19 Jun 2009
18 Jun 2009

Hivi karibuni watunga sheria (wabunge) wetu watatu "waliungana" kuandika kitabu walichokipa jina "BUNGE LENYE MENO".Ukiangalia sehemu ndogo tu ya wasifu wa wabunge hao utamaizi kuwa "muungano huo wa uandishi" ulikuwa ni mithili ya "ndoa za makaratasi" (marriages of inconvenience).
Dkt Wilbroad Slaa,Spika Samuel Sitta na John Momose Cheyo!Nadhani kitu pekee kinachoweza kuwafanya wafanane ni "wote ni wabunge",and the similarity stops there.Wakati Dkt Slaa amejijengea jina kubwa kama kinara wa mapambano ya ufisadi,ni vigumu kum-define Spika Sitta linapokuja suala la mapambano dhidi ya ufisadi.Lakini si vigumu kukumbuka kuwa ni Sitta huyuhuyu aliyempa kadi nyekundu Zitto Kabwe alipombana ex-waziri Nazir Karamagi kuhusu sakata la Buzwagi.Na ni Sitta huyuhuyu aliyetishia kumshtaki Dkt Slaa alipoibua tuhuma ufisadi ndani ya Benki Kuu akidai kuwa ni ushahidi wa kufoji!Eti leo tunaambiwa Spika huyuhuyu nae ni kinara wa mapambano ya ufisadi!
Tukija kwa John Cheyo,nadhani amebaki kuwa UDP,kwa maana ya one-man party.Sera yake ya mapesa ilijaa utani ambao ungekuwa na maana zaidi kwenye sanaa za maigizo kuliko katika siasa makini.Amebaki kuwa jina tu.Sidhani kama kunamfano wowote hai unaoweza kutumika kumtambulisha Cheyo kama mwanaharakati wa mapambano dhidi ya ufisadi.
Sasa hao ndio waandishi wa kitabu BUNGE LENYE MENO.Lakini kwa vile nafahamu kwamba uchambuzi makini unahitaji kwenda mbali zaidi ya kuangalia personalities,naomba kugeukia hoja yangu ya kupingana na ya akina Sitta kuwa bunge la sasa lina meno.Binafsi nasema kama ni meno basi ni ya plastiki.Nadhani unafahamu mtoto mchanga anapoanza kuota meno huwa yanaota meno ambayo yanaitwa meno kwa vile tu yamekaa sehemu yalipo meno.Ukimnywesha uji wa moto basi kilio chake hapo ni balaa!Ni meno machanga yasiyomudu kutafuna vitu vigumu.
Na ndio bunge letu lilivyo.Utasikia kelele,vitisho,na vitu kama hivyo kila waheshimiwa wanapokutana hapo Dodoma ambapo mwisho wa siku akaunti zao zinaingiza kipato cha zaidi ya mwezi mzima kwa Mtanzania wa kawaida,huku kila mwisho wa mwezi wakiondoka na mamilioni lukuki.Basi angalau kipato chao kingeendana na hali halisi ya uchumi wa nchi yetu.
Wabunge wa CCM,ambao wanatengeneza zaidi ya robo tatu ya bunge letu,ndio vichekesho zaidi.Utamsikia huyu akisema hili kabla ya mwenzie kumkalia kooni akitaka mwongozo wa Spika kwa madai ya "kukiuka kanuni za bunge".Lakini ukifuatilia kwa makini,mara nyingi mwongozo huo huombwa pale anapojitokeza mbunge mmoja kuelezea yale yanayozungumzwa na Watanzania wengi mitaani,kwa mfano ishu ya ufisadi.Sasa kwa vile kuna wabunge wenye deni kubwa zaidi kwa CCM na vigogo wake,njia pekee ya kulipa deni hilo ni kuomba mwongozo wa Spika ili kuwaziba midomo wale wanaoongea yasiyopendeza masikioni mwa watawala.
Majuzi,Mbunge wa Nzega Lukas Selelii amemwomba Mungu awalaani mawaziri kwa madai kwamba wamekuwa sehemu muhimu ya maendeleo ya ufisadi nchini.Mbunge wa Pangani Mohammed Rished akaomba mwongozo....sijui kuonyesha anafahamu zaidi sheria za Bunge au kwa vile yaliyoongelewa na Selelii hayakumpendeza mbunge Rished.Kwani si kweli kwamba maamuzi mengi yaliyopelekea skandali za ufisadi yalipitishwa na Baraza la Mawaziri?Kabineti ingetimiza wajibu wake tungekuwa na Richmond?au Kiwira?Au TICTS?au Buzwagi?Au IPTL?Orodha ni ndefu.Sasa Rished alihitaji mwongozo kwa vile Selelii kumuomba Mungu awalaani watu waliofanya maamuzi yaliyopelekea ufisadi ni kosa la jinai au?Halafu tunaambiwa tuna "bunge lenye meno"!In this case,haya wala si meno ya plastiki bali ni mapengo kabisa.
Fuatilia kwa karibu mjadala wa Bajeti unavyoendelea huko Dodoma.Kuna kauli za uchungu kutoka kwa baadhi ya wabunge kama Selelii,Mwambalaswa,Mpendazoe na,kama kawaida,wabunge wa upinzani kama vile Dkt Slaa.Lakini kauli pekee hazimsaidii Mtanzania masikini asiyejua hatma ya maisha yake.Kelele hizi zimekuwepo tangu bunge hili linaanza.Ndio,zimesaidia kuundwa kwa kamati mbalimbali kama ile ya Mwakyembe.Lakini kuunda kamati kisha kutofanyia kazi mapendekezo yake ni sawa na ufisadi tu.Ikumbukwe kuwa kamati hizo hutumia mamilioni ya fedha za walipa kodi.Ukubwa wa gaharama za kuendesha kamati za aina hiyo ungeweza kupunguziwa maumivu laiti mapendekezo yanayotolewa yangekuwa yanafanyiwa kazi.Hadi leo wahusika wa Richmond (achana na yule decoy mwenye kesi mahakamani) wanaendelea "kupeta".
Laiti Bunge lingekuwa na meno,isingetosha kwa Lowassa,Msabaha na Karamagi kujiuzulu tu.Walipaswa wakabidhiwe kwa vyombo vya dola.Kadhalika,watendaji wa serikali waliotajwa kuhusika walipaswa kuwajibishwa mara moja.Badala yake,hadithi zimeendelea kila kinapojiri kikao kingine cha bunge,huko waandishi wetu mahiri wa kunukuu wakija na vichwa vya habari kama "Moto kuwaka Bungeni","Ishu ya EPA kuibuliwa tena Bungeni"...Huwezi kuwalaumu sana kwa vile vyombo vya habari vinaendeshwa kibiashara na kichwa cha habari chenye mvuto kinauza gazeti!
Bunge lenye meno lisingekuwa linapigwa danadana na Waziri Ngeleja kuhusu ishu ya Kiwira.Bunge lenye meno lisingekubali mkataba wa TICTS uendelee kuwa hoja ya moto kila kikao lakini inayoishia kuwa ya moto pasipo mabadiliko,only for it kuwa ya moto tena kwenye kikao kingine.Yayumkinika kusema kuwa kama ni moto wa hoja,basi ni wa njiti ya kiberiti kwenye upepo mkali;hudumu kwa sekunde tu.
Sintajadili zaidi kwa vile itakuwa sawa na kupre-empty muswada wa chapisho naloandaa kama mapitio (majibu?) ya kitabu hicho cha wabunge hao.Ila kwa kifupi,si rahisi kuwa na bunge lenye meno wakati wabunge wenyewe wanaishi maisha tofauti na hao wanaopaswa kuwawakilisha bungeni (nikimaanisha maslahi yao).Tusidanganyane,mtu anayelipwa milioni 6 na ushee kwa mwezi hawezi hata chembe kuwa mwakilishi mzuri wa mtu asiye na uhakika wa kukamata angalau shs 10,000 kwa mwezi.Haya ni matabaka mawili tofauti,na japo kinadharia wabunge wanapaswa kuwa sehemu ya tabaka tawaliwa kwa maana ya uwakilishi wa wananchi,maslahi yao makubwa yanawaingiza kwenye tabaka tawala na hivyo kuwaweka kwenye mgongano wa moja kwa moja direct confrontation) na tabaka tawaliwa la wananchi wa kawaida.Katika hali hiyo,serikali kwa maana ya the executive branch of the government,inapata free pass kwani wanaopaswa kuihoji nao wanajikuta wakihojiwa na wanaowawakilisha.Kiuhalisia,mpiga kura is hardly represented bungeni.
Lakini tukiweka kando suala la kipato na matabaka,tatizo la msingi zaidi kwenye bunge hili ni kutanguliza mbele maslahi ya chama badala ya maslahi ya nchi.Umoja na mshikamano ndani ya CCM unatafsiriwa kuwa ni muhimu zaidi kuliko umoja na mshikamano wa kitaifa.Wengi wa wabunge wa CCM wanahofia kuzungumzia baadhi ya masuala yanayolihusu taifa ambayo kwa namna moja au nyingine yanaifanya CCM inyooshewe kidole.Hakuna mbunge wa CCM anayeweza kuzuia bajeti ya wizara flani,hata kama ni mbovu namna gani,kwa vile akifanya hivyo atatafsiriwa kuwa anavunja mshikamano wa chama.Mbunge katika bunge lenye meno hawezi kuogopa tafsiri ya chama chake,bali wapigakura wake.
Kwa anayehitaji nakala ya bure ya kitabu hicho cha BUNGE LENYE MENO (as an ebook),tuwasiliane.
Kwa anayehitaji nakala ya bure ya kitabu hicho cha BUNGE LENYE MENO (as an ebook),tuwasiliane.
17 Jun 2009
17.6.09
Evarist Chahali
CCM, CHENGE, UFISADI
No comments

Ni dua pekee linaloweza kubadili viumbe wa aina hii.Sijui ni kujikomba,sijui uhaba wa tafakari au...!!!Soma kwanza stori hii kisha utafakari
Chenge asimikwa utemi
na Sitta Tumma, Magu
MBUNGE wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge, ambaye amekuwa akiandamwa na kashfa mbalimbali, ametawazwa kuwa mtemi wa kabila la Wasukuma-Bagole, Kanda ya Itilima, wilayani Bariadi.
Chenge alichaguliwa katika sherehe maarufu za kabila hilo, maarufu kama Bolabo, mwishoni mwa wiki, wilayani hapa, ambazo mbali naviongozi wa kimila, Mkuu wa Mkoa, Abbas Kandoro, alikuwa ni miongoni mwa waliohudhuria.
Baadhi ya watu waliokuwepo kwenye sherehe hizo, waliuelezea utemi wa Chenge kwa mtazamo tofauti, huku baadhi wakidai kaupata ili kuweka mambo yake sawa, na wengine wakidai anastahili kupata nafasi hiyo kwa kuwa ni miongoni mwa watu wa kabila hilo.
Mbunge huyo ambaye alilazimika kujiuzulu nafasi yake ya uwaziri alisema, utemi huo ni karama aliyopewa na Mungu na kwamba wajibu huo ni sawa na daraja la kuunganisha jamii ya kabila husika.
"Utemi niliopewa naweza kusema ni karama iliyotoka kwa Mwenyezi Mungu! Kazi hii ya utemi ni nzito kwa sababu ina masuala yake yanayohusiana na mambo ya kimila pamoja na kuunganisha jamii ya kabila husika," alisema Chenge.
CHANZO: Tanzania Daima
Ndio maana wakati mwingine hawa "wazungu" wanapata wakati mgumu kutuelewa.Hivi inaingia akilini kweli kwa mtuhumiwa wa ufisadi wa zaidi ya shilingi bilioni moja,Mzee wa Vijisenti Andrew Chenge,kutunikiwa utemi?Watoto wanaozaliwa leo na kesho na kukuta mtemi wao ni miongoni mwa watu waliochuma utajiri kwa njia za miujiza kabisa (fedha alizonazo haziwezi kuwa zimepatikana kwa njia halali,piga ua) watawaelewa kweli wazazi wao?
Mtemi wa nini?Au wanamaanisha utemi wa kuifanya sheria imwogope?Maana kesi yake ya kuua ni vituko vitupu.Mara iundiwe tume,mara iahirishwe kwa hili na lile!Mtu kasababisha ajali huku gari ikiwa na bima iliyoisha muda wake,mnamuundia tume ya nini?Na kwanini hiyo tume iwe kimya kama haikuundwa vile?
Mtuhumiwa huyu wa ufisadi ameendelea pia kuwa kwenye kamati ya maadili ya CCM.Halafu ukisema CCM chama cha kifisadi kuna waungwana wananuna!
Kaaazi kwelikweli
16 Jun 2009
16.6.09
Evarist Chahali
ALI G, BORAT, BRUNO, COMEDY, SACHA BARON COHEN
No comments
Posing for GQ,Sacha as BRUNO
In Paris at the premiere of his latest movie BRUNO
Cohen's (real-life) other half ISLA FISHER.With Cohen,it seems necessary to state clearly if something about him is real or sheer comedy. 
Please copy the sample letter and write to your representatives in the government, asking them not to recognize the presidency of Mr. Ahmadinejad. Please also ask others to do the same.
Dear Sir or Madam:
On June 12, 2009, the Iranian people went to the polls in record numbers to choose the next president of the Islamic Republic of Iran. Only four candidates were allowed to compete: the incumbent President Mahmoud Ahmadinejad, Mir Hussein Mousavi, MehdiKaroubi, and Mohsen Rezaie. The Iranian reform movement was united behind Mr. Mousavi’s
candidacy.
Based on numerous polls carried out a few days before the elections, Mousavi had a commanding lead over Ahmadinejad. Unfortunately, in total disregard for the people’s choice, the interior ministry haphazardly declared Mr. Ahmadinejad the winner, giving him 63.62% of the votes. The absurdity of the government’s election engineering is that none of the candidates managed to get more than a fraction of the votes even in their hometowns! In his birthplace, the village of Lali, Rezaie received fewer than 70 votes of the total of 900 votes cast, while 830 votes went to Ahmadinejad. Likewise, Karoubi did not do much better in his birthplace Aligoudarz, garnering only 14,512 votes, while Ahmadinejad received 39,690 votes. Finally, Mousavi, in his birthplace, Shabstar, was given only 2,000 of the total of 7,000 votes cast, while the rest went to Ahmadinejad.
How could all these candidates get defeated in their own hometowns, while we know that in the past presidential elections, all the candidates got the majority of the votes in their hometowns? Evidently, those who manufactured these figures got their lesson from Nazi propaganda minister Joseph Goebbels that the bigger the lie, the more believable it is. They must have thought that if Ahmadinejad is declared the winner even in his rivals’ hometowns, the Iranian people would believe his victory everywhere.
The unofficial results from the interior ministry tell quite a different story. Accordingly, Mr. Mousavi was the absolute winner with 54% of the votes, followed by Karoubi and Ahmadinejad with 31% and 13% of the votes,respectively.
Given that days before the election the Revolutionary Guards made a scarcely veiled threat to the followers of the reform movement that they will stifle swiftly any attempt at a “velvet revolution,” that a day before the elections the SMS network of mobile users were disconnected in the country, and that the websites belonging to the reformist candidates were filtered—all were indicative of the fact that the regime had staged a political coup. If Ahmadinejad was so popular, why should the Revolutionary Guards be so concerned about an impending velvet revolution? Why should they be compelled to disconnect the SMS network of mobile users?
The Iranian people do not accept the shenanigans engineered by the regime. They are demanding an investigation. They demand an honest and objective counting of the votes. Without their demands being met, the result has no validity.
Please do not recognize the official results of the elections. Please do not recognize the presidency of Mr. Mahmoud Ahmadinejad.
Democracy in Iran means peace in the Middle East. I appreciate your support.
Below are links to more information and report on Iran’s elections.
http://www.nytimes.com/2009/06/15/opinion/15iht-edcohen.html?_r=1&th&emc=th
http://garysick.tumblr.com/
www.truthout.org/061409Z?print
Miongoni mwa nukuu muhimu kuhusisna na Mwenyekiti Mao wa China ni hii: usiseme kitu kama hujakitafiti (tafsiri yangu isiyo rasmi kwenye usemi no research,no right to speak).Sasa sijui tumweleweje huyu Sekulu MUSTAFA MKULO anapodai kwamba kuna baadhi ya taasisi za dini zimekuwa zikitumia vibaya misamaha ya kodi,lakini hakuweza kutaja angalau jina la taasisi moja.Hizi ni dalili za ubabaishaji na uoga.Uoga huo wa kutaja hadharani watumishi wa Mungu wanaotuhumiwa kuvunja sheria unasababishwa na mtoa tuhuma kutokuwa mkamilifu.Ni mithili ya mama anayechelea kutaja madhambi ya bintie kwa kuwa naye yumo katika mchezo huohuo.

Kama kuna wachunga kondoo wa Bwana walikuwa wakitumia misamaha ya kodi vibaya lakini hawakuchukuliwa hatua,inamaanisha chombo kinachoitwa Mamlaka ya Mapato kiko kwenye usingizi wa pono.Kwanini wahusika hawakuchukuliwa hatua?Au kulikuwa na utatu usio mtakatifu wa vigogo serikalini,wafadhili ughaubuni na watumishi wa Mungu?
Hata kama tukiafikiana na maelezo za Mheshimiwa Mkulo kuhusu hako kamchezo kasikopendeza ,ni dhahiri kwamba vitendo vya watenda dhambi hao wachache havimaanishi kuwa dhehebu lote analotoka mtenda dhambi nalo lina makosa.Kuwepo kwa viongozi kadhaa wa dini ambao wamekuwa wakitumia vibaya misamaha ya kodi hakumaanishi kwamba mantiki nzima ya mpango huo imepoteza maana.

Na lini utaratibu huu wa "akikosea mmoja basi wamekosea wote" ulianza?Mbona hapo Benki Kuu palipozaliwa ufisadi wa EPA na nduguye wa Maghorofa Pacha bado wahusika wameendelea "kupeta"?Kama Ballali ndio kinara cha wizi huo,kwanini basi wasaidizi wake (ikiwa ni pamoja na huyu gavana wa sasa) wameachwa kuendelea na kazi?Je Liyumba anapotuhumiwa kufanya ubadhirifu wa fedha za Maghorofa Pacha,kwanini basi menejimenti yote ya Benki Kuu nayo isipandishwe kizimbani kwa vile,kwamujibu wa Mkulo,akikosea mmoja basi wamekosea wote!Mbona Mattaka kalikoroga ATCL kapelekwa NIC,Peter Noni anahusishwa na EPA kapewa ulaji TIB,Mzee wa Vijisenti na mabilioni yake visiwani Jersey bado yuko kwenye kamati ya maadili ya chama tawala!
Kwa madhambi haya,dnio maana hutosikia yeyote akidiriki kutaja jina la kiongozi wa dini anayetuhumiwa kufuja misamaha ya kodi (kama yupo).Mtu asiye msafi hawezi kuonyesha uchafu wa mwenzie.
Lakini binafsi natafsiri kuwa hatua hii ina ajenda mbalimbali zilizofichika ikiwa ni pamoja na kuonyeshana nani mwenye nguvu zaidi: mamlaka za kidunia au za kiroho.Usisahau kauli za hivi karibuni kutoka kwa madhehebu mbalimbali ya Kikristo kwamba mafisadi wameteka nchi....na kuandaa mkakati wa kupata viongozi bora katika uchaguzi mkuu wa 2010.

Wizara ya Fedha na Uchumi imesema, siasa za Tanzania ni nzuri na kuna mipango mizuri ya maendeleo ndiyo maana umasikini wa kipato unapungua. Hata hivyo Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Omar Yussuf Mzee amesema, bungeni mjini Dodoma kuwa, kuna watanzania wengi wanaishi kwa kula mlo mmoja. Kiongozi huyo wa Serikali amesema leo kuwa, umasikini ni mchakato, unapungua siku hadi siku.
Mzee ameyasema hayo wakati anajibu maswali ya Mbunge wa Viti Maalum, Magdalena Sakaya aliyetaka kufahamu ni kwa nini watanzani wengi bado ni masikini wakati nchi imepata uhuru miaka 48 iliyopita.
Mbunge huyo pia alidai bungeni kuwa, watanzania wengi bado ni masikini kabisa kwa kuwa hakuna siasa safi, na pia hakuna mipango mizuri ya kuwawezesha wananchi wapate maendeleo.
Naibu Waziri Mzee amewaeleza wabunge kuwa kuna umasikini wa aina tatu ukiwamo wa elimu, afya na kipato.Amesema, kama Tanzania isingekuwa na siasa safi na mipango mizuri ya maendeleo, takwimu zisingeonyesha kupungua kwa umasikini wa kipato nchini.

Amewaeleza wabunge kuwa, mwaka 1991, asilimia 21.6 ya watanzania wote milioni 24.8 walikuwa masikini kabisa. Kwa mujibu wa kiongozi huyo, mwaka 2001, Tanzania ilikuwa na watu milioni 31.9, asilimia 18.7 kati yao walikuwa masikini kabisa, na mwaka 2007, asilimia 16.5 ya watanzania milioni 38.3 walikuwa masikini kabisa.
Mzee amelieza Bunge kuwa, watanzania wengi bado ni masikini kwa kwa wengi wao ni wakulima wanaotumia jembe la mkono, bei za pembejeo za kilimo zimepanda, na pia mabadiliko ya hali ya hewa yanathiri uzalishaji kwa kuwa sehemu kubwa ya kilimo nchini hutegemea mvua. Ametaja sababu nyingine kuwa ni ukuaji mdogo wa sekta ya viwanda, wakulima kukosa mitaji, na pia ukosefu wa ajira.
Mzee ameyasema hayo wakati anajibu maswali ya Mbunge wa Viti Maalum, Magdalena Sakaya aliyetaka kufahamu ni kwa nini watanzani wengi bado ni masikini wakati nchi imepata uhuru miaka 48 iliyopita.
Mbunge huyo pia alidai bungeni kuwa, watanzania wengi bado ni masikini kabisa kwa kuwa hakuna siasa safi, na pia hakuna mipango mizuri ya kuwawezesha wananchi wapate maendeleo.
Naibu Waziri Mzee amewaeleza wabunge kuwa kuna umasikini wa aina tatu ukiwamo wa elimu, afya na kipato.Amesema, kama Tanzania isingekuwa na siasa safi na mipango mizuri ya maendeleo, takwimu zisingeonyesha kupungua kwa umasikini wa kipato nchini.

Amewaeleza wabunge kuwa, mwaka 1991, asilimia 21.6 ya watanzania wote milioni 24.8 walikuwa masikini kabisa. Kwa mujibu wa kiongozi huyo, mwaka 2001, Tanzania ilikuwa na watu milioni 31.9, asilimia 18.7 kati yao walikuwa masikini kabisa, na mwaka 2007, asilimia 16.5 ya watanzania milioni 38.3 walikuwa masikini kabisa.
Mzee amelieza Bunge kuwa, watanzania wengi bado ni masikini kwa kwa wengi wao ni wakulima wanaotumia jembe la mkono, bei za pembejeo za kilimo zimepanda, na pia mabadiliko ya hali ya hewa yanathiri uzalishaji kwa kuwa sehemu kubwa ya kilimo nchini hutegemea mvua. Ametaja sababu nyingine kuwa ni ukuaji mdogo wa sekta ya viwanda, wakulima kukosa mitaji, na pia ukosefu wa ajira.

Professor Duncan Rice, Principal and Vice Chancellor of the University of Aberdeen, has been honoured with a Knighthood in the Queen’s Birthday Honours.
Professor Rice has been awarded the honour for services to higher education.
Professor Rice said: "On a personal level this is a wonderful honour, and I'm very proud of it. But I know it's intended to recognise all the University has achieved in the last decade. I am just the vehicle, and the real congratulations go to the whole of our community. It is being transformed by the commitment, quality and vision of all my colleagues, and my knighthood is a way of honouring them."
He added: "By the standards of where we were a decade ago, we have manoeuvred ourselves into being one of the top handful of universities in Scotland. That makes this something of a minor golden age. What we really want to do now is to advance into a real golden age, where we are one of the top handful of universities in the world."
Professor Rice has been awarded the honour for services to higher education.
Professor Rice said: "On a personal level this is a wonderful honour, and I'm very proud of it. But I know it's intended to recognise all the University has achieved in the last decade. I am just the vehicle, and the real congratulations go to the whole of our community. It is being transformed by the commitment, quality and vision of all my colleagues, and my knighthood is a way of honouring them."
He added: "By the standards of where we were a decade ago, we have manoeuvred ourselves into being one of the top handful of universities in Scotland. That makes this something of a minor golden age. What we really want to do now is to advance into a real golden age, where we are one of the top handful of universities in the world."
14 Jun 2009

Israeli Prime Minister Benjamin Netanyahu has announced he will back a Palestinian state - but only if it is completely demilitarised.
He said a Palestinian state must have no army, no control of its air space and no way of smuggling in weapons.
And a Palestinian state must recognise Israel as a Jewish nation, he said.
Mr Netanyahu's speech, laying out his plans for regional peace, came a month after US President Barack Obama urged him to accept a two-state solution.
The BBC's Paul Wood says Mr Netanyahu broke ground by accepting the principle of a demilitarised Palestinian state, albeit with conditions, and this will be what the White House is looking for.
But our correspondent says the question is whether this will be enough to make up for the lack of movement on the issue of Jewish settlements in the occupied West Bank.
Mr Obama has stressed that he wants all settlement activity to stop.
But in his speech Mr Netanyahu said settlers were not "enemies of peace" and did not move from his position of backing "natural growth" in existing settlements.
Guarantee needed
The Israeli leader offered to talk to the Palestinians immediately and with "no preconditions".
"We want to live with you in peace as good neighbours," he said.
Mr Netanyahu also said he was willing to go to Damascus, Riyadh and Beirut in pursuit of a Middle East peace deal.
He said Israel would "be prepared for a true peace agreement [and] to reach a solution of a demilitarised Palestinian state alongside the Jewish state".
But only if "we receive this guarantee for demilitarisation and the security arrangements required by Israel, and if the Palestinians recognise Israel as the nation of the Jewish people.
He said a Palestinian state must have no army, no control of its air space and no way of smuggling in weapons.
And a Palestinian state must recognise Israel as a Jewish nation, he said.
Mr Netanyahu's speech, laying out his plans for regional peace, came a month after US President Barack Obama urged him to accept a two-state solution.
The BBC's Paul Wood says Mr Netanyahu broke ground by accepting the principle of a demilitarised Palestinian state, albeit with conditions, and this will be what the White House is looking for.
But our correspondent says the question is whether this will be enough to make up for the lack of movement on the issue of Jewish settlements in the occupied West Bank.
Mr Obama has stressed that he wants all settlement activity to stop.
But in his speech Mr Netanyahu said settlers were not "enemies of peace" and did not move from his position of backing "natural growth" in existing settlements.
Guarantee needed
The Israeli leader offered to talk to the Palestinians immediately and with "no preconditions".
"We want to live with you in peace as good neighbours," he said.
Mr Netanyahu also said he was willing to go to Damascus, Riyadh and Beirut in pursuit of a Middle East peace deal.
He said Israel would "be prepared for a true peace agreement [and] to reach a solution of a demilitarised Palestinian state alongside the Jewish state".
But only if "we receive this guarantee for demilitarisation and the security arrangements required by Israel, and if the Palestinians recognise Israel as the nation of the Jewish people.
SOURCE: BBC
14.6.09
Evarist Chahali
BENKI KUU, EPA, PETER NONI, TANZANIAN ECONOMY, UFISADI
No comments

Majuzi,Watanzania wametahadharishwa kuhusu athari za mdodoro wa uchumi wa dunia na madhara yake kwa nchi yetu.Kadhalika,bajeti ya mwaka ujao wa fedha imeandaliwa kwa kuzingatia tahadhari hiyo huku kukitangazwa mpango wa kuchochea uchumi (economic stimulus plan).
Hata hivyo,kama nilivyojadili HAPA,uwezekano wa bajeti na stimulus plan hiyo kufanikiwa,sambamba na umuhimu wa tahadhari iliyotolewa,utategemea zaidi hatua kali na za makusudi dhidi ya ufisadi na mafisadi.Yayumkinika kubashiri kwamba pamoja na imani kwamba mipango hiyo inalenga kulinusuru taifa,wanaufaika wakubwa wanweza kuwa mafisadi wanaojua vema namna ya kubuni mikakati ya ulaji huku wakiwa hawana hofu ya kuchukuliwa hatua yoyote kutokana na siasa za kulindana na kishkaji.
Hebu soma kwanza habari ifuatayo,kisha tujadili kidogo mwishoni.
CHANZO: Tanzania Daima.
Katika mazingira kama haya,itakuwa kosa kweli kuyamkinisha kwamba hiyo stimulus plan inaweza kuishia kutengeneza dili ya kuifanya EPA ionekane "cha mtoto"?
Hata hivyo,kama nilivyojadili HAPA,uwezekano wa bajeti na stimulus plan hiyo kufanikiwa,sambamba na umuhimu wa tahadhari iliyotolewa,utategemea zaidi hatua kali na za makusudi dhidi ya ufisadi na mafisadi.Yayumkinika kubashiri kwamba pamoja na imani kwamba mipango hiyo inalenga kulinusuru taifa,wanaufaika wakubwa wanweza kuwa mafisadi wanaojua vema namna ya kubuni mikakati ya ulaji huku wakiwa hawana hofu ya kuchukuliwa hatua yoyote kutokana na siasa za kulindana na kishkaji.
Hebu soma kwanza habari ifuatayo,kisha tujadili kidogo mwishoni.
Wingu zito fedha za EPA
• Chegeni: Zimekwenda kusikojulikana
na Mwandishi Wetu
UTATA umegubika mahali zilipo na matumizi ya fedha zilizorejeshwa na kampuni zilizoshiriki katika wizi wa fedha za Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), uliofanyika Benki Kuu ya Tanzania (BoT).
Rais Jakaya Kikwete alipokuwa akilihutubia Bunge mjini Dodoma Agosti mwaka jana, alibainisha fedha hizo zilizorejeshwa na baadhi ya kampuni si mali ya serikali lakini zitawekwa kwenye akaunti maalumu kabla ya kupelekwa katika Benki ya Rasilimali Tanzania (TIB) kwa ajili ya kufungua dirisha dogo la kuwakopesha wakulima wakati nchi ikielekea katika mchakato wa kuanzisha Benki ya Kilimo.
Ingawa Rais Kikwete na Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo, kwa nyakati tofauti walieleza kuwapo kwa fedha hizo katika akaunti maalumu, taarifa ambazo Tanzania Daima Jumapili imezipata zinasema hadi sasa fedha hizo hazijaingia katika Benki ya TIB, licha ya kuwapo kwa taarifa kuwa fedha hizo zimetumika kununulia mbolea iliyotolewa kwa mfumo wa vocha kwa baadhi ya wakulima hapa nchini.
Chanzo kimoja cha habari kilichomo ndani ya TIB kimedai fedha hizo wamekuwa wakizisikia kupitia katika vyombo mbalimbali vya habari kutoka kwa wanasiasa, ambao wamekuwa wakijinadi kuwa fedha hizo zitatumika kunyanyua kilimo ili kuchochea ukuaji wa uchumi na kuboresha maisha ya wananchi.
Chanzo hicho kilibainisha kuwa hadi sasa dirisha la kilimo lililosemwa bado halijaanza kufanya kazi iliyotarajiwa, ingawa maneno ya watu mbalimbali yamekuwa yakibainisha kuanza kazi kwake ambako kungetarajiwa kuwasaidia wakulima kupata mikopo ya muda mrefu, baada ya kuikosa fursa hiyo kwa kipindi kirefu kutokana na kutokopeshwa na taasisi za fedha za hapa nchini.
“Haya mambo huwa tunayasoma, kuyasikia na kuyaona kwenye hivyo vyombo vyenu vya habari, lakini kwenye makaratasi hali ni tofauti, sasa sijui niseme siasa inatawala au muda bado haujafika,” kilisema chanzo hicho.
Tanzania Daima Jumapili, ilifanya juhudi za kumtafuta Mkurugenzi Mtendaji wa TIB, Peter Noni, ambaye ameteuliwa hivi karibuni kushika wadhifa huo na Rais Jakaya Kikwete, lakini Ofisa Mwanadamizi wa Mambo ya Uhusiano wa benki hiyo,Catherine Magambo, alisema mkurugenzi wake hawezi kutoa ufafanuzi hivi sasa, kwa kuwa ameanza kazi siku si nyingi na ni busara akapewa wiki moja ili aweze kujipanga.
Catherine, alipotakiwa kueleza kama ana taarifa zozote za kutokuwapo kwa fedha zilizoahidiwa na rais kupelekwa katika benki hiyo, alisema anachokifahamu ni kile kilichoelezwa wakati fulani na Mkurugenzi aliyestaafu, William Mlaki, kuwa hawajapokea fedha hizo na kama kungekuwa na mabadiliko vyombo vya habari vingejua kama walivyofanya hapo awali.
“Nyinyi Tanzania Daima Jumapili, habari kama hii unayoniuliza au unayotaka mkurugenzi wangu akujibu, najuakwamba hakuna kitu ambacho kimebadilika lakini kama mnataka habari zaidi msubiri mkurugenzi mpya azoee ofisi kwa muda wa wiki, halafu ndipo uje kumuuliza maswali yako,” alisema Magambo.
Pia alibainisha kuwa hajaona mabadiliko yoyote juu ya ahadi iliyotolewa pia na Rais Kikwete ya kutoa kiasi cha sh bilioni 15 kwa ajili ya kuendeleza benki hiyo ili iweze kutoa mikopo kwa wakulima.
“Jamani maswali yenu mbona yamezidi, si nimewaambia hakuna mabadiliko na hayo maswali yenu msubirini mkuu? Mbona mnanibana kwa mambo nisiyo na uwezo wa kutoa majibu? Kwani kila ofisi ina utaratibu wake,” alisema Magambo.
Wakati fedha hizo zikionekana kugubikwa na utata, baadhi ya watu wamekuwa wakiiona hatua ya serikali kutangaza kurejeshwa kwa fedha hizo ni kiini macho au zimetumika katika matumizi mengine badala ya kupelekwa katika kilimo kama ilivyoahidiwa, kwa kuwa viwanda vingi vya mbolea kwa mwaka huuvimejikuta vikishindwa kujiendesha baada ya kuzalisha bidhaa hiyo na kukosa wanunuaji.
Dhana hiyo inachagizwa na baadhi ya wakulima ambao wamekuwa wakilalamikia kutokupata mbolea hiyo, licha ya serikali kutangaza kutenga fungula fedha kwa ajili ya kutoa ruzuku ya mbolea kwa wakulima ili kukuza kilimo na kuleta mapinduzi ya kijani.
Baadhi ya wachambuzi wa masuala ya siasa na wanasiasa mbalimbali wa hapa nchini walikuwa wakihusisha wizi huo wa fedha na mkakati maalumu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwaagiza baadhi ya makada wake na wanachama wakwapue fedha hizo kwa ajili ya matumizi ya kampeni za uchaguzimkuu wa mwaka 2005 uliokiwezesha chama hicho kuibuka na ushindi wa ‘kishindo.’
Hisia hizo zilipata nguvu baada ya kuwapo tetesi kuwa kampuni iliyochota kiasi cha sh bilioni 40 ya Kampuni ya Kagoda Agriculture Limited, inadaiwa kumilikiwa na baadhi ya vigogo wa chama hicho, jambo lililochangia ugumu wa kukamatwa kwa wamiliki wa kampuni hiyo ambayo inaaminika ndiyo iliyosuka mpango wa uchotaji wa fedha hizo.
Tuhuma hizo mara kadhaa zimekuwa zikikanushwa na viongozi waandamizi wa chama hicho, akiwamo Katibu Mkuu wake, YusufMakamba, ambaye aliweka bayana kuwa CCM haijamtuma mwanachama wake afanye wizi huo na kama kuna mwanachama amehusika na wizi huo apewe lawama hizo binafsi na si chama.
Naye Mbunge wa Busega, Dk. Raphael Chegeni, katikati ya wiki alinukuliwa na vyombo vya habari mjini Dodoma akisema kuwa fedha za EPA zinaonekana kwenda sehemu zisizoonekana kirahisi kwa wananchi, ingekuwabusara kama zingetumika katika ujenzi wa barabara ambayo ingepewa jina la EPA, ili kila
mwananchi aweze kuamini kinachosemwa na viongozi wa serikali.
Alisema mazingira ya fedha hizo tangu awali yalionyesha utata, hivyo ingekuwa busara hata matumizi yake yakafanyika bila kuwapo kwa usiri, ili kuondoa fikra potofu kuwa hakuna fedha iliyorejeshwa.
“Hizi fedha za EPA mimi nafikiri zingetumika kujengea barabara na tukaziita barabara za EPA, ili yeyote anayetaka kuzusha lake ashindwe kufanya hivyo au tumuonyeshe vithibitisho,” alisema Chegeni.
Alisema sekta ya kilimo ni pana na hata fedha zinazotumbukizwa huko ni lazima ziandaliwe mipango mizuri na mapema ili ziweze kufikia walengwa na zilete tija inayotakiwa kuliko inavyoonekana sasa ambapo serikali inasema imetoa mbolea ya ruzuku kwa wingi, lakini wakulima wanalalamika kutoipata mbolea hiyo kwa kiwango kinachohitajika.
Wizi wa fedha za EPA ulibainika baada ya Kampuni ya ukaguzi ya kimatifa ya Ernst &Young kubaini wizi wa sh bilioni 133, ambapo baada ya uchunguzi huo, Rais Kikwete aliamua kumfukuza kazi aliyekuwa Gavana wa benki hiyo, marehemu Daudi Ballali na kuagiza mamlaka husika kufanya uchunguzi kwa maofisa wa benki hiyo ili kufikishwa mbele ya vyombo vyasheria.
CHANZO: Tanzania Daima.
Katika mazingira kama haya,itakuwa kosa kweli kuyamkinisha kwamba hiyo stimulus plan inaweza kuishia kutengeneza dili ya kuifanya EPA ionekane "cha mtoto"?
Halafu,habari hiyo hapo juu ina kitu kingine cha ziada,nacho ni kuhusu PETER NONI.Huyu jamaa anahusishwa kwa karibu na skandali la EPA.Awali wasiwasi wangu ulikuwa kwenye kuteuliwa kwake kuwa Mkurugenzi wa TIB.Kilichonifumbua macho katika habari hii ni ukweli kwamba marejesho ya fedha za EPA yalipangwa kupelekwa TIB.You see the connection?NONI anahusishwa na ishu ya EPA kwa wadhifa aliokuwa nao BoT.Sasa anapokwenda TIB ambako tunaambiwa ndiko zitakapopelekwa marejesho ya fedha za EPA ni mithili ya "kula denge" kuelekea lilipo fungu hilo.
Ndio Tanzania yetu hiyo!

'I don't hate or have any problem with black people other than I hope very much that they remain black people. Other than I hope their children will look as black as they are and as different and as interesting. And where it doesn't happen: it's not my business. No I haven't got a problem, so where does it come from? I don't really know'. That's NICK GRIFFIN,a racist leader of a Nazi British National Party,in an interview with the Independent On Sunday (CLICK THE LINK FOR A FULL TRANSCRIPT OF THE INTERVIEW)
RELATED STORY: (In the Sunday Times) Profile: Nick Griffin.
Laiti jicho lingekuwa risasi,basi hapa Ferguson angekuwa majeruhi,au zaidi...
Hii inajieleza yenyewe.Kama Ferdinand hatukani kimoyomoyo basi anajikaza kumtoa mtu ngeu.Ni siku Man United waliofungwa na Barca kwenye fainali ya Champions League.
Japo Rooney anafarijiana na Tevez,anaonekana mawazo yake yako zaidi kwa mshambuliaji mwenzie Ronaldo.Wachambuzi wa soka la Uingereza wanadai kwamba mara nyingi Rooney alijitoa mhanga kubadili nafasi uwanjani ili kum-accommodate Ronaldo,ambaye anatuhumiwa kuwa m-binafsi uwanjani.


Yote ni katika kuendeleza mila.Ni katika kabila la wahamaji (nomads) la Vadi katika jimbo la Gujarat nchini India.Kabila hilo lenye takriban watu 600 hivi,lina mila ya kuwapatia watoto mafunzo ya sanaa ya kucheza na nyoka (snake charming).Lakini,hilo sio suala la siku moja,wiki,mwezi au mwaka bali ni muongo mzima (mika 10)!
Watoto huingizwa kwenye mafunzo hayo wanapotimiza miaka miwili tangu wazaliwe.Inatarajiwa kuwa watapofikisha umri wa miaka 12,watoto hao watakuwa wakielewa kila kitu kinachohusiana na nyoka.
CHANZO: The Daily Mail
13 Jun 2009
Kwa mujibu wa televisheni ya taifa ya Iran,Rais Mahmoud Ahmadinejad amefanikiwa kutetea nafasi yake kwenye uchaguzi mkuu uliofanyika nchini humo wiki hii.Kwa mujibu wa taarifa hizo,Ahmadinejad amepata asilimia 67 ya kura huku mgombea wa mwenye mrengo wa mageuzi,Waziri Mkuu wa zamani Mir Hossein Mousavi,akiambulia asilimia 30.
SURA YA MAGEUZI.UKURASA WA MOUSSAVI KWENYE FACEBOOK.12 Jun 2009
Bajeti ndio hiyo ishasomwa.Ila nimeonelea nami niiweke hapa.Isome hapo chini baada ja mjadala huu kiduchuTunaambiwa kuna maeneo takriban sita yaliyopewa kipaumbele katika bajeti hiyo.Naamini hata bajeti ya mwaka jana ilikuwa na vipaumbele vilevile lakini sote tunajua hali ikoje muda huu.Tatizo letu kubwa halipo katika kuainisha vipaumbele.Wala hatuna tatizo kuja na grand schemes zinazoweza kabisa kukuaminisha kuwa huenda sooner or later "maisha bora kwa kila Mtanzania yatakuwa sio tena slogan bali ukweli halisi".Tatizo la msingi ni kuvifanya vipaumbele hivyo viwe na maana,in the sense of kuvitafsiri kwa vitendo na si porojo.Sambamba na hilo ni namna vipaumbele hivyo vitakavyoweza kuruka vihunzi vya mafisadi.
Anyway,hilo sio la muhimu sana kwa sasa kulinganisha na uwezekano wa kufanikiwa kwa hizo tahadhari tunazoelezwa.Kwanza,yote yaliyoelezwa yanawezekana kwa sababu nia ipo,sababu zipo na njia zipo pia.Kinachoweza kukwamisha utekelezaji wa mpango mzima wa kunusuru uchumi ni ufisadi.
Nilitarajia bashasha zilizoambatana na bajeti hii zingegusia ishu ya ufisadi lakini wapi!Tuwe wakweli,hivi kuna uhakika gani kuwa hizo fedha zinazotengwa kwa ajili ya kufidiwa sijui watu gani hazitaishia kwa mafisadi?Ni muhimu kuuliza hilo kwa vile akina Kagoda bado wako huru uraiani na yayumkinika kuamini kuwa watashawishika kuchangamkia tenda hii ya "kunusuriwa na mtikisiko wa uchumi wa dunia."Simple logic ni kwamba kama waliweza kuiba bilioni 40 za EPA na taasisi husika zinaogopa hata kuwataja hadharani,kwanini safari hii wasikwapue tena fedha za umma kwa "njia halali"?
Naomba nitoe mfano hao katika kupigia mstari wasiwasi wangu kuhusu hatma ya hizo tahadhari tulizopewa kuhusu mtikisiko wa uchumi duniani.Hivi karibuni ulifanyika mheshimiwa mmoja aitwaye Peter Noni aliteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Benki wa Raslimali Tanzania (TIB).Uteuzi huu unaweza kuashiria ni kwa namna gani kelele dhidi ya watu wanaohusishwa kwa namna moja au nyingine na ishu za ufisadi zinavyopuuzwa.Jina la Noni limekuwa likitajwa sana kwa wanaojua undani wa ishu nzima ya EPA.Sasa sijui inamaanisha nini kumpeleka sehemu kama TIB,ambayo kwa hakika itapaswa kuwajibika ipasavyo kama tunataka tahadhari ya bajeti iwe na maana.Hii si ni mithili ya kumpa "teja" usimamizi ya stoo ya madawa?
Pasipo kudhibiti ufisadi na mafisadi,yayumkinika kuamini kuwa jitihada zote hizi zitaishia kunufaisha mafisadi na nyumba ndogo zao.Ni kweli kwamba Watanzania wengi wameonyesha umahiri mkubwa wa kukabiliana na hali ngumu ya uchumi na wameshazowea "kukaza mikanda kila wanapotakiwa kufanya hivyo" lakini hii inapswa iwe kwa Watanzania wote na si walalahoi pekee.Ikumbukwe kuwa mikanda hiyo imekuwa ikikazwa tangu wakati na baada ya Vita vya Kagera,na hatujawahi kusikia tamko kwamba WAKATI UMEFIKA KULEGEZA MIKANDA HIYO.Inwezekana kuwa tamko kama hilo halijatolewa kwa vile wakati huo (wa kulegeza mikanda) bado haujafika lakini inauma kuona kufunga mikanda kwa wengi kunatoa fursa kwa walafi wachache kufumuka vitambi (kiasi cha kushindwa hata kuvaa hiyo mikanda,let alone kuikaza) kwa matendo yao ya ufisadi.
Tuweke ushkaji pembeni,tuweke siasa za 2010 pembeni,tutambue kuwa mtikisiko wa uchumi ulimwengini ni kitu halisi na hata wafadhili wetu wanasumbuliwa nao.Tukiendeleza hadithi nzuri pasipo utekelezaji mzuri,tutajikuta pabaya.Tukumbuke kwamba tulikuwa masikini kabla hata ya huu mtikisiko wa sasa.Kinachotuweka pabaya kwa muda huu ni ukweli kwamba tofauti na huko nyuma,sasa hivi wafadhili wetu nao wana matatizo pia.Na kwa vile hakuna uhakika as to lini mtikisiko huu utapungua makali,ni vema pia tukatambua kuwa wafadhili hao wanaweza kutusahau kabisa ili waweze kumudu matatizo yao binafsi.
Inawezekana,only if kukiwa na dhamira thabiti pamoja na kuweka mbele maslahi ya nchi badala vikundi vya watu wachache.Na katika hilo,tayari kuna ishara isiyopendeza kwani waliofikiriwa katika stimulus plan ni wafanyabiashara (kwa maana ya taasisi na watu binafsi) pekee huku wakulima wakipuuzwa.Yet,tunaambiwa KILIMO KWANZA!I hope sio kilimo cha fedha za walipakodi kitachopelekea mavuno mwanana kwa mafisadi na kampeni zao za 2010!
Mungu ibariki Tanzania,na waadhibu pasipo huruma mafisadi wote.
BAJETI YA SERIKALI KWA MWAKA WA FEDHA 2009/2010
Subscribe to:
Posts (Atom)




























