamika kuwa iwapo taarifa hizo zilitolewa kwa Chuo Kikuu cha Garisa pia.

Wounded: A man with a leg injury arrived at hospital in Kenya's capital. The death toll has risen to 147

Grace Kai, mwanafunzi wa Chuo cha Ualimu cha Garisa, alieleza kuwa walipewa tahadhari kuwa kuna uwezekano wa kutokea shambulio la kigaidi. Alisema, "Sura ngeni zilionekana Garisa, na kulikuwa na hisia ni magaidi."

"Jumatatu, Mkuu wa Chuo alitupa tahadhari...kwamba kuna sura ngeni zimeonekana maeneo ya chuoni hapo."
Kenyan officials had warned that al-Shabaab were suspected of planning a major assault on the college 
"Kisha Jumanne, tuliruhusiwa kurejea majumbani, na chuo kufungwa., lakini kampasi iliendelea kuwa wazi...na sasa wameshambulia."

CHANZO: The Mail Online


6 Oct 2013

Taasisi za usalama nchini Kenya zitaendelea kusuasua kuepusha umwagaji damu kama uliotokea mwezi uliopita kwenye shambulizi kwenye eneo la  maduka ya Westgate, iwapo watendaji wa kada za chini wa vyombo hivyo wataendelea kuwa wanahongeka kirahisi na endapo uhasama baina ya vyombo hivyo utaendelea kuathiri ushirikiano wa kupashana habari za kiusalama.

Shambulio la kigaidi  lililofanywa Septemba 21 mwaka huu na kupelekea zaidi ya vifo 67, na kudumu kwa siku kadhaa, limeishtua nchi hiyo inayojivunia wanausalama wenye uzoefu mkubwa katika kupambana na ugaidi.

Lakini wakati uchunguzi unaendelea katika eneo la tukio ili kuwatambua wahusika na mbinu walizotumia, changamoto mbalimbali kwa taifa hilo lililo mshirika muhimu wa nchi za Magharibi katika kupambana na magaidi wa Kiislam zinaanza kujitokeza.

Maafisa Usalama wa zamani na wa sasa, wanadiplomasia na wataalam wanaelezea vyombo vya usalama vinavyotumia isivyo ujuzi uliopatikana kwa msaada wa Marekani na Uingereza na wakufunzi wengine kwa vile watuhumiwa wanaweza kuhonga na kuepuka kukaguliwa na polisi, huku ushirikiano duni kati ya vymbo vya usalama ukimaanisha ni vigumu kukamilisha taarifa za kiusalama.

Pia wanaharakati wanasema kuwa vyombo vya dola vimeingizwa mno kwenye siasa za ndani ya nchi hiyo badala ya kuweka mkazo kwenye majukumu yao ya kiusalama.

Hakuna anayetarajia kuwa Kenya itaweza kuzwia kila shambulio la kigaidi, na kwa hakika wanadiplomasia wa nchi za Magharibi wanazipongeza taasisi za usalama za nchi hiyo kwa kufanikiwa kuzuwia mashambulizi kadhaa kabla ya hilo la Westgate.

Lakini, kikundi cha kigaidi cha Al-Shabaab,ambacho kimekiri kuhusika na shambulio hilo,  kimedhirisha kuwa Somalia itaendelea kuwa kiota cha kuanzishia mashambulizi ya kigaidi kama hayo.Kenya kama jirani wa Somalia haiwezi kumudu kupuuza mapengo yanayosababishwa na mapungufu ya kitaasisi na utumishi.

"Hata kama utawekeza nguvu kiasi gani katika taasisi za usalama, ruhswa bado itaathiri malengo yako," anasema Meja Jenerali Mstaafu Charles Mwanzia, ambaye alikuwa mkuu wa idara ya usalama jeshini hadi mwaka 2005.

"Ni fundisho chungu na wito wa kuamka ili kuboresha usalama wa nchi hii katika maeneo ya kukusanya na usimamizi wa taarifa za usalama" anasema Jenerali huyo kuhusiana na shambuliz la Westgate.

Dalili za uhasama miongoni mwa vyombo vya dola vya nchi hiyo zilionekana wakati wa mapambano kati ya wanasualama na magaidi katika eneo hilo la maduka jijini Nairobi.

Afisa upelelezi mmoja, ambaye kama wengine, aliongea  na Shirika la Habari la Reuters kwa masharti ya kutotajwa jina, alieleza jinsi kikosi maalum cha jeshi na polisi (General Service Unit) kilichokuwa cha kwanza kufika eneo la tukio kilivyosukumwa kando baada ya askari wa Jeshi la Ulinzi (KDF) kuwasili.

MAADUI DHIDI YA URAFIKI

Kutokuwepo ushirikiano wakati wanajeshi hao wa KDF wanaingilia kati mapambano hayo kulitoa fursa kwa magaidi kujipanga upya, na pengine hiyo ilichangia kurefusha harakati za kuwadhibiti magaidi hao (zilzodumu kwa angalau siku 4). "Maafisa wa ngazi za juu wa GSU na KDF hawakuwa na ushirikiano wa kutoa mwongozo," anaeleza afisa upelelezi huyo.

Serikali ya Kenya ilidai kuwa operesheni ya kukabiliana na magaidi hao iliendeshwa kwa ushirikiano wa vymbo mbalimbali vya dola vikifanya kazi kwa ushirikiano. KDF imejitetea kuwa jeshi la polisi ndilo lililoongoza operesheni hiyo.KDF pia imesema itachunguza tuhuma kuwa baadhi ya askari wake walishiriki kupora mali katika maduka mbalimbali ya Westgate wakati wa operesheni hiyo.

Pamoja na kukoselewa huko, wataalam wa usalama na wanadiplomasia wa nchi za Magharibi walieleza kuwa chombo chochote cha usalama kingekuwa na wakati mgumu kupambana na magaidi hao wenye mafunzo na uwezo wa hali ya juu, katika eneo kubwa kama maduka ya Westgate.

Hata hivyo, wanaona mapungufu katika hatua za kujiandaa na operesheni hiyo dhidi ya magaidi. Wanasema kuwa taasisi za usalama za Kenya hufanya kazi kama maadui baina yao badala ya kushirikiana, hukataa kujumuisha taarifa za kiusalama pamoja, kiasi kwamba tetesi za matishio ya kiusalama zinaweza kutoonekana na pia dondoo zinazopatikana kwenye ufuatiliaji wa washukiwa (surveillance) zinakuwa vigumu kuunda picha ya kuwezesha kfanya maamuzi stahili.

"Ni wazuri katika wanachofanya, hususan katika ukusanyaji wa taarifa za kiusalama...lakini hawajui nini cha kufanya na wanachokipata, na jinsi ya kutengeneza picha kubwa (putting together the big picture)," alisema mtaalam mmoja wa usalama ambaye amefanya kazi na majeshi na idara za usalama za Afrika Mashariki kwa miaka kadhaa.

"Nina hakika hawana mawasiliano kati yao,"alisema kuhusu Idara ya Usalama wa Taifa, kitengo cha usalama wa taifa jeshini na idara za upelelezi na ushushushu za jeshi la polisi.

Wanasiasa wa Kenya na wanahabari wameeleza viokezo mbalimbali ambavyo havikuonwa mapema.Taarifa moja ya kiusalama iliyochapishwa kwenye magazeti, ambayo hata hivyo haikuweza kuthibitishwa rasmi, iliorodhesha nyendo za waliodhaniwa kuwa memba wa Al-Shabaab nchi humo, sambamba na dalili kwamba kuna uwezekano wa shambulizi la kigaidi katika maduka ya Westgate au kanisa.

Wakongwe wa usalama na wanadiplomasia wanaeleza pia kuwa taasisi za kishushushu za nchi za Magharibi nazo zilitetereka katika kuzuia shambulio hilo, kutokana na mawasiliano hafifu miongoni mwao, lakini tatizo hilo ni la dharura zaidi nchini Kenya.

Uratibu hafifu unaweza kuathiri utajiri mkubwa wa Kenya katika uwezo wake kuwafuatilia magaidi, kutoka kwenye mashushushu, majeshi yake nchini Somalia hadi vikosi vya kupambana na ugaidi, ambao hupokea misaada ya vifaa na mafunzo kutoka Marekani, Uingereza na nchi nyingine za Magharibi.

Israeli pia ilitoa msaada wa mafunzo ya kiintelijensia na ilipeleka 'washauri wa usalama' wakati wa tukio la Westgate.

Lakini hata kama intelijensia ingekuwa imara, bado rushwa ingeathiri ufuatiliaji wa watuhumiwa.Kwa fedha zenye thamani ya dola mia kadhaa tu, mtuhumiwa anaweza kununua passport, kupita vikwazo vya upekuzi wa polisi (police checkpoints) pasi kupekuliwa, na kununua silaha, wanaeleza maafisa na wataalam wa usalama.

Hiyo inamaanisha hata kama kuna nyenzo za kisasa kabisa za ufuatiliaji, bado washukiwa wanaweza 'kupotea kwenye rada' na kulazimisha ufuatiliaji usiwe na faida.

KUFIKIA ENEO KUSUDIWA (TARGET)

"Kenya inakabiliwa na tatizo kubwa katika safu ya kati,kwa sababu rushwa imetawala mno kwa polisi wa nchi hiyo" anaeleza mwanadiplomasia mmoja wa nchi ya Magharibi.

"Wamekuwa na mafanikio sana kuwazuwia Al-Shabaab...lakini kitu kisichoweza kukubalika ni jinsi magaidi walivyoweza kuingia nchini na kufikia eneo kusudiwa (target)" anasema mwanadiplomasia huyo.

Hiyo inafanya vigumu kujipenyeza ndani ya vikundi vya kigaidi, jambo ambalo ni muhimu katika kuvidhibiti.

"Inahitaji polisi mmoja tu mlarushwa kuwezesha ukiukwaji mkubwa wa kiusalama, kupita mpakani isivyostahili, kwa shilingi kutumbukizwa mfukoni na mtu kufanikiwa kuvuka mpaka," anaeleza mtaalam mwingine.

Jeshi la polisi linadai linauhamasisha umma kuripoti rushwa na kuchukua hatua stahili za kinidhamu.

"Hatuwezi kusema hakuna rushwa," alikiri Msemaji wa Polisi, Gatiria Mboroki, lakini akaongeza kuwa "Ukisharipoti, tukio hilo huchunguzwa."

Afisa mmoja wa zamani wa usalama wa taifa anaeleza kuwa wakati flani alijaribu kuwathibitishia wenzake jinsi rushwa ilivyo sugu, ambapo aliweza kuwaingiza nchini humo watoa habari wake kutoka Somalia baada ya kununua passport kwa dola 300 kila moja.

"Nikwenda mbali kuthibitisha kuwa udhibiti katika mipaka yetu ni dhaifu," alisema.

Mageuzi kwa jeshi la polisi yalikuwa moja ya vipaumbele vya Katiba mpya ya Kenya ya mwaka 2010. Lakini ukiweka kando uteuzi wa maafisa waandamizi, mageuzi kwa polisi hayajaleta chochote cha maana.

"Wanasema lakini hawafanyi lolote kuhusu hicho wanachosema. Haihitaji fedha.Inahitaji mabadiliko ya mtazamo," anasema mpigania haki Maina Kiai. "Mashushushu wanapaswa kufahamu kuwa kazi yao sio ya kisiasa, ni ya kiusalama."

Kauli hiyo iliungwa mkono na afisa wa zamani wa Idara ya Usalama wa Taifa ambaye alieleza kuwa wanausalama walivurugwa na Uchaguzi Mkuu uliopita. "Usalama wote umeelekezwa kwenye usalama wa kisiasa badala ya usalama wa taifa," alisema.

Ushindi wa Rais Uhuru Kenyatta katika uchaguzi mkuu uliopita ulionyesha kuwa ukabila bado ulikuwa na nafasi muhimu kwa wapiga kura, suala ambalo pia linaathiri teuzi za watendaji mbalimbali katika taasisi za usalama.

Serikali imedai kuwa teuzi hufanywa kwa kuzingatia uwezo, sio asili ya mteuliwa. Msemaji wa Polisi Mboroki kuwa jeshi la polisi haliyumbishwi na wanasiasa kwani ni taasisi ya umma.

Hata hivyo, wanaharakati na wataalam wanasema hatua zaidi zinahitajika.

"Pasipo mfumo wa kuwawajibisha kwa matendo yao na kuondoa rushwa," anasema mataalam wa usalama, "hakuna chochote kitakachobadilika."

Imetafsiriwa kutoka wavuti ya Reuters






23 Sept 2013

Fleeing: A child runs to safety across the shopping mall following the deadly attack in Nairobi, Kenya

Terror: Armed police guide a woman carrying a child to safety at Westgate shopping centre in Nairobi

Nadhani utakuwa umemuona huyu jamaa (kushoto) kwenye picha za TV zinazoeleza kilichotokea na kinachoendelea katika tukio la kigaidi kwenye Mall ya Westgate , jijini Nairobi nchini Kenya. Kwa hakika ninamuona kama mmoja wa mashujaa wakubwa katika harakati za kukabiliana na magaidi na kuokoa maisha ya wahanga wa tukio hilo.Sina hakika kama ni polisi au shushushu lakini picha mbalimbali zinazomwonyesha, zinathibitisha kuwa ni mmoja wa mashujaa wanaoweza kuingia kwenye kumbukumbu za muda mrefu kuhusu tukio hili la kusikitisha. Anaglia baadhi ya picha zinazomhusu.



Kenya Westgate siege

Helping out: British High Commissioner to Kenya, Christian Turner (left) lies on a bed after donating blood, following the overwhelming numbers of casualties from the shooting

Balozi wa Uingereza nchini Kenya, Christian Turner, alikuwa miongoni mwa waliojitolea damu kuokoa maisha ya majeruhi wa tukio hilo. Huu ni mfano wa kuigwa.

BOTTOM LINE IS, tuna mengi ya kujifunza kutoka kwa wenzetu Wakenya na katika tukio hili kwa ujumla.

7 Apr 2011


Wakenya wanne wanaodai waliteswa na utawala wa kikoloni wa Uingereza katika jitihada zake za kukandamiza harakati za kundi la Mau Mau,wamefungua kesi jijini London.

Kundi hilo linalodai fidia katika mahakama kuu ya hapa linadai kuwa walishambuliwa na maafisa wa serikali ya kikoloni ya Uingereza nchini Kenya kati ya mwaka 1952 na 1961.

Maelfu ya wanaharakati wa Mau Mau waliwekwa kwenye kambi za wakoloni hao na kuteswa huku wengine wakiuawa,wanasema wanaharakati hao.

Serikali ya Uingereza inadai kuwa muda mrefu umepita tangu yalipotokea matukio hayo,na hivyo inadai haiwajibiki nayo.

Hatua hiyo ya kisheria inachukuliwa na wanaume watatu na mwanamke mmoja ambao umri wao ni kati ya miaka 70 na 80.

Mawakili wao wanadai kuwa Wakenya hao wanne wanawakilisha sehemu kubwa ya jamii ya Wakenya walionyanyaswa kutokana na ushiriki wao,au kuhusiswa na harakati za mapambano dhid ya wakoloni katika miaka ya 1950s.

"Wizara" ya Mambo ya Nje ya Uingereza (Foreign Office) inakiri kwamba suala la Mau Mau linazua hisia kali na kwamba zama hizo zilisababisha maumivu makubwa kwa pande zote.

Hata hivyo,"Wizara" inaeleza kuwa Uingereza itajitetea kikamilifu dhidi ya madai yaliyomo kwenye kesi hiyo,ikidai kuwa haiwajibiki.

Uchambuzi wa nyaraka zinazohusiana na kesi hiyo umepelekea kugundulika kwa maelfu ya mafaili ya tawala za kikoloni za Waingereza,ikiwa ni pamoja na nchini Kenya,na "Wizara" ya Mambo ya Nje inatarajia kuweka rekodi hizo hadharani.

Harakati za Mau Mau zilianza miaka ya 1950s kwa lengo la kudai ardhi iliyoporwa na utawala wa kikoloni.

Wanahistoria wanadai kuwa harakati za Mau Mau zilichangia katika kupatikana uhuru wa Kenya.

Hata hivyo,harakati hizo pia zilishutumiwa kwa ukatili dhidi ya wakulima wa kizungu na mapambano ya umwagaji damu dhidi ya askari wa utawala wa kikoloni.

Kamisheni ya Haki za Binadamu nchini Kenya imesema kuwa zaidi ya Wakenya 90,000 waliteswa au kuuawa katika kipindi hicho,na watu 160,000 waliwekwa kizuizini katika mazingira ya kuogofya.

Ripoti rasmi iliyochapishwa mwaka 1961 ilidai kuwa zaidi ya Waafrika 11,000,wengi wao wakiwa raia wa kawaida,na wazungu 32 waliuwa katika kipindi hicho.

Habari hii imeandaliwa kutokana na habari kwenye kipindi cha "Breakfast" cha BBC1 Scotland na tafsiri isiyo rasmi kutoka kwenye tovuti ya BBC

16 May 2009


Na Leon Bahati

MAKAMU wa Rais wa Kenya, Kalonzo Musyoka amekiri kuwa mlima Kilimanjaro umekuwa ukiisaidia nchi yake kukuza sekta ya utalii kutokana na Wakenya wengi kuutumia katika kujitangaza hasa wawapo kwenye nchi za ulaya.

Pamoja na kufaidika huko, alisema kuwa hiyo haifuti ukweli kwamba mlima huo mrefu kuliko yote Afrika, upo Tanzania, ingawa pia huweza kuonekana kutokea Kenya.

Musyoka alisema hayo kwenye hafla fupi ya chakula cha mchana alichoandaliwa na mwenyeji wake, Makamu wa Rais wa Tanzania, Dk Ali Mohamed Shein.

“Wakenya wanapoenda Ulaya wanawaambia wazungu: Njooni Kenya ili muone mlima Kilimanjaro,” alisema Musyoka katika ziara hiyo ya kiserikali kwa mwaliko wa Tanzania...
endelea

CHANZO: Mwananchi


WELL,HUWEZI KUWALAUMU IWAPO SIE "WENYE MLIMA HUO" TUNAENDEKEZA ZAIDI POLITIKI KULIKO KUTANGAZA VIVUTIO VYETU.WANAOPEWA DHAMANA YA KUTANGAZA RASLIMALI ZETU WAKO BIZE ZAIDI NA "TENI PASENTI" YA MIKATABA YA MATANGAZO KULIKO UFANISI WA MATANGAZO HAYO.

3 Nov 2008

Nyumbani kwa Obama kijijini Kogelo,Kenya.

Kwa mujibu wa ripota wa CNN aliyeko kijiji cha Kogelo huko Kenya,ambacho kinahusiana kwa karibu sana na asili ya Barack Obama,kuna kundi la viumbe-hai wanaoombea mgombea wa urais huyo asishinde kesho ili viumbe hao wasalimike.Hao ni ng'ombe ambao wanaandaliwa kwa ajili ya sherehe kubwa pindi Obama atapotangazwa mshindi.Ni dhahiri kwamba asiposhinda,ng'ombe hao nao watasalimika.Who would you  have felt more sorry for?

Wakati ng'ombe hao wakisubiri hatima yao,sangoma mmoja kijijini hapo ametabiri kuwa Obama atashinda uchaguzi huo wa kesho.Of course,sangoma huyo-John Radima-sio pundit wa major TV networks au pollster kutoka Gallup,lakini ameweza kukamata attention ya vyombo vya habari vya kimataifa.

Kwa upande wa grandmother wa Obama,yeye anasema hawezi ku-take things for granted hadi hapo mshindi atapotangazwa,na anafuatilia kwa karibu maendeleo ya mjukuu wake kwenye runinga inayotumia solar power kwa vile hakuna umeme katika makazi yake.Sarah Onyango Obama,wenye miaka 86,anasema kwamba katika soka huwezi kutabiri ushindi mpaka goli lipatikane.Wakati bibi Sarah (pichani chini) akisubiria kwa hamu matokeo ya kesho,upanuzi wa uwanja wa ndege wa Kisumu umewafanya baadhi ya watu kutania kwamba huenda ni maandalizi ya ujio wa Air Force One ikiwa na Obama.


1 Feb 2008

Makala yangu hii ilitoka katika toleo la jana la gazeti la Mtanzania

Miongoni mwa adha za kumiliki runinga hapa Uingereza ni kuilipia ada ya leseni (TV Licence Fee).Ada hiyo kwa kiasi kikubwa hutumika kuendesha BBC ambalo ni shirika la utangazaji la nchi hii.Wananchi wengi wamekuwa wakilalamika kwamba baadhi ya vipindi vya BBC havina ladha inayoweza kuhalalisha shirika hilo kuendelea kupewa ruzuku inayotokana na ada ya leseni za runinga.Hata hivyo,BBC imeendelea kuwa shirika la habari maarufu na lenye mtandao mkubwa sio tu ndani ya Uingereza bali duniani kwa ujumla.Na miongoni mwa vipindi maarufu vya shirika hilo la habari ni Newsnight,kipindi kinachoonyeshwa siku za wiki kuanzia saa 4.30 usiku.

Kipindi hicho huchambua habari muhimu zilizojitokeza katika siku husika ndani na nje ya nchi hii.Hivi karibuni,Newsnight ilizungumzia machafuko yanayoendelea nchini Kenya.Kwa hakika ilikuwa inatia uchungu kuona namna watu wanavyotaabika nchini humo.Moja kati ya mambo yaliyolinisikitisha zaidi ni mahojiano mafupi kati ya mtangazaji wa BBC aliyeko nchini Kenya na mwanamama mmoja ambaye wakati wa mahojiano hayo alikuwa kamanda wa polisi wa eneo flani (jina la afande huyo na mahala alipokuwa anaongoza vimenitoka kidogo).

Kamanda huyo alianza mahojiano hayo kwa kukanusha madai kwamba jeshi la polisi la Kenya limekuwa likiuwa raia wasio na hatia katika kutekeleza sera ya “piga risasi kuua” (shoot-to-kill policy).Alidai kuwa wanachofanya wanausalama ni kudhibiti machafuko na uhalifu.Mwishoni mwa mahojiano,afande huyo alieleza uchungu alionao kuona nchi yake ikiteketea.Alisema kwamba ameshatembelea sehemu nyingi duniani na kuona watu wa nchi hizo wakiwa na fahari na nchi zao,jambo ambalo lilimwongezea mapenzi kwa nchi yake.Aliwalaumu wanasiasa wa Kenya kwa kuzorotesha jitihada za kuleta amani.

Cha kusikitisha ni kwamba kamanda huyo aliyeonekana kuguswa sana na madhila yanayowakumba Wakenya wenzie aliondolewa kwenye usimamizi wa operesheni za mitaani na kukabidhiwa majukumu ya kiofisi (desk job).Yaani aliadhibiwa kwa kusema ukweli wa moyoni mwake kuhusu namna wanasiasa wanavyoendekeza maslahi yao kuliko ya nchi na wananchi.Naamini mwanamama huyo ni mmoja tu kati ya askari wengi ambao wanalazimika kupiga na hata kuua Wakenya wenzao katika kutekeleza amri “halali” za serikali.

Ilielezwa katika kipindi hicho cha Newsnight kwamba licha ya matokeo ya uchaguzi mkuu wa rais na wabunge mwezi Desemba mwaka jana kuwa chanzo kikuu cha machafuko hayo yasiyoonyesha dalili ya kupungua,msingi wa matatizo ulijengwa miaka kadhaa iliyopita.Kwa mujibu wa uchambuzi wa wajuzi wa siasa za Kenya,kwa muda mrefu kumekuwa na manung’uniko miongoni mwa baadhi ya makabila kuhusu umiliki wa njia za uchumi ambapo inadaiwa Wakikuyu wamekuwa na upendeleo zaidi.

Tofauti za kikabila na kidini ni miongoni mwa vyanzo vikubwa vya machafuko sehemu mbalimbali duniani hususan barani Afrika.Lakini tofauti hizo hustawi vizuri zaidi mahala ambapo kuna manung’uniko kuhusu haki na usawa hasa katika uchumi.Ni rahisi kumshauri fukara aingie mtaani “kujikomboa” kuliko kumshawishi mtu afunge biashara zake akashiriki maandamano.Pia ni vigumu kwa watu wa makabila au dini tofauti wanaoshirikiana katika ajira na utoaji au upokeaji huduma kuanzisha vurugu ambazo kwa vyovyote zitapelekea kuathiri mahusiano yao (kwa mfano, mahusiano kati ya mfanyabiashara na mteja au mwajiri na mwajiriwa).

Tofauti na nchi kama Uingereza ambapo mvuto wa kisiasa miongoni mwa wapiga kura uko chini hasa kwa vijana,wengi wetu tulishuhudia namna kampeni za uchaguzi nchini Kenya zilivyogusa karibu kila sehemu ya maisha ya Wakenya,kama ambavyo chaguzi zetu huko nyumbani zinavyokuwa na mvuto mkubwa.Ni dhahiri kwamba amani ingeshapatikana iwapo nguvu nyingi zilizotumiwa na wanasiasa wa Kenya na vyama vyao kushawishi wapiga kura zingeelekezwa pia kwenye kutafuta mwafaka katika vurugu zinazoendelea.

Ni vigumu kubashiri namna gani vurugu hizo zitadhibitiwa na kumalizwa kwa vile Kibaki na Raila wanaonekana kutokubaliana katika njia sahihi za kuleta amani.Yayumkinika kusema kwamba hakuna uwezekano wa Kibaki na serikali yake kukubali mapungufu yaliyojitokeza kwenye uchaguzi huo kwa vile kwa kufanya hivyo watakuwa wameongeza nguvu kwenye hoja za Raila na wafuasi wake kwamba matokeo ya uchaguzi huo ni feki.

Kwa upande mwingine,Raila anafahamu gharama kubwa ya maisha na mali wanayoipata wafuasi wake kwa kupinga matokeo ya uchaguzi huo,na kukubali kushirikiana na Kibaki pasipo makubaliano ya kutengua ushindi wa rais itakuwa ni sawa na usaliti wa daraja la kwanza.Historia nayo haitoi matumaini ya amani kwa jirani zetu wa Kenya kwani hakuna rais yeyote (hasa barani Afrika) anayeamini alishinda uchaguzi kwa njia halali aliye tayari kukubali uchaguzi urejewe kwa minajili tu ya kuridhisha wapinzani wake au kutuliza machafuko nchini mwake.

Madhara ya muda mrefu ya kinachoendelea nchini Kenya ni kuzaliwa kwa kizazi chenye kinyongo.Ni kipi kinachoweza kufuta kinyongo cha mtoto aliyepoteza wazazi wake katika machafuko hayo?Kibaya zaidi ni kwamba kadri machafuko yanavyoendelea ndivyo kizazi hicho cha kinyongo kinavyozidi kuongezeka.

Miezi michache iliyopita Watanzania walitoa maoni kuhusu wazo la kuunda muungano wa nchi za Afrika Mashariki,na wengi wao walipinga uharakishaji wa muungano huo.Ni kama walifahamu kwamba kelele za kuwa na muungano zilikuwa za kisiasa zaidi kuliko kuzingatia hali halisi ndani ya nchi husika. “Mikoa” ambayo ingeunda “nchi” hiyo (yaani sie na Uganda,na pengine Burundi na Rwanda) imeshindwa kuwa na mchango wa maana wakati “mkoa mwingine” (Kenya) unazidi kuteketea.Sijui ingekuwaje iwapo haya yangekuwa yanatokea ndani ya muungano huo!

Baadhi ya wapinzani wa muungano huo walieleza bayana kwamba japo wanafahamu umuhimu wa ushirikiano,au hata kuungana kisiasa,ukweli unabaki kwamba nchi husika zina matatizo yake lukuki ambayo yanapaswa kushughulikiwa kwanza kabla ya kuyakuza kwa kuunda “nchi” kubwa zaidi iliyojaa vipande vyenye matatizo binafsi.

Jeuri za wanasiasa wa Kenya kutosikiliza vilio vya wananchi wao na kupuuza jitihada mbalimbali zinazofanywa na wasio Wakenya ni onyo muhimu kwa wenye ndoto za ya muungano wa Afrika Mashariki kwamba kama wanashindwa kuweka mbele maslahi ya nchi yao na wananchi wao watajali vipi maslahi ya Watanzania au Waganda.

Kubwa la kujifunza katika sakata hili ni jinsi ilivyo amani iliyojengwa kwa miaka miongo kadhaa inavyoweza kuyeyuka ndani ya kipindi kifupi kabisa.Harakati za kumfukuza mkoloni nchini Kenya zilichukua miaka mingi na kugharimu maisha mengi.Wakenya walikuwa bado wako katika harakati za kupata uhuru wa kweli hadi wakati machafuko yanaanza nchini humo.Kinachoendelea sasa ni sawa na kusigina jitihada na damu za mashujaa waliopigania uhuru wa nchi hiyo.

Kwa Watanzania,wakati tunaendelea kuwaombea jirani zetu amani (yaelekea hakuna la ziada tunaloweza kufanya zaidi ya hilo) ni muhimu kutambua kwamba amani na utulivu tulionao unaweza kudumu milele iwapo tu jitihada za makusudi zitafanyika kuondoa umasikini,kuhakikisha pato la taifa linatumika kwa maslahi ya wote na “haki” kuwa haki ya kweli kwa kila Mtanzania bila kuangalia tabaka.Kelele dhidi ya ufisadi na mafisadi ni sehemu muhimu ya harakati za kuhakikisha amani na utulivu nchini inadumu milele.

6 Jan 2008


Nimesoma makala moja ndefu katika toleo la leo la Sunday Times (la hapa Uingereza) kuhusu hali ilivyo kwa majirani zetu wa Kenya.Kwa kweli inatisha na kusikitisha.Mauaji na ubakaji ni miongoni mwa unyama unaozidi kushamiri nchini humo.Lakini inasikitisha zaidi kuona hata watoto wadogo wa miaka 12 wanakumbwa na ukatili huo.

Lakini kilichonikurupusha kuandika makala hii ni habari kwamba vurugu hizo zinahusisha pia makundi mawili hatari:Mungiki (la Wakikuyu) na Taliban (la Waluo).Kwa namna inavyoonekana,makundi haya ni sawa na magenge ya wahalifu ambayo kwao vurugu za aina yoyote ni sawa na msimu wa mavuno.Inaelezwa kwamba Mungiki wamekuwa wakiwatahiri kwa nguvu "mateka" wao wa Kiluo (kwa mila zao,wanaume wa Kiluo huwa hawatahiri) huku Taliban wakijibu mashambulizi kwa kuwafyeka mapanga Wakikuyu.

Inatisha na kusikitisha kusikia kwamba watu kadhaa waliuawa kinyama kwa kuchomwa moto wakiwa ndani ya kanisa walilojihifadhi.Kwa nchi ambayo asilimia kubwa ya wakazi wake ni Wakristo,hiyo ni ishara kwamba chuki kati ya makundi yanayopingana zimevuka nguvu za mshikamano wa jamii kama dini na utaifa,na inaelekea kinachoangaliwa sasa ni ukabila tu.

Haihitaji ujuzi wowote wa mambo ya uchaguzi kubaini kwamba Kibaki amejirejesha kwa nguvu madarakani.Hivi anajisikiaje wakati yeye yupo Ikulu,mamia ya Wakenya wenzake,ikiwa ni pamoja na Wakikuyu wenzie,wanapoteza maisha yao kila siku huku wengine wanaishi kwa hofu na mashaka ya kuuawa,kubakwa,kutahiriwa kwa nguvu na udhalilishaji mwingine usiopaswa kufanyika katika jamii yoyote ile iliyostaarabika.Damu inayomwagika kila kukicha (sambamba na mateso yanayowakuta wananchi wasio na hatia) iko mikononi mwa Kibaki.

5 Jan 2008

MAKALA HII ILITIOKA KWENYE GAZETI LA "MTANZANIA" LA ALHAMISI JANUARI 3,2008.

Nianze kwa kutoa salamu za heri na Baraka ya mwaka mpya 2008.Kwa sie wenye imani katika dini,kufikia mwaka mpya kunapaswa kuambatana na sala na dua za shukrani kwa Muumba kwa kutuwezesha kuona mwaka huu.

Wiki ya mwisho ya mwaka jana ilishuhudia matukio makubwa mawili:kuuawa kwa Waziri Mkuu wa zamani wa Pakistan,Benazir Bhutto,na uchaguzi mkuu nchini Kenya.Kwa bahati mbaya,asilimia kubwa ya vyombo vya habari vya kimataifa vilizipa uzito zaidi habari za kifo cha Bhutto kuliko uchaguzi wa Kenya,na hivyo kutunyima fursa sie wengine kufuatilia kwa karibu nini kilichokuwa kinaendelea kwa majirani wetu hao.Hata hivyo,kituo cha runinga cha Al Jazeera English kilijitahidi kwa kiasi kikubwa kuhakikisha watazamaji wake wanajulishwa maendeleo ya uchaguzi huo.

Tukianza na kifo cha Bhutto,hadi sasa kuna maswali mengi zaidi kuliko majibu kuhusu nani aliyehusika na mpango wa kumuondoa duniani mwanasiasa huyo mahiri ambaye alikuwa amerejea hivi karibuni tu kutoka kwenye hifadhi ya kisiasa.Lakini lililo dhahiri ni kwamba mwanamama huyo alikuwa na maadui wengi,na yeyote kati yao anaweza kuwa mhusika mkuu wa mauaji hayo.

Wachambuzi wa siasa za Pakistan wanaeleza kwamba baadhi ya makundi yenye nguvu hayakupendezwa na uamuzi wa Bhutto kurejea nchini humo.Waziri huyo Mkuu wa zamani na kiongozi wa chama pinzani cha PPP alishajitengenezea maadui kadhaa wakati wa utawala wake ulioisha kwa kung’olewa madarakani mara mbili kwa tuhuma za ubadhirifu.Wengi wa maadui hao bado wako kwenye taasisi mbili zenye nguvu kubwa nchini Pakistan,yaani jeshi na Idara ya Usalama ya nchi hiyo (ISI).Kimsingi,taasisi hizo mbili zimekuwa mhimili mkubwa wa siasa za Pakistan sambamba na shutuma dhidi yao kuwa zimekuwa zikishirikiana na vikundi vya kigaidi kama vile Al-Qaeda.Katika mazingira hayo,kuna uwezekano wa baadhi ya mashushushu na majenerali waliopo madarakani au wastaafu (waliokuwa wakimpinga Bhutto) kuwatumia wahalifu kama Al-Qaeda kutekeleza mpango wa mauaji ya mwanasiasa huyo.

Sababu nyingine iliyoongeza idadi kubwa ya maadui dhidi ya Bhutto ni msimamo wake dhidi ya vikundi vyenye msimamo mkali wa kidini uliokwenda sambamba na ukaribu wake na nchi za Magharibi.Wakati anarejea nyumbani hivi karibuni,mwanasiasa huyo alitangaza bayana dhamira yake ya kupambana na vikundi vya Kiislamu vyenye msimamo mkali,ambavyo kwa hakika vina wafuasi wengi nchini humo.Machoni mwa vikundi hivyo na hata miongoni mwa wapinzani wake wa kisiasa,Bhutto alionekana kibaraka wa nchi za Magharibi hasa Marekani.

Kuna habari kwamba Marekani na Uingereza ndizo zilizoandaa mpango wa Bhutto kurejea Pakistan na kumshinikiza Rais Pervez Musharaf aandae mpango utakaopelekea wanasiasa hao wawili kushirikiana katika uongozi wa nchi hiyo (ambapo Bhutto alitarajiwa kuwa Waziri Mkuu wa nchi hiyo).Ikumbukwe kwamba Pakistan ni sehemu muhimu katika kile kinachojulikana kama “vita dhidi ya ugaidi wa kimataifa” (war on terror),na ilitarajiwa kuwa vita hiyo ingekuwa imepata mshirika mzuri iwapo Bhutto angeshika hatamu za uongozi nchini humo.

Tukiachana na habari hizo za mauaji ya Bhutto,uchaguzi mkuu nchini Kenya ulionekana kutugusa Watanzania wengi hasa ikizingatiwa kwamba lolote linalotokea nchini humo linaigusa pia nchi yetu kwa namna flani.Hadi wakati naandaa makala hii,tayari kuna idadi ya watu kadhaa walioripotiwa kuuwawa kufuatia kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi huo ambapo Rais Mwai Kibaki alirejea madarakani “kwa mbinde”.Ni mapema mno kutabiri hatma ya Kenya hasa ikizingatiwa kwamba Raila Odinga na wafuasi wake wanaamini kwamba waliporwa ushindi kwenye uchaguzi huo.

Kinachowafanya wengi kukubaliana na hoja ya Raila na chama chake cha ODM kuwa ushindi wa Kibaki ni wa kupikwa ni uzembe wa tume ya uchaguzi ya Kenya kutangaza matokeo katika muda stahili.Ikumbukwe kwamba hadi dakika za mwisho,Raila aliripotiwa kuongoza kwa asilimia kubwa lakini ghafla upepo ukabadilika na ushindi kuelekea kwa Kibaki.Kibaya zaidi,matokeo yaliyobadili mwelekeo wa ushindi kwa Raila ni kutoka katika maeneo ambayo yalichelewa kuwasilisha matokeo.Lakini kibaya zaidi ni taarifa kwamba baadhi ya wasimamizi wa uchaguzi huo waliojitokeza hadharani kudai kwamba kulikuwa na wizi wa kura uliokuwa na lengo la kumpatia ushindi Kibaki.

Kama “mchambuzi mchanga wa siasa za kimataifa” sikushangazwa na kilichotokea katika uchaguzi mkuu wa Kenya.Mimi ni muumini wa “kanuni isiyo rasmi” kuhusu chaguzi barani Afrika kwamba chama tawala hakipaswi kushindwa uchaguzi,na iwapo kitashindwa basi sababu kubwa itakuwa sio nguvu za vyama pinzani au hasira za wananchi bali uzembe wa chama tawala katika kujiandaa vizuri kuendelea kuwa madarakani.Vyama vingi tawala barani Afrika ni sawa na kile Waingereza wanakiita “judge,jury and prosecutor” yaani jaji,wazee wa baraza na mwendesha mashtaka.Kama kwenye soka,basi vyama hivyo ni sawa na timu yenye zaidi ya wachezaji 15 ikimjumuisha refa,washika vibendera na kamisaa.Katika mazingira kama hayo,ni vigumu sana kwa vyama vya upinzani barani Afrika kukiondoa chama tawala madarakani.

Hakuna ubaya kwa chama tawala kuendelea kuwa madarakani hata milele ikibidi.Kinachogomba ni ukweli kwamba vingi ya vyama hivyo hung’ang’ania madarakani kwa manufaa ya kikundi cha watu wachache wanaoendelea kufaidi “keki ya taifa” huku asilimia kubwa ya wananchi wakihangaika kumudu maisha yao ya kila siku.

Lakini kuna sababu nyingine kubwa inayovifanya vyama tawala vingi barani Afrika kuhakikisha kuwa vinabaki madarakani milele,nayo ni kuogopa hukumu ya umma dhidi ya ufisadi unaoendekezwa na vyama hivyo wakati viko madarakani.Kwa vile mara nyingi uongozi barani Afrika hutumika kama pazia la kuikamua nchi kwa maslahi ya watu binafsi,vyama tawala vinafahamu fika kwamba pindi vikishindwa uchaguzi kuna uwezekano mkubwa wa viongozi wake wasio waadilifu kudakwa na mkono mrefu wa sheria.

Tatizo kubwa zaidi katika mfumo wa siasa barani Afrika ni ile hali ya taasisi za uongozi kubinafsishwa na kuwa mali ya chama au viongozi wa vyama hivyo.Kinachowasaidia sana wenzetu wa nchi za Magharibi ni uimara wa taasisi kama tume za uchaguzi,mahakama,bunge na vyombo vya dola ambavyo japo baadhi ya viongozi wake huchaguliwa na wanasiasa,utendaji wake wa kazi huweka mbele zaidi maslahi ya taifa kuliko chama cha siasa.

Ni jambo la kawaida katika siasa za Afrika kuona watu waliokabidhiwa dhamana ya kuhakikisha taasisi za umma zinaendeshwa kwa kuzingatia taratibu na maadili wakigeuka wanasiasa na kuonyesha upendeleo wa waziwazi dhidi ya vyama pinzani.Hawa wanasumbuliwa na ubinafsi kwani wanajua dhahiri kwamba udhaifu wao katika utekelezaji wa majukumu yao unalelewa na waliowaweka madarakani.

Inakubalika kwamba kwa ujumla siasa ni mchezo mchafu lakini kwa sehemu nyingi barani Afrika,siasa ni zaidi ya mchezo mchafu.Ni mkusanyiko wa mazingaombwe,maigizo,ubabaishaji na mambo mengine yanayoweza kumfanya mtu akubaliane na hisia za wabaguzi wa rangi wanaodai kwamba matatizo yanayolikabili bara la Afrika yanatokana na udhaifu wa kibaiolojia na kinasaba miongoni mwa watu wanaoitwa Waafrika.Japo sikubaliani na hisia za aina hiyo,lakini tunawezaje kuelezea mambo ya ajabu yanayojiri kila kukicha katika bara hili?

Heri ya mwaka mpya

30 Dec 2007

Hatimaye Mwai Kibaki ametangazwa mshindi katika uchaguzi mkuu nchini Kenya.Ni rahisi kuhisi Raila Odinga ameporwa ushindi kutokana na namna matokeo ya uchaguzi huo yalivyochukua muda mrefu kuliko ilivyopaswa.Wakati matokeo haya yanaweza kuwaacha watu wengi,hususan wafuasi wa Raila,wakiwa hawaamini kinachoendelea,binafsi naona ni mwendelezo wa "kanuni isiyo rasmi" ya siasa za Afrika ambapo mara nyingi CHAMA TAWALA HAKISHINDWI UCHAGUZI ISIPOKUWA PALE KINAPOLEWA MADARAKA NA KUJIONDOA CHENYEWE KWA UZEMBE.KANU haikushindwa uchaguzi na NARC (enzi hizo) kwa vile wapinzani walikuwa na nguvu sana au wananchi walikuwa wameichoka sana,bali ilijifunga "own goal" kwa kusimamisha mgombea butu.Vyama pinzani vinaweza kufanya kila jitihada kukiondoa chama tawala madarakani lakini tatizo linabaki kuwa katika chaguzi nyingi za Afrika,vyama pinzani ni sawa na mshtakiwa aliyeko mahakamani ambapo hakimu,mwendesha mashtaka na baraza la wazee wanatoka upande wa mshtaki (ni dhahiri hapo hakutakuwa na haki kwa mshtakiwa).Na katika soka,mkiwa mnashindana na timu ambayo refa,kamisaa na washika vibendera ni manazi wa wapinzani wenu,basi hapo ni kipigo tu hata mtumie mbinu za Brazil.

Kwanini vyama tawala vya Afrika vipo tayari kufanya lolote linalowezekana kuhakikisha vinabaki madarakani?Well,jibu jepesi ni kwamba viongozi wengi wa vyama hivyo ni mafisadi wanaojua bayana kwamba wakiondoka madarakani wanaweza kujikuta wanaishia jela kwa maovu yao.Japo kwa ujumla siasa ni mchezo mchafu,kwa Afrika siasa ni zaidi ya mchezo mchafu,na pengine sio mchezo at all bali mazingaombwe.

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.