16 Nov 2011





Mishahara mipya kwa wabunge ni ujambazi

Uskochi
AWALI, nilitaraji wiki hii ningeendelea na uchambuzi wangu kuhusu changamoto mbalimbali zinazovikabili vyama vyetu vya siasa nchini kuelekea Uchaguzi Mkuu ujao, mwaka 2015. Lakini wakati najiandaa kuingia kwenye mada hiyo nikakutana na habari ambayo siyo tu ilinitia hasira bali pia ilinichefua.
Habari yenyewe inahusiana kwa namna fulani na mada niliyozungumzia wiki iliyopita katika safu hii, yaani suala la unafiki. Wakati unafiki niliouchambua ulihusu sakata la ushoga (kufuatia tamko la Waziri Mkuu wa Uingereza kwamba nchi yake inafikiria kuzikatia misaada nchi zinazominya haki za mashoga), unafiki ninaouzungumiza leo unahusu baadhi ya wabunge wetu.
Wiki iliyopita, vyombo mbalimbali vya habari huko nyumbani viliripoti kwamba baadhi ya wabunge wetu wamekumbushia “kilio chao cha siku nyingi” wakidai posho na mishahara yao viongezwe. Naomba nitamke mapema kuwa huu ni ujambazi wa mchana kweupe (daylight robbery).
Ninatambua kuwa waheshimiwa wetu wamezoea kusifiwa tu hata pale wanapoongea masuala yasiyo na msingi na sitashangaa iwapo hitimisho langu kwamba madai yao ya kuongezewa posho na mishahara ni ujambazi, likaibua malalamiko makali kutoka kwao.
Lakini kwa vile Tanzania haiwezi kuendelea kufanywa shamba la bibi la walafi wachache (ambao zama za Mwalimu Nyerere tuliwaita kupe wanaoishi kwa kutegemea jasho la wengine) ni lazima tuwakemee watu hawa pasipo uoga wala aibu.
Ili kuelewa kwa nini nimeandika kuwa wanachofanya wabunge wanaodai nyongeza ya posho na mishahara ni unafiki wa hali ya juu (na kuufananisha na ujambazi) ni muhimu kusikia hoja zao za ovyo ovyo zinazojaribu kuhalalisha wanachodai.
Mbunge wa Rombo kupitia CHADEMA, Joseph Selasini, alinukuliwa na gazeti moja akidai kuwa eti “uwakilishi umekuwa mzigo kwani wakati mwingine amekuwa akitumia fedha anazopata kwenye vyanzo vyake binafsi kuwatumikia wananchi.”
Gazeti hilo liliendelea kumnukuu mbunge huyo akisema kwamba “Hapa nina mialiko 26 ya kwenda kuchangia ujenzi wa shule na shughuli nyingine za maendeleo kule Rombo, zote hizi zinanihitaji kama mbunge nitoe fedha, sasa jamani fedha hizi zinatoka wapi?”
Swali analopaswa kuulizwa Selasini na wabunge wenzie wenye mawazo kama yake ni hili: “kama uwakilishi ni mzigo, nani alimshikia mtutu wa bunduki kwamba lazima agombee uwakilishi huo? Na kama wakati anagombea ubunge hakufahamu kuwa kutumikia umma ni jukumu linalohitaji kujitoa muhanga kwa nini basi asitue mzigo huo?
Haihitaji japo kozi ya saa chache ya jinsi ya kutumia busara zetu ipasavyo kutambua kuwa kama umewania nafasi fulani na kuipata lakini hatimaye unagundua kuwa nafasi hiyo ni mithili ya mzigo mzito wa gunia la misumari, kinachopaswa kufanywa siyo kudai (tena kwa ubabe badala ya unyenyekevu) usaidiwe bali kuacha nafasi hiyo kwa wenye uwezo wa kuimudu.
Kwa hiyo kama Selasini anaona jukumu la uwakilishi linamfilisi basi kuna shughuli nyingi tu za kufanya ambazo hazitamfanya alalamikie “mshahara na posho kidogo.” Anaweza kabisa kuachana na ubunge na akabaki na jukumu dogo la kuhudumia familia yake pasipo kutaka kuwabebesha walipakodi wa Kitanzania mzigo mkubwa zaidi ya wanaoubeba sasa kuhudumia maisha ya kitajiri ya wabunge wetu.
Lakini katika kuonesha kuwa tuna tatizo kubwa na baadhi ya watu tuliowakabidhi dhamana ya kutuwakilisha, Selasini ananukuliwa na gazeti hilo akikiri kwamba “...wabunge hukutana na kero ya wananchi kuomba fedha ili wakatatue matatizo yao mbalimbali na kwamba ni vigumu kukwepa jukumu hilo kutokana na hali ya maisha ilivyo sasa nchini.”
Ahaa, kumbe wakati anaomba kuongezewa posho na mshahara anafahamu fika kuwa wanyonge anaotaka wakamuliwe zaidi ili posho na mishahara ya wabunge iongezwe si tu wana matatizo mbalimbali bali pia wanakabiliwa na hali ngumu kutokana na hali ya maisha ilivyo sasa nchini.
Sijui tatizo la wabunge kama Selasini ni kuishi katika sayari nyingine ambayo wenye haki ya maisha ya anasa ni wao tu au ni ulafi tu wa kutaka kila kidogo tulichonacho kikusanywe na kukabidhiwa wao wenye mahitaji muhimu kuliko wanyonge “wanaopigika” tangu mawio hadi machweo.
Naye Mbunge wa Mtera kwa tiketi ya CCM, Livingstone Lusinde alinukuliwa akiitaka Ofisi ya Spika, Anne Makinda, kufanya jitihada za kuwaelimisha wananchi kuhusu wajibu wa mbunge ili wafahamu kazi nyingine wanazofanya wawakilishi hao wa wananchi ni nyongeza nje ya majukumu yao ya msingi.
Lusinde alidai kwamba “Malipo yetu ni kidogo sana, hayatoshelezi kabisa lakini wananchi tunaowawakilisha hawatuelewi katika hili, maana wanadhani tuna fedha nyingi, sasa hapa kuna tatizo. Nadhani kuwapo utaratibu wa kuwaelimisha, wajue hata kazi nyingine tunazofanya siyo wajibu wetu ila tunajitolea na nyingine hizi zina gharama kubwa.”
Huu ni zaidi ya unafiki. Ni matusi kwa Watanzania masikini. Hivi Lusinde anafahamu pato la Mtanzania wa kawaida ni kiasi gani? Hivi kigogo huyu ana taarifa zozote kuhusu kuporomoka kwa kasi thamani ya shilingi yetu? Na anaposema hayo mamilioni wanayolipiwa ni kidogo anataka kutuambia kiasi gani ndio stahili kwa mbunge wa nchi yetu masikini kabisa duniani?
Ni hivi,  Lusinde sio kwamba wananchi mnaowawakilisha hawawaelewi kwa nini mnadai marupurupu zaidi ya hayo makubwa kabisa mnayopata sasa. Wasichowaelewa ni mnaishi sayari gani? Hivi mnapolalamika kuwa mamilioni mnayolipwa hayawatoshi, watumishi wengine wa umma kama vile walimu, madaktari na wengine waseme nini?
Tatizo la waheshimiwa hawa wakishapata kura wanageuka viumbe tofauti kabisa na wale waliokuwa wakijifanya wana uchungu kweli na wapiga kura wao. Wanasahau kuwa wengi wa wananchi waliowapigia kura waheshimiwa hao kuingia bungeni ni masikini wa kutupwa na hawana wa kumlalamikia (na hata wakilalamika ni kazi bure maana wawakilishi wao nao wapo ‘bize’ kulalamikia mishahara na posho).
Labda msomaji mpendwa unaweza kuwa unajiuliza ninapoandika waheshimiwa hawa wanapata mishahara ya mamilioni ninazungumzia kiasi gani hasa. Kwa hesabu za haraka haraka, mshahara wa mbunge ni Sh milioni 2.3 kwa mwezi na pamoja na posho kiwango cha juu anachopokea kwa mwezi kinafikia takriban shilingi milioni saba.
Hivi mtu anayelipwa shilingi milioni saba kwa mwezi lakini bado “analilalia” kuwa fedha hizo hazitoshi tumwite jina gani? Binafsi nimehitimisha hapo awali kuwa huu ni ujambazi wa mchana kweupe kwa sababu wanachofanya wabunge wanaodai maslahi zaidi ya hayo lukuki wanayopewa ni matusi kwa mamilioni ya Watanzania ambao, wastani wa pato la kila mmoja wao kwa mwaka ni dola za Marekani 500  (takriban shilingi 870,000). Kwa maana hiyo, kwa wastani, pato la Mtanzania kwa mwezi ni shilingi 70,000.
Sasa kuna uhalali gani kwa wabunge kutoridhika na mshahara ambao ni takriban mara 100 ya “mshahara” wa Mtanzania wa kawaida (yaani pato la wastani kwa mwezi)? Ninafahamu kuwa waheshimiwa wabunge hawatopenda kusikia nikihitmisha kuwa neno pekee mwafaka la kuelezea hali hii ni ujambazi lakini huo ndio ukweli wenyewe.
Kwa lipi hasa wanalofanya huko bungeni hadi wadai kuwa malipo mara 100 zaidi ya Mtanzania wa kawaida hayawatoshi? Kama ubunge umekuwa mzigo basi waachie ngazi. Kuna haja gani ya kuwa na watu zaidi ya 300 wanaolipwa mamilioni ya fedha huku nchi ikizidi kuwa masikini tena siyo kwa bahati mbaya bali ni matokeo ya wengi wa wabunge hao kutanguliza mbele maslahi ya chama (na matumbo yao) badala ya yale ya walalahoi waliowatuma kuwawakilisha?
Nimalizie kwa kutoa rai kwa Watanzania wenzangu kufuatilia kinachoendelea hivi sasa kwenye nchi tajiri kama Marekani, hapa Uingereza na kwingineko ambapo umma umeamua kuingia mtaani katika kile kilichoanza kama “Occupy Wall Street” na sasa kinaelekea kusambaa sehemu mbalimbali duniani. Lengo la harakati hizo ni kupinga tamaa na ulafi wa taasisi za fedha hususani benki. Lakini lengo kubwa zaidi ni kupambana na mfumo wa kiharamia ambao mwenye nacho si tu anaongezewa bali anafanya ujambazi kuwapora wale wasio nacho.
Nanyi wabunge nawasihi muache matusi dhidi ya mamilioni ya walalahoi wa Kitanzania ambao licha ya mzigo mkubwa mnaowabebesha kumudu kuwalipa ninyi posho na mishahara yenu ya kufuru, muda huu hawajui watamudu vipi mlo ufuatao, achilia mbali mlo wa siku inayofuata.
Msipoacha kebehi zenu kuwa mamilioni mnayolipwa hayatoshi na mnataka zaidi, ipo siku mtashitukia mkipita mitaani mkiwa ndani ya magari yenu ya kifahari mnakumbana na makelele ya “mwizi, mwizi...” Labda hiyo ndio itawashitua mtambue kuwa ninyi ni wabunge wa nchi masikini kabisa duniani na mishahara na posho mnazopewa sasa haziendani hata chembe na umasikini wetu.





Miraj Kikwete (kushoto)


MTOTO wa Rais Jakaya Kikwete, Miraj Jakaya Kikwete, amekitetea Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), akipinga chama hicho kuhusishwa na vurugu mbalimbali zinazotokea nchini, zikiwemo zile za Wamachinga, zilizotokea jijini Mbeya hivi karibuni.

Mtoto huyo wa Rais alionyesha kukerwa na watu wenye mtazamo wa kukisingizia chama hicho kikuu cha upinzani kwa kukihusisha na vurugu, wakati hali halisi inaonyesha wazi kuwa wananchi wenyewe hawaridhishwi na hali ya mambo ilivyo na hivyo kuamua kuwa mstari wa mbele kupigania haki zao.

Miraj aliweka wazi msimamo wake huo kupitia mtandao wake wa facebook akichangia mjadala mzito uliohoji kwa nini CHADEMA inasingiziwa vurugu Mbeya?

Mtoto huyo wa Rais, aliweka wazi ujumbe wake huo baada ya mchangiaji mmoja, kuchangia kwa jazba akitabiri machafuko kutokea kabla ya 2015.

Mchangiaji huyo alisema yeye si mtabiri, lakini kwa hali ilivyo nchini, tunaelekea kwenye vita na haina hata mpito wa chaguzi mbili mbele kwa maana ya 2015 na 2020.

Mchangiaji mwingine, Gallus Mpepo, ambaye ndiye aliyekuwa akijadiliana na Miraj, alianza kwa kumrushia lawama Mkuu wa Mkoa mpya wa Mbeya, Abbas Kandoro, kwamba kila mkoa anaokwenda, amekuwa ukikumbwa na vurugu za Wamachinga.

Mpepo alisema anashangaa kuona baadhi ya wachangiaji wa mjadala huo, wanahusisha vurugu za Mbeya na maandamano ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), licha ya kwamba chanzo chake kiko wazi kwamba wafanyabiashara hao walikuwa wakipinga kuondolewa kwenye maeneo yao ya biashara bila kupewa maeneo mbadala.

Alisema hii inatokana na hali ya kutaka kuficha makosa yaliyofanywa na uongozi wa mkoa huo chini ya Kandoro, kutoongoza kwa busara katika kutatua kero za wananchi.

Katika ujumbe huo, Mpepo alieleza kufurahishwa na ujumbe wa mtoto wa Rais Kikwete na kwamba ameupenda ufafanuzi wake kuhusu mjadala huo.

Akichangia mjadala huo, Miraj ambaye ni nadra kujihusisha na masuala ya siasa, alihoji nani anayedai haki Mbeya kati ya CHADEMA na wananchi hadi kusababisha vurugu hizo.

Mtoto huyo wa Rais Kikwete alisema ni makosa kuihusisha CHADEMA na vurugu hizo kwani CHADEMA si nchi.

“CHADEMA si nchi ni chama na si kwamba wanachama wa CHADEMA ndio pekee wenye shida na matatizo, ni Watanzania wote,” alisema mtoto huyo wa Rais.

Miraj alienda mbali kwa kusema ni fikra potofu kufanya kama vile kuna Tanzania na CHADEMA.

“Maana serikali ndiyo Tanzania na CHADEMA ni chama ndani ya Tanzania, ni chama cha Watanzania kwa ajili ya Watanzania, kama kilivyo Chama cha Mapinduzi (CCM), NCCR-Mageuzi na kadhalika.

“Tofauti ni harakati na sera... tupendane Watanzania, tutafika mbali kwa umoja na mshikamano wetu na wala si kwa kejeli na matusi…, wenye haki tuwasimamie wote na penye haki tusimame sote,” alisema Miraj


12 Nov 2011

Vitanda vilivyokuwa vikitumiwa na wangonjwa katika Zahanati ya Ipinda, iliyopo Mwanjelwa jijini Mbeya vikiwa wazi baada ya wagonjwa kukimbia mara baada ya bomu la machozi lililopingwa na Jeshi la polisi kutua ndani ya Wadi

02. Mgonjwa aliyekuwa akitibiwa Zahanati hapo akiwa amezirai baada ya bomu la machozi lililopingwa na Jeshi la polisi kutua ndani ya Wadi.

03.  Mganga Mkuu wa zahanati ya Ipinda jijini Mbeya Dk. Lute Kibopile ambaye pia ni mmiliki wa zahanati hiyo akionesha Bomu la machozi lililopigwa na Jeshi la polisi na kuingia ndani ya Wadi.

04.  Mganga Mkuu wa zahanati ya Ipinda jijini Mbeya Dk. Lute Kibopile ambaye pia ni mmiliki wa zahanati hiyo akielezea jinsi bomu la machozi lilivyopingwa.

05. Muuguzi akionesha eneo ambalo bomu la machozi lilipotua katika Zahanati ya Ipinda, eneo la Mwanjelwa jijini Mbeya.

06. Mtaalamu wa masuala ya maabara katika Hospitali ya UHAI BAPTIST Dk Ngangele Lisukile akiwa ameshika kigae kilichodondoka mara baada ya bomu la machozi lililopingwa hospitalini hapo majira ya saa 5:30 asubuhi.
 CHANZO:  www.mbeyayetu.blogspot.com
:

11 Nov 2011





Tatizo ni unafiki wetu, si ushoga

Uskochi
MOJA ya mambo yaliyonishitua sana nilipofika hapa Uingereza kwa mara ya kwanza ni jinsi Ukristo ulivyopoteza nguvu yake (hususan mahudhurio kanisani na watu wanaofuata Ukristo). Kilichonishitua ni ukweli kwamba Ukristo uliletwa huko nyumbani na “wazungu” hawa na nilitarajia wangekuwa wacha Mungu wakubwa.
Dalili za Ukristo kupoteza nguvu yake zinaonekana katika namna makanisa yanavyoishia kugeuzwa kumbi za starehe baada ya kukosa waumini. Kadhalika, asilimia kubwa ya waumini makanisani ni wageni kutoka nje ya nchi hii. Na japo Malkia wa Uingereza ni Mkuu wa Kanisa la Anglikana na Askofu Mkuu wa Canterbury ni mithili ya Baba Mtakatifu (Papa) kwa Kanisa hilo, idadi kubwa ya Waingereza inajitambulisha kama watu wasiofuata dini. Na kuna kundi kubwa tu la wanaojitambulisha kama Wakristo lakini wasiotia mguu kanisani.
Hakuna jibu jepesi kuhusu kwa nini Ukristo unazidi kupoteza nguvu nchini hapa lakini baadhi ya watu niliowahoji wanadai huenda maendeleo katika nyanja mbalimbali ni chanzo kwa baadhi ya watu “kupuuza” umuhimu wa imani katika maisha ya mwanadamu.
Lakini pamoja na Ukristo kupoteza nguvu yake miongoni mwa Waingereza, kwa kiasi kikubwa uadilifu katika nyanja mbalimbali za maisha umeendelea kuwa wa kiwango cha juu. Na hapa ndipo unaweza kubaini tofauti kubwa kati ya Waingereza “wanaopuuza dini” na akina sie huko nyumbani ambao dini inaonekana kuwa sehemu muhimu kwa maisha yetu.
Neno mwafaka linaloweza kuelezea tofauti hiyo ni UNAFIKI. Ni hivi, ni bora kuwa na watu wasio na dini au wasioabudu uwepo wa Mungu lakini wakaishi na kutenda mambo kiadilifu kuliko kuwa na ‘washika’ dini wasiokosekana makanisani au misikitini lakini uadilifu wao ni haba kama sio sifuri kabisa.
Na suala la unafiki linaweza kuchukua nafasi muhimu katika mjadala mkali uliosababishwa na kauli ya Waziri Mkuu wa Uingereza kuwa nchi yake itasitisha misaada kwa nchi zinazokiuka haki za mashoga. Tayari Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, ameweka bayana msimamo wa Serikali kwamba Tanzania ipo tayari kukosa misaada ya Uingereza kuliko kubadilisha sheria za nchi zinazopiga marufuku ushoga.
Lakini kabla sijaingia kwa undani katika kujadili suala hili ni vema nikaweka wazi msimamo wangu. Imani yangu kama Mkristo wa madhehebu ya Katoliki (ambaye almanusura ningekuwa padre iwapo nisingeghairi kujiunga na seminari mwaka 1986) sio tu inapinga ushoga bali pia inauona kama dhambi. Kwa hiyo, naomba ifahamike kuwa lengo la makala hii si kuunga mkono ushoga.
Kwa upande mmoja, Waziri Mkuu wa Uingereza, David Cameron, alikuwa na haki ya kuweka masharti katika misaada wanayotoa. Ifahamike kuwa misaada hiyo inatokana na fedha za walipa kodi wa Uingereza na inatarajiwa ielekezwe kwa nchi zinazoonekana machoni mwa Waingereza kama zinazoendana na maadili yao. Na moja ya masuala yanayopewa kipaumbele na nchi hii ni haki za binadamu (ikiwa ni pamoja na haki za mashoga).
Kwa hiyo basi si kwamba Cameron alikurupuka tu na tamko hilo ambalo baadhi ya wenzetu wamelitafsiri kama ajenda ya kueneza ushoga, bali anawakilisha hisia za wananchi wake ambao kimsingi ndio chanzo za fedha tunazopatiwa kama misaada.
Ni wazi kuwa kiongozi yeyote yule anayejua anachofanya atahakikisha anasimama upande wa wananchi wake. Kwa mantiki hiyo wananchi wake wanapotaka fedha yao wanayotupatia kama msaada ielekezwe tu kwa nchi zinazojali haki za binadamu (ikiwa ni pamoja na haki za mashoga) tu basi hana budi kufanya hivyo.
Japo siungi mkono ushoga lakini ninaelewa mantiki ya Cameron kutoa tamko hilo linaloakisi matakwa ya wananchi wake. Lakini kwa vile matakwa ya Waingereza kuhusu haki za binadamu hayaishii kwa mashoga pekee, ingeleta maana zaidi iwapo tishio la kukata misaada lingeelekezwa pia kwenye tatizo sugu la rushwa (na ufisadi kwa ujumla) ambalo si tu linakwaza haki za binadamu za masikini (ambao ni wengi kuliko mashoga) bali pia linaweza kusababisha wanyonge kupoteza maisha (kwa mfano rushwa inayowezesha  vyombo vya usafiri vyenye hitilafu kuendelea na kazi na hatimaye kusababisha ajali).
Sasa nigeukie unafiki unaoandamana na jinsi tamko la Cameron lilivyopokelewa. Haihitaji utafiti wa kina kubaini kwamba si tu Tanzania (na nchi nyingine zinazolengwa na tishio hilo la kukatiwa misaada) ina mashoga lakini pia ushoga unazidi kuongezeka. Hivi nani anayesoma magazeti ya burudani au blogu hajamwona shoga mmoja aliyejipachika jina Seduction ambaye ni kama yupo kwenye kila shughuli za mabinti maarufu jijini Dar?
Nilipokuwa huko nyumbani mwaka 2005 na niliporejea tena mwaka 2008 nilishuhudia idadi kubwa tu ya mashoga katika maeneo mbalimbali ya burudani jijini Dar es Salaam. Na uchunguzi usio rasmi ulionesha kuwapo kwa mashoga kwenyekitchen parties ni kama suala la kawaida tu. Nilibaini kwamba kumbi za muziki wa mwambao zilikuwa ni chaguo kubwa la mashoga.
Lakini jambo moja la wazi ni kwamba hakukuwa na upinzani, chuki au hasira dhidi ya mashoga hao. Na sijawahi kusikia kuna shoga amekamatwa na polisi, kupelekwa mahakamani na hatimaye kufungwa kwa “kosa” la kuwa shoga. Na ukidhani hilo la kutokamatwa kwa mashoga ni la kushangaza sana, basi kubwa zaidi ni uteuzi wa kigogo mmoja (mstaafu sasa) wa shirika la umma ambaye kila aliyemjua alikuwa anafahamu  tabia yake ya ushoga (kwa maana ya tendo la ndoa na watu wa jinsia yake).
Nina hakika aliyemteua alikuwa anafahamu hilo lakini haikuzuia kigogo huyo kupewa nafasi ya kufisadi shirika hilo hadi alipoondoka huku akijimwagia sifa za vichekesho.
Tuache unafiki, hivi maadili tunayodai ni haya ya wengi wa vigogo wetu kutumainia waganga wa kienyeji katika kila wanalofanya? Maadili haya ya “wachunga kondoo wa Bwana” kuishi maisha ya kifahari kama matajiri wakubwa ilihali waumini wao hohehahe wakihimizwa kuongeza kiwango cha sadaka? Au maadili haya ya Wakristo na Waislamu wasiokosekana kwenye nyumba za ibada lakini ndio wahusika wakuu wa ufisadi? Au haya ya ushirikina kuwa muhimu kuliko kumtumainia Mungu?
Au maadili tunayodai kuwa nayo ni haya ya majambazi wanaotupora utajiri wetu kisha kuibukia makanisani au misikitini na kutoa sadaka au zaka kubwa (iliyotokana na fedha ileile waliyotuibia)? Au maadili tunayodai Waziri Mkuu Cameron anayapuuza ni haya ya wengi wa wasanii wetu wa kike kwenye fani ya filamu ambao licha ya kupendelea kuvaa nusu uchi, hawana mishipa ya aibu kutangazia umma uchafu wanaofanya katika maisha yao? Maadili haya ya wasanii wa Khanga Moja na Kitu Tigo wanaoigiza u-Sodoma na Gomora hadharani kwa kisingizio cha burudani lakini hakuna wa kuwachukulia hatua?
Ni maadili gani anayozungumzia Kikwete na Waziri wake Membe ilihali katika hotuba yake iliyogusia mafisadi wa EPA alikumbushia umuhimu wa haki zao za binadamu (na ikambidi aliyekuwa Spika, Samuel Sitta, amkumbushe Rais kuwa haki za wananchi ni muhimu kuliko za mafisadi)?
Mbona hakukuwa na maandamano ya kumlaani Kikwete kwa kutetea haki za binadamu ambao ni mafisadi lakini leo tunawalaani Waingereza kwa kutishia kutunyima fedha zao kama tusipofuata matakwa yao?
Lakini unafiki mkubwa zaidi ni huu: viongozi hawa hawa ambao licha ya kukiri hadharani kuwa hawajui kwa nini nchi yetu ni masikini (labda pia hawajui kwa nini waliamua kutuongoza) pia ni washiriki wakubwa wa ufisadi unaotufanya tuishi kwa kutegemea fadhila za wafadhili kama Uingereza, wanatuhadaa kuwa ni bora tunyimwe misaada kuliko kukiuka maadili yetu. Lakini wababaishaji hawa hawatuambii jinsi watakavyofidia pengo litakalotokana na kukatwa misaada hiyo.
Na hawatuambii kwa sababu hajui watafidia vipi na hawajali kwa vile wao hawataathiriwa na kukatwa misaada hiyo. Na kama ambavyo tatizo la umeme linavyodumishwa na mafisadi ili kujaza akaunti za vijisenti huku nje, si ajabu tukikatiwa misaada mafisadi watapata kisingizio kipya cha “imebidi mabilioni haya ya shilingi yatumike kufidia pengo lililotokana na uamuzi wa Uingereza kutukatia misaada.”
Nimalizie makala hii kwa kutamka bayana kuwa kama ambavyo sipingi uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi kwa vile hainihusu mie Mkristo, sina tatizo na kurekebisha sheria za ushoga kwa vile si tu mashoga wapo na wanazidi kuongezeka (na hakuna anayewachukulia hatua kwa kuvunja sheria) lakini pia sheria hizo hazinihusu mimi au yeyote yule asiye shoga.

9 Nov 2011


Sad news out of Los Angeles this evening, as TMZ reports that rapper Heavy D has died.

The 44-year-old star, who found fame with his 1991 hit Now That We Found Love and appeared in several movies, was reportedly rushed to a hospital this afternoon after a 911 call was made from his

Officials tell TMZ that no foul play is suspected, and they are investigating the death.

Heavy D, whose real name is Dwight Arrington Myers, had just performed at two special events last month: the Michael Jackson tribute concert in Wales and the BET Hip Hop Awards in Atlanta. He also has a minor role in the new Eddie Murphy comedy Tower Heist.

The overweight star tweeted a simple final message earlier today: "BE INSPIRED!"

Famous fans from throughout Hollywood are taking to Twitter to remember Heavy D and express shock at his sudden death. A roundup of who's saying what:

-Samuel L. Jackson: "Ahhh man! Heavy D?! Dwight wz a dear friend. Fond memories of a truly cool brutha."

-Usher: "This is too heavy, I can't believe it. HEAVY D was just here. Truly gone too soon. My heart and support goes out to his family. R.I.P HEAVY"

-Ne-Yo: "Man. I was just with Heavy D recently in London. Had I known it'd be the last time I'd see him, I woulda told him he was truly great. RIP..."

-LL Cool J: "May GOD embrace the soul of Heavy D and Bless his family. I respected you Heavy and I always will."

-Fred Savage: "Rest in Peace Heavy D. You provided the soundtrack to some of the best times of my teenage years. Your music will always make me smile."

-Eve: "RIP HEAVY D... Sending my prayers and condolences to family and friends"

-Joel Madden: "Heavy D was a truly positive and uplifting man. Rest in peace Heavy. Its a very Sad day today."

-Keyshia Cole: "When I met Heavy D.. He said 'believe U have a good soul, Sing with always having Something to say'"

-Big Boi: "R.I.P Heavy D a true pioneer may god bless your soul"

-Sinbad: "It is a sad day today .. My younger yellow brother from another mother 'heavy D' passed away today. I loved that brother. He was a good man"

-Alyssa Milano: "Heavy D gave me advice when I was pregnant. He said, 'Cherish every single moment. It goes by way too fast.' Rest in peace, Heavy D."

-Jill Scott: "Oh my heart aches!! In shock. Can't believe Heavy D is gone. Such a positive sweet hearted man. Please pray for his daughter."

-Wilmer Valderrama: "We have lost another member of Hip Hop's legacy, a TRUE Rap legend... 'Heavy D' RIP...... WV"

-Missy Elliott: "U will be missed Heavy D so many laughs we've shared but your Music is Timeless and will Always be Around 4ever Love u Heav..."


7 Nov 2011


CHANZO GLOBAL




So homosexuality is unAfrican? What about living on handouts?

For a country that once had ambitions of becoming a self-reliant nation, Tanzania is a surprisingly donor-dependent place.

The Arusha Declaration, Julius Nyerere’s blueprint for socialism and self-reliance, argued that dependency on external economic assistance would be detrimental to the country’s independence.

In a brief but closely argued document, a strong case was made for reliance on our own resources and treating foreign aid with care, especially shunning financial grants, for whereas loans and credit lines impose the responsibility of repayment, free money makes the recipient a virtual beggar and keeps him beholden to the donor.

And yet Tanzania, even under the old man himself, went ahead and accepted foreign money, loans and grants, in huge sums, especially in sectors such as education, health and water and sanitation.

The dependency grew so great that when Olof Palme, the Swedish social democrat who had underwritten Nyerere’s education programme, lost power, Tanzanians felt the impact probably more acutely than the Swedes.

The rightwing government that came in scrapped the whole aid package to Tanzania, declaring, rather cruelly, that we had become a bottomless pit.

Since then our education programmes have struggled, our schools have staggered along, and our rulers have remained largely clueless as to what we need to do to liberate ourselves from the mire of growing dependency.

Indeed, a few years ago we reached some benchmark that convinced our donor countries that we had become a highly indebted poor country (HIPC). And we celebrated with a beggar’s dance, bowl in hand.

Our government has continued to borrow and to receive cash handouts in what has come to be known as general budget support (GBS) that gives it unfettered licence to place those monies wherever it pleases.

At some stage in the past, our beggar practices were streamlined in such a way that we could only borrow or beg to meet capital, or development programmes.

Now we can borrow to pay government employees and other charges (OT), which gives dependency a new and menacing dynamic.

This has meant that when a donor government decides to withdraw its GBS grant, the beggar government finds itself in an awkward situation, for whereas a road construction programme can easily be put off or postponed, civil service pay and running the government cannot.

So, when the Brits announced, a couple of weeks ago, that they intend to cut their GBS handouts, the Tanzanian government put on a brave face, making it appear like it was a small matter. But it’s likely to hurt.

All this was, of course, before David Cameron made his remarks about his intention to cut aid to governments that suppress homosexual rights, so we don’t know what the real motive for the aid cut was.

African men are a macho lot, and for many the very idea of a man-on-man sexual partnership is anathema.

Woman-on-woman also. A man was created specifically to have liaison with a woman, and a woman was created as a tool, exclusively to serve the man, in both productive and reproductive pursuits.

It is inconceivable that two such tools would dream of having a liaison other than with the man.

Rather like the tractor dating the combine harvester on the farm.

Apart from the viewpoint of a woman being a centre for economic and biological production, I do not have much against those who claim that homosexuality is un-African.

But let us push this macho thing to its logical conclusion.

No self-respecting African man would let another man pay for his and his wife’s and his children’s upkeep.

Indeed, a man who allows that to happen would be considered as having been married by the provider man, call them economic homos. Rejecting the one, reject the other too.

SOURCE: The East African

6 Nov 2011

CCM dhaifu mtaji imara wa urais CHADEMA, CUF

Uskochi
NIANZE makala hii kwa kutoa salamu za pongezi kwa jarida hili la Raia Mwemaambalo limetimiza miaka minne tangu kuanzishwa Oktoba 30, 2007. Binafsi, jarida hili limekuwa sehemu muhimu ya maisha yangu tangu nilipopewa fursa ya kuandika safu hii.
Lakini kubwa zaidi ni jinsi jarida hili lilivyosimama imara na kuwa sauti ya wasio na sauti (wanyonge), likifukua ufisadi na kuhabarisha umma pasipo upendeleo.
Pasi na shaka yoyote, Raia Mwema linastahili kuitwa gazeti la rekodi, yaani unaloweza kulitumia kunukuu chochote kile bila hofu kuwa huenda kimekosewa au kimeandikwa kwa unazi. Sitoi sifa hizi kwa vile ni mwandishi wa makala gazetini humu lakini ninaamini kila anayependa kuhabarishwa kwa ufasaha na umakini ataafikiana nami kuwa Raia Mwema limeonyesha njia sahihi ya uandishi wa habari na makala.
Baada ya pongezi hizo za dhati nielekee kwenye mada ya wiki hii. Mada hii ni mwendelezo wa ile ya wiki iliyopita ambayo iliangalia mazingira yanayotarajiwa ya chama tawala katika kuelekea Uchaguzi Mkuu ujao hapo mwaka 2015.
Wiki hii ninajaribu kuangalia hali ilivyo katika vyama viwili, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na Chama cha Wananchi (CUF), ambavyo kwa sasa vinastahili kuitwa vyama vikuu vya upinzani.
Urais ndani ya CUF
Kuna msemo mmoja wa Kiingereza ambao katika tafsiri yake ya Kiswahili ni kama hivi: “Jambo zuri si lazima liwe jambo sahihi.” Kwa mfano, kumpatia chakula kingi mtu mwenye njaa kali kunaweza kusababisha kumuua mtu huyo bila kukusudia.
Mantiki ya usemi huo ni kwamba kuna nyakati tunafanya mambo kwa kuamini ni vizuri kufanya hivyo, lakini matokeo yake yanaweza kuwa mabaya kuliko matarajio. Kwa kurejea msemo huo wa Kiingereza, sote tunafahamu kuwa mtu mwenye njaa kali anahitaji chakula.
Lakini kabla ya kumpatia chakula ni vema kumpatia kinywaji cha moto kama vile chai au uji (kama wanavyofanya watu waliofunga). Kumpatia mtu huyo ugali mwingi kunaweza kusababisha akavimbiwa na pengine kuishiwa pumzi au hata kumpotezea uhai.
Chama cha CUF kililazimika kukaa meza moja na wapinzani wao wa CCM huko Zanzibar na hatimaye kufikia mwafaka na kuunda Serikali ya Umoja wa Kitaifa. Hilo lilikuwa jambo zuri (kama kumpatia chakula mtu mwenye njaa kali).
Lakini matokeo ya uamuzi huo wa busara yameiacha CUF huku Bara (na pengine hata huko Zanzibar) ikiwa haina mwelekeo. Kimsingi, chama hicho ni nusu ya serikali inayotawala kwa vile kimetoa Makamu wa Kwanza wa Rais kuongoza Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
Na katika kutekeleza kanuni ya uwajibikaji wa pamoja, CUF hawawezi kuinyooshea kidole CCM huko Zanzibar pindi mambo yakienda kombo.
Naomba ieleweke kuwa si kama ninailaumu CUF kwa kukubali mwafaka na CCM bali ninachoonyesha hapa ni madhara yasiyokusudiwa ya uamuzi huo. Ni vigumu kubashiri chama hicho kitaendeshaje kampeni “za maana” mwaka 2015.
Katika mazingira ya siasa za Zanzibar ni dhahiri kuwa kutakuwa na umuhimu wa kuendelea na serikali ya umoja wa kitaifa baada ya Uchaguzi Mkuu ujao.
Lakini ili hilo liwezekane itabidi kampeni katika uchaguzi huo ziwe za “kistaarabu” (ambalo ni jambo zuri isipokuwa tu linaweza kupunguza hamasa ya kisiasa kwa baadhi ya wapigakura).
Hoja hapa ni kwamba kama CCM itashinda na kisha kuunda serikali ya pamoja na CUF kuna haja gani basi ya kufanya kampeni za nguvu ambazo hazitabadili picha ya matokeo ya uchaguzi huo?
Na hata kama CUF wataamua waendeshe kampeni za nguvu ili kupata ushindi mkubwa, watawezaje kuonyesha kuwa CCM haistahili ushindi ilhali vyama vyote viwili vilikuwa madarakani (na hivyo kustahili sifa kwa mema au lawama kwa mabaya waliyofanya katika muhula wa 2010-2015)?
Kwa nini mazingira ya Zanzibar ni muhimu kwa hatima ya CUF kwa nchi nzima? Kwa sababu kila anayefahamu siasa za nchi yetu anatambua kuwa nguvu kubwa ya chama hicho ipo huko Visiwani. Lolote linalotokea huko linakigusa chama hicho kwa upande wa Bara na Muungano kwa ujumla.
Urais ndani ya CHADEMA
Sote tunakumbuka yaliyoikumba NCCR-Mageuzi baada ya mgombea wake Augustine Mrema kubwagwa na mgombea wa CCM, Rais Mstaafu Benjamin Mkapa, katika uchaguzi wa mwaka 1995.
Licha ya kushindwa katika chaguzi mbili mfululizo (mwaka 2005 na mwaka jana), CHADEMA imeendelea kuwa imara huku mgombea wake katika uchaguzi uliopita Dk. Willibrod Slaa akiendelea kuwa na hadhi ileile aliyokuwa nayo kama mgombea urais.
Kulikuwa na hofu kuwa laiti Dk. Slaa angeshindwa kwenye uchaguzi uliopita basi angepotea kabisa kwenye ulingo wa siasa za nchi yetu lakini hali imekuwa tofauti kabisa. Licha ya kubaki Katibu Mkuu tu wa CHADEMA (wadhifa aliokuwa nao kabla ya kugombea urais na kushindwa), mwanasiasa huyo ameendelea kuwa na mvuto mkubwa huku mikutano anayohutubia ikiendelea kupata wasilikizaji.
Lakini si Dk. Slaa pekee ambaye ameendelea kuwa na umaarufu na mvuto bali hata chama chake kimemudu kubaki tishio kwa chama tawala CCM.
Ukifuatilia kwa karibu malumbano ya kisiasa yanayoendelea nchini, unaweza kudhani kuwa bado tupo kwenye kampeni za Uchaguzi Mkuu uliopita au uchaguzi mwingine utafanyika hivi karibuni tu.
Moja ya mitaji mikubwa ya CHADEMA ni msimamo wake kuhusu mustakabali wa taifa. Chama hicho kimefanikiwa kwa kiasi kikubwa kujitambulisha na kukubalika kama kitovu cha harakati za mapambano dhidi ya ufisadi.
Bahati nzuri kwa CHADEMA ni namna CCM inavyoshindwa kujiondoa kwenye utando wa ufisadi, ambapo pamoja na mambo mengine suala la kujivua magamba ni kama kuafikiana na CHADEMA kuwa CCM ni kichaka cha mafisadi na hivyo chama hicho kikongwe hakina budi kujisafisha.
Mtaji mwingine wa CHADEMA ni mshikamano miongoni mwa viongozi wake wakuu na wa kada ya kati. Sina hakika sana hali ipo vipi katika ngazi za chini lakini kwa kiasi kikubwa CHADEMA inainyima usingizi CCM.
Kama mazingira yatabaki jinsi yalivyo sasa, kuna uwezekano wa CHADEMA kumteua tena Dk. Slaa kuwa mgombea wake hapo 2015. Mwanasiasa pekee anayeweza kubadili hali hiyo ni Naibu Katibu mkuu wa chama hicho, Kabwe Zitto, ambaye aliwahi kunukuliwa akisema kuwa angegombea urais kwenye uchaguzi mkuu ujao.
Mtaji mwingine mkubwa kwa CHADEMA ni hali ya mambo ndani ya CCM na mazingira yanavyotarajiwa kuwa katika mchakato wa chama hicho tawala kupata mgombea wake katika Uchaguzi Mkuu ujao (ambayo niliyaelezea kwa kirefu katika makala iliyopita).
Kama kuna nafasi yoyote kwa CHADEMA au chama kingine cha upinzani kuindoa CCM madarakani ni mwaka 2015 kwani kuna kila dalili kuwa sokomoko linaloendelea ndani ya chama hicho tawala litadumu hadi kitakapofanikiwa kupata mgombea wake. Laiti CHADEMA wakiafikiana mapema kuhusu mgombea wao katika uchaguzi huo basi watakuwa na muda wa kutosha kuandaa mazingira ya ushindi huku CCM wakiendelea kupigana vikumbo.
Lakini kuna busara moja ya kuzingatia katika msemo ufuatao: “Siasa si kama fumbo la hesabu ambapo siku zote 2 kujumlisha 2 jibu ni 4. Katika siasa jibu linaweza kuwa 100 au kwa kukatisha tamaa zaidi jibu likawa 0.” Licha ya kuwa siasa ni mchezo mchafu, kipindi cha miaka minne kabla ya Uchaguzi Mkuu ujao ni kirefu sana katika siasa na lolote linaweza kutokea kinyume kabisa cha uchambuzi huu.
Katika moja ya makala zijazo nitaingia kwa undani kujadili mambo yanayoweza kuikwamisha CHADEMA (au chama kingine cha upinzani) kuing’oa CCM kwenye Uchaguzi Mkuu ujao. Lakini kwa leo tuishie hapa

5 Nov 2011

Mustakabali Wa Chadema Mwanza


4 Nov 2011




Waziri Membe asema kama ni misaada yao basi
Raymond Kaminyoge 
TANZANIA imesema ipo tayari kukosa  misaada yote kutoka Serikali ya Uingereza  na kamwe haiwezi kuruhusu sheria inayotambua mashoga na kuhalalisha ndoa za jinsia moja.Msimamo huo mzito wa serikali umekuja siku chache baada ya Waziri Mkuu wa Uingereza, David Cameron, kutamka kwamba nchi yake ina mpango wa kusitisha misaada yake kwa nchi ambazo sheria na katiba zao, hazitambui mashoga na ndoa za jinsia moja.

Cameron alikaririwa akithibitisha kuwa tayari amewajulisha juu ya suala hilo Wakuu  wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Madola waliokuwa wakihudhuria mkutano wa Jumuiya hiyo uliomalizika siku nne zilizopita,  mjini Perth , Austaralia ambao pia ulihudhuriwa na Rais Jakaya Kikwete.

Waziri Mkuu huyo kutoka chama cha Conservative ambacho kilishinda uchaguzi Mei mwaka jana, alisema  suala hilo la mashoga na ndoa za jinsi moja ni moja ya mambo yanayoongoza sera ya serikali yake kuhusu misaada kwa mataifa mbalimbali na kwamba tayari imeanza kutekelezwa katika maeneo kadhaa duniani.

Kauli ya Cameron imechukuliwa kama kielelezo cha ukoloni mamboleo ambao Uingereza inajaribu kuupandisha daraja  kwa mataifa yanayoendelea kwa kigezo cha misaada  

Akizungumza na waandishi wa habari  jijini Dar es Salaam, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard Membe,  alisema pamoja na umasikini wake, Tanzania kamwe haitaruhusu upuuzi huo kwa kigezo cha misaada.

“ Tanzania ni nchi maskini lakini hatutakubali kuruhusu upuuzi huo eti kwa sababu ya misaada yake na fedha zao, lakini ushoga si utamaduni wetu, hata sheria zetu zinakataa,” alisema Membe.

Alifafanua kuwa katika kuonesha msimamo wa kutokukubaliana na masharti hayo, Tanzania imeshikilia msimamo thabiti kupinga  upuuzi huo ambapo  Januari mwaka huu,  ilimkataa balozi shoga ambaye aliteuliwa na nchi yake kuja kuiwakilisha hapa  nchini. Hata hivyo Waziri Membe hakutaja jina la balozi huyo wala nchi  anayotoka.
“Niwape siri moja ambayo tuliificha lakini leo ngoja niwaambie, mwanzoni mwa mwaka jana nililetewa barua  kunijulisha ujio wa balozi mmoja anayekuja kuiwakilisha nchi yake, mwanamume mwenye ndoa ya jinsia moja. Nilikwenda kumweleza Rais Jakaya Kikwete kuhusu wasifu wa balozi huyo mtarajiwa naye akajibu kwa maneno matatu, yarabi toba! Mkatae!” 
Waziri Membe alifafanua kuwa serikali ilimkataa balozi huyo kwa kuwa ni kinyume cha utamaduni wetu na sheria za nchi kuwa na watu wenye tabia hizo.

Alisema alimjulisha waziri wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo kwamba balozi huyo haruhusiwi kuja kufanya kazi nchini kwa kuwa ni kinyume na utamaduni wetu.  “ Waliendelea kuniomba kwamba balozi huyo akija hatatoka kwenye makazi yake akiwa na mwenza wake hivyo watu hawatamuona lakini tulimkataa kabisa, wakatuelewa,” alisema Membe.

 Alieleza kuwa  tamko hilo la Waziri Mkuu Cameron linaweza kusababisha hatari ya kuvunjika kwa uhusiano miongoni mwa nchi wanachama wa Jumuiya ya Madola na koloni mama  Uingereza na waziri huyo atabeba lawama hizo

 Akisisitiza msimamo huo wa serikali, Membe,  alisema  Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971 kifungu cha tisa, kinatambua ndoa ya jinsia mbili tofauti,  yaani mume na mke.  “ Sheria hizi tunazozitumia hivi sasa tumezirithi kutoka Uingereza ambako leo wanatukuza ndoa za jinsia moja na ushoga,” alisema Membe.
Suala la kile kinachoitwa haki za binadamu kuhusu ushoga ilikuwa moja ya ajenda ambazo viongozi kadhaa walishindwa kuafikiana katika mkutano  Perth .
Hoja ya  kukomesha vizuizi dhidi ya ushoga na ndoa za jinsi moja lilikuwa moja ya mapendekezo yaliyokuwamo katika ripoti ya ndani kuhusu matarajio ya baadaye ya Jumuiya hiyo ya Madola.
  
Itakumbukwa kwamba, Malawi tayari imeathirika na mpango huo wa Uingereza kwa sehemu ya misaada yake kusitishwa kutokana na msimamo wa nchi hiyo kuhusu kile Uingereza na nchi za Magharibi zinazokiita haki za mashoga. Ikumbukwe pia kuwa, mjadala mzito ulioibuka katika Bunge la Uganda mwaka 2009 kuhusu ndoa za jinsi moja ilikuwa sehemu ya utekelezaji wa sera hiyo ya Uingereza na washirika wake.
CHANZO: Mwananchi






Vigogo watafuna marejesho ya EPA
Thursday, 03 November 2011 21:27
Leon Bahati na Furaha Maugo
KAMATI ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC), imebaini ufisadi mwingine wa mabilioni ya fedha kwenye marejesho ya zile zilizochotwa awali kifisadi katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA).Fedha hizo zaidi ya Sh50 bilioni zilizorejeshwa na Rais Jakaya Kikwete kutangaza kuwa zitatumika kwa ajili ya kuendeleza shughuli za kilimo nchini, zinadaiwa kuchotwa kwenye Benki ya Rasilimali Tanzania (TIB) kwa amri iliyotoka kwa vigogo serikalini.

Mkurugenzi wa TIB, Peter Noni alikiri jana mbele ya POAC kuwa sehemu ya Sh20 bilioni zilizotolewa na Hazina kwenda kwenye benki hiyo kwa ajili ya dirisha la kilimo, Serikali iliamuru zitolewe kama mkopo kwa wafanyabiashara ambao iliwataja kwa majina.

"Mbaya zaidi, baadhi ya wafanyabiashara waliopewa mikopo hiyo wanaonekana kukwama kurejesha, huku wakitoa ahadi ambazo hawazitekelezi," Noni alisema.

Wabunge wengi wa POAC walionyesha kushangazwa na jinsi serikali ilivyoingilia kati TIB na kuchagua watu ambao wanapaswa kupatiwa mikopo.Huku miongoni mwa wabunge hao wakisema wana taarifa za vigogo walioingia mlango wa nyuma na kuchukua tena fedha hizo katika mazingira ya kifisadi, waliendelea kumbana Noni kwa maswali.

Ingawa baadhi ya wabunge walimtaka mkurugenzi huyo wa TIB awataje kwa majini vigogo hao, Makamu Mwenyekiti wa POAC, Deo Filikunjombe, alisita na kumtaka Noni asitaje majina hayo.

Miongoni mwa wabunge waliotaka majina ya vigogo hao yawekwe hadharani ni Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Ester Bulaya aliyesema, “Nina habari kuwa baadhi ya vigogo walihusika katika kupata mikopo hiyo… Naomba uyataje majina yao.”

Filikunjombe, alisema hakuna haja ya kutaja majina ya vigogo hao ambao alisema miongoni yamo kwenye taarifa waliyopatiwa kuhusu utendaji mzima wa TIB.

Lakini Noni ambaye alikuwa anasaidiwa pia na wasaidizi wake kujibu baadhi ya maswali mazito yaliyoulizwa na wabunge, alisema hakuna tatizo kutaja baadhi ya kampuni zilizohusika kwenye mikopo hiyo ambayo sasa inawatoa jasho TIB.

Noni alitaja mbele ya kamati hiyo kuwa moja ya kampuni zilizochukua fedha hizo na sasa zinaonyesha wasiwasi katika kuzirejesha ni Simon Group Ltd.Nyingine ni kampuni tano za kuuza maua nje ya nchi zenye makao yake makuu mjini Arusha, zikiwepo Tengeru Flowers na Mount Meru Flowers.

Kuhusu Kampuni ya Simon Group, ambayo ilielezwa kuwa ilikopeshwa Sh5 bilioni Noni alisema; “Tumekutana nao mara kadhaa na kutoa ahadi lakini hawakuzitekeleza.”

Aliongoza kuwa kampuni za kuuza maua nje ya nchi zilieleza tatizo lililowafanya kushindwa kurejesha mikopo hiyo kulingana na makubaliano kwamba, ni hasara waliyoipata kutokana na mdororo wa kiuchumi duniani.

Alifahamisha kuwa kutokana na hali hiyo, Serikali iliwaonea huruma na kuwaongezea kipindi cha miaka miwili kulipa deni hilo, muda ambao pia umeonekana kutotosha.

Ila akaahidi kwamba TIB itaanza mchakato wa kuwabana wadeni hao kwa kunadi mali ambazo ziliwekwa rehani wakati wa kuchukua mikopo hiyo.

“Uandaaji na usafirishaji wa maua walisema unahitaji gharama kubwa… Walilazimika kupitia Nairobi (Kenya)… Serikali iliona huruma ikawaongezea kipindi cha kulipa deni hilo,” alisema Noni huku wabunge wengi wakionyesha shauku ya kuendelea kumbana kwa maswali.

Miongoni mwa maswali yaliyoulizwa ni kwa nini TIB ilikubali kutoa mkopo kwa biashara ambazo hazitabiriki? Noni aliweka wazi kwamba, benki hiyo haikuhusika katika mchakato wa kuchambua na kuridhia mikopo kutolewa kwa kampuni hizo.

Filikunjombe ambaye ni Mbunge wa Ludewa, alishangazwa na jinsi Serikali ilivyoingilia uhuru wa TIB na kuweka wazi kwamba si mara ya kwanza Serikali kuingilia mashirika ya umma kiutendaji na kwamba, historia inaonyesha kila ilipofanya hivyo iliziingiza taasisi hizo kwenye mzozo.

“Serikali iliwahi kuingilia kati na kushawishi Tanesco (Shirika la Umeme Tanzania) kuingia mikataba (ya kuzalisha umeme wa dharura) na Richmond na Dowans na kusababisha mzozo,” alitoa mfano Filikonjombe.

Hivyo, akaonya TIB kuhusu kupokea maagizo holela Serikalini kwa sababu mzigo wa matatizo yatakayotokea, itajiweka kando na kuiachia taasisi hiyo ya umma lawama na vibano kutoka kwa wananchi.

Mapendekezo ya Kamati
Ili kuikoa benki hiyo, Filikunjombe alitoa mapendekezo sita ambayo miongoni mwake ni kuitaka TIB ijitegemee na kufanya kazi zake kama shirika la umme lenye uwezo wa kufanya maamuzi yake ya kiutendaji bila kuingiliwa na wanasiasa serikalini.

“Mhakikishe hamuingiliwi na Wizara ya Fedha au Serikali katika suala la utoaji wa mikopo,” alishauri Filikonjombe.
Mapendekezo mengine ni muundo wa manunuzi katika taasisi yao uendane na sheria ya manunuzi, kuwa ni mikakati ya kushindana kibiashara na benki nyingine na kuhakikisha kuwa mtaji unakua.

Katika hatua nyingine, POAC ilishangazwa kuona kuwa kati ya zaidi ya Sh50 bilioni zilizokusanywa kwenye marejesho ya fedha zilizochotwa EPA, ni Sh20 bilioni pekee zilizoifikia TIB.
Wabunge hao walielezea kushangazwa na kitendo cha Menejimenti ya TIB kupokea fedha hizo tu na kushindwa kuishinikiza Serikali itoe fedha zaidi.

Noni alisema kuwa TIB haikuwa na mamlaka ya kuishinikiza Serikali ili iipatie fedha zote za marejesho ya EPA.
“Sisi tulichopewa ndiyo hicho. Hatukuwa na sababu ya kudai fedha zaidi,” alisema huku akizidi kuzua mtafaruku wa maswali kwa wabunge hao.

Wabunge wengi walionyesha kuamini kuwa fedha zote zilipelekwa TIB baada ya Serikali kuahidi kuwa fedha za marejesho hayo zitapelekwa kwenye shughuli za kilimo.

TIB ndiyo benki iliyoanzishwa na Serikali kwa malengo ya kuinua kilimo nchini ambacho kinategemewa na asilimia 80 ya Watanzania.Wananchi wengi wanaojishughulisha na kilimo nchini ndio wanaogubikwa na wimbi la umasikini kuliko sekta nyingine.

Hata hivyo, Serikali imeamua kuanzisha kampeni ya Kilimo Kwanza, yenye lengo la kufanya sekta hiyo kuwa yenye manufaa na inayoweza kuleta utajiri tofauti na mwonekano wa sasa wa kuwa ni ya kundi la wasio na taaluma.
Taarifa nyingine zilizopatikana jana baada ya kamati hiyo kumaliza kikao chake ni kwamba sehemu ya marejesho ya fedha za EPA, mbali na zile Sh20 bilioni zilizopelekwa TIB, zilitolewa kwa moja kwa moja kwa kampuni za pembejeo za kilimo.

Hata hivyo, baadhi ya wabunge walielezea kutokuwa na imani kama fedha hizo zilitumika kikamilifu kwa ajili ya pembejeo hizo za kilimo.

Mmoja wa wabunge kutoka CCM ambaye hakutaka jina lake kutajwa gazetini alisema kuna uwezekano fedha hizo zimeliwa na wajanja.

“Hata ukiangalia suala la marejesho halikuwekwa wazi, maana Rais (Kikwete) mwenyewe alisema zimekusanywa Sh53 bilioni, mara wengine wakasema 60 bilioni na wengine 70 bilioni.Alisema kama ufisadi uliweza kupenya hadi fedha zilizotolewa kwenye taasisi makini ya benki (TIB) basi hakuna shaka hata zilizotolewa kimyakimya ziliingia kwenye mikono hiyo ya mafisadi.

Hata hivyo, gazeti la serikali liliwahi kumnukuu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Mohamed Muya, akisema katika mgawanyo wa fedha za EPA, wizara hiyo ilipewa Sh40 bilioni ambapo Sh30 bilioni zilitumika kwa ruzuku ya pembejeo ya mbolea hali ambayo imesaidia katika uzalishaji. 



“Kutokana na ruzuku hizi, hata idadi ya wakulima wanaopata vocha za ruzuku hiyo imeongezeka kutoka wakulima 500,000 hadi wakulima milioni 1.5 mwaka huu na kupitia Kamati ya Maafa na ya Usalama wa Chakula, hali ya chakula mwaka huu ni nzuri kuliko mwaka jana,” alisema Muya. 



Alisema katika fedha hizo za EPA, Sh10 bilioni zilizobaki zilitumika katika maeneo matatu ya kilimo ambayo ni Mfuko wa Pembejeo ambao ulipewa Sh3 bilioni, Wakala wa Mbegu wa Taifa Sh1 bilioni na kutatua matatizo ya visumbufu kama vile nzige, kweleakwelea na viwavijeshi Sh6 bilioni.

CHANZO: Mwananchi


Body Dear Friend,

Let this message not surprise you, I am contacting you due to the problem in my family since the problem of my country and the death of my beloved father and my half brother Saif al-Arab who died by NATO air strike.

I am Aisha Gaddafi daughters of Muammar Gaddafi, the embattled president of Libya; I am currently residing in West Africa, unfortunately as a refugee. Our investments and bank accounts in several countries have been freeze by the London.

Insha Allahu, I will make you a part of my family heritage, if you can help me out at this difficult time of my life. All I need from you is for you to open an online account in at least 2 banks, one in Indonesia and the other in Benin Republic. I have accounts with big sums of money in these banks. All you do is to open an online account with these banks and I will transfer all my money to your accounts. I don't want anybody to know about this or my accounts will be freeze. There is an international conspiracy to seize our family accounts/investments around the world.

If you are interested to assist me in this regards kindly get back to me as soon as possible for more details on how to proceed. Needless to say that I will compensate you handsomely once the transfer is effected into your nominated bank account.

Please get back to me for more detail and make sure you keep this issue strictly confidential for my own safety.

Your urgent reply means a lot to me.

Yours sincerely

Aisha Gaddafi

2 Nov 2011


KWA NIABA YANGU BINAFSI NA  WASOMAJI WA BLOGU NINATOA SALAMA NYINGI ZA POLE KWA PRODUCER WA SPORAH SHOWSOPHIA MWANAUTA, KWA MSIBA MKUBWA WA KUONDOKEWA NA MDOGO WAKE MPENDWA.

HAKUNA MANENO MWAFAKA TUNAYOWEZA KUKUPA KATIKA KIPINDI HIKI KIGUMU LAKINI MAANDIKO YANATUFUNDISHA KUWA SOTE NI WAJA WA MUUMBA NA HUTUCHUKUA KATIKA MUDA NA WAKATI ATAKAO YEYE.LAKINI KWA VILE MWENYEZI MUGNU NI MWINGI WA HURUMA NA UPENDO BASI SIO TU ATAWALIWAZA WAFIWA KATIKA KIPINDI HIKI KIGUMU LAKINI PIA ATAMJAALIA MAREHEMU PUMZIKO LA AMANI

YEYE NDIYE MUUMBA,ANAPOMCHUKUA MMOJA WETU NI KWA VILE LICHA YA KUWA TULIMPENDA MAREHEMU LAKINI MOLA ALIMPENDA ZAIDI NA KUAMUA KUMCHUKUA.

POLE SANA SANA SOPHIA.MOLA AKUJAALIE WEWE BINAFSI NA FAMILIA,NDUGU NA JAMAA NGUVU NA MOYO WA KUSTAHILIMILI MAJONZI MLIYONAYO

INNA LILLAHI WA INNA ILAYHI RAJI'UN

من المؤكد أننا ننتمي إلى الله وإنا إليه راجعون يجب

SURELY WE BELONG TO ALLAH AND TO HIM SHALL WE RETURN




Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.