Showing posts with label UNAFIKI. Show all posts
Showing posts with label UNAFIKI. Show all posts

9 Feb 2017

MWEZI Machi mwaka jana, watafiti kutoka Chuo Kikuu cha Nottingham cha hapa Uingereza walichapisha matokeo ya utafiti wao kuhusu kushamiri kwa tabia ya uvunjaji wa sheria. Katika matokeo hayo ya utafiti uliochunguza nchi 159, Watanzania tuliibuka vinara kwa kuwa watu wanafiki kupita kiasi, tukifuatiwa na watu wa Morocco.
Na mifano ya unafiki wetu ipo mingi tu, sisi ni miongoni mwa wapinzani wakubwa wa suala la ushoga. Lakini ukitaka kufahamu unafiki wetu katika suala hilo, nenda kwenye mtandao wa kijamii wa Instagram, shuhudia lundo la mashoga wa Kitanzania waliojitundika huko, wakifanya vitu vichafu kabisa, huku wakiwa na “followers” hadi laki kadhaa, hao si tu ni Watanzania wenzetu bali ni miongoni mwa sisi ‘wapinga ushoga.’ Unafiki wa daraja la kwanza.
Na sababu kuu tunayoitumia kupinga ushoga ni imani zetu za kidini. Na kwa hakika tumeshika dini kweli, hasa kwa kuangalia jinsi nyumba za ibada zinavyojaa. Lakini kuthibitisha unafiki wetu, ucha-Mungu huo sio tu umeshindwa kudhibiti kushamiri kwa ushoga (na usagaji) bali pia kutuzuia tusishiriki kwenye maovu katika jamii.
Kwa taarifa tu, kwa mujibu wa utafiti uliofanywa miaka michache iliyopita na taasisi ya Pew ya Marekani, Watanzania tunaongoza duniani kwa kuamini ushirikina. Na kwa mujibu wa taarifa ninazozipokea kutoka huko nyumbani, ushirikina umeshamiri mno kiasi kwamba sasa ni kama sehemu ya kawaida ya maisha ya Watanzania.
Wacha-Mungu lakini tumebobea kwenye ufisadi, rushwa, ujangili na biashara ya dawa za kulevya. Na asilimia kubwa ya kipato haramu kinachotokana na uhalifu huo kinachangia kushamiri kwa “michepuko” na “nyumba ndogo.”
Mfano wa karibuni kabisa kuhusu unafiki wetu ni katika mshikemshike unaoendelea hivi sasa huko nyumbani (Tanzania) ambao watu kadhaa maarufu aidha wametakiwa kuripoti polisi au ‘kuhifadhiwa’ na polisi wakichunguzwa kuhusiana na biashara ya dawa za kulevya. Hali hiyo inatokana na tangazo rasmi la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, ‘kujitoa mhanga’ kukabiliana na biashara hiyo haramu.
Lakini licha ya kuwepo kwa lundo la lawama mfululizo kwa serikali kuwa imekuwa ‘ikiwalea’ watu wanaojihusisha na biashara ya dawa za kulevya, tangazo la Makonda limesababisha kuibuka kwa lawama lukuki dhidi yake, huku wengine wakidai anatafuta ‘kiki (sifa) za kisiasa’ na wengine kudai amekurupuka kwa kutaja majina ya watu maarufu, na wengine wakimlaumu kwa kukamata ‘vidagaa’ na kuacha ‘mapapa.’
Kwa watu hao, na wapo wengi kweli, Makonda atashindwa kama alivyoshindwa kwenye amri zake nyingine. Sawa, rekodi ya Mkuu wa Mkoa huyo katika ufanisi wa maagizo yake sio ya kupendeza. Hata hivyo, kwa mara ya kwanza katika historia ya Tanzania, kiongozi sio tu ametangaza vita dhidi ya biashara ya dawa za kulevya bali pia ametaja baadhi ya majina ya wahusika, na kuwafikisha polisi. Hili ni tukio la kihistoria.
Lakini ‘wapinzani’ wa RC Makonda sio wananchi wa kawaida tu. Kuna ‘wapinzani wa asili,’ mbunge wa Chadema, Tundu Lissu, ambaye aliandika ujumbe mtandaoni, “kuwataja vidagaa na kuwaacha nyangumi/papa si ajabu ni moja kati ya mambo ya ovyo ya awamu ya tano.” Huyu ni mnafiki wa mchana kweupe. Sasa kama anawajua hao nyangumi/papa si awataje?
Kilichonisikitisha zaidi ya vyote ni kauli za Waziri Nape Nnauye alipozungumza na waandishi wa habari huko Dodoma. Pamoja na mambo mengine, Waziri Nape alidai kuwa, “ …watumiaji ni wengi lakini wanaoonekana zaidi ni wale wenye majina makubwa,” (sijui kwa mujibu wa utafiti gani); “Kama wizara tunaunga mkono juhudi za kupambana na dawa za kulevya, tatizo ni namna ya kushughulika na wahusika ikiwemo busara” (sijui alitaka tatizo lishughulikiwe kwa namna gani – na kwa nini hakuongoza kwa mfano kwa kutumia namna hiyo – na sijui busara ipi iliyokosekana katika utekelezaji wa agizo la Makonda); “Tunaunga jitihada za mapambano lakini ni vizuri lifanywe katika namna ya kulinda haki ya mtuhumiwa ili heshima yake isipotee” (haelezi hiyo ‘namna ya kulinda haki ya mtuhumiwa ili heshima yake isipotee’ ni kitu cha aina gani)
Nilimshutumu vikali Waziri Nape kupitia mtandao wa kijamii wa Twitter (nilim-tweet yeye mwenyewe), na kumweleza bayana kuwa alihitaji kutumia busara badala ya kukurupuka kutetea wasanii wanaotuhumiwa kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya. Kadhalika, kama mtendaji wa serikali, alikuwa na nafasi nzuri kuzungumza na watendaji wenzake wa serikali faragha badala ya kuongea suala hilo hadharani. Kadhalika, kuonekana anahofu zaidi kuhusu “brand” (thamani/hadhi ya msanii, kwa tafsiri isiyo rasmi) badala ya athari kubwa zinazosababishwa na biashara ya dawa za kulevya sio busara hata kidogo.
Nihitimishe makala hii kwa kutoa wito kwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba naye ajitokeze hadharani kuongelea suala hili maana amekuwa kimya mno. Awali, naibu wake alipohojiwa na wanahabari alikuwa mkali na alitoa kauli zisizopendeza. Ili vita hii ifanikiwe ni lazima serikali iwe kitu kimoja na viongozi na wananchi kwa ujumla waache unafiki, na wampe ushirikiano RC Makonda na Jeshi la Polisi.
Tanzania bila dawa za kulevya inawezekana

Barua-pepe: [email protected] Blogu: www.chahali.com Twitter: @chahali

22 May 2016



Taarifa mbalimbali zinaonyesha kuwa kuna ongezeko kubwa la Watanzania wanaojihusisha na ushoga na usagaji japokuwa vitendo hivyo ni kinyume na sheria za nchi na haviendani na mila na desturi zetu.

Hata hivyo, yawezekana kushamiri kwa vitendo hivyo kunaendana na taarifa za kitafiti kuwa sie Watanzania twaongoza kwa unafiki. Wiki chache zilizopita niliweka bandiko hapa bloguni lililohusu ripoti ya utafiti wa kundi la wasomi katika chuo kikuu cha Nottingham, hapa Uingereza, ulivyobainisha kuwa Tanzania yaongoza duniani kwa unafiki.

Binafsi sikushangazwa na ripoti hiyo hasa kwa vile kuna maeneo mawili yanayothibitisha bayana unafiki wetu. La kwanza ni uhusiano kati ya ucha-Mungu wetu na maovu.

Asilimia kubwa ya Watanzania ni wacha-Mungu. Takwimu zaashiria kuwa takriban asilimia 70 ya Watanzania ni aidha Wakristo au Waislam. Wengi kati ya hao ni watu wasiokosekana kanisani au misikitini. Swali: kama wengi wetu ni waumini kiasi hicho, ni akina nani basi wanaojihusisha na ufisadi, rushwa, biashara ya madawa ya kulevya, ushirikina, na maovu mengine katika jamii?

Tofauti na huko nyumbani, ucha-Mungu hapa Uingereza ni wa kusuasua mno. Watu wengi hapa hawamtambui Mungu na wanajitambulisha kuwa hawana dini. Makanisa mengi yanageuzwa kuwa baa au kumbi za starehe kutokana na uhaba wa waumini.



Lakini licha ya udhaifu katika mahusiano kati yao na Mungu, wenzetu hawa kwa kiasi kikubwa sio wanafiki. Asilimia kubwa kabisa ya watu hawa wanaishi kwa kipato halali, wanaamini katika ukweli, kwa maana ya kusema ukweli na sio wadanganyifu, wanafuata sheria na taratibu mbalimbali, kwa mfano moja ya dhambi kuu hapa ni ukwepaji kodi, kitu ambacho ni kama hobby ya wengi wa wafanyabiashara huko nyumbani.

Eneo la pili ni suala la ushoga na usagaji. Kwa huko nyumbani, suala hili ni mwiko mkubwa, ni laana, ni kinyume na maadili yetu. Lakini kuthibitisha unafiki wetu, sio tu ushoga na usagaji upo bali pia unakua kwa kasi kubwa.

Nenda katika kitchen parties za watu maarufu na 'wakata viuno' ni mashoga huku wengi wa 'makungwi' wakituhumiwa kuwa wasagaji. Inaelezwa kuwa njia moja maarufu ya kusambaa kwa usagaji huko nyumbani ni 'makungwi' wanaofundisha mabinti (kwa malipo) jinsi ya kufanya tendo la ndoa. Hawa wametapakaa jijini Dar na baadhi wanahamia mikoani. Kimsingi, 'darasa la tendo la ndoa' wanalofundisha ni kwa kusagana na 'wanafunzi' wao.

Shughuli za 'madada wa mujini' hazijakamilika kama hakuna akina 'anti naniliu au anti nanihino.' Lakini watu haohao ndio wanaohubiri kwa sauti kubwa kuwa "habari za ushoga na usagaji huko huko kwao (wazungu)."

Kuna kitu kingine 'kichafu' ambacho Watanzania twasifika mno, nacho ni umahiri katika tendo la ndoa kinyume cha maumbile. Kwa kifupi, hii ndio sababu ya kushamiri kwa biashara ya "dawa za makalio feki ya Mchina." Tendo la ndoa kinyume cha maumbile limekuwa kama 'fasheni' kwa wengi wetu huko nyumbani na huku ugenini tunakoishi. 

Sasa, japo tendo la ndoa kinyume cha maumbile sio ushoga per se, kuna hisia kuwa wazoefu wa tabia hiyo "wakikosa nyama wanaweza kula majani." Yaani wanaume wanaopenda tabia hiyo wakikosa mwanamke wanaweza kufanya hivyo na mwanaume shoga.

UTHIBITISHO wa unafiki wetu: Well, sehemu mwafaka zaidi ya kutambua unafiki wetu kuhusu ushoga na usagaji ni INSTAGRAM. Huko, kuna mashoga wanaojinadi waziwazi. Lakini tatizo sio wao kujinadi tu bali ni idadi ya 'followers' wao. Ni wazi kuwa laiti ingekuwa watu wanachukia ushoga 'kihivyo' basi mashoga huko Insta wasingekuwa maarufu kiasi cha kupata followers hadi laki na zaidi.

Profiles hizi pichani chini ni za baadhi tu ya mashoga wa Kitanzania huko Instagram.  Je kama sie sio wanafiki na laiti tungekuwa tunauchukia ushoga 'kihivyo' hao maelfu kwa malaki ya followers kwa hao mashoga wangetaka wapi?


Ukitaka kuchimba zaidi kuhusu 'unafiki' wetu, geukia suala jingine maarufu huko nyumbani: USHIRIKINA. Kwa mujibu wa utafiti wa hivi karibuni wa taasisi moja ya kimataifa inayoheshimika kwa utafiti ya PEW ya Marekani, Tanzania ipo 'matawi ya juu' katika masuala ya juju, ndumba na ngai, tunguri, kamati ya ufundi, wanga...USHIRIKINA... kama inavyoonyeshwa kwenye chati na ramani hapo chini.




Kwa vile lawama pekee hazijengi, ni muhimu kujaribu kuangalia njia zinazoweza kutuondoa katika lindi hilo la unafiki. Binafsi, ninashauri tuwekeze zaidi katika dua na sala za dhati na sio za kinafiki. Au wewe msomaji mpendwa una maoni gani?



30 May 2013

Magufuli amkana Sitta, asema hana ubia naye urais 2015


Siku chache baada ya Waziri wa Afrika Mashariki Samuel Sitta kumhusisha Dk John Magufuli na kundi la urais la mwaka 2015, Waziri huyo wa Ujenzi, ameibuka na kupinga kauli hiyo, akisisitiza hafikirii kuwania nafasi hiyo.
Waziri Sitta alinukuliwa na gazeti hili juzi akieleza kuwa wakati ukifika, yeye na rafiki zake Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, Waziri wa Ujenzi, Dk Magufuli na Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe, watachagua mmoja wao watakayeona anafaa kuwania urais katika Uchaguzi Mkuu wa 2015. Alisema hayo juzi kwenye Kongamano la Mawasiliano katika Nyanja za Digitali la wanafunzi wa Idara ya Uhusiano na Masoko, Chuo Kikuu cha St. Augustine (SAUT), Mwanza.
Kabla ya hapo alikuwa amewataja rafiki zake hao wakati wa hafla ya kuchangia Kanisa Katoliki, Josephine Bakita, Parokia ya Igoma, Mwanza, Jumapili iliyopita.
Alisema hatagombea tena ubunge mwaka 2015, baada ya kuwa katika ulingo wa siasa kwa miaka 35 na badala yake ataangalia namna nyingine ya kuwatumikia wananchi huku akigusia mchakato wa kuwania urais ambao alieleza anamwachia Mungu.
“Kwa ubunge nimekwishawaeleza inatosha, sitagombea tena kwani miaka 35 inatosha, … lakini hatima yangu ni nini siwezi kujua lakini nina afya nzuri na mmoja wa wanasiasa wakongwe, wenye afya nzuri, mnaona ninavyopendeza... kwa urais namwachia Mungu tutaona,” alisema Sitta.
Kauli ya Magufuli
Akizungumza na gazeti hili nje ya ukumbi wa Bunge jana, Dk Magufuli alisema haelewi msingi wa kauli ya waziri mwenzake huyo, kwani hajui chochote katika mtandao wa urais alioutaja.
Magufuli alisisitiza kusema hana kundi, hakuwahi kuzungumza wala kuhudhuria vikao vya kundi lolote, na kwamba kundi lake ni CCM na Mwenyekiti wake ni Jakaya Kikwete.
“Sina kundi. Sijawahi kuwa na kundi na sitarajii kuwa na kundi lolote. Ninachojua kundi langu ni CCM na kiongozi wake ni mwenyekiti wake, Rais Kikwete,” alisema Dk Magufuli.
Hata hivyo, Dk Magufuli pia alipuuza taarifa kuwa alichangia harambee hiyo akisema, “Si kweli, Mwanza sijatoa hata senti na hata siku ilipofanyika hafla hiyo, nilikuwa Dar es Salaam katika mkutano na makandarasi.” Licha ya kutajwa kuwa miongoni mwa vinara wa urais 2015, Magufuli alieleza kuwa hakuwahi kuzungumza na Sitta suala hilo linalohusu makundi ya urais mwaka 2015.
CHANZO: Mwananchi
WAKATI HAYO YAKITOKEA, JANA PIA ILIKUWA SIKU CHUNGU  KWA SITTA,KAMA INAVYOONYESHA HABARI HII HAPA CHINI
Wassira amvaa Sitta
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais Mahusiano na Uratibu, Stephen Wassira, amemtaka waziri wa ushirikiano wa Afrika Mashariki Samwel Sitta, aweke wazi njia anazotumia kupambana na ufisadi nchini ambazo mawaziri wengine wa serikali ya CCM hawawezi kuzitumia.

Wakati Wassira akitaka ufafanuzi huo, Waziri wa Katiba na Sheria Mathias Chikawe kwa upande wake alikataa kuzungumzia mbinu anazotumia Samwel Sitta kwa kile alichoeleza kuwa hawezi kuongelea masuala ya serikali na mtu asiyemjua.

Wassira na Chikawe walitoa kauli hiyo jana wakati gazeti hili lilipotaka maoni yao juu ya kauli ya Sitta iliyonukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari akisema kuwa katika serikali nzima ni mawaziri wanne waliojipambanua kupambana na ufasadi na kutetea wanyonge.

Wassira alisema kwa sasa hawezi kuchangia jambo lolote juu ya kauli hiyo ya Sitta kwa kuwa hajaliona katika vyombo vya habari au kumsikia waziri huyo akisema hadharani.

Alisema kama kauli hiyo imetolewa na Sitta ni vema angefafanua mbinu anazotumia ili wengine waige.
“Mimi siwezi kuzungumzia hayo; mmeyasema nyie pia ingekuwa ni vema kama angeulizwa Sitta mwenyewe na atueleze mbinu zake tuone na wengine wanafanya nini,” alisema Wassira.

Alipoulizwa kama majina yaliyotajwa ni miongoni mwa makundi yanayodaiwa kujipanga ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM), kwa ajili ya urais wa 2015; Wassira alisisitiza jambo hilo aulizwe Sitta.

Kwa upande wake Waziri wa Katiba na Sheria Mathias Chikawe, alipopigiwa simu kwa ajili ya ufafanuzi wa kauli hiyo, alikataa kuzungumzia jambo lolote kwa madai kuwa alishajeruhiwa kwa kutoa habari kwa njia ya simu.

“Sitaki na sizungumzi mambo ya serikali na mtu nisiyemjua tena katika simu…siku moja alinipigia mtu akasema anatoka Daily News nilipompa habari akaandika anavyojua na ikaniletea matatizo, kwanza kwa sasa niko Arusha,” alisema Chikawe na kukata simu.

Juzi wakati Waziri Sitta, akishiriki harambee ya kuchangia ujenzi wa Kanisa la Mtakatifu Joseph katika Parokia ya Igoma jijini Mwanza, aliwataka Watanzania kujihadhari na watu wasio waadilifu katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwaka 2015.

Alisema watuhumiwa wa kashfa ya ufisadi wa kampuni ya kufua umeme ya Richmond na Dowans ni hatari na hawastahili kuungwa mkono katika uongozi.

Alisema kutokana na hali hiyo ya ufisadi yeye pamoja na mawaziri wengine watatu wako pamoja katika fikra za kupambana na vitendo vya kifisadi, uonevu na mikataba tata.

Aliwataja mawaziri hao kuwa ni Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard Membe, pamoja na Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli.


6 Apr 2009

MIMI SI MWANASIASA JAPO MALENGO YANGU YA BAADAYE NI KUWA MCHAMBUZI WA SIASA (POLITICAL ANALYST).BINAFSI SIICHUKII CCM ILA NAKERWA NA BAADHI YA KASUMBA ZILIZOOTA MIZIZI NDANI YA CHAMA HICHO KIKONGWE.NA KASUMBA KUU INAYONITATIZA KUHUSIANA NA CHAMA HICHO NI UNAFIKI.

JUZI JUZI TUMESIKIA KAULI ZA MMOJA WA WAKONGWE WA CCM,MZEE JOHN MALECELA,AMBAPO PAMOJA NA MAMBO MENGINE ALIAMUA "KUSIGINA DEMOKRASIA" KWA KUWATAKA BAADHI YA VIONGOZI WA CHAMA HICHO WANAOLUMBANA WAKOME MARA MOJA.>
SWALI LA MSINGI HAPA NI JE KWA KUKOMESHA MALUMBANO HAYO NDIO UFUMBUZI WA "KINACHOLUMBANIWA" UTAKUWA UMEPATIKANA?BUSARA NDOGO TU INAWEZA KUTUELEZA KWAMBA MTOTO ANAPOLIA INAWEZA KUASHIRIA KUWA ANA TATIZO (NJAA,KIU,ANAUMWA,NK).KUMFINYA MTOTO HUYO ANYAMAZE BADALA YA KUCHUNGUZA KINACHOMLIZA HAIWEZI KUWA SOLUTION YA TATIZO.

HUHITAJI KUWA MCHAMBUZI WA SIASA KUBAINI KUWA MALUMBANO YANAOENDELEA NDANI YA CCM NI MKINZANO WA WATETEZI WA UFISADI vs WAPINZANI WA UFISADI,WABINAFSI vs WANAOJUA JUKUMU LAO KWA TANZANIA,WANAFIKI vs WASEMA KWELI,NA MAKUNDI KAMA HAYO.KITU PEKEE KINACHOWEZA KUYAPATANISHA MAKUNDI HAYO NI KWA CCM KUWA WAZI-SI KWA MANENO PEKEE BALI KWA VITENDO-INASIMAMIA UPANDE UPI KATIKA MIKINZANO HIYO.IWAPO CCM IKISEMA INAPINGANA NA UFISADI HALAFU IKACHUKUA HATUA ZINAZOSTAHILI DHIDI YA BAADHI YA VIONGOZI WAKE WANAOTUHUMIWA KWA UFISADINI DHAHIRI BASI MALUMBANO YANAYOENDELEA YATAKOMA.LAKINI TUSITEGEMEE "UKIMYA" KWA HALI ILIVYO SASA AMBAPO,KWA MFANO, MTU KAMA MZEE WA VIJISENTI PAMOJA NA TUHUMA ALIZONAZO ANAENDELEA KUWA MJUMBE WA KAMATI YA MAADILI NDANI YA CHAMA HICHO.

KAULI YA MZEE MALECELA IMEANZA KUPATA SAPOTI KUTOKA KONA MBALIMBALI NDANI YA CHAMA HICHO.JANA,WAKONGWE FLANI WA CCM WAMEITISHA MKUTANO NA WAANDISHI WA HABARI AMBAPO PAMOJA NA MAMBO MENGINE WAMEKEMEA MALUMBANO HUKU WAKIONEKANA KUKEMEA BAADHI YA VIONGOZI WA CCM WALIOSHIKILIA BANGO VITA DHIDI YA UFISADI.KWA BUSARA ZA WAZEE HAWA,WANATAKA SUALA HILO LIACHWE MIKONONI MWA CCM.HIVI LAITI CCM INGEKUWA IMEMUDU KUFANYA HIVYO,AKINA MWAKYEMBE,KILANGO NA SELELII (KWA MFANO) WANGEKUWA WANAPIGA KELELE KUHUSU UFISADI?

WANACHOJARIBU KUFANYA WAZEE HAWA (PAMOJA NA MALECELA) NI KUJIAMINISHA KUWA HAKUNA TATIZO NDANI YA CHAMA HICHO,NA KELELE ZINAZOPIGWA NA BAADHI YA VIONGOZI WAKE NI SAWA TU NA UTOVU WA NIDHAMU.YALEYALE YA KUMFINYA MTOTO ANYAMAZE PASIPO KUFANYA JITIHADA ZA KUJUA KINACHOMLIZA.

KUNA WENZETU AMBAO KWA MTIZAMO WAO UKIZUNGUMZIA MABAYA YA CCM BASI UMETENDA KOSA LA JINAI.TATIZO LA WATU WA AINA HII NI KUPUUZA NAFASI YA CCM KATIKA ULINZI WA AMANI NA HATMA YA TAIFA LETU KWA UJUMLA.DHAMANA YA NCHI IKO MIKONONI MWA CHAMA HICHO KWA VILE NDICHO KILICHO MADARAKANI KWA SASA.SOTE TUNAWEZA KUBASHIRI KILICHO MBELE YETU IWAPO TUKIIRUHUSU CCM IENDESHE MAMBO INAVYOTAKA-HATA KAMA INATUPELEKA PABAYA-NA SIE TUENDELEE KUKAA KIMYA!

ANYWAY,HEBU SOMA BUSARA ZA WAZEE WETU HAWA HAPO CHINI:

Wenyeviti wastaafu wa CCM waonya

Wenyeviti wastaafu wa mikoa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wamevunja ukimya na kuwataka viongozi wa chama hicho wanaotaka kuyatumia mapambano dhidi ya rushwa kama mtaji wa kisiasa na kujipatia umaarufu, kuacha mara moja. Sambamba na hilo, wazee hao wametaka mapambano dhidi ya rushwa yasiwe kichaka cha kuficha ubovu wa uongozi na kushindwa kuwajibika. Akizungumza kwa niaba ya wenyeviti wastaafu wa chama hicho Dar es Salaam jana, Mwenyekiti mstaafu wa Mkoa wa Dodoma, Pancras Ndejembi alisema mapambano dhidi ya rushwa ni ya CCM na si mwanachama binafsi au kikundi cha wanachama wachache.

“Tunashuhudia baadhi ya viongozi wa CCM kurushiana maneno wenyewe kwa wenyewe kwa kutaka kuonyeshana nani zaidi na nani ni vinara kuliko wengine katika mapambano dhidi ya rushwa, hii si sawa,” alisema Ndejembi aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa CCM Tanzania. “Tusingependa kuona mapambano haya yanatumiwa kama njia ya kujipatia umaarufu binafsi, mwenyekiti wetu Rais Kikwete ambaye ndiye jemedari wa mapambano haya humsikii anafanya hivyo na sisi wengine tusifanye hivyo…. kama wewe ni kiongozi na hutekelezi wajibu wako kwa wapiga kura wako wakikuuliza uko wapi, usisingizie kupigwa vita na mafisadi,” walionya.

Ndejembi aliyeambatana na wenyeviti wastaafu Hemed Mkali (Dar es Salaam), Tasil Mgoda (Iringa) na Jumanne Mangara (Pwani), alisema wazee hao wamesikitishwa na malumbano ya hadharani baina ya viongozi wa CCM ambao wengine wa ngazi ya juu ya uongozi ndani ya chama. Alisema tabia inayoonyeshwa na viongozi hao ya kushutumiana, kunyoosheana vidole, kuwekeana visasi, kuonyeshana ubabe na kuwekeana nadhiri ya kupambana baina ya viongozi, kunadhoofisha na kukipunguzia heshima chama hicho.

“Lakini pia kufanya hivyo hadharani, kwa nia ya kutaka kuungwa mkono katika shutuma na visasi hivyo kunajenga chuki, uhasama na migawanyiko katika jamii, viongozi hatupaswi kuwajaza watu chuki na uhasama ndani ya mioyo yao,” alisema Ndejembi kwa niaba ya wenzake na kutaka neno ufisadi lisitumiwe kuelekea kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwakani. Alisema kumuita mtu fisadi kwenye vyombo vya habari haitoshi katika kushinda mapambano dhidi ya rushwa, bali watu waipigie kelele serikali iimarishe taasisi na vyombo vya kupambana na rushwa kama Polisi, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) na Mahakama ambako watuhumiwa wanafikishwa.

Licha ya kuwapo malumbano baina ya viongozi hao wa CCM, wastaafu hao walisema kuhitilafiana ni kitu cha kawaida na kamwe watu wasitarajie chama hicho kitameguka. Wastaafu hao walieleza kumuunga mkono Rais Jakaya Kikwete iwapo atagombea tena urais mwakani na kutaka watu wengine wamuunge mkono, kwa maelezo kuwa anafaa kuongoza nchi. Walitoa sababu za kumuunga mkono kuwa ni kukubalika na anaowaongoza, anawapenda watu wote, mvumilivu, mkereketwa wa maendeleo ya wananchi na hana jazba.

Wazee hao walisema wameamua kuzungumza na waandishi wa habari kuhusu mambo hayo ili ujumbe uwafikie viongozi, wanachama na mashabiki wa CCM, lakini yote hayo waliyoyaeleza wameshayawasilisha kwenye vikao wanavyoshiriki vya matawi na mashina na wamezungumza na viongozi wa sasa wa chamahicho. Ingawa wastaafu hao hawakuwataja kwa majina viongozi wa CCM waliolumbana hadharani, lakini hivi karibuni Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe ambaye ni mwanahisa wa Kampuni ya kuzalisha umeme wa upepo ya East Africa Power Pool, amelumbana na Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz.

Dk. Mwakyembe anadai Rostam anatumia vyombo vyake vya habari kumchafua huku Rostam akitaka mbunge huyo ambaye kitaaluma ni mwanasheria na mwandishi wa habari, kuelezea mgongano wa maslahi wakati alipochaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini. Mbali na wazee hao, pia Makamu Mwenyekiti mstaafu wa CCM Tanzania Bara ambaye ni Mbunge wa Mtera, John Malecela alitaka malumbano hayo yakome, kwani hayana faida kwa mwananchi na wahusika watumie vyombo husika vya chama kufikisha malalamiko yao.
CHANZO:
HabariLeo

WITH ALL DUE RESPECT,BAADHI YA HAWA WAZEE NDIO WAMETUFIKISHA HAPA TULIPO KUTOKANA NA ITIKADI HIZIHIZI ZA "KUJENGA UMOJA NA MSHIKAMANO NDANI YA CHAMA" PASIPO KUANGALIA ATHARI ZAKE KWA JAMII KWA UJUMLA (AFTERALL,SIO KILA MTANZANIA NI MWANA-CCM).

HATUJACHELEWA.INAWEZEKANA IWAPO UZALENDO NA MASLAHI YA TAIFA YATAWEKWA MBELE YA (in front of) KUJIPENDEKEZA NA UNAFIKI.

27 Feb 2008

Makala yangu ndani ya toleo la wiki hii la gazeti la Raia Mwema inazungumzia UNAFIKI: Ule wa Profesa Mwandosya kuitaka Dawasco isiwataje hadharani mawaziri wanaodaiwa maji na Mamlaka hiyo;ule wa Askofu Thomas Laizer wa KKKT Dayosisi ya Arusha kutumia neno la Bwana kuwapiga vijembe wanamwandama Lowassa,na ule wa "mabilioni ya EPA yanayorejeshwa kwa kasi."Makala hiyo imeanza kwa stori za hapa na pale,mambo ya muziki wa kufokafoka na albamu ya Jay-Z ya American Gangster ilivyosahau matatizo ya Black Americans.Stori hizo ni zinaunganishwa katika namna ile ile ya conversational style,napenda sana makala iwe mithili ya kupiga stori na msomaji,iwe kijiweni,kwenye pub,au hata barazani.Pamoja na habari na makala zilizokwenda shule,bingirika na makala hiyo kwa KUBONYEZA HAPA

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.